Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104688 articles
Browse latest View live

Sakata la Lema na Gumbo Arusha Lamuibua Dr Slaa Mafichoni..

$
0
0
Dr Slaa anaandika!

Mrisho Gumbo,
Naamini hii ID ni ya kwako na hasa kwakuwa kwenye post unaonekana ukizungumza, napata uhakika kuwa ni wewe.

1) Mkuu wa Mkoa, nakuheshimu kwa kuwa cheo chako ni kikubwa sana. Hata hivyo, ulichokifanya leo na " propaganda unazopiga zimenifanya nikudharau na kukupuuza. Ningeliweza kuishia katika kukudharau na kukupuuza, lakini

2) Aibu uliyoiletea Taifa letu leo, inanifanya " nipige kelele" kuwa " siasa za maji taka siyo wakati wake huu.
a) Mhe.Mrisho Gumbo, wewe kama Mkuu wa Mkoa unayo au mamlaka au vyombo vya dola kukusaidia kufanya utafiti wa maana kuliko aibu kubwa uliyoiletea Taifa letu mbele ya Wahisani/ Wafadhili wetu kupitia Maternity Africa. Hukufanya hivyo, umeamini propaganda kuliko busara na hekima. Kwa hilo siwezi kukusamehe wala kukuheshimu pamoja na cheo au vyeo vyote ulivyonavyo.

b) Mrisho Gumbo, ungelikuwa wa busara iwapo ungelimwomba kiongozi au mwakilishi wa ADF ( ulikuwa na uwezo wa kujua ADF ni nani na historiaya yake ni ipi- kwa kupenda propaganda hukufanya hivyo) au Mwakilishi wa Maternity Africa hasa Happy ( ambaye alisaini pia barua ya kukualika kuwa mgeni rasmi, au hata Mhe. Mbunge Lema ambaye kimsingi ndiye chimbuko la upatikanaji wa Ardhi hiyo kutoka kwa Marehemu Advocate Mawala ( Mwenyezi Mungu amlaze mahala pema peponi), na pia chimbuko la Upatikanaji mradi kutoka kwa wafadhili wetu. Kutokupenda kushauriwa na hao wenye kujua mradi imekufanya "kuonekana ****" na " mwongo" kwa kuwa historia haifutwi kwa " propaganda za jukwaani". Lakini kwa bahati mbaya athari ya propaganda imeenda mpaka kuichafua Taifa letu kwa wahisani. Ujenzi ndiyo kwanza unaanza. Umeombwa kufanya "Ground Breaking ceremony", unadhani wawakilishi wa wahisani na hasa kule kwenye chimbuko la fedha wanapata picha gani ya Taifa letu.

c) Mrisho Gumbo, busara na hekima ya kawaida ingelikuwezesha kuelewa barua ya mwaliko ambayo imesisitiza mara mbili hivi, kuwa wahusika ni taasisi isiyojihusisha na siasa. Wakasema mradi kwa muda sasa umekumbwa na matatizo yenye sura ya kisiasa. Ulipaswa kutafakari, kutafiti na kutafiti njia makini zaidi ya kuona wakina mama wajawazito, wenye fistula na watoto wachanga hawakosei au hata hawacheleweshewi kupata huduma hiyo kwa sababu za kipuuzi tu. Eti unasoma historia! Unsijua historia au unaota ndoto! Nimepiga kelele kwa kuwa ninaijua vizuri hiyo historia A to Z. Sikuambii ungeliniuliza, lakini wapo kwenye kikao hicho ambao wasingelihitaji kuisoma bali kuitoa kichwani historia hiyo, tangu kupatikana kwa Ardhi, mchakato wa kuchora ramani, kuisajili na kupata vibali vyote vya Kituo hicho cha Afya( japo kwa kweli ni hospitali ( inaitwa kituo cha Afya tu kwa. Sababu za kisheria).

3) Mrisho Gumbo, kwa hili Watanzania wa Arusha na wote wenye kujua ukweli hatutakusamehe kwa aibu uliyotupatia, na kujenga misingi ya kutufungia miradi mingine kwa wahisani wetu. Kama una chembe dogo la busara:

a) Utakaa chini na kutafakari umekosea wapi. Ikiwa lazima

b) uwe na unyenyekevu uwaite wahusika wote ofisini kwako waombe wakupe " historia kamili" na wakupe mchakato mzima mpaka kufikia siku hii muhimu ya " Ground Breaking ceremony( uzinduzi wa Kazi ya ujenzi).

c) Ukipata Taarifa kamili, uwe na unyenyekevu, acha kiburi. Kiburi hakikusaidii wala haitasaidia jamii unayopaswa kuwatumikia ( unless una malengo tofauti). Kwa unyenyekevu mkubwa Waombe msamaha Wahisani wetu kwa kuwaingiza katika " siasa ya Arusha" ambayo hawahusiki nayo; awaombe msamaha wakina mama, watoto na jamii ya Wananchi wa Arusha wapenda maendeleo kwa kuwachafua na kuwaletea vurugu kiasi cha kuifanya Arusha ionekane kila leo ni mahali pa vurugu, kumbu vurugu husababishwa na viongozi wasiotumia busara na hekima. Uongozi ni busara na hekima siyo mabavu wala nguvu ya mamlaka.

Nimeyasema haya kuuchungu mkubwa. Mimi siko kwenye siasa, na wala sina interest na siasa. Siangalii uso w a mtu. Kama ambavyo niliaga kuwa " Nastaafu Party Politics, lakini nitapiga kelele pale maslahi ya Taifa langu yanavyokanyagwa" nitakuwa mwendawazimu kunyamaza wakati mradi wa Tshs Takriban 9 Billioni unahatarishwa na upuuzi na uzembe wa kiongozi mnoja mwenye kuendekeza propaganda zisizo na msingi.

Nawaomba sana Radhi wahisani wetu. Mtuvumilie siyo kwa ajili yetu bali kwa ajili ya kina mama na watoto walengwa wa huduma itakayotolewa na " Kituo cha Mama na Mtoto" ( propaganda ya Hospitali ya mke wa Lema zipuuzeni). Happy, umevumilia mengi katika miradi mingi uliyofadhili na kuisimamia. Usirudi nyuma. Timiza ndoto yako iliyoanza katika umri mdogo sana. Matunda yanaonekana pamoja na vikwazo vya mara kwa mara vya wapinga maendeleo. Viongozi, " Tenganisheni siasa na Maendeleo" Watumikieni Watanzania bila kuangalia nyuso zao, mrengo wao. Siasa ni sayansi na siasa sayansi ni utumishi.

By Dr Slaa
Source:Chingaone/Jamii Forums

Kama ni Rahisi Kununua Tuzo, Wanaosema Hivyo na Wao Wakanunue – Babutale

$
0
0
Babutale amezijibu shutuma za baadhi ya mashabiki nchini kuwa wasanii wa WCB wamekuwa wakinunua tuzo.

Akiongea na Prince Ramalove wa Kings FM, Tale alikuwa na maneno mafupi tu kuwajibu. “Kama ni rahisi na wao wakanunue,” alisema meneja huyo.

Jumamosi iliyopita Diamond na Harmonize walishinda tuzo za Afrimma zilizofanyika jijini Dallas, Marekani.

Alidai kuwa tuzo hizo ni za Tanzania nzima na imeonesha jinsi gani mashabiki wako nao pamoja. Amesisitiza kwa kuwaomba waendelee kuwapigia kura wasanii wote waliotajwa kwenye tuzo za MTV MAMA wakiwemo wasanii wake wa WCB, Diamond na Raymond.

Wengine ni Alikiba, Navy Kenzo, Yamoto Band na Vanessa Mdee.

Aunty Lulu Awachana Mr Bond na Wastara...Adai Alimuokota Mr Bond Jalalani na Kumlea

$
0
0
Bifu Jipya mjini.....Aliyekuwa mpenzi wa zamani wa Mr Bond Aunty Lulu ameibuka pasipo julikana na kuanza kuwashambulia kwa maneno Mr Bond na Mpenzi wake Wastara...

Ameandika haya kwenye ukurasa wake wa Instagram:

Auntylulukimwana
"Nilikuokota jalalani mbwa wewe hujui hata kuvaa..ulikuja kwangu umevaa suruali kama alusi mabele au kanda bongoman wa zamani..ukaishi kwangu hata kazi huna mbwa wewe nikakutafutia mwenyewe channel 10..tena nikakuasa usije kuniacha..maana wakikuona watakutaka ukasema hatuwez kuachana...umepata kazi kwa mgongo wangu mwenzangu ukadindisha na kuwapa mti baadhi ya mastar(siwataji japo nawajua)na huyo ngedere wako kwa ujane akaamua kuwa wako..kumbuka mm ndo nilikupa taarifa ya kifo cha mumewe,,,alfajiri tumepata taarifa tulikuwa tumelala..we si ndo uliniomba turudiane ulivyoachwa akaenda kwa mbunge?nilikataa kwa kuwa nna mtu tayari!!leo hii kakurudia..utaishia hvyohvyo kukimbiwa ngoja atokee mkubwa zaidi ya mbunge yakukute..na usirudi hapa"Amendika Aunty Lulu

Mr Bond Amjibu Auntylulu ' Nilipokuwa na Wewe Ulinikondosha Kwa Kero Nikawa Kama Mbuzi"

$
0
0
Bond Amjibu Auntylulu kupitia Ukurasa wake wa Instagram, Ameandika haya hapa chini baada ya Aunty Lulu Kudai alimuokota jalalani, kumlea na kumtafutia kazi ya kufanya Dar es Salaam..
____
From bond_bin_sinnan 
"Dah hii dunia hii jamani, Huyu nae sijui anamuda mrefu hajatoka kwenye magazeti?
Eti Leo anafufuka na kumtukana mke Wangu eti ameniiba mimi..
Hahahaha we Lulu wewe hebu muogope mungu wako wewe. Hivi una muda gani hata sura yangu hujawahi kuiona ? Zaidi ya miaka minne hata kuniona hujawahi Leo unaanza kuleta shida kwa mke Wangu.
We siunapenda umalaya na pombe sasa zimekukifu eti ndo unaamka usingizini? Basi kama umeamka Leo fahamu tulishaachana kitambo sana na Nina mke Wangu nampenda sana anaitwa Wastara
Naomba umuache ale raha kwa uwezo wake we subiri Global wakupe kiki upate mabwana wapya.
Nilipokuwa na wewe ulinikondosha kwa kero nikawa kama mbuzi wa sadaka mpaka kuku walinikimbia. Leo mtoto wa kiarabu ananisinga nang'ara navutia mpaka unanitamani tena unifuje. Hebu niache nipumue
Maskini sijui ndo uzee unakusumbua hahahaha.. Uwiii aleyo bhagosha lelaha le pogopogo lya bhose nzogi mlyee"Ameandika Mr Bond

Mr Bond na Mpenzi wake Mpya Wastara Juma

Zitto Atoa Neno Ugomvi wa RC Arusha na Godbless Lema

$
0
0
Kiongozi Mkuu wa ACT Wazalendo, Zitto Kabwe ameamua kutoa ya moyoni kufuatia hali iliyojitokeza jana mkoani Arusha wakati wa uzinduzi wa Hospitali ya Mama na Mtoto. Katika uzinduzi huo, Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo alisema kuwa eneo la hospitali hiyo lilitolewa na familia ya Nyaga Mawalla, jambo ambalo wananchi walilipinga wakishirikiana na Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema (Chadema) na kuzua sintofahamu kama inavyoonekana katika video hii….


Zitto kupitia akaunti yake ya Facebook ameandika hivi;
“Nakasirishwa sana kuona viongozi vijana wanafanya mambo ya hovyo. Mkuu wa Mkoa wa Arusha mdogo wangu Mrisho Gambo una dhamana zaidi Kwa vijana. Mnapofanya mambo ya kijinga mnaharibu nafasi ya vijana kuaminiwa zaidi. Kaa Na Mbunge Godbless Lema mnywe kahawa pale New Arusha Na muanze upya. Ndugu yangu Lema nashauri punguza munkari. Juhudi zako Arusha haziwezi kufutika kirahisi. Nakushauri kaa chini Na Mkuu wa Mkoa wako mpige mstari muanze Kazi upya Kwa pamoja.
Viongozi jiepusheni kuonyesha hasira zenu hadharani. Sio hekima.”

Mahakama Yamfutia Shtaka la Unyang’anyi wa Kutumia Silaha Scorpion

$
0
0
Mahakama ya Wilaya Ilala jijini Dar es Salaam leo imemfutia shtaka la  unyang’anyi wa kutumia silaha, Salum Njwete maarufu kwa jina la Scorpion baada ya upande wa mashtaka kuomba shtaka hilo liondolewe mahakamani hapo kwa sababu hawana nia ya kuendelea na kesi hiyo.

Mtuhumiwa huyo ambaye ni mkazi wa Buguruni kwa Mnyamani anatuhumiwa kumchoma visu na kisha kumtoboa macho, Said Ally mkazi wa Mabibo Hostel hivi karibuni.

Taarifa ya Uteuzi wa Mkuu wa Mkoa wa Arusha Kutenguliwa Inayosambaa Mitandaoni...Ikulu Yatoa Tamko

$
0
0
Hii  Taarifa (katika picha)  inasambazwa  mitandaoni  kwamba  Imetoka  IKULU. Mkurugenzi  wa  Mawasiliano ya  Rais ,Gerson Msigwa  kasema  ni  ya  uongo, imetengenezwa  na  watu  wenye  nia  ovu  hivyo  ipuuzwe

Lulu Diva, Amber Lulu Hakuna Bifu

$
0
0
Muuza sura kwenye video za Kibongo, Lulu Abass ‘Lulu Diva’ (pichani juu) na mwenzake Amber Lulu (pichani chini) hawana bifu lolote isipokuwa kuna watu wana mpango wa kuwagom-banisha.

Akichonga na Risasi Vibes, Lulu Diva alifunguka kuwa awali aliposikia kuwa Amber alimpaka matope kwenye ‘interview’ aliyofanya na redio fulani Bongo, alipaniki na kumtafuta ili amueleze kulikoni, lakini Amber alimwambia hakuna kitu kama hicho na kumtaka kuchunguza mwenyewe.

“Nilichunguza na kukuta kumbe si kweli, niligundua ni watu wasiopenda ushoga wetu ndiyo walikuwa wanajaribu kutukosanisha na si vinginevyo,” alisema Lulu Diva.

Wema Sepetu, Jackline Wolper, Bosi wa GSM ndani ya China kunani?

$
0
0
Kwenye Instagram zao mastaa hao wamepost waki safiri toka dar siku moja na wote wamepost picha wakiwa dubai same day then wote wamepost wakiwa china same place Canton Kama Picha zinavyoonesha Location ila hawajapiga picha pamoja.. Ambapo mdogo wa GSM counselor Salaah amepost akiwa Canton fair na wema na wolper wakipost wakiwa canton railway station same area ila wamekuwa makini kutopiga picha pamoja au labda hawafahamiani. Au labda ma baby wao idriss na harmonize ndo wamegharamia safari yao ya china.. Au labda yule MCM aliyempost kawasponso



Jeshi la Polisi Dar Laua Majambazi Hatari 6

$
0
0
Watu sita wanaotuhumiwa kuwa majambazi hatari, wameuawa katika majibizano ya risasi na Polisi katika eneo la Mbezi kwa Yusuf Makondeni katika Manispaa ya Kinondoni, Dar es Salaam.

Kwa mujibu wa Kaimu Kamanda wa Kanda Maalumu, Naibu Kamishna wa Polisi, Lucas Mkondya, watuhumiwa hao waliuawa katika majibizano ya risasi na Kikosi Maalumu cha Kupambana na Ujambazi wa Kutumia Silaha.

Mkondya alisema wamepata taarifa kutoka kwa raia mwema kuwa kuna kikundi cha watu wenye silaha, wamejipanga kufanya tukio la ujambazi kwa kutumia silaha kwa mfanyabiashara aliyekuwa akitoka Benki ya Diamond Trust Bank (DTB), tawi la Barabara ya Nyerere, ambaye angepita katika barabara hiyo kwenda mkoani Morogoro.

Alisema baada ya kupata taarifa hizo, polisi waliweka mtego na majambazi hao wakitumia gari aina ya Toyota Carina lenye namba za usajili T970 DGZ rangi ya fedha, walionekana wakilifukuza gari la mfanyabiashara huyo, kisha kulipita na kumsimamisha kwa nguvu.

“Majambazi wawili wakiwa na bastola walishuka katika gari hilo. Baada ya kugundua kuwa wameingia kwenye mtego wa polisi, walianza kufyatua risasi kwa askari wakitumia bastola na wenzao waliokuwa wamejaa kwenye gari yao walianza kushuka huku wakifyatua risasi kuelekea kwa askari,” alisema Kaimu Kamanda Mkondya.

Alisema kutokana na hali hiyo, askari walianza kujibu mashambulizi na kuwaua majambazi hao na baada ya upekuzi, zilipatikana bastola mbili, moja ya kijeshi aina ya Chinese ikiwa na risasi moja ndani ya kasha la risasi; na nyingine aina ya Browning ikiwa imefutwa namba zake na maganda sita ya risasi yaliyookotwa katika eneo la tukio.

Miili ya watuhumiwa hao imehifadhiwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) na upelelezi unaendelea ili kubaini mtandao mzima wa ujambazi.

Katika tukio lingine la Oktoba 17, mwaka huu saa 2:00 usiku katika maeneo ya Tegeta Masaiti, watuhumiwa watatu wa ujambazi wakiwa wamepakizana kwenye pikipiki aina ya Fekon yenye namba MC370 BEY, wakiwa na bunduki aina ya shotgun iliyokatwa mtutu na kitako, walivamia duka la Abdallah Juma (46), mkazi wa Tegeta na kupora fedha za mauzo na kuiba vocha za mitandao mbalimbali, ambazo thamani yake haijafahamika.

“Polisi baada ya kupata taarifa waliwafukuza majambazi hao, walipoona wanakaribiwa na askari, walitupa chini begi walilokuwa nalo na kutelekeza pikipiki yao kisha kukimbia, begi lilipopekuliwa lilipatikana na silaha hiyo,” alisema.

Aidha, wananchi wenye hasira waliendelea kuwakimbiza majambazi hao na kumuua mmoja huku wengine wakikimbilia kusikojulikana.

Katika hatua nyingine, Mkondya alisema wamekamata watuhumiwa wawili wa unyang’anyi kwa kutumia nguvu wakiwa na pikipiki moja na funguo bandia 75.

Alisema watuhumiwa hao, Ally Makwega (53) mkazi wa Tandika na Fabian Greyson (39) mkazi wa Yombo walikamatwa Oktoba 4, mwaka huu saa 6:00 usiku.

Watuhumiwa hao walikamatwa wakiwa na pikipiki yenye namba MC292 AMD aina ya Boxer rangi nyekundu, wanayoitumia kufanya uhalifu, wakiwa na funguo bandia 75 ambazo huzitumia katika kuvunja nyumba mbalimbali ya biashara za kulala wageni, maghala ya kuhifadhia bidhaa na maduka.

Baada ya watuhumiwa hao kuhojiwa, walikiri kuhusika na matukio mbalimbali ya uvunjaji wa maghala na kuiba katika mikoa ya Dar es Salaam, Morogoro na Dodoma.

Watuhumiwa hao watafikishwa mahakamani baada ya upelelezi kukamilika.

Kamati ya Bunge Yakataa faini ya 500,000/- Kwa Kila Kosa Barabarani

$
0
0
Kamati  ya Bunge ya Katiba, Sheria na Utawala imekataa mapendekezo ya kufanyia marekebisho Sheria ya Leseni za Uchukuzi ya mwaka 1973 yenye lengo la kuongeza kiwango cha adhabu ya faini hadi kufikia asilimia 500 kwa watakaokiuka masharti ya leseni hizo.

Mapendekezo hayo yaliwasilishwa mbele ya kamati hiyo mjini Dodoma jana na Mamlaka ya Usafiri wa Majini na Nchi Kavu (Sumatra).

Baada ya kuyakataa mapendekezo hayo, kamati hiyo imetoa muda wa siku mbili kwa Sumatra kuhakikisha inawasilisha mbele ya kamati hiyo mapendekezo yanayokubalika.

Sumatra inapendekeza kuongeza kiwango cha adhabu ya faini kutoka kati ya Sh 10,000 na Sh 50,000 hadi Sh 200,000 na 500,000 kwa watoa huduma za uchukuzi, watakaokiuka masharti ya leseni zao.

Mwenyekiti wa kamati hiyo, Mohammed Mchengerwa alisema mapendekezo hayo, yatazidi kuwaongezea mzigo Watanzania badala ya kuwasaidia.

Alisema kiwango hicho cha faini kubwa, kamwe hakitazuia tatizo la ajali za barabarani, zaidi ya kuongeza ukubwa wa tatizo la rushwa.

“Serikali ya Awamu ya Tano imejipanga kuwasaidia wananchi, lakini mapendekezo haya yatazidi kuwaongezea mzigo kwa sababu kiwango cha faini hizi kama kitapitishwa, watoa huduma za uchukuzi watahamishia hasara yao kwa wananchi,” alisisitiza.

Aliitaka mamlaka hiyo, kwenda kuyafanyia kazi tena mapendekezo hayo kwa kuwasiliana na Mwanasheria Mkuu wa Serikali na kuwasilisha viwango vya faini vinavyokubalika.

Mmoja wa wajumbe wa kamati hiyo, Joseph Mhagama ambaye pia ni mbunge wa Madaba, alisema mapendekezo hayo hayana nyongeza yoyote, itakayoisaidia serikali katika kudhibiti tatizo la ajali barabarani.

“Kwa sasa serikali imeweka nguvu zake katika kupunguza ajali za barabarani, lakini kiwango cha faini hizi hakina uhusiano wowote na jitihada hizi zaidi ya kuiongezea Sumatra mapato na kuwapa mzigo walipa kodi,” alisema.

Akiwasilisha mapendekezo ya mamlaka hiyo mbele ya Kamati hiyo, Mkurugenzi Mkuu wa Sumatra, Gilliard Ngewe alisema mapendekezo ya marekebisho ya sheria hiyo, yamelenga  kuiboresha zaidi sheria hiyo ya leseni za uchukuzi.

Alisema marekebisho hayo, pia yatasaidia mamlaka hizo kuendana na mahitaji ya sasa hasa katika eneo la adhabu ya faini, hali itakayopunguza kiwango kikubwa cha kukiukwa kwa masharti ya leseni hizo za uchukuzi.

Kauli ya Mkuu wa Mkoa wa Arusha Baada ya Habari Kuzagaa Ametumbuliwa

$
0
0
Saa chache baada ya kusambaa taarifa zilizokanushwa na Ikulu zilizodai kuwa uteuzi wa Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo umetenguliwa, Mkuu huyo wa Mkoa ameandika ujumbe mzito unaoonekana kuwalenga mahasimu wake.

Taarifa hizo zilizothibitishwa kuwa za uongo ziliibuka siku moja baada ya tukio la kusikitisha la kuzuka ugomvi wa maneno kati ya Mkuu huyo wa Mkoa na Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema katika hafla ya uwekaji wa jiwe la msingi kwenye hospitali ya mama na mtoto inayojengwa eneo ya Burka nje kidogo ya jiji la Arusha, mbele ya wafadhali wa mradi huo.

Kupitia ukurasa wake wa Facebook, Gambo ameandika, “Mara nyingi ukisikia huyu ana kufa leo au kesho, huwa anaishi miaka mingi zaidi! Nazungumzia utamaduni wetu sisi Watanzania!”

Mvutano kati ya Gambo na Lema ulianza tangu Gambo alipokuwa Mkuu wa Wilaya ya Arusha huku kila mmoja akimtupia lawama mwenzake kwa kutofuata taratibu na protokali.

RC Mrisho Gambo apigiwa simu Rais Magufuli. Soma walichozungumza

$
0
0
Mkuu wa Mkoa wa Arusha amesema kuwa Rais Dkt John Pombe Magufuli amempigia simu  na kumwambia kuwa ana imani naye na kuwa hajafikiria kutengua uteuzi wake labda kumpandisha cheo.

Hayo yamesemwa jana na Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari  baada ya taarifa kuhusu Rais kutengua uteuzi wake kusambaa kwenye mitandao ya kijamii.

Mkuu wa mkoa alisema kuwa alipigiwa simu nyingi na watu wengi lakini kabla hajawajibu Rais Magufuli akampigia simu na kumueleza kuwa ana imani naye na kuwa ahakikishe anawatumikia wananchi wa Arusha kwani yeye sio bosi wao bali ni mtumishi wao.

Pia mkuu wa mkoa alieleza kuwa Rais amempa maagizo ya kuhakikisha anasimamia wananchi wa mkoa wa Arusha walipe kodi kwa ajili ya maendeleo ya mkoa huo na nchi kwa ujumla.

Aidha, ili kuthibitisha kuwa ni Rais Magufuli ndiye aliyempigia simu, Rais aliomba kuongea na yeyote aliyekuwa karibu ndipo mkuu wa mkoa akampa mmoja wa waliokuwa katika mkutano huo kuthibitisha kuwa ni Rais Magufuli.

Habari ya kutenguliwa kwa mkuu wa mkoa wa Arusha imekuja ikiwa ni siku moja baada ya kuibuka mvutano mkali kati ya mkuu huyo wa mkoa na Mbunge wa Arusha Mjini Godbless Lema kuhusu mradi wa ujenzi wa hospitali itakayotoa huduma kwa mama na mtoto mkoani humo.

Jipatie Dawa Asili za Kutengeneza Shepu, Kuondoa Michirizi Chunusi, Kurefusha Nywele Toka Markson Beauty Products

$
0
0
HABARI NJEMA MARKSON BEAUTY PRODUCTS
Baada ya kupata cheti cha bidhaa bora kwa mwaka 2015-2016, Sasa kampuni hii inasambaza huduma zake ndani na nje ya nchi kwa vibali maalum. Bidhaa zetu zimetengenezwa kwa mimea na matunda na kudhibitishwa. Hazina kemikali wala madhara. DAWA ZETU NI YA:-

  1. kurefusha nywele na kuzuia kukatika ovyo @100,000/=
  2. Kuongeza shepu (hips na makalio) kwa/= (a)Dawa ya kunywa au kupaka @150,000/=(b)Vidonge @170,000/=
  3. Kuwa mweupe na softi mwili mzima kwa:- (1)Mafuta @100,000/= (11)Vidonge @150,000/=
  4. Kupunguza unene na manyama uzembe @120,000/=
  5. Kuongeza uume pamoja na nguvu za kiume kwa:-(a) Gely ya kupaka @100,000/= (b) Vidonge maalum @120,000/= (c) Handsome up original @170,000
  6. Kuondoa mvi milele zisiludi tena @100,000/=
  7. Kuongeza unene wa mwili mzima na uzito @120,000/=
  8. Kupunguza tumbo (kitambi) na nyama za pembeni kwa:- (a) Dawa ya kunywa au kupaka @120,000/= (b) Mkanda wa kawaida @100,000/= (c) micro-computer belt unaovaibret @200,000/=
  9. Kupunguza maziwa na kuyasimamisha @90,000/=
  10. Kushepu miguu na kuwa minene @100,000/=
  11. Kuondoa mipasuko mwilini (michirizi) @90,000/=
  12. kubana uke na kuongeza hamu ya tendo la ndoa kwa mwanamke @100,000/=
  13. Taiti za hips na makalio @150,000/=           
NB: Hakikisha unapata risiti yenye muhuri halisi wa MARKSON CO pamoja na garantii kwa bidhaa halisi. Wasiliana nasi :-(+255) 0767447444 na 0714335378 Google MARKSON BEAUTY.
Follow us
@Markson_beauty_pr
@Markson_beauty_pr

Watumia Jina la Tibaijuka Kutapeli

$
0
0
MBUNGE wa Muleba Kusini, Profesa Anna Tibaijuka amehadharisha umma dhidi ya ukurasa uliotengenezwa katika mtandao wa kijamii wa Facebook ukitumia jina lake, kuwa anakaribisha maombi ya watu wa kuajiriwa kwenye shirika linalosaidia watu kuondokana na umasikini.

Profesa Tibaijuka ambaye amesisitiza kuwa ukurasa huo si wake, ametaka taarifa zilizomo zipuuzwe akisema umetengenezwa na matapeli wanaochafua jina lake ambao wanadai watu watakaopitishwa, watapata fursa ya kufanya kazi katika nchi mbalimbali Afrika.

“Ukurasa huu sio wa kwangu wala siufahamu. Hivyo basi na taarifa zote zilizoandikwa kwenye ukurasa huu ni uongo na hazitoki kwangu…nawaomba mpuuze taarifa hizi na wala msitume taarifa zenu kupitia parua pepe kama inavyoelekeza,” Profesa Tibaijuka aliliambia gazeti hili jana.

Taarifa zilizopo kwenye ukurasa huo, zinakaribisha watu kutuma maombi ya kufanya kazi na shirika lisilo la kiserikali (NGO) linaloshughulika na kupunguza umasikini uliokithiri katika Afrika.

Wenye uhitaji wanatakiwa kutuma taarifa kwenye barua pepe iliyoonesha jina la Profesa Tibaijuka huku ikielezwa kuwa sifa zinazotakiwa ni kuanzia elimu ya sekondari na kwamba wanaohitaji wawe tayari kufanya kazi katika nchi nyingine za Afrika.

Aidha, taarifa hizo zinasisitiza kuwa wanachama wa skauti na klabu ya Lions watapewa kipaumbele. Mbunge huyu aliyewahi kuwa Mkurugenzi wa Shirika la Makazi Duniani (UN-Habitat), alisema taarifa juu ya utapeli huo zimekwishavifikia vyombo vya usalama na wanaendelea na uchunguzi kubaini na kuwakamata mara moja wahusika.

Flora Mvungi Kaitaja Kashfa Ambayo Hatoisahau Maishani Mwake…

$
0
0
Ni headlines za msanii Flora Mvungi ambae leo October 19,  2016 amefunguka na kutaja kashfa ambayo hatoweza kuisahau maisha mwake.


Mimi sio mgeni macho mwa watu na wengi wananifahamu tabia yangu ikoje na wengi wanafahamu page yangu ya instagram ikoje na sijawahi kumtukana mtu bila sababu ya msingi kitu kikubwa’
‘Kikubwa ni kwamba ilivyotokea taarifa kwamba mimi ndio mmiliki wa ukurasa wa instagram uitwao Marashi ya pemba iliniumiza sana na kuniharibia hata kwa watu wengi ninaowaheshimu kwahiyo ningekupenda kuwaambia mashabiki wangu kwamba zile taarifa za mimi kumiliki huo ukurasa sio za kweli’


Beny Kinyaiya Afungukia Ishu Ya Ushoga, Awaanika Wanaye

$
0
0
From Global
Mtu Kati: Vipi katika kupigapiga ‘gemu za nje’, umewahi kupata mtoto au watoto?

Kinyaiya: Yaah! Nina watoto wawili, wa kwanza anaitwa Ben Kinyaiya Junior, ana miaka minne na nusu na wa pili anaitwa Nilla, huyu ni wa kike na ana miaka mitatu.

Mtu kati: Kwa muda mrefu kumekuwa na madai ambayo hayajathibitishwa kwamba unajihusisha na mapenzi ya jinsia moja (ushoga), unalizungumziaje hili?

Kinyaiya: Ni mawazo yao tu, kwanza nikwambie mimi huwa siabudu majungu. Watu walianza kunizungumzia vibaya kitambo wakinihusisha na hayo mambo, wengine wakawa wanasema eti hawajawahi kuniona na mwanamke, nikawapuuzia tu. Baadaye kibao kikageuka, wakaanza kuniita eti mimi ni malaya kwa sababu nina wanawake wengi, pia sikuwajali. Nikaendelea na maisha yangu na sasa hivi ndiyo kama hivyo tena, tayari nina watoto wawili, waliokuwa wakinizushia mambo mabaya wote wamenyamaza kimya.

Mi nafanya shughuli zangu za kimaendeleo, sina haja ya kujibizana na watu wanaozusha maneno ya uongo juu yangu, kama mtu anahisi mimi nina matatizo yoyote basi aniunganishe na dada yake atampa majibu (anacheka).

Wema Sepetu a.k.a Tanzania Sweatheart Kuolewa Hivi Karibuni

$
0
0
Kwa taarifa nilizozinyaka hivi karibuni hukooo Instagram ni kuwa kipenzi cha wengi ( najua wengi mtabisha) si mwingine mrembo wetu Miss TZ 2006 na CEO wa kampuni ya ENDLESS FAME the one & only WEMA ABRAHAM ISAC SEPETU anaolewa hivi karibuni na model anaekuja kwa spidi ya 4G CALISAH ABDULHAMID.

Though hawaja comfirm wenyewe kuhusiana na habari hii ila nimejiongeza tu mwenyewe baada ya kuzinyaka picha hizi...

Feza Kessy Anahisi Nando Anadata ‘Atafutwe na Asaidiwe’

$
0
0
Staa aliyewahi kuiwakilisha Tanzania katika shindano la Big Brother Africa, Feza Kessy, amesema kuwa anaamini Nando aliyewahi kushiriki naye kwenye shindano hilo, amepatwa na tatizo au anaugua kwakuwa tabia anazozionyesha zinampa mashaka.

Akiongea kwenye kipindi cha Kubamba kupitia Times FM, Feza amesema anaona akili ya Nando kama imevurugika kwa sasa. Anasema amekuwa tofauti na Nando, yule kijana mwenye nidhamu na mpole aliyekuwa akimfahamu.

“Naamini Nando ana tatizo asaidiwe,” alisema Feza. “Sijui kwanini lakini naamini Nando ana something hayupo sawa, sio yule Nando ninayemfahamu, naomba atafutwe asaidiwe,” alisisitiza.

Feza ambaye kwa sasa ni mtangazaji wa Choice FM, amedai kuwa aliwahi kukutana na Nando na akampa noti ya shilingi elfu 10. Anasema badala yake yake staa huyo aliitupa chini kwa madai kuwa haiwezi kumsaidia kitu.

Juma Nature: Kuna Watu Wanahonga Ili Ngoma Zangu Zisipigwe

$
0
0
Ukizungungumzia historia ya muziki wa Bongo Flava, haiwezi kukamilika bila kulitaja jina la mkongwe Juma Kassim Nature aliyewahi kutamba ngoma kama ‘Jinsi Kijana’, ‘Hili Game’ na zingine kibao.

Hatimaye mkongwe huyo amaibuka na kudai kuwa kuna watu wanahonga ili nyimbo zake na za TMK Halisi zisichezwe redioni.

Nature amesema kuwa miongoni mwa watu hao ni uongozi wake wa zamani lakini hakuwa tayari kuwataja kwa majina.

“Sasa hivi kuna urasimu, kuna watu wanaenda kuhonga nyimbo zangu zisipigwe za Halisi zisipigwe, wapo watu wanafanya issue kama hizo na tayari tumeshaingia in deep kujua nini tatizo kwanini nyimbo hazichezwi,” ameniambia Nature nilipozungungumza naye nyumbani kwake Temeke.

Ikumbukwe Nature alikuwa akifanya kazi chini ya kundi la Wanaume Family kundi linalomilikiwa na Said Fella kabla ya kujitoa kwenye kundi na baadhi ya wasanii wengine waliokuwa kwenye kundi hilo na kuanzisha kundi lao jipya linalofahamika kama Wanaume Halisi.
Viewing all 104688 articles
Browse latest View live




Latest Images