Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104709 articles
Browse latest View live

Shaffii Dauda Apita Katika Jumba la Diamond Nchini South Afrika na Kuandika Haya

$
0
0

BY @shaffih - Nikiwa njiani#afcon2017gabon nimekutana na @diamondplatnumz kwenye flight moja,connection ya another flight to Libreville-Gabon ilikuwa ni baada ya masaa 7,akanikaribisha nyumbani kwake kupata chai ikiwa ni pamoja na kusalimia kidogo familia yake ambayo inaishi hapa Pretoria-SA, asante sana shemeji @zarithebosslady pamoja na bi mkubwa wetu Sandra. Photo credit @kendrah_michael. Now on our way to Gabon!!!

Hali Tete Kwa Waziri Prof Muhongo, Yabainika Alishiriki Vikao vya Kupandisha Bei ya Umeme

$
0
0
Siku chache baada ya Waziri wa Nishati na Madini, Prof. Sospeter Muhongo kusitisha kupandishwa kwa gharama mpya za umeme kwa madai kuwa hakushirikishwa katika mchakato huo, taarifa zimebainisha kuwa waziri huyo alishiriki katika kikao kilichoshauri uamuzi wa kulitaka shirika hilo liwasilishe mapendekezo ya bei mpya ya nishati hiyo.

Kwa mujibu wa taarifa iliyochapishwa kwenye gazeti la mwananchi toleo la Alhamisi, Januari 12, 2017 zilizeleza kuwa waziri alizuia kupandishwa kwa gharama za umeme kwa asilimia 8.5 kuanzia mwaka 2017  akisema kwa utaratibu TANESCO wanatakiwa ipeleke maombi ya bei EWURA maonbi ya bei mpya na kabla ya mamlaka hiyo kutangaza ni lazima waziri mwenye dhamana akabidhiwe ripoti ya mwisho.

Waziri Muhongo wakati akisitisha ongezeko hilo alisema kuwa alishtushwa na kutangazwa kwa bei mpya bila kupokea ripoti ya mwisho. Waziri alisema kuwa matatizo ya shirika hilo hayawezi kutatuliwa kwa kuwabebesha mzigo wananchi.

Licha ya waziri kueleza hayo yote lakini taarifa za uhakika zinaonyesha wazi kuwa alishiriki kikao cha wadau kujadili mpango kazi wa TANESCO Septemba 28 mwaka jana ambapo walikubaliana shirika hilo lipeleke maombi ya kuongeza bei EWURA kabla ya siku mbili yaani, Septemba 30. Kikao hicho  kilifanyika jijini Dar es Salaam kikiwashirikisha wadau kutoka Wizara ya Nishati na Madini, Benki ya Dunia (WB) na TANESCO.

Siku mbili baada ya kikao hicho Waziri Muhongo aliandika barua kwenda kwa Waziri wa Fedha, Dkt Mpango akimueleza maazimio ya kikao hicho.

Waziri Muhongo alipoulizwa kuhusu barua hiyo na kufanya kikao hicho cha mpangokazi ambapo alisema kuwa kufanya kikao si jambo la kushangaza kwa kuwa amekuwa akifanya mikutano hiyo na wahisani mbalimbali kama Umoja wa Ulaya (EU), Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) na Benki ya Dunia (WB).

Alipoulizwa kuhusu kushiriki vikao vya kupandishwa bei na kuandika barua kwa waziri wa fedha, Waziri Muhongo alisema kuwa nyaraka zote alizoandika hakuna sehemu pameonyesha kuongezwa bei ya umeme

Kwa upande mwingine EWURA imekiri mara kadhaa kuwa wamekuwa wakiishirikisha Wizara ya Nishati na Madini katika hatua mbalimbali za mchakato wa kupitia na hatimaye kutazanga bei ya umeme.

Mkurugenzi Mkuu wa EWURA, Felix Ngamlagosi alisema alishtushwa sana na kauli ya Waziri Muhongo kuwa hakushirikishwa kwenye upandaji wa bei ya umeme. Alisema mara kadhaa wamekuwa wakiandika barua kwenda wizara yenye dhamana kuhusu hatua za mchakato mzima.

Ukweli wa Nuh na Shilole Mwanza, Huu Hapa

$
0
0
Msanii Nuh Mziwanda ambaye bado anafanya vyema na wimbo wake ‘Jike shupa’ amekanusha tetesi za yeye kuwa pamoja na mpenzi wake wa zamani Shilole jijini Mwanza siku mbili hizi.


Shilole na Nuh Mziwanda Enzi za Penzi lao
Akiongea kwenye kipindi cha Planet Bongo, Nuh Mziwanda anasema ni kweli alimuona Shilole Mwanza kwenye club ambayo yeye alikuwa anafanya show na aliambiwa kuwa yupo pale lakini hakukutana naye wala ku-kiss na yeye kama ambavyo watu wanadai kuwa waliwaona wakali hao wakiwa pamoja na waki kiss.

“Mimi nimekuja Mwanza kwenye show zangu nimekutana naye tu Club hivyo mimi siwezi kumkataza mtu kuingia sehemu hivyo hilo ni jambo la kawaida, mimi mwenyewe niliambiwa yupo humu so sikujali maana mimi nilienda kufanya kazi na yeye alikwenda kufanya kazi kimpango wake. Kwa hiyo hayo maneno mengine yanayoongeleka mimi mwenyewe siyajui mimi nimekuja Mwanza kutafuta pesa” alisema Nuh Mziwanda

Mbali na hilo Nuh Mziwanda anasema kwa yeye saizi ni mume wa mtu hivyo hawezi kufanya mambo ya ajabu ajabu kama hayo kwa kuwa yeye anajiheshimu na kuheshimu ndoa yake

“Mimi nimeoa najiheshimu siwezi kufanya vitu ambavyo si vya maadili au ambavyo sitakiwi kuvifanya kilichonileta Mwanza ni kufanya show na kufanya makubaliano na kusaini mkataba wa show yangu nyingine itakayofanyika Dar es Salaam” alisema Nuh Mziwanda


Darasa Akiri Kuwa Aliwahi Kwenda Kwa Mganga ili Afanikiwe Kimuziki

$
0
0
Mwanamuziki wa bongofleva nchini Tanzania anayefanya vizuri na wimbo wake wa Muziki, Darassa kwa mara ya kwanza amekiri kuwa aliwahi kwenda kwa mganga wa kienyeji ili amsaidie atoke kimaisha.

Darassa aliyasema hayo jana usiku alipokuwa katika kipindi za Ala za Roho cha Clouds Fm ambapo mtangazaji alitaka kujua kama aliwahi kwenda kwa mganga tangu azaliwe.

Nimewahi kwenda kwa mganga mara moja, ni kipindi cha nyuma kidogo. Nilikwenda kwa mganga baada ya maisha kuwa magumu sana nikiamini ataweza kunisaidia. Unajua mimi nimekulia uswahilini na kule ukiwa kijana kunakuwa na mambo mengi sana, hivyo nilishawishiwa nikakuta nimeenda, alisema Darassa.

Darassa alisema baada ya kufika kwa mganga aliona kuwa mganga hawezi kumsaidia na tangu alipoondoka hakurudi tena. Aidha, alisema kuwa aliacha kuamini kwenye masuala ya kishirikina kwani ndio kikwazo kikubwa cha wakazi wengi wanaoishi uswahilini hawaendelei.

Darassa amewaasa watu mbalimbali wanaoamini katika imani za kishirikina kuwa hazitawasaidia na badala yake Mungu yupo na wakimuamini atawasaidia kama ambavyo imekuwa kwake ambapo ametoka kwenye maisha ya dhiki sana.

Alipoulizwa kama ajali yake iliyotokea mwezi uliopita aliuhususha na kulogwa, alisema kuwa yeye hakuihusisha na imani za kishirikina na kuwa sababu kubwa ya ajali ni uchovu tu licha ya baadhi ya watu kusema kuwa na mambo ya kishirikina.

Maneno ya Dully Skykes Juu ya Hali ya Chid Benz Kwa Sasa

$
0
0


"Chid namchukulia kama mgonjwa, mwathirika yeyote ni
mgonjwa na ndio maana kuna rehab/soba house kwahiyo
yule ni mgonjwa na ninamchukulia kama mgonjwa kwahiyo
tumuombee mungu atakapoweza kupona tumpe na ushauri
pia asikae na watu ambao wanamletea au watu wanaotumia
pamoja nae ili tumpate ChidBenz ambaye sisi tunamuhitaji"
alisikika @princedullysykes kwenye XXL wakati akitambulisha
wimbo wake mpya #yono

BASATA: Diamond Amestahili Kukabidhiwa Bendera ya Taifa Kwajili ya Show yake ya Ufunguzi wa AFCON 2017

$
0
0
Kumekuwa na sitofamu katika mitandao ya kijamii kuhusu ni nani anastahili kukabidhiwa bendera ya Taifa ili kuwakilisha nchi, baada ya Diamond Platnumz kukabidhiwa bendera ya Taifa jana na Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Nape Moses Nnauye kwajili ya show yake ya kutumbuiza ufunguzi wa michuano ya Afcon 2017 inayofanyikia nchini Gabon weekend hii.

Diamond akikabidhiwa bendera ya Taifa na Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Nape Moses Nnauye

Mashabiki wengi katika mitandao hiyo wamekuwa wakizozana bila kupata jibu kwamba ni kwanini Daimond alikabidhiwa bendera hiyo kwa ajili ya kuwakilisha Tanzania wakati anaenda kufanya show yake binafsi.

Akiongea na Bongo5 Alhamisi hii kuhusu suala hilo Katibu mkuu wa na Baraza la Sanaa la Taifa (Basata) Godfrey Mngereza amesema bendera ya Taifa anaweza kupewa mtu yeyote ambaye anaenda nje ya nchi, na safari yake ina manufaa kwa taifa lake.

“Suala wa Waziri Nape ambaye ndiye Waziri mwenye dhamana ndani ya Wazira wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kumkabidhi Diamond bendera ya Taifa ni jambo zuri kwa sababu ingawa Diamond anakwenda kufanya show yake lakini tukumbuke yule ni mtanzania pekee pale ambaye anakwenda kuliwakilisha Taifa lake kwa show yake mbele ya maelfu ya watu Afrika nzima, jina lake linatambulika pale lakini wao wanamtambua yule kama mtanzania na hata akifanya vizuri sifa zinaenda kwa yeye pamoja na Taifa lake,” alisema Nngereza.

Pia Nngereza alidai mtanzania yeyote anaweza kukabidhiwa bendera ya katifa kama anaenda kufanya tukio lolote ambalo linaweza kuipatia sifa nchi yake kwa namna yoyote.

“Mtu yoyote ambaye anaenda nje ya nchi kwa ajili ya matamasha makubwa au kama kuna namna ambavyo anaenda kufanya kitu ambacho kimpatia yeye faida pamoja na Taifa lake anaweza kukabidhiwa bendera, awe mtanzania tu. Kwa hiyo hata ukiwa mtangazaji, mchezaji, vikundi vya ngoma na sanaa mbalimbali wanaweza kukabidhiwa bendera kama wakihiitaji kwa sababu kuna wengine hawatoi taarifa kuhusu matukio yao lakini kama ukitoa taarifa na mamlaka ikaona kuna umuhimu wa kufanya tunafanya hivyo kwa sababu ni kwa ajili ya taifa letu,”
Sikiliza Hapa:

Hoja za Zitto baada ya Rais Magufuli Kusema Nchi Haina njaa

$
0
0
Kiongozi wa chama cha ACT Wazalendo ametoa hoja zake baada ya Rais Dkt John Mafuguli kusema kuwa nchi hii haina balaa la njaa.



Zitto ameyaainisha hayo katika ukurasa wake wa Facebook kama ifuatavyo:

Rais umeamua kuchagua upande wa wanaokupa Taarifa za uwongo na majungu. Muda utasema. Wengine tumesema, tumeonya kwa mapenzi mema ya nchi. Wewe ndio mwenye vyanzo vingi na mkono mrefu. Umetamka hakuna njaa. Umefunga mjadala. Lakini uwe tayari kubeba mzigo wa maamuzi yako yanayotokana na habari za majungu, uwongo na kutaka kukufurahisha.
Anayejua kuna njaa nchi hii ni Rais,mimi ndio naejua wapi kuna njaa na wapi hakuna.Tanzania hii haina njaa wala watu hawana njaa,anasema Rais JPM kutoka Simiyu
Wanaotangaza kuna njaa ni watu wanaolipwa pesa na wafanyabiashara na wanasiasa ili kusema nchi ina njaa na ukame wa kuuwa watu na mifugo.
=========
Yapo magazeti yanayotumiwa na wafanyabiashara na wanasiasa ili kusema Tanzania kuna njaa.Kuna mfanyabiashara mmoja ana tani elfu25 za mahindi bandarini anataka aingize bila kodi kwa kisingizio cha njaa Tanzania,Rais anasema ameagiza alipe kodi na asipitishe mahindi hayo bure kwa kisingizio cha njaa,Tanzania haina njaa.

Kuna mfugaji mwingine walimlipa hela wanasiasa huko Mvomelo,akaenda mbele ya Tv na kusema ana mifugo inakufa kwa ukame.Nimeagiza wamwambie auze hizo ng’ombe ili aepukane na ukame.Huwezi kuwa na ng’ombe karibu elfu na zaidi na wanakufa ng’ombe 16 unaanza kulialia badala ya kuuza upate hela ya kula na ujikimu kimaisha.

Rais anasema hatapeleka chakula Simiyu na Bariadi eti kisa ukame.Wananchi walitakiwa kujua kama mvua ni ndogo basi walime mazao yanayostahimili ukame na si kulazimisha kulima mahindi yanayohitaji mvua nyingi.JPM anasema msema ukweli ni mpenzi wa Mungu,na yeye anasema ukweli kuwa hataleta chakula popote kwa sababu ni wanasiasa na wafanyabiashara ndio wananunua magazeti kutangaza njaa.
Rais kamuumbua Dr Kamani,mwenyekiti wa CCM mkoa wa Simiyu anayemtaka Rais aruhusu kuingiza mifugo kwenye hifadhi,wakati yeye akiwa waziri wa Mifugo wakati wa JK hakufanya hivyo,sasa kama sio unafiki ni nini?JPM anasema yeye sio mnafiki,hataruhusu mifugo kuingia kwenye hifadhi kwa sbb ya sifa za kisiasa huku akiharibu mazingira.

Rais anasema Watanzania walizoea kuambiwa maneno “matamu matamu” na wanasiasa huku muda ukienda bila kuwa na maendeleo.Yeye anataka watanzania wasahau maneno matamumatamu.Ataongea ukweli tu,tena ukweli mchungu hata kama utawaudhi watu,kama ni jiwe atasema jiwe na sio mchanga mgumu uliokusanyika pamoja.

Rais amewaomba Watanzania wazidi kumuombea,wapo “wapinzani” wake wanamsimanga kwa kununua ndege,na wakati kwa miaka mingi Tanzania haikuwa na ndege,na hao wanaomkosoa ndio hao hao wanaokimbilia kuzipanda.

Baadae Rais akamuita mhandisi Maji wa Mkoa wa Simiyu ili aje aelezee mpango wa Maji kutoka Ziwa Victoria kuja mkoa wa Simiyu na Wilaya zake…Mhandisi hakutoa majibu mazuri,akaja RAS ambaye akasema kikwazo ni mlima wa Ngasamo ambao una madini ya Nikel(?)ambao ndio ilipaswa kuwa na tank la kuleta maji.Eneo hilo tayari kuna muwekezaji na hawawezi kuweka tank.

Rais ameamuru mgodi huo usipewe leseni na huyo muwekezaji apewe taarifa kuwa huo mgodi haupo tena na watu wapewe eneo la kuweka Tank.Amemuagiza Kamishna wa madini aifute leseni na ujumbe umfikie Waziri wa Madini na autekeleze.

Na mwisho Rais amesisitiza watu wafanye kazi,hakuna wa kugawiwa chakula bure.Hawezi akawasomeshea watoto bure,ajenge barabara,anunue ndege,ajenga hospital na kuweka madawa ktk hospital,alete huduma ya maji na bado watu wakae tu na kusubiri eti serikali itawatafutia chakula.Watu wafanye kazi ili wapate chakula na si kusubiri chakula cha serikali.”SERIKALI YANGU HAITATOA CHAKULA,NINAPOSEMA SILETI CHAKULA SILETI KWELI,WALA SIMUNG’UNYI MANENO NA SITALETA KWELI,MLIZOEA MANENO MATAMU SASA MIMI SINA MANENO MATAMU”alisisitiza Rais Magufuli.

Mwishoni Rais amemalizia kwa kusema “Naweza kuwa sio mwanasiasa mzuri sana,Lakini ipo siku mtakuja kunikumbuka”


Rais Magufuli apigilia msumari kwa wapiga dili nchini

$
0
0
RAIS John Magufuli ameendelea kupigilia msumari kwa watanzania na viongozi wasiopenda kujishughulisha na kuwajibika na kutegemea zaidi fedha za bure za umma.

Amehakikishia kuwa hali zao zitaendelea kuwa mbaya, isipokuwa kwa wale watakaowajibika na kujishughulisha.

Amesema wale wote wanaolalamika kuwa hawana fedha mfukoni kwa hivi sasa, walizokuwa nazo hazikuwa zao, ndio maana wanalalamika.

Katika hotuba zake mwaka jana katika sehemu mbalimbali nchini, Rais alisema wanaolalamika hawana hela mfukoni ni ‘wapiga dili’.

Rais alibainisha kuwa Serikali ya Awamu ya Tano, itahakikisha inamaliza hali mbaya iliyokuwa inalikumba taifa la watanzania, ambapo watu wachache ndio waliokuwa wakinufaika na fedha za umma huku wananchi wengi wakiendelea kuumia na umasikini.

Alisema hayo mkoani Shinyanga jana wakati akizungumza na wananchi kuhusu maendeleo ya mkoa huo na kumbukumbu ya maadhimisho ya Miaka 53 ya Mapinduzi ya Zanzibar. “Nimejitoa sadaka kwa ajili ya nchi hii, mimi sikuwa na urais ila mmenipa nyie, sasa nawaahidi mimi na serikali yangu tutawatetea kwa nguvu zote dhidi ya mafisadi.

Nasikia kuna watu wanalalamika kuwa eti fedha hamna, kwani zilikuwa zinauzwa sokoni? alihoji. Alisema watu wote wanaolalamika kuwa fedha zimepotea mitaani, ni wale waliokuwa wamezoea kupata fedha za bure bila kuzitolea jasho.

Aliwahakikishia kuwa wataendelea hivyo hivyo kutaabika, huku wale waliokuwa wakijishughulisha wakineemeka. Alisema fedha zilizotumiwa na mafisadi kipindi cha nyuma ni nyingi mno, kwani kila serikali ikitenga na kutoa fedha za maendeleo, zimekuwa zikiishia mikononi mwa mafisadi.

“Watu walikuwa wanajipatia tu fedha bila kuzitolea jasho, unakuta mtu anaenda nje kila siku, wapo waliofikia kufanyia mikutano ya taasisi zao za ndani nje ya nchi, mfano pale Muhimbili (hospitali ya taifa) nilipoenda nilikuta akinamama wanajifungulia chini huku fedha zipo lakini zimetengwa kwa ajili ya starehe,” alifafanua.

Alisema wakati serikali yake inaingia madarakani ilikuta nchi ina hali mbaya hali iliyoilazimu asafishe kila kona ya idara, ndipo walipopatikana watumishi hewa zaidi ya 18,000, wanafunzi hewa 65,000, mikopo ya elimu ya juu hewa yenye thamani ya Sh bilioni 3.5.

Alisema hata fedha za Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF), zinazotolewa kwa kaya maskini, zilitolewa kwa kaya hewa 55,000.

Rais alisema ni wakati sasa Watanzania na serikali kwa ujumla wakashirikiana kuijenga Tanzania mpya, itakayomkomboa kila mwananchi akiwemo masikini, kwani kutokana na utajiri ambao Tanzania inayo, imekuwa ikichekwa kwa kuendelea kuwa masikini.

Utumbuaji majipu
Alisema pamoja na kwamba wapo baadhi ya watu wanachukizwa na hatua ya utumbuaji majipu kwa watumishi wasiowajibika, serikali yake itaendelea kuwatumbua watumishi na viongozi wanaokwenda kinyume na maadili yao.

“Ni bora nichukiwe na watu wachache kuliko kupendwa na wengi huku mambo yakienda mrama. Wale wote wanaodai mtindo wangu wa kutumbua ni mbaya hawa ndio majipu. Kabla ya utumbuaji watanzania walikuwa wanaishi maisha ya ajabu, na kusisitiza kuwa alikuwa mtumishi wa serikali kwa kipindi cha miaka 10 anajua anachoongea,” alisisitiza.

Aliomba Watanzania wamuombee ili aweze kuendeleza jitihada zake za kupambana na mafisadi kwani serikali yake ya awamu ya tano imejipanga kuendelea kuongoza kwa ukali kwa faida ya watanzania wote wakiwemo wanyonge na masikini.

“Lengo langu ni kuhakikisha wale wote waliokuwa wakila na kuchekelea kipindi cha nyuma wakati wenzao wanataabika, sasa waishi kama mashetani na wale waliotaabika waishi kama wafalme,” alisema.

Hatua za maendeleo
Dk Magufuli alisema kutokana na kutambua adha wanayoipata watanzania kutokana na huduma mbovu, serikali yake imejitahidi kupambana na kuboresha maendeleo mengi ikiwemo sekta za elimu, miundombinu usafiri na afya.

Alitolea mfano namna serikali hiyo ilivyofanikiwa kukusanya mapato kwa kubana maeneo yote yenye ubadhirifu na kufanikiwa kuongeza mapato kutoka Sh bilioni 31 hadi Sh trilioni moja, hali iliyosaidia serikali hiyo kununua ndege sita, mbili zikiwa tayari zimewasili.

Pia alisema serikali imefanikisha kusimamia elimu bure kwa kutenga kiasi cha Sh bilioni 18.77 kila mwezi, zinazokwenda moja kwa moja shuleni kwa ajili ya kuwezesha wanafunzi kusokma bure katika shule za msingi na sekondari.

Alisema pia serikali yake kwa kipindi kifupi, imefanikiwa kuongeza bajeti ya afya na kufikia Sh trilioni 1.99 na kati ya fedha hizo bajeti ununuzi wa dawa imeongezeka kutoka Sh bilioni 31 hadi Sh bilioni 250.

Mikakati
Aidha, kiongozi huyo alisema serikali yake imejipanga kuendelea kuwaletea maendeleo wananchi, ambapo pamoja na kununua meli mbili katika Ziwa Victoria na Tanganyika, pia imeanza mchakato wa kujenga reli ya kisasa ambayo imetengewa jumla ya Sh trilioni moja katika bajeti ya mwaka 2016/17.

Alisema Tanzania imebarikiwa kuwa na rasilimali za kutosha ikiwemo bahari, mito, maziwa, madini kama vile dhahabu na wanyama, lakini bado imeendelea kuwa na umasikini.

Alisema kutokana na hali hiyo, serikali yake imejipanga kuijenga Tanzania mpya ikiwemo viwanda ili kuweza kutimiza lengo la kuifanya Tanzania kuwa miongoni mwa nchi zenye kipato cha kati.

“Hapa Shinyanga kuna mwekezaji ambaye ana takribani miaka 10 sasa tangu nikiwa waziri wa mifugo na uvuvi na baadaye ujenzi, hajaendeleza kiwanda cha nyama, naagiza uongozi wa mkoa wawekezaji kama hawa waondolewe wapewe wengine tusonge mbele,” alisisitiza.

Pamoja na mwekezaji huyo, pia alipotembelea mgodi wa Maganzo alipatiwa taarifa za kuwepo kwa migogoro ya ardhi na kuwataka mawaziri wa ardhi na mazingira, kushughulikia suala hilo haraka iwezekanavyo.

Maji
Akizungumzia kero ya maji iliyowasilishwa mbele yake na Mbunge wa Shinyanga Mjini, Steven Masele, Dk Magufuli alibainisha kuwa atamtuma Waziri wa Maji kufuatilia bei inayotozwa kwa wakazi hao, ili kuwaondolea mzigo wa kutozwa bei kubwa ya maji.

Hata hivyo, Rais huyo aliweka wazi kuwa endapo atabaini bei inayotozwa kwa wakazi hao, haiendani na bei zinazotozwa katika miji mingine, atahakikisha ama anaipunguza au kuiongeza ili iendane na miji mingine.

Mapinduzi
Pamoja na hayo, Dk Magufuli alizungumzia maadhimisho ya siku ya mapinduzi ya Zanzibar na kubainisha kuwa kuanzia sasa serikali itakuwa inaadhimisha sikukuu za kitaifa katika mikoa mbalimbali ili kila mtanzania afaidike na sherehe hizo.

Alisema yeye na Rais wa Zanzibar, Dk Ali Mohammed Shein walipanga kila mmoja aadhimishe sherehe hizo katika maeneo tofauti, ambapo Dk Shein alikuwa visiwani Zanzibar yeye akiwa Shinyanga.

“Watu wamezoea wakisikia sherehe za kitaifa basi viongozi ni kulundikana sehemu moja. Sasa hili hatutolifanya, hizi ni sherehe za kitaifa kila mtanzania ana haki ya kuziadhimisha akiwa na viongozi wa kitaifa” alisema.

Chadema kukata rufaa hukumu ya Mbunge

$
0
0
CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimesema hakikubaliani na hukumu iliyotolewa na Mahakama ya Wilaya ya Kilombero dhidi ya Mbunge, Peter Lijualikali na kwamba imepanga kukataa rufaa katika Mahakama Kuu.

Lijualikali ambaye ni Mbunge wa Kilombero, alihukumiwa kwenda jela miezi sita baada ya mahakama kumtia hatiani kwa kosa la kufanya fujo na kusababisha taharuki na uvunjifu wa amani.

Akizungumza na waandishi wa habari jana katika Makao Makuu ya chama hicho yaliyopo Kinondoni, Dar es Salaam, Mwanasheria Mkuu wa Chadema, Tundu Lissu alisema Lijualikali ni mfungwa wa kisiasa na amefungwa kwa sababu ya vita ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Upinzani.

Lissu alisema, wanachokifanya ni kukataa rufaa Mahakama Kuu na kisha kupeleka maombi ya dhamana mahakamani ili mbunge huyo apate dhamana wakati rufaa yake ikisikilizwa.

Aliongeza kuwa taarifa ya kusudio la kukata rufaa imeshapelekwa mahakama ya wilaya ili kuharakishiwa kupewa nakala ya mwenendo wa kesi na hukumu kwa ajili ya kukata rufaa hiyo.

“Sisi kama chama tunaamini kwamba mheshimiwa Lijualikali ni mfungwa wa kisiasa. Kesi iliyofunguliwa dhidi yake ilikuwa ya kisiasa ili kutekeleza malengo ya kisiasa ya CCM dhidi ya Chadema na hata adhabu yake imetolewa kwa sababu za kisiasa,” Lissu.

Alisema wamekuwa wakimuandama mbunge huyo tangu akiwa diwani na kwamba walimshitaki mara mbili wakati wa kampeni za uchaguzi mkuu wa mwaka jana ili wamfunge lakini walishindwa na mbunge huyo alishinda uchaguzi.

Lissu alisema kutokana na kumkosa katika kesi walizomfungulia ndio sababu ya kumfunga miezi sita bila faini, wakiamini kuwa wanaweza kumuondolea ubunge wake aliopewa na wananchi wa Kilombero waliomchagulia.

“Timu ya wanasheria wa chama imeshaanza taratibu za kukata rufaa, kwa kuandaa notisi ya rufaa na maombi ya dhamana ya dharura wakati uamuzi juu ya rufaa yake unasubiriwa. Tunatazamia kukamilisha taratibu hizi hadi kufikia Jumatatu ijayo,” alisema.

Lissu aliongeza kuwa viongozi, wanachama na wafuasi wa Chadema katika jimbo la Kilombero, hawatakiwi kuwa na wasiwasi kwa kuwa adhabu hiyo haina athari zozote kwa hadhi yake kama mbunge.

Alifafanua kuwa Katiba iko wazi kwamba katika kifungu cha 67 (20) (c) kinaeleza kuwa mtu hatakuwa na sifa ya kuwa mbunge “…ikiwa mtu huyo amehukumiwa na Mahakama yoyote katika Jamhuri ya Muungano na kupewa adhabu … ya kufungwa gerezani kwa muda unaozidi miezi sita kwa kukutwa na hatia ya kosa lolote, vyovyote linavyoitwa, linaloambatana na utovu wa uaminifu.”

Adhabu ya kifungo aliyopewa Lijualikali haijazidi miezi sita. Katika hatua nyingine, Lissu alisema kesho akiambatana na Mwenyekiti wa Chama hicho, Freeman Mbowe wataenda kumtembelea Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema ambaye yuko katika Gereza la Kisongo mjini huo.

Alisema baada ya kumtembelea Lema watazungumza na vyombo vya habari kwa ajili ya kupaza sauti ili haki ya mbunge huyo aweze kuachiwa kwa kuwa wanaamini naye ni mfungwa wa kisiasa kama alivyo Lijualikali.

Amuua baba yake, afungia maiti stoo

$
0
0
MKAZI wa Kijiji cha Kebeyo Kata ya Mbogi wilayani hapa, Marwa Nyakogera (28) anatafutwa na Polisi kwa tuhuma za kumuua baba yake mzazi Nyakogera Ramadhan (55) kwa kumpiga na nondo kichwani.

Mtuhumiwa huyo baada ya kuua mzazi wake alimfungia ndani ya stoo ya nyumba aliyokuwa akihifadhi vyuma chakavu.

Diwani wa Mbogi ambaye pia ni Mwenyekiti wa kijiji cha Kebeyo, Ezekel Kebaki na kaka wa marehemu, Werema Chacha, wameeleza hayo kwa nyakati tofauti.

Kebaki amesema tukio hilo lilitokea kijijini Kebeyo jana usiku nyumbani kwa Nyakogera (marehemu) wakati alipokuwa akiingia katika stoo, kukagua vyuma chakavu katika stoo yake anayotunzia vifaa hivyo.

Kebaki alisema Marwa (mtuhumiwa), alikuwa katika stoo hiyo akiwa amepitia kwenye tundu alilotoboa na kukumbana na baba yake huyo mzazi na kuanza kumshambulia kwa nondo kichwani na kufa papo hapo.

Alisema baada ya kitendo hicho, mtuhumiwa alifunga mlango kwa nje na kutoroka.

Kaka wa marehemu, Chacha alisema iligundulika kuwa Nyakogera (marehemu) amekufa baada ya watu kwenda kumuangalia baada ya kutotoka katika stoo hiyo kwa muda mrefu.

Chacha alisema kulikuwa na mgogoro kati ya mdogo wake (marehemu) na mtoto wake.

Inadaiwa kuwa, Novemba mwaka jana kijana huyo alimwibia baba yake Sh 900,000 za mauzo ya asali kutoka mizinga 200 aliyonayo.

Alisema baba yake alimkamata na kumfungulia kesi ambayo ipo mahakamani na kijana huyo alidhaminiwa hivyo alikuwa nje kwa dhamana.

"Kumekuwa na vitisho kwa mzazi wake huyo na kwa sasa baada ya tukio hili la mauaji ya baba, kijana huyo haonekani na anatafutwa kwani alikuwepo kabla ya mauaji, lakini sasa hivi ametoroka haonekani, tunasaidiana na wananchi na Polisi kumsaka" amesema Chacha.

Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Tarime/Rorya, Andrew Satta alithibitisha kutokea kwa tukio hilo.

Alisema Polisi inamsaka mtuhumiwa.

Aliwaomba wananchi washirikiane na Polisi kuhakikisha anatiwa mbaroni.

Alichokizungumza Tundu Lissu Kuhusu Mbunge wa Kilombero Kufungwa Miezi Sita

$
0
0
HATUA ya Mahakama ya Wilaya ya Kilombero, Morogoro kumfunga Peter Lijualikali, Mbunge wa Jimbo la Kilombero miezi sita jela, inatokana na visa vya kisiasa

Ni kauli ya Tundu Lissu, Mwanasheria wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) leo mbele ya waandishi wa habari aliokutana nao kwenye Makao Makuu ya chama hicho, Kinondoni jijini Dar es Salaam.

Lissu ambaye ni Mbunge wa Singida Mashariki amesema kuwa, vita kati ya upinzani na Chama Cha Mapinduzi (CCM) vimesababisha Lijuakali (Chadema) kupata hukumu hiyo ya kisiasa.

Mbele ya waandishi wa habari Lissu amesema kuwa, “hiyo ni hukumu ya kisiasa” na kwamba, Jeshi la Polisi nalo limeingizwa kwenye vita hivyo.

Lissu amesema, chanzo cha hukumu hiyo kinatokana na mgogoro wa uongozi ndani ya Halmashauri ya Kiliombero ambapo Chadema na washirika wake wa vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) walishinda madiwani wengi.

Hivyo, kwa mujibu wa Lissu, Halmashauri ya Kilombero ilipaswa kuongozwa na mwenyekiti anayetoka na Ukawa na awe Chadema.

“Ili hilo lisiwezekane, na ili CCM wachukue Halmashauri ya Wilaya ya Kilombero licha ya kushidwa kwenye udiwani, ilibidi wamfanyie Lijualikali mambo ya ajabu,” amesema Lissu.

Lijualikali (30) amehukumiwa jana kwa kosa la kufanya fujo na kusababisha taharuki. Huku Stephano Mgata (35), Dereva wake ambaye ni mshtakiwa wa pili katika kesi hiyo akifungwa kifungo cha miezi sita nje.

“Kifungo cha Mh. Lijualikali ni adhabu ya kisiasa. Mh Lijualikali ni mfugwa wa kisiasa. Amefugwa kwa sababu ya siasa.

“Adhabu ya kisisa ni vita ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) dhidi ya Chadema na wanatumia Jeshi la Polisi, wanatumia mahakama na kwingineko. Vita hii hii wanawatumia akina Lipumba (Profesa Ibrahim Lipumba,” amesema Lissu na kuongeza;

“Kwingine wamemweka Lema (Godbless Lema, Mbunge wa Arusha Mjini) mahabusu kwa miezi mitatu. Hakuna jinai yoyote. Tuliwashinda kwenye uchaguzi.

“Sasa baada ya uchaguzi walimfungulia Lijualikali kesi ya kupinga matokeo mahakama kuu, tukawapiga chini. Wamefungua rufaa na tunawatandika.”

Mwanasheria huyo amesema kuwa, nchi hii ina wafungwa wa kisiasa na kwamba, pamoja na CCM kudhani kwamba, kumfungulia kesi Lijuakali kutawapa afueni. Wasahau.

“Tuna wafungwa wa kisiasa nchi hii. Wale wanaofikiria kwamba kumfunga Lijualikali CCM itapendwa na wananchi wa kilombelo wasahau hilo.

“Huwezi kuwatesa wananchi, ukatesa viongozi waliowachagua kwa mapenzi yao halafu ukategemea wakupende. Wasahau,” amesema Lissu.

Aidha, Lissu ametoa ufafanuzi kuwa Ibara ya 67 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inamlinda Lijualikali hivyo hawezi kupoteza ubunge wake kutokana na hukumu hiyo.

Amesema Chadema hakijaridhika na hukumu hiyo, hivyo kwa sasa wanaandaa utaratibu wa kisheria ili kukata rufaa kuipinga ambapo hatua hiyo inaweza kuchukua siku mbili kukamilika.

Timothy Lyon, Hakimu Mkazi wa Mahakama hiyo alisema, amemhukumu Lijualikali baada ya kumtia hatiani kwa kosa yeye na dereva wake na kwa kuwa, mbunge huyo alipatikana na hatia katika kesi tatu huko nyuma na kuhukumiwa kulipa faini hivyo alistahili kutumikia adhabu hiyo.

Kesi zilkizotajwa na Lyon zinazomuhusu Lijualikali ni namba 338, namba 220 na namba 340 zote za mwaka 2014.

Katika kesi hiyo, Dotto Ngimbwa, Inspekta wa Polisi aliiambia mahakama kuwa, Lijuakali akiwa mshtakiwa namba moja pamoja na Mgata walitenda kosa hilo Machi Mosi mwaka 2016 eneo la Kibaoni katika ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kialombero na kwamba, walifanya fujo kinyume cha sheria.

Alisema tukio hilo lilitokea Machi Mosi mwaka huo saa 4 asubuhi ambapo washtakiwa walikana mashtaka lakini upande wa mashtaka ukathibitisha bila kuacha shaka kwamba, walitenda kosa.

SBL inalaani Kusambazwa Kwa Video isiyo na Maadili Kwenye Mitandao ya Kijamii

$
0
0
TAARIFA KWA UMMA

Dar es Salaam Januari 12, 2017- Kampuni ya Bia ya Serengeti inapenda kuwataarifu wateja wake na  umma na kwa ujumla kuwa kuna  video isiyo na maadili   inaiyosambazwa katika mtandao ya kijamii ikionesha msanii akiigiza  na kuimba wimbo wenye  mahadhi ya taarabu  mbele ya bango lenye nembo ya bia Serengeti Premiur Lager.

Tunapenda kuweka bayana kuwa onesho la msanii huyo halikuidhinishwa wala kudhaminiwa na SBL Pia  msanii huyo sio sehemu na hajawahi kuwa mmoja wa mawakala wetu wanaotoa huduma za kutangaza bidhaa zetu.


Video hiyo ambayo haizingatii maadili ya sanaa  inatoa picha mbaya  jambo ambalo ni kinyume na sera ya SBL ya kuzingatia maadili mema katika shughuli za kutangaza bidhaa zake. 

Aidha ikumbukwe kwamba SBL imekuwa mstari wa mbele  katika kulinda na  kusimamia maadili katika shughuli zake  za kijamii  ikiwa ni pamoja na kuhamasisha  unywaji wa pombe kistaarabu.

Tunauhakikishia umma na wateja wetu kuwa  SBL inafanya shughuli zake za kijamii kwa kuangalia mambo yenye tija kwa jamii na sio vinginevyo.

Tunapenda kuwashukuru sana wateja wetu na umma kwa ujumla kwa kuendelea kushirikiana nasi.

Imetolewa na 

Mkurungezi wa Mahusiano
Serengeti Breweries Limited.

Tembelea Tovuti Pendwa ya ASILI ZETU inayohusiana na Masuala ya Tiba Asilia Kama Kusafisha Nyota na Kumvuta Mpenzi

$
0
0
Tembelea  tovuti  pendwa  ya ASILI ZETUinayohusiana na masuala ya tiba asilia, kusomewa dua na visomo, kusafisha nyota,  kumvuta mume au mpenzi aliyekuacha, tiba ya magonjwa mbalimbali yaliyoshindikana,  mvuto wa biashara.

Pia tunatoa dawa za uzazi kwa wale kina mama wenye matatizo ya uzazi walio angaika kwa muda mrefu bila kupata mafanikio yoyote, kupandishwa cheo kazini, mali isiyohuzika kama vile kiwanja, shamba, nyumba, gari n,k.

Bonyeza Hapa: https://asilizetu.wordpress.com

Sehemu ya Uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere(JNIA) Yateketea Kwa Moto Usiku wa Kuamkia leo.

$
0
0
Moto mkubwa umezuka kwenye Uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere (JNIA) usiku wa leo na kusababisha taharuki kubwa kwa wasafiri na watumiaji wa uwanja huo, ambapo imelazimu shughuli zote uwanjani hapo kusitishwa kwa muda wakati vikosi vya zimamoto vikiendelea na kazi yao kwenye uwanja huo mkubwa zaidi nchini Tanzania.

Kamanda wa Polisi wa Viwanja vya Ndege, Martin Otieno amesema kuwa wamefanikiwa kuudhibiti moto huo na kwamba uchunguzi wa kina juu ya chanzo cha moto huo na hasara iliyosababisha, unaendelea kufanyika na kwamba tayari shughuli zote za kawaida zinaendelea kama kawaida.

Aidha Meneja wa Uwanja huo ameeleza kuwa kwa sasa shughuli zote za usafirishaji zimeamishiwa Terminal One na zinaendelea kama kawaida huku wakiweka sawa maeneo yalioathirika.

“Kwanza naomba niwatoe hofu Watanzania na wasafiri wote wanaotumia Uwanja wetu, ni kweli moto umezuka kuanzia majira ya saa 6 hadi saa 7 usiku wa kuamkia leo.
“Lakini madhara kidogo yametokea kwenye jengo la kuhifadhia mizigo pekee, hakuna mtu aliyepoteza maisha wala kujeruhiwa kutokana na moto, mashine zote zipo salama na sasa shughuli zote za usafirishaji tumezihamishia kule terminal one (Uwanja wa zamani) zinaendelea kama kawaida”. Amesema Meneja huyo.
“Baada ya kuudhibiti moto huo tumerudi kuangalia chanzo tukakuta, mfumo wa umeme uko sawa, hivyo hatujajua chanzo hasa cha moto huo ila tunajitahidi kufanya utafiti ili tujue.” Aliongeza Meneja na kusema taarifa zaidi, zitatolewa baadaye.

Lowassa Akerwa na Gazeti Lililoandika Uongo Dhidi Yake, Adai ni Mbinu Chafu Zinazofanywa na CCM

$
0
0

Waziri  Mkuu wa zamani na Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema, Edward Lowassa, amesema kasi ya kuimarika kwa umoja na mshikamano miongoni mwa vyama vya upinzani nchini, kunaitia kiwewe CCM kiasi cha kuanzisha mbinu chafu za kisiasa.


Kauli hiyo aliitoa jana mjini Kahama katika Hoteli ya Gaprina ambapo alifikia kabla ya kuanza safari ya kuelekea mkoani Kagera katika ziara ya kuimarisha chama chake.


Alisema kuimarika kwa mshikamano huo chini ya mwavuli wa Vyama Vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi  (Ukawa) ni hatua kubwa katika kuelekea kuing’oa CCM.


“Wameanza mbinu zao za kutaka kutuondoa katika umoja wetu, wameanza kuwalisha viongozi wetu maneno, mfano  gazeti (nalitaja jina) la leo (jana) wamenilisha maneno ya kwamba eti nimeitabiria CCM ushindi katika uchaguzi mdogo wa udiwani kule Arumeru.


“… mambo ya ajabu kabisa hili  gazeti linaishi kwa kodi zetu sisi wananchi leo linaamua kutumika kuvunja demokrasia inasikitisha sana.


“Wanaandika uongo mchana kweupe kuwa nilikuwa katika kampeni kwenye kitongoji Ematasia..mimi sikwenda huko..lakini mbinu zao hizi wananchi wameshazijua na hawako tayari kuona hamu yao ya kupata mabadiliko inapotea,” alisisitiza.


Wakati huo huo mamia ya wakaazi wa mji wa Kahama waliizingira Hoteli ya Gaprina alikofikia Lowassa, wakiwa na nia ya kutaka kumwona.


Akiwa njiani kuelekea Bukoba, Lowassa na msafara wake alipata nafasi ya kusalimiana na wananchi katika mnada wa Lusaunga wilayani Biharamlo, ambako wananchi hao walimwambia kuwa hali yao ya maisha ni ngumu pamoja na hali mbaya ya ukame inayowakabili.


Hata hivyo Lowassa hakutoa kauli yoyote kwao zaidi ya kusema kwa sasa mikutano ya hadhara imepigwa marufuku na asingependa kuvuja sheria kwa kile alichodai amri kandamizi.

Rais Shein Atangaza Kupandisha Kima cha Chini cha Mshahara Mwaka huu (2017).

$
0
0


Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Ali Mohamed Shein ametangaza neema mpya kwa wafanyakazi visiwani humo baada ya kuwakikishia kupandisha kima cha chini cha mshahara kuanzia mwaka huu (2017).

Dkt. Shein ametoa hakikisho hilo jana wakati akiwaongoza watanzania kuadhimisha Miaka 53 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar katika sherehe zilizofanyika katika uwanja wa Amani visiwani humo.

Alisema kuanzia mwaka huu kima cha chini cha mshahara kitaongezeka kutoka Tsh. 150,000 hadi Tsh. 300,000 ikiwa ni ongezeko la asilimia 100.

Dkt. Shein alitoa tathmini yake ya mwaka mmoja tangu achanguliwe tena kuiongoza Zanzibar, ambapo alisema mwaka 2016 umekuwa ni wa mafanikio makubwa katika nyanja mbalimbali ikiwemo elimu, kilimo, viwanda, huduma za jamii ikiwemo afya na huduma za maji, miundombinu n.k.

Akihutubia kwenye uwanja wa Amani Dkt. Shein alisema, serikali yake itaendelea kudumisha na kuenzi umoja na mshikamano ambao uliasisiwa na viongozi wa mapinduzi hayo.

Alisema, mafanikio yaliyopatikana ni pamoja na kukuza pato la taifa hadi kufikia 6.6% licha ya kuongezeka kwa mfumuko wa bei kutoka 5.7% katika mwaka 2015 hadi kufikia 6.7% mwaka 2016.

Pia Dkt. Shein alieleza utekelezaji wa sera ya kulipa pensheni kwa wazee, ambapo amesema hadi mwezi Desemba mwaka 2016, jumla ya shilingi bilioni 4.3 zimetumika kuwalipa wazee 25,259 waliosajiliwa kiasi cha shilingi 20,000 kila mwezi, zoezi ambalo litaendelea kutekelezwa.

Katika hatua nyingine, Dkt Shein alitangaza rasmi kuwa matangazo yote ya TV yatahama kutoka mfumo wa 'Analogue' na kuhamia mfumo wa 'kidigitali' kuanzia mwezi April mwaka huu.


Moto Wazuka na kuteketeza Sehemu ya Uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere(JNIA) Usiku wa Kuamkia Leo!

$
0
0

Moto mkubwa umezuka kwenye Uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere (JNIA) usiku wa leo na kusababisha taharuki kubwa kwa wasafiri na watumiaji wa uwanja huo, ambapo imelazimu shughuli zote uwanjani hapo kusitishwa kwa muda wakati vikosi vya zimamoto vikiendelea na kazi yao kwenye uwanja huo mkubwa zaidi nchini Tanzania.

Kamanda wa Polisi wa Viwanja vya Ndege, Martin Otieno amesema kuwa wamefanikiwa kuudhibiti moto huo na kwamba uchunguzi wa kina juu ya chanzo cha moto huo na hasara iliyosababisha, unaendelea kufanyika na kwamba tayari shughuli zote za kawaida zinaendelea kama kawaida.

Aidha Meneja wa Uwanja huo ameeleza kuwa kwa sasa shughuli zote za usafirishaji zimeamishiwa Terminal One na zinaendelea kama kawaida huku wakiweka sawa maeneo yalioathirika.

“Kwanza naomba niwatoe hofu Watanzania na wasafiri wote wanaotumia Uwanja wetu, ni kweli moto umezuka kuanzia majira ya saa 6 hadi saa 7 usiku wa kuamkia leo.

“Lakini madhara kidogo yametokea kwenye jengo la kuhifadhia mizigo pekee, hakuna mtu aliyepoteza maisha wala kujeruhiwa kutokana na moto, mashine zote zipo salama na sasa shughuli zote za usafirishaji tumezihamishia kule terminal one (Uwanja wa zamani) zinaendelea kama kawaida”. Amesema Meneja huyo.

“Baada ya kuudhibiti moto huo tumerudi kuangalia chanzo tukakuta, mfumo wa umeme uko sawa, hivyo hatujajua chanzo hasa cha moto huo ila tunajitahidi kufanya utafiti ili tujue.” Aliongeza Meneja na kusema taarifa zaidi, zitatolewa baadaye.




 Chanzo: GPL

Ahukumiwa Kwenda Jela kwa Shtaka la Kuvua Condom Mapenzini!!

$
0
0

Mwanaume mmoja ambaye ametajwa kuwa ni raia wa Ufaransa kwenye taifa la Switzerland amehukumiwa kwenda jela miezi 12 baada ya mpenzi wake kumshtaki kutokana na kuivua kinga ‘Condom’ wakiwa mapenzini.

Mwanamke alisimulia kuwa walianza kufanya tendo la ndoa wakiwa na kinga na walipomaliza mwanamke aligundua kinga imevuliwa kinyume na matakwa yake hivyo alitoa taarifa hiyo polisi, Mwanaume huyo alikamatwa na baadae kufikishwa mahakamani na akashtakiwa kwa ubakaji.

Akiwa mahakamani mwanaume huyo alidai kuwa lengo lake lilikuwa ni kuvaa kinga lakini ilipasuka. Mwanamke alisisitiza kuwa angejua jamaa hatumii kinga asingekubali kufanya tendo hilo, Mwanaume huyo amefungwa jela miezi 12 lakini ameonyesha nia ya kukata rufaa..


Medali ya Rais Obama Yamtoa Machozi Biden

$
0
0
Rais wa Marekani Barack Obama amemtunuku makamu wake Joe Biden Medali ya Rais ya Uhuru, ambayo ndiyo nishani ya hadhi ya juu zaidi anayoweza kupewa raia nchini Marekani huku Biden, akionekana kushangazwa na hatua hiyo hali iliyosababishwa atokwe na machozi alipokuwa anatunukiwa medali hiyo.

Obama alimsifu Biden na kumwambia maneno haya, “Imani yako katika Wamarekani wenzako, kwa upendo wako kwa taifa na kwa utumishi maisha yako yote.”

Tuzo hiyo imetolewa kwa Bw Biden wakati wawili hao wanapojiandaa kuondoka madarakani Donald Trump wa Republican atakapoapishwa kuwa rais mpya tarehe 20 Januari. Bw Biden amesema anapanga kuendelea kushiriki siasa katika chama cha Democratic.

Joe Biden, aliyeonekana kutekwa sana na hisia, alisimama na kuonekana kushangaa Bw Obama alipomlimbikizia sifa na kumtaja kuwa “Chaguo bora zaidi, si kwangu tu, bali kwa Wamarekani”.

Medali hiyo ilikuwa na hadhi ya ziada, kwa mujibu wa gazeti la New York Times ambapo hadhi hiyo ya ziada, katika serikali za Marekani zilizotangulia, ilitunukiwa watu wachache sana, akiwemo Papa John Paul II.

Bw Obama alifanya mzaha kwamba mtandao sasa utakuwa na fursa ya mwisho ya kucheka na kufanyia mzaha kile ambacho kimekuwa kikiitwa “bromance”, maana yake upendo na urafiki wa dhati kati ya Obama na Biden.

Wafaransa watatu wasaini mikataba mipya Arsenal

$
0
0
Wachezaji wa Arsenal wakati wa kusaini mikataba mipya

Wachezaji wa klabu ya Arsenal, Olivier Giroud, Laurent Koscielny na Francois Coquelin hatimaye wamekubali kuongeza mikataba yao mipya na klabu hiyo ya ligi kuu ya soka nchini Uingereza.

Wachezaji hao wa Kifaransa, beki Koscielny na Giroud wamesaini mikataba hadi 2020, huku mchezaji Coquelin yeye amesaini hadi 2021.

Wafaransa hao wote watatu wamekuwa wachezaji muhimu kwa Arsenal kwa sasa, ambapo Giroud amekuwa gumzo kwa kufunga mabao manne katika michezo minne iliyopita, kujumuisha na bao la kiufundi ‘Scorpion Goal’ alilofunga hivi karibuni kwenye mchezo dhidi ya Crystal Palace.
Viewing all 104709 articles
Browse latest View live


Latest Images