Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104756 articles
Browse latest View live

PICHA ZIKIONESHA MCHUMBA WA NEY WA MITEGO SIWEMA AKIVALISHWA PETE NA JAMAA MWINGINE

$
0
0
Akivishwa Pete

Aki wow baada ya Pete Kuvikwa

Full Ma Deep Kisses

Akionyesha Waaalikwa
 Insta Kuna Umbea kila siku yanaibuka mapya..Mweee....Hizo ni Picha Nilizozicapture kwenye Video ikionyesha Siwema ambae ni mchumba wa Ney wa Mitego Akivalishwa Pete na Jamaa Mmoja :


NEY WA MITEGO AMTETEA MCHUMBA WAKE NI BAADA YA MITANDAO KUDAI AMECHUMBIWA NA JAMAA MWINGINE.

$
0
0
Kuna baadhi ya mitandao imepost na kuandika habari kuwa mchumba wake msanii wa kizazi kipya anetamba na kibao chake NASEMA NAO na MUZIKI GANI ame chumbiwa na mwanaume mwingie. Katika kukanusha uvumi huo msanii huyo amepost picha ifuatayo Instagram na kuandika ujumbe chini yake unao dhihirsha mapenzi yake kwa mchumba wake huyo.

MAUAJI YA MZEE KARUME ..ACHA SASA TUHOJI YASIO HOJIKA

$
0
0
The stong man in the world is the one with the best information……..

Hii ni kauli ya waziri mkuu wa zamani wa Uingereza Benjamin Disarel ambaye aliwahi kutawala kipindi nchi hiyo wakati wa vuguvugu la vyama vya wafanyakazi mwaka 1967, tofauti na watangulizi wake Disarel yeye aliwataka makundi yote ya waingereza wanyonge waliokuwa wanapambana kwa ajili ya maslahi yao kuwa na taarifa sahihi kwa wakati mwafaka hakika haya ni maneno mazito sana.

Naam! Leo tunapoadhimisha Karume Day kuna haja ya kuwa na taarifa sahihi kuhusu kifo cha Mzee Karume ambaye anatajwa kuwa mwasisi wa mapinduzi ya Zanzibar ya januari 12 , 1964. Nalisema hili kwa jinsi mambo yanavyofichwa nabashiri kuna uwezekano mkubwa huko mbele tuendako wazungu wakaja kutusaidia kufanya utafiti wa kifo cha shujaa huyo, ili kuelewa nayoyasema rudia makala za mwandishi nguli wa Raia Mwema Bw Joseph Mihangwa au nenda visiwani Zanzibar halafu uliza wakazi wa visiwa hivyo vya karafuu wakwambia sababu za mzee huyo kupigwa risasi mnamo mwaka tarehe7 mwezi wa 4 mwaka 1972? Kisha kwa wingi na mkanganyiko wa majibu ndio utakubaliana nami umefika wakati tuhoji yasiyohojika.

Kwanza swali rahisi hivi ni kweli serikali zetu hizi za Zanzibar na ya Muungano hazifahamu sababu za kifo cha mzee huyo? Hivi ni kweli kabisa mpaka leo tumeshindwa kuweka wazi swala hili? Kwanini? Imefika sehemu tumeruhusu mapambano na malumbano ya wanahistoria kutafiti chanzo cha mauaji hayo ilihali tumeukalia ukweli? Tunaogopa nini? kwa maana tunapojadili mauaji hayo kuna maswali na mtiririko wa kimantiki unaotushawishi kuwa mzizi haswa wa mauaji hayo ni siasa za chuki na kama tunakubaliana katika hili ni lazima twende mbele tujihoji je tumezimaliza hizo siasa za chuki? Au bado zipo?

Hoja ya kwanza katika mtiririko huu ni kuwa kwanza Karume hakuuawa kwa bahati mbaya la hasha! Ilikuwa ni mipango ya watu Fulani na ndio maana ttunasikia matokeo yake ni kuwa baada ya kifo hiko watoto wa mzee huyo walianza kunyimwa fursa zza kimaendeleo kama vile walinyimwa ajira na baadhi yao walifukuzwa kazi haya kayasema mke wa marehemu Karume mama Fatuma Karume akiongea kupitia TBC1 mapema leo, hii ina maana kuwa baada ya kifo hiko chuki haikuisha ikahamia kwa watoto na mke wake ambaye anaweka bayana kuwa ni Nyerere tu aliyewahi kumfariji mama huyo wengine wote walimtoa kwenye kumbukumbu zao hakika hii ni chuki kubwa!

Kutokana na hali hii tunapaswa tujihoji kina nani walihusika na mauaji haya? Na nini kiliwasukuma? Na kwanini chuki hiyo ilifika kwa watoto wake? Je ikiwa bado watoto wa karume wako hai tutaaminije kuwa chuki hiyo imekwisha? Nini mzee karume alifanya mpaka ikatokea hiyo chuki? Lakini tusiishie hapa kwenye mauaji haya kuna jingine , inadaiwa kuwa mzee Karume aliuwawa na mwanajeshi, je kama mwanajeshi ndiye alimwua je hayo siyo mapinduzi ya kijeshi? Kwanini? Lakini pia ingawaje Karume aliuwawa na mwanajeshi cha ajabu ni kuwa uongozi wan chi haukutwaliwa na jeshi bali alipewa mwanasiasa tu Aboud Jumbe!, haya ni maajabu mengine sasa, hivi huyo Hamid aliyemwua mzee karume alitumwa na wanasiasa? Au? Na kama hajatumwa kwanini baada ya mauaji hayo yaliyofanywa na mwanajeshi tunaambiwa kuwa jeshi lilitaka limpe madaraka kanali Seif Bakari hata hivyo baadaye tunaambiwa liliachana na mpango huo, je nini kiliwasukuma kuacha mpango huo? Na nani aliwakataza kufanya hivyo? Hatuoni kuwa iwapo jeshi lingempa uongozi kanali Seif Bakari ambaye pia ni mwanajeshi hatuoni kuwa hayo yangekuwa ni mapinduzi ya kijeshi au uasi wa jeshi? Kwanini jeshi limfanye hivo mzee karume? Aliwakosea nini wapiganaji wake hawa?

Kwa maswali mengi kama haya yasiyo na majibu ndiyo inaibuka haja ya kufahamu je nini sababu za mauaji hayo? Nani alikuwa nyuma ya mauaji hayo? Ni wanajeshi au wanasiasa kwa mgongo wa jeshi? Kina nani hao? Na kwanini? Je chuki zilizopelekea mauaji hayo zilikoma au zingalipo hadi leo? Tukiyajua haya itatuweka huru kwa maana ukweli pekee ndio utatuweka huru vinginevyo tunaficha historia yetu kwa hasara yetu wenyewe! Naam ! wakati ni huu watanzania acha sasa tuhoji yasiyohojika!

...Tafakari!

PENNY: MAPENZI YA SIRI SIYAWEZI

$
0
0
Stori: Imelda Mtema

PREZENTA wa Runinga ya DTV, Peniel Mungilwa ‘Penny’ amefunguka kuwa siku zote hawezi kudumu katika penzi la siri.
Penny alifunguka hayo alipokuwa akizungumza na paparazi wetu na kuainisha kuwa tangu amwagane na Diamond (Nasibu Abdul) ambaye kila mtu alikuwa anamjua, bado hajabahatika kuwa na mtu mwingine.

“Bado nipo nipo sana na kama ujuavyo, mimi siwezi kuyaficha mapenzi kama  nimepata mpenzi wala haichukui muda kila mtu atajua tu,” alisema Penny.
GPL

KIKWETE KUVUNJA TUME YA KATIBA LENGO SEREKALI KUUTEKA MCHAKATO WA KATIBA

$
0
0
KITUO cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), kimestushwa na kitendo cha Rais Jakaya Kikwete kuivunja mapema Tume ya Mabadiliko ya Katiba na kusema haikustahili kuvunjwa wakati Bunge Maalumu la Katiba bado linaendelea.

Kauli hiyo ilitolewa mjini hapa juzi na mjumbe wa Kamati Maalumu ya Katiba kutoka LHRC, Exavery Lwaitama, alipokuwa akitoa mada kwenye warsha ya jukwaa la mchakato wa katiba mpya, ulioandaliwa na Mtandao wa Kufuatilia Sera Mwanza (MPI), na kuwashirikisha viongozi wa asasi na mashirika mbalimbali kutoka wilaya za Ukerewe, Nyamagana, Ilemela, Magu za mkoani Mwanza, pamoja na Wilaya ya Karagwe, Kagera.

Lwaitama ambaye pia ni mhadhiri mwandamizi mstaafu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), alisema kuvunjwa kwa tume hiyo wakati Bunge la Katiba halijamalizika, ni kuharibu mwenendo na mchakato mzima wa Watanzania kupata katiba wanayoitaka.

Alisema haiwezekani Rais Kikwete aivunje tume hiyo kisha majukumu yake kuchukuliwa na serikali ambayo tangu awali imekuwa ikikataa kutungwa kwa katiba mpya. “Utavunjaje tume wakati Bunge la Katiba halijaisha? Sasa hii rasimu ya katiba inayojadiliwa bungeni itasimamiwa na nani kama tume imevunjwa? Itawezekanaje isimamiwe na serikali ambayo tangu mwanzo haitaki kutungwa kwa katiba mpya?

“Tunakumbuka mwaka 2011 Mwanasheria Mkuu wa Serikali (Jaji Fredrick Werema), na viongozi wengine wa serikali walikataa kutungwa katiba mpya. Sasa leo rais anaivunja tume, hivi tunategemea kuna upatikanaji wa katiba hapa?” alihoji Lwaitama.

Wakizungumza katika warsha hiyo, viongozi wa mashirika na asasi hizo, walisema hawaoni mwelekeo wa Watanzania kupata katiba mpya wanayoitaka, hivyo wakasema ni bora Bunge hilo likavunjwa, ili kuepusha matumizi mabaya ya fedha.

Mratibu wa MPI, Jonathan Kassim, alisema wameandaa warsha hiyo ili kutoa sauti ya pamoja kwa asasi na mashirika hayo kuhusu mwenendo wa Bunge hilo na kuwaomba wajumbe na serikali kwa ujumla kuwatendea haki wananchi kwa kupitisha maoni yao.

HALIMA KIMWANA MBABE WA WEMA SEPETU

$
0
0
Imeelezwa kuwa Diamond hapindui kwa halima kimwana kutokana na ukaribu wao wa mda mrefu, Wakati mpenzi wake Wema sepetu akiwa hapatani na kimwana kama paka na panya, hiyo haijasababisha Diamond kuwa mbali na kimwana, kwani ameshawahi kukiri kuwa hakuna atakayeweza kuwatenganisha na best wake huyo wa long time.

Kama ilivyo kwa kimwana, Diamond hawezi kupindua kwa wema sepetu .wakati kimwana yupo very close na familia ya Dangote, kitendo ambacho kinamuumiza zaidi madame kwani familia ya diamond imekuwa ikimchukia madame na kumkubali zaidi penny na halima, kitendo kinachomfanya penny awe karibu na kimwana kwni anajua fika diamond hapindui kwa kimwana.

MASKINI LULU MICHAEL "HICHI NDIO ALICHO ANDIKA LEO SIKU YA KUMKUMBUKA KANUMBA"

$
0
0

Leo ni siku ya kutimiza miaka miwili tangu kutokea kwa kifo cha Steven Kanumba aliyekuwa star mkubwa wa filamu na kufanikiwa kutoa njia kwa tasnia ya filamu nchini. Kupitia mtandao wa kijamii Elizabeth Michael "Lulu" ambaye anakabiriwa na kesi ya mauaji ya Kanumba bila kukusudia ameandika kwa uchungu kuonyesha kuwa mpaka leo bado haamini kuwa Kanumba alikwishafariki.

Kupitia mtandao mmoja maaruffu wa kijamii, Lulu ameandika

"Bado Siamini kama mwaka wa pili unakatika bila kukuona wala kukusikia baba, Ninaamini bado tupo nawe kiroho na ninaamini zaidi nasfi yako huko ilipo inasimama kunitetea na kunipigania. Inaweza kuchukua miaka na miaka kukuelezea. You still live in me daddy and you are dearly missed. R.I.P daddy yangu."

TIMU YA WATOTO WA MITAANI YA TANZANIA YACHUKUA KUMBE LA DUNIA

$
0
0
Timu ya Taifa ya Watoto wa Mitaani ya Tanzania jana April 06 imefanikiwa kutwaa ubingwa wa Dunia wa Watoto wa Mitaani baada kuifunga Burundi mabao 3-1 katika mchezo wa fainali uliochezwa jijini Rio de Janeiro Brazil.
Mshambuliaji Frank William alifunga mabao matatu katika mechi hiyo iliyochezwa uwanja mkongwe na maarufu wa klabu ya Fluminense huku mgeni rasmi kwenye mechi hiyo akiwa Waziri wa Fedha wa Uingereza George Osborne.
Tanzania ilipata tiketi ya kucheza fainali baada ya kuitandika Marekani mabao 6-1 ambapo hadi mapumziko ilikuwa mbele kwa mabao 4-0,Burundi ilipata tiketi ya kucheza fainali baada ya kuifunga Pakistan mabao 4-3 katika mechi ya nusu fainali ya pili.
Timu ya Tanzania inarejea nchini Alhamisi (Aprili 10 mwaka huu) ambapo itatua Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) saa 10 jioni kwa ndege ya Emirates.

KIMENUKA:WALE WANAWAKE WANAO UZA NA KUWAFANYISHA WADADA UMALAYA CHINA WAKAMATWA

$
0
0
Baada ya kuweka audio clips za hao mabiniti wakilalamika na kuomba msaada ndipo nilipo amua kuanzisha campaign ili kuwasaidia mabinti hao walioko MACAU. Nilijaribu kwa hali na mali kutafuta mawasilano ili kujua wako wapi na kama habari hizi ni za ukweli. Nilibahatika kuongea na baadi ya watu wanao ishi huko na wakanihakikishia kwamba habari hizo ni za kweli na walinihakikisha kwamba kuna mabinti wadogo sana wanaotumiwa katika biashara hiyo haramu  na wanahitaji msaada haraka iwezekanavyo ingawa wanaogopa kutokana na vitisho wanavyopewa na hao wanaojiita  mabosslady au mama zao. Baada ya hapo ndipo harakati za kuwasaidia zilipo anza na kwa kushirikaina na kaka yangu KWAME tukawasiliana na shirkia la IOM (International Organization for Migration) ambao ndo mara nyingi husaidia watu wenye matatizo kama haya kurudi nyumbani wakatushauri cha kufanya so tukawasiliana na police wa MACAU na kuwaelezea tatizo zima na ndipo jana Jumamosi 5 April 2014 walifanikisha zoezi hilo kama inavvyo repotiwa hapa chini kwenye taarifa ya habari ya TDM ENGLISH NEWS ya MACAU:



Natoa wito kwa Serikali kupitia wizara yake husika kuliangalia kwa ukaribu hili suala na kuweza kuwaelimisha mabinti huko nyumbani juu ya mambo haya na athari zake. Yaelekea wengi wanapelekwa nchi za watu bila kuelimishwa vizuri au bila kuwa na ufahamu wa nini haswa wanaweza kukutana nacho huko. Tuna penda kuishukuru Serikali ya Macau kupita jeshi lake la Polisi kwa kuweza kuwafikisha katika vyombo vya sheria wahusika wa biashara hii harua ya Human Trafficking.

Kwame you're the best my brother may God bless you in whatever you do. Together we did it.

'We can all do something to fight for freedom'

Source:Jestina Blog

HALIMA KIMWANA AFUNGUKA KUHUSU MASTAA KUMTONGOZA DIAMOND

$
0
0
Aliyejipachika kuwa dada wa hiyari wa Mbongo-Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ ambaye ni zao la Shindano la Kimwana Manywele, Halima Haruna ‘Kimwana’ amefungukia ishu ya mastaa kibao kujitongozesha wenyewe kwa jamaa huyo

Halima Kimwana alielezea sakata hilo wikiendi iliyopita baada ya kuulizwa undani wa skendo inayomkabili ya kumkuwadia au kumtongozea Diamond kwa mastaa na kuwabadilisha kama nguo.
Kwa mujibu wa Halima Kimwana, huwa Diamond hajisumbui kumtongoza mwanamke zaidi ya hao mastaa kujitongozesha wenyewe kwake.

Halima Kimwana alidai kwamba yeye kama dada wa mwanamuziki huyo (hakutaka kufafanua dada kivipi), amefikia hatua ya kusumbuliwa na wasichana wa kila aina hasa mastaa wakimuomba awatongozee kwa Diamond tena kwa ahadi kemkemu.
“Kwani unafikiri Diamond anajihangaisha kuwatongoza hao mastaa? Wao ndiyo kila kukicha wanamsumbua na kutuhangaisha sisi wakitaka tuwatongozee kwa kaka yetu.

Tena wengine wanatoa ahadi nyingi tu kama tukiwafanikishia,” alisema Halima Kimwana na kuongeza kuwa katika listi hiyo ya mastaa wanaojitongozesha kwa Diamond, wapo mastaa wakubwa ambao anawahifadhi ili asiwavunjie heshima.

GPL

BABA DIAMOND "MWANANGU SI RIDHIKI YANGU...HANISAIDII KITU"

$
0
0
Baba Mzazi wa Mwanamuziki Maarufu na Mwenye Pesa nyingi Kutokana na Mziki Kuliko Wanamuziki Wote Bongo Diamond Amefunguka na Kuliambia Gazeti Moja hapa Bongo Kuwa Mwanamuziki huyu Si Ridhiki Kwake kwani Hamjali wala kumsaidia kama Baba yake ...Mpaka Leo haijulikani kwanini Diamond hamkubali huyu jamaa kama baba yake...Mapenzi yote amehamishia kwa mama yake ambae ndio aliyemleta toka akiwa mdogo......Diamond Msamehe Mzee Hata kama alikutosa ukiwa Mdogo......!!!

TAZAMA PICHA JINSI SHOW ROOM YA MAGARI KARIBU NA MLIMANI CITY ILIVYOUNGUA MOTO

$
0
0
Duka la Magari (showroom) iliyokuwa karibu na eneo la Mlimani City barabara ya Samnujoma jijini Dar es Salaam imeteketea kwa moto na kusababisha hasara ambayo bado haijafahamika, ambapo mpaka sasa chanzo cha moto huo hakijafahamika.
Magari yakiwa yameteketea kwa moto
Hapa moto ulikuwa ndiyo umeanza kuwaka kabla ya kuanza kuunguza magari.

WASANII/WATU MAARUFU BONGO AMBAO WAPENZI WAO HAWAJULIKANI

$
0
0

1. Martin Kadinda

Ni mwanamitindo maarufu apa bongo, na anayefanya vizuri kwenye tasnia hiyo, pia ni manager wa wema sepetu. Huyu amekuwa akipiga picha na warembo tofauti tofauti , ila haijawahi kuripotiwa popote mrembo anayetoka nae ata kwa kupakaziwa.

2. Salama Jabir

Huyu ni mtangazaji wa mkasi TV show, mbali na muonekano wake wa kuvutia ila hadi Leo haijawahi kuripotiwa mtu anayemmliki hata kwa kusingiziwa. 

3.Ben Pol

mwanamuziki classic wa bongo fleva, achilia mbali muonekano wake wa kuvutia , naye mpaka Leo mpenzi wake hajulikani, na wala haijawahi kuripotiwa popote kama ana mpenzi au la.

4. DJ Fettty

Huyu ni mtangazaji wa clouds FM, ana sura na umbo la kuvutia , ila hadi Leo haijulikani mtu anayekula mzigo nani, japo kwa kusingiziwa

5.Millard Ayyo

Mtangazaji machachari kutoka clouds FM, pamoja na utanashati wake ila haijawahi kuripotiwa popote kama yupo kwenye mahusiano na haijulikani mpenzi wake ni nani

6. B 12

Huyu kama ilivyo kwa Millard, hajawahi kuhusishwa na scandal yeyote ya kuwa kwenye mahusiano ya kimapenzi, haijulikani kama yupo au la.

7. Adam Mchonvu

huyu pia hajawahi kusikika au kuhusishwa na mahusiano ya aina yeyote.

8.Ally Rehmtulah

Mbunifu wa mavazi, naye huyu hajawahi kuhusishwa na wala haijuilikani kama ana mpenzi au la.

REDIO MPYA DAR 93.7 YAWANYIMA WATU USINGIZI..JE NI KWELI NI YA LADY JAY DEE?

$
0
0

Miezi ikapita, mawiki yakasonga hatimae siku, masaa na dakika zake zikapotea na sasa EFM inayopatikana katika masafa ya 93.7 imesikika hewani kwa majaribio kwa mara ya kwanza.

Redio hii iliobeba watangazaji mahiri, waandaaji wa vipindi wenye umakini, ma DJ wanao sadikiwa kuwa walishushwa kwa ajili ya kazi hii, uongozi thabiti na yenye usikivu mujarab, habari zake zilianza kupenya kwenye masikio ya washashi mwishoni mwa mwaka jana na kupelekea wamiliki na wadau wa redio nyengine kukosa usingizi na hata siku wakiupata basi huweweseka usiku na kupiga mayowe ama kujikuta wakikosa hata nguvu ya kuzuia haja ndogo kutoka.

Redio hii itadili kwa asilimia 85 na burudani...na watakaoongoza balaa hilo ni watu wenye kulijuwa game kwa kipindi kirefu saana na burudani iliolengwa hapa hakika ndio mwiba mchungu utaowatesa weengi waliowanyonya na kuwanyanyasa wasanii kwa miongo kadhaa sasa.
Kuna Minong'ono kuwa inamilikiwa na Lady Jay Dee....Kwa mwenye Ukweli Funguka Hapa basiiiii....

Nanga ndio imeshainuka, Unyonyaji ndio umekwisha, Wanyonge mtafarijika, Game sasa litabadilika, Walio Vilaza wataaibika, makini watasikika, Sina imani nina hakika.


MBINU MPYA YA KUSAFIRISHA MADAWA YA KULEVYA YANGUNDULIKA..WAJAWAZITO WATUMIKA

$
0
0
Baada ya Mambo kuwa magumu kwa wasafirishaji wa madawa ya kulevya ..sasa wamegundua njia mpya ya kusafirisha madawa ya kulevya kwa kuwatumia waja wazito kwa kuwa huwa hawakaguliwi kwenye x ray za airport ....siku za karibuni wamekamatwa wanawake kadhaa wajawazito ambao walikuwa wamemeza madawa ya kulevya ...Njia nyingine inayotumika ni kusafirisha madawa hayo kwa kutumia Cargo ambayo ni mizigo mikubwa ambayo huwekwa nyuma ya ndege chini .

MKE WANGU HAJAWAHI NIAMBIA NIMECHOKA..JE NI MWAMINIFU?

$
0
0
Nimekuwa nikimpa dozi za uhakika,nimekuwa nikimpiga romance za nguvu. namfikisha hata mara nne lakini haniambii kama kachoka bado anaguna utamu tu mpaka mimi nichoke.

Nimekuwa nikiwa na tabia ya kunywa wine au wisk siku za weekend kiasi kwamba hujikuta namsugua hata masaa matatu mpaka manne yeye hajawahi sema kama kachoka, nambadilisha staili nyingi zote anaenda tu mpaka pale ambapo mimi nafika nakuamua kupumzika.muda mwingine kama jmosi humsugua kama mara nne hapo home yeye kila nikumvuta nikipiga romance analainika namsugua hasemi kama kachoka.

sasa swali linalonijia kama kila nikitaka namsugua tu je ni mwaminifu huko kazini kwake? maana kama kila baada ya masaa mawili naweza msugua inamaanisha hata nikimsugua vipi huko kazini anaweza suguliwa tena maana inaonekana hachoki.Naombeni ushauri wadau.

By Mjali Tumbo

IZZO BUSINESS ALIGOMA KUMPIGIA KAMPENI RIDHIWANI JAPO ALIOMBWA KUFANYA HIVYO

$
0
0
Jumapili iliyopita (April 6), Ridhiwani Kikwete alitangazwa na tume ya Taifa ya Uchaguzi kuwa mshindi wa kiti cha ubungo wa jimbo la Chalinze mkoani Pwani.

Hii ilikuwa habari njema pia kwa Izzo Bizness ambaye aliwahi kumuimbia mbunge huyo ambaye ni mtoto wa Rais Kikwete akimtaka aongee na ‘mshua’ kuhusu hali halisi ya mtaani.

Izzo Bizness ameuambia mtandao wa Bongo5 kuwa tangu atoe wimbo huo amekuwa karibu na Ridhiwani kimawasiliano na hata wakati wa kampenzi za ubunge wa jimbo la Chalinze alimuomba amsaidie lakini alishindwa kufanya hivyo kutokana na hali ilivyokuwa kwa upande wake.

“Kuna vitu vidogo tu ambavyo tulipishana, niliangalia pia katika upande wangu. Hakikuwa kitu cha kusaidiana kimasihala kwa kuwa unapoamua kuingia kwenye kampeni kumsaidia mtu ujue ushaamua kutake risk. Na hapo mimi nilikuwa naenda kukipa tafu chama cha CCM lakini mimi natokea jimbo ambalo limeshikiliwa na CHADEMA na wananchi asilimia kubwa ni CHADEMA”. Amesema Izzo Bizness.

Source: Bongo5

AY KUKIPELEKA KIPINDI CHA TV MKASI SHOW KENYA

$
0
0
Mkasi ni kipindi cha TV kilichoanzishwa na msanii na mfanyabiashara Ambwene Yessaya aka AY, kipindi kilichojipatia umaarufu mkubwa nchini Tanzania.

AY yuko nchini Kenya ambako pamoja na mambo mengine ameenda kuzindua video yake mpya ya ‘Asante’ iliyotoka weekend iliyopita.

Kwa mujibu wa Nairobi Wire, AY ameenda Kenya na crew ya Mkasi ambao ni Salama Jabir na Josh Murunga, kwa ajili ya kuangalia fursa zinazoweza kupatikana nchini humo kwa lengo la kutaka kupanua wigo wa kipindi hicho.

“Tuko hapa kwanza kuangalia uwezekano wa kupanua biashara ya kipindi chetu” Alisema AY.

Wiki iliyopita msimu wa mkasi ulimalizika kwa Salama kumhoJi AY, na moja ya vitu alivyovisema AY kuhusu kipindi ni pamoja na hiki:

“Season inayokuja itakuwa ni revolution kama ambavyo tumefanya mwanzo…kwa kweli ni kuwa watu ambao wana akili zao watu ambao wana lengo moja kwa pamoja ni timu ambayo inafanya kitu pamoja na tunafanya kitu kimoja ambacho kinawafundisha na watu wengine”.

Msimu mpya wa Mkasi ambayo hurushwa kupitia EATV unatarajiwa kuanza Julai Mosi.
-Bongo5

NJEMBA YAMBAKA MTOTO WA MIAKA MINNE

$
0
0
Stori: Haruni Sanchawa, Nyemo Chilongani

NI AIBU!Jamaa mmoja anayejulikana kwa jina la Iddi Mgosi anashikiliwa na Polisi wa Kituo cha Wazo jijini Dar es Salaam kwa tuhuma za kumbaka mtoto mwenye umri wa miaka minne (jina linahifadhiwa) huko Mivumoni, Madale Machi 18, mwaka huu

Mgosi, ambaye umri wake haukuweza kupatikana mara moja, anadaiwa kumrubuni mtoto huyo kutoka nyumbani kwao na kumpeleka kwake, ambako alimuingilia kwa nguvu na baadaye kumtisha kutosema lolote kwa wazazi wake.

Mama mzazi wa mtoto huyo, aligundua mwanaye kuwa na maumivu makali wakati akimuogesha, kwani alipomshika sehemu zake za siri, binti huyo alipiga kelele za maumivu na alipoulizwa kilichomsibu ndipo alipoelezea alichofanyiwa.

Akizungumza kwa masikitiko makubwa, mama huyo aitwaye Hadija, alisema alikuwa akimuogesha mtoto wake huyo bila kugundua kwamba alikuwa amebakwa na kuharibiwa vibaya sehemu zake za siri. Alipomshika kwa ajili ya kumsafisha, mtoto huyo akaanza kulia na kulalamika kwamba alikuwa akimuumiza.

Bi Hadija alisema mara baada ya kuambiwa hivyo, akawaita ndugu zake na kuwasimulia alichoambiwa hivyo wote kwa pamoja wakachukua jukumu la kumfuata Mgosi, kumkamata na kumpeleka katika Kituo cha Polisi Wazo.

Baada ya kumuogesha binti yake, wakampeleka katika hospitali ya Mwananyamala alikochukuliwa vipimo kadhaa na kuambiwa wampeleke mtoto huyo katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili.
“Hospitalini walituambia kwamba sehemu zake za siri zimeharibiwa sana na hata kibofu chake cha mkojo pia kimeharibiwa kwani wametoa uchafu mwingi. Kwa sasa amelazwa hospitalini huku akiendelea kupatiwa matibabu na hawajajua ni siku gani ataruhusiwa.”

MTOTO AFUNGUKA
Waandishi wetu hawakuishia hapo, walimfuata mtoto na kumuuliza maswali kadhaa kwa lengo la kujiridhisha ambapo alisema:

“Mgosi alinichukua, akaniambia twende kwake, tulipofika huko akanivua nguo na kunilalia...ameniumiza,” alisema mtoto huyo huku akionekana bado kuwa kwenye maumivu makali.
Baada ya kumpeleka Mgosi katika kituo cha Wazo, aliwekwa rumande na kufunguliwa jalada la mashtaka WH/RB/1891/2014KUBAKA.
GPL

MASTAA MATAJIRI WACHUNGUZWA KISA MADAWA YAKULEVYA

$
0
0
Stori: MAKONGORO OGING’

KIMENUKA! Jeshi la Polisi Tanzania kwa kushirikiana na taasisi mbalimbali za serikali zimeanza kuwachunguza watu wenye majina makubwa ‘mastaa’ Bongo ambao wameibuka na utajiri wa ghafla, Uwazi limeambiwa.

Kwa mujibu wa chanzo nyeti ambacho kiko ‘jikoni’ kwenye jeshi hilo, mbali na mastaa, wengine ambao tayari orodha yao ipo ni wafanyabiashara, wafanyakazi wa serikali na viongozi wa dini ambao wameibuka kuwa mamilionea kwa muda mfupi huku shughuli zao za wazi zikiwa haziwezi kuwatajirisha.

BIASHARA YA MADAWA YA KULEVYA NDIYO KIINI CHA YOTE
Chanzo: “Imeonekana kuwa mastaa wengi wanaibuka kuwa na utajiri siku hizi, huenda wanajihusisha na kusafirisha madawa ya kulevya.

“Ndiyo maana wengi wao kila kukicha, mara wapo China, mara India, wengine wanakwenda mpaka Thailand. Hao wanachunguzwa kwa mtindo wa nyendo, kila mmoja ambaye yumo kwenye orodha ya jeshi amewekewa askari wawili wa kumfuatilia.”

KUKAMATWA
Chanzo hicho kikaendelea kusema kuwa wale ambao watathibitika kwamba biashara zao za wazi haziwezi kutoa utajiri wa ghafla watakamatwa na kuhojiwa.


DIDA AMESHAKAMATWA, AMESHAHOJIWA
Chanzo hicho kilieleza kuwa katika oparesheni hiyo maalum, watu kumi wameshakamatwa, akiwemo Mtangazaji wa Kituo cha Redio cha Times FM, Hadija Shaibu ‘Dida’.
“Watu kumi tayari wamekamatwa na kuhojiwa. Yumo yule mtangazaji Dida wa Mchops (siku hizi si wa Mchops). Saba wamekwenda na maji, watatu akiwemo Dida waliachiwa baada ya kuthibitika kwamba mali zao ni halali,” kilisema chanzo.

IKOJE KWA VIONGOZI WA DINI?
Chanzo kilisema kuwa kuhusu viongozi wa dini ambao nao wameibuka kuwa matajiri wa kutupwa, wamejenga mahekalu ya maana, nao wanachunguzwa na kati ya watu kumi waliokamatwa, yumo mchungaji mmoja (hakumtaja jina) ambaye aliachiwa.

“Lakini orodha ya hawa ni ndefu, kumbe wengi wanajihusisha na kuuza madawa ya kulevya. Nao wamewekewa askari wawiliwawili ambao wanaingia hadi kwenye ibada zao lakini wenyewe hawajui,” kilisema chanzo. 

JOTI WA KOMEDI  ATAJWA
Katika hali ya kushangaza, chanzo hicho kilidai kuwa staa ambaye alikuwemo kwenye orodha na akafuatiliwa na kuachiwa ni msanii wa Kundi la Orijino Komedi, Lucas Mhuvile ‘Joti’ ambapo ilidaiwa hakuonekana kuwemo kwenye cheni ya wauza unga nchini.

“Lakini hata hiyo orodha nyingine si kwamba wamehukumiwa kuhusika kufanya biashara hiyo ila wanachunguzwa,” kilisema chanzo hicho.

YAMEKUJAJE?
Hatua hiyo, kwa mujibu wa chanzo, imekuja kufuatia madai ya wananchi wengi kwamba matajiri waliopo mtaani wengi ni wauza unga ambao hufanya biashara hiyo waziwazi, wengine wakisema kuna polisi wanaojua kila kitu lakini kwa sababu wanakatiwa kitu kidogo wanawalinda.

“Si kwamba serikali haitaki watu wawe  na maendeleo makubwa, bali utajiri wao uwe wa wazi wenye vielelezo vinavyokubalika. Kwa sasa vijana wengi wakiwemo wasanii na wachezaji wanashindana kwa utajiri lakini baadhi yao ndiyo hivyo tena wamegundulika wanajihusisha na biashara ya madawa ya kulevya, wengine wamekamatwa nje ya nchi na wanakabiliwa na hukumu ya kifo,” kiliongeza chanzo hicho.

UWAZI LAWASAKA WALIOIBUKA NA UTAJIRI
Kama kigezo kikubwa ni utajiri wa ghafla, Uwazi liliwasaka mastaa ambao walishaandikwa na Magazeti Pendwa ya Global Publishers (likiwemo Uwazi lenyewe).

DIDA
Katika Gazeti la Ijumaa Wikienda toleo la wiki mbili nyuma kulikuwa na kichwa cha habari ukurasa wa mbele; UTAJIRI WA DIDA GUMZO.
Katika habari hiyo Dida alisema:

“Mimi sipendi kuanika vitu ninavyomiliki ila ni kweli nina nyumba mbili, moja Kigamboni na nyingine Goba ya gorofa. Magari ninayo matatu, hilo Vogue mchakato unaendelea, ukikamilika nitaliingiza nchini.
 “Kuhusu miradi yangu mingine siwezi kuianika hadharani kwa sababu, kwanza sipendi kabisa mambo hayo.”

Hata hivyo, Dida alikiri kukamatwa Machi, mwaka huu na kuhojiwa kisha kuachiwa. Alikuwa anakwenda Hong Kong, China.
GPL
Viewing all 104756 articles
Browse latest View live




Latest Images