Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104766 articles
Browse latest View live

Wanaswa na Magamba ya Kakakuona ya Bil 1.4/-

$
0
0
WATU wanne wakiwemo raia watatu wa Burundi, wanashikiliwa na Polisi mkoani Morogoro baada ya kukutwa na magamba ya kakakuona, yenye thamani ya zaidi ya Sh bilioni 1.4.

Walikuwa wamehifadhi magamba hayo kwenye mifuko 67, yakisubiri kusafirishwa kwenda nje ya nchi kuuzwa. Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Morogoro, Ulrich Matei, alisema watu hao walikamatwa saa tano na nusu usiku wa Oktoba 28, mwaka huu eneo la mtaa wa Reli, kata ya Kichangani, Manispaa ya Morogoro.

Walinaswa ndani ya ghala moja, lenye mashine ya kukoboa na kusaga nafaka.

Alisema, askari wa jeshi hilo wakiwa katika msako, walipokea taarifa za kiintelejensia kutoka kwa raia wema kuhusu mazingira ya watu katika eneo hilo. Walipofika, walikuta watuhumiwa hao wanne.

Baada ya upekuzi kwenye ghala hilo, polisi walikamata magamba ya kakakuona katika mifuko 67, baaadhi yake yakiwa tayari kwa ajili ya kusafirishwa kwenda nje ya nchi.

Kamanda Matei aliwataja raia wa Burundi waliokamatwa kuwa ni Kibonese Golagoza ( 35), Nuru Athuman (32) na Benjamin Gregory Luvunduka (41) ambao pia ni wakazi wa Morogoro, wakati Mtanzania ni Shukuru Mwakalebela (25) mkazi wa Stesheni mjini hapa.

Alisema magamba hayo, yalifungwa katika mifuko yenye kilo 50 na kisha kutumbukizwa kwenye viroba vikubwa vya kilo 100, vilivyochanganywa na maharage. Aidha alisema watuhumiwa raia wa Burundi, wanakabiliwa pia na tuhuma za kuingia nchini bila kibali cha Uhamiaji.

Alisema wote wanaendelea kuhojiwa na Polisi na watafikishwa mahakamani upelelezi utakapokamilika. Hata hivyo, Kamanda huyo alisema ni mapema kueleza kakakuona hao wanauawa katika maeneo gani ya nchi, na mahali liliko soko kubwa kwa vile suala hilo lipo katika uchunguzi na utakapokamilika, taarifa itatolewa.

Ofisa Maliasili wa Mkoa wa Morogoro, Joseph Chuwa aliyekuwepo katika upekuzi huo, alisema katika mifuko 67 iliyokamatwa, kila mmoja ulikuwa na wastani wa magamba ya kakakuona 1,000.

Alisema kakakuona mmoja, kwa wastani anakuwa na magamba 60 hadi 100, hatua iliyofanya kila mfuko kuwa na wastani wa kakakuona wapatao 10 waliouawa kwa ajili ya biashara hiyo haramu.

Alisema kutokana na idadi ya mifuko hiyo, wastani wa kakakuona 670 waliuawa, ambapo kilo moja ya magamba yake huuzwa kwa dola za Marekani 960, hivyo kutokana na viwango vya sasa vya thamani ya dola kwa fedha ya Tanzania, ni sawa na Sh bilioni 1.4.

Chuwa alisema kutokana na wingi wa magamba hayo ya kakakuona, ujangili huo hauwezi kuwa umefanyika mkoani Morogoro pekee, bali pia katika maeneo mengine ya hapa nchini, kwa kuwa kiwango hicho ni kikubwa na hayakupatikana kwa wakati mmoja. Alisema soko kubwa la bidhaa hiyo ni katika Bara la Asia.

Kakakuona kwa ufupi

Kakakuona ndiye mnyama pekee duniani, ambaye mwili wake wote umefunikwa na magamba makubwa kuliko ya viumbe wengine. Hutumia magamba hayo, kama silaha ya kujilinda dhidi ya maadui. Jina la kakakuona lilianzia nchi za Mashariki ya Mbali za Malaysia, Indonesia na Brunei, likimaanisha kitu kinachojikunja.

Kwa kawaida, Kakakuona hupenda kujikunja kama mpira. Hiyo ni mbinu anayotumia kujilinda dhidi ya maadui. Kakakuona akiona adui, hujilinda kwa kujikunja, lakini akiona hali inakuwa mbaya zaidi, hutema sumu kali mithili ya tindikali inayoweza kumdhuru adui.

Pia, wakati mwingine hunyoosha mkia wake na kuuzungusha na kumkamata adui aliyekaribu yake. Licha ya kutumia mbinu hiyo kujilinda, lakini anapojikunja ndiyo inakuwa rahisi kwa watu kumkamata na kumbeba. Kuna aina nane za kakakuona duniani, zilizopo duniani kwa zaidi ya miaka milioni 80 ya mabadiliko yao.

Kati ya hizo, aina nne zinapatikana Bara la Ulaya na nyingine barani Afrika. Kakakuona ana ulimi wenye urefu unaozidi mwili wake. Akiurefusha kwa kuutoa nje ya kinywa, unafikia urefu wa sentimita 40. Ulimi huo ambao pia unanata, huutumia kwa ajili ya kukusanya wadudu, ambao ndiyo mlo wake wa pekee.

Hana mlo mwingine zaidi ya huo kutokana na kukosa meno. Baadhi ya kakakuona huishi juu ya miti. Wengine hujichimbia ardhini na kuishi ndani ya mashimo. Wanaoishi juu ya miti ni wenye mikia mirefu wanaopatikana barani Afrika. Wengine huchimba mashimo marefu ardhini na kuishi humo ili wasikutane na binadamu.

Inakadiriwa kuwa kakakuona 100,000 hukamatwa kila mwaka barani Afrika na Ulaya na kuuzwa. China na Vietnam ndizo nchi maarufu ambazo nyama na magamba yake huuzwa. Inakadiriwa kuwa mamilioni ya wanyama hao, wameuawa na kuuzwa katika miaka 10 iliyopita.

Utafiti: Kukumbatiwa na Umpendaye Wakati wa Maumivu Kuna Nguvu zaidi ya Paracetamol

$
0
0
Kumbatio kutoka kwa mtu umpendaye, linaweza kuwa na nguvu zaidi ya Paracetamol pale unapokuwa na maumivu, kwa mujibu wa utafiti.

Wanasayansi wamebaini kuwa hisia za ukaribu tunazozipata kupitia mtu anayetushika, kunaweza kusaidia kupunguza maumivu. Lakini kushikwa na mtu usiyemjua, kunaweza kusiwe na matokeo yale yake, kwasababu hatuna hisia nao.

Utafiti huo unaonesha nguvu ya ubongo kuzuia hisia za maumivu. Utafiti huo ulifanywa na wataalam katika chuo kikuu cha Haifa, Israel na ulihusisha wanawake kadhaa ambao waliwatengenezea maumivu kwa kuwaunguza na chuma chenye moto kiasi.

Katika jaribio la kwanza, mtu wasiyemjua aliwashika mkono akijaribu kuwaliwaza kwa maumivu hayo. Kwenye la pili waliwaita waume na wapenzi wao kukaa karibu nao na kugusanisha ngozi.

Katika jaribio la mwisho, wapenzi wao waliruhusiwa kuwashika mkono wakati chuma hicho cha moto kikigusishwa kwenye ngozi zao. Wanasayansi walibaini kuwa mguso wa mtu wasiyemjua pamoja na kuwa na mpendwa wao karibu hakukuwa na tofauti katika jinsi walivyosikia maumivu.

Lakini pale mtu wanayempenda alipowagusa kwenye ngozi, maumivu yalipungua.

Walibaini pia kuwa kadri mpenzi wa mwanamke alivyoonesha huruma na support kwake wakati wa zoezi hilo, alipata afueni zaidi.

Nataka Kumpeleka Mke Wangu Chuo Lakini Roho Inasita..Naogopa Kugongewa

$
0
0
Ndugu zangu,

Mke wangu ni mmojawapo wa mwanachuo aliyechaguliwa kujiunga na chuo fulani hapa nchini. Nimeamua kuja kuomba ushauri kwenu kwa sababu upande mmoja wa roho yangu unaniambia usimruhusu na upande mwingine unaniambia mruhusu.

Hili limetokana na tetesi nyingi zinazowahusu wake wa watu kutafunwa kirahisi sana hasa wakiwa mavyuoni. Tuna watoto watatu na sasa hivi anamimba ya miez 4. Mimi nimfanyabishara nataka nimuendeleze mke wangu ili tuweze kuendeleza vizuri biashara zetu.

Naomba ushauri wenu ndugu zangu

Mariah Carey Anataka Alipwa Mamilioni na ex Wake Bilionea Baada ya Kupigwa Chini

$
0
0
Mariah Carey anaweza kubaki na pete ya dola
milioni 10 aliyovishwa na mchumba wake James
Packer waliyeachana. Lakini hiyo haitoshi,
muimbaji anataka zaidi.

Wawili hao waliachana baada ya kuzuka ugomvi
walipokuwa wakila bata kwenye yacht nchini
Ugiriki mwezi September kufuatia tetesi kuwa
diva huyo anachepuka na dancer wake, Bryan
Tanaka.
Kwa mujibu wa ripoti, Carey anataka alipwe dola
milioni 50 kutoka kwa Packer baada ya
kumhamishia LA na anadai kuwa ameathirika na
kuachana kwao kiasi cha kukatisha ziara yake
ya Amerika Kusini.
Hata hivyo vyanzo vilivyo karibu na bilionea huyo
vimedai kuwa Carey asahau kupewa hata senti.
“Ni ujinga kudai kuwa James ni sababu ya
kusitisha ziara yake ya Amerika Kusini. Siku
chache zilizopita aliwalaumu mapromota,”
kilisema chanzo.
Sababu kubwa inayoelezwa kuwa chanzo cha
wawili hao kuachana ni usaliti wa Carey na
matumizi makubwa ya fedha. Wawakilishi wa
muimbaji huyo wanakanusha

Jipatie Dawa Asili za Kutengeneza Shepu, Kuondoa Michirizi Chunusi, Kurefusha Nywele Toka Markson Beauty Products

$
0
0
HABARI NJEMA MARKSON BEAUTY PRODUCTS
Baada ya kupata cheti cha bidhaa bora kwa mwaka 2015-2016, Sasa kampuni hii inasambaza huduma zake ndani na nje ya nchi kwa vibali maalum. Bidhaa zetu zimetengenezwa kwa mimea na matunda na kudhibitishwa. Hazina kemikali wala madhara. DAWA ZETU NI YA:-

  1. kurefusha nywele na kuzuia kukatika ovyo @100,000/=
  2. Kuongeza shepu (hips na makalio) kwa/= (a)Dawa ya kunywa au kupaka @150,000/=(b)Vidonge @170,000/=
  3. Kuwa mweupe na softi mwili mzima kwa:- (1)Mafuta @100,000/= (11)Vidonge @150,000/=
  4. Kupunguza unene na manyama uzembe @120,000/=
  5. Kuongeza uume pamoja na nguvu za kiume kwa:-(a) Gely ya kupaka @100,000/= (b) Vidonge maalum @120,000/= (c) Handsome up original @170,000
  6. Kuondoa mvi milele zisiludi tena @100,000/=
  7. Kuongeza unene wa mwili mzima na uzito @120,000/=
  8. Kupunguza tumbo (kitambi) na nyama za pembeni kwa:- (a) Dawa ya kunywa au kupaka @120,000/= (b) Mkanda wa kawaida @100,000/= (c) micro-computer belt unaovaibret @200,000/=
  9. Kupunguza maziwa na kuyasimamisha @90,000/=
  10. Kushepu miguu na kuwa minene @100,000/=
  11. Kuondoa mipasuko mwilini (michirizi) @90,000/=
  12. kubana uke na kuongeza hamu ya tendo la ndoa kwa mwanamke @100,000/=
  13. Taiti za hips na makalio @150,000/=           
NB: Hakikisha unapata risiti yenye muhuri halisi wa MARKSON CO pamoja na garantii kwa bidhaa halisi. Wasiliana nasi :-(+255) 0767447444 na 0714335378 Google MARKSON BEAUTY.
Follow us
@Markson_beauty_pr
@Markson_beauty_pr

Sumaye Adai Amepata Taarifa ya Kutimuliwa Nyumbani kwake pia

$
0
0
Aliyekuwa Waziri Mkuu wa Serikali ya Awamu ya Tatu, Frederick Sumaye amesema kuwa baada ya kutangazwa mchakato wa kunyang’anywa shamba lake la Mwabwepande, amepata taarifa ya kutaka kuondolewa anapoishi pia.

Sumaye ametoa kauli hiyo ikiwa ni siku chache baada ya Waziri Wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi kueleza kuhusu kuanza rasmi kwa mchakato wa kumnyang’anya mwanasiasa huyo shamba la Mwabwepande kwa madai ya kutoliendeleza kwa muda mrefu.

“Hapa ninapoishi naambiwa kuna maelekezo yametoka juu kuwa sijapaendeleza. Sasa kama sijapaendeleza mbona ninaishi hapahapa,” Sumaye amekaririwa na gazeti la Nipashe.

Aidha Sumaye amesema kuwa ingawa alimsikia Waziri Lukuvi akieleza kuwa tayari wameshampa notisi ya siku 90 kuhusu kunyang’anywa shamba lake la Mwambwepande, hadi jana hajaipata notisi hiyo licha ya kufanya jitihada za kuifuatilia.

Alisema kuwa anashangazwa na uamuzi huo wa Waziri kwani kesi inayolihusu shamba hilo bado inaendelea mahakamani kutokana na uvamizi wa wananchi na kwamba Mahakama imezitaka pande zote mbili kutofanya chochote kwenye ardhi hiyo.

Mwanasiasa huyo ambaye pia ni Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Chadema alisema kuwa anachokifahamu ni kwamba alipokea notisi ya kuondolewa katika shamba lake la Mvomelo kwa madai ya kushindwa kuliendeleza kwa muda mrefu.

“Ninachokijua ninaandamwa kisiasa. Shamba langu la Mvumelo naambiwa sijaliendeleza. Kwenye hilo shamba nimejenga nyumba ya kuishi, ghala, kuna trekta na vifaa vingine. Ninalima mazao na nimefuga zaidi ya ng’ombe 200, nina kondoo 300 na nimechimba visima viwili vya maji halafu serikali inasema sijaliendeleza,” alisema Sumaye.

Alisisitiza kuwa ingawa anaamini anaandamwa kisiasa kwa kunyang’anywa mashamba yake, hatarejea CCM hata akinyang’anywa mashamba yote aliyoanayo.

Sumaye alihama CCM mwaka jana, miezi michache kabla ya kufanyika kwa Uchaguzi Mkuu na kujiunga na harakati za kumpigia kampeni mgombea urais kwa tiketi ya Chadema, Edward Lowassa. Baada ya uchaguzi huo alitangaza kujiunga rasmi na Chadema.

Samatta Atokea Benchi Genk Ikiua 2-1 Ubelgiji

$
0
0
MSHAMBULIAJI wa kimataifa wa Tanzania, Mbwana Ally Samatta amecheza benchi timu yake, KRC Genk ikishinda 2-1 dhidi ya Westerlo katika mchezo wa Ligi Daraja la Kwanza A Ubelgiji, Uwanja wa Laminus Arena.

Kiungo Mspaniola, Alejandro Pozuelo aliifungia bao la kwanza Genk dakika ya 54 kabla ya mshambuliaji Mgiriki, Nikolaos Karelis kufunga la pili dakika ya 66, wote wakimalizia pasi za mshambuliaji Mjamaica, Leon Bailey.

Na ni Nikolaos Karelis aliyempisha Samatta, Nahodha wa timu ya taifa ya Tanzania 'Taifa Stars' dakika ya 66 mara tu baada ya kufunga bao la pili. Bao pekee la wageni lilifungwa na kiungo Mbelgiji, Jamo Molenberghs dakika ya 82.

Huo unakuwa mchezo wa 31 kwa Samatta tangu amejiunga na Genk Januari mwaka huu kutoka TP Mazembe ya DRC, 18 msimu uliopita na 12 msimu huu, akifunga mabao nane, matatu msimu huu na matano msimu uliopita.

Katika mechi hizo, ni 16 tu ndiyo alianza, 10 msimu uliopita na tano msimu huu, wakati 14 alitokea benchi nane msimu uliopita na 11 msimu huu – na mechi tisa hakumaliza akitolewa, sita msimu uliopita na tatu msimu huu.

Kwa Mara ya Kwanza Rais wa Tanzania John Pombe Magufuli Kutembelea Nchini Kenya....

$
0
0
Kwa mara ya kwanza Rais wa Tanzania John Pombe Magufuli, atazuru taifa jirani la Kenya hapo kesho Jumatatu.

Ziara ya Magufuli nchini humo, inatukia wakati ambapo uhusiano wa mataifa hayo mawili umekuwa ukilegea.

Kwenye ajenda ya ziara hiyo rasmi ya kiserikali, kati yake na mwenyeji wake Rais Uhuru Kenyatta, ni kuimarisha biashara kati ya mataifa hayo mawili, kwani Rais magufuli amekosa kuhudhuria mikitano mikuu miwili jijini Nairobi, iliyowaleta pamoja marais wengi wa Afrika.

Tangu aingie mamlakani mwezi Oktoba mwaka jana, Rais Magufuli ambaye ameamua kukabiliana na ufisadi nchini mwake amezuru tu Rwanda na Uganda.


Pia ziara ya Dkt Magufuli inahusia na hatua ya Rais Uhuru Kenyatta kumpendekeza waziri wa mashauri ya nchi za kigeni wa Kenya Amina Mohammed kwa kinyanganyiro cha wadhifa wa mwenyekiti wa muungano wa afrika-AU.

Tofauti na Tanzania, kashfa za mamilioni ya dola inafichuliwa mara kwa mara nchini Kenya, huku pesa za umma zikinyakuliwa na baadhi ya watu mashuhuri serikalini na walio na uhusiano wa karibu na watawala wa nchi hiyo.

Rais Uhuru Kenyatta atamkaribisha mgeni wake jijini Nairobi, baada ya Kenyatta kukamilisha ziara ya siku mbili huko Khartoum, alipokutana na Rais wa Sudan- Omar Al- Bashir.

Vanessa Mdee Aja na Muonekano Mpya Sasa Kama Bob Marley

$
0
0
Vanessa mdee ameamua kuingia kwenye utamaduni mpya huku akiwashangaza mashabiki wake
Ameamua kuingia kwenye utamaduni wa watu wa Raggie kama bob marley na lucky dube
Baaadhi ya mashabiki wameonekana kutokubali na muonekano huu

Ushauri: Nimeshika Simu ya Mpenzi Wangu, Sina Hamu Naye

$
0
0
Mimi ni kijana umri miaka 26 mchumba wangu anafanya kazi katika kampuni moja hivi ya binafsi ,japo hatujaoana lakin tuna kawaida ya kutembeleana mara kwa mara,yeye anaishi Kinondoni Mkwajuni mimi naishi Ubungo Riverside,

Weekend hii nilienda kumtembelea akanipa simu yake nimwekee vocha nikiwa naweka vocha nikashangaa sms inaingia "honey uko wapi". Sikumwambia chochote na wala sikuifingua iyo sms ila niliweza kuisoma coz simu yake ni smartphone aina ya Sony yaan sms ikitumwa uwa inapita kwa juu unaweza kuisoma yote.

Niliamua kufungua whatsApp yake nikaanza kupitia baadhi ya chatting zake cha ajabu nikakutana na chatting moja amechat na mwanaume nilijua ni mwanaume coz niliangalia profile picture yake na sms zao zilinitsha sana jamaa kuna sms anasema " Juzi nilifurah mno nilipokuingizia nyuma" halafu mchumba wangu alisms akajibu". Mwenzio sijazoea nyuma". Kuna sms nyingine jamaa alituma akisema " Mwezi wa 6 inabd nikutie mimba".Daah niliishiwa pozi lakini sikusema kitu chochote hadi leo bado niko kimya nafikiria cha Kufanya......

Naombeni ushauri wenu

Lulu Diva Agawa Penzi Kisa Pesa Sh Milioni Moja na Nusu

$
0
0
MUUZA sura kwenye video za Kibongo, Lulu Abbas ‘Lulu Diva,’ amefunguka kuwa katika maisha yake hata siku moja hawezi kusahau jinsi alivyolazimika kugawa penzi kwa mzee, kisa pesa za kumtibisha mama yake mzazi ambaye alikuwa anaumwa hoi!

 Lulu aliongeza kuwa wakati akifanya tukio hilo alikuwa ni msichana mwenye umri wa miaka 18, ambaye hakuwa na kazi na ilihita kiasi cha shilingi milioni moja na nusu kwa ajili ya kulipia ghalama za matibabu ya mama yake, pesa ambazo kama familia walikuwa hawana uwezo wa kuzipata.

“Unajua mimi nyumbani nimezaliwa mwenyewe, baba alifariki kitambo nikiwa mdogo na sina kaka wala dada, sasa mama yangu alipokuwa anaumwa wakati huo, kuna mzee mmoja mwenye uwezo tu nilikwenda kumuomba msaada ili anipe pesa nimpeleke mama hospitali, baada ya kumlilia shida alikataa kunisaidia bila kufanya naye mapenzi.

“Kwa kuwa nilikuwa ninashida ilibidi kukubali ili tu mama yangu apate matibabu lakini kiukweli, tukio hilo mpaka leo halijafutika akilini mwangu!” alimaliza Lulu Diva.

Show ya Diamond Malawi Yafana Licha ya Mvua Kubwa Kunyesha

$
0
0
Licha ya mvua kubwa kunyesha, Diamond amefanikiwa kupiga show iliyofana kwenye Sand Music Festival iliyofanyika kwenye fukwe za Living stone Jumamosi hii.

Mpiga picha wake, Kifesi amedai kuwa mvua kubwa ilinyesha na kulazimu show yake kusimama kwa muda. Hata hivyo mashabiki waliokuwa na hamu kumuona akitumbuiza, walisubiri hadi ilipokata.


Kwenye picha hii Kifesi ameandika: Picha juu ni usiku watu wakiwa na shauku ya Diamond but mvua ikanyesha, but walingoja hadi hali ilipotulia.. Picha chini na alfajiri saa 12 hali ilipotulia na Diamond kupanda na hakuna alokua kuchoka or kuondoka

Kwenye show hiyo Diamond alitumbuiza live. Hizi ni picha zaidi:

Ukweli Kuhusu Degree ya Miss Tanzania Mpya

$
0
0
Katika pita pita zangu mitandaoni nimekutana na hii Video ya Miss Tanzania. Kipindi ambapo anatafutwa miss kinondoni. Ni kweli alisema ana miaka 18 lakin hakusema kuwa ana degree. Zaid alichosema ni kuwa yeye ni Applicant wa IFM. Sasa sijajua hiz rumors zinatoka wapi. Please cheki hii video kuanzia dk ya 8.

Miss kinondoni 2016.

Basi La Abiria Lateketea Kwa Moto Kimara Stop Over Jijini Dar......Mtu mmoja Afariki, 16 Wajeruhiwa

$
0
0
Basi lenye namba za usajili T990 AQF mali ya kampuni ya Safari Njema liililokuwa likitokea Dodoma kuja jijini Dar, jana liliteketea kwa Moto maeneo ya Kimara Stop Over-Suka, mara baada ya kugongana na Lori lililokuwa limebeba shehena ya mifuko ya Cement (namba zake za usajili hazikujulikana mara moja).

Imeelezwa kuwa mali zote zilikuwemo katika basi vimeteketea kabisa kwa moto.

Jeshi la Polisi limeeleza kuwa mtu mmoja amefariki Dunia katika ajali hiyo na wengine 16 wamejeruhiwa na baadae kukimbizwa Hospitali ya Taifa Muhimbili kwa matibabu.

HESLB Yafafanua vigezo Utoaji mikopo, Waliokosa sababu zatajwa, wapewa nafasi ya kukata rufaa

$
0
0
Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) imetoa ufafanuzi kuhusu vigezo inavyotumia katika kuchambua, kupanga na kutoa mikopo kwa wanafunzi 20,183 (asilimia 74) wa mwaka wa kwanza hadi sasa kati ya 25,717 iliyopanga kuwapa mikopo katika mwaka huu wa masomo, 2016/2017.

Idadi iliyobaki (asilimia 26) ya wanafunzi wa mwaka wa kwanza itajazwa na waombaji ambao baadhi ya nyaraka walizowasilisha zinaendelea kuchambuliwa ili kuthibitisha uhalisi wake na baadhi zitajazwa na waombaji ambao wanakata rufaa na kuwasilisha nyaraka zinazothibitisha uhitaji wao kwa mujibu wa vigezo vya mwaka huu.

Aidha, katika mwaka huu wa masomo, Serikali imepanga kutumia jumla ya Tshs 483 kutoa mikopo kwa wanafunzi 93,295 wanaoendelea na 25,717 wa mwaka wa kwanza.

Katika mkutano na waandishi wa habari jana (Jumapili, Oktoba 30, 2016), Mkurugenzi Mtendaji wa HESLB Bw. Abdul-Razaq Badru alisema vigezo vikuu vinavyotumika mwongozo uliotangazwa na Bodi hiyo wakati ilipotangaza kuanza kupokea maombi mwezi Juni mwaka huu ambao unataja makundi makuu matatu ya watakaopata mikopo.

Vigezo vilivyotumika kutoa mikopo
Kwa mujibu wa Bw. Badru, kundi la kwanza linajumuisha wanafunzi waombaji wa mikopo wenye uhitaji maalum kama wenye ulemavu uliothibitishwa na Waganga Wakuu wa Wilaya na yatima ambao katika maombi yao waliwasilisha nakala za vyeti vya vifo zilizothibitishwa na makamishna wa viapo.

“Kundi la pili linajumuisha waombaji wa mikopo ambao baada ya uchambuzi wa taarifa zao walizowasilisha na baada ya kulinganisha na gharama za jumla za masomo yao ya sekondari, wamebainika kuwa wana uwezo mdogo wa kugharamia masomo yao ya elimu ya juu na hivyo kuwa na uhitaji zaidi wa mikopo,” alisema Bw. Badru.

Katika mkutano huo uliofanyika katika Ukumbi wa Idara ya Habari (MAELEZO), Bw. Badru alitaja kundi la tatu na la mwisho kuwa linajumuisha waombaji wa mikopo ambao wenye ufaulu wa juu katika matokeo yao ya kidato cha sita na wamechaguliwa kujiunga na fani za kipaumbele kwa taifa.

Fani hizo ni Sayansi za Tiba, Ualimu wa Sayansi na Hisabati, uhandisi wa Kilimo, Mafuta na Gesi na Sayansi za Ardhi, Usanifu Majengo na Miundombinu.

Makundi ya wanafunzi waliopata mikopo
“Hivyo basi, hadi sasa tumetoa mikopo kwa wanafunzi 20,183 wakiwemo wanafunzi yatima 4,321, wenye ulemavu 118, wanafunzi wenye uhitaji waliosomeshwa na taasisi mbalimbali katika masomo ya sekondari (87), wanafunzi wanaosoma kozi za kipaumbele 6,159 na wanafunzi wanaosoma kozi zisizo za kipaumbele lakini wanaotoka kwenye familia duni 9,498,” alifafanua Bw. Badru.

Sababu za kukosa mikopo
Katika mkutano huo, kiongozi huyo wa HESLB pia alieleza kwa kina sababu nyingine za waombaji 27,053 ambao hawajapangiwa mikopo.

Ametaja sababu hizo kuwa ni pamoja na baadhi ya waombaji (90) kuwa na umri wa zaidi ya miaka 30, waombaji mikopo waliopata udahili kwa sifa linganishi (equivalent qualifications) na waombaji waliomaliza masomo ya kidato cha sita zaidi ya miaka mitatu iliyopita.

Kundi jingine la waombaji waliokosa mikopo katika awamu ya kwanza ni waombaji waliopata nafasi katika vyuo kwa ufaulu wa mitihani waliyofanya kama watahiniwa binafsi (Private Candidates) na waombaji ambao hawakurekebisha fomu zao za maombi ingawa waliitwa kufanya hivyo.

Nafasi ya rufaa na uhakiki wa wanafunzi wanaoendelea na masomo
Katika mkutano huo, Mkurugenzi Mtendaji huyo pia amewataka waombaji ambao hawajaridhika na upangaji wa mikopo unaotangazwa, kuwasilisha rufaa zao kwa njia ya mtandao utakaofunguliwa kuanzia katikati ya wiki hii.

“Tunafahamu kuwa kuna baadhi ya wanafunzi wamekosa mkopo kwa kutowasilisha baadhi ya nyaraka ingawa tuliwaomba kufanya hivyo, hawa na wengine wenye sababu za msingi, watapata fursa ya kuwasilisha rufaa zao kwa njia ya mtandao na nakala kuzituma kwa utaratibu tutakaoutangaza wiki inayoanza kesho(leo),” alisema Bw. Badru.

Aidha, katika mkutano huo, Bw. Badru alisema bodi ya Mikopo inatarajia kuanza kazi kuhakiki taarifa za wanafunzi wanaoendelea na masomo ambao wanapata mikopo ya elimu ya juu kwa lengo la kubaini kama ni wana uhitaji wa mikopo hiyo kwa mujibu wa vigezo au hapana.

Katika zoezi hili linalotarajiwa kufanyika kwa siku 30 kuanzia mwezi ujao (Novemba, 2016), wanafunzi wote ambao ni wanufaika watalazimika kujaza dodoso maalum litakalokusanya tarifa za kiuchumi za wazazi na walezi wao ili kuweza kupata uhalisia wa sasa.

“Wanafunzi watakutana na dodoso katika akaunti zao katika mtandao wetu wa maombi ya mikopo (OLAMS) na watapaswa kujaza. Wale ambao hawatajaza dodoso hili kwa njia ya mtandao tutasitisha mikopo yao na wale ambao baada ya uchambuzi tutabaini hawana uhitaji, nao tutasitisha mikopo yao na watapaswa kuanza kurejesha fedha walizokopokea,’ alifafanua.

HESLB ilianzishwa mwaka 2004 na kuanza kazi rasmi mwezi Julai mwaka 2005 kwa lengo la kutoa mikopo kwa watanzania wahitaji waliopata nafasi za masomo katika vyuo vya elimu ya juu na kukusanya mikopo iliyoiva kutoka kwa wadaiwa walionufaika na mikopo tangu mwaka 1994.

Ufafanuzi Kuhusiana na Umri wa Miss Tanzania 2016 Diana Edward Loy Watolewa

$
0
0
Usiku wa Jumamosi, mrembo wa Kinondoni, Diana Edward Loy alitwaa taji la Miss Tanzania 2016 katika fainali zilizofanyika jijini Mwanza.

Hata hivyo pamoja na ushindi huo, haikuchukua muda akaanza kuubeba mzigo wa umaarufu kwa kusambaa taarifa zinazohusiana na umri wake.

Taarifa iliyosambaa ilisema:

MISS TANZANIA 2016
🙊🙊🙊🙊🙊🙊
JINA:Diana Edward Lukumai
UMRI:Miaka 18
ELIMU:Shahada(degree)
Hii ina maana;
Alianza Chuo akiwa na miaka 15
Alianza Form one akiwa na miaka 9
😂😂😂😂😂😂
Ingawa sio mshabik wa haya mambo napenda nchukue hii nafasi kuwapongeza Wazazi wote kama wazazi wa Diana ambao watoto wao wameanza shule ya msingi wakiwa na miaka miwili.

Kaimu afisa habari wa mrembo huyo, Charles William amelazimika kutoa taarifa sahihi kwa vyombo vya habari za mshindi huyo:

Napenda kuujulisha Umma yafuatayo;

1. Miss Tanzania 2016/2017 aliyeshinda taji jana jijini Mwanza, anaitwa Diana Edward Loy na siyo Diana Lukumai kama inavyotajwa mitandaoni.

2. Mlimbwende huyo amemaliza kidato cha nne 2015 Shule ya Sekondari Arusha Day na si 2011 kama inavyotajwa mitandaoni kwa malengo ovu.

3. Diana hajawahi kujiunga na Elimu ya Chuo Kikuu chochote Tanzania au duniani bali anatarajia kujiunga mwaka huu katika chuo cha IFM kusomea masula ya kodi ngazi ya stashahada (cheti) ingawa kulingana na ratiba zake na majukumu yake mapya ikiwemo kushiriki Miss world mapya huenda akaahirisha mwaka wake wa masomo.

4. Tunawasihi watanzania kutumia vyema mitandao ya kijamii na si kufanya “Character assassination” lakini pia tunaheshimu haki yao ya msingi ya kuhoji masuala ya msingi kabisa kuhusu mtu ambaye ni Public figure na ataliwakilisha taifa katika anga za kimataifa.

Tumuunge mkono mlimbwende wetu ili atuletee Taji la Dunia.

Tazama Video Fupi Aliyofanya Miss Tanzania Huko Umasaini Kuhusu Ukeketaji wa Wasichana wa Kike

$
0
0
Kwa wasichana wengi wanaoshiriki shindano la Miss Tanzania, ushindi huja kwa surprise na muda mfupi kugubikwa na matarajio makubwa kutoka kwenye jamii.

Lakini si kwa Miss Tanzania 2016, Diana Edward aliyevishwa taji Jumamosi hii, jijini Mwanza. Tangu ameanza kushiriki shindano hilo katika hatua za vitongoji, mrembo huyo alikuwa amejianda kuwa Miss Tanzania.

Diana mwenye asili ya kimasai, kwa muda wote wa ushiriki wa shindano hilo, aliuweka mbele utamaduni wake, kitu ambacho ni nadra kwa Mamiss wengine ambao wengi wao wamekulia mjini.

Amekuwa akijihusisha na shughuli za utetezi wa masuala ya kijamii, hasa watu wanaoishi mazingira magumu, pamoja na kampeni za kutokemeza ukeketaji. Wiki moja iliyopita alitoa documentary fupi kuhusu ukeketaji unaofanyika katika jamii yake ya kimasai. Yeye mwenyewe ni mhusika. Video:

Unaamini Kuna Uchawi Katika Mapenzi? Soma Hii Inakuhusu

$
0
0
BILA shaka msomaji wangu uko poa, kwa wewe ambaye unasumbuliwa na shida mbalimbali za kidunia, nakuombea kwa Mungu upate ahueni. Wiki iliyopita tulianza kujadiliana kuhusu mada hii kama inavyojieleza. Je, wewe unaamini kwamba kwenye mapenzi kuna uchawi? Unaamini kwamba kuna kitu kinaitwa limbwata? Je, ni kweli mtu anaweza kwenda kwa mganga na akafanikiwa kumpumbaza mwenzi wake akili? Nakushukuru wewe uliyetumia muda wako kunipa majibu ya jinsi unavyoyaelewa mambo haya.

 Majibu niliyoyapata yalikuwa katika makundi mawili; wapo waliosema wanaamini ni kweli kuna uchawi katika mapenzi, wakaenda mbali na kutoa mifano iliyowatokea au waliyoishuhudia na kuwafanya waamini kwamba kweli kuna uchawi katika mapenzi. Msomaji wangu mmoja kutoka Unguja, Zanzibar, alisema anao ushahidi wa jinsi mume wa rafiki yake alivyoendewa kwa mganga na kimada wake hadi akafikia hatua ya kutelekeza familia ya mke na watoto watatu, akahamia kwa kimada. Unaambiwa mpaka leo hasikii haambiwi, ameikana familia yake kisa kimada.

Kundi jingine lilisema haliamini katika uchawi! Kwamba mume kumsaidia mkewe kuosha vyombo, kufua, kupika, kumpa kila anachokitaka au kutii kila anachoambiwa, siyo lazima awe amerogwa bali akioneshwa mapenzi ya dhati, yupo tayari kufanya chochote ilimradi mwenzi wake afurahi! Kwa wale walionitumia ushuhuda kuhusu limbwata, wengine wakilalamika kwamba wenzi wao wamebadilishwa mawazo na wanawake au wanaume wa nje mpaka kufikia hatua ya kuwakana wapenzi wao wa awali kwa sababu ya ndumba, nataka waelewe kitu kimoja muhimu sana.

 Mapenzi ya dhati yana nguvu kuliko hata mauti, vitabu mbalimbali vya dini vinathibitisha hili. Kwamba, ukimpenda na kumuonesha mapenzi ya dhati mwenzi wako, naye akakupenda, mkashibana, hakuna nguvu inayoweza kuingia katikati yenu, iwe uchawi, ndumba au majini na kuwatenganisha.

Hata kama kuna mtu anautazama uhusiano wenu kwa husuda, hata akikesha kwa waganga kwa lengo la kuwatenganisha ili yeye apate nafasi, ni sawa na kazi bure! Penzi la dhati lina nguvu asikwambie mtu! Hata hivyo, mapenzi ya dhati yanapokosekana ndani ya uhusiano, uwe ni uchumba, ndoa au mahusiano ya kawaida, ni dhahiri kwamba hata vitu vidogovidogo tu, vinaweza kuwatenganisha mkaishia kusingizia uchawi!

 Kama hampendani, mtu anaweza kuingiza maneno ya kuwafitinisha tu, mkaachana. Kama hampendani kwa dhati, ugomvi mdogo tu, unaweza kuwatenganisha, kama ni ndoa ikavunjika, kama ni uchumba ukaishia njiani na mambo ya namna hiyo! Kwa hiyo jambo la msingi, siyo kukimbilia kwa waganga mambo yanapoharibika ukiamini mwenzi wako amerogwa na mpenzi wa nje. Unachotakiwa kufanya kuanzia sasa, kabla mambo hayajaharibika, ni kuhakikisha kila siku iendayo kwa Mungu, unaishi vizuri na mwenzi wako.

Mpende kwa dhati, kuwa mwaminifu, mjali, msamehe anapokosea, mtimizie mahitaji yake ya msingi na usichoke kumrekebisha kwa njia nzuri ili mwisho aje kuwa bora!

Mkiishi hivi, hata atokee mchawi kutoka kuzimu, wala hawezi kuvunja ndoa yenu wala wewe hutahitaji kwenda kwa mganga ili kumroga au kumpumbaza akili asikuache, mapenzi yako ndiyo yatakayokuwa uchawi tosha. Lakini ikitokea mkaishi kwa mazoea tu, hakuna mapenzi ya dhati ndani ya nyumba, kila mmoja anajiona yeye ni bora, kiburi, dharau, usaliti, maudhi, uongo na kero za namna hiyo zimetawala, uhusiano wenu hauwezi kwenda popote na ninyi ndiyo mtakuwa wachawi wa penzi lenu.

Hata ukihangaika kwa mitishamba na hirizi, kama humuoneshi mapenzi ya dhati mwenzi wako, ni kazi bure! Siku akimpata anayemjali na kumuonesha mapenzi ya dhati, itakula kwako. Ni hayo tu kwa leo, tukutane wiki ijayo kwa mada nyingine murua.

Breaking News: Bondia Thomas Mashali Auwawa, Mwili Wake Waokotwa Vichakani Dar

$
0
0
Bondia maarufu wa ngumi za kulipwa nchini, Thomas Mashali amefariki dunia usiku wa kuamkia leo October 31 2016 maeneo ya Kimara DSM, Taarifa zinadai kuwa alishambuliwa na wananchi baada ya madai ya kuitiwa mwizi kwa kushambuliwa na wananchi kwa madai ya kuitiwa mwizi.
Promota Siraji Kaike amesema watu aliokuwa anagombana nao walimwitia mwizi na wakapiga mapanga akawa ametupwa na bodaboda waliokuwa wanamjua Thoams Mashali walimuokota na kumpeleka hospitali ambapo baadaye zilitolewa taarifa kuwa amefariki.


Yassin Abdallah maarufu kama Ustaadhi, mmoja wa viongozi wakongwe wa mchezo wa ngumi amethibitisha na kusema mwili wa Mashali upo kwenye chumba cha kuhifadhia maiti katika Hospitali ya Rufaa ya Muhimbili jijini Dar es Salaam.

"Tumethibitishiwa hizo taarifa za majonzi kabisa, mwili upo Muhimbili na msiba upo kwao Tandale," alisema Ustaadhi.

Faraja Kotta Azungumza Hili Baada ya Miss Tanzania 2016 Diana Edward Kuandamwa Mitandaoni

$
0
0
Aliyewahi kuwa mshindi wa Miss Tanzania kwa mwaka 2004, Faraja Kotta Nyalandu amechukizwa na yale yanayoendelea katika mitandao ya kijamii juu mshindi wa taji la Miss Tanzania 2016, Diana Edward.
faraja

Hatua hiyo imekuja baada ya watu katika mitandao ya kijamii kuanza kumshambulia mshindi huyo juu ya umri wake. Hata hivyo kamati ya Miss Tanzania ilitolea ufafanuzi juu ya suala hilo.

Miss Faraja Kotta ambaye na yeye pia alipitia kipindi kigumu pindi alipotangazwa mshindi, ameandika ujumbe huu:


"Niliposhinda Miss Tanzania, kuna mtangazaji fulani (tena wa kiume) wa kipindi cha redio cha asubuhi alitumia kama saa nzima hewani kusema ambavyo sikustahili kushinda. Asubuhi ya Jumatatu kama leo baada ya weekend ya shindano.

Nilipigiwa simu kuamshwa. Nakumbuka niliamka nikawasha redio na nikasikiliza kipindi chote, peke yangu, chumbani.
Nilitetemeka, nilishindwa kuoga, kula, nilijifungia ndani siku nzima nikilia. Niliwaza sana ambavyo pengine ni kweli sikustahili. Nilijuta kushiriki Miss Tanzania.

I was young and naive. I had just turned 19, coming straight from the safety nets of Catholic nuns boarding schools. Sikujua kuna watu wanaweza kuwa na roho mbaya hata kwa watu wasiowajua.

It took my parents (RIP) na kila busara waliyonayo kunifanya nijisikie vizuri. I had to dig deep inside me to regain my purpose. I was exposed to a cruel world and yes, I quickly learnt, it is what it is.

Leo hii hakuna binadamu mwenye hiyo nguvu niliyompa yule mtangazaji. I learnt the hard way but I am grateful for the lesson. Thank God I learnt early. Kuna sehemu ya nguvu niliyo nayo leo iliyotokana na kujeruhiwa na binadamu na kupona. Lakini si kila mtu atapata bahati ya kupona, unaweza kumjeruhi mtu na akapotea moja kwa moja. Usijitafutie laana za reja reja.
To the newly crowned Miss Tanzania, Do you honey!

To the rest of us, tujenge zaidi ya kubomoa. Love doesn’t cost a thing!
God bless,
Faraja"
Viewing all 104766 articles
Browse latest View live




Latest Images