Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104670 articles
Browse latest View live

Dada wa Diamond Esma Platnumz Akiri Kumpenda Sana Petit Man Awaomba Nyaku Nyaku Wasimyakue

$
0
0

Dada wa Diamond ameamua kufunguka ya moyoni na kudai anampenda sana mume wake Petit Man ambae walitengana kwa muda kutokana na kutokuelewa hapa na pale lakini kwa sasa inaonekana wameweka mambo sawa...Ameandika haya kwenye ukurasa wake

_esmaplatnumz
Baby dady mkimuona mwambieni mi Nampenda tuu ukiniuliza hata sijui... kuna wakati unaweza kufichaficha au kujionesha hupendi au ukajikaza usiseme unachojisikia kusema but mi naona bora uwe muwazi ili roho yako Iwe na Amani... Jamani mi Nampenda huyu kaka plz nyakunyaku kuweni makini huyu mi nahisi km kafika kigoma mwisho wa reli...na natania msije nikomoa...hamchelewi...

Hatuhusiki Kumtafutia Mtu Ajira - Bodi ya Mikopo

$
0
0
Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu imesema kuwa haihusiki kumtafutia mnufaika wa mkopo ajira badala yake inahusika kumpatia mwanafunzi mkopo na akishamaliza muda wa masomo atatakiwa kurejesha mkopo wake.

Hayo yamesemwa jana Jijini Dar es salaam na Mkurugenzi Msaidizi wa Habari, Elimu na Mawasiliano kutoka Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu Cosmas Mwaisobwa wakati akijibu maswali ya wananchi kupitia kipengele cha Kikaango cha EATV.

“Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu inatoa mikopo suala la kutafuta ajira halituhusu hivyo mnufaika yoyote asiwe na kigezo kwamba hajapata kazi , hiyo siyo kazi yetu, kazi yetu ni kuwawezesha kupata elimu basi” Alisema Mwaisobwa.

Aidha Mwaisobwa alisema wanufaika wote ambao walipata mikopo wanatakiwa kukatwa asilimia 8% ya pato la mwezi, na kama mtu anafanya kazi binafsi na hakatwi popote atatakiwa kutoa kiwango cha 120,000/= na kwa ambao wamenufaika na hawataki kuanza kulipa mkopo watapigwa penati ya 10% ya mkopo kwa mwaka.

Pamoja na hayo Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu imewataka walioomba mikopo kuvuta subira kwani Bodi inasubiri majina kutoka Tume ya Vyuo Vikuu ili Bodi ya Mikopo iweze kufahamu vyuo walivyopangiwa na kiwango cha ada ili haki iweze kutendeka kwa waombaji.

Gavana BOT Afichua Siri ya Kilio Cha Fedha Kupotea Mtaani

$
0
0
Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania, Profesa Benno Ndulu jana alitolea ufafanuzi hali ya kiuchumi nchini huku akieleza siri ya kilio kinachovuma cha fedha kupotea mtaani na nyingine zikidaiwa kufichwa.

Akizungumza na waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam, Profesa Ndulu alisema kuwa kwakuwa taasisi hiyo ndiyo inayofahamu fedha zote zilizopo benki na zilizopo mtaani, inafahamu kuwa hakuna fedha iliyopotea bali fedha zimepotea kwa watu waliokuwa wanazipata kwa njia ya udanganyifu kwakuwa sasa Serikali imebana mianya hiyo.

“Hakuna fedha iliyopotea, Serikali imebana shughuli za watu na ‘mission town’ sasa shughuli zote zinafanywa na Serikali. Hivyo, kwao fedha zimepotea, lakini kwetu hazijapotea,” alisema Profesa Ndulu.

Hata hivyo, Profesa Ndulu alikiri kupungua kwa fedha katika mabenki nchini hali iliyopelekea kupunguza kasi ya utoaji mikopo kwa wananchi. Alisema hali hiyo ilitokana na kuhamishwa fedha za mashirika ya umma na taasisi kutoka benki za biashara kwenda BoT.

“Fedha hizo zitarudi katika benki hizo wakati zitakapopelekwa kwenye Halmashauri kwa ajili ya kutekeleza miradi mbalimbali,” Profesa Ndulu aliahidi.

Katika hatua nyingine, Gavana huyo wa Benki Kuu alisema kuwa uchumi unatarajiwa kukuwa kwa asilimia 7.2 mwaka huu, huku akibainisha kuwa moja kati ya sababu zinazopelekea ukuaji huo ni  ongezeko la uzalishaji wa umeme na saraju.

Akizungumzia hali ya deni la taifa, alisema kuwa deni la taifa la ndani limeongezeka kutoka shilingi  trilioni 8.6 Mwezi Desemba mwaka jana hadi shilingi trilioni 10 mwezi Juni mwaka huu.

Profesa Ndulu alibainisha kuwa wakati deni linalotokana na kukopa ndani likipaa, deni linatokana na ukopaji wa limepungua baada ya Serikali kupunguza ukopaji nje ya nchi.

Faiza Ally Afunguka Kumpenda Sugu Kutoka Moyoni..Adai Haogopi Kuchekwa Kwa Kigeugeu Chake

$
0
0
Faiza Ally Amefunguka haya Katika ukurasa wake wa Instagram:



Leo nimeamka akili yangu inawaza mapenzi tu... Mkatae mkubali mapenzi yana nafasi kubwa sana ktk maisha... Na mapenzi hayana baunsa...😅 Mimi nampenda sana baba mtoto wangu - Nina mpenzi yes lkn nampenda yeye zaidi - ana mpenzi Sawa lkn hainizui kuongea hisia zangu... Nachekwa Sawa lkn wanao nicheka hawako ktk maisha yangu Kwa hiyo sio muhimu sana na sioni aibu kusema hisia zangu Kwa mtu ninae mpenda... Nampenda Kila siku Kila mwaka Na sijui nta Acha lini kumpenda.... Ila naamini Kama Mungu alivyo mleta-alivyo muondoa Ndio atakavyo nisahaulisha Na kuniletea mwingine au pengine kum rudisha .... Mapenzi kwangu yana sound hivi➡️➡️➡️➡️ muonyesha unampenda - ajue unampenda- kuwa mkweli- usimuogope- simama Kwenye ukweli- kuwa halisi Na uache maisha yaendelee - usilazimishe- usijikaze -usijifiche- usijifanye ..... Mimi ni Karatasi jeupe nisome lkn ni hiari yako kunielewa sio lzm unielewe lkn mwisho wa siku silazimishi yote heri ..... Nakupenda sana baba mtoto - pengine una niona uchafu au sina dhamani lkn moyo wangu ndio ume kuchagua - usinihukumu -usinichukie iko siku Mungu ataleta heri zake ntakusahau utapata Amani Na mpenzi wako Na mm Na wangu au labda ntakufa hutanisikia Tena ila Kwa sasa Naomba uniache vile najisikia .....Nakupenda Joseph Tanzania inajua.... Mama yangu anajua... Mtoto wetu anajua na nitaka dunia ijueeeeeeeeeee😭 Nakupenda sanaaaaa baba Sasha - usiniulize Kwa nini.... mm mwenyewe sijui Nakupenda tu hivyo yani ........ Tag him mwambie mama Sasha anakupenda zaidi Kila siku Na hakunaga Na sizani Na Kama unapendwa zaidi ya ninavyo kupenda ! Na Kama unapendwa Basi una bahati sana mshukuru Mungu Maana Natamani kupendwa Kama ninavyo kupendwa.....💔💔💔 Acha nichoreke haina kwere kuchoreka Kwa ninae mpenda sio kesi ...😭

Malawi Yadai Kuishtaki Tanzania Kwenye Umoja wa Afrika(AU)

$
0
0

Foreign Affairs and International Cooperation minister Francis Katsaira said Tanzania has released a new Lake Malawi map which shows the east African country has taken a chunk of Lake Malawi, which is potentially rich in oil and gas..

“We have already reported them to the African Union and very soon we will be reporting them to Comesa and Sadc,” he said.

Kasaira said Tanzanian authorities have threatened to beat up and arrest Malawians who will disregard the new map.

The old map, drawn up by Germany and Britain gives the whole Lake Malawi, except a small part to Malawi.

Tanzania has taken much interest in the lake after oil was discovered in the lake popularly known as lake of stars.

Katsaira said both Malawi and Tanzania were supposed not to interfere with the Lake Malawi issue as the matter was with the African Union and a mediation team.

He therefore said the government is waiting for a response from Tanzsnia on the proposal for Mutharika and Magofuli to meet inorder to iron out the misunderstanding over the lake.

Malawi disputes Tanzania’s claim to half the lake – Africa’s third biggest.

It has accused Tanzania of raising tension by allegedly intimidating Malawian fishermen on the lake.

Malawi awarded oil exploration licences to firms to search for oil in the lake, which Tanzania calls Lake Nyasa.

Utafiti wa Twaweza: Watazania 96% wanampongeza Rais Magufuli

$
0
0
Taasisi inayojishughulisha na kufanya tafiti mbalimbali nchini ya TWAWEZA. Leo imetoa ripoti inayoonyesha kuwa asilimia 96 ya Watanzania wapongeza utendaji wa Rais Magufuli, huku asilimia 68 wapongeza uwajibikaji wa wabunge wao.

Aidha katika ripoti hiyo inabainisha kuwa jambo maarufu alilofanya Rais Magufuli ni uondoaji watumishi hewa huku zuio la kuingiza sukari likikosa umaarufu.

Kiwango cha kukubalika cha Rais Magufuli katika utafiti mpya ni cha juu kuliko marais 128 wa Afrika.

Wasanii na viongozi wa WCB waalikwa nyumbani kwa rais mtaafu Jakaya Kikwete

$
0
0
Rais mstaafu wa awamu ya nne Jakaya Kikwete Jumatano hii aliwaalika wasanii wa label ya WCB pamoja na viongozi nyumbani kwake na kula nao chakula cha mchana.

JK ambaye ni mmoja kati ya marais ambaye amesupport sana wasanii wa muziki nchini, aliwaalika wasanii hao nyumbani kwake na kuzungumza nao mambo mbalimbali kuhusu muziki wao.

Mmoja kati ya viongozi wa juu wa label hiyo, Sallam alimshukuru rais huyo kwa kuwaalika nyumbani kwake na kuzungumza nao mawili matatu kuhusu muziki.

“Former President JM Kikwete and Former First Lady Mama Salma Kikwete. Asanteni kwa mwaliko wenu!! Allah awape afya njema,” Sallam aliandika instagram.

Congo DRC: Waasi wa Mai Mai wamewateka madereva 5 wa Tanzania, wanataka $ 4,000 kwa kila Dereva

$
0
0

KUNA TAARIFA KUWA waasi wa Mai Mai wamewateka madereva wa Tanzania watano na kuchoma baadhi ya magari. Wanadai usd 4000 kwa kila Dereva amasivyo watawapiga risasi. Wametoa deadline ya majeshi kuondoka pia.

Chama cha Wamiliki wa Magari ya Mizigo nchini Tanzania (TATOA) kinaripoti kwamba, waasi wa Mai Mai nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), wamewateka nyara madereva wa Tanzania na kuchoma baadhi ya magari ya mizigo. Waasi hao wanadai dola za Kimarekani elfu nne (karibu shilingi za Kitanzania milioni tisa) kwa kila dereva ama sivyo watawapiga risasi madereva wote. Pia waasi hao wametoa siku ya mwisho (deadline) ya majeshi yanayolinda amani nchini humo kuondoka.

TATOA inasema imezungumza na mmiliki wa kampuni ya Simba Logistics, Mzee Azim Dewji ambaye amethibitisha taarifa hizi na pia balozi wa Tanzania DRC pamoja na Wizara ya Mambo ya Nje tayari serikali inashughulikia suala hili. Jumla ya magariyaliyotekwa ni 12 kati ya hayo magari 8 ya Tanzania na 4 ya Kenya. Magari 4 ya Tanzania yamechomwa moto na madereva wote walichukuliwa na waasi lakini bahati nzuri madereva wawili wa Tanzania walifanikiwa kuwatoroka. Tukio hilo limetokea sehemu inaitwa Kasebebena na Matete, wastani wa kilomita 30 kutoka mji wa Namoya.

TATOA inawashauri wanachama waliopakia mzigo kuelekea huko kuwasiliana na madereva wao ili wasitishe safari, kusubiri taarifa ya hali ya usalama kutolewa.

Mai Mai Kata ni kundi la waasi nchini DRC ambalo linadai kupigania uhuru wa jimbo la Katanga, na linaongozwa na Gédéon Kyungu Mutanga, ambaye aliunda kundi hilo mara tu alipotoroka kutoka gerezani mwaka 2011.


Tumezungumza na mmiliki wa kampuni ya Simba Logistics Mzee Azim Dewji amethibitisha taarifa hizi na tayari tumezungumza na balozi wa Tanzania DRC pamoja na wizara ya mambo ya nje tayari serikali inashughulikia swala hili. Jumla ya gari zilizotekwa ni 12 kati ya hizo gari 8 za Tanzania na 4 za Kenya.

Gari 4 za Tanzania zimechomwa moto na madereva wote walichukuliwa na waasi lakini bahati nzuri madereva wawili wa Tanzania walifanikiwa kuwatoroka. Tukio limetokea sehemu inaitwa Kasebebena na Matete kilometer 30 kutoka mji wa Namoya.

Tunawashauri wanachama waliopakia mzigo kuelekea huko kuwasiliana na madereva wao wasitishe safari ili kusubiri taarifa ya hali ya usalama kutolewa.

Tutazidi kuwapatia update information.


Namanga: Edward Lowassa asimamishwa na wananchi wamweleze ugumu wa maisha

$
0
0
Mh Edward Lowassa Mjumbe wa kamati kuu wa chama Cha demokrasia na maendeleo (CHADEMA ) na Chama kikuu cha Upinzani TANZANIA na Waziri Mkuu mstaafu amesimamishwa na Wananchi wa Namanga Mpakani mwa Tanzania na Kenya . 

Wananchi wamemueleza Ugumu na ukali wa Maisha walionayo ikiwa ni pamoja na kudorora kwa mzunguko wa fedha mpakani hapo leo hii akiwa safarini Toka Nairobi Kenya alipokwenda kuhudhuria mazishi ya Marehemu Ole Ntimama.

Kanitafutia Kazi Sasa Nimekua Mtumwa wa Ngono Kwake

$
0
0
Hi guys, niaje?

Ni miezi miwili sasa tangu nimeacha kazi kampuni ya zamani, na sasa nipo kwenye kampuni nyingine, hii kazi mpya nimetafutiwa na Boss wangu ambae ndie mkuu wa idara yetu, nimepanda cheo kidogo, kule nilikuwa Karani na huku kupya mimi ni Supervisor.

Sasa huyu Boss alieniingiza kazini nimekua na urafiki nae tangu nimeingia hapa, kitu kinachonikwaza ni mwenendo wa huyu Boss wangu, yaani nimekua kama mtumwa, wakati wote anataka tufanye ngono, jioni wakati wa kuondoka anataka tubaki ofisini kwake, najikuta nafika home saa tatu hivyo kumkuta Mr wangu amesharudi Muda, inakua ugomvi, inabidi nimdanganye kuwa kazi mpya imekua too demanding kwangu, nachelewa kutoka.

Weekend ni hivyo hivyo, inabidi nisingizie home kuwa tunatakiwa kazini hata Jumapili, nimejikuta naishi kama mtumwa kwa sababu ya hii kazi aliyonipa huyu Boss, maneno maneno yamekua mengi hapa kazini miongoni mwa Staff wenzangu kuhusu mwenendo wangu na huyu Boss, nina wasi wasi maneno haya yanaweza kumfikia Mr wangu ikawa shida.

Natamani kuirudia ile kazi yangu ya awali, kazi hii mpya napata mshahara mzuri lakini nimekua kama mtumwa, wakati mwingine nikionesha dalili za kumgomea kubaki jioni anakua mkali na kuanza vitisho kwamba eti '' unasahau nani kakuweka hapo ''Inabidi tu nishiriki nae ingawa sipendi.

Naombeni ushauri nifanyeje?

Rubby Atangaza Kujisimamia Mwenyewe Baada ya Kutemana na Clouds FM, Adai Sasa ni yeye na Mashabiki wake

$
0
0
Msanii wa Bongo Fleva, mwanadada Ruby ambaye amewahi kutamba na wimbo wake wa “Na Yule’ amefunguka na kusema kwa sasa amebadili uongozi wake na kujisimamia yeye kwani anataka kusimama yeye pamoja na mashabiki zake.

Ruby alisema hayo kwenye kipindi cha eNewz na kudai kuwa yeye aliamua kubadili uongozi kwa sababu anataka kusimama yeye kama yeye kwenye muziki kwa kutegemea mashabiki wake, pia Ruby anadai Tanzania ukimchana mtu ukweli unaonekana wewe ni mkorofi au mgomvi.

“Unajua hata mtoto anapokuwa kwa wazazi inafika wakati anahitaji kuanza maisha yake mwenyewe, hivyo mtoto akiondoka kwa wazazi haina maana kuwa hauna wazazi ‘No’ wala haina maana kuwa umeondoka nyumbani kuna matatizo bali unakuwa umeanza maisha yako mwenyewe, ni sawa na mimi saizi nimebadili uongozi wangu na niko mimi kama mimi kwani nataka kusimama pamoja na mashabiki zangu. Watu wanasema sijui mimi ni mkorofi hao ni wao kwani mtu ukimchana ukweli unaonekana wewe ni mkorofi ni bora ukamwambia mtu ukweli kwani ukweli utakuweka huru” alisema Ruby

Mwanamuziki Billnass Awa Lulu , Label Kubwa za Mziki Zamgombania Bongo

$
0
0
Msanii wa muziki wa Hip Hop anayefanya vizuri na wimbo ‘Chafu Pozi’ Billnas amesema yupo kwenye mazungumzo ya kuhamia katika label kubwa ya muziki hapa nchini hivi karibuni.

Rapper huyo ambaye kwa sasa yupo chini ya label yake ya ‘LFLG’, ameiambia Bongo5 kuwa kuna label nyingi zinamtaka kufanya naye kazi.

“Kusema kweli kuna mambo makubwa yanakuja, huwenda kazi yangu mpya ikaja nikiwa ndani ya label mpya,” alisema Billnas. Kuna label nyingi zimekuja na bado nipo kwenye mazungumzo, nadhani muda ukifika mtasikia tu,”

Billnas alianza kufanya vizuri na wimbo ‘Ligi Ndogo’ akiwa Rada Entertainment lakini baadae alihama katika label hiyo na kuanzisha label ya ‘LFLG

Serikali Yaanza Mazungumzo ya Kuwaokoa Madereva 12 Waliotekwa Kongo

$
0
0
Serikali imeingilia kati na kuanza mazungumzo ya kuwaokoa madereva 12 wa malori kutoka Tanzania waliotekwa nchini Kongo (DRC) na kundi la waasi wa Mai Mai.
loritanzania

Waasi hao mbali na kuwateka madereva hao wametoa saa 24 kuanzia juzi saa 10 jioni walipwe fedha kiasi cha Dola za Marekani 4,000 kwa kila dereva ili waweze kuwaachia.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mindi Kasiga, alisema waasi hao wametishia kuwaua mateka hao endapo hawatalipwa kiasi hicho cha fedha hadi kufikia jana saa 10 jioni.

Mindi alisema katika tukio hilo, madereva wawili wa Kitanzania walifanikiwa kutoroka na ndiyo waliosaidia kutoa taarifa kuhusu tukio hilo.

“Serikali imepokea taarifa za kutekwa kwa malori 12 katika eneo la Namoyo Jimbo la Kivu Kusini, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, jana (juzi) Septemba 14, 2016. Kati ya malori hayo manane yanamilikiwa na mfanyabiashara wa Kitanzania, Azim Dewji na mengine yanamilikiwa na wafanyabiashara kutoka Kenya.

“Kwa taarifa zilizopatikana watekaji ni kikundi cha waasi cha Mai Mai ambao baada ya kuyateka magari hayo, waliwashusha madereva na kuwapeleka porini na kisha kuteketeza kwa moto malori manne ambayo yote ni ya Dewji.

“Waasi hao wametoa saa 24 kuanzia jana saa 10 jioni walipwe fedha kiasi cha Dola za Kimarekani 4,000 kwa kila dereva ili waweze kuwaachia,” alisema Mindi.

Alisema Serikali kupitia Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki imeshachukua hatua za awali za kuwasiliana na Serikali ya DRC ili kuhakikisha kuwa madereva hao wanaachiwa haraka iwezekanavyo wakiwa salama kabisa.

Alisema tukio la aina hiyo ni la pili kutokea ambapo katika mwaka jana masheikh kutoka Tanzania walitekwa nchini DRC lakini kwa ushirikiano wa Serikali hizo mbili juhudi ziliweza kuzaa matunda na masheikh hao kuachiwa huru bila madhara yoyote.

“Serikali ingependa kuushauri umma wa Watanzania hususan wafanyabiashara kuomba taarifa ya hali ya usalama kwa maeneo yenye matatizo ya kiusalama kama Mashariki ya Kongo hususan Kivu ya Kusini kabla ya kusafiri kwenda maeneo hayo,” alisema Mindi.

FIESTA Yarudisha Penzi la Shilole na Nuh Mziwanda....

$
0
0
Wapenda Kunyapia nyapia Udaku wa Mastaa wa Bongo wameachwa njia panda baada ya mastaa Nuh Mziwanda na Shilole kuanza tena kuwa karibu kwa kupostiana kwenye page zao za mitandaoni, Wawili hao ambao siku za njuma walikuwa wapenzi wa kupika na kupakuwa waliachana na kila mmoja kuchukua hamsini zake lakini msimu huu wa Tamasha la Fiesta inasemekana wamekuwa karibu kutoka na kuwa ni wamoja wapo katika watumbuizaji wa Tamasha hilo huku wakisafiri mikoa mbali mbali kitu ambacho kimewaweka karibu zaidi

Nuh Amepost Picha hii katika ukurasa wake wa Instagram:

Baada ya Muda Shilole naye Akajibu Mapigo kwa kuweka picha ambayo inaonyesha alimpiga Nuhu Mziwanda wakiwa katika Chumba cha Hotel.....
Wajuzi wa Kunyapia nyapia Udaku Wanadai Picha hiyo aliyopost shilole na kuiifuta inaujumbe mzito ndani yake , Kuwa inawezekana wawili hao huko walipo kwenye Tamasha wanalala chumba kimoja....


Mziwanda na Shilole Waeleza Kilichotokea Mpaka Wakapostiana Instagram Jana

$
0
0
Nuhu Mziwanda na Shilole Katika Pozi la Mahaba
Wasanii wa bongofleva Shilole na Nuh Mziwanda waliwahi kuwa wapenzi lakini wakaachana na baada ya hapo Shilole alionekana kutotaka hata kusamiliana na Nuh japokua walifikia kupatanishwa.

Banda ya haya yote September 15 2016 wawili hawa wamepostiana Instagram kwa mara ya kwanza toka kuachana kwao, hapa chini ukibonyeza play utawasikia wakieleza ilivyokua mpaka wakapatana.


Kinywaji Kilichopewa Jina ‘Poteza Ubikira’ Chazua Gumzo China

$
0
0
Kinywaji maarufu kwa jina ”blackout in a can’ nchini Marekani kimeingia nchini China na kuzua gumzo kwa watumiaji wa kinywa hicho.

Four Loko , ni kinywaji kilicho na ladha ya matunda na asilimia 12 ya pombe kilitumika sana katika sherehe nchini Marekani kabla ya kuondolewa madukani katika majimbo kadhaa hadi pale viungo vyake viliporekebishwa.

Na sasa kimepata umaarufu mkubwa nchini China , huku raia wakikiita ‘Lose Virginity’ kwa kuwa wanahisi kinywaji hicho kina nguvu zaidi.

Wananchi kadhaa wamepakia kanda za video wakinywa kinywaji hicho cha mililita 695.

Kinywaji hicho kiligonga vichwa vya habari hivi majuzi baada ya wanawake watatu walio katika umri wa miaka 20 kuficha na kuingiza kinywaji hicho katika baa moja ya karaoke,kupoteza fahamu baada ya kunywa na kupoteza vitu vyao vyote kwa wezi.

Four Loko kimeelezewa katika mitandao ya kijamii nchini China kuwa kinywaji kilicho na pombe pamoja na kafeini.

Baadhi ya watu wanadai kwamba mchanganyiko huo unakifanya kinywaji hicho kuwa na nguvu na kina uwezo wa kumfanya mtu kupoteza fahamu baada ya kunywa chupa moja tu

Ukifanya Haya Mambo Mapenzi Yatanoga Kwa Asilimia 90

$
0
0
Wanaume wengi hupuuzia hili, huona kama ni jambo lisilo na maana sana kwao na wenzi wao. Hali ni tofauti sana kwa wanawake ambao hupenda kuwasifia wanaume zao. Nitakupa mifano miwili ya namna wanandoa wa jinsia mbili tofauti wanavyotambulishana kwa jamaa zao. Kwa mafano manakutanata kwenye majumuiko ya harusi na sherehe kama hizo. Mme 1 akamtambulisha mkewe kwa jamaa zake, huyu ni mama Rick mke wangu. Mme wa 2 akamtambulisha mkewe, huyu ni my lovery sweetheart wife, nampenda sana kuliko wanawake wote duniani. Kama upo kwenye huu utambulisho umeona tofauti gani? hao wanawake wa pande mbili watajisikiaje? Nahisi umejifunza kitu hapo

MALENGO SHIRIKISHI
Wanaume wengi wana ulemavu mmoja; hawapendi kuwashirikisha wanawake katika mambo yao. Wanapenda kufanya mambo yao kwa siri na wakati mwingine ikilazimika kumwambia mkewe basi kwa mshtukizo baada ya kukamilisha jambo husika. Siku hizi dunia imebadilika, kuna mambo mengi. Kuna suala la hasara katika biashara, utapeli, kifo cha gafla, ajali n.k. Mkeo ndiye rafiki yako mkubwa kuliko wote, ndiye ndugu yako wa karibu zaidi kuliko yeyote. Mmeshirikiana kuzaa watoto na kujenga maisha pamoja. Yeye anapaswa kujua mambo yako, ndiye mtetezi wako nambari wani. Mweleze juu ya malengo yako, wakati mwingine anaweza kukusaidia sehemu ambayo hukutarajia. Hata hivyo, kumshirikisha katika malengo yako, kunampa nguvu na nafasi ya kujiona mama katika familia yenu. Lakini ngoja nitoe angalizo, kuna wanawake ambao huwezi kumshirikisha from A to Z ya malengo yako kutokaa na tabia na mienendo ya maisha, hope kila mtu anafahamu strength and weakness ya wake na waume zetu, so be careful in some extent.

KIPAUMBELE/CONCERN
Kuna wakati wanawake huwa na mambo yao binafsi. Kazini au kifamilia. Inawezekana akatatizika katika eneo fulani ambalo kwa namna moja ama nyingine atahitaji usaidizi wako. Ikitokea mkeo akawa katika hali hiyo, msikilize. Mathalani ana tatizo la kifamilia, amekuambia mmoja wa wazazi wake anaumwa, msaidie. Si lazima kifedha, lakini kuonesha kujali kwako tu, kutampa matumaini na faraja kwamba anaishi na mtu sahihi. Acha kupuuza mambo yake; hata yale madogo, kama ya ‘mtoto wa dada amerudishwa ada shuleni’. Msikilize, mshauri panapofaa kufanya hivyo na ukiweza msaidie hata kifedha. Katika upande wa pili ni hivyo hivyo. Labda una tatizo binafsi, kikazi au kifamilia, mshirikishe. Unaweza kushangaa jambo ambalo uliamini unaweza kulimaliza peke yako, kwa kumshirikisha likawa jepesi zaidi na mambo yakaenda vyema. Kipaumbele kwa namna yoyote ile, kunaongeza mapenzi zaidi kwa mwanamke.
"Together we swim in the same pool"

USAFI
Asilimia kubwa ya wanawake wanapenda sana usafi. Ni aghalabu kukutana na mwanamke asiyejipenda. Ndiyo maana wanaitwa mapambo ya nyumba au ua la nyumba! Ni kwa sababu ya hulka yao ya kupenda sana usafi. Mwanamke anavutiwa sana na mwanaume mtanashati. Usafi wako unamfanya ajiamini kuwa na wewe. Hata nyumbani kwako, lazima uishi katika nyumba safi. Hata anapokuja kukutembelea, anakuta mazingira masafi kuanzia sebeleni hadi chumbani. Anapokukuta katika hali ya usafi, inakuwa rahisi zaidi yeye kuanzia hapo alipokukuta na kuendelea mbele. Rafiki yangu, kama uko mbali na usafi, ujue kuwa itakuwa vigumu kupata mdada wa ukweli – yule wa ndoto zako. Wanaume wengine wanapanga kutoka outing na wapenzi wao, mkifika huko mwanamke anajuta WHY amekubali kukutana na wewe maana utamkuta mwanaume hajapasi Tshirt/shirt, kwapa linapumua, ukiongea mdomo unatoa harufu inakuwa tabu tupu. Mwanume ukijipenda unatakuwa mtanashati tu

KUJIAMINI
Mwanamke anajisikia salama zaidi akiwa na mwanaume ambaye anajiamini – mwenye uwezo wa kutetea hoja zake na kujieleza sawia. Siyo anayebabaika. Suala la msimamo binafsi, kwa mwanamke ni kubwa kuliko hata kumnunulia manukato mapya! Mathalani unakuwa naye katika mtoko, angependa kukuona ukiwa katika hali halisi ya maisha yako, usiyeyumbishwa na mwenye kutoa maamuzi yasiyoyumba. Wakati mwingine, mwanamke anaweza kukupima hata katika jambo ambalo amekosea yeye, ataangalia unavyotoa maamuzi yako, lakini pia atafuatilia kuona kama utakuwa mwepesi wa kuyabadilisha. Anataka kuona msimamo wako muda wote. Mwenye kujiamini na mawazo yasiyo na matege wala makengeza! Usiyebadilika kama kinyonga! "Men believe on your standing hills"

ANAYEJALI na KUFUATILIA
Wanawake wanapenda sana wanaume wanaowajali. Wanaowaona wao ni kila kitu na wanaotoa kipaumbele kwao. Kama huna tabia hiyo, ujue upo katika nafasi kubwa ya kumkwaza mpenzi wako. Mjali mpenzi wako kwa kila hali lakini pia uwe na kiasi. Kumjulia hali kila wakati na kutaka kujua maendeleo yake, kutakupa nafasi kubwa ya kuendelea kudumu katika uhusiano hai. Wanaume wengi ni wavivu, si tu kuwatumia hata SMS za “mambo dia?” wapenzi wao lakini hata kujibu tu, “niko poa, Si hulka ya wanaume kutumatuma SMS – inajulikana, lakini angalau ukiweza kulifanya hili hata kidogo tu hata mara moja kwa wiki, utakuwa unajiongezea pointi kwa mwenzi wako na kumpa courage ya kufurahia mapenzi ya ndoa.

MAANDALIZI YA TENDO LA NDOA
Tendo la ndoa halina maana ya kukomoana. Jenga mazoea ya kufanya maandalizi kamili kabla ya tendo. Sikiliza hisia za mwenzako. Ukiweza kumjulia mke wako katika eneo hili, ni wazi kwamba utazidisha upendo wake kwako, lakini pia atakuwa katika kuta za uaminifu. Unapokuwa kazini mchokoze "aisee nasikia hamu leo" hayo ndo maandalizi ya saikolojia. kupitia sms hiyo utasikia feeling zake, ataji-express. Kufikia jioni/usiku utashangaa unashikwa mkoni kupelekwa kitandani. Akatafute nini nje wakati wewe ndiye mganga wake unayeweza kumtibu barabara? Jiamini katika shughuli, fanya mazoezi ya viungo hata kukimbia ili uongeze pumzi ya kutoa dozi kitandani.
Epuka mapenzi ya kubakana, unafika tu bed unamvuta unamvua na kuanza kupanda kifuani......nooooooo hapo hakuna maandalizi ya kisaikolojia wala ya kimwili, hii itampekea kuchukia tendo because there is no any enjoyment

OUTING SOMETIMES
Kulingana na budget yako, si vibaya mara moja kumtoa mpenzi wako outing walau mara moja ndani ya miezi sita hata mwaka kama budget ni shida. Kwa wale wenye familia unaweza toka mkaspend 1 or 2 days outing na mkeo. Kuna mambo mmeo/mkeo anaogopa kukufanyia kulingana na mazingira ya hapo nyumbani na familia kwa ujumla. Lakini mkitoka nje LAZIMA mta-experience the difference for SURE. Pia ni njia mojawapo ya kuboresha na kupalilia penzi lenu na kuongeza uaminifu kati yenu

Naomba niishie hapo kwa leo

Sakata la Redio Kufungwa, Magic FM Yatakiwa Kuomba Radhi Siku Tatu Mfululizo, Redio 5 Yafungiwa Miezi

$
0
0
August 29 2016 Waziri wa habari, utamaduni, sanaa na michezo Nape Nnauye alitangaza kuvifungia vituo viwili vya radio kwa muda usiojulikana ambavyo ni Magic Fm ya Dar es salaam na Radio 5 ya Arusha kwa makosa ya kutangaza na kutoa habari za kichochezi.

Waziri Nape alielekeza kamati ya maudhui kuviita vyombo hivyo na kuwasikiliza kwa kina kisha kushauri hatua zaidi ya kuchukua.

Leo September 16 2017 kamati imetoa maamuzi ambapo Magic FM wamepewa onyo kali na kutakiwa kuomba radhi kwa siku tatu mfululizo kuanzia kesho September 17 2016, Redio 5 imepewa adhabu ya kulipa shilingi milioni 5, kufungiwa miezi 3 na kuwekwa chini ya uangalizi wa mwaka mmoja.

Alichokizungumza Waziri wa Mambo ya Ndani Congo kuhusu madereva waliotekwa

$
0
0
Jana ziliripotiwa habari za kutekwa kwa madereva wa malori kutoka Tanzania na Kenya kutekwa na kundi la waasi nchini Congo. Leo September 16 habari zilizoripotiwa na BBC Swahili zimedai kuwa watu wameokolewa na jeshi la nchi hiyo.

BBC imezungumza na waziri wa mambo ya ndani wa nchi hiyo ambapo kuwa madereva wote wameokolewa na vikosi vya jeshi la nchi hiyo na wako salama. BBC imesema utekaji wa madereva hao ulifanywa na watu wenye silaha katika kijiji cha Matete kuelekea Namoya kilichopo Mji wa Kivu Kusini Mkoa wa Manyema.

Waziri wa Mambo ya Ndani wa Congo alipoongea na BBC kwa njia ya Simu, amesema ni magari saba ya kampuni ya Simba inayomilikiwa na mfanyabiashara Azim Dewji kutoka Tanzania ndio yaliyochomwa.

Waziri huyo amesema tukio hilo halijafanywa na waasi kama ilivyoanza kuripotiwa, ila ni majambazi tu ndio waliofanya tukio hilo.

>>>Ni majambazi tu wanatoka porini walipoona magari yanatembea wakayasimamisha katikati ya pori na kuangalia kama kuna pesa wanyang’anye lakini hawakukuta pesa wakaamua kuwachukua madereva na kukimbia nao porini kisha wakayachoma magari 6 na moja halikuteketea.:- Waziri Mambo ya Ndani Congo

Zombe Aachiwa Huru, Mshirika Wake Ahukumiwa Kunyongwa Hadi Kufa

$
0
0
Mahakama ya Rufaa imemhukumu aliyekuwa Mkuu wa Upelelezi Wilaya ya Kinondoni, Christopher Bageni kunyongwa hadi kufa katika kesi ya vifo vya wafanyabiashara wa madini iliyokuwa ikimkabili yeye pamoja na aliyekuwa Mkuu wa Upelelezi Mkoa wa Dar es Salaam (RCO) Kamishna Msaidizi wa Polisi Abdallah Zombe na maofisa wenzake wawili.

Katika hukumu hiyo, Zombe na maafisa wengine wawili wameachiwa baada ya kushinda rufani hiyo dhidi yao.

Hukumu hiyo imehitimisha mvutano wa muda mrefu wa kisheria kati ya Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) na maofisa hao kwani baada ya kimya kirefu hukumu hiyo imetolewa.

Watuhumiwa wengine katika kesi hiyo walikuwa ni, aliyekuwa Mkuu wa Upelelezi wa Kituo cha Polisi Urafiki, Mratibu Msaidizi wa Polisi (ASP) Ahmed Makelle na Rajabu Bakari.

Hukumu hiyo imekuwa ikisubiriwa kwa muda mrefu, wakiwamo ndugu wa marehemu hao, wanasheria na jamii kwa jumla baada ya miezi minne, majuma mawili na siku mbili, tangu rufaa iliposikilizwa.

DPP alikata rufaa akipinga hukumu ya Mahakama Kuu iliyowaachia huru Zombe na wenzake wanane katika kesi ya mauaji ya wafanyabiashara wawili wa madini kutoka Mahenge, Morogoro na dereva wa teksi, mkazi wa Dar es Salaam.

Katika kesi ya msingi, Zombe na wenzake walidaiwa kuwaua kwa kukusudia wafanyabiashara Sabinus Chigumbi, maarufu Jongo na ndugu yake, Ephrahim Chigumbi, Mathias Lunkombe na Juma Ndugu, aliyekuwa dereva wa teksi wa Manzese.

Walidaiwa kutenda makosa hayo Januari 14, mwaka 2006, katika msitu wa Pande, uliopo wilayani Kinondoni baada ya kuwakamata wafanyabiashara hao Sinza, walipokuja Dar es Salaam kuuza madini.

Agosti 17, 2009, Mahakama Kuu iliwaachia huru washtakiwa hao ikisema baada ya kusikiliza ushahidi na hoja za mawakili wa pande zote iliridhika kuwa hawakuwa na hatia ya mashtaka yaliyokuwa yakiwakabili.

Badala ya kosa la mauaji ambalo adhabu yake ni kunyongwa hadi kufaa, DPP aliiomba Mahakama imtie hatiani Zombe kwa kosa la kuwalinda wahalifu, ambao adhabu yake ni kifungo kisichozidi miaka saba jela.

Wakili wa Serikali Mkuu (PSA), Timon Vitalis alidai DPP alifikia uamuzi huo baada ya kujiridhisha kuwa hakuna ushahidi wa kumtia hatiani Zombe kwa kosa la mauaji.

Viewing all 104670 articles
Browse latest View live




Latest Images