Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104432 articles
Browse latest View live

Maandalizi ya Kushinda Uchaguzi: Kenyatta Amezindua Magari 525 ya Polisi ya Kulinda Doria...!!!

0
0
RAIS Uhuru Kenyatta amezindua sehemu ya tatu ya mahari ya polisi na vifaa vilivyopatikana kupitia mpango wa kukodi wa serikali. 


Kenyatta amezindya magari 525, yakiwemo 25 maalumu kwa ajili ya kujilinda na mabomu ya kutegwa ardhini ama Mine-Resistant Ambush Protected (MRAP), huko Uhuru Park Nairobi, kama sehemu ya mpango wa serikali kulifanya jeshi la polisi la nchi hiyo kuwa la kisasa. 

Katika hotuba yake, rais huyo wa Kenya alirudia dhamira ya serikali yake katika kuimarisha mazingira ya kazi ya polisi na maafisa wengine wa usalama. 

Baadhi ya magari yalikopwa kutoka kampuni ya General Motors East Africa, ambayo itahusika katika kuyahudumia magari hayo.

Magari mengine 500 yanategemewa kuwasaidia polisi katika kazi zao za kila siku katika kaunti, na mijini.
Jumla ya magari 2,220 yalizinduliwa wakati wa awamu ya kwanza nay a pili ya mpango huo. 

Hatua hii ina lengo la kuimarisha doria ya polisi kwa kuwapa magari, pamoja na njia nyingine za usafiri.

Ni Maajabu na Kizaazaa Mbeya:Mtoto Aliyezikwa Jana Akutwa Akiwa Amelala Chumbani Kwake,Tazama Video Hapa..!!

0
0

Wakazi wa eneo la Isanga katika jiji la Mbeya wameendelea kushuhudia visa na mikasa, ushilawadu na matukio ya vioja, baada ya mtoto wa miaka 9 aliyekuwa amezikwa jana kwenye makaburi ya Isanga kukutwa akiwa kitandani kwake amelala usingizi mara baada ya kurejea kutoka makaburini.


Mara baada ya kufika nyumbani familia ikiwa inaingia ndani mwao, walipigwa na butwaa baada ya kukuta mtoto wao amelala kitandani kwake, na baada ya kuitana na kumwamsha mtoto huyo aliamka na kuonekana akishangaa hali aliyoiona pale nyumbani.


Kwa pamoja wananchi na wanafamilia walikubaliana asubuhi hii kwenda kufukua kaburi hilo ili waone nini kilichozikwa, na hivi dakika hizi zoezi hilo linaendelea na picha za makabuni hapo .

UPDATES KUTOKA ENEO LA TUKIO

KABURI LIMEFUKULIWA, HAKUNA KILICHOKUTWA NDANI YA KABURI YAANI MAITI ILIYOZIKWA JANA HAIMO!! POLISI WAMELAZIMIKA KUPIGA MABOMU ILI KUTAWANYA WATU PALE MAKABURINI BAADA YA KUANZA HALI YA SINTOFAHAMU JUU YA NINI KIMETOKEA?

Kutoka katika kipindi cha Leo Tena cha Clouds FM wamemuhoji Kamanda wa Polisi wa Jiji la Mbeya ambaye amatoa maelezo kuwa, ushahidi wa kimazingira unaonyesha kuwa mwili wa mtoto huyo ulisahaulika kuwekwa katika sanduku na baada ya ibada mwili haukuagwa (Familia iliomba hivyo na ni kawaida).
Baada ya kuzika waliporudi nyumbani ndipo waliukuta mwili wa mtoto huyo ukiwa umelala kitandani. Jeshi la Polisi liliimarisha ulinzi katika maeneo hayo ya msiba.

Mmoja ya watangazaji wa Leo Tena amesema kuwa amewasiliana na mmoja ya wadau wake huko Mbeya na amemthibitishia kuwa kaburi limefukuliwa na jeneza limekutwa likiwa tupu halina kitu.

Inavyoonekana kuna uzembe katika kuandaa mwili na kuuweka katika jeneza, ingawa pia majirani na watu wanaoishi mazingira hayo wanahusisha na imani za kishirikina.

Kama Ulikuwa Hujui:Huu Ndio Mkataba Mpya aliosaini Diamond na Kampuni Kubwa ya Huko Afrika Kusini,Huu Ndio Mkwanja Atakaolamba..!!!

0
0
diamond-m1UMEISIKIA HII? Mwanamuziki mwenye taito kubwa kwa sasa, mtoto wa Tandale, Mkurugenzi wa Kampuniya WCB, Nassib Abdul ‘Diamond Platnumz’ na mzazi mwenzake, Zarina Hassani ‘Zari’ wamelamba shavu kubwa baada ya kuvuta mkata wakupiga picha za kupendezesha jarida maarufu la Afrika Kusini, Papas And Mamas.



Mara baada ya picha hizo kusambazwa, zimekuwa gumzo kila kona kitu kinachowafanya watu wengi kulisubiria
mamas mitaani ambapo litaanza kutoka mwezi ujao (Februari). Kuhusu mkwanja waliolipwa mpaka kupiga picha hizo bado hauja wekwa wazi ila mtu wa karibu na Diamond alisema jamaa amevuta mkwanja mnono.

Ebwana Ehe!!,Unakumbuka Ile Issue ya Madee Kupora Simu Uswazi,Basi Kumbe Hiki Ndio Chanzo cha Yote ..!!

0
0
madee1
DAR ES SALAAM: Zikiwa zimepita siku chache tangu msanii wa bongo Fleva na staa wa wimbo ya Pombe, Hamad Ally ‘Madee’ kudaiwa kumpora simu mama mmoja aliyefahamika kwa jina la Mama Makavaka maeneo ya uwanja wa ndege Julius Nyerere Dar es Salaam.


  Katika mitandao ya kijamii mapema leo zimesambaa picha zikionesha wimbo mpya wa Madee uitwao ‘Hela’. Wadau na mashabiki wa Bongo Fleva wamehusisha ‘skendo’ ya Madee kupora simu na ujio wa wimbo wake mpya ambao utasikika leo katika vituo mbalimbali vya redio. Skendo hiyo imeonekana kama ni kutafuta ‘Tention’ ili aweze kutoa kibao chake kipya.
madee4
Wimbo huo umeandaliwa katika studio za ‘Mj Record’  kwa ushirikiano wa waandaaji wawili ambao ni Marco Chali na Daxo Chali.

Miujiza ya Shekh Sharifu Rashid Kutoka Bagamoyo..Anarudisha Mausiano ya Mapenzi na Kusafisha Nyota

0
0

MIUJIZA YA SHEKH SHARIFU RASHID KUTOKA BAGAMOYO PWANI, (RUDISHA MAHUSIANO YAKO NDANI YA MASAA 48 TU) ASANTE KWA KUENDELEA KUMPIGIA SIMU SHEKH SHARIFU RASHID KWA WALE WENYE MATATIZO NA WALE WANAOTOA SHUKRANI:

SHEKH SHARIFU RASHIDI ni mtaalamu wa tiba mbalimbali za asili, anatumia kitabu cha quran, dawa za asili, dawa za kiarabu na majini, anazo dawa za mapenzi, nguvu za kiume, chango, ngiri maji na n.k, anakuvutia mpenzi alie kuacha au alie mbali, pia anatoa pete za bahati zilizoambatanishwa na jini mali kulingana na nyota yako, anaouwezo mkubwa wa kutumia jina la muhusika kwa kutatua tatizo lako, anaouwezo wa kumrudisha mtu aliepotea kimiujiza, pia anatibu kwa njia ya simu popote ulipo,

WASILIANA NAE KWA SIMU NA WHATSAPP NO: 0718-668347. 0685-224047, 0767-204308 na 0627-251404 au follow@shekh_sharifu_rashid, Email:shekhsharifurashid@gmail.com

Duh: Tazama Picha Za Gari la Kubeba Kinyesi Likimwaga Maji Machafu Barabarani Maeneo ya Ubungo Leo Asubuhi

0
0
ubungo-mavi-7
DAR ES SALAAM: Mapema leo asubuhi, lori la maji taka limechafua hali ya hewa kwenye Barabara ya Morogoro baada ya kumwaga ‘mzigo’ (maji yenye kinyesi) katikati ya barabara hiyo maeneo ya Ubungo Mataa na kusababisha taharuki na harufu kali.



ubungo-mavi-1
Kwa mujibu wa mshuhuda wa tukio hilo, inasemekana kuwa lori hilo lilikuwa likitokea maeneo ya Rombo Kimara ambapo baada ya kufika Ubungo kwenye mataa ya foleni, mfuniko wa tanki uliftyatuka ndipo likaanza kumwaga uchafu huo barabarani. ubungo-mavi-3
Baada ya kuona hali hiyo, dereva wa lori hilo alitoka mbio na kwenda kuziba eneo ambapo uchafu huo ulikuwa ukitoka.ubungo-mavi-4
Hata hivyo watumiaji wa barabara hiyo na wafanyabiashara wa eneo hilo hasa wamachinga wameshangazwa tukio hilo huku wakieleza kuwa ilitakiwa dereva na kondakta wa gari hilo wahakikishe mfuniko wa tanki umekaza kabla ya kuanza safari ili kuzuia ajali kama hizo ambazo zinaweza kuepukika kwa kuzingatia umakini wa kazi.ubungo-mavi-5
Aidha wananchi hao wameitaka Manispaa ya Jiji la Dar  es Salaam imchukulie hatua zinazostahili mmiliki wa gari hilo na dereva wake ikiwa ni pamoja na kumtoza faini au kusafisha barabara kutokana na adha aliyoisababisha ili liwe funzo kwa wamiliki na madereva wengine wa magari ya maji taka.

Mwana FA Afungukia Bifu Lake na Lady Jay Dee.....

0
0
Mwanamuziki Hamis Mwinjuma maarufu Mwana FA au Binamu akifanya mahojiano siku za karibuni jijini Dar es Salaam amezungumzia tofauti kati yake na mwanamuziki mwenzake Judith Wambura maarufu Lady JayDee.

Mwana FA alisema kuwa yeye hana tatizo lolote na Lady JayDee na wala wawili hao hawajawahi kukutana kisha mmoja akamwambia mwenzake kuwa anatatizo na mwingine.

“Kila mtu anafanya shughuli zake na mimi sijawahi kumwambia chochote sababu sina tatizo na yeye, kwa hiyo sioni kama kuna haja ya kupatanishwa sababu naona kila mtu anafanya shughuli zake” alisema Mwana FA.

Mwana FA alisema kuwa kwa sasa yeye na mwanamuziki huyo hawapo karibu kama walivyokuwa kipindi cha nyuma lakini anaamini hakuna tatizo ni kila mtu tu ameamua kufanya kazi zake kivyake.

Duh!! Umesikia Alichosema Niyonzima Juu ya Kocha Wake Lwandamina,Soma Hapa Kujua kama Yuko Sahii Kusema Haya Au Amerocharocha

0
0
 
Nahodha wa Yanga, Haruna Niyonzima, amesema kuwa anaamini kocha wao George Lwandamina atakipeleka mbali zaidi kikosi hicho kwenye michuano ya kimataifa na kutwaa ubingwa wa ligi kutokana na ubora wake na kudai kuwa kinachotakiwa apewe muda na si watu kuanza kumlalamikia kwa matokeo yoyote yatakayopatikana.

Kumekuwa na tuhuma kuwa Lwandamina amekuwa akiwapa mazoezi magumu wachezaji wake hadi siku ya mechi, hivyo kusababisha wachezaji hao kuchoka na kushindwa kufanya vyema kwenye mechi.

Niyonzima amesema kuwa, siyo wakati muafaka kwa sasa kutoa lawama kwa kocha huyo kwa kuwa bado hajakaa na timu kwa muda mrefu, hivyo anahitaji kuyasoma mazingira kisha ndipo aweze kufanya vyema.
 
“Lwandamina ni mwalimu mzuri na tunamuelewa sana tofauti na watu wanavyodhania, pia watu wanahitaji kutambua kuwa, kocha huyo anatakiwa apewe muda wa kutosha kuweza kuinoa timu hiyo na hasa ukizingatia yeye ni mgeni, hivyo hawezi kukopi kila kitu kwa wakati mmoja.

“Anatakiwa kupewa muda wa kuweza kuelewa kila kitu ndipo aweze kufanya kazi yake ipasavyo na si tuhuma ambazo amekuwa akipewa kwani naamini atatufikisha mbali zaidi kwenye ligi na mashindano ya kimataifa,” alisema Niyonzima.


Aidha, alimalizia kwa kusema kuwa, anaamini wataweza kufanikiwa kutetea ubingwa wa ligi kwa kuwa wamejiandaa vyema, licha ya kutambua kuwa mzunguko wa pili ni mgumu na wanahitaji kujipanga na kujituma ili waweze kufanikiwa kutetea taji lao hilo.

Inasikitisha Sana: Mwanamke Ajinyonga kwa Mtandio,Kisa Kizima Hiki Hapa Livee..!!!

0
0

Mwanamke mmoja aliyejulikana kwa jina la Anastazia Francis miaka 48 amekutwa akiwa amejinyonga hadi kufa katika mtaa Nyasaka wilaya ya Ilemela jijini Mwanza. 


Taarifa ya jeshi la Polisi mkoa wa Mwanza imesema kuwa mnamo tarehe 16.01.2016 majira ya saa 11:00 asubuhi, mwanamke huyo alikutwa akiwa amejinyonga hadi kufa ndani ya chumba chake kwa kutumia mtandio ambao alikuwa ameuning’iniza kwenye dirisha juu.

Inadaiwa kuwa mwanamke huyo baada ya mumewe kuondoka alimtuma mwanae mkubwa aliyemaliza kidato cha nne aende dukani na mwingine mdogo mwenye umri wa miaka 06 aende kufagia na ndipo alipopata mwanya wa kwenda kujinyonga hadi kufa.

Tukio hilo lilijulikana baada ya mtoto wake mdogo kurudi ndani chumbani kuchukua shati na kumkuta mama yake akiwa amejining’inizi ndipo aliita watu ili waje kumsaidia.

Taarifa hiyo ya jeshi la polisi imesema kuwa upelelezi unaendelea ili kufahamu chanzo cha tukio hilo.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza DCP Ahmed Msangi amewaasa wananchi pindi wanapopata matatizo waombe ushauri kwa watu wengine ili kuweza kuepusha maamuzi ambayo ni hatari katika maisha yao.

Polepole Amtaja Anayeifitinisha Serikali

0
0

Katibu wa Itikadi na Uenezi, Humphrey Polepole amefunguka na kusema kuwa wanasiasa wa vyama vingine ambavyo siyo CCM wamekuwa na jihudi kubwa ya kuwachonganisha wananchi na kuwafitinisha na serikali.

Humphrey Polepole amesema hayo leo na kutoa wito kwa wananchi na kuwataka wawapuuze wanasiasa wanaotumia matatizo na majanga kuwa mtaji wao kisiasa kwani serikali ipo kwa ajili ya kuwahudumia.


"Wanasiasa wa vyama ambavyo si CCM wamekuwa na juhudi kubwa kufanya uchonganishi na kuifitinisha serikali na wananchi, tunatoa wito kwa wananchi kuwapuuza wanasiasa wanaotumia matatizo na majanga kuwa mtaji wao kisiasa, Serikali ipo ili kuwahudumia. Siasa yetu ni ya Ujamaa na Kujitegemea, tutaendelea kuhimiza Watanzania kujitegemea na kuongeza juhudi katika kazi" alisema Humphrey Polepole


Aidha amesema mageuzi makubwa yanayoendelea ndani ya CCM yanalenga kukiimairisha Chama kuisimamia Serikali na kushughulikia matatizo ya watu

Vijana wafariki Wakipiga 'Selfie' Mbele ya Treni Delhi

0
0

Mkasa huo uliangaziwa katika vyombo vya habari vya eneo hilo

Vijana wawili wamefariki walipokuwa wanajipiga picha katika barabara ya reli katika mji mkuu wa India Delhi.

Kundi la vijana lilikwenda katika kituo cha reli kupiga selfie mbele ya treni zilizokuwa zinawadia.

Lakini wawili walichelewa kuondoka katika reli hiyo na treni ikawakanyaga, polisi imesema.

Utafiti mwaka uliopita umeonyesha kuwa kumeshuhudiwa vifo vingi vinavyohusisha watu kupiga Selfi India kuliko nchi nyingine yoyote.

Wasomi kutoka chuo kikuu cha Carnegie Mellon na taasisi ya mawasiliano ya Indraprastha mjini Delhi wanasema kuwa kati ya vifo 127 vinavyotokana na watu kupoiga Selfie kati ya mwaka 2014 - 2015, visa 76 vimeripotiwa India.

Tukio la hivi karibuni limejulikana baada ya vyombo vya habari katika eneo hilo kutoa taarifa Jumanne.

"Wakati wa kupiga picha, waliiona treni ikija wakasongea kando. Lakini treni nyingine ilitokezea upande wa pili na walikwama katikati. Waligongwa na mojawapo ya treni hizo," Indian Express ilimnukuu afisa wa polisi.

Afisa mmoja wa polisi wa reli ameongeza kuwa vijana hao walimkodisha mpigaji picha mtaalamu kwa kazi hiyo.

"Tumeipata kamera kutoka kwa vijana iliotumika. Mlikuwa na picha na video, Video inakaguliwa, wakati picha hizo zinathibitisha kuwa walikuwa wanaruka kutoka reli moja hadi nyengine," Naibu kamishna wa polisi Parwaiz Ahmed ameiambia Hindustan Times.

Mwaka jana wanafunzi wawili walizama walipokuwa wanapiga selfi katika mto uliofurika katika eneo la jimbo la kaskazini la Uttar Pradesh.

Na polisi mjini Mumbai imetaja maeneo 15 ambapo 'ni hatari' kupiga Selfie baada ya msichana wa miaka 18 kuzama baharini wakati akijipiga selfie.

Tundu Lissu :Mamlaka Zinazotakiwa Kusema Kuna Njaa Zinamuogopa Rais Magufuli

0
0

Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu amesema mamlaka zinazotakiwa kusema kuna njaa zinamuogopa Rais Magufuli kwa sababu ameshatangaza msimamo wake hadharani hakuna njaa.

Amedai Rais Magufuli anaamini kazi ya vyombo vya habari ni kuandika yanayompendeza pekee.

Kwa Mara ya Kwanza Leo, CCM Wakiri Hali Mbaya ya Njaa Huku Wakirusha Dongo Kwa Vyama Vya Upinzani..!!

0
0
 
Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimewasihi viongozi wa vyama vya wapinzani kujikita katika siasa safi na uongozi bora, kwa kuachana na matamko ya uongo yanayosababisha taharuki katika nchi na kuchonganisha wananchi na serikali yao, kwa kuwa vitendo hivyo havina manufaa kwa mustakabali wa maendeleo ya taifa.
 
Hayo yamesemwa na Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi, Huphrey Polepole, wakati akizungumza na waandishi wa habari, leo Januari 17, 2017, katika Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba Jijini Dar es Salaam, kutoa ufafanuzi kuhusu masuala mbalimbali ya Kichama.
 
Polepole amsema, wapinzania wamekuwa wakitumia matatizo ya wananchi na kutoa matamko ya uongo ili kutia nchi katika taharuki kwa lengo la kujitafufia umaarufu wa siasa vitendo ambavyo alisema, havisaidii wananchi wala wanasiasa  wa vyama hivyo katika kuleta maendeleo ya nchi.
 
Alisema, mbali na matamko ya viongozi wa vyama hivyo kutosaidia, katika ujenzi wa maendeleo yamaendeleo ya nchijambo ambalo alisema za kueneza maneno ya yasiyofanyiwa utafiti kwa lengo la kusababisha taharuki kwa wananchi, jambo ambalo alisema, si miongoni mwa siasa safi wala uongozi bora.
 
Polepole alisema, wapinzani wamekuwa wakifanya siasa za aina hiyo wakiwa wanajua ubaya wake, kwa kuwa wao lengo lao ni kujaribu kuchonganisha wananchi na serikali hata pale ambapo serikali inaonyesha juhudi za dhali za kuijenga Nchi yenye uchumi imara wa viwanda.
 
“Nawaonba Watanzania tuwapuuze wanasiasa wa vyama hivi,  tuendelee kuiunga mkono serikali, ili itimize mipango na malengo iliyoweka, ikiwemo kuhakikisha Tanzania inakuwa kiuchumi kwa kuwa nchi ya viwanda, hali ambayo itasaidia sana kutukwamua Watanzania kutoka katika umasikini”, alisema Polepole.
 
Polepole alitaja kuwa miongozi mwa mambo ambayo katika kipindi hiki wanayatumia kupotosha ili kujaribu kuletea taharuki wananchi ni pamoja na kueneza propaganda kuwa Tanzania imekumbwa na baa la njaa na pia kutumia matatizo waliyopata wananchi wakati wa janga la tetemeko la ardhi lililotokea Bukoba mkoani Kagera kama mtaji wao kisiasa.
 
“Kwanza mjue, kutungaza taarifa ambazo zitaleta taharuki katika jamii ni kosa la jinai, lakini pia inajulikana na wenyewe wanajua, kwamba Duniani kote zipo taratibu ya utangazaji wa majanga katika nchi yoyote. Baa la njaa ni janga kubwa linapofikia kiwango kibaya, mwenye mamlaka ya kutangaza ni Mkuu wa nchi”, alisema Polepole na kuongeza;
 
Alisema, Tanzania haijawahi kupata  njaa yenye kiwango cha kuitwa baa la njaa, katika kipindi cha miaka 30 iliyopita, hivyo wanaojaribu kutangaza kuwa Nchi ipo katika baa la njaa ni kushindwa kufanya siasa safi na kukosa uongozi bora kama ilivyo CCM ambayo mambo hayo inayo.
 
“Ingawa tumekuwa na tatizo la njaa katika sehemu chache za na kuwepo upungufu wa mvua katika maeneo kadhaa ya nchi hali ambayo inaweza kusababisha upungufu wa chakula katika maeneo husika, bado hili siyo baa la njaa. Na kwa kuwa hili serikali inalijua inaendelea kuweka mazingira mazuri ili kuweza kupelekwa vyakula maeneo yote kuondoa uhaba, na kipindi hiki hatujafikia huko”, alisema Polepole.
 
“Baada ya kuona hali ipo hivi nilitarajia viongozi wote bila kujali vyama , tuhimize wananchi kutumia chakula vizuri wasikitumie katika mambo ya anasa au kukiuza hovyo, lakini wao wanakimbilia kutangaza baa la njaa wakati njaa yenyewe haijatokea, hawa watu wa ajabu sana’, alisema Polepole.
 
Alisema, kila kiongozi anayeongozwa na misingi ya uongozi bora na mzalendo kwa nchi yake, analo jukumu la kuwahamasisha wananchi kutunza vyakula walivyonavyo.
 
Kuhusu tetemeko lilitokea Bukoba  na kusababisha uharibifu na vyumba za watu na miundombinu mbalimbali alisema kama ilivyo ulimwenguni kote, inapotokea mambo haya ya majanga serikali hujenga uwezo wake kwanza ili kusaidia wananchi wake.
 
“Baada ya tetemeko lile, Serikali ilichofanya ni kujengea uwezo wa wananchi wasiwe mbali na huduma  ndiyo maana ikaimarisha miundombinu ya elimu, afya na barabara, kwa sababu watu waendelee kupata huduma”. alimalizia Polepole

Kudadeki: Yanga ya Lwandamina Yavunja Mwiko wa Miaka 30 Kwa Staili Hii Mpya..!!!

0
0

Goli la mshambuliaji Deus Kaseke limeivunja Yanga kuvunja mwiko wa miaka 30 zaidi  katika uwanja wa Majimaji mkoani Ruvuma na kuondoka na alama tatu muhimu mchezo wa Ligi kuu Vodacom Tanzania bara dhidi ya wenyeji Majimaji.


Dakika ya 14 Kaseke alifunga goli baada ya mlinda mlango wa Majimaji kuutema Mpira uliokuwa umepigwa na Nahodha wa Yanga Haruna Niyonzima na kumkuta mfungaji akiwa katika hali nzuri na kuweza kutikisa nyavu za wenyeji.

Simon Msuva na Amis Tambwe wangeweza kufunga magoli mengi zaidi kutokana na kukosa nafasi nyingi za wazi hadi Mapumziko Yanga walienda wakiwa kifua mbele kwa goli hilo moja.

Kipindi cha pili kilikuwa kigumu kwa kila timu na kupelekea kufanya mabadiliko mbalimbali huku Yanga wakicheza kwa kushambulia na kukaba zaidi kutokana na Mpira kukosa radha kutokana na ubovu wa uwanja huo.

Mpaka dakika 90 Mwamuzi Hussein Athumani anapuliza kipyenga cha mwisho Yanga wameibuka na pointi tatu muhimu na kuweza kumsongelea mtani wake Simba ambaye anaongoza Ligi Kuu.

Kwa Matokeo hayo Yameifanya Majimaji kuwa katika Mstari wa kushuka daraja hivyo wanatakiwa kubadilika kwa mechi ambazo zimebaki wakati Yanga wamefikisha pointi 43 nyuma ya moja dhidi ya Simba wenye 44.

Ligi Kuu ya Tanzania inatarajia kuendelea tena kesho kwa michezo miwili kucheza katika viwanja mbalimbali macho ya wengi yatakuwa mkoani Morogoro Mtibwa Sugar watawakaribisha Vinara wa Ligi timu ya Simba wakati Mabingwa wa Kombe la Mapinduzi Azam FC watacheza na Mbeya City majira ya saa moja usiku kwenye uwanja wa Azam Complex Chamazi nje kidogo ya jiji la Dar es salaam.

Kikosi cha Yanga ; Deogratius Munish ‘Dida’, Juma Abdul, Haji Mwinyi, Andrew Vincent, Kelvin Yondani, Thaban Kamusoko, Simon Msuva, Haruna Niyonzima/Oscar Joshua dk90, Amissi Tambwe, Juma Mahadhi na Deus Kaseke/Said Juma ‘Makapu dk’80.

Maji Maji; Agathon Anthony, Salehe Mohammed, Mpoki Mwakinyuke, Keneddy Kipepe, Bahati Yussuf/Emmanuel Semwanza dk25, Yakoub Kibiga/Paul Nyangwe dk58, Iddi kipwagile, Kelvin Kongwa, George Mpole, Hassan Hamisi na Lucas Kikoti/Peter Mapunda dk46.

TRA Wazidi kukusanya Matrilion ya Kodi,Wakusanya Trilioni 7.27 Kwa miezi Sita Iliyopita..!!!

0
0

Katika kipindi cha miezi sita ya mwaka wa Fedha 2016/17 yaani kuanzia Julai hadi Disemba 2016, Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imekusanya kodi jumla ya shilingi trilioni 7.27 ikilinganishwa na shilingi trilioni 6.44 ambazo zilikusanywa kipindi kama hicho mwaka wa fedha  2015/16.

 
Ukusanyaji wa mapato katika kipindi cha nusu mwaka wa fedha 2016/17 umeongezeka kwa asilimia 12.74.

Mlinganisho wa makusanyo ya mapato kwa mwaka wa fedha 2015/16 na 2016/17 ni kama ifuatavyo:
MWEZIMWAKA 2015/16MWAKA 2016/17Ongezeko
JULAI925,384.71,069,458.515.57
AGOSTI923,316.91,154.222.525.01
SEPTEMBA1,132,310.31,378,048.921.70
OKTOBA1,037,179.81,131,094.99.05
NOVEMBA1,027, 939.61,123,509.79.30
DISEMBA1,403, 189.81,414,921.80.84
JUMLA6,449,321.17,271,256.2612.74
Jitihada mbalimbali zinafanywa ili kuhakikisha TRA inaongeza makusanyo kwa kuongeza ufanisi katika ukusanyaji, kuhimiza maadili mema kwa watumishi, kuboresha mifumo ya ukusanyaji, kushirikiana na vyombo vingine vya dola na wananchi katika kuziba mianya ya upotevu wa mapato pamoja na kufuatili, kuhimiza matumizi ya mashine za kielektronik na kuhimiza ulipaji wa kodi ya majengo.  

TRA inaendelea kuhimiza wafanyabiashara wote waliosajiliwa na Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) kuwasilisha ritani za VAT kabla ya tarehe 20 ya kila mwezi kama ilivyobadilishwa katika Sheria ya Fedha ya 2016.

Pamoja na hayo tunawakumbusha na kuwahimiza wananchi wa Dar es Salaam ambao hawajafanya uhakiki wa taarifa za Namba ya Utambulisho wa Mlipakodi (TIN) kuhakiki taarifa zao kabla ya tarehe 31 Januari 2017 ili zoezi hilo liweze kuanzishwa katika mikoa mingine.

TRA inatoa wito kwa wafanyabiashara kulipa kodi stahiki kwa hiari na wakati ili serikali ipate mapato yake ambayo yataiwezesha kuwahudumia wananchi wake kikamilifu.

Kwa wafanyabiashara wenye madeni ya nyuma wanashauriwa kujitokeza kuonana na Mameneja wa Mikoa na Wilaya kujadiliana jinsi watakavyolipa madeni yao bila kuathiri biashara zao.

Wamiliki wa majengo wanaaswa kutoa ushirikiano kwa kulipia ankara zao za kodi ya majengo kwa hiari .

‘Pamoja Tunajenga Taifa Letu’

Richard M. Kayombo

MKURUGENZI WA HUDUMA NA ELIMU KWA MLIPAKODI

Hatarii: Soma Hapa Alichokisema Nuh Mziwanda Baada ya Dada Msagaji Kumtaka Kimapenzi..!!!

0
0
binti (3)
MSANII wa muziki wa Bongo Fleva Naftal Mlawa ‘Nuh Mziwanda’ amejikuta akiishiwa pozi baada ya kupata taarifa kuwa, msichana ambaye aliwahi kujianika kufanya mambo ya usagaji, Malkia Said ‘Malkiz’ amemzimikia na yupo tayari kuolewa naye hata mke wa nne.


Ishu hiyo ambayo ilizua viulizo ilijiri siku chache zilizopita ambapo mwanadada huyo aliweka ujumbe huo kwenye mtandao wa kijamii wa Instagram, akishikilia msimamo wake wa kuacha usagaji na kudai kwa mara ya kwanza amejikuta akipagawishwa na Nuh japo ni mume wa mtu.

Malkis alipoulizwa alisema; Pale nilivyoandika nilisema nilikuwa nimelewa, lakini nikuhakikishie sikukosea kuandika vile nikiwa kama binadamu mwenye hisia, niliona niweke wazi hisia zangu, sijawahi kuvutiwa na mwanaume ila Nuhu natamani hata anioe sababu dini yetu ya Kiislamu inaruhusu wake wanne na nipo tayari kubadilika hata kimavazi.”

Nuh alipotafutwa kuhusiana na jambo hilo alistaajabu na kujikuta akiangua kicheko mwanzo mwisho, kisha akaomba shushushu wetu amuache kwanza kwa kuwa hakuwa na cha kujibu.

Sikia Hii,Gigy Money Afunguka Jinsi Alivyodate na Ali Kiba na Tetesi za Kumwambukiza Ukimwi,Soma Hapa Livee Kujua A - z

0
0
ali kiba
DAR ES SALAAM: Video queen matata ambaye pia ni mtangazaji wa kituo cha redio moja jijini hapa, Gift Stanford ‘Gigy Money’, ametema cheche akisema kuwa, watu wote wanaomsema kwamba kutokana na kuvaa nusu utupu na kujiachia na midume mbalimbali huenda ana maambukizi ya virusi vya Ukimwi, waache kwani kama ni kweli basi wengi wangekufa kwa sababu ameshatembea na mastaa kibao Bongo.


Akizungumza , Gigy alisema kwamba amekuwa na uhusiano wa kimapenzi na mastaa mbalimbali wakubwa Bongo akiwemo Mbongo Fleva, Ali Kiba na kudai kuwa, kama kuambukizwa virusi angeanza yeye na wengine wangefuata.

“Unajua watu wanashangaza sana. Kama mtu ana virusi vya Ukimwi hawezi kuwa na uhusiano wa kimapenzi na mtu anayempenda, ningependa watu waache unyanyapaa. Ninachojua mimi sina Ukimwi kwa kuwa nilipima kwa shinikizo la mpenzi wangu wa sasa (Moulad Alpha ‘Moj’) na watu niliotembea nao wanaendelea vizuri tu, wengine wachumba zao wananyonyesha,” alisema Gigy.

Video queen huyo alikwenda mbele zaidi kwa kusema kuwa, kuvaa nusu utupu ni kitu anachopenda kufanya toka ndani ya moyo wake hivyo hakuna mtu wa kumwambia kitu au kumkataza hata siku moja na wala siyo mgonjwa wa akili bali anafanya kitu kujifurahisha nafsi yake si ya mtu mwingine.

“Mimi nasikilizaga moyo wangu unasema nini, si mtu anasema nini juu yangu hivyo kama kuvaa nusu uchi wana hofu na mimi waondoe hilo kwa maana kama ni Ukimwi wengi wangeondoka siku nyingi kwenye ramani ya dunia hii maana hakuna niliyemuacha kwa mastaa unaowajua,” alisema Gigy kwa kujiamini.

Gigy ameshatoka kwenye magazeti mbalimbali akidaiwa kutembea na mastaa kama Hemed Suleiman ‘PHD’, Richard Martin Lusinde ‘Rich Mavoko’, Ali Saleh Kiba ‘King Kiba’, Emmanuel Elibariki ‘Nay wa Mitego’, Seif Shaban ‘Matonya’ na Omar Nyembo ‘Ommy Dimpoz’.

Mwingine aliyewahi kutajwa ni Mtangazaji Gardner G. Habash ‘Captain’ na Mshindi wa Big Brother Africa 2014, Idris Sultan

Duh!Unamkumbuka Z Anto ,Basi Jamaa Katangaza Kuuanza Mwaka Huu kwa Kushusha Mjengo Huu wa Maana zaidi ya Wa Daimond

0
0

Mwanamuziki Z-Anto ambaye aliwahi kufanya vyema katika muziki miaka ya nyuma na kuamua kukaa pembeni huku akifanya biashara zake ameanza vyema mwaka 2017 kwa kujenga nyumba ya nne nje ya kazi yake ya sanaa. 


Z-Anto ambaye makazi na shughuli zake za kila siku zipo Kigamboni Dar es Salaam, amefunguka na kusema ameamua kuanza mwaka 2017 kwa kujenga nyumba yake ya nne ambazo amejenga nje ya kazi yake ya muziki na sanaa kiujumla.

"Wiki mbili za mwanzo za mwaka 2017. House namba 4. Mwaka ndivyo tulivyouanza. #Thnxgod nje ya sanaa" aliandika Z Anto 
 
Z-Anto mwaka kupitia kipindi cha Planet Bongo aliahidi kurudi kwenye muziki na kusema kuwa label mbalimbali kubwa nchini zaidi ya nne zimemfuata ili wafanye kazi na kusema yeye anahitaji kuchanganua ili ajue ni label ipi ambayo inaweza kumpeleka mbali kimuziki na kufikia malengo yake kwenye muziki.

Mhh!! Umesoma Alichokiandika Mpoto Leo Kuhusu Vijana Wanaotaka Kujikwamua Kiuchumi,Pitia Hapa Hutajuta Kusoma

0
0

Msanii wa mashairi na kughani Mrisho Mpoto ametoa somo kwa vijana wa watanzania kwa kuwapa njia mbalimbali ambazo zinaweza kuwafanya kujikwamua kiuchumi endapo watazitumia kuanzisha biashara ya kutumia mtaji mdogo au bila ya kuwa na mtaji kabisa. 


Mrisho Mpoto ametumia ukurasa wake wa facebook kutoa fursa tano ambazo anaona kama vijana watazitumia zinaweza kuwa na tija katika maisha yao. 

Biashara hizo alizozitaja Mpoto ni kama ifuatavyo:_

"1. Toa huduma.

Kama huna mtaji wa fedha, basi nina uhakika una mtaji wa muda. Sasa tumia muda wako kutoa huduma ambayo wengine wanaihitaji. Toa huduma kulingana na utaalamu wako, uzoefu wako au ujuzi ulionao. Angalia ni namna gani unaweza kutumia muda wako kuongeza thamani zaidi kwenye maisha ya wengine.

Kwa mfano kama wewe ni mwalimu, basi unaweza kutenga muda wako wa ziada kutoa huduma ya kufundisha watoto shuleni au hata majumbani mwao. Kama wewe unaweza kufanya kitu fulani, basi tafuta wenye uhitaji wa kitu hiko na wasaidie kwa muda ulionao. Unaweza kuwasaidia watu kwa kazi zao za nguvu au hata kazi zao za kitaalamu. Unaweza kuwasaidia watu wanaofanya tafiti mbalimbali kwa muda wako na utaalamu wako kwenye tafiti.

2. Biashara ya mtandao (network marketing).

Najua wengi mkisikia hii huwa mnakunja sura na kuona kama mnapotezwa. Bado naendelea kusisitiza kama unataka kuingia kwenye biashara na hujui wapi uanzie, basi ingia kwenye biashara ya mtandao. Hii ni biashara ambapo unatumia bidhaa au huduma fulani, kisha unawashawishi wengine nao watumie na unalipwa kamisheni kwa manunuzi wanayofanya.

3. Biashara ya taarifa na maarifa.

Unaweza kuingia kwenye biashara ya kutoa taarifa na maarifa. Kwa dunia ya sasa ambapo watu wengi wanatumia mtandao wa intaneti, unaweza kutumia mtandao huu kutoa taarifa na maarifa na kuweza kutengeneza kipato.

4. Kilimo biashara.

Kuna fursa kubwa sana kwenye kilimo cha kib
iashara, hasa kwa kilimo cha muda mfupi cha mboga mboga na matunda. Kilimo hiki unaweza kuingia kwa mtaji kidogo na kama una muda wa kutosha kukifuatilia kwa makini basi unaweza kuanza kidogo na kukua kadiri muda unavyokwenda. Angalia kilimo kipi unaweza kuanza nacho na ukaribu wako ili uweze kupata matokeo mazuri.

5. Biashara yoyote unayotaka kuanza, ila anza kidogo.

Unaweza kuanza biashara yoyote unayopenda kuanza, hata kama ina uhitaji wa mtaji mkubwa, wewe anza kidogo. Anza kwa hatua ya chini kabisa, weka juhudi kubwa na endelea kuikuza.

Ukishaanza kuona matokeo mazuri, yaani faida kwa hatua hiyo ndogo unayopiga, ni rahisi kuwakaribisha watu wengine na wakakuchangia mtaji. Au hata kwenda kwenye taasisi za kifedha na kuchukua mkopo."

Hiyo ni kwa mujibu wa Mrisho Mpoto

Mchungaji wa Kanisa Awanywesha Waumini Wake Oili ya Gari Akidai Inafukuza Mapepo

0
0

PICHA: NABII AWANYWESHA WAUMINI KEMIKALI YA KUSAFISHIA INJINI

Mtu mmoja anayejiita Nabii nchini Afrika Kusini amezua taharuki baada ya picha kusambaa kwenye mitandao ya kijamii zikimuonyesha akiwanywesha waumini wake kemikali ya kusafishia injini na kusema kuwa ina ladha kama asali.

Nabii Theo Bongani Maseko wa kanisa la Breath of Christ Ministries lililopo mjini Johannesburg amesema kuwa kemikali hiyo inashambulia virusi ndani ya mwili wa binadamu na kutambua mapepo.

Maseko alisema kuwa unywaji wa kemikali hiyo hauna madhara yoyote kiafya kwani yeye mwenyewe amewahi kunywa.

“Ina ladha kama asali, nimewahi kunywa mara mbili” alisema Maseko.

Aidha, alisema kuwa waumini wake wote ambao tayari wameshatumia dawa hiyo hakuna hata mmoja aliyepata matatizo ya kiafya na kwamba wote wamekuja na ushuhuda wa kuponywa matatizo yao. Alisema kuwa Mungu alimpa wito huo kabla hata hajazaliwa.

Nabii huyu si yeye pekee aliyefanya vitu vya kushangaza kwani kuwa mwingine alikuwa akiwapulizia waumini dawa ya kuuwa wadudu na mwingine akiwanywesha petroli.



Viewing all 104432 articles
Browse latest View live




Latest Images