Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104785 articles
Browse latest View live

Samatta Kaweka Tena Kambani Ubelgiji

$
0
0

Mbwana Samatta ameendelea kufanya kweli kwenye ligi ya Ubelgiji baada ya kuifungia tena timu ya KRC Genk wakati ikichomoka na ushindi wa magoli 3-0 dhidi ya Kortrijk kwenye mchezo wa ligi.

Ni goli la pili mfululizo baada ya siku chache zilizopita Samatta kuifungia timu yake bao pekee lililoipa pointi tatu za ugenini wakati ikicheza dhidi ya AS Eupen.

Samatta alifunga goli lake dakika ya 42 akiunganisha kwa kichwa krosi ya Schrijvers na kuandika bao la pili.

Magoli mengine ya Genk yamefungwa na Siebe Schrijvers dakika ya 38 na Alejandro Pozuelo dakika ya 68 na kuipa Genk ushindi wa magoli 3-0.

Genk ipo nafasi ya nane (8) kwenye msimamo wa ligi yenye timu 16 ikiwa na pointi 34 baada ya kucheza mechi 22. Imeshinda michezo 10, sare nne na kupoteza michezo nane.

Gavana wa Benk Kuu Atoa Tamko Juu ya Kuporomoka Kwa Sarafu ya Tanzania dhidi ya Dola ya Marekani..!!

$
0
0



KUPOROMOKA kwa sarafu ya Tanzania dhidi ya Dola ya Marekani kwa takribani asilimia 15 ndani ya mwezi mmoja, kumeonesha kuwashtua baadhi ya wachumi ambao wanasema huenda ukatokea mfumuko wa bei.

Wakati hali ikiwa hivyo mijadala mizito imeibuka katika mitandao ya kijamii mbalimbali kuhusu kuporoka huko kwa Shilingi dhidi ya Dola ya Marekani.

Kutokana na hali hiyo Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Profesa Benno Ndulu, ambaye alikiri kuwapo kwa hali hiyo na kusema ofisi yake imeanza kushughulikia suala hilo kuhakikisha mporomoko huo unatengemaa kabla hayajatokea madhara makubwa.

Kwa sasa katika maduka mbalimbali ya kubadilishia fedha, jijini Dar es Salaam Dola moja ya Marekani inanunuliwa kwa kati ya Sh 2,270 na Sh 2, 290 kutoka Sh 2,180 mwanzoni mwa Januari mwaka huu.

Kwa mara ya mwisho katika miaka ya karibuni, shilingi iliporomoka zaidi Juni mwaka 2015 ambapo Dola moja ya Marekani ilibadilishwa kwa Sh 2,400 na baada ya BoT kuingilia kati ilishuka na kufikia Sh 1,967.

“Sisi kazi yetu ni kujaribu kutafuta utulivu (wa soko la fedha), kuna mambo yanasababishwa na ya nje, kuna mambo ambayo tunaweza kufanya sisi, hivi ninavyokueleza nia yetu ni kuhakikisha panautulivu na tunachukua hatua kwa madhumuni hayo,” alisema.

Alipoulizwa athari za kushuka kwa shilingi, Prof. Ndulu, alisema. “Hiki kitu kimetokea kwa muda mfupi hapa, tunajua namna tunavyotaka kudhibiti kwa hiyo kama itakaa kwa muda mfupi athari sijui kama zitakuwepo kwa hiyo subirini tufanye hiyo kazi,” alisema .

Alisema kwa sasa wanafanya juhudi za kuleta utulivu kutokana na mporomoko huo wa shilingi dhidi ya Dola ya Marekani huku akikataa kueleza mikakati hiyo kwa undani kwa sababu za kiufundi.

“Siyo kuuondoa (ushukaji wa shilingi) ni kwamba tutafanya juhudi zile zinataka kuleta utulivu, ndiyo kazi yetu, sasa tunafanya nini haswa hapa, hiyo itakuja kutuharibia shughuli yetu tusifanye  sawasawa, hatufanyii magazetini,” alisema.

Mwandishi alipomwuliza hatua ya kupanda huko kwa dola kama kunaweza kuathiri deni la Taifa la nje na la ndani, Profesa Ndulu alisema kama haijafika tarehe ya kulipa hayawezi kutokea madhara ya aina yoyote ila kwa siku husika ya malipo ndiyo inaweza kuwa hivyo kama dola itabaki kama ilivyo sasa.

“Sikia hii valuation (hesabu) unaweza kuifanya siku yoyote lakini madhara yake kama kutokea yanatokea unalipa, kama haijafikia tarehe ya kulipa itakupaje madhara? Labda tarehe ya kulipa haitakuwa (dola) huko juu itakuwa iko chini ndiyo ukweli,” alisem Profesa Ndulu.

Wataalamu wachambua

Wakizungumzia hatua hiyo baadhi ya wachumi walisema hali hiyo inaweza kusababisha mfumuko wa bei, jambo litakalo athiri moja kwa moja wananchi.

Mhadhiri wa Uchumi katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Profesa Haji Semboja, alisema kuporomoka kwa shilingi ni kiashiria kwamba mahitaji ya dola kwa Watanzania yameongezeka kwa kiasi kikubwa.

Alisema hali hiyo itasababisha madhara ya kiuchumi kwani fedha nyingi zitalazimika kutolewa huku zitakazoingizwa zikiwa chache.

“Kuna kupanda kwa uchumi na kushuka kwa uchumi, tusipaniki tuwe waangalifu tusiliingilie soko kwani tunaweza kuleta madhara zaidi, lazima tujue dunia inakwendaje,” alisema Profesa Semboja.

Hata hivyo alisema hali hiyo ya kuporomoka kwa shilingi inaweza ikadumu kwa muda mfupi au ikaongezeka hadi mwezi Machi kama mvua hazitanyesha.

Profesa Moshi

Mhadhiri wa Uchumi katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Profesa Humphrey Moshi, ameainisha sababu kadhaa zilizochangia kuporomoka kwa shilingi kuwa ni pamoja na ukame na kupungua kwa kasi ya uwekezaji.

“Inawezekana uagizaji umeongezeka lakini uzalishaji wa shilingi umepungua na inawezekana jinsi kulivyo na ukame mazao ya kupeleka nje yamepungua. Pia kunaweza kuwa na utoroshaji wa fedha kwenda nje.

“Tulitegemea wakati huu ambapo safari za watumishi kwenda nje zimepungua mahitaji ya dola yangekuwa machache lakini inashangaza kwamba hali imebadilika kiasi hiki,” alisema Profesa Moshi.

Pia alisema wawekezaji ambao walitaka kuweka fedha zao ndani wanaweza kuona sera hazijakaa sawasawa wakaamua wasiwekeze kwanza wasubiri.

Alisema hali hiyo itasababisha madhara ya kiuchumi kama vile kuongezeka kwa mfumuko wa bei hasa katika vyakula.

“Huko tuendako tunaona hali ya chakula si nzuri na kuna uwezekano kikaagizwa zaidi kutoka nje hivyo, hali ya maisha itazidi kuwa mbaya kwa sababu gharama zitaongezeka wakati uzalishaji hauongezeki,” alisema.

Profesa Moshi alishauri viwanda visukumwe vizalishe badala ya kuagiza vitu kutoka nje ili kupunguza mahitaji ya dola.

“Wataalamu wa ndani tukizungumza hatusikilizwi hadi waje wataalamu wa nje lakini tunasema kila siku ni lazima tuwekeze kwenye kilimo cha umwagiliaji. Tuna maziwa makubwa ya kutosha na tunaweza kujitegemea kwa chakula na kulisha nchi nyingine,” alisema.

Kafulila

Naye mwanachama wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), David Kafulila, ambaye pia kitaaluma ni mchumi, alisema athari za kuporomoka kwa shilingi ni kubwa kwa malipo ya nje pamoja na deni la taifa kuongezeka.

Akifafanua alisema mwanzoni mwa mwezi huu deni la nje ambalo lilikuwa Sh trilioni 35.67 sasa limefikia trilioni 37.556 kutokana na kuyumba kwa shilingi.

“Shilingi ya Kenya imeyumba kwa asilimia 1.76 lakini shilingi yetu imeyumba kwa asilimia 5.28 na sababu ya kushuka kwa kasi zaidi mbali na kupungua kwa uuzaji bidhaa nje pia kukwama kwa misaada na mikopo kumechangia,” alisema Kafulila.

Baadhi ya bidhaa zinazoagizwa nje ya nchi ikiwa ni pamoja na nishati ya mafuta kama shilingi itaendelea kuporomoka bidhaa hiyo huenda bei yake ikapaa mara dufu jambo ambalo linaweza kuleta madhara kwa wananchi.

Msimamo wa Trump Kuitafuna Afrika ..!!!

$
0
0

SIKU chache baada ya Rais wa 45 wa Marekani, Donald Trump ‘kuwatumbua’ mabalozi wa nchi hiyo duniani, wasomi wameibuka na kusema hilo ni suala la kawaida, lakini kama misaada itasitishwa Bara la Afrika litaathirika zaidi kuliko mataifa mengine.

Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), Dk Hellen Kijo-Bisimba alisema Marekani ni moja kati ya nchi zinazochangia zaidi, hivyo bila shaka wanufaika wataathirika, ukiwamo Umoja wa Mataifa (UN) wenyewe.

Alisema kama Rais Trump ataendelea na msimamo wake wa kusitisha misaada kupitia UN, wafanyakazi wa Umoja huo watakosa ajira kwa vile ni kati ya wanufaika namba moja.

“Lazima tufahamu uchumi wa wanufaika wa misaada wataathirika na wengine kukosa ajira, hilo litakuwa anguko la mwaka,” alisema.

Mjumbe wa Kamati Kuu ya CHADEMA, Profesa Mwesiga Baregu alisema hatua iliyochukuliwa na Rais Trump ni ya kawaida ili kujipatia fursa ya kupanga safu mpya ya uongozi.

Alisema lakini kutokana na falsafa ya Rais huyo amekuja kubana matumizi kwa nchi tegemezi, ikiwamo kutoa misaada ya fedha kwa ajili ya bajeti na misaada mingine ya kiuchumi.

“Nchi zilizotegemea misaada kutoka Marekani zinapaswa kujiandaa, inawezekana misaada itakayotolewa isiwe kwa kiwango kilichotarajiwa,” alisema.

Wakili wa Kujitegemea, Alex Masaba alisema kitendo cha kusimamishwa kwa mabalozi wa mashirika ya kimataifa kimetokana na kusuasua kwa UN katika utendaji wake.

Alisema hiyo itakuwa njia bora kwa Rais Trump kuionesha Dunia kuwa hafurahishwi na utendaji wa taasisi hiyo ya kimataifa na kutaka kubadili muundo wa kiutawala.

“Kila mtawala anapoingia lazima afanye mabadiliko ya uongozi ili kutekeleza majukumu yake kuendana na kasi ya Serikali husika,” alisema.

Mwenyekiti wa Jukwaa la Katiba Tanzania (Jukata), Deus Kibamba alisema hakuna kitu kipya alichofanya Rais Trump kwa vile huo ni utaratibu wa Marekani.

Alisema baada ya chama cha Damocratic kumaliza muda wake na Republican kutangazwa mshindi, mabalozi wote walikosa sifa ya kuendelea na nyadhifa zao.

“Unajua Trump alipotangazwa kuwa Rais, mabalozi waliokuwa wakiwakilisha nchi hiyo walifunga virago kurudi kwao, hivyo hilo si jambo jipya kwa Wamarekani, bali ni utamaduni wao,” alisema.

Jinsi Kijana wa Miaka 22 Alivyombaka Mtoto wa Miaka 5 Karibu na Ziwa Victoria..!!!

$
0
0

Kijana aliyejulikana kwa jina la Petro Magayane miaka 22 mkazi wa Igombe Jijini Mwanza anashikiliwa na jeshi la polisi kwa kosa la kumbaka na kumjeruhi katika sehemu zake za siri mtoto mwenye umri wa miaka 5 ambaye ni mkazi wa eneo hilo. 

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza DCP Ahmed Msangi amesema kuwa tukio hilo limetokea tarehe 23.01.2017 majira ya saa 2 usiku katika kijiji cha Igombe “A” kata ya Bugogwa wilaya ya Ilemela mkoani Mwanza.

Inadaiwa kuwa mtuhumiwa akiwa amelewa  alifika maeneo ya nyumbani anapoishi mtoto huyo kisha akamtuma dukani maeneo ya mwaloni Igombe.

Aidha baada ya muda mchache kupita mtuhumiwa alimfuata mtoto huko dukani kisha kumfanyia ukatili wa kumbaka na kusababisha majeraha na maumivu makali katika sehemu za siri za mtoto huyo.

Wananchi walitoa taarifa polisi kuhusiana na tukio hilo, askari walifika eneo la tukio na kufanikiwa kumkamata mtuhumiwa huyo ambaye yupo katika mahojiano na jeshi la polisi, pindi uchunguzi ukikamilika atafikishwa mahakamani.

Msangi amesema kuwa uchunguzi wa awali unaonesha chanzo cha tukio hili ni ulevi. Mtoto amepatiwa matibabu hospitali na hali yake inaendelea vizuri.

Coutinho Ajifunga Liverpool Hadi 2022..!!

$
0
0

Kiungo wa Liverpool Philippe Coutinho ameongeza mkataba wa muda mrefu na klabu hiyo ya ligi kuu ya soka nchini Uingereza. 

Taarifa zinasema Mbrazil huyo, amesaini mkataba utakaomuweka Anfield hadi mwaka 2022, huku kukiwa hakuna kipengele cha kumwachia mchezaji huyo.

Mara baada ya kusaini mkataba huo, Coutinho amesema kuwa anawashukuru watu wote wa Liverpool, na kuahidi kuitumikia klabu hiyo kwa nguvu zake zote, ili kulipa thamani anayopewa na klabu hiyo.

Coutinho aliyetoka kuuguza majeraha ya kifundo cha mguu kwa mwezi mmoja na nusu hadi sasa ameifungia klabu yake mabao 6, katika michezo 18, kwenye msimu huu.

Snura Afunguka Jinsi Anavyomtamani Leo Kesho Shilole..!!!

$
0
0

MWANADADA anayetamba na ngoma ya ‘Shindu’ Mwaga Maji Tucheze Kama Kambare, Snura Mushi (pichani) ameeleza kiu yake ya kutaka kufanya kazi na mwanadada mwenzake Zuwena Mohammed ‘Shilole’ endapo atakuwa tayari.
 
Snura amebainisha hayo usiku wa Jumanne, Januari 24, 2017 wakati akijibu swali kwenye interview ya kipindi cha Redio EFM. Snura amesema kuwa  kwa sasa hana bifu kabisa na Shilole, hayo yalikuwa mambo ya zamani na yalisha kwisha kitambo na endapo ikitokea nafasi ya wawili hao kukaa chemba na kufanya kazi pamoja yuko tayari kwa asilimia zote.shilole-15
Shilole
“Kwa sasa sina bifu lolote na Shilole, tuko sawa, hayo yalikuwa mambo ya zamani sana tulishayamaliza, tupo sawa. Muziki wake na wangu uko tofauti hatuwezi kugombana”snuraSnura
“Kwanza natamani sana kufanya kazi pamoja na Shilole, ikiwezekana tufanye wimbo wa pamoja au movie (filamu) kwa kuwa yeye ni msanii mzuri wa kuigiza naamini tukifanya hiyo tutatengeneza pesa nzuri mimi na yeye”

“Kingine ni kwamba natamani pia kufanya naye shoo moja jukwaani hata kama ni hapa Dar es Salaam au popote, kwa maana sisi wasanii tupo kwa ajili ya kutafuta pesa, kwa hiyo ikitokea nafasi kama hiyo itakuwa poa sana.” Alisema Snura.shilole-4Shilole
Mbali na hayo Snura hakusita kueleza jitihada zake za kumtafuta Shilole licha ya yeye kuonekana kama hayuko tayari kufanya hivyo.

“Nimewahi kumtafuta kwa jitihada zangu ili tuweze kufanya angalau jambo moja kati ya hayo (shoo, wimbo au filamu) lakini inavyoonekana mwenzangu kama hayuko tayari.” Alimalizia Shilole.

Ecowas Wabaini Kemikali ya Sumu Ikulu ya Gambia,Iliachwa na Rais Yahya Jammeah ..!!!

$
0
0

Askari wa Jumuiya ya Kiuchumi ya Nchi za Afrika Magharibi (Ecowas) wamegundua kemikali ya sumu kali iliyokuwa imetegwa kwenye vyumba vya Ikulu.

Kwa mujibu wa taarifa zilizotolewa na Ecowas kupitia gazeti la Freedom la Gambia, kemikali hiyo ilitegwa kwa lengo la kuua mtu yeyote atakayeingia ndani ya Ikulu hiyo.

Kutokana na hali hiyo, kiongozi mpya wa Gambia, Adama Barrow anatakiwa kuendelea kukaa Senegal kwa usalama wake huku uchunguzi ukiendelea kufanyika.

Baada ya Kushindwa Uchaguzi wa Marudio ZNZ,CUF Wakimbilia Kushitaki kwa Mwamunyange..!!!

$
0
0

Kikao cha kutathmini uchaguzi mdogo wa Jimbo la Dimani  cha  Chama cha  Wananchi (CUF), kimekusudia kumwandikia barua ya malalamiko Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Tanzania (JWTZ), Jenerali Davis Mwamunyange wakidai wanajeshi walishiriki kuleta hofu.

Hata hivyo, jeshi hilo limekana madai ya CUF likisema ni uzushi.

Madai hayo yalitolewa na Naibu Katibu Mkuu wa CUF Zanzibar, Nassor Ahmed Mazrui alipozungumza kwa simu na mwandishi wetu kuhusu uamuzi wa kikao hicho kilichofanyika jana Unguja chini ya uenyekiti wa Katibu Mkuu, Maalim Seif Sharif Hamad na kuhudhuriwa na wajumbe 14.

Alidai kikao hicho kilichojadili mwenendo mzima wa uchaguzi kuanzia kampeni, kilifikia uamuzi wa kuandika barua ya malalamiko kwa Jenerali Mwamunyange wakidai wanajeshi walionekana wakizunguka mitaani katika jimbo, siku ya kuamkia uchaguzi na siku ya kupigakura.

Umeme Uliokatika Ghafla Nchi Nzima Waanza Kurejea..!!!

$
0
0

Mikoa yote iliyounganishwa kwenye gridi ya Taifa imekumbwa na tatizo la umeme kutokana na hitilafu iliyotokea katika mtambo wa kupooza na kusambaza umeme Ubungo, Dar es Salaam.

Hata hivyo Tanesco imeeleza kuwa umeshaanza kurejea katika baadhi ya maeneo.

Akizungumza kwa njia ya simu leo asubuhi, Kaimu Meneja Uhusiano wa Tanesco, Leila Muhaji amesema wataalam wanaendelea kushughulikia tatizo hilo na hali itarejea kama kawaida.

“Tatizo hili limetokea leo saa 12:32 asubuhi katika mtambo wa kilovolti 220 ambao ni wa kupoozea na kusambaza umeme uliopo Ubungo lakini kwa kuwa wataalam wameshagundua

Kudadeki Pata Hii..Trump Kuamuru Ujenzi wa Ukuta Mpakani mwa Mexico, Kuzuia Wageni wa Kiislamu Kuingia US Kuanzia Jumatano Hii

$
0
0

Rais Donald Trump ataanza kupitisha maamuzi ya juu kuhusiana na masuala ya uhamiaji kuanzia Jumatano hii, akianza na kuimarisha ulinzi wa mpakani, ikiwemo ujenzi wa ukuta mpakani mwa Mexico na Marekani.

Rais huyo pia anatarajiwa kupiga marufuku kwa muda kuingia kwa wahamiaji kutoka katoka nchi za Kiislamu wanaoweza kuhusika na ugaidi zikiwemo Syria, Iran, Iraq, Libya, Yemen, Sudan na Somalia.

‘Big day planned on NATIONAL SECURITY tomorrow,Among many other things, we will build the wall,” alitweet.

Uamuzi huo ni miongoni mwa mambo aliyokuwa ameahidi wakati wa kampeni.

Jinsi Wanadunia Tunavyoandaliwa Kuwa Mazombi na Maroboti Bila Kujua..!!

$
0
0

Unaweza ukapaniki nitakapokwambia mawazo mengi unavyodhani ni yako sio yako ni vitu ulivyopandikiziwa Bila kujua. Sisi tunaamini uwepo wa Mungu na uumbaji tunaamini pia Mwanadamu aliumbwa na Uwezo huru wa kufikiri na kuchagua.

Vita kubwa inayoendelea Sasa chini ya ardhi sio dhidi ya Magaidi, waasi au religious extremists Bali ni kumuondolea mwanadamu zawadi hii ya pekee aliyopewa na Mungu na vita hivi hadi sasa imefanikiwa kwa zaidi ya asilimia 50 duniani kote. Waandisi jamii ndio Moyo na silaha ya maangamizi katika vita hivi.
[​IMG]
Lengo la bandiko hili sio kutishana Bali ni kuongeza uelewe halisi wa mambo maana ushahidi usio na Shaka umeonyesha kujua michezo hii kutakupunguzia asilimia kubwa ya kuwa muhanga wa janga hili. Mambo haya yanafanyika kupitia Mind control techniques,Brain Washing techniques, subliminal sensations na vifaa vikubwa vinavyowezesha ni TV, Movies, Adverts, Social Media hivi ndio mama.

Zifuatazo ni jinsi 06 unavyoweza kunaswa katika mtego ya kutawaliwa bongo

1:Matangazo ya Biashara na Propaganda
[​IMG]
Asilimia kubwa ya watu wanavyovaa, kula, kunywa, kunyoa style, aina ya vitu wanavyopenda sio matokeo ya uamuzi wao wa Hiyari Bali Matangazo na ushawishi wake.

 Leo duniani habari ikathibitika kama ni ya kweli, au kitu kitaonekana ni sahihi au kizuri au chafaa kutumika katika jamii kama kimeandikwa kwenye vyombo vya habari mbalimbali vya kimataifa visivyohusiana. Lakin ukweli ni kwamba asilimia kubwa ya habari zinazoenea duniani na asilimia kubwa ya vyombo vya habari vikubwa ulimwenguni vinamilikiwa na Makampuni sita tu tena yenye uhusiano wa karibu.

 Kwa maana nyingine wanaweza kuamua kuja na habari yoyote kukuaminisha jambo lolote wakati wowote. Simaanishi tusiangalie habari Bali tujiongeze kwa akili zetu pia ktk kupambanua. Kwa nini kuna uwezekano zikwepo jumbe (subliminal messages) ambazo zimechujwa na kurushwa kwenye media zote duniani Bila kujua asilimia kubwa zinauhusiano au Kuna mipango nyuma ya propaganda hizo.

 Leo Kuna watu wanawachukia waarabu kwa sababu media zimesema, na Kuna watu wanawachukia wamarekani kwa sababu media zimesema wanawaonea waarabu.Mfano kwenda kuangalia Movies ukiwa na Bisi na Soda au wanawake kuacha vifua nusu wazi au kutamani kuwa na vifua/boobs vikubwa wengi sio kwa hiyari zao bali ni matokea ya group thinking inayotokea kidogo kidogo ila kwa uhakika.
2:Watu kupangwa kukubali matukio kabla hayajatokea /Predictive programming
Dhana hii bado wengi haiwaingii akilini. Hii mbinu inatumika kwa mapana na kwa Muda mrefu hasa kupitia werevu wa Hollywood, Kuna vitu vingi ambayo zamani vilionekana kama ni fiction lkn Sasa katika jamii vimekubalika. Mfano mdogo kwenye cartoons Mind Blowing Examples of Predictive Programming in Cartoons | The Ghost Diaries

3:Michezo, Dini na Siasa na Ushabiki wa Mipira ya kimataifa
[​IMG]
Vitu hivi navyo kwa sehemu Kubwa vimechukua sehemu ya fikra za mwanadamu huru. Tuliwaona wafuasi wa kibwetele wakiteketea kwa moto kanisani ili waende mbinguni kama matokeo ya kutawaliwa fikra na kuoshwa ubongo. Michezo ilipaswa kuwa sababu kubwa kuleta umoja na afya, leo imekuwa kichocheo cha uadui kama zilivyo siasa. Umoja wa msingi kwa mambo yenye manufaa umekufa kutokana na akili zinazokumbatia mipasuko ya kisiasa, michezo na dini. Ukiangalia duniani hakuna vita ambayo dini na siasa haitakuwepo hata kwa mbali.

4:Vya kila, Vinywaji na Hewa
[​IMG]
Tunaishi kwenye dunia ambayo Mtu akiishi chini ya hewa bandia ndio tunamsifia na kumuona anapewa na ndio wa kuigwa, vyakula vilivyojaa sumu, maji yaliyojaa contents ambazo zingine hazieleweki kwa nini siwepo na kwa kiwango hicho ndiyo vinavyosisitizwa kila kona hata penye uwezekano wa kupatikana vitu Asili na original. Vitu hivi vimethibitika kushusha Uwezo wa kiakili, vingine vinahamasisha hasira na jazba, vingine vinadhoofisha Uwezo wote wa mwanadamu taratibu ila kwa uhakika.

5: Madawa na addictions
[​IMG]
Lengo kuu la wenye hekima na werevu wachache duniani ni kuhakikisha kila mmoja anakuwa addicted na kitu kinachomshusha Uwezo wake, kama sio drugs, movies, football, video games, pornography, chochote kile. Silaha kubwa ni kuhamasishwa kwa uwepo wa gonjwa la akili au saikolojia na kuwafafaua au kuwaelezea watu wote duniani au kwenye taifa flani kwa mwelekeo wa ugonjwa wa akili badala ya mwelekeo wa Uwezo wa mwanadamu kiakili. Na madhara yake wengi wanajikuta wako katika misongo na kujishuku kama wako Sawa, na hii inatengeneza mwanya wa kuweka rehani Uwezo wake wa kibinadamu na kukabidhi wengine wampangie cha kufanya.

6:Computers, TV na Smartphone/simu[​IMG][​IMG]
Vitu hivi vyote sio vibaya, ila kwa dunia ya Sasa vimetengeneza uteja kw kuweka visismuzi vitakavyokufanya usibanduke. Social engineers au waandisi jamii wanaweka vitu vitakavyokufanya usibanduke na kuwepo kwako mbele ya screen kwa muda mrefu Kuna effects hadi ndani ya ubongo.

 Melatonin ni hormone inayotawala mzunguko wa usingizi kwa mwanadamu. Adui namba moja wa hormone hii ni mwanga hasa pale unapohitaji usingizi. Kukaa mbele ya kioo muda mrefu hasa usiku kutaathiri mzunguko wako wa usingizi. 

Kumbuka pale tunapolala ndipo ubongo unapata muda wa kujifanya usafi na kujiweka Sawa, madhara ya kukaa na simu au mbele y TV muda mrefu hasa usikuni kutengeneza shambani la kujitoa muhanga dhidi ya ubongo wako.

Mwisho :mwanadamu ni kiumbe mwenye Uwezo mkubwa, kuweka rehani Uwezo huu na kutufanya kuwa watumwa wawanadamu wenzetu ni kitu cha kukiepuka na kukikwepa sana. Unaweza usiamini au ukaamini ila lengo hapa nikuongeza ufahamu wa mambo ili kuongeza uelewe zaidi wa mienendo yetu.

Nini kifanyike

njia kuu ni kuwekeza zaidi ktk kusoma vitabu vinavyofikirisha na kukufanya utoe maoni yako kabla upinge au uunge mkono. Movies, TV programs nyingi, news nyingi zimekutwa programmed
Ukusisimua na sio kuufikirisha. Vipindi na scripts nyingi zinapelekwa haraka haraka ili ukoswe muda wa kufikiri.

Kama unaamini bibilia chukua Muda jisomee pia inashuriwa ujiunge na vikundi au taasisi za kidini zinzazotoa kipaumbele mijadala yenye changamoto na sio kuburuzwa na kuambiwa cha kufanya muda wote. Jifunze jinsi ubongo unavyofanya kazi hasa sehemu hisa Conscious na Subconscious Minds.

Simba Kutupwa Nje Kombe la Shirikisho..!!!

$
0
0

Klabu ya Simba huenda ikatupwa nje ya michuano ya kombe la shirikisho kufuatia kumpanga beki wake Novalt Lufunga kwenye mchezo walioshinda mabao 2-0 dhidi ya Polisi ya Dar es salaam huku akiwa na kadi nyekundu aliyoipata kwenye michuano iliyopita.

 Kwa mujibu wa rufaa ya klabu ya Polisi inadai kwamba Lufunga alilimwa kadi nyekundu kwenye mchezo wa mwisho wa michuano hiyo msimu uliopita dhidi ya Coastal Union ya Tanga ambapo Simba ilitupwa nje ya mashindano.

 Makamu wa Rais wa Klabu ya Simba Geofrey Nyange 'Kaburu' ambaye amelitolea ufafanuzi suala hilo huku akikanusha kuwa Lufunga hakucheza mchezo uliofuata baada ya ule wa Coastal, lakini pia akasema kuwa kanuni za mashindano hayo ni tofauti na kanuni za ligi.

Breaking News: Katibu Mkuu wa Simba Patrick Kahemele Aachia Ngazi ..!!!

$
0
0

Taarifa tulizozipata kutoka kwa  Kahemele zinaeleza aliandika barua na kamati ya utendaji ya Simba, imepitisha hilo.

Upande mwingine wa taarifa, umeeleza Kahemele anarejea na kujiunga na Azam TV ambako alikuwa akifanya kazi kabla.

“Kweli anaondoka, leo kamati ya utendaji ya Simba imekubaliana naye,” kilieleza chanzo.

Juhudi za kuwapata viongozi wa Simba walizungumzie hilo, zinaendelea.

JPM Atangaza Makubwa Zaidi Mabasi ya Mwendo Kasi,Aendesha Basi la Abiria la Mwendokasi(Video)

$
0
0

Rais wa Tanzania, Dk. John Magufuli, amesema serikali itajenga barabara za juu tatu za kuchepuka katika eneo la Ubungo ili kuupa maana Mradi wa Mabasi Yaendayo Haraka (BRT) ulioanzia Jijini Dar es Salaam 

Amesema lengo ni kuondokana tatizo la mabasi hayo kutumia muda mwingi kukatiza katika eneo hilo.

Rais Dk. Magufuli ametoa kauli hiyo leo Jijini Dar es Salaam wakati wa ufunguzi wa awamu ya kwanza ya mradi wa miundombinu ya utoaji huduma kwa mradi huo wa BRT uliogharimu shilingi bilioni 403, ambapo ametaka kuharakishwa kwa mchakato wa kukamilisha kuanza kwa ujenzi wa barabara hizo za juu za kuchepuka.

Rais Magufuli amesema awamu ya pili ya mradi mabasi yaendayo kasi itahusisha barabara ya urefu wa kilometa 19.3 inayotoka barabara ya Kilwa katikati ya jiji la Dar es Salaam hadi Mbagala rangi tatu, pamoja na ujenzi wa barabara ya juu katika makutano ya barabara ya Nyerere na Kawawa.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Makamu wa Rais wa Benki ya Dunia Kanda ya Afrika Makhtar Diop wa kwanza kulia wavivuta kitambaa kuashiria ufunguzi rasmi wa Awamu ya Kwanza ya Miundombinu na Utoaji Huduma ya Mabasi yaendayo Haraka katika jiji la Dar es Salaam. Wengine katika picha ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais –TAMISEMI George Simbachawene pamoja na  Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa.

Akitaja awamu nyingine amesema kuwa itahusisha barabara ya Nyerere hadi Gongolamboto yenye jumla ya urefu wa Kilometa 33.6 mradi, awamu ya nne ni barabara yenye kilomita 25.9 ikihusisha barabara ya Ali Hassan Mwinyi na Tegeta, yenye urefu wa Kilometa 22.8 awamu ya tano yenye urefu wa Kilometa 27.9 kwa awamu ya sita miradi yote hiyo itafadhiliwa na Benki ya Dunia.

Kwa upande wake Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Prof. Makame Mbarawa amesema wizara yake itatekeleza mikataba iliyowekwa na Banki ya Dunia ili kukamilisha miradi mingine ya maendeleo ikiwa ni pamoja na reli na umeme.

Maajabu; Kuwait Ina Walimu Wanne (4) Tu wa Physics..!!!

$
0
0

Mkuu wa kamati ya bajeti katika bunge la Kuwait, Adnan Abdulsamad ametahadhrisha kuwa hivi sasa kuna walimu wanne tu nchini humo wanaofundisha somo la Fizikia na kusisitiza kuwa idadi hiyo haikubaliki kwa namna yoyote.

Waziri wa Elimu ya Juu wa Kuwait Muhammad Al-Faris naye pia ameashiria uhaba mkubwa wa walimu ilionao nchi hiyo katika masomo muhimu kama Fizikia na Hesabati na kupendekeza kuwa ili kukabiliana na tatizo hilo serikali iwaajiri Wakuwaiti wasio na vitambulisho vya uraia wanaojulikana kama 'Bedoons'; kwa kuzingatia kuwa wengi miongoni mwao wanafaulu kwa kiwango cha juu lakini kutokana na utambulisho wao, vyuo vikuu vya nchi hiyo haviko tayari kuwapatia fursa za kuendelea na masomo ya juu.

Akizungumzia suala hilo, Abdulsamad amesema ni heri kuwapa mafunzo na kuwatumia Bedoons kuliko kuajiri walimu kutoka nje ya nchi kwa ajili ya kutatua tatizo la uhaba wa walimu.

Nchini Kuwait kuna idadi ya Waarabu zaidi ya laki mbili waishio majangwani wanaojulikana kama Bedoons. Serikali ya Kuwait inawachukulia waarabu hao kuwa ni watu wasio na utambulisho na haiko tayari kuwapatia uraia wa nchi hiyo…/

Papa Amtimua Kiongozi wa Dini kwa Kusambaza Kondomu..!!!

$
0
0

Kiongozi wa kanisa katoliki anayewasaidia raia wa Malta amejiuzulu kufuatia mgogoro na Vatican kuhusu mpango wa kusambaza mipira ya kondomu kulingana na kanisa hilo.

Mathew Festing mwenye umri wa miaka 67 alijiuzulu baada ya papa Francis kumtaka kufanya hivyo katika mkutano siku ya Alhamisi.

hatua hiyo inafuatia ufichuzi kwamba tawi la hisani la kanisa hilo huko Malta lilisambaza maelfu ya mipira ya kondomu katika taifa la Myanmar.

Kanisa katoliki linakataza utumizi wa mipira ya kondomu.Papa Francis alimtaka kujiuzulu na alikubali.

Tawi hilo la Malta lina uwezo mwingi kama ule wa taifa zima. Hutoa pasipoti, stampu na leseni na pia lina uhusiano wa kidiplomasia na mataifa 106 ,ikiwemo Vatican.

Ijapokuwa tawi hilo linaonekana kuwa na wanaume pekee, viongozi wake sio wanaume pekee.

Kufikia 2013 wanawake walikuwa asilimia 30 wakijulikana kama Dames.

Kundi hilo lilo katika kuondoa sura yake ya kibwenyenye na kuvutia vipaji ili kuendelea kazi zake za kibinaadamu.

Kutana na Roberto Esquivel Cabrera Mwanaume Mwenye Uume Mrrefu Zaidi Duniani Una Inchi 19,Hajawai Kusexy ,(+18Video)

$
0
0

Rekodi ya mwanaume mwenye maumbile ya kiume makubwa imevunjwa na jamaa mmexico anaeitwa Roberto Esquivel Cabrera ambae ana uume wenye urefu wa takribani inchi 19 (18.9 inches to be exact).

Hata hivyo licha ya kujaliwa kuwa na mashine kubwa namna hiyo, Roberto Cabrera hana amani wala furahamaishani mwake. Uume wake umegeuka kuwa kero badala ya kumletea fahari maishani. kwanini?

i. Jamaa mpaka leo ni bikira na hana mke wala mtoto. Bikira kivipi? Hadi leo hii akiwa na umri wa miaka 52 hajawahi kufanikisha kufanya tendo la ndoa. Baadhi ya wanawake wameogopa hata kufanya jaribio la kusex nae wakiogopa kuharibiwa kizazi. Na mwanamke pekee aliejifanya nunda na kujaribu kumu-accomodate jamaa aliishia kulia kilio cha mbwa mwizi na kutoka nduki kabla jamaa hajaingia hata nusu!


ii. Pia, mr. Cabrera amekuwa akikabiliwa na maambukizi ya njia ya mkojo (UTI) mara kwa mara kwasababu anashindwa kuutoa mkojo wote nje wakati wa kukojoa. Hii ni kwasababu ya urefu uliozidi wa urethra.

iii. Pia jamaa ameshindwa kupata kazi yoyote nchini Mexico kwasababu serikali inamuona jamaa kuwa ni mlemavu na anahitaji msaada maalumu.

iv. Pia jamaa anashindwa kutembea comfortably kwasababu uume wake umekuwa ukimsumbua kila anapojaribu kupiga hatua. Huko mitaani nako kila mtu anatokea kushangaa umbile la jamaa ambalo jamaa ameshindwa kabisaaaa kulizuia hata akivaa magunia na kanzu nzito.

Katika harakati za kumsaidia jamaa, ilishauriwa na wataalamu wa tiba kuwa jamaa afanyiwe operation ya kuupunguza uume wake ili ubaki at least 6 inches. Ila jamaa alikataa katakata akidai kuwa ukubwa wa mshindende wake ndio unaompatia fahari na umaarufu kokote aendako. Huku akijidai kuwa mwanaume mwenye mashine kubwa ndie anaeonekana mwanaume wa kweli!

Pia jamaa ana malengo ya kuhamia Marekani ili akawe porn star na apate kujitengenezea utajiri na umaarufu wa kutosha kwasababu mtaji wa maumbile anao!

Kutana na Ania Lisewska.Binti Mwenye Mpango wa Kulala na Wanaume 100,000,Hadi Sasa Kashalala na Wanaume 284..!

$
0
0

Mwanamke mmoja raia wa Poland ameripotiwa kuweka nadhiri ya kusafiri katika kila mji duniani katika uchunguzi usio wa kawaida kulala na wanaume 100,000.

Ania Lisewska kutoka mjini Warsaw ameingia katika mpango huo usio wa kawaida kwenye mji aliozaliwa mwezi uliopita na mpaka sasa amefanikiwa kuongeza idadi hiyo kufikia 284, kwa mujibu wa gazeti la Huffington Post.

Lakini wakati rafiki yake wa kiume wa muda mrefu mwenye umri wa miaka 21 akimsamehe zaidi kuliko wote - hajamtosa pamoja na yote hayo - anaeleweka kwamba 'hajasisimuliwa' na wazo hilo.

Ania alisema kwamba rafiki yake huyo amelazimika 'kukubaliana na wazo hilo'.

Alilieleza gazeti la Austrian Times: "Nataka wanaume kutoka Poland, Europe na duniani kote. Ninapenda ngono, kufurahi na wanaume.

"Nchini Poland somo la ngono bado ni haramu na yeyote anayetaka kukidhi matakwa yao ya ngono huchukuliwa kama aliyepotoka, au mgonjwa wa akili."

Ania anasema kwamba atalenga tu kumaliza jukumu lake wakati wa siku za mwishoni mwa wiki na ameanzisha ukurasa wa Facebook na tovuti kusawiri mawazo ya wachimbaji kurasa wake ambao ni kidogo kuliko rafiki yake wa kiume anayevutiwa anaweza asipende kuwasevu kama watu wake muhimu.

Anaongeza kwamba anatarajia kutumia takribani dakika 20 na kila mpenzi mmoja.

Lakini taarifa za tamaa yake ya sasa ya kutaka makuu imeibua mashaka katika uhalalishwaji wake, huku ripoti kadhaa zikisema kwamba inaweza kuwa mzaha.

Kwa mujibu wa ripoti, kufanya ngono na watu wengi kiasi hicho kwa dakika 20 kwa wakati mmoja kunaweza kumchukua Ania miaka mitatu na miezi nane kumaliza kama hakutakuwa na mapumziko kwa ajili ya chakula au kulala.

Akionekana kanakwamba anapanga kuchukua nafasi ya siku za Jumamosi na Jumapili, jukumu hilo litamchukua miaka 20 mfululizo.

Ikichukuliwa anaishi hadi umri wa miaka 81, kufikisha 100,000 Ania atakuwa na hadi kiasi takribani wanaume 16 katika siku zote za mwishoni mwa wiki.

Fahamu Chumba cha Maajabu Kilichopo Juu ya Dunia..!!!

$
0
0

Sayansi ya Teknolojia ikiwa inaendelea kushika kasi siku hadi siku, chumba hiki maalum kilichojengwa juu ya safu za milima ya Alpine iliyopo Ufaransa kimepata kuwa kivutio kikubwa kwa watalii wanaotokea sehemu mbalimbali Duniani kutokana na staili ya aina yake walivyokitengeneza kwa kutumia vioo vilivyozunguka kichumba hicho kidogo hivyo kumuwezesha mtalii kuona kama vile yupo juu ya Dunia.

Unaambiwa sio rahisi kwa mtu mwenye roho nyepesi kuweza kusimama kwenye kichumba hicho kidogo kutokana na kuwa kileleni mwa mlima Alpine takribani umbali wa mita 3800 kutoka usawa wa bahari ambapo utengenezaji wake ulichukua takribani muda wa miaka miwili na ada ya kutembelea kwenye kivutio hicho ni kiasi cha Euro 55 ambazo ni sawa na Tsh 80,000 bila chenji (NADHANI WATAKUULIZA BARUA KUONESHA UMEAGA KWENU)

Treni za Umeme na Mafuta Kuanzishwa Tanzania..!!!

$
0
0

Rais wa Jamhuri ya Muungano Dkt. John Pombe Magufuli, amesema kuwa serikali imepanga kuondoa msongamano wa magari Jijini Dar es Salaam, ikiwa ni pamoja mpango wa kuanzisha safari ya treni ya mafuta na umeme kutoka Dar es Salaam hadi Morogoro. 

Rais Dk. Magufuli ametoa kauli hiyo leo Jijini Dar es Salaam wakati wa ufunguzi wa awamu ya kwanza ya mradi wa miundombinu ya utoaji huduma kwa mradi huo wa BRT uliogharimu shilingi bilioni 403 ambapo amesema ujenzi huo utakuwa ni wa jumla ya kilometa 200 ambapo mchakato wa kumpata mkandarasi umeanza na kuwa awamu ya pili itakuwa ni njia ya treni inayoelekea katika mkoa wa Dodoma.

Hata hivyo Rais amewataka mawaziri wa ujenzi, Tamisemi na pamoja na uongozi wa DART kuwasilisha taarifa ya faida ya mradi huo kuanza ili kufahamu kama mradi huo unaendeshwa kwa faida au hasara.

"Mawaziri mmetoa taarifa nzuri sana hapa lakini mmeninyima raha kwa kutonipa taarifa ya pesa za faida zilizopatikana kutokana na mradi huu" alisema Rais Magufuli

Amesema alitaka kujua kama zipo fedha za faida za mradi huo ili atoe maagizo kuhusu eneo la  Kimara kujengwa kituo kingine kikubwa sehemu ya kuegesha magari ili wenye magari binafsi waegeshe na kupata magari ya mwendo wa haraka.
Viewing all 104785 articles
Browse latest View live




Latest Images