Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104789 articles
Browse latest View live

BIF la Jokate na Flavian Matata Linapamba Moto Chinichini, Kisa?

$
0
0
Bifu la Jokate na Flavian Matata linazidi kukua siku baada ya siku. 

Chanzo ni Jokate kuiba idea ya Flavi ya kutengeneza mabegi ya mgongoni kisha kutangulia sokoni. Sasa imebaki ni vijembe mtindo mmoja kwenye social media. 



PENDEZA na Markson Beauty Products...Kukuza Makalio, Kungarisha Ngozi na Kwa Wanaume Kukuza Cassava

$
0
0

HABARI NJEMA
MARKSON BEAUTY
PRODUCTS

Baada ya kupata cheti cha bidhaa bora kwa mwaka 2015-2016, Sasa kampuni hii inasambaza huduma zake ndani na nje ya nchi kwa vibali maalum. Bidhaa zetu zimetengenezwa kwa mimea na matunda na kudhibitishwa. Hazina kemikali wala madhara.

DAWA ZETU NI YA:-
1. kurefusha nywele na kuzuia kukatika ovyo @100,000/=
2. Kuongeza shepu (hips na makalio) kwa/= (a)Dawa ya kunywa au kupaka @150,000/=
(b)Vidonge @170,000/=
3. Kuwa mweupe na softi mwili mzima kwa:- (1)Mafuta @100,000/=
(11)Vidonge @150,000/=
4. Kupunguza unene na manyama uzembe @120,000/=
5. Kuongeza uume pamoja na nguvu za kiume kwa:-
(a) Gely ya kupaka @120,000/= (b) Vidonge maalum @120,000/= (c) Handsome up original @170,000
6. Kuondoa mvi milele zisiludi tena @100,000/=
7. Kuongeza unene wa mwili mzima na uzito @120,000/=
8. Kupunguza tumbo (kitambi) na nyama za pembeni kwa:-
(a) Dawa ya kunywa au kupaka @120,000/= (b) Mkanda wa kawaida @100,000/= (c) micro-computer belt unaovaibret @200,000/=
9 .Kupunguza maziwa na kuyasimamisha @90,000/=
10. Kushepu miguu na kuwa minene @100,000/=
11. Kuondoa mipasuko mwilini (michirizi) @90,000/=
12. kubana uke na kuongeza hamu ya tendo la ndoa kwa mwanamke @100,000/=
13. Taiti za hips na makalio @150,000/=
NB: Hakikisha unapata risiti yenye muhuri halisi wa MARKSON CO pamoja na garantii kwa bidhaa halisi.
Wasiliana nasi :-
(+255) 0767447444 na
0714335378
Google MARKSON BEAUTY.
Follow us @Markson_beauty_pr
@Markson_beauty_pr

TAARIFA Toka Ikulu Kuhusu Uzushi Dhidi ya Taasisi ya Wanawake na Maendeleo (WAMA)

$
0
0
Katika siku za karibuni baadhi ya vyombo vya habari na mitandao ya kijamii imechapisha taarifa zinazomhusisha Mke wa Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne Mhe. Mama Salma Kikwete na Taasisi anayoiongoza ya Wanawake na Maendeleo (WAMA) kwamba imeshindwa kulipia kodi mizigo mikubwa iliyoiingiza nchini na hivyo kuwa hatarini kupigwa mnada.


Taarifa hizo zimemhusisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli kuwa anahusika kuzuia mizigo hiyo bandarini mpaka hapo itakapolipiwa kodi.

Tunapenda kuutarifu umma kuwa taarifa hizo sio kweli na ni uzushi, kwani Rais Magufuli hajawahi kuzuia wala kuagiza kuzuiwa kwa mizigo ya Mama Salma Kikwete.

Rais Magufuli amesikitishwa sana na uzushi huo unaofanywa kwa lengo la kumchafua Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete na familia yake na amewataka waandishi wa habari na vyombo vya habari nchini kuacha kuandika na kuchapisha taarifa za uzushi na badala yake vizingatie weledi na kufuata sheria.

“Nimesikitishwa sana na uzushi unaofanywa dhidi ya Rais Mstaafu Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete na Mke wake Mama Salma Kikwete, tafadhali wale mnaotengeneza uzushi huu acheni mara moja na muacheni Rais Mstaafu Kikwete apumzike.

“Rais Mstaafu Kikwete amefanya kazi kubwa ya kulitumikia Taifa hili, amestaafu anapumzika, narudia muacheni apumzike, Serikali haitaendelea kuvumilia uzushi na uchonganishi huu unaofanywa kwa makusudi ili kuwachafua viongozi wastaafu” ameonya Rais Magufuli.

Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar es Salaam

04 Desemba, 2016

LEMA Alishawaandaa Watoto Wake Kisaikolojia - Mkewe Afunguka

$
0
0
Neema Lema, mke wa Mbunge wa Arusha mjini, Godbless Lema, amesema yeye na watoto wake hawajutii kutokuwa na mwanasiasa huyo ambaye yuko mahabusu kwa kuwa anapigania haki ya kidemokrasia.


Lema, ambaye alikamatwa Novemba 2 mjini Dodoma, hatakuwa pamoja na familia yake msimu huu wa sikukuu baada ya Mahakama Kuu kutupa hoja zake za kupinga kunyimwa dhamana katika kesi inayomkabili ya kutoa maneno ya uchochezi dhidi ya Rais John Magufuli. Mbunge huyo atakaa mahabusu hadi Januari.

“Mimi na hata watoto wangu, hatusikitiki kumkosa Lema ambaye yupo mahabusu. Tungejisikia vibaya sana kama Lema angekuwa mahabusu kwa kesi kama ya wizi au makosa mengine ya jinai,” alisema Neema

BAADA ya Kimya Kirefu BOB Junior Anakukaribisha Kutazama VIDEO Yake Mpya Hapa....

$
0
0
Baada ya ukimya flani hivi, leo Nov 3 Bob Juniour ameamua kuwakata kiu mashabiki wake na kuachia video  mpya ya wimbo wake wa ‘Chuku chuku’. Karibu uitazame na pia usiache kuniachia comment yako ili Bob Juniour akisoma ajue watanzania na mashabiki wake wameipokeaje hii. TAZAMA VIDEO HAPA ALAFU TOA MAONI YAKO:

MANJI Asalimu Amri...Aanza Kuamisha Kampuni zake Kutoka Jengo la Quality Plaza

$
0
0
Wapangaji katika jengo la Quality Plaza lililopo barabara ya Nyerere jijini Dsm wametekeleza Amri ya Mahakama kuu kitengo cha ardhi cha Kuondoka katika jengo hilo baada ya kutolewa saa 24 ambazo zimemalizika asubuhi ya leo,huku kampuni ya Yono ikisimamia zoezi hilo lililoendeshwa Chini ya Ulinzi mkali .

Majira ya Saa mbili Asubuhi Channel ten imeshuhudia wapangaji katika jengo hilo wakihamisha samani zao,huku ikielezwa kuwa makampuni zaidi ya matano yaliyopangishwa chini ya Kampuni mama ya Quality Group ilianza kuondoa mali zao usiku wa kuamkia leo.

Mkurugenzi wa Yono ambayo imepewa Kibali cha kuwahamisha wapangaji hao na Mfuko wa hifadhi ya jamii -PSPF amesema jengo hilo hivi sasa liko chini ya Usimamizi wao mpaka pale wapangaji wote watakapondoka. w

Dalali wa Mahakama kuu kitengo cha Ardhi Yono Steven Kevela amesema zoezi hilo la kuwahamisha wapangaji sugu wasiolipa pango na kukamata mali zao na kuzipiga mnada litaendelea kwa kasi na kuwataka wote waliopewa notisi za kulipa katika kipindi cha Siku saba kutekeleza kinyume chake sheria itachukua Mkondo wake.

MWANZA Ni Hatari....Polisi Wakamata Silaha za Kivita

$
0
0
MWANZA ni hatari. Ndivyo alivyosema Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Ahmed Msangi, baada ya matukio mawili yaliyotokea usiku wa kuamkia jana, likiwamo la nyumba moja kukutwa silaha za kivita, za jadi na watoto 10 waliokuwa wakifundishwa mafunzo yanayoashiria kuwa ni ya kigaidi.

Silaha zilizokutwa katika nyumba hiyo iliyopo Bugaka, Kata ya Kishili jijini Mwanza, ni bunduki aina ya AK 47, mabomu ya kurusha kwa mkono, bunduki aina ya Maker 4, risasi zaidi ya 150, majambia na visu.

Akizungumza na MTANZANIA Jumapili katika mahojiano maalumu, Kamanda Msangi alisema kuwa aliongoza vijana wake kufika katika nyumba hiyo baada ya kupata taarifa kutoka kwa baadhi ya watuhumiwa wanaowashikilia kwa matukio mbalimbali, kwamba wafadhili wao wapo Kishili na Buhongwa.

Msangi alisema kutokana na taarifa hizo, aliunda vikosi viwili kufanya operesheni maalumu usiku wa kuamkia jana, kimoja kilikwenda eneo la msitu wa Deo uliopo Buhongwa na kingine Kishili.

Akizungumzia kikosi cha Kishili alichokiongoza, alisema walipofika katika nyumba hiyo waliizingira na watu waliokuwamo ndani wakaanza purukushani za kutaka kujihami ndipo askari walilazimika kufyatua risasi moja kuwatuliza.

Kamanda Msangi alisema wakati wanatafuta namna ya kuingia ndani ya nyumba hiyo iliyo na uzio, kijana mmoja alifanikiwa kuruka ukuta kwa upande wa nyuma na kutoroka, lakini wakafanikiwa kuwadhibiti wenzake zaidi ya 15.

“Baada ya kuwadhibiti na kuingia ndani, tulifanya ukaguzi na kufanikiwa kupata mabomu ya kurusha kwa mkono yaliyokuwa yameandaliwa kwa matumizi, bunduki za kivita aina ya AK 47, magazine tano na kila moja ikiwa na risasi 30, majambia, bunduki ndogo aina ya Maker 4, visu na gari moja ambayo inawezekana ndiyo wanayotumia kufanya doria zao kabla ya kufanya matukio.

“Tulipoingia tumewakuta watoto wadogo 10 waliokuwa wakifundishwa mafunzo maalumu ya namna ya kutumia silaha walizokuwa nazo na namna ya kujilinda na adui, pia kulikuwa na wanaume wanne wakubwa na wanawake wawili ambao inaelezwa ndio watoaji mafunzo kwa watoto hao.

“Katika mahojiano ya awali, tumeelezwa kwamba watu hao wana vikosi katika mikoa mbalimbali ya Kanda ya Ziwa, ikiwamo Tabora, Mwanza na Kigoma,” alisema.

Kamanda Msangi alisema wakati wanapambana na watuhumiwa hao, wananchi walijikusanya eneo hilo, wakiwa na nia ya kutaka kuwaua watuhumiwa hao, lakini askari walisimama imara na kufanikiwa kuondoka nao wakiwa hai.

Alisema baada ya kuondoka na watuhumiwa hao, baadaye alipata taarifa kwamba wananchi waliamua kuteketeza nyumba hiyo kwa moto alfajiri ya jana.

WAWILI WAUAWA

Akizungumzia kikosi cha pili kilichokwenda msitu wa Deo, alisema kiliambatana na vijana wanne ambao baadhi yao ni waendesha bodaboda, waliokuwa wakishikiliwa kwa matukio ya hivi karibuni.

Alisema walipofika katika msitu huo, walionyesha silaha zilipo na katika ukaguzi walifanikiwa kupata bunduki moja aina ya SMG, magazine mbili huku moja ikiwa na risasi 15 na nyingine 30, pia walikamata bastola moja.

“Wakati askari hao wakifanya upekuzi katika msitu huo, ghafla watuhumiwa hao walianza purukushani ya kutaka kutoroka, ndipo askari waliwafyatulia risasi na kuwaua wawili.

“Tunaendelea kuwahoji watuhumiwa ili kupata mtandao wote, lakini hapa Mwanza ni hatari, kibaya zaidi vijana hawa wa bodaboda wanajihusisha na vitendo hivi, tunaomba wananchi kuwa makini na kundi hili,” alisema.

MGOGORO CUF, Pro Lipumba Azomewa na Wananchi Mkoani Lindi

$
0
0
Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi (CUF) anayetambuliwa na Msajili wa Vyama vya Siasa nchini, Prof. Ibrahim Lipumba amekutana na wakati mgumu baada ya wananchi wilayani Ruangwa mkoani Lindi kumzomea.

Prof. Lipumba alikumbana na hali hiyo alipokuwa mkoani humo katika ziara aliyoeleza kuwa ni ya kujenga chama. Akiwa anapita katika barabara huku gari lake likilindwa na vyombo vya ulinzi, wananchi waliokuwa wamesimama kando kando ya barabara walisikika wakiimba wimbo “Hatumtaki”, huku wengine wakimuita msaliti.

Mbali na wananchi hao waliokuwa wakimzomea, wengine walikuwa na mabango yaliyokuwa yakisomeka “CUF kwanza Lipumba baadaye”, “Hatukutaki msaliti wewe.”

Wakati hayo yote yakiendelea, Prof. Lipumba na viongozi wanaomuunga mkoani walikuwa ndani ya gari na hawakusema jambo lolote.

Kwa muda sasa kumekuwa na mgogoro wa uongozi ndani ya chama hicho kuhusu nafasi ya Mwenyekiti ambapo baadhi wanamtambua Prof. Lipumba kama mwenyekiti halali huku wengine wakumtambua Julius Mtatiro kuwa ndiye mwenyekiti halali.

Licha ya Prof. Lipumba yeye kuendelea kufanya mikutano ya ndani huku akipata ulinzi wa vyombo vya dola, Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif alizuiwa kufanya mkutano wa ndani uliokuwa umepangwa kufanyika mkoani Mtwara.

Itazame hapa chini video ya wananchi hao wakimzomea Prof. Lipumba.

KWANINI Wanawake Wanapenda Wanaume Masharobaro aka Bad Boys

$
0
0
Wanawake kuchagua wanaume masharobaro aka badboys kuwaliko wanaume wa kawaida si jambo geni na hutokea mara kwa mara. -aidha katika vyuo, vilabuni, sinema, maktabani ama sehemu yeyote ile. Wanaume masharobaro, kama wanaume wengine, wao pia wanamaumbo ya kila aina, shepu na mvutio wa kijinsia. Kama wewe ni mwanamume wa kawaida ambaye humaliza wa mwisho ama ushawahi kupoteza mpenzi wako kwa sharobaro fulani, hapo chini kuna nadharia ambazo zitasaidia kueleza kwa nini  wanawake wanapenda sana kuvutiwa na wanaume masharobaro.

1. Hamu ya kufuata
Kufuata kitu ambacho unakipenda huwa kuna msisimko fulani mtu hupata. Lakini msisimko zaidi hutokea wakati ambapo mtu anajaribu kufuata mtu ambaye hataki kujulikana mienendo yake ya kimaisha, kufuatwa ama kueleweka kimaisha. Haya ndio maisha anayoishi mwanamume sharobaro. Wanawake wanapenda sana wanaume ambao hawaeleweki kimaisha (yaani hawatambuliki) ama kutaka kujua maisha yao. Na wewe kama mwanamume unataka kutumia huu udhaifu kwa manufaa yako, wakati mwingine unafaa kumfanya mwanamke abaki na maswali chungu nzima kutaka kukujua zaidi. Kama unampenda, jaribu kadri iwezavyo kutojaribu kumuonyesha.  Badala yake mpe pia yeye changa moto kwa kuweka ujanja wa kutoeleweka mara kwa mara. Hii ni njia moja murua ya kuhakikisha utaingia katika akili yake.

2. Kutaka kuwafunga fundo
Kitu kingine ambacho wanawake huvutiwa kwa sharobaro ni kutaka nafasi ya kuwafunga fundo ama kuwajeuza tabia zao. Mwanamke, amezaliwa naturally na hisia za uzazi, yaani kutaka kujeuza mtu mwenye tabia ovyo kuwa na tabia nzuri. Hii huibua hisia halizi za uzazi ndio maana kama mwanamume unapaswa wakati mwingine kumsumbua mwanamke hikisia, kimawazo na kadhalika. Unafaa kuwa mpinzani lakini usiwe mhalifu. Unafaa kuwa hatari lakini usipitishe kiwango ambacho kitamwogopesha. Kimtazamo, unafaa kumfanya mwanamke auonyeshe uke wake wote ili kujaribu kukubadilisha, mpe nafasi ajaribu kuubadilisha upande wako wa kiza na mwishowe kukufanya uwe mwanamume thabiti katika mchakato mzima.

3.Uanaume uliothabiti
Wanaume masharobaro (na si wale feki) karibu nyakati zote huwashinda wanaume wa kawaida kwa sababu ya mambo mawili makuu. Kwanza ni kuwa ni wanaume majasiri na pili wanaudhibiti uanaume wao kwa kuwa ngangari kimaisha. Kutoogopa kwao kwa jambo lolote ndiko kunawafanya wanawake kuvutiwa nao. Wanawake wengi wanavutiwa na wanaume ambao ni hatari, ngangari na wenye nguvu kwa sababu si rahisi kuchezewa au kufanyiwa masihara. Ukismama  kumtetea mwanamke kuhusu mahitaji yake na uovu, hii inamaana ya kuwa una uwezo wa kusimama kando yake na jambo lolote lile.  Kuweza kuonyesha level ya kuwa wewe ni mtu usiekuwa na woga wowote, unafaa kumwonyesha mwanamke wako kuwa una uwezo wa kuwa ngangari mahali popote pale ili mradi kumlinda yeye tu.

4. Uoga wa kujitwika majukumu
Wanaume masharobaro hupenda kuhepa majukumu yanayohusiana na mahusiano. Kwa wanawake ambao wana uoga huo huo wa kuwa na majukumu, masharobaro huwavutia sana na kuwaona kama hakuna wanaume wazuri kama hao. Kwa kuwa wanawake hawatajitweka majukumu, huwa hawana haja ya kujishughulisha na hisia za kipenzi ambazo ni stress. Pia ni habari njema kwa wanawake ambao wako tayari kwa uhusiano wa kimapenzi wa muda mfupi pekee. Lakini kama kawaida, mwisho wa siku lazima mwanamume sharobaro au mwanamke mtundu lazima kuna sehemu fulani ndani ya mawazo yake anatamani kuwa na mahusiano ya kudumu na pia kupendwa. Hivyo siri hapa ni kuipima miondoko yake na uangalie level yake ya kujitwika majukumu katika mapenzi halafu sasa uanze na hapo.


Upende usipende, wanaume masharobaro watakuwa na nafasi kubwa katika moyo wa mwanamke. Kuna kitu ndani yao ambacho kinawasababisha wanawake kuangua mwili mzima kihisia na kimapenzi kwao. Lakini hii haimaanishi kuwa lazima kila mwanamume ajeuke na kuwa sharobaro ili aweze kuwa na nafasi rahisi ya kutongoza mwanamke aliye kwa ndoto zako. Kile unachotakiwa kufanya ni kucheza mchezo mzima kiwastani. Daima unafaa kuwa vile ulivyo huku ukiingiza tabia flani za usharobaro hivi katika miondoko yako. Kama kuna kitu nzuri kati yenu wawili, basi pia kuna sehemu mbaya ambayo unaweza kuitumia ili ukajinufaisha nayo

Mchezaji Mbao FC Aanguka Afa Uwanjani Baada Ya Kugongana Na Beki Wa Mwadui

$
0
0

Mshambuliaji wa timu ya vijana ya Mbao FC, Khalfan Ismail amefariki baada ya kugongana na kuanguka uwanjani.

Mechi hiyo ilikuwa inachezwa kwenye Uwanja wa Kaitaba mjini Bukoba ambako michuano ya vijana chini ya miaka 20 inaendelea.

Ismail aligongana na beki wa Mwadui FC wakati wakiwania mpira na kuanguka na juhudi za kuokoa maisha yake zilionekana kukakwama.

Wakati mauti yanamkuta Ismail, dakika chache kabla alikuwa amefunga bao dhidi ya Mwadui.

Pamoja na kukimbizwa hospitali ya Rufaa ya Kagera, taarifa baadaye zilizopatikana zilieleza, Ismail alifariki palepale uwanjani.

DOGO Janja Afiwa na Baba yake

$
0
0
Msanii wa muziki wa hip hop kutoka Tip Top Connection Dogo Janja amefiwa na baba yake mzazi, Abubakari Chande.

Mzazi wake huyo ambaye alikuwa akiishi mkoani Arusha, ni mmoja kati ya watu wake wa karibu ambao walikuwa wanamshauri katika muziki wake.

Kupitia instagram, Dogo Janja ameandika:
PUMZIKA KWA AMANI BABA YANGU KIPENZI.😭 Hakika MUNGU Amefanya Maamuzi Yake Siwezi Kukufuru Zaidi Ya Kukuombea kwa ALLAH akupe kauli Thebeet! Umelala baba yangu sitakuona tena😭 EEH MWENYEZI MUNGU UMPOKEE,UMUONDOLEE ADHABU ZA KABURI. Lala baba hakika wote njia yetu ni moja.. siku moja tutaonana tena baba! R.I.P Kamanda ABUBAKARI CHENDE!
Kiongozi wa Tip Top Connection, Babu Tale amempa pole rapa huyo.

“Pole Dogo Janja Mungu akutie nguvu katika kipindi hiki kigumu na amuweke Baba katika njia inayo stahiki,” aliandika Babu Tale instagram.

JE DADA Unahitaji Kuwa na Makalio Mazuri na Rangi Nzuri na Mkaka Kuwa Handsome? African Beauty Inakuletea Dawa Hizi

$
0
0

AFRICAN BEAUTY EXPRESS PRODUCTS ,DAWA ZETU ZIMETHIBITISHWA KIAFYA.
je Dada unahitaji Kuwa Mrembo? na kaka unahitaji Kuwa mtanashati?African beauty imewaletea products nyingi sana zenye ubora WA hali ya juu,hazina madhara wala kemikali,zinamatokeo ya haraka ndani ya wiki mbili tu,products hizi niuhakika sana% tunazo za
(1)kuongeza hipsi,MAKALIO,na mapaja @100000
(2)kunenepesha MIGUU na Kuwa soft(chupa ya Bia)@100000/=
(3)Kupunguza Kitambi(slimming)@100000/=
(4)Kupungua MWILI MZIMA(weight loose)@130000/=
(5)Kuwa Mweupe MWILI MZIMA (njano)@100000/=
(6)kunenepa MWILI mzima@90000/=
(7)Kupunguza MATITI na kuyasimamisha@80000/=
(8)kuongeza matiti@80000
(9)kurefusha NYWELE na kuzuia kukatika@80000/=
(10)kuondoa CHUNUSI,MADOA na makovu@80000/=
(11)kuondoa Michirizi ya uzazi na cream@80000/=
(12)kurefusha na kunenepesha uume kwa size uipendayo@100000/=
(13)kuongeza NGUVU za kiume@100000/=
Ndugu MTEJA bidhaa za African beauty in uhakika sana,ukitumia dose moja hauwezi kurudi tena,MTEJA atakapo nunua bidhaa kwetu ni lazima afuate dose ili aweze kuona matokeo mazuri,MTEJA nilazima afuate maelekezo ya wahusika WA kampuni,MTEJA kama Yupo bize na kazi zake anaweza kupelekewa Huduma Mpaka alipo,kwa Wateja WA mikoani Huduma utatumiwa kwa mabasi kiofisi zaidi,kama MTEJA hayupo bize na kazi anaweza kufika ofisini kwetu zilizopo kariakoo,mnazi mmoja,na Mlimani city kwa maelezo zaidi piga sim(+255)-0756697906,0716805391,0783300397 Whatsapp namba 0756697906 Facebook page AFRICAN BEAUTY unaweza kunifollow instagran
👇👇👇👇👇👇👇👇👇👇👇👇👇
@AFRIC_IS_BEAUTY
@AFRIC_IS_BEAUTY


MZEE wa Upako Atuhumiwa Kulewa Pombe..Mwenyewe Adai Wataje Alikunywa Pombe Gani na Baa Gani

$
0
0
Mchungaji wa Kanisa la Maombezi (GRC), Anthony Lusekelo ‘Mzee wa Upako’ baada ya kudaiwa kumfanyia fujo jirani yake ameendelea kujibu madai hayo kwa mtindo wa ‘kudonoa donoa’ na jana aliwataka wanaodai kuwa alilewa siku hiyo wataje alikunywa pombe gani na katika baa gani.

Wiki mbili zilizopita, taarifa kwenye vyombo vya habari zilisema kwamba Mchungaji Lusekelo alikwaruzana na majirani zake huku akidaiwa kuwa alikuwa amelewa jambo ambalo lilifanya achukuliwe na kuhojiwa na polisi.

Lakini, tangu kuibuka kwa tukio hilo alikataa kulitolea ufafanuzi licha ya kutafutwa na vyombo vya habari, hata pale alipohudhuria ibada kanisani kwake aliwaambia waumini wake hatalizungumzia na badala yake alidonoadonoa baadhi ya matukio.

Alipokwenda kanisa kwake kwa mara ya kwanza Novemba 25, Mchungaji Lusekelo alisema; “Kuna kitu nilikuwa nataka nikiseme, lakini sitakisema ili waendelee kusema haohao waliokuwa wanasema.Wakawaulize wenyewe. Nimeyaona magazeti hapa, ooh Mzee wa Upako, ooh Mzee wa Upako, sisemi. Sasa leo yupo hapa, na kwa taarifa yao watashindana sana, lakini hawatashinda. Hii ni kama kumpiga chura teke.”

Lakini, Novemba 28, Mchungaji huyo akajibu baadhi ya hoja akisema kwanza, maneno aliyotumia ambayo ni mshenzi, mpumbavu na mjinga siyo matusi kwani yameandikwa kwenye Biblia. Pili, watu hao ndiyo walianza kumtukana yeye baada ya kuwauliza wanatafuta nini eneo la getini kwake.

 Hoja nyingine alisema watu hao hawakuwa jirani zake kama inavyodaiwa kwani mtaani kwake wanaishi kama majambazi kutokana na mazingira ya kutofahamiana.

Jana, Mchungaji Lusekelo akiwahubiria waumini wake alidonoa tena eneo jingine linalohusiana na tukio hilo, kwamba wanaodai alikuwa amelewa pombe, waeleze alikunywa pombe gani na baa gani.

Akikaribishwa kwa wimbo wa kuabudu uitwao, ‘Nina haja nawe’ kabla ya kuanza kumtunza kwa sadaka, Mchungaji Lusekelo alisema watu wanaotuhumu kuwa alilewa, wanatakiwa kueleza alikunywa pombe gani na alikunywa akiwa eneo gani.

“Wiki iliyopita nilikuwa Wizara ya Mambo ya Ndani, baadhi ya maofisa wakaniona , wewe Mzee wa Upako… Mzee wa Upako, askari mmoja akaniuliza wewe Mzee wa Upako unachukua sadaka halafu unaenda kunywa pombe. Nikawauliza, hiyo pombe nilikunywa wapi, halafu pombe zipo za aina nyingi, taja ni pombe gani, ukienda mbali zaidi ungeuliza nililewa nini, maana hata upako wa roho mtakatifu ni ulevi,” alisema.

“Lakini kuna majina ya watu, mitaani inaitwa pombe, sasa sijui ni pombe gani hiyo….watashindana sana. Lakini kushindana siyo tatizo, je, mtashinda? Eti oooh hayo maneno tu hata kwenye kanga yapo, subiri tusiandikie mate na wino upo, ukitaka kummaliza Mzee wa Upako we mpige risasi tu,” alisema huku akishangiliwa na waumini wake.

 Alisema hakuna mwanadamu atakayeweza kumwangusha kwa kipawa na kalama Mungu aliyompatia.

“Ndiyo maana unapojiita mtume leo unakuwa unajirusha kwenye harakati ambazo zilijengwa na baba zetu, ndiyo maana kumshinda shetani ni lazima, kuna mfumo umejengwa na mfumo huu uko imara kama chuma cha pua,” alisema.

Katika ibada ya wiki iliyopita, mchungaji huyo alisema taarifa zinazosambazwa kumchafua hazitamvunja moyo wa kuendelea kufanya kazi ya uchungaji, huku akihoji kwanini magazeti yanaandika mabaya pekee na hayaandiki habari za uponyaji anaofanya kanisani kwake.

PICHA za Mchezaji wa Mbao FC Alivyo Fariki baada ya kugongana na mchezaji wa Mwadui FC

$
0
0
Mshambuliaji wa timu ya vijana ya Mbao FC U-20 Ismail Mrisho Khalfan anayevalia jezi nambari 4 amefariki  Dunia jana jioni  baada ya kuanguka uwanjani Kaitaba wakati wa mtanange wao dhidi ya timu ya vijana wa Mwadui FC ikiwa ni mechi ya mwisho ya kumaliza duru la kwanza la ligi ya Vijana.

Ismail Khalfan  alifariki baada ya kufikishwa Hospitali ya Serikali ya mjini Bukoba.

Ismail Khalfan kabla ya kufikiwa na umauti aliweza kuifungia timu yake bao la kwanza na bao la pili lilifungwa kwa mkwaju wa Penati hivyo mtanange kumalizika kwa 2-0.

Kabla ya kuanguka Ismail aligongana na beki wa Mwadui FC  na baadae akiwa peke yake alianguka chini lakini akainuka halafu akaanguka tena na kutokana na ukosefu wa huduma ya kwanza na gari la wagonjwa katika Uwanja wa Kaitaba kulipelekea marehemu kupandishwa kwenye gari la zima moto na kupelekwa hospital ambapo mauti yalimkuta.

ZARI Amejifungua? Diamond Aandika Ujumbe Huu Instagram Akielekea SA Akiwa na Mama yake

$
0
0
Diamond Platnumz weekend hii amepost picha instagram akiwa safarini na Mama yake kuelekea Afrika Kusini huku kwenye picha hiyo akiwa ameandika ujumbe ambao unaonyesha huwenda mpenzi wake Zari amejifungua.

Mapema mwezi uliopita katika hatua za kujiandaa na mapokezi ya mtoto huyo, Zari alifanya baby shower nchini Afrika Kusini na kuwashirikisha marafiki zake na watu wa karibu.

Jumapili hii Diamond akiwa safarini na mama yake kwenda Afrika Kusini, ameandika :
Na mama Chibu D Chibu De … flying to our new Second home, South africa For my New Born… #MiniMe #ChibuJunior #YoungSimba #YoungLion Ungependa nimpe jinangani eti?😊
Kama Zari amejifungua basi huyo ni mtoto wake wa pili na Diamond. Pia atakuwa mtoto wake wa tano kwa ujumla.

TAZAMA VIDEO: Tukio la Mchezaji wa Mbao FC (U 20) lililopelekea Kupoteza Maisha vs Mwadui FC

$
0
0
Ismail Khalfan mchezaji wa Mbao FC chini ya umri wa miaka 20, amepoteza maisha katika michuano ya timu za vijana wa umri chini ya 20 katika mchezo wa mwisho wa round ya 7 Kundi A kituo cha Kaitaba Bukoba, Ismail Khalfan alikuwa anavaa jezi namba 4 katika mashindano hayo  lakini ndio aliyefunga goli la la kwanza kwa Mbao FC dhidi ya Mwadui FC katika ushindi wa goli 2-0.
VIDEO:

UZUSHI Wamkera Rais Magufuli

$
0
0
RAIS John Magufuli amesikitishwa na uzushi unaofanywa kwa lengo la kumchafua Rais mstaafu wa Awamu ya Nne, Jakaya Kikwete na familia yake, na amewataka waandishi wa habari na vyombo vya habari kuacha kuandika na kuchapisha taarifa za uzushi na badala yake vizingatie weledi na kufuata sheria.

Amesema taarifa zinazomhusisha kwamba amezuia mizigo ya mke wa Rais mstaafu Kikwete, Mama Salma Kikwete bandarini hadi hapo itakapolipiwa kodi, si kweli na ni uzushi, kwani hajawahi kuzuia wala kuagiza kuzuiwa kwa mizigo ya Mama Salma Kikwete.

Dk Magufuli aliyasema hayo katika taarifa iliyotolewa jana na Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais, Ikulu, baada ya siku za karibuni, baadhi ya vyombo vya habari na mitandao ya kijamii kuchapisha taarifa zinazomhusisha Mama Salma Kikwete na Taasisi anayoiongoza ya Wanawake na Maendeleo (WAMA) kwamba imeshindwa kulipia kodi mizigo mikubwa iliyoiingiza nchini na hivyo kuwa hatarini kupigwa mnada.

Aidha, taarifa hizo zimemhusisha Rais Magufuli kuwa anahusika kuzuia mizigo hiyo bandarini mpaka hapo itakapolipiwa kodi.

“Tunapenda kuutaarifu umma kuwa taarifa hizo si kweli na ni uzushi, kwani Rais Magufuli hajawahi kuzuia wala kuagiza kuzuiwa kwa mizigo ya Mama Salma Kikwete,” ilieleza taarifa ya Ikulu.

“Rais Magufuli amesikitishwa sana na uzushi huo unaofanywa kwa lengo la kumchafua Rais mstaafu wa Awamu ya Nne, Dk Jakaya Kikwete na familia yake na amewataka waandishi wa habari na vyombo vya habari nchini kuacha kuandika na kuchapisha taarifa za uzushi na badala yake vizingatie weledi na kufuata sheria,” ilibainisha taarifa ya Ikulu na kuongeza:

“Nimesikitishwa sana na uzushi unaofanywa dhidi ya Rais mstaafu Jakaya Kikwete na mke wake Mama Salma Kikwete, tafadhali wale mnaotengeneza uzushi huu, acheni mara moja na muacheni Rais mstaafu Kikwete apumzike.

“Rais mstaafu Kikwete amefanya kazi kubwa ya kulitumikia Taifa hili, amestaafu anapumzika, narudia muacheni apumzike, Serikali haitaendelea kuvumilia uzushi na uchonganishi huu unaofanywa kwa makusudi ili kuwachafua viongozi wastaafu,” ameonya Rais Magufuli.

Mwishoni mwa wiki, WAMA ilikanusha taarifa zilizochapishwa na gazeti moja la kila wiki kwa lugha ya Kiswahili kuwa Mwenyekiti wake, Mama Salma Kikwete ana mzigo mkubwa bandarini ambao haujalipiwa ushuru na kodi.

Taarifa ya Wama iliyosainiwa na Katibu Mtendaji wake, Daudi Nassib, ilisema taarifa hizo ni za uongo na hazina ukweli wowote. Kwa mujibu wa taarifa hiyo, gazeti hilo lilichapisha habari hiyo iliyokuwa na kichwa cha habari, “Mali za Salma Kikwete kuuzwa kwa mnada?” Katika toleo lake hilo la Novemba 30, mwaka huu,

“Kumetolewa madai eti kwamba taasisi ya Wama inayoongozwa na Salma Kikwete inao mzigo mkubwa bandarini ambao haujalipiwa ushuru na kodi, hivyo Mamlaka ya Mapato Tanzania imepanga kuuza mali hizo.

“Kwa niaba ya Taasisi ya Wama napenda kutoa masikitiko yetu kwamba habari hizo ni za uongo na hazina ukweli wowote.

“Kwa maoni yetu gazeti hilo lina dhamira mbaya dhidi ya Taasisi ya Wama na Mwenyekiti wake Salma Kikwete. Nia yao ni kupaka matope na kuchafua majina na sifa ya taasisi yetu na kiongozi wake.”

Katibu Mtendaji huyo alisema ukweli kuhusu jambo hilo ni kwamba, Wama ilitumiwa maboksi 11 ya vitabu vikiwa ni zawadi kutoka Taasisi ya Nakayama ya Japan ambayo ndiyo iliyofadhili ujenzi wa Shule ya Sekondari ya Wama-Nakayama iliyopo Nyamisati, Kibiti na yalishatolewa bandarini tangu Agosti 10, mwaka huu na tayari vitabu viko shuleni na vinatumika.

“Hakuna mzigo wowote wa Taasisi ya Wama uliopo bandarini unaosubiri kutolewa wala kuuzwa na TRA,” ilisema sehemu ya taarifa hiyo na kulitaka gazeti hilo kuomba radhi kwa Salma Kikwete na kwa Wama kutokana na taarifa hizo.

SHISHA yatajwa Chanzo cha Mapato ya Serikali

$
0
0
LICHA ya kupigwa vita na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda, imebainika kwamba shisha ni chanzo cha mapato ya Serikali.

Utafiti uliofanywa na MTANZANIA na kuthibitishwa na baadhi ya wabunge, shisha inatambuliwa na sheria ya kodi ya mwaka 2016 iliyopitishwa na Bunge Juni mwaka huu kama chanzo cha mapato.

Katika bajeti kuu ya Serikali iliyosomwa bungeni na Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Philip Mpango Juni mwaka huu shisha ni mojawapo ya vyanzo hivyo ikiwa katika kundi la mazao yatokanayo na tumbaku.

Sehemu ya hotuba hiyo inaelekeza kufanyika kwa marekebisho ya viwango maalumu vya kodi (specific duty rates) kwenye ushuru wa sigara zisizo na kichungi zinazotengenezwa kutokana na tumbaku inayozalishwa hapa nchini kwa kiwango cha angalau asilimia 75, kutoka shilingi 11,289 hadi shilingi 11,854 kwa kila sigara elfu moja.

Aidha ushuru wa “cigar” pamoja na sigara nyingine za kutoka nje, zilielezwa kuwa unabaki kuwa asilimia 30 huku tumbaku ambayo iko tayari kutengeneza sigara (cut filler) ikipanda kutoka shilingi 24,388 hadi shilingi 25,608 kwa kilo.

Aidha baadhi ya wabunge wa Kamati ya Bunge ya Bajeti waliiambia MTANZANIA kuwa kilevi hicho (shisha) ni miongoni mwa vyanzo halisi vya mapato ya Serikali na kwamba kuipiga marufuku ni kukataa mapato halali ambayo yamewekwa kisheria.

Mbunge wa Momba, David Silinde (Chadema) alisema katazo lolote kuhusu bidhaa hiyo ya shisha ni batili kisheria.

Silinde ambaye pia ni mjumbe wa Kamati ya Bunge ya Bajeti alisema katika vyanzo vya mapato kwa mujibu wa hotuba ya bajeti ya Serikali iliyosomwa mwaka huu na Dk. Mpango, shisha inaangukia katika kundi la sigara nyinginezo na bidhaa hizo zinatozwa asilimia 30 ya kodi.

“Hivi nyinyi hamshangai, statement (taarifa) inatoka kwa mtu mmoja ambaye kimsingi anatafuta chiep politics (umaarufu) asiokuwa nao.

“Shisha sio bangi, duniani kote watu wanatumia shisha kama kiburudisho chao, ni kama sigara ambavyo inatajwa kuwa na madhara lakini watu wanatumia. Ni suala la mtu binafsi kutumia au kutotumia.

“Kama ni madhara ya kiafya wizara yenye dhamana na afya wajitokeze watoe tamko ambalo halitapingana na taasisi nyingine zikiwamo za kimataifa” alisema Silinde.

Mjumbe mwingine wa kamati hiyo, Mbunge wa Babati,  Vrajilal Jituson (CCM) yeye alikiri kuwa kilevi hicho ni miongoni mwa vyanzo vya mapato vya serikali na imeorodheshwa katika Sheria ya fedha (Finance bill Act) ya mwaka 2016.

Hata hivyo alisema licha ya kuwapo kwa sheria ya kodi inayoruhusu kuingizwa nchini kwa bidhaa hiyo si jambo la ajabu kupiga marufuku bidhaa hiyo.

“Ninavyofahamu mimi shisha haina ubaya ila nadhani kinachofanyika Dar es Salaam wauzaji wanachanganya na dawa za kulevya, bangi, tumbaku na vitu vingine inageuka kuwa kilevi kisichofaa.

“Utumiaji wa shisha ni utamaduni wa kiarabu ambapo watu wote wanawake kwa wanaume walikuwa wakivuta kama kiburudisho na kusema kuwa shisha ni kama ‘pool table’ ambao ni mchezo kama michezo mingine lakini umegeuzwa na kuwa kamali hivyo kuharibu maana halisi ya mchezo huo” alisema Jituson.



Waziri kivuli wa Fedha

Waziri Kivuli wa Fedha, Halima Mdee (Chadema) yeye alisema suala la shisha ni matokeo ya watendaji wa serikali kufanyakazi kwa matukio.

Mdee ambaye pia ni Mbunge wa Kawe (Chadema) alisema shisha ni chanzo halisi cha mapato kwa mujibu wa sheria ya fedha iliyopitishwa na Bunge Juni mwaka huu.

Alisema marufuku yoyote dhidi ya bidhaa hiyo  ni suala ambalo halitekelezeki kwa sababu limefungwa na sheria na kwamba wale wanaolizungumza kisiasa wapuuzwe.

“Tatizo ninaloliona hapa ni serikali kufanyakazi kwa matukio, lakini pia hawa wenzetu hawasomi vitu, hiyo sheria ya shisha waliipitisha wenyewe sisi tukiwa nje katika Bunge la bajeti mwaka huu.

“Siku zote sisi tukiwa mle ndani huwa tunapitia na kusoma nyaraka kwa umakini, leo sheria waliyoitunga wao hawaikumbuki” alisema Mdee.

Kilevi hicho kwa mara ya kwanza kilipigwa marufuku na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiwa katika hafla ya kufuturisha waumini wa dini ya Kiislamu wa madhehebu ya Shia Juni mwaka huu.

Waziri Mkuu alidai kuwa shisha ni kilevi ambacho huchanganywa na vitu vingine vikiwamo viroba na pombe nyingine haramu.

Baadaye Mkuu wa Mkoa, Paul Makonda aliendelea kushikia bango suala hilo ambapo hivi karibuni alikwenda mbali zaidi kwa kuwatuhumu Kamanda wa Polisi, Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Simon Sirro pamoja na Kamanda wa Polisi wa Kinondoni kuwa huenda wanapokea rushwa kutoka kwa wauza shisha.

Katika salamu zake wakati wa uzinduzi wa Mradi wa Uboreshaji wa Miundombinu ya Umeme katika Jiji la Dar es Salaam, Makonda alimweleza waziri mkuu kuwa wafanyabiashara wa shisha walikwenda ofisini kwake na kumwahidi kumpa Sh milioni 5 kila mwezi ili asiwasumbue.

“Shisha imerudi katika mkoa huu lakini nimeona kama Sirro ana kigugumizi… sijajua kama hizi tano tano zimepita kwake na pia RPC wa Kinondoni nimemuona hapa, sijui kwa nini hawa wana kigugumizi, sijui kama hizi tano tano zimepita kwao,” alisema Makonda.

Katika majibu yake, Waziri Mkuu, Majaliwa alisema atamwajibisha Makonda iwapo hatasimamia ipasavyo kukomesha matumizi ya dawa za kulevya, aina ya shisha.

Wizara ya Fedha

Akizungumzia suala hilo, Kaimu Msemaji wa Wizara ya Fedha na Mipango, Benny Mwaipaja alisema kuwa lengo la serikali yoyote ni kulinda afya za wananchi wake kadiri iwezekanavyo na ikiwa itabainika kuna madhara yanayotokana na matumizi ya shisha basi uamuzi huo utakuwa si sahihi.

“Kama wafanyabiashara wa shisha Dar es Salaam wamekiuka masharti na vigezo vya kuendesha biashara hiyo uamuzi wa mkuu wa mkoa ni sahihi” alisema Mwaipaja.

Aidha Mwaipaja alisema wizara itaendelea kulifuatilia suala hilo kufahamu kama kuna madhara ya kiafya yanayotokana na matumizi ya shisha pamoja na kuangalia kama uamuzi wa kuzuia kuuzwa kwa shisha pia ni sahihi.

Source: Mtanzania

KIFO cha Mchezaji wa Mbao FC Uwanjani, Baba Mzazi Afunguka

$
0
0
Wadau wa soka nchini wameendelea kumlilia mchezaji Ismail Halfan wa timu ya vijana wenye umri wa chini ya miaka 20 wa Mbao FC ya Mwanza, aliyefariki dunia  Desemba 4, 2016 baada ya kuanguka kwenye Uwanja wa Kaitaba, Bukoba mkoani Kagera

Mchezaji Ismail Mrisho Halfan wa timu ya Mbao U-20 akitolewa uwanjani na watu wa msalaba Mwekundu baada ya kuanguka uwanjani wakati wa mchezo wao uliokuwa .
Akizungumzia msiba huo, baba mzazi wa Ismail, Halfan Mrisho akiwa Jijini Mwanza ameelezea kupokea kwa masikitiko msiba huo, na kusema kuwa hiyo ni kazi ya Mungu, na kwamba mambo ya michezo ndivyo yalivyo.

Halfan amesema pia msiba huo ni pigo kubwa kwa taifa kwa kuwa mwanaye alikuwa na ndoto kubwa katika soka la Tanzania na alikuwa mahiri katika nafasi yake.

Kwa upande wake moja ya wanafamilia ambaye pia ni mlezi katika kituo ambacho Ismail alikuwa akilelewa, bwana Felicious, amesema kituo hicho kimepata pigo kubwa kumpoteza Ismail katika mazingira hayo kwani alikuwa ni moja ya wachezaji ambao walikuwa na ndoto kubwa.
"Ismail alikuwa tayari amepata nafasi ya kwenda kwenye kituo kimoja cha soka nchini Marekani, alikwenda kwa wiki mbili kufanya majaribio, akafaulu, na alirudi nchini kumalizia mitihani yake ya kidato cha nne, ili aende rasmi kwenye kituo hicho, lakini imekuwa bahati mbaya, kazi ya Mungu haina makosa" Amesema Felicious.

Mwili wa marehemu unataraji kuwasili Mwanza leo kwa ajili ya taratibu za maziko.
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), limetuma salamu za rambirambi na kusema kuwa limepokea kwa masikitiko makubwa taarifa za kifo cha kushtukiza cha Mchezaji huyo wa timu ya vijana wenye umri wa chini ya miaka 20 wa Mbao FC.

Timu hiyo ya Vijana wa Mbao, kama vilivyo timu nyingine 7 za Ligi kuu ya Vodacom, ilikuwa Kituo cha Bukoba katika Ligi ya vijana ambayo kwa msimu huu imefanyika kwa mara ya kwanza.
Timu nyingine Nane zilikuwa kituo cha Dar es Salaam.

CHIKI 'Ampigia Magoti' JB Baada ya Kusikia Ameacha Kuigiza Bongo Movies

$
0
0
Msanii wa bongo movie Chiki amesema JB hana sababu ya kustaafu kuigiza kwa kuwa ni mtu ambaye bado sanaa inamuhitaji na kuna wasanii wachanga na wakongwe wanamuhitaji kwa ushauri zaidi.

Akiongea kupitia eNewz Chiki amesema anamkumbusha JB kurudi bongo movie kwa kuwa sanaa haina kustaafu na kama kuna malengo ambayo aliyaweka yakawa hayajatimia asikate tamaa arudi kuendeleza chipukizi ambao wanakuwa lakini pia kama malengo yake yametimia basi awasaidie na waliopo chini yake.

Pia Chiki amesema hana mpango wa kustaafu kuigiza kwa kuwa anaamini kuwa kuna mashabiki zake ambao bado wanatamani kuona kazi zake na wanamkubali lakini pia anajipanga ili kuirudisha bongo movie kama zamani.
Viewing all 104789 articles
Browse latest View live




Latest Images