Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104689 articles
Browse latest View live

Viongozi wa UKAWA Watoa Tamko Baada ya Kushindwa Vibaya Katika Uchaguzi wa Marudio..!!!

$
0
0

Viongozi wa vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), wamelalamikia kuchezewa rafu katika uchaguzi mdogo wa ubunge na madiwani baada ya CCM kuibuka na ushindi, wakiachia kata moja tu.

Lakini, CCM Zanzibar imesema ushindi ilioupata Jimbo la Dimani ni ishara kwamba Watanzania bado wanaendelea kukiamini chama hicho na kukipa dhamana ya kuwaongoza.

Juma Ali Juma aliiwezesha CCM kutetea kiti chake cha ubunge wa Dimani, jimbo pekee lililorudia uchaguzi baada ya kuachwa wazi na Hafidh Ali Tahir aliyefariki dunia Novemba mwaka jana akiwa bungeni mjini Dodoma.

CCM pia imeibuka mshindi katika kata 18 kati ya 19 za Tanzania Bara.

Za kunyapia Nyapia Hizi Hapa..!!! Eti Hjai Manara wa Simba Amefunguka Juu ya Kumposa Wema Sepetu,Stori Kamili iko Hapa..!!!

$
0
0

Mkuu wa Kitengo cha Habari na Mawasiliano wa Klabu ya Simba, Haji Sunday Manara amelipa mtihani mwingine Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) kwa kuahidi kufanya maamuzi makubwa endapo ratiba ya ligi kuu haitabadilishwa hadi mwisho wa msimu.

Maamuzi ambayo Haji ametangaza kuyafanya ni kumposa mrembo wa Tanzania (Miss Tanzania) mwaka 2006 Wema Sepetu na kumuoa endapo atakubali, lakini kama hatakubali, Haji ameahidi kutembea akiwa amevaa nguo ya ndani pekee (Boxer) kutoka nyumbani kwake hadi katika ofisi za TFF zilizoko Ilala Dar es Salaam.

“Nimalizie Kwa kuwapa mtihani mwingine TFF na bodi ya Ligi, iwapo Kama ratiba yao ya Ligi kuu na Kombe la shirikisho haitabadilishwa kuanzia sasa hadi mwisho wa msimu, ntamposa mlimbwende Wema Sepetu, na akikubali ntamuoa, akikataa ntatembea na boxer toka Nyumbani kwangu hadi TFF” Amesema Manara

Hatua hii ya Haji imekuja ikiwa ni saa chache baada ya Bodi ya Ligi kusogeza mbele mchezo kati ya Simba na Yanga uliokuwa umepangwa kufanyika Februari 18, mwaka huu na sasa utachezwa Februari 25 mwaka huu.

Hatua hiyo ya Bodi ya Ligi imekuja kama kutimiza kile ambacho Manara alikiahidi awali mwanzoni mwa msimu, ambapo alisema kuwa angetembea akiwa mtupu endapo ratiba ya ligi isingebadilishwa.

Katika tamko lake la sasa kupitia ukurasa wake wa Facebook, Manara ameeleza kusikitishwa kwake na kile alichokiita ubabaishaji katika upangaji ratiba, na kulitaja suala hilo kuwa ni moja ya sababu ya Tanzania kukwama katika soka.

“Ninajiuliza iwapo ratiba ya Ligi yetu ni muhali kuipanga,vipi kuhusu program nyingine za maendeleo? Itakuwaje kuhusu timu yetu ya taifa juu ya ndoto zetu za mchana wa jua kali? vipi kuhusiana na zile programu hewa za soka la vijana, watoto na wanawake?”

Ameendelea kusema “Hakika kwetu hayo ni sawa na bahari ya Mediterranean au bahari kuu ya hadithi za Alfu Leila uleila, hatuwezi ratiba tutaweza kwenda Afcon 2019? hatuwezi kupanga ratiba tutaweza kuwa na mipango madhubuti ya kuendeleza mchezo huu ambao yatajwa watu bilioni tatu duniani kote wanaushabikia?”

Rasmi Okwi Afunguka Kuhusu Kujiunga Yanga ,Atoa Msimamo Juu ya Simba..!!!

$
0
0

HATIMAYE kwa mara ya kwanza straika anayesubiriwa kwa hamu na Wanasimba, Emmanuel Okwi, amefunguka kuhusu uwezekano wa yeye kutua Msimbazi.

Okwi hivi karibuni amevunja mkataba wake katika kikosi cha Sonderjyske ya nchini Sweden aliyokuwa akiitumikia baada ya kujiunga nayo mwaka 2015.

Tangu avunje mkataba huo, gumzo kubwa limekuwa ni kuhusu kurejea kwake Simba huku Wanasimba wakimsubiri kwa shauku kubwa.

Wiki iliyopita, Klabu ya Sonderjyske ilitoa taarifa kuwa imeachana na Okwi ambaye tangu ajiunge na klabu hiyo hakuwa na nafasi ya kucheza katika kikosi chake cha kwanza, hivyo kuanzia sasa ni mchezaji huru na anaruhusiwa kujiunga na klabu yoyote itakayomhitaji.

Okwi, jana mchana akiwa nyumbani kwao Kampala, Uganda na ametamka kuwa hajafanya mazungumzo yoyote na Simba kama ilivyokuwa ikisemwa awali.

Ameeleza kuwa yupo nyumbani kwao ametulia na hakuna kiongozi yeyote aliyemfuata kuzungumza naye kuhusu mambo ya kimkataba.

Okwi ameenda mbali zaidi kwa kutamka kuwa hana mpango wowote wa kujiunga na Simba hivi sasa.
“Kwa sasa huo mpango sina na wala hamna makubaliano yoyote, mimi nilikuambiaga kama kuna lolote nitakuambia, lakini kwa sasa hakuna lolote na wala sina mpango huo,” alisema Okwi.

Okwi ambaye msimu wake wa mwisho Msimbazi (2014/15) alifunga mabao 10 na ambaye amekuwa akisifika kwa kuifunga Yanga, ameongeza: “Mimi nipo nimetulia zangu nyumbani, sitaki kuzungumza chochote hivi sasa kuhusu wapi nitakwenda. Kama tulivyozungumza wakati ule, mimi bado sijafanya mawasiliano yoyote na Simba,” alisema Mganda huyo.

Alipotafutwa Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Simba, Zacharia Hans Poppe, ili aweze kulitolea ufafanuzi suala hilo hakupatikana kutokana na simu yake ya mkononi kuita tu bila ya kupokelewa kama ilivyokuwa kwa katibu mkuu wa timu hiyo, Patrick Kahemele pamoja na mkuu wa kitengo cha habari na mawasiliano wa timu hiyo, Haji Manara.

Simba walikuwa na matumaini ya kumtumia Okwi katika mchezo dhidi ya Yanga, Februari 18, mwaka huu, ingawa baadaye ilikuja kubainika kuwa kanuni za TFF haziruhusu ingizo lolote wakati dirisha likiwa limefungwa, hata kama mchezaji ni huru, tofauti kabisa na kanuni za Fifa.

Simba inapambana kusaka ubingwa wa Ligi Kuu Bara msimu huu. Inaongoza ligi kwa tofauti ya pointi mbili tu dhidi ya wapinzani wao Yanga, hasa baada ya Simba kubanwa mbavu kwa sare ya 0-0 na Mtibwa Sugar katika mechi yake iliyopita.

Aidha, katika mchezo wa jana wakati wa Simba na Polisi Dar, mashabiki wa Yanga walimshangilia Mwenyekiti wa Usajili wa Simba, Zacharia Hans Poppe kwa kuimba: Okwi, Okwi, Okwi… alipokuwa akipita mbele yao wakati akielekea msalani kutoka jukwaa kuu alipokuwa amekaa kwenye Uwanja wa Uhuru, Dar.

Hatariii...!! Ajali ya Basi na Lori la Mbao Yaua na Kujeruhi 32 Iringa ..!!!

$
0
0

Mtu mmoja amefariki dunia na wengine 32 kujeruhiwa vibaya baada ya basi la Vitu Laini linalofanya safari zake kutoka vijiji vya Kilolo kwenda Iringa Mjini kugongana na lori la mbao karibu likiwa limekaribia kufika Iringa Mjini.ajali-iringa-4
Akizungumza  Kamanda wa Polisi Mkoa wa Iringa, ACP Peter Kakamba amethibitisha kutokea kwa ajli hiyo na kueleza kuwa majeruhi wote wa ajali hiyo wamelazwa katika Hospitali ya Mkoa wa Iringa.ajali-iringa-2“Ni kweli ajali imetokea leo asubuhi nje kigogo ya Mji wa Iringa, basi ndilo limelogonga lori kwa nyuma na kusababisha kifo cha mtu mmoja aliyeaga dunia palepale na kusababisha majeruhi 32.
“Majeruhi wote tumewapeleka katika Hospitali ya Mkoa wa Iringa ambako wanaendelea kupatiwa matibabu mpaka sasa. ajali-iringa-1Alisema Kamanda Kakamba.Kuhusu chanzo cha ajali hiyo haijafahamika kama ni matatizo ya gari au mwendoksasi wa dereva hivyo Kamanda Kakamba amesema watatoa taarifa rasmi baabdaye kuhusu tukio hilo.

Hii ni Zaidi ya Habari..!!! Ridhiwani Amua Kuanika Maisha Yake ya Nyumbani Mitandaoni,Ona Hapa Anavyofanyaga Akiwa Home Kwake..!!

$
0
0

MBUNGE wa Jimbo la Chalinze, Ridhiwani Kikwete ametupia picha mtandaoni ikimuonesha akiwa nyumba kwake huku akitimiza majukumu yake ya malezi na upendo kwa mwanaye yeye akiwa kama baba mzazi.

Ridhiwani ameonekana akimtengeneza nywele binti yake na kutupia picha hiyoa akisindikiza na maneno haya Instagram

Kwa namna moja ama nyingine jambo hilo ni la kuigwa kwani Ridhiwani kupitia picha maneno aliyoandika amewahimiza baba wengine kuwa karibu na watoto wao na kuwasaidia vitu vidogo vidogo wanavyovihitaji kutoka kwa wazazi wao hasa wa kiume ili kuhakikisha wanakuwa katika malezi yaliyo bora na wafikie malengo yao.

@home attending Fatherhood duty while watching H.E Donald Trump taking Oath of the Office.

CCM Yawashukuru Watanzania Kwa Ushindi wa Ubunge, Madiwani ..!!!!

$
0
0

CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) kimewashukuru Watanzania kwa kukipa ushindi katika uchaguzi wa ubunge wa Jimbo la Dimani, Unguja, na  udiwani katika kata nyingi  uliofanyika Jumapili iliyopita.

Hayo yalisemwa na Katibu  wa Siasa, Itikadi na Uenezi wa CCM,  Humphrey Polepole, alipozungumza na wanahabari leo katika ofisi ndogo za chama hicho zilizopo mtaa wa Lumumba jijini Dar es Salaam.

Polepole alisema kwamba mchawi wa kushindwa kwa mgombea wa Chama cha Wananchi (CUF) yuko ndani ya chama hicho na kisitafute kisingizio kingine.

Mgombea wa CCM huko Dimani alishinda ambapo pia chama hicho kilishinda katika kata 19 kati ya 20 ambapo moja imechukuliwa na upinzani.

“Nawashukuru sana wananchi kwa kuendelea kukiamini Chama Cha Mapinduzi na  ujio wake mpya wa Hapa Kazi Tu chini ya Mwenyekiti wake, Rais John Pombe Magufuli na hivyo vyama vingine vitaendelea kukifuata chama hicho kwa nyuma,” alisisitiza katibu huyo.

Kutana na Maalim Hussein Mtabibu wa Nyota za Binadamu Africa na Dunia Nzima,

$
0
0

Kutana na Maalim Hussein Mtabibu wa nyota za binadamu Africa na dunia nzima,
Anatoa TIBA MAENEO YOTE NCHINI, KWA WALE WENYE KUHITAJI TIBA ANATIBU YAFUATAYO,
Husafisha nyota na kutoa Pete za bahati na kwa wale walia sumbuka kwaajili ya matiba na hawakufanikiwa njoo ujionee muujiza wa papo kwa papo-humpa mtu jini la mali kwa yule anaetaka kumiliki mali bila masharti yoyote,
Anatibu magonjwa yalio shindikana-Mpenzi/MUME/MKE Aliekukimbia Anakurudishia Ndani ya saa 72 tu, Pia tunatoa dawa za Nguvu za KIUME na Kurefusha kwa saizi unayo Taka-Anatoa Dawa za BIASHARA NA MVUTO-Tunatoa Dawa za Uzazi kwa kina Mama kwa wale wenye Tatizo Sugu-Anatoa Zindiko ya Nyumba,Mwili, na Mvuto kazini- Tunamaliza kesi zilizo kaa muda Mrefu bila kumalizika, Tung'arisha Nyota na Cheo kazini. Tunarudisha Mali zilizopotea au Kuibiwa na Mengine Mengi ya Siri tuwasiliane kwa Simu-Whatsapp +255674835107
+255 629254849

Trump Like Magufuli Bana, Naye Kaanza Kutumbua Majipu, Aawafuta Kazi Mabalozi Wote wa Marekani Duniani

$
0
0

Kwa mujibu wa  The Independent na ParsToday wanasema kuwa Rais Donald Trump wa Marekani amewafuta kazi mabalozi wote wa nchi hiyo kote duniani na wanaohudumu katika mashirika ya kimataifa ambapo uamuzi huo umefanyika katika siku yake ya kwanza kazini.

Trump ambaye aliapishwa Ijumaa January 20, 2017 kuwa Rais wa 45 wa Marekani, amewataka mabalozi wote walioteuliwa na mtangulizi wake, Barack Obama kuondoka kazini mara moja bila hata kuwapa muda wa kujitayarisha kuondoka kama ilivyo kawaida.

Inaelezwa kuwa zaidi ya mabalozi 80 wa Marekani katika nchi mbalimbali duniani walifutwa kazi Ijumaa tarehe 20 Disemba saa sita mchana ikiwa ni mara baada ya Trump kuapishwa.

Hatua hiyo ya Trump inatazamiwa kuvuruga uhusiano na washirika muhimu kama vile Ujerumani, Uingereza na Canada ambapo ripoti zinasema nchi hizo zinaweza kukaa bila mabalozi kwa miezi kadhaa kwani baada ya Trump kuteua mabalozi wapya watalazimika kuidhinishwa na Bunge la Congress kabla ya kuanza kazi zao.

Donald Trump anakosolewa kwa kuacha nafasi nyingi wazi na hivyo kuvuruga shughuli za kawaida za serikali ya Marekani na hii haya yanajiri huku maandamano yakiripotiwa kuendelea sehemu mbalimbali kupinga utawala wa kiongozi huyo.

Nchini Marekani katika siku ya pili ya utawala wa Trump kumeripotiwa maandamano ya watu milioni tatu na imeripotiwa kumefanyika maandamano 637 katika maeneo mbalimbali ya Ulaya, Asia na Afrika kumpinga rais mpya wa Marekani.

Lulu Diva Afichua Udhaifu wa Nay wa Mitego kwa Wanawake..!!!

$
0
0

Muuza sura kwenye video za Kibongo na msanii mpya wa bongo Fleva, Lulu Abbas maarufu 'Lulu Diva' amefunguka na kuweka wazi kuwa aliamua kumuacha rapa Nay wa Mitego kutokana na tabia zake za hapa na pale.

 Lulu Diva aliyasema hayo kwenye kipindi cha Planet Bongo ya EATV na kudai kuwa alimua kufikia maamuzi hayo kutokana na tabia za Nay wa Mitego kutotulia na mtu mmoja na kuwatolea tolea macho wanawake.

"Niliamua kumwaga Nay wa Mitego kwa kuwa hajatulia, akiona kila mwanamke macho yanamtoka na kumuwaka, ila naweza kumzungumzia kuwa Nay wa Mitego ni mtu poa sana ukimuona kwenye TV na maisha anayoishi yuko tofauti sana, msafi sana, anajali ni mshikaji poa na ni mtu muelewa sana ila tu ni mtata sana na hizo tabia zingine za kibinadamu ambazo mimi zilinishinda na kuamua kumuacha" alisema Lulu Diva

Serengeti Boys 'Yachungulia' Fainali za Afrika...!!!

$
0
0
Shirikisho la Soka nchini TFF limesema linasubiri maamuzi ya Kamati ya Utendaji ya Shirikisho la Mpira wa Miguu (CAF) kuhusu hatma ya timu ya taifa ya vijana ya Serengeti Boys kufuzu ama kutofuzu michuano ya Afrika kwa vijana. 

Hii ni baada ya kukamilika kwa siku 10 walizopewa Shirikisho la Mpira wa Miguu la Jamhuri ya Congo (FECOFOOT) kumpeleka mchezaji Langa Lesse Bercy Cairo, nchini Misri kwa ajili ya kipimo kipya cha MRI. 

Afisa habari wa TFF Alfred Lucas amesema, kamati ya utendaji ya CAF ilikaa kikao chake Januari 12 na kutoa nafasi ya mwisho kwa FECOFOOT kuhakikisha wanampeleka mchezaji Langa nchini Misri kwa ajili ya kipimo kipya cha MRI lakini mpaka jana ambayo ilikuwa ni mwisho mchezaji huyo alikuwa hajawasilki nchini humo hivyo wanaendelea kusubiri ili kujua maamuzi yatakayotolewa na CAF.

"Kwa mujibu wa kanuni za mashindano ya kimataifa ya vijana wenye umri wa chini ya miaka 17, vijana waliohitajika kucheza ni wale wenye umri wa chini ya miaka 17," amesema Alfred.

Langa Lesse Bercy, amelalamikiwa na Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) kwamba amezidi umri hivyo kuhitajika kumpeleka kwani hakustahili kucheza hatua ya kufuzu kwa michuano hiyo ya Kombe la Mataifa ya Afrika kwa vijana.

Rais Magufuli Kuzindua ‘Mwendo Kasi’ Dar, Kesho..!!

$
0
0

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mh. Dk. John Pombe anatarajia kufanya uzinduzi rasmi wa huduma ya mabasi yaendayo kasi jijini Dar es Salaam siku ya kesho.

Uzinduzi huo unaotarajiwa kufanyika kwenye stendi kuu ya mabasi hiyo ya Gerezani jijini Dar es Salaam, utaanza majira ya asubuhi.

Kwa mujibu wa matangazo yanayotolewa na kampuni inayosimamia mradi huo ya UDART, rais Magufuli anatarajia anatarajiwa kuzungumza na wananchi watakaojitokeza kushuhudia tukio hilo.

Mabasi ya mwendo wa haraka maarufu kama ‘Mwendo Kasi’ yalianza kazi mwishoni mwa mwezi Aprili mwaka jana baada ya kukamilika kwa zoezi la majaribio ya utoaji huduma pamoja na kupangiwa njia za kusafirisha abiria.

Asha Boko Afunguka,Adai Anataka Mume wa Kumuoa ila Kwa Sharti Hili..!!!

$
0
0

Msanii wa maigizo ya vichekesho Asha Boko amesema ameishi katika maisha ya upweke kwa miaka 8 baada ya mume wake kufariki. 

 Akiongea kupitia eNewz Asha amesema aliamua kukaa peke yake baada ya mume wake kufariki na aliamua kulea watoto wake peke yake bila kuwa na baba wa kufikia kwa kuwa aliogopa usumbufu wa wanaume kwani huenda wangewanyanyasa watoto wake.

Hata hivyo Asha amesema kwa sasa akitokea mtu ambaye yupo tayari kumuoa na ambaye atakubaliana na kazi yake yupo tayari kufunga ndoa kwa kuwa yeye ni mtoto wa kiislam na dini ina ruhusu.

P-Funk Athibitisha Msichana Anayeonekana Kwenye Video Chafu iliyosambaa si Mwanae

$
0
0
Wiki iliyopita kulikuwa na tetesi kwenye mitandao ya kijamii kuwa mtoto wa Kajala aliyezaa na P-Funk, Paula ameonekana kwenye video chafu ya ngono.

Tetesi hizo zilidai kuwa kwenye video hiyo Paula anaonekana akifanya mapenzi na mwanaume ndani ya gari. Mama yake, Kajala alikanusha vikali kuwa anayeonekana si mwanae na kwamba tofauti na wengi wanavyodhani kuwa anamlea vibaya, amekuwa na msimamo mkali katika malezi yake.

Na sasa baba yake, Majani amezungumzia upande wake na kudai kuwa yeye pia ameiona video hiyo na kwamba msichana anayeonekana si Paula wake. Anadai kuwa atakuwa mzazi asiye na akili kushindwa kumtambua mwanae.

“Yule sio mtoto wetu amefanana naye labda kidogo tu,labda kiduku chake kile na nywele hivi,” Majani alikiambia kipindi cha Amplifaya cha Clouds FM.

Majani anadai kuwa kama Paula angehusishwa kwenye uchafu huo, pangechimbika. “Angekua mwanangu mnanijua mimi nilivyo,huyo mtu aliyeshoot hiyo video si kungekua na video yake na yeye labda anapewa kitu ushanielewa,” alisisitiza.

Majani alisema angemsaka mhusika, hata kama ni mtoto wa kizito na kumpeleka mbele ya sheria.

Mtayarishaji huyo mkongwe alisisitiza kile Kajala amewahi kusema kuwa, mtoto wa Paula hajawahi kuwa na simu na kwamba akaunti za Instagram zenye jina lake ni feki.

Manara Aahidi Kumtolea Posa Wema Sepetu Kama TFF Wasipofanya Kitendo Hiki

$
0
0
Afisa habari wa klabu ya Simba, Haji Sunday Manara amelipa mtihani Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) kwa kuahidi kufanya maamuzi ya kumtolea posa Wema Sepetu endapo ratiba ya ligi kuu haitabadilishwa hadi mwisho wa msimu.


Aidha msemaji amedai kama muigizaji huyo atakataa basi atatembea akiwa amevaa nguo ya ndani pekee (Boxer) kutoka nyumbani kwake hadi katika ofisi za TFF zilizoko Ilala Dar es Salaam.

Kupitia taarifa ambayo ameichapisha kupitia mtandao wa facebook, ameonyesha kuchukuzwa na kitendo cha TFF kubadilisha ratiba ya Lig Kuu mara kwa mara.

“Nimalizie Kwa kuwapa mtihani mwingine TFF na bodi ya Ligi, iwapo Kama ratiba yao ya Ligi kuu na Kombe la shirikisho haitabadilishwa kuanzia sasa hadi mwisho wa msimu, ntamposa mlimbwende Wema Sepetu, na akikubali ntamuoa, akikataa ntatembea na boxer toka Nyumbani kwangu hadi TFF” Amesema Manara

Hatua hii ya Haji imekuja ikiwa ni saa chache baada ya Bodi ya Ligi kusogeza mbele mchezo kati ya Simba na Yanga uliokuwa umepangwa kufanyika Februari 18, mwaka huu na sasa utachezwa Februari 25 mwaka huu.

Hatua hiyo ya Bodi ya Ligi imekuja kama kutimiza kile ambacho Manara alikiahidi awali mwanzoni mwa msimu, ambapo alisema kuwa angetembea akiwa mtupu endapo ratiba ya ligi isingebadilishwa.

Katika tamko lake la sasa kupitia ukurasa wake wa Facebook, Manara ameeleza kusikitishwa kwake na kile alichokiita ubabaishaji katika upangaji ratiba, na kulitaja suala hilo kuwa ni moja ya sababu ya Tanzania kukwama katika soka.

“Ninajiuliza iwapo ratiba ya Ligi yetu ni muhali kuipanga,vipi kuhusu program nyingine za maendeleo? Itakuwaje kuhusu timu yetu ya taifa juu ya ndoto zetu za mchana wa jua kali? vipi kuhusiana na zile programu hewa za soka la vijana, watoto na wanawake?”

Ameendelea kusema “Hakika kwetu hayo ni sawa na bahari ya Mediterranean au bahari kuu ya hadithi za Alfu Leila uleila, hatuwezi ratiba tutaweza kwenda Afcon 2019? hatuwezi kupanga ratiba tutaweza kuwa na mipango madhubuti ya kuendeleza mchezo huu ambao yatajwa watu bilioni tatu duniani kote wanaushabikia?”

Yupi Anayefaa, Tajiri ila Hana Muda na Mimi au Mwenye Uwezo wa Kawaida ila yupo Nami Muda Wote

$
0
0
Kama kichwa cha Habari kinavyojielezea mimi ni binti mrembo tu Nina kaxi yangu nzuri Namshukuru Mungu, nimepita kwenye mahusiano kadhaa changamoto hazikosekani Nimekutana na wenye uwezo wanaoweza kanipa Nitakacho na wenye uwezo wa kawaida tu.

Nilichojifunza ni kwamba Unaweza kuwa kwenye mahusiano na mtu Anaejiweza akakupa kila utakacho ila hana muda na wewe hamna out wala muda wa kukaa mkayajenga hata mazungumzo ya kawaida maana mimi ni mpambanaji 

Mkikutana ni show basi siku zinaenda mwaka umekatika hamna la maana na sio kwamba anamahusiano mengine Hapana ingawa Mwanaume huwezi msemea ila ni mtu ambaye uko nae huru ila yuko busy muda wote hawezi kujenga muda kwa ajili yako ila muda wa kufanya mengine kama kwenda Bar, karaoke nk anao

Pili Mwanaume Ambae hawezi kukuhudumia kwa chochote mnapata muda wa kuzungumza kushauriana kupanga Mambo ya maendeleo ingawa hamuwezi kwenda out nk kutokana na kipato ila mapenzi mnayafurahia hata kwa kukaa ndani tu coz mimi sio mtokaji na haijawahi kunipa chochote wala sijawahi kumuomba coz namjua Hali yake 

Ingawa ana wasiwasi na mimi kutokana na uwezo wake na urembo wangu ila mimi sina tatizo coz najimudu kwa kila kitu. sasa huyo mwenye uwezo miezi4 hatuko vizuri na naona nimeshindwa mimi kwa moyo mweupe coz sijawahi kuenjoy nae hata siku moja nataka kumpokea huyu wa Hali ya kawaida kwa moyo mmoja tujenge familia maana kule naona utumwa naombeni Ushauri ndugu zangu

By Vantz


Mwana FA: Sina Mpango wa Kufanya Kazi Tena na Lady Jay Dee

$
0
0
Rapa mwana fa anaefanya vizuri na wimbo wake wa "Duke Suruali " amefunguka na kuweka wazi hana tena mpango wa kufanya kazi na msanii lady jaydee.
Mwana FA alisema hayo kupitia kipindi cha planet bongo kunachorushwa na east Africa radio " kwasasa sina mpango tena kufanya Kazi na lady jay dee na hili swali sijui kwanini linajirudia Mara kwa mara na wasanii wengine na sina tatizo nao

Hatua Nne Za Kujifunza Kutokana Na Makosa.

$
0
0

Mara nyingi tumekuwa tukisema ili ufanikiwe ni muhimu sana kujifunza kutokana na makosa. Tumekuwa tukiongea sana kuhusu juu ya hilo mara kwa mara na kukusisitizia juu ya umuhimu wake.

Pamoja na msisitizo huo wa kujifunza kutokana na makosa ambao tumekuwa tukikupa, leo tumeona vyema tukuongezee kitu cha cha ziada katika huko kujifunza kutokana na makosa.

Kitu hiki si kingine bali hatua ambazo unatakiwa uchukue ili uweze kujifunza kwa makosa kiuhakika. Kwa kujifunza hatua hizi itakusaidia wewe  kuvuka hapo ulipo na kwenda ng’ambo nyingine kimafanikio.

Ili kunielewa vizuri katika hili hebu twende pamoja tuangazie nukta kadhaa zitakazo tusaidia kuzielewa hatua nne za kujifunza kupitia makosa tunayoyafanya kila siku kwenye maisha yetu.

Hatua 1.  Andika makosa yako.

Unapojikuta upo katika kitu kipya unachofanya, tambua makosa yapo na ni lazima utafanya. Kitu cha kwanza cha kufanya ili uweze kujifunza vizuri kutokana na makosa yako, andika makosa yako. Hakuna mkato katika hili, andika makosa yako ili ikusaidie wapi pa kuanzia pale unapotaka kujirekebisha. 

Hatua 2. Jifunze kutokana na makosa ya wengine.

Usisubiri sana kujifunza kutokana na makosa yako, angalia pia wengine wanafanya makosa gani, pia yachukue makosa hayo na ya andike mapema ili yasije yakajirudia na kwako pia.  Unapoandika makosa ya wengine mnaofanya kitu kinachofanana inakusaidia na wewe kuwa makini sana.

Hatua 3. Andaa orodha ya makosa ya kuyafanyia kazi.

Katika hatua ya kwanza na ya pili utakuwa umefanya zoezi la kuandika makosa yako. Hapa katika hatua hii andaa sasa makosa ambayo unataka kuyafanyia kazi lakini ambayo yametoka kwenye orodha uliyoandika kwenye hatua mbili zilizotangulia, kisha chukua hatua.

 Hatua 4. Hakikisha usiridhike mapema.

Hata mara baada ya kurekebisha makosa yako, usibweteke na kuridhika na kujiona wewe ni wewe. Endelea kujifunza kutokana na makosa mengine tena na tena na kurudia hatua hizo, hiyo itakufanya uzidi kuwa bora sana siku hadi siku

Fanya Mazoezi Haya kwa Wiki Tatu Kuongeza Nguvu za Kiume..!!!!

$
0
0

Kuna jambo linanishangaza sana, utakuta mwanaume anapata muda wa kukaa kitako muda wa dakika tisini au zaidi akiangalia mpira, au masaa manne, matano na wengine wanakesha kabisa katika baa wakinywa na kula tu, lakini wanasahau kabisa kutenga muda tena mdogo tu kama dakika tano mpaka nane kwa siku kwa ajili ya kuimarisha nguvu za kiume kwa kufanya mazoezi ya kuongeza nguvu za kiume.

Mwanaume anefanya mazoezi ya kuimarisha misuli ya uume hawezi kuwa sawa na mwanaume asiyefanya mazoezi haya sio tu katika kuimarisha nguvu zake za kiume lakini pia kuweza kujitawala katika tendo la ndoa na kuweza kumfikisha mwanamke katika raha ile inayotakiwa.

Mazoezi  haya yakifanywa kwa dhati yanaweza kumpa mtu matokeo mazuri sana ilimradi afuate utaratibu atakao takiwa aufuate.

Hizi ni miongoni mwa faida zinazopatikana kwa kufanya mazoezi haya ni hizi zifuatazo:

Kwanza humpa uwezo mwanaume kuweza kusimamisha uume wake kwa muda mrefu zaidi kuliko ambavyo alikuwa anaweza kuusimamisha  kabla ya kufanya mazoezi haya.

Pili mazoezi haya hufanya mtiririko wa damu kwenye uume uwe mzuri hivyo kuufanya uume uwe na nguvu na kuondoa kabisa tatizo la nguvu za kiume.

Tatu humpa uwezo mfanyaji wa mazoezi haya kukawia kumwaga mbegu hivyo kumpa nafasi mwanamke aweze kufikia katika kilele chake pasi na kumkatishia njiani.'

Vifaa Unavyohitaji

1.   Mafuta ya mizeituni (Olive Oil) au mafuta ya nazi au Alizeti au mafuta ya mgando (gel)

2.   Jiko  lolote ili upate mvuke wa kutosha unaweza kutumia jiko la mchina, stove, au hata la mkaa lakini isiwe moto mwingi uwe kiasi tu lengo ni mvuke

3.   Kitambaa kisafi na laini na maji safi ya uvuguvugu
Namna ya kufanya mazoezi ya Kuongeza nguvu za kiume

1. Loweka kitambaa chako katika maji ya uvugu vugu kisha anza kwa kuusafisha uume wako kwa kitambaa laini cheye maji ya uvugu vugu kama unauchua uume kwa kuuvuta mbele. Fanya zoezi hili kwa dakika tatu.

2.  Pakaa mafuta yako kwenye viganja vyako viwili vya mikono yako kama vile unataka kujipaka mafuta mwilini.

3.  Weka viganja vyako ili vipate mvuke wa moto kutoka katika ama jiko la mchina, stove au kitu chochote utakachotumia. Ukiona viganja vimepata joto kiasi cha kutosha siyo mpaka uungue mikono, kisha

4.  Kamata uume wako ukiwa unauchua kwa kuuvuta mbele kwa nguvu kidogo sana ukianza na mkono wa kulia alafu wa kushoto au kushoto halafu kulia vile utakavyoona inafaa. Joto kwenye mikono likiisha rudisha mikono yako uipashe tena ili ipate joto kisha rudia  kuuvuta vuta tena uume kwa muda wa dakika kumi.
Kumbuka

Mazoezi haya hufanywa mara mbili asubuhi tu mtu ukiamka na wakati ukitaka kwenda kulala na ni kwa muda wa wiki tatu. Utaona matokeo yake.

Mawaziri Wachekelea Mikatba Tisa Waliyoisaini na Uturuki...!!!

$
0
0

BAADHI ya mawaziri wameielezea mikataba tisa ambayo Tanzania imeingia makubaliano na kusaini na nchi ya Uturuki na kubainisha kuwa, mikataba hiyo, imelenga kuongeza zaidi ufanisi wa kiutendaji katika sekta za afya, elimu, kilimo, uchukuzi, diplomasia, utalii , viwanda na ulinzi.

Mawaziri hao waliyasema hayo kwa nyakati tofauti wakati wakizungumza na waandishi wa habari kuhusu undani wa mikataba waliyoisaini juzi wakati wa ziara ya Rais wa Uturuki, Recep Tayyip Erdogan iliyomalizika juzi jioni.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu alisema katika mkataba aliousaini utawezesha ushirikiano baina ya nchi hizo mbili katika sekta ya afya ikiwemo ujenzi wa kiwanda cha dawa.

Aidha, alisema kupitia mkataba huo, pia nchi hiyo ya Uturuki itawezesha mafunzo ikiwemo kubadilishana uzoefu kwa madaktari bingwa wa magonjwa sugu kama vile figo, saratani na moyo, hali itakayoongeza idadi ya madaktari bingwa nchini waliobobea katika kutibu magonjwa hayo.

“Lakini pia watatusaidia kupata mafunzo ya kutumia katika hospitali zetu mfumo wa udhibiti wa taarifa za hospitali (HMIS) ambao ni wa kieletroniki unaotumika kuhifadhi taarifa zote za wagonjwa na takwimu za wagonjwa wa magonjwa mbalimbali,” alifafanua Ummy.

Alisema kupitia mfumo huo, kwa sasa itakuwa ni rahisi Serikali kupata takwimu ya magonjwa mbalimbali kama vile kifua kikuu na moyo lakini pia mfumo huo utarahisisha katika eneo la ukusanyaji mapato kwa kuwa mfumo mzima uko wazi.

Waziri wa Maliasili na Utalii, Profesa Jumanne Maghembe alisema mkataba aliousaini umelenga katika kuikuza sekta ya utalii nchini ambapo nchi hizo mbili zote kwa pamoja zitakuwa na ushirikiano katika kutangaza utalii unahusu pande zote mbili.

“Lakini pia tutabadilishana wataalamu kwa lengo la kujifunza na kuongeza ujuzi katika eneo la sekta ya utalii, tutaangalia namna wenzetu walivyofanya hadi kufanikiwa kuvutiwa idadi kubwa ya watalii kuliko sisi ambao tuna vivutio vingi vya utalii lakini tunapokea watalii wachache,” alifafanua.

Alisema kwa takwimu zilizopo Uturuki inapokea watalii takribani milioni 10 kwa mwaka wakati Tanzania inapokea kwa sasa watalii milioni moja kwa mwaka pekee.

Naye Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Mafunzo ya Ufundi, Stella Manyanya alisema amesaini mkataba wa ushirikiano baina ya Tanzania na Uturuki katika eneo la kubadilishana uzoefu kwenye kilimo.

Alisema Uturuki ni nchi ya saba duniani katika kuzalisha mazao ya kilimo na kwa kuwa Tanzania takribani asilimia 80 ya wakazi wake wanajishughulisha na kilimo, hiyo ni fursa nzuri ya kuikuza sekta hiyo kwa manufaa ya taifa na wananchi kwa ujumla.

Aidha, alisema kwa upande wa teknolojia, nchi hiyo ni moja ya kati ya nchi zinazoongoza duniani katika masuala ya teknolojia hivyo kupitia mkataba huo, Tanzania itanufaika kwa kupata mafunzo mbalimbali katika eneo hilo la teknolojia.

Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Charles Mwijage, kupitia mkataba aliousaini wamekubaliana kushirikiana na nchi hiyo katika eneo la kuendeleza viwanda ambapo nchi hiyo itaanzisha viwanda mbalimbali hapa nchini kikiwemo kiwanda cha nguo.

Aidha alisema kupitia mkataba wa Shirika la Maendeleo ya Viwanda vidogo (SIDO) na shirika la viwanda vya Kati Uturuki, mkataba huo unahusu makubaliano ya kupatiwa mafunzo, ikiwa ni pamoja na kubadilishana wataalamu kwa lengo la kuongeza ujuzi na uzoefu.

Mikataba iliyosainiwa ni pamoja na mkataba wa ushirikiano baina ya Shirika la Ndege Tanzania (ATCL) na shirika la ndege Uturuki, ushirikiano baina ya Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) na Shirika la Utangazaji Uturuki na mkataba wa ushirikiano katika maendeleo baina ya nchi hizo mbili.

Mikataba mingine ni pamoja na ushirikiano katika sekta ya elimu na utafiti, ushirikiano baina ya Shirika la Viwanda Vidogo (SIDO) na Shirika la Viwanda vya Kati Uturuki na ushirikiano katika sekta ya Utalii kwa nchi zote mbili.

Taarifa ya Kutokea Kwa Hitilafu Katika Grid ya Taifa

$
0
0

Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) linawataarifu Wateja wake na Umma kwa ujumla kuwa kumetokea hitilafu katika Kituo kikubwa cha kupoza na kusambaza Umeme cha Ubungo, hitilafu hiyo imesababisha Grid ya Taifa kutoka na kusababisha Mikoa yote iliyounganishwa katika Grid ya Taifa kukosa Umeme.

Mafundi wanaendelea na jitihada ya kurejesha Umeme katika hali yake ya kawaida.

Uongozi unaomba radhi kwa usumbufu wowote unaojitokeza.

Imetolewa na; Ofisi ya Uhusiano

TANESCO Makao Makuu
Viewing all 104689 articles
Browse latest View live




Latest Images