Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104706 articles
Browse latest View live

JE Mwanamuziki Billnass Amejiunga na Label ya The Industry ya Nahreel? Jibu Liko Hapa

$
0
0

Msanii na mtayarishaji wa muziki wa The industry, Nahreel ameweka wazi kuwa label ya The industry ina project nyingi na rapper Billnas anayefanya vizuri na wimbo ‘Chafu Pozi’.
billnas

Rapper Billnas hivi karibuni aliwapa taarifa mashabiki wake ujio wa project nyingi kutoka The industry.

Akiongea na Bongo5 Jumamosi hii, Nahreel amesema kwa sasa wana kazi nyingi na rapper huyo.

“Yeah Billnas na The Industry kuna kazi nyingi zinakuja, nisingependa kuziweka wazi kwa sasa kwa sababu ni mapema,” alisema Nahreel. “Lakini pia wasanii wa label ya The Industry tayari wana kolabo nyingi na wasanii wa kubwa hapa nchini, kwa hiyo naweza sema mambo mazuri yanakuja soon,”

Kwa upande wa Kundi la Navy Kenzo, Nahreel amewataka mashabiki wa muziki kukaa mkao wa kula kwa ajili ya ujio wa kazi mpya za kundi hilo.

DUDU Baya a.k.a Mamba Aichana Chana Clouds Fm, Amwagia Sifa Rubby

$
0
0
Msanii mkongwe na asiyesahaulika katika tasnia ya muziki wa kizazi kipya dudu baya amekivua nguo kituo cha clouds fm kwa kuwaita ni wanafki wakubwa, wanyonyaji wa wasanii, na wenye kuharibia wasanii ndoto za mziki wao
Mamba alitolea mfano wasanii wanazungushwa mikoani kwenye tamasha la fiesta na kuambulia ujira mdogo, huku akisema pesa wanayopata kwenye hilo tamasha huishia hukohuko mikoani na hurudi dar wakiwa wamepayuka hawana kitu mfukoni

Dudu alisema hayo akipokuwa kwenye kipindi cha usiku cha FRIDAY NIGHT LIVE... FNL kinachorushwa na EATV

Alienda mbali zaidi kwa kumpongeza msanii mwenye kipaji anayekuja juu ruby kwa kusema ametoka kwenye minyororo ya wafu FM akawasihi na wasanii wengine wamuige ruby kwani ameonesha mfano

Akionekana mwenye afya km alivyokuwa zamani, amesema wafu fm hawajapiga nyimbo zangu kwa miaka sita sasa lakini sijatetereka naendelea na maisha yangu kama kawaida

Wakati akiendelea kuwatolea uvivu clouds fm mtangazaji wa kipindi hicho sam misago alitumia mbinu ya ziada kumtoa kwenye kile akichokuwa nacho moyoni
Hata hivyo alipongeza redio ambazo zipo chini ya IPP km East africa radio, radio one, capital fm na kusema hajawahi kuombwa pesa na mtangazaji au dj yeyote wa kituo hicho ili wimbo wake uchezwe hewan
Amevitaka vituo vingine kuiga vyombo vya ipp media

Kwa maneno ya dudu baya ni dhahiri wasanii wengi ni watumwa wa baadhi ya media house

RAIS Magufuli: Tetemeko Halijaletwa na Serikali, Watu Wafanye Kazi

$
0
0
Mkuu Anasema waathirika wasikae tu huko wanangoja hela za serikali kwa sbb wanasikia zimechangwa,waanze kujisaidia kwanza wao na serikali itawasaidia pale waliposhindwa.

Mkuu anasema mtu ukuta umedondoka, anataka asubiri serikali ndio imtengenezee! Watu wajue tetemeko ni janga la asili halijaletwa na CCM. Waanze kwa kujenga wenyewe kuta zilizodondoka sio wasubiri serikali, sababu maisha yanendelea na watu wanatakiwa wafanye kazi kwa kujenga nyumba zao na sio kila kitu serikali itafanya.

Na wale wanasiasa wanaotaka kutumia janga hili kujinufaisha kisiasa mkuu anasema waache mara moja....Na kasema wote wanaotumia janga hili kukusanya misaada kwa njia ya kitapeli, basi wakamatwe mara moja.

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumapili ya Septemba 18

$
0
0


Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumapili ya Septemba 18

Naongoza kwa Kutukanwa Kwenye Muziki, Lakini Najivunia Kuupeleka Muziki Sehemu Fulani – Ruge

$
0
0
Mkurugenzi wa Uzalishaji wa Vipindi Clouds Media Group, Ruge Mutahaba amesema yeye ni mtu ambaye anaongoza kwa kutukanwa katika tasnia ya muziki kutokana na harakati zake za kuupigania muziki.

Akiongea Ijumaa hii katika semina ya wasanii wachanga wa Dodoma iliyofanyika katika Ukumbi wa Royal Village, Ruge amewataka wasanii hao kuacha kukata tamaa katika harakati wanazopitia.

“Mimi ni mtu ninaeongoza kwa kutukanwa kwenye tasnia ya muziki,” alisema Ruge. “Nimetukanwa sana lakini hilo haliniumizi, najivunia kwa kuwa tumepambana sana kuusimamisha muziki wetu hadi kufika hapa,”.

Ruge Mutahaba ni mmoja kati ya watu waliosaidia kwa namna moja kuchochea kukuwa kwa muziki wa bongofleva nchini licha ya baadhi ya watu kutokubali harakati zake.

Itizame hapa video mpya ya Diamond Platnumz ft. Rayvanny – Salome

$
0
0
Staa wa muziki nchini, Diamond Platnumz ameachia nyimbo ambayo amemshirikisha msanii mwenzake ambaye yupo katika lebo yake ya WCB Wasafi, Rayvanny ambayo ameipa jina la Salome. Video ameshoot, Nicorux kutoka Afrika Kusini Aprili, 10 mwaka huu, itizamehapa.

EDWARD Lowassa Kumwanika Profesa Lipumba

$
0
0
Aliyekuwa mgombea urais wa Chadema akiungwa mkono na vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), Edward Lowassa, anajiandaa kuweka wazi ushiriki wa aliyekuwa Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahimu Lipumba katika mchakato wake wa kuhamia Chadema mpaka kuwa mgombea urais.

Akizungumza kwa simu na mwandishi wa habari hii akiwa Nairobi nchini Kenya jana, Lowassa ambaye pia alikuwa Waziri Mkuu, wakati wa Serikali ya Awamu ya Nne ya Rais Jakaya Kikwete, alisema akirudi kutoka safari hiyo, atafafanua mbele ya vyombo vya habari, tuhuma dhidi yake zilizotolewa na Profesa Lipumba.

“Kwa sasa naomba uniache kwanza maana nipo safarini Nairobi, nikija Dar es Salaam nitazungumzia suala hilo kwa undani kupitia vyombo vya habari, hivyo subirini nirudi,” alisema Lowassa.

Madai ya Lipumba
Hivi karibuni Profesa Lipumba alitupa lawama moja kwa moja kwa Lowassa, kwamba ujio wake ndani ya Ukawa, unaoundwa na Chadema, CUF, NCCR-Mageuzi na NLD, ndiyo ulisababisha matatizo katika vyama hivyo kwa kiasi kikubwa.

Kwa mujibu wa Profesa Lipumba, kabla ya kujiunga kwa Lowassa Ukawa, vyama hivyo walikaa kikao ambacho aliwashauri viongozi wenzake wa Ukawa kutazama mtu anayeweza kuendana na mahitaji yao awe ndani au nje ya umoja huo.

Alisema ni kweli aliona wangeweza kupata ushindi kupitia Lowassa, lakini hata ushindi huo ungepatikana, wangeenda kusimamia mambo gani? Maana suala ni kusimamia katika eneo fulani.

Alifafanua kuwa suala lililopo katika siasa ni baada ya kuchaguliwa, uunde serikali ili usimamie misingi fulani ambayo itakidhi mahitaji ya wananchi.

“Sisi tulisema tunahitaji serikali inayowajibika, itakayopambana na rushwa, itakayotumia rasilimali za nchi vizuri, na itakayohakikisha mali ya asili ya Tanzania inawasaidia Watanzania wote,” alisema na kuongeza kuwa hayo Lowassa asingeweza.

Baada ya kikao hicho cha kumjadili Lowassa, Profesa Lipumba alisema walifanya kingine wakiwa na Mbowe (Freeman, Mwenyekiti wa Chadema); Mbatia (James, Mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi) na Lowassa kujadili suala hilo kwa mara ya pili kuwa ni vyema CUF, wakaribishwe kwanza ambapo walikuwa hatua za mwisho.

Alisema baada ya mchakato huo kwisha, Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif Sharif Hamad, alianza vikao vingine visivyomshirikisha yeye Lipumba, kwa kumwalika Mbowe ili wafanye mazungumzo.

Lipumba alidai kuwa Mbowe alipoitwa na Maalim Seif kwenda Zanzibar, alimfuata na kumweleza kuwa ameitwa na Makamu wa Rais wa Kwanza wa Zanzibar.

“Mbowe alinipigia simu akaniambia kuwa ameitwa kwenye kikao na kwamba ndio kulikuwa na hoja ya Lowassa kuingia Ukawa, wakati Chadema walikuwa na msimamo kuwa kwenye Ukawa asikaribishwe mtu wa nje,”alifafanua.

Alisema Mbowe aliendelea kumweleza kuwa, baada ya kikao kile ndipo Chadema waligundua kuwa kuna sintofahamu ndani ya CUF, jambo lililowafanya wao Chadema watoe hoja ya kuwa na mgombea wao, kwakuwa watakuwa na wabunge wengi basi hata Waziri Mkuu atatoka huko na CUF itatoa mgombea mwenza.

Lipumba alisema baada ya hali hiyo kutokea; ya Maalim Seif kufanya vikao vingine bila kumshirikisha, alikuwa katika wakati mgumu maana hata mazungumzo yale hakushirikishwa, ilihali yeye ndio Mwenyekiti wa CUF na yalikuwa yanafanywa na Katibu kimnya kimnya.

ACT-Wazalendo Wambipu Magufuli......Watangaza kufanya kongamano la kidemokrasia Septemba, 24

$
0
0
Chama cha ACT – Wazalendo kimetangaza azma yake ya kufanya mkutano mkuu wa kidemokrasia Jumamosi ijayo licha ya kuwapo kwa amri ya Polisi iliyokataza kufanyika kwa mikutano yote ya kisiasa nchini.

Jeshi la Polisi lilipiga marufuku maandamano na mikutano yote ya hadhara tangu Juni 7 hadi pale hali ya usalama itakapotengemaa.

Jeshi hilo lilisema limefikia hatua hiyo baada ya kupokea taarifa kutoka kwa vyama vya siasa vikitaka kufanya mikutano na maandamano kwa lengo la kuwahamasisha wananchi kutotii sheria za nchi.

Lakini jana, Katibu wa Itikadi, Mawasiliano na Uenezi wa ACT – Wazalendo, Ado Shaibu alisema wamepanga kufanya mkutano huo kwa sababu Katiba inawaruhusu.

“ACT kimekusudia kuitisha mkutano mkuu wa kidemokrasia, hii ni haki yetu kikatiba na hata kwa dunia nzima si ajabu kwa kuwa vyama vya siasa hufanya hivyo. Kongamano hili litawaleta pamoja wanachama, wadau na wafadhili wa ACT ambao watajadili hali ya maendeleo ya nchi,” alisema na kuongeza.

“Hatutaji mahali na ukumbi tutakaoufanyia kwa sasa, wakati ukifika tutawajulisha.Na hatutaomba kibali kwa kuwa katiba haisemi vyama vya siasa viombe  kibali vinapotaka kufanya mikutano ya ndani.”

Shaibu alisema kuwa endapo serikali itazuia kufanyika kongamano hilo watachukua hatua za kisheria kupinga maamuzi hayo kwa madai kuwa katiba ya nchi na ya vyama vya siasa inarushusu kufanyika.

“Serikali ilituzia kufanya mikutano na vikao vya ndani, tulikaa kimya awali tukiamini kuwa tutaishawishi kwa hoja na itajirekebisa lakini haikufanya hivyo.Tunaamini serikali itarudi nyuma na kuamini haina mamlaka ya kuzuia mikutano na vikao vya ndani kwa sababu kuizuia inamaana unafuta shughuli za siasa na sisi tutakuwa wa mwisho kukubali vyama kufutwa ,” alisema.

Alisema ACT haitokuwa nyuma kuiunga mkono serikali inapofanya vyema na kwamba endapo chama hicho kitakosoa utendaji kazi wake, serikali isikichukie kwa kuwa kinatekeleza wajibu wajibu wake.

Kwa upande mwingine, Shaibu alisema Kamati Kuu ya Uongozi wa Chama cha ACT imefanya baadhi ya marekebisho ya muundo wa uendeshaji kwa kuteua baadhi ya makatibu wa kamati za chama hicho.

“Kikao cha tatu cha kamati kuu kilichoketi Septemba 5,2016 kilifanya teuzi mbalimbali za makatibu, sambamba na kugawa baadhi ya kamati ikiwemo iliyokuwa kamati ya Ulinzi, Usalama na Uadilifu ambapo kwa sasa imegawanyika na kuwa kamati ya Usalama na Ulinzi na mpya ni Kamati ya Uadilifu, ” alisema.

Aliwataja makatibu wapya wa kamati walioteuliwa akiwemo aliyewahi kuwa Mwenyekiti wa Jumuiya ya Vijana Chama cha Wananchi CUF (JUVICUF) Mohamed Babu ambaye kwa sasa ni Katibu wa Kamati ya Ulinzi na Usalama, Ally Kifu ameteuliwa kuwa Katibu wa kamati ya Fedha na Miradi ya Kujitegemea. Katibu mwingine aliyeteuliwa ni Sabrah Mohamed ambaye ameshikilia Kitengo cha Kushughulikia Maendeleo ya Zanzibar.

Ruby: Namuonea hurama Diva, namwombea kwa Mungu amrudishie akili zake!

$
0
0
Baada ya mtangazaji wa Clouds FM, Diva kudai kwamba hamjui msanii wa muziki Ruby, Ruby ameendelea kutema cheche kuhusiana na kauli hiyo.

Muimbaji huyo ambaye ameachana na uongozi wake wa zamani wa THT, ameonyesha kuchukizwa na kauli hiyo ya Diva na kila akiulizwa kuhusu kauli hiyo amekuwa akitoa maneno makali.

“Kuhusu Diva, bora tu niachane naye maana sioni vitu vya kumuongelea kama anavyofanya yeye,” Ruby aliliambia gazeti la Mtanzania “Zaidi namuonea huruma tu, namsikitikia na ninamwombea kwa Mungu amrudishie akili zake. Nahisi ana ugonjwa wa kusahau, jambo ambalo ni baya sana kulingana na umri wake,”

Pia muimbaji huyo amesema kwa sasa amefunga ukurasa wa kuzungumzia masuala ya uongozi wake uliopita kuhu akidai kwa sasa ana nafasi ya kufanya vizuri zaidi kimuziki.

Jipatie Dawa Asili za Kutengeneza Shepu, Kuondoa Michirizi Chunusi, Kurefusha Nywele Toka Markson Beauty Products

$
0
0
HABARI NJEMA MARKSON BEAUTY PRODUCTS
Baada ya kupata cheti cha bidhaa bora kwa mwaka 2015-2016, Sasa kampuni hii inasambaza huduma zake ndani na nje ya nchi kwa vibali maalum. Bidhaa zetu zimetengenezwa kwa mimea na matunda na kudhibitishwa. Hazina kemikali wala madhara. DAWA ZETU NI YA:-

  1. kurefusha nywele na kuzuia kukatika ovyo @100,000/=
  2. Kuongeza shepu (hips na makalio) kwa/= (a)Dawa ya kunywa au kupaka @150,000/=(b)Vidonge @170,000/=
  3. Kuwa mweupe na softi mwili mzima kwa:- (1)Mafuta @100,000/= (11)Vidonge @150,000/=
  4. Kupunguza unene na manyama uzembe @120,000/=
  5. Kuongeza uume pamoja na nguvu za kiume kwa:-(a) Gely ya kupaka @100,000/= (b) Vidonge maalum @120,000/= (c) Handsome up original @170,000
  6. Kuondoa mvi milele zisiludi tena @100,000/=
  7. Kuongeza unene wa mwili mzima na uzito @120,000/=
  8. Kupunguza tumbo (kitambi) na nyama za pembeni kwa:- (a) Dawa ya kunywa au kupaka @120,000/= (b) Mkanda wa kawaida @100,000/= (c) micro-computer belt unaovaibret @200,000/=
  9. Kupunguza maziwa na kuyasimamisha @90,000/=
  10. Kushepu miguu na kuwa minene @100,000/=
  11. Kuondoa mipasuko mwilini (michirizi) @90,000/=
  12. kubana uke na kuongeza hamu ya tendo la ndoa kwa mwanamke @100,000/=
  13. Taiti za hips na makalio @150,000/=           
NB: Hakikisha unapata risiti yenye muhuri halisi wa MARKSON CO pamoja na garantii kwa bidhaa halisi. Wasiliana nasi :-(+255) 0767447444 na 0714335378 Google MARKSON BEAUTY.
Follow us
@Markson_beauty_pr
@Markson_beauty_pr

LULU Michael Atangaza Kuhitaji Kupata Mtoto....

$
0
0
Msanii mahiri wa filamu Bongo, Elizabeth ‘Lulu ‘ Michael amedai kuwa anahitaji mtoto kwa sasa.

Muigizaji huyo ameandika ujumbe kwenye mtandao wake wa Instagram akimuomba Mungu huku akidai kuwa yupo tayari kwa sasa na anahitaji mtoto.

“Okay…I’m ready noooow😫😫😫😫and I want a Baby Boy😭😭😫In Jesus Name🙏,” ameandika Lulu kwenye mtandao huo.

Kwa sasa muigizaji huyo yupo kwenye mahusiano na bosi wa EFM, Majay.

WCB Waonyesha Jinsi Walivyomalizana na Uongozi wa Saida Karoli ili Kurudia Wimbo wa Salome

$
0
0
Sallam kutoka WCB ameonyesha baadhi ya nyaraka ambazo zimewapitia kibali cha kutumia sehumu za wimbo ‘Maria Salome’ wa Saida Karoli katika wimbo mpya wa Diamond, ‘Salome’.


Wimbo ‘Maria Salole’ wa Saidi Karoli ni miongoni mwa nyimbo za asili zilizofanya vizuri miaka ya 2000.

Hali hiyo iliufanya uongozi wa Diamond kuzungumza na uongozi wa Saida Karoli ili upate kibali cha kutumia sehemu za nyimbo hiyo.

“Tunakushukuru sana uongozi wa Saida Karoli na mzee Felician Mutakyawa kutupa haki na baraka zote kutumia wimbo wa Maria Salome,” aliandika Sallam instagram. “Tunatambua kwamba nyimbo hii itaendelea kuwa moja ya nyimbo bora kuwahi kutoka katika nchi ya Tanzania,”

Diamond kupitia wimbo huu amerudi tena katika nyimbo za asili baada ya kufanya vizuri na wimbo ‘Mdogo Mdogo’ miaka miwili iliyopita.

Ndege moja kati ya mbili za ATCL Alizonunua Rais Magufuli Itatua Kesho Nchini

$
0
0
Ndege ya kwanza kati ya mbili zilizonunuliwa na Serikali za Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL), inatarajiwa kuingia  nchini kesho ikitokea Canada.

Taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari jijini Dar es Salaam jana na Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa ATCL, Patrick Itule alisema ndege hiyo aina ya Bombardier Q400 inatarajiwa kutua katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) saa 7:00 mchana.

Itule alisema ndege hiyo yenye uwezo wa kubeba abiria 76, tayari imeanza safari ya kuja nchini tangu mwishoni mwa wiki iliyopita ikipitia miji ya Reykjavík, Southampton, Malta, Luxor, Addis Ababa Ethiopia kabla ya kutua nchini ikiwa na timu ya marubani wanne kutoka Canada.

“Ndege ya pili inatarajiwa kukabidhiwa Septemba 22 na kuanza safari ya kuja Tanzania Septemba 23,’’ alibainisha.

Mwenyekiti wa UVCCM afikishwa mahakamani kwa kujifanya Afisa Usalama wa Taifa

$
0
0
Mahakama ya Hakimu mkazi Arusha imemsomea mashtaka mawili Mwenyekiti wa umoja wa vijana (UVCCM) Lengai Ole Sabaya ambaye pia ni diwani wa kata ya Sambasha Wilaya ya Arusha vijijini .

Miongoni mwa makosa hayo aliyosomewa mahakamani hapo kosa la kwanza alituhumiwa kujifanya Afisa mtumishi wa serekali (TISS)huku kosa la pili ikiwa kugushi moja ya nyaraka za serekali(kitambulisho ).

Akisoma mashtaka hayo mahakamani hapo Wakili wa serekali Lilian Mmasi alisema kuwa Mnamo May 18 katika hotel ya Skyway iliopo makao mapya jijini Arusha Mshitakiwa alijitambulisha kama Afisa utumishi wa idara ya usalama wa taifa na kufanya Utapeli .

Wakili Mmasi alitaja kosa la pili ambalo Mshitakiwa Lengai Ole Sabaya alisomewa kuwa ni kugushi kitambulisho cha idara ya usalama wa Taifa kilichokuwa kikisomeka jamuhuri ya muungano wa Tanzania idara ya usalama wa Taifa (TISS) Lengai Ole Sabaya kikosi maalumu Agent (undercover)chenye code no MT 86117 huku akitambua kuwa ni kinyume cha kisheria .

Hata hivyo mara baada ya kusomewa mashtaka hayo mahakamani hapo mtuhumiwa alikana mashtaka ndipo Hakimu Mkazi aliyekuwa akisikiliza kesi hiyo Gwantwa Mwamkuga Alisema dhamana ipo wazi iwapo wathamini watakithi vigezo vinavyotakiwa na mahakama hiyo.

Hata hivyo Mshitakiwa alipata dhamana baada ya kukithi vigezo vilivyowekwa na mahakama ambapo ilikuwa ni wadhamini wawili wenye sifa ambapo kwanza awe mtumishi wa serikali pili awe na mali isiyohamishika yenye thamani ya shilingi milioni tatu kwa kila mmoja.

Kesi imeaihishwa na hakimu mkazi hadi itakapotajwa tena October 5 ambapo uchunguzi unatarajiwa kukamilika na kesi hiyo kuanza kusikilizwa.

Mara baada ya kupata dhamana mahakamani hapo wakili wa mtuhumiwa Yoyo Asubui alisema kuwa mshtakiwa amesomewa mashtaka yote mawili na kukana mashtaka ambapo wanatarajia uchunguzi ukikamilika kesi itaanza kusikilizwa mapema na haki kutendeka ,huku akimtaka mteja wake kuendelea na majukumu ya mandeleo kwa wananchi wa kata ya Sambasha.

“kwakweli kesi hii sio ya kweli na naweza kusema ipo kisiasa na nashukuru jeshi la polisi kwa kunishikilia na kukaa na mimi vyema hadi kunileta mahakamani ambapo naamini haki itatendeka na ukweli utabainika “Alisema Sabaya mara baada ya kupata dhamana

Alisema kuwa hili limetokea mara baada ya kuwatoa wabadhilifu wa mali za umoja wa vijana (UVCCM) ambapo kwa muda mrefu wamekuw a mali za umoja huo kujinufaisha wenyewe na vijana kukosa maendeleo kupitia miradi ya umoja huo.

Tegeta Escrow: TANESCO Yashindwa Kesi Dhidi ya IPTL...Yaamriwa Kulipa Zaidi ya Sh. Bilioni 320

$
0
0
Shirika la umeme Tanzania (TANESCO) limeshindwa kwenye kesi yake IPTL -Independent Power Tanzania Limited.

Hukumu hiyo imefikiwa mwisho wa wiki iliyopita ambapo World Bank tribunal (international centre for settlement of investment disputes.

ICSID imeamuru TANESCO kuilipa Standard Chartered Bank Hong Kong (SCB HK) kiasi cha dola za kimarekani milioni 148.40 pamoja na tozo riba.

SCB HK ndio walionunua mkopo wa IPTL kutoka bank ya Malaysia Danaharta kwa gharama ya dola za kimarekani milioni 76.1

Kwa habari zaidi soma the Guardian la leo:

Mjengo wa Navy Kenzo Uliogharimu Tsh Milioni 700 kukamilika Disemba

$
0
0
Msanii wa Kundi la muziki la Navy Kenzo, Nahreel amesema ujenzi wa nyumba yao inayogharimu zaidi milioni 700 unatarajiwa kukamilika mwezi Disemba mwaka huu.

Akiongea na Bongo5 Jumamosi hii, Nahreel amesema anashangaa kuona watu hawaamini kama pesa zote za ujenzi wa nyumba hiyo zimepatikana kwenye muziki.

“Watu kuongea ni kawaida lakini mwisho wa siku sisi tunajua pesa zote zimepatikana kwenye muziki, karibu asilimia 97 ni muziki, kwa hiyo hivyo ni vitu vya kawaisa,” alisema Nahreel. “Na Mungu akipenda Disemba mjengo utakuwa umekamilika na kila kitu kinaenda sawa mpaka sasa,”

Pia Nahreel amewataka mashabiki wa muziki wao kukaa mkao wa kula kwa ajili ya video mpya ambayo tayari wameshoot Afrika Kusini.

Ndege Mpya Ziwe Mali ya Serikali, ATCL Wakodishwe tu..Wakishindwa Kazi Wanyang'anywe

$
0
0
Ili kuhakikisha hizi ndege zinakuwa katika hali bora na kutumika ipasavyo nashauri hizi ndege ziwe mali ya serikali, ATCL wakodishwe na wakishindwa kulipia wanyang'anywe. Hii pia itasaidia mashirika mengine kuzikodi na kuongeza ufanisi wa shughuli zao. Tukifanya hivyo hata fastjet badala ya kuleta ndege zingine wanaweza kodi hizihizi, hivyohivyo kwa Precision air. pia tunaweza zikodisha hata mashirika ya nje na mashirika ya umoja wa mataifa.

Pili, hii itasaidia hizi ndege kutokuzongwa na madeni ya nyuma ya ATCL na kutumika kwa fedha kinyume ma matarajio, pia hii itasaidia ATCL kumia vizuri faida wanayopata baada ya kutoa gharama za ukodishaji.

Mwanamke Subiri Uvuliwe, Usivue Mwenyewe

$
0
0
Kuna tabia fulani kwa baadhi ya wanawake mnapokua faragha kukimbilia kuvua nguo, badala ya kusubiri kuvuliwa na mpenzi wake.

Jamani zile steps za kuvuana nguo zina raha yake na msisimko wa pekee, especially kutoa jeki, kufuli na boxer.

Nashangaa mtu mko ndani dakika nyingi mtu amevua nguo amevaa taulo.

Ikishindikana basi baki ata na kufuli kushusha kufuli ishara ya ushindi hasa inapofika kwenye magoti na visigino.

RAIS Dkt. Magufuli Amjulia Hali Spika Mstaafu Samuel Sitta Pia Atembelea Kwa Kushtukiza Ofisi Za Magazeti Ya Uhuru Na Mzalendo Jijini Dar Es Salaam

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Dkt. John Pombe Magufuli, leo tarehe 19 Septemba, 2016 amefanya ziara ya kushitukiza katika Ofisi za Gazeti la Uhuru zilizopo Mtaa wa Lumumba Jijini Dar es Salaam na kuzungumza na wafanyakazi.

Katika Mazungumzo hayo, wafanyakazi wa Gazeti la Uhuru linalomilikiwa na CCM wamelalamikia kutolipwa mishahara yao kwa miezi saba, kutotolewa kwa michango ya wafanyakazi kwa Shirika la Hifadhi ya Jamii (NSSF), kuuzwa kwa mtambo wa kuchapisha magazeti katika hali ya kutatanisha, kutotambuliwa katika ajira kwa baadhi ya wafanyakazi, kutolipwa kwa madeni wanayozidai taasisi za Serikali na wanaostaafu kutolipwa mafao yao.

Wafanyakazi hao pia wamemueleza Dkt. Magufuli kuwa Bodi na Menejimenti ya kampuni ya vyombo vya habari vya chama inayoendesha Gazeti la Uhuru na Redio Uhuru zimeshindwa kuendesha vyombo hivyo na wamemuomba aingilie kati ili kuvinusuru vyombo hivyo ambavyo kwa sasa vina hali mbaya kutokana na kukabiliwa na madeni makubwa, na biashara yake imeshuka kwa kiasi kikubwa.

Akijibu malalamiko hayo Rais Magufuli aliyetembelea ofisi za Gazeti la Uhuru akitokea Ofisini kwake katika jengo la Makao Makuu ya chama, Ofisi Ndogo ya Lumumba Jijini Dar es Salaam amemuagiza Katibu Mkuu wa CCM Ndg. Abdulrahaman Kinana kuhakikisha mishahara yote wanayodai wafanyakazi inayofikia Shilingi Milioni 609 inalipwa ndani ya Mwezi huu wa Tisa, ameagiza kupatiwa orodha ya taasisi za Serikali zinazodaiwa na Magazeti ya Uhuru na Mzalendo, na pia ameagiza deni linalodaiwa na NSSF kutokana na kutowasilishwa kwa makato ya wafanyakazi lilipwe.

Kuhusu malalamiko dhidi ya Bodi na Menejimenti ya Kampuni hiyo, ajira za wafanyakazi, mafao kwa wastaafu, kuuzwa kwa mtambo wa kuchapisha magazeti na mazingira magumu ya kazi Dkt. Magufuli ameahidi kuyafanyia kazi.

Aidha, Dkt. Magufuli amewapongeza wafanyakazi wa Gazeti la Uhuru kwa kazi kubwa na nzuri wanayoifanya licha ya kukabiliwa na changamoto kubwa na amewakikishia kuwa anatambua umuhimu wao na kwamba atahakikishia anaboresha hali ya chombo hicho muhimu.

Wakati huo huo, Rais Magufuli amemjulia hali Spika Mstaafu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samwel Sitta ambaye anaendelea kupata matibabu Jijini Dar es Salaam na hali yake inaendelea vizuri.

Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar es Salaam

19 Septemba, 2016

ZITTO Amshauri Haya Rais Magufuli Baada ya Tanesco Kushindwa Kesi ya IPTL na Kuamriwa Kulipa Sh320 Bilioni

$
0
0
Shirika la umeme Tanzania, Tanzania limeshindwa kesi yake dhidi ya IPTL na kuamriwa kulipa dola milioni 148.4 ambazo ni zaidi ya shilingi bilioni 320 za Kitanzania.

Hukumu hiyo imetolewa na mahakama ya inayoshughulika na migogoro ya uwezekaji, ICSID yenye makao yake mjini Washington DC, Marekani na ipo chini ya benki ya dunia.

Tanesco ilikuwa ikiwakilishwa na makampuni mawili ya wawanasheria R.K. Rweyongeza & Co. Advocates na Crax Law Partners ya Tanzania, pamoja na lile la Zurich, Kellerhals Carrard.

Pesa hizo zinatakiwa kulipwa kwa Standard Chartered Bank-Hong Kong (SCB-HK).
SCB-HK ililinunua deni la IPTL kwa punguzo la bei ya milioni 76.1 kutoka Danaharta Bankin ya Malaysia, August 2005 baada ya Danaharta kushindwa kuchukua mkopo wake kutoka kwa IPTL.

Hiyo ina maana kuwa SCB-HK imepata faida ya dola milioni 172. IPTL ilikopa dola milioni 100 mwaka 1998 kutoka kwenye kundi la benki za Malaysia ili kujenga mtambo umeme Tegeta wenye megawatt 100.

TANESCO ilifungua kesi ICSID baada ya kubaini kuwa imekuwa ikitozwa zaidi na IPTL. Kesi hiyo inahusiana na ripoti ya uchunguzi wa kashfa ya IPTL iliyohusisha uchotwaji wa shilingi bilioni 306 za kitanzania.

Novemba mwaka jana, mwenyekiti wa kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali wakati huo, Zitto Kabwe alisoma ripoti na kulithibitishia Bunge hilo kwamba viongozi na wafanyakazi wa serikali, wafanyabiashara, viongozi na taasisi za dini, mabenki na watu binafsi wanahusika kufanya katika ufisadifu.

Kufuatia Tanesco kushindwa kwenye kesi hiyo, Zitto amemtaka Rais John Magufuli kuchukua hatua.

“Kwanini Rais Magufuli hafanyii kazi suala la IPTL? Matapeli hawa wataendelea kuipa hasara nchi yetu mpaka lini? Sasa mahakama ya ICSID imeamua kuwa Benki ya Standard Chartered ilipwe tshs 300bn na riba. TANESCO wanaingia Hasara hii Kwa sababu ya wizi wa Fedha za TEGETA Escrow na Rais bado anavuta miguu kuchukua hatua dhidi ya suala hili. Nini kimemkuta Rais Magufuli? Rais anataka tuamini kuwa IPTL/PAP Ni kweli waligharamia Mkutano Mkuu wa CCM uliompa yeye Uenyekiti,” ameandika Facebook.

“Tanzania hapo Ni hasara tupu 1)mmelipa matapeli Fedha zilizokuwa kwenye TEGETA escrow account. 2) mmewapa mtambo wa kuzalisha umeme matapeli hao na mnaendelea kuwalipa capacity charges mpaka sasa. 3) mnawalipa standard chartered Fedha zao Kwa mtambo ambao sio wenu na Kwa Fedha ambazo mngezitoa escrow a/c lakini sasa mtazitoa hazina,” ameongeza.

“Rais achukue hatua zifuatazo – awafikishe mahakamani watu wote waliohusika na kuitia Nchi hasara katika sakata la TEGETA Escrow – aitwae mitambo ya IPTL kisheria na kuimilikisha Kwa TANESCO – amkamate Bwana Harbinder Singh Seth na wafuasi wake wote na kuwafikisha mahakamani Kwa makosa ya utapeli, wizi, uhujumu uchumi, utakatishaji wa Fedha.”

“Benki iliyotumika kupitisha Fedha za TEGETA escrow ndio ilipe Hilo deni tunalotakiwa kulipa. Rais aamue kusimama na watanzania au kusimama na matapeli wa TEGETA escrow.”
Viewing all 104706 articles
Browse latest View live




Latest Images