Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104690 articles
Browse latest View live

Jamaa Yake Amemwekea Tego, Msichana Yupo Tayari Kunipa Papucha ila Anaogopa Tutanasiana au Ntapata Tatizo

$
0
0
Nimempata dada mmoja mitaa fulani, ni mzuri sana na she is sexy. Kiukweli tumependana nami nilivyomuona tu siku ya kwanza pale ofisini nilimpenda nikaomba tuwe na ukaribu. Tukaanza ukaribu basi juzi juzi hapa nikamwambia mi natamani mambo flani. Yule dada alinikubalia lakini akasema shida kubwa ni kuwa jamaa yake mshirikina alimwekea dawa hivyo tukikutana naweza pata matatizo, anasema watu wa Morogoro/waruguru ndo zao hizo.

Sasa hajui atafanyaje maana anasema aliwahi achana na jamaa akawa na mtu mwingine yule jamaa aliyetembea naye alipata matatizo makubwa sana hadi ikabidi yule dada arudi akamwambie Mluguru amwachie jamaa awe salama. Toka kipindi hicho dada amekuwa hana amani anashindwa sasa afanyeje. Aliniambia maneno haya kwa uchungu sana nami nikimwona kiukweli anataka sana nimkandamize yaani hata tukiongea hivi namwona tu jinsi macho yanavyochoka nami mzuka unapanda natamani nimnaniii hivyo hivyo lakini ananikataza anasema coz she loves me hapendi nipate shida.

Sasa hapa wadau nifanye nini? Mambo kama haya sisi wengine hatushiriki ushirikina matatizo yetu ni K tu lakini kwa waganga hatujawah kwenda. Sasa hapo nafanyaje?

Tusaidiane tafadhali maana hali inakuwa ngumu sana kwetu sote.

By Komeo

Safari ya Ulaya Imeiva – Ulimwengu

$
0
0
Mshambuliaji wa Tanzania Thomas Ulimwengu aliyemaliza mkataba wake na klabu ya TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo amekiri tayari kuna vilabu kadhaa vya Ulaya ambavyo vimeonesha nia ya kutaka kumsajili.

Ulimwengu ambaye hakutaka kuongeza mkataba mwingine TP Mazembe amesema, anachosubiri kwa sasa ni wakati ufike ili aweze kusaini mkataba na kuanza maisha mapya barani Ulaya. Nyota huyo aliyecheza na Samatta kabla ya Samagoal kutimkia Ubelgiji hakuwa tayari kuvitaja vilabu vilivyoonesha nia ya kutaka saini yake, lakini akaahidi kila kitu kitakuwa wazi pindi atakapokamilisha usajili wake.

“Nilikuwa nimeshapanga tangu zamani kwamba, nikimaliza mkataba wangu na TP Mazmbe ni lazima nitoke kwasababu nilijaribu kutoka nikiwa ndani ya mkataba lakini ilishindikana kwahiyo nikapanga mkataba ukimalizika nitasogea mbele kwa ajili ya mafanikio zaidi, kilichobaki ni kuomba Mungu ili mambo yaende kama yalivyopangwa.”

“Ofa tayari zipo kilichobaki ni kukamilisha, ni kufikiria tu niende wapi na manager wangu kwa ajili ya kukamilisha mchakato.”

“Kwa sasa sifikirii tena kucheza Afrika, ila siwezi kuziweka wazi timu ambazo zinanihitaji, lakini baada ya kusaini kila kitu kitakuwa wazi.”

Faida aliyonayo Ulimwengu ni kuwa mchezaji huru kwahiyo sio lazima asubiri hadi dirisha la usajili lifunguliwe, kwa mujibu wa taratibu za FIFA, mchezaji ambaye amemaliza mkataba wake na timu aliyokuwa akiitumikia mwanzo, anaweza kusajiliwa kwenda klabu nyingine bila kusubiri kipindi cha usajili kufunguliwa.

Tazama Video ya Diva Loveness Akicheza Huku Akionyesha Kiuno na Nyonga zake

PICHA:Hans Van Pluijm Alivyotua Mazoezini Kuagana na Wachezaji wa Yanga

$
0
0
Baada ya kuamua kujiuzulu nafasi ya ukocha mkuu wa Yanga, Hans van Pluijm alienda kwenye mazoezi ya klabu hiyo kwa ajili ya kuagana na wachezaji wake pamoja na baadhi ya viongozi wa benchi la ufundi waliosalia kwenye klabu hiyo.

Van Pluijm aliamua kujiuzulu nafasi hiyo baada ya kupata taarifa kwamba, uongozi wa Yanga umemleta kocha kutoka Zambia George Lwandamina ili kuchukua nafasi yake.

Kwa sasa, timu itakuwa chini ya kocha Juma Mwambusi ambaye alikuwa msaidi wa Hans van Pluijm mpaka hapo klabu itakapomtangaza kocha mkuu.

Rose Ndauka Aswekwa Lupango

$
0
0
Staa wa Bongo Movie Rose Donatus Ndauka anadaiwa kuswekwa lupango kwa takriban saa nne kabla ya kuchomolewa kwa dhamana.

Sosi wetu ambaye ni mtu wa karibu wa Rose alinyetisha kuwa, staa huyo alikuwa kwenye misele na gari lake maeneo ya Kawe jijini Dar ambapo alitanua barabarani hivyo akakamatwa kisha kukaibuka tafrani iliyosababisha kufikishwa kwenye Kituo cha Polisi cha Kawe alikosota kwa muda huo kabla ya kuachiwa.

Baada ya Wikienda kunyetishiwa habari hiyo, lilimtafuta Rose ambaye alifunguka kwa kifupi:
“Duh! Hii ishu mmeipata? Kweli ninyi siyo watu wa mchezomchezo, baada ya kuandika kuhusu Lebo ya Ndauka mnataka umbeya tu, sasa hivi nna lebo imeanza na msanii Casso aliyeimba Wimbo wa Kitonga.”

Rose alisema kukaa kwake lupango amejifunza kwani saa nne aliziona kama miezi na kuwakumbusha watu kuheshimu sheria za usalama barabarani.

Bond: Watoto Wa Wastara Hawakupenda Aolewe

$
0
0
SIKU chache baada ya kuripotiwa kupika na kupakua na staa wa filamu za Kibongo, Wastara Juma, Bond Suleiman ameibuka na kusema watoto wa mke huyo wa zamani wa Mbunge wa Donge, Sadifa Juma, hawakupenda mama yao aolewe na mtu mwingine zaidi yake.

Akipiga stori na Za Motomoto News, Bond alisema alipokuwa kwenye ndoa, watoto hao walimfuata na kumwambia kuwa hawakufurahishwa mama yao kuolewa na mtu mwingine kwa sababu ya mapenzi ya dhati aliyokuwa akimuonesha mama yao enzi za uhusiano wao.

“Upendo wangu ndiyo uliomrudisha Wastara maana niliamua kubadilika na kuachana na pombe kwa ajili yake, nawaomba wanawake wanaonisumbua kunitaka kimapenzi waache kwani ninaye Wastara, mwanamke wa maisha yangu, siwezi kumsaliti tena, ndani ya mwaka huu tutafunga ndoa,” alisema Bond ambaye pia ni muigizaji.

Wapi Ney wa Mitego?

$
0
0
Fiesta not reachable, duuuuh.....!!

Longa nasi msaani wetu Ney wa mitego, nini kimekukuta? Au ulikuwa kanjanjaa bro ukatulisha matango poli..!?

Nimemis ili ngoma, ITAFAHAMIKA TU.. au unasoma game uje kama KING GK?

Maisha mema brooo, mwenzio nimeshakuwa mganga wa kienyeji. Naamka na kaniki, naenda kwenye kijumba cha kazi aka Msonge.. naagiza kuku na mbuzi kwa sana, siagizi tembele..

Rais Magufuli ametajwa kuwania tuzo ya ‘Forbes Africa Person of The Year’, ingia hapa kumpigia kura

$
0
0
Rais Dkt John Pombe Magufuli ametajwa kuwania tuzo ya ‘Forbes Africa Person of The Year.’

Anachuana na watu wengine wanne wakiwemo: Rais wa Mauritania, Ameenah Gulib, Mwanzilishi wa Capitec Bank, Michiel Le Roux na Thuli Madonsela wa Afrika Kusini pamoja na watu wa Rwanda.

Zimebaki siku 22 za kupiga kura. Unaweza kumpigia kura Rais Magufuli kwa kubonyeza hapa. Hadi sasa Rais Magufuli anaongoza kwa asilimia nyingi (73%).

Mwaka huu tuzo hizo zitatolewa jijini Nairobi, Kenya November 17.

Wafuatao ni washindi wa tuzo hiyo miaka ya nyuma

Mohammed Dewji (Tanzania)– 2015
Aliko Dangote (Nigeria)– 2014
Akinwumi Adesina (Nigeria) – 2013
James Mwangi (Kenya) – 2012
Sanusi Lamido Sanusi (Nigeria)- 2011

Jipatie Dawa Asili za Kutengeneza Shepu, Kuondoa Michirizi Chunusi, Kurefusha Nywele Toka Markson Beauty Products

$
0
0
HABARI NJEMA MARKSON BEAUTY PRODUCTS
Baada ya kupata cheti cha bidhaa bora kwa mwaka 2015-2016, Sasa kampuni hii inasambaza huduma zake ndani na nje ya nchi kwa vibali maalum. Bidhaa zetu zimetengenezwa kwa mimea na matunda na kudhibitishwa. Hazina kemikali wala madhara. DAWA ZETU NI YA:-

  1. kurefusha nywele na kuzuia kukatika ovyo @100,000/=
  2. Kuongeza shepu (hips na makalio) kwa/= (a)Dawa ya kunywa au kupaka @150,000/=(b)Vidonge @170,000/=
  3. Kuwa mweupe na softi mwili mzima kwa:- (1)Mafuta @100,000/= (11)Vidonge @150,000/=
  4. Kupunguza unene na manyama uzembe @120,000/=
  5. Kuongeza uume pamoja na nguvu za kiume kwa:-(a) Gely ya kupaka @100,000/= (b) Vidonge maalum @120,000/= (c) Handsome up original @170,000
  6. Kuondoa mvi milele zisiludi tena @100,000/=
  7. Kuongeza unene wa mwili mzima na uzito @120,000/=
  8. Kupunguza tumbo (kitambi) na nyama za pembeni kwa:- (a) Dawa ya kunywa au kupaka @120,000/= (b) Mkanda wa kawaida @100,000/= (c) micro-computer belt unaovaibret @200,000/=
  9. Kupunguza maziwa na kuyasimamisha @90,000/=
  10. Kushepu miguu na kuwa minene @100,000/=
  11. Kuondoa mipasuko mwilini (michirizi) @90,000/=
  12. kubana uke na kuongeza hamu ya tendo la ndoa kwa mwanamke @100,000/=
  13. Taiti za hips na makalio @150,000/=           
NB: Hakikisha unapata risiti yenye muhuri halisi wa MARKSON CO pamoja na garantii kwa bidhaa halisi. Wasiliana nasi :-(+255) 0767447444 na 0714335378 Google MARKSON BEAUTY.
Follow us
@Markson_beauty_pr
@Markson_beauty_pr

Edward Lowassa Anena Mwaka Mmoja wa Rais Magufuli

$
0
0
 Aliyekuwa mgombea urais kupitia Chadema, Edward Lowassa amechambua mwaka mmoja wa uongozi wa Rais John Magufuli tangu aingie madarakani akisema kuna mafanikio machache katika baadhi ya maeneo, lakini maisha ya wananchi yamezidi kuwa magumu.

Lowassa ambaye katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 25, 2015 aliungwa mkono na vyama vya upinzani vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), alisema hayo jana katika andishi lake kwa vyombo vya habari.

Mwanasiasa huyo aliyewahi kuwa waziri mkuu katika Serikali ya Awamu ya Nne kabla ya kujiuzulu mwaka 2008, amesema katika andishi hilo kwamba, “kile ambacho tulikisema wakati ule kwa nini tunataka mabadiliko, hivi sasa kila mtu anakiona.

“Kwamba pamoja na mafanikio machache katika baadhi ya maeneo, lakini maisha yamezidi kuwa magumu, ajira imeendelea kuwa bomu linalosubiri kulipuka, elimu bure iliyoahidiwa siyo inayotekelezwa, utumishi wa umma umekuwa kaa la moto.”

Rais Magufuli Aongoza Kura Kuwania Tuzo ya ‘Forbes Africa Person of The Year’

$
0
0
Rais John Magufuli anaongoza  kura za kuwania tuzo ya ‘Forbes Africa Person of The Year’, ambayo hutolewa kwa watu walioonyesha mchango kwa jamii.

Huku zikiwa zimebaki siku 21 kwa mshindi wa tuzo hiyo kutangazwa, Rais Magufuli anachuana na Rais wa Mauritius,  Ameenah Gulib;  Mwendesha Mashtaka wa Afrika Kusini, Thuli Madonsela; Mwanzilishi wa Capitec Bank, Michiel Le Roux na Taifa la Rwanda.

Mpaka jana jioni, Dk Magufuli alikuwa anaongoza kwa asilimia 75 likifuata Taifa la Rwanda na nafasi ya tatu alikuwa Madonsela wa Afrika Kusini.

Rais Magufuli anayetimiza mwaka mmoja madarakani wiki ijayo, utendaji wake umeonekana kuwagusa wananchi wa kipato cha chini, hasa kwa falsafa yake ya Hapa Kazi, uwajibishaji na mikakati yake ya kubana matumizi ili kuokoa fedha kwa kuzuia sherehe zisizo na tija.

Diamond Platnumz Awatupia Madongo Walio Kuwa Wanasema Hajanunua Nyumba South Afrika...Adai Uswahili wake Unamlipa

$
0
0
Diamond Jana amefika kwa mara ya kwanza kwenye nyumba ambayo alinunua South Afrika na Kuandika Yafuatayo....

"Asa kunya nakunya mie makalio yanawauma wengine, eti inahuu....? Wambie wasininunie mie, wakazane....halaf hii clip naomba wanangu mnisaidie kuwatag wote waliokuwa busy kupost na kuzungumza Kuwa nyumba hii si yangu....waambie hizi ndio kwanza rasharasha clip hata kupost sijaanza bado....soon naamia ndani😂😂...halaf nlisahau, wakikwambia mie mswahili wambie Mswahili haswaaa👌... halaf uswahili wangu najua kuutumia na umefanya leo niwe na kibanda south asa wao Uzungu wao Umewapa mini"

UKOCHA: Pluijm Amwaga Mboga Yanga

$
0
0
Usemi wa Waswahili kuwa, ukimwaga ugali, nami namwaga mboga umetimia kwa klabu ya soka ya Yanga  ambayo licha  ya uongozi wake jana kukanusha kuajiriwa kwa kocha Mzambia George Lwandamina na kuachana na Mdachi Hans van der Pluijm, mzungu  huyo ametangaza kujiuzulu kazi hiyo.

Mapema jana,  katibu mkuu wa Yanga, Baraka Deusdedit alisema uongozi wao hauna taarifa  za ujio wa Lwandamina wala haujafanya mawasiliano yoyote na mkufunzi huyo. “Kwanza, hizo taarifa nasikia kwako, hatujazungumza naye na wala hatujui kama amekuja, anaweza kuwa amekuja kwa shughuli zake. Kocha Yanga ni Hans Pluijm,” alisema Baraka.

Lwandamina alikanusha akisema kwamba ujio wake nchini hauna maana kwamba amekuja kusaini mkataba Yanga, ingawa alikiri kwamba timu hiyo inamhitaji na kama ikichangamka yuko tayari kufanya kazi nchini.

Sababu za uamuzi wa Pluijm

Akizungumza uamuzi wake wa kujiuzulu, Pluijm alisema uwapo wa kocha huyo nchini umemchukiza na kuamua kumuandikia mwenyekiti wa klabu hiyo, Yusuf Manji barua ya kujiuzulu nafasi yake.

Pluijm alisema hajafurahishwa na mambo yalivyokuwa yakifanyika na kwamba licha ya uongozi wa klabu yake wakati wote kukanusha hawana mpango na Lwandamina, lakini anao uhakika wako katika mazungumzo na kocha huyo wa Zesco United.


Alisema kuna nafasi Yanga walitaka kumpa, lakini ameshindwa kukubaliana nayo kutokana na mambo yalivyofanyika.

Pluijm alitajwa kubadilishiwa wadhifa na kuwa mkurugenzi wa ufundi wa klabu hiyo na nafasi yake kuchukuliwa na Lwandamina. “Unajua hakuna siri katika dunia ya sasa, sijafurahi mambo yalivyokuwa yanafanyika hawakutanguliza heshima kwangu, nimewaandikia barua ya kujiuzulu ili waniache niondoke vyema,” alisema Pluijm na kuongeza: “Sikupanga kuondoka Yanga kwa ubaya, lakini hili sikulifurahia, nawashukuru wanachama na mashabiki pamoja na uongozi na wachezaji wangu kwa kunipa nafasi ya kufanya kazi hapa na kesho (leo) nitakwenda kuwaaga wachezaji wangu,” alisema Pluijm.

Jana asubuhi, Pluijm alisema hana nafasi ya kuzungumzia ujio wa Lwandamina na kusisitiza kuwa kwa sasa anahitaji kutuliza akili kwani anasubiri taarifa rasmi.

Huku akicheka Pluijm alisema: “Nimesikia mengi, yameandikwa na kusemwa juu yangu kuondoka Yanga, lakini najiamini, mimi ni kocha mwenye kiwango, nimefanya kazi kubwa Yanga na ninazidi kuendelea kufanya, ingawa sishangazwi na yanayosemwa kwani vitu kama hivyo ni kawaida kutokea duniani.

“Nimeifanyia Yanga vitu vingi tangu iliponiajiri hadi sasa, kama kuna mabadiliko nitaambiwa na waajiri wangu, nami nitaeleza misimamo wangu.”

Wengine wanasemaje

Kocha msaidizi wa Simba, Jackson Mayanja alisema kuondolewa kwa Pluijm hashangazwi nako kwani ndivyo mpira ulivyo kokote duniani. “Hata Mourihno (Jose) alitimuliwa Chelsea, hivyo ni kawaida ya makocha, lakini mimi sioni udhaifu wa Pluijm naangalia mafanikio aliyowapa Yanga hadi imecheza mashindano ya kimataifa na kufika mbali tu,” alisema Mayanja.

Mwanasoka wa zamani wa Yanga na Pan African ambaye pia ni kocha, Mohammed Adolph ‘Rishard’ alisema timu kucheza mfululizo kwa kiwango kile kile ni ngumu hivyo haoni sababu ya Yanga kumuondoa Pluijm.

“Sioni kama Yanga iko katika kiwango kibovu nafikiri ni uchovu kwani hata ukiangalia Azam  ndiyo tatizo linalowasumbua, timu haiwezi kucheza misimu miwili mfululizo kwa kiwango kile kile, sasa wanapobadilisha kocha wategemee mambo mawili, timu kuendelea kuwa kama ilivyo au kuzidi kuporomoka zaidi,” alisema Rishard.

Aunty Ezekeil na Mtoto Wake Wamtua Machozi Wema Sepetu...

$
0
0
Kama ulikuwa bado upo kwenye ndoto ya Wema Sepetu na Aunty Ezekiel kuwa maadui – amka!

Wawili hao wameonekana kutokuwa na tatizo baada ya madam Sepenga kuweka picha ya Aunty akiwa na mwanae Cookie aliyezaa na dansa wa Diamond, Mose Iyobo kwenye mtandao wake wa Instagram na kuandika ujumbe ambao umeonekana kutoa watu machozi.

Wema ameandika kwenye mtandao huo:

My Picture of the day…!!! This is tooo Cute…. Mola akukuuzie Cookie wako Tiake…. #Priceless 😍😍😍 Dah… Iko siku na mimi Inshallah…. Hii pic imenitoa hadi chozi…. You are sooo blessed mumy… @auntyezekiel @auntyezekiel

Ali Kiba Aikana Nyumba Inayoonyeshwa Kwenye Mitandao Kuwa ni yake

$
0
0
Ally Kiba aikana nyumba inayoonekana mitandaoni wakisema ni yake, hii ni alipokua akihojiwa kwenye moja ya radio maarufu nchini
.
"Aliyekwambia mi Nina nyumba nani, naishi nyumba ya kupanga hata ingekuwa yangu mi sipendi show off ni maisha yangu" alisema

Ushauri: Nimegundua Mdogo Wangu Kabisa na Dada wa Kazi Wanasagana, Je, Nifanye Nini?

$
0
0
Kiufupi mimi ni mwanamke niliyeolewa miaka 5 iliyopita na kubahatika kupata watoto 2 wa kiume.
Mmoja ana 4 yrs na mdogo ana miezi 9.
Mume wangu yeye yuko Morogoro Manispaa anakofanyia kazi, na mara nyingi wakati wa weekend huja nyumbani Dar ili kujumuika na familia yake na wakati mwingine huwa ikitokea nafasi ya kuja Dar kikazi, basi huja kutuchungulia na kuendelea na shughuli zake.

Wakati najifungua huyu mtoto wangu wa pili, nilienda nyumbani kwetu Mwanza kumchukua mdogo wangu wa kike ili anisaidie kazi za hapa na pale wakati nikiwa kazini.
Na mtoto alipofikisha miezi 6, mdogo wangu aliniomba arudi Mwanza nyumbani ili akaendelee na masomo ya chuo.
Nilimkubalia na kumwambia kuwa kama atabahatika kunitafutia msichana wa kazi, nitamshukuru.
Baada ya kuondoka, kazi ikawa ni kutembea na yule mdogo kwenda nae ofisini huku mkubwa nikimpeleka Day care akashinde huko na kucheza.

Baada ya mwezi, mdogo wangu akaniambia kuwa amepata dada wa kazi na atakuja nae, nilishukuru sana na nikaanza maandalizi ya chumba cha kukaa msichana wa kazi.
Nilituma nauli na walikuja wote.
Baada ya kufika tuliongea kuhusu mshahara na taratibu zingine za kazi za pale kwangu.
Kisha baadae nikamuonesha chumba ambacho atakuwa anakitumia akiwa pale.

Tulikaa sebuleni tukipiga stori na muda wa kulala tuliagana vizuri, msichana akaenda chumbani kwake,mdogo wangu akaenda kwake nami nikaelekea kwangu.
Wakati nikiwa usingizini nikahisi sebuleni kuna watu wanaongea na kucheka...nikaamka ili nione ni nani wako sebuleni usiku ule, nikagundua kuwa ni mdogo wangu na yule dada wa kazi, wakasema wamerudi ili kuangalia tamthilia.
Sikutilia shaka, nikarudi zangu kulala.

Asubuhi kulipokucha msichana akaendelea na kazi zake kama kawaida na mdogo wangu akimsaidia.
Mwezi ulipita na nilipomuhoji mdogo wangu kuhusu chuo akawa ananiambia ataenda hivo nisiwe na shaka.
Basi nikaendelea na maisha yangu ila nilikuja kugundua ukaribu uliokuwepo kati ya mdogo wangu na msichana wa kazi.
Mdogo wangu ilikuwa akienda shopping huwa anamnunulia sidiria au chupi dada wa kazi, nikiuliza husema kuwa ameamua kumnunulia kama mwanamke mwenzake.
Sikutilia shaka japo niliona si hali ya kawaida kivile.
Baada ya tukio hilo ilipita siku kama 3 wakati naamka usiku nikaangalie milango kama imefungwa vizuri, wakati nakatiza sebuleni nikamuona msichana wa kazi na mdogo wangu wamekaa sebuleni wamelaliana kifuani.
Kwanza nilishtuka, mdogo wangu akasema, sio vibaya kumlalia mwanamke mwenzake kifuani.
Nikapita zangu nikarudi kulala.

Jumamosi moja mida ya saa 6 usiku, mume wangu alirudi toka Morogoro alichelewa maana gari ilipata pancha, alifika usiku na kwa vile simu yake iliisha chaji, aliamua kuzunguka dirishani kwangu ili anigongee...wakati anakatiza dirisha la msichana wa kazi, akasikia minong'ono na kilio cha mahaba cha kulalama.
Ilibidi aniamshe taratibu ili kama kaingiza mtu tujue.
Nilifungua mlango na kuzunguka dirishani, kweli nilisikia kilio hiko cha mahaba, yaani kama mtu yuko katika sex.
Basi tutaingia ndani na kwenda kumgongea mdogo wangu, tuligonga sana ila haukufunguliwa na tukaenda kwa msichana, alipofungua tukamuuliza mdogo wangu yuko wapi?
Akasema yuko kwake...tukaenda tena kugonga ila kulikuwa kimya.
Nahisi alijificha chumbani kwa msichana wa kazi.

Asubuhi kulipopambazuka niliwatuma gengeni wote, hapo sasa nikaingia kwa dada wa kazi kufanya upekuzi, tulipekua kila mahala kwa uangalifu na tulipofungua kabati tulikutana na kifaa cha kufanyia mapenzi pamoja na mafuta mbalimbali.
Baada ya hapo tukaenda chumbani kwa mdogo wangu, tukapekua kila mahala na tulipofunua begi lake, tukakuta picha za uchi za dada wa kazi na zingine wakiwa wamepiga huku wananyonyana maziwa, nyingine ni za aibu sana.
Kitandani kulikuwa na simu ya mdogo wangu, nikaichukua na kwebda kwenye gallery na kukuta picha za aibu na chafu.
Kumbe walikuwa wanashirikiana na mdada mwingine wa kazi wa jirani yangu.
Yaani sex group ya wanawake 3.
Kwenda kwenye message tukakuta mdogo wangu akimsifia dada wa kazi kuwa mtamu na anamkuna na kuahidi kutomuacha na hata dada mkubwa, yaani mimi nikimfukuza, basi lazima anifanyizie mimi au mwanangu.
Nilikaa chini na kuanza kulia, mme wangu akanibeba na kunipeleka chumbani.
Nikamuangalia mwanangu aliyelala kitandani haelewi chochote, huku akiwaziwa kufanyiwa kitu kibaya na mama yake mdogo.

Mpaka sasa mwanangu ana miezi 9 sasa, dada wa kazi yupo na mdogo wangu yupo...na mbaya zaidi mama ameniambia kuwa nimtafutie chuo huyu mdogo wangu hukuhuku Dar, asirudi Mwanza.
Niko njia panda, wanangu nawapenda, mdogo wangu nae nampenda, mie na mume wangu tumekosa cha kufanya.
Na msichana tangu afike pale...ni mchapa kazi na anawajali sana watoto na watoto wanampenda sana sana.
Niko njia panda, naombeni ushauri wenu.

TAMBWE Atokea Benchi Na Kupiga Mbili, Yanga Yaua 4-0

$
0
0
Mshambuliaji wa Yanga, Amissi Tambwe akishangilia baada ya kutokea benchi na kufunga mabao mawili, Yanga ikishinda 4-0 dhidi ya JKT Ruvu jioni ya leo Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam katika mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara

Wafungaji wa mabao mengine ya Yanga leo, Obrey Chirwa (kulia) na Simon Msuva (kushoto)

Meneja wa Diamond Platnumz Amemposti Mtandaoni Meneja wa Alikiba

$
0
0
Katika zile lugha za Kimitandao siku ya Jumatano hupewa ‘Kinashi’ cha ‘WCW’ (Woman Crash Wednesday) yaani kumposti Mwanamke aliyekonga hisia zako na kumuhusudu zaidi.

Kilichowashangaza Mashabiki wengi zaidi kutokana na kile kinachotajwa kuwa ni bifu baina yao.

Leo meneja wa Kimataifa wa Muimbaji Diamond Platnumz, Sallam ‘Mendez’, amemposti Meneja wa Hasimu wao Kibiashara, Mrembo Seven Mosha kama #WCW wake.

H: Baba Amponda Diamond Kwa Kupost Nyumba, Asema Kama ni Mkweli Aonyeshe Hati

$
0
0
H Baba amemponda Diamond kwa kupost nyumba kisa eti Ali Kiba katuma, amesema kama yeye ni mkweli ana nyumba aposti hati ya nyumba, sio mwenzake akipost nyumba naye anapost

Ali Kiba: Sina Nyumba Bado, na Hata Nikiwa Nayo Sitajitangaza

$
0
0
Msanii Ali Kiba amekataa nyumba inayosambazwa kwenye mitandao ya kijamii ikuhusishwa na yeye na kusema bado anaishi kwenye nyumba ya kupanga na hata kama alikuwa amejenga nyumba hawezi kufanya show off:

Msikie Hapa:
Viewing all 104690 articles
Browse latest View live




Latest Images