Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104417 articles
Browse latest View live

Shirikisho la Wanafunzi wa Elimu ya Juu (Tahliso) Watoa Tamko Kali Kwa Bodi ya Mikopo

0
0

Dar es Salaam. Shirikisho la Wanafunzi wa Elimu ya Juu (Tahliso) imevikumbusha vyuo vikuu nchini mambo wanayotakiwa kufanya ikiwamo kuelewa mikataba na nafasi ya wanafunzi katika masuala ya malipo ya ada vyuoni mwao.

Katika waraka wake uliotolewa kwa vyombo vya habari, Tahliso walilaani vikali kitendo cha Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustino kutangaza kuwazuia wanafunzi kufanya mahafali kwa kisingizio cha ada.

“Tahliso tumepokea malalamiko yenye kusikitisha kutoka kwa wanafunzi wanufaika wa mikopo ya elimu ya juu wa Chuo Kikuu cha Mtakatifu Agustino (SAUT) - MWANZA ambao wamehitimu katika mwaka wa masomo 2015/2016” amesema  Stanslaus Kadugalize, Mwenyekiti wa Tahliso

Waraka huo umesema Mkataba wa malipo ya ada ni kati ya vyuo hivyo na HESLB na kuwa zipo taratibu zinazotumika kulipana ada hizo kati ya vyuo na Serikali kupitia HESLB;

“Wanafunzi hawajawahi kushiriki katika kupanga ada hizo, kufuatilia malipo ya ada hizo wala kutafuta fedha za kulipa ada hizo.” umesema waraka huo na kuongeza:

“Kwa sababu hizo, TAHLISO tunapinga vikali hatua hiyo iliyochukuliwa na uongozi wa Chuo Kikuu cha Mtakatifu Agustino na kuwataka wakuu wa taasisi za elimu ya juu nchini kutozuia wanafunzi kuhitimu masomo yao.”


Katika waraka huo Tahliso ilizitaka taasisi za elimu ya juu ambazo zinadai ada kutoka HESLB, kufuata utaratibu uliopo ambao umezoeleka wa kuidai HESLB na sio kuwaadhibu wanafunzi wahitimu.

Wema Sepetu Ampongeza Ommy Dimpoz

0
0

Baada ya hapo jana Ommy Dimpoz kufunguka kiundani kwenye kipindi cha XXL cha Clouds FM kwa kuelezea kilichopelekea akosane na rafiki yake wa zamani, Diamond Platnumz – Wema Sepetu amempongeza kwa kile alichokifanya.

Malkia huyo wa filamu nchini, amempongeza hitmaker huyo wa Kajiandae kwa kumsifia kuwa ni mpole na mwenye busara ila alipenda kile alichokifanya kwenye mahojiano yake hayo.

Kupitia mtandao wa Instagram, Wema ameandika.

Busara, Upole, Hekma… Thats wat u r made of… Im very very Proud and Impressed kwakweli… Mnyonge mnyongeni haki yaki mpeni… Sasa sio mje muanze kusema sijui napick sides… Nooooo…!!! Sina side maana na mimi pia ni outsider tu… But kwa leo nimependa ulichofanya Ommy…. Forever Bae… 👌🏽Sometimes being the bigger person doesnt hurt… @ommydimpoz

Darassa Ajigamba Adai Muziki Wake Hauwezi Kuchuja

0
0

Rapper Darassa amedai kuwa muziki anaofanya ni wa kuishi milele ndio maana nyimbo zake haziwezi kuchuja.

Akiongea na Times FM, Darassa amesema, “Natengeneza muziki wa kuishi milele, ndio maana ‘Utanipenda’ na ‘Too Much’ hazichuji.”

Kwa sasa Darassa ni mmoja kati ya rapper wa kizazi kipya ambao wanafanya vizuri huku wimbo wake aliouachia siku chache zilizopita ‘Muziki’ aliomshirikisha Ben Pol ukionekana kufanya vizuri kwenye vituo mbalimbali vya redio na runinga.

RUGE "Tulisha Maliza Bifu na Lady Jay Dee, Tunasubiri Ruksa ya Kucheza Nyimbo Zake tu....

0
0
Ruge Mutahaba amesema siku Lady Jaydee akiwaambia waanze kucheza nyimbo zake watafanya hivyo.

Bosi huyo wa Clouds Media Group, ametoa kauli hiyo Ijumaa hii kwenye mahojiano na kipindi cha XXL cha kituo hicho. “Tatizo ni kwamba hakuna ambacho hatujamaliza, tulimaliza, tunasubiri order. Unajua kimsingi ulipopewa order ya kwamba ‘nyimbo zangu usipige, jina langu usiseme kwenye chombo chako, vyovyote itakavyokuwa mimi sitaki kusikia hiyo kitu’ hiyo ndio order. Kwahiyo labda tukikutana, nimuombe tena @jidejaydee kama tutaruhusiwa kufanya hiyo kitu,” alisema.
Ruge amesema ana muda mrefu hajawahi kukutana na Lady Jaydee, japo amedai ‘hata leo nikipata nafasi ya kahawa nitashukuru sana kwa huo mwaliko.’
.
Wiki kadhaa zilizopita Ruge na Joseph Kusaga walishinda kesi ya kuchafuliwa (defamation) iliyokuwa imefunguliwa dhidi ya #LadyJaydee na muimbaji huyo kuamriwa kuwaomba radhi.
.
“Tunashukuru walau tulishinda ile kesi lakini at least ilitengeneza mfano wa watu kuelewa kwamba tusipende kutuhumu vitu kama watu huna uhakika. Bahati nzuri pia hata katika hiyo kesi alisema mwenyewe hajawahi kusikia tunasema, aliambiwa na watu. Lakini ni mambo yashapita hayo.”

Sikiliza Hapa:

Audio: Rais Magufuli Aongea na Makonda Live Akiwa Kwenye Mkutano wa Wananchi

0
0
Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Paul Makonda amempigia simu Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli na kuongea naye ‘live’ akiwa katika mkutano wa ziara yake ya wilaya ya Ubungo ya kusikiliza changamoto za wananchi pamoja na kuzitatua.

Makonda alimpigia simu mkuu huyo wa nchi ili kuomba ufafanuzi juu ya changamoto za wananchi wa Ubungo hasahasa kwa wale ambao wanabomolewa nyumba kutoka na utanuzi wa barabara. Sikiliza Hapa:

MSIKILIZE Ruge Akizungumzia Ruby, Rama Dee, Diamond, THT, Fiesta na Muziki wa Bongo Fleva ndani ya XXL

0
0
Ruge Mutahaba Ambae ni Mmoja wa Wakurugenzi wa Clouds Media Group siku ya Leo ameongea kwenye kipindi cha Radio Clouds cha XXL na kuongelea mambo mengi sana, Hapa chini nimekuwekea Maongezi yote aliyoongea A to Z

Sikiliza Hapa:



Part1
Part2

Mimi Sihitaji Kiki ili Muziki Wangu Upenye

0
0

Ni kwenye Clouds E ya Clouds TV na Shadee Weriss ambapo Ben Pol alikuwa na interview kuzungumzia muziki mpya ambao ameshirikishwa na Darassa unaoitwa Muziki.

Ben Pol amefunguka kuwa kwa kipindi hiki ambacho ni ngoma kibao zimetoka kwa mkupuo itachukua takriban wiki 3 ili ngoma hizo kujichuja na muziki mzuri kuendelea kuishi muda mrefu zaidi ya hapo  na zingine ambazo zimetoka kwa kiki kuishia hewani.

Idris Sultan aishia ‘Kula Kwa Macho’ Kwa Mrembo Sanchoka

0
0
Na Musa Mateja, Ijumaa
DAR ES SALAAM: Licha ya mbwembwe alizoonesha Mtangazaji wa Redio Choice FM, Idris Sultan katika kumtambulisha mwanadada Sanchoka anayedai ni mpenzi wake mpya baada ya kuachana na Wema Sepetu, inadaiwa jamaa huyo hajaona ‘ndani’ bado kwa mtoto huyo mzuri.

Rafiki wa karibu wa Idris aliyeomba hifadhi ya jina lake alilitonya Ijumaa kuwa, licha ya mshindi huyo wa BBA mwaka 2014 kumchombeza Sanchoka akitaka awe wake, bado hajaambulia kitu kwani modo huyo anaonekana kuwa si ‘maharage ya mbeya’.
“Ni kweli Idris alikutana na Sanchoka kule Sauzi kwenye Tuzo za MTV Africa (Mama) lakini alishia kula kwa macho tu, mtoto anaonekana kuwa na kamsimamo f’lani hivi na ndiyo maana licha ya kuvuma sana mpaka leo hajatia maguu Dar,” alidai mtoa ubuyu huyo.

Katika kubalansi habari hii Ijumaa lilifanya jitihada za kumtafuta Sanchoka kuzungumzia kilichopo kati yake na Idris lakini simu yake iliita bila kupokelewa.
Idris alipopatikana alisema kuwa, watu watasema mengi kama ilivyokuwa kipindi kile alipokuwa na Wema lakini ukweli ni kwamba ana malengo makubwa na modo huyo na si kwamba ana tamaa za kingono kwake.

“Watu wamekaa kingonongono tu, mimi nina future na yule mtoto na ikishakuwa hivyo kuna mambo lazima yasubiri, sasa wanaosema nakula kwa macho wao kinachowauma ni nini?” alihoji Idris.

GPL

MAAMBUKIZI Ya Ukimwi Mkoani Simiyu Yanachangiwa na Wanaume Ambao Hawajatairiwa

0
0
MKUU wa Mkoa wa Simiyu, Anthony Mtaka amesema maambukizi ya virusi vya Ukimwi yanachangiwa kwa asilimia 60 na wanaume ambao hawajafanyiwa tohara.

Mtaka aliyasema hayo jana katika kikao cha wadau wa Ukimwi cha kujadili mipango na mikakati mbalimbali ya kudhibiti maambukizi hayo kilichofanyika wilayani Bariadi mkoani Simiyu.

Akifungua mkutano huo, Mtaka alisema maambukizi ya Ukimwi yanachangiwa kwa asilimia 60 kwa wanaume ambao hawajafanyiwa tohara hivyo kusababisha baadhi ya wilaya wenye idadi kubwa ya wanaume wasiofanyiwa tohara kuwa na kasi kubwa ya maambukizi.

Mratibu wa kudhibiti maambukizi ya virusi vya Ukimwi mkoani hapa, Dk Hamis Kulemba alisema wilaya ya Busega inaongoza kwa asilimia 5.8 ikifuatiwa na Halmashauri ya Bariadi Mjini kwa asilimia 3.8 kwa kuwa na maambukizi ya virusi vya Ukimwi.

Alibainisha kuwa mpaka sasa zaidi ya wanaume 138,844 wamefanyiwa tohara kwa kipindi cha miaka miwili ambapo kipindi cha mwaka 2015 wananchi waliopima walikuwa 262,862 na kati ya hao wananchi 8,631 sawa na asilimia 3.3 waligundulika kuwa na maambukizi ya ukimwi.

Mtaka alisema pia wananchi wamekuwa wakiacha kutumia dawa za kufubaza virusi hivyo, wakijiona wanaendelea vizuri ambapo watu wanaotumia dawa hizo kwa mwaka huu ni watu 40,426 huku wengine wapya 18,246 wamesajiliwa kuanza kumeza dawa hizo.

WAZIRI Mkuu Amshukia Waziri Mwakyembe..Ataka Majibu Ndani ya Wiki Moja

0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ametoa wiki moja kwa Waziri wa Katiba na Sheria, Dk. Harrison Mwakyembe kumpa maelezo kuhusu sababu za Tanzania kutokukamilisha mkataba wa Mawakili wa Afrika Mashariki kutambuana katika utendaji wao.

Ametoa agizo hilo leo (Ijumaa, Novemba 25, 2016) wakati akimuwakilisha Rais Dk. John Magufuli katika ufunguzi wa mkutano wa 21 wa mwaka wa Chama cha Wanasheria wa Afrika Mashariki kwenye Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC) jijini Dar es Salaam.

“Nimeshtushwa kidogo kusikia kwenye taarifa yenu kuwa mkataba huo uliolenga nchi zote za Afrika Mashariki hautaihusisha Tanzania kutokana na kutokukamilisha sehemu yao ya kuufanyia kazi, nitahitaji maelezo,”

“Nitapenda kupata maoni yako wewe mwenyewe Mheshimiwa Waziri wa Katiba na Sheria wa Tanzania kwa vile wewe ni Mwanasheria mwandamizi na siyo Mwanasheria wa Tanganyika Law Society peke yake kwa nini Tanzania haijakamilisha mkataba huu,” amesisitiza.

Waziri Mkuu amesema kwa mujibu wa maelezo ya awali aliyopewa kuhusu mkataba huo, utakuwa na umuhimu mkubwa kwenye ukanda wa Afrika Mashariki kama ilivyo kwenye sekta nyingine zinazoshirikiana ikiwemo uhandisi, uhasibu, uthamini na uchoraji wa majengo.

Katika hatua nyingine Waziri Mkuu amewataka Wanasheria hao kuzisaidia nchi zao ili ziondokane na umaskini uliokithiri na Serikali zipate muda wa kushirikisha watu wake katika kufanya kazi kwa lengo la kuwapatia maendeleo.

Amesema nchi zilizoendelea na zinazoendelea, baada ya chaguzi hufanya shughuli za ujenzi wa taifa lao na maendeleo ya watu wake. Ili kudumisha demokrasia wana muda wa mikutano na maandamano na kazi.

“Hawaandamani tu bila kupata kibali cha Polisi, hawaruhusiwi kuzuia magari yasipite, kuzuia kazi isifanyike. Mfano kifungu cha 115 cha Sheria ya Taifa ya Uchaguzi, kinataka kesi zinazotokana na uchaguzi ziwe zimefunguliwa mahakamani ndani ya siku thelathini tangu kutangazwa kwa matokeo ya uchaguzi na ziwe zimesikilizwa na kutolewa maamuzi ndani ya miezi kumi na miwili tangu tarehe ya kufunguliwa mahakamani,” amesema..

Amesema “kwa uelewa wa kawaida, Kifungu hiki ni kuwa jamii inataka masuala ya siasa za uchaguzi yawe na muda wake wenye ukomo maalum ili baada ya hapo wananchi waelekeze muda, nguvu na rasilimali zao nyingine katika kazi au shughuli nyingine za maendeleo na ujenzi wa Taifa lao”.

Aidha, Waziri Mkuu amesema eneo jingine ambalo ni muhimu kulitupia jicho ili kukuza ushindani wa kibiashara katika Jumuia ya Afrika Mashariki ni la uendeshaji wa mashauri mahakamani hasa kwa mashauri ya madai.

“Wote tunakubaliana kuhusu misingi na haki za kidemokrasia kuwa kila mtu anayo haki kikatiba na kisheria kusikilizwa madai yake na kutetea haki zake; na kuwa chombo chenye mamlaka ya kutoa haki ni Mahakama”. Amesema.

Amesema kuna taarifa za kuwepo kwa kesi zenye kuhusisha mali za thamani kubwa zinazochukua muda mrefu sana kumalizika mahakamani huku baadhi ya sababu za kuchelewa kwa kesi hizo ni utoaji wa maombi ya kuziahirisha mara kwa mara kwa sababu binafsi jambo linalosababisha uendeshaji wa kesi kuwa mgumu na kuchukua muda mrefu.

Waziri Mkuu amesema wakati mwingine hata kesi zilizosikilizwa huendelea kubaki mahakamani muda mrefu kutokana na maombi na rufaa za hapa na pale zinazoishia kumnyima mwenye haki fursa ya kutekelezewa haki yake.

“Ni wazi kesi kama hizi zinapohusisha mahusiano ya kibiashara na au mitaji mikubwa ya biashara, matokeo yake ni kudumaza na hata kuua biashara, achilia mbali ushindani wa kibiashara. Ni wajibu wenu Wanasheria kupata ufumbuzi wa tatizo hili lenye athari hasi kibiashara,’ amesema.

Amesema haki ya wadaiwa kusikilizwa kikamilifu na Mahakama, haki na uhuru mlionao Mawakili kuwawakilisha wadaiwa wao bila hofu au shinikizo lolote, viwe chachu ya maendeleo ya ushindani wa kibiashara na visiwe kikwazo.

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
2 MTAA WA MAGOGONI,
S. L. P. 3021,
11410 DAR ES SALAAM.
IJUMAA, NOVEMBA 25, 2016.

Mwana FA Alaani Bifu za Wasanii Zinazoelea..Adai Busara Inahitajika la Sivyo Watatoana Macho

0
0
Mwana FA ameonya kuhusu bifu zinazoendelea kwenye muziki wa Bongo Flava kwamba zinakoelekea, watu wanaweza kufanyiana vitu vya hatari zaidi.
Akiongea kwenye kipindi cha 360 cha Clouds TV jana, FA amesema busara zinahitajika kumaliza tofauti baina ya wasanii wanaohusika kwenye bifu hizo.
.
“Tufike mahali kwamba tujiwekee mipaka kama binadamu kwamba hivi vitu ambavyo tunaambiana kama ungekuwa unaambiwa wewe na familia yako ingekuwa sawa? Maana yake tunavyoelekea tutatoana macho hivi karibuni,” alisema rapper huyo.
.
“Watu pekee wanaoweza kufanya ni wao wenyewe wanaohusika. Nafikiri watu wawe humble, warudi chini kidogo, wanaelea sana juu, turudi chini kidogo, tujikumbuke sisi nani na kama malengo yetu ni kutoana roho ama kuendelea kufanya muziki tuweze kujitengenezea vipato,” amesisitiza.
Ushauri wa Mwanafa umekuja katika wakati ambao uhasama kati ya kambi ya Diamond na Alikiba unazidi kushika kasi.
Rapper huyo ameachia video ya wimbo wake mpya #DumeSuruali aliyomshirikisha vanessamdee.

Ujumbe wa Mbunge Hussein Bashe Kwa Rais Magufuli

0
0
November 25 2016 kupitia ukurasa wake wa facebook mbunge wa Nzega mjini Hussein Bashe aliamua kuandika ujumbe mrefu kwa lengo la kufikisha ujumbe wake kwa Rais John Pombe Magufuli katika utendaji kazi wake pamoja na kumpa ushauri.

‘Napenda kuchukua fursa hii kwa heshima kubwa kabisa na kwa niaba ya wananchi wenzangu wa Jimbo la Nzenga Mjini kumpongeza Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Joseph Pombe Magufuli kwa uamuzi aliouchukua wa kuivunja Bodi ya Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) na kumfuta kazi mwenyekiti wa Bodi hiyo‘

‘Bw. Bernard Mchomvu, kwa kutofuata maagizo ya Mhe. Rais na matakwa ya Sheria ya Benki Kuu ya Tanzania ya mwaka 2006, kifungu cha 31 na 32 ambavyo vinaelekeza Mashirika ya Umma na Taasisi za Serikali kuweka fedha zao katika akaunti maalumu zilizopo Benki Kuu.’

‘Uamuzi huo sio tu unawanufaisha walipa kodi wa Taifa letu lakini pia unakomesha tabia za matumizi mabaya ya madaraka na fedha za umma kwa kujitajirisha na kujinufaisha isivyo halali kwa baadhi ya Watendaji Wakuu wa Mashirika ya Umma‘

‘Pamoja na kuwa Rais Mstaafu Mhe. Jakaya Kikwete alisaini Sheria namba 5 ya Benki Kuu tarehe 7 Juni 2006 miaka takribani kumi iliyopita hakuthubutu kuchukua uamuzi mgumu na wenye manufaa kwa Taifa kama uliochukuliwa na Rais Magufuli wa kuamua kuweka fedha za mashirika ya Umma katika Akaunti Maalumu zilizopo Benki Kuu‘

‘Kutokana na uamuzi huu wa Rais Magufuli, zaidi ya Shilingi bilioni 564.6 za ikiwa ni jumla aya shilingi na fedha za kigeni katika akaunti 267 za Mashirika ya Umma na Idara za Serikali zimeokolewa zisiingie katika mikono ya ‘wapiga dili’ ambao walizoea kutumia mwanya huo kujinufaisha isivyo halali kwa fedha za walipa kodi wa Taifa letu‘

‘Katika hatua za kuendelea kumuunga mkono Mhe. Rais Magufuli, ninamshauri achukue hatua zaidi ya zile alizozichukua kwa iliyokuwa Bodi ya TRA, kwa kuwa mtindo wa kuweka fedha za umma katika mabenki ya biashara una harufu ya ufisadi, wizi wa fedha za umma na dalili za matumizi mabaya ya madaraka ndani ya miaka 10 iliyopita‘

‘Ni vema Mhe. Rais ikimpendeza akafikiria kuanzisha uchunguzi maalumu (forensic audit) kubaini kupitia mwanya huo wa kuweka fedha za umma kwenye benki za biashara Je Serikali ilipoteza fedha kiasi gani kwa njia ya dili chafu, na kubaini endapo kulikuwa na matumizi mabaya ya madaraka, kufunua mwanya wa kuondoa hisia na viashiria vya ufisadi, wizi na rushwa katika hatua za kuwekwa fedha hizo katika akaunti za fixed deposits‘

‘Hatua hii italisaidia Taifa kuwafikisha mbele ya mkono wa Sheria maharamia wote na wapiga dili walioliingiza Taifa letu katika hasara kubwa kwa manufaa yao wenyewe. Ikiwezekana hatua dhidi yao zichukuliwe kwa mujibu wa Sheria za uhujumu uchumi ili mahakama ya Mafisadi iliyoundwa na Mhe. Rais Magufuli ifanye kazi yake kwa kasi‘

‘Aidha, katika hatua nyingine ili kuziba kabisa mianya ya upotevu wa fedha za umma katika hatua za kudumu, ninamshauri Mhe. Rais Magufuli katika Bunge lijalo mapema mwaka 2017 apeleke Bungeni kwa hati ya dharura, marekebisho ya Sheria Namba 5 ya Benki Kuu ya mwaka 2006 ili kurekebisha vifungu vya 31 na 32 na vifungu vyake vidogo‘

‘Katika uchambuzi wangu wa Sheria hii nimebaini ipo mianya ya kisheria ambayo inaweka ulaini katika masharti ya kulazimisha Mashirika ya Umma na Idara za Serikali na Serikali za Mitaa kuweka ulinzi wa fedha za umma kwa kuzitunza katika akaunti zilizopo Benki kuu na badala yake kufungua dirisha la kuziweka fedha hizo katika benki za biashara kwa mujibu wa sheria‘

‘Kwa mfano, kifungu cha 32 cha Sheria Na. 5 ya BoT ya mwaka 2006 kinasema kuwa, ninanukuu “32.–(1) The Bank, in its capacity as a banker and fiscal agent of the Governments or of any public authority, may be the official depository of the Governments or public authority concerned and accept deposits and effect payments for the account of the Governments or public authority.” Katika taaluma ya Sheria, neno “may be”

‘Linamaanisha sio lazima kwa mujibu wa sheria kuweka fedha za Mashirika ya Umma na idara za Serikali katika akaunti za BoT. Huu ndio ulaini wa sheria ninauzungumzia ambao ulitumiwa miaka 10 iliyopita kuweka fedha za umma katika akaunti za Benki za Biashara. Ili kuweka msingi mzuri wa uamuzi wa Mhe. Rais Magufuli ni vema kifungu hiki kikabadilishwa ili kulazimisha Mashirika ya Umma kutunza fedha zao BoT kwa mujibu wa Sheria‘

‘Pia kwa kuwa juhudi za Mhe. Rais Magufuli zimeongeza ukasanyaji wa mapato kwa kodi, ninamshauri kwa kuwa sasa Serikali inaondoa zaidi ya Shilingi 1 trilion kwa mwezi kutoka kwenye mifuko ya Watanzania kwa njia ya tozo za kodi na wakati huo huo kupitia sheria tumeondoa fedha za mashirika ya Umma kutoka kwenye Mabenki ya Biashara kuna Umuhimu wa Serekali kuhakikisha Fedha zilizotengwa kwenda kwenye Miradi ya Maendeleo zinakwenda kwa kasi ili kuchochea mzunguko wa fedha kwenye Uchumi. Hatua hii itasaidia sana ku-stimulate uchumi na kupunguza mdororo unaoanza kujitokeza‘

‘Aidha pia, Namshauri Mhe. Rais kufanya marekebisho makubwa katika mfumo mzima wa uanzishaji, uendeshaji na uratibu wa biashara nchini ili kuongeza ajira nchini, kwa kuwa ripoti ya Benki ya Dunia (2016) ya kufanya biashara Tanzania (Doing Business Tanzania- 2016)‘

‘Inaonesha Tanzania kutofanya vizuri katika Sera na Sheria za usajili wa biashara mpya na mazingira ya uendeshaji wa biashara kuwa kushika nafasi ya 129 kati ya nchi 189. Kwa mujibu wa ripoti hiyo mjasiriamali akitaka kuanza biashara rasmi lazima avuke vihunzi 9 ndani ya takribani siku 26 ili aweze kufungua biashara yake! Vihunzi hivyo vinavunja moyo na kupunguza kasi ya ongezeko la ajira binafsi kwa njia ya ujasiriamali na pia inalipa Taifa hasara kwa kutokusanya kodi kutoka kwenye biashara hizi mpya kwa haraka na kwa wakati kutokana na urasimu uliopo‘

‘Pamoja na hayo pia, namshauri Mhe. Rais, agize wizara ya wiwanda na biashara na wizara ya fedha kurekebisha sheria za kodi na biashara ili kuwezesha wepesi, urahisi na uharaka wa kukusanya kodi na kuwezesha wafanyabiashara wadogo kufanya biashara kwa uhuru‘

‘Ripoti ya Doing Business Tanzania, (2016) imebainisha kuwa makampuni yanayolipa kodi huchukua saa 179 kujaza fomu za marejesho hivyo kuifanya Tanzania kuwa na utaratibu mgumu wa kulipa kodi na kushika nafasi ya 150 kati ya nchi 189 duniani kwa ugumu wa taratibu za kulipa kodi. Tukiondoa ugumu huo na kuweka wepesi, kasi ya kukusanya mapato ya kodi itaongezeka na mapato pia yataongezeka!‘

‘Kwa umahususi Serikali inaweza kuanzisha kituo kimoja cha biashara kwa wafanyabiashara wadogo (one stop business center) kitakachotoa motisha kwa kuratibu uanzishaji wa biashara husika mpaka kulipa kodi kwa njia za digitali na mifumo ya TEHAMA. Vituo hivi viwepo kuanzia ngazi ya Serikali za Mitaa ili kurahisisha shughuli za uanzishaji wa Biashara na uwekezaji kutokea chini‘

‘Marekebisho hayo ya sheria za kodi na biashara yalenge zaidi kutengeneza ‘Business Incubation’ na Misamaha ya kodi (Tax holidays) kwa wafanyabiashara wadogo wanaoanza biashara ili kusaidia kukuza biashara kuliko hali ilivyo hivi sasa ambapo biashara ndogo zinakabiliwa na mzigo mkubwa wa kodi na Tozo za ushuru mbalimbali katika halmashauri zetu kwa mfano Leseni, kodi ya huduma, kodi ya mapato, na kodi za majengo‘

‘Pia kama taifa umewadia wakati Mhe. Rais awaagize BoT na Wizara ya Fedha katika kipindi cha miaka hii mitano ya awali kubadili ‘Modeli ya Uchumi’ wetu kutoka ‘Consumption module’ kwenda kwenye ‘Investment module’ na hii iendane na mabadiliko makubwa ya ‘Tax structure’ yetu na sheria za Uwekezaji na Biashara na kutengeneza motisha (Incentive package) za kisekta na si motisha za ya mwekezaji mmoja mmoja‘

‘Sekta muhimu ambazo zinahitaji kupewa kipaumbele kwenye hiyo new module ni sekta ya ngozi, na viwanda vya mazao ya kilimo‘

‘Mwisho kabisa napenda kumhakikisha Mhe. Rais kuwa mimi binafsi kama mbunge, wananchi wa Jimbo la Nzega na Watanzania wengine wote tunaoamini katika uadilifu katika ofisi za umma, tunaendelea kumuombea ulinzi kwa Mungu, na tupo nyuma yake kumuunga mkono dhidi ya vita hii ngumu ya kupambana na ‘wapiga dili’ walioligeuza Taifa letu miaka 10 iliyopita kuwa shamba la bibi‘

Jihan Ndio Ametangazwa Miss Universe Tanzania 2016 Usiku wa Jana

0
0
Shindano la kumtafuta Miss Universe Tanzania kwa mwaka 2016 limefanyika usiku wa November 25 Dar es salaam ambapo Jihan Dimack ametangazwa mshindi.

Jihan ni mrembo aliyeshinda taji la Miss Ilala mwaka 2014 na kuingia tatu bora Miss Tanzania mwaka huohuo, Wazazi wake ni mchanganyiko wa Tanzania/Lebanon.

Nafasi ya pili ya shindano la Miss Universe 2016 ilichukuliwa na Lilian Loth kutoka Kampala University na nafasi ya tatu ilichukuliwa na Lilian Felix ambaye alikuwa aniwakilisha UDSM.

Rais za Zamani wa Cuba, Fidel Castro Afariki Dunia

0
0
Rais wa zamani wa Cuba na kiongozi wa mapinduzi ya kikomunisti, Fidel Castro amefariki akiwa na umri wa miaka 90, mdogo wake Raul ametangaza.

Amefariki usiku wa saa nne na dakika 22, kwa mujibu wa Rais Raul Castro.

Fidel Castro aliiongoza Cuba kama nchi ya chama kimoja kwa takriban miaka 50 kabla ya Raul kushika madaraka mwaka 2008.

Mazishi yake yanafanyika Jumamosi hii kwa mwili wake kuchomwa moto. Kutakuwepo na siku kadhaa za maombolezo ya nchi nzima.

Je Dada Unahitaji Kuwa na Makalio Mazuri na Rangi Nzuri na Mkaka Kuwa Handsome? African Beauty Inakuletea Dawa Hizi

0
0

AFRICAN BEAUTY EXPRESS PRODUCTS ,DAWA ZETU ZIMETHIBITISHWA KIAFYA.
je Dada unahitaji Kuwa Mrembo? na kaka unahitaji Kuwa mtanashati?African beauty imewaletea products nyingi sana zenye ubora WA hali ya juu,hazina madhara wala kemikali,zinamatokeo ya haraka ndani ya wiki mbili tu,products hizi niuhakika sana% tunazo za
(1)kuongeza hipsi,MAKALIO,na mapaja @100000
(2)kunenepesha MIGUU na Kuwa soft(chupa ya Bia)@100000/=
(3)Kupunguza Kitambi(slimming)@100000/=
(4)Kupungua MWILI MZIMA(weight loose)@130000/=
(5)Kuwa Mweupe MWILI MZIMA (njano)@100000/=
(6)kunenepa MWILI mzima@90000/=
(7)Kupunguza MATITI na kuyasimamisha@80000/=
(8)kuongeza matiti@80000
(9)kurefusha NYWELE na kuzuia kukatika@80000/=
(10)kuondoa CHUNUSI,MADOA na makovu@80000/=
(11)kuondoa Michirizi ya uzazi na cream@80000/=
(12)kurefusha na kunenepesha uume kwa size uipendayo@100000/=
(13)kuongeza NGUVU za kiume@100000/=
Ndugu MTEJA bidhaa za African beauty in uhakika sana,ukitumia dose moja hauwezi kurudi tena,MTEJA atakapo nunua bidhaa kwetu ni lazima afuate dose ili aweze kuona matokeo mazuri,MTEJA nilazima afuate maelekezo ya wahusika WA kampuni,MTEJA kama Yupo bize na kazi zake anaweza kupelekewa Huduma Mpaka alipo,kwa Wateja WA mikoani Huduma utatumiwa kwa mabasi kiofisi zaidi,kama MTEJA hayupo bize na kazi anaweza kufika ofisini kwetu zilizopo kariakoo,mnazi mmoja,na Mlimani city kwa maelezo zaidi piga sim(+255)-0756697906,0716805391,0783300397 Whatsapp namba 0756697906 Facebook page AFRICAN BEAUTY unaweza kunifollow instagran
👇👇👇👇👇👇👇👇👇👇👇👇👇
@AFRIC_IS_BEAUTY
@AFRIC_IS_BEAUTY



Muuguzi Anayedaiwa Kumwambia Mama wa Mgonjwa ‘Ataisoma Namba Kumchagua Magufuli’ Atumbuliwa

0
0

Mbeya. Muuguzi wa Hospitali ya Mkoa wa Mbeya anayedaiwa kumkamshifu Junes Elias, mkazi wa Mbozi mkoani Songwe na Rais John Magufuli ametambuliwa.

Mganga mkuu wa hospitali hiyo, Dk Gloria Mbwille alisema muuguzi huyo ametambuliwa na kwamba tume imeundwa kuchunguza tuhuma zinazomkabili.

Hata hivyo, alikataa kuzungumzia zaidi kuhusu muuguzi huyo wala kumtaja jina akisema taarifa zaidi zitatolewa na Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Amos Makalla baada ya tume kukamilisha uchunguzi huo. Juzi mchana, Junes alimueleza Makalla kwamba alifika hospitalini hapo Novemba 22 asubuhi akitokea wilayani Mbozi.

Alisema baada alifuata taratibu za kufungua kadi kwa gharama ya Sh5,000 kwa ajili ya kutaka matibabu ya mtoto wake, Joyce Asifiwe (9), lakini alikashfiwa kwenye dirisha la dawa akiambiwa ataisoma namba kwa kumchagua Rais Magufuli.

Alisema baada ya kumuona daktari aliandikiwa dawa za kwenda kuchukua kwenye dirisha ambako ndiko alikotolewa maneno ya kashfa.

“Kwenye dirisha hilo nilimkuta muuguzi mmoja ambaye aliniambia kwamba dawa zote zinauzwa. Hapa hakuna dawa za bure, si mlimchagua Magufuli, sasa mtaisoma namba,’’ alisema akidai kumnukuu aliyemtaja kuwa ni muuguzi.


Baada ya kumsikiliza malalamiko hayo, Makalla aliagiza mganga mkuu aitwe, lakini ilielezwa alikuwa safarini, hivyo kaimu wake, Dk Ismail Macha alifika.

Makalla alimueleza Dk Macha kwa kifupi yaliyojiri kutoka kwa mlalamikaji huyo na kumtaka waongozane hadi hospitalini na kuwaita wauguzi waliokuwa zamu Novemba 22 dirisha la dawa ili amtambue mhusika na achukuliwe hatua jambo ambalo limefanyika.

UPUNGUFU wa Marubani Waikwamisha Air Tanzania

0
0
Shirika la Ndege Tanzania (ATCL) limekiri kuwepo kwa changamoto mbalimbali zikiwemo ucheleweshwaji wa ndege wakati wa kutoa huduma katika maeneo ambayo yalipaswa kuhudumiwa.


Akizungumzia changamoto hizo, Mwenyekiti wa Bodi ya Shirika hilo, Mhandisi Emmanuel Korosso, amekiri kuwepo kwa changamoto ya marubani ikizingatiwa mpaka sasa shirika hilo linatarajiwa kumaliza mafunzo ya marubani 13 katikati ya mwezi Desemba.

Amesema kuhusu wafanyakazi, bodi yake imeagiza menejimenti ya shirika hilo kusimamia kusimamisha kwa muda mktaba wa hiari ambao unatoa mwanya kwa wafanyakazi kutumia vibaya ruhusa za matumizi ya tiketi za bure.

Mwenyekiti wa Bodi ya ATCL, Mhandisi Emmanuel Korosso (Katikati) akizungumza na wanahabari leo.

Aidha, Bodi imemuagiza Mtendaji Mkuu wa Shirika hilo kutangaza mara moja nafasi zote za wakurugenzi na pia nafasi za mameneja zilizo wazi kwa kufuata muundo wa muda uliopitishwa na bodi huku ikiwaondoa katika nafasi zao wakurugenzi wote ispokuwa Mkurugenzi Mtendaji kutokana na utendaji dhaifu pamoja na kutokuwa na sifa stahiki za elimu za kushika nafasi walizonazo.

Kocha Lwandamina Akanusha Kuja na Wachezaji wake Yanga

0
0
Klabu ya Yanga hii leo imemtambulisha kocha Geroge Lwandamina kuwa kocha mpya wa klabu hiyo akirithi nafasi ya kocha wa zamani wa klabu hiyo Hans van der Pluijm ambaye amepewa majukumu mapya ya kuwa Mkurugenzi wa Ufundi ndani ya klabu hiyo.


Makamu Mwenyekiti wa Yanga Clement Sanga amesema, anaamini Kocha Lwandamina atashirikiana na aliyekuwa kocha wa Klabu hiyo ambaye kwa sasa ni mkurugenzi wa benchi la ufundi Hans van der Pluijm ambaye anaielewa vizuri timu hiyo ili kuweza kuipeleka mbele zaidi.
Sanga amesema, wamefanya mazungumzo na aliyekuwa kocha wa Klabu hiyo Hans na wameshabadili majukumu yake ndani ya klabu hiyo na Kocha Lwandamila amesaini mkataba wa miaka miwili kuitumikia Klabu.

Lwandamina amesema,anaamini Pluijm amefanya kazi nzuri na atahakikisha anashirikiana naye kwa kufuata nyayo zake na atashirikiana naye bega kwa bega kuhakikisha Yanga inapata mafanikio zaidi.
Lwandamina pia amekana juu ya madai kwamba amependekeza wachezaji wawili aliokuwa nao Zesco United ya nchini Zambia kiungo Misheck Chaila na mshambuliaji Mkenya Jesse Were wasajiliwe pia ndani ya Klabu ya Yanga.

Gavana wa BOT Asema Akaunti Maalumu ( “Fixed Deposit Account”) Si Kosa

0
0
Sakata la Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kuweka fedha katika akaunti maalumu kwenye benki za biashara limechukua sura mpya baada ya Gavana wa Benki Kuu Tanzania (BoT), Profesa Benno Ndulu kusema si kosa kisheria.

Profesa Ndulu, ambaye ni mmoja wa wajumbe wa Bodi ya TRA iliyovunjwa na Rais John Magufuli Jumapili iliyopita, alisema mjini Arusa jana kuwa hakuna hasara kiuchumi kuweka fedha kwenye akaunti maalum isipokuwa hilo suala lilikuwa na hali nyingine.

Japokuwa Profesa Ndulu hakutaka kufafanua zaidi kwa maelezo lilichomekewa tu katika mkutano na waandishi wa habari wa kuelezea hali ya uchumi, alisema hali hiyo ndiyo suala lililozungumzwa na siyo kusema “fixed deposit account” ni mbaya.

“Kwani amesema fixed account zote ni mbaya, pamoja na za watu binafsi? Ndo hivyo sasa. Nilijua mtachomekea hilo kwa hiyo nilikuwa tayari,” alisema mhadhiri huyo wa zamani wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.

Profesa Ndulu alisema hayo alipokuwa akijibu maswali ya waandishi wa habari walipotaka kujua athari za kiuchumi kwa taasisi za umma kuweka fedha kwenye akaunti maalumu tena benki binafsi.

Kauli hii ya Profesa Ndulu imekuja siku moja baada ya Rais Magufuli kueleza kilichochangia kuchukua uamuzi wa kutengua uteuzi wa Mwenyekiti wa Bodi, Bernard Mchomvu na pia kuivunja bodi yake iliyokuwa na wajumbe tisa. Kati ya wajumbe hao tisa, watano wanaingia kwa mujibu wa sheria na wanne ni wa kuteuliwa.

Wajumbe wanaoingia kwenye Bodi kwa mujibu wa sheria ni Gavana wa BoT, Profesa Beno Ndulu; Kamishna Mkuu wa TRA, Alphayo Kidata; Katibu Mkuu Wizara ya Fedha wa Jamhuri ya Muungano, Doto James; Katibu Mkuu Wizara ya Fedha Zanzibar, Khamis Mussa Khamis; na Katibu Mkuu Mipango. Bodi hiyo ilivunjwa Jumapili iliyopita.

Rais Magufuli alisema juzi kuwa Bodi ya TRA iliyokuwa na watendaji hao wakuu wa idara na taasisi za Serikali ilifanya dhambi ya kuidhinisha uamuzi wa menejimenti kuweka mabilioni ya shilingi katika benki za binafsi.

“Juzi hapa tumekuta Sh26 bilioni zilizokuwa zimetolewa TRA kwa ajili ya matumizi ya TRA zikapelekwa kwenye mabenki matatu kama ‘fixed deposit account’ na bodi ikapitisha. Ndiyo maana nilipozipata hizo hela; hela nikazichukua na bodi kwaheri,” alisema Rais Magufuli alipokuwa mgeni rasmi kwenye mahafali ya 31 ya Chuo Kikuu Huria cha Tanzania (OUT) yaliyofanyika mjini Kibaha mkoani Pwani ambako jumla ya watu 4038 walihitimu shahada mbalimbali

Ukwasi wa mabenki
Katika hatua nyingine Profesa Ndulu amesema ukwasi wa fedha katika mabenki umeshuka ikilinganishwa na kipindi cha nyuma hatua inayotatiza utoaji wa mikopo ya muda mrefu kwa ajili ya uwekezaji nchini.

Akizungumza jana na waandishi wa habari mara baada ya kufungwa mkutano wa 18 wa taasisi za fedha uliofanyika kwa siku mbili jijini Arusha alisema hali hiyo inafanyiwa kazi na wadau wa taasisi hizo ili kuja na mbinu kufanya kuwa endelevu kwani uchumi unategemea uwekezaji unaotegemea mikopo ya muda mrefu.

Profesa Ndulu alisema BoT itahakikisha inaziwezesha benki kuendelea na jukumu lao la kutoa mikopo pia kuwa wabunifu wa kutafuta pesa kwa ajli ya amana badala ya kutegemea Serikali pekee.

“Benki zinaweza kukusanya amana kwa kiwango kikubwa lakini kama nilivyosema jana (juzi) kuwa katika kila Sh60 kati ya Sh100 zipo kwenye mikono ya watu badala ya kuwekwa akiba benki hivyo ni muhimu zikawekwa mbinu ya kuzipata kwa ajili ya kuwawezesha wawekezaji kuzitumia kwenye uzalishaji,” alisema.

Alisema katika kufanikisha mpango huo lazima kuvutia mitaji kutoka nje kwani hakuna nchi yoyote duniani inayoweza kupiga hatua kwa kutegemea fedha za maendeleo na uwekezaji zitokane na mapato ya ndani pekee akitolea mfano wa China kuwa ni mfano uchumi wake kutegemea mitaji inayotoka nje ya nchi hiyo.

Katika hatua nyingine Profesa Ndulu alisema amekubaliana na wadau wa sekta ya fedha kuongeza nguvu katika kutoa mikopo na kuboresha mifumo ya taarifa kwa wale wanaotaka mikopo kwa ajili ya kilimo katika mnyororo mzima wa thamani kuanzia uzalishaji hadi kufika kwenye soko.

Profesa Ndulu alisema Tanzania imekaa vizuri kijiografia kufanya biashara na nchi zisizo na bahari zikiwemo Malawi, Uganda, DRC na Zambia katika kuwezesha sekta ya fedha kusaidia eneo la usafirishaji, bandari kufanya kazi na huduma kutolewa inavyotakiwa.

Mwenyekiti wa wenye mabenki ambaye ni Mkurugenzi Mkuu wa Benki ya CRDB, Dk Charles Kimei amesema waendeshaji wa mabenki wamenufaika na kuelewa mikakati na fursa za Serikali ambayo itawawezesha wao kutoa fedha kwa wafanyabishara.

Alisema wao kama CRDB wameweza kukusanya amana za Sh500 bilioni zinazokopeshwa kwa wafanyabiashara katika kipindi cha miaka miwili iliyopita na kufungua matawi madogo madogo 100 nchi nzima.

Dk Kimei alisema serikali inapobanwa kifedha kutokana na kutegemea mashirika ya umma inawapa fursa sekta binafsi kupanua wigo wao kuwafikia wananchi wengi.

Madee Ajibu Tuhuma Zinazomkabili Babu Tale Kuitelekeza Tip Top na Kumganda Diamond Platnumz

0
0
Msanii Madee ambaye ni miongoni mwa wasanii viongozi wa Tip Top inayosimamiwa na Babu Tale, amejibu tuhuma za meneja wao huyo kuitelekeza Tip Top na kuegemea zaidi kwa Diamond Platnumz.


Akizungumza kwenye Planet Bongo ya East Africa Radio, Madee amesema hawezi kupinga maneno yaliyopo mtaani kwani ni kitu kinachoonekana kwao, lakini ukweli ni kwamba Babu Tale hajaitelekeza Tip Top, isipokuwa Diamond amekuwa na projects nyingi zinazohitaji uwepo wake kama meneja.
Hivi karibuni mashabiki wameibua hoja kuwa Babu Tale ameipotezea Tip Top na "kugandana" na Diamond, kwa sababu anafanya vizuri na safari za nje hazimuishi, kauli ambayo hata Niki Mbishi ameiimba kwenye wimbo wake wa Babu Talent.

Sikiliza sauti ya Madee akizungumzia suala hilo kwenye Planet Bongo ya East Africa Raio.
Viewing all 104417 articles
Browse latest View live




Latest Images