Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104785 articles
Browse latest View live

ATCL Kuanza na Kosa la Kwanza

$
0
0


ATCL kama yalivyo mashirika mengine ya umma, kila mara imekuwa ikizaliwa na kufa kutokana na muundo wake usiokuwa wa kibiashara. TANESCO isiyo na mshindani yeyote, TTCL ambayo awali haikuwa na mshindani, na mengine mengi yaliyokwishakufa na yaliyouzwa, mashirika yote hayo yalikufa kwa sababu yalianzishwa, kuendeshwa na kusimamiwa kiserikali/kisiasa.

Serikali haijawahi kuendesha biashara ikafanikiwa. Tatizo linaanzia kwenye muundo wa haya mashirika/makampuni. Wanasiasa/viongozi wa serikali ambao kimsingi si wafanyabiashara ndiyo waliotengeneza muundo wa uendeshaji na ndiyo wenye kauli ya mwisho. Vigezo vya wajumbe wa bodi na watendaji wakuu wanavyo wao. Na siku hizi PhD imekuwa ni kigezo kikubwa sana ingawa kiuhalisia, kwa Dunia nzima, ni nadra sana kuwaona wenye PhD wakiwa wafanyabiashara wazuri na waliofanikiwa.

Juzi wakati Mh. Rais akizindua ujio wa ndege mpya alisema ATCL imezaliwa upya, ina ndege mpya, bodi mpya na uongozi mpya, sikusikia kama ina muundo mpya wa uendeshaji na usimamizi. Bado inaonekana ATCL itandeshwa kwa mkono wa serikali.

RAIS - 'ATCL ISITUMIE MAWAKALA WA KUKATISHA TIKETI'

Hili tayari ni agizo ambalo naamini ni agizo lisilo sahihi. Tayari serikali imeanza toka hatua za mwanzo kuingilia uendeshaji wa ATCL. Rais anapoagiza ATCL isitumie mawakala wa kukatisha tiketi inamaanisha ATCL iwe na wafanyakazi waajiriwa kila mahali nchini. Gharama za maelekezo hayo itakuwa kama ifuatavyo:
ATCL italazimika kuwalipa wakatisha tiketi mishahara, matibabu, posho, michango kwenye mifuko ya hifadhi ya jamii, usafiri, n.k. ATCL italazimika kulipia gharama hizo zote bila ya kujali mkatisha tiketi anakatisha tiketi ngapi au kama amepata wateja au hakupata kabisa
ATCL italazimika kulipia ofisi na kuweka miundombinu ya ukatishaji ticket nchi nzima. Ifahamike kuwa ukitaka kuwa na ufanisi unalazimika kuwa na ofisi za ukatishaji tiketi hata mahali ambapo ndege haitui, kwaajili ya kuhudumia abiria wanaotoka maeneo hayo wanaotarajia kutumia usafiri wa ATCL kutokea uwanja ulio karibu
ATCL italazimika kuwapa mafunzo wakatisha ticket watakaotapakaa nchi nzima
Wakati ATCL watakapokuwa wanahangaika na kuwa na wakatisha ticket wao na ofisi zao, washindani wao wataendelea kuwa na wafanyakazi wachache, wakiwa na mawakala wengi wanaolipwa kutokana na idadi ya ticket na thamani ya ticket walizokatisha. Hawalipii ofisi, hawalipii matibabu, hawalipii michango ya hifadhi ya jamii, hawalipii likizo ya mfanyakazi. Mawakala wao wanalipwa kutokana na wanachozalisha, wasipozalisha hawalipwi chochote.

ATCL wanaanza na quandary ya kwanza, wafuate maagizo ya mwenye mali au kanuni za biashara? Je, hii ni ya mwanzo na ya mwisho au zitaendelea kuja na nyingine? Kwa kuwa tatizo la msingi la uendeshaji biashara zilizo chini ya serikali halijatatuliwa, haitakuwa jambo la ajabu ATCL kufuata projectile ya mashirika/makampuni ya umma.

By Msambichaka Mkinga

Chadema kutoa msimamo wa Oparesheni UKUTA Leo

$
0
0
Mwezi mmoja baada ya Chadema kusitisha Operesheni Ukuta kupinga inachokiita ukiukwaji wa haki za binadamu na ukandamizaji wa demokrasia, leo inatarajia kutoa mwelekeo wa mkakati huo.

Operesheni hiyo ilipangwa kuzinduliwa Septemba mosi nchini kwa maandamano na mikutano ya hadhara kama maazimio ya Kamati Kuu ya Chadema, baada ya chama hicho kukumbwa na vikwazo kadhaa kuendesha shughuli zake, ikiwa ni pamoja na kuzuiwa kufanya mikutano ya hadhara.

Siku moja kabla ya kufanyika kwa operesheni hiyo, Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe alitangaza kuisitisha kwa mwezi hadi kesho, ili kutoa fursa kwa viongozi wa dini kusemezana na Rais John Magufuli na Serikali yake.

Jana, Mwanasheria Mkuu wa Chadema, Tundu Lissu alisema: “Kuhusu Ukuta, kesho (leo) tutatoa msimamo wetu juu ya kitu tutakachofanya.”

Alisema operesheni hiyo ilisitishwa kutokana na sababu za msingi zilizoelezwa, hivyo kauli ya chama hicho leo itafafanua kwa kina kuhusu mambo yote yaliyojitokeza katika kipindi hicho cha mwezi.

Wakati viongozi hao wakieleza hayo, hadi jana hakukuwa na taarifa zozote za kufanyika kwa kikao kati ya viongozi wa dini na Serikali.

Viongozi hao waliitaka Serikali na Chadema kufikiria amani ya nchi na kutafuta njia mwafaka za kumaliza msuguano wa kisiasa hasa baada ya chama hicho kushikilia msimamo wake wa kufanya mikutano na maandamano.

Wakati Chadema wakijipanga kutoa tamko lao, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda jana alisisitiza kuwa Oktoba mosi ni Siku ya Kupanda Miti jijini humo ambapo viongozi mbalimbali watahudhuria.

Wasanii 10 Waliobuma Pamoja na Kutoa Nyimbo Kali Mwaka Huu

$
0
0
Mara baada ya team za pande mbili kuendelea kushamiri katika mitandaoni hali hii imewanyima nafasi wasanii wengine wa bongo kufanya vizuri nyimbo 10 ambazo zimeshidwa kufanya vizuri 2016 ni hizi

1. Kassim Mganga _Manuari
Pamoja na kutoa nyimbo nzuri yenye mahadhi ya pwani kama kawaida yake lakini nyimbo imeshindwa kufanya vizur kama ilivotegemewa ina miezi kadhaa lakini hakuna kitu

2. Mo _music_ Ado ado
Msanii aliyekuja kwa kishindo kwenye sanaa baada ya kutoa basi nenda ilikuwa kama wimbo wa taifa sasa amekuja na ya ado adi watu kama hawana habar nayo hata baada ya kufanya kichupa kikali

3. Lady Jay Dee_Sawa na wao
Baada ya kutoa ndi ndi ndi ilifanya vizuri akaachia nyimbo mpya
ni nyimbo iliyobuma kabisa

4. Chid Benz ft Raymond _Chuma
Baada ya chid benz kutoka sober alitoa nyimbo aliyemshirikisha kijana wa diamond lakini haijapata mapokezi makubwa

5. Linah Sanga_Raha Jipe Mwenyewe
Nayo ni miongoni mwa nyimbo ambazo azijafanya vizuri wala kusikika

6. Young killer ft mr blue 
Msanii young kila alikuja moto sana wakati anakuja ila amejikuta anawakati mgumu baada ya hizi siku zakalibuni kutoa nyimbo mbili zote zimebuma kwa kuendelea kutumia style zile zile

7. Banana Zolo ft Peter Msechu_Mama 
Hii ni nyimbo ya mama iliyobuma pamoja ujumbe uliopo ndani awali kipindi cha nyuma banana alishatoa nyimbo ya mama ilishafanya vizur mama zingine zilizofanya vizur ni ya bela na yamoto

8. Kala Jelemaya _ Wanandoto
Pamoja na ujumbe ulioimbwa ila watu wameuupuuza sababu pia nyimbo imewaendea walengwa pekeyao

9. Ommy Dimpoz_Hawapendagi
Nayo mashabiki hawajaielewa imebuma mazima

10.Baraka da prince ft alikiba _ Nisamee Unaionaje?

Wema Sepetu:Timu Wema Wameniganda Kama Ruba..Japo Niliwadiss

$
0
0
Wemasepetu
I never wanted a party this Year.... Cuz ni yale yale tu kila mwaka... So i said to myself sitofanya party mwaka huu na hata mwakani.... But Inshaaaaallllaaaaah panapo majaaliwa tuombeane uhai na uzima 2018 Tunafanya bonge la party maana ndo ntakuwa nagonga 30... But mumumu wangu akasema siku isiende hivi hivi so akaniandalia Dua and chakula cha jioni... Majirani zangu nd all my childhood friends bila kuwasahau Team Wema Damu walikuwepo.... Aisee hawa watu ni Ruba

Makahaba Arusha Wamiminika Kujifunza Kiingereza Kuvutia Wateja wa Kigeni

$
0
0
Wasichana wanaojiuza jijini Arusha, wanalazimika kutafuta madarasa ya kujifunza kimombo kwakuwa ni lulu katika maisha ya kazi yao hiyo. Ni kwasababu wale wanaojua Kiingereza hupata wateja wa kigeni ambao hutoa dau kubwa zaidi kwa huduma wanayopewa kuliko wateja wa nyumbani.

Mwandishi wa BBC Swahili, Humphrey Mgonja alisafiri hadi Arusha na kushuhudia jinsi biashara hiyo inavyokwenda kwenye mji huo wa kitalii. Alizungumza na msichana anayefanya kazi hiyo aitwaye Warda aliyekiri kuwa Kiingereza kina umuhimu mkubwa kwenye biashara yake.

“Sometimes nakutana na wateja ambao hawajui Kiswahili kabisa, unakuta anakuwa ananiongelesha, nasikia lakini nashindwa jinsi ya kumjibu. Kwahiyo nakuwa nakosa hela,” anasema Warda.

“Sehemu kama Dar es Salaam niliona sehemu moja kwa Macheni, niliona kuna mademu waliokuwa wanajua Kiingereza walikuwa wanatoka na wazungu. Mimi sometimes wazungu walikuwa wananipenda lakini kwa colour yangu the way nilivyo lakini tulikuwa tunashindwa yaani ni lugha gongana. Kwahiyo unajikuta mwisho wa siku unapewa dola 100 wakati nilikuwa nipewe 200,” aliongeza.

Warda alikiri kuwahi kuikosa bahati ya mtende ya kuchukuliwa na ‘bwana wa kizungu’ aliyetaka aondoke naye kwenda ng’ambo lakini lugha ilimponza. Anadai kuwa mzungu huyo alikuwa anamtumia mkarimani kuwasiliana naye na ambaye mara nyingi alimfikishia ujumbe tofauti na Warda aliotaka ufike.

“Nilikuwa namsikia anamuambia kabisa yule kijana, ‘mimi niko tayari kumtengenezea passport, watoto wake nitawapangia nyumba kila kitu, namtangulia yeye halafu baadaye atawachukua watoto wake.’ Lakini akifika kwangu mimi anabadilisha maongezi, au mimi nikimtuma anaenda kumwambia vitu tofauti. Kiukweli nilimkosa halafu alikuwa baba mtu mzima anajielewa, anajiheshimu,” Warda alisema kwa uchungu.

“Iliniuma sana, nadhani mpaka sasa hivi nisingekuwa kwenye hii biashara.”

Kituo kimoja kinachofundisha Kiingereza jijini humo kimekiri kuwa na wateja wengi wa kike na kwamba dalili za kuwa na wanawake wanaofanya biashara hiyo kituoni hapo ni kubwa.

Alichofanya Mfakanyazi wa Shirika la Ndege la Ethiopia Alipookota Bahasha Yenye Milioni 21.8

$
0
0
Shirika le Ndege la Kimataifa la nchini Ethiopia limempongeza hadharani mmoja wa wafanyakazi wake kwa kurejesha fedha kiasi cha dola elfu 10 (sawa ni shilingi milioni 21.8) zilizokuwa zimesahauliwa na mmoja wa abiria aliyekuwa kwenye ndege.

Shirika la ndege la Ethiopia lilichapisha pongezi hizo kwenye ukurasa wake wa Facebook na kumpongeza mfanyakazi wa ndege hiyo Roza Shiferaw kwa kurudisha dola elfu 10 zilizokuwa ndani ya bahasha mali ya mmoja wa abiria.

Shirika hilo liliongezea kuwa kitendo alichokifanya Roza ni ushahidi tosha kuwa shirika hilo lina wafanyakazi wenye maadili na heshima kwa wateja wao.

Uongozi wa shirika hilo haukueleza zaidi kuwa abiria aliyesahau fedha hizo ni nani na mfanyakazi huyo alizikuta wapi.

UKUTA Ndio Basi Tena "UMEBUMA"...Chadema Watangaza Kuairisha Tena Maandamano ya Oparesheni UKUTA

$
0
0
Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Taifa, Freeman Mbowe ametangaza kuwa Operesheni UKUTA iliyokuwa ifanyike Oktoba Mosi haitofanyika tena.

Mbowe amesema hayo leo baada ya kimya cha muda mrefu tangu kuahirishwa kwa maandamano Septemba Mosi. Aidha, Mbowe amesema kuwa hawatataja tarehe ya kufanya maandamano ili kutompa adui nafasi ya kujipanga. Amesisitiza kuwa maandamano yapo, ila tarehe hawataweka hadharani.

Operesheni hii ilikuwa ifanyike Septemba Mosi mwaka huu lakini iliahirishwa ili kuwapa nafasi viongozi wa dini kuweza kukutana na kujadiliana na Rais Dkt Magufuli juu ya mustakabali wa hali ya kisiasa nchini kufuatia kuzuiwa kwa shughuli mbalimbali za kisiasa.

Hadi leo viongozi wa dini bado hawajakutana na Rais Magufuli licha ya wao kueleza kuwa Rais Magufuli hajakataa kukutana nao kama inavyoelezwa na baadhi ya vyombo vya habari

Wema Sepetu Amkataa Idriss Sultan Mchana Kweupeee Pee!

$
0
0
Wema amkataa Idriss Mchana kweupeee pee!!!!!
Ashasema hataki kuwa nae sasa nyie endeleeni kupost ohh shem shem sijui kamuoa dada yenu au???? Watabaki kuwa marafiki kama zamani tuuuu...wema so wamchezo mchezooo...
unalakusema hapo mdau ???Habari ndo hiyooo... Tukutane katika uwanja wa comments. ..

Soma Alichoandika Mtandaoni:



Diamond Ataja Bei ya Kuuza Page yake ya Instagram Yenye Followers Milion 2

$
0
0
AKIONGEA KUPITIA KITUO CHA TELEVISION CHA CLOUDS TV KUPITIA KIPINDI CHA SHILAWADU ,ALIULIZWA SWALI KUHUSU GHARAMA YA PAGE YAKE KAMA AKITAKA KUIUZA..BILA KUTAFUNA MANENO DIAMOND ALISEMA PAGE YAKE ANAWEZA KUUZA KWA BEI YA DOLA MILIONI 2 SAWA NA TSH BILIONI 4 ZA KITANZANIA.

Billnas Aungana na Nuh Mziwanda Kumvaa Petit Man

$
0
0
Mwanzilishi wa kundi la LFLG rapa Billnas ameunga mkono tuhuma za Nuh Mziwanda kwa kumshukia meneja wao Petit Man juu ya uongozi mbaya na upigaji wa hela kupitia mgongo wao.

Billnas akipiga story za eNewz na kusema kuwa matatizo ni kweli yametokea lakini akamshauri Nuh Mziwanda ni vyema kwa sasa wakatafuta namna ya kumaliza mzozo huo.
"Petit ni mmoja kati ya watu wa LFLG, So kama mmoja wetu ana matatizo then wengine wanaweza kutumika kusuluhisha, au vinginevyo anaweza kupunguzwa ili wengine waendelee vizuri na kazi" aliongeza Billnas.
Hapo awali mzozo kati ya Petit Man na wasanii anaowasimamia yaani Nuh Mziwanda na Billnas ulianza kusikika baada ya Nuh Mziwanda kujitoa chini ya usimamizi wa Petii Man kwa madai kuwa ni "mpigaji" na kwamba hutumia majina yao vibaya kupata pesa na pia si meneja anayewajali wasanii wake.

Bob Junior AmchanaJose Chameleone Kuhusu Video yao

$
0
0
Producer na muimbaji tokea Sharobaro Records, Bob Junior amemchana mkali tokea pande za Uganda, Jose Chameleone baaa ya kufanya wimbo pamoja ambao video yake haijatoka, wimbo unaofahamika kwa jina la "Siachani Naye" mwanzoni mwa mwaka huu.

Bob Junior alidai kuwa alikuwa na nia ya kufanya video ya wimbo huo lakini kila alipokuwa anapanga ratiba za ku'shoot, Chameleone
alikuwa akikwepa.

Akipiga story na eNewz Bob Junior alisema "Tukipanga siku ya ku'shoot, ikifika siku hiyo nikimtafuta basi hajibu meseji zangu, sasa mimi nitafanyaje? Hata hivyo sitaki kusema mengi kwa ubaya, labda kuna vitu kweli vinamzuia".

Hata hivyo Bob Junior alisema baada ya kushindwa kufanikisha kufanya video hiyo, sasa anajipanga kwa kazi nyingine, huku akisema anatarajia kuachia wimbo alioshirikiana na Q Chief na Baraka da Prince, wimbo unaoitwa "Kidege" na kama si wimbo huo basi ataachia mwengine unaoitwa "Mpasuo"

NO Bifu...Diamond Amuombea Kura Alikiba Kwenye Tuzo za MTV EMA 2016

$
0
0
Kuna uwezekano mkubwa kukawa hakuna bifu kati ya Alikiba na Diamond lakini wapo wachache wanaokuza hilo jambo kwa maslahi yao binafsi. Diamond ameonekana kulipa fadhila kwa Alikiba baada ya kumuombea mashabiki wampigie kura kwenye tuzo ya MTV EMA 2016 akiwa msanii pekee kutoka Afrika Mashariki anayewania tuzo hiyo.

Kiba atachuana na wasanii wengine wakiwemo Wizkid na Olamide wa Nigeria na Black Coffee na Cassper Nyovest wa Afrika Kusini huku mshindi katika hatua ya kwanza ataendelea kwenda kuwania kipengele cha Worldwide Act: Africa/India ambacho mwaka jana alishinda Diamond Platnumz.

Akiongea kwenye kipindi cha D’Wikend Chatshow cha Clouds TV, hitmaker huyo wa Salome amesema, “Nimesikia Alikiba amechaguliwa kwenye tuzo za MTV EMA. Tufute zile zama za kusema kwasababu wewe unam-support Diamond ndio huwezi kumpigia kura Alikiba. Akikosa tuzo hiyo haiji kabisa Tanzania na itaonekana watanzania wote tumeikosa. Kwahiyo tuhakikishe tuna VOTE ili tuirudishe tuzo hiyo nyumbani.”

Alikiba aliwahi kusema kama hivyo mwezi Juni, mwaka huu kwenye kipindi cha Planet Bongo cha East Africa Radio alipowataka mashabiki wampigie kura Diamond kwenye tuzo za BET

Diamond Awajibu Wabaya Wake Kwa Njia Hii

$
0
0
Ijumaa hii Diamond Platnumz ameachia verse ya pili ya remix ya wimbo wa ‘All the way up’ wa Fat Joe & Remy Ma huku akioekana kuwa jibu wanaomfuatilia kwenye anga zake huku pia mashairi hayo yakidaiwa kuwalenga baadhi ya wasanii wenzake kwenye mistari hiyo.

Hivi karibuni mwimbaji huyo alidaiwa kuwa anatoka na model wa kwenye video yake mpya ya Salome, Hamisa Mobetto kitu ambacho muimbaji huyo hajawahi kukiongelea lakini kupitia wimbo huo amepigilia msumari kwenye mifupa ya wabaya wake. “Mara nakula Hamisa Mobetto, eti Sepenga kaja magheto, ilimradi Zari apate mchecheto, Tale waambie waache unambinambi hata nikila wote dini yangu sio zambi,” amerap Diamond kwenye wimbo huo.

Mstari mwingine unaodaiwa kuleta utata ni ule unaosema, “Siachi pengo hadi waombe poo, wao wakipost tembo si tunapost show.” Sikiliza wimbo huo hapa chini.

Chadema yamtangazia vita Profesa Lipumba

$
0
0
Wakati  Mwenyekiti wa CUF aliyefutiwa uanachama, Profesa Ibrahim Lipumba akitangaza masharti kwa Katibu Mkuu Maalim Seif Sharif Hamad ya kuingia kwenye ofisi za chama hicho Buguruni, Dar es Salaam Chadema imetangaza kutoshirikiana naye.

Akizungumza kwenye makao makuu ya Chadema jana, Mwenyekiti wa chama hicho, Freeman Mbowe aliwataka viongozi wa chama chake, kutotoa ushirikiano kwa Profesa Lipumba, badala yake wampuuze na wamwone kuwa msaliti wa harakati za kudai haki.

Wakati akisema hayo, Profesa Lipumba akiwa katika Ofisi Kuu za CUF, alitoa masharti kwa Seif kama anataka kufika ofisini hapo, kuwa lazima akiri kumtambua na kumkubali kuwa Mwenyekiti halali wa chama hicho.

Mbowe katika mkutano wake na waandishi wa habari, alisema Lipumba, Msajili wa Vyama vya Siasa na taasisi ya utafiti ya Twaweza, ni mawakala wa Serikali wa kuzia harakati za kupigania demokrasia nchini.

Alisema harakati za kuzuia wapinzani kupigania haki, hazifanywi moja kwa moja na Serikali, bali na wakala wao ambao wanakuja kwa sampuli mbalimbali.

“Kamati Maalumu ya Kamati Kuu inatambua mgogoro ndani ya CUF, hivyo chama chetu hakimtambui Profesa Lipumba kama Mwenyekiti wa CUF wala Mwenyekiti Mwenza wa Ukawa.

“Kamati inalaani uamuzi wa Jaji Francis Mutungi wa kuivuruga CUF kwa kujaribu kumrudisha madarakani Lipumba ambaye alijiuzulu katika mazingira yanayoashiria kununuliwa na CCM, kwa lengo la kusaliti Ukawa kwenye uchaguzi mkuu wa mwaka jana,” alituhumu.

Kuhusu Jaji Mutungi, Mbowe alimtangaza kama adui wa demokrasia na vyama vingi na kudai kuwa pamoja na kuwa Jaji, hana weledi wa kusimamia vyama vya siasa.

Alitumia nafasi hiyo kubainisha kuwa chama hicho hakina sababu hata moja ya kumheshimu mtu kama Jaji Mutungi ambaye alisema anaonekana kutumika na CCM.

“Mtu ambaye tunamwona msomi, ambaye hapewi mamlaka yoyote ya kisheria ya kuamua ndani ya vyama vya siasa, badala ya kusaidia vyama kumaliza migogoro, amekuwa akichangia migogoro.

“Anaona vyama vinaminywa na Serikali anakaa kimya, lakini kila akizungumza anavikandamiza zaidi, huyu mtu ni adui mkubwa sana,” alisema.

Alimhakikishia Jaji Mutungi kuwa mbinu zake za kudhoofisha vyama vya upinzani hazitafanikiwa, kwani hakuwa Msajili wa kwanza, na kwamba matendo hayo hayatafifisha vyama hivyo.

Kuhusu Twaweza, alidai kuwa imekuwa ikilipwa na Serikali itangaze mambo mbalimbali siku moja kabla ya Ukuta kwa kutoa takwimu alizoziita za kipumbavu na kwamba wamekubali kujitwisha uendawazimu.

“Hawa ni mawakala wa Serikali na wanajulikana. Ni Mtanzania mwendawazimu pekee ambaye utamwambia kwamba hali ya nchi, Serikali inakubalika kwa asilimia 96, lazima uwe mwendawazimu na utafiti huo hauwezi kulisaidia Taifa,” alisema.

Wakati Chadema ikitoa kauli hiyo, hali ya kisiasa ndani ya CUF ilizidi kuwa mbaya kutokana na pande mbili zinazosigana kutunishiana misuli.

Akijibu maswali ya waandishi wa habari waliofika Ofisi Kuu zaCUF jana, Profesa Lipumba alisema alipata taarifa kwamba Maalim Seif angefika ofisini hapo juzi, hivyo alimsubiri ampangie kazi.

Alisema kama Seif angefika, kabla ya kufanya kazi na Mwenyekiti jambo la kwanza ingekuwa ni kumtambua kwa nafasi hiyo ambayo alivuliwa na kikao kisicho halali.

“Ni lazima akija hapa afanye kazi na Mwenyekiti na walinzi wetu wanamfahamu, wasingemfanya chochote kwa kuwa ni kiongozi wao pia,” alisema na kuongeza:

‘’Huwezi kuja ofisi za chama, halafu ukasema humtambui Mwenyekiti, analijua hilo kwamba akija hapa ni lazima afanye hivyo, kwani anajua kikao kilichokaa Zanzibar ni cha ujanjaujanja.’’

Profesa Lipumba alisema ndiye kiongozi wa walinzi wote wa chama, hivyo wana haki ya kumlinda wanavyotaka wao kwa maslahi ya chama.

Alisema Maalim Seif anatakiwa kujiamini na kufika kwenye ofisi hiyo ili afanye kazi na Mwenyekiti wake za kujenga chama na hakuna kikundi kilichokuwa kimeandaliwa kufanya vurugu au kugombana na kiongozi huyo.

“Anaweza akaja lakini hawezi kusema kuwa kuna kikundi, hawa ni walinzi wanaomlinda tangu anagombea nafasi hiyo mwaka 2014, hatuna kikundi ni Blue Guard na anapaswa kuwaheshimu na si kuwaita kikundi,’’ alisema Lipumba.

Alisema hakuwa na taarifa rasmi ya ugeni wa Maalim Seif, bali alisikia kwenye vyombo vya habari, kwamba atakuja na wabunge pamoja na wajumbe kutoka Zanzibar, hivyo alikuwa anasubiri ujio wake kwa kuwa ana ofisi yake.

‘’Maalim Seif ana ofisi hapa, yeye kuja ni jambo la kawaida, ila tangu nimeanza kufanya shughuli za chama sijamwona ofisini, hana haja ya kutangaza anaweza akaja ofisini kwa Mwenyekiti wake, apate miongozo ya kazi,’’ alisema.

Kuhusu ujio wa wabunge na wajumbe wa Baraza Kuu alisema atawajulisha muda wa kukutana, kwa kuwa hajawaita hawapaswi kufika katika ofisi hiyo kama kikundi.

Habari za ndani kutoka ofisi hizo, zilidai kuwa Lipumba alilala ndani ya ofisi hizo usiku wa kuamkia jana pamoja kundi la wafuasi wake waliokuwa wakihofia kwamba upande wa Maalim Seif ungefika usiku kuchukua ofisi yao.

Mmoja wa wafuasi wa Lipumba ambaye alikuwa katika ofisi hizo jana, alidai baadhi ya wafuasi wa kiongozi huyo walikesha hapo kwa lengo la kumlinda kwani alikuwa anafanya kazi zake.

‘’Lipumba hakubaki ofisini kwa kuogopa kundi la Maalim Seif ila alikuwa akifanya kazi zake kwa kuwa ni muda mrefu tangu ajiuzulu hakuwa ofisini hivyo kazi zimezidi,’’ alisema.

Hata hivyo, Lipumba alikana kulala ofisini bali alifika saa 1:45 asubuhi.Katika ofisi hizo magari ya Polisi yalikuwa hayakauki kuanzia saa moja asubuhi huku Lipumba akieleza kwamba hakuomba msaada wala ulinzi wowote wa Polisi, kwa kuwa alikuwa ofisini.

Juu ya taarifa kwamba Maalim Seif aliomba ulinzi Polisi, wamsindikize alisema ni jambo la ajabu.

‘’Ikiwa kuna ukweli katika hilo nastaajabu, unaomba ulinzi kwenda ofisini kwako, ina maana walinzi alionao wa Serikali na wana chama hawatoshi?’’ Alihoji Lipumba.

MATOKEO Ya Simba na Yanga leo Haya Hapa

$
0
0
Mechi ya Simba na Yanga Jioni ya leo imekwisha kwa timu zote kufungana boa moja kwa moja, Simba walikuwa wakicheza pungufu baada ya Jones Mkude kutolewa kwa kadi nyekundu...

MAJIBU ya Feza Kessy Kuhusu Kuwa Mapenzini na Chid Benz

$
0
0
Mrembo kutoka Bongoflevani Feza Kessy ambaye ameshawahi kuzichukua headlines baada ya kushiriki shindano la Big Brother Africa leo October 1 2016 amejibu taarifa iliyokuwa ikimuhusisha Mrembo huyo kutoka na Mkali mwingine anayefanya vizuri kwenye midundo ya Hiphop Chid Benz, haya ndio yalikuwa majibu ya Feza Kessy kuhusu kuwahi kuwa na mahusiano na rapper Chid Benz.

‘Hata mimi nilisikiaga hizo taarifa lakini sio ukweli Chid Benz ni mshikaji wangu sana maana hata juzi nimetoka kuongea nae kwenye simu‘ Feza Kessy

DIAMOND Platnumz Ametaja Gharama Alizonunulia Nyumba South Afrika

$
0
0
September 23 2016 Diamond Platnumz aliingia kwenye headlines baada ya kupost Nyumba ambayo aliandika kuwa ni zawadi kuwa Mpenzi wake ambaye ni Mrembo Zari, Baada ya Diamond Platnumz kupost Nyumba hiyo ambayo iko South Africa zimepita  siku saba na amehojiwa na kipindi cha Weekend Chat Show na kazitaja Gharama alizonunulia Nyumba hiyo. Tazama Hapa:

SIMBA Vs Yanga: Mabomu ya machozi yalindima Uwanjani

$
0
0
Mashabiki wa Simba uzalendo uliwashinda baada ya bao la Amissi Tambwe na kumua kurusha viti uwanjani wakipinga bao hilo, kutokana na kitendo hicho askari wa kutuliza ghasia waliamua kurusha mabomu ya machozi jukwaani.

Mabomu hayo ya machozi yaliwafanya mashabiki wa Simba waliofurika uwanjani hapo kuanza kukimbia hovyo kujinusuru na mabomu hayo huku wengine wakitoka nje kabisa ya uwanja. Mashabiki baadhi wameumia kutokana na vurugu hizo.

Kutokana na vurugu hizo mchezo huo ulisimama kwa dakika kadhaa kabla ya mwamuzi Martin Saanya kutoa kadi nyekundu kwa nahodha wa Simba, Jonas Mkude.

Awali baada ya bao la Yanga, mzee mmoja shabiki wa Simba aliyevalia jezi nyekundu alitaka kuingia katika vyumba vya kubadilishia nguo vya Yanga. Kitendo hicho kiliwaudhi makomandoo wa Yanga ambao walimkamata na kuanza kumpiga kabla ya askari wa kutuliza ghasia kuingilia kati kumnusuru na kipigo hicho.

Kabla ya mechi kuanza Mzee huyo alikuwa amekaa katika mlango wa kuingilia vyumba vya kubadilishia nguo wachezaji wa Simba.

BINTI Karume ‘Amchana’ Lipumba

$
0
0
Fatma Karume, mtoto wa rais wa zamani wa Zanzibar, ameshangazwa na kitendo cha Profesa Ibrahim Lipumba  kutaka kurudi kwenye nafasi yake ya awali ya uenyekiti wa Chama cha Wananchi (CUF) wakati alijiuzulu mwenyewe.

Fatma, mtoto wa Amani Abeid Karume ambaye ni rais wa sita wa Zanzibar, alisema hayo alipoulizwa kuhusu hali iliyoukumba uongozi kwenye chama hicho kikuu cha upinzani visiwani Zanzibar baada ya tamko la Msajili wa Vyama vya Siasa kuwa, anamtambua Profesa Lipumba kuwa mwenyekiti halali wa CUF.

Msajili huyo, Jaji Francis Mutungi alitoa uamuzi huo baada ya kuziita pande zinazosigana kwenye mgogoro, kusikiliza hoja zao baadaye kutoa maoni na msimamo wa ofisi yake kuwa Profesa Lipumba alifuta uamuzi wake kwa maandishi kabla ya mkutano mkuu wa CUF haujajadili barua yake ya kujiuzulu, hivyo anaendelea kuwa mwenyekiti halali.

“Profesa Lipumba alijiuzulu mwenyewe. Aliandika barua akaipeleka kwa katibu mkuu, kisha akautangazia umma na dunia nzima ikafahamu kwamba siyo tena mwenyekiti wa CUF,” alisema.
i

(AUDIO) DIAMOND Platnumz Kwenye Remix Hii Nyingine na Kawataja Wema Sepetu, Hamisa Mobeto na Zari

$
0
0
(AUDIO) DIAMOND Platnumz Kwenye Remix Hii Nyingine na Kawataja Wema Sepetu, Hamisa Mobeto na Zari

Bonyeza Play Hapa Chini:


Viewing all 104785 articles
Browse latest View live




Latest Images