Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104709 articles
Browse latest View live

MAAMUZI mapya ya Waziri Mwigulu Nchemba kuhusu mauaji ya wakulima na wafugaji

$
0
0

January 3, 2017 Waziri wa Mambo ya Ndani, Mwigulu Nchemba amefika katika kijiji cha Tindiga kilichopo wilaya ya Mikumi zilipotokea vurugu zilizopelekea mkulima mmoja kuchomwa mkuki mdomoni na kutokea shingoni na kusikiliza kero zinazowasumbua wananchi wa Kilosa kabla ya kutoa maamuzi. 

Waziri Mwigulu amesema kuanzia sasa likitokea tukio lolote la watu kuuana kwa mapanga, mikuki, sime  na silaha zozote za jadi zinazotumiwa hasa na wakulima na wafugaji, serikali itafuta utaratibu wa kubeba silaha hizo na atakayebeba atakamatwa na kuchukuliwa hatua kama watuhumiwa wengine.

Kinginie alichoagiza Waziri Mwigulu ni wakuliam na wafugaji kwa pamoja kuwakamata watu wote watakaohusika na kuanzisha vurugu na kuwafikisha kwenye vyombo vya dola kabla jeshi la polisi halijafanya maamuzi yake.

“Kuanzia leo tunaanza kuhesabu pakitokea tukio lolote la vurugu na zikatumika silaha kuwadhuru wananchi, tutafuta utaratibu wa watu kutembea na silaha mitaani, na ukikutwa nayo unakamatwa kama ambavyo mtu mtu mwenye silaha ya moto na hajaiandikisha. Hatuwezi kuruhusu hii ikawa nchi ya watu wanakatanakatana tu” – Waziri Mwigulu Nchemba

IDRIS Sultan – Nando is on the recovery road

$
0
0

It is certainly going to be rough year for Nando, especially now that few of his friends are penning out words of encouragement on social media. Apart from Feza Kessy and Nikki Mbishi who are crying out to fans support, former Big Brother Africa winner, Idris Sultan and had to say to Bongo5.


“I did not see the need to post anything about Nando firstly because he is not my friend. We are more of acquaintances ever since we were in big brother in 2014. We used to meet in events and parties but I still cannot consider him as close. Together with some of the housemates we have had some hard time to look for his mother’s contact and make her aware of her sons’ state therefore he is now checked into rehab at Kigamboni. I can gladly say he on the recovery road.”

“Nando is a smart, creative and real than I can be, so I can admit at first I did not know he was using drugs until he confessed to me. Honestly, I did not expect him to be in such a state however his appearance could tell a lot. Telling him to stop was not necessary since at the end of the day it’s his initiative to decide so.”

He adds, “As for now, together with my friends, his family and close friends we have taken responsibility to contribute money and make sure he gets assistance till the day they will release him. However, my main goal towards Nando is once he is released I will get mentors to regularly talk to him in that he does not slip as former stars have done. I will support him because he is an incredible person. It my prayer together with former big brother housemates that Nando will fully recover.

TEMBELEA Blog ya Tiba za Asili Kwa Maswala ya Tiba Asilia, Kusomewa Dua na Visomo, Kusafisha Nyota na Kumvuta Mpenzi

$
0
0
Tembelea  tovuti  pendwa  ya ASILI ZETU inayohusiana na masuala ya tiba asilia, kusomewa dua na visomo, kusafisha nyota,  kumvuta mume au mpenzi aliyekuacha, tiba ya magonjwa mbalimbali yaliyoshindikana,  mvuto wa biashara.

Pia tunatoa dawa za uzazi kwa wale kina mama wenye matatizo ya uzazi walio angaika kwa muda mrefu bila kupata mafanikio yoyote, kupandishwa cheo kazini, mali isiyohuzika kama vile kiwanja, shamba, nyumba, gari n,k.  Ingia HAPA

UVCCM Wampongeza Rais Magufuli Kwa Kumtumbua Mkurugenzi Mtendaji TANESCO

$
0
0
Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM), umesema kuwa umefurahishwa na kitendo cha Rais Magufuli cha kupigania maslahi ya wanyonge na kuzuia kupandisha bei ya umeme nchini.

Hayo yamesemwa na Kaimu Katibu Mkuu wa UVCCM, Shaka Hamdu Shaka wakati wa kikao cha watumishi wa umoja huo wa kutathmini utendaji kazi wa mwaka 2016 na kuweka utendaji wa mwaka huu.

Shaka amesema kitendo cha Rais Magufuli kumsimamisha kazi Mkurugenzi wa Shirika la Umeme Nchini (Tanesco), Mhandisi Felchesm Mramba, ameonyesha uzalendo, ujasiri na upendo kwa wananchi ambao walimpa dhamana ya kuongoza nchi.

“UVCCM tunaunga mkono uamuzi wa Rais wa kuzuia kupanda kwa bei ya umeme na ametazama maslahi ya wananchi waliomchagua kuingia madarakani,”amesema Shaka.

Hata hivyo, amesema kuwa Tanesco kupitia kwa Mkurugenzi wake Mramba aliyetumbuliwa na Waziri wa Nishati na Madini, Prof. Sospeter Muhongo waliwaahidi wananchi kutopandisha bei ya umeme.

YOUNG Dee Azijibu Tetesi za Kurudia Unga

$
0
0
Hatimaye rapper Young Dee amejibu kwa ufupi kuhusiana na tetesi kuwa amerudi tena kwenye matumizi ya dawa za kulevya.

Akiandika maneno mafupi sana kwenye post yake mpya ya Instagram, Young Dee amedai kuwa ‘muda utaongea.’

“Time will Tell… Mi sina tatizo na mtu… Tuombeane kheri tu… Siwezi shindana na maneno,” ameandika rapper huyo.

Wiki hii tetesi za kuwa Dee amerejea tena kwenye utumiaji wa dawa hizo zilianza kufuatia maneno ya meneja wake Max mtandaoni. Max alida kuwa rapper huyo ameanza tena kuubwia unga na kwamba amechoka kusumbuka naye.

Tetesi za Young Dee zimekuja katika kipindi ambacho watanzania wanasikitishwa na hali walizonazo Chidi Benz na Nando kutokana na kuathirika vibaya na madawa hayo.

TANZIA: Anna Senkoro, mwanamke wa kwanza kugombea Urais nchini Tanzania(2005), afariki dunia

$
0
0
Aliyekuwa mgombea urais wa kike wa kwanza Tanzania (Uchaguzi 2005) kupitia chama cha APPT-Maendeleo, Dr. Anna Claudia Senkoro ameaga dunia.

Inadaiwa aliugua ghafla usiku wa kuamkia leo na amefariki baada ya kukimbizwa hospitali asubuhi ya leo.

Msiba upo nyumbani kwake, Tabata Segerea jijini Dar.

Taarifa zaidi zitafuatia...

FEROOZ " Inaniwia Vigumu Kuacha Madawa ya Kulevya"

$
0
0
Msanii mkongwe wa muziki Ferooz Mrisho ambaye katika miaka ya 2000 alitamba na wimbo wa Starehe ambaye kwa sasa ameathirika na dawa na matumizi ya Madawa ya kulevya, amedai inamuwia vigumu kuachana na matumizi ya dawa hizo. Muimbaji huyo amedai amejikuta akitenga bajeti kubwa ya fedha kwa matumizi ya kutumia dawa.

“Ninawaomba wasanii wenzangu wasitumie dawa maana ni vigumu kuacha. Natamani sana kurudi kama zamani ili heshima yangu iwepo ila inanisumbua, lakini naamini iko siku,” Ferooz aliliambia gazeti la Mtanzania. Hata hivyo muimbaji huyo alipoulizwa ni wapi anaponunua Madawa hayo hakuwa tayari kutaja.

WASANII Wanaosambaza Ujumbe wa Matumizi ya Mihadarati Kusakwa

$
0
0
Kamanda wa Polisi Kikosi cha Kuzuia na Kupambana na Madawa ya Kulevya, ACP Mihayo Msikhela amedai wamejipanga kufanya msako dhidi ya wasanii wanaosambaza ujumbe wa matumizi ya mihadarati.

Akiongea na gazeti la Mtanzania, Kamishna huyo alisema hivi sasa wapo kwenye msako dhidi ya wasanii ambao wamekuwa wakisambaza ujumbe wa matumizi ya mihadarati hiyo kwa kuwa wasanii hao ambao ndio kioo cha jamii, sasa wamekuwa wa kwanza katika kusambaza ujumbe wa matumizi hayo.

“Mimi binafsi simfahamu Chid Benz kama ni mtu maarufu aliyekuwa akifahamika kwa kiasi hicho, lakini baada ya kumuona kwenye mitandao ya kijamii ndipo nikaanza kumfuatilia,” alisema Kamishna Msikhela.

Alisema endapo wakipata taarifa ya kwamba wanatumia hadharani na kuwakamata, basi watachukuliwa hatua kama wahalifu wengine.

“Hawa wasanii tunawasaka nao watuhumiwe kama wahalifu wengine na wakichukuliwa hatua itakuwa fundisho kubwa kwa vijana ambao walikuwa na nia ya kujiingiza katika mtandao huo,’’ alisema.

Alisema ni vema kwa vijana wasiwafuate watu maarufu ambao kwa namna moja ama nyingine wanaushawishi mkubwa kiasi katika matumizi ya dawa hizo.

Kamishna Msikhela alisema wimbi kubwa la vijana wenye umri kati ya miaka 15 na 30 ndilo ambalo linajiingiza katika matumizi ya dawa za kulevya jambo ambalo ni hatari kwa Taifa.

“Vijana hawa ndio ambao wangekuwa tegemeo, vijana wa umri huo ndio ambao wangekuja kuwa viongozi wa baadaye, yaani kwa umri huo ndiyo wanaandaliwa kuwa madereva, mawaziri, wakulima, lakini leo wanakuwa mateja, ni jambo la hatari sana,’’ alisema.

Kamishna Msikhela alisema Jeshi la Polisi kwa sasa liko katika mkakati maalumu wa kuhakikisha elimu katika jamii inatolewa ili wananchi waweze kuelimika.

Alisema ulimaji wa bangi mashambani ni mkubwa kuliko mirungi, lakini aliongeza kuwa kama mateja mitaani wanapungua basi hata uingizaji wa dawa hizo kwa sasa nao umepungua.

HILI ni jibu la Diamond kuhusu kwanini anataja majina ya wacheza soka kwenye ngoma zake.

$
0
0

Sio kitu cha ajabu kusikia wasanii wakiwarusha wanamichezo kwenye ngoma zao. Hiki kitu kimeanza muda mrefu sana ndani ya Africa hadi nje ya Africa. Mmoja kati ya wanamichezao waliohi kutajwa sana kwenye nyimbo za HipHop huko marekani ni Michael Jordan au M.J kama wanavyomuita.

Tumeongea na Diamond Platinumz ambapo yeye na wasanii wake wa WCB wamekua wakitaja majina ya wana michezo mara kadhaa kwenye ngoma zao hasa Ronaldo na Mbwana Samatta.

Diamond tulipomuuliza kuna faida gani kwake na kipi kinamvutia kutaja majina ya wachezaji hao kwenye ngoma zake. Jibu lilikua hili “Hata kama mtu anafanya kazi kiasi gani kama jamii haijamkubali basi bado ana kazi ya ziada ya kufanya hadi akubalike.”

Aliendelea “Sasa mimi nawataja watu ambao wamefanikiwa kukubalika na jamii, ukiangalia watu kama Ronaldo na Samatta inaongeza chachu ya nyimbo na kupendwa zaidi. Hata wao pia wanafarijika kuona kwamba sisi kwa sisi pia tunakubaliana kwa kila kitu tunachofanya.”

Kocha Mpya wa Taifa Stars Atamba Kuipeleka Timu AFCON, 2019

$
0
0
Baada ya Shirikisho la soka Tanzania TFF, kumtangaza kocha wa Mtibwa Sugar Salum Mayanga, kuwa kocha mkuu wa timu ya taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars’ kocha huyo amesema yupo tayari kwa kazi hiyo na kuwataka wadau mbalimbali wa mchezo huo kumpa sapoti ili kufanikisha adhamira yake ya kuifikisha mbali timu hiyo.

Mayanga ameongea na mtandao wa Goal amesema, ameupokea kwa mikono miwili uteuzi huo ingawa ni kazi ngumu na yenye kuhitaji ushirikiano wa watu wengi, lakini atajitahidi kuhakikisha mambo yanakwenda sawa na timu ya taifa kufanya vizuri katika michuano ambayo inaikabili.

“Kuwa kocha wa timu ya taifa siyo kitu cha mchezo kwasababu kuna vitu vingi hasa ukizingatia timu hii kila mtu anasauti nayo kwahiyo nawaomba wadau tushikamane na kupeana sapoti ili kila tutakacho kifanya iwe ni kwa umoja wetu na mafanufaa ya wote,”amesema Mayanga.

Kocha huyo amesema jukumu lake kubwa ni kuhakikisha anakuwa makini katika kuwafatilia wachezaji na kuteua kikosi ambacho kitakubalika na Watanzania wote ili pindi timu inapopata matokeo mabaya watu wasimtupie lawama kocha.

Kocha huyo ameelezea mikakati yake ya kujenga timu imara ambayo itawashirikisha wachezaji wote wanaofanya vizuri kwenye klabu zao za ndani na nje ya Tanzania.

“Niwaombe wachezaji wazingatie na kulinda viwango vyao tunajenga timu yetu sote hivyo nilazima kwanza tuwe na uchungu nao na tuweke wivu wa mafanikio, kwani hatuwezi kuwaona Uganda wanakwenda kushiriki AFCN, na sisi tupo tukiwaangalia,” amesema Mayanga.

Kocha huyo amesema ataendeleza mikakati ya kocha aliyepita Boniface Mkwasa ambaye alikuwa akisisitiza nidhamu na uwanjibikaji wa kila mchezaji kwenye timu yake hivyo hatomuita mchezaji kwenye kikosi chake kutokana na jina lake au umaarufu aliokuwa nao.

Mayanga anachukua nafasi ya Mkwasa ambaye amemaliza mkataba wake wa mwaka mmoja kuifundisha timu hiyo akiwa kama kocha mzawa, akichukua mikoba ya Mholanzi Mart Nooij, ambaye alikatishiwa mkataba wake kutokana na mwenendo mbaya wa timu hiyo.

Source: Goal.com

Simu Ambazo Hazitakuwa na Huduma ya Whatsapp Kuanzia June 30 2017

$
0
0
Kampuni ya Facebook inayomiliki huduma ya Whatsapp imesema kuna baaadhi ya simu za zamani zikiwemo zile zinazotumia mfumo wa Windows Phone 7.1, Android 2.2 na simu aina ya iPhone 3GS/iOS hazitakuwa na huduma za whatsapp kwa sababu wanataka kuendana na mifumo inayotumiwa na watu wengi.

Hatua hiyo ilitangazwa na Facebook mapema ya mwezi february mwaka 2016 ambapo huduma ya whatsapp ilitakiwa kuacha kazi katika mifumo hiyo ya programu mwishoni mwa Desemba 2016 na ilikuwa  imeorodhesha simu za BlackBerry OS, BlackBerry 10, Nokia S40 na Nokia Symbian S60 kuwa miongoni mwa simu ambazo zingekatiwa huduma mwishoni mwa mwaka 2016 lakini ikabadilisha uamuzi wake na kuongeza muda hadi Juni 30, 2017.

Kampuni hiyo imesema wakati wa kuanzishwa kwa WhatsApp mwaka 2009, asilimia 70 ya simu wakati huo zilikuwa za BlackBerry na Nokia hivyo imeshauri wanaotumia simu za aina hiyo kununua simu za kisasa zaidi.

Akiwa na Umri wa Miaka 50, Janeth Jackson Amepata Mtoto wa Kwanza

$
0
0
Janeth Jackson (50)  dada wa marehemu Michael Jackson ni mwanamziki ambaye amekuwa na mafanikio makubwa  kupitia mziki wake, heshima ya mziki wake ikitambulika duniani kote. Lakini jambo moja ambalo amekuwa akitamani maishani mwake ni kupata mtoto. Imeripotiwa kuwa Janeth na mumewe Wissam Al Mana wamefanikiwa kupata mtoto wa kiume na kumuita Eissa Al Mana

Godbless Lema Arudishwa Tena Gerezani

$
0
0
Mahakama Kuu Kanda ya Arusha, leo imeshindwa kusikiliza rufani ya Jamhuri dhidi ya Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema kupinga dhamana yake, baada ya mawakili wa Serikali kuwasilisha notisi ya kukata rufaa katika Mahakama ya Rufaa wakipinga kusikilizwa kwa rufani hiyo .

Jaji wa Mahakama Kuu Kanda ya Arusha, Salma Maghimbi   alitarajiwa kutoa uamuzi juu ya rufaa ya Jamhuri iliyopinga  Lema kupatiwa dhamana Novemba 11 na Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Mkoa wa Arusha, Desderi Kamugisha katika kesi namba 440 na 441/2016 ya kutoa lugha za uchochezi dhidi ya Rais John Magufuli, ambapo siku hiyo Jamhuri iliwasilisha notisi ya mdomo.

Baada ya Lema kufikishwa mahakamani saa 3.25 asubuhi akiwa chini ya ulinzi mkali, huku pia polisi wakiwa wametanda viwanja vya Mahakama Kuu ndani na nje sanjari na gari moja la maji ya kuwasha, baada ya  mawakili wa pande zote kujitambulisha Jaji Maghimbi alisoma notisi ya Jamhuri kupeleka shauri hilo Mahakama ya Rufaa na kueleza kufungwa kisheria kutoa uamuzi wa rufani hiyo.

Madhara Ya Kuchaguliwa Mwenzi Wa Kuishi Naye Katika Mahusiano Ndoa

$
0
0
Ni imani yangu kuwa uko salama rafiki na unaendelea vizuri katika harakati zako za kila siku kuhakikisha unapata kile unachokitaka kwenye maisha yako. Tunamshukuru Mungu kwa zawadi ya siku hii ya leo ameweza kutustahilisha tena kuiona siku hii ya leo. Kwa hiyo rafiki, tutumie muda huu wa leo vizuri kwani leo ni siku bora ambayo haitokuja tena kutokea katika maisha yetu hapa duniani.

Mpendwa rafiki, napenda kukualika tena katika makala yetu ya leo tuweze kujifunza kwa pamoja yale ambayo nimeweza kukuandalia siku hii ya leo. Hivyo basi, nakusihi ungana nami mwanzo hadi mwisho wa makala hii ili tuweze kusafiri wote kwa pamoja. Leo tutakwenda kujifunza juu ya madhara ya kuchaguliwa mwenza wa kuishi naye kwenye maisha ya mahusiano. Je ni madhara gani rafiki? Karibu rafiki tuweze kujifunza wote kwa pamoja.

Katika moja ya matatizo yanayowasumbua watu duniani basi moja wapo ni mambo ya mahusiano. Mahusiano haya yanaweza kuwa mahusiano ya uchumba, mahusiano ya ndoa na nk. Sasa katika mahusiano ya ndoa wapo watu wengi sana wanaruka hatua muhimu sana ambazo baadaye zinakuja kuwaumiza vibaya. Hatua hizo muhimu ni urafiki na uchumba kwa hiyo, ikitokea watu wamekutana ndani ya miezi miwili, mmoja na kukimbilia kufunga ndoa ndio hawa wale wanaokuja kujuta kwa nini walifanya maamuzi hayo.

Mpendwa msomaji, malengo mahususi ya somo letu la leo ni madhara ya kuchaguliwa mwenza katika maisha ya mahusiano. Ziko jamii tofauti duniani zenye utaratibu au utamaduni wa kuwachanguliwa watoto wao wenza pale wanapokua wamekaribia ule umri wa kuishi ya maisha ya ndoa kama mke au mume. Wazazi wa jamii za kuwatafutia watoto wao wenza bado wapo mpaka leo katika zama hizi za taarifa na pengine unafahamu watu ambao wanafanya jambo hili kwenye jamii iliyokuzunguka.

Kwa mfano, mtoto tokea akiwa mdogo anawekewa ‘’ oda’’ mapema kuwa wewe utaolewa na mtu fulani au utamuoa mtu bila kujali unataka au la. Kwa hiyo, tabia hii inawanyima watoto wengi kuwa na mtu Yule anayempenda badala yake wanakuwa na watu ambao siyo chaguo lao la kutoka moyoni. Utamaduni huu unakuwa ni kama kumnyima mtu kuishi maisha anayotaka hapa duniani.
Unaporuhusu wazazi wakuchagulie mwenza wa kuishi naye katika maisha ya ndoa kwanza inakuwa ni utumwa wa hali ya juu. Kwanini?

Kwa sababu kuchaguliwa kufanya kitu ambacho hukipendi katika maisha yako ni utumwa. Vivyo hivyo, kuchaguliwa mwenza wa kuishi naye ni utumwa pia. Unapokuwa unachaguliwa mwenza wa kuishi naye unakuwa unavunja hatua muhimu sana katika kuelekea maisha ya ndoa ambayo ni urafiki na uchumba. Kupitia hatua hizi unaweza kumchunguza mwenzako ni mtu wa namna gani, falsafa yake ya maisha ikoje, ni mtu chanya au hasi, ni mtu wa kuigiza maisha au ni mtu halisi anayeishi bila kuigiza maisha na mambo mengine mengi unayotaka kuyajua kutoka kwa mwenzako.

Rafiki, watu wanaoishi na wenza wao kwenye maisha ya ndoa kwa kuchanguliwa na kwenda kuanza kuishi maisha ya urafiki, uchumba na ndoa kwa wakati mmoja huwa wanashinda sana. unakuta mwenzako anaishi falsafa tofauti kabisa na wewe ulivyotarajia. kwa mfano, wewe falsafa yako ni kuishi chini ya kipato chako na unakuta mwenzako anataka kuishi juu ya kipato kwa kufanya mambo ambayo hayana ulazima kwenye maisha. Lakini kama ulikuwa umemgundua mwenzako na kumsoma vizuri katika hatua za uchumba ungeweza kufanya maamuzi mapema kwa kumpima kama mtu huyo anakufaa au la kulingana na vigezo vyako.

Kuchaguliwa mwenza wa kuishi naye katika zama hizi ni aibu kwa kweli kwani ni kuchaguliwa kufanya chochote ambacho hukipendi ni utumwa katika maisha yako. Kumbuka rafiki, hata mzazi akikuchagulia mpenzi ambaye wewe humpendi na ukakubali utakua umejichagulia wewe mwenyewe kuingia shimoni. Kwa hiyo, hata wazazi wakikuchagulia kuishi na mwenza ambaye wanampenda wao ni kama kuchaguliwa maisha ya kuishi hapa duniani. Licha ya kuchaguliwa maisha wewe ndiye utakayeenda kuishi hayo maisha na wala siyo wazazi watakaopata raha au shida, ukiingia shimoni wao hawatakuwepo bali wewe ndio utawajibika.

Hatua ya kuchukua leo; usikubali kuchaguliwa mwenza wa kuishi naye katika maisha yako. Ishi na mtu unayempenda kutoka moyoni, ishi na mtu ambaye mliweza kupitia hatua za urafiki, uchumba ukamjua vizuri tabia zake ni mtu wa namna gani. Fanya kitu ambacho unakipenda ndio furaha ya kweli katika maisha ambapo utapata mafanikio makubwa yenye furaha na ubora wa hali ya juu.

Kwa kuhitimisha, tunaishi karni ya ishirini na moja na hatuko tena katika zama za mawe bali tupo katika zama za taarifa. Kuwa chachu ya mabadiliko kwa kuvunja utumwa huo katika jamii uliyopo siyo unasoma na kupata elimu ya juu bado ukirudi nyumbani wazazi wanakushurutisha kuoa au kuolewa na mtu Fulani bila ya ridhaa yako mwenyewe. Wewe ndio mwenye maamuzi ya maisha yako kwa sababu hakuna mtu mwingine atakaye ishi maisha yako zaidi ya wewe mwenyewe.

Jike Shupa Awaanika Mastaa Anaowauza Kwa Vigogo, Yumo Wolper, Masogange

$
0
0

DAR ES SALAAM: Imefichuka! Wakati mastaa mbalimbali wakijinasibu mara kwa mara kupitia vyombo vya habari kuwa hawafanyi biashara ya kuuza miili yao kama inavyodaiwa na baadhi ya watu, Zena Abdallah ‘Jike Shupa’ amekiri kuwauza wenzake kibao kwa vigogo, Risasi Mchanganyiko linakuwa la kwanza kukujulisha.

Jike Shupa ambaye ni ‘video queen’ kwenye nyimbo mbalimbali za wasanii wa Bongo Fleva, bila kujijua, amejikuta akiingia kwenye mtego wa kitengo cha Oparesheni Fichua Maovu (OFM) cha Global Publishers na kutaja idadi ya mastaa huku akieleza kila msanii ana dau lake tofauti, hakuna bei maalum.

ILIKUWA HIVI

Baada ya OFM kupata habari kutoka kwa vyanzo vyake mbalimbali kwamba mwanamama huyo anawauza wenzake, wakiwemo mastaa na kudaiwa kuwa ni kinara mkubwa wa biashara hiyo, OFM iliingia mzigoni na kupata majibu chanya.



AANZA KUINGIZWA KINGI

Makachero wa OFM waliwasiliana na Jike Shupa na mmoja wao akamuomba waonane ili aweze kupata huduma ya kuunganishwa na msanii atakayepatiana kwa bei ya wastani.

Jike Shupa baada ya kuelezwa hivyo alimuomba kachero huyo aliyejitambulisha kwake kama mfanyabiashara kuwa wakutane maeneo ya Kinondoni kwenye mgahawa mmoja maarufu majira ya saa moja usiku ili waweze kuzungumza vizuri kuhusu dili hilo.

OFM YAWAHI KUFIKA MGAHAWANI

Saa moja usiku kachero wa OFM alikuwa katika eneo la tukio, alipofika kwenye mgahawa huo alikaa na kumsubiri Jike Shupa ambaye aliingia na vijana wawili aliowatambulisha kuwa ni wadogo zake, ikiwa ni dakika 15 zaidi ya muda wa makubaliano.

OFM: Karibu sana Jike Shupa.

Jike Shupa: Asante, umenisubiri sana eeeh?

OFM: Yeah, lakini siyo tatizo.

Jike Shupa: Pole sana.


Baada ya Jike Shupa kukaa na mhudumu kumsikiliza anachohitaji (OFM ililipia bili yote), mazungumzo kati yake na OFM yalipamba moto na baada ya muda, alielezwa moja kwa moja kuwa dili alilotaka kumpa lilikuwa ni kumpata Amber Lulu ili awe naye kimapenzi, jambo ambalo lilionekana kuwa jepesi mno kwa Jike Shupa.

ATANGAZA DAU

Jike Shupa alimhoji OFM kama alikuwa na fedha za kutosha maana kazi yake yeye ‘anadili’ na watu wenye fedha tu na kwa kumuuza Amber Lulu, alisema atachukua shilingi milioni moja na nusu ikiwa ni nje ya fedha ambazo Amber Lulu atataka kulipwa.

‘MFANYABIASHARA’ FEDHA SI TATIZO

Kuonesha kwamba fedha si chochote, kachero wa OFM hakubisha juu ya hilo, alichofanya ni kumwambia kuwa nusu ya fedha alizokuwa anahitaji  angemlipa muda mchache wakati wakiendelea na mazungumzo, lakini akataka kujua kutoka kwa mwanamke huyo kama amewahi kuwauza mastaa wengine kama anavyofanya kwa Amber Lulu?


Jike Shupa: Wako wengi tu, ambao huwa ‘ninawa-connect’ (kuwaunganisha) na mabwana, mfano, (akataja jina la msanii mkubwa ambaye tunahifadhi jina lake kwa sababu hatukumpata), Tunda, Masogange, Wolper na wengine wengi.

ETI HAKUNA ANAYEMCHOMOLEA

“Hakuna staa wa kike ambaye simfikii, ni wewe tu kusema unamtaka yupi, unatoa pesa halafu mimi namaliza mchezo wote.

“Unawaona hata hao vijana niliokuja nao (anawanyooshea kidole walipokuwa wamekaa)? Hao ni mashoga, huwa nawaunganishia watu (wanaume) wanaowataka kufanya nao mapenzi.”


OFM YAMMWAGA KIAINA

Baada ya OFM kukamilisha upelelezi wake na kujiridhisha kuwa kweli Jike Shupa ni kuwadi na anawauza wasanii wenzake wa kike pamoja na mashoga kwa mapedeshee, ilimtoka ‘kisanii’ mwanadada huyo huku ikiwa na ushahidi wa kutosha.

WATUHUMIWA WAFUNGUKA

Alipotafutwa Masogange na kusomewa mashitaka yake, awali alianza kwa kusema hana urafiki kivile na Jike Shupa na kwamba waliwahi kukutana naye mara moja tu.


“Sina urafiki kivile, nachukia sana mtu kuzungumza kitu ambacho sijafanya, kwanza huyo Jike Shupa mwenyewe hana mtu wa kuniunganisha naye. Hebu ngoja nimpigie sasa hivi nimpe vidonge vyake, sipendagi ujinga mimi,” alisema Masogange na baada ya kumpigia na kumkosa, alimuandikia meseji ndefu Jike Shupa ya kumsuta ambayo aliikopi na kuipiga picha kisha kumtumia mwandishi wetu.

Jike Shupa hakujibu ujumbe huo wa kichambo ambao ulionesha umefika kwenye simu yake.

AMBER LULU NAYE ANENA

Kwa upande wake Amber alikanusha vilivyo madai hayo ya kuuzwa na kama haitoshi, alisema hana hata urafiki naye.

“Huyo labda anatafuta kiki, sina hata urafiki naye ataniuza kivipi? Sinaga hizo habari,” alisema Amber.


WOLPER NAYE AMKANA

Alipotafutwa Wolper na kuelezwa kama amewahi kupigwa bei na Jike Shupa, alimkana kuwa hamtambui na kusema anaomba atumiwe picha ili japo amuone anafananaje, kwani watu wa aina hiyo anashindwa kuwaelewa awaweke kwenye kundi gani.

“Unajua kama ana akili timamu si mwezi mchanga, inabidi nidili naye na ikiwezekana nimshtaki maana atakuwa amenizushia jambo ambalo sijawahi kulifanya lakini kama ni mwezi mchanga (hajakamilika kiakili), naweza nikamsamehe,” alisema Wolper.

MASTAA ZAIDI WAFUNGUKA

Mastaa wa kike mbalimbali walipotafutwa na kuelezwa habari hizo kila mmoja alionesha kukasirika na kuzungumza lake.


BABY MADAHA

“Huyo Jike Shupa hawezi kuniuza mimi labda hao anaoonana nao na suala la kuuzwa ni la mtu binafsi huwezi kuuzwa kama ng’ombe.

“Huyo msanii ana uwezo wa kuwauza wale anaowamudu kwangu atagonga mwamba kwani hatuongei lugha moja, yaani viwanja ninavyoenda ni tofauti na vyake, wanaume anaokutana nao ni tofauti na wale nitakaokutana nao mimi, kwanza Kinondoni na Mbezi ni wapi na wapi?”

SHAMSA FORD

“Mimi nimeolewa hilo haliwezi kunitokea kabisa waulizeni hao ambao hawaeleweki nina mume ndani tayari.”

ISABELA MPANDA

“Huyo Jike Shupa hawezi kuniuza kwa sababu ninajitambua labda hao wengine na sina shida na siwezi kuuzwa kama karanga, huwa naenda kwa mwanaume ninayemtaka.”

ROSE NDAUKA

“Jamani hivyo ni vitu vya kipumbavu siwezi kuvizungumzia wala kumzungumzia mtu kama huyo.”

NENO LA MHARIRI

Kwa kuwa OFM imemnasa Jike Shupa ‘live’ akithibitisha madai ya kuwa anawauza wenzake, anapaswa kuachana na vitendo hivyo mara moja kwani vinakwenda kinyume na mila na desturi za Kitanzania.

Ni tabia ambazo zinakwenda kinyume na mafundisho ya imani za dini zote, ni wakati wa Jike Shupa na mastaa wenzake wote wanaojihusisha na vitendo hivyo vya kikahaba kuachana navyo na kutafuta mkate wa kila siku kwa njia halali.

Stori: waandishi Wetu, Risasi Mchanganyiko, Jan 4-6, 2017, Toleo 1388

Hali si Shwari Wolper na Harmonize....Meseji Aliyopost Wolper Yaonyesha Wameachana

$
0
0

Jacline Wolper ame post hii halaf ghafla kafuta, hii maana yake nini wadau?
Jisomee alichoandika kupitia kwenye ukurasa wake wa Instagram:

Jeshi la Polisi Laua Majambazi Watatu Dar es Salaam

$
0
0
Watu watatu wanaosadikiwa kuwa ni majambazi, wameuawa katika tukio la kurushiana risasi na polisi katika eneo la Mikocheni, karibu na Shule ya Sekondari Feza jijini Dar es Salaam.

Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Simon Sirro watuhumiwa hao waliuawa jana asubuhi na majina yao bado hayajafahamika.

Alisema marehemu hao ni waliohusika katika tukio la kupora zaidi ya Sh milioni 26 katika makutano ya barabara ya Mandela na Nyerere, eneo la Tazara, Dar es Salaam.

Hata hivyo, alipoulizwa ufafanuzi zaidi wa tukio hilo na je watuhumiwa hao walikuwa na usafiri gani, Sirro alisema kuwa hizo ni taarifa za awali na taarifa rasmi atazitoa leo.

Alisema kwamba miili ya marehemu, imehifadhiwa katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili.

Taarifa zaidi zinadai kwamba watuhumiwa hao akiwemo mwanamke aliyejisalimisha, ambaye ndiye alikuwa dereva wao, walikuwa na mpango wa kufanya uvamizi katika maeneo hayo, ambapo pia baadhi yao walifanikiwa kukimbia.

Lakini, Polisi haijathibitisha taarifa hizo na imeeleza kuwa itatoa taarifa  zaidi leo.

Panga Lapita Tanesco...Habari Zilizopo Katika Magaeti Ya Leo Alhamisi ya January 5

$
0
0


Panga Lapita Tanesco...Habari Zilizopo Katika Magaeti Ya Leo Alhamisi ya January 5

Wakurugenzi TANESCO Wasimamishwa Kazi, Mmoja Ajiuzulu!

$
0
0
Wakuu huku Tanesco hali si shwari mpaka sasa Wakurugenzi wetu watatu wameshushwa vyeo na kuhamishiwa katika chuo cha TANESCO (TSS).

Declan Mhaiki aliyekuwa Deputy Managing Director - Transmission
Sophia Mgonja aliyekuwa Deputy Managing Director - Distribution
Mr Kachwamba aliyekuwa Deputy Managing Director - Generation.

Aidha Watson Mwakyusa, Mkurugenzi wa Idara ya Rasilimali Watu yeye ameamua kuachia ngazi.

Source:Jamii Forums

Kalapina Amlaumu Mama Chid Benz Kwa Kumdekeza na Kumwendekeza Chid Benz Mpaka Ameshindwa Kuacha Madawa

$
0
0
Rapa Kalapina ambaye ni mwanaharakati wa kuwasaidia watu ambao wameingia kwenye matumzi ya dawa za kulevya amefunguka na kusema kuwa mama yake mzazi Chid Benz kama mtu anayemuendekeza Chid na kumfanya asitoke kwenye matumizi ya dawa za kulevya.
Kalapina amesema mama huyo anampenda sana mtoto wake kiasi cha mtoto kujua na kuona kwamba hata akifanya jambo fulani yupo mama yake ambaye atasimama na yeye.

Kalapina alisema hayo jana kupitia kipindi cha Planet Bongo na kusema wazazi wengi wamekuwa chanzo cha watoto wao kuingia kwenye matumzi ya dawa za kulevya na kuingia hata kwenye mahusiano ya jinsi moja sababu ya wazazi wamekuwa wakiwadekeza sana watoto au kuwapa uhuru mkubwa na kuruhusu maisha ya uzungu kutawala.

"Kiukweli mama yake mzazi Chid Benz anampenda sana mwanaye na hali hiyo inampelekea mdogo wangu yule kuona hata nikizingua mama atanitafuta tu, au kuona mama atasimama na yeye tu sababu mama yake anampenda sana, lakini siyo Chid Benz tu wazazi wengi wanawalea watoto kwa kuwadekeza sana, wazazi hawana muda na watoto na hili linachangia vijana kuingia kwenye madawa ya kulevya hata kwenye ushoga pia, lakini sisi wazazi wetu zamani ulikuwa ukizingua unapigwa sana hivyo lazima utanyooka tu" alisema Kalapina.

Source:EATV
Viewing all 104709 articles
Browse latest View live




Latest Images