Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104709 articles
Browse latest View live

WAFUASI wa CUF Wavamia Makao Makuu ya Chama Zanzibar

$
0
0
MTENDENI, ZANZIBAR: Wafuasi wa Chama cha Wananchi (CUF), Zanzibar leo wamevamia Ofisi za Makao Makuu ya Chama hicho yaliyopo eneo la Mtendeni visiwani humo wakitaka kufahamu hatma ya maamuzi yao ya Okt 25, 2015, ambapo chama hicho kinadai kilishinda uchaguzi kabla ya kufutwa.

DONEDEAL: Mrisho Ngasa Kasaini Mbeya City

$
0
0
Picha inayo-trend kwa sasa kwenye mitandao ya kijamii ni ya Mrisho Ngasa na afisa habari wa Mbeya City Dismas Ten ambayo inaashiria tayari nyota huyo wa zamani wa Yanga ameshakamilisha deal na ‘wagonga nyundo wa Mbeya’ Mbeya City.

Mwezi Septemba mwaka huu Ngasa alijiunga na Fanja FC inayoshiriki ligi kuu nchini Oman (Oman Professional League) ikiwa ni wiki tatu tu, baada ya kuvunja mkataba na klabu ya Free State Stars ya South Africa.

Nyota huyo wa zamani wa vilabu vya Kagera Sugar, Yanga, Azam FC na Simba vyote vya VPL hajadumu Oman na hatimaye amerejea tena nchini na kusajiliwa na klabu ya Mbeya City ambapo ataungana na kocha wake wa zamani Kinna Phiri aliyemsajili kutoka Yanga kwenda Free State Stars kabla ya kocha huyo kutimuliwa kufatia mfululizo wa matokeo mabovu.

Afisa habari wa Mbeya City Dismas Ten ame-post picha kwenye ukurasa wake wa Instagram akiwa pamoja na Mrisho Ngasa na kuandika maneno yanosomeka: “Mnapokamilisha jambo kutakiana heri ndio uungwana. Kila la heri anko @mrisho_ngasa_17.”

Habari za Ngasa kujiunga na Mbeya City zilianza tangu aliporejea nchini akitokea South Africa baada ya kuvunja mkataba na Free State lakini ghafla akaibukia Oman na kusajiliwa na Fanja FC siku chache baada ya klabu hiyo kumsajili mtanzania mwingine Danny Lyanga mshambuliaji wa zamani wa Simba.

Jana jioni zikaenea tena habari kwamba Mbeya City wameshakamilisha usajili wa Ngasa. Lakini uongozi wa klabu hiyo haukuwa tayari kuthibitisha badala yake ukasema utatoa taarifa rasmi, mwisho wa siku raundi ijayo ya VPL Ngasa atakuwa miongoni mwa wachezaji watakaokipiga Mbeya City.

NIMEFANYA Video Karibia 10 Lakini ya Diamond Mnaniuliza Kila Saa, Who is Diamond Motherf**** – Tunda

$
0
0
Tunda amechoka kuulizwa maswali kuhusiana na kuonekana kwenye video ya Diamond ya wimbo Salome aliomshirikisha Ray Vanny.

Ni kwasababu anajiuliza, iweje ameshaonekana kwenye video takriban 10, lakini tangu aonekane kwenye video ya Diamond, swali limekuwa lile lile na ni kama vile watu ndio wameanza kumuonea kupitia video hiyo.


Kutokana na kuchoshwa na swali hilo, Tunda anayedaiwa kurudiana na mpenzi wake Young Dee, amempa jibu kavu mtangazaji wa Jembe FM, Natty E aliyemrushia swali lile lile limkeralo.

“Nimefanya video ngapi? Nimefanya video karibia 10 lakini hii ya Diamond mnanifanyia interview kila saa,” Tunda alimjibu Natty.

“Diamond, Diamond, who is Diamond motherf*cker. Weka hiyo kwenye gazeti lako,” aliongeza.

Natty alijikaza na kumjibu ‘Anyway, Unaweza acha hilo swali la kuhusu Diamond, it’s not a big deal.’

Tunda alijibu kikauzu zaidi, “Maswali yote jibu lake ndio hilo.”

Anachoshindwa kukielewa Tunda ni kuwa kushiriki kwenye Salome ya Diamond ni hatua kubwa zaidi katika career yake so far hivyo swali hilo hawezi kulikwepa! Hadi sasa video hiyo ina views milioni 9.2 na ni video ya Diamond inayopata views nyingi kwa kasi kuliko zote alizowahi kutoa.

Fredrick Bundala

JINSI Ya Kumtext Mwanamke Hadi Akupigie Simu Wa Kwanza

$
0
0
Kutumia sms kuanzia wiki hadi mwezi bila kupiga simu ni VIBAYA. Unahatarisha kuitwa boyfriend wa sms, na labda hautakuwa boyfriend wake wa ukweli. Kuondoa hizi athari unapaswa kutumia maujanja haya matatu.

Mbinu #1: Toa majibu yasiyokuwa moja kwa moja.
Wanawake wanapenda majibu ya moja kwa moja kama wanataka kujua kitu flani kutoka kwako. Mwanamke anaweza kukuuliza "Wewe unafanya kazi gani?" ama "Uko na tatoo kwa mwili wako?" Usijibu maswali haya moja kwa moja. Badala yake mzungushe  kwa kumwambia "Mimi ni jasusi siku za juma halafu wikendi nafanya kazi kwa club kama bausa." Kama ataudhika na jinsi umekataa kujibu swali lake moja kwa moja, unaweza kumwambia "Nitakwambia tukikutana" ama "Nitakwambia wakati tunaongea kwa simu."

Mbinu #2: Mtumie meseji ya utani kama hakukujibu.
Kama atashindwa kukutumia meseji baada ya lisaa moja, mwambie "Umefutwa kazi." Atakupigia na kutaka kujua ni kwa nini umemwambia hivyo na atataka ueleze kwa upana umemaanisha nini.

Mbinu #3: Weka ratiba ya kupiga simu.
Kama mnatext na moto, kama vile anareply texts zako chini ya dakika moja baada ya kumtumia text, katiza maongezi yanu kwa kumwambia "Hey, nataka kwenda, lakini nitakupigia simu kesho jioni." Kama utafanya hivi vile inavyotakikana atataka akupigie wewe simu na atakuwa active wakati wote.

Wakati unatimiza mbinu hizi, kuna sheria ambazo unahitajika kufanya ili akuheshimu wakati wote.

Sheria #1:  Moja kwa moja - Anapaswa kutuma angalau jumbe mmoja kwa kila jumbe ambayo utamtumia.

Sheria #2: Kama hatajibu meseji yako moja, usimtumie meseji siku nzima. Kama hatajibu meseji yako ya pili usimtumie jumbe wiki nzima.

Sheria #3: Usimtext ukimwambia jinsi unahisi vibaya kwa kuwa anakataa kujibu meseji zako badala yake umpigie simu na umsunze kuhusu simu yake.

Waweza kusema "Hi, najua kuna kampuni ambayo itakulipia bili ya wiki nzima ya mjazo wako wa simu kwa kufanya kazi mfano wa mhudumu wa hoteli. Je unataka nikuunganishe?

Kwa kutumia mbinu hizi tatu + hizi sheria tatu utakuwa uko sawa katika gemu ya kutext.

NB Mbinu hizi zitafanikiwa kirahisi iwapo umejenga tenshen ya kimapenzi kati yako na mwanamke. Hivyo kama unaanza kumtext mwanamke siku ya kwanza mbinu hii haitafanikiwa.

By Nesi Mapenzi

NISHA Akanusha Kupewa Mimba na Nay wa Mitego

$
0
0
Baada ya msanii wa filamu Salma Jabu, Nisha kulalamika kubakwa na kupewa mimba na msanii wa muziki na baadaye kudai msanii huyo ameikataa mimba hiyo. Mashabiki katika mitandao ya kijamii walidhani mimba hiyo ni ya Nay wa Mitego hali ambayo ilimfanya rapa huyo kukanusha uvumi huo.


Rapa huyo kupitia kipindi cha U head cha Clouds FM amekanusha kumpachika mimba mrembo huyo huku akidai hajaonana naye kwa kipindi cha miaka 3.

“Mimi sielemi nimeshirikishwaje kwenye suala la mimba, tena naambiwa nimembaka, hivi mimi ninavyogombaniwa na wanawake naanzaje kumbaka?,” alisema Nay wa Mitego.

Baada ya kauli hiyo, muigizaji huyo wa filamu za vichekesho ameweka mambo sawa kupitia Instagram yake kwa kusema kuwa hakuwai kusema kuwa ana mimba ya mpenzi wake huyo wa zamani, Nay wa Mitego.

“Naywamitego iko hivi kabla hujaandika kitu chunguza sio unakurupuka tu na kuandika ujinga. Ulinisikia na kuniona wapi nimekutaja kwamba wewe ndo baby dady wangu???? hivi naanzaje kuzaa na wewe Nay?? kifupi pamoja na mapungufu na makosa yaliyojitokeza kwa baba k wangu humfikii hata kwa kucha labda umemshinda hizo tatoo zako kama bibi harusi. Nikuombe msamaha kwa kipi acha kudandia treni kwa mbele.??? tena watishe hao hao WANAUME SURUALI mimi simuogopi yeyote anayekojoa akiwa amesimama wala amechutama,” aliandika Nisha

NAFASI za TTCL na Nyingine Nyingi Zilizotangwa Katika Magazeti Leo

$
0
0

BREAKING News: Bifu la Lady Jay Dee na Clouds Lazikwa Rasmi..Management ya Jay Dee Yaruhusu Clouds Ipige Nyimbo zake Iwezavyo

$
0
0
Unaambiwa Kwa Sasa hakuna cha Komando wala nini, ile bifu kubwa kuwahi kutokea kwenye game ya Bongo Flava kati ya Clouds FM na Lady Jay Dee imezikwa rasmi baada ya Uongozi wa Lady Jay Dee Kuruhusu kituo hicho cha radio kupiga nyimbo za Lady Jay Dee iwezavyo kuanzia sasa...

SCORPION Akana Hoja 6, Akiri Hoja 3 Ikiwemo Kupata Mafunzo ya Kareti

$
0
0
MSHITAKIWA katika kesi ya unyang’anyi wa kutumia silaha, Salum Njwete (34) ‘Scorpion’, amekiri kupata mafunzo ya kareti kutoka chuo cha mafunzo cha Ifakara aliyoyafanya mwaka 1989 hadi 1995.

Aidha, upande wa mashitaka katika kesi hiyo umemuongezea mashitaka ya shambulio kupitia kifungu namba 234 cha Sheria ya Makosa ya Jinai ambacho kinaruhusu kuongeza au kubadilisha mashitaka.

Wakili wa Serikali, Nassoro Katuga alidai jana mbele ya Hakimu Mkazi, Flora Haule kwamba kesi hiyo imekuja kwa ajili ya mshitakiwa kusomewa maelezo ya awali ambapo katika maelezo ya zaidi ya saa nane, alikiri kuhusu jina lake, sehemu anayoishi ya Machimbo Yombo na mafunzo hayo.

Hata hivyo, alikana kuhusu jina la Scorpion, mashitaka yake na kwamba hakukamatwa wala kuhojiwa na Polisi kuhusu mashitaka hayo.

Katuga alidai kuwa Septemba 6, mwaka huu, mshitakiwa alikuwa maeneo ya Buguruni Sheli na kwamba Septemba 12, alihojiwa na kukamatwa na polisi maelezo ambayo aliyakana.

“Mashahidi watakaotoa ushahidi katika kesi hii wapo sita ambapo upande wetu wa mashitaka utawasilisha vielelezo viwili ikiwemo Fomu namba tatu ya Polisi (PF3) na ripoti ya daktari kwa ajili ya kuthibitisha mashitaka hayo,’’ alidai Katuga.

Hakimu Haule aliahirisha shauri hilo hadi Desemba 14 mwaka huu, kesi hiyo itakapokuja kwa ajili ya kusikilizwa. Katika mashitaka yake, mtuhumiwa inadaiwa alitenda kosa hilo Septemba 6, mwaka huu katika maeneo ya Buguruni Sheli, wilaya ya Ilala.

Inadaiwa, Njwete aliiba mkufu rangi ya fedha wenye uzito wa gramu 34 wenye thamani ya Sh 60,000, bangili ya mkononi na fedha taslimu Sh 331,000, vyote vikiwa na thamani ya Sh 476,000 mali ya Said Mrisho.

Inadaiwa kabla na baada ya wizi huo, alimchoma kisu machoni, tumboni na mabegani mlalamikaji ili ajipatie mali hizo.


MSAJILI wa Hazina Atoa Ufafanuzi Kuhusu Fedha Kukauka Mifukoni Mwa Watu Pamoja na Sababu za Benki Kulalamika Kufilisika

$
0
0
Msajili  wa Hazina nchini, Lawrence Mafuru amesema benki nchini zinashindwa kueleza ukweli juu ya kuyumba kwao na kwamba madai ya kuwa hali zao ni mbaya kutokana na agizo la serikali la kutaka fedha zake zitunzwe Benki Kuu ya Tanzania (BoT), hazina ukweli.

Mafuru amesema taarifa ambazo serikali wanazo ni kwamba benki hizo zaidi ya 50 zimekopesha fedha nyingi kwa watu mbalimbali, lakini marejesho ya madeni hayo yamekwama kiasi cha kusababisha benki hizo ziwe katika hali hiyo.

Akizungumza jana Dar es Salaam, Msajili wa Hazina licha ya kukiri kuwa mzunguko wa fedha umepungua kutokana na Tanzania kuchagua kwamba fedha inazozipata zitumike katika miradi ya maendeleo badala ya matumizi ya kawaida, benki zinazolalamika zimeshindwa kurejesha fedha ilizokopesha watu na taasisi mbalimbali.

Akizungumzia taarifa zinazoenezwa kwamba benki zimekosa fedha za kujiendesha, Mafuru alisema taarifa walizozipata ni kwamba Septemba mwaka huu, benki hizo zaidi ya 50 nchini zimekopesha zaidi ya Sh trilioni 16.3 kwa watu mbalimbali.

Hata hivyo, alisema kati ya fedha hizo, Sh trilioni 1.43 zimekopeshwa bila ya kurudishwa katika benki husika na kwamba benki hizo zinashindwa kueleza ukweli uliopo badala yake wanalalamika kwamba hatua ya serikali kuamua fedha zake zitunzwe BoT badala ya katika benki za kibiashara, ndio sababu ya hali yao (benki) mbaya.

Kwa mujibu wa Mafuru, serikali imeamua kuchukua uamuzi huo wa kuzitoa fedha zake kutoka katika benki mbalimbali za kibiashara nchini kwa ajili ya kuwezesha serikali kujua mapato wanayopata kutoka katika taasisi zake.

Msajili wa Hazina amesema zaidi ya Sh bilioni 515 zimeingizwa BoT baada ya uamuzi huo wa Serikali ya Awamu ya Tano ambao ulitangazwa na Rais John Magufuli baada ya kushika madaraka mwaka mmoja sasa.

Mafuru alikiri kuwa ni kweli kwamba mzunguko wa fedha umekuwa mdogo na kueleza kuwa chanzo chake si kwamba benki zimekosa fedha kwa ajili ya kujiendesha.

Alifafanua kuwa awali watu wengi walitegemea safari na posho ambazo baada ya chenji kubaki, walikuwa wakitumia bila ya malengo, lakini sio kwamba mzunguko huo wa fedha unawaathiri watu wote.

“Tumeona tusitegemee wahisani badala yake tujiwekeze katika miradi mikubwa ya maendeleo ambayo kwa sasa haitaonekana, lakini baadaye itasaidia kuondoa nafasi iliyopo sasa,’’ alisema Mafuru.

“Tayari shilingi bilioni 515 zimeingizwa BoT na mpaka Septemba mwaka huu fedha hizo zilikuwa kwenye akaunti hiyo. BoT ni sehemu ya mfumo wa benki, kwani itakuwa inafanya kazi ya kukopesha kama zilivyo benki nyingine,” alifafanua Mafuru ambaye ofisi yake inasimamia mashirika na taasisi za umma.

Alifafanua kuwa ofisi yake ambayo ina jukumu la kusimamia mapato na matumizi, awali walikuwa wanapata shida kupata taarifa za mapato na matumizi katika benki hizo zilizopo kila kona nchini na kwamba baada ya BoT kuchukua dhamana hiyo, imewasaidia, kwani wanaandika barua na kupatiwa taarifa hizo kwa muda mfupi.

Alisema serikali inategemea mapato yake kutoka katika makundi matatu ambayo ni Serikali Kuu, Serikali za Mitaa na kupitia mashirika na taasisi mbalimbali.

Alisisitiza kuwa itasaidia kujua mashirika hayo zaidi ya 260 namna wanavyotumia fedha zake katika miradi mbalimbali na kwamba suala la kuchukua fedha bila ya kuzitumia lisiwepo.

BAADA ya Weusi Kuwa na Kigugumizi Kuhusu Lord Eyes..Baraka The Prince Aamua Kumchukua Kwenye Lebo yake

$
0
0

Na mwimbaji wa bongofleva Baraka The Prince ameingia kwenye headlines za kusimamia wasanii na sasa kaanzisha Label iitwayo BANA itakayosimamiwa na watu wawili ambao ni Baraka na mpenzi wake Naj.

BANA tayari imeshafanya mazungumzo na kujiweka kwenye mstari wa kufanya kazi kwa kuwasimamia Wasanii watatu akiwemo Rapper Lord Eyes

SABABU za Kuanguka kwa Ndege ya Brazil Zatajwa, Mnusurika Aaanika Mazito!

$
0
0
Ndege iliyokuwa imewabeba wachezaji wa timu ya mpira kutoka nchini Brazil ambayo ilipata ajali nchini Colombia inasemekana kwa muujibu wa taarifa zilizovuja ndege hiyo iliishiwa mafuta kutoka katika kifaa cha kurekodia mawasiliano.

Katika mnara wa mawasiliano ya ndege, rubani alisikika akirudia mara kadhaa akiomba ruhusa ya kutua kwa dharura kutokana na hitilafu ya umeme iliyokuwamo ndegeni pamoja na kuishiwa mafuta ya ndege.

Kabla hata mawasiliano hayo yaliyorekodiwa kufikia mwisho, rubani alisikika akisema yuko angani umbali wa futi elfu tisa sawa na mita elfu mbili mia saba na arobaini na tatu.Taarifa za mawasiliano hayo zimekuwa gumzo katika mitandao kadhaa nchini Colombia na hata katika vyombo vya habari nchini humo, na hivyo kumekuwepo fununu za taarifa hizo kuwa huenda zikawa na chembe ya ukweli kwamba kuishiwa kwa mafuta ndiyo chanzo zha ajali ya ndege hiyo.


Wanajeshi wa Colombia waliliambia shirika la habari la AFP, kwamba pamoja na ndege hiyo kuanguka kuna shaka juu ya ajali hiyo kwani pamoja na ndege hiyo kuanguka hakukuwa na mlipuko wowote na kwamba huenda kulitumika nguvu ingine tofauti na nadharia ya kwisha kwa mafuta ndegeni.

Wadadisi wa mambo na wachunguzi bado hawako tayari kufungua mdomo na kuzungumzia juu ya chanzo chochote cha ajali hiyo na kwamba taarifa kamili ya uchunguzi itatolewa baada ya miezi kadhaa.

Wachezaji wa timu ya Chapecoense walikuwa safarini kuelekea nchini Colombian kwenye mji wa Medellin mahali kulikotarajiwa mechi kubwa ya mpira wa miguu ya kihistoria na badala yake wachezaji hao wameacha historia .Kufuatia vifo vya wachezaji wa timu hiyo, ulimwengu mzima umeungana kuomboleza vifo vyao.kifaa-cha-ndege

Kwa muujibu wa taarifa zilizopatikana kutoka katika shirika la ndege la Lamia watu wanne waliokuwa wasafiri na ndege hiyo wameponea chupuchupu kuwa miongoni mwa waliokufa baada ya kukosa tiketi.

Mmoja wa manusura wa ajali hiyo ambaye ni fundi wa ndege Erwin Tumiri, ameeleza namna alivyokwepa kifo, kwamba yeye alifuata maelekezo yote ya namna ya kujiokoa ,anasema abiria wenzie , walio wengi walisimama na kuanza kupiga kelele nay eye aliamua kuweka sanduku lake la kusafiria kati kati ya miguu yake na kuamua kubaki hivyo.

Visanduku viwili vya mawasiliano vya ndege hiyo vyote vilipatikana na tayari vimeanza kufanyiwa uchunguzi na wataalamu wa masuala ya anga.

Wachunguzi wataalamu kutoka nchini Uingereza wanasaidiana na mamlaka za Amerika Kusini kwasababu ndege iliyopata ajali ilitengenezwa na wana anga wa Uingereza BAE nchini Uingereza.Brazil imeanza siku tatu za maombolezo wakati maelfu ya watu na washabiki wa timu ya Chapecoense wako katika mji yaliko makao makuu ya timu hiyo Chapeco wanaendelea mkesha wa maombolezo wakati maandalizi ya kuchukua mabaki ya wachezaji hao inafanywa na jeshi kurejeshwa Brazil ili kuzikwa kwa pamoja katika uwanja wa Chapeco.

Nchi ya Bolivia tayari imekwisha tuma ndege ya kuchukua mabaki ya raia wake waliokufa katika ajali hiyo nchini Colombia.

Timu hiyo iliandika historia ya mafanikio katika soka kwa kuwa kileleni mwa ligi ya Brazil kwamara ya kwanza mwaka 2014.Kati ya watu 77 waliokuwa wameabiri ndege hiyo miongoni mwao ni watu sita tu ndiyo walionusurika .Abiria walio wengi walikuwa ni wachezaji wa timu ya Chapecoense na waandishi habari wapatao ishirini walikuwa miongoni mwa walipoteza maisha.

JIKE DUME Lilivyokamatwa Baada ya Kuwatapeli Wanaume Wakware Wakijua Mwanamke Kamili

$
0
0
Uganda: DUNIANI kuna mambo! Kijana Ivan Bebeto (28) yamemkuta ya kumkuta baada ya hivi karibuni kushikiliwa kwenye Kituo cha Polisi cha Katwe jijini Kampala kwa madai ya kuwatapeli wanaume kwa kujifanya ni mwanamke ‘jike dume’ huku akivaa mavazi ya kike, kujipodoa na  kuvaa mawigi.

Habari zilizotua kwenye dawati la Wikienda zinadai kuwa, jike dume huyo hufanya biashara katika nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki hususan jijini Kampala (Uganda), Bujumbura (Burundi), Nairobi (Kenya) akitokea pia Dar es Salaam (Tanzania).

ANATUMIA JINA LA QUEEN

Kwa mujibu wa chanzo, Ivan baada ya kujibadili na kuwa katika mwonekano wa mwanamke hujiita Queen kwa maana ya jina la kike, wanaume wengi wanaomjua akiwa hivyo humwita kwa jina hilo.

“Uzuri wake si rahisi kutambua kuwa ni mwanamke  kwani  amekuwa akijipamba, anatumia manukato ya kike na anapoingia kwenye klabu za usiku, hujichanganya na warembo wengine waliotoka kwenda viwanja ili kutofahamika kuwa ni mwanaume,” kilisema chanzo.

SASA MKASA WAKE WA KUKAMATWA NI HUU

Mkasa mzima wa kukamatwa kwa jike dume huyo hivi karibuni nchini Uganda ulianza pale alipokutana na  mwanaume mmoja ambaye hakujulikana jina mara mmoja.

Mwanaume huyo alitokewa na ‘Queen’, akaingia mzimamzima na baada ya mazungumzo, aliamua kumlipa kabisa chake na kumtaka waende kwenye nyumba ya wageni ‘gesti’ moja jijini Kampala kwa ajili ya kumalizana kama makubaliano yao yalivyo.

AKATAA KWENDA NYUMBA YA WAGENI

Inadaiwa kuwa, baada ya malipo hayo ambayo kiasi cha pesa hakijatajwa, Bebeto alikataa kwenda nyumba ya wageni na kumtaka mteja wake huyo waende kwenye nyumba aliyodai kuwa, huwa anahifadhia mizigo yake huku akimsisitizia kuwa atafurahi kwa sababu watakuwa wote usiku mzima.

ASHTUKIWA

Ikazidi kudaiwa kuwa, kutokana na mtazamo wake, mwanaume huyo alimshtukia Bebeto kwamba anaweza kuwa mtu mbaya, ndipo aliamua kuwajulisha polisi wa kituo hicho ambao walifika haraka sana kumkamata.

MAMBO HADHARANI

Baada ya tukio la kukamatwa, ndipo aligundulika kuwa, Bebeto ni kidume na si mwanamke na hajawahi kuwa mwanamke tangu azaliwe hali ambayo iliwashangaza na  polisi wenyewe.

WATU KIBAO KITUONI

Habari za mwanaume kukamatwa kwa madai ya kujibadili kuwa mwanamke ili apige pesa zilisambaa kwa kasi, watu wa eneo hilo wakakusanyika kituoni Katwe kwa ajili ya kumshuhudia Bebeto na kila aliyemuona hakuamini kutokana na uzuri aliokuwa nao lakini alipovua wigi alionekana kichwa chake halisi ingawa hata kama asingekuwa na wigi bado ilikuwa vigumu kumjua ni ‘meni’ mpaka kumchunguza.

AFUNGULIWA RB

Polisi wa Kituo cha Katwe waliamua kumfungulia kesi kijana huyo yenye faili la kumbukumbu REF65/04/11/2016 ambapo ameshikiliwa mpaka gazeti hili linakwenda mtamboni.

GPL

MAJINA ya Wadaiwa Sugu Shirika la Nyumba yatua Kwa JPM

$
0
0

SHIRIKA la Nyumba la Taifa (NHC), limewasilisha ripoti ya wadaiwa sugu wa shirika hilo, zikiwamo wizara, taasisi za Serikali na watu binafsi kwa Rais Dk. John Magufuli, huku wizara mbili zikiwa na deni kubwa.

Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, Mkurugenzi wa Mikoa na Utawala wa NHC, Raymond Mndolwa, alisema uamuzi huo umekuja baada ya Rais Magufuli kuwataka kukusanya madeni hayo na kuwasilisha taarifa hiyo ofisini kwake ili aweze kuipitia.

Mndolwa alisema NHC ilitoa notisi ya siku 90 ambayo ilianza  Septemba, mwaka huu, huku wadaiwa hao wakitakiwa kulipa madeni  ndani ya muda uliopangwa.

Alisema kuwa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Wazee, Jinsia na Watoto na Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo bado zinadaiwa kiasi kikubwa cha fedha, licha ya kuwapo kwa mazungumzo ya kulipa madeni yao.

“Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Wazee, Jinsia na Watoto inadaiwa Sh bilioni 1.4, huku wakilipa Sh milioni 300, wakati Wizara ya Habari, inadaiwa Sh bilioni 1.14, lakini imelipa Sh milioni 700,” alisema Mndolwa.

Mndolwa alisema shirika hilo hadi sasa limekusanya Sh bilioni 5.9 kati ya Sh bilioni 9.3 ambalo ni deni la Serikali kupitia wizara na taasisi mbalimbali, huku Sh bilioni 2.5 zikikusanywa kutoka kwa wadaiwa binafsi ambao awali walikuwa wanadaiwa Sh bilioni 4.

Alisema lengo la shirika hilo ni kuhakikisha madeni yanalipwa ili fedha hizo ziweze kutumika kwenye shughuli nyingine za maendeleo, ikiwamo ujenzi wa nyumba za kisasa 300 mkoani Dodoma.

Alizitaja wizara zinazodaiwa ni Wizara ya Katiba na Sheria, Wizara ya Fedha na Uchumi, Wizara ya Uchukuzi, Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi na iliyokuwa Wizara ya Ujenzi.

Wadaiwa wengine ni Ofisi ya Waziri Mkuu, Hospitali ya Taifa ya Muhimbili na Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC)

Mambo Yazidi Kuwa Magumu kwa Wadaiwa Bodi ya Mikopo, Sasa Kukatwa 15% ya Kipato Chao kwa Mwezi

$
0
0

MAMBO yanazidi kuwa magumu kwa wadaiwa wa mikopo ya elimu ya juu baada ya asilimia ya marejesho ya mkopo huo kwa kila mwezi kuongezeka kutoka 8% hadi 15%.

Mabadiliko haya yamekuja baada ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Magufuli kuwa tayari amekwishasaini mabadiliko ya sheria yanayomtaka mwajiri kukata asilimia 15 ya mshahara wa mwajiriwa ambaye ni mnufaika wa mkopo wa elimu ya juu kwa ajili ya kulipa deni lake analodaiwa na Bodi ya Mikopo.


Hatua hii imekuja ikiwa wadaiwa hao tayari wamepewa siku 30 na Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu, Abdul Razaq, aliyesema wadaiwa hao sugu watachukuliwa hatua kali iwapo hawatarejesha mikopo hiyo ndani ya mwezi mmoja.

Katika maelezo yaliyotolewa jana na Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi Mhandisi Stella Manyanya, wakati akijibu maswali ya wananchi kupitia kipindi cha KIKAANGONI kinachoendeshwa kupitia mtandao wa facebook wa East Africa Television, Naibu Waziri Manyanya alisema sheria hiyo tayari imesainiwa na siku za hivi karibuni itaanza kutumika.

“Hii asilimia 15, kimsingi ninavyofahamu ilishasainiwa, baada ya hapo kuna kuiangalia iendane na kanuni zetu, baada ya kuicheki imeendana na kanuni zetu kama kuna sehemu itahitaji kuboreshwa kidogo haitazidi miezi miwili au mitatu, baada ya hapo tutaweza kutumia hiyo 15%, na asilimia 15 ya safari hii ni tofauti na siku za nyuma, siku za nyuma tulikuwa tunachaji asilimia 8”, alisema Manyanya.

Hapo awali wadaiwa hao wa mikopo walikuwa wanakatwa asilimia 8, lakini sheria ya sasa itaruhusu wadaiwa wa mikopo ya elimu ya juu kukatwa asilimia 15 ya kipato chao.

Pia Manyanya amesisitiza kuwa kwa wale ambao hawajaajiriwa, lakini wanafanya biashara zao wanatakiwa kuwasilisha angalau shilingi 120,000 kila mwezi na kuwashauri kuwa ni vema wakapeleka zaidi ili wamalize haraka madeni yao.

Kuhusu wasio na kazi, amesema haiwezekani mtu asome halafu akose shughuli ya kufanya na kuwataka kutafuta shughuli yoyote ya kufanya ili waanze mapema kulipa madeni yao ndani ya miaka miwili baada ya kuhitimu masomo.

Ziara ya Uingereza ya Diamond na Ne-Yo yasogezwa mbele

$
0
0

Kama ulijipanga kufuatilia ziara ya Diamond na Ne-Yo ya nchini Uingereza mwezi Disemba mwaka huu basi jipange upya. Ziara hiyo imesogezwa mbele.

Kwa sasa ziara hiyo itaanza Machi 29 na kufikia mwisho April 8 ya mwakani. Awali ziara hiyo ilitarajiwa kuanza Jumatano ya Disemba 7 kwenye ukumbi wa Clasgow Barrowland na kufikia mwisho Disemba 14 ya mwaka huu.

Kupitia mtandao wa Instagram, Ne-Yo ameandika, “The December dates have been postponed! But don’t worry U.K. I’m still headed your way with NEW DATES and my bro @diamondplatnumz. 2017, let’s turn up! Tickets available at RoboMagicLive.com #NEYOUKLive.”

Naye meneja wa Diamond, Sallam kupitia mtandao huo ameandika, “UK New Dates…!! @neyo and @diamondplatnumz 😎.”

TAHARUKI...Panya Road Wavamia Nyumba na Kupora..Majirani Washindwa Kusaidia

$
0
0

DAR: Kundi kubwa la vijana wanaosadikika kuwa ni 'Panya Road' wavamia nyumba moja na kupora vitu mbalimbali usiku wa kuamkia leo.

Inadaiwa kuwa mhanga wa tukio hilo alijaribu kuomba msaada kwa majirani bila mafanikio kwakuwa majirani hao waliogopa kutoka na kupambana na Panya Road hao.

Mmoja wa majirani amenukuliwa akisema kuwa Vijana hao walikuwa na Mapanga Marungu, Jambia na Baruti walizokuwa wakizilipua ili kutisha watu kuwa ni Risasi.

NUHU Mziwanda Aonyesha Live Ujauzito wa Mke Wake....

$
0
0

Mziwanda sio mtu wa sport sport.. ashafanya yake. ..na sasa ni baba Kijacho.!!! Raha iliyoje😛😛😛😛

SIMU za Smart Phone Zimetufanya Tupoteza Ubinadamu....

$
0
0

IT'S VERY SAD....hapa ndipo tulipofikia. Juzi nipo katika gari mzee aliyekuwa na baskeli aligongwa AKIWA KATI YA BARABARA...Watu wanapiga PICHA huku wakitania...ATAKUWA AMEVUNJIKA KIUNO(mocking).. Huku wengine wakijipiga Selfie Badala ya Kumsaidia .....Very sad. You DON'T KNOW UR TOMORROW

UTAFITI: Ripoti ya Taasisi ya Twaweza Yaonyesha Asilimia 92 Wanataka Bunge Live

$
0
0

UTAFITI: Ripoti ya Taasisi ya Twaweza yaonyesha asilimia 92 ya wananchi wanapendelea vipindi vya Bunge kuonyeshwa moja kwa moja.

Pia katika utafiti huo asilimia 65 wanasema Vyombo vya Habari havijawahi au kama vimeshawahi, ni mara chache sana vimekuwa vikitumia vibaya uhuru wake kwa kutangaza vitu ambavyo si vya kweli.

Utafiti pia unaonyesha wananchi wanaunga mkono kwa kiasi kikubwa uhuru wa maoni na kupata taarifa. Karibu wananchi wote (95%) wanasema wananchi wawe huru kuikosoa serikali pale ambapo wanaona imekosea.

NIKKI MBISHI Akutana Live na Chid Benzi na Kuandika Haya...." He is Finished"

$
0
0
Nikki Mbishi Aka BabaMalcom amedai kuwa amekutana na Mwanamuziki Mwenzake Chid Benz na kudai kuwa amekwisha, Akiwa na maana ana hali mbaya nadhani kutokana na matumizi ya Madawa ya kulevya...
Ameandika hivi kwenye ukurasa wake wa facebook:

Nikki Mbishi BabaMalcom: "I met Chid Benz,damn he's finished!"

Chid Benz amekuwa katika matumizi ya madawa ya kulevya muda mrefu sasa, Babu Tale alijitolea kumsaidia lakini nadhani imeshindikana kwani kuna tetesi kuwa jamaa karudi kwenye matumizi ya madawa hayo
Pichani ni Chidi Benzi, Akiwa Rehab Bagamoyo ambapo alikaa mwenzi mmoja na kuondoka
Viewing all 104709 articles
Browse latest View live


Latest Images