Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104414 articles
Browse latest View live

Tamko: CCM Yawajibu Lowassa na Zitto Pia Yakana Kushiriki Kwenye Kuivuruga CUF

0
0
Ikiwa imepita siku mbili tangu aliyekuwa mgombea wa kiti cha Urais kwa tiketi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kwa mwamvuli wa UKAWA, Edward Lowassa kueleza tathimni ya utendaji kazi wa serikali ya awamu ya tano chini Rais John Magufuli, ambapo alidai kuwa, katika kipindi cha mwaka mmoja wa uongozi huo, kumekuwepo na ukiukwaji wa misingi ya demokrasia na utumishi wa umma kuwa kaa la moto.

Chama cha Mapinduzi (CCM) kimevunja ukimya na kumjibu kwa kusema kuwa katika kipindi cha uchaguzi mkuu uliopita alikuwa wa kwanza kukiuka misingi ya demokrasia. Kuhusu utumishi wa umma kuwa kaa la moto, imemjibu kuwa wanao lalamika hivyo ni wale wanaotumiwa kuficha mafisadi na wakwepa kodi.

Msemaji wa CCM, Christopher Ole Sendeka amewaambia waandishi wa habari kuwa Lowassa hastahili kuituhumu serikali ya Rais Magufuli kuwa inakiuka misingi ya demokrasia.

“Demokrasia ya kweli lazima ianze ndani ya chama, ni demokrasia ipi iliyotoa mamlaka kwa vyama vinavyounda UKAWA kuwanyima wanachama wao haki ya kuomba kupeperusha bendera za vyama walivyoviasisi, kuvitetea kuvigharamia kwa kuamua kumteua mgombea mtunguo ambaye hajapimwa wala hajawahi kuvipigania?,” amehoji.

Ole Sendeka ameongeza kuwa “Kitendo hicho cha kutowashirikisha wanachama na kuwanyima haki yao kikatiba ya kuchagua na kuchaguliwa kulidhihirisha usaliti wa hali ya juu wa misingi ya demokrasia.”

Amesema CCM haigopeshwi na matamko ya Lowassa anayotoa katika vyombo vya habari kwa kuwa havitaiathiri na kwamba imemamua kumjibu kwa madai kuwa anapotosha umma kwa kueleza mambo yasiyo na ukweli.

Ametoa wito kwa vyama vya siasa nchini kutochukulia kwa wepesi masuala ya demokrasia na mabadiliko.

“Wanasayansi wa masuala ya siasa waiangalie demokrasia ya CHADEMA na UKAWA inavyofanya kazi maana ni kihoja, watuambie njia iliyotumika kuwapata wabunge viti maalumu. Kila kiongozi aliteua maswahiba zake na wengine kwa ugeni wao ndani ya CHADEMA,” amesema.

Pia Sendeka amemtaka kiongozi wa Chama cha ACT-Wazalendo kutoichukia serikali ya Rais Magufuli kwa kuwa inatekeleza yale aliyokuwa anayapigania.

“Chuki ya Zitto ya kuendelea kunyooshea kidole serikali ya CCM haina tija, sababu inatekeleza yote aliyokuwa akiyapigania,” amesema.

Katika hatua nyingine, Sendeka amedai kuwa CCM haijashiriki kukihujumu chama cha Wananchi (CUF) kama inavyodaiwa na baadhi ya wanasiasa kuwa kinawachonganisha viongozi wa chama hicho ili kigawanyike.

“Hatuna haja ya kuhangaika na CUF na wapanga siasa za uongozi CHADEMA, hatujashiriki kukivuruga na hatuna muda huo,” amesema.

=======

Ndugu wanahabari,

Kwa muda sasa kumekuwepo na usambazaji wa taairifa za upotoshaji zinazotolewa na baadhi ya wanasiasa wakishirikiana na baadhi ya vyombo vya habari zinazolenga kukejeri, kudhihaki, kukatisha tama, kubeza na kudhoofisha jitihada zinazofanywa na Chama Cha Mapinduzi na Seikali zake katika kuleta maendeleo kwa Watanzania

Kumekuwepo na makala zinazoandikwa na magazeti mawili ya nje ambazo hutolewa kila baada ya miezi miwili na ambazo zinapotosha na kuandika habari zisizo za kweli kuhusu Tanzania

Pia, yapo magazeti mawili ya ndani ambayo yamekuwa yakitoa makala mfululizo kwa kila wiki zinazolenga kumchafua Mheshimiwa Rais na kuichafua taswira ya nchi yetu.

Tumesikitishwa na waandishi wa makala hizo walioamua kujivua uzalendo na kushiriki mpango wa kuiharibu heshima na taswira ya nchi yetu kwa maslahi ya maadui zetu wa nje na baadhi ya wanasiasa. Tunafuatilia kujua nini kinawasukuma kufanya hivyo na kwa maslahi ya nani ilhali sote ni watanzania. Je ni tama ya madaraka tu au mengine?. Hakuna anayepinga ukosoaji bali unapaswa uwe ukosoaji wenye nia njema

Ndugu wanahabari,

Mtakumbuka hivi karibuni aliyewahi kuwa Waziri Mkuu aliyejiuzulu kwa tuhuma za ufisadi ambaye ni mjumbe wa Kamati Kuu ya CHADEMA, Edward Lowassa, alisambaza taarifa kwa vyombo vya habari aliyoiita tathimini ya mwaka mmoja baada ya uchaguzi mkuu wa octoba 25,2015

Katika taairifa yake, alidai kuwa alileta msisimko mpya katika siasa za Tanzania, kwamba ameshirikiana na wenzake kuionyesha nchi yetu maana ya demokrasia na kukosoa juhudi za serikali na wateule wa Rais.

Demokrasia kimsingi ni dhana inayohusisha ushiriki na kuheshimu mawazo ya wengi katika kufikia uamuzi. Ikiwa maana halisi ni hii, tunajiuliza ni ipi demokrasia aliyoionyesha Lowassa ambayo leo anajisifu kuwa nayo?

- Tulishuhudia akiwa mgombea Urais wa chama ambacho hakijui, hakushiriki kukijenga wala kutoa mchango wowote unaompa hadhi ya kupeperusha bendela huku katiba na kanuni ya chama hicho ikivunjwa. Kidemokrasia anayepewa fursa ya kupeperusha bendela ya chama chochote makini duniani ni kiongozi au mwanachama aliyethibitika kwa imani na matendo, kuzielewa, kuzitekeleza, kuzitetea falsafa, itikadi na malengo ya msingi ya chamahicho. Mgombea ni taswira halisi na alama muhimu inayoakisi dhamira ya chama husika machoni kwa wananchi.

- Demokrasia ya kweli lazima ianzie ndani ya chama, ni demokrasia ipi inayotoa mamlaka kwa vyama vinavyounda UKAWA kuwanyima wanachama wao haki ya kuomba ridhaa ya kupeperusha bendera za vyama walivyoviasisi, kuvitetea, kuvigharamia na walivyovitumikia kwa kuamua kumteua mgombea “MTUNGUO” (ambaye hajapimwa wala hajawahi kuvipigania). Kitendo hicho cha kutowashirikisha wanachama na kuwanyima haki yao ya kikatiba ya kuchagua na kuchaguliwa kilidhihirisha usaliti wa hali ya juu wa misingi ya demokrasia

- CHADEMA watuambia njia iliyotumika kuwapata wabunge wa viti maalumu. Ni demokrasia gani inayotoa fursa kwa baadhi tu ya viongozi kuteua wabunge ambao wanakiwakilisha chama chote. Ambapo kila kiongozi aliteua maswahiba zake na wengine kwa ugeni wao ndani ya CHADEMA walikosa watu wanaowafahamu na kuamua kuwateua wanawake maswahiba wao ndani ya CCM. Msingi wa kawaida wa kupata wabunge wa viti maalumu ukiacha kura za maoni, kigezo kingine muhimu ni mchango wa mgombea / mwanachamahuyo katika kukijenga na kukitumikia chama chake. Yaliyotokea kwa CHADEMA kwenye wabunge wake wa viti maalumu ni mapya kwenye ulimwengu wa demokrasia. Inahitaji wataalamu wa sayansi ya siasa kufanya utafiti wa aina hii mpya ya demokrasia

Tulidhani baada ya mwaka mmoja kupita, wenzetu hawa wangelikuwa wamejifanyia tathimini, kujikosoa, kujisahihisha, na hata kufanya uungwana wa kuwaomba radhi wanachama wao kwa uvunjifu mkubwa wa misingi ya demokrasia, katiba na kanuni za vyama vyao

Tunatoa wito kwa vyama vya siasa nchini kutokuchukulia kwa wepesi masuala ya demokrasia na mabadiliko, yasiwe ni nyimbo za kuburudisha au kutoa matumaini hewaq kwa wanachama na wananchi. Kanuni mojawapo ya demokrasia ndani ya vyama ni lazima ionekane katika muundo wake na katika utekelezaji wa muundo huo

Umefika wakati vyama vya siasa vinapaswa kujifunza kuuza sera ili kujenga na sio kusubiri matukio kwa ajili ya kupata huruma ya wananchi. Tunasubiri kushuhudia na kusikia demokrasia demokrasia itakavyoendeshwa katika uchaguzi wa ndani wa vyama hivyo ambapo kuna taarifa mmoja wa vigogo amefanikiwa kupata kiasi cha dola milioni 15 zitakazomsaidia kupanga safu yake ya uongozi

Katika kutimiza mpango huo, tayari yapo mawasiliano ya mara kwa mara ya baadhi ya viongozi wakitoka Zanzibar na sehemu zingine za nchi kuja Dar es Salaaam, na imeonekana dhahiri mazungumzo yao kutowashirikisha viongozi wenzao waandamizi kwani yanalenga kafanikisha mpango huo.

Mheshimiwa Rais Dk John Pombe Magufuli, ameendelea kufanya juhudi kubwa katika kujenga nchi kwa kuimarisha utendaji na nidhamu ya utumishi serikalini, kukusanya mapato na kusimamia matumizi sahihi ya fedha, kupambana na kuzuia mianya ya rushwa pamoja na kusimamia haki, usawa na wajibu kwa raia. Mwenzetu anayaona haya kuwa ni kuufanya utumishi wa umma kaa la moto.

Juhudi hizi na nyinginezo ikiwemo ununuzi wa ndege mpya, ujenzi wa miundombinu ya barabara, reli, afya na kununua vitanda vya wazazi, kutoa elimu burekuanzia shule ya msingi mpaka sekondari na nyinginezo hazipaswi kukatishwa tama kwa maslahi ya wachache ni vyema kuziunga mkono kwa maslahi ya taifa letu

Katika kipindi hiki cha mwaka mmoja wa Rais Dk. Magufuli madarakani, CCM inawaomba wananchi kuendelea kummunga mkono katika dhamira yake safi yakuwaondolea kero, kuboresha huduma za jamii na kuwaletea maendeleo ya kiuchumi na kijamii.

KIDUMU CHAMA CHA MAPINDUZI

Imetolewa na;-

CHRISTOPHER OLE SENDEKA

MJUMBE WA NEC NA MSEMAJI WA CCM

28/10/2016

PICHA: Trump Atumiwa Nywele za Siri Kama Mchango wa Kampeni

0
0
Katika hali ya kustaajabisha mwanamke mmoja wa Florida amemtumia Donald Trump nywele za siri ikiwa ni muitikio wa barua aliyopokea ikimuomba kuchangia kampeni za Trump.

Wema Sepetu na Kujikomba Kote Kwa Aunty Ezekiel atoswa Kwenye Birthday

0
0

Aunty ezekiel kweli ka move on past wema.. Pamoja na wema kujikomba kote kumuwish happy birthday aunt na kumpost mapicha kibao insta, aunty ezekiel kamkaushia mikausho mikali na hata hajamualika kwa birthday yake leo. Kweli wema kaisoma namba na leo ni namba 168.

Nahisi zarithebosslady katumia cheo
Video:

Sumaye: Sirudi CCM hata waninyang’anye Mashamba Yangu Yote

0
0
Siku moja baada ya Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi kutangaza nia ya Serikali kumnyang’anya shamba Waziri Mkuu wa zamani, Frederick Sumaye, mwanasiasa huyo mkongwe amedai hilo halimtikisi.

Sumaye ambaye tayari ameshakabidhiwa notisi ya siku 90 kutokana na kutoliendeleza, amesema kuwa tayari suala hilo ameshaliwasilisha mahakamani na kwamba mwanasheria wake ndiye anayefahamu tarehe iliyopangiwa kesi hiyo.

“Nilienda mahakamani na ikaamuriwa kusiwe na shughuli yoyote, nasubiri tarehe ya kesi ambayo mwanasheria wangu ndiyo anaijua,” Sumaye anakaririwana MwanahalisiOnline.

Mwanasiasa huyo aliyehamia Chadema miezi michache kabla ya kufanyika kwa Uchaguzi Mkuu mwaka jana, amesema kuwa kama CCM wanataka kumdhoofisha kwa kumnyang’anya mashamba ili arejee haitawezekana.

“Kama walidhani kwa kunifanyia hivi nitarudi Chama Cha Mapinduzi (CCM) wasahau, hata kama nilikuwa na nia hiyo sirudi,” amesema Sumaye.

Serikali imetangaza kuanza mchakato wa kumnyang’anya Sumaye shamba lake lililoko Mwabwepande jijini Dar es Salaam kwa madai kuwa ameshindwa kuliendeleza kwa muda mrefu, kinyume na matakwa ya sheria.

Mr Blue Ataja Jina Analotumia Baada ya ‘Simba’ Kupokonywa

0
0
Mr Blue amelitaja jina lake jipya analolitumia baada ya lile la ‘Simba’ kuchukuliwa na Diamond Platnumz.

Rapper huyo amesema kuwa kwa sasa anatumia jina la ‘Nyani Mzee’ kama jina lake jingine la utani.

“Actually kwa sasa jina la Simba nimeliacha ila kwa sasa natumia jina la ‘Nyani Mzee’ nikimaanisha nimekwepa mshale mingi. Nasubiri na hilo wachukuwe nitafute jina jingine,” amekiambia kipindi cha Planet Bongo cha EA Radio.

Mwezi Disemba mwaka jana Mr Blue na Diamond waliingia kwenye mzozo kuhusiana na jina la ‘Simba’ huku kila mmoja akidai ni lake.

Aibu Niliyoipata Kesho Nahama Nyumba Hii, Jifunzeni Wanaume Wenzangu

0
0
Jaman hiki kiitwacho wadudu wanaonyevuanyevua a.k.a ny-ge ni hatari na yanaweza kukudhalilisha yamenikuta mwenzenu.

mi naishi sinza nyumba ya tatu baada ya hotel ya vatcan city nimepanga kwa mama mmoja maaruf kama mama k------- kiukwel kati ya wapangaji 6 wa bi mkubwa huyu mi ndo nilikuwa mfano wa kuigwa kwa tabia ya kujiheshimu kwa kutoingiza wanawake ovyovyo kama jamaa wawili wa vyumba vya uwani na madada wa chumba cha mbele wanaosifika kwa kuingiza wanaume waziwazi.

basi jioni ya Jana nlikuwa ktk hali ya mwili kutamani tendo kupita kiasi na kwa bahati nzuri hapa mtaani hii nyumba nnayokaa ndiyo maarufu kwa majirani kuja kuchota maji,saaasa si ndo nkamuona msichana mmoja huwa napewa sifa zake kwamba ana roho nzuri sana pia nlishamshuhudia Mara kadhaa akitoka ktk vyumba tofauti vya jamaa wa vyumba vya uani hivyo nami nkaadhimia kuua tembo kwa ubua nkamwomba awe mgeni wangu akaniambia nimuandalie castle light 3 ataingia saa NNE nne hivii.

basi ilipofika saa nne bint akaja tukaingia zetu ndani,akapiga zake bia mi kwa kawaida situmii kilevi.basi mida ya kama saa 6 usiku tukaanza mambo yetu sasa katikati ya shughuli mwenzangu akaanza kunifinya nikajua ndo mizuka yake tu,Mara akaanza kutoa sauti ya kuinguruma mi nkajua ndo utamu umekolea nkawa naendelea tu,akaanza kunipiga makofi ya mgongo la kwanza nkaona kawaida la Pili nkasema isiwe tabu nkashuka,kumbe binti ana mashetani bwana akanisogelea na kuanza kunikamata kichwa na kunigongeza ukutani mi nlikuwa nagugumia kimyakimya nikihofia kuwaamsha watu watajua nimeingiza mwanamke.

akaendelea kunigongeza nikaona ataniua nikapiga kelele wapangaji wote na familia ya mwenye nyumba wakaamka.wakafanikiwa kuvunja mlango na kutukuta tukiwa uchiii huku mi nimekabwa na msichana akiongea lugha isiyoeleweka.

heshima yangu niliyoijenga imeharibiwa kwa siku moja tu kisa ny-g- mtaa mzima nimekuwa tangazo.

wanaume wenzangu ogopeni kuvamiavamia wanawake msiowajua vizuri mtaaibika

By Mbagokizega

Jipatie Dawa Asili za Kutengeneza Shepu, Kuondoa Michirizi Chunusi, Kurefusha Nywele Toka Markson Beauty Products

0
0
HABARI NJEMA MARKSON BEAUTY PRODUCTS
Baada ya kupata cheti cha bidhaa bora kwa mwaka 2015-2016, Sasa kampuni hii inasambaza huduma zake ndani na nje ya nchi kwa vibali maalum. Bidhaa zetu zimetengenezwa kwa mimea na matunda na kudhibitishwa. Hazina kemikali wala madhara. DAWA ZETU NI YA:-

  1. kurefusha nywele na kuzuia kukatika ovyo @100,000/=
  2. Kuongeza shepu (hips na makalio) kwa/= (a)Dawa ya kunywa au kupaka @150,000/=(b)Vidonge @170,000/=
  3. Kuwa mweupe na softi mwili mzima kwa:- (1)Mafuta @100,000/= (11)Vidonge @150,000/=
  4. Kupunguza unene na manyama uzembe @120,000/=
  5. Kuongeza uume pamoja na nguvu za kiume kwa:-(a) Gely ya kupaka @100,000/= (b) Vidonge maalum @120,000/= (c) Handsome up original @170,000
  6. Kuondoa mvi milele zisiludi tena @100,000/=
  7. Kuongeza unene wa mwili mzima na uzito @120,000/=
  8. Kupunguza tumbo (kitambi) na nyama za pembeni kwa:- (a) Dawa ya kunywa au kupaka @120,000/= (b) Mkanda wa kawaida @100,000/= (c) micro-computer belt unaovaibret @200,000/=
  9. Kupunguza maziwa na kuyasimamisha @90,000/=
  10. Kushepu miguu na kuwa minene @100,000/=
  11. Kuondoa mipasuko mwilini (michirizi) @90,000/=
  12. kubana uke na kuongeza hamu ya tendo la ndoa kwa mwanamke @100,000/=
  13. Taiti za hips na makalio @150,000/=           
NB: Hakikisha unapata risiti yenye muhuri halisi wa MARKSON CO pamoja na garantii kwa bidhaa halisi. Wasiliana nasi :-(+255) 0767447444 na 0714335378 Google MARKSON BEAUTY.
Follow us
@Markson_beauty_pr
@Markson_beauty_pr

U Heard: Picha za Mpenzi Mpya wa Baraka The Prince Zimevuja Mitandaoni

0
0
Hit maker wa mdundo wa Nisamehe Baraka the Prince ambaye ni mpenzi wa mrembo kutoka Bongoflevani Naj, leo kwenye U Heard ya Soudy Brown ya Clouds FM ameingia kwenye headlines baada ya kubainika kuvuja kwa picha za msichana anayedaiwa kuwa ni mpenzi wake mpya kwenye mitandao ya kijamii

‘Mimi na baraka tumeshamalizana na jana tulienda Polisi yameshaisha alafu ukiniambia kuwa eti Naj atanipiga kwani yeye ni nani au kisa amenizidi weupe na Nywele ndefu, alafu naniamekwambia mahusiano yangu na Baraka yamevunjika‘ Betty 
‘Unajua hizo video zinaoendelea kwenye mitandao ya kijamii na ni tulikuwa location tunashoot nyimbo ya msanii mpya anaitwa Brian na wala mimi sijampeleka mtu Polisi‘ Baraka the Prince

Kuisikiliza U Heard ya October 28 2016 bonyeza Play Hapa chini..

Maneno ya Linah Sanga Baada ya Kumpost Mpenzi Wake Mpya Instagram

0
0
Ni msanii wa Bongo Fleva, Lina Sanga ambae October 28, 2016 amechukua headlines mitandaoni baada ya kumpost rasmi mpenzi wake mpya.

Staa huyo kupitia kwenye ukurasa wake wa instagram aliyaandika haya
"Penzi si kama nyanya itokayo sokoni, nipe penzi ❤️mwanana niliote ndotoni 😂😂😂 i love u cheusi wangu, Mara moja moja, Raha jipe mwenyewe"

WEMA Sepetu Achoshwa na Timu Wema Aanza Kuwa Block Vinara wa Timu hiyo Instagram..Aanza na Huyu

0
0
Wema Aanza kuwapa Block Vinara wa Team Wema....Msikie huyu......



#Regrann from #myboowemasepetu - Msema ukweli kipenzi cha mungu. Msione najichekesha chekesha mkazani nimefurahi. Ukweli ni kwamba nimeumia sana adi chozi limenidondoka 😢 inachoma kama pasi 😭😭😭😭. Wema ulianza kumblock legend wetu katika team anaitwa @kimbwi222 iliniuma sana, leo mimi @myboowemasepetu kesho sijui nani. To be honest naumia 😢😭😭😭 un follow ilikuwa haitoshi madam ukaona unipe sollex. Umesahau mazuri yote umekumbuka baya moja tu la jana kisa kumponda aunt. Na sijamponda nimeongea ukweli sasa unataka tufagilie adi ujinga unaofanya. Wema your loosing amka kwenye huo usingizi mzito ulionao. Wanajua hakuna team inanguvu insta kama teamwema, wanakupoteza ukose mtetezi daaaaah nashindwa ata cha kuandika. Mungu mwenyewe ndo anajua kuwa ninamapenzi ya kweli kwako. Watakaonicheka na wanicheke nimeongea ukweli kutoka moyoni. Na asante sana kwa block 🙏🙏🙏🙏. Life goes on .... "
MPE ushauri....

Mambo 10 Ambayo ni Sumu Katika Mapenzi

0
0
KATIKA harakati zako za kutafuta mpenzi, unaweza kukutana na mwanamke ambaye kwa sababu moja au nyingine anakwondolea uwezo wako wa kufikiri, kutumia mantiki na pia kutumia akili yako ya kuzaliwa. Si lazima awe amekufanyia kitu, lakini inaweza kuwa ni ulevi wako tu unaosababisha ufanye mambo yasiyo ya kawaida. Pengine ndiyo maana baadhi ya wasanii huzungumzia suala la “kudata” kutokana na mapenzi.

Ni jambo jema kudhani kuwa wewe na mpenzi wako mnapendana kwa dhati na kwamba kila mmoja amefika kwa mwenzake, lakini kama mojawapo ya mambo haya kumi yaliyoelezwa hapa chini litajitokeza, basi fahamu kuwa yamkini umependa kuliko kawaida, yaani ni kama umenyweshwa sumu ya penzi. Kumbuka kupenda ni kuzuri, lakini kupenda kupindukia kunaweza kukutumbukia nyongo, kwani katika kila jambo kinahitajika kiasi.

1. WIVU WA KUPINDUKIA
Ni jambo jema kwa mwanamume kumtakia heri mpenzi wake na kufanya kila awezalo kuhakikisha kuwa hapati madhara, lakini iwapo utakuwa mtu wa wasiwasi na mashaka pale unapomwona mpenzi wako akizungumza na mwanamume mwingine, au anapotoka na marafiki zake wa kike, au anapovaa nguo inayomfanya atamanishe, basi fahamu kuwa tayari umekunywa sumu ya mapenzi.

Katika uhusiano wa kimapenzi, kuaminiana ni jambo muhimu sana. Kama kweli unataka mpenzi wako akupende kwa dhati, mwoneshe kuwa unamwamini na unaheshimu maamuzi yake, ikiwa ni pamoja na maamuzi ya kutoka na marafiki zake wa kike na kuwa na marafiki wa kawaida wa kiume. Ondoa hofu na acha kabisa kumpeleleza, maana wapo wanaume ambao hutumia muda wao mwingi kuwapeleleza wapenzi wao ikiwa ni pamoja na kuwategeshea kamera na rekoda za simu.

2. KUTOMWACHIA NAFASI MPENZI
Kama huishi na mpenzi wako ni jambo la kawaida kuwa na hamu ya kumwona mara kwa mara, lakini kumbuka kuwa mpenzi wako naye ana maisha yake na anahitaji nafasi ya kuwa peke yake kwa ajili ya mambo yake binafsi.

Hisia za kutaka kuwa na mpenzi wako muda wote zinaweza kudhaniwa kuwa ni za mapenzi ya dhati, lakini kwa hakika hiyo si ishara njema ya mapenzi ya kudumu. Hebu jiulize kama unaweza kuendeleza hali hiyo maisha yako yote. Ni wazi kuwa utachoka. Kwa hiyo, mpe mpenzi wako fursa ya kupumua. Namna hii mpenzi wako atajenga hamu ya kutaka kukutana nawe lakini ukiwa naye muda wote hamu hiyo itaisha.

3. KUMWAMULIA MPENZI MAMBO YAKE
Unaweza kujikuta ukisukumwa kumwambia mpenzi wako awe anavaa nini wakati gani, akutane na nani na kwa wakati gani au ale nini. Ukiona hivyo, fahamu kuwa hayo si mapenzi, bali umepitiliza na pengine mwisho wa uhusiano wenu unanukia.

Hata ukiachilia mbali suala zima la usawa wa jinsia, hakuna mwanamke ambaye angependa apangiwe kila kitu kuhusiana na maisha yake. Kama ilivyodokezwa hapo juu, kila mtu ana maisha yake na kilichowaunganisha ni mapenzi tu. Kama utataka kumpangia kila kitu ni wazi kuwa utaishia kuishi peke yako.

4. KUMUULIZA MPENZI MASWALI
Iwapo utajikuta ukimuuliza mpenzi wako maswali mengi yanayoonesha wasiwasi wako kuhusiana na mwenendo wake, fahamu kuwa kuna tatizo na tatizo hilo lisipopatiwa ufumbuzi utakuwa mwanzo wa mwisho wa uhusiano wenu.

Mwanamke angependa umuulize maswali ya kawaida kuhusiana na jinsi siku yake ilivyokuwa na kama marafiki zake hawajambo au la, lakini kila jambo lina mpaka wake. Mwanamke hatarajii kuwa kila mnapokutana atakuwa kama ameingia kwenye chumba cha mtihani au usaili wa kazi.

5. KUTOAMINI ANACHOKWELEZA MPENZI
Wakati mwingine watu hushindwa kuwaamini wenzao, lakini kwa sababu ambazo ni za msingi, lakini kuna wakati ambapo mtu hushindwa kumwamini mwenzake bila sababu yoyote ya msingi, au kwa sababu zisizo sahihi, kisingizio kikiwa ni mapenzi.

Kuna tatizo la kisaikolojia la kujishuku au kuwashuku wenzako. Hili ni jambo ambalo linaweza kukuharibia mustakabali wako katika mapenzi, maana husababisha kujengeka kwa mazingira ya kutokuaminiana. Ili uweze kwenda sanjari na mpenzi wako, amini kila anachokweleza hadi pale utakapokuwa na sababu za msingi za kutokumwamini. Na hata unapokuwa umelithibitisha jambo, endelea kuwa katika uhalisia wako.

6. KUACHA HOBI, MARAFIKI
Mahusiano ya kimapenzi mara nyingi huhusisha kila mmoja kuacha baadhi ya mambo yake kwa ajili ya mwenzake. Hata hivyo, lengo ni kuweka tu uwiano wa mahitaji, si kuacha kila kitu ulichokuwa nacho kwa ajili ya mwenzako, ama kwa shinikizo, au kwa kulewa penzi.

Iwapo utabaini kuwa marafiki zako sasa wamekuwa ni marafiki zako wa zamani na hobi zako zimebaki tu katika kumbukumbu japo kwa hakika bado unahisi mapenzi katika hobi hizo, basi tambua kuwa huyo mrembo wako amekunywesha sumu ya penzi na sasa huwezi hata kuitumia vema mantiki yako.

Mbaya zaidi, iwapo utabaini kuwa marafiki zako wapya ni marafiki wa siku zote wa mpenzi wako na hobi zako ni zile za mpenzi wako, basi tambua kuwa huna tena nafsi yako, bali umejisalimisha mzima mzima kwa mpenzi wako. Lakini msemo mmoja wa hekima unatwambia usiweke mayai yako yote kwenye kikapu kimoja. Yamkini unaelewa.

7. KUKUBALI KUPELEKESHWA
Pengine unakumbuka kuwa kuna nyakati ambapo ulikuwa na uwezo wa kujikita katika jambo moja na kulifanya kwa umakini, huku ukiwa pia mwerevu, mjanja na unayejisimamia, lakini leo unayeyuka kirahisi tu kama barafu iliyowekwa juani! Hii ni hatari kwa mustakabali wa maisha yako.

Mbaya zaidi ni pale utakapoiacha kazi yako inayokulipa vizuri na kufanya kazi nyingine kwa ajili ya kumfurahisha mpenzi wako. Ukifika hali hii ujue wewe mwenyewe kuwa hapo hakuna mwanamume.

8. UTAYARI WA KUFA KWA AJILI YAKE
Umewahi kujisikia kuwa na utayari wa kufa kwa ajili ya mpenzi wako? Kama jibu ni “ndiyo”, basi fahamu kwa hakika kuwa hayo uliyo nayo si mapenzi bali ni upumbavu. Pengine huku ndiko kunywesha sumu ya mapenzi. Kwa hakika, hakuna mwanamke ambaye anastahili kumfanya mwanamume yeyote kufa kwa ajili yake.

Yamkini wanaume wanaolengwa katika makala haya si wavulana wanaosoma sekondari, waliobalehe majuzi, ambao wakipenda au kupendwa hujiona kama wako katika sayari yao. Mwanamume aliyepevuka hujiamini na hayaweki maisha yake yote mikononi mwa mwanamke, hata kama mwanamke huyo angekuwa ndiye mrembo wa dunia.

Iwapo, ama kwa ujinga au kwa kufahamu umewahi kumwambia mpenzi wako: “Ukiniacha nitajiua,” na ukawa unaamini hivyo kabisa, basi yamkini unahitaji kutafuta msaada wa ushauri nasaha, maana kwa hakika umepotoka.

9. MUDA WOTE UNAWASILIANA NAYE
Vijana wa siku hizi ni watumiaji wazuri sana wa simu, lakini iwapo utabaini kuwa asilimia kubwa ya muda wako unautumia ama kwa kuongea au kuwasiliana kwa ujumbe mfupi na mpenzi wako, basi fahamu kuwa kuna tatizo ambalo linahitaji ufumbuzi wa haraka.

Kumbuka kuwa mapenzi hayachukui nafasi ya kila kitu. Yamkini huyo mpenzi wako amekukuta unaishi na kuna mambo ya muhimu ya kufanya. Hebu achana na simu kwanza ufanye mambo ya muhimu kuhusiana na maisha yako. Kama mpenzi wako hakwelewi katika hili basi hakufai.

10. NDUGU ZAKE WANAKUFUATILIA
Iwapo utabaini kuwa marafiki, ndugu na jamaa za mpenzi wako wanamtonya mpenzi wako kuhusiana na kile wanachokiita mwenendo wako mbaya, usipuuze hali hii. Kuna uwezekano mkubwa kuwa watu hawa wanayo sababu ya kuwa na wasiwasi na mwenendo wako, kwa hiyo jichunguze na kuangalia jinsi unavyoenenda.

Hata hivyo, jambo hili si ishara njema ya mustakabali mwema wa uhusiano wenu. Iwapo mpenzi wako ataweka watu wake wakufuatilie, maana yake halisi ni kwamba hakuamini. Katika hali kama hii, haitarajiwi kuwa mustakabali wa uhusiano wenu utakuwa mzuri, kwani kutakuwa na uingilizi mwingi wa ndugu, jamaa na marafiki zake. Unaweza kukubali kuendelea kuishi katika hali hii kwa kisingizio cha mapenzi, lakini ukweli ni kwamba hayatakuwa mapenzi bali karaha.

KUWA MAKINI
Kama unavyoona, hizi ni baadhi tu ya dalili kuwa mapenzi yako kwa mwanamke sasa yanaelekea katika ulevi, mithili ya ule wa dawa za kulevya. Jambo moja la kukumbuka ni kwamba kweli mapenzi ni kitu kizuri, lakini pia mapenzi yanahitaji kuwa jambo linaloashiria mustakabali mwema kwa wahusika wawili. Yakiwapo mambo haya kumi hauwezi kuwapo mustakabali mwema katika mapenzi.

Madudu NSSF yaweka rehani ubalozi wa Dk Dau

0
0
Methali isemayo samaki mmoja akioza wote wameoza haisaili hali inayoendelea katika Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF) ambako hadi sasa wakurugenzi sita na maofisa sita wako nyumbani kusubiri hatima yao kuhusu ushiriki wao kwenye miradi inayotiliwa shaka.

Wakati wakurugenzi hao wakiwa gizani kusubiri hatima yao, aliyekuwa mkurugenzi wao mkuu, Dk Ramadhani Dau  yuko Kualar Lumpa, Malaysia akiwakilisha nchi kama balozi.

Kwa kawaida, samaki mmoja akioza ni nadra kukuta wengine ndani ya tenga moja wakiwa hawajaharibika, na hata harufu huwa ni moja.

Lakini ni vigumu kutumia msemo huo kuelezea sakata hilo la NSSF kutokana na maofisa hao waandamizi kusimamishwa kutokana na miradi kadhaa ya ujenzi wakati bosi wao akipandishwa cheo kuwa balozi na baadaye kupelekwa Malaysia ambako anaendelea na kazi za kibalozi.

Dk Dau aliteuliwa kuwa balozi katika kipindi ambacho taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) ikiwa imevuja kwenye vyombo vya habari, ikionyesha harufu ya ufisadi kwenye miradi ya shirika hilo kubwa ya hifadhi ya jamii iliyopo Kigamboni.

Alikuwa akiongoza kikao cha viongozi wa mikoa wa shirika hilo, lakini akaacha ghafla baada ya kupokea simu na kutoweka. Baadaye ilitangazwa kuwa ameteuliwa kuwa balozi.


Lakini, taarifa ya Ikulu ya Februari 15 haikueleza chochote kuhusu sakata hilo zaidi ya kusema atapangiwa kituo baadaye.

Wakati hali ikiwa haieleweki, Julai 15, wakurugenzi hao sita wa NSSF na mameneja watano na ofisa moja walitangazwa kusimamishwa kazi hadi uchunguzi wa masuala yanayohusu miradi ya ujenzi na ardhi itakapokamilika.

Lakini wakati hali ikiwa bado haijaeleweka, mwezi Septemba, Rais John Magufuli alitangaza kumpangia Dk Dau kituo cha kazi na baadaye kumuapisha tayari kwa kazi hiyo ya kuwa Balozi Malaysia.

Kwa kawaida, Mkurugenzi Mkuu wa shirika ndiye kiongozi wa vikao vya menejimenti vinavyohusisha wakurugenzi wote. Menejimenti ndiyo huhusika na uendeshaji wa shughuli za kila siku za shirika, ikiwa ni pamoja na miradi.

Mkurugenzi mkuu pia ni mjumbe wa Bodi ya Wakurugenzi wa shirika. Bodi hupanga na kutoa mwongozo wa shughuli zote za kibiashara na shirika.

Alipoulizwa kuhusu suala hilo, mhadhiri wa zamani wa Chuo cha Diplomasia, Profesa Abdallah Safari alisema upo uwezekano kuwa Dk Dau aliachwa kwa makusudi wakati uchunguzi ukiendelea kufanywa dhidi yake.

Lakini, msemaji wa Serikali ambaye ni Mkurugenzi wa Habari (Maelezo), Hassan Abbas alisema: “Mashirika ya umma yana bodi zake. Watafutwe viongozi na Msajili wa Hazina ambaye mashirika yote yako kwake. Mimi siwezi kuzungumzia masuala ya shirika.”

Kati ya Januari na Februari kumekuwa na mgogoro wa malipo katika uwekezaji wa miradi iliyobuniwa na Bodi ya NSSF kwa ushirikiano na kampuni ya Azimio Housing Estate Limited (AHEL). Vibarua karibu wote walifukuzwa kazi baada ya kukosekana fedha za kuwalipa.

Baadaye iligundulika kuwa kampuni ya Azimio ilishindwa kutoa fedha kwa mujibu wa mkataba wa miradi ya ujenzi wa mji wa kisasa wa Dege Eco Village, Kigamboni, Dar es Salaam wenye thamani ya Dola za Marekani 653 milioni (Sh1.2 trilioni), na wa Arumeru, Arusha uliokuwa na thamani ya dola 3.34 bilioni (sawa na Sh7.2 trilioni).

Januari 21, NSSF na Azimio walilazimika kusitisha mradi wa Arumeru huku shirika likiwa limetoa Sh43.9 bilioni kwa ajili ya ushauri. Februari, mradi wa Dege ulisitishwa huku shirika likiwa limechangia Sh270 bilioni.

Matokeo tofauti

Dk Dau, ambaye amekuwa nembo ya mafanikio au kupanda na kushuka kwa shirika hilo, alipewa kazi mpya huku wakurugenzi sita na maofisa sita wakisimamishwa kazi kupisha uchunguzi kuhusu ushiriki wao katika miradi yenye kashfa.

Februari 15, Rais John Magufuli aliteua watu watatu kuwa mabalozi wapya, akiwemo Dk Dau hali iliyotafsiriwa kwamba anaondolewa katika nafasi ya mkurugenzi mkuu na kupewa cheo kikubwa. Wengine walioteuliwa ni Dk Asha-Rose Migiro na Mathias Chikawe na ilielezwa kwamba wangepangiwa vituo baadaye.

Machi 6 yaani siku 22 tangu Dk Dau aondolewe, lilifanyika jaribio la kujaza nafasi hiyo baada ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Jenister Mhagama kumtangaza Carina Wangwe, lakini uteuzi huo ulidumu kwa saa tano tu kabla ya kutenguliwa usiku.

Machi 18-31, mwaka huu, vyombo vya habari, likiwamo Gazeti la Mwananchi viliibua na kuripoti kwa kina ufisadi ulivyofanyika katika miradi ya NSSF;  kuanzia wa Dege, Mwanza, Mtwara hadi Arusha. Uozo ulihusisha makandarasi kulipwa fedha zaidi ya zilizoidhinishwa au kulipa mara mbili kwa kazi ileile.

Machi 19, Rais Magufuli alimteua Profesa Godius Kahyarara kuwa mkurugenzi mkuu mpya wa NSSF.

Aprili 19, wakati wa uzinduzi wa Daraja la Mwalimu Nyerere linalounganisha wakazi wa eneo la Kurasini na Kigamboni, Rais Magufuli alimsifu Dk Dau kwa ubunifu na usimamizi wa ujenzi wa daraja hilo ambalo alisema ni msaada mkubwa kwa wakazi wa Dar es Salaam.

“Watanzania huwa tunasahau sana, mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpeni,” alisema Rais Magufuli hali iliyotafsiriwa na wachambuzi wa masuala ya siasa kuwa alifurahishwa na utendaji wake.

Aprili 25, CAG, Profesa Mussa Assad aliwasilisha bungeni ripoti ikitia muhuri uchunguzi wa vyombo vya habari juu ya namna NSSF ilivyoingia ubia na kampuni binafsi ya Azimio isiyo na mtaji kujenga miradi mikoani Dar es Salaam na Arusha na ili kurahisisha kazi walianzisha kampuni ya Hifadhi Builders Limited.

Ripoti ya CAG ilionyesha udanganyifu katika mradi wa Dege. Azimio, iliyodai ina ekari 20,000 ilibainika kuwa na ekari 3,503 tu baada ya uchunguzi na hata ekari 300 ilizotoa katika awamu ya kwanza zilikuwa pungufu.

Vilevile, CAG alieleza kusikitishwa katika mradi wa Dege ambako ekari moja ilithaminishwa kwa Sh800 milioni huku katika mradi wa Arumeru ekari moja ilithaminishwa kwa Sh1.8 bilioni wakati wenyeji wanauza ekari moja chini ya Sh5 milioni.

Juni 29, Rais Magufuli alimteua Profesa Samwel Wangwe kuwa mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya NSSF.

Julai 18, Bodi ya Wakurugenzi ilitumia msemo wa bahati ya mwenzako usiilalie mlango wazi baada ya kutoa taarifa ya kuwasimamisha wakurugenzi sita na maofisa wengine sita kupisha uchunguzi juu ya ushiriki wao katika mradi wa ujenzi wa mji wa kisasa wa Dege Eco Village, Kigamboni ambako ripoti ya CAG ilionyesha ufisadi wa kutisha.

Waliosimamishwa ni Yakub Kidula (mipango, uwekezaji na miradi), Crescentius Magori (uendeshaji), Ludovick Mrosso (fedha), Chiku Mattesa (raslimali watu na utawala), Pouline Mtunda (ukaguzi wa ndani), Sadi Shemliwa (udhibiti athari), Amina Abdallah (meneja ununuzi), Chedrack Komba (meneja mkuu Kinondoni), Davis Kalanje (mhasibu mkuu), Abdallah Mseli (meneja miradi na uwekezaji), John Msemo (meneja miradi) na John Ndazi (ofisa umiliki).

Julai 19, mwenyekiti wa Bodi ya NSSF, Profesa Wangwe aliiambia Mwananchi kwamba hawezi kuzungumza lolote kuhusu hatima ya Dk Dau kwa vile si mwajiri wao.

“Bodi haiwezi kuchukua hatua dhidi yake, vyombo husika vitaamua kuhusu hilo,” alisema Profesa Wangwe.

Septemba14, Dk Dau aliapishwa kuwa Balozi wa Malaysia. Kuapishwa kwa Dk Dau na kisha kupangiwa kituo kulihitimisha minong’ono na mijadala katika mitandao ya kijamii kuhusu hatima ya mkurugenzi huyo.

Oktoba 26, Profesa Kahyarara aliiambia Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) kuwa mradi wa Dege umesimama na wanahofia kupoteza Sh270 bilioni kutokana na kushirikiana na mbia ambaye hakuwa na fedha.

Profesa Kahyarara aliwaambia wajumbe kuwa mradi huo ulisimama tangu Februari na kwamba juhudi zinafanyika kuhakikisha mbia huyo AHEL anarejesha fedha.

“Tukitoka kwenye ubia huu tunaweza kupoteza fedha hizo tupo makini kuhakikisha mwekezaji huyo Azimio anarejesha fedha hizo,” alisema Profesa Kahyarara.

Wachambuzi

Akizungumzia hali hiyo, Profesa Abdallah Safari alisema: “Binafsi sioni kama ubalozi ni kupandishwa kutoka nafasi aliyokuwa nayo kama mkurugenzi wa shirika kubwa halafu kupelekwa kuwa balozi. Naweza kusema ameshushwa.

“Huenda wameona yeye ni mtu mzito ndiyo maana wakamtoa hapa ili uchunguzi uendelee labda uwepo wake ungeharibu.”

Mbunge wa Kaliua, Magdalena Sakaya alisema kitendo cha Dk Dau kuachwa hadi leo ni ishara serikali imeshindwa kuzingatia utawala bora.

“Ni heri basi angepelekwa mahakamani halafu ikathibitika hajahusika, lakini kuteuliwa kwake kwenda kuiwakilisha nchi nashindwa kuelewa kama kweli vita dhidi ya ufisadi inatekelezwa kwa haki,” alisema.

Mbunge wa zamani wa Kigoma Kusini (NCCR-Mageuzi), David Kafulila alisema hicho ni kipimo kikubwa kwa Rais Magufuli katika vita yake dhidi ya ufisadi.

Kafulila alisema ufisadi wa NSSF ni zaidi ya ule wa Escrow na hatua hazichukuliwi kutokana na mfumo wa Serikali kuhusika katika hilo.

“Inavunja moyo kama ufisadi unaogusa mamlaka za juu za Serikali hauguswi, unaishia kuwatumbua watendaji wa chini,” alisema Kafulila.

“Watanzania wanasubiri kuona makali ya JPM katika hili. Kama ameamua kupambana kweli na ufisadi basi afanye hivyo kwa haki na usawa kwa wote bila kujali sura au uwezo. Wengine wanafukuzwa kazi bila hata kuhojiwa wakati Dau anapewa heshima ya ubalozi,” alisema.

Bibi Aliyejichongea Jeneza Afariki Dunia

0
0
Mkazi wa Kijiji cha Lindusi Peramiho mkoani Ruvuma aliyejichongea jeneza, Scholastica Mhagama amefariki dunia  kwa ugonjwa wa pumu.

Mapema mwaka huu wakati alipohojiwa na gazeti hili, bibi huyo alitaja sababu za kujichongea jeneza kabla ya kifo kuwa, ni kuhofia kuzikwa kama mnyama baada ya kuwa na ugomvi wa mara kwa mara na kaka zake.

Kaka yake mkubwa aliyekuwa akimhudumia kabla ya kufariki dunia, Felix Mhagama (82) alisema dada yake alikufa Jumanne ya wiki iliyopita kwa ugonjwa huo.

Mhagama alisema licha ya kipindi cha uhai wa dada yao, kugombana mara kwa mara walikuwa wakipatana na kumaliza tofauti zao.

“Ingawa mdogo wangu alikuwa na upungufu niliendelea kuzungumza naye na kumhudumia, kwani hakuwa na uwezo wa fedha na alinitegemea kwa kila kitu,” alisema. Alisema alikuwa akiumia kuona dada yake akiishi na jeneza hilo na kwamba, kuna wakati alimuuliza sababu za kufanya hivyo, alimjibu kuwa ni kutokana na kutokuelewana kwao.

Alibainisha kuwa kabla ya kifo chake, kuna watu walikwenda nyumbani kwake na kuvunja jeneza hilo na kuahidi kumtengenezea jingine.


Kuhusu chanzo cha ugomvi wa Scholastica na kaka zake, jirani yao, Cassian Kazimoto alisema  alikata tamaa ya kuishi kutokana na maradhi hayo ya pumu yaliyokuwa yakimsumbua na ulemavu baada ya kukatwa mguu.

Alisema  Scholastica alikuwa akiona kama anaonewa na kaka zake kutokana na ugomvi wao.

Mpenzi Mpya wa Wema Sepetu Afungukia Kwanini Alisema Hamjui Idris Sultan

0
0
Model Calisah ambaye anadaiwa kutoka kimapenzi na Wema Sepetu amekataa kuzungumzia mahusiano yake na Wema Sepetu pamoja na kueleza kwanini alisema hamjui aliyekuwa mpenzi wa zamani wa Wema Sepetu na mshindi wa Big Brother 2014, Idris Sultan.

wema-sepetu-1

Wiki moja iliyopita kupitia kipindi kimoja cha runinga, model huyo alisema hamjui Idris Sultan.

Akiongea na Bongo5 Jumanne hii, Calisah alisema ni kweli kwamba hamjui Idris Sultan na wala hakuongea kwa nia mbaya au kutafuta kiki.

“Mimi nashangaa kwanini watu wamepanic kisa kusema simjui Idris Sultan, kwani yeye ni nani kila mtu amjue?,” aliuliza Model huyo. “Wewe kuna wanamichezo wangapi wameshachukua tuzo kubwa duniani hawajui?. Kwahiyo mimi nadhani watu ambao wananishambulia katika mitandao hawajui nini wanafanya,”

Aliongeza,”Sikusema hivyo kuonyesha dharau, kwa sababu nipo karibu na Wema lakini hajawai kuniambia kuhusu mtu kama huyo na sijawahi kumuona naye, na kama ukiwa na mwanamke halafu akawa azungumzia mwanaume mwingine hizo ni dharau sana. Kwahiyo kiukweli mimi jamaa nimeanza kumjua baada ya watu kinitag picha zake katika mitandao ya kijamii,”

Pia model huyo alisema kwa sasa hawezi kuweka wazi kama ni kweli anatoka kimapenzi na Wema Sepetu huku akidai Wema ndiye atayekuwa na jibu sahihi juu yake.

Ufisadi NSSF: CCM Yataka Akaunti za Zitto Kabwe Zipekuliwe.

0
0
CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimeitaka Serikali kuhakiki akaunti na mali za Mbunge wa Kigoma Mjini, Zitto Kabwe (ACT) na wenzake waliokuwa katika kamati za fedha za Bunge, ili kubaini kama zinalingana na kipato walichokuwa wakipata.

Msemaji wa chama hicho, Christopher Ole Sendeka, amesema hayo jana alipozungumza na waandishi wa habari, akimuhusisha Kiongozi huyo Mkuu wa ACT na tuhuma za ufisadi wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii (NSSF), alipokuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC).

”Nilikuwa najiuliza hivi chuki ya Zitto kwa Serikali ya Awamu ya Tano, inayopambana na mafisadi imetoka wapi wakati yeye alikuwa anasimamia mashirika hayo.

“Miongoni mwa taasisi hizo alizokuwa akisimamia na baadhi ya marafiki zake ndiyo hao walionunua hekari moja kwa Sh milioni 800, wakati ilikuwa ikiuzwa kwa Sh milioni 25 na walikuwa wamejificha kwa maslahi binafsi,” alisema katika ofisi ndogo za Makao Makuu, Lumumba Dar es Salaam.

NSSF ndiyo iliyonunua hekari 20,000 Kigamboni jijini Dar es Salaam kwa Sh milioni 800 kwa kila hekari, badala ya Sh milioni 25 na kujikuta katika hatari ya kupoteza Sh bilioni 270, katika mradi wa ujenzi wa mji wa kisasa wa Dege Eco Village.

Kutokana na tuhuma hizo za NSSF zilizoibuka upya katika kamati ya PAC wiki hii, Sendeka alisema ni vema Serikali ikague  kuona kama akaunti za viongozi wa zamani wa kamati hizo, maisha yao na mali walizonazo, zinafanana na mapato halali waliyokuwa wakilipwa.

Alisema alikuwa anaangalia msukumo wa ghafla na mapenzi ya akina Zitto waliyokuwa wanayapata kwa nchi, kumbe ilikuwa ni kichaka cha kuficha baadhi ya maswahiba zao wasichukuliwe hatua.

Aliwahakikishia wananchi kuwa Serikali ya Rais Magufuli haina nia ya kurudi nyuma katika jambo lolote na kuwa itasonga mbele huku akiamini kuwa Serikali iliyochaguliwa na watu haiwezi kufa.

“Tunahakika Serikali ya Magufuli iliyopata ridhaa ya kutumikia watu, haitafutika kwa kelele za mlango wa baadhi ya makuwadi na watu waliolipwa kuchafua taswira ya Tanzania,” alisema.

Aliongeza kuwa Serikali hiyo itaendelea kushughulikia wakwepa   kodi pamoja na kuchunguza mambo aliyoanzisha Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa alipokuwa bandarini.

Kauli ya Zitto
Akizungumzia tuhuma hizo, Zitto Kabwe alisema hana muda wa kujibu alichoita kuwa ni porojo na vioja vya Sendeka.

Alifafanua kuwa CCM ni chama dola na kuna taasisi nyingi za uchunguzi za Serikali, ikiwemo Taasisi ya Kupambana na Kuzuia Rushwa (Takukuru) na Mkurugenzi wa Mashitaka ya Jinai (DPP) na kushangaa kwa nini vyombo hivyo havisemi, aseme Sendeka?

Majibu ya ACT Wazalendo kwa Ole Sendeka baada ya kutaka Zitto achunguzwe

0
0
Chama cha ACT-Wazalendo kimesema kimeshtushwa na tuhuma dhidi ya kiongozi wake wa chama, Zitto Kabwe kwamba ana miliki mali za kifisadi pamoja na kuhusishwa na ununuzi wa ardhi maeneo ya Kigamboni uliofanywa na NSSF kwa bei ya milioni 800 kwa ekari moja, wakati bei halisi ni milioni 25 na kwamba kitendo hicho kimeitia hasara serikali .

Tuhuma hizo zilitolewa jana na Msemaji wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Christopher Ole Sendeka, ambapo alivitaka vyombo vya uchunguzi kufanya uchunguzi katika shirika hilo ili kubaini waliohusika kwa ajili ya kuchukuliwa hatua za kisheria, huku akimhusisha Zitto katika uchunguzi huo.

Ole Sendeka alitaka akaunti za benki za Zitto pamoja na maisha yake binafsi kuchunguzwa kama yana uhalisia na kipato chake halali.

Tuhuma hizo zimekiibua chama cha ACT, ambapo leo Katibu wa Bunge na Serikali za Mitaa ACT, Habibu Mchange amevitaka vyombo vya uchunguzi haraka iwezekanavyo kuchunguza mali, madeni, akaunti zote za benki pamoja na mfumo wa maisha ya Zitto.

“ACT imeshtushwa na tuhuma, kashfa, porojo na matusi mbalimbali yaliyotolewa jana na Ole sendeka dhidi ya kiongozi wa chama chetu,” amesema.

Amesema kuwa, katiba ya chama hicho huwataka viongozi wote kuweka hadharani matamko ya mali zao na madeni na kwamba Zitto alitekeleza matakwa hayo ya kisheria hivyo mali na madeni yake yako hadharani na mtandaoni.

“Tunaamini kama kuna kiongozi ambaye mali, madeni, maslahi, na akaunti zake viko wazi basi ni ndugu Zitto,” amesema.

Aidha, Mchange amedai kuwa, kilichomsukuma Sendeka kutoa tuhuma hizo kwa Zitto ni harakati zake za kuupinga muswada mpya wa habari.

“Tuhuma za ole sendeka kuna kitu nyuma yake, jitihada za zito za kupambana na mswada wa habari ndizo zilizomuibua, sababu wanataka upitishwe ili kuviua vyombo vya habari,” amesema.

Amesema ACT itaendelea kuisimamia serikali katika mambo ya bungeni kama anavyofanya mbunge na kiongozi wao wa chama.

Ujumbe wa Rais Magufuli kwa Watanzani katika siku yake ya kuzaliwa

0
0
Leo Oktoba 29 ni kumbukumbu ya siku ya kuzaliwa Rais Dkt John Pombe Joseph Magufuli ambapo alizaliwa Oktoba 29, 1959.

Rais Magufuli alizaliwa mkoani Geita na kitaaluma yeye ni mwalimu aliyebobea katika somo la Chemistry.

Katika siku yake hii ya kuzaliwa, Rais Magufuli amewashukuru Watanzania wote kwa kuendelea kumuombea ambapo amesema kuwa ataendelea kufanyakazi kwa bidii na kuwatumikia watanzania wote kwa ajili ya maendelo ya nchi.

Kupitia akaunti yake ya Twitter, Rais Magufuli ameandika jumbe hizi;

 Dr John Magufuli
Ninamshukuru Mungu kufikia siku yangu ya kuzaliwa,ninawashukuru watanzania nyote kwa kuniombea.Nitafanya kazi kwa moyo&nguvu zangu zote 1/2.

 Dr John Magufuli
Ninaahidi kuendelea kufanya kazi kwa moyo na nguvu zangu zote kwa ajili ya maendeleo ya Taifa. Mungu Ibariki Tanzania 2/2.

Breaking Newssss: Rais Dkt Magufuli Atengua Uteuzi Wa Mkurugenzi Wa Upelelezi Makosa Ya Jinai (Dci) Diwani Athumani Leo

0
0
Taarifa kutokea Ikulu Dar es salaam leo October 29 2016 ni pamoja na hii ya Rais Dk. John Pombe Magufuli kutengua uteuzi wa mkurugenzi wa Makosa ya Jinai Nchini (DCI) Diwani Athumani.

Picha 20: Tukio zima la Miss Tanzania 2016, lilofanyika Mwanza kwa Mara ya Kwanza

0
0
Leo kwa mara nyingine tena Tanzania imeingia kwenye Headline ya kumpata Miss Tanzania 2016 baada ya miaka miwili kupita bila kufanyika shindano la Miss Tanzania, Shindano la Miss Tanzania limefanyika Mwanza kwa mara ya kwanza na mrembo kutokea Kinondoni Dar es salaam Diana  Edward Lukumai amekuwa mshindi kwa kati ya warembo 30
3x6a0495
3x6a0504
3x6a0520
3x6a0491
Wa pili kushoto Lilian Kamazima, Miss Tanzania 2014
3x6a0535
Christian Bella, akitoa Burudani
3x6a0563
3x6a0500
3x6a0487
3x6a0472
3x6a0428
Host wa shinadno la Miss Tanzania 2016, Jokati Mwegelo
3x6a0574
Miss Tanzania 2006, Wema Sepetu
3x6a0606
3x6a0615
3x6a0622
Mshindi wa Miss Tanzania 2016, Diana Edward Lukumai
3x6a0631
3x6a0662
3x6a0659
3x6a0650
Zawadi ya Miss Tanzania 2106
3x6a0652
ULIKOSA HII YA RAIS MAGUFU KUTENGUA UTEUZI WA MKURUGENZI? UNAWEZA UTAZAMA HII VIDEO

Amini Akisema Mimi Nimepotea Kwenye Muziki Yeye Mwenyewe Yupo Wapi – Linah

0
0
Baada ya Amini kudai msanii mwenzake Linah Sanga amebadilika na kupoteza ule uimbaji wake wakuvutia, Linah amefunguka na kuizungumzia kauli hiyo.

Muimbaji huyo ambaye aliwahi kufanya vizuri na wimbo ‘Ole Themba’ amesema kwa sasa yeye yupo juu zaidi ya Amini.

“Unajua soko letu lilivyo linabadilika badilika na hii ni biashara kusema nifuate ‘Ulinah’ sana naweza nikapotea kwa sababu watu walianza kuongea toka kwenye ‘Ole Themba’ lakini ‘Ole Themba’ ni wimbo ambao uliniweka sehemu nzuri sana,” alisema Linah. “Hii hali ya kusema nataka kubaki pale pale inatuangusha sana sisi wasanii ambao tumekuwa pamoja. Yaani tumejiwekea sisi ni wahivi hivi, hapana tunatakiwa tujichanganye ili tubadilike. Kwa sababu mbona yeye bado yupo kule kule lakini yupo wapi?. Usiseme mimi nimepotea yeye mwenyewe yupo wapi? na tukisema kwenye kupotea yeye na mimi nani amepotea?,”

Muimbaji huyo ambaye kwa sasa anafanya vizuri na wimbo ‘Raha Jipe Mwenyewe’ amewataka wasanii wenzake kubadilika ili kukabiliana ushindani iliyopo kwenye game.
Viewing all 104414 articles
Browse latest View live




Latest Images