Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104785 articles
Browse latest View live

MOVIE YA SIWEMA WA NEY WA MITEGO BADO YAENDELEA INSTAGRAM...DOUGIE MASTA13 AMPA ZINGINE ZA USO

$
0
0
Huko Instagram kuna Jamaa Anajiita Dougiemasta13 sijui Siwema ambae ni mchumba wa Ney wa Mitego kamkosea nini Maana madogo anayomshushia...Duuuhhh ...Baada ya Jana Kuweka Video ya Wema akivishwa pete na Jamaa mwingine leo Kaja na Mpya....
JIONEEE.....


UMBEA WA INSTA:CATHERINE SHAWA APEWA USHAURI KUACHA KUUZA MADAWA YA KULEVYA

$
0
0

Catherine shawa mamaa Ya sembe , sister duu muuza sembe aliebakia baada Ya beach baby kukamatwa (jacky Cliff) na walikua mabeste kabla Ya ugomvi wao maana Catherine ndio alimpa mchongo jacky baada Ya jacky na jacky akashika usukani vizuri tenda nyingi alikua anapewa yeye wivu kidonda ndio makwaruzano yakaanza wakawa paka na chui ila enzi zao walikua poa sana ... Harafu jamani hawa wauza sembe mademu wanapenda sana kujiita ma boss lady hahaha ni shiiida!! Na shooping zao ni CL, LV magucci yaani wao na majina tu na kuringishia pesa ... Catherine nakupenda tulia tu umlee mwanao sasa Leo ukishikwa maana njia zote zinakaba yaani pamekua pagumu sasa ukienda jela jamani mwanao atalelewa na nani na hivi baba mwenyewe haonekani hizo safari ulizoenda zinatosha tulia ufungue biashara au ndio pesa Za shetani hua hazikai ?? Trip Za Ghana, Nigeria, brazil zinatosha mama ... Si unaona mjin sasa hivi hapafai kabisa ! Fanya mambo basi hata baadae uje usemw kweli niliuza unga dondosha mjengo , hizi CL ni mpito tu ukishavaa mara mbili tatu hutaki tena ila Nyumba ni asset Ya kudumu.....Agness Masogange sasa hivi katulia hata fujo Za kuonyeswha pesa hana sasa hivi tunaonyeshwa makalio tuuu...

Source:Team UkwelinaUwazi ..Intagram

SINTA SAHAU SIKU NILIYOLALA NA MKE WA MTU

$
0
0
Nikiri kwamba hakuna kitu nilichowahi kufanya kikanikosesha amani kama kulala na mke wa mtu.

Ilikua hivi,huyo mwanamke alikua mpangaji mwenzangu,mme wake alikua yupo huko mikoani,alikua mara kwa mara anatengeneza mazingira ya kuliwa,mara anitanie,hivi na vile nk.

Kufupisha story,alikuja siku moja rum kwangu,akanitega nikategeka,tukalala,baada ya kumlala nafsi yangu ilikosa amani,nikajuta,nikaona dunia nzima imeniona,ilikua usiku nikaona kama ni mchana,nikatamani nikimbie usiku huo,nikafunga mizigo yangu usiku huo huo nihame,nikaona kama dunia nzima imenielemea mimi.

Nikajuta usiku kucha,sikulala,asubuhi sa 11 nikaondoka kutoka nyumbani na kibegi kidogo cha mgongoni nikimbie aibu,nikawa na wasiwasi na mashaka yasioisha,naona kama kila mtu anajua,nikaenda stendi ila sijui naenda wapi,baadae nikaenda kwa rafiki yangu,nikalala mchana kutwa.

Niliposhtuka kama sa 10 jioni nawasha sim nakutana na meseji za yule mwanamke akinisifia sijui najua kufanyaje,kidogo akapiga sim,nikaikata,hofu yangu ikaongezeka mara dufu. Sikurudi nyumbani kama wiki nzima niko kwa rafki yangu.

Nikabadili namba ya sim ili yule mwanamke asinipate,sijui aliitoa wapi tena namba yangu mpya,kunichanganya zaidi akaniambia hajaona siku zake,nikachanganyikiwa,nikatam an dunia ipasuke niingie,nikawa na mawazo ya kujinyonga(kumbukumbu haikuja kama nilitumia mpira,kumbe nilitumia)

sitasahau hilo tukio,kwa kweli kulala na mke wa mtu ni vibaya sana,hata Bible imekataza hiyo dhambi. Kati ya dhambi zote nilizowahi kufanya hii ndio ilinikosesha amani,wala sitakuja tena kuirudia.

JAJI AKATAA MAOMBI YA KUFUTA KESI INAYOMKABILI CHRISS BROWN

$
0
0
Kesi ya Chris Brown itaendelea kuunguruma baada ya jaji Patricia Wynn wa Washington kukataa maombi ya wanasheria wa mwimbaji huyo yaliyomtaka amfutie kesi inayomkabiri.

Mwanasheria wa Chris Brown, Mark Geragos alimuomba jaji afute kesi hiyo kwa madai kuwa waendesha mashitaka walitumia ‘grand jury’ kuuzima ushahidi uliotolewa na mtu ambaye alidai alishambuliwa na Chris Brown na walinzi wake mwezi October, huko Washington.

Jaji huyo alieleza kuwa waendesha mashitaka walikuwa na haki yakutumia ‘grand jury’ kuangalia ukubwa wa kesi yao.

Grand Jury ni huundwa na watu waliopewa mamlaka ya kisheria kupeleleza uzito wa kesi na kuamua kama inapaswa kufunguliwa mashitaka au la, na huwa tofauti na mahakama.

Katika hatua nyingine Jaji huyo ameamua kuwa Chris Brown na mlinzi wake binafsi wasishitakiwe pamoja.

Chris atafikishwa makamani April 17.  

DULLY SYKES" DIAMOND HAENDI KWA WAGAGA ..HII NDIO SIRI YA MAFANIKIO YAKE"

$
0
0
Jina la Diamond Platinumz mtoto wa Tandale mwenye historia ya kuishi maisha ya ukata, sasa hivi ni moja kati ya majina makubwa kimuziki barani Afrika huku akishiriki kwenye project kubwa kama One Campaign iliyoongozwa na D’Banj huku akipewa mashavu na wasanii wakubwa wa Afrika Magharibi.

Dully Sykes ameuambia mtandao wa Times Fm moja kati ya sababu ambazo zinambeba mwimbaji huyo na kumpeleka kwenye level ya juu ya mafanikio kuwa ni kiu kubwa aliyonayo inayomfanya afanye kazi usiku na mchana huku akiwasumbua maproducer bila kusubiri wamuite studio.

“Wasimuone Diamond anafanya vizuri, Diamond anafika mbali wakafikiria Diamond anafanya kazi kwa kumsubiria hadi producer amuite studio, no sio kweli. Diamond anashinda usiku kila siku studio.” Amesema Dully Sykes.

Dully ameeleza kuwa hata yeye pia hukesha studio akifanya kazi na ndio sababu inayomfanya aendelee kufanya vizuri tangu alipoanza muziki bila kupotea na kwamba wasanii wengi wasiofanya hivyo huishia kuporomoka na kudai kuwa walioko juu wanafanya uchawi.

Mwimbaji huyo ambaye ni mmiliki wa studio ya 4.12 ameongeza kuwa akili ya kuwekeza kwenye vitega uchumi pindi uwapo juu ni moja kati ya sababu zinazomsaidia msanii kuendelea kuwa juu kwa muda mrefu.

“Kama wangekuwa wajanja sasa hivi wangekuwa na vitega uchumi…kitu kama studio ni kama jiko. Unakula kwa kutumia studio. Hata kama mtu haji lakini unaweza kutengeneza muziki kwa kutumia akili yako ukasema ‘leo bwana nimeamka saa kumi ya usiku nina idea yangu hebu ngoja niingie studio nidumbukize hii sauti pengine kesho itanifaa. Na kweli unakaa unapata idea nzuri na unatengeneza kitu kizuri.”

MZUNGU KICHAA AMPONDA ALI KIBA KWA KUDANGANYA ANGELIPWA MIL 100 KWA SHOW MOJA UJERUMANI

$
0
0
Kati ya vitu ambavyo husaidia kuongeza thamani ya msanii katika macho ya mashabiki ni pamoja na watu kuona akipata dili kubwa na kulipwa pesa nyingi katika shows.

Lakini kumekuwepo baadhi ya wasanii ambao wakati mwingine hutengeneza mazingira ya uongo hasa kupitia mitandao ya kijamii, na wengine hata kufanya na Interviews ili tu kufanya watu waamini kuwa thamani yao pia iko juu.

Mzungu Kichaa yuko tofauti kidogo katika hilo, sababu haoni sababu ya msanii kudanganya kwa kitu ambacho sio kweli. Msanii huyo wa Denmark aliyeishi Tanzania kwa miaka mingi alizunguzungumzia swala hilo katika kipindi cha Sporah.

“Mimi siwezi kwenda kwenye vyombo vya habari na kusema ooh nimetengeneza milioni 100 kwenye show halafu media zote ziseme ‘oooh wow’…kama alivyofanya Alikiba kipindi fulani” Alisema Mzungu Kichaa. “Alisema alikuwa anataka kwenda kufanya show Ujerumani, na alikuja kusema ameahirisha kwenda, tena aliahirisha siku moja kabla, na kusema kuwa angelipwa shilingi milioni 100…Kwahiyo akadai kwamba alikuwa anapewa hiyo hela lakini mikataba haikwenda kama ilivyotakiwa so aliahirisha show siku moja kabla, na kama mwanamuziki mimi najua jinsi mambo ambavyo hua yanakuwa, siamini watu waliokuwa tayari kumlipa kiasi cha pesa kama hicho…na kwa wao kutafuta media publicity kupretend we are getting big money to perform nadhani hilo ni kosa.” Alimaliza.

KAMA BADO UNATUMIA WINDOW XP KWENYE COMPUTER YAKO HII HABARI INAKUHUSU

$
0
0
Are you still using Windows XP as your operating system? From today Microsoft will no longer offer support their operating system Windows XP. I am one of those culprits who have refused to upgrade because I feel this is not a change I need when I considering my PC uses. This will also mean I will have to say goodbye to a laptop I have had and become attached to since 2007 since it does not have the specs to upgrade to Windows 7 or 8.


So what does this mean exactly? from today if faults detected within the operating system, they will go unfixed.Banks are urged to upgrade their ATMs to a newer OS release as soon as possible as we know 95% of all banks in the world still use Windows XP. There has been efforts from the European banks to get continued support and they have a high price to pay as the UK government agreed to pay more than £5.6 million to Microsoft to continue its support for Windows XP by one year.

If you cannot move on and choose to remain on windows XP you have to ensure that you are protected do this by keeping away from Internet Explorer and use Chrome instead, have a strong antivirus in place, make sure the firewall is set and finally do not store personal information on the browser.
However there are benefits of upgrading for example you will notice that with the newer versions of Windows there are significant changes in the interface and vast improvements in the services available and the overall aim of this is to make the computer less of an appliance and more like a personal device, similar to a phone.

What will you do now that Windows XP won’t be supported by Microsoft? will you finally upgrade? or will you buy a mac or do you want to try linux? Share your resolutions with us.

KIKWETE AKUBALI KUONGEZA MUDA BUNGE LA KATIBA

$
0
0
RAIS Jakaya Kikwete amekubali kuongeza muda wa Bunge Maalumu la Katiba katika mazungumzo aliyofanya na mwenyekiti wake, Samuel Sitta.

Hayo yalisemwa na Mwenyekiti huyo wakati akijibu swali la waandishi wa habari katika mkutano wake jana, Dar es Salaam, baada ya kumaliza mkutano wake na Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo katika Kanisa la Mtakatifu Yosefu.

Ziara hiyo ambayo amesema ni utaratibu aliouanza kukutana na viongozi wa dini, pia ilimkutanisha na Mufti wa Baraza la WaislamU Tanzania (BAKWATA), Shekhe Issa Bin Shaaban Simba. Sitta alikutana na Rais Kikwete juzi.

Hata hivyo, kwa mujibu wa Sitta, Rais Kikwete hajataja ni lini Bunge hilo litaanza tena kwa nyongeza ya siku 20 kwa mujibu wa sheria, baada ya siku 70 zinazomalizika mwezi huu, kuisha ili kufanya jumla ya siku 90. Lakini amesema uongozi wa Bunge umekusudia lianze tena Agosti mwaka huu.

Alisema lengo la kukutana na viongozi hao wa kidini ni kuwaeleza kinachoendelea Dodoma, kwa kile alichodai viongozi hao wana ushawishi na wafuasi wengi nyuma yao, hivyo si busara kusikia mitaani.

Katika mkutano huo Sitta alikanusha habari ya gazeti moja lililodai anakwenda kuwaangukia viongozi hao na kusema hana dhambi za kufanya hivyo.

“Leo (jana) nimepanga kukutana na viongozi wa dini zetu na si hawa tu nitakaokutana nao, nitaendelea na utaratibu huu kwa viongozi wengi hata wenye wafuasi wachache, hawa wana ushawishi japo hawahusiki sana na siasa lakini ni viongozi wa jamii, wanapaswa kupata taarifa sahihi ya nini kinachoendelea Dodoma,” alisema Sitta.

Alisema katika mazungumzo yake na Kardinali Pengo jana asubuhi, amemweleza kwa kifupi mchakato unavyoendelea Dodoma na yeye (Pengo) alimhakikishia kuwa Kanisa Katoliki linaliombea Bunge Maalumu la Katiba na wajumbe wote ili lengo lifikiwe na Watanzania wapate Katiba mpya na yenye ubora.

Baada ya kutoa maelezo hayo mafupi ya mkutano wake na Pengo, Sitta akijibu maswali ya waandishi wa habari kuhusu mwenendo wa Bunge hilo, ikiwemo kama muda wa takribani wiki tatu uliobaki unatosha kumaliza kazi iliyo mbele yao, alisema muda huo hautoshi.

“Ni dhahiri mpaka Aprili 28 tutakuwa hatujamaliza Bunge, itabidi tupishe Bunge la Bajeti la Muungano, Wawakilishi watarejea Zanzibar na sisi wengine tutabaki Dodoma, bajeti itafanyika si chini ya miezi miwili, yaani Mei na Juni,” alisema na kuongeza: “Jana nilionana na Rais Jakaya Kikwete nikamweleza hali halisi ilivyo, kimsingi alikubali ataongeza muda ingawa hatukufikia kutaja ni lini. Ila sisi tunakusudia tuanze tena Agosti, nimemweleza kwa undani maana hata baadhi ya nchi nyingi zimechukua muda kuandika Katiba, akaona ukweli huu akatuongezea”.

Sitta alisema Bunge litatangaza rasmi utaratibu huo utakapokamilika ila alisisitiza kuwa, kwa hali inavyoendelea hawawezi kuendelea kubaki Dodoma kwa ajili ya Katiba kwa kuwa kisheria siku zitakwisha na pia mwingiliano wa sikukuu za Pasaka na Muungano Aprili 26, zitapunguza siku.

Muundo wa Muungano:

Awali, akizungumzia kuhusu muundo wa muungano hasa baada ya kuibuka kwa madai ya kutaka Hati ya Muungano wakati wa mjadala wa sura ya kwanza ya sita ya Rasimu ya Katiba uliofanyika katika kamati, Sitta aliwataka wabunge kutopoteza muda kujadili serikali ngapi ziwepo.

Aidha, Sitta amesema ipo hatari ya kupoteza muda mwingi kuzungumzia muundo wa serikali uweje, jambo analoona kwa baadhi ya watu, wanataka serikali nyingi kwa uchu wa madaraka wakijua wakikosa uongozi upande mmoja, watapata upande mwingine.

Alisema ingawa suala la serikali ni muhimu kwa kuwa ndio linalotoa dira, ila haja kubwa ipo katika kuipitia rasimu Ibara kwa Ibara kama alivyoagiza Rais Kikwete.

Alitolea mfano suala la uadilifu na kushauri wajumbe wakipitia vizuri, watashauri mfumo gani uwekwe kuwabana zaidi viongozi.

“Kiongozi anapaswa ajue anaingia katika utumishi wa umma si kuchota fedha na kufanya ufisadi bali suala kubwa ni maendeleo ya nchi, ustawi wa wafanyakazi, wakulima na vijana, kuhakikisha sheria zinakuwepo kuzuia mikataba mibovu, kwa mfano Tanesco (Shirika la Umeme Tanzania) inavyopandisha umeme, wananchi wanaumia.”

“Tukiingia katika sura nyingine za rasimu, Katiba lazima ibane tutunge sheria zilizo wazi, angalia suala la Tume ya Maadili ya Viongozi wa Umma, tunajaza fomu kisha zinakuwa siri, sasa zina haja gani, ni za nini, si bora tuache, maana naweza kujaza nina kijumba kibovu kimoja, kumbe nina majumba,” alitoa mfano Sitta.

Alisema, “Ili kuzuia viongozi kujitajirisha, ni lazima sheria ziwe kali la sivyo wizi utaendelea, sheria inapaswa kuwakwamisha wanaopenda madaraka…., maombi yangu kuhusu mchakato, pamoja na purukushani, kutaka kuonekana, vijana machachari, lakini wengi wanataka Katiba mpya ipatikane.”

Sitta akifafanua kuhusu ama serikali tatu ama mbili, alinukuu alichowahi kusema mwanasiasa mkongwe nchini, Kingunge Ngombale- Mwiru kuhusu suala hilo kwamba ni kama wanaotaka serikali tatu wanataka madaraka, kwamba akikosa uongozi katika upande mmoja, apate kwingine.

Hati ya Muungano;

Sitta aliwaambia waandishi wa habari kumekuwepo na madai ya hati ya Muungano katika kamati na kwamba, ni ajabu kuona ndoa iliyodumu kwa miaka mingi, wahusika sasa wamekuwa vikongwe, anatokea mtu anadai cheti cha ndoa.

“Ni kama haamini kwamba hiyo ndoa ilifungwa ama! Ni ajabu kweli, vielelezo ni pamoja na Sheria ya Bunge ya Aprili 5 mwaka 1964, Msekwa akiwa Katibu wakati huo alikwenda katika kamati kueleza yaliyotokea wakati ule, Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Jaji Frederick Werema amekwenda kueleza.” “Ndoa watu wamefunga miaka, wamekuwa vikongwe, wajukuu leo wanadai cheti cha ndoa, ni upuuzi, mtu anayehitaji utafiti aendelee, hakuna anayemzuia ila haituzuii sisi kuendelea,” alieleza Sitta.

Ripoti za Kamati;

Kwa mujibu wa Sitta, Alhamisi na Ijumaa wiki hii, taarifa za kamati zitatolewa bungeni na maoni ya wengi na ya wachache yataelezwa ili kuruhusu mjadala kuanza ndani ya ukumbi na kwamba katika sura ya kwanza hadi ya sita, kila mjumbe atachangia.

“Baada ya hapo kazi itakuwa nyepesi, siwezi kutabiri kitakachotokea lakini hoja yenye maana itashinda, ukiacha wachache wenye utamaduni wa fujo, wengi wanataka ifike mahali tupate Katiba mpya, tusichezee mabilioni ya Watanzania bure.

Uzoefu wa Kenya;

Sitta alitumia nafasi hiyo kutolea uzoefu wa nchi jirani ya Kenya mwaka 2007 walipoingia katika machafuko ya kisiasa baada ya kushindwa kufanya mabadiliko katika Katiba yao na kufanya uchaguzi.

Alisema kazi inayofanyika Dodoma ni kubwa hivyo inapaswa kufanyika kwa umakini mkubwa vile vile. Akiwa na Mufti Mkuu Akizungumza mara baada ya kukutana na Mufti wa Tanzania, Shekhe Issa Bin Shaaban Simba, Sitta alisema ujumbe wake ulipokewa vizuri katika Ofisi za Bakwata, Dar es Salaam na kwamba Mufti alishukuru hatua hiyo ya Waislamu kushirikishwa.

“Ukweli Mufti amefurahia huu ujio wangu hapa na kuueleza kuwa anafuatilia kwa makini kile kinachoendelea kwa sasa kule Dodoma na zaidi ameuombea mchakato huu uweze kuisha kwa amani na utulivu hadi katiba mpya itakapopatikana” “Zaidi ametutaka wajumbe wote kuvumiliana na kufanya kazi yetu tukitanguliza maslahi ya Taifa na kuachana na misuguano ili hatimaye katiba iweze kupatikana,” alisema Sitta.

CHADEMA ARUSHA WAZIDI KUMONG'ONYOKA

$
0
0
CHAMA Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) mkoani Arusha kimeendelea kumeguka baada ya jana vigogo wake wanne wakiwemo wenyeviti wawili wa wilaya kutangaza kujiuzulu nyadhifa zao pamoja na uanachama kutokana na ufisadi unaodaiwa kuwepo ndani ya chama hicho ngazi ya taifa.

Wakitangaza uamuzi huo jana mbele ya waandishi wa habari jijini Arusha Mwenyekiti wa Chadema wilaya ya Monduli, Amani Silanga na Mwenyekiti wa wilaya ya Ngorongoro, Revocatus Parapara walisema baada ya kujiuzulu nyadhifa na uanachama wanatafakari kuona chama gani watajiunga nacho.

Akizungumza wakati wa kutangaza azma hiyo, Silanga alisema amefikia uamuzi huo kutokana na manyanyaso na uvunjaji wa katiba unaofanywa na viongozi wa chama hicho mkoa kwa mashinikizo ya uongozi wa taifa ili kutimiza malengo yao.

Silanga alisema moja ya hatua za uvunjaji wa katiba ni pale alipotangazwa kusimamishwa uongozi na katibu wa chama hicho kanda, Amani Golugwa kufuatia msimamo wake wa kupinga kusimamishwa uongozi kwa naibu katibu mkuu Zitto Kabwe, mjumbe wa kamati kuu Dk Kitila Mkumbo na aliyekuwa mwenyekiti wa wake mkoa wa Arusha, Samson Mwigamba.

Alisema kutokana na msimamo wake huo katibu huyo alitangaza kumsimamisha uongozi pasipo vikao husika kukaa na kumjadili.

Naye mwenyekiti wa wilaya ya Ngorongoro alisema ameamua kujiuzulu nafasi zake hizo kutokana na kutambua kuwa Chadema sio chama cha ukombozi wa kizazi hiki kama wanavyodai kwa kuwa kimeonekana kuwa na maslahi na baadhi ya watu siyo Watanzania.

Alisema hatua za yeye kusimamishwa uongozi na mtu mmoja tu bila vikao kukaa tena kwa madai ya usaliti kwa kukataa kuunga mkono kusimamishwa uongozi kwa Zitto Kabwe na wenzake kulisababisha kukata tamaa na chama hicho.

Alisema kwa muda aliokaa madarakani wilayani humo aliweza kuanzisha matawi ya chama hicho katika kata 20 na kupata wanachama 15,000 ambao kwa sasa wapo nyuma yake kujiunga na chama atakachojiunga nacho yeye kwa maslahi yao na jamii.

Vigogo wengine waliotangaza kujiuzulu nafasi zao za uongozi na uanachama ni mwenyekiti Chadema kata ya Terati jijini Arusha, Gerald Majengo na Katibu mwenezi wa kata ya Olorien, Prosper Mtinanga ambao wote kwa pamoja wamedai kuchoshwa na utapeli na ufisadi wa kisiasa uliopo ndani ya Chadema.

Aidha aliongeza kuwa Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema amekuwa akifanya kazi za viongozi wa chama kwa kutangaza kuwafukuza wanachama wanaozungumza ukweli ambapo yeye binafsi aliwahi kupigwa na kutangazwa kufukuzwa uanachama na Mbunge huyo kwa kuhoji tu kiwanja alichopewa na wafadhili kwa ajili ya ujenzi wa hospitali ya akina mama.

Naye Mtinanga alieleza kuwa chama hicho kimekuwa na ufisadi sio wa fedha tu au mali za chama bali hata katika nafasi za uongozi ambazo zimekuwa zikitolewa kwa upendeleo kwa ukabila, ukanda na hata kifamilia, jambo ambalo linaonesha kuwa chama hicho kinaendeshwa kama Saccos.

Mpasuko huu unatokea kipindi ambacho Chadema kimeonekana kuangukia pua vibaya katika chaguzi mbalimbali za marudio za ubunge na udiwani nchini ambapo katika chaguzi za kata 27 Chadema iliambulia kata 3, dhidi ya 23 zilizochukuliwa na CCM wakati kati uchaguzi wa wabunge katika majimbo ya Kalenga na Chalinze CCM iliibuka mshindi kwa asilimia zaidi ya 80.

YANGA..AZAM UKILALA UMELIWA

$
0
0
YANGA na Azam FC leo zinaendelea na mchuano wao mkali wa kuwania ubingwa wa soka wa Tanzania Bara wakati zitakaposhuka dimbani katika viwanja viwili kuwania pointi tatu muhimu.

Vinara Azam FC watasafiri hadi Mlandizi mkoani Pwani kwenye Uwanja wa Mabatini kuikabili Ruvu Shooting Stars ya huko wakati wanaoshika nafasi ya pili, mabingwa watetezi, Yanga watakuwa kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kuwakabili Kagera Sugar ya Missenyi mkoani Kagera.

Azam FC inayosaka ubingwa wa Tanzania Bara kwa mara ya kwanza, iko kileleni ikiwa na pointi 53 baada ya timu zote kushuka dimbani mara 23, wakati Yanga ni ya pili kwa kuwa na pointi 49.

Zikishinda mechi zao tatu zilizobaki zikiwamo za leo, Azam FC itafikisha pointi 62 na Yanga itafikisha pointi 58, hivyo vijana hao wa Chamazi, kutawazwa bingwa kwa mara ya kwanza.

Mbali ya mechi ya leo, Azam FC itashuka dimbani Aprili 13, kwenye Uwanja wa Sokoine jijini Mbeya kuikabili Mbeya City na kumalizia ligi Aprili 19, mwaka huu kwa kuivaa JKT Ruvu kwenye Uwanja wa Azam Complex.

Yanga mbali ya kuivaa Kagera Sugar leo, itakuwa mwenyeji wa JKT Oljoro, Aprili 13, mwaka huu jijini Arusha, kabla ya kumalizia na watani wao wa jadi, Simba, Aprili 19 kwenye Uwanja wa Taifa.

Kwa hiyo, kwa hesabu hizo, hakuna timu inayohitaji kulala kwani endapo mojawapo italala, uwezekano wa mwenzake kuwa bingwa ni mkubwa na hasa kwa upande wa Yanga ambayo ikiteleza tu, Azam bingwa.

Ni kwa msingi huo, kila mechi kwa kila timu ni fainali kwao ndio maana macho na masikio ya mashabiki wa soka leo yataelekezwa Mabatini, Pwani na Taifa, Dar es Salaam kufahamu nini kitatokea.

Katika kujiimarisha na mechi ya leo, wachezaji wa kimataifa wa Yanga, Haruna Niyonzima na Emmanuel Okwi, watakuwa ni miongoni mwa wachezaji watakaoivaa Kagera Sugar.

Wachezaji hao pamoja na David Luhende na Athuman Idd hawakuwemo kikosi kilichoivaa JKT Ruvu mwishoni mwa wiki iliyopita wakidaiwa kuwa ni wagonjwa.

Kwa mujibu wa tovuti ya Yanga, wachezaji hao wanaendelea vizuri na kwamba walijiunga kwenye mazoezi toka juzi.

“Wachezaji wote wanaendelea vizuri na mashabiki wategemee kuwaona uwanjani leo,” alisema Kocha Mkuu wa Yanga, Hans van der Pluijm.

Pluijm alisema vijana wake 20 walioingia kambini wote wapo kwenye hali nzuri, kiafya, kifikra na morali ya kusaka pointi tatu kwani wanahitaji kutetea ubingwa tena kwa msimu wa pili mfululizo.

Katika mchezo wa awali uliozikutanisha Kagera Sugar na Yanga kwenye Uwanja wa Kaitaba mjini Bukoba, Yanga ilishinda mabao 2-1, wafungaji wakiwa ni Mrisho Ngasa na Hamisi Kiiza. Ligi hiyo itaingia raundi ya 25, Aprili 12 na 13 mwaka huu ambapo timu zote 14 zitakuwa viwanjani.

Aprili 12 mwaka huu itakuwa Mtibwa Sugar dhidi ya Ruvu Shooting (Manungu, Morogoro), Coastal Union itaikabili JKT Ruvu (Mkwakwani, Tanga), na Tanzania Prisons itakuwa mwenyeji wa Rhino Rangers (Sokoine, Mbeya).

Aprili 13, mwaka huu ni Mgambo Shooting itacheza na Kagera Sugar (Mkwakwani, Tanga), Simba itakuwa mwenyeji wa Ashanti United (Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam), Mbeya City itaialika Azam (Sokoine, Mbeya) na Oljoro itawakaribisha Yanga (Sheikh Kaluta Amri Abeid, Arusha).

LINAH KUNA STAA ALITAKA TUFANYE USAGAJI

$
0
0
Makala: Joseph Shaluwa
NIKISEMA msichana huyu ni kati ya mastaa wa Bongo Fleva wanaofanya vizuri nitakuwa sijampa sifa za bure! Ni kweli anaweza. Sauti yake, anavyoweza kutawala jukwaa ni kati ya mambo yanayosherehesha sifa hiyo.

Ni msichana mdogo tu, mzaliwa wa tatu kati ya watano kutoka familia ya mzee Peter Sanga. Jina lake halisi ni Estelina lakini maarufu zaidi kwa jina la Linah akiwa zao la Nyumba ya Vipaji Maalum Tanzania ‘THT’.

Kibao cha Atatamani ndicho kilichomtambulisha kwenye ramani ya muziki mwaka 2009, leo miaka mitano baadaye, tayari Linah ni gumzo kwenye ulimwengu wa muziki. Achilia mbali kazi zake kisanii, kutokana na umaarufu wake, maisha yake binafsi yamegeuka kuwa habari.

Hapa kwenye Exclusive Interview, Linah ameeleza mambo mengi yanayohusu maisha yake nje na ndani ya sanaa. Kwanza nilimwulizwa kuhusu madai ya kuandikiwa nyimbo zake. Hapa anajibu bila wasiwasi: “Hilo siwezi kubisha, unajua kila mtu ana kipaji chake, mimi naweza zaidi kuimba. Nyimbo nyingi nimeandikiwa na Amini (Mwinyimkuu) na Barnaba (Elius).”

Inasemekana bado una uhusiano na Amini, ikoje?
Mh! Nadhani watu wanashindwa kuelewa. Kweli Amini alikuwa mpenzi wangu, tena tulioshibana na kufikia hatua ya mbali kabisa lakini  tumeachana.

Hata hivyo, kutokana na kazi zetu, huwa tunakutana mara kwa mara, naonekana naye mahali popote, labda ndiyo maana watu wanafikiri bado tunaendelea.

Mimi nina mtu wangu na kila mtu anamjua – Nagari Kombo (yule  aliyemkumbatia mchezaji wa Timu ya Taifa ya Brazil, Ricardo Kaka, Uwanja wa Taifa) na Amini naye ana maisha yake.

Nini kiliwatenganisha?
Hakuna kitu cha moja kwa moja ambacho naweza kukitaja kuwa ni sababu ya kuachana kwetu. Nilimpenda sana Amini, naye alinipenda pia, lakini kuna mambo tulikuwa hatuendi sawa.
Ilifikia mahali tukaona kwa namna hali ilivyokuwa, hatuwezi kuendelea kuwa wapenzi. Tukaamua kuachana ingawa lazima nikiri kuwa tuliachana tukiwa bado tunapendana.

Unatajwa kwenye usagaji, ni kweli?
Usagaji upo sana kwa mastaa, nausikiasikia lakini mimi sijawahi kusagana na wala sifikirii. Lakini ni kweli kuna staa mmoja, naomba nisimtaje, alianza kuonyesha dalili za kunitaka kwenye huo mchezo mchafu, nikavunja urafiki naye.

Vipi bifu lako na Jaydee?
Aisee katika wanamuziki wa kike wanaonivutia, Jide (Judith Wambura) ni wa kwanza. Ni kweli kulitokea kutokuelewana kati yetu, ni mambo ya kawaida kwenye kazi. Natamani sana siku moja nifanye naye kazi.

Unajifunza nini kupitia Ray C?
Ray C (Rehema Chalamila) ni mzuri, anaimba vizuri, ana mwonekano mzuri na anajua anachokifanya kwenye game. Mambo yaliyopita hapo kati naweza kusema ni ajali tu, lakini uzuri ni kwamba ameshaachana na hayo mambo (matumizi ya madawa ya kulevya).

Inawezekana aliingia kwa kujaribu au kuwaiga mastaa wenye mchezo huo, lakini matokeo yake yamekuwa tofauti. Nashauri wasanii wenzangu, tuwe makini, siyo kila kitu cha kuiga.

Nini kinaendelea kati yako na Mchungaji Gwajima?
Mchungaji Josephat Gwajima (wa Kanisa la Ufufuo na Uzima) ni baba yangu wa kiroho. Alinisaidia sana. Kuna wakati nikiwa nasoma, nilisumbuliwa sana na mapepo. Wazazi wangu walihangaika sana na mimi, baadaye wakanipeleka kanisani kwake.

Niliishi pale karibu mwaka mzima. Ilibidi nihairishe mwaka mmoja wa kidato cha tatu. Ilikuwa maombi muda wote. Nashukuru Mungu nilipona na nikafanikiwa kumaliza masomo yangu. Mpaka sasa naendelea vizuri.

Mafanikio yako kimuziki yakoje?
Nashukuru muziki umenisaidia mengi. Kwanza najulikana, napata dili kila kukicha. Kuna nyumba ya familia tunajenga Mbezi, kuna biashara zangu nipo mbioni kufungua na naihudumia familia yangu vizuri.

Siishi kwetu, nimepanga nyumba yangu mwenyewe na ninajilipia kodi, naweza kujihudumia kwa kila kitu! Kwangu hayo ni mafanikio, mengine yatakuja taratibu.

Kwanini umesisitiza unajilipia kodi mwenyewe?
(Anacheka) Mh! Unajua wasichana wengi wa mjini wanalipiwa nyumba na mabwana zao, ndiyo maana mimi naona ni heshima kufanya hivyo mwenyewe na kuliweka wazi.

Mahojiano haya yanapatikana Global TV Online iliyo ndani ya mtandao namba moja wa burudani Bongo,  www.globalpublishers.info ambapo utakutana na mastaa wengine kibao.
GPL

GODBLESS LEMA AMWANDIKIA RAIS KIKWETE WARAKA ..USOME HAPA

$
0
0
Mh Rais Nakusalimu . Wakati mwingine unapaswa kupewa pole na kuombewa na kufanyiwa dua kwani wewe ndie unatumikia ofisi kubwa kuliko zote Nchini na wakati huo huo unapaswa kupewa hongera kufikia malengo yako hayo ya kutumikia ofisi kubwa na ya Heshima kuliko zote Nchini , nimekuwa nikitafakari sana suala la Udini katika Taifa letu na huko Nyuma mwaka jana nilikuandikia pia waraka kuonya na kukumbusha hatua mathubuti kabla mambo hayajaaribika sijui kama ulisoma lakini naamini Usalama wa Taifa ambao siku hizi wanatumikia CCM watakuwa walisoma na Nape na wenzake pia walipata fursa ya kuusoma .
Mh Rais katika waraka hule nilisema hivi “ Mh Rais Taifa linahitaji Tiba “ siwezi leo kuandika kile nilichosema katika waraka ule ila niliweza kubashiri sumu ya udini inayoendelea katika Taifa lako na langu, Mh Rais , ukweli nakwambia ukifanya mchezo kidogo sana Taifa hili linapotea likiwa mikononi mwako kwani hali ya Nchi sio nzuri hata kidogo na watu waliokuwa wanaishi kwa umoja na upendo sasa wanaanza kutafuta mbinu za kugombana na kuuwana.
Mh Rais, Siasa ya Udini na Ukanda makusudi yake yalikuwa kudhoofisha vyama vya upinzani na yalifanikiwa kwa baadhi ya vyama kudhoofishwa sana na mkakati huo unaendelea dhidi ya Chadema lakini kinachosikitisha ni kuwa wale waliobuni mkakati huo walishindwa kutafakari au kuona madhara yake mbele .
Mh Rais, mkakati wa kudhoofisha Chama cha Siasa kwa Udini na Ukanda hauishi tu kuangamiza hicho Chama bali kuwagawa Watu na Taifa kwa Ujumla , Mtu anapojaribu kusema Chadema ni Chama cha Wakristo kimsingi matamshi hayo hayaangamizi Chadema tu bali yanagawa Watu kwa matabaka ya Udini wao na na kufanya Dini moja iamini kuwa Dini nyingine ni mbaya na hivyo mpango huo unafanya Watu waanze kutazamana kwa Udini na Ukabila na matokeo yake ndiyo haya tunaanza kuyaona leo . Mh Rais, Taifa linahitaji tiba , Hivi karibuni Waziri Mkuu alienda Geita kwenye mgogoro wa Waisilamu na Wakristo na niliona mawazo ya Waziri Mkuu kwenye vyombo vya habari na kwa kweli nilisikitika kwa busara zile zilizokuwa zimejaa hofu kubwa . Tatizo lile lilianza na nani kati ya Mkristo na Muislamu anayepaswa kuchinja?
Mh Rais , Nilipoona jambo hili nilianza kujiuliza maswali mengi sana, kwanza , umakini huu kwa pande zote mbili juu ya jambo hili umeletwa na nini na nani? Kwani yako mambo mengi yaliyokatazwa na Biblia na Msaafu ambayo watu wote wa dini hizi mbili wamekataa kuyatii au kuyafuata , kwa mfano waislamu na wakristo vijana kwa wazee wanakunywa pombe pamoja baadhi yao kujenga mahusiano hata ya kimapenzi yasiyo rasmi bila hata kufuata utaratibu wa Msaafu wala Biblia lakini hapa hutaona ugomvi mkubwa sana japokuwa ni masuala yanayo mkera na kumuudhi mwenyezi Mungu sana.
Mh Rais , ndio maana katika suala hili la nani achinje kati ya Muislamu na Mkristo niliposikia maafa yake nikakumbuka waraka niliokuandikia mwaka jana kuhusu choko choko za Udini ambazo zimeanza kuleta maafa ambazo Mwanzilishi wake ni CCM .
Mh Rais Chama chako unachokiongoza , Team yako imekuwa ikifanya sana propaganda hizi za, Udini , Ukabila , na Ukanda usiku na mchana , lakini nimekuwa nikikerwa sana na Jinsi kabila la Wachaga linavyochukuliwa katika propaganda hizi na wanaofanya hivyo asilimia kubwa ni mashemeji wa Wachaga na mimi najiuliza wanaweza vipi kufanya Siasa za Ukanda na Ukabila wakati wao wenyewe ni familia moja ?
Kwa mfano , Mh Mwigulu Nchemba , Mh David Mathayo , Mh January Makamba , Mh Benjamin Mkapa , Mh Fredrik Sumaye , Mh Theo , Mh Dr Faustin Ndungulile , Mh Prof Ibrahimu Lipumba , Pro Mahalu , Mh Dr Hamis Kigwangala , Mh John Mgufuli , Mh Sospeter Muhongo , Mh Jaji Warioba, Idd Simba, Mh Salmin Amour , na wengine wengi wote hawa wameoa Kilimanjaro . Sasa unajiuliza hawa wote ni Viongozi ndani ya CCM na wengine ndio mabingwa wa kufanya Siasa za Udini na Ukanda , je wake zao ndani ya nyumba wanajisikiaje wanapoona waume zao wanatukana kabila za ndugu zao kwa sababu ya Siasa ? Hii ni hatari kubwa Mh Rais kama kuchinja ni suala zito kiasi hicho katika Imani ya Kiislamu na pia ni neno kutoka katika Kitabu cha Imani yao basi ni haki na kweli kuwa wao wanapaswa kuchinja kwa Imani ya Dini yao na wala wasilazimishwe kumkosea Mungu wao kwani hakuna maarifa na Busara inayozidi imani, lakini vile vile Wakristo wasilazimishwe kushiriki Ibada ambayo sio yao. Waislamu kama wanaamini kuwa wao kuchinja ndio jambo lililoamrishwa katika vitabu vyao basi sasa Jambo hilo liheshimiwe na kutafutiwa utaratibu na vile vile Wakristo wasipuuzwe kugoma kushiriki jambo ambalo kwa wengine lina sura ya Imani.
Nini Kifanyike?
Kwanza Chama chako na Viongozi wake uwakanye na kuwashauri mara moja kabisa kuacha propaganda za udini na ukanda , kwani katika hili hakuna namna Nchi inaweza kubaki salama , kwani hizo choko choko hazitokani na nia mbaya ya Waislamu na Wakristo bali ni siasa chafu iliyopandikizwa ili kuangamiza vyama vya Siasa na sasa imekwenda zaidi na imeanza kuwatesa wakati ambao Nchi ina matatizo mengi , Kwa mfano Chadema tulipoandama Arusha kupinga Uchaguzi wa Meya feki , Kiongozi mmoja wa Mkoa wa CCM hapa Arusha , alinukuliwa na vyombo vya habari akidai tunafanya maandamano hayo kwa sababu za Udini na ndio maana hatumtaki Meya , lakini kitu cha kushangaza huyu Meya Feki ni Mkristo tena Mchaga Kabila langu , lakini niliambiwa na tunampinga na Maaskofu wanampinga kwa sababu Chadema ni Chama cha Udini ‘ sasa najiuliza kama Meya huyu Feki ni Mchaga na ni Mkristo je hayo madai ya kijinga yanatoka wapi ? Kama Ukristo ni ajenda kubwa kwetu kwani nini tulimpinga sasa ? Huu ni mfano mmoja iko mingi sana inayoashiria mkakati wa makusudi wa kuangamiza Chadema na huku mkisahau kuwa maliangamiza Taifa , na ndio Mkuu wa Mkoa wa Arusha alipokuja tu alidai kuwa amekuja kupambana na Chadema na Wachaga , ila nimuhakikishie hataweza na asijaribu kamwe na mikutano ambayo amekuwa akiifanya aiche mara moja .
Pili, Mh Rais, ninaamini kuwa wewe umesafiri Nchi mbali mbali kuliko mimi , Ukienda Marekani , Spain , Brazil , China , Hong Kong , UK, Italy , Sweden, Botswana , Namibia , South Afrika , Zimbabwe na Nchi nyiongi utaona Maduka au Mabucha ya Nyama yameandikwa (Halal ) au unanua bidhaa yeyote ya aina ya Nyama na kukuta imeandikwa “Halal” na ni ustarabu kwamba bidhaa hiyo machinjio yake yamezingatia maadili ya Dini ya Kiislamu na Waislamu wenye Imani thabiti na Imani yao hapo ndipo watakapofanya manunuzi yao katika bidhaa hiyo ya aina ya Nyama. Lakini maeneno hayo hayo unaweza kupata nyama katika maduka mbali mbali yasiozingatia utaratibu huo na kwa hivyo watu wasiojali sana masuala ya Imani wala hawatasumbuka kuuliza na kusoma kama Nyama hiyo imezingatia masuala ya matakwa ya Imani Fulani.
Hivyo, Mh Rais, nafikiri ni vyema utaratibu huu ukaletwa hapa kwetu ili tuonyeshe Kujali Imani ya Waislamu katika Jambo hili ambalo limekuwa kwazo katika Jamii hizi mbili kubwa na kama ufumbuzi wake hautakuwa kuzingatia hili basi tarajia uchungu kuendelea kutembea kwenye vifua vya watu bila kusema na siku moja hali inaweza kuwa mbaya na tukapoteza Taifa.
Mh Rais, naiona hofu isiyokuwa ya kweli ya Mh Waziri Mkuu kuwa tukiruhusu hilo kuwa Wakristo na Waislamu wataweza kutengana kwenye mambo mengine mengi haswa katika Biashara na mambo mengine , kitu ambacho nasema sio kweli kwani , Sukari ,Mchele , Soda na Juisi na bidhaa nyingi hazina makatazo na maelekezo katika Imani , Mfano kila Mkristo anajua kuwa Mwislamu hatumi Nguruwe na Nguruwe kwa mwislamu ni haramu na hivyo Mkristo hawezi kupika Nguruwe na huku akijua kuwa wageni wake siku hiyo ni Waislamu.
Kwa hiyo hofu ya kuligawa Taifa kwa kurusu jambo hili haliwezi kutokea kwani ni miiko ya Kiimani ambayo pande zote zinapaswa kuheshimiana ili upande mmoja usione umekandamizwa na kupuuzwa , na hofu ya kibiashara inayoweza kutokea katika suala hili inapaswa kupuuzwa kwani IMANI ni zaidi ya Biashara japokuwa sioni jambo hili likitokea .
Mh Rais, nisikuchoshe sana, lakini haya ni maoni yangu na Mke wangu na sio Chama changu tumeamka leo Asubuhi tukasema tukuandikie tena kwani wewe ni Mkuu wa Nchi , Najua unaweza kuwa busy sana kusoma waraka huu mrefu ila najua Mwigulu na Nape lazima wausome na Rizwan pia hivyo niwaombe wakufikishe ujumbe huu kwa niaba ya familia yangu.
Mh Rais , We are pressed on every side by troubles, but not crushed and broken. We are perplexed because we don,t know why things happen as they do . But we don’t give up and quit, we are hunted down BUT God never abandons Us, We get knocked down BUT we get up again and keep going. The root of life need commitment and there’s a lot of suffer to get at the Climax. Don’t Give Up Mr President please, Help our Country now.
Godbless Jonathan Lema

RAIS KIKWETE ACHAGULIWA KIONGOZI BORA AFRIKA

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amechaguliwa kuwa Kiongozi Mwenye Mchango Mkubwa Zaidi katika Maendeleo Barani Afrika kwa mwaka 2013 .

Heshima hiyo kwa Rais Kikwete imetolewa na jarida maarufu la kimataifa la African Leadership Magazine Group na Tuzo la heshima hiyo itatolewa jioni ya leo, Jumatano, Aprili 9, 2014, katika sherehe iliyopangwa kufanyika Hoteli ya St. Regis mjini Washington, D.C ikiwa ni pamoja na chakula cha jioni.

Tuzo hiyo ya heshima kubwa hutolewa kwa viongozi wa Afrika ambao hutoa mchango mkubwa zaidi wa kiuchumi na kijamii kila mwaka kwa watu wao na limetolewa kwa Rais Kikwete kwa mwelekeo wake usiokuwa wa kawaida na wenye mafanikio makubwa kwa masuala ya utawala bora.

Source: East Africa Radio

TUWEKE USHABIKI PEMBENI..CCM INAMGOMBEA GANI WA URAIS ANAYEKUBALIKA ZAIDI YA LOWASSA?

$
0
0

Ni wazi wote humu jamvini kuna wanachama na wakereketwa wa vyama mbali mbali na vilevile ni wazi wote tunawafahamu viongozi wote wa chama cha mapinduzi.

Sasa ningeomba kwa hekima na busara tuweke ushabiki pembeni na mahaba ya vyama pembeni na hata kwa wale wanachama wa CHADEMA tunaomba mtusaidie kwa hili kwasabu wote tunaifaham CCM japo najuwa ci wote wanaoikubali lakin mnaweza mkatoa uchambuzi wa kina.

Sasa naomba mtuambie kwa sasahv CCM ilipofikia hapo ndani ya CCM nani anayekubalika na mwenye uwezo wa kupeperusha bendera ya chama cha mapinduzi zaidi ya Lowassa?kama yupo tunaomba kwa mwenye jina tofauti na lowassa amtaje na tujaribu kumchambuwa kama ana uwezo wa kumzidi Lowassa.

Nawasilisha

KENYA AIRWAYS WAMENUNUA DREAMLINER 6, ATC WANAKODI KANDEGE KA MOJA KA KWENDA MIKOANI KWA MBWEMBWE

$
0
0
Ndugu zanguni,

Jana wenzetu wakenya wameshuhudia historia mpya katika sekta ya biashara ya anga nchini mwao pale Rais wao alipozindua ramsi ndege ya Boeing 787 DREAMLINER. Ndege hii ni moja kati ya ndege sita ambazo wameagiza kutoka marekani. Na sasa jumla wana ndege kubwa 45.

Wakati huo huo, Air Tanzania wamekuja kwa mbwembwe na matangazo kibao kuwa wamekodi ka ndege ka abiria hamsini ka kwenda mikoani.

Tuweke siasa pembeni tuongelee uhalisia, ni kwa nini ATC wanashindwa hata kuungana ubia na mashirika makubwa ili na sisi tuonekane? Ni aibu kuona tundege twetu hatuwezi hata kwenda Zimbabwe tu. 

Hawa wenzetu hawanunui bali wanakopa, kwa nini na sisi tusikope? au hatukopesheki? hata used? 

BA wamekatisha safari za moja kwa moja Dar hivyo KQ na Swis Air ndio wamechukua soko ambalo kama tungekuwa na uwezo hilo lingekuwa soko letu kubwa. 

Inawezaje Precision air iwe na ndege nyingi kuliko ATC ya serikali? Watalii wote wanaokuja nyumbani wanapanda ndege za kuunga unga tu wakati kama tukiamua tuna uwezo wa kuwa na direct flights from US na Europe kuja home.

Kama mjuavyo, kwa sasa tumekuwa tunapendwa na kila mtu kwa sababu tuna gesi ya kumwaga, hivyo inabidi tutumie mwanya huu kuongea na hao marafiki wa sasa kutusaida na sisi tuwe na mapipa makubwa ya kwenda nje ya nchi sio hutu tu debe twa kwenda mwanza tu. Tuwaombe watukodishe kama hawataki kutuuzia. Hata tukiwa na jumbo mbili tu za kwenda masafa marefu tutakuwa tumemaliza kila kitu

Wivu sina, ila karoho kanauma sana...

KAJALA,WEMA HEBU NISIKILIZENI KIDOGO!

$
0
0
KWENU,Mastaa wa filamu Bongo, Kajala Masanja na Wema Sepetu. Poleni kwa tifu linaloendelea kati yenu. Hongereni kwa kazi za kila siku za kujipatia kipato. Tuweke mambo yote pembeni, mimi kama kaka yenu, hebu tuzungumze kirafiki kidogo leo.

Nimefuatilia kwa karibu ugomvi unaoendelea kati yenu, moyoni imeniuma na nimeona naweza kuwashauri mawili matatu, nanyi mkiona inafaa, muyachukue kama dira ya tatizo lililopo kati yenu.

Kwanza kabisa, kiini cha ugomvi wenyewe mpaka sasa ni kama hakina mashiko. Ugomvi unaendeshwa kwa maneno maneno zaidi ya uhalisia. Nilisikia eti, sababu ya ugomvi wenu ni hii; mlikutana saluni Masaki, Kajala akiwa amelowana kwa jasho kwa vile alitokea mazoezini, Wema alipotaka kumkumbatia, Kajala akakataa kwa nia nzuri ya kutomchafua mwenzake – hapo bifu likaanza.

Inawezekana wakati Kajala akifanya hivyo, alikuwa na nia njema tu, lakini Wema akahisi labda mwenzake anajisikia! Ni kawaida, hatuwezi kufanana mioyo na mawazo.

Tatizo ni pale wanapotokea watu wengine ambao wanakuza huo ugomvi. Kuna watu wanajiita Team Wema, hao nadhani hawana kazi. Wanakesha kwenye mitandao ya kijamii kuchochea huo ugomvi.

Mara inasemwa sijui mmenyang’anyana bwana, mara mmepigana na mengine mengi. Ya nini yote hayo? Kuna wakati hao Team Wema walianza kusema Kajala anatakiwa kurudisha milioni 13 za Wema ambazo alilipa faini mahakamani.
Jamani, thamani ya milioni 13 kwenye matatizo inafanana na kiasi kama hicho kwenye furaha? Siamini kama Wema anazitaka hizo fedha. Alizitoa kwa moyo kwa lengo la kumsaidia rafiki yake.

Niliona picha zilizopigwa mahakamani, wote mlikuwa mnamwagika machozi. Naamini hayakuwa ya kinafiki – ilikuwa furaha. Kwa nini leo mtofautiane kwa jambo dogo? Hata kama ni kubwa, maana inawezekana mna kitu kingine mnachogombania ambacho sikijui, lakini bado nasema kuna kila sababu ya kumaliza hizi tofauti.

Amini msiamini, tofauti zenu hazina maana yoyote. Mtashindwa kufanya mambo makubwa ya maana kwa faida yenu na kubaki mnaendekeza ugomvi ambao mnaweza kuuepuka.

Ninyi ni binadamu, najua mna mioyo, najua kila mmoja anaamini katika imani yake. Uadui umekatazwa kwenye vitabu vyote vitakatifu. Visasi vimezuiwa kabisa kwenye vitabu vyote. Hekima na busara ni sifa njema.

Kusameheana ni kitu kinachoonesha uungwana wa hali ya juu kwa binadamu mkamilifu. Bado mnayo nafasi ya kuzungumza. Hakika nawaambia, mnapoteza mambo mengi ya maana kwa kuendekeza hilo bifu.

Hebu tulieni, vuteni picha wakati Wema unamsaidia mwenzako pale mahakamani, ilikuwaje? Siamini kama ulikuwa unajionyesha kuwa unazo! Sitaki kuamini kuwa una pesa za kuchezea. Bila shaka ulikuwa ni msaada wako kwa kuguswa na matatizo ya mwenzako.

Asitokee mtu akatumia kigezo hicho kuwagombanisha. Huu ugomvi unaweza kuwa na faida kwa watu wengine, siyo ninyi. Mlaanini shetani.
Nawapenda sana dada zangu. Ni furaha yangu kuwaona pamoja tena mkili songesha kwenye tasnia yenu. Ni wakati wenu wa kutafakari! Inawezekana.
Yuleyule,
Mkweli daima,
............................
Joseph Shaluwa

LADY JAY DEE ATOA NAFASI YA MASHABIKI KUHUDHURIA BURE UZINDUZI WA WIMBO WAKE MPYA

$
0
0
Lady Jay Dee anatarajia kuzindua audio na video ya wimbo wake mpya unaoitwa ‘Nasimama’, Jumamosi, April 12. Lakini anahitaji kuwa na mashabiki ambao watapata nafasi ya upendeleo kutokana na kufuatilia hatua zake kimuziki.

Jana, mwimbaji huyo alitoa nafasi kwa mashabiki 15 kushinda nafasi ya kuhudhuria uzinduzi huo bila kiingilio kwa kujibu swali lililouliza Studio ambayo amerekodi ‘Nasimama’ na tayari ilipata majibu sahihi kutoka kwa mashabiki hao kuwa ni Sharobaro Records.

Leo, Anaconda ameongeza swali lingine na nafasi nyingine 15 kupitia akaunti yake ya Facebook na Twitter kwa wale watakaoweza kutaja kampuni aliyofanya nayo video.

“Hii ni kwa walioko Dar es salaam tu, Shughuli inafanyika Nyumbani Lounge Jumamosi April 12.

SWALI: Video ya wimbo Nasimama imetengenezwa na kampuni gani?” Inasomeka sehemu ya maelezo ya Jide.

Kama unataka kuwa sehemu ya uzinduzi huo kupitia nafasi hii maalum, nafasi hii inaweza kuwa yako. Uzinduzi huo utafanyika Nyumbani Lounge.

DIANA"SIWEZI KUMVULIA NGUO NA KULIWA URODA NA MWANAUME ALIYETEMBEA NA LULU MICHAEL"

$
0
0
Msanii wa bongo movie Diana Kimaria ameibuka na kukanusha vikali kuwa kamwe hawezi kuliwa uloda na mwanaume aliyempitia rafiki yake Lulu Michael kwa sababu kwani wao ni zaidi ya rafiki.
Akizungumza na gazeti namba moja nchi kwa habari zaa uchunguzi la Maskani Bongo baada ya kutokea taarifa kuwa amekuwa akiiba wanaume za rafiki zake akiweo huyo Lulu, Diana alisema" Katu siwezi kufanya hivyo hivyo mwanaume yeyote anaemla uloda LULU mimi ni shemji yangu hivyo siwezi fanya upuuzi huo" Alisema Diana ambae amewahi kuishi kinyumba na msanii fuska Manaiki Sanga zaidi ya nusu mwaka huku Mama yake na Diana akitoa baraka za wawili hao kuoana kabisa

DUDU BAYA AKANA TAARIFA ZILIZOZAGAA KUWA AMEMKATA MAMA YAKE MASIKIO

$
0
0
Siku ya leo zimesambaa habari katika mitatandao kuwa Mwanamuziki Dudubaya Amemkata Mama yake Masikio na amekimbia na kujificha huku Polisi wanamtafuta, Dudubaya Amehojiwa na Gossip Cop na kusema hata yeye anazisikia hizi habari na kupigiwa simu tu hajui chochote na wala hatafutwi na Polisi...Lakini amesema anajua wanao sambaza hizo Story ni ndugu zake mwenyewe ambao wanamuonea wivu baada ya kumjengea mama yake Nyumba.....

WADADA WALIOKUWA WANAFANYISHWA BIASHARA YA NGONO CHINA WARUDISHIWA PASSPORT ZAO

$
0
0
Wiki iliyopita kupitia kipindi cha XXL na Gazeti la Makorokocho online niliweka hewani ule waraka wa wazi wa sauti uliosomwa kutoka China na Mwanadada Candy kwa niaba ya Wanadada wenzake wa Kitanzania walikua wakilalamikia kushikiliwa kama watumwa na kufanyishwa biashara ya ngono kwa lazima, waraka ule ulikua maalum kwa wizara ya mambo ya nje na watanzania kwa ujumla kwani kinadada wale walikua wakiomba msaada warudishiwe Passport zao zilipokonywa na watanzania wenzao, Binafsi Candy anashikiliwa nchini china tangu December mwaka jana,
sasa kwa mujibu wa chanzo cha habari cha kuaminika ni kwamba Candy na Wenzake wamerudishiwa Passport zao ila simu zao za mkononi wamepokonywa, Candy anawashukuru watanzania wote kwa kuonyesha kuguswa na kwa vyombo vya habari kwa kuweka hewani waraka wao, na sasa hivi wako wanatafuta shughuli za kufanya kwani zipo nyingi sanaaaa China.
- See more at: http://www.makorokocho.co/2014/04/hatimaye-wadada-waliokuwa-wanafanyishwa.html#sthash.ZFu8H0Fx.dpuf
Viewing all 104785 articles
Browse latest View live




Latest Images