Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104712 articles
Browse latest View live

Safi Sanaa!! Wanafunzi wa Diploma Eti nao Watapewa Mikopo,Soma Hapa Livee..!!!

$
0
0

SERIKALI imewasilisha pendekezo la mabadiliko ya Sheria ya Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu ili kuwezesha wanafunzi wanaochukua Stashahada katika vipaumbele vya kitaifa, kupewa mikopo ya kuwawezesha kuchukua elimu husika.


Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Mafunzo ya Ufundi, Profesa Joyce Ndalichako alisema mabadiliko hayo, yamelenga kuwezesha kasi katika uchumi wa viwanda.

Profesa Ndalichako alisema mabadiliko katika Sheria Namba 4 ya Mwaka 2016 ya Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB), yamelenga kutoa nafasi ya kada ya Stashahada inayohitajika ambao wamekuwa hawapati mikopo.

“Kwa lengo la kupata balance (mizania) na kwa kuwa Diploma nayo iko kwenye elimu ya juu, watoto ni wale wale. Kuna wengine nao wanashindwa kumudu gharama na ili serikali ipate uwiano mzuri tumeona ni vizuri kuwe na marekebisho ya sheria,” alieleza Profesa Ndalichako.

Profesa Ndalichako alisema kuna umuhimu mkubwa wa kada ya Stashahada, hasa wanaokwenda sanjari na vipaumbele vya kitaifa kwenye msukumo wa Serikali ya Awamu ya Tano wa ujenzi wa taifa la vijana, kama ilivyo kwa wenye Shahada.

“Kama taifa tunazungumzia uchumi wa viwanda,wadau wote hata wale wa ngazi ya kati ni muhimu katika kuhakikisha kwamba ajenda hii inafanikiwa kama vile ambavyo wale wa digrii wangelifanya,” aliongeza waziri huyo.

Mwaka 2004, kulikuwepo na mabadiliko katika sheria hiyo iliyowezesha wanaochukua masomo ya sayansi, hisabati na elimu ya msingi (kwenye msisitizo wa sayansi na hisabati), kupata mikopo ya elimu, nafasi iliyoanza kutumika mwaka 2014, lakini hatua hiyo ilisimamishwa wakati wa muhula wa masomo wa mwaka 2016/17.

Hata hivyo, HESLB ilikaririwa ikisema kwamba maamuzi ya kusitisha utoaji wa mikopo, ililenga kutekeleza maagizo ya serikali. Hata hivyo, jana Profesa Ndalichako alisema kwamba uamuzi wa kusimamisha mikopo hiyo,ulitokana na nia ya serikali kufanya mabadiliko katika sheria hiyo ili kuipa wigo mpana zaidi kuliko kujikita katika eneo la sayansi pekee.

“Mwaka 2004 tuliingiza diploma, lakini kwa masomo ya sayansi pekee sasa, tunataka kuwa na kipengele kinachopanua wigo ili tuweze kuhusisha kozi nyingine za diploma ambazo zinaenda sanjari na vipaumbele vya kitaifa,” alifafanua waziri huyo.

Kwa mwaka wa masomo 2016/17, serikali ilipanga bajeti ya Sh bilioni 483 ambazo zitakopeshwa kwa wanafunzi wa mwaka wa kwanza na wale wanaoendelea. Katika mwaka huo, wanafunzi wa mwaka wa kwanza waliopata mikopo walikuwa ni 25,715.

Wakichangia mjadala huo, Mbunge wa Malindi, Ally Saleh (CUF) alitahadharisha kuhusu vipaumbele vya kitaifa na kutaka kuwapo na ufafanuzi ili kuondoa utata. “Sijafurahi sana na phrasing of national priority.

Naogopa isije ikajibana au ikatumika katika hali itakayoleta utata. Hivi karibuni tulikuwa na utata mkubwa wa nani apewe mikopo...sasa tunasikia kuwa tunaenda kwenye uchumi wa viwanda isije fedha zote zikapelekwa kule.

“Kutafutwe njia ya kudetermine hizo priority za kitaifa na kujua watakuwa wangapi ili tujue kichumi itagharamu kiasi gani ilitusishindwe huko mbele,” alisema Saleh.
 
Fikra ya kutanua wigo kwa wanafunzi wa Stashahada ilifafanuliwa na watu wa Bodi ya Mikopo kwamba imezingatia kuwa katika sekta zote kutatakiwa uwiano wa wataalamu wa kada mbalimbali. Aidha, imeelezwa kuwa waziri kwa kushirikiana na wadau mbalimbali, wataweza kushauriana na kuona hitaji ya kada mbalimbali zinavyokwenda.

Kachumbari Yasababisha Mauaji ya Mke

$
0
0
MKAZI wa mtaa wa Mageuzi, kata ya Ngokolo, manispaa ya Shinyanga, Ibrahimu Daniel (42) amemuua mke wake, kwa kushindwa kuhifadhi vizuri kachumbari na kupika mboga isiyo na kiwango.

Aidha mauaji hayo yaliyofanyika kwa kumporomoshea kipigo yalifanyika kwa kuwa alipika chakula kingine wakati kilichobaki mchana kilikuwepo.

Aliyeuawa ni Stella Ibrahimu (39) na alipigwa baada ya mumewe Daniel kurudi nyumbani na kuuliza kachumbari ambayo alikula jana yake ndipo mtoto aliyekuwa akimlea Elizabeth Ibrahimu (13) alipomuonesha, lakini hakuridhika nayo na kuanza kuuliza maswali kwa nini haikuhifadhiwa vizuri.

Baadhi ya waandishi wa habari waliofika eneo la tukio walielezwa na mtoto wa marehemu, Daniel Ibrahimu (12) kuwa baba yake alipofika nyumbani saa moja usiku alimkuta yeye akiwa na Elizabeth ndipo alipoanza kumhoji Eliza akimuuliza kachumbari yake iko wapi.

Daniel alisema baada ya Eliza kumuonesha baba yake kachumbari hiyo aliyoila na kuibakisha Jumatatu wiki hii, aliiona imechacha na kuonekana na uchafu, ndipo alitoka nje na kuchukua fimbo anayoihifadhi juu ya nyumba na kutaka kuanza kumpiga lakini kabla ya kumpiga mtoto huyo alichoropoka na kukimbia nje.

Aliendelea kusimulia kuwa baada ya kukimbia na binti huyo, mama yake ambaye alikuwa kazini alifika nyumbani wakati huo mfarakano ukiendelea na alimkuta baba yao akifoka na baada ya kuuliza kuna nini, aliambiwa kwa nini hakupika mboga yenye kiwango na kwa nini alipika ugali mwingine wakati kulikuwa na ugali uliobaki mchana.

“Mama alifika na kuanza kunywa chai lakini baba aliendelea kufoka ndipo mama alimjibu kwa hasira ndipo alipomuuliza baba uliacha fedha ya matumizi ya kuweza kupika mboga yenye kiwango, alianza kumpiga baadaye alimpiga na kikombe na mateke akaanguka ndipo mimi nilikimbia kwa majirani kuwataarifu mama anapigwa, walikuja na kukuta mama ameanguka chini baba akiwa anamruka ruka,” alisema Daniel.

Baadhi ya majirani waliofika katika tukio hilo, Gloria Shija na Retisia Mashalah, walisema kwa nyakati tofauti kuwa, walikuta baba huyo amefunga mlango na walipomgongea afungue, alikataa na kusema kuwa kuna kazi kidogo anaifanya wasubiri, lakini baada ya kuchungulia dirishani walimuona anampuliza puani na masikioni huku akimmwagia maji ili azinduke, baada ya kuona hazinduki.

Shija alisema kuwa waliingia ndani na kumkuta akiwa amemkalisha chini huku akiwa ameinamisha shingo ambapo walimbeba na kumtoa nje, walijaribu kummwagia maji tena lakini ilishindikana ndipo walichukua uamuzi wa kumpeleka hospitalini walifika na kuanza kupimwa, lakini alionekana tayari alishafariki muda mrefu.

Kwa mujibu wa majirani, waliporudi nyumbani, mwanaume huyo alionekana kumtuma mara kwa mara mwanawe wa kiume na wakaingiwa na hofu na kutoa taarifa polisi ambapo walifika na kuwachukua watoto wawili; Daniel na Eliza kwa mahojiano.

Shangazi wa marehemu, Getruda Vitalis alisema ugomvi huo ulikuwa ukitokea mara kwa mara. Mwenyekiti wa mtaa wa Mageuzi, Emmanuel Sama alisema yeye alikuwa amelala nyumbani kwake aligongewa mlango na kuambiwa kuna tukio la mwanamke kupigwa na mume wake na ana hali mbaya ndipo aliamka na kwenda katika tukio.

Baada ya kuuliza aliambiwa chanzo ni kachumbari iliyobaki jana haikuhifadhiwa vizuri na mtoto waliokuwa wakimlea, Elizabeth.

Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga, Elias Mwita, alithibitisha na kueleza kuwa mtuhumiwa anashikiliwa na Polisi. Alisema uchunguzi wa awali katika mwili wa marehemu umeonesha kuwa na jeraha katikati ya kichwa na waliruhusu usafirishwe kesho wilayani Ngara, Kagera kwa maziko.

Unaikumbuka Ile Issue ya Serikali Kuhamia Dodoma,Sasa Sikia Hili Jipya Juu ya Suala Hilo..!!

$
0
0

WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Walemavu, Jenista Mhagama amesema ratiba ya kuhamia Dodoma kwa mawaziri, manaibu, makatibu wakuu na manaibu iko palepale.

Amesema watakaoshindwa kufanya hivyo, Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa atatoa mwongozo. Jenista alisema jana kuwa baada ya Februari 28, mwaka huu kutafanyika tathimini na kuangalia utekelezaji wake umefikia wapi, na kwamba kwa wale ambao hawatatekeleza agizo hilo, Waziri Mkuu Majaliwa atatoa mwongozo.

Akizungumza na waandishi wa habari mjini hapa jana, Jenista alisema uamuzi ulitolewa na Rais John Magufuli uko palepale.

Alisema hata Waziri Mkuu amekuwa akisisitiza ratiba ya kuhamia Dodoma kwa awamu ya kwanza Februari mwaka huu ambayo itahusisha mawaziri, manaibu mawaziri, makatibu wakuu na manaibu wao na baadhi ya watumishi wa wizara.

"Kazi yetu itakuwa ni kuangalia utekelezaji utakuwa umefikia wapi na asiyetekeleza Waziri Mkuu atatoa mwongozo,” alisema Jenista.

Pia alisema amekuwa akikagua nyumba ambazo zinafanyiwa ukarabati kwa ajili ya watumishi watakaohamia Dodoma ikiwemo nyumba za Mamlaka ya Ustawishaji Makao Makuu (CDA) eneo la Kikuyu, ambapo ukarabati wake unaendelea vizuri.

Alisema nyumba hizo za ghorofa, zitawezesha baadhi ya watumishi kupata nyumba za makazi, ambapo pia taasisi nyingine zinaendelea na ujenzi wa nyumba za watumishi.

Julai mwaka jana, Rais Magufuli alitangaza kuhusu serikali yake kuhamia Dodoma kabla ya kumalizika kwa muhula wake wa kwanza wa miaka mitano, na tayari Waziri Mkuu Kassim Majaliwa alikwisha kuhamia katika makao makuu hayo ya nchi yaliyotangazwa mwaka 1973.

Akiahirisha Mkutano wa Nne wa Bunge la 11 mwishoni mwaka jana, Waziri Mkuu Majaliwa alisema serikali itahamia Dodoma kwa awali, na kueleza kuwa awamu ya kwanza itakuwa kati ya Septemba 2016 hadi Februari, 2017 ikiwahusisha Waziri Mkuu, mawaziri, makatibu wakuu, manaibu makatibu wakuu na walau idara mbili za kila wizara.

Alisema awamu ya pili itakuwa Machi 2017 hadi Agosti 2017, ya tatu Septemba 2017- Feb 2018, ya nne Machi 2018- Agosti 2018, na ya tano Septemba 2018-Februari 2019; na kwamba awamu hizo zitatumika kwa ajili ya kuendeleza mchakato wa kuhamisha watumishi hadi wote wawe wamehamia Dodoma.

Aina 10 za Waume Ambao Wake zao Wanakereka Kuwa nao

$
0
0
1. Wanaojiona Kama Wafalme (King Husband).
HIi ni aina ya wanaume ambao hutaka kusujudiwa kama wafalme na hupenda kuwafanya wake zao kuwa kama watumwa. Hawafanyi chochote ndani ya nyumba kazi yao ni kutumatuma hata kama mke anaumwa atapaswa kuamka na kupika, wanataka waheshimiwe wao tu na mwanamke akikosea kidogo ni maneno au kipigo. Mwanamke hana kauli ndani na mume akiingia nyumbani ni kama bosi anavyoingia ofisini, wote kimya hakuna hata kuongea.

2. Wanaume Wanaojihisi Bado Hawajaoa (Bachelor Husband).
Hii ni aina ya wanaume ambao hawawashirikishi wake zao kwa chochote. Hufanya mambo kama vile bado hawajaoa, hutumia muda wao mwingi na marafiki zao wakifanya mambo ambayo mke hata hayajui mke anaweza kustukizia tu mume kanunua gari bila kumshirikisha na mume haonyeshi hata kujali kuweza kumshirikisha. Hajali kama ana mke na mda mwingi huutumia akiwa na marafiki kufanya mambo yasiyo na msingi ambayo hayana mnanufaa yoyote katika ndoa yake.

3. Wanaume Wenye Gubu (Acidic Husband).
Hawa hukasirika kila mara tena bila kua na sababu ya misngi, mambo hayaishi, kosa la mwaka juzi anaweza kukukasirikia leo. Wamemuudhi kazini hataki kusemeshwa na mnanuniwa nyinyi, mwanamke akiomba hela ya chakula ni shida ni kununa kutwa nzima, wanahasira na nirahisi kumpiga mke.

4. Mume Wa Kila Mtu (Genarel Husband).
 Hawa wanajifanya wasamaria wema, wanajali kila mwanamke, wanajali marafiki wakike wa mke na wakwao kuliko wanavyowajali wake zao. Mke anaweza kuwa na shida akasema hana hela lakini rafiki akampa. Wana marafiki wengi wakike na mara nyingi huwa hawaachani kabisa na ma X wao, wakiwalalamikia wanawasaidia kuliko hata wanavyowasidia wake zao wakati wakiwa na shida.

5. Wanaume Wanaojifanya Wagumu (Dry Husband).
Hawa wanajifanya wagumu sana, hawana yale mambo ya kimahaba na wao hujua kuwa ndoa ni kuleta chakula tu na kushughulika kitandani. Hakuna kuongea na hawajali hata hisia za mke, mke akiongea kwao wala hawajali wanajifanya ni vidume sana na wanaona mambo kama vizawadi, kupiga simu, kutuma sms, kusema nakupenda, kununua maua ni mambo ya kike, yaani hawaonyeshi juhudi yoyote kuwafurahisha wekea zao.

6. Wanaume Wanaopenda Kutumia Wake Zao (Panadol Husband).
Hawa huwa wanaume pale tu wanapokuwa na shida, wanakuwa na wake wazuri wanaowajali lakini wao wala hawajali. Wanapomhitaji mwanamke, wanapotaka mwanamke awafanyie kitu flani basi huja na maneno mazuri na hata kuleta vizawadi, wanajua udhauifu wa wake zao na huutumia kuwalaghai kuwatimizia mahitaji yao lakini wanapotimiziwa tu basi husahau hata kama wanawake, hawajali tena.

7. Wanaume Ambao Hawataki Kukua (Baby Husband).
 Bado wanatabia za kitoto, hawawezi kufanya maamuzi yao wenyewe mpaka kuuliza kwa ndugu zao, mtu kaoa lakini kila siku humpigia simu Mama yake kuuliza hiki na kile. Yaani wakiongea kitu na mke nilazima aulize ndugu kwanza ndiyo kipitishwa na mke akifanya kosaa kidogo kazi nikulinganisha mke na ndugu zake, mbona flani alifanya hivi, flani anaweza fanya zaidi na mambo kama hayo. Kwakifupi hawawezi kufanya maamuzi na mkewe, ndugu zake hasa Mama yake anakuwa kama shemeu ya ndoa.

8. Mume Mtalii (Visiting Husband). 
Hawa wanakuja nyumbani kama wageni vile, mume ataihudumia familia yake kwa kila kitu lakini hawezi kuipa muda wake. Akirudi mke na watoto wamelala ni kugonga na hana sababu za msingi za kuchelewa, hata mwisho wawiki hupenda kutumia na marafiki au ndugu lakini si na mke. Hakuna kitu cha pamoja ambacho anafanya na mkewe au watoto wake, kila akiingia tu anakua na safari ya kutoka yaani hata atoke akakae nnje tu lakini si kukaa na mke au watoto.

9. Wanaume Wanaofuatilia Kila Kitu (Stalking Husband). 
Hii ni aina ya wanaume ambao hufuatilia kila kitu, huchunguza kila kitu mwanamke anachofanya na hawampi pumzi. Akienda sehemu atachunguza anaenda na nani na alikutana na nani, huwa na wivu wa ajabu ajabu na kila saa huhisi wake zao ni wasaliti. Kila mtu mwanamke anayeongea naye wa jinsia tofauti huhisi ni mchepuko na hata marafiki wa mke wakike pia huhisi wanamkuwadia, kwakifupi hampi pumzi mwanamke.

10. Mwanaume Mbahili (Miserly Husband).
Huyu anaweza kuwa na hela lakini mbahili ajabu. Akimpa mwanamke hela atafuatilia matumizi yake mpaka senti ya mwisho, anafuatilia mpaka mambo ya jikoni. Sukari ikiisha naataka ajue iliisha ishaje na kila mara huhisi mke anamuibia hela labda akajenge kwao, huwa msumbufu sana na mgumu kutoa hela. Mwanamke akifikiria mchakato wa kuomba hela kwa mume hukata tamaa na wakati mwingine kuamua tu kukaa kimya na matatizo yake.

Breaking Newss... Rais Magufuli Amvua Ubunge na Uwaziri Dkt. Possi, Ampa Ubalozi

$
0
0

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli, jana tarehe 19 Januari, 2017 amemteua Dkt. Abdallah Possi kuwa Balozi.
 
Kituo cha kazi na tarehe ya kuapishwa kwa Dkt. Abdallah Possi itatangazwa baadaye.
 
Kabla ya uteuzi huo Dkt. Abdallah Possi alikuwa Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Walemavu aliyekuwa akishughulikia Ulemavu.
 
Kufuatia uteuzi wa Dkt. Abdallah Possi kuwa Balozi, nafasi ya Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Walemavu (Ulemavu) itajazwa baadaye.
 
Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar es Salaam

Jeshi la Senegal Laingia Gambia Kukabiliana na Rais Jammeh Aliyegoma Kuondoka Madarakani

$
0
0
GAMBIA: Vikosi vya majeshi kutoka nchini Senegal vimethibitisha kuingia katika ardhi ya Gambia katika muda ambao rais mpya Adama Barrow alipokuwa akiapishwa kwa lengo la kumuondoa madarakani Rais Jammeh aliyeng’ang’ania uatawala baada ya kushindwa uchaguzi.

Msemaji wa Jeshi la Senegal Kanali Abdou Ndiaye amethibitisha kwamba vikosi hivyo vimevuka mpaka na kupiga hatua kuelekea katika Mji Mkuu wa nchi hiyo, Banjul na kusema kwamba vikosi hivyo mpaka sasa havijakabiliana na ukinzani wa aina yoyote ingawa viliweka bayana kwamba vilikuwa vimejizatiti kwa mapigano ikibidi.

Mapema Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa inasemekana kwa siri limekuwa likiunga mkono juhudi za vikosi vya ECOWAS, kuhakikisha kwamba rais Barrow anachukua madaraka kutoka kwa rais aliyemaliza muda wake Yahya Jammeh. Rais huyo wa zamani wa Gambia, awali aligoma kuachilia madaraka.

Rais wa sasa Adama Barrow ameapishwa leo katika nchini jirani kwenye ubalozi wa Gambia ulioko mjini Dakar nchini Senegal na kufuatiwa na shamra shamra ubalozini hapo.

Mpaka sasa haijafahamika wazi lini rais mpya wa Gambia ataweza kurejea nchini mwake na kuchukua hatamu za uongozi kwa mara ya kwanza akiwa rais.

Miujiza ya Shekh Sharifu Rashid Kutoka Bagamoyo , Anarudisha Mapenzi na Kusafisha Nyota

$
0
0

MIUJIZA YA SHEKH SHARIFU RASHID KUTOKA BAGAMOYO PWANI, (RUDISHA MAHUSIANO YAKO NDANI YA MASAA 48 TU) ASANTE KWA KUENDELEA KUMPIGIA SIMU SHEKH SHARIFU RASHID KWA WALE WENYE MATATIZO NA WALE WANAOTOA SHUKRANI:

SHEKH SHARIFU RASHIDI ni mtaalamu wa tiba mbalimbali za asili, anatumia kitabu cha quran, dawa za asili, dawa za kiarabu na majini, anazo dawa za mapenzi, nguvu za kiume, chango, ngiri maji na n.k, anakuvutia mpenzi alie kuacha au alie mbali, pia anatoa pete za bahati zilizoambatanishwa na jini mali kulingana na nyota yako, anaouwezo mkubwa wa kutumia jina la muhusika kwa kutatua tatizo lako, anaouwezo wa kumrudisha mtu aliepotea kimiujiza, pia anatibu kwa njia ya simu popote ulipo,

WASILIANA NAE KWA SIMU NA WHATSAPP NO: 0718-668347. 0685-224047, 0767-204308 na 0627-251404 au follow@shekh_sharifu_rashid, Email:shekhsharifurashid@gmail.com

Install APP ya Blog Hii ya UDAKU SPECIAL Kwenye Simu yako Kutoka Google Play Kusoma Habari Kirahisi

$
0
0
Download  Application ya Udaku Special Blog Kwenye Simu yako Kutoka Play Store Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi

Bonyeza Hapa CLICK HERE 


Au Kama Unayotayari Bonyeza Hapa Ku Update Uweze Kupata Ikiwa na Muonekano Mpya

Imefichuka: Kumbe Ujenzi wa Uwanja Mpya wa Ndege Unasuasua Kwa Sababu Hii Hapa..!!!

$
0
0

Deni la mkandarasi kwa Serikali limesababisha ujenzi wa jengo la tatu la  Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) kusuasua huku  baadhi ya vifaa vikiwa vimekwama bandarini.

Mkandarasi huyo ambaye ni Kampuni ya Bam International ya Uingereza, anadai Sh21.4 bilioni huku mkandarasi mshauri akidai Sh1.8 bilioni na Sh279.7 bilioni zinadaiwa kwa ajili ya kukamilisha mradi huo, ambazo bado hazijapatikana.

Mradi huo ambao ulianza kujengwa mwaka 2013, unatakiwa uwe umekamiliaka Desemba mwaka huu.

Kaimu Mkurugenzi wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), Salum Msangi amesema mradi huo umekamilika kwa asilimia 66 mpaka sasa.

Kaimu Mkurugenzi huyo alimesema hayo jana kwenye ziara ya  Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa aliyetembelea mradi huo.

Profesa Mbarawa amesema mradi huo utagharimu Sh560 bilioni hadi kukamilika kwake.

Serikali Yatoa Tamko Hili Juu ya Uwepo wa Ugonjwa wa Mafua ya Ndege..!!!

$
0
0

SERIKALI imesema hakuna binadamu yeyote aliyeonekana kuwa na dalili za ugonjwa wa mafua ya ndege nchini.


Akizungumza  katika mahojiano maalumu  jana, Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu alisema hakuna mgonjwa yeyote aliyepatikana na ugonjwa huo nchini hadi sasa.

Ummy alisema hayo akitoa ufafanuzi baada ya kuenea uvumi kwamba kisiwani Zanzibar, amepatikana mgonjwa mwenye mafua ya ndege.

Alisema kutokana na kuibuka kwa ugonjwa huo nchi jirani serikali imetuma watalaamu mpakani mwa Tanzania na Uganda kutoa elimu kwa wananchi namna ya kujihadhari na ugonjwa huo.

Aliwataka madaktari wote nchini wakimwona mgonjwa mwenye dalili au mafua yasiyo ya kawaida, kumpima na kumpa tiba haraka kabla hajaugua au hajaambukiza.

Pitia Magazeti ya Leo 20/1/2017..!!!

Baada ya Okwi Kuvunja Mkataba Denmark,Simba Wamfanyia Mapango Aje Kucheza Mechi ya Yanga..!!

$
0
0

UONGOZI wa Simba umesema unafanya mpango wa kumrejesha kikosini mshambuliaji wake wa zamani Emmanuel Okwi aliyevunja mkataba na klabu ya Sonderjyske ya Denmark.

Taarifa za kwenye mtandao wa klabu hiyo juzi ziliandika kwamba Okwi amefikia makubaliano ya kuvunja mkataba baada ya kukosa nafasi ya kucheza kwenye kikosi hicho.

Jana jioni Ofisa habari wa Simba, Haji Manara aliandika kwenye kurasa zake za mitandao ya kijamii: “Kocha Omog (Joseph- kocha mkuu wa Simba) ikimpendeza, Emmanuel Okwinho (Okwi) dimbani Feb 18, hiyo ndio habari mpasuko, ukinuna ongeza limao,”.

Simba inatarajia kucheza na Yanga katika mechi ya raundi ya pili ya Ligi Kuu baada ya kutoka sare ya bao 1-1 katika mechi ya kwanza.

Alipoulizwa  kuhusu taarifa hizo, Manara alikiri kuwa uongozi wake uko kwenye mchakato wa kumnasa mchezaji huyo na ikiwezekana atumike kwenye mechi zilizosalia za Ligi Kuu.

“Ni kweli tutamsajili kama mchezaji huru,” alisema.

Hata hivyo, tayari dirisha dogo la usajili kwa klabu za ligi limeshafungwa mpaka msimu ujao. Akilizungumzia hilo, ofisa habari wa Shirikisho la soka Tanzania (TFF), Alfred Lucas alisema Simba haiwezi kumtumia Okwi kwa sababu dirisha la usajili limeshafungwa.

“Ingewezekana kama usajili wa dirisha dogo ungekuwa haujafungwa, lakini dirisha limeshafungwa hivyo kama wanataka kumtumia, wasubiri mpaka usajili mwingine,” alisema.

Wakati wa usajili wa dirisha dogo Desemba mwaka jana Simba ilitaka kumsajili mshambuliaji huyo Mganda lakini ilishindwa baada ya klabu ya Sonderjyske kutaka ilipwe karibu sh milioni 240.

Hasimu wa Simba, Yanga pia ilijaribu kutaka kusajili mshambuliaji mwingine ili ashindane na Donald Ngoma baada ya kudaiwa kugoma kucheza kwenye mechi za kombe la Mapinduzi lakini ilishindikana kwa vile dirisha la usajili lilishafungwa.

Sonderjyske ilimsajili Okwi Julai 2015 kutoka Simba kwa mkataba wa miaka mitano uliotakiwa kumalizika mwaka 2020 ambapo tangu amesajiliwa Okwi alicheza mechi nne tu za Ligi Kuu ya Denmark na mbili za kombe la DBU ambapo alifunga mabao mawili.

Simba pia iliwahi kumuuza Okwi Etoile du Sahel ya Tunisia mwaka 2013 kwa dola za Marekani 300,000 kabla ya kusajiliwa na Yanga alipocheza kwa muda mfupi na kurejea Simba.

Okwi ni mshambuliaji kipenzi cha wanasimba kutokana na mafanikio aliyoipatia timu hiyo ambapo jana baada ya Manara kuweka suala lake kwenye mitandao ya kijamii, karibu mashabiki wengi wa soka walikuwa wakimzungumzia.

Pitia Hapa Ratiba ya Tukio Zima la Kuapishwa kwa Rais wa 45 wa Marekani Donald Trump Leo..!!!

$
0
0
483208412-real-estate-tycoon-donald-trump-flashes-the-thumbs-up-jpg-crop-promo-xlarge2Mshindi wa uchaguzi mkuu wa mwezi Novemba Donald Trump anatarajiwa kuapishwa kuwa rais wa 45 wa Marekani leo Ijumaa tarehe 20 Januari, 2017.

Bw Trump wa Chama cha Republican anatarajiwa kuapishwa mbele ya watu 750,000 mbele ya majengo makuu ya bunge la Marekani, Capitol Building, Washington D.C.

Kisheria, rais anafaa kuapishwa kabla ya saa 6:00 mchana saa za Amerika Mashariki ambazo Afrika Mashariki ni saa mbili usiku.

Hii hapa ni ratiba fupi ya matukio yanayotarajiwa siku hiyo.

Saa 17:30 (Saa za Afrika Mashariki) Wanamuziki walioalikwa wataanza kutumbuiza.
19:30 Hotuba za kufungua sherehe zitaanza kutolewa.

20:00 Muda mfupi kabla ya saa Mbili Afrika Mashariki Donald Trump atalishwa kiapo cha kuwa rais wa Marekani na Jaji wa Mahakama ya Juu John Roberts.

Baadaye, kutakuwa na msafara baada ya sherehe ya kuapishwa ambao utaanza katika vidato vya jumba la Capitol Building kuelekea ikulu ya White House kupitia barabara maarufu ya Pennsylvania Avenue.

Bw Trump na mkewe Melania baadaye watacheza densi katika matamasha matatu, mawili katika ukumbi wa mikutano wa Walter E Washington na jingine katika ukumbi wa Jengo la Makumbusho ya Taifa.

Miaka minane iliyopita, Rais Obama alipokuwa anaapishwa kura rais, waliohudhuria walikuwa 1.8 milioni.
Siku moja baada ya kuapishwa kwa Bw Trump, wanawake takriban 200,000 wanatarajiwa kuandamana Washington DC na miji mingine kumpinga Bw Donald Trump.

Hillary Clinton na mumewe Bill wamethibitisha kwamba watahudhuria sherehe hiyo, sawa na George W Bush na mkewe Laura.

Wamesema wanataka “kushuhudia kukabidhiwa madaraka kwa rasi mwingine kwa njia ya amani.”

Rais mwingine wa zamani Jimmy Carter atahudhuria pia, lakini George HW Bush, 92, na mkewe Barbara hawataweza kwa sababu za kiafya.

Hatarii!! Waziri wa Mkapa Ashusha Kombora Zito Juu ya Urais wa Zanzibar...!!!

$
0
0

MWANASIASA mkongwe na waziri katika serikali ya awamu ya tatu, Ali Ameir Mohamed, ameibua hoja nzito kuhusu urais wa Zanzibar huku akipinga suala la uongozi wa kurithishana.

Katika hoja hiyo ambayo imekuja wakati kukiwa na madai ya baadhi ya Wazanzibari wenye historia kuanza kampeni za chini chini kwa ajili ya kugombea Urais 2020, Ameir amesema si busara kumpata kiongozi wa ngazi yoyote ya kisiasa au serikali kwa kigezo kwamba baba, babu au bibi yake alikuwa ama Rais, Mwakilishi, Mbunge au Mtendaji wa chama. 

Badala yake, Ameir ametaka kiongozi apatikane kutokana na uchapakazi, uzalendo, ufahamu, uhusiano na uwezo binafsi.

“Wakati wa kumtafuta na kumpata kiongozi kwa sababu ya Ukaskazini, Ukusini, Upemba, Uunguja au Uumjini wake, umepita na usikubalike tena kama kigezo cha msingi chenye umuhimu na maana kabla ya kiongozi mhusika hajakabidhiwa dhamana ya uongozi,” alisema Ameir ambaye aliwahi kuwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Habari na Siasa).

Akizungumza jana  nyumbani kwake Donge, mkoa wa Kaskazini Unguja, alisema kwa miaka mingi wakati Zanzibar ikitawaliwa kisultani, kiongozi hakupatikana kwa sifa, uwezo wake, elimu au uaminifu wake bali kwa sababu tu alitoka katika ukoo wa kifalme.

"Kwa muda mrefu baadhi ya watu hususan baada ya Mapinduzi ya Zanzibar mwaka 1964, ilijengeka nadharia kuwa Rais lazima apatikane kwa asili ya maeneo. Zama hizo zimekwisha, amepatikana toka Mjini, Kusini, Kaskazini na Pemba, sasa sifa, uwezo binafsi, uchapakazi, uzalendo, upeo na ujasiri ziwe ndizo sifa za msingi," alisema.

Pia alisema serikali za vyama vya TANU na ASP, baada ya Uhuru na Mapinduzi, zilipiga marufuku tawala za kichifu, kisultan na kimwinyi hatimaye ikafunguliwa milango ya demokrasia, kuundwa kwa katiba kwa mujibu wa sheria bila kutazama nasaba, rangi, kabila au imani ya dini.

Kwa mantiki hiyo, alisema haipaswi mtu kupewa madaraka yoyote kwa kigezo cha baba, bibi au babu yake aliwahi kushika wadhifa fulani na haitakuwa haki akanyimwa mtu anayeonekana anatosha kivigezo kwa sababu huko nyuma mtu mmoja katika familia yake alishika wadhifa fulani. 

"Kusudio la kuundwa katiba za Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na (ya) Zanzibar hatimaye kuwepo kwa sheria zake ni kutoa haki katika muktadha wa usawa, demokrasia na wajibu. Azma yoyote au ishara ya kurudisha usultani au uchifu ipingwe bila muhali.” 

Ameir alisema kiongozi anayepatikana kwa sababu ama ya ukabila, udini, asili au nasaba hawezi kuwa na nafasi au kutazama maslahi mapana kulingana na matakwa ya dunia ya sasa wala vyeo au madaraka ya kisiasa na utawala yasitegemee nguvu za fedha, urithi au nasaba kwani mnaweza kujikuta mkirudi mahali mlikokukataa.

Pia mwanasiasa huyo mkongwe alisema kuendeleza ukabila, asili au mgombea wa ngazi yoyote aungwe mkono kwa minajili ya misukumo hiyo, alionya akisema hiyo si msingi iliyowekwa na waasisi wa taifa kwa mustakabali wa kukuza dhana ya maendeleo ya kisiasa, kiuchumi, kiutamaduni na demokrasia.

"Alipatikana Rais Julius Nyerere kwa sifa, uwezo na uzalendo wake, akaja Mzee Ali Hassan Mwinyi, akafuata Benjamin Mkapa, baadaye Dk. Jakaya Kikwete na sasa yupo Rais Dk. John Magufuli kwa msingi ile ile iliyowekwa ambayo imelipatia heshima ya juu taifa letu,” alisisitiza.

MACHO MAKINI

Dhamana ya uongozi wa juu, kwa mujibu wa Ameir, inahitaji kwanza mtu apimwe na wenzake wanaomtazama kwa macho makini na utayari wake badala yeye mwenyewe au wapambe wake kuanza kupitapita na kumpiga debe mitaani wakimsemea anatosha au anafaa.

Ameir alisema heshima inayopewa Tanzania na mataifa mbalimbali duniani ni kutokana na uongozi wake wa juu unavyoweza kuchemsha bongo, kutafakari kwa kina au kupitisha uamuzi na kuthubutu kusema fulani amekiuka taratibu na maadili, hivyo hastahili hatimaye akaondolewa bila kuutazama uso au rangi yake.

"Uamuzi au hatima yenye kubeba dhamana ya maisha na uhai wa binadamu unahitaji sana tahadhari na umakini, mkiendesha mambo ambayo nyeti kienyeji na kwa urahisi huku mkitazamana usoni na kuoneana aibu, hamtafika mbali," alionya mwanasiasa huyo nguli. "Mtajikuta siku moja mnaharibikiwa."

Mtazamo wa mwanasiasa huyo mkongwe Zanzibar umekuja siku chache tangu Rais Dk. Ali Mohamed Shein kuonya wanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wanaojinadi chinichini kuwania urais katika uchaguzi mkuu ujao kuacha kufanya hivyo.

Akizungumza katika mahojiano maalumu ya maadhimisho ya miaka 53 ya Mapinduzi ya Zanzibar na televisheni ya Azam, Rais Shein alisema wanaotamani urais wajue muda bado.

Mwendo wa Kupinga Tuu!! CHADEMA Kwenda Mahakamani Kuzuia Uteuzi wa Wabunge Wapya Uliofanywa na Magufuli

$
0
0

BARAZA la Wanawake la Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Bawacha), limesema linakusudia kwenda mahakamani kuomba tafsiri ya sheria kuhusu uhalali wa Rais John Magufuli kuteua wabunge wawili wanaume wiki hii.

Wabunge walioteuliwa Jumatatu ni Mwenyekiti wa Taifa wa Jumuiya ya Wazazi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Abdallah Bulembo na msomi wa sheria kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Prof. Palamagamba Kabudi.

Mwenyekiti wa Bawacha, Halima Mdee, aliwaeleza waandishi wa habari jijini hapa jana kuwa hatua hiyo ya Rais, inakiuka matakwa ya sheria inayoelekeza kutenga nafasi maalum kwa wanawake.

Mdee ambaye pia ni mwanasheria na Mbunge wa Kawe, alinukuu baadhi ya vifungu vya sheria akisema katika nafasi 10 za uteuzi alizopewa Rais kisheria, anatakiwa kutenga nafasi zisizopungua tano kwa wanawake, jambo alilodai limekiukwa na Rais. 

Kwa mujibu wa Mwenyekiti huyo wa Bawacha, mpaka sasa Rais ameshazidisha idadi ya wanaume inayozidi nusu ya nafasi yake aliyotengewa kisheria ambayo ni wabunge 10.

Mdee alisema watawasilisha dai hilo mahakamani kupitia hati ya dharura kuiomba itoe zuio la wabunge hao wapya kuapishwa.

Kwa upande wake, Mbunge wa Bunda Mjini ambaye pia ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema, Esther Bulaya, alisema suala hilo linawahusu wanawake wote wakiwamo wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), na kuwataka waungane kudai mahitaji hayo ya Katiba.

“Hadi sasa, Rais Magufuli ameteua wabunge wawili wanawake akiwamo Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi, Prof. Joyce Ndalichako na Naibu Spika wa Bunge, Dk. Tulia Ackson kati ya wabunge wanane aliokwisha kuwateua... wanawake wote tuungane katika kudai haki yetu ya Kikatiba, hivyo UWT na Chama cha Wabunge Wanawake, wajitokeze," alisema Bulaya.

Yeleuwii!! Eti Huyu Ndiye Pacha wa Nay wa Mitego,Embu Tazama Hapo Chini Picha Zake kisha Utupe Maoni yako..!!

$
0
0
ney-1
Emmanuel Elibariki ‘Nay wa Mitego’.

Baada ya kuibuka msanii chipukizi wa Bongo Fleva anayefanana sana kwa sura na msanii kutoka WCB, Harmonize kiasi cha kubatizwa jina la ‘Pacha wa Harmonize’, Harmorapa, katika mitandao ya kijamii inasambaa picha ikimuonesha pacha wa msanii wa Bongo Fleva, Emmanuel Elibariki ‘Nay Wa Mitego’, aliyebandikwa jina la ‘Ney wa Mitego Rapa’.screenshot_2017-01-20-06-17-50-1
Picha ya utani mtandaoni  iliyofananishwa na Ney wa Mitego (kushoto) na (kulia) ni Emmanuel Elibariki ‘Nay Wa Mitego.

Mashabiki wa Ney wa Mitego hawajapendezwa na picha ya pacha wa Ney wa Mitego, japo ni utani mashabiki hao wamedai inamdhalilisha Ney true boy.

Mpaka muda huu Ney wa Mitego hajatoa tamko lolote juu ya picha hiyo ya pacha wake mtandaoni.

Ezekiel Wenje Ashinda Uchaguzi wa Uenyekiti CHADEMA Kanda ya Ziwa..!!!

$
0
0
 
BAADA ya kuwa nje ya ulingo wa siasa takribani mwaka mmoja, hatimaye mbunge wa zamani wa Nyamagana, Ezekiel Wenje amechaguliwa kuwa Mwenyekiti wa Chama hicho Kanda ya Ziwa Victoria.

Wenje alitangazwa juzi kupitia uamuzi wa Kamati Kuu ya Chadema kuwa mgombea uenyekiti wa chama hicho kabla ya kuibuka mshindi katika uchaguzi uliojumuisha wagombea kutoka mikoa ya Geita, Mwanza na Kagera yenye majimbo ya uchaguzi 25.

Mbunge huyo wa zamani alikuwa akichuana na Meya wa Manispaa ya Bukoba Mjini, Chifu Kalumuna ambapo katika uchaguzi huo uliofanyika juzi saa tatu usiku, Wenje aliibuka mshindi.

Hadi juzi jioni wagombea wanne ndio waliotajwa kuwania nafasi hiyo, akiwamo aliyewahi kuwa Mhariri Mtendaji wa Gazeti la Tanzania Daima, Ansbert Ngurumo, ambaye katika uchaguzi huo alihamishiwa kugombea nafasi ya Umakamu Mwenyekiti na kuibuka mshindi.

Awali, wagombea wengine wa nafasi hiyo akiwamo aliyekuwa Mwenyekiti wa Kanda hiyo, Peter Makere na Ofisa wa Chama hicho, Tungaraza Njugu waliondolewa kuwania nafasi hiyo.

Akizungumzia kuchaguliwa kwake kushika nafasi hiyo, Wenje alisema: “Nitafanya kazi kwa kushirikina na viongozi wenzangu kuhakikisha tunaijenga Kanda ya Ziwa. Tutahakikisha tunashinda katika uchaguzi ulio mbele yetu, kasi yangu niliyokuwa nayo nitaendelea nayo hiyo hiyo.”

Itakumbukwa kuwa katika uchaguzi wa mwaka jana, Wenje aliyekuwa na nguvu katika jimbo la Nyamagana aliangushwa na Stanslaus Mabulab wa CCM.

Katika hatua nyingine, Mbunge wa Viti Maalumu Mwanza, Suzan Masele aliyekuwa akigombea nafasi ya uhazini aliangusha na Bugomba Mzuba.

Unaikumbuka Ile Story ya Madee ya Kupora Simu,Sasa Sikia Alivyojitetea Juu ya Tukio Hilo..!!!

$
0
0

Msanii wa bongo fleva Madee amesema hajutii matusi yanayotukanwa kupitia  mitandao ya kijamii kuwa amepora simu kwa kuwa wanaomtukana hawaujui ukweli na wakiujua watatulia.

Akionge kupitia eNewz Madee amesema hajapora simu bali alikuwa anadai pesa ambayo aliitoa kwa
 ajili ya kufanyiwa kazi na badala yake haikufanyika jambo lililomfanya aende kwenye vyombo vya sheria kwa ajili ya kurudishiwa pesa yake, na ndipo hayo yakatokea.

"Baada ya kuona pesa yangu ipo tu imekaa hafanyi kazi yoyote, nikafuatailia sheria, nikaenda polisi, nikasaidiwa kupata haki yangu, nashukuru nimepata haki yangu, wala sijutii kinachoendelea, sasa mi naweza kupora simu rafiki yangu, mi natumia simu yangi iPhone 7 na hiyo simu nayoambiwa nimepora ni S4, halafu kama ni kupora nisingeenda na polisi" amefafanua Madee

 Pia Madee amesema pesa yake huwa haipotei hata kama ikiwa imechukuliwa na maiti. 

Hata hivyo Madee amesema uongo huwa hauishi muda mrefu hivyo hawalaumu  wale ambao wamemtukana kwa kuwa hawaujui ukweli na anaamini kuna siku watu wote wataujua ukweli.

Mzee Jangala Awachana Wasanii wa Kiume Wanaovaa Nguo za Kubana na Kutoboa Masikio..!!!

$
0
0

Mkongwe wa sanaa za maigizo nchini Mzee Jangala amewachana wasanii wa kiume wanaovaa nguo zinazobana, kutoboa masikio na kuonesha maumbile yao.

Akiongea kupitia eNewz amesema vijana wanapaswa kujitambua na kuelewa maana ya utandawazi na siyo kuiga mambo mbalimbali ikiwemo kukaa uchi mbele za watu wazima kubadilisha maumbile yao halisi na kudai kuwa wanafuata utandawazi na kupotosha jamii zima.

Hata hivyo Mzee Jangala hakusita kuwasihi wasanii wa kizazi kipya kujitambua na kufanya mambo ya msingi katika jamii kwa kuwa wao ni watu ambao wana mashabiki ambao wanawaufatilia maisha yao na kuiga kila kinachofanywa na watu maarufu.
 

Ubuyu wa Moto Moto:Chale 21 za Diamond Zazua Mjadala Mzito,Watu Wahoji Juu ya Kazi Zake Kugubikwa na Ushirikina.!!

$
0
0
dai1
Daimond Platnumz
 Alama 21 zinazodaiwa ni chale zinazopatikana mgongoni mwa mwanamuziki Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ zimezua mambo baada ya juzikati picha yake kutupiwa mtandaoni ikizionesha kwa uwazi na kuibua mjadala mzito.

Picha hiyo iliyotupiwa mtandaoni ilimuonesha Diamond akiwa kwenye moja ya shoo alizofanya hivi karibuni huku akizungushiwa eneo ambalo lilionekana kuwa na chale, jambo lililowafanya wadau kibao wazijadili.

Mmoja wa mashabiki hao aliandika hivi: “Duh! Huyu jamaa hakamatiki aisee, kwenye shoo zake ni nyomi, anang’ara kimataifa, utajiri wake usiseme, au ndiyo tuseme hizi chale zake alizochanjwa ndiyo sababu?

“Yaani kama ni hivyo na mimi aniambie tu kachanjwa wapi ili na mimi niende kwa huyo mganga wake.” dai-3
Daimond Platnumz
Mwingine akaandika hivi: “Acheni zenu, huyu Mond ana nyota yake tu, hizo chale inawezekana ilikuwa ni tiba ya kawaida.

Akizungumza  mmoja wa wasanii anayefanya poa licha ya nyota yake kutong’ara sana, D-Malick alisema:

“Unajua nasikia tu kwamba huwa wasanii wakubwa wanaendaga kwa wataalam ‘kutengenezwa’ ili washaini, niliona picha moja inaonesha Diamond akiwa amechanjwa chale mgongoni, aisee kama ndizo zinamfanya awe na mafanikio hayo makubwa ipo siku nitamfuata anielekeze na mimi niende.”

  jitihada za kumtafuta Diamond kuzungumzia mjadala huu ulioibuka kuhusiana na chale zake zikihusishwa na kung’ara kwake lakini hakuweza kupatikana mara moja.
dai-2
Daimond Platnumz
Hata hivyo, siku za nyuma Diamond aliwahi kuongea  na kusema kwamba, madai kuwa kufanya kwake vizuri kwenye muziki kunatokana na mambo ya kishirikina siyo kweli bali juhudi binafsi ndizo zilizomfikisha mahali alipo.

“Mafanikio yangu hayatokani na mambo ya kishirikina, juhudi na maarifa ndiyo siri ya mafanikio yangu,” aliwahi kusema hivyo Diamond.
Viewing all 104712 articles
Browse latest View live




Latest Images