Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104689 articles
Browse latest View live

AJINYONGA Kwa Katani Kisa Ugumu wa Maisha

$
0
0
Watu wawili wamekufa katika matukio tofauti mkoani Rukwa, likiwamo la mmoja kujiua kwa kujinyonga kwa kutumia kamba ya katani kwa madai ya ugumu wa maisha.


Katika tukio la kwanza lililotokea usiku wa kuamkia juzi, mkazi wa kijiji cha Chipu Manispaa ya Sumbawanga, Ignas Mambi (52) alijiua kwa kujinyonga.

Mwenyekiti wa kijiji hicho, Deus Masanja, alisema chanzo cha kujiua kwa mtu huyo kinadhaniwa kuwa ni ugumu wa maisha.

Alisema mara kwa mara marehemu alikuwa akilalamikia ugumu wa maisha, huenda ndiyo sababu inayodhaniwa kuchukua uamuzi mgumu na kujinyonga porini katika mti kwa kutumia kamba ya katani.

Katika tukio la pili, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Rukwa, George Kyando, alisema lilitokea Desemba 13, saa tano asubuhi katika kijiji cha Kanyezi, wilayani Kalambo.

Katika tukio hilo, Kamanda Kyando alisema bibi kizee Noelia Pintilila (80) aliuawa kwa kupigwa na kitu kizito kichwani.

Kyando alisema mtuhumiwa baada ya kutenda kosa hilo, alikimbia kusikojulikana na kwamba alimuua bibi huyo kutokana na kuwa mtuhumiwa alikuwa akianguka kifafa na mara kwa mara alikuwa akimtuhumu bibi huyo kuwa ndiye anayemloga.

Kutokana na kitendo hicho, Kyando aliwasihi wananchi wa mkoa huo kuachana na imani za kishirikina na kujichukulia sheria mikononi kwa kuwa zimekuwa chanzo cha vifo vya watu wengi.

Soucre: Nipashe

WAKILI Albert Msando Akatwa Katwa Mapanga Dar

$
0
0
Ndugu zangu, nawashukuruni wote mliojaribu kunitafuta na kunipa pole toka jana. Sikuwa napatikana kwa sababu walionivamia waliiba simu pamoja na vitu vingine.

Kilichotokea: Usiku wa saa tano siku ya Alhamisi (juzi) nilisimamishwa na gari baada kupigiwa honi na kuwashiwa taa na gari iliyokuwa nyuma yangu. Niliposhusha kioo driver akawa anaongea haraka haraka kwamba nimewagonga wakati narudi nyuma parking na nakimbia. Nikamjibu kwamba sijamgonga.

Akaniambia umetugonga angalia bampa. Kweli bampa lilikuwa limelegea. Ila sikuwa nimewagonga hivyo nikaendelea kubisha. Akaniambia shuka uangalie hata pembeni. Alikuwa amevaa smart tu so nikashuka. Wakati naangalia anaposema nimemgonga wakashuka wengine wawili kutoka kwenye gari na kunishika. Wakaanza kunishambulia huku wakinipora wallet, saa nk. Then wakanikata panga kichwani na kupekua gari wakaondoka na laptop na simu pamoja na funguo wa gari.

Kwa sasa naendelea vizuri baada ya kupata matibabu. Nawashukuru wote.

Albert Msando

VIDEO:Msanii Darasa akiwa na Hanscana wapata ajali ya gari huko Kahama

$
0
0
Mwanamuziki Darasa amepata ajali maeneo ya Ntobo barabara yakuelekea mgodi wa Bullyanhulu wilaya ya Kahama mkoa wa Shinyanga. Waliokuwa garini wote wamenusurika.

Katika gari hiyo pamoja na watu wengine alikuwa na mtayarishaji wa video aliye kwenye chart Hanscana.

TAZAMA VIDEO

VIDEO ya Ommy Dimpoz na Mpenzi Wake Ndani ya Mapenzi ya Show Off

$
0
0
Baada ya kuandamwa sana ana matatizo ndio maana hajawahi kuonekana na mwanamke na hana hata mtoto wa kusingiziwa na Nay wa Mitego, 
Kisha Diamond kuandika kuwa aligoma kumpumulia ndio maana ana visasi naye, Ommy katupia picha akiwa na mpenzi wake huko Instagram

ANGALIA VIDEO:

WAZIRI Mkuu: Kaburi la Faru John Litafukuliwa na Masalia yake Kupimwa DNA

$
0
0
WAZIRI Mkuu: Kaburi la Faru John Litafukuliwa na Masalia yake Kupimwa DNA
Mtazame hapa Chini Waziri Mkuu Akifunguka Hayo:


MWIGIZAJI Nisha Bebee Anywa Mkojo wake ili Amsahau Mwanaume Aliyemuumiza Kimapenzi

$
0
0
Mambo ndo yamefikia Huku, Kule kuumizwa kwa Nisha Bebee na Mwanaume aliyembaka na kumpa ujauzito kumemlazimu Nisha Bebee Kunywa mkojo wake ili Amsahau

Nimekuwekea Video Hapa Akiwa chooni na Kunywa:

HARUFU ya Maiti Saba Mto Ruvu Yafanyiwa Kazi

$
0
0
Siku moja baada ya gazeti hili kuripoti taarifa za kuwapo harufu mbaya na majimaji yanayotoka ilipozikwa miili ya watu saba waliofungwa kwenye viroba, Bibi Afya wa Wilaya ya Bagamoyo, Joyce Nganzo ametembelea eneo hilo kuona hali halisi.

Desemba 8, mwaka huu maiti saba ziliokotwa katika Mto Ruvu na muda mfupi baadaye zilizikwa kando ya mto huo huku Serikali ikiahidi kuendelea na uchunguzi.

Akizungumza na Mwananchi kwa simu jana, Nganzo alisema atakabidhi taarifa ya alichokiona kwa mkurugenzi wa halmashauri ya Bagamoyo kwa ajili ya kuifanyia kazi.

“Nilikwenda, taarifa nitampa Mkurugenzi, yeye ndiyo atakuwa na maamuzi zaidi,” alisema Nganzo.

Katibu wa Kitongoji cha Mtoni, kata ya Makurunge, Mukhtari Shebule alisema,

“Tunashukuru mmeliweka wazi suala hili, bibi afya alikuja kuangalia hali halisi, tunasubiri hatua zitakazochukuliwa kunusuru afya zetu,” alisema Shebule.

Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo, Hemed Mwanga alisema hana cha kuzungumza na baada ya kukamilika uchunguzi watatoa taarifa.

Kuhusu hali wasiwasi wa usalama kwa wanaotumia maji ya mto huo alisema, “Kuhusu suala hilo sikuwa nalifahamu nitafuatilia nijue unazungumzia nini.”

Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Hamad Masauni alisema kwa sasa uchunguzi wa suala hilo unaendelea na taarifa ya awali imeshatolewa na bosi wake, Mwigulu Nchemba.

“Muwe na subira kwa sasa , hadi hapo uchunguzi utakapokamilika mtapewa taarifa,” alisema.

Waziri Nchemba hakupatikana kuzungumzia hatua zilizofikiwa hadi sasa na simu yake iliita bila kupokea.


WAZIRI Mkuu Aunda Tume Ya Kuchunguza Taarifa Za Uhamisho Wa Faru John........Aagiza Kaburi Lake Litafutwe.

$
0
0
WAZIRI Mkuu Kassim Majaliwa amesema Serikali imeunda tume kuchunguza taarifa inayoelezea utaratibu uliotumika kumhamisha faru John kutoka Hifadhi ya Ngorongoro kwenda Sasakwa Black Rhino Sanctuary iliyoko kwenye Hifadhi ya Grumeti Serengeti pamoja na kutafuta kaburi la faru huyo.

Amesema timu hiyo ya wataalamu tayari imeshafika Sasakwa  VIP Grumet kwa ajili ya kutafuta kaburi na kuchukua vinasaba vya masalia ya faru John na kisha watakwenda kwenye Hifadhi ya Ngorongoro kuchukua vinasaba vya watoto wake  na kuvilinganisha na pembe hiyo ili  kubaini kama kweli pembe aliyopelekewa ni  ya faru John au la.

Waziri Mkuu ametoa kauli hiyo Jumapili, Desemba 18, 2016 wakati wa majumuisho ya ziara yake ya kikazi mkoani Arusha. Ziara hiyo ililenga kukagua utekelezaji wa shughuli za maendeleo na kuona utoaji wa huduma kwa wananchi.

"Tume niliyounda kwa ajili ya uchunguzi wa faru John imetua VIP  Grumet Serengeti kujiridhisha kama kuna kaburi la faru John na kama lipo wachukue vinasaba na baada ya hapo watakwenda Creter na kuchukua vinasaba vya watoto wa faru John na kuvipima kwa pamoja. Lengo ni kutaka kubaini kama pembe iliyowasilishwa kwangu Disemba 9 mwaka huu ni ya faru John,” alisema.

Waziri Mkuu alisema wakati faru John akiwa V I P Grumet taarifa zilisema ni mgonjwa na daktari alipompima mara ya kwanza akabaini faru huyo hakuwa na ugonjwa wowote.”Daktari alimpima tena kwa mara ya pili taarifa zikasema tena si mgonjwa  ghafla wakasema amekufa. Hili  haliwezekani,”.

Waziri Mkuu alisema ameiagiza timu hiyo kufanya kazi ya uchunguzi wa taarifa hizo kikamilifu kwa sababu Serikali imetumia fedha nyingi kuwaleta faru hao kutoka nchini Afrika Kusini. Ni lazima nyara hizo za Serikali zilindwe kwa manufaa ya Taifa.

Waziri Mkuu alipokea taarifa inayoelezea utaratibu uliotumika kumhamisha faru John kutoka Hifadhi ya Ngorongoro kwenda Sasakwa Black Rhino Sanctuary iliyoko kwenye Hifadhi ya Grumeti Desemba 9, 2016 katika kikao kilichofanyika kwenye makazi ya Waziri Mkuu Oysterbay jijini Dar es Salaam.

Kikao hicho kilihudhuriwa na Waziri wa Maliasili na Utalii, Prof. Jumanne Maghembe na baadhi ya watendaji wa wizara yake, Baada ya kupokea taarifa hiyo Waziri Mkuu alisema taarifa hiyo itafanyiwa kazi na wataalamu wa ofisi yake.

Akisoma taarifa hiyo mbele ya Waziri Mkuu, Prof. Maghembe alisema hadi kufikia Desemba 2015 wakati faru John anahamishwa alikuwa na watoto 26 (sawa na asilimia 70.2) ya faru wote waliokuwepo ndani ya kreta.

“Kati ya faru 37 waliokuwepo ndani ya kreta, watoto wake walikuwa 26 sawa na asilimia 70.2. Uamuzi wa kumuondoa John ulikuwa ni muhimu ili kuwezesha kuongezeka kwa faru weusi na kupunguza tatizo la ‘inbreeding’ ndani ya Hifadhi ya Ngorongoro,” alisema Waziri Maghembe.

Baada ya kuhamishiwa Sasakwa, Waziri Maghembe alisema Julai 10, 2016 afya ya faru John ilianza kudorora na alikufa tarehe 18 Agosti, mwaka huu.

 Taarifa hiyo iliandaliwa na Kamati ya Taifa ya Kuwalinda Tembo na Faru. Kamati hiyo inaundwa na Mkurugenzi Mkuu wa TAWIRI, Mkurugenzi Mkuu wa TANAPA, Mkurugenzi Mkuu wa NCAA na Mhifadhi Mkuu wa Ngorongoro.

 Akikabidhi pembe za faru huyo mbele ya Waziri Mkuu, Kaimu Mkurugenzi Msaidizi wa Kitengo cha Kupambana na Ujangili wa Wanyamapori, Bw. Robert Mande alimweleza kwamba pembe kubwa ya faru John ilikuwa na uzito wa kilo 3.6 na pembe ndogo ilikuwa na uzito wa kilo 2.3.

Desemba 6, mwaka huu, akiwa ziarani mkoani Arusha, Waziri Mkuu aliuagiza uongozi wa Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro (NCAA), umletee nyaraka zote zilizotumika kumhamisha faru maarufu kwa jina la ‘John’ kutoka kwenye hifadhi hiyo ifikapo Alhamisi, Desemba 8.

Alitoa agizo hilo alipotembelea ofisi za makao makuu ya NCAA zilizoko wilayani Ngorongoro, mkoani Arusha na kuzungumza na watumishi wa mamlaka hiyo pamoja na Wajumbe wa Baraza la Wafugaji ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kikazi mkoani humo.

IMETOLEWA NA:                                                      
OFISI YA WAZIRI MKUU, VIDEO:

MSHINDI wa Miss World 2016 Ndio Huyu… Afrika Yaingia Top5

$
0
0
Najua watanzania na waafrika wote walikuwa wanahamu ya kufahamu mshindi wa Miss World 2016 atakuwa ni mrembo kutoka nchi gani, mashindano hayo ambayo yamefanyika Washington Marekani, Afrika ilipata nafasi ya nchi za Kenya na Ghana kuingia TOP 20.


Muda ulifika na waandaaji wa Miss World walitangaza mshindi ambapo Miss Puerto Rico ndio alifanikiwa kushinda taji la Miss World 2016, lakini muwakilishi wa Tanzania Diana Edward kwa bahati mbaya hakufanikiwa kufika nafasi za juu.

Hata hivyo Afrika Mashariki imepokea good news baada ya nchi ya Kenya kufanikiwa kuingia TOP 5 na ndio nchi pekee ya Afrika iliyofanikiwa kuingia TOP 5, huku Miss Dominician Republic akishika nafasi ya pili na Miss Indonesia akishika nafasi ya tatu.

TAZAMA VIDEO ILIVYOKUWA:


VIDEO: Goli la Samatta lililoiokoa KRC Genk na kipigo dhidi ya Standard Liege Dec 18 2016

$
0
0
Jumapili ya December 18 2016 KRC Genk inayochezewa na mtanzania Mbwana Samatta iliwakaribisha Standard de Liege katika uwanja wao wa Luminus kucheza mchezo wao wa 18 wa Ligi Kuu Ubelgiji msimu wa 2016/2017.

Genk wakiwa katika uwanja wao wa nyumbani walianza kupata goli la uongozi dakika ya 3 kupitia Omar Colley kabla ya dakika ya 16 Orlando Carlos kufunga goli la kusawazisha na dakika ya 25 Ishak Belfodil kuongeza goli la pili na kuanza kuwa makini na ulinzi wa goli lao kuwadhibiti Genk.

Mchezo ulienda mapumziko KRC Genk wakiwa nyuma kwa goli 2-1 hali ambayo iliwawia vigumu kupata goli la kusawazisha mapema, Samatta ndio alikuwa mkombozi wa KRC Genk baada ya dakika ya 77 kupachika goli la kusawazisha kwa kichwa kupitia krosi iliyopigwa na Jere Uronen na kuufanya mchezo kumalizika kwa sare ya 2-2.

UJAMBAZI FNB Bank, Dada Mrembo Adakwa Kwa Ujambazi

$
0
0
Wakuu hii kitu inazunguka sana kwenye "social media",kuwa huyu dada alikuwa mfanyakazi wa FNB,alifukuzwa na baadae kaamua kuingia kwenye mtandao wa majambazi uliotengeneza mchoro kwa kwenda kuiba kwenye bank hiyo.

Mchoro wake uligonga mwamba,na hatimaye polisi kuwathibiti.Binti anaonekana mrembo,mwenye haiba lkn yamemshinda na kuamua kujiripua kwa kuvamia bank....HATARI SANAAAA


VIDEO: TUNDU LISSU ASOMA MESEJI ZA VITISHO ALIZOTUMIWA SAANANE KABLA YA KUPOTEA 

Dk Mwele Avunja Ukimya

$
0
0
Siku mbili baada ya Rais John Magufuli kutengua uteuzi wa aliyekuwa Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Utafiti wa Tiba na Magonjwa ya Binadamu (NIMR), Dk Mwele Malecela, mwanasayansi huyo amesema yupo imara na atazungumza wakati muafaka ukifika.

“Kwa leo siwezi kuzungumza lolote kutokana na hali ilivyo, na namna jinsi watu wanavyoendelea kulizungumzia jambo hili lakini nitazungumza wakati ukifika na mtajua,” alisema

Dk Mwele kwa sauti ya uchangamfu.

Uteuzi wake ulitenguliwa Ijumaa usiku baada ya kutoa ripoti ya mwaka ya taasisi hiyo iliyoonyesha kuwa watu 80 waliofanyiwa utafiti waligundulika kuwa na virusi vya homa ya zika.

Taarifa ya utafiti huo ilionyesha kuwa kati ya watu 533 waliopimwa, 83 (asilimia15.6) walikuwa wameambukizwa virusi vya homa zika. Pia, kati ya watoto wachanga 80 waliozaliwa na ulemavu wa aina mbalimbali, asilimia 43.8 walikuwa wameambukizwa virusi vya homa ya zika.


VIDEO: Muigizaji Nisha bebee anywa mkojo wake kisa kumsahau mwanaume aliemuumiza moyo wake 

BELLE 9 Ajibu Mapigo ya Darasa na Diamond Kwa Kishindo

$
0
0
Ama kwa hakika masikio yetu yalisikiliza nyimbo mbili ndani ya huu mwezi mpka nafikiri wengine walianza kuchoka. Kila kona ilikuwa ni Salome ya Diamond au Muziki ya Darasa.

Sasa Belle 9 ni kama kaja kujibu mapigo ya hizi ngoma mbili.

Sikiiza mdundo na mapigo alafu utagundua kitu.

Waliokuwa wanasema Belle 9 ana gundu hapa amewakata kauli na kudhiirisha muziki sio umahiri pekee na timing + kuielewa biashara hii.

NB; wimbo huu umetengenezwa kabla ya Salome na Muziki.

DIAMOND Kumdondosha Hasimu wa Zari Kwenye Wasafi Beach Party

$
0
0
Diamond Platnumz ni mfanyabiashara kwenye muziki asiyeogopa ‘kutake risk’ kwaajili ya kukamilisha azma yake, hata kama uamuzi atakaouchukua unaweza ukaleta mzozo ndani ya familia yake.

Katika kunogesha tamasha lake kubwa la Wasafi Beach Party, hitmaker huyo anamdondosha hasimu mkubwa wa mchumba wake Zari, Huddah Monroe. Kama umesahau, Huddah aliwahi kuingia kwenye bifu kali na Zari baada ya kudai kuwa amewahi kutembea na Diamond na kwamba staa huyo ni ‘mali ya umma.’

Diamond ameweka picha ya mrembo huyo kwenye Instagram akiwa ameipa kamera mgongo na kuwataka mashabiki wake kubashiri ni nani.


Katika kuthibitisha kuwa anakuja, mrembo huyo alipost video Instagram akiiimba wimbo maarufu wa Darassa, Muziki na kuandika: Coming HOME soon…
Niliota naolewa TZEEE,Single men mkuje kwa wingi tukamilishe ndoto😉
Na blah blah blahhh Sitaki kusikia….😜 Kamwili kangu kanatosha kujigamba..😂 #mistressofalltrades.”

HANSCANA Aeleza Chanzo Cha Ajali Mbaya ya Gari Aliyopata Akiwa na Darassa

$
0
0
Muongozaji wa video za muziki nchini, Hanscana amefunguka na kueleza nini kilitokea hadi wakapata ajali mbaya ya gari akiwa na rapa Darassa pamoja na watu wengine wawili.

Ajali hiyo ilitokea wakati wakiwa njiani wakitokea Kahama mkoani Shinyanga kwenda Kakola mkoani humo kwaajili ya show.

Akiongea na Bongo5 Jumatatu hii, Hanscana amedai hajui chanzo cha ajali hiyo huku akidai hata yeye anashangaa kwani walikuwa kwenye mwendo wa kawaida sana.

“Dereva alikuwa Darassa wakati tunapata ajali na kusema kweli tulikuwa kwenye mwendo wa kawaida sana, ghafla tukashangaa kuona gari ina serereka na kupinduka mara nne. Kwa hiyo ni ajali kama ajali nyingine sema sisi tunashangaa mazingira ya ajali lakini yote ya yote tunamshuru Mungu kwa sababu wote ni wazima,” alisema Hanscana.

Aliongeza, “Kwa sasa tunaangalia namna gani tunaweza kurudi Dar es salaam kwa sababu huku tuliko ni mbali sana na tulikuja kwa ajili ya show,”

Mastaa mbalimbali wametumia mitandao ya kijamii kuwapa pole.

HATIMAYE: Mmiliki wa Jamii Forums Atoka Selo Baada ya Kupatiwa Dhamana leo

$
0
0

Maxence Melo amepatiwa dhamana muda huu katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, baada ya kukaa mahabusu kwa takribani siku 7.

Anakabiliwa na mashtaka matatu likiwemo la kuendesha tovuti ambayo haijasajiliwa nchini.

SUGU Aomba Radhi Kwa Familia ya Marehemu Baada ya Gari Lake Kumgonga Mtoto na Kumuua....

$
0
0


Sugu amesema moja ya matukio mabaya kutokea akiwa mbunge ni la kupoteza Neema ambaye ni mkazi wa Mbeya na raia wa Mtanzania.

“Naomba mnisamehe. Kifo hiki kimeniumiza, nawaomba radhi ndugu wanafamilia na wananchi wa Mbeya,” ameeleza Sugu kwenye msiba huo.

Dhahiri Kidavashari, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya amesema Gabriel ambaye ni dereva wa Sugu, anashikiliwa na jeshi hilo.


VIDEO:MCHUNGAJI AMFUFUA MTU KANISANI KWAKE DODOMA

HAMADAI adai alitongozwa na Shilole, aeleza sababu ya kuachana naye

$
0
0
Mpenzi wa zamani wa Shilole, Hamadai amefunguka na kueleza jinsi alivyokutana na Shilole na kuanza mahusiano.

Muimbaji huyo mchanga wa bongofleva alifahamika mara baada ya kuwa katika mahusioano na Shilole.

Akiongea katika kipindi cha Enewz cha EATV, muimbaji huyo amesema kuwa kwa sasa ameamua kuachana kabisa na Shilole kwa sababu kuna mambo ambayo alikuwa akiona hayaendi sawa na sasa ameamua kujikita katika muziki wake.

“Shilole ndiye aliyenitongoza mimi na siyo mimi, na sasa nimeona niachane naye kwa sababu kuna vitu ambavyo nilikuwa naona haviendi sawa, pia mimi siwezi mzungumzia vibaya. Kabla yangu alikuwa na watu kadhaa ambao tayari ameachana nao, akawa na mimi na tukaachana na sasa ana mtu mwingine ambaye pia anaweza kuachana naye, hayo ni maisha yake na mimi siwezi kumuingilia” Alisema Hamadai.

Pia aliongezea kuwa yeye sasa hivi amejikita sana katika muziki na kuachana na Shilole hakujampunguzia chochote katika maisha yake.

WANANCHI 21 wafikishwa mahakamani kwa kuvamia na kufanya vurugu katika kituo cha polisi.

$
0
0
Jumla ya watuhumiwa 21 akiwemo mwanamke mmoja wamefikishwa katika mahakama ya Wilaya ya Chunya kwa kuhusika na vurugu zilizotokana na wananchi wilayani humo kuvamia kituo cha polisi kwa lengo la kuwatoa watuhumiwa wa mauaji ili kuwaadhibu.

Watu hao waliofikishwa mahakamani ni sehemu ya watuhumiwa 41 waliokamatwa, kati yao wanaume wakiwa 34 na wanaweke 7 baada ya vurugu zilizotokea jana na kusabababisha jumla ya watu 7 kujeruhiwa wakiwemo askari polisi wanne, na wananchi watatu huku mwananchi mmoja aliyefahamika kwa jina la AMOKE MBILINYI (25) akifariki dunia.

Taarifa ya Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya imeeleza kuwa tukio hilo limetokea mnamo tarehe 18.12.2016 majira ya saa 11:45 asubuhi katika Kituo cha Polisi Makongolosi kilichopo Kata ya Makongolisi, Wilayani Chunya ambapo kundi la wananchi walioamua kujichukulia sheria mkononi walivamia kituo hicho cha Polisi na kufanya fujo kwa kuwarushia  mawe hovyo askari.

Kwa mujibu wa jeshi hilo, lengo la uvamizi huo ilikuwa ni kuwatoa watuhumiwa wawili waliofahamika kwa majina ya 1. ERASTO ROBERT, mkazi wa Kilombero na 2. BASI LINUS mkazi wa Makongolosi waliokuwa wanakabiliwa na kosa la mauaji kwa lengo la kuwatoa nje na kuwauawa kwa kuwachoma moto.

Aidha wananchi hao walifunga barabara ya Chunya/Makongolosi kwa kuweka mawe makubwa na magogo hali iliyosababisha usumbufu mkubwa wa watumiaji wengine wa barabara hiyo.

Jeshi hilo limesema thamani ya uharibifu bado kufahamika na hali imerejea kuwa shwari

Awali mnamo tarehe 11.12.2016 majira ya saa 23:20 katika Kitongoji cha Manyanya, mtu mmoja aliyefahamika kwa jina la JACOB BROWN Mkazi wa Manyanya alivamiwa na watu wasiojulikana akiwa peke yake shambani kwake na kuuawa ambapo Polisi walifanya msako na kuwakamata watu hao wawili kwa mahojiano zaidi kuhusiana na tukio hilo.

UTEUZI: Rais Dkt Magufuli Ateua Wenyeviti 7 wa Bodi za Taasisi za Serikali

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli, amefanya uteuzi wa Wenyeviti 7 wa Bodi za Taasisi za Serikali, na pia ameteua Mwenyekiti wa Baraza la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi Tanzania na Mjumbe mmoja wa Baraza la Taifa la Biashara.

Taarifa iliyotolewa leo tarehe 19 Desemba, 2016 na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi imewataja walioteuliwa kama ifuatavyo;

1. Rais Magufuli amemteua Bw. Ali Mufuruki kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya Mfuko wa Taifa wa Dhamana ya Hifadhi ya Mazingira.

Ali Mufuruki ni Afisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni za Infotech Investment na Mwenyekiti wa Taasisi ya Afrika inayojihusisha na uendelezaji wa vipaji vya uongozi katika ukanda wa Afrika Mashariki.

2. Rais Magufuli amemteua Mhandisi Christopher Kajolo Chiza kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (TanTrade)
Mhandisi Christopher Kajolo Chiza anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Sabetha Mwambenja ambaye amemaliza muda wake.

3. Rais Magufuli amemteua Bw. Peter M. Maduki kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA)

Peter M. Maduki anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Prof. Idrissa Mshoro ambaye amemaliza muda wake.

4. Rais Magufuli amemteua Dkt. Yamungu Kayandabila kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka ya Usimamizi wa Bima Tanzania (TIRA).

Dkt. Yamungu Kayandabila ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi na anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Bw. Peter Ilomo ambaye amemaliza muda wake.

5. Rais Magufuli amemteua Prof. Godwin Daniel Mjema kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Kampuni ya Huduma za Fedha na Mikopo (UTT-MFI)

Prof. Godwin Daniel Mjema ni Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Balozi Fadhili D. Mbaga ambaye amemaliza muda wake.

6. Rais Magufuli amemteua Kepteni Ernest Mihayo Bupamba kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Ushauri ya Chuo cha Bahari (DMI)

Kepteni Ernest Mihayo Bupamba ni Mwendesha Meli Mkuu (Principal Captain) Katika Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi.

7. Rais Magufuli amemteua Dkt. Aloyce S. Hepelwa kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Taasisi ya Miradi ya Maendeleo ya Miundombinu (UTT-PID)

Dkt. Aloyce S. Hepewa ni Mhadhiri Mwandamizi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.

Aidha, Rais Magufuli amemteua Dkt. John Jingu kuwa Mwenyekiti wa Baraza la Uwezeshaji wananchi Kiuchumi Tanzania.

Dkt. John Jingu ni Mhadhiri katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.

Halikadhalika, Rais Magufuli amemteua Dkt. Rashid Adam Tamatama kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Utafiti wa Uvuvi (TAFIRI).

 Dkt. Rashid Adam Tamatama ni Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.

Pia, Rais Magufuli amemteua Bibi. Zuhura Muro kuwa Mjumbe wa Baraza la Taifa la Biashara (Tanzania National Business Council – TNBC).

Bibi. Zuhura Muro ni Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi inayojihusisha na huduma za ushauri wa ubora na mafunzo (Service Limited) katika ofisi zake za Dar es Salaam.

 Wateule wote waliotajwa hapo juu, uteuzi wao umeanza tarehe 17 Desemba, 2016

 Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar es Salaam
19 Desemba, 2016
Viewing all 104689 articles
Browse latest View live


Latest Images