Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104747 articles
Browse latest View live

SERENGETI Boy Afunguka Jinsi Shilole Alivyomtongoza na Kumtumia Kisha Kumtosa

$
0
0

Shilole amekuwa na tabia ya kutoka na viserengeti Boy na kila anayekutana naye anampost mtandaoni wakiwa mapozi tata au wakifanya utata utata, 
Mmoja wa serengeti boy anadai shilole alimkomaia kumtongoza sanaa akakosa uhuru kwa kuwa alikuwa dansa wake ikibidi amkubali, lakini aliishia kupata maumivu kwani alitoswa katikati
Shilole alipohojiwa anadai hajamtongoza ila kijana huyo anajifariji

WAZIRI Mkuu Kassim Majaliwa Apokea Msaada Wa Maafa Ya Tetemeko La Ardhi Kagera

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amepokea fedha taslimu sh. milioni 10 kutoka Kanisa la Evangelistic Assemblies of God Tanzania (EAGT) zikiwa ni msaada kwa ajili ya watu waliopatwa na maafa kutokana na tetemeko la ardhi mkoani Kagera.

Makabidhiano ya mchango huo yamefanyika leo mchana (Alhamisi, Oktoba 22, 2016) kwenye Makazi ya Waziri Mkuu, Oysterbay, jijini Dar es Salaam.

Akikabidhi mchango huo, Askofu Mkuu wa Kanisa la EAGT, Dk. Brown Mwakipesile amesema kanisa hilo limeona lina wajibu wa kuisadia Serikali kuwapunguzia machungu watu waliopatwa na maafa kutokana na tetemeko la ardhi lililotokea mkoani Kagera, Septemba 10, mwaka huu na kusababisha vifo vya watu 17.

“Tumeona ni vema kanisa la EAGT lishiriki kuisadia Serikali kuwafariji wananchi waliopata maafa kutokana na tetemeko hilo. Tumeona ni wajibu wetu kwa sababu waliopatwa na maafa ni watu wetu wote. Tunawaombea wote waliopatwa na shida waweze kupata nafuu mapema zaidi,” amesema.

Askofu Mkuu Dk. Brown ametumia fursa hiyo kuipongeza Serikali kwa kusimamia vema suala hilo tangu lilipotokea hadi sasa na kuongeza kuwa wanamuomba Mwenyezi Mungu awape nguvu viongozi wa Serikali ya awamu ya tano ili waweze kutimiza majukumu yao ipasavyo.

“Ukiacha hili la tetemeko, tumeona jinsi Serikali ilivyosimamia vizuri suala la madawati hadi sasa kuna baadhi ya maeneo wamevuka hadi malengo. Tunamshukuru Mheshimiwa Rais Magufuli na Serikali nzima kwa kusimamia jambo hilo vizuri,” amesema.

Amesema kanisa hilo linatoa shukrani nyingi kwa Mheshimiwa Rais Dk. John Pombe Magufuli kwa jitihada zinazofanywa na Serikali yake kukabili mambo mbalimbali yanayowagusa wananchi walio wengi.

Akitoa shukrani kwa Baba Askofu Mwakipesile na viongozi wa kanisa hilo aliombatana nao, Waziri Mkuu ameahidi kuwa Serikali itahakikisha michango hiyo inafikishwa Kagera kwa walengwa. “Nawashukuru sana kwa jinsi mlivyoguswa na kuamua kuwachangia wenzetu waliopatwa na maafa, tutahakikisha inawafikia walengwa,” amesema.

Waziri Mkuu amesema anawashukuru sana viongozi wa dini zote kwa jinsi wanavyoisadia Serikali kuwahudumia wananchi kupitia sekta mbalimbali. “Tunatambua juhudi zinazofanywa na taasisi za dini zote kuunga mkono juhudi za Serikali, tunafarijika mno na tunawashukuru sana,” ameongeza.

Amemuomba Askofu huyo pamoja na viongozi wengine wa dini wawaombee kwa Mungu viongozi waliopo madarakani ili awape hekima na busara na awawezeshe kuwaongoza vema Watanzania.

Tetemeko hilo la ardhi liliharibu miundombinu ya barabara, shule, zahanati na kujeruhi watu 440. Pia lilisababisha nyumba 2,063 kuanguka huku nyingine 14,081 zikiwa katika hali hatarishi na 9,471 zikipata uharibifu mdogo huku wananchi 126,315 wakihitaji misaada mbalimbali.
                         

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,

DIANA Edward 'Miss Kenya Ndio Aliyeniharibia Miss World, She is Fake'

$
0
0
Miss Tanzania, Diana Edwards recently came back with all smiles after the Miss World competitions. On a follow up, we all knew she was very social and jovial with all beauty pageants. However she was quite disappointed to find out that Miss Kenya, who she thought was a close friend, stabbed her on the back.

Her documentary, ‘Maasai Dondosha Wembe’ took the position at top twenty four and she was to hold position one for Beauty With Purpose competition, but apparently Miss Kenya complained she did the same project.

“I am not happy with what she did, I asked her if she knew some Kenyan designer she denied yet she has ever been designed by him. So I wore his design not knowing she has ever worn it and did a photo-shoot with it. All along she was a fake, going behind my back, saying as Africans we have to support each other yet she knew exactly what she was up-to,” said Diana.

DARASSA Awekwa Benchi na Madaktari Kutokana na Maumivu ya Kichwa

$
0
0

Rapa Darassa baada ya kunusurika kifo katika ajali mbaya ya gari akiwa na muongozaji wa video nchini Hanscana huko Kahama, Jamatano hii alienda katika hospitali ya Muhimbili jijini Dar es salaam kwaajili ya kucheki afya yake.

Darassa aliamua kwenda kucheki afya yake baada ya
kunusurika kifo kwenye ajali aliyopata jumapili iliyopita
.
.
. “Nipo hospitalini Muhimbili sasa hivi nawashukuru sana madaktari
wa hapa wamenipokea vizuri wamenipa huduma nzuri sana,” alisikika Darasa kupitia kipindi cha XXL cha Clouds FM
.
.
.
“Wamenicheki kwa sababu nilikuwa najisikia vibaya sana sehemu za kichwani nashukuru Mungu majibu yanaonyesha kila kitu kipo poa kabisa kuna damage ndogo wanaifanyia kazi naendelea na matibabu ila nimeshauriwa kupunguza mizunguko kwa wiki moja ili niweze kupumzika na kutibu hayo maumivu ya kichwa,” alisema Darasa

WANAOMSHAURI Darassa Akatae Show zile Wanazoziita za ‘Vichororoni’ Wanataka Kumwigiza Choo cha Kike?

$
0
0
Darassa ni hadithi ya mafanikio ambayo kila mdau wa muziki ataikumbuka kwa mwaka 2016. Na hadithi yake ina funzo kubwa katika namna ambayo hit song hupatikana. Pengine nilichojifunza zaidi ni kuwa hakuna formula ya jinsi ya kupata hit.


Kwamba ‘don’t bother, just hit the studio do what you love’ mengine yatajulikana mbele ya safari, right? Kwasababu wakati mwingine ule wimbo ambao msanii aliurekodi kwa kujiachia tu studio kuwapa mashabiki wake zawadi, hugeuka kuwa mkubwa hadi humshangaza yeye mwenyewe. Na wakati mwingine, wimbo ambao msanii huuwekea mikakati mikubwa, kufanya uwezekaji wa kufa mtu na promo nzito, hugeuka kuwa ‘flop’ na ‘disappointment’ kubwa.

Kilichotokea mwaka huu kwa Darassa ni mawimbi ambayo kila kona imeyahisi. Muziki umegeuka kuwa wimbo wa hadhi ya ‘national anthem’ kwa muda mfupi. Ndio wimbo wenye rotation kubwa zaidi nchini kwa sasa. Huwezi kuukwepa. Usipousikiliza kwenye redio, utaona video yake kwenye TV. Usipousikia kwenye baa ya jirani, utausikia kwenye bajaj au bodaboda inayokatiza wakati ukitembea barabarani. Kwa ufupi katika mzunguko wako saa 12 za siku, uhakika wa sikio lako kuguswa na mawimbi ya mdundo wake ni mkubwa, utake ustake au labda uweke pamba sikioni.

Na kwa muda mfupi, Darassa amegeuka kuwa msanii wa rap mwenye show nyingi. Darassa amegeuka ‘hot cake.’ Hivyo inamlazimu kusafiri muda mwingi kwaajili ya kutumbuiza. Mfano siku kadhaa zilizopita alikuwa na show tatu katika mikoa miwili tofauti, Iringa na Shinyanga. Ni katika safari yake ya kutoka Kahama kwenda Kakola mkoani Shinyanga ndipo yeye na timu yake walipopata ajali ambayo kama si rehema za Mungu, angegeuka kuwa #hashtag.

Katika wakati huu ambao Darassa anafanya vizuri, amekuwa akipata ushauri mwingi kutoka kwa watu wanaotaka afike mbalimbali zaidi na kwamba asije siku moja akapotea tena baada ya kufika kwenye kilele cha mafanikio kimuziki. Hofu hiyo haikwepeki sababu kuna mifano mingi ya watu waliowahi kutoa nyimbo za ukubwa huo lakini leo hii wanapumulia mashine.

Miongoni mwa ushauri anaoupata ni kuwa apunguze show anazofanya kwa kuweka dau kubwa zaidi ili kuzichuja. Moja ya waliompa ushauri wa aina hiyo ni Sebastian Ndege, ambaye katika sehemu ya alichomshauri anasema, “Usichukue show za mapromoter uchwara waka dissapoint mashabiki wako kuwatia hasira na kukushusha hadhi. Bora ufanye shows chache lakini za ukweli, with detailed showcase.”

Mwingine ni Le Mutuz ambaye anamshauri kuwa ni muda wa yeye kuanza kuchukua malipo ya shilingi milioni 15 hadi 20. Na pia kuwapa masharti mapromota wa maeneo ya mbali kumtafutia usafiri wa ndege. Kwa upendo, wote, wametoa ushauri unaoweza kumjenga japo mwingine unakuwa ni nje ya uhalisia.

Nakubali kuwa kutokana na alipofika, Darassa hapaswi kulipwa kiasi kile kile kama ambacho alikuwa anatoza miaka miwili iliyopita, lakini hilo linapaswa kwenda kwa process. Ni haraka mno kutoka kulipwa mfano milioni 4 kwa show hadi kuwa milioni 20. Inahitaji justification zaidi ya kuwa na hits mbili kuweza kulipwa kwa ukubwa huo.

Watu wasimjaze maneno Darassa na kuanza ajisikie kuwa anapaswa kuanza kuchukua kiasi kile kile ambacho wasanii kama Diamond au Alikiba wanachukua – kumbuka safari ya wawili hawa na nguvu waliyojikusanyia hadi sasa. Hapo alipofika Darassa, kuna rappers kibao nyuma waliwahi kufika, lakini hawakulazimisha kupaa juu ghafla na kutaka walipwe mamilioni ya shilingi ambayo hayaendani na uhalisia.

Huu ndio muda ambao Darassa anaendelea kujijenga kujitengenezea ukubwa huo wa kutoza fedha nyingi au kuzikataa zile zinazoitwa ‘show za vichochoroni.’ Kumbuka kabla ya kuachia Muziki, hakuwa na ‘demand’ hiyo ya hata kuitwa kwenye utitiri wa show hizo. Show za milioni 3, 4 ndizo zinaweza kumjengea na kumtengenezea mazingira ya kudai shilingi milioni 15 au 20 kwa show moja baadaye. Hizi ni show zinazompa mtaji wa kujitengenezea himaya yenye nguvu itakayompa kiburi ya kukataa milioni 5 ili alipwe milioni 15.

Kuna wasanii wanaofanya vizuri ambao kupata show ya milioni 2 au 3 ni ngekewa, haiwezakani Darassa kuzikataa kisa ametoa hit ndani ya mwezi mmoja. Isitoshe, show za vichochoroni ndizo zinaonesha ukubwa wa msanii na dalili kuwa muziki wake umefika mbali. Ehh, ndiyo, haiwezekani kujiita msanii mkubwa wakati unajulikana mjini tu.

Ushauri wangu kwa Darassa ni kwamba aendelee kuwa mnyenyekevu hivyo hivyo kama alivyo sasa bila kuanza kuweka attitude kuwa hataki kwenda baadhi ya sehemu ambazo hazifikiki kwa ndege. Wanasema Roma haikujengwa kwa siku moja, ama hata mbuyu ulianza kama mchicha.. Ni process, inahitaji muda kutengeneza ukubwa, hauji ndani ya siku moja.

By Fredrick Bundala

ALIYENAJISI Binti wa Miaka 9 Ahukumiwa Miaka 30 Jela

$
0
0
Mahakama  ya Wilaya ya Ilala, imemhukumu Shabani Huseni (29), kifungo cha miaka 30 jela, baada ya kupatikana na hatia ya kunajisi mtoto wa miaka tisa.

Akisoma hukumu hiyo jana Hakimu Mkazi Catherine Kihoja alisema upande wa mashitaka ulipeleka mashahidi watano ambao wameweza kuthibitisha mashitaka bila kuacha shaka yoyote.

“Kutokana na ushahidi uliotolewa mahakamani hapa umeweza kuthibitisha mashitaka hivyo, mshitakiwa ninamtia hatiani kama alivyoshitakiwa,’’alisema Hakimu Kioja.

Kabla ya kutolewa kwa adhabu hiyo Wakili wa Serikali, Neema Moshi, aliomba mahakama kutoa adhabu kali kwa mujibu wa sheria kwa kuwa mtoto aliyefanyiwa kitendo hicho ameathirika kisaikolojia na kupata madhara kiafya kutokana na kutokwa na harufu mbaya sehemu zake za siri.

Aidha, mshitakiwa aliomba mahakama impunguzie adhabu kwa kile alichodai kwamba hana ndugu, ombi ambalo lilitupiliwa mbali.

Inadaiwa kuwa mshitakiwa alitenda kosa hilo tarehe isiyofahamika Julai mwaka jana eneo la Kipunguni B, Moshi Baa wilayani Ilala ambapo alimbaka mtoto wa miaka tisa.

MWANDISHIi wa ITV Aliyekamatwa Kwa Amri ya Mkuu wa Wilaya Aachiwa Kwa Dhamana

$
0
0
Mwandishi  wa kujitegemea wa kituo cha televisheni cha ITV, Halfani Lihundi ameachiwa kwa dhamana kutoka katika kituo cha Polisi cha Changamoto, Usa River wilayani Arumeru mkoani Arusha alikokuwa anashikiliwa tangu juzi, na kutakiwa kuripoti kituoni hapo Desemba 27, mwaka huu.

Alikuwa anashikiliwa kwa amri ya Mkuu wa Wilaya ya Arumeru, Alexander Mnyeti, baada ya kuripoti habari inayoelezwa na mkuu huyo wa wilaya kuwa haikuwa sawa na kuamuru kukamatwa kisha, kulala mahabusu na hatimaye kufanikiwa kutoka jana saa tisa alasiri.

Awali, waandishi wa habari wa Arusha walikusanyika kituoni hapo ili kujua hatma ya mwenzao na baadaye kuamua kwenda kumuona Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi ili kumweleza kuwa mwenzao amekamatwa kwa sababu ya migogoro ya wananchi.

Wakati Lukuvi anatoka kwenye kikao cha kujadili migogoro ya ardhi kilichofanyika ukumbi wa Mkuu wa Mkoa wa Arusha, waandishi waliimba wimbo wenye lengo la kufikisha ujumbe kuwa, wanataka wenzao aachiwe huru. Waliimba; “Solidarity Forever, Bring Back Halfani Lihundi.”

Lukuvi alisema hahusiki na suala hilo na kuwasihi wanahabari kwenda naye Usa River kwenye mkutano ambapo Mnyeti atatoa tamko juu ya suala hilo.

Lakini Mnyeti alipokuwa akitoka kikaoni hapo aliulizwa na waandishi kuhusu suala hilo na kosa lipi limefanya Lihundi kushikiliwa Polisi, lakini hakuzungumza chochote na kuelekea kwenye gari lake kusubiri msafara wa Lukuvi.

Awali, ilidaiwa kuwa Mnyeti ndiye aliyeamuru Lihundi akamatwe kwa madai ya kuandika habari za uchochezi za kijiji cha Leguruki, Arumeru.

Alisema alipotaka kujua kosa analoshitakiwa nalo Lihundi, alijibiwa hana kosa ila yupo kwa amri ya Mkuu wa Wilaya. Hata hivyo, RB ya Polisi Usa River 4763/2016 inaonesha ana kosa la uchochezi.

MGANGA Abambwa Akimroga Mwanamuziki Darassa

$
0
0
Kufuatia uwepo wa madai kwamba wapo waganga wanaotumika kuwaroga wasanii, hususan wale ambao nyota zao zipo juu, Kitengo Maalum cha Oparesheni Fichua Maovu (OFM) cha Global Publishers kimeingia mzigoni na kufanikiwa kumnasa sangoma mmoja maarufu ambaye aliingia kazini kuvuta nyota ya mkali wa Hip Hop anayesumbua kwa sasa, Shariff Thabeet ‘Darassa’, twende pamoja!

TUJIUNGE NA CHANZO

Chanzo makini kilinyetisha kuwa, wengi wa waganga hao wapo maeneo ya Tandale, Mwananyamala na Bagamoyo, Pwani ambapo chanzo kiliahidi kutoa ushirikiano kwa mganga huyo ambaye kijiwe chake kipo maeneo ya Mwananyamala jijini hapa.

“Mbona wapo wengi tu, wakiona staa anatamba kama vile Diamond (Nasibu Abdul), Ali Kiba na wengineo, anawapokea hawa wasanii wadogowadogo wanaochipukia na kuwaambia atamshughulikia mmoja wa wasanii hao wanaowika na kudai anaichukua nyota yake kisha kumpa huyo mchanga,” kilisema chanzo hicho makini.

AJALI YA DARASSA YATAJWA

Kama hiyo haitoshi, chanzo hicho kiliweka wazi kuwa kutokana na wimbi la wasanii hao chipukizi kusaka nyota za wasanii wakubwa, watu wamekuwa wakiihusisha ajali ambayo Darassa ameipata hivi karibuni mkoani Shinyanga kwamba kuna mtu alikuwa anaisaka nyota yake.

“Yaani we acha tu, unaambiwa ile ajali nayo pia ilipangwa ili watu wampoteze, wachukue nyota,” kilisema chanzo hicho.


Baada ya kupata madai hayo na kuyafanyia ‘upembuzi yakinifu’, haraka sana OFM iliingia mzigoni kwa kuanza kupanga mikakati ya kumuweka kwenye rada zake mganga huyo ambaye ni maarufu sana maeneo hayo.

SKRIPTI IKAPANGWA HIVI

OFM ilimchagua kamanda wake mmoja ambaye alijifanya ni msanii chipukizi wa Bongo Fleva hivyo anataka kutoka na kwamba anaihitaji nyota ya Darassa anayetarajia kuangusha shoo kali ya michano na mkali wa Hip Hop, Ibrahimu Mussa ‘R.O.M.A’ kwenye mkesha wa Mwaka Mpya ndani ya Ukumbi wa Dar Live, Mbagala-Zakheem jijini hapa.

Mipango yote ilipokamilika, ‘msanii’ huyo aliongozana na OFM wengine wawili waliojifanya ni watu wanaomsapoti kwenye kazi zake kwenda kwa sangoma huyo, baada ya kufika walimkuta akiwa ndani na baadaye aliwakaribisha kwenye chumba chake.

MANDHARI YA CHUMBA

Chumba hicho kilionekana si cha ‘mbavu za mbwa’, kama sangoma wengine wanavyotumia kuishi huko msituni, ni chumba cha kawaida na ndani yake kuna kitanda kikubwa pamoja na vioo kila kona na mazagazaga mengine vikiwemo vyombo na majani makavu na mabichi ambayo sangoma huyo alidai kuwa ni dawa za kienyeji.

Baada ya kukaribishwa msanii (OFM) alieleza shida yake kuwa alikuwa anataka kufanikiwa kimuziki na ikiwezekana achukue nyota ya Darassa, yule sangoma akamwambia asikonde, amefika na shida yake imeshakwisha.

“Yaani hapa ndiyo umefika, ondoa shaka hilo ni dogo sana kwangu,” alisikika mganga huyo.

AVUJISHA SIRI ZA WATEJA

Kuonesha kwamba yupo vizuri na amebobea kwenye fani hiyo, mganga huyo alizidisha mbwembwe za kujinadi hadi kujikuta akivujisha siri za wateja wake bila kujua.

“Yaani hapa mmefika, wenzenu kibao wamefika hapa na nimewasaidia…kina (anataja majina), wote hao wamefanikiwa kutokea hapa kwangu,” alijinasibu mganga huyo mbele ya vinasa sauti vya OFM.


AWAVUTA HADI WASINDIKIZAJI

Mganga noma, akaona asiishie kwa yule msanii pekee, alianza kutaja pia matatizo ya waliomsindikiza msanii huyo huku akiwaambia kama wote walikuwa wanataka kusaidiwa watoe kila mtu shilingi 10, 000.

WAMUOMBA WAKAJICHANGE

OFM hawakuwa na ubishi, walichofanya ilikuwa ni kumuomba sangoma waende wakamchukulie pesa hizo (lengo ni kujipanga vizuri kimbinu) na kumuahidi kuwa baada ya muda wangerejea.



WAREJEA

Baada ya nusu saa, OFM walirudi tena kwa sangoma na baada ya kufika walimwambia msanii peke yake ndiye afanyiwe matambiko ili afanikiwe kwenye mambo yake ya kimuziki na wale wengine, watafanyiwa siku nyingine.



SHUGHULI YAANZA

Yule sangoma alikubali na akamwambia OFM msanii akae kwenye kigoda kisha akampa kibuyu na kumwambia azungushie miguuni, kiunoni, kifuani na kichwani mara saba na baada ya hapo akaanza kumchanja chale kwa wembe (ni mpya, OFM ilihakiki kwanza) akimpaka dawa.


AMTABIRIA ‘MSANII’ MAZITO

Baada ya zoezi hilo, mganga alimhakikishia baada ya hapo ni lazima angekuwa juu kiasi cha kumfunika Darassa ikiwezekana kupiga kolabo mpaka za kimataifa na wakali wa Marekani kama akina Curtis Jackson ‘50 Cent’.

TUJIUNGE NA SANGOMA LIVE

Sangoma: Nyota yako nikiiangalia hapa naiona ipo juu sana! (alimwambia OFM huku akiendelea na zoezi la kumchanja chale.)

Msanii: Aisee….

Sangoma: Ndiyo hivyo! We umewahi kuwa karibu na Darassa?

Msanii: Ndiyo, kuna kipindi nilitaka kufanya naye ngoma (wimbo).

sangoma-akimroga-darassa-13Kamanda wa OFM akitekeleza masharti ya Sangoma.

Sangoma: Ni kweli masharifu wangu wananiambia, tena alichukua nyota yako, wewe ni msanii mkubwa sana, umefungwa usijiamini, tena hata ukiingia kwenye mambo ya kuigiza utafanya vizuri sana.

Msanii: Aisee nifanyie mambo niwike.

Sangoma: Usijali. Mimi ndiye Chief (anataja jina lake kamili) kijana wa Usambaani, kwangu mwisho wa reli, ndiyo maana sihitaji kuweka hata bango, kazi yangu inajitangaza yenyewe.

Ukweli ni kwamba sangoma huyo wakati wote alionekana akihenya sana akidai anaichukua nyota ya Darassa lakini alikuwa akizungumza mambo mengi juu ya msanii wa OFM maana hata kuwa karibu na Darassa, OFM huyo  hajawahi.


MASHARIFU WAWATAKA NA WASINDIKIZAJI

Baada ya mganga huyo kupiga porojo nyingi, sangoma huyo aliwaambia pia jamaa wa karibu waliomsindikiza msanii huyo kuwa masharifu wake wamemwambia ni lazima nao wachanjwe pia dawa.

Hilo lilifanyika na baada ya hapo sangoma alimtaka yule aliyejitambulisha kama ni msanii kwenda kuoga dawa bafuni pamoja na ndugu zake, baada ya hapo akawaambia kuwa zoezi lililofuatia ni yeye kwenda kununua dawa zingine kwa ajili ya kwenda kuoga baharini kisha kuchinja kuku na tayari msanii wa OFM angekuwa amesafishwa na kumfunika Darassa.

OFM WAKABIDHI MTONYO

Baada ya hapo, OFM waliweka fedha kwenye chombo maalum cha huyo sangoma kisha kuondoka zao, huku mbele wakitafakari kwani maneno mengi aliyokuwa  akiyazungumza mganga huyo hayakuwa na ukweli wowote.

DARASSA ANASEMAJE?

Amani lilimvutia waya Darassa na kumueleza kuhusu ishu hiyo ya mganga, alipopatikana hewani, alicheka na kupuuza.

“Hahaha! Huyo anajisumbua, namtegemea Mungu. Niwasihi mashabiki wangu wazidi kunisapoti na mkesha wa Mwaka Mpya waje pale Dar Live kushuhudia michano yangu na ya R.O.M.A,” alisema Darassa.

NENO LA MHARIRI

Ni vyema waganga wa namna hii wakajirekebisha na serikali ikiwezekana iingilie kati kwani wapo waganga wanaochukua pesa za watu wengi kwa kigezo cha kuwatafutia nyota. TAZAMA VIDEO:

ROBOTI Inayoweza Kushiriki Ngono Kutengezwa

$
0
0
Hii teknolojia sasa imekuwa too much! Kila kukicha wenzetu wazungu wamekuwa wakibuni vitu vipya tofauti kabisa na fikira za kawaida za kibinadamu na kuendelea kuushangaza ulimwengu na viumbe vyake, hatujui tunaelekea wapi na hizi teknolojia zinazobuniwa na wenzetu kila siku.

Je ungependelea kushiriki ngono na roboti? Ungefunga ndoa na roboti? Je roboti anaweza kuwa na haki ya kupinga ndoa hiyo?

Haya ni baadhi ya maswali machache yanayoulizwa katika mkutano wa pili wa kuwa na mpenzi wa roboti mbali na kushiriki naye ngono katika Chuo Kikuu cha Goldsmith mjini London nchini Uingereza baada ya Serikali ya Malaysia ambayo ndio iliokuwa taifa la maandalizi ya mkutano huo kuupiga marufuku.

Hatua hiyo imezua utata sio tu kwa mataifa yenye maoni ya Kihafidhina na hapakuwepo na wawakilishi kutoka kwa sekta ya ngono wala roboti za ngono katika mkutano huo.

Kampuni ya Real Dolls inayotengeza wanaserere wa ngono (roboti) ilidai kwamba itatengeza roboti wanaoweza kushiriki ngono na mwenye akili bandia kama za binadamu mwaka ujao. Uzinduzi huo iwapo utafanyika utakuwa ushahidi wa David Levy ambaye amekuwa akitabiri ujio wa roboti zinazofanana na binadamu zenye akili bandia.

Alitoa hotuba ya kufunga mkutano huo ambapo alipendekeza utengezaji wa roboti za ngono. ”Tuna roboti za urafiki na sasa roboti ambaye anaweza kuwa mpenzi ndio mtindo mpya”. Alisema.

roboti-inayoweza-kushiriki-ngono-kutengezwa-3Katika kipindi cha miaka 10 ijayo, inawezakana kutengeza roboti ambayo watu wataihitaji kama mpenzi, ina upendo, inaaminika, inaheshima na hailalamiki alisema.

Wengi watapendelea uhusiano huo wa roboti na huenda wakataka kufunga nao ndoa. Wanaharakati wa masuala ya ndoa nchini humo wameeleza kuwa, mpango huo wa mpenzi wa aina ya roboti huenda akazua maswali kadhaa ya kimaadili, hususana wakati ambapo sheria italazimika kutambua roboti kama binaadamu.

WABUNGE Wavurugana Tena Bungeni Nchini Kenya

$
0
0
NAIROBI, KENYA: Wabunge wa upinzani nchini Kenya wametoka bungeni kwa hasira mapema leo asubuhi desemba 22, 2016 katika Mji Mkuu wa Nairobi nchini humo kwa madai kuwa baadhi yao wamekuwa wakinyanyaswa

Kikao hicho maalum ambacho vyombo vya habari havikuruhusiwa kuingia kilitarajiwa kupigia kura marekebisho ya sheria ya uchaguzi ambayo inaruhusu kuhesabiwa kwa kura moja baada ya nyingine katika uchaguzi wa urais utakaofanyika mwakani.

Serikali inataka mfumo ambao utasaidia shughuli ya kuhesabu kura iwapo mfumo wa kielektroniki utafeli lakini upinzani unasema kuwa ni njia moja wapo ya kuiba kura.

Awali hatua ya kuupigia kura mswada huo ili ufanyiwe marekebisho ilisababisha kuzuka kwa ghasia juzi, Jumanne.

Upinzani wa CORD umesema kuwa mmoja ya wabunge wake aliumizwa hadi kuvuja damu usoni kufuatia vurugu na wabunge wa chama tawala mapema siku ya Jumatano.

Cord imeenda mahakamani ikitaka marekabisho hayo kutopitishwa bungeni lakini chama tawala kimepitisha marekebisho hayo.

U HEARD: Maneno ya Nay wa Mitego kwa Nisha baada ya kufeki mimba

$
0
0
Baadaa ya staa wa bongo movie Salma Jabu maarufu Nisha kukaa na Ayo TV katika exclusive interview na kuelezea ukweli kuwa hana mimba bali alidai alikuwa anafikisha sehemu ya ujumbe katika filamu yake ijayo.

Leo December 22 2016 Soudy Brown amezungumza na Nisha akimuomba awaombe msamaha kutokana na kusingizia msanii wa bongo fleva kumpa ujauzito lakini yeye akasema hakumtaja mtu.

Aidha Soudy Brown amezungumza na Nay wa Mitego ambaye Soudy Brown aliwahi kusema ndiye mhusika wa ujauzito wa Nisha…..

‘nimemsamehe sinaga tatizo kabisa na mtoto wa kike, alifanya hivyo labda kuna kitu chake alitaka kitimie, unajua upande wa movie biashara imekufa kabisa ili aendelee kusikika lazima atengeneze kiki, nadhani hiki siyo kitu kigeni tutasikia mengi’

KAULI ya Kocha wa Argentina Baada ya Maneno Kuzidi Kuwa Messi Anamchagulia Wachezaji

$
0
0
Moja kati ya vipindi vigumu kwa staa wa soka wa kimataifa wa Argentina anayeichezea FC Barcelona Lionel Messi ni kipindi hiki ambacho Argentina haifanyi vizuri sana, Lionel Messi ambaye ni nahodha wa Argentina aliwahi kulaumiwa na kuandikwa kuwa hajitumi timu ya taifa.

Lionel Messi pia amewahi kutuhumiwa kuwa amekuwa na sauti katika uchaguzi wa wachezaji wa timu ya taifa mbele ya kocha wao Edgardo Bauza madai ambayo kocha Bauza amekuwa akiyapuuzia na kukaa kimya.

Kocha Bauza ameamua kuzungumzia kuhusiana na maneno hayo “Kwa wale wanaofikiria kuwa Lionel Messi anachagua wachezaji wa kuunda kikosi cha timu ya taifa, sidhani kama kuna haja ya kuwajibu, kama Messi akichagua wachezaji basi nitakuwa nje ya timu”

Kama utakuwa unakumbuka October 14 Lionel Messi alidaiwa kuhusika na kuzuia mchezaji Mauro Icardi asiitwe timu ya taifa, kwa sababu alimchukua mke wa mchezaji mwenzake wa Argentina na rafiki yake ambaye amewahi kucheza nae FC Barcelona Maxi Lopez.

RAPPER Chemical Aeleza Kilichokwamisha Movie yake na Wema Sepetu

$
0
0
Rapper wa kike na mwanafunzi wa UDSM, Chemical leo Dec 22, 2016 ameeleza sababu zilizokwamisha album yake pamoja na movie mpya aliyomshirikisha mwigizaji Wema Sepetu.

Rapper huyo akizungumza na millardayo.com & Ayo TV aliyaongea haya>>>‘Labda naweza kusema nilikuwa nimepanga kuachia album mimi na mwenzangu ila kutoka na mimi kubanwa na masomo chuoni sikuweza kukamilisha album hiyo ambayo sasa hivi ingekuwa madukani’

‘Kitu kingine ambacho nilikuwa nimepanga ni kuachia movie mpya ya Wema ambayo tulikuwa tumepanga kuitoa mwaka 2016 tumeshoot tangu mwezi wa 11 lakini ndio hivyo mambo hayajakamilika kwasababu shule inabana’

‘Kama utakuwa umesikiliza wimbo wangu wa Mary Mary ni wimbo ambao unahusiana na watoto wa mtaani kwahiyo tukaona tuilete kwenye movie ili stori iwe nzuri mtu anapoona kile nilichokiimba kwenye hiyo movie’

PAUL Makonda Amtaka DC wa Ubungo Kufuata Nyayo zake

$
0
0
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda leo (Alhamisi) amemwapisha Mkuu mpya wa Wilaya ya Ubungo, Kisale Makori na kumtaka kutokaa ofisini na kusubiri taarifa  badala yake atoke nje na kusikiliza kero za wananchi wa wilaya hiyo.

Makonda amesema changamoto kubwa ya watendaji ni uwajibaki na kwamba baadhi yao hupenda kusubiri kupelekewa taarifa za wananchi ofisini badala ya kuwafuata wananchi katika maeneo yao.

"Naomba Makori usiwe mtu wa kusubiri taarifa ofisini pekee.Wanaubungo  wanamatumaini  makubwa na wewe kwa sababu umeaminiwa na Rais (John Magufuli),"amesema Makonda.

MANENO ya Mourinho Kuhusu Kubakia Man United Kama Atapewa Mkataba Mpya

$
0
0
Kocha wa klabu ya Manchester United Jose Mourinho amefunguka kuwa anataka kubakia katika kalbu hiyo kwa muda mrefu zaidi kwa kuwa anapenda maisha yake na timu hioyo.

Mourinho ambaye kwsasa ana umri wa miaka 53, alijiunga na klabu hiyo mwezi Julai, na sasa wako katika nafasi ya sita katika jedwali la ligi baada ya mechi 17.

Najua kwamba ipo siku moja wataleta mkataba mpya, nitatia saini. alisema Mourinho wakati akingea na waandishi.

Mourinho pia amesema kwamba hatoelekea kufanya kazi nchini China , japokuwa amekiri kwamba fedha za China zinavutia kila mtu.

Nataka kusalia katika timu yenye changamoto kubwa ya kujipatia ushindi

POLISI Wanne Waliotengeneza Tukio la Ushoga Kwa Mchungaji wa Kanisa Wafukuzwa Kazi

$
0
0
Askari polisi wanne mkoani Kilimanjaro waliotuhumiwa kutengeneza tukio la ushoga kwa mchungaji wa kanisa la kiinjili la kilutheri Tanzania(KKKT) wamefukuzwa kazi.

Polisi hao walidaiwa kumkamata mchungaji huyo na mwanaume mwingine katika nyumba ya kulala wageni wilayani Hai, kumshurutisha avue nguo, kumpiga picha na kudai awalipe shilingi milioni 10 .

Hata hivyo mchungaji huyo ambaye jina lake limehifadhiwa aliwalipa shilingi 5.4 milioni polisi hao kumuachia baada ya kumshikilia kwa masaa sita.

DEREVA Bodaboda Akatwa Sikio Kwa Tuhuma ya Kufumaniwa na Mke wa Dereva Teksi

$
0
0
Dereva bodaboda wa Mji Mdogo wa Qatesh wilayani Hanang’ Mkoa wa Manyara, amekatwa sikio kwa kisu kwa tuhuma za kufumaniwa akiwa na mke wa dereva wa teksi.


Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Manyara, Kamishna Msaidizi, Francis Massawe alisema tukio hilo lilitokea Desemba 21 saa 6:10 usiku kwenye Kitongoji cha Qendangonyi, Kata ya Ganana wilayani Hanang’.

Kamanda Massawe alisema chanzo cha tukio hilo ni wivu wa mapenzi na majeruhi amepata kilema cha maisha baada ya sikio kutolewa.

Alisema wanamshikilia dereva teksi kwa uchunguzi wa tukio hilo kabla ya kumfikisha mahakamani.

Source: Mwananchi

SERIKALI yapiga Marufuku Kuagiza Nyama ya Kuku Kutoka nje ya Nchi

$
0
0
Serikali imepiga marufuku kuagiza na kuingiza nyama za kuku waliochinjwa kutoka nje ya nchi ili kulinda afya za walaji wa bidhaa hiyo ya nyama nchini.

Katazo hilo limetolewa na Naibu Waziri wa Kilimo Mifugo na Uvuvi, Mhe. William Tate Ole Nasha kwenye mahojiano maalum na EATV ilipotaka kupata ufafanuzi wa serikali kuwa inahakikisha vipi nyama na vitoweo kutoka nje ya nchi zinaingizwa nchini zikiwa na ubora unaokidhi viwango vya afya kwa walaji.

Ole Nasha amesema hairuhusiwi kuagiza wala kuuza kuku waliochinjwa kutoka nje ya nchi kwakuwa kwa sasa nchi inajitosheleza na inajitegemea kwa kiwango kikubwa cha nyama.

Amewataka wafugaji na wafanyabiashara kutumia fursa za kuzalisha nyama kwa tija na ubora zaidi ili nchi ianze kuuza vitoweo vya nyama hasa kuku nje ya nchi.

Ameongeza kuwa tayari serikali inaendelea kuchukua hatua za kisheria kwa viongozi wanaoshirikiana na wafanyabiashara wasio waaminifu kuingiza nyama hizo za kuku wa nje nchini.

JESHI la Polisi Latoa Tahadhari Msimu Huu wa Sikukuu

$
0
0
Jeshi la Polisi kupitia msemaji wake, Kamishna Msaidizi wa Polisi na Msemaji wa Jeshi hilo, Advera John Bulimba, lilitoa tahadhari za kiusalama kuhusiana na sikukuu hizo mbele ya waandishi wa habari jana huku pia wazoefu wa masuala ya biashara na wakuu wa dini wakitoa usia wao kuhusiana na mambo muhimu ya kuzingatia ili sikukuu isiharibiwe kwa habari mbaya za misiba na majanga.

Katika taarifa yao kwa umma, polisi walichimba mkwara mzito kwa kuahidi kuchukua hatua za kisheria kwa wote watakaofurahia sikukuu hizo kwa namna inayokiuka sheria na kuhatarisha usalama, huku Askofu Mkuu wa Jimbo la Mahenge, Agapiti Ndorobo, akionya kuwa kila mmoja anapaswa kuhakikisha kuwa hatendi mambo ya ovyo na kumchukiza Mungu.

Mhadhiri wa Uchumi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Dk. Joel Silas, aliwashauri Watanzania kutumia vyema rasilimali zao katika kipindi hiki ili sikukuu zikimalizika wasibaki bila kitu mikononi mwao.

Keshokutwa, Watanzania wataungana na watu wengine duniani kote kusherehekea Krismasi kabla ya kufuatiwa na siku ya kupeana zawadi (Boxing Day) katika siku inayofuata na mwaka mpya ifikapo mwisho wa mwezi huu.

TAHADHARI YA POLISI

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Kamishna Bulimba alisema baadhi ya wahalifu hutumia vipindi vya sikukuu kufanya vitendo vya kihalifu, lakini akaonya kuwa yeyote atakayejaribu kufanya hivyo atachukuliwa hatua kali kwa sababu wamejipanga kuhakikisha kuwa amani na utulivu vinaendelea kudumishwa wakati wote.

“Tumejipanga vya kutosha, siwezi kuweka mbinu hadharani hapa kwa sababu za kiusalama, lakini itoshe tu kuwaambia kwamba Jeshi la Polisi liko vizuri na asithubutu mtu yeyote kufanya uhalifu mahali popote maana tuna mkono mrefu… tutamkamata,” alisema Bulimba.

Aliwataka wananchi kutoa ushirikiano kwa kufikisha taarifa haraka wanapobaini kuwa kuna mtu, kundi au watu wanaowatilia shaka, huku kila mmoja akiwa mlinzi wa jirani yake katika biashara, makazi na mahali pengine. “Ukiona kuna mtu anaingia kwa jirani yako halafu humfahamu au unamtilia shaka, mpigie simu au piga simu polisi kupitia namba 111 na 112,” alisema.

Aliongeza kuwa jeshi hilo limejipanga pia kwa kuimarisha ulinzi katika maeneo ya kuabudia, sehemu za fukwe za bahari, sehemu za starehe na maeneo mengine ambayo yatakuwa na mikusanyiko mikubwa ya watu. Bulimba aliwataka waendeshaji wa kumbi za starehe kuzingatia uhalali wa matumizi ya kumbi zao na kuepuka kuzidisha idadi ya watu tofauti na uwezo wa kumbi zao na kwamba kwa yeyote atakayebainika kufanya hivyo atachukuliwa hatua kali.

Kuhusu ulinzi katika barabara, Bulimba alisema jeshi hilo pia limejipanga kudhibiti matukio ya kizembe ikiwamo madereva walevi na kwamba wameandaa vituo vya polisi vya kuhamishika ambavyo vitawekwa katika maeneo tofauti ili kuwarahisishia wananchi kuripoti moja kwa moja matukio yanayotishia usalama wa raia na mali.

Aidha, Bulimba alikumbushia vilevile kuwa ni marufuku kusherehekea sikukuu hizi kwa kupiga fataki, kuchoma matairi barabarani na kuandaa ‘disco toto’ kwa sababu matendo yote hayo ni uhalifu na wahusika watachukuliwa hatua za kisheria.

Yafuatayo ni kati ya mambo mengi ya kuzingatia, yapo takribani tisa ya msingi kuyakumbuka katika kipindi hiki cha sikukuu za mwisho wa mwaka.

1. TUMIA FEDHA KWA MPANGO

Kati ya mambo muhimu ya kuzingatia kuelekea sikukuu ya Krismasi na pia zile za ‘Boxing Day” na Mwaka Mpya ni kutumia fedha kwa umakini.

Tahadhari hii inatolewa kutokana na ukweli kuwa baada ya kumalizika kwa sikukuu hizo, hali huwa ngumu. Isitoshe, Januari ni mwezi unaombatana na changamoto nyingi. “Kuna masuala ya kodi za pango, ada za watoto shuleni na majukumu mengine mbalimbali.

Yeyote yule asipokuwa makini, dunia yote ataiona chungu na Januari ataiona ndefu. Ni muhimu kukumbuka kuwa kuna maisha baada ya sikukuu hizi,” mmoja wa wafuatiliaji wa masuala ya kiuchumi aliiambia Nipashe jana.

Akizungumzia hilo, Dk. Silas alisema ni lazima Watanzania wabadilishe muundo wa maisha kwa kuelekeza matumizi ya fedha katika mambo ya msingi kwa kuepuka kuishi kwa mazoea.

2. ZINGATIA SHERIA BARABARANI

Hili ni eneo jingine la kuchunga sana, hasa kwa madereva na watu wengine watakaosafiri kutoka eneo moja hadi jingine kwa nia ya kufurahia sikukuu.

Kwa mujibu wa Polisi, ajali nyingi zinazotokea katika kipindi cha kuelekea mwisho wa mwaka husababishwa na watu wanaopuuza sheria za usalama barabarani, hasa kwa kuendesha vyombo vya moto kwa kasi kubwa na pia kujazana kwenye vyombo hivyo kupita kiasi.

Wapo pia wanaotembea kwa miguu barabarani bila ya uangalifu. Ili kutimiza ndoto ya kuuona mwaka mpya, kila mmoja anapaswa kuzingatia sheria awapo barabarani.

3. ULEVI KUPITILIZA NI KUITA KIFO

Ulevi wa pombe kupitiliza kwa baadhi ya madereva ni chanzo kimojawapo kikubwa cha ajali za mwisho wa mwaka. Baadhi ya ajali hizi zilisababishwa na ulevi na hivyo, ni muhimu kujua kuwa unywaji holela ni sawa na kujiweka karibu na kifo au ulemavu wa kudumu.

4. ACHA MICHEPUKO, IPE RAHA FAMILIA

Viongozi wa dini, akiwamo Askofu Ndorobo, wanasisitiza juu ya upendo kwa familia, na hasa katika kipindi kama hiki cha kuelekea sikukuu. Kwa sababu hiyo, inashauriwa kuwa ni vizuri kwa kila mmoja kuachana na wapenzi wa nje ya ndoa na badala yake kufurahi na familia. Madhara ya kutenda kinyume chake ni pamoja na kuyumbisha ndoa baada ya sikukuu hizi kumalizika.

Askofu Ndorobo alisema ni vyema Watanzania wakajenga utaratibu wa kufurahi kwa pamoja kwenye matukio ya kifamilia kama kumbukumbu za siku za kuzaliwa, maisha ya ndoa miaka mitano na zaidi na sherehe nyinginezo, na kwamba kwa kufanya hivyo yatapunguza maovu mengi kwenye jamii.

5. USILE BATA PEKE YAKO, WAKUMBUKE YATIMA

Inashauriwa kwa kila mmoja kuwakumbuka yatima, masikini, walemavu na watu wengine wenye mahitaji maalumu na siyo kufaidi sikukuu na watu wachache wa familia peke yake. Lengo kubwa katika hili ni pamoja na kusambaza upendo, kuleta furaha kwa kila mmoja walau katika sikukuu hizi.

6. UMAKINI UNUNUZI WA ZAWADI ZISIWE ‘FEKI’

Mama au baba wa familia anapokwenda dukani kununulia bidhaa za zawadi kwa ajili ya sikukuu anapaswa kuwa makini wakati wote kutokana na mrundikano wa bidhaa bandia katika baadhi ya maeneo. Kwenda kufanya manunuzi holela kunaweza kuwasababishia kero wapendwa wako badala ya kuwaletea furaha iliyokusudiwa. Umakini huu uwe maradufu.

7. USIACHE WATOTO PEKE YAO KUOGELEA, DISCO

Kati ya makosa makubwa hufanyika katika siku za sikukuu ni pamoja na kuwaachia watoto waende kusherehekea siku hiyo kwenye maeneo mbalimbali bila ya uangalizi makini. Kwa mfano, ni hatari kuwaachia waogelee peke yao na pia siyo busara pia kuwaacha warundikane kwenye kumbi za disco, maarufu kama ‘disco toto’ wakiwa peke yao.

Kutozingatia maelekezo hayo yaliyosisitizwa jana na Jeshi la Polisi ni sawa na kujiweka tayari kwa kulia na kusaga meno kutokana na taarifa mbaya kuhusiana na usalama wa watoto. “Kuna uzembe ambao huwa unafanywa na wazazi wa kuwaachia watoto kuzurula ovyo na wakati mwingine kuhatarisha maisha yao.

Sasa nataka ieleweke hivi, mzazi akibainika amezembea kumlinda mtoto wake na akaletwa kituoni, lazima atakuwa na kitu cha kujibu na tutamwajibisha,” alisema Bulimba na kuongeza: “Kwa suala la disco toto, tulishalipiga marufuku. Halipo kabisa.”

8. EPUKA UCHOMAJI MATAIRI, ULIPUAJI FATAKI

Kusherehekea sikukuu kwa kuchoma matairi barabarani au kulipua mafataki kiholela ni miongoni mwa makosa makubwa yanayoweza kuharibu furaha na kuwa kilio kwa wahusika baada ya kukamatwa na kwenda kuwekwa mahabusu. Bulimba alilikumbushia hilo jana na kuonya kuwa wakiukaji wa maelekezo hayo wajiandae kukamatwa na kuwekwa mbaroni.

9. KUMUOGOPA MUNGU

Jambo lingine muhimu ni kuendeleza amani kwa kufanya matendo yanayozingatia uwapo wa Mungu. Askofu Ndorobo alisema wapo watu waliozoea uhalifu kwa kutomhofia Mungu na hilo ni tatizo kubwa linalopaswa kufanyiwa kazi sasa na hata baada ya kipindi hiki.

“Kinachopungua kwa (baadhi ya) Watanzania ni hali ya kutomuogopa Mungu kwa dhambi. Kila Mtanzania ni mlinzi wa mwenzake na pia ni mtunza uhai wa mwenzake. Ndiyo maana kila mmoja akiheshimu uhai wa mtu… matukio mabaya hayatatokea,” alisema Askofu Ndorobo.

DIAMOND na Timu yake Kuchoma Gari Moto Jukwaani Kesho Wasafi Beach Party

$
0
0
Kama Kichwa cha habari kinavyojieleza Meneja wa Diamond Sallam Sk Mendez Akihojiwa na XXL leo Live pale mlimani City amesema wanapanga kupandisha gari Jukwaani na kulipiga kiberiti live watu wakishuhudia siku ya kesho Kwenye Party ya Wasafi ...

Amedai stunt kama hizo zinasaidia kufanya mziki wetu uendelee kuwa gumzo Afrika na kukua zaidi.....
Viewing all 104747 articles
Browse latest View live




Latest Images