Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104785 articles
Browse latest View live

'Rais Magufuli Ndiye Rais wa Kwanza Duniani Kuwa na Asilimia 96%' Lemutuz

$
0
0
Kwa Mujibu wa Gallup Polls by British Institute of Public Opinion iliyofanywa Mwezi uliopita the FACT is utafiiti wao wa kisayansi unaonyesha katika Mwaka wake mmoja madarakani Rais Magufuli amefanikiwa kukubalika sana na Wananchi kwa 96%, utafiti ulifanywa kwa kutumia Mobile Survey through Wananchi 1,813.

- Kwa mujibu wa matokeo hayo Rais Magufuli, amefanikiwa kufanya yafuatayo kwa ufanisi unaokubalika na Wananchi wengi:- (1). Kuishinda Rushwa 75%, (2). TRA sasa ipo on the right track 85%, (3). Education has improved by 75%, (4). Mahakama zetu sasa zipo mstari unaotakiwa kwa 73%, (5). Afya improved by 72%, (6). Maji Safi kwa Wananchi 67%, na kubwa kuliko zote ni Wafanyakazi Serikalini na Mashirika yake sasa wamekuwa 95% kwa Accountability na Fast Response.

- Now Rais Magufuli sio Malaika, na sio siri kwamba Wananchi wote tulikubaliana kwenye uchaguzi uliopita kwamba Taifa letu lilihitaji mabadiliko na tulihitaji kumchagua Rais wa kutuletea mabadiliko, matatizo yetu makubwa ya Taifa siku zote yamekuwa ni Respect to the Rule of Law na Uchumi Mwalimu Baba wa Taifa the greatest ever alikuwa na mapungufu kwenye hizo two lines na zimetusumbua kwa muda mrefu sana hili taifa ni only now Rais Magufuli ameanza kuyatafutia ufumbuzi na matokeo yameanza kuonekana.

- Wananchi wengi hapa Mjini sasa hawana tena pesa za kuchezea kama zamani ambapo ilikuwa kawaidaa kukuta Kijana mdogo akiendesha gari la kifahari na akiwa na mabunda ya Mamilioni ya pesa kwenye gari lake, kuna Vijana hapa mjini walikuwa wakitengewa meza zao kwenye Vilabu vya starehe yaani haruhusiwi kugusa mtu kwa sababu wanatumia pesa nyingi sana wanapokwenda pale, Mikutano ya Bodi za Wakurugenzi wetu mingine ilifikia mpaka kufanyika Johannesburg, au Singapore ambapo wajumbe wa bodi waliruhusiwa kwenda na familia zao, Bandari yetu ilikuwa unakusanya Billioni 40 tu kwa mwezi badala ya Tsh. Billioni 300, na mengineyo mengi ambayo yalisababisha Taifa letu kuwa na tabaka fulani la wachache wenye pesa na wengi Masikini, katika Mwaka mmoja wa Rais Magufuli tumejionea mabadiliko makubwa sana na kwa mara ya kwanza katika historia ya Taifa letu wale walioitwa Vigogo au the untouchables sasa wapo Rumande Keko wanasubiri kesi zao.

- I understand that baada ya kuona hawana upenyo wa kuingilia au kutokea kwenye mfumo mpya wa sasa zaidi ya kutakiwa kufanya kazi zao kwa mistari ya Kisheria, Wapinzani wameamua kutumia Social Media na hasa Media kwa ujumla kumshambulia sana Rais Magufuli, kuna pahali wameanza hata kumsifia Rais JK kwamba ni bora zaidi, lakini hatujawasahu hawa ndugu zetu na tabia yao ya kubadilika badilika kama Kinyonga wakifuatia masilahi yao aidha ya Vyama vyao au binafsi, Waliwahi kutuambia kwamba CUF ni Chama cha Mashoga lakini walipotaka Umoja wa UKAWA wakajiunga nao, Waliwahi kumshambulia sana Waziri Mkuu Mstaafu Lowassa mpaka walienda mbali sana na kutaka apigwe Risasi hadharani kwa Ufisadi, leo wamebadilika kwamba Ushahidi upo wapi kwa sababu amejiunga nao,

- Infact wameanzisha hoja moja dhaifu sana kwamba mbona Rais JK alikuwa anawaita Wapinzania na kuwasikiliza ushauri wao kwenye uongozi, sasa tunatakiwa kuwauliza kwamba mlikuwa mnamshauri Rais JK on what lines na huku wote tunakubaliana kwamba Taifa lilikuwa limeoza? Rais Magufuli awasikilize nini hasa kizuri mlichowahi kulifanyia Taifa hili huko nyuma? The Americans wanasema kama kuna Kiongozi mahali ameoza basi ni system nzima so kama as a nation tulikubaliana kwa kauli moja kwamba tunataka mabadiliko basi iilikuwa na maana kwamba 360 Degrees U turn ambayo ndio tunayoyapitia sasa yaani total mabadiliko, ninawaomba huko upande wa pili muwacheni Rais afanye aliyoyaahidi kwenye kampeni zake za kuomba Urais na Ilani ya CCM, subirini Mwaka 2020 kwenye uchaguzi unaofuata kwa sasa uchaguzi umekwisha.

- MUNGU IBARIKI TANZANIA!!

Le Mutuz Nation

TID Pokea Ushauri, Rudi Kwenye Fani ya Utangazaji

$
0
0
Nilianza kumfahamu msanii Khaleed Mohammed au Top in Dar (TID) alipotoa wimbo pendwa wa Zeze miaka ile ya 2000s akiwa na Jay Moe..

Jina lake likakua na kukubalika ndani na nje ya mipaka ya Tanzania huku akijivunia sauti yake na kujiita 'Golden Voice' yaani Sauti ya Dhahabu, jina ambalo alilipa album yake ya kwanza iliyojaa nyimbo zilizobamba tupu kwa wakati huo..

Kuna kituo maarufu cha redio, kiliwahi kutumia sauti yake kufanyia 'jingle' matata sana kwa miaka mingi kabla TCRA haijabadili 'masafa' kwa vituo vya redio zote nchini. Ile Jingle ni shida (92.9, Magic Fm, Dar es salaam)..

Historia tamu ya SAUTI YA DHAHABU ninayo, ila kwa leo acha niishie hapo.

Kucheza? Nani hakumbuki 'shekisheki' za TID zilivyovuruga vijana mitaani kwetu? Kuna aliyesahau kwamba TID ndiye msanii pekee aliyebuni michezo mingi ya kuvunja (breakdance) hapa Bongo, kiasi cha kupachikwa jina la 'Wacko Jacko', likimaanisha 'Michael Jackson', jina la mfalme wa muziki wa Pop na 'michezo ya kuvunja' duniani (apumzike kwa amani).

Jina la TID liliuza magazeti, lilivuta mapromota (mameneja waliitwa mapromota wakati huo), lilileta hamasa ya vipindi vya muziki kwenye televisheni zetu nchini.. Alitamba kila siku.. Alikuwa NEMBO ya muziki wa kizazi kipya..

TID alijua kuimba na kucheza. Andaa show, usimuite TID, imekula kwako! Inakadiriwa kuwa ndiye mwanamuziki wa kwanza kwenda kufanya ziara ya kimuziki Uingereza. Yes, wa kwanza kutoka Bongoflevani. Huko akafyatua na video ya wimbo wake wa 'Pekee'. Wapo waliokoma kwa hili!

Sijasahau, umaarufu wa TID ndio uliibeba filamu bora ya maisha na muziki kuwahi kutokea hapa nchini, Girlfriend, akiwa kama mhusika mkuu akishirikiana na dada Monalisa wa Natasha. Hata leo hii, tunakubaliana kwamba hapakuwahi kutokea filamu ya Kiswahili iliyotazamwa na kukubalika nchini zaidi ya hiyo. Kila mtu alimwangalia zaidi TID humo. Mungu ampumzishe kwa amani mtayarishaji George Tyson.

Hayo yamepita.

Kuna fani TID aliyosomea. Fani ya Utangazaji. Sio kusomea tu, huko ndiko alikotokea kabla ya kuingia kwenye muziki. Wengi hawakulijua hili la utangazaji mpk pale jina lake lilipokuwa kubwa kupitia muzikia.. Mimi nikiwa mmojawapo. Kama kuna ambaye halijui hilo, habari imfikie rasmi leo.

Ngoja nikueleze, TID alikuwa anasifika kwa umahiri wa kutangaza redioni. Hakuwa maarufu kwa sana, lakini alikuwa hodari na machachari sana akiwa nyuma ya maiki. Sifa yake kubwa ilikuwa ni sauti ya bashasha na umahiri wa kutumia lugha ya kiingereza 'kimjini mjini'. Acha bwana! Ulikuwa ukimsikiliza TID siku za weekend usiku, hata kama ulikuwa na mpango wa kwenda club utaghairi. Taji Liundi heshima kwako kwa kukivumbua hiki kipaji..

Sina data nyingi kuhusu 'utangazaji' wa TID, lakini naamini ni kitu anachoweza kufanya zaidi na kukubalika hasa katika kipindi hiki ambacho muziki una 'vurugu' na fitina za kutosha.

Hapa namuwazia Mtangazaji TID mwenye makeke lakini yasiyo na utani utani. Namjengea picha akiwa ni mtangazaji anayeheshimu wasikilizaji wake na mwenye nidhamu ya kazi.

Nani asingependa kumsikiliza TID nyakati za jioni? Rudi kazini TIDI.

By Interest

Alikiba AQkanusha Kutumbuiza Kwenye Shindano la Miss Tanzania 2016

$
0
0
Alikiba amekanusha taarifa zilizoenea kuwa atatumbuiza kwenye shindano la Miss Tanzania 2016 litakalofanyika Jumamosi hii mjini Mwanza.

Taarifa hizo zilizosambaa zimedai kuwa Alikiba na Christian Bella ndio wasanii watakaotumbuiza kwenye tamasha hilo lakini Kupitia mtandao wa Instagram, hitmaker huyo wa wimbo wa ‘Aje’ ameandika, “Taarifa Muhimu : Napenda Kuwajulisha Ya Kuwa Sitakuwepo.”

Tamasha hilo litakuwa likifanyika mkoani humo kwa mara ya kwanza tangu kuanzishwa kwa mashindano hayo nchini.

Jokate Adai Alimpenda Sana Hasheem Thabeet, Ataja Sababu za Kuachana Naye

$
0
0
Hasheem Thabeet kwa mujibu wa Jokate Mwegelo, alikuwa ni ‘first love’ na huenda kuachana naye kilikuwa ni kitu kibaya zaidi kuwahi kutokea katika maisha yake.

Mrembo huyo alikuwa akijibu swali la PapiChulo_Chuly kwenye Twitter aliyeuliza, “Ni tukio gani baya huwezi sahau maishani?”

“Kumwacha mtu ambaye nilikuwa nishapanga vitu vingi sana nae kichwani. Very very disappointing but it’s life,” alijibu Jokate.

October 2013, kwenye jarida la Vibetz, alifunguka kuwa japo uhusiano wake na Hasheem ulidumu kwa miaka mitatu, walifanikiwa kuufanya usijulikane sana kwa wengi na walikuwa wakipendana sana.
“With Hasheem, I think it was more than love. He was my first real love,” aliliambia jarida hilo.

“Siku zote nilidhani he was my soulmate. Kiukweli nilimpenda sana. He is like the only guy I would drop anything at anytime for. Nilikuwa tayari kufanya lolote kwaajili yake, that’s how deep I loved that guy,” aliongeza.

“Nilimpenda kiukweli Hasheem, and yes kama mwanamke mwenye kutaka kufanikiwa I’m drawn to ambitious/successful men, you know the go getters but my family haikunilea katika maadili ya kujenga mahusiano yoyote katika mhimili wa fedha,” Jokate alieleza kujibu swali kama aliamua kuwa na Hasheem kwasababu ya fedha zake. “I had never wanted to use Hasheem, all I wanted was to love him.”

Jokate alidai kuishi mbali na Hasheem ni moja ya sababu iliyochangia kuvunjika kwa uhusiano wao.

“Yes kuishi mbalimbali pia inaweza kuwa sababu japo ndogo iliyochangia kuvunjika mahusiano yetu cause sometimes I would hear a lot of stuff and that would upset me. Nilikuwa naogopa sana kumpoteza, I ended up doing vitu vya kijinga kama dating Diamond. I had issues with Hasheem na Diamond came in picture. It was a very frustrating time for me. I was super confused. I cried for a whole year. Like every night I would just cry like crazy.”

Kwa sasa Jokate ana uhusiano na Alikiba.

Nay wa Mitego Adai Wema Sepetu ndiye Aliyemfilisi Idris Sultan (Video)

$
0
0
Msanii wa muziki wa hip hop Nay wa Mitego ameanza kuitupia madogo kambi ya malkia wa filamu Wema Sepetu kwa kudai mwigizaji huyo ambaye zamani alikuwa mpenzi wa Idris Sultan ndiye aliyemfilisi mshindi huyo wa BBA 2014.

Rapa huyo ambaye yupo kimya kwa sasa, alipost video katika mtandao wake wa instagram akieleza ni kwanini mshindi huyo wa BBA 2014 alifilika.

“Huwa najiuliza kitu kimoja ni mwanamke gani amemaliza mahela ya Idris?,” aliuliza Nay kupitia video hiyo. “Ni yule Msouth au madam (Wema). Mimi nadhani atakuwa madam maana madamu ni mtu wakukwarua mahela mengi, tena kabla hajatua Tanzania walimwambi, huku nyumbani kuna wanawake wacheza sinema maharamia wakikukamata na hizo hela utajikuta huna hata mia,”

Kambi ya malkia huyo wa filamu haijajibu chochote juu ya tuhuma hizo.

Huyu Mwanafunzi Mzuri Kutoka Arusha Atatimiza Ndoto zake? Angalia Video

$
0
0
Huyu atatimiza hizo ndoto zake kweli ? Kuja kuwa muigizaji bora?

Au ataanza kuvunja ndoa za watu mapema sana?

Ajitokeze mtu humu awe Manager wake la sivyo wajanja watamuharibia future...

Nawaza tu..

Ripoti ya Mkataba wa Lugumi, Polisi Yafika kwa Spika wa Bunge, Job Ndugai.

$
0
0
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Projestus Rwegasira amewasilisha taarifa ya utekelezaji wa maagizo ya Bunge ya kuhakikisha mfumo wa vifaa vya utambuzi wa alama za vidole unafungwa katika wilaya za kipolisi 108 nchi nzima kwa muda wa miezi mitatu.

Zabuni ya kufunga na kusambaza mashine hizo za utambuzi wa vidole katika Jeshi la Polisi ulifanywa na Kampuni ya Lugumi.

Kwa mujibu wa Mwenyekiti wa kamati hiyo Naghenjwa Kaboyoka, aliwathibitishia waandishi wa habari mjini Dodoma jana kuwa ripoti hiyo tayari imekabidhiwa kwa Ofisi ya Spika wa Bunge, Job Ndugai.

Kaboyoka alisema ripoti hiyo baada ya kukabidhiwa kwa Spika Ndugai ataipitia na baadaye kuiwasilisha kwa kamati hiyo ya PAC.

Juni 30, mwaka huu, Naibu Spika wa Bunge, Dk Tulia Ackson baada ya kuahirisha Bunge la Bajeti aliiagiza serikali kuhakikisha mfumo huo unafanya kazi kwa ajili ya kuwadhibiti wahalifu na kuitaka Kamati ya PAC ifuatilie suala hilo.

Dk Tulia alitoa agizo hilo baada ya kupokea taarifa yenye utata ya kuhusu zabuni yenye thamani ya Sh bilioni 37 ya kufunga mashine hizo katika vituo vyote vya Polisi baina ya Jeshi la Polisi na Kampuni ya Lugumi Enterprises Limited iliyotolewa mwaka 2011.

“Ninashauri serikali ihakikishe mradi huu unakamilika ndani ya kipindi cha miezi mitatu kuanzia leo…, mradi huu utasaidia Jeshi la Polisi kuwatambua kwa haraka watu waliohusika katika matukio ya uhalifu mbalimbali,” alisema.

Katika mkataba huo, Lugumi inatakiwa kusambaza na kufunga mashine hizo za utambuzi wa vidole katika wilaya 108 za kipolisi nchi nzima.

Hata hivyo, mashine hizo zilifungwa kwenye vituo 14 pekee wakati tayari kampuni hiyo ilishapokea kiasi cha asilimia 99 za malipo yake.

Katika ripoti ya Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) ya mwaka wa fedha 2013/14 ilionesha kuwa pamoja na kampuni hiyo ya Lugumi kulipwa asilimia 99 ya malipo sawa na Sh bilioni 34, bado haijakamilisha mradi huo kwa muda wa miaka mitano sasa.

Aprili, mwaka huu, PAC iliunda kamati ndogo kwa ajili ya kuchunguza mkataba huo wa utata baina ya Kampuni ya Lugumi na Jeshi la Polisi.

Bangi Yawatokea Askari 10 Puani..Watiwa Mbaroni

$
0
0
 Jeshi la Polisi limetikiswa baada ya maofisa wake 10 kutiwa mbaroni wilayani Siha mkoani Kilimanjaro kwa tuhuma za kuwaachia watuhumiwa wa shehena ya bangi.

Tukio hilo ambalo limekuwa gumzo, lilitokea Jumanne iliyopita kwenye Kijiji cha Olmolok baada ya maofisa hao kudaiwa kukamata magunia manane yaliyosheheni bangi yakisafirishwa kwenda nchini Kenya.

Ofisa Mnadhimu wa jeshi hilo Mkoa wa Kilimanjaro, Koka Moita kwa niaba ya Kamanda wa Polisi mkoani hapa, Wilbroad Mutafungwa, alithibitisha kuwapo kwa tukio hilo.

Shahidi Aeleza Askofu Gwajima Alivyofikishiwa Bastola

$
0
0
MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu imeelezwa kuwa washtakiwa watatu walipeleka bastola kwa Askofu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima wakati amelazwa katika Hospitali ya TMJ baada kubaini wanaihifadhi kinyume cha sheria.

Ofisa Upelelezi kutoka Ofisi ya Mkuu wa Upelelezi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Sajini Abogasti (46) alidai hayo jana wakati akitoa ushahidi katika kesi ya kushindwa kuhifadhi silaha inayomkabili Gwajima na wenzake Yekonia Bihagaze, George Mzava na Geoffrey Milulu.

Akiongozwa na Wakili wa Serikali Mwandamizi, Shedrack Kimaro kutoa ushahidi wake, Sajini Abogasti alidai kuwa Bihagaze, Mzava na Milulu, walipeleka silaha kwa Gwajima wakati akiwa amelazwa katika Hospitali ya TMJ.

Alidai mbele ya Hakimu Mfawidhi, Cyprian Mkeha kuwa Mkuu wa Upelelezi Kinondoni alimuunganisha na Mkuu wa Kituo Kawe, Pamphil ambaye alimkabidhi begi lililokuwa na bastola namba CAT 5802, risasi tatu zilizokuwa katika kasha lake (magazine), CD mbili, risasi 17 za bastola na kitabu cha umiliki silaha, chupi na hati ya kusafiria ya mchungaji huyo.

Wakili Kimaro alimtaka shahidi huyo kuionesha Mahakama kitabu cha umiliki wa silaha, shahidi alihangaika kutafuta kwa zaidi ya dakika mbili bila mafanikio na baadaye akadai ameshakirejesha kwa Gwajima.

Akiendelea kutoa ushahidi, Abogasti alidai baada ya kukabidhiwa begi hilo katika Kituo cha Polisi Osterbay alianza kufanya upelelezi lakini Gwajima alikuwa Arusha kwenye mkutano wa Maaskofu pamoja na washtakiwa wenzake.

Alidai Machi 26,2015 Gwajima alipewa wito wa kufika Kituo cha Polisi Dar es Salaam, kesho yake alifika na aliwaachia washtakiwa wenzake begi lililokuwa na silaha, na washtakiwa hao walikaa nalo kwa siku mbili jambo ambalo ni kinyume cha taratibu.

Shahidi huyo, alidai kuwa Gwajima aliitwa Polisi kwa kosa la kumdhihaki Askofu wa Kanisa Katoliki, Mwadhama Polcarp Kardinal Pengo lakini wakati akihojiwa, alipata maradhi ya ghafla na kupelekwa Hospitali ya Temeke, kisha Hospitali ya Taifa ya Muhimbili na kuhamishiwa Hospitali ya TMJ kutokana na hali yake.

Sumaye Kunyang’anywa Shamba na Serikali, Apewa Notisi ya Siku 90

$
0
0
Waziri wa Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi William Lukuvi amesema hati ya shamba lililopo maeneo ya Bunju la aliyekuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Fredrick Sumaye liko katika hatua ya kufutwa na kwamba Afisa Ardhi Mteule wa Wilaya ya Kinondoni Rehema Mwinuka ameshatoa barua ya notisi ya siku 90.

Lukuvi ameyasema hayo jana jijini Dar es Salaam wakati akizungumza na wandishi wa habari.

“Shamba la Sumaye hati yake iko katika hatua za kufutiwa,
Afisa Ardhi Mteule wa Wilaya ambaye anajukumu la kutoa notisi, ameshatoa notisi kwamba hajaendeleza eneo hilo kwa muda mrefu hivyo kwa mujibu wa sheria hati yake inatakiwa kufutwa,” alisema.

Alisema serikali haitofumbia macho wamiliki wa ardhi na mashamba ambao hawajayaendeleza kwa muda mrefu.

Pia, kufuatia ongezeko la matapeli wanaotumia nyaraka za kughushi za barua za toleo (ofa) zinazodaiwa kutolewa na Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam, Lukuvi alitoa agizo hususani kwa wakazi wa jiji hilo wanaomiliki ardhi pasipo kuwa na hati miliki, kujisalimisha kwa kupeleka barua zao za ofa kwa Kamishna wa Ardhi ili wapatiwe hati halali.

“Wamiliki wote wanaomiliki ardhi kwa karatasi za ofa halali wazibadilishie ili wapewe hati halali, na atakaegundulika kumiliki ofa feki polisi watawakamata na kupelekwa mahakamani,” alisema.

Alisema asilimia 60 ya watu wanaopeleka kesi za migogoro ya ardhi wizarani, chanzo cha migogoro hiyo ni karatasi za ofa zinazotoka katika halamshauri za jiji na manispaa.

“Natoa miezi mitatu ili karatasi hizi zisitokee tena kila mtu alete barua ya ofa watapewa hati zao ndani ya mwezi mmoja ,wazilete kwa kamishna wa ardhi wa mkoa, baada ya hapo sitasikiliza malalamiko ya watu walioibiwa ardhi wakiwa na ofa ya namna hii.

“Tumieni miezi mitatu vizuri kubadilisha ofa,” amesema.

Hali kadhalika, Lukuvi alipiga marufuku vitendo vya uvamizi wa ardhi na mashamba vinavyofanywa na baadhi ya wananchi, na kuwataka wananchi kutoa taarifa pindi watakapobaini kuwa kuna shamba au ardhi isiyoendelezwa.

“Serikali ina laani uvamizi wa ardhi na mashamba unaofanywa na baadhi ya wananchi sababu baadhi yao yanamilikiwa kihalali na yana hati, serikali ipo na sheria zipo zitafanya kazi yake,” alisema.

Bia ya Serengeti Yasherehekea Kutimiza Miaka 20

$
0
0


 Mkurugenzi Mkuu wa SBL Helene Weesie akizungumza na waandishi wa habari katika mkutano na waandishi wa habari  ambapo alitangaza maadhimisho ya miaka 20  tangu kuanzishwa kwa bia ya Serengeti Premium Lager (SPL)  mwaka 1996. Anayefuatia ni Meneja masoko wa SBL  Anitha Msangi na kulia  mwishoni ni Mkurungezi wa Masoko wa SBL , Cesear Mloka  .Mkutano huu umefanyika mapema leo katika Hoteli ya Hyatt Regency Jijini Dar es salaam

Mkurungezi wa Masoko wa SBL , Cesear Mloka akifafanua jambo kwa waandishi wa habari mara baada ya kutangazwa kwa maadhimisho ya miaka 20  tangu kuanzishwa kwa bia ya Serengeti Premium Lager (SPL)  mwaka 1996.Anayefuatia katikati ni Meneja Masoko wa SBL Anitha Msangi na mwishoni kulia ni Mkurungezi mkuu wa SBL  Helene Weesie.Mkutano huu umefanyika mapema leo katika Hyatt Regency Hotel Jijini Dar es salaam.

Mpishi Mkuu mtanzania  Winston Kagusa aliyefanikiwa kuchanganya mbinu ya utengenezaji wa bia za kijerumani na  vionjo vya hapa nchini kupata  kinywaji hiki  cha Serengeti Premium Lager kinachopendwa na wengi.


 Mkurugenzi Mkuu wa SBL Helene Weesie akiongoza katika kuzindua chapa mpya ya Serengeti Premium Lager sherehe ambazo zinaambatana na maadhimisho ya miaka 20 ya bia hiyo kulia kwake ni Meneja Masoko wa SBL Anitha na kushoto kwake wa kwanza ni Mpishi Mkuu wa kwanza wa Serengeti Premium Lager Winston kagusa na mwishoni ni Mkurungezi wa Masoko  Cesear Mloka.Hafla hii ilifanyika katika hotel ya Hyatt Regency Jijini Dar es salaam.

Mkurugenzi wa Mawasiliano, SBL John Wanyacha akifafanua jambo kwa waandishi wa habari katika Mkutano wa waandishi wa habari ambapo Bia ya serengeti premium lager inatimiza miaka 20 toka kuanzishwa kwake na pia kuzinduliwa kwa chapa yenye muonekano mpya.Mkutano huu ulifanyika mapema leo katika hotel ya Hyatt Regency
Waandishi wa habari wakichukua matukio katika mkutano huo uliofanyika mapema leo

  • SBL yaizindua bia hiyo katika muonekano mpya


  • Yashinda zaidi ya medali 10 za ubora wa kimataifa


Dar es Salaam  Oktoba 27, 2016- Kampuni ya Bia ya Serengeti (SBL) leo  imetangaza kuanza kwa sherehe maalumu kuadhimisha miaka 20  tangu kuanzishwa kwa bia ya Serengeti Premium Lager (SPL)  mwaka 1996. Sherehe hizo zinaambatana na uzinduzi upya wa bia hiyo ikiwa katika muonekano mpya.


Akizungumza  leo jijini Dar es Salaam katika mkutano na waandishi wa habari, Mkurugenzi Mkuu wa SBL Helene Weesie, amesema mbali na kuonesha mafanikio ya bia ya Serengeti kwa kipindi cha miongo miwilil iliyopita, kampuni ya SBL itatumia kipindi hiki kuwashukuru wateja  wake na umma wa Watanzania  kwa kuikubali bia ya Serengeti kama chaguo lao la hivyo kuifanya kuwa mingoni mwa bia zinazoongoza hapa nchini.


 “Tunawashukuru  wateja wetu, wafanya biashara, wasambazaji, mashirika ya sekta binafsi, serikali na wadau wote  ambao kimsingi wametusaidia  na kuwa nasi  katika safari yetu hii ya mafaniko,” amesema Weesie.


Bia ya Serengeti Premium Lager ni ya kwanza kutengenezwa kwa kimea kwa asilimia 100hapa nchini ikiwa ni ubunifu wa Mpishi Mkuu mtanzania aitwaye Winston Kagusa  ambaye alichanganya mbinu ya utengenezaji wa bia za kijerumani na  vionjo vya hapa nchinikupata kupata kinwaji hiki kinacopendwa na wengi.


Kwa mujibu wa Mkurugenzi Mkuu, bia ya Serengeti ilizalishwa kwa mara ya kwanza ikilenga kufikia sehemu ndogo maalumu ya soko lakini azma hii ilibadilishwa na kuzalishwa kwa wingi kutokana na ongezeko kubwa la mahitaji ya bidhaa hiyo jambo ambalo lilisababisha kuanzishwa uzalishaji zaidi katika viwanda vya SBL vilivyoko Moshi na Mwanza.


Aidha Mkurugenzi huyo ameendelea kusema kwamba katika kipindi chote cha miongo miwili bia ya Serengeti imekuwa na vifungashio vya muonekano tofauti tofauti vinavyoakisi mabadiliko ya kinyakati na mahitaji ya wateja wake. “muonekano mpya tunaouzindua leo hii ni muendelezo wa kielelezo hiki kwamba daima SBL tunajali mahitaji ya wateja wetu na tuko karibu nao, amesema Weesie.


“Tunaona fahari kuzalisha Bia ya Serengeti Premium Lager  katika  ubora uleule wa hali ya juu katika viwanda vyote vitatu, na huu ni uthibitisho halisi kutokana na kutambuliwa  na wateja wetu wa ndani  pamoja na medali  zaidi ya 10  za kutambulika kimataifa  ambazo bia hii imeshinda. Tunaahidi wateja wetu kwamba tutaendeleakuzalisha Serengeti Premium Lager  katika ubora wa hali ya juu  kwa kuzingatia vigezo vya ubora vilivyoanishwa na Shirika la Viwango Tanzania (TBS) na Shirika la Viwango la Kimataifa (ISO),” amesema Weesie.


Uzinduzi wa muonekano mpya wa  bia ya Serengeti pia umekuja na kauli mbiu mpya wa kinywaji hicho cha “Taifa Letu. Fahari Yetu. Bia Yetu.” Aidha kampuni hiyo imewakaribisha wateja wake na wadau mbalimbali kutoka sekta za umma na binafsi katika hafla ya maadhimisho ya miaka 20 ya bia ya Serengeti yatakayofanyika leo jijini Dar es Salaam.



Sita Wafutiwa Adhabu ya Kunyongwa Hadi Kufa

$
0
0
Mahakama ya Rufani imewafutia adhabu ya kunyongwa hadi kufa na kuamuru kuachiwa huru watu sita waliohukumiwa kwa mauaji  ya askari wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU) na mfanyakazi wa Benki ya NMB, tawi la Wami Morogoro.

Uamuzi huo ulisomwa jana na Jaji Projest Rugazia wa Mahakama Kuu, Kanda ya Dar es Salaam baada ya kutolewa na jopo la majaji watatu wa Mahakama ya Rufani lililoongozwa na Jaji Mkuu, Mohamed Chande. Wengine ni Jaji Ibrahimu Juma na Jaji Augustine Mwarija.

Jopo hilo lilikubali hoja za warufani waliowakilishwa na mawakili Richard Rweyongeza, Majura Magafu, Barnabas Luguwa, Samson Mbamba na Gabinus Galikano kuwa Mahakama Kuu ilikosea kuwatia hatiani kwa kuwa haikuwa na ushahidi wa kutosha.


Diamond Platnumz na Mohombi Kuja na Kolabo

$
0
0
Tuzo za MTV MAMA huwakutanisha wasanii wengi wa Afrika kwa wakati mmoja. Si kila anayehudhuria huwa ametajwa kuwania tuzo, bali wengine huenda kwaajili ya kutafuta connection.

Na wengine hutumia fursa hiyo kwenda kufanya video na wasanii waliowashirikisha ili kupunguza gharama za kuwasafirisha kuwapeleka SA kwaajili hiyo. Miongoni mwa watu waliotumia fursa hiyo ni rapper wa Malawi, Tay Grin aliyewahi kuweka wazi nia yake ya kutaka kufanya kazi na Diamond.

Na sasa huenda hilo limekamilika baada ya kuungana na muimbaji huyo wa ‘Salome’ jijini Johannesburg kufanya video ya wimbo unaonekana amemshirikisha Diamond pamoja na msanii wa Sweden, Mohombi.

“We out here with the boy @diamondplatnumz video shoot,” ameandika Tay Grin kwenye picha hiyo ya juu aliyoiweka Instagram. “It’s fire trust! With @mohombimusic ( I wanna boom bang bang with your body ) @iamlumino @chronicles_of_karim_cazal colin the “boss” it’s all love out here! Great things in the pipeline.”

Naye Mohombi aliweka picha akiwa na Diamond kwenye mtandao huo na kuandika: Big Things Coming !!!! #AfricaUnite with my bro @diamondplatnumz

Singeli ni Muziki wa Kihuni, Hautodumu – Juma Nature

$
0
0
Singeli ni muziki ulioibuka kwa kasi na kujizolea mashabiki lukuki na kufanikiwa kuzalisha vipaji kadhaa.

Licha ya kuonekana kufanya vizuri mpaka kufikia kiasi cha kuwashawishi wasanii wa muziki mwingine kujiingiza katika muziki huo, wapo baadhi ya watu wameonekana kutokuwa na imani nao.

Nilifanikiwa kupiga story na msanii mkongwe wa Bongo Flava, Juma Nature, mapema wiki hii katika studio zake za Halisi Records kuhusu muziki huo ambapo yeye alidai kuwa Singeli ni muziki ambao hautoishi kwa muda mrefu bali unapita tu kwasababu ni muziki wa kihuni.

“Singeli itapita tu kwasababu ya uhuni,” alisema. “Unajua raia wengi wa Bongo hawapendi mambo ya kipumb*vu pumb*vu na mashabiki wetu wengi sana sio wahuni ila wahuni wanakuja katika hizi section, so wakija kwenye section hapo muziki hakuna tena,” alisema Nature ambaye hivi karibuni aliachia ngoma yake mpya iitwayo Mtumba.

By Edward Fabian

AliKiba: Walioshinda tuzo za MTV Mama Awards 2016 wamestahili kushinda

$
0
0
Mkali wa wimbo ‘Aje’ AliKiba amefunguka na kuzungumzia ushiriki wa watanzania kwenye tuzo za MTV Mama Awards 2016.

Muimbaji huyo ambaye alikuwa miongoni kati ya wasanii watakaotumbuiza kwenye tuzo hizo na pia aliwania tuzo ya ‘Best Collaboration’ ya wimbo wa Unconditionally Bae alioshirikiana na Sauti Sol, amesema watanzania walijitahidi lakini walizidiwa na wasanii wa nje ndiyo maana wakashindwa kutamba.

“Katika ushindani kuna kushinda na kushindwa sisi hatusemi kuwa tumeshindwa na naamini Tanzania ina vipaji sana na kila msanii anajitahidi kufanya kwa uwezo wake ili aweze kufikisha nchi yetu sehemu nzuri,” AliKiba alikiambia kipindi cha Clouds 360. “Kwasasa muziki wetu umekuwa kwa kasi sana na unazidi kutanuka. Kwa washindi ambao wameshinda kwenye tuzo za ‘MTV Mama Awards’ wanastaili kwasababu kazi wamefanya na tumeziona”

Katika hatua nyingine muimbaji huyo amewataka mashabiki wa muziki wake kukaa makao wa kula kwa ajili ya ujio wa kolabo yake mpya yakimataifa.

TID na Bill Nas Wapatana...Waingia Studio Kuandaa Wimbo

$
0
0
Msanii mkongwe wa muziki TID pamoja na rapa Bill Nas wameingia studio kuandaa project mpya ambayo bado hawajaweka wazi ni project ya namna gani.

Miezi kadhaa iliyopita, TID alilalamika kuwa Bill ni mtu mwenye tamaa na asiye na shukrani baada ya kuondoka Radar Entertainment licha ya kumlea na kumfikisha pahali.

Kwa sasa wawili hao wapo pamoja na wanaonyesha ushirikiano katika mambo yao ya muziki.

Alhamisi hii Bill Nas alipost picha instagram akiwa na TID na kuandika:
#inthekitchen with @tidmusic !! #NENGA #itsbeenawhile Yo! 2ko Around Mazeee
Bill Nas aliwahi kumshirikisha TID kwenye wimbo ‘Ligi Ndogo’ ambao ulifanya vizuri.

Yanga Wamrejesha Kazini Kocha Wao Hans Van Pluijm Leo .......Mwigulu Nchemba Aokoa Jahazi

$
0
0
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi na Mwanachama wa Klabu ya Yanga, Mwigulu Nchemba akiwa katika Mazungumzo na Kocha wa Yanga aliyetangaza kujiuzulu kuitumikia klabu hiyo hivi karibuni, Hans Van Pluijm na kumtaka ajeree kwenye kibarua chake cha kuendelea kukinoa kikosi cha Yanga kinachoshikilia Ubingwa wa Ligi Kuu Tanzania Bara. Kushoto ni Kaimu Katibu Mkuu wa Yanga, Baraka Deusdedit.

CHADEMA yapinga kununuliwa na Lowassa, yashindwa kuzungumzia tuhuma za ufisadi.

$
0
0
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimesema ni uongo na ni propaganda za wapinzani wao kwamba Waziri Mkuu Mstaafu Edward Lowassa alimhonga Mwenyekiti Freeman Mbowe ili kupata nafasi ya kugombea urais mwaka 2015.

Dkt.  Mashinji ameyasema hayo katika kipindi cha Kikaangoni  kinachorushwa na kituo cha EATV kupitia ukurasa wa facebook ambapo wananchi walikuwa wakimuuliza maswali ya papo kwa papo naye anayajibu.

“Si kweli kwamba Mwenyekiti Freeman Mbowe alimhonga Lowassa ili agombee urais kupitia CHADEMA , ni propaganda zinazoenezwa na wapinzani wetu ili kuwadanganya wananchi” Amesema Dkt. Mashinji.

Amesema Lowassa alijiunga na CHADEMA kwa njia halali kwa mujibu wa taratibu za chama, na maamuzi ya kumteua kugombea urais yalifanywa na vikao halali kuanzia ngazi ya Kamati Kuu hadi Mkutano Mkuu.

Kuhusu sababu za CHADEMA kumkaribisha Lowassa licha ya kumtaja miaka mingi kuwa alihusika na ufisadi, Dkt Mashinji, hakutaka kulifafanua kwa undani, lakini aliishia kusema kuwa wao walijiridhisha kuwa hakuwa na hatia yoyote na kwamba kama kweli alikuwa ni fisadi, basi vyombo vya dola vingemchukulia hatua.

"Kama mtu kweli alikuwa ni fisadi, kwanini hakuwahi kuchukuliwa hatua, hata kufikishwa mahakamani?, nadhani hilo tuliache" Alisema kwa ufupi Dkt Mashinji.

Aidha Dkt. Mashinji amewataka watanzania na wapenzi wa CHADEMA kufahamu kwamba chama hicho hakipo kimya bali kinaendelea na mikakati ya kuhakikisha kwamba kinawafikia watanzania kwa kuwatetea kwa kila hali kutokana na mambo yanayoendelea nchini.

Mimi ni Mwanamke Nisiyeweza Ficha Hisia zangu Hata Mkiniona Mshamba – Shamsa Ford

$
0
0
Msanii wa filamu na mama wa mtoto mmoja Shamsa Ford amesema yeye ni mwanamke ambaye hawazi kufisha hisia zake za mapenzi.


Malkia huyo wa filamu ambaye alifunga ndoa miezi mitatu iliyopita na mfanyabishara wa maduka ya nguo Chidi Mapenzi, amesema amekuwa akijiachia katika mitandao ya kijamii kueleza hisia zake juu mume wake kutokana na kudai kushindwa kuzizuia hisia zake.

“Kuna muda huwa natamani dunia nzima ijue ni jinsi gani nakupenda na kukuthamini kwasababu mimi ni mwanamke nisiyeweza ficha hisia zangu hata mkiniona mshamba,” aliandika Shamsa kupitia instagram.

Aliongeza, “Ulikutana na wasichana wengi katika maisha yako lakini ni mimi pekee ndo niliyepata bahati ya kuwa mke wako. Naomba niseme naheshimu siku uliyonitamkia unanipenda, naheshimu siku uliyonitolea barua, naheshimu siku uliyonitolea mahali lakini kubwa kuliko vyote naheshimu siku uliyoapa ndani ya nyumba ya Mungu (Msikiti) kuwa mimi ndo mke wako. Hakika Mungu ndiye aliyetuonganisha mimi na wewe na inshaallah kwa kudra zake tutazikana, nakupenda mume wangu kipenzi aliyenipa Mungu,”

Pia mwigizaji huyo amewataka mashabiki wake wa filamu kukaa makao wa kula kwa ajili ya ujio ya filamu zake mpya.

Picha: Aunty Ezekiel Asherehekea Birthday yake Kimya Kimya

$
0
0
Alhamisi hii ilikuwa ni siku ya kuzaliwa kwa Malkia wa filamu nchini, Aunty Ezekiel ambaye anadaiwa kutimiza miaka 30 lakini kwenye sherehe hiyo imeonekana kuwa ya siri huku akisherehekea na watu wachache aliowaalika.

Viewing all 104785 articles
Browse latest View live




Latest Images