Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104687 articles
Browse latest View live

Soma Hapa Kama Wewe Mwanaume Una Tatizo la Kufika Kileleni Haraka Kabla Mpenzi Wako Hajaridhika

$
0
0
Pre mature ejaculation ni nini?
Hii ni hali ambayo mwanaume anatoa mbegu mapema sana kipindi cha tendo la ndoa na mara nyingi huambatana na kushindwa kumridhisha mpenzi wake.

Tatizo hili limekua likiwapata wanaume wengi na kujisikia aibu mbele za wenzi wao pale wanaposhindwa kuendelea kabisa baada  ya hali hii kutokea.

Kimsingi  mwanaume anatakiwa achukue dakika nne mpaka nane kabla ya kutoa mbegu za kwanza lakini watafiti wanasema tatizo hili hugundukiwa mtu anapotoa mbegu ndani ya dakika moja au kabla ya dakika moja.

Tatizo hili huweza kutokea mara tu baada ya kubalehe,{primary pre mature ejaculation} mda mrefu baada ya kubalehe{secondary PE} au kutokana na aina ya mwanamke uliompata.{situational PE}

Chanzo ni nini?
Tatizo hili halina sababu za kitaalamu zilizofanyiwa utafiti zikakakubalika ila wanasayansi wanaamini sababu zifuatazo zinaweza kua chanzo kikuu cha tatizo hilo.

Kupiga punyeto au kujichua; 
mara nyingi watu wanaopiga punyeto hua wanafanya haraka kwa kujificha ili wasikutwe na mtu. tabiaile ya kulazimisha mbegu zitoke haraka huweza kuleta tatizo hili.

Kukaa muda mrefu bila kushiriki tendo la ndoa; 
kukaa mda mrefu sana bila kushiriki tendo la ndoa husababisha mkusanyiko mkubwa wa mbegu za kiume ambazo zinaleta msisimko mkubwa na ukichelewa sana kushiriki tendo la ndoa zitatoka kwenye ndoto nyevu. kawaida mwanaume anatakiwa ashiriki tendo angalau mara nne kwa wiki.

Kuwa na wasiwasi wakati wa tendo la ndoa; 
mtu akiwa na historia ya kupata  hali hii kabla, hua hajiamini na kua na wasiwasi kwamba litatokea tena na matokeo yake hulipata kweli.

Madhara ya dawa zinazofanya kazi kwenye mishipa ya fahamu;
baadhi ya dawa za usingizi, mawazo na zingine zinazofanya kazi kwenye mishipa ya fahamu huleta tatizo hili mfano amitriptyline.

Kurithi;
baadhi ya koo au familia fulani hurithi vimelea vya kua na ugonjwa huu kwa vizazi mbalimbali vya familia husika.

Magonjwa ya mfumo wa uzazi wa mwanaume mfano prostatitis.

Diagnosis{ kuutambua ugonjwa]
Mwanaume yeyote ambaye anatoa mbegu chini ya dakika moja au mbili ni muhanga wa hili tatizo na anatakiwa apewe matibabu.
 

Matibabu
Matibabu ya ugonjwa huu yamegawanyika sehemu kuu mbili kulingana na ukali wa tatizo husika.


Non pharmacological treatment{matibabu yasiyo hitaji dawa}:  matibabu haya hupewa watu ambao wanahimili mpaka dakika tatu bila kutoa mbegu.
Pharmacological treatment{matibabu yanayohusu dawa}: matibabu haya hupewa watu ambao hutoa mbegu ndani ya dakika moja baada ya kuanza kushiriki tendo la ndoa, watu hawa hushauriwa kutumia na mbinu zote mbili za matibabu.


Yafuatayo ni matibabu yasiyohitaji dawa.

Tumia condom:
Condom ni moja ya tiba nzuri ya tatizo hili kwani hufanya kazi kwa kupunguza hisia kali za mapenzi mtu anazozipata pale ambapo hatumii condom.

Kandamiza perineum kwa kidole:
Perineum ni eneo kati ya mkundu na korodani, ile sehemu ikikandamizwa na kidole huweza kuzuia kukojoa haraka wakati wa tendo la ndoa.

Punguza wasiwasi: 
hebu lifikirie tendo hili kama njia ya kujifurahisha sio njia pekee ya kutafuta kutoa mbegu,  hii itakusaidia kuondoa mawazo ya kutafuta mbegu na kuchelewa kumaliza.

Fanya taratibu: 
picha za ngono zinadanganya sana watu kwamba kulala na mwanamke lazima ufanye kwa haraka haraka kama mbwa. HAPANA; ukifanya taratibu ndio njia nzuri ya kumfikisha mwenzako na wewe kuchelewa kufika kileleni.

Badilisha style: 
ile style ya zamani ya kumlalia mwanamke kwa juu{missionary position} inaleta msuguano mkubwa kwenye kichwa cha uuume hivyo itakufanya ufike haraka sana.

Tumia style ya wewe mwanaume kutangulia chini afu mwanamke juu au kulala kwa upande wote mnaangalia upande mmoja hii itakusaidia sana kuchelewa

Toa mawazo kwamba unafanya ngono: 
hebu jaribu kufikiria mambo mengine ya kikazi au masomo wakati unafanya tendo hilo, hii itakupunguzia hisia kali za mapenzi na kuchelewa kufika.

Fanya na kuacha: 
hii ni ile hali ya kuzuia msuguano pale unapoona unakaribia kutoa mbegu kwa kama sekundi 30 kisha unaanza upya. Hakikisha haufiki “point of no return”. pointi ambayo huwezi kujizuia tena kumaliza.

Kandamiza sehemu ya shingo la uume:
hii sehemu ya shingo ya uume kwa chini ambayo ukiibana itakusaidia kuanza upya tena kihisia. Nimetumia shingo la uume kwasababu najua uume hauna mabega.

Tumia kilevi:
unywaji wa pombe mfano bia mbili kwa siku kwa wanaume pombe hupunguza kidogo nguvu ya mishipa ya fahamu na kufanya mtu aliyekunywa kuchelewa sana kufika kileleni, [watu wanaokunywa pombe lazima mtakubaliana na hili] hivyo unaweza kunywa bia, wine au whisky nusu saa kabla ya tendo na kuondoa shida hii.

·    
Matibabu ya kutumia dawa.
hizi hupewa iwapo tatizo lako ni kubwa sana na hizo njia hapo juu zimeshindikana...
1. Serotonin reuptake inhibitors mfano paroxetine na  clomipramine zimefanya kazi nzuri ya kuzuia kufika kileleni haraka..... humezwa saa moja kabla ya tendo la ndoa.[dawa hizi hazipatikani ndani ya nchi hivyo tunaagiza nje, ukihitaji wasiliana nasi kwa namba hapo chini]

2. anesthetic creams:  hii hupakwa kwenye kichwa cha uume saa moja kabla ya tendo la ndoa kuzuia msisimuko na kufanya mwanaume achelewe kufika kileleni wakati wa tendo.[dawa hizi hazipatikani ndani ya nchi hivyo tunaagiza nje kama ukihitaji wasiliana nasi kwa namba hapo chini]

Hili la Perfume, Diamond Ataandika Historia Nyingine Muhimu Kwake

$
0
0
Kwanza nikiri kuwa, Diamond ana fursa nyingi za wazi wazi ambazo ameziacha tu zipite. Kwa umaarufu aliojikusanyia hadi sasa katika bara zima, alipaswa kuwa na miradi mingi chini ya jina lake ambayo ingekuwa inamuingizia mamilioni ya fedha, ukiacha zile anazopata kutokana na muziki wake.

Lakini bado hajachelewa na kwakuwa ukubwa wake unaanza kuizidi nguvu timu yake, mambo mengine yatakuja pole pole, na uzuri tayari tumeanza kuyaona. Nafahamu kuwa aliwahi kuonesha interest ya kuanzisha clothing line yake ya WCB ambayo hata hivyo aliishia kutoa bidhaa chache tu zilizovaliwa na watu wa karibu na hazikuwahi kuingia sokoni kwa ukubwa uliotarajiwa. Hicho ni kitu ambacho huenda akawa amekiweka pending kwa muda.

Leo nichukue fursa kumpongeza kwa kuonjesha mradi wake mkubwa wa perfume aliyoipa jina la utani, Chibu. Ni hatua kubwa sana, tena kutoka kwa msanii wa Tanzania. Sina idadi kamili ya celebrity wa Afrika wenye bidhaa ya aina hiyo, na kama wapo basi ni wachache sana. Tumezoea perfume kuwa ni kitu kinachofanywa na mastaa wakubwa duniani kama Nicki Minaj, Beyonce, Diddy, David Beckham na wengine, hivyo kwa msanii wa Tanzania kuja na kitu kama hicho na tena kinachoonekana kuwa si cha mzaha, si suala la kuchukulia poa.

Diamond anastahili pongezi kwa uthubutu huo na kuionesha Afrika kuwa, Mtanzania anaweza kufanya kitu kikubwa. Ujio wa perfume yake, ni udhihirisho tosha kuwa sasa muimbaji huyo anazidi kujitambua kuwa brand yake imekuwa kubwa na anaingia rasmi kwenye biashara ya muziki yenye matawi mengi. Katika daraja analoingia sasa, Diamond ataanza kuifaidi fedha wanayoifaidi mastaa wakubwa katika nchi zilizoendelea.

Ametambua kuwa kwa hatua aliyofikia, si muziki wake pekee unaouza, bali ni jina lake ndilo lenye thamani zaidi ya kitu chochote kwa sasa. Ametambua kuwa, amefika katika anga ambazo hamlazimu tena kutegemea muziki, endorsement na show peke yake, bali kwa mtaji wa jina lake na wafuasi wake, anaweza kutengeneza fedha kubwa zaidi.

Hatua hiyo inazidi kumweka katika ligi ya juu inayochezwa na wanamuziki wenzake nguli Afrika. Na kwakuwa si nguli wengi wa level yake wana mradi kama huo, inampa upekee zaidi na kuipa heshima Tanzania. Na pengine jambo kubwa zaidi, ni ari ya uthubutu anayoipandikiza kwa mastaa wengine wa Bongo na kuwatengenezea njia za kupita watakapo kufanya uwezekazaji wenye sura ya ukubwa kama huo anaoenda kuufanya punde.

Heko kwa Diamond na bila shaka perfume yake itapata mapokezi mazuri nje na ndani ya Afrika.

Samatta Acheza Dakika Sita Tu Genk Yaua 2-0 Ubelgiji

$
0
0
MSHAMBULIAJI wa kimataifa wa Tanzania, Mbwana Ally Samatta ametokea benchi na kuisaidia timu yake, KRC Genk kushinda 2-0 dhidi ya AS Eupen katika mchezo wa Ligi Daraja la Kwanza A Ubelgiji.

Samatta aliingia uwanjani dakika ya 84 kuchukua nafasi ya mshambuliaji Mgiriki, Nikolaos Karelis katika mchezo ambao mabao ya Genk yalifungwa na beki wa Mali, Ibrahim Diallo aliyejifunga dakika ya 20 na Alejandro Pozuelo dakika ya 38.

Huo unakuwa mchezo wa 33 kwa Samatta tangu amejiunga na Genk Januari mwaka huu kutoka TP Mazembe ya DRC, 18 msimu uliopita na 13 msimu huu, akifunga mabao nane, matatu msimu huu na matano msimu uliopita.

Katika mechi hizo, ni 17 tu ndiyo alianza, 10 msimu uliopita na tano msimu huu, wakati 15 alitokea benchi nane msimu uliopita na 12 msimu huu – na mechi 10 hakumaliza akitolewa, sita msimu uliopita na nne msimu huu.

Kikosi cha KRC Genk kilikuwa: Bizot, Nastic, Colley, Brabec, Castagne, Ndidi, Pozuelo, Susic/Heynen dk65, Bailey, Buffalo dk76' Trossard) and Karelis (82 'Samatta).

KAS Eupen: Crombrugge, Diallo, Abdourrahman, Diagne, Lazare/Dufour), Garcia, Bassey, Sylla (80 Taulemesse) Onyekuru, Blondelle (88' Hackenberg) Oncansey.

Wasira: Uzee Haunizuii Kudai Haki Yanu

$
0
0
Waziri wa muda mrefu na mbunge wa zamani wa Bunda, Steven Wasira amewajibu wanaodai kwamba amelazimika kustaafu siasa baada ya mpinzani wake, Ester Bulaya kuwashinda wapigakura wanne waliokuwa wakipinga ushindi wake wa ubunge wa Bunda Mjini na kusema hajastaafu na uzee haumzuii mtu kudai haki yake.

Juzi, Mahakama Kuu Kanda ya Mwanza ilimpa ushindi Bulaya katika kesi ya uchaguzi hali iliyotafsiriwa na wadadisi wa kisiasa kwamba huo ndiyo ulikuwa mwisho wa kisiasa wa Wasira.

Lakini jana, Wasira alipopigiwa simu na waandishi wetu kuelezea hatima yake ya kisiasa baada ya kesi hiyo, alisema wanaodai kuwa anatakiwa kustaafu siasa kwa sababu ni mzee hawana budi kuangalia kauli zao kwa sababu wapo wazee wengi anaowafahamu kwa majina na bado wapo madarakani.

“Suala la kusema nimestaafu siasa silijui na sijawahi kusema. Kesi hiyo inahusiana nini na siasa? Wapigakura wameona kuwa uchaguzi haukuwa huru na haki. Hakuna uhusiano na uhusiano uliopo ni kwa sababu mimi ni shahidi na mimi niligombea,” alisema na kuongeza:

“Nataka wanipe ‘definition’ (maana) ya kustaafu siasa. Je, ni kunyamaza, nisitoe maoni. Mbona wapo watu walikuwa wanasiasa na bado wanatoa maoni ya kisiasa tena yenye manufaa makubwa?”

Dar Mpya ya Makonda: Makonda Aitaka Takukuru Kuchunguza Madai ya Ufisadi katika Mradi wa Nyumba ‘Avic Town’

$
0
0
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda amenusa ufisadi katika mradi wa ujenzi wa nyumba za Avic ‘Avic Town’ na kuitaka taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), kuuchunguza mradi huo uliopo Kigamboni jijini humo.
makonda-new-jpg-oo

Hatua hiyo imefika baada ya kupata malalamiko kutoka kwa wananchi waliokuwa wakiishi eneo hilo na kutolewa pasipo kupewa fidia zao huku ekari 18 za Chama cha Mapinduzi (CCM),zikichukuliwa kwa matumizi katika mradi huo.

Akizungumzia hatua hiyo, Makonda amewataka watendaji wa serikali wanaohusika na taarifa za mradi huo kutoa taarifa sahihi katika vyombo vya dola kwani hataki kuona wananchi wakidhulumiwa haki zao.

“Sitaki kuona kigogo wala kijiti anahusika katika mradi huo. Nitasimamia na polisi waliohusika katika kuwatoa wananchi hawa waseme walitumia vigezo gani kuwatoa,”alisema.

Alisema wananchi walioondolewa eneo hilo wafike kwa Mkuu wao wa Wilaya huku akiitaka Takukuru kuchunguza mafaili ya mradi huo wa nyumba.

Akizungumza huku akilia mkazi wa eneo hilo ambaye pia ni mwathirika wa mradi huo, Pascalina Walioba alisema tangu mradi utambulishwe na kuanza kujengwa hawajalipwa stahiki zao.

“Mimi ni mwathirika wa mradi huo, tangu unaanzishwa na tukahamishwa kipindi hicho nilipaswa kulipwa Sh 700,000 lakini hadi leo sijalipwa na thamani ya fedha inaongezeka,”alisema na kisha kuangua kilio.

Mbunge wa Jimbo hilo, Faustine Ndungulile alisema kuwa wapo watu walikuwa wakidai kuwa ujenzi ule unahusisha nyumba za ulinzi wa usalama.

“Kuna hekari 18 za Chama cha Mapinduzi (CCM) zipo humo lakini tutalifualia,” alisisitiza Ndungulile.

Katika hatua nyingine Wilaya hiyo imeahidiwa na Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco), hadi kufikia February mwakani watakuwana umeme wa uhakika.

Aidha wananchi wa eneo hilo walitolewa hofu juu ya upatikanaji wa maji safi kwani tayari maji yapo ya visima lakini hakuna mabomba ya kusafirisha maji hayo.

Akizungumzia mradi wa maji katika mji huo, Mwakilishi kutoka Shirika la Maji saifi na Maji taka(Dawasco),….alisema fedha zilizotengwa katika kusambaza maji katika wilaya hiyo ni Sh bilioni 40 huku fedha zinazoitajika ili kukamilisha mradi huo ni Sh bilioni 146.

Bashe Adai Lowassa Alionewa CCM, Aeleza Uhusiano wao Kwa Sasa

$
0
0
Mbunge wa Nzega, Hussein Bashe (CCM) amesema kuwa anaamini waziri mkuu wa zamani, Edward Lowassa aliondolewa kwa kuonewa katika mchakato wa kugombea urais ndani ya CCM.

Bashe amesema kuwa kitendo hicho alichokiita cha kiuonevu ni changamoto kubwa ndani ya CCM na kwamba wengi wameonewa katika michakato ya kuwania nafasi mbalimbali.

“Yaliyomkuta Lowassa yamewakuta wengi ndani ya CCM, hivyo jambo hilo sio geni,” Bashe anakaririwa na Mwananchi. “Wapo waliobaki na wapo walioamua kuhama chama kwa sababu ni binadamu. CCM ina historia hiyo, hii ndiyo changamoto yake kubwa,” aliongeza.

Mbunge huyo alifafanua kuwa kwakuwa Lowassa alituhumiwa kwa mengi ndani ya chama hicho, alipaswa kuitwa na kuelezwa tuhuma zake na sababu za kuondolewa jina lake ili umma ufahamu.

Alisema kuwa katika chama hicho, kashfa nyingi hufanywa kwa sababu maalum na hubuniwa kwa ajili ya kufikia lengo fulani dhidi ya mtu au kikundi cha watu.

Alisema kuwa mbali na sakata la Richmond lililopelekea Lowassa kujiuzulu nafasi ya uwaziri mkuu, masakata ya Lugumi na Tegeta Escrow ni sehemu yale yaliyobuniwa kwa lengo maalum.

“Tazama wanavyofunika sakata la Lugumi. Usiende mbali angalia sakata la Escrow. Tumeadhibu waliopata fedha kutoka benki ya Mkombozi, vipi wa Stanbic? Wizi mwingine uliofanywa nchi hii una uhusiano kati ya Serikali na vikundi vya watu wenye uhusiano na Serikali,” Bashe aliliambia Mwananchi.

Akizungumzia uhusiano wake na Lowassa ambaye alikuwa anamuunga mkono wakati wa mchakato wa kugombea urais kupitia CCM, Bashe alisema hivi sasa hawana uhusiano tena wa urafiki wa kisiasa.

Alisema kuwa alimshauri sana Lowassa kutohama CCM, avumilie, lakini hakufanikiwa kumshawishi, hivyo waliagana.

“Lowassa ni mzee wangu. Ni mtu ambaye namheshimu na nitaendelea kufanya hivyo, ingawa kwa sasa hatuna uhusiano wa kisiasa,” alisema.

Lowassa alihama CCM baada ya jina lake kukatwa katika mchakato wa kuwania urais, alihamia Chadema na kupewa nafasi ya kugombea urais katika uchaguzi unaotajwa kuwa na ushindani mkali zaidi tangu kuanzishwa kwa mfumo wa vyama vingi.

Dimpoz Afunguka Kuhusu Mubenga

$
0
0
Msanii Ommy Dimpoz amekanusha tetesi za kuwa na ugomvi na aliyekuwa ‘business partiner’ ambaye pia alikuwa meneja wake maarufu kwa jina la Mubenga, baada ya kila mmoja kuchukua hamsini zake na kufanya yake.

Akizungumza kwenye FNL ya East Africa Television Ommy Dimpoz amesema Mubenga ameamua kufanya biashara zake mwenyewe bila kushirikiana naye, kitu ambacho ni jambo zuri kwake na kwa maendeleo pia, lakini hawana tofauti na hata akihitaji msaada wake, yupo tayari kumsaidia.

“Mubenga ameenda kuanzisha kitu chake, hiyo ni pongezi na hayo ni maendeleo, mnataka kila siku awe chini ya Ommy! yeye ameenda kuazisha kitu chake, kampuni yake, ana wasanii wake anawasimamia, anajua kwamba afanye vipi anahitaji ku’move on’, kwa hiyo ilikuwa ni movement yake yeye kwamba ameamua kufanya kazi zake mwenyewe which is good, na mimi hata leo akisema Ommy nataka suport hii kwa wasanii wangu i’m ready”, alisema Ommy Dimpoz.

Ommy Dimpoz amesema hata tetesi za kuchukua hela za Mubenga na gari hazina ukweli wowote, ni maneno tu ya uzushi ya mashabiki, na bado anamchukulia kama ndugu yake.

Pichaz: Zari The Boss Lady Afanya ‘Baby Shower’

$
0
0
Siku zinayoyoma na mwezi ujao panapo majaliwa, Zari atajifungua mtoto wake wa pili na Diamond. Huyo atakuwa mtoto wake wa tano kwa ujumla.

Katika kujiandaa na mapokezi ya mtoto huyo, staa huyo wa Uganda amefanya baby shower nchini Afrika Kusini na kuwashirikisha marafiki zake na watu wa karibu.

Kajala Masanja: Afunguka Kuhusu Msamy Baby, Makonda na Mme Wake Faraji

$
0
0
STAA wa Bongo anayetesa kwenye filamu, Kajala Masanja amevunja ukimya na kufunguka kuhusu maneno yanayozagaa mitaani yakimtaja kuwa kwenye uhusiano wa kimapenzi kwa nyakati tofauti na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda na mwanamuziki wa Bongo Fleva, Msamy Baby.

Kwa muda mrefu sasa, minong’ono hiyo imekuwa ikizagaa kwenye mitandao mbalimbali ya kijamii tangu wakati Makonda akiwa Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni katika Serikali iliyopita ya Dk. Jakaya Kikwete.

Tetesi za uhusiano wake na RC Makonda, zilianza wakati Makonda (alipokuwa DC wa Kinondoni) akishirikiana na msanii huyo kwenye shindano la kusaka vipaji vya wasanii wa Wilaya ya Kinondoni lililojulikana kama Kinondoni Star Search.

Katika mahojiano na Polisi wa Swaggaz, Kajala alipoulizwa kuhusu madai ya kuwa na uhusiano na Makonda, alijibu kwa kifu sana: “Hapana sijawahi kutoka naye kabisa. Hilo halipo.”

Awali, RC Makonda aliwahi kuzungumzia madai hayo akiwa bado Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, ambapo alisema wabaya wake wa kisiasa wamekuwa wakisaka mbinu za kumchafua kila kukicha.

Makonda, alikwenda mbali zaidi akisema kuwa, propaganda ya kumchafua ilianza tangu wakati wa Bunge Maalum la Katiba, alipokwenda Bungeni na msanii mwingine wa filamu, Yobnesh Yusuf ‘Batuli’, akazushiwa kuwa alitoka naye.

Katika maelezo ya Makonda, alisema anawashangaa wengi wanavyomhusisha kuwa na uhusiano usiofaa na Kajala kwa vile ameshirikiana naye kwenye project hiyo ya kusaka vipaji wakati pia ameshirikiana na wasanii wengi wa kiume.

Kwa Kajala inakuwa mara ya kwanza kuzungumzia hilo katika mahojiano maalum na mwandishi wa Swaggaz.

Kuhusu msanii wa Bongo Fleva, Msami Baby Kajala alisema: “Hata huyo sijawahi kutembea naye, lakini nakiri kwamba ni rafiki yangu wa karibu kama msanii mwenzangu ila hatujawahi kuwa wapenzi hata siku moja.”

SWAGGAZ: Vipi kuhusu picha zilizozagaa kwenye mitandao ya kijamii zikiwaonesha wewe na Msami mkiwa sehemu mbalimbali za starehe?

KAJALA: Kwahiyo nikipiga picha na msanii basi natoka naye?  Mtu unaweza kujisikia kupiga picha na yeyote kwa ajili ya kurusha Insta, kwahiyo ukifanya hivyo tu basi tayari unatoka naye?

Mfano leo (juzi Jumatano) nimepiga picha na Petty Man, kwahiyo nikiweka Insta basi itakuwa Kajala anatoka na Petty. Siyo jambo zuri, nadhani wangekuwa na uhakika kwanza, mimi sijawahi kutembea na Msami.

SWAGGAZ: Ok! Vipi kuhusu uhusiano wako na mzazi mwenzako P Funk kwa sasa?

KAJALA: Kawaida tu! Yeye ana maisha yake na mimi nina yangu, ameoa na mimi niko kivyangu.

SWAGGAZ: Umezungumzia upande wako, vipi kuhusu mwanenu Paula, anawasiliana na baba’ake?

KAJALA: Hapana na hiyo ni kwa sababu mtoto niko naye mimi.

SWAGGAZ: Kwahiyo tangu uachane na P Funk, mtoto hajawahi kwenda kumuona baba yake?

KAJALA: Aliwahi kwenda kipindi fulani na aliishi naye wakati huo, lakini nilipomchukua na kuishi naye hawajawahi kuonana naye tena.

SWAGGAZ: Labda P Funk amewahi kutaka kuonana na mwanaye?

KAJALA: Hapana… nadhani ni kwa kuwa ana watoto wengine anaona wanamtosha huyu hana haja naye. Lakini nisingependa kuendelea kuongelea hayo mambo tena.

SWAGGAZ: Vipi uhusiano wako na mumeo Faraji aliyeko gerezani? Je, huwa unakwenda kumtembelea?

KAJALA: Nilikuwa nakwenda kumwangalia lakini kwa sasa nisiwe muongo, nina muda kidogo kutokana na kazi za hapa na pale, nimejikuta sijaenda kumuona lakini mwanzo nilikuwa nakwenda kila Jumamosi na Jumapili.

SWAGGAZ: Mara ya mwisho kwenda ilikuwa lini?

KAJALA: Mwezi mmoja umepita sasa.

SWAGGAZ: Vipi mipango yako ya kiuhusiano? Maana mumeo yupo jela. Utamsubiri atoke muendelee na uhusiano wenu au unatarajia kuingia kwenye ndoa mpya? Nimekuuliza hili kwa sababu hivi karibuni ulisema unatamani kupata mtoto wa kiume.

KAJALA: Hiyo siwezi kuongelea in public (hadharani) kwa sababu ni maisha yangu binafsi.

SWAGGAZ: Ahsante sana kwa ushirikiano wako.

KAJALA: Nawe pia karibu tena.

Mtanzania

Wasafi Kumleta Amber Rose Dar Mwezi ujao?

$
0
0
Wasanii wote wa label hiyo wakiongozwa na Diamond watatumbuiza. Lakini huenda kukawa na ugeni mkubwa wa staa wa nje na tayari meneja wa Diamond, Sallam ametease jina.

Akiweka picha ya mrembo wa Marekani, Amber Rose, Sallam ameandika kwenye Instagram, “Wangapi watu wanataka huyu dada ashuke bongo siku akinukishe watu wale nae Bata???”

Naye Diamond alichombeza kwenye post yake: Eti Manager @sallam_sk anauliza wangapi wangependa huyu dada @amberrose siku ashuke Bongo watu wale nae Bata???”

Huenda label hiyo ikawa imepanga kumleta mrembo huyo kuwa host wa tamasha lenyewe.

Hiyo haitakuwa mara ya kwanza kwa ex huyo wa Wiz Khalifa kuja Afrika. Mwaka jana alienda Lagos, Nigeria kwa mwaliko wa D’Banj ambako hata hivyo alikaa jukwaani kwa dakika 7 tu.

Madhara ya Chai na Kahawa Kiafya

$
0
0
Kafeina ni nini?:

1. Kafeina ni madawa ya kulevya kundi la ‘Stimulants drugs’.
Utashangaa. Habari ndiyo hiyo. Hii ndiyo sababu kwa mtu aliyezoea kunywa chai hii kila siku au kahawa, siku asipokunywa kichwa humuuma, ni kwa sababu amekuwa mtegemezi au teja wa kafeina.

Kafeina ni kiungo mhimu karibu katika soda zote zenye rangi nyeusi; Coca-cola, Pepsi, Sayona nyeusi, Azam cola na kadharika. Kafeina huongezwa pia katika Red bull, Malta na katika baadhi ya dawa za kupunguza maumivu mwilini.

Kwahiyo Kafeina ambayo hupatikana katika chai na kahawa ni aina mojawapo ya madawa ya kulevya.

2. Kafeina ni kikojoshi (diuretics).
Kafeina ni dawa ya kukufanya ukojowe. Ukinywa kikombe kimoja cha kinywaji chenye kafeina yaani chai au kahawa, basi muda si mrefu utaenda kukojoa vikombe viwili. Kwa sababu kafeina ni taka isiyotakiwa mwilini, mwili utafanya kila uwezalo ikibidi ujikamuwe wenyewe kupata maji ya ziada kuweza kuitoa kafeina hii uliyoinywa kwa kisingizio cha chai, kahawa au soda.

Madhara yake ni nini?, Moja; kama unakunywa kinywaji na muda si mrefu unalazimika kwenda kukitoa inamaanisha kinywaji hicho hakikutumika vema na mwili. Pili; kumbuka ulikunywa kikombe kimoja na umeenda kutoa viwili, hivyo umekopwa maji mwilini mwako na ukumbuke kuwa MAJI NI UHAI.

3. Kafeina husababisha KANSA.
Seli ndani ya mwili lazima zibaki katika kiasi kidogo cha alkalini kutoka 7.2 mpaka 7.4, wakati 7.0 ni ya kati au husemwa sifuri katika kipimo cha PH (potential hydrogen). Chini ya 7.0 ni asidi na juu ya 7.0 ni alkalini. Kafeina yenyewe ni asidi, hivyo ikiwa mtu anafanya chai au kahawa ndivyo vinywaji vyake vya kila siku basi mtu huyo lazima atakuja kupatwa na kansa katika siku za usoni kwakuwa seli za kansa huishi katika hali ya uasidi pekee na kafeina ndimo mazingira mazuri ya kuishi asidi.

Jarida moja la afya la Uingereza, ‘The British Medical Journal Lancet’, limeripoti uhusiano mkubwa uliopo baina ya utumiaji wa kahawa na kansa ya kibofu cha mkojo na kupungua kwa uzarishwaji wa mkojo.

4. Kaffeina huchangia upotevu wa madini na vitamin mhimu mwilini.
Kafeina ambayo ni kikojoshi, huyalazimisha maji kukimbia nje ya mwili kwa haraka na kuziacha seli bila muda wa kutosha kuyatumia maji hayo, maji yanapokimbia kwa haraka nje ya mwili huyakimbiza pia madini mhimu nje ya miili yetu.

5. Kaffeina husababisha kisukari.
Mwili una vyanzo 3 vya nguvu ambavyo ni Sukari, Mafuta, na Maji/Chumvi. Tumesema kaffeina ni kikojoshi, hivyo kaffeina hupelekea upotevu usio wa lazima wa maji mwilini, mwili unapokosa maji kama chanzo chake cha nguvu, moja kwa moja huhamia kuitegemea sukari kama chanzo chake cha nguvu na mwishowe kisukari lazima kitokee.

6. Uchovu sugu.
Wapenzi wengi wa chai ya rangi na kahawa mara nyingi wanapojisikia uchovu hukimbilia kikombe cha kahawa au chai. Kaffeina iliyomo katika chai au kahawa huenda kuiamsha na kuitumia nguvu iliyokuwa imehifadhiwa na mwili kwa ajili ya matendo ya dharura na kukuacha wewe ukiwa huna nguvu ya ziada kwa ajili ya kazi za dharura, matokeo yake ni mwili unakuwa upo katika hali ya msukosuko muda wote.

Utolewaji wa sukari iliyokuwa imehifadhiwa, kunapelekea mfadhaiko mkubwa kwenye mfumo wa dharura wa mwili. Unaposhitushwa kidogo tu, unakuwa na nguvu za haraka (Unahamaki) kushughurika na tatizo. Hali hii hatimaye inaweza kupelekea kukauka kwa tezi ya adreno kutakakosababisha damu chache yenye sukari (hypoglycemia), udhaifu, na kuumwa sana iwapo sukari haitachukuliwa mapema kupandisha juu damu sukari.

Kwa sababu ya biashara kuunda vyakula vyetu vyote maalumu na vinywaji vyenye radha mpya, radha nzuri na nguvu ya kutosha kwa kutumia kafeina toka katika mimea na mitishamba kama vile ginseng kuisisimua tezi ya adreno, kunasababisha Ini kutoa sukari iliyokuwa imehifadhiwa mwilini kwa ajili ya matumizi yake ya dharura.

Hakuna nguvu iliyomo kwenye kafeina au ginseng. Kuna majina mengine mengi ya visisimuwaji hivi kama vile, kokwa za guru, kokwa za cola na mfalme wa yote ni guarana. Mbegu za guarana zina kiasi cha kafeina mara tatu zaidi ya zile za kahawa, na hawatakiwi kuliorodhesha neno kafeina kwenye vifungashio (packages) au kontena.

Ungaunga wa guarana hutumika kutengenezea vidonge vya kupunguza uzito kwa sababu kafeina itazisambaratisha hisia za njaa, lakini hakuna mahala neno kafeina linaonekana kwenye vifungashio vya dawa hizi.

Kuna mimea, kokwa na kemikali nyingi ambazo zitaisisimua tezi ya adreno na kusababisha ini kuitoa sukari iliyokuwa imehifadhiwa au hata kuitengeneza toka tishu za mwili wenyewe ‘(gluconeogenesis)’.

Imethibitika pia kuwa kafeina imekuwa ikiingilia na kuathiri unakilishaji wa kinasaba (DNA), namna ambavyo seli mpya hutengenezwa. Kafeina inaweza kusababisha upotevu toka mwilini wa vitamini nyingi za kundi B, kundi C, zinki, potasiamu na madini mengine. Kahawa huongeza hali ya uasidi kwenye utumbo mdogo.

Kafeina inaweza kusababisha msukosuko ndani ya mwili.
Kafeina siyo kwamba tu huimaliza nguvu iliyokuwa imehifadhiwa kwenye ubongo, bali pia huzuia mfumo vimeng’enya katika kutengeneza kumbukumbu kwenye ubongo.

Kituo cha Sayansi kwa maslahi ya umma (Center for Science in Public Interest) kimewashauri kinamama wajawazito kukaa mbali na kafeina kwa kuwa tafiti zimeonesha kwamba kiasi cha kafeina kilichomo kwenye vikombe 4 vya kahawa kwa siku kinaweza kusababisha matatizo wakati wa kujifungua kama yalivyoonwa katika majaribio kwa wanyama.

‘Madawa na wewe’, kwa mjibu wa Dr. Earl Mindell, mwandishi wa kitabu; ‘Earl Mindell’s New Vitamin Bible’ (zaidi ya nakala milioni 10 zimeuzwa), anasema katika ukurasa wa 414 wa kitabu hicho kuwa ‘kafeina ni dawa yenye nguvu kubwa, uwezekano ni kuwa, hauifurahii tu kahawa au cola yako ya kila siku, bali umekuwa mtegemezi au teja (addicted) wa hiyo kafeina’.

Madhara ya chai ya rangi na kahawa mwilini ni mengi sana na tatizo moja litapelekea lingine na orodha inakuwa haiishi.

Namna ya kuepuka kaffeina kwenye kahawa na chai:
Badala ya kutumia majani hayo ya chai meusi, wewe chemsha maji yako ya chai kama kawaida na unaweza kutumia vifuatavyo kukamilisha chai yako; unaweza kutumia tangawizi na kumbuka pia tangawizi ni dawa ya zaidi ya magonjwa 72 mwilini.

Kwahiyo unapoinywa chai ya tangawizi siyo tu unaepuka madhara ya kaffeina peke yake, bali pia unakuwa umekunywa dawa ya zaidi ya magonjwa 72 mwilini!. Unaweza pia kuweka mdalasini, mchaichai, kukamulia ndimu, pia unaweza kutumia mchanganyiko wa viungo vingi vya chai (spiced tea) ambavyo vinapatikana kwa wingi katika soko la Kariakoo Dar – Es – Salaam na Zanzibar.

Kajala: Sijawahi Kuwa na Mahusiano ya Kimapenzi na Paul Makonda

$
0
0
Msanii wa filamu za kibongo, Kajala Masanja amevunja ukimya na kufunguka kuhusu maneno yaliyokuwa yanazunguka mwa muda mrefu mitaani yakimtaja kuwa kwenye uhusiano wa kimapenzi kwa nyakati tofauti na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda tangu akiwa DC wa kinondoni alipokuwa akishirikiana kwa karibu na msanii huyo kwenye shindano la kusaka vipaji vya wasanii wa Wilaya ya Kinondoni lililojulikana kama Kinondoni Star Search.

Katika mahojiano na mwandishi wa habari hizi, Kajala alipoulizwa kuhusu madai ya kuwa na uhusiano na Makonda, alijibu kwa haraka na kwa kifupi: “Hapana sijawahi kutoka naye kabisa. Hilo halipo.”

RC Makonda aliwahi kuzungumzia madai hayo akiwa bado Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, ambapo alisema ni propaganda zinazoelezwa na wabaya wake wa kisiasa ambao wamekuwa wakisaka mbinu za kumchafua kila kukicha.

“Ni muda mrefu tu, walianza kipindi kile wakati wa Bunge la Katiba nilipokwenda Bungeni na mwigizaji Yobnesh Yusuf ‘Batuli’, wakasema natembea naye, wakanyamaza. Sasa wamehamia kwa Kajala baada ya kufanya naye kazi", alisema Makonda.

“Hakuna ukweli wowote wanatungatunga tu mambo, watakuwa na sababu zao kwa sababu mtu kama Kajala, maneno yameibuka baada ya kufanya naye project ya kutafuta vipaji vya wasanii.“

"Nimeshirikiana na wasanii wengi wa kiume katika project hiyo lakini kwa kuwa wameona mwanamke ni Kajala peke yake, wanasema vitu ambavyo havina kichwa wala miguu. Najua kuna wengine wanaoeneza haya mambo wanatumika kisiasa lakini mimi sijali".

Picha: Lady Jaydee Amefunga Ndoa na Rasta Huyu?

$
0
0
Huenda Lady Jaydee akawa amepata mwanaume wa kumkabidhi moyo wake. Tangu aachane na mume wake, Gardiner G Habash, muimbaji huyo mkongwe hajawahi kuonekana na mwanaume aliyehisiwa kuwa ni mpenzi wake. Na sasa kwa picha alizoweka Instagram, uwezekano wa kuwa amerejea kupenda tena ukawa ni mkubwa.

Na tena kwa anachokiandika mwenyewe kwenye Instagram, Jide anamaanisha kuwa amefunga ndoa tayari! “Big shout out kwa Coastal air
Kwa kufanikisha safari yangu kwenda honeymoon #ZanzibarIsland,” ameandika Jide kwenye picha akiwa amesimama pembeni ya ndege waliyokodi na mwanaume huyo ambaye ni mgeni machoni pa wengi.

Kwenye picha nyingine hiyo juu, Jide ameandika: Thank you Serena Hotel for the amazing dinner 🙏 we really enjoyed #ZanzibarIsland.”

Pia rafiki yake wa siku nyingi, Monica Joseph ameweka picha za wawili hao na kuandika: My BFF is better than yours .. looking Good My People .. Love Lives here.”

Ni kweli Jide amefunga ndoa? Majibu yatapatikana punde!

VIDEO: “Ushindani wa Diamond na Alikiba Uendelee”- Bien wa Sauti Sol

$
0
0
Baada ya kundi kutokea nchini Kenya , Sauti Sol kutua Tanzania mkoani Arusha kwaajili ya show itakayofanyika leo Nov 19 2016 Millardayo.com na AyoTv imeweza kuwapata katika interview na katika maswali waliyoulizwa moja wapo ilikuwa inayosemekana ni beef kati ya Diamond Platnumz na Alikiba.

Member wa Crew hiyo Bien Sol amejibu hivi.
’Iyo ni biashara na hata sisi Sauti Sol wengine ni mashabiki wa Diamond na wengine wa Alikiba tumefanya nyimbo na Kiba labda wengi hawakufurahi so tutafanya ngoma na Diamond pia iyo bif iendelee cause inacreate job, news, so me naona vyema iyo bif iendelee kwa mtandao tu ni sawa kwasababu kwenye muziki pia kunahitajika ushindani’ – Bien

Taarifa:Rais Mstaafu Jakaya Kikwete na Ujumbe Wake Hawakuzuiwa Kusafiri Uwanja wa Ndege Dar es Salaam

$
0
0
Jana Asubuhi iliandikwa Habari iliyokuwa imechapishwa kwenye gazeti la Tanzania la kila siku ‘Mtanzania’ ambapo kichwa cha habari cha taarifa hiyo kilikuwa kikisomeka ‘Rais Mstaafu, Jakaya Kikwete azuiwa kusafiri nje ya nchi uwanja wa ndege Dar es Salaam.’

Katika habari hiyo, gazeti hilo liliandika kuwa kutokana na taarifa lililozipokea ni kuwa Rais Mstaafu Dkt Jakaya Kikwete na ujumbe waka jana walishindwa kusafiri kwa ndege ya Shirika la Ndege la Emirates kwenda Abudhabi kupitia Dubai baada ya mmoja wa wajumbe aliokuwa ameambatana nao kutokuwa na viza ya kusafiria wakati wa ukaguzi.

Aidha, taarifa hiyo iliendelea kueleza kuwa hata baada ya mjumbe huyo kupata viza yake nusu saa kabla ya safari kuanza, walishindwa kuendelea kwani zoezi la ukaguzi wa abiria wanaosafiri na ndege hiyo lilikuwa limekwisha fungwa na ndege ikaondoka.

Kutokana na hali hiyo, gazeti hilo lilieleza kuwa Rais Mstaafu Dkt Jakaya Kikwete aliyekuwa ameambatana na mkewe pamoja na wajumbe wengine wangesafiri leo baada ya kukamilisha taratibu zote za safari.

Kwa taarifa za uhakika ambazo Swahili Times imethibitisha ni kwamba Rais Mstaafu Dkt Jakaya Kikwete na ujumbe wake hawakuzuiwa katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) na waliendelea na safari na ratiba yao kama kawaida bila ucheleweshwaji wowote.

Hii hapa chini ni picha ya Rais Mstaafu Dkt Kikwete akiwa katika banda la maonyesho la UNICEF Dubai leo asubuhi.

Bibi Mbaroni Kwa Kumlisha Kinyesi Mjukuu Wake

$
0
0
MWANZA: BIBI mmoja aliyejulikana kwa jina la Amina Hamisi (56) mkazi wa Mtaa wa Mahina, Kata ya Butimba, Jijini Mwanza, anashikiliwa na Jeshi la Polisi mkoani humo baada ya kumlazimisha mjukuu wake Rehema Sadiki (7) kula kinyesi.

Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Kamishina Msaidizi wa Polisi Augustino Senga amedai kuwa tukio hilo limetokea Novemba 11, mwaka huu ambapo mtoto huyo alikwenda chooni kujisaidia na kushindwa kumwagia maji ili kuondoa kinyesi chake ndipo bibi yake ili kumuadhibu alimuamuru kula kinyesi hicho kitendo ambacho mtoto huyo alikitekeleza.

Baada ya tukio hilo kutokea raia wema walitoa taarifa polisi ambao walifika eneo la tukio na kufanikiwa kumkamata mtuhumiwa huyo.

Kamanda Senga ametoa wito kwa wakazi wa jiii la Mwanza kutoa ushirikiano kwa jeshi la polisi ili kudhibiti vitendo vya kikatili hasa kwa watoto wadogo na kuongeza kuwa ukatili ni kosa kisheria hivyo wananchi waache kufanya vitendo hivyo na watakao bainika sheria itachukua mkondo wake.

Moses Machali Aamua Kurejea CCM. Adai CCM ya Magufuli si CCM ya zamani!

$
0
0
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI NA WATANZANIA WOTE. ​

Kutoka mezani kwangu Moses Joseph Machali, Tarehe: 21/11/2016

Napenda kuutaarifu umma wa Watanzania kupitia kwenu waandishi wa habari kwamba ni jambo la ajabu na aibu kwa watu makini na wenye kuhitaji mabadiliko ya kweli Kuacha kuunga Mkono juhudi zinazofanywa na serikali ya awamu ya tano chini Uongozi wa Rais Dr. John Pombe Joseph Magufuli bila kusahau utendaji makini wa Waziri Mkuu wake Mhe. Majaliwa Kasim Majaliwa (Mb) pamoja na mawaziri mbalimbali wameonesha kutaka kufuata mwenendo wa Rais Magufuli na Waziri Mkuu wake.

Mimi Moses Joseph Machali niliyefanya sana siasa za Upinzani hapa nchini na niliyepiga kelele na kupinga siasa za kifisadi zilizoitawala nchi hii; niliyepinga pia ufisadi uliokuwa umeitawala serikali huko nyuma kwa nguvu na uwezo wangu wote nikishirikiana na wapinzani wenzangu, ninaamua kujiunga na watu wanaonesha dhamira safi ya kuiendeleza nchi yetu Tanzania. Watu wenye mwelekeo na dhamira ya kuijenga nchi yetu kwa maendeleo enedelevu ni jamii ya akina Magufuli, Kasim Majaliwa, nk.

Mwaka mmoja wa Uongozi wa Rais Magufuli na baadhi ya wasaidizi wake kupitia hatua mbalimbali zilizochukuliwa dhidi ya ufisadi uliokuwa umeigubika nchi yetu, inatosha kabisa kwa mtu yeyote makini kufanya uamuzi wa kumuunga mkono au kutokumuunga mkono Rais Magufuli.

Mimi nimechagua kumuunga Mkono Rais kwa vitendo, kwa sababu ninaposoma Rekodi yangu ya enzi nikiwa Mbunge (Hansard) na kabla ya kuwa mbunge ni kwamba nilipinga mnoo wizi na ufisadi wa kila aina; Nilipinga Matumizi ya fedha serikalini yasiyo ya lazima na yasiyo na tija kwa taifa (Rejeeni hotuba yangu ya Bajeti ya Wizara ya Uchukuzi, nikiwa Waziri Kivuli wa wizara hiyo ya mwaka 2014/2015 na 2015/2016), vilevile bila kusahau hotuba zangu mbalimbali Bungeni na nje ya Bunge.

Kwa kushirikiana na wapinzania wenzangu enzi hizo tulishauri na kupinga ufisadi wa kila aina, tuliitaka serikali kufanya mambo yenye tija kwa taifa na sasa kila mwenye macho anaona hatua zinazochukuliwa na serikali ya awamu ya tano. Miradi kama ya Ujenzi wa Reli, Ununuzi wa ndege mbili na mipango ya kununua ndege zaidi kama namna ya kulifufua shirikia la ATCL ni mambo tuliyoyahitaji kuyaona wapinzani; sasa yanafanyika. Wale wenye dhamira ya dhati ya kuona nchi yetu ikipiga hatua, kamwe hatuwezi kubeza mambo hayo bali kuyaunga mkono.

Wale tuliosema na kupiga kelele kwamba Serikali ni dhaifu ktk kuwachukulia hatua watu mbalimbali wenye dhamana serikalini walioonekana kufanya vibaya serikalini ktk nafasi zao, leo tunaona kumekuwepo na kasi nzuri ktk kuwachukulia hatua watu hao. Hata hivyo leo hii upinzani umepiteza mwelekeo kwa sababu unapingana na kile ulichokihubiri nchini.

Agenda ya kupinga ufisadi siyo ya upinzani tena bali ya JPM na CCM yake au yao. Wapinzani wamegeuka kuwa watu wanaokataa yale waliyoyasimamia na kuyahubiri huko nyuma. Hakika huo siyo uungwana bali aina mpya ya ufisadi nchini na usaliti kwa agenda zao.

Kama kweli sisi tumeokuwa wapinzani na tulioonesha kupinga kwa nguvu zote ufisadi ulioiumiza nchi hii tulimaanisha yale tuliyoyahubiri na kuwaaminisha watu basi tunao wajibu wa kuacha tabia ya kuwa vigeugeu kwa mambo tuliyoyaamini na kuyahubiri. Kutofanya hivyo basi ni mwendelezo wa ufisadi kwa maslahi binafsi.

Ni nani asiyeona kwamba serikali ya awamu ya tano inafanyia kazi mambo mengi tuliyoyapigia kelele? Au tunajifanya kutokukubali ukweli unaoishi kwa ule msingi wa upinzani wa Tanzania kwamba Tukimuunga mkono Mtawala kamwe hatutapata kuaminiwa na wapiga kura nchini na hivyo tupinge tu hata kama ni ukweli? Nadhani kinachofanyika ni mwendelezo wa kupinga hata mazuri ili kutafuta fursa ya wapinzani kukubalika kisiasa zaidi hata kwa njia na mbinu haramu kama kawaida ya siasa zilizo zoeleka hapa nchini kwa miaka mingi.

Taifa hili haliwezi kuendelea kwa kuwa na siasa za kutokukubaliana na ukweli unaoishi. Kama dhamira ya kila mtanzania ikiwemo wapinzani ni kuona nchi ina move basi hatuhitaji kuwa watu wa kupingapinga hata yaliyo mema bali kuyaunga mkono yale yaliyo mema bila kujali yanafanywa na nani bali msingi mzuri unapaswa kuwa ukweli kwa kila jambo.

Serikali ya awamu ya tano imeonesha njia ktk mambo mengi na inastahili kuungwa mkono. Safari ni hatua na ninaamini kwamba hata yale yanayoonekana kutokufanyiwa kazi ndani ya mwaka mmoja uliopita na ambayo yalishindikana huko nyuma, bado yanaweza kuja kufanyiwa kazi huko mbeleni. Serikali ya JPM imejitahidi sana tukilinganisha na huko tuliko toka. Uongozi huu unafanana sana na ule wa akina Hayati EDAWARD MORINGE SOKOINE chini ya hayati Baba wa Taifa Mwl Julius Kambarage Nyerere.

Daima ninaamini ktk yale ninayoyaamini pasipo kufungwa na ukada bali kuangalia ukweli ni upi. Hata kelele wanazopiga baadhi ya watu kwamba maisha yamekuwa magumu kwa sababu ya Magufuli ni propaganda tu kwa sababu hakuna uhusiano wa maisha magumu na suala la KUDHIBITI wapiga dili wa fedha na mali za umma bali tukubali kwamba wapiga dili waliozoea kupiga dili na kuziingiza fedha walizopiga ktk mzunguko kwamba siyo jambo la msingi ktk kujenga uchumi imara.

Uchumi imara hauwezi kujengwa kwa kuruhusu ubadhirifu wa fedha na mali za umma au hata za mtu mmoja mmoja. Kinachoonekana hivi sasa ni kama nchi inasukwa upya na hivyo tuwaunge mkono viongozi wa serikali ya awamu ya tano kwa mema wanayoyafanya na kuwashauri kurekebisha ktk yale ambayo hayajakaa vizuri. Tuachane na siasa nyepesi za kutaka kuona kwamba mazuri ni yale yanayofanywa na wapinzani huku mambo hayohayo yakifanywa na CCM yaonekane hayafai na kutajwa kuwa ni ya hovyo. CCM ya JPM siyo ile ya 2015 kurudi nyuma kidogo. Hii ni tofauti na ninaiunga mkono.

Hivyo basi leo Tarehe 21/11/2016 ninatangaza rasmi kwamba ninajiunga na timu JPM kwa maslahi ya taifa kwa kuwa sioni sababu ya kupingana na yale niliyoyapigania na itakuwa ni sawa na mtu kupigana na kivuli chake mwenyewe. Kwaherini Upinzani nimeamua kuanza siasa mpya za masuala yale niliyoyaamini na ninayoyaamini. Imani ni Matendo Na Matendo ni imani. Piga vita ufisadi kwa imani na Matendo.

Moses Joseph Machali 
X-mbunge, Kasulu Mjini 2010-2015,

Mwana FA Aleta Msiba Mkubwa Kwa Kina Dada wa Mjini Kwa Huu Wimbo Wake Mpya...Dume Suruali ft. Vanessa Mdee

$
0
0
Leo Mwana Fa ameachia ngoma yake ambayo ni mwiba mchungu kwa kina dada wa mjini wanaopenda na kuishi kwa kuombaomba. Ngoma inaitwa Dume Suruali.

Nihonge nanunua nini? Kwa nini yani? Kwa kipi nsichokijua ina TV ndani?

Asante FA kwa hii fimbo ya kufungia mwaka haswa kipindi hiki cha Magufuli #TeamDumeSuruali

Dume Suruali ft. Vanessa Mdee - Mwana FA

Usikilize Hapa chini:

Chemical: Kwanini Watu Wanashindwa Kuamini Kuwa Mimi ni Bikira?

$
0
0
Rapper wa kike mwenye swaga za hatari Chemical amesema anashangazwa kwa kitendo cha baadhi ya watu wanaompinga kuwa hajawahi kufanya mapenzi.

Hitmaker huyo wa ‘Am Sorry Mama’ amekiambia kipindi cha Kubamba cha Times FM, kuwa aliwahi kuwa na mpenzi lakini waliachana kwa kuwa alikuwa na haraka ya kufanya mapenzi.

“Sijawahi kufanya mapenzi hata siku moja. nimeachana na mpenzi wangu kwa sababu hataki kusubiri, nipo single sasa hivi. Sijui watu kwanini hawaamini wanahisi ni kitu ambacho hakiwezekani aisee,” amesema Chemical.

Kwa sasa rapper huyo anafanya vizuri na wimbo wake wa ‘Mary Mary’ aliouachia siku chache zilizopita.

Tunaheshimu Maamuzi ya Moses Machali Kuhamia CCM- Ole Sendeka

$
0
0
Baada ya kutolewa taarifa ya aliyekuwa Mbunge wa zamani wa Kasulu Mjini, Moses Machali  kuhusu kuunga mkono serikali ya awamu ya tano hivyo na kujiunga na Chama cha Mapinduzi, Msemaji wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Ole Sendeka amezungumzia uamuzi huo.

Haya ndio machache aliyoyatoa Msemaji wa Chama cha Mapinduzi baada Machali kuhamia CCM akitokea chama cha ACT.

“Sisi kama chama cha mapinduzi tunaheshimu uamuzi wake na hatua ya pili kumpokea kwenye chama katiba za kikanuni zitafuatwa na hasa ukizingatia mimi namfahamu ni mtu mwenye msimamo, kwahiyo naheshimu maamuzi yake na hatua zingine zitafuata kwa mujibu wa katiba na kanuni zetu za chama kuwapokea wananchama wanaoingia katika chama chetu kutoka upande wa vyama vingine,”amesema Sendeka.

Taarifa ya aliyekuwa mbunge wa Kasulu Mjini imetolewa na kiongozi huyo yeye mwenyewe.
Viewing all 104687 articles
Browse latest View live


Latest Images