Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104785 articles
Browse latest View live

Habari Picha:Rais wa Uturuki Alivyopokelewa na Mwenyeji Wake Rais Magufuli Ikulu Jijini Dar es Salaam..!!!

$
0
0

Rais wa Jamhuri ya Uturuki Mhe Recep Tayyip Erdogan na mkewe wakipokea mashada ya maua kutoka kwa watoto walipowasili Ikulu jijini Dar es salaam leo Januari  23, 2017 kwa mapokezi rasmi na mazungumzo na mwenyeji wao Rais Dkt John Pombe Magufuli.
FULL 1
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli na mkewe Mama Janeth Magufuli wakiwalaki Rais wa Jamhuri ya Uturuki Mhe Recep Tayyip Erdogan na mkewe Emine Erdogan walipowasili Ikulu jijini Dar es salaam leo Januari  23, 2017 kwa mazungumzo
FULL 2
FULL 3
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli na mgeni wake Rais wa Jamhuri ya Uturuki Mhe Recep Tayyip Erdogan wakipiga ngoma Ikulu jijini Dar es salaam leo Januari  23, 2017
FULL 4
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli na mkewe Mama Janeth Magufuli wakiwazawadia Kinyago cha Umoja na Mchoro wa Mlima Kilimanjaro Rais wa Jamhuri ya Uturuki Mhe Recep Tayyip Erdogan na mkewe Emine Erdogan walipowasili Ikulu jijini Dar es salaam leo Januari  23, 2017 
FULL 5
Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli na mke Rais wa Jamhuri ya Uturuki Mama  Emine Erdogan wakipeana mikono baada ya maongezi  Ikulu jijini Dar es salaam leo Januari  23, 2017 
FULL 7
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli na akiongea katika kongamano la wawekezaji wa Tanzania na Uturuki katika ukumbi wa BoT jijini Dar es salaam  leo Januari  23, 2017
FULL 6
 Rais wa Jamhuri ya Uturuki Mhe Recep Tayyip Erdogan  akiongea baada ya yeye na mwenyeji wake Rais Dkt Magufuli ushuhudia uwekaji saini mikataba mbalimbali ya ushirikiano kati ya serikali ya Tanzania na Uturuki Ikulu jijini Dar es salaam leo Januari  23, 2017 
FULL 8
Rais wa Jamhuri ya Uturuki Mhe Recep Tayyip Erdogan  akiongea katika kongamano la wawekezaji wa Tanzania na Uturuki katika ukumbi wa BoT jijini Dar es salaam  leo Januari  23, 2017
FULL 10
Rais wa Jamhuri ya Uturuki Mhe Recep Tayyip Erdogan  akiongea na mwenyeji wake Rais Dkt John Pombe  Magufuli katika kongamano la wawekezaji wa Tanzania na Uturuki katika ukumbi wa BoT jijini Dar es salaam  leo Januari  23, 2017
FULL 9
Rais wa Jamhuri ya Uturuki Mhe Recep Tayyip Erdogan  na mwenyeji wake Rais Dkt John Pombe  Magufuli wakishuhudia ubadilishanaji hati baada ya kusaini baina ya mwenyekiti wa Wafanyabiashara wa sekta binafsi Dkt Reginald Mengi na kiongozi wa msafara wa wafanyabiashara wa Uturuki katika kongamano la wawekezaji wa Tanzania na Uturuki katika ukumbi wa BoT jijini Dar es salaam  leo Januari  23, 2017
PICHA NA IKULU

Tanzania na Uturuki Zasaini Mikataba Tisa ya Makubaliano ya Kiuchumi..!!!

$
0
0

Serikali ya Tanzania na Serikali ya Uturuki zimesaini mikataba tisa ya makubaliano ya kiuchumi inayolenga katika kuimarisha uhusiano na ushirikiano wa maendeleo baina ya nchi hizo.

Mikataba hiyo inahusisha sekta za uchukuzi, mawasiliano, habari, elimu, utalii, utafiti, viwanda, afya na ulinzi.
Akizungumza mara baada ya kusaini kwa mikataba hiyo  leo Ikulu Jijini Dar es Salaam, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Magufuli alisema ujio wa Rais wa Uturuki na ujumbe wake ni kielelezo cha ukuaji wa mahusiano baina ya Tanzania na Uturuki katika nyanja ya biashara na kimaendeleo baina nchini hizo.

Rais Magufuli alisema katika mazungumzo yake aliyofanya na Rais Recep Erdogan kuhusu ujenzi wa Reli ya Standard Gauge nchini, alimjulisha kiongozi huyo kuwa miongoni mwa wakandarasi walioomba zabuni ya ujenzi wa reli hiyo kuwa ni kampuni kutoka Uturuki, hivyo endapo itashinda zabuni hiyo itasaidia kukuza uhusiano uliopo baina ya nchi hizi mbili.

Aidha, Rais Magufuli alisema kuwa, Serikali ya Tanzania inatarajia kuomba  mkopo kupitia Benki ya Exim ya Uturuki katika kujenga sehemu ya kipande cha ujenzi wa reli hiyo.

Rais magufuli alisema Tanzania inaendelea kunufaika na uwepo wa Shirika la Ndege la Uturuki kwa kufanya safari zake za moja wka moja kutoka nchini Uturuki, kwa kuwa utasaidia kuongezeka kwa idadi ya watalii nchini na hivyo kukuza uchumi wa nchi hizo.

Kwa upande wake Rais wa Uturuki, Recep Erdogan alisema kuwa uwepo wa mikataba hiyo baina ya Tanzania na Uturuki itasaidia kupata matokeo mazuri ya uhusiano pamoja na fursa mbalimbali za ushirikiano katika nyanja ya Kilimo, Utalii, Ulinzi, Reli ambazo zitawezesha kukuza uchumi wa mataifa hayo.

Rais Erdogan alisema kuwa Uturuki imelenga kukuza ushirikiano uliopo baina yake na  Tanzania kupitia makongamano ya wafanyabiashara yenye malengo ya kukuza uchumi, kuongeza ajira pamoja na kukuza ujasiriamali baina ya Tanzania na Uturuki.

“Kiwango cha Biashara ya uwekezaji katika nchi ya Uturuki ni Dola za kimarekani 150 ambapo lengo letu ni kufika Dola za kimarekani 500” alisema Rais huyo.

Aidha Rais Erdogan alisisitiza kuwa kufanya kazi kwa pamoja kutasaidia nchi hizi kusonga mbele na kufanikiwa katika nyanja mbalimbali.

Nae Waziri wa Maliasili na Utalii Prof. Jumanne Maghembe alisema kuwa makubaliano ya mkataba baina ya Tanzania na Uturuki katika Sekta ya Utalii yatasaidia katika kutangaza vivutio vilivyopo nchini, kubadilishana wataalamu, kubadilishana taarifa na kuongeza idadi ya watalii nchini.

Prof. Magembe aliongeza kuwa makubaliano hayo yatakuza sekta ya utalii katika kuvutia uwekezaji wa katika maeneo ya hoteli, fukwe na mbuga za wanyama zilizopo nchini.  

Baada ya Madai ya Hoteli Yake Kudaiwa Kodi na Serikali,Mbowe Ambanga Kutoa ya Moyoni..!!!

$
0
0

MWENYEKITI wa Chadema, Freeman Mbowe, amesema atafunguka na kuzungumzia mambo yote yanayohusu deni linaloelezwa kuwa inadaiwa hoteli yake ya Aishi Machame atakapofika jimboni kwake Hai.

Mbowe ametoa kauli hiyo baada yakutakiwa azungumzie tuhuma zinazomkabili, baada ya Mkuu wa Wilaya ya Hai, mkoani Kilimanjaro, Gellasius Byakanwa kudai amekwepa kulipa kodi ya huduma ya biashara kwa miaka mitano.

Alisema kwa kipindi hiki hawezi kuzungumzia sakata hilo hadi atakapowasili katika jimbo lake la Hai ili kujua ukweli wa tuhuma hizo ambazo zimetangazwa na Mkuu wa Wilaya.

“Siwezi kuzungumza chochote, kwani sifahamu kinachoendelea. Lakini nikifika jimboni nitafunguka na kubainisha ukweli wa tuhuma hizo,” alisema.

Katika sakata hilo jipya la Hoteli ya Aishi Machame Mkuu wa wilaya Byakanwa alidai kuwa Hoteli hiyo iliandikiwa barua Januari 21, mwaka jana na kutakiwa kulipa kodi lakini barua hiyo haikujibiwa.

Mbali na barua hiyo kutojibiwa Byakanwa alidai kuwa Hoteli hiyo haijapeleka taarifa ya mauzo ya kila mwaka katika Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kwa miaka mitano kwani taarifa hiyo ingetumika kukadiria kodi.

Kutokana na madai hayo, Byakanwa aliamua kutoa siku 14 kwa Uongozi waHoteli hiyo kulipa kodi hiyo ya huduma ya biashara inayofikia sh. milioni 13.5, vinginevyo huduma hiyo itasitishwa.

Katika hatua nyingine Byakanwa amesitisha shughuli za kilimo katika shamba linalimilikiwa na Mbowe kwa madai kuwa lipo ndani ya chanzo cha maji yam to Weruweru.

Hivyo aliagiza Baraza la Taifa la Usimamizi wa Mazingira (NEMC) kufanya tathmini ya uharibifu wa mazingira katika eneo hilo uliofanywa na Mbunge wa Hai ili hatua zichukuliwe.

Pia Mkuu wa Wilaya ya Hai Byakanwa aliwataka maafisa Maliasili wa Wilaya kufanya tathmini ya miti iliyokatwa bila kibali na kuleta kiasi cha faini ndani ya siku 14 ili hatuya zifanyike.

“Huyu ni kiongozi wa kitaifa tena kioo cha jamii anapaswa kuwa mfano kwa wananchi anaowangoza, sfanyi hilo kwa kumwonea mtu hali nazingatia sheria,” alisema.

Njaa Yaichanganya Kenya..Rais Kenyatta Apiga Marufuku Mahindi Kuuzwa Ng'ambo

$
0
0
President Uhuru Kenyatta has banned maize exports to the country with immediate effect.

This follows ravaging drought in many parts of the country that has affected the grain reserves.

Uhuru said a stern action will be taken against those who will be found exporting grain or hoarding stocks in order to sell at inflated prices during the dry season.

''We will not allow any trader to buy maize in large amount so as to store and eventually cash in following the ravaging drought in the country,'' the president said on Friday during a tour of Isiolo, which is among the drought stricken counties in the country.

According to the government, drought is worst in the Coastal region, specifically in Kilifi, Kwale, Tana River and Taita Taveta counties.

Other counties that have been hit include Kitui, Garissa, Mandera, Marsabit, Makueni, Samburu and Wajir.

Uhuru said the national government will revise its budget in order to address the drought menace in the country.

“I'm also urging county governments to relook their budgets in order to cushion Kenyans against the effects of the drought,” he said.

The country consumes about 29 million bags of maize every six months but there is biting shortage due to poor rains which reduced harvests and affected stocks in the national grain reserve in the past season.

Reports from the Ministry of Agriculture indicates the country has 21 million bags of maize as of now, translating to a deficit of eight million bags.

The stocks include those held by farmers and the Strategic Grain Reserve and can only last until June.

Agriculture Cabinet Secretary Willy Bett however said there is no plan to import maize since there is enough stock of other types of foods grains and legumes.

The CS said the government will purchase two million bags of maize from farmers before end month to increase the stocks.

The government is offering Sh3000 for a bag of maize, which the CS said is “fair enough”.

“So far, we have bought 1.4 million bags of 90 kilogrammes each,” he said noting purchases would have been higher if farmers were not hoarding maize.

Hii Hapa Video ya Mtangazaji wa Clouds Fm Diva Akidendeka Ndani ya Gari na Underground wa Bongo Flevai(+18 Video)

$
0
0

Mtangazaji wa Kipindi cha Ala za Roho cha Clouds Fm,Loveness Love maarufu kama Diva mapema hivi karibuni akiwa na anayedaiwa kuwa ni mpenzi wake waliweka video kwenye mitandao ya kijamii ianyowaonyesha wakilana denda.

Diva ambaye katika video hiyo ameonekana akiwa amelegea kimahaba alikuwa akimbusu busu mpenzi wake hali ambayo ukiitazama huenda ikaamsha hisia zako,zaidi tazama video hiyo hapooo


Diva Anaswa Akila Denda na Dogo Aliyemzidi Umri...

$
0
0
Tazama Video Jinsi Diva Alivyoweka Video kwenye Ukurasa wake wa Instagram Akidendeka na Mwanamiziki Henry Muziki Ambae ni mdogo wake sana kiumri

VIDEO:

P-Funk: Yule Angekuwa Binti Yangu Kwenye ile Video..Ningemzibua Mtaro Aliyemfanyia Kitendo Hicho,

$
0
0
Akihojiwa kwenye kipindi cha "on point" kuhusu video ilisambaa akionekana binti akifanya mapenzi na kufanishwa na binti yake anaitwa Paula aliezaaa na msanii wa bongo movies, Kajala, Producer P-Funk amesema binti huyo anaeonekana sio mwanae Paula.

"Umeona nimekaa kimya ujue yule sio binti yangu. Yaani angekuwa mwanangu ungeona video mbili , ya binti yangu na ya yule jamaa nae akiwa analiwa, yaani watu wanazibua mtaro".

Kwanini Kipindi cha Orijinal Komedi Hakionyeshwi Kwenye Luninga Siku Hizi? Joti Asema Haya

$
0
0
Kwako mfwatiliaji wa mabingwa wa kuchekesha wanaoishikilia rekodi ya wachekeshaji waliotazamwa sana kwenye TV nchini Tanzania kuanzia time hiyo ya Ze Comedy mpaka Orijino Komedi walivyokuwa wanawafanya watu wawahi TV zao kila Alhamisi jioni.

Ni kitambo kidogo hatujawaona Orijino Komedi kwenye TV (TBC 1) na inawezekana maswali tuliyonayo ni mengi lakini hakuna hofu tena maana tumempata Joti na amekubali kuongelea kwa ufupi.

‘Kama kundi tuna taratibu zetu na ndio maana tumejaribu kutumia muda wa mwaka mmoja kupumzika maana toka tuanze kufanya kazi hatujawahi kupumzika, tulivyopumzika pia sio kukaa kimya tukaangalia project za kila mtu binafsi na ndio maana unaona kila mtu na shughuli zake‘ – Joti

‘Ukimfatilia Mpoki kuna shughuli zake anafanya na inajulikana, Masanja pia vivyo hivyo… na mimi nimefungua Youtube channel yangu ya Joti TV, nafikiri mwaka huu tunaweza kurudi kazini pia.

Je mazungumzo ya huyu bwana mdogo yana ukweli? au baada ya huu utawala wa kiimla walipigwa stop,mpaka watakapopangiwa vyakuigiza. karibuni kwa mjadala

Tanzania na Uturuki Kubebana Kiuchumi,Rais wa Uturuki Asimulia Alivyotaka Kupinduliwa..!!

$
0
0

RAIS wa Uturuki, Recep Tayyip Erdogan ameimwagia neema Tanzania ambapo takribani mikataba tisa inayogusa maeneo ya kilimo, afya, elimu, diplomasia, uchukuzi, habari, ulinzi na viwanda imesainiwa.

Aidha, nchi hiyo ya barani Ulaya pamoja na Tanzania zimekubaliana kuongeza thamani ya biashara baina yake kutoka dola za Marekani milioni 160 mpaka milioni 190 za sasa hadi kufikia dola za Marekani milioni 250.

Pamoja na hayo, Erdogan ameihakikishia Tanzania na Afrika kwa ujumla kuwa sera ya nchi yake kwa Afrika ni usawa na si sera zinazofurahisha upande mmoja na kuukandamiza mwingine. Marais hao wawili akiwemo Rais John Magufuli, walishuhudia mikataba hiyo tisa ikisainiwa na mawaziri wa pande zote mbili Tanzania na Uturuki Ikulu jijini Dar es Salaam.

Mikataba iliyosainiwa ni pamoja na mkataba wa ushirikiano baina ya Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL) na Shirika la Ndege Uturuki (Turkish Airline), ushirikiano baina ya Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) na Shirika la Utangazaji Uturuki na mkataba wa ushirikiano katika maendeleo baina ya nchi hizo mbili.

Mikataba mingine ni pamoja na ushirikiano katika sekta ya elimu na utafiti, ushirikiano baina ya Shirika la Viwanda Vidogo (SIDO) na Shirika la Viwanda vya Kati Uturuki na ushirikiano katika sekta ya utalii kwa nchi zote mbili.

Pia mikataba mingine iliyosainiwa ni ushirikiano katika viwanda na ulinzi, kwenye sekta ya afya na ushirikiano baina ya Chuo cha Diplomasia cha Tanzania na cha Uturuki.

Mawaziri wa Tanzania walishiriki kusaini mikataba hiyo ni Waziri wa Maliasili na Utalii, Profesa Jumanne Maghembe, Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Philip Mpango, Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu na Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi, Stella Manyanya.

Wengine ni Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Augustine Mahiga, Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Dk Hussein Mwinyi, Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Charles Mwijage na Mkurugenzi Mkuu wa TBC, Dk Ayoub Rioba.

Akizungumza katika shughuli hiyo, Dk Magufuli alimshukuru Rais Erdogan kwa kuichagua Tanzania kuwa nchi ya kwanza kuitembelea katika ziara yake Afrika, jambo lililosababisha nchi hiyo kumwagiwa neema ya mikataba tisa yenye lengo la kuboresha na kuimarisha sekta husika kwa nchi zote mbili.

“Katika kabila langu kuna methali inayosema ukiwa wa kwanza kunywa maziwa maana yake utakunywa mengi zaidi. Hili limejidhihirisha kupitia mikataba hii tuliyotiliana saini itakayonufaisha zaidi Tanzania,” alisisitiza Dk Magufuli.

Alisema hivi karibuni Tanzania imeteua Balozi wa Tanzania nchini Uturuki kwa mara ya kwanza, Profesa Elizabeth Kiondo, ikiwa ni ishara na msingi imara kuimarisha ushirikiano baina ya nchi hizo mbili hasa katika kushirikiana kibiashara na kiuwekezaji.

Rais Magufuli alisema anaamini kupitia ushirikiano huo mpya wa kidiplomasia nchi hizo zitaimarisha zaidi uhusiano wake kwa upande wa maendeleo kwani tayari katika mazungumzo aliyoyafanya na Rais Erdogan amemuomba kupitia Benki ya Exim ya Uturuki kuikopesha Tanzania fedha zitakazotumika katika ujenzi wa reli ya kisasa.

“Tanzania tuko kwenye mchakato wa ujenzi wa reli ya kisasa itakayounganisha nchi yetu na nchi nyingi za jirani. Kwa sasa tupo kwenye hatua ya kutafuta mkandarasi na nafahamu moja ya kampuni kutoka Uturuki imeomba kuijenga reli hii. Tuombe Mungu mfanikiwe katika hili,” alisema Dk Magufuli.

Aidha, alifafanua hali ya biashara baina ya Uturuki na Tanzania kuwa inazidi kuimarika kwani kwa sasa biashara imefikia kiasi cha dola za Marekani 190 na kampuni 30 za Uturuki zimewekeza nchini kwa thamani ya dola za Marekani 305.08 zilizotengeneza ajira 2,950.

“Nina uhakika kupitia ushirikiano huu, sasa tutaongeza kiwango cha biashara zetu kutoka dola za Marekani 190 hadi 250 na kuimarisha maeneo mengine ya uwekezaji. Uturuki ni nchi ya saba duniani kwa kuzalisha mazao ya kilimo hivyo kuja kwakwe nchini kwetu ambako kuna takribani asilimia 80 ya Watanzania wakulima, kutatunufaisha,” alifafanua.

Kwa upande wake, Rais wa Uturuki Erdogan alisema mazungumzo yake na Rais Magufuli yameonesha mafanikio makubwa baina ya nchi hizo mbili na yamegusa maeneo nyeti yanayowagusa wananchi ambayo ni elimu, afya, uchukuzi, diplomasia na viwanda.

Alisema katika ziara yake nchini ameambatana na wafanyabiashara takribani 150 ambao aliihakikishia Tanzania kuwa wako tayari kuwekeza katika nyanja mbalimbali, jambo ambalo pamoja na kuchangia katika uchumi lakini pia litaongeza ajira.

Aidha, aliahidi kuongeza fursa zaidi katika maeneo ya elimu na ulinzi ambayo nchi hiyo imekuwa ikitoa udhamini wa mafunzo. Kwa sasa takribani wanafunzi 4,500 hupata ufadhili wa kwenda kusoma Uturuki.

Akizungumzia mchango wa nchi hiyo kwa nchi za Afrika, Rais huyo alibainisha kuwa sera ya nchi yake kwa nchi za Afrika ni usawa hivyo makubaliano yote waliyoyasaini na kukubaliana kushirikiana yamelenga kuwaletea maendeleo wananchi wa Tanzania na Uturuki.

Alisema Tanzania imeingia makubaliano ya mikataba mbalimbali na Uturuki ikiwemo katika eneo la uchukuzi kupitia shirika la ndege la Uturuki ambalo kwa sasa ndio linalounganisha nchi zote za Afrika. “Tunataka kuwapa uzoefu, tumefanya hivi kwa sababu Tanzania ni nchi yenye amani, ukarimu, upendo na utulivu.

” Pamoja na hayo, Rais Erdogan alielezea tukio la kuponea chupuchupu kupinduliwa Julai 15, mwaka jana ambapo watu 240 walipoteza maisha na wengine 2,900 kujeruhiwa. “Nashukuru Mungu raia wa Uturuki waliitetea demokrasia ya nchi yao na napenda kuwataarifu kuwa tuna ushahidi wa kutosha kuwa waliofanya jaribio lile la mapinduzi ni wanachama wa chama cha kigaidi cha kundi la Fethullah,” alisema.

Alizionya nchi za Afrika na Tanzania kwa ujumla kuwa makini na kundi hilo kwani lipo katika nchi mbalimbali duniani ikiwemo Afrika. “Naamini rafiki yangu Magufuli atanisaidia katika hili, nchi yangu imejipanga kupambana na kundi hili kikamilifu,” alieleza.

Ushindi wa CCM Uchaguzi wa Marudio Wampa Kiburi Rais Magufuli,Arusha Dongo Upinzani..!!!

$
0
0

MWENYEKITI wa Taifa wa CCM, Rais John Magufuli amesema ushindi wa CCM wa ubunge na madiwani katika Uchaguzi Mdogo uliofanyika juzi nchini ni ishara ya ushindi wa chama chake katika uchaguzi ujao kutokana na wananchi kuonesha imani kwake na serikali yake.

Rais Magufuli aliyasema hayo kwa waandishi wa habari muda mfupi kabla ya kumpokea Rais wa Uturuki, Recep Tayyip Erdogan aliyefika Ikulu, Dar es Salaam jana akiwa kwenye ziara yake ya siku mbili nchini.

Rais Magufuli alisema ushindi huo ni kipimo cha utendaji wake kwa wananchi na hivyo umemuongezea ari ya kuwatumikia wananchi kwa moyo wake bila ya kujali changamoto mbalimbali zilizopo.

“CCM Oyee! Mnaonaje ushindi wa CCM? Hii inadhihirisha ni namna gani wananchi walivyo na imani na mimi na serikali yangu. Tumeshinda ushindi wa kishindo katika kata na Jimbo, wenyewe mmeshuhudia namna tulivyowapiga. Au mnasemaje?” Rais Magufuli aliwaambia waandishi wa habari na kisha akawashukuru na kuelekea eneo lake maalumu akimsubiria Rais wa Uturuki kwa ajili ya kumpokea.

CCM mbali ya kushinda kiti cha ubunge cha Dimani visiwani Zanzibar, imeshinda kata 18 kati ya kata 19 zilizofanya Uchaguzi Mdogo wa Udiwani juzi kutokana na sababu mbalimbali zikiwamo za kufa kwa waliokuwa wakishikilia nyadhifa hizo na kufutwa kwa matokeo kwa amri ya mahakama.

Kata ambazo CCM imeshinda ni Nyarenanyuki (Arumeru, Arusha), Isegehe (Kahama, Shinyanga), Nkome (Geita), Kiwanja cha Ndege (Manispaa Morogoro), Lembeni (Mwanga, Kilimanjaro), Ihumwa (Dodoma), Matevez (Meru, Arusha), Kimwani (Muleba, Kagera), Igombavanu (Iringa), Kijichi (Mbagala, Dar es Salaam), Ng’hambi (Dodoma), Kinampundu (Singida), Kasansa (Katavi), Malya na Kahumulo (Mwanza), Mkoma (Mara), Misugusugu (Kibaha, Pwani).

Aidha, CCM imeshindwa katika Kata ya Duru mkoani Manyara, ambako mgombea wa Chadema, Ali Shaaban ameibuka mshindi. Kwa upande wao, baadhi ya wasomi wamesema kwamba chama cha mapinduzi kimeshinda kutokana na kutekeleza ahadi za kuondoa kero za wananchi.

Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Dk Francis Michael alisema kwamba wananchi wa kada za chini wanaiamini CCM kwa sasa hivi kwa kuwa Rais John Magufuli amejikita kushughulikia masuala yanayowakera.

Alitoa mfano kwamba kitendo cha serikali kuondoa kero ya kodi katika mazao mbalimbali yamefanya wananchi wengi hasa wakulima waiamini Serikali ya Awamu ya Tano.

Pia alisema kitendo cha kupata huduma ya uhakika katika taasisi za serikali hasa hospitali tofauti na miaka ya nyuma ni jambo ambalo pia limechangia chama hicho kipate ushindi katika maeneo mengi ambako Uchaguzi Mdogo ulifanyika.

Aliongeza kuwa licha ya kuwepo watu ambao wanalalamika kuwa fedha hazipatikani, wanaolalamika sio wananchi wa chini bali ni watumishi ambao walizoea kuchukua rushwa na sasa mirija hiyo imekatika.

Pia alisema fedha imekosekana kwa wapiga dili ambao nao hawana athari katika masuala ya kura. Alitoa mfano kitendo cha Rais Magufuli kuzuia wamachinga wasihamishwe maeneo wanakofanyia biashara badala yake waachwe au watafutiwe maeneo mbadala kwanza pia yamesaidia kuwapa matumaini wananchi wa kawaida ambao ndio wapiga kura.

“Mimi naona kama Serikali ya Awamu ya Tano itaendelea na mwendo huu wa kushughulikia kero za wananchi sidhani kama wapinzani watafurukuta huko mbeleni,” alisema Dk Michael.

Naye Dk Eve Maria Semakafu alisema CCM imeshinda katika kata hizo kuliko vyama vya upinzani kwa sababu kata hizo nyingi zilikuwa zinaongozwa na CCM yenyewe na hivyo kushinda huko ni sawa na kurejesha kiti chao.

Pia alisema kata nyingi ambako CCM imeshinda ni vijijini ambako vyama vya upinzani havina mizizi na vingine havina ofisi jambo ambalo lifanya chama tawala kuwa na wafuasi wengi kuliko vyama vya upinzani.

Akizungumzia iweje CCM ishinde wakati maeneo mengi kuna njaa, Dk Semakafu alisema kwamba huko vijijini hakuna njaa bali maeneo ambayo yana kawaida ya ukame ndio upungufu wa chakula na sio kwa sababu ya Rais Magufuli.

Alisema maeneo ya Shinyanga, Mwanza, Dodoma, Singida na Mara kwa miezi ya kama hii ni kawaida kuwa na ukame hivyo akasema kwamba jambo hilo haliwezi kuwafanya wananchi wakichukie chama tawala kwa sababu ni kawaida yao.

“Mimi nimefanya utafiti katika maeneo hayo kwa miaka mingi, nafahamu ukame wa maeneo hayo, hivyo suala la njaa ni kwa wanasiasa na sio kwa wananchi,” alisema.

Wizara Nyingine Yahamia Dodoma...!!!

$
0
0

AWAMU ya kwanza ya watumishi 87 wa Ofisi ya Rais - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, inahamia Dodoma ikiwa ni utekelezaji wa ahadi ya Serikali ya Awamu ya Tano ya kuhamishia shughuli zote za serikali mkoani humo ifikapo 2020.

Hiyo inakuwa ni wizara ya pili kutangaza hadharani kwamba inahamia Dodoma baada ya mwishoni mwa wiki Wizara ya Katiba na Sheria inayoongozwa na Dk Harrison Mwakyembe kutangaza kuhamia Dodoma kwa viongozi wake wa juu kama ilivyobainishwa katika maelekezo ya kuhamia Makao Makuu ya nchi.

Akizungumza jana Dar es Salaam, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora), Angellah Kairuki alisema ofisi hiyo itafunguliwa rasmi mjini Dodoma Januari 30, mwaka huu.

“Nimewaita kuwafahamisha kwamba safari yetu ya kuhamia Dodoma inaanza rasmi sasa... Ahadi ya wizara zote kuhamia Dodoma aliitoa Rais John Magufuli wakati wa maadhimisho ya kumbukumbu ya Siku ya Mashujaa yaliyofanyika Julai 25, 2016,” alisema Kairuki.

Alisema baadaye Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa alitoa maelekezo na kuainisha utaratibu wa wizara na taasisi zote za serikali kuhamia makao makuu ya nchi mkoani Dodoma kwa awamu nne.

“Maelekezo hayo yalitaka awamu ya kwanza inayowahusu Mawaziri, Naibu Mawaziri, Makatibu Wakuu na Naibu Makatibu na baadhi ya watumishi ikamilike ifikapo Februari 28 mwaka huu...Waziri Mkuu alihamia Dodoma Septemba mwaka jana na wizara nyingine zimeendelea na maandalizi ya kutekeleza azma hii ya serikali,” alieleza.

Kutokana na hayo, Kairuki alisema ofisi yake imekamilisha maandalizi ya kuhamia Dodoma, na jana vifaa vya ofisi vya kundi la kwanza la watumishi wa ofisi hiyo vimesafirishwa kwenda Dodoma.

“Kundi hili la kwanza linahusisha uongozi wa juu wa wizara ukiwajumuisha Waziri, Katibu Mkuu na Naibu Katibu Mkuu, baadhi ya wakurugenzi, wakurugenzi wasaidizi, maofisa waandamizi na watumishi wengine ambao jumla yao ni watumishi 87 wanahamia Dodoma,” alibainisha waziri huyo.

Alisema ofisi yao itakuwa katika Jengo la ‘College of Humanities and Social Sciences’ katika eneo la Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) kama makao yake ya muda mpaka hapo itakapoelekezwa vinginevyo na anuani ya posta itakuwa ni Ofisi ya Rais-Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Sanduku la Posta 670, Dodoma.

Kairuki alisema wale wote wanaohitaji kukutana na Waziri, Katibu Mkuu na Naibu Katibu Mkuu wafike katika ofisi za Dodoma na kufuatia uhamisho huo masuala yote yanayohusu sera na sheria za utumishi wa umma na utawala wa utumishi wa umma kwa ujumla yatatekelezwa katika ofisi ya Dodoma.

Alisema kwa upande wa masuala ya mishahara, uendelezaji, raslimali watu, ukuzaji maadili, anuani za jamii, uchambuzi ushauri na utendaji kazi na huduma ya teknolojia ya habari na mawasiliano yataendelea kushughulikiwa na ofisi ya Dar es Salaam kwa sasa.

Serikali - Wanasiasa Wanaotangaza Uwepo wa Njaa Nchini Wakamatwe Mara Moja..!!!

$
0
0

NAIBU Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Hamad Masauni ameonya kuwa watu wakiwemo wanasiasa wanaoeneza taarifa za uongo za kuwepo kwa baa la njaa, ni kosa na wachukuliwe hatua ikiwemo kukamatwa.

Masauni amesema bado kuna watu wanajichukulia mamlaka ambayo sio yao na kueneza uongo kuwa kuna njaa nchini, hilo ni kosa kwa kuwa kwa kueneza propaganda hiyo kunaweza kusababisha uvunjifu wa amani nchini.

“Hizo ni propaganda za watu wasioitakia mema nchi hii ….. mtu anapofanya kosa lazima achukuliwe hatua …… Jeshi la Polisi liangalieni hili,” alisisitiza.

Masauni alitoa onyo hilo wakati wa ziara yake ya siku moja aliyoifanya jana mkoani Rukwa ambako Mkuu wa Mkoa wa Rukwa, Zelothe Steven alimhakikishia kuwa mkoa huo hauna njaa, bali una ziada ya kutosha.

“Nyie wenyewe mmemsikia mkuu wa mkoa (Zelothe) amethibitisha kuwa hakuna njaa mkoani hapa lakini sio hapa tu, pia mikoa ya Mbeya na Songwe wamenithibitishia kuwa hawana njaa,” alisema Naibu Waziri Masauni na kuongeza: “Sasa wapo wanasiasa uchwara wanaeneza propaganda kuna njaa, sio mamlaka yao kutangaza kuwa kuna njaa, kueneza uongo kama huo ni si sawa kwa kuwa kunaweza kusababisha uvunjifu wa amani nchini, wanastahili kuchukuliwa hatua ikiwemo kukamatwa,” alisisitiza.

Awali Mkuu wa Mkoa wa Rukwa, Zelothe alimweleza Naibu Waziri Masauni kuwa hali ya kiusalama katika mkoa huo ni shwari ambapo amani na utulivu umeshamiri kwa kuwa una chakula cha kutosha.

Miaka Mitano Baada ya Kufariki,Huu Hapa Ukweli Juu ya Kifo cha Patrick Mafisango kwa Saa 24 Kabla na Baada ya Ajali..!!!

$
0
0

USIKU wa Jumanne ya Aprili 15, 2012 vijana wawili wachezaji wa soka wanabishana kuhusu kuondoka mahali walipokuwa ili wakapumzishe miili yao baada ya pirika za kutwa nzima. Hao ni viungo wa soka, Ramadhan Chombo ‘Redondo’ na Patrick Tabu Mutesa aliyekuwa maarufu kama Patrick Mutesa Mafisango ambaye kwa sasa ni marehemu.

Kwa mujibu wa Redondo, Mafi sango alitaka waendelee kukaa katika klabu moja ya usiku kwa muda kidogo lakini kwa kuwa ilishakuwa usiku sana yapata saa 7:00, yeye alimsihi waondoke na kweli wakaondoka. Haikuwa rahisi kwa Mafisango kuondoka mahali hapo lakini ushawishi mkubwa wa Redondo uliwezesha wawili hao kuondoka na kurudi nyumbani kupumzika.mafisango7Wachezaji wakiwa wamebeba jeneza lenye mwili wa Mafisango.

KIONGOZI SIMBA ATOA FEDHA

Asubuhi ya Jumatano Apri- l i 16, 2012 akiwa ny- umbani kwake Chang’ombe jijini Dar es Salaam, Mafi sango aliletewa fedha na kiongozi mmoja wa Simba kwa ajili ya matumizi mbalimbali. Baada ya kupokea fedha hizo, Mafisango akiwa na Redondo alianza kulazimisha waanze kupata ‘moja moto moja baridi’ lakini mwenzake alikataa hadi watakapopata chakula cha mchana.

“Alionekana kutaka kinywaji sana lakini nilimsihi kwamba si vizuri kutumia kinywaji muda huo badala yake asubiri hadi tutakapopata chakula cha mchana kwanza,” anasema Chombo. Baadaye Mafi sango aliletewa gari Toyota Chaser GX 100 kwa ajili ya kulitumia siku hiyo, lakini mpwa wake Orly Ilemba na Ally Hassan ‘Bozy’ walitoka na gari hilo kwenda Magomeni. Baada ya kuwasubiri kwa muda mrefu, Mafi sango na Redondo waliamua kuwafuata Magomeni akina Orly baada ya kuona wanachelewa kurejea Chang’ombe na gari hilo.mafisango3Lari lakebaada ya ajali.

MAFISANGO APIGA USINGIZI WA AJABU

Walipofi ka Magomeni, Mafi sango na Redondo waliungana na akina Orly kisha wakalekea Kinondoni ambako walipata chakula lakini jambo la kushangaza baada ya kula, Mafi sango alilala usingizi mzito. “Wakati analala nikawaambia watu tuliokuwa nao kwamba wamuache apumzike na alilala usingizi mzito sana hadi alipozinduka baada ya kama saa mbili hivi,” anasema.

Kabla ya kula Mafi sango aliwarushia maneno akina Orly ambao hawakuonyesha hamu ya kula chakula hasa baada ya kuwasema kwa kuchelewa kuwafuata Chang’ombe.mafisang02AGAWA FEDHA NA KUAGA

Karibu muda mwingi wa mchana, Mafi sango alikuwa akitoa fedha au vinywaji kwa watu huku akisema kwa utani, kunyweni hamjui labda ndiyo tunaagana au maisha haya mafupi sana. Hata fedha alikuwa akitoa kwa baadhi ya watu aliokuwa akifahamiana nao na karibu wote alikuwa akiwapa na kuwaambia maneno hayo. 

“Sisi tuliona kama kitu cha kawaida lakini kumbe yeye sijui kuna kitu alihisi au la, lakini alikuwa akitoa fedha na kutamka maneno ya kuaga,” anasema Bozy.mafisango5SAFARI YA MAISHA CLUB

Mafisango alikuwa na asili ya DR Congo licha ya kuwa na uraia wa Rwanda, alihamia Rwanda akiwa mkubwa na ni katika harakati za maisha ya soka tu. Huko ndiko alikopata jina la Mafi sango ambalo ni la ukoo wa mwanamke aliyezaa naye mtoto mmoja aitwaye Crespo, hivyo Mafi sango alitumia jina la mkwewe.

“Safari ya kwenda Maisha Club ilianzia katika Pub moja iliyopo Kinondoni ambapo tulikuwa watu kama sita au saba kwani walikuwepo Bozy, Orly, Nyomaa (Gaspar Karemera) na wanawake wawili akiwemo Zai ambaye alikuwa akituhudumia vinywaji. “Lakini Zai alijiunga nasi katika ile hali ya kawaida ya kampani na ilikuwa mara yetu ya kwanza kwenda naye club,” anasema Redondo.

ATUNZA FEDHA NA CHENI YA THAMANI

Wakiwa Maisha Club katika onyesho la Bendi ya Muziki wa Dansi ya FM Academia, Mafisango alikuwa akitunza fedha kila mara na waimbaji wakawa wanamuimba. Bozy ndiye aliyekuwa akitumwa fedha hizo kuzipeleka kwa waimbaji na ilifi ka wakati kabla hata ya kuwafi kia walikuwa wakianza kumuimba Mafisango.

 Ndipo ulipofi ka muda alitoa cheni yake ya silva ili nayo ipelekwe kwa muimbaji mmoja, lakini Bozy akahoji vipi aitoe cheni hiyo? Lakini akaambiwa; “Peleka”. “Alinipa cheni yake ya silva ili nikamtunze muimbaji mmoja, ilikuwa ya gharama na nilipomuuliza akaniambia nimwambie muimbaji yule kwamba hiyo ni kumbukumbu yake kwani wanaweza wasionane tena.
mafisango6“Tangu mchana alisema anataka kutumia fedha zote alizonazo siku hiyo hadi ziishe ndipo arejee nyumbani, na kweli hilo alilitekeleza,” anasema Bozy. Mafi sango alikuwa akigawa dola 100 (sasa ni zaidi ya Sh 220,000) kwa watu mbalimbali aliokutana nao na hata klabu alikuwa akitoa fedha hizo kwa waimbaji ambao walikuwa rafi ki zake.

REDONDO AONDOKA KLABU

Kabla ya saa 8:15 usiku, Redondo na rafi ki wengine wa Mafi sango waliondoka Maisha Club kwa kutumia usafi ri mwingine wa kukodi na kuwaacha wao watano yaani Mafi sango, Orly, Bozy, Nyomaa na yule dada Zai. Waliendelea na burudani huku wakinywa na kabla ya kuondoka, Orly na Bozy walikuwa hawaonekani ndipo Mafisango na yule dada wakatoka nje wakitaka kuondoka.

Baadaye akina Orly waliporudi walipoketi kina Mafi sango na kutowakuta, waliamua kwenda nje kuwafuata ndipo walipomkuta kiungo huyo wa zamani wa Simba akiwa amekasirika na kutaka funguo zake za gari huku akiwataka waondoke.

“Tangu asubuhi mimi ndiye niliyekuwa naendesha gari kwani Mafisango hakuwa mzoefu wa kuendesha gari Dar es Salaam hasa barabara kuu, nilisita kumpa funguo ili atuendeshe lakini sikuwa na jinsi. “Aliniambia yeye ndiye mwenye gari hivyo nimpe funguo, halafu kama kuna kitu kibaya anataka kimtokee yeye mwenyewe na siyo mtu mwingine pia alisema anataka aendeshe gari hilo mpaka mwisho wake.

“Hatukuelewa ana maana gani ila tuliona ni jambo la kawaida tu, nikampa funguo na  safari ya kurejea nyumbani ikaanza,” anasema Bozy. Kabla ya kuelekea Chang’ombe walipitia Kinondoni kwanza kwa Redondo kumjulia hali kama amefi ka salama halafu wakaendelea na safari yao.

PALE KEKO KUMBE WALIGONGWA

Tofauti na ilivyoripotiwa awali kwamba Mafi sango alikuwa akiikwepa baiskeli ya matairi matatu maarufu kama Guta, ukweli ni kwamba waligongwa na gari lingine kwa nyuma.

Kama ilivyoelezwa awali kwamba, Mafi sango hakuwa na uzoefu sana barabarani hivyo baada ya kugongwa licha ya kuzidiwa na gari, asingeweza kuchukua hatua yoyote ile zaidi ya kuacha gari liende linavyotaka. “Ukweli kabla ya ajali ile kuna gari lilitugonga nyuma na dereva wa gari letu ambaye ni Mafi sango alipoteza uelekeo. “Baada ya kugongwa, Mafi sango alipoteza uelekeo na gari likaenda kugonga mti lakini kilikuwa ni kishindo kikubwa mno, gari lililotugonga halikuwa kubwa kama yale y a mizigo bali lilikuwa gari la saizi ya kati kama Nissan Patrol lakini lenye ngao kwa mbele.

“Baada ya kile kishindo mimi nilipoteza fahamu kwa muda kama wa dakika mbili hivi na nilipozinduka nikajikuta nipo nje ya gari chini ya mchanga, nikarudi katika gari na kumkuta Mafi sango ameumia akiwa ameinamia usukani,” anasema mmoja wa abiria waliokuwemo ndani ya gari hilo. Bozy aliyekuwa kwenye gari hilo wakati wa ajali, naye alithibitisha maneno ya abiria mwenzake kwa kusema: “Ni kweli tuligongwa kwa nyuma na gari lililotugonga lilikimbia.

“Ninachokumbuka ni kwamba Mafisango alikuwa akiendesha kwa mwendo wa spidi kati ya 80 hadi 100 na hakuwa mzuri sana barabarani, lakini licha ya kutokuwa na uzoefu na barabara za Dar es Salaam, huku mwanzo hakuweza kusababisha ajali hadi tulipofi ka Keko na kugongwa. “Lakini inauma sana kwani sielewi Mafi sango alikufaje kwani wote hatukuwa tumefunga mikanda ya usalama,” anasema Bozy.

Abiria wote yaani Zai, Nyomaa, Orly na Bozy hawakuumia sana na wala hawakutibiwa kwa muda mrefu, lakini Mafi sango alionekana kuumia sana kichwani katika paji na jichoni. Ikumbukwe kuwa Bozy si aliyetoa maelezo Polisi bali ni Orly na Nyomaa ndio waliofanya hivyo.

Hakika hizo ndizo saa 24 za mwisho za Mafisango!

Trump Aanza na Netanyahu wa Israel ...!!!!

$
0
0

Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu amesema amepokea mwaliko kutoka kwa Rais wa Marekani Donald Trump kumuhitaji aende nchini Marekani mwezi ujao ili waweze kujadiliana kuhusiana na uhusiano baina ya mataifa hayo mawili.

Katika  taarifa yake kwa vyombo vya habari nchini Israel,Netanyahu amesema mwaliko huo ni muhimu kwake kwani anatumai utaweza kumsaidia kupata ushauri ya nini kifanyike ili eneo la Mashariki ya kati liwe na amani.

Mkutano huo baina ya Trump na Netanyahu unakuja siku chache baada ya baadhi ya viongozi wakuu wa nchini  Israel kuidhinisha ujenzi wa nyumba 560 kwa ajili ya walowezi, mashariki mwa Jerusalem.

Ujenzi huo kwa namna moja ama nyingine unadaiwa utachochea uhasama uliopo hivi sasa baina ya Waisraeli na Wapalestina  ambapo Wapalestina wanatumai kuwa Jerusalem Mashariki itakuwa mji mkuu wa taifa lao litakapoundwa siku zijazo.

Picha Linaendeleaah..!! Baada ya Jecha Kudai Alikuwa Sahii Kufuta Uchaguzi ZNZ,Maalim Seif Aibuka na Haya..!!!

$
0
0

Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif Sharif Hamad amesema ameshamalizana na mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC), Jecha Salim Jecha na haoni umuhimu wa kuzungumzia wala kumjibu, kwa sababu atampa sifa asizostahili.

Akihojiwa katika kipindi cha Funguka cha kituo cha televisheni cha Azam TV juzi, Jecha alisema hakumshirikisha Rais wa Zanzibar, Dk Ali Mohamed Shein katika kufuta matokeo ya uchaguzi wa mwaka 2015 visiwani humo.

Jecha alifuta matokeo hayo Oktoba 28, 2015, siku ambayo alitakiwa atangaze mshindi wa uchaguzi wa rais, huku ZEC ikiwa imeshatangaza matokeo ya majimbo 31 na mengine tisa yaliyosalia yakiwa yameshahakikiwa.

Alitangaza uchaguzi mpya Machi 20, 2016 ambao ulisusiwa na CUF na Dk Shein kuibuka mshindi.

Pitia Vichwa vya Magazeti ya Leo 24/1/2017..!!!

Mkuu wa Wilaya Atoa Amri ya Kumweka Rumande Diwani wa Chadema,Kisa Hiki Hapa..!!!

$
0
0

Mkuu wa Wilaya ya Meatu mkoani Simiyu, Joseph Chilongani amemweka rumande Diwani wa Bukundi, Joseph Masibuka (Chadema) kwa tuhuma za kubomoa nyumba 20 za wananchi kwa madai ya kujengwa katika eneo lake.

Hata hivyo, Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Simiyu, Jonathan Shanna alisema jana kuwa wanachunguza madai hayo kubaini kama kuna kosa ili hatua za kisheria zichukuliwe.

Shanna aliwapongeza wananchi kutojichukulia sheria mkononi wakati wa ubomoaji wa nyumba hizo wilayani hapa.

Kubomolewa kwa nyumba hizo na kampuni ya udalali, kumesababisha zaidi ya kaya 100 kukosa makazi.
Hata hivyo, Chilangoni aliwataka wananchi kurejea kwenye makazi yao na kwamba gharama za ujenzi zitafanywa na diwani huyo.

Baadhi ya wakazi hao walisema nyumba za nyasi na magodoro yalichomwa moto wakati wa ubomoaji.

Alichokisema Zitto Kabwe Baada ya ACT Wazalendo Kuangukia Pua Katika Uchaguzi wa Marudio..!!!

$
0
0

Nachukua fursa hii kuwapongeza Sana kwa kazi kubwa mliyoifanya kwenye chaguzi ndogo za udiwani na ubunge zilizomalizika hivi punde nchi nzima. Ingawa hatukushinda hata kata moja katika kata 20 zilizokuwa zinashindaniwa, lakini tumefanya vizuri kwenye matokeo.

Chama chetu kilisimamisha wagombea katika Kata 5 kati ya Kata 20 nchi nzima, Isagehe (Kahama), Kijichi (Dar es salaam), Kiwanja cha Ndege (Morogoro), Nkome (Geita) na Tanga (Songea). Na pia tulisimamisha Mgombea katika Uchaguzi wa Ubunge Dimani (Zanzibar).

Baada ya kufanya kampeni kubwa mzunguko wa kwanza tuliweza kutazama na kuamua kuwekeza kwa nguvu kwenye Kata 3.

Pamoja na kuwa hatukushinda Udiwani wala Ubunge katika Uchaguzi , matokeo yameonyesha kukua kwa kasi kubwa kwa Chama chetu. Tukishika nafasi ya 2 katika Kata ya Isagehe (Halmashauri ya Mji wa Kahama) kwa kupata mara 2 ya Kura ya zile ambazo tulipata katika Uchaguzi mkuu wa mwaka 2015, hali hiyo ipo pia katika Kata ya Kijichi jijini Dar es salaam na Nkome mkoani Geita.

Ni dhahiri kuwa sauti yetu imesikika, Kampeni zetu zilizojikita juu ya masuala ya wananchi zimeleta matunda kiasi.Nawapongeza sana viongozi wetu wa Chama katika Jimbo la Kahama Mjini kwa kazi kubwa tulioifanya na kupiga hatua kubwa. Nawaomba wasikate Tamaa bali wawekeze kwenye kuimarisha uongozi wa Chama Jimbo zima, kwenye kata zote ili kuwa tayari kwa uchaguzi wa Serikali za Mitaa.

Katika Kata za Nkome mkoani Geita na Kijichi mkoani Dar Es salaam tumefanya kazi kubwa Sana. Wagombea na viongozi wetu wa Chama wa mikoa hii na kata hizi wamepigana kwenye mazingira magumu sana ya ushindani mkali wa kisiasa. Kata hizi zimetupa fundisho kuwa wananchi wanataka ushirikiano wa vyama vya upinzani. Ujumbe huo umefika na nawaomba viongozi wetu wa Chama wajiandae kufanya kazi na vyama vingjne. Ubinafsi, roho mbaya, chuki na kukomoana hakuwezi kutusaidia. Lazima tubadilike sisi wenyewe kwanza kabla ya kutaka kuleta mabadiliko kwa wananchi.

Katika Kata ya Tanga Manispaa ya Songea na kata ya Kiwanja cha Ndege Manispaa ya Morogoro wanachama wetu na viongozi walifanya kazi kubwa kuonyesha uwepo wa Chama kwenye maeneo yao. Wamepanda mbegu za Chama na kwa uwezo wa mungu mbegu hizi zitamea na kuzaa matunda.

Ni muhimu kukemea hali ya uchaguzi ya Dimani, Naibu Katibu wa Itikadi, Uenezi na Mawasiliano ya Umma – Zanzibar, ndugu Seif Hamad, ni miongoni mwa waliojeruhiwa kutokana na kipigo baada ya kutolewa Kituoni alipokuwa Wakala wa Chama kwa kupinga udanganyifu wa uchaguzi. Bado uchaguzi kwa upande wa Zanzibar hauendeshwi katika misingi ya haki na demokrasia.

Nawapongeza na kuwashukuru sana wanachama wote wa ACT Wazalendo mliojitoa kwa Hali na Mali kushiriki kampeni katika uchaguzi huu. Shukran za dhati Kabisa kwa madiwani wetu waliotumia gharama zao kwenda kuishi vijijini kutafuta kura za Chama chetu. Sina cha kuwalipa mungu atawalipa. Mmeonyesha mapenzi ya dhati kwa Chama chenu. Mmeonyesha uzalendo wa dhati kwa vitendo.

Nawapongeza viongozi wa Chama wote wakiwemo wale kwa Kitaifa kuanzia Mwenyekiti wetu – Mama Anna Elisha Mghwira, Makamu Mwenyekiti – Mzee Shaaban Mambo, Kaimu Katibu Mkuu – ndugu Said Sanani, na Naibu Katibu Mkuu – ndugu Msafiri Mtelemwa kwa kazi kubwa walioiafanya. Nawapongeza pia makatibu wa Kamati za Makao Makuu ya Chama kwa kuwa waratibu wa kata zilizoshiriki uchaguzi na kwa wale waliokuwa makao makuu kwa kufanya kazi kubwa ya kuwasadia wenzao waliokuwa kwenye mapambano. Kwa Kweli tumefanya kazi kama timu na sote tumechangia matokeo haya tuliyoyapata.

Uchaguzi umekwisha. Badala ya kutumia muda wetu kujadili matokeo, tukubali tumeshindwa na kuanza kujipanga kujenga Chama kwenye maeneo yetu. Tuwaunge mkono walioshinda lakini pia tuwakosoe wanaposhindwa kuwajibika. Tusiache kuwasemea wananchi na kuhangaika na changamoto zao za maisha – msingi wetu wa Siasa zinazojikita juu ya masuala ya wananchi ni muhimu sana.

Ndio kazi yetu hii Kama Chama cha siasa. Tulitumia fursa ya kampeni za chaguzi ndogo kupaza sauti kwenye masuala ya kitaifa na tulifanikiwa Sana kwenye masuala mbalimbali na kutengeneza ajenda za kitaifa. Tusichoke kuendelea kuwa Chama cha masuala na sio matukio. Chama cha hoja Badala ya viroja. Chama cha UTU.

Tuendelee kutaka shughuli za kisiasa kuendelea kwa mujibu wa Sheria. Tuendelee kulaani vikali uamuzi wa Serikali kuzuia vyama vya siasa kufanya mikutano ya hadhara.

Ahsanteni Sana

Kabwe Z. Ruyagwa Zitto
Kiongozi wa Chama (KC)
ACT Wazalendo
Januari 23, 2017

Hofu Yatanda, Ngoma Hatacheza Tena Yanga,Arudi Kwao Zimbabwe..!!!

$
0
0

Mzambia, Donald Ngoma, hivi sasa yupo nchini kwao Zimbabwe alipokwenda baada ya kupata matatizo ya kifamilia kufuatia msiba wa kaka yake.

Hata hivyo, nyota huyo aliondoka nchini akiwa ni majeruhi ambapo alikuwa akisumbuliwa na maumivu ya goti aliyoyapata huko visiwani Zanzibar ambako timu hiyo ilikuwa ikishiriki michuano ya Kombe la Mapinduzi jambo ambalo liliufanya uongozi wa Yanga umtafutie daktari maalum wa kumtibu ili aweze kupona mapema na kurejea uwanjani na hivi karibuni ulikuwa ikisubiria ripoti yake ili kujua maendeleo yake.

Lakini mpaka nyota huyo anaondoka nchini ripoti hiyo ilikuwa bado haijafika mikononi mwa Daktari Mkuu wa Yanga, Edward Bavu, ili aweze kujua maendeleo yake kama amepona au la.

Kutokana na hali hiyo uongozi wa Yanga umeingiwa hofu kubwa na unahofia kuwa unaweza kumkosa mchezaji huyo katika mechi zake zote za Ligi Kuu Bara zilizobakia lakini pia zile za Kombe la FA pamoja na za kimataifa.

Habari za kuaminika kutoka ndani ya Yanga zimedai juzi Jumamosi uongozi wa klabu hiyo umelazimika kuwasiliana na Ngoma na kumtaka arejee nchini haraka iwezekanavyo baada ya kumalizika kwa muda aliopewa ili aweze kuendelea matibabu.

“Lakini yeye amewaambia viongozi kuwa anaendelea vizuri na wasiwe na hofu lakini pia huko alipo anaendelea na matibabu kama kawaida,” kilisema chanzo hicho cha habari.

Alipoulizwa kuhusiana na hilo Bavu alisema: “Ni kweli kabisa hofu ipo lakini hali yake kwa sasa ni nzuri na nimewasiliana naye jana (juzi) na nimemwambia kuwa huko alipo aendelee na matibabu ili atakaporejea awe vizuri lakini suala la kupigiwa simu na uongozi hilo mimi silijui,” alisema Bavu.

Hatariii..!!,Mlango wa Ndege ya Bombardier Q400 Wazua Kizaa zaa Angani,Abiria Wapata Hofu Kubwa..!!!

$
0
0

Abiria waliokuwa wakisafiri kwa ndege aina ya Bombardier Q400 ya Shirika la Ndege Tanzania (ATCL) kutoka Mwanza kuelekea Dar es salaam, walipata hofu baada ya ndege yao kuruka na muda mfupi baadaye kulazimika kutua tena katika Uwanja wa Ndege wa Mwanza

Tukio hilo lilitokea jana saa 2.20 asubuhi uwanjani hapo, baada ya ndege hiyo kuruka kisha ikatua ndani ya dakika 20

Wakati ndege hiyo ikitua, Rubani aliwataarifu abiria kuwa wanalazimika kurejea uwanjani hapo kutokana na dharura iliyojitokeza

Wakizungumza kwa sharti la kutotaja majina yao , baadhi ya watumishi wa uwanja huo walisema walishangazwa na ndege hiyo kurejea muda mfupi baada ya kuruka, hali ambayo hutokea pindi ndege inapokuwa na hitilafu ya kiufundi

"Unajua ndege nyingi huanguka wakati wa kuruka na kutua, ndiyo maana jambo hili lilitisha abiria hata wafanyakazi.

"Lakini hakukuwa hitilafu kubwa ya hatari kwani baada ya kurejea na kukaguliwa, ilionekana mlango wa mizigo ya ndege hiyo ulifungwa vibaya, hivyo kuwasha taa ya tahadhari na Rubani kuamua kutua kwa dharura"alisema mmoja wa watumishi hao

Akielezea tukio hilo, mmoja wa abiria waliokuwa uwanjani hapo ajitarajia kusafiri na ndege nyingine, alisema wakati ndege hiyo inatua kwa dharura, wafanyakazi wa uwanja huo walionekana kuchanganyikiwa

"Wafanyakazi walikuwa 'bize' mpaka tukashtuka, tulipouliza tukaambiwa ndege imeruka na kurudi kwa sababu imepata matatizo angani"alisema mfanyakazi huyo

"Ilipotua abiria wote waliteremka na wataalamu na mafundi wengine wakaanza kuikagua na mwishowe wakagundua mlango wa chumba cha mizigo ulikuwa haukufungwa vizuri

"Kwa hiyo, tatizo hilo waliteremsha na baadaye ndege iliondoka tena"alisema abiria huyo

Wakati hao wakisema hayo, Meneja wa Uwanja wa Ndege wa Mwanza, Easter Madale, alikiri kuwapo kwa tukio hilo ingawa alisema hakujua sababu zake

"Tukio hilo lipo, lakini siwezi kulizungumzia kwa sababu linawahusu watu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege

"Kwa hivyo nakuomba uwatafute hao kwasababu ndio wanaojua, ingawa linaonekana halikuwa tatizo kubwa kwani baada ya kutua, ilikaa muda mfupi na kuondoka tena", alisema
Viewing all 104785 articles
Browse latest View live




Latest Images