Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104689 articles
Browse latest View live

Utalipenda jibu la Martin Kadinda baada ya kuulizwa na shabiki kama Wema anatumia Madawa ya kulevya

$
0
0
Wiki hii kumekuwa na tetesi ambazo zinasambaa kwa kasi katika mitandao ya kijamii zikidai kwamba malkia wa filamu, Wema Sepetu anatumia Madawa ya kulevya ‘Unga’.

Tetesisi hiyo ambazo sio nzuri kwa mwigizaji huyo pamoja na watu wake wakaribu, zimeonyesha pia kuwagusa baadhi ya mashabiki wa mwigizaji huyo ambapo wanalazimika kutafuta ukweli wa tetesi hizo kwa namna yoyote.

Mmoja kati ya mashabiki wa malkia huyo kupitia mtandao wa instagram, aliamua kumuuliza meneja wa Wema Sepetu, Martin Kadinda kuhusu tuhuma hizo.

Pia rafiki wa karibu wa malkia huyo wa filamu aitwae Muna, kupitia mtandao wa Global Publisher amekanusha kumwingiza shosti wake Wema Sepetu kwenye matumizi ya Madawa ya kulevya kwa kusema madai hayo hayana ukweli.

Waliotimuliwa BoT 1993 Wapiga Hodi Kazini Bank Kuu Baada ya Kushinda Kesi

$
0
0
Wafanyakazi 31 waliopunguzwa katika Benki Kuu Tanzania (BoT) miaka 22 iliyopita wanatua ‘mzigoni’ tena baada ya Mahakama ya Rufani kuwarejesha.

Wafanyakazi hao walifukuzwa kazi bila kufuata utaratibu wakati Serikali ilipotekeleza masharti ya upunguzaji wafanyakazi kama njia ya kurekebisha uchumi.

Wafanyakazi hao kupitia wakili wao, Barnaba Luguwa wamemwarifu Gavana wa BoT, Profesa Beno Ndulu kuhusu dhamira yao ya kurejea kazini kuanzia kesho kufuatia matokeo ya uamuzi wa Mahakama ya Rufaa.

Kiongozi wa wafanyakazi hao, Samson Magoti amesema wanakusudia kuripoti kazini Oktoba 11, 2016 ili wakapige kazi baada ya ushindi walioupata katika kesi iliyoendeshwa kwa miaka 22.

Amesema uamuzi wa jopo la majaji wa Mahakama ya Rufaa katika Shauri la Mapitio Na. 3 la 2014 lililofunguliwa na BoT dhidi yao unawawezesha kuripoti kazini baada ya kusota mahakamani kwa miaka 22.

Magoti aliwataja wenzake watakaoripoti kazini kuwa ni Nuhu Msuya, C.B. Fande, Mbaraka Katundu, Fabian Nguyeje, Omari Hassani, Alfonsi John, Audax Rugaimukamu, Ally Ndaro na Julius Haule. Wengine ni Hellen Warioba, Louis Mapunda, Yusufu Bakari, Laila Ntenja, James Chambala, E. Nyamoga, George Joseph na Simon Mashigasi.


DC KINONDONI Aagiza Kusimamisha Ujenzi Tegeta..Baada ya Mfanyabiashara Kumnyanyasa Bibi Mjane

$
0
0
-Ni unaofanywa bila vibali na mfanyabiashara anayedaiwa kuziba njia, kumnyanyasa bibi mjane
-Aagiza OCD amkamate kwa tuhuma za kudai serikali iko mfukoni mwake.
Na Mwandishi wetu.

Mkuu wa wilaya ya Kinondoni Ally Salum Hapileo asubuhi amewatembelea wananchi wa Tegeta kwa ndevu eneo ambalo bibi anayefahamika kwa jina la Habiba Mustafa alionekana kwenye taarifa ya habari ya itv jana kulalamika kufanyiwa hila njama na mfanyabiashara mmoja ajulikanae kwa jina la Emily Reshea aliyechimba shimo mbele ya nyumba yake na kuziba njia za wananchi kupita kama mbinu ya kuwalazimisha wamuuzie maeneo yao.

Hapi akiwa katika eneo hilo akiambatana na wataalamu wa mipango miji, muhandisi wa manispaa na askari wa jeshi la polisi ameagiza kuvunjwa kwa ukuta ulioziba njia za wananchi kupita, kufukiwa kwa shimo lililochimbwa kabla ya saa 12 jioni leo na kumtaka OCD Kawe kuchunguza tuhuma za mfanyabiashara huyo kudaiwa kusema kuwa
"serikali iko mfukoni mwake"

na ikibainika kuwa ni kweli akamatwe mara moja na kuhojiwa na vyombo vya dola.
Wataalamu wa makazi na mazingira wa manispaa ya Kinondoni wamesema mfanyabiashara huyo atazuiwa kuendelea na ujenzi na wamemtaka kuwasiliha nyaraka zake zote katika ofisi za manispaa.
Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni amefika Tegeta baada ya kusikia kilio cha mama huyo mjane kwenye kituo cha Televisheni ya ITV jana usiku.

Bibi Habiba amemshukuru Mkuu wa wilaya ya Kinondoni kwa kusikia kilio chake na kufika kumsaidia.

Kinazidi Kunuka Kati ya Baraka Da Prince na Stan Bakora..Stan Amjibu Baraka Kama Ifuatavyo

$
0
0
Unaambiwa utani ni Mzuri ila Utani ukiwa wa Ukweli sana Unauma na Ukimuuma aliyetaniwa akikosa Kifua tu cha kujizuia, Ugomvi anaweza akakuzulia.

Tunajua kabisa kwamba barakah The Prince ni Mweusi ila sasa Weusi alioutengeneza Stan Bakora kwenye Cover yake ya Wimbo wa Barakah The Prince ft. Ali Kiba, Stani alizidisha Weusi kwenye Kumuiga Barakah.

Sasa Hiki ndicho alichokipost barakah kwenye Instagram Account yakeKuonyesha kwamba Amekerwa na Utani wa Stan Bakora.


Baada ya Barakah Kufunguka hayo kwenye Instagram, Stan Bakora naye Amefunguka kwenye Account yake ya Instagram

Rais Magufuli Aokoa Bilioni 1.2/- Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC)

$
0
0
JITIHADA za Rais John Magufuli katika kubana matumizi yasiyo ya lazima serikalini, ambazo alizihamishia katika Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), ikiwamo kuzuia safari zisizo za lazima katika jumuiya hiyo, zimewezesha kuokoa zaidi ya Sh bilioni 1.2.

Rais Magufuli ni Mwenyekiti wa Jumuiya ya Afrika Mashariki na aliahidi kuchukua hatua za kubana matumizi yasiyo ya lazima na ikibidi kutumbua watendaji wa EAC, baada ya kuchaguliwa kushika wadhifa huo Machi mwaka huu jijini Arusha.

Katibu Mkuu wa EAC, Balozi Liberat Mfumukeko alisema jana jijini hapa kuwa jitihada za kubana matumizi yasiyo ya lazima, zimeokoa Dola za Marekani 588,768 (zaidi ya Sh bilioni 1.2) ndani ya kipindi cha miezi mitatu kuanzia Mei hadi Agosti mwaka huu.

Akizungumza na waandishi wa habari kwa mara ya kwanza tangu ashike wadhifa huo Aprili mwaka huu, Balozi Mfumukeko alisema kiasi hicho cha fedha kiliokolewa kutokana na kubana safari zisizo za lazima za watumishi na watendaji wa jumuiya katika kipindi hicho.

“Utekelezaji wa ubanaji wa matumizi yasiyo ya lazima unategemewa kuokoa dola za Marekani milioni sita kwa mwaka huu wa fedha 2016/2017 na tutakuwa tunatoa taarifa hizi kwa watu wa Afrika Mashariki kila baada ya muda,” alisema Balozi Mfumukeko ambaye ni Katibu Mkuu wa Tano wa EAC.

Kuhusu mafanikio ya utekelezaji wa makubaliano mbalimbali ya jumuiya hiyo, Balozi Mfumukeko alieleza kwamba utekelezaji unaendelea vyema pamoja na changamoto mbalimbali zinazojitokeza.

Alisema katika utekelezaji wa kuwa na vituo vya ukaguzi wa mizigo vya pamoja mipakani, vituo 10 kati ya 15 vinatekeleza ukaguzi huo kwa mafanikio na kupunguza gharama za kufanya biashara.

“Kutokana na vituo hivyo kuanza kazi, hivi sasa kusafirisha mizigo kutoka Mombasa hadi Kampala inachukua siku nne badala ya siku 20 za awali, jambo linalowasaidia wasafirishaji kupunguza gharama za kufanya biashara,” alisisitiza.

Tangu alipoingia madarakani, Rais Magufuli amedhibiti mianya ya rushwa ikiwemo kupunguza safari za nje pamoja na kutumbua majipu mbalimbali kwa nia ya kubana matumizi sanjari na kuhakikisha kila mtu ananufaika na matunda ya nchi yake pamoja na kurejesha heshima ya kazi kwa watumishi wa umma.

Jinsi Ya Kumfanya Mwanamke Apagawe Kwako

$
0
0
Kuna vitu vingi ambavyo unaweza kutumia kwa manufaa yako ili kufanya wanawake wakuone unavutia. Amini usiamini, hivi vitu si lazima uwe tajiri wala uwe na urembo wowote. Mwanzo kati ya vitu hivyo vingi ni rahisi kuvitumia kwa urahisi. Hii hapa ni orodha ya mambo ambayo ukiyazingatia yatakufanya wewe uwe na mnato kwa mwanamke yeyote yule.

1. Uwezo wako wa nishati
Nishati inaweza kuwa na mkusanyiko wa vitu kadhaa, kama vile kuhisi kwa vipepeo ndani ya tumbo, kusuka, wasiwasi ama vitu tofauti kabisa. Kwa mtizamo wa moja kwa moja, nishati inahusiana na yote yale ambayo yanamfanya mwanamke kujiskia raha wakati anapokuona ama kutaka kuutumia muda wake mwingi akiwa na wewe. Nishati inacheza nafasi kubwa katika mapenzi kama wataka kumtongoza mwanamke na ufaulu kwa urahisi. Ili kupeana nishati zaidi kila wakati unapokuwa na mwanamke, hakikisha kile kikuu unachohitaji kufanya ni kumchekesha, kumsapraiz, umguse kwa bahati mbaya mara kwa mara, kuwa mwenye michezo nk. Zote hizo zitamfanya kukufikiria wewe mara 24/7.

2. Mbinu utakayoitumia kumsifu
Kulingana na utafiti kutoka NBC unadai ya kwamba wanawake wengi hawajiskii huru kupewa ama kupokea sifa kutoka kwa wanaume. Lakini usikatwe na tamaa! Vile ambavyo utampongeza mwanamke inaweza kucheza pakubwa kufaulu kumpata mwanamke unayempendae baada ya muda. Afterall ukimsifu kitofauti tofauti anaweza kukubali ama kukuona kama wewe ni mzaha kwake. So kuhepa aibu kama hizi ndogo ndogo, unafaa umsifu mwanamke kwa jambo ambalo ni la kwake pekee, yaani kitu ambacho utamsifu nacho hakipatikani kwa mwingine. Mfano waweza kumakinika kwa kitu ambacho anafanya wakati flani na utumie ujuzi wako wa kiume kumsifia na jambo hilo. Mfano unaweza kumsifu kwa uwezo wake wa kuimba, kuchora, mtindo wake wa kutembea nk. [Soma: Mbinu ya kutongoza kwa wale wanaojifunza]

3. Upambo wako
Si lazima uwe mwanamume wa kuvutia ili umvutie mwanamke. Utafiti umebainisha kuwa wanawake hawavutiwi na urembo wa mwanamume, nywele zake wala ngozi yake. Mwanzo kuwa mrembo kama mwanamume kuna ubaya wake mwingi ikizingatiwa kuwa unaweza kuonekana kama pleya ambaye unapendwa na wanawake wengi.

Kile ambacho unachohitajika hapa ni uhakikishe kuwa uwe nadhifu kimwili na mavazi yako. Kufanya hivi kutakusaidia wewe kuonekana mtu timamu halikadhalika inakufanya wewe kuwa na confidence ya kapproach demu yeyote yule.

4. Ujuzi wako wa kutangamana
Lazima atleast uwe na ujuzi ambao utakusaidia wewe kuweza kutangamana na wengine. Kama mwanamume lazima uwe na ujuzi ambao utakusaidia wewe kutangamana na wengine kwa urahisi. Hii inamaanisha kuwa lazima uwe na ujuzi flani wa kuongea na wanawake ndipo utakapojua jinsi ya kumfanya apagawe na wewe.

5. Kiwango chako cha kujiamini
Kitu cha mwisho ambacho ni muhimu kwako kuwa nacho ni kujiamini. Kujiamini ni njia moja wapo ya lazima uwe nayo ili uweze kuiteka hisia ya mwanamke yeyote yule.[Soma: Njia za kuwa na confidence kama mwanaume]

KUMBUKA: Vitu vyote tulivyoeleza hapo juu havitakuwa na manufaa yeyote yale iwapo kama hutaweza kujiamini kama mwanamume. Hivyo ni lazima kwako kuhakikisha kuwa mwanzo unajijenga kwa kuwa na confidence. Hii ni kuanzia kujitambua wewe mwenyewe bila kujishuku, kuongea bila woga wowote wala kutoingiwa na wasiwasi wakati wowote ukiwa karibu na mwanamke.

Model Maarufu wa Bongo Alitosa Kutokea Kwenye Video ya Salome, Alitaka Pesa Nyingi...Diamond

$
0
0

Kuna model maarufu wa Bongo aliyetosa kuonekana kwenye video ya wimbo wa Diamond ‘Salome.’

Model huyo anadaiwa kutaka alipwe fedha nyingi ambazo zilikuwa nje ya bajeti ya staa huyo.

“Bajeti yangu haikuweza kumuafford, na siwezi kufanya kitu kimashauzi wakati bajeti yangu ndogo,” Diamond alikiambia kipindi cha The Playlist cha Times.


Diamond anasema alichokikosa model huyo baada ya kukataa kufanya video hiyo si fedha tu, bali exposure ambayo angeipata baada ya hapo.

“Si uchawi, sio uongo, sio ushirikina, unavyofanya video na mimi unakuwa mkubwa na inakuongezea dau,” alisisitiza kwa kuongeza kuwa watu kibao humuomba waonekane kwenye video zake bure lakini hukataa kwakuwa ni lazima awalipe.

Diamond amedai hiyo ndio sababu hatokuja kulitaja jina lake kwakuwa atampa kiki na atakuwa mkubwa.

“Nilimuambia, angalia angle zote mbili, angalia kwamba nakulipa kiasi lakini kushiriki kwako kwenye hii video itakuongezea ukubwa zaidi, itakupa biashara nyingi.”

Alitoa mfano kuwa show nyingi za MTV alizowahi kutumbuiza alifanya bure kwasababu alizitumia kukuza jina lake. Anasema wakati mwingine hadi dancers huwasafirisha kwa gharama zake mwenyewe.

“Lakini najua show ninayoifanya pale ikitoka itanipa hela nyingi baadaye. Niliheshimu alichokisema ndio maana sikumind, nilisema naheshimu sababu umejitambua na umeona thamani yako ni nini, lakini bahati mbaya sisi bajeti yetu haikufika huko.”

Angalia Video hapa:

Sakata la Ali Kiba Kushushwa Jukwaani Show ya Mombasa..Mdau Adai ni Kawaida ya Ali Kiba Kulalamika

$
0
0
Jana Sakata la Mwanamuziki Ali Kiba kushushwa Jukwaani kwenye show ya Mombasa ili Chriss Brown apande jukwaani kuimba jana lilichukua sura mpya baada ya Video kutoka Ali Kiba akiongea kuhusu hilo na kusema kuwa anahisi kuhujumiwa hasa baada ya meneja wa Diamond kuonekana akiwa backstage...Ali Kiba amedai haelewi Meneja huyo wa Diamond alikuwa anafanya nini backstage wakati msanii wake hakuwa na show siku hiyo..
Sasa watu mbali mbali wametoa maoni yao embu soma ya huyu alafu uniambie kama kuna ukweli:



Wasira Atumia Saa 2 Kupinga Ushindi wa Mbunge wa Bunda Mjini Ester Bulaya Mahakama Kuu Mwanza

$
0
0
Shahidi wa tatu katika kesi namba moja ya mwaka 2015 ya kupinga matokeo ya ubunge wa jimbo la Bunda Mjini, Stephen Wasira leo amepanda katika kizimba cha mahakama kuu kanda ya Mwanza, inayoketi mjini Musoma kutoa utetezi wake, huku ulinzi mkali wa askari polisi wenye silaha za moto, mabomu ya machozi na mbwa ukiwa umeimarishwa.

Wasira ambaye alitumia muda wa saa 2 na dakika 26 kutoa ushahidi wake huku akihojiwa na wakili wa mlalamikiwa wa kwanza Ester Bulaya, ameiambia mahakama kuu chini ya jaji Noel Chocha kwamba uchaguzi katika jimbo la Bunda mjini ulikuwa haramu kutokana na kugubikwa na ukiukwaji wa sheria, taratibu na kanuni kulikofanywa na msimamizi wa uchaguzi kufuatia kuwepo kwa ongezeko la vituo vya kupigia kura kutoka 190 hadi 199, sambamba na ongezeko la idadi ya wapiga kura kutoka watu 69,369 hadi 164, 794 bila taarifa yoyote.

Mwanasiasa huyo mkongwe, ambaye aliangushwa na mgombea wa chama cha demokrasia na maendeleo ( CHADEMA ), katika uchaguzi mkuu uliopita kwa kura 19,000 dhidi ya 28,568 alizopata mshindi Ester Bulaya, amemlalamikia msimamizi wa uchaguzi jimbo la Bunda mjini kuongeza vituo 9 kwenye kata za kabasa, Bunda mjini, Bunda stoo, Manyamanyama, Nyamakokoto, Wariku na Guta pamoja na kuhamisha kituo cha Mchalo na kukipeleka mahali kusikojulikana bila kuvishirikisha vyama vitano vya siasa vilivyoshiriki uchaguzi huo.

Mapema wakili Tundu Lissu, baada ya kupitia kiapo cha shahidi huyo Stephen Wasira aliiomba mahakama hiyo kuondoa aya ya 3b, kirumi i (ii), ( iii ) na ( iv ) pamoja na 3c, ambazo zingewezakuleta mambo mapya katika shauri hilo kinyume na masharti ya 23 ya kanuni za uendeshaji wa uchaguzi za mwaka 2013 kama zilivyofanyiwa marekebisho, hoja ambayo ilikubaliwa na jaji Noel Chocha.

Mara kwa mara jaji chocha alilazimika kuingilia kati kwa kumtaka wasira kujibu maswali ya wakili Tundu Lissu, huku Wasira akionekana dhahiri kuwa na majibu ya kujiamini; ambayo wakati mwingine yaliwafanya wasikilizaji kuangua kicheko hasa pale alipodai kuwa hamfahamu katibu mkuu wa Chadema Dk. Vincent Mashinji zaidi ya Dk. Wilbroad Slaa, ili kujiridhisha iwapo Ester Bulaya aliwahi kujaza fomu ya bajeti za gharama za uchaguzi ambayo kisheria hupelekwa kwa msajili wa vyama vya siasa mwenye uwezo wa kumwekea pingamizi mgombea aliyekiuka utaratibu.

Kipindi cha mchana kilianza kwa mawakili Costantine Mutalemwa, Yasin Memba na Hajra Mungula wanaowatetea wapiga kura wanne wa jimbo la Bunda mjini waliofungua kesi hiyo mahakama kuu kanda ya Mwanza kumhoji shahidi huyo wa tatu Stephen Wasira baada ya wakili Tundu Lissu kuhitimisha maswali yake.

Nchi Kumi Zinazoongoza Kwa Kuwa na Wasichana Warembo Barani Afrika

$
0
0
Afrika ni miongoni mwa Bara lililobarikiwa tamaduni, lugha na watu tofauti wenye tabia zinazoshabihiana ikiwamo ukarimu.

Miongoni mwa watu wa Bara hili wapo wasichana warembo wa kuvutia tofauti na wengine, katika hili kuna mjadala mpana huku baadhi wakikubali kuwa kuna watu wanaovutia kuliko wengine huku baadhi yao wakidai kuwa uzuri, urembo wa mtu unatafsiriwa kulingana na anayemtizama.

Lakini katika hili tukubali tukatae miongoni mwa wanawake wa Afrika bila kujali wanatizamwa na nani ni wazuri na warembo na wanavutia kuliko wengine.

Ifuatayo ni orodha ya nchi 10 zenye wanawake wenye mvuto barani Afrika, mwaka jana Tanzania ilishika nafasi ya 10 mwaka huu imepanda nafasi moja na inashika nafasi ya tisa.

10: Ghana

Nchi ya Ghana inashika namba 10 kwa kuwa na wanawake wazuri Barani Afrika kwa mujibu wa ripoti iliyotolewa Machi mwaka huu na tovuti mbalimbali za masuala ya urembo ikiwamo Afrojuju, Urbanviralmedia.

Jambo wanalolingana wanawake wa Ghana kuwa wana mvuto wa asili ambao huuongezea kwa kujiremba.

Mwaka jana Ghana ilishika namba nane, mwaka huu imeshuka nafasi mbili na kushika nafasi ya 10.

9: Tanzania

Nafasi ya tisa mwaka huu imeshikiliwa na Tanzania iliyokuwa inashikilia nafasi ya 10 mwaka jana hivyo imepanda nafasi moja.

Miongoni mwa sifa za wanawake wa Tanzania ukiachilia mbali uzuri wa asil ni ni pamoja na kutunza nyumba, ujuzi wa kukisafisha chumba na kukipamba. Katika orodha hii wametajwa kuwa wanawake bora wachapa kazi na wanaojali familia.

8: Kenya

Imepanda nafasi moja kwa kuwa mwaka jana ilishika nafasi ya tisa.

Sifa za wanawake wa nchi hiyo ni pamoja na kuwa wajuzi katika mapenzi, wachapa kazi na watuamiaji wa pombe, jambo linalowatofautisha na watu wengine ni rangi yao ya kuvutia.

7: Nigeria

Kwa miaka miwili mfululizo warembo wa Nigeria wanashikilia nafasi ya saba.

Wanawake wa Nigeria licha ya kuwa na rangi za kuvutia, pia wana maumbo ya yaliyojazia na wamejaaliwa kuwa na uwezo wa kuzaa watoto wengi, kati ya 1970 na 2011 Nigeria iliongezeka idadi ya watu mara tatu na kuifanya kuwa nchi yenye wakazi wengi barani Afrika. Kama unataka mwanamke mzuri na atakayekuzaliwa watoto wengi Nigeria inakuhusu.

Kwa wale wanaotaka mwanamke mwenye sifa za kuwa mke, wa nchi hiyo wanafaa. Sifa ya kipekee wanajua kupika na kutunza familia.

6: Ivory Coast

Mwaka huu namba sita imeshikiliwa na Ivory Coast ambayo mwaka jana haikuwepo kabisa, hivyo imeingia kwenye 10 bora kwa mara ya kwanza, nafasi hiyo mwaka jana ilishikwa na nchi ya Afrika Kusini.

5: Afrika Kusini

Nchi hii imewapa jina warembo wake “Upinde wa Mvua wa Taifa”. mwaka huu imepanda nafasi moja kutoka nafasi ya sita iliyoshika mwaka jana.

Ni miongoni mwa nchi zenye wasichana warembo wa kuvutia katika Bara la Afrika. Miji ya Cape Town, Johannesburg, Pretoria na Durban ndiyo yenye wanawake wenye mvuto. Wanawake wa Afrika Kusini wanang’aa na kuvutia kutokana na ngozi zao nyororor.

Unapofika nchini humo hasa katika Jiji la Pretoria kuwa makini kwa sababu unaweza kugongwa na gari kutokana na kuwashangaa warembo hao ambao kwa kawaida huvaa tofauti kidogo, nguo zao huwa fupi.

4: Rwanda

Wanaume wao hujivunia kwa kuwaita “Tufaa Lililojificha”, mwaka jana nchi hiyo ilishika nafasi ya kwanza kwa kuwa na wanawake warembo, mwaka huu imekamata nafasi ya nne.

Wanawake wa nchi hii sifa ya kipekee ikiwamo urefu unaopendeza, shepu ya Kiafrika kabisa, wasomi na wanaotaka kufahamu kila jambo.

Kitu kinachowafanya wawe juu licha ya kuwa warembo, ni wachapa kazi wanaojali muda na kupigania wanachokitaka bila kujali wanapambana na nani na ana nafasi gani ikiwamo kutoogopa mashindano na wanaume katika nyanja mbalimbali ikiwamo za kisiasa, kielimu au kiutendaji.

3: Somalia

Sifa yao maarufu na wanayopendwa kuitwa na wanaume wa nchi yao ni “Vita Aiharibu Urembo”, mwaka jana walishika nafasi ya pili. Licha ya urembo na kuwa karibu maeneo mengi katika Bara la Afrika bado wana utamaduni wa kuoana wao kwa wao. Wanatajwa pia kuwa miongoni mwa wanawake wanaoamini katika ndoa na kuitendea haki.

2: Eritrea

Ni miongoni mwa nchi zenye wanawake wenye mvuto barani Afrika, licha ya asilimia kubwa ya wanawake wake kujihifadhi kwa kuvaa ushungi na mavazi marefu bado asili ya urembo wao ipo pale pale.

1: Ethiopia

Wanawake wa nchi hii huitwa “Asili ya Ubinadamu”. Huo ni utambulisho wao mbele ya macho ya dunia.

Inaelezwa kuwa ustaarabu kwa wanawake ulianzia katika Ethiopia, hivyo inatajwa kuwa ni nchi yenye wanawake wenye mvuto zaidi barani Afrika.

Wengine wanasema matokeo ya mvuto wao yanatokana na mchanganyiko wa watu wa kale wa Yemen na Ethiopia. Wakati mwingine inakuwa ngumu kuwatofautisha kutokana na baadhi yao kufanana sana, maumbile, sura na uzungumzaji.

Nay wa Mitego Adai Bifu la Baraka Da Price na Stan Bakora Linaweza ni Kiki tu

$
0
0
Nay wa Mitego amedai kuwa kinachoendelea kati ya Barakah The Prince na Stan Bakora, kinaweza kuwa kitu cha kutengeneza.

Akiongea na mtangazaji wa Kings FM, Prince Ramalove, rapper huyo amewaita wawili hao wote watoto na kwamba umri wao unawaruhusu kufanya wwanachokifanya.

“Siwezi kusimama upande wowote, hao ni watoto, wote ni wadogo mimi ni wadogo zangu,” alisema.

“So inapofika time wanagombana wataelewana tu. Hatuwezi kujua labda ni kiki, haiwezi kuwa beef kiasi hicho, inawezekana labda kiki, watu mkachukulia serious kumbe wamekaa wametengeneza,” ameongeza Nay.

Barakah ameonekana kuchukizwa na parody aliyofanya Stan ya wimbo wake Nisamehe ambapo amejipaka masizi usoni kuwa mweusi kama muimbaji huyo.

Stan amejipatia umaarufu kwa kuigiza sauti ya Nay wa Mitego

Lulu Adai Amekataa Dili Kadhaa Kutoka Kwa Wasanii wa Nigeria

$
0
0
Msanii mahiri wa filamu Bongo, Elizabeth ‘Lulu ‘ Michael amefunguka kwa kudai kuwa tangu alipopata tuzo ya AMVCA 2016 amekataa dili kadhaa kutoka kwa wasanii wa muziki wa Nigeria.

Muigizaji huyo ameitaja sababu ya kukataa dili hizo imetokana na yeye si mwanamuziki wala video vixen.

“Nimepata dili kama mbili tatu kutoka Nigeria za kuigiza filamu na kuna wengine walidhani nafanya muziki,” amekiambia kipindi cha Clouds E cha Clouds TV.

“Nimeshatafutwa na wanamuziki wa Nigeria ambao wengine walitaka niimbe na wengine nitokee tu kwenye video zao, siwezi nikawataja,” alisema.

March mwaka huu, Single Mtambalike (Rich Rich) na Elizabeth Michael (Lulu) walishinda tuzo za African Magic Viewers’ Choice Awards (AMVCA2016) zilizotolewa nchini Nigeria.

Raymond: Nyimbo ya Salome Imenipa Kiki Kubwa Sana Natafutwa Dunia Nzima Nikafanye Kolabo

$
0
0
Msanii Raymond amesema nyimbo ya salome aliyofanya na diamond imempa umaarufu maradufu na sasa anapigiwa simu kutoka sehemu mbalimbali duniani akiombwa afanye kolabo
aesema amepigiwa simu kutoka marekani, italia, india na kwingineko wakitaka kolabo 
 Video:

VIDEO ya Mrembo Gigi Money Akitikisa Makalio Yake Bichi Inayosambaa Mitandaoni

$
0
0

Video ya Mrembo Asiye na Mshipa wa Aibu Gigy Money akifanya yake bichi huku mrembo mwenzake akisifia makalio yake...
Itazame Hapa:


Alikiba na Wizkid Nusura Watie Doa Show ya Chris Brown Mombasa...Watunishiana Misuli

$
0
0
Wanamuziki Alikiba na Wizkid walitunishiana misuli juu ya nani aimbe kabla ya mwenzake kwenye show ya Mombasa

Alikiba alikataa kuimba kwanza kwa madai kuwa yeye ni mwanamuziki mkubwa Kenya kuliko Wizkid, kwahiyo hastahili kuimba kabla ya mwanamuziki huyo kutoka Nigeria

Baada ya vuta nikuvute hiyo Alikiba aliibuka mshindi kwani Wizkid alipanda jukwaani kabla ya Alikiba.

===============================

Show of might and abrupt ending of performances marred Saturday’s much hyped show that was headlined by American singer Chris Brown, Nairobi News can reveal.

Sources say that there was a standoff when Tanzania’s Alikiba declined to perform before Nigeria’s Wizkid.

“Kiba felt he is bigger in Kenya than Wizkid hence he could not understand why he was scheduled to perform before,” said our source.

In the end, Alikiba had his way, which saw him perform after Wizkid and just before Mr Brown

Walinzi wa Chriss Brown Ndio Waliomzimia Microphone Ali Kiba Alipokuwa Jukwaani Mombasa

$
0
0
Tanzanian artiste Ali Kiba found himself swimming in murky waters when he appeared late for his performance at the Mombasa Rocks Festival held at the Mombasa Golf Club last Saturday. The event, which was headlined by American double platinum R&B sensation Chris Brown, saw Ali Kiba perform only two songs, Aje and Macmuga, before leaving the stage prematurely; visibly frustrated.

Ali Kiba performed after Nigeria’s Wizkid had taken to the stage, leaving many revelers confused on the protocol that was being used to call artistes to the dais. Known to many, Wizkid was one of the two main acts of the event – deputising Chris Brown in terms of hierarchy – at least according to the event’s organizers. So when Kiba took to the stage after Wizkid, questions were raised.

It now emerges that Chris Brown’s security issued a threat to Kiba to vacate the stage so that the Loyal hit-maker could thrill fans – as the time allocated for Brown’s performance (minutes to 1am) had clocked. “Go tell that man (Ali Kiba) to leave the stage in less than two minutes or else we will physically get him out of the podium,” Chris Brown’s security was heard, by our resident DJ, telling the floor manager. The floor manager obliged. He went toward Kiba and whispered the order to him.

However when the singer overstayed his welcome on stage, the microphone was switched off. Ali Kiba in an October 10 interview with Radio Citizen’s Mambo Mseto host Willy Tuva claimed that someone played a dirty trick on him. “Every artiste had a special agreement with the event organizers.

Chris Brown’s contract stated he performs for 80 minutes and leave the stage right after,” Ali Kiba told Willy Tuva. “I don’t know what transpired to an extent someone came and disconnected my microphone while I was on stage. I was not impressed. Many things happened, that left me confused,” said Ali Kiba.

Source: ekenya

Majibu ya Amber Lulu Baada ya Kudaiwa Alikamatwa na Madawa ya Kulevya

$
0
0
Leo mtangazaji Soudy Brown amepiga story na  Amber Lulu, mwanadada maarufu kwenye mtandao wa Instagram ambaye inaelezwa kuwa aliwahi  kutoka kimapenzi na Rapa Young Dee. Sasa wiki iliyopita kupitia U Heard ilitoka stori kwamba Amber Lulu amekamatwa na madawa ya kulevya akiwa uwanja wa ndege.

Soudy Brown amempata Amber Lulu kwenye line na ameeleza kuwa sio kweli kuwa alikamatwa na madawa ya kulevya kama inavyodaiwa na hajawahi kujihusisha na ishu za aina hiyo isipokua wakati anadate na Young Dee ndio stori za kutumia madawa ya kulevya zilianza kuzagaa mtaani.

Watu wanasema mimi nilikamatwa sijui sipatikani kitu ambacho sio kweli, mi nilikwa Arusha na sikuaga mtu kwasababu ni maisha yangu na hua sina utaratibu huo, na huyo Gigy Money aache maisha yangu afanye mambo yake, mimi nimetoka Arusha kuja Dar kutafuta maisha.  kwetu Kurasini hapo, Mimi Passport yangu ilisumbua na sio kukamatwa na madawa ya kulevya:- Amber Lulu

Tetesi za Hemed PHD Kutoka Kimapenzi na Mwigizaji Tausi...Tausi Afunguka

$
0
0
Muigizaji na mchekeshaji kwenye tasnia ya Bongo Movie, Tausi, amesema hana mahusiano yeyote nje ya kazi na Hemed PHD huku akisema huwa wanakutana kambini na hana hata namba ya simu ya msanii huyo.

Tausi ameibuka na kusema hivyo baada ya kuwepo uvumi wa kujimwaga na staa huyo ambapo aliiambia eNewz “Hemedy ni msanii mwenzangu tu na nilipokuwa nyumbani nilikuwa namuona tu kwenye TV na mara ya kwanza nilipokutanishwa naye na meneja wangu Lamata ilikuwa ngumu hata kuongea naye na nilitetemeka saana na nilikuwa mwoga saana”

Mbali na hilo, Tausi, alizungumza kuhusiana na wavulana ambao wamekuwa wakitamani kuwa naye huku wakijiuliza wataishi vipi na yeye akisema hakuna jambo ambalo haliwezekani kwani hata yeye ana ndoto za kuishi na mwanaume na kuwa na watoto wasiopungua 12.

Diamond Ndiye Msanii Tajiri zaidi Kwa Sasa Africa Mashariki

$
0
0
Jarida la Forbes la nchini marekani limetoa wasanii matajiri zaidi duniani ,Africa na kanda mbali mbali ambapo kwa upande wa Africa mashariki.

Diamond platinum ameongoza kwa kuwa na utajiri wa dollar million 4.5 ambazo ni zaidi ya bilioni 10 za kitanzania hasa baada ya kununua Nyumba yake ya south Africa.

Vitu vingine anavyomiliki ni Majumba ya kifahari Dar,Magari ya kifahari , Berber shop, Maduka ya nguo za mitindo ya kisasa na vingine Vingi.

Amefatiwa na Dr Jose Kamilioni wa Uganda ambaye anakadiliwa kuwa na utajiri wa dollar milioni 3.9 ... Wanafatia Akothee na Jaguar anashika nafasi ya 4

Wanachokiangalia zaidi sio pesa kwenye account Bali thamani ya vitu anavyomiliki.....

Katika jarida hilo linaonyesha diamond akiwa anafanya wastani wa show 2 kwa wiki show 8 kwa mwezi na show 100 kwa mwaka ambapo show yake ya chini anakadiriwa kulipwa wastani wa dollar elfu 20,000 na show ya juu analipwa wastani wa dollar elfu 75,000 .

Mikataba yake na makampuni kama Cocacola,Vodacom na DSTV

Jarida ilo linaonyesha pia diamond anaweza vaa vitu vyenye thamani ya dollar laki 150,000 ambazo ni zaidi ya milioni 350,000,000 za tanzania mwilini mwake kwenye shoo moja ambavyo ni Pete,cheni,viatu kofia,shati na suruali na vingine.

Kiukweli huyu mwenzetu yupo kwenye another level kabisa.

Ongera kwa diamond platinum na wapenda maendeleo wote wa nchi hii tuendelee kumsaport msanii huyu aweze kufika mbali zaidi....

Serikali Yajikanyaga Yenyewe..Kauli ya Waziri Ummy Mwalimu Yapinzana na ya Samia Hassan

$
0
0
Baada ya  Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu kusema kuna dawa za kutosha nchini, Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan amesema ukosefu wa dawa unaojitokeza hivi sasa ni wa muda mfupi.

Waziri Ummy amekanusha taarifa zilizokuwa zimeenea kwamba kuna uhaba wa dawa za binadamu na kusisitiza kuwa, zipo nyingi na zinaendelea kuingia nchini. Pia, Waziri huyo alithibitisha kuwapo  vifaatiba vya kutosha na kwamba, chanjo za watoto ndizo zilikuwa zimeisha lakini hivi sasa tayari zimeletwa.

Hata hivyo, kauli hiyo inakinzana na ya Samia aliyoitoa wakati akiweka jiwe la msingi katika ujenzi wa wodi ya wazazi Hospitali ya Mwananyamala.

Samia alisema ukosefu wa dawa unaojitokeza hivi sasa ni wa muda mfupi, kwani Serikali inajipanga kuondoa tatizo vifaatiba.

Makamu wa Rais ametoa kauli hiyo baada ya kuelezwa na Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Mwananyamala, Dk Daniel Nkungu  kuwa wamekuwa wakikabiliwa na upungufu wa dawa.

Samia amesema licha ya Serikali kujipanga kukabiliana na tatizo hilo, uongozi wa hospitali hiyo unatakiwa kusimamia vizuri  ukusanyaji wa mapato.

Viewing all 104689 articles
Browse latest View live




Latest Images