Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104709 articles
Browse latest View live

Masanja Mkandamizaji Adai Anampenda Monica Mpaka Wanawake Wengine Anawaona ni Wavulana

$
0
0
Mchekeshaji Masanja Mkandamizaji amefunguka ya moyoni kuhusu mkewe wake na kuandika yafuatayo.....



Fuata Njia Hizi, Mwanamke Hakukatai Ng`oo Hata Awe Vipi

$
0
0
Kifupi unakuta mwanaume ana status nzuri tu lakini anakosa mwanamke anayejielewa.yaani wengine hadi wananiuliza sometimes mimi "hivi wewe unawapataje wanawake wazuri na wanaojimbua hivo".

Sasa leo nimeona ni vyema nikishare na nyinyi namna ya kumnasa demu hata awe ni anajitambua vipi!

1: Unapoomba namba ya simu hakikisha huombi kwa papara, yaani usioneshe kama una shida sana na usioneshe kama unataka kumtongoza, bali onesha kama unataka tu ulafiki wa kawaida,yaani lafiki wa kuchati nae tu kawaida.

2: Akikupa namba leo kausha usimtafute leo leo, mtafute baada hata ya wiki,msalimie tu na umpigie, hapa uangalie na muda ambao unadhani mtu anakuwa free, sio kupiga simu asubuhi sana au mchana au usiku sana, piga mida ya saa mbili usiku,na usiongee nae zaidi ya dakika 5.

3: Hakikisha kila siku unamtumia msg mara 3 na kumpigia simu mara moja, yaani asbh mtakie asbh njema, mchana, jioni na usiku piga kumpa pole na heka heka za mchana, ongea nae si zaidi ya dakika 5 ili usimchoshe.

4: Hakikisha hutumii maneno ya mtaani sana mfabo oya,inakuwaje,michongo vipi, barida, mzuka, poa n.k. Tumia maneno mazuri ya busara mfano sawa, haya, umeshindaje, habari yako, n.k. yaani asikuone wewe hujitambui.

5: Weka nae urafiki wa kudumu kiasi kwamba awe anakumiss, na ukimtext asipojibu mtumie vocha hata ya buku. Ila angalia usitumie pesa sana.

6: Omba outing nae, na akikubali basi mpeleke sehemu tulivu yenye adabu na sio mnaenda bar, mkiwa huko ongelea zaidi maisha ya kawaida ya mwanadamu, usiongelee ishu za X wako kamwe, ishu za mapenzi usiongelee kabisa, weka vistory vya kuchekesha ili awe anafurahi na kukumiss mkitoka hapo.

7: Ukiwa unapiga nae stori kwenye simu usiwe unaongea sana, na hata mkiwa pamoja basi usiongee sana kama chiriku, pangilia maneno sana ya kuongea(waza kabla ya kusema).

Baada ya urafiki wa kama miezi miwili hivi, hapo sasa mtamkie wazi wazi kwamba unampenda tangu muda mrefu, na umtongoze kwa heshima sana. Nakuhakikishia hapo hachomoki hata kwa dawa.

NB: Mbinu hizi ni za kuwapata tu wanawake wanaojielewa, wanaotaka mwanaume/mpenzi na sio wanaotaka pesa. Kwa wale wanawake vicheche, we tumia pesa tu, ukimtongoza leo jioni basi kesho unamfunua

Makamu wa Rais Samia Suluhu Aokoa Milioni 33 Kwa Kupanda ndege ya ATCL kwenda Mwanza

$
0
0
Katika  kuendelea kujenga dhana ya kubana matumizi ya fedha za serikali, Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan amesafiri kwa ndege ya abiria ya Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL) kutoka Dar es Salaam kwenda Mwanza na kuokoa zaidi ya Sh milioni 33.

Kabla ya kuanza safari hiyo jana kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) jijini Dar es Salaam, Makamu wa Rais akizungumza na waandishi wa habari, alisema kwa kupanda ndege hiyo ameokoa fedha za serikali na kodi za wananchi.

Alisema ameona ashirikiane na Watanzania kuonesha uzalendo kwa kutumia huduma ambazo zinatolewa na serikali na kuwataka Watanzania wote kutumia ndege hizo.

“Ningepanda ndege ya kukodi ningetumia shilingi milioni 40 kwa safari hii, lakini nikaona hapana nikaamua mimi pamoja na msafara wangu tutumie ndege hii ya Shirika la Ndege Tanzania ambapo tumetumia Shilingi milioni 7.6 pekee,” alisema Makamu wa Rais aliyeambatana na watu 16 katika safari hiyo.

Makamu wa Rais ambaye alipanda ndege hiyo pamoja na abiria wengine wa kawaida, aliwataka viongozi wengine pia kufuata mfano huo kusafiri kwa kutumia ndege za shirika hilo.

Alisema ameona kwenye televisheni watu wakitoa maoni yao juu ya kampuni hiyo ya ndege kuwa ni nzuri kwa sasa na yeye akaamua kusafiri na ndege hiyo.

“Niliona kwenye televisheni watu wakitoa maoni mazuri tu juu ya shirika hili na mimi nikaona nitumie nafasi hiyo,” alifafanua Makamu wa Rais.

Hivi karibuni, serikali imenunua ndege mbili aina ya Bombardier Q400 na kuzikabidhiwa kwa ATCL na zimeanza kufanya kazi katika mikoa mbalimbali nchini huku zikiwa na gharama nafuu, lakini pia zikiwa na gharama nafuu ya uendeshaji.

Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa ambaye alikuwepo uwanjani akimsindikiza Makamu wa Rais, alisema Watanzania waelewe kwa sasa kampuni hiyo iko kwa ajili ya kufanya biashara.

Alimpongeza Makamu wa Rais kwa kuonesha ushirikiano mkubwa na pia uzalendo kwa kusafiri na ndege ya ATCL, kwani angeweza kutumia ndege nyingine yoyote.

“Leo hii kwa kutumia ndege ya Tanzania yeye pamoja na wasaidizi wake ni jambo jema sana alilolifanya na pia ni jambo la kizalendo tunampongeza sana, kwani angeweza kutumia ndege nyingine yoyote anayoitaka,” alisema Profesa Mbarawa.

Alisema ndege za ATCL gharama zake ni nafuu na pia huduma zao zimeboreshwa zaidi, na kwamba ifikapo mwaka 2018 serikali itanunua ndege nyingine moja na pia mwaka 2019 inatarajia kununua ndege nyingine.

Mkurugenzi Mkuu wa ATCL, Ladislaus Matindi alisema kampuni hiyo inaboresha huduma zake ambako kwa sasa wanaboresha huduma za mtandaoni kwa ajili ya watu kushika nafasi ya safari na hata kulipia kupitia mitandao ya simu.

Unakumbuka Bifu ya TID na Dully Sykes...Dully Afunguka Haya

$
0
0
Hapo zamani, Dully Sykes na TID walikuwa kama paka na panya. Na sasa Dully ameibuka na kudai umri wake na pia kuwa na majukumu mengi, vilimfanya asione umuhimu wa kuendelea na tofauti zao.

Alikuwa akizungumza tofauti zilizopo kati ya Diamond na Alikiba na kudai kuwa ipo siku wakikua, wataacha.

“Hata mimi pia ilivyofikia kwenye age moja hivi nilikuwa na matatizo na TID, zamani. Lakini nilipoweza kukua niliacha hivyo, nilivyoanza kupata majukumu nikasahau kwamba tulikuwa na matatizo,” Dully alimweleza Lil Ommy kwenye kipindi cha The Playlist cha Times FM.



Ugomvi wa TID na Dully ulitokea mwaka 2002 wakati ambapo wote walikuwa wa moto na kushindanishwa kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee walipokuwa wakizindua album zao.

May 2014, Dully alikumbushia kuwa alimfunika TID kwenye show hiyo. Kauli hiyo haikumpendeza TID aliyeamua kujibu kwa kusema: TID unaweza kumfunika mzee Mnyama wewe? Alivaa nguo zake za Kariakoo, kama mapazia hivi,unafikiri Dully Sykes anaweza akanifunika mimi? Nimesoma shule za kishua, nimefanya muziki kwa intelligence, hao watu wa Kariakoo washamba.”

Naye Dully alijibu kauli hiyo ya TID kupitia XXL ya Clouds FM na kusema: Ngoja nikwambie kitu kimoja TID mimi nimempita miaka mingi, nimempita kila kitu yeye kanipita kasoma ndio alichonipita TID. Mimi kipindi hicho ndiye nimemkaribisha kwenye industry ‘mimi ndio Dully Sykes nipo juu mwaka 2002’, miaka mitatu nyuma mimi ndio nimetoka TID anatoka ndio nimemkaribisha. Halafu uzinduzi wetu TID alikuwa amelipa kosta mbili pale Magomeni akawaahidi atawapa hela wakifika pale Diamond round ya pili hajawapa hela ikabidi wale aliowaleta kwenye kosta mbili wamzomee yeye. Kwahiyo TID kaamua kuongea uongo. Halafu TID ni mdogo wangu anajua mimi ni kaka yake, historia ipo na picha ninazo. Mimi ndio nilipendeza kushinda TID. TID alikuja kama mgambo pale alikuja kama mgambo na nguo za mgambo nikisema mwanajeshi atakuwa juu kidogo. Mimi na miaka mitatu nyuma TID ndo anatoka 2002 na Zeze. Rafiki yangu kusoma hujui hata hata picha pia, inaeleweka na inajulikana kijana wangu mdogo ndio hivyo.”

Hivi karibuni bifu hiyo tena ilionekana kufufuka baada ya verse za Dully zilizokuwepo kwenye wimbo wa TID, Confidence alioshirikishwa Joh Makini kuondolewa.

U Heard: Kilichotokea Kwenye Familia ya Calisah Baada ya Video yake na Wema Kuvuja

$
0
0
November  14 2016 kwenye U Heard ya Soudy Brown amezungumza na Calisah kuhusu video iliyomuonesha yeye akiwa na  staa wa Bongo Movie, Wema Sepetu wakikiss, Calisah amesema baada ya video hiyo kuvuja, bibi yake alipoambiwa kwa sababu alikuwa anamtetea sana Calisah alipata mshituko na kufariki……

’Hayo mambo yamesababisha mpaka nimepoteza mtu, amepata presha amefariki leo, siko sawa kabisa imenicost sana hata siwezi kuongea nimepoteza bibi yangu kwa sababu ya hivi vitu imeniumiza sana halafu mimi sijafanya hivyo vitu nivujishe video ili iweje‘ ;-Calisah

Kupata Full Stori, Bonyeza play hapa chini

Serikali Yasema Haya Kuhusu MISS TANZANIA’ – Waziri Nape

$
0
0
November 14, 2016 Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nnauye alikutana na waandishi wa habari kuzungumza masuala mbalimbali ya michezo ikiwemo matatizo yaliyotatuliwa kwenye mashindano ya  Miss Tanzania 2016.

Akizungumza mbele ya waandishi wa habari Waziri Nape aliyasema haya……….>>>Yapo baadhi ya mapungufu yaliyojitokeza nyuma kwenye mchakato wa kumpata Miss Tanzania na ndio maana serikali ikaingilia kati ikalisimamisha shindano hili’

’Wakati shindano lililoposimamisha kulikuwa kunafanyika mazungumzo kujua wapi pamekosewa, matokeo ya uchambuzi yalituonyesha hatua za kuchukua hili tusirudie makosa yaliyofanyika ndio maana tukaruhusu kulianzisha upya shindano, mimi naamini mapungufu mengi yaliyojitokeza nyuma waliyafanyia kazi na serikali tumeridhika’ ;-Waziri Nape

Samuel Jackson Agoma Kuhama Marekani Kama Alivyohaidi Baada ya Donald Trump Kushinda urais

$
0
0
Ahadi ni deni – muigizaji mkongwe wa Marekani, Samuel L. Jackson ameonekana kuipinga ahadi yake aliyowahi kuitoa kuwa atahamia Afrika Kusini endapo Donald Trump atateuliwa kuwa Rais wa nchi hiyo.

Kupitia mitandao yake ya kijamii, Jackson aliandika, “If that motherf- -ker becomes president, I will move my black ass to South Africa.”

Hatimaye muigizaji huyo amekuja na ujumbe mpya kupitia mtandao wake wa Twitter, ameandika, “Why y’all so anxious for me to leave?! I pay More Taxes than All U Trumpafukkaz… Him too!!.”

Trump alichaguliwa kuwa Rais wa Marekani Jumatano ya Novemba 9, kwa kushinda majimbo ya uchaguzi 276 huku Clinton akishinda 218.

Calisah Anashikiliwa Na jeshi la Polisi Baada ya Kuvujisha Video Akidendeka na Wema Sepetu

$
0
0
Habari zimeenea kuwa Model Calisah ambae alikuwa mpenzi wa Wema Sepetu anashikiliwa na jeshi la polisi, Shilawadu wana ripoti kuwa chanzo Cha Calisa kusakwa Hatimaye kutupwa ndani ni kutokana na kutishia kuachia video na mapicha Picha aliyowahi kupiga na dada etu Enzi Za Penzi Lao, Inasemekana eti Bwana Calisah baada kupigwa kibuti na Sepenga Ndo akaamua kusambaza video Yao wakila denda Kama kionjo na kutishia kuachia mapilauuuu ya kwichy kwichy ambayo yapo kwenye simu aliyopewa na Wema Sepetu...

Chanzo:Shilawadu/Soudybrown

HEKAHEKA: Majibu ya Cheki Budi Kuhusu Mtoto Anayedaiwa ni Wake

$
0
0
Leo November 15 2016 Heka Heka ya Leo Tena ndani ya Clouds FM imefanya muendelezo wa hekaheka ya jana iliyohusu mtoto ambaye alifika katika Studio za Clouds FM siku ya Ijumaa November 11 2016 na kukutana na Geah Habibu akiomba kukutanishwa na baba yake mzazi ambaye ni msanii wa Bongo Movie aitwaye Cheki Budi.

Heka Heka ilizungumza na mama mzazi wa wa binti huyo ambaye ameeleza kuwa alikuja Dar es salaam kwa mara ya kwanza mwaka 2005 akiwa ni mke wa mtu na alikaa kwa siku 9 tu na wakati akikaribia kuondoka alienda Club ambako alikutana na mwanaume ambaye anatajwa kuwa ni Cheki Budi ambaye muigizaji wa Bongo Movie na ni siku hiyo hiyo alipata ujauzito.

Sasa Leo Geah Habib amempata Cheki Budi kazungumzia kuhusu yeye kudaiwa kuwa yule ni mtoto wake, Cheki Budi amesema……
’Nipo tayari kuonana naye, ikiwa maelezo hayajanitosheleza nitapima DNA  kama mtoto ni wa kwangu mimi nitampokea, hivi kweli mimi nitakumbuka miaka 11 iliyopita halafu mtu mwenyewe anasema ametembea na mimi siku moja’

Kusikiliza Full Stori, Bonyeza Play Hapa chini:

Calisah Azidi Kuvujisha Picha za Wema Sepetu

$
0
0
Hii ni fundisho kwa wanawake wote usiparamie Mwanaume hovyo kabla hujamjua vingenevyo muanze na system ya Kugegendwa gizani..Baada ya Video wakilana Denda sasa ni hizi Picha

Kesi ya Godbless Lema na mkewe kumtukana Mkuu wa Mkoa wa Arusha Yakwama Kusikilizwa..

$
0
0
Kesi ya kumtukana Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mrisho Gambo, inayomkabili Mbunge wa Jimbo la Arusha Mjini, Godbless lema na mke wake Neema Lema (33), imeshindwa kusikilizwa maelezo ya awali.

Hatua hiyo ni baada ya Mbunge huyo kukwama kuletwa Mahakamani toka Mahabusu kwa sababu zisizojulikana.

Kukosekana kwa Mbunge huyo kuonekana Mahakamani, kulimlazimu Hakimu Mfawidhi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Arusha Agustino Rwezile kutoa amri ya kutolewa hati ya kumtoa Mahabusu mshitakiwa huyo na kumleta mahakamani hapo ili kesi hiyo isikilizwe maelezo ya awali.

Hata hivyo tangu amri hiyo itolewe saa nne asubuhi hadi saa saba mchana mshitakiwa hakuweza kuletwa mahakamani hapo, licha ya mke wake kuwepo mahakamani hapo.

Rwezile alimtaka wakili wa serikali kueleza sababu za kushindwa kumleta Lema Mahakamani wakati Mahakama imetoa amri.

Wakili wa serikali Fotunatus Mhalila alisema mshitakiwa ameshindwa kuletwa Mahakamani kutokana na sababu zisizozuilika , ila kwa sababu upelelezi umekamilika aliomba Mahakama ipange tarehe ya usikilizaji wa hoja za awali.

Majibu hayo yalipingwa vikali na Wakili wa utetezi, John Mallya ambaye alitaka kufahamu sababu za kutomleta Lema anazodai hazikuweza kuzuilika ni zipi na kwa nini zisitajwe  mahakamani.

“Mheshimia hakimu hizo sababu zisizoweza kuzuilika ni zipi, Wakili wa seriali atueleze, tujue kama siyo amedharau mahakama licha ya kutakiwa kumleta mshitakiwa,” alisema.

Baada ya hoja hizo kutolewa Hakimu Rwezile aliendelea kusisitiza hati ya kumtoa Mahabusu itolewe ili aletwe Mahakamani leo katika kesi hiyo, ambayo itasikilizwa hoja za awali.

Awali katika kesi hiyo Godbless Lema na mke wake Neema, alisomewa mahitaka kuwa kati ya Agosti 20 Mwaka huu ndani ya Arusha,walimtumia ujumbe wa simu ya kiganjani Mkuu huyo wenye lugha ya matusi , huku wakijua ni kosa kisheria.

Ilidaiwa kuwa ujumbe huo ulitumwa kutoka 076415**47 namba 075655**18 kwenda namba 0766-75**75 ukidai, “Karibu, tutakuthibiti kama Uarabuni wanavyothibiti mashoga.” Washitakiwa walikana shitaka hilo na walipatiwa dhamana

Orodha ya Vyuo 26 Vilivyofutiwa Usajili na NACTE Leo

$
0
0
Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi (NACTE) limevifungia vyuo vya ufundi 26 kutokana na makosa mbalimbali, ikiwamo kushindwa kuzingatia masharti yaliyowekwa katika cheti cha usajili wa vyuo hivyo, huku likisimamsisha utoaji wa programu zilizokuwa zikitolewa katika vyuo 20 ambazo hazijasajiliwa.

Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam, Kaimu Katibu mtendaji wa NACTE, Dkt. Adolf Rutayuga, alisema kuwa wamekuwa wakifuatilia vyuo vya ufundi ili kutathmini kama vinafuata viwango vya ubora wa kitaaluma vilivyowekwa na NACTE katika kutoa mafunzo.

Katibu huyo amesema kuwa baada ya kufanya uchunguzi huo, wamebaini vyuo 26 vilishindwa kuzingatia masharti yaliyowekwa na NACTE katika cheti cha usajili, huku vyuo 20 vikitoa mafunzo ambayo hayajathibitishwa chini ya idara isiyotambulika,wakati vyuo viwili vikiwa na vituo vya satellite/Kampasi ambavyo navyo havijathibitishwa na chombo husika.

NACTE ni bodi iliyoanzishwa kisheria chini ya Sheria ya Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi, kifungu cha 129, kusimamia na kuratibu utoaji wa elimu ya ufundi na mafunzo nchini Tanzania.  Chini ya sheria hiyo, ili kufikia na kudumisha hali ya mtoa mafunzo, vyuo vyote vinatakiwa viwe vimesajiliwa, vibali na kuwa mitaala iliyopitishwa na baraza. Vyuo haviruhusiwi kuanza kutoa kuanza kutoa huduma yoyote ya mafunzo bila idhini ya baraza.

Hapa chini ni mgwanyo wa vyuo katika makundi matatu na hatua zilizochokuliwa dhidi ya kila kundi

Vyuo vya Ufundi vilivyofutiwa usajili
S/NCHUO
1Institute of Management and Development Studies – Iringa
2Green Hill Institute – Mbeya
3Institute of Business and Social Studies – Mbeya
4Loyal College of Africa – Mbeya
5Mbeya Training College – Mbeya
6Mbengwenya College of Business and Information Technology –Mbinga
7New Focus College – Mbeya
8Shukrani International College of Business and Administration –  Mbeya
9Majority Teachers College – Mbeya
10Rukwa College of Health Sciences – Sumbawanga
11MAM Institute of Education – Mbeya
12Belvedere Business and Technology College – Mwanza
13Geita Medical Laboratory Sciences and Nursing Training College – Geita
14Global Community College – Geita
15Muleba Academy Institute – Muleba
16St. Bernard Health Training Institute – Katoro, Geita
17Victoria Institute of Tourism and Hotel Management – Mwanza
18Gisan Institute of Health Sciences – Mwanza
19Dar es Salaam Institute of Business Management – Dar es Salaam
20SAMFELIS College of Business Studies – Dar es Salaam
21Ellys Institute of Technology – Bunda, Mara
22Tanzania Institute of Chartered Secretaries and Administrators – Arusha
23Emmanuel Community College – Kibaha
24Modern Commercial Institute – Dar es Salaam
25Marian College of Law – Dar es Salaam


Vyuo vya Ufundi vinavyotoa mafunzo ambayo hayajathibitishwa
S/NCHUO-MAFUNZO

1MISO Teachers College – MafingaCompetence Building Network (CBN) – a Certificate in Early Childhood Education
2Tusaale Teachers College – MafingaCompetence Building Network (CBN) – a Certificate in Early Childhood Education
3The St. Joseph’s College Institute of Business and Management (SJCIBM) – Morogoro
4The Golden Training Institute – Dar es Salaam
5Nkrumah Mkoka Teachers College – Kongwa, Dodoma
6National Institute of Agriculture (Chuo cha Kilimo cha Taifa) – Arusha
7Musoma Utalii Training College – Musoma
8Mwanza Polytechnic Institute – Mwanza
9Mwanza Polytechnic Institute – Maswa
10Ruter Institute of Financial Management – Mwanza
11Dar es Salaam Institute of Journalism and Mass Communication – Mwanza
12Dar es Salaam Institute of Journalism and Mass Communication – Geita
13Dar es Salaam Institute of Journalism and Mass Communication – Bukoba
14Singni International Training Institute – Bukoba
15Dar es Salaam Institute of Journalism and Mass Communication – Kahama
16Dar es Salaam Institute of Journalism and Mass Communication – Simiyu
17Richrise Teachers College – Geita
18Twiga Training Institute – Musoma
19Zoom Polytechnic Institute – Bukoba
20St. Thomas Training College – Shinyanga

Vyuo vya Ufundi vyenye Vituo vya Satellite / Kampasi
S/NCHUO

1MISO Teachers College – Mafinga
2Rungemba Teachers College – Mafinga

Wanafunzi Wakumbwa na Ugonjwa wa Kuanguka Ovyo

$
0
0
Wanafunzi wa kike 12 wanaosoma Shule ya Msingi Nditi, Wilaya ya Nachingwea, mkoani Lindi, wamekumbwa na ugonjwa wa kuanguka ghafla na wengine kupoteza fahamu, walipokuwa wakicheza katika viwanja vya shule hiyo.

Mwalimu Mkuu wa shule hiyo, Amon Livigha, alikiri kutokea tukio hilo katikati ya wiki iliyopita, saa mbili asubuhi.

Alisema baada ya tukio hilo, baadhi ya wazazi walifika shuleni hapo na kuwachukua watoto wao na kwenda nao nyumbani.

“Nilipata taarifa ya kuanguka kwa wanafunzi hao nikiwa darasani nafundisha, hivyo kutokana na uzito wa tatizo, nililazimika kukatisha masomo na kwenda kuwahudumia watoto hao.

“Wakati tukiendelea kufanya utaratibu wa kuwakimbiza wanafunzi hao kituo cha afya kupatiwa huduma, baadhi ya wazazi walikataa watoto wao wasipelekwe hospitali na kuondoka nao,” alisema.

Mwalimu Livigha alisema kutokana na tukio hilo, kamati ya shule, wazazi na uongozi wa Serikali ya kijiji na kata hiyo wamekutana kujadili suala hilo.

Mtendaji wa kata hiyo, Juma Mng’anga, alikiri kutokea tukio hilo na kueleza kuwa tayari wameshatoa taarifa makao makuu ya wilaya, Nachingwea.

Calisah Aachiwa Baada ya Kulala Polisi Kwa Tuhuma ya Kusambaza Video ya Utupu ya Wema Sepetu

$
0
0
Mode Calisah ameachiwa jioni hii baada ya siku ya jana kushikiliwa na jeshi la polisi kwa tuhuma za kusambaza mitandaoni video ya utupu ya Wema Sepetu.

Akiongea na Bongo5 jioni kwa njia ya simu wakati akielekea nyumbani kwake, Calisah alisema ni kweli alikamatwa toka jana kutokana na tuhuma za kusamba video hizo mtandaoni.

“Kweli nilikamatwa toka jana lakini nimeachiwa,” alisema Calisah.

Pia model huyo amesema atatoa taarifa zaidi ya nini kinaendelea kuhusu suala hilo.

Naibu Waziri wa Afya Anasa Kiwanda cha Viroba FEKI

$
0
0

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe. Dkt. Hamisi Kigwangalla, akiwa ameongzana na timu ya Serikali yenye wataalamu na wanausalama wameendesha operesheni kali ya kusaka viroba feki na pombe nyingine haramu katika maeneo ya Jiji la Dar es Salaam  na kufanikiwa kukama shehena kubwa ya bidhaa hizo feki na haramu kwenye maeneo  hayo.

Katika operesheni hiyo, pia wamefanikiwa kukibaini kiwanda bubu kinachotengeneza kinywaji aina ya konyagi na Smirnoff feki maeneo ya Sinza Jijini Dar  es Salaam. 

Kiwanda hicho kinatengeneza vinywaji hivyo kwa kutumia ‘spirit’ ambayo inachanganywa na ‘gongo’; spirit, gongo, chupa tupu na zilizojazwa, vizibo, vifungashio vimekamatwa.

Kwa hatua hiyo Jeshi la Polisi linawashikilia watu wawili ambao inasemekana wanafanya kazi pamoja na bwana Yusuf Abdul Kalambo, ambaye anatafutwa na polisi mpaka sasa kwa tuhuma za kuendesha shughuli hizo.



Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe. Dkt. Hamisi Kigwangalla  akiwa ameshika vifuniko vya bidhaa za pombe feki katika moja ya kiwanda bubu cha kutengeneza pombe hizo aina ya Konyagi. katika zoezi hilo eneo la Sinza

Staili Nyingine Yaibuka Sakata la Godbless Lema

$
0
0
Arusha. Sakata la mbunge wa Arusha Mjini (Chadema), Godbless Lema dhidi ya vyombo vya dola limeendelea kwa staili nyingine ya kushindwa kumpeleka mahakamani jana kujibu tuhuma za uchochezi dhidi ya Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo.

Lema amesota rumande kwa siku 13 ambazo ni sawa na saa 312.

Mbunge huyo amekuwa kwenye msukosuko wa kisheria na Jamhuri iliyomshtaki kwa tuhuma za kutoa maneno ya uchochezi na mapema wiki hii alipewa dhamana ambayo haikufanikiwa baada ya mawakili wa Serikali kuwasilisha taarifa ya kusudio la kukata rufaa kabla ya hakimu kuruhusu kutekelezwa kwa utaratibu wa dhamana.


Mgonjwa ashindikana kutibiwa Muhimbili kwa kuwa mrefu kuliko binadamu wa kawaida

$
0
0
Kijana Baraka Elias Mashauri mwenye umri wa miaka 35 mkazi wa Musoma mkoani Mara ameshindwa kupata matibabu katika Taasisi ya Mifupa Muhimbili (MOI) kutokana na urefu wake usio wa kawaida.

Baraka anayesumbuliwa na tatizo ya nyonga ana kimo kirefu cha zaidi ya  futi 7 na hii kufanya kushindwa kupatiwa matibabu kufuatia vifaa katika taasisi hiyo ikiwemo mashine za X- ray vitanda vya kufanyia upasuaji kuwa vifupi ukilinganisha na urefu wake.

Tatizo hilo la nyonga linalomsumbua Baraka limemfanya ashindwe kutembea na kulazimika kutumia magongo ambayo anasema yanamtesa kutokana na urefu alionao.

Akizingumzia jinsi watu wanavyomshangaa kutokana na urefu wake alisema kuwa kwake anaona fahari kwani ni maisha ambayo ameyazoea kila anapokwenda. Amesema kuwa hiyo haimpi shinda kwani anajua wanamshangaa kutokana na urefu wake kitu ambacho si kibaya.

Kuhusu ugonjwa unaomsumbua na baada ya kushindikana kupatiwa matibabu nchini, Baraka ameomba wasamaria wema waweze kumsaida ili apatiwe matibabu nje ya nchi ili arudie  kwenye hali  yake ya kawaida kwani magongo anayotumia kutembelea yanamtesa.

Hapa chini ni video yake alipokuwa Hospitali ya Taifa Muhimbili kitengo cha Mifupa. TAZAMA VIDEO:

Edward Lowassa Afafanua Kutoonekana Kwake Misiba ya Sitta na Mungai

$
0
0
Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa ametoa ufafanuzi kuhusu kutoonekana kwake kwenye misiba ya viongozi wawili wa zamani serikalini, Samuel Sitta na Joseph Mungai.

Sitta, aliyekuwa Spika wa Bunge la Tisa, alifariki dunia Novemba 7, akiwa Ujerumani alikokwenda kutibiwa tezi dume na siku iliyofuata alifariki Mungai, aliyekuwa Waziri wa Elimu wa Serikali ya Awamu ya Tatu.

Gumzo kwenye mitandao ya kijamii lilikuwa ni kutoonekana kwa Lowassa, ambaye hivi sasa ni mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema.

Lowassa aliliambia gazeti hili jana kuwa, kilichomkwamisha kufika kwenye misiba hiyo ni kuwa safarini Afrika Kusini alikokwenda kumuangalia mdogo wake, Bahati Lowassa aliyekuwa mgonjwa.


Picha ya Jokate Akiwa Amekumbatiana Yazua Gumzo, Mwenyewe Adai ilikuwa Event

$
0
0
Watu Wabaya, Picha ya Jokate ya zamani akiwa amekumbatiana na Calisah imeubuliwa na kuzua sintofahamu huku wengine wakisema Jokate alishatoka na Mwanaume huyo ambae amekuwa gumzo kipindi hiki baada ya kutoka na Wema Sepetu na kusemekana anavujisha Picha za Faragha akiwa na Wema...

Jokate amejibu kwa kuandika haya:

Saida Karoli Adai Haujui Mkataba Aliosaini Meneja wake na Diamond Kuhusu Wimbo ‘Salome’ (Video)

$
0
0
Msanii wa zamani wa muziki wa asili Saida Karoli amedai yeye anasikia kama watu wengine kwenye vyombo vya habari kwamba Diamond ameiangia mkataba na meneja wake wa zamani kuhusu kutumia vionjo vya nyimbo zake katika kutengeneza wimbo ‘Salome’ wa Diamond.
saida-karoli

Muimbaji huyo amedai hizo asilimia 25 za mapato za wimbo ‘Salome’ ambazo zilielezwa na viongozi wa WCB hazijui kwa kuwa hakuhusishwa kwenye hilo.

“Tatizo limekuja kwa meneja wangu aliyempatia Diamond kazi, mimi nimempatia bure Diamond hiyo kazi aitumie,” alisema Saida katika runinga ya KUTV ya nchini Kenya. “Lakini kwenye kusikia masikioni kwangu na kwenye vyombo vya habari kwamba Diamond amempatia pesa milioni 25 meneja wangu wakawa wametengeneza mkataba kwamba huu wimbo utatumika hivi na hivi ila mimi kama mimi huo mkataba siujui na wala sikuuona na wala hawakunionyesha. Mimi ninachojua nimempatia kazi Diamond bure ili aitumie tuinuane wasanii wa Tanzania,”

Pia muimbaji huyo amedai yeye alishiriki kiasi fulani katika kuandaa kiitikio cha wimbo huo kwa kuingiza sauti yake.

Diamond na uongozi wake baada ya kuachia wimbo huo, walionyesha picha wakati wakifanya makubaliano na meneja wa zamani wa Saida.

“Kitu tulichokifanya kabla ya kurelease wimbo, tulizungumza na uongozi wake, tukawaambia tunafanya hiki na hiki na kuna kiasi pia tukakitoa ili kiende kwake halafu tukampa 25% ya publishing. Kila income ya publishing ikiwa inaingia katika huu wimbo, mama atakuwa anapata percent,” Diamond alikiambia kipindi cha 255 cha Clouds FM.
Viewing all 104709 articles
Browse latest View live




Latest Images