Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104709 articles
Browse latest View live

Inahuzunisha Sanaa..!! Mtoto Ambaka Mama`ke Hadi Kifo ,Stori Kamili Hii Hapa..!!!

$
0
0

Dunia imekwisha! Hiyo ndiyo lugha nyepesi na rahisi unayoweza kuitumia kuelezea tukio hili. Januari 11, mwaka huu Tambani, Mbande wilayani Temeke jijini hapa, kijana mdogo, Hamis Lutani Kilumbi (21) anadaiwa kumbaka mama yake mzazi, Fatuma Mohammed Matutu (48) sambamba na kumchoma visu shingoni hali iliyomfanya apate maumivu makali hadi kufariki dunia Januari 21, mwaka huu katika Hospitali ya Taifa Muhimbili.dsc02127
Kaka wa mtuhumiwa
HII HAPA SIMULIZI YAKE

Akizungumza kwa uchungu na Amani wakati wa mazishi ya mwanamke huyo, mtoto mkubwa wa marehemu aitwaye Mohammed Ali, alisema kuwa siku ya tukio, mtuhumiwa ambaye ni mdogo wake anayemfuata kuzaliwa, alifika nyumbani kwao, alipokuwa akiishi mama yake majira ya mchana lakini hakumkuta.

“Baada ya kumkosa mama, alikuja nyumbani kwangu maana si mbali na anapoishi mama. Lakini pia mimi, mke wangu na mdogo wetu wa mwisho wa kike, Asma, ambaye naishi naye hatukuwepo. Kwa hiyo, Hamis aliacha ujumbe kuwa, tukirudi tupewe taarifa yeye alifika na mama alikuwa anatuhitaji.dsc02074
Kaka wa Marehemu
UJIO WA MTUHUMIWA WATIA SHAKA
“Sasa baada ya mimi kurudi nyumbani na kupewa taarifa hizo nilishangaa sana, kilichonishangaza si kuitwa na mama bali ujio wa Hamis nyumbani kwangu, maana nilikuwa sijaonana naye kwa muda usiopungua mwaka mzima kwa vile tuliwahi kutofautiana nikampiga marufuku kuja nyumbani kwangu na yeye akaahidi akiniona popote atanipiga na nondo,” alisema Mohammed.dsc02079
…Mwili wa Marehemu ukitolewa Mochwari
Hata hivyo, Mohammed alisema baada ya kuuliza juu ya wito wa mama yake, aliambiwa kuwa, Asma alishakwenda nyumbani na hakuwa anawaita kama alivyosema Hamis.

Mohammed akaendelea kueleza kuwa, baada ya maelezo hayo, aliamua kuendelea na mambo yake na alikwenda kutazama mechi ya mpira wa miguu kati ya Simba na Yanga runingani zilizokuwa zikicheza Zanzibar.

MLANGO WAGONGWA, WATOLEWA UJUMBE MBAYA

“Baada ya mechi nilirudi nyumbani na kulala. Jambo ambalo sikulitegemea ni kwamba, kufika usiku wa manane, ilikuwa yapata kama saa 8 hivi, majirani wa nyumbani kwa mama walikuja kunigongea, wakaniambia mdogo wangu Hamis anamuua mama.

“Nilikimbia mpaka eneo la tukio. Kiukweli nilimkuta mama akiwa na hali mbaya, alikuwa akivuja damu sana, kitenge na kanga alizokuwa amevaa vilikuwa vimelowa damu chapachapa.”dsc02078
…Mwili wa Marehemu ukitolewa Mochwari

“Niliumizwa mno na hali aliyokuwa nayo mama. Nilimuuliza nini kilimpata na kauli yake ya mwisho alisema; ‘mdogo wako Hamis anataka kuniua.’ Bila kupoteza muda, haraka tulimbeba mama na kumkimbiza kwa mwenyekiti lakini hatukumkuta, tukampeleka kwa mjumbe, akatuandikia karatasi kwa ajili ya kumkimbiza polisi.”

MAJERUHI ALALA NA MAUMIVU
Mohammed alizidi kusimulia kuwa, kutokana na mazingira wanayoishi, haikuwa rahisi kumkimbiza muda huohuo, wakasubiri kupambazuke kwanza na alfajiri walimpeleka kwenye Kituo cha Polisi cha Maturubai, wakaandikiwa PF3 na kisha kumpeleka Hospitali ya Temeke.

MADAKTARI WABAINI MAZITO
Mohammed: “Mama alifanyiwa vipimo na madaktari walithibitisha kuwa, aliingiliwa kinyume na maumbile lakini pia alichomwa visu shingoni. Alianza kupewa matibabu lakini hali yake ilizidi kuwa mbaya, tukamhamishia Hospitali ya Muhimbili kwenye wodi ya Kibasila. Bado hali ilizidi kuwa mbaya zaidi na Jumamosi ya tarehe 21, alipoteza maisha.”dsc02081
…Mwili wa Marehemu ukitolewa Mochwari

HUYU HAPA KAKA WA MAREHEMU

Naye kaka wa marehemu, Said Matutu, mkazi wa Mbagala Kokoto, Dar  alisema kuwa, amesikitishwa sana na tukio hilo lililosababisha kifo cha dada yake na kuongeza kwamba, mtuhumiwa anatafutwa na polisi ili aweze kufikishwa kwenye vyombo vya sheria.

“Kiukweli hili suala linasikitisha mno, huwezi kumfanyia mama yako mzazi kitendo kama hicho. Huo ni unyama uliopitiliza, mtu wa namna hii ni wa kuogopwa katika jamii,” alisema Said ambaye msiba ulifanyikia nyumbani kwake.dsc02089
…Jeneza likiandaliwa kuswaliwa.
TABIA ZA MTUHUMIWA
Hata hivyo, kaka huyo aliongeza kuwa, kabla ya tukio hilo alikuwa akipata malalamiko kutoka kwa dada yake (marehemu) juu ya tabia za uvutaji bangi, utovu wa nidhamu na tabia nyingine nyingi mbovu alizokuwa nazo mtuhumiwa, lakini pia aliwahi kuambiwa kijana huyo alikuwa ni mmoja wa vijana wahalifu maeneo ya Posta Mpya.dsc02098
…Mwili ukiswaliwa
MAZISHI YAKE
Marehemu Fatuma alizikwa Jumatatu iliyopita kwenye Makaburi ya Mbagala Mponda na ameacha familia ya watoto wanne, akiwemo mtuhumiwa.

KAMANDA WA POLISI TEMEKE
Naye Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Temeke, SSACP Gilles Muroto, alipotafutwa na mwandishi wetu na kuulizwa kuhusu tukio hilo, alisema taarifa hizo bado hazijamfikia lakini atafuatilia ili kujua kilichotokea.

Maajabu ya Mwaka 2017..Kijana Miaka 18 Ageuka ‘Mtoto’ Ghafla! Tazama Hapa Video..!!!

$
0
0

Katika hali isiyokuwa ya kawaida na kushangaza,  wananchi wa Kijiji cha Rokili, Halimashauri ya Wilaya ya Siha mkoani hapa, wapo kwenye mshangao kufuatia tukio la Kennedy Josia Nkini (18), kukumbwa na ugonjwa wa ajabu uliomsababisha kuwa mfupi ghafla.

Akizungumza na Gazeti la Amani juzi, mama mzazi wa mtoto huyo, Mary ambaye pia ni mgonjwa,  alisema mwanaye alizaliwa mwaka 1999 akiwa mzima wa afya ambapo aliendelea kukua vizuri hadi alipofikisha umri wa miaka  11 (2006), kipindi hicho akiwa mrefu tu, akaanza darasa la kwanza katika Shule ya Msingi Rokili iliyopo Siha.

Mama huyo alisema familia ni ya watu warefu sana hivyo mwanaye akiwa na miaka 10 tu tayari alikuwa mrefu,  sasa katika hali ya kushtua, siku moja mwanaye aliporudi shule alianza kunyonyoka nywele  kichwani na kuwashwa na kila alipojikuna nywele zilitoka. “Nilimuuliza labda ameiba maparachichi ya watu shambani akakataa, akasema hali hiyo ilimtokea ghafla.

Ndipo nilipompeleka Hospitali ya KCMC Moshi ambako alilazwa kwa ajili ya uchunguzi. “Siku iliyofuata asubuhi, niliitwa chumba cha daktari na kuulizwa mtoto wangu alikula chakula gani? Nikawaambia sikumpa chochote, wakanipeleka kumshuhudia. 

“Nilipigwa butwaa baada ya kumuona mwanangu. Hakuwa tena yule niliyeingia naye usiku wa jana yake, alikuwa mfupi kupita kiasi. Nilishangaa sana. Nikaangua kilio nikiwauliza madaktari kulikoni mwanangu amekuwa vile?

Na wao hawakujua kilichotokea,” alisema mama huyo. Mama huyo alisema, mtoto wake  aliendelea kulazwa KCMC miezi nane akimuuguza ambapo tayari ngozi yake ilikuwa imebadilika na kuwa na magamba kama ya mnyama,  miguu ikizidi kuwa midogo kama ya mtoto na kukosa nguvu ya kutembea. 

Alisema madaktari walijitahidi kumsaidia mtoto huyo lakini ikashindikana, hatimaye walimruhusu kuondoka naye kwa ajili ya kwenda kujaribu dawa za miti shamba ambazo pia hazikumsaidia.

Mama alisema, licha ya Kennedy kuwa hivyo, waliona aendelee na shule lakini na yeye mtoto licha ya maumivu makali, alipenda kusoma hivyo waliongea na walimu wa shule na kumruhusu kuendelea kusoma licha ya kwamba kulikuwa na hali ya kutengwa na baadhi ya wanafunzi wenzake ambao walikuwa wakimuogopa. 

“Baba yake anaitwa Josia Zefania Nkini ana miaka 59, alipata kazi ya ziada ya kumbeba mgongoni kumpeleka shuleni umbali wa kama kilomita tatu  na alitakiwa kumpeleka asubuhi na jioni kumfuata hadi alipomaliza darasa la saba mwaka jana na kufanikiwa kufaulu. 

Hapa anatakiwa kujiunga na kidato cha kwanza mwaka huu.” Kijana huyo amefaulu kutoka Shule ya Msingi Rokili ambayo ipo mlimani lakini sekondari aliyopangiwa kwenda ni ya Suumu, pia ipo Halmashauri ya Siha na  ipo mlimani juu kabisa ambapo kwa hali aliyonayo itakuwa ndoto kufika huko.

Kilio cha majirani, familia ya kijana mwenyewe  ni kwa Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi, Profesa Joyce Ndalichako na Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Said Mecky Sadick wamsaidie kumtafutia shule  itakayoendana na hali yake. 

Amani lilifanikiwa kuongea na kijana Kennedy ambaye licha ya hali yake lakini yeye anaona kawaida na anajichukulia kama binadamu wengine na ni mcha Mungu kwani hata Amani mara baada ya kufika nyumbani kwao, kabla ya mazungumzo alianza kumpa Mungu utukufu kwa kusali ndipo maongezi yaliendelea. 

Alisema: “Kaka mimi nimeshakubaliana na hii hali ya ulemavu ingawa bado nina tumaini siku moja Mungu anaweza kuniokoa na nikarejea kama zamani pamoja na urefu wangu, lakini kinachonipa mawazo muda mwingi ni kuhusu kusoma.

Napenda sana kusoma ndiyo maana hata darasani nimekuwa mtu wa kumi na kufanikiwa kufaulu.” 
“Naiomba serikali kupitia kwa waziri wa elimu inisaidie kunipatia shule ya walemavu, lakini nguo sina, baiskeli yangu imeisha, matairi yalishapasuka mwaka wa tatu sasa na mama yangu anaumwa mwaka wa pili huu,” alimaliza kusema.

Wajiua Huku Wakijirekodi Facebook ..!!!

$
0
0
Jay Bowdy (Kushoto) na  Nakia Venant (Kulia).

MWANAUME mmoja nchini Marekani anayejulikana kwa jina la Jay Bowdy, 34, ambaye pia ni muigizaji chipukizi amekutwa akiwa amejiua garini huku taarifa zikisema kwamba kabla ya kujiua, aliwaambia wafuasi wake kwenye Mtandao wa Kijamii wa Facebook kwamba anajiua hivyo wawapigie simu polisi kutoka hapo Los Angeles na kuwaambia kwamba alikuwa akijiua.

Baada ya kupewa taarifa na raia wema, polisi kutoka katika kituo kikuu hapo Los Angeles walijaribu kumpigia jamaa aliyelipaki gari lake katika ya Mitaa ya Cumpston na Fulcher lakini hawakuweza kumpata kwa kuwa tayari alikuwa amekwishatekeleza kile alichokitaka.

Watu waliokuwa wakifuatilia tukio hilo katika video hiyo iliyokuwa ikirekodiwa ‘live’ walipigwa na bumbuwazi kwani wengi walihisi kwamba alikuwa akiigiza kutokana na kazi yake hiyo kumbe mshikaji alikuwa akijiua kweli. Baadaye video hiyo ikatolewa mtandaoni na Facebook.

SABABU YA KUJIUA

Chanzo kilichokuwa hapohapo Los Angeles kinasema kwamba inawezekana Jay mwenye watoto wanne alijiua baada ya kupata msongo wa mawazo kwani alikuwa akikabiliwa na kesi ya kumdhalilisha kijinsia mwanamke mmoja huku akitakiwa kumlipa kiasi cha dola laki moja ambazo ni zaidi ya shilingi milioni 200.

MWINGINE NAYE AJIUA

Huku zikiwa hazijapita hata saa 12, msichana mmoja, Nakia Venant ‘14’ anayeishi Jijini Miami alifanya kama alivyofanya Jay kwa kujirekodi akiwa bafuni na kisha kujiua kwa kujinyonga kwa kutumia taulo lake alilolifunga bafuni mapema wiki hii.

Kifo cha Nakia kimezua hofu kwa wazazi wa maeneo hayo na polisi wa Jimbo la Florida wamesema kwamba wanaendelea kuchunguza kifo cha msichana huyo ambacho kimeonekana kuwa cha kipekee kwa kitendo cha kujirekodi ili wafuasi wake watazame anavyokufa.⠀

Mtu aliyeona tukio hilo na kumtambua mhusika alikuwa rafiki wa msichana huyo ambapo mara moja akawataarifu polisi na kuwaeleza kilichokuwa kikiendelea ambapo mpaka polisi wanafika eneo la tukio, tayari Nakia alikuwa amekwishafariki dunia.

Polisi hao wamewaambia waandishi wa habari kwamba kilichowafanya kuchelewa kufika huko ni kwamba rafiki wa Nakia alikosea kuwapa anwani ya kufika huko, kitu kilichowafanya kupotea, mpaka wanapata anwani yenyewe, wakawa wamekwishachelewa kufika huko kwa wakati.

Mbeya Tena..Mwalimu Amvua Nguo Mwanafunzi na Kumtembeza Uchi Madarasani ili Azomewe na Wenzake..!!!

$
0
0

MIEZI michache imepita jamii haijasahau tukio la walimu wa sekondari ya Mbeya kumdhalilisha mwanafunzi, tukio linalokaribiana na hilo limetokea kwenye sekondari ya Ihanga jijini hapa kwa mwanafunzi wa kidato cha pili, Caleb Mwita kuchaniwa suruali na kutembezwa uchi madarasa yote akizomewa na wanafunzi.

Akisimulia tukio hilo jana, mzazi wa mwanafunzi huyo, Joseph Mwita wa Soweto jijijni hapa, alisema lilitokea mwishoni mwa wiki baada ya kijana huyo kuvaa suruali isiyotakiwa siku hiyo shuleni ndipo Mwalimu Mapunda alipomwadhibu kwa kumchapa viboko tisa.

Kama haitoshi, Mwalimu Bathlomew Kibona alimchania suruali hiyo ikidaiwa haiendani na sare za shule hivyo alimvua mwanafunzi viatu akaichana na kumwacha viungo vikionekana na kumtembeza madarasani kuanzia kidato cha kwanza hadi cha nne huku wanafunzi wa jinsi zote wakishuhudia.

Mkuu wa Shule, Theresia Mwaifwani alikiri kutokea kwa tukio hilo, lakini akasema Mratibu wa Elimu Kata ndiye mwenye jukumu la kulizungumzia.

Mratibu, Magdeni Sindika naye alikiri kuwapo tukio hilo na kusema mwanafunzi Caleb alikiuka kanuni za shule.

Aidha, Sindika alisema adhabu ya walimu hao ilikuwa kubwa kwa mujibu wa sheria na watajadiliana na Ofisa Elimu wa Jiji, ili kuona adhabu wanayostahili walimu hao na kumwomba mzazi awasamehe kwa walilofanya na kuahidi kumtafutia shule nyingine mwanafunzi huyo ili asome bila fadheha.

Mzazi Mwita alisema hapingi adhabu ya walimu hao lakini kitendo cha kuchaniwa suruali na kudhalilishwa kwa wanafunzi wenziwe hali na kumfanya kijana wake aathirike kisaikolojia hakikubaliki.

Caleb alisema suruali aliyovaa ni ya shule isipokuwa siku hiyo alivaa nyeusi badala ya kahawia na haikuwa inabana kama ilivyodaiwa na walimu na pia adhabu ya viboko ilitosha na si kuchaniwa suruali na kutembezwa madarasani akiwa uchi.  

Ofisa Elimu Taaluma wa Mkoa, Protas Mpogole alikiri kupata taarifa ya kutokea kwa tukio hilo na
kwamba Halmashauri ya Jiji Kitengo cha Elimu inashughulika suala hilo.

Kudadadeki..Harmonize aanza Kumfukuzia Diamond kwa Mkwanja,Anunua Mikufu ya Dhahabu Mikali Zaidi ya Mikufu ya Diamond,(VIDEO)

$
0
0

Katika kudhihirisha naye zimo,Staa kutoka label ya WCB,Harmonize ameanza kumwaga manoti ovyo katika matumizi mbalimbali anayoyafanya.

Harmonize ambaye hivi karibuni inasemekana kuwa Amemwagana na Wolper,Aliingia katika duka la sonara na kununua vito vya thamani kubwa vya rangi ya dhahabu kama vile pete,saa na mkufu .

Haikuweza kufahamika mara moja gharama alizolipa staa huyo,ila inakadiriwa si chini ya milioni 10 ili kufanikisha manunuzi hayo.


TAHADHARI: DECI mpya zaibukia Mwanza..Hii Ni Kauli ya Jeshi la Polisi Jijini Mwanza

$
0
0
Jeshi la Polisi Mkoani Mwanza, linamshikilia Mkurugenzi wa kampuni binafsi iitwayo AQ Computer  Co.Ltd na wenzake 7 kwa tuhuma za kukusanya fedha zaidi ya shilingi 100,000,000/= kutoka kwa wananchi kwa njia za udanganyifu.



Kamanda wa Polisi mkoa wa Mwanza DCP Ahmad Msangi amesema mkurugenzi huyo anayefahamika kwa jina la Happy Aloyce Mbuya miaka 35 mkazi mtaa wa Ilemela, kwa kushirikiana na wenzake 7 kupitia taasisi ya AQ Power Club wamekuwa wakiendesha moja ya vikundi vinavyojihusisha na biashara ya upatu jijini Mwanza, inayotambulika kwa jina lisilo rasmi la kupanda mbegu na kuvuna.

Amesema upelelezi umebaini kuwa watuhumiwa hao wamekuwa wakiwashawishi wananchi kwa kuwadanganyana kuwarubuni wajiunge na biashara ya upatu ambapo wananchi hao hushawishiwa kuwekeza fedha kidogo kwa muda mfupi katika vikundi hivyo na baada ya hapo wanaahidiwa kulipwa fedha nyingi zaidi ya zile walizowekeza bila kufanya kazi yeyote.

Aidha Kamanda huyo wa Polisi mkoa wa Mwanza anatahadharisha wananchi kuhusu shughuli zinazofanywa na kikundi/ kampuni nyingine binafsi ya Bega kwa Bega Microfinance Company Ltd, kutokana na watu wengi kuripoti polisi juu ya kutapeliwa fedha zao na kampuni hiyo.

Taasisi nyingine aliyoitaja kufanya biashara hiyo ya upatu ni 'Amka Mwanamke' (AMWA) na kwamba uchunguzi unafanywa ili kuweza kubaini ukweli wa taarifa hizo.

Amesema tayari jeshi hilo limewatia mbaroni wakurugenzi na baadhi ya wafanyakazi wa kampuni hiyo na majalada ya kesi hizo yapo kwa mwanasheria wa serikali kwa hatua zaidi za  kisheria.

Endapo tuhuma hizi zitathibitik, taasisi hizo ambazo ni AQ Power Club, Bega kwa Began a AMWA zitakuwa ni sawa na taasisi ya aina hiyo iliyojulikana kwa jina la DECI ya Jijini Dar es Salaam ambayo ilibainika kufanya utapeli wa njia hiyo mwaka 2008 na kuchukuliwa hatua za kisheria

Kiasi cha Fedha Serikali ilichopata Tangu Kuanza Mradi wa Mabasi ya Mwendokasi

$
0
0
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), George Simbachawene amesema kuwa kwa kipindi cha kati ya mwezi Mei hadi mwezi Disemba mwaka jana, serikali ilifanikiwa kukusanya kiasi cha fedha TZS bilioni 19 katika mradi wa mabasi yaendayo haraka.

Hayo yamesemwa na Waziri Simbachawene leo jijini Dar es Salaam alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari ikiwa ni siku moja tangu Rais Dkt Magufuli alipomtaka waziri huyo kwa kushirikiana na Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Prof. Makame Mbarawa kueleza umma nikiasi gani wamekusanya ili ifahamike kama mradi huo unaingiza faida au ni hasara.

Waziri Simbachawene pia ameagiza vikosi vya ulinzi na usalama kuhakikisha vinawaondoa wafanyabiashara wadogo maarufu kama machinga wanaofanya biashara zao ndani ya eneo la barabara hiyo kitu ambacho ni kinyume na sheria.

Aidha, wakati huo huo Waziri Simbachawene amewaagiza Wakuu wa Mikoa yote nchini kuhakikisha wanawachukulia hatua za kisheria wazazi wote wanaotekeleza watoto wao au kuwatuma kwenda kuwa ombaomba jambo linalopelekea ongezeko la watoto wa mitaani.

Mkuu wa Wilaya Tabora Ajiuzulu...Amwandikia Barua Rais Magufuli

$
0
0
Mkuu wa Wilaya ya Uyui mkoani Tabora, Gabriel Simon Mnyele amejiuzulu nafasi hiyo leo Alhamisi Januari 26, 2017 na kuwaaga madiwani wa Chama cha Mapinduzi (CCM) katika mkutano alioufanya wilayani humo.

Akieleza sababu ya kufanya uamuzi huo, Mkuu huyo wa wilaya alisema kuwa alimwandikia Rais Dkt Magufuli barua ya kujiuzulu nafasi hiyo akielezea kusongwa na majukumu binafsi.

Mkuu wa Wilaya, Gabriel Simon Mnyele alikuwa miongoni mwa Wakuu wa Wilaya 139 walioteuliwa na Rais Dkt. John Pombe Magufuli tarehe 26 Juni, 2016.

Mtazamo:Ngoma Mpya ya Joh Makini Waya ni Dhaifu Kuliko Ngoma zote Alizowahi Kutoa

$
0
0
Baada ya kutuhumiwa kwamba anabebwa, sasa kakurupuka na kutuletea ngoma ambayo kwa mtazamo wangu ni dhaifu kuliko zote alizowahi kuzitoa.

Kiukweli hii ngoma haitakua na maisha marefu katika game hii yenye ushindani mkubwa yaani labda aendelee kubebwa kama kweli madai ya Young Msodoki ni kweli..

Namshauri ajitafakari na akajipange upya au arudi kwa producer wake wa zamani

By DJ Zappa

Isikilize Hapa:

Hivi zile Zaidi ya Millioni Mia Tano za yule Mshindi wa Big Brother zimeyeyuka?

$
0
0
Wakati huu wa maisha magumu na pesa imekuwa ngumu kupatikana,
Nikawaza zile millioni mia tano za yule aliyekuwa mshindi wa shindano la Big brother Afrika, bwana Idriss Sultan ni kwamba ametumbua zile pesa zote zimeisha na kubaki kapuku bila ya kuwa na uwekezaji wowote mpaka sasa kubaki mweupe na kushiwa kabisa?

Maana nusu billioni navyofikiria mimi kama ningeipata wakati huo nafikiri rafiki zangu wangekuwa Magufuli au Kikwete labda ningekuwa level hizo za maisha kwa mafanikio.

Sasa ni kweli huyu jamaaa kafirisika kabisa bila kuwa hata na uwekezaji?

By Tomahawk/JF

Waziri TAMISEMI, Simbachawene Amtega Makonda, Ampa Siku 3 Kuwaondoa Machinga Katika Barabara za DART

$
0
0
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais - TAMISEMI, George Simbachawene amemwagiza Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Paul Makonda pamoja na Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Sophia Mjema kuwaondoa wamachinga wanaofanya biashara katika miundombinu ya barabara za mwendokasi (DART) ndani ya siku tatu kuanzia leo

Simbachawene amezitaka mamlaka ya Mkoa wa Dar es salaam, na Wilaya ya Ilala kuhakikisha kwamba wamachinga hawarudi katika maeneo hayo kwa namna yoyote ile na kwamba hilo likishindikana, viongozi husika watakuwa wameshindwa kazi

"Ninaagiza wamachinga waondoke katika miundombinu ya barabara za BRT, Rais John Magufuli alipoagiza wasibughuziwe hakumaanisha wakae eneo lisilostahili, au wawe wanakaa barabarani, alimaanisha wamachinga wastaarabu wanaofuata sheria na wala hakuwaagiza wavunje sheria na kukiuka haki za baadhi ya watu", alisema na kuongeza 

"Nikiona wamerudi, Mkuu wa Mkoa na Wilaya kazi itakuwa imewashinda". 

Aidha, amewataka wamachinga kuondoka kwa hiari yao na kwamba kama wakikaidi agizo hilo mamlaka husika zitawaondoa kwa nguvu

"Wengi wanakaa katika makutano ya barabara hasa maeneo ya Fire, Kariakoo na kituo kikuu cha Gerezani. Hali hii inahatarisha usalama wa waenda kwa miguu sababu wengi hunusurika kupata ajali", alisema 

Pia amesema wamachinga hao ni changamoto kwa usafiri wa mwendokasi

"Changamoto ya Dart ni wamachinga kufanya biashara katika barabara za DART. Hii suala halikubaliki kabisa na halivumiliki na tutatumia nguvu kuwaondoa", alisema 

Chanzo : Dewji blog

VIDEO: Anna Mugwhira ACT Ajibu Swali la Zitto Kabwe Yuko Wapi?

$
0
0
Baada ya taarifa kutoka jeshi la polisi Shinyanga kuhusu kukamatwa kwa gari alilokua analitumia kiongozi wa chama cha ACT WAZALENDO ambae pia ni Mbunge wa Kigoma mjini Zitto kabwe.

Ilidaiwa kwamba sababu ya gari hilo kukamatwa ni kosa la kutokuwa na vibali halali huku Polisi ikimtaka Zitto ajitokeze.

Mwenyekiti wa chama cha ACT Wazalendo Mama Anna Mugwhira ameongea na AzamTV kuhusu uwepo wa taarifa za kutoonekana kwa kiongozi wa ACT Zitto Kabwe.

‘Zitto alikuwa anatafutwa na polisi na mimi nilikuja kusikia gari limekamatwa lakini yeye aonekani, inaonekana yeye aliposhuka aliondoka na njia nyingine tofauti hakuondoka na gari lake, sisi kama chama hatukufikia mahali pa kufikiri kwamba hayupo au haonekani na taarifa zilizokuwa zinapatikana zilisema yupo Kahama, taarifa rasmi haijatolewa na yeye mwenyewe’;-Anna Mugwhira
Tazama Video:

Taarifa Kuhusu Mchezaji Emmanuel Adebayor Kuja Kucheza Yanga ya Tanzania Hii Hapa

$
0
0
Emmanuel Adebayor 
Jana January 25 2017 moja kati ya taarifa zilizokuwa zimeenea katika mitandao ya kijamii ni kuhusiana na mshambuliaji wa kimataifa wa Togo aliyewahi kucheza Arsenal, Man City, Tottenham Hotspurs na Crystal Palace  Emmanuel Adebayor kuripotiwa kujiunga na  timu ya Yanga.

Habari kutoka soka25east.com na mitandao mingine mitatu ya Kenya zilisema kuwa staa huyo atajiunga na Mabingwa watetezi wa Ligi Kuu Tanzania bara Yanga ambayo pia inachezewa na Vincent Bossou anayechezea timu moja ya taifa na Adebayor na walikuwa pamoja AFCON juzi.

Saa 24 baada ya taarifa hizo kupita mitandao ya Skysports na BBC SPORTS imeripoti na kumnukuu Adebayor kuhusu mpango wake wa sasa katika soka akiwa mchezaji huru, anasema bado ana mpango wa kurejea ligi kuu England na hajaizungumzia Yanga hata tone, hiyo imedhihirisha kuwa tetesi za kujiunga na Yanga sio za kweli.

Nimepokea ofa chache kutoka timu za ligi kuu England na wote mnajua napenda kucheza England, licha ya kuwa mimi sio moja kati ya wachezaji wanaopendwa England nimecheza England kwa miaka kumi, ieleweke pia sikuja AFCON kucheza ili nipate timu nilikuja kuwakilisha taifa langu

Hawa Ndio Mastaa 20 wa Kike Bongo Wenye Followers Wengi Instagram

$
0
0
Mtandao wa Instagram kwa sasa unaonekana kutumiwa zaidi na watu wengi sio Tanzania pekee bali ni dunia nzima kwa ujumla. Ila kwa Afrika mastaa wa Bongo wanaonekana kupata followers wengi zaidi kwenye mtandao huo wakifuatiwa na mastaa wa Nigeria.

Kwa mujibu wa utafiti uliofanywa na Bongo5, tumekuletea awamu ya kwanza ya orodha ya mastaa 20 wa kike Bongo wenye followers wengi kwenye mtandao huo wakiongozwa na malkia wa filamu nchini Madam Sepenga.

Tazama hapa chini orodha hiyo iliyowajumuisha mastaa kibao wakiwemo waigizaji, wasanii wa muziki, wanamitindo na wafanyabiashara kwenye tasnia ya burudani.

1.@ wemasepetu – 2.5M


2.@ wolperstylish – 2.4M



3.@ jokatemwegelo – 2.3M



4. @shilolekiuno_badgirlshishi – 2.2M



5.@auntyezekiel – 2.2



6.@vanessamdee – 2.1M



7.@shamsaford – 2M



8.@ elizabethmichaelofficial – 1.9M



9.@ officiallinah – 1.9M



10.@rossendauka – 1.7M



11.@new_kajala – 1.7M



12.@jidejaydee – 1.3M



13.@hamisamobetto – 1.3M



14.@queendarleen_ – 913K



15.@flavianamatata – 729K



16.@ireneuwoya8 – 747K



17.@j_n_mengi – 678K



18.@faizaally_ – 657K



19. @mspaulsen – 654K



20.@mwasitij – 642K

Wanawake Waliosoma Sheria (Law) Ndio Wanaoongoza Kuwa 'Single Mothers' Tanzania

$
0
0
Habarini Wadau,

Hilo nililoliandika nimelifanyia utafiti wa kina.

Tofauti na mabinti/wanawake waliosoma courses zingine...waliosoma Law wengi hawajaolewa ila wanamegwa tu kisela na wengi wao wana mtoto au watoto ila hawana waume.

Sababu kubwa ni hizi:

◆ Hakuna Mwanaume anayetaka kuletewa vifungu vya sheria kwenye nyumba yake na ujinga ujinga wa haki sawa.

◆ Wanawake wa hivyo wanakuwaga na ukatili na kujiamini kupita kiasi, nafikiri ni kutokana na hukumu wanazosoma

◆ Wakati huo huo waalimu ndio wanaoongoza kwa kuolewa na kuishi vizuri ndoani.


Nawasilisha.
Azarel



Kwanini Sisi Wanawake/Wasichana Wanene na Wenye Makalio Hatupati Waume wa Kutuoa?

$
0
0
Nimefanya uchunguzi yakinifu na nikajiridhisha kwa 95% kuwa sie wanawake wanene na wenye makalio makubwa huwa ni ngumu sana kuolewa, kwa nini?

1. Tunaongoza kwa kuwa vimada kwa waliooa, lakini sisi hatuolewi:
(a) Miili yetu imepitwa na wakati?
(b) Labda wanadhani tutashindwa mechi?.

2. Tufanyaje ili nasi tupate wanaume wa kutuoa?
(a) Tuifanyie miili yetu diet/tujikondeshe ili tuwe wembamba,
(b)Tuanze kuwatongoza wanaume.

NALILETA MEZANI TULIJADILI.

Wazee 2 Mbaroni kwa Ubakaji, Ulawiti Watoto 11

$
0
0

WAKAZI wawili akiwemo Mustafa Kassimu (75) ambaye ni mganga wa tiba za asili katika wilaya ya Korogwe mkoani Tanga na fundi wa kushona nguo, Rashidi Singano (70) wa wilayani Lushoto, wanashikiliwa na polisi kwa tuhuma za kubaka na kulawiti wanafunzi 11 wa shule za msingi.

Katika tukio la kwanza la Januari 24, mwaka huu, Polisi inamshikilia fundi cherehani huyo ambaye anaishi Kijiji cha Mshwamba Kata ya Lunguza wilayani Lushoto kwa tuhuma za kubaka na kulawiti kwa nyakati tofauti watoto 10 (majina yamehifadhiwa).

Mtuhumiwa huyo inadaiwa alitumia ushawishi wa kuwapa fedha kati ya Sh 300, Sh 600 hadi Sh 1,000 na kuwavizia njiani, kama mbinu ya kuwanasa watoto hao, ambao wote ni wanafunzi katika moja ya shule ya msingi iliyopo Kata ya Lunguza.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga, Benedict Wakulyamba alithibitisha tukio hilo kwa kuwaeleza waandishi wa habari kwamba walipata taarifa za ukatili dhidi ya watoto hao kutoka kwa mwalimu wa watoto hao, ambaye jina lake limehifadhiwa.

“Tulipokea taarifa kuhusu tukio hilo kutoka kwa mwalimu wa shule wanayosoma watoto hao, akidai kwamba siku hiyo akiwa shuleni, aligundua kuwa wanafunzi kumi wa kike kati yao sita wote wakiwa wamebakwa, huku wengine wanne wakiwa wamelawitiwa kwa nyakati tofauti na fundi cherehani huyo,” alieleza.

Aliongeza, “Mwalimu huyo alitaja wanafunzi wengine watano na kudai kwamba hao wamenusurika kunaswa kwenye mtego wa kutendewa ukatili huo na Mzee Singano ambaye anaishi maeneo ya jirani na shule hiyo,” alieleza Kamanda Wakulyamba.

Alisema katika uchunguzi, imebainika kwamba mtuhumiwa alikuwa akifanya vitendo hivyo vya kubaka na kulawiti watoto hao ndani ya nyumba anayoishi pamoja na kufanyia shughuli hizo za ushonaji, na aliwapata wakati walipokuwa wakienda kupeleka nguo na wakati wa mchana wanapotoka shuleni kurejea nyumbani.

“Chanzo cha tukio hili kwa kweli ni tamaa mbaya za kimwili alizokuwa nazo mtuhumiwa ambapo alikuwa akiwalaghai wanafunzi hao kwa kuwapa fedha kati ya shilingi mia tatu hadi mia sita wakati wanapopeleka nguo zao kushonwa,” alifafanua.

Tukio la pili linamhusisha mtoto mwingine mwenye umri wa miaka 12, ambaye ni mwanafunzi wa darasa la tatu (jina limehifadhiwa) wa Kijiji cha Fune wilayani Korogwe aliyelawitiwa na Kassimu (75) wakati alipokuwa akimpatia matibabu ya asili, yaliyolenga kumwongezea nguvu za kiume.

Hii Hapa Sababu ya Mkuu wa Wilaya ya Uyuni Kuamua Kujiuzulu,Kumbe Aliandika Barua ya Kujiuzulu Toka Mwaka Jana..!!!

$
0
0

MKUU wa Wilaya ya Uyui mkoani Tabora, Gabriel Mnyele ameachia ngazi wadhifa huo kuanzia jana.

Mnyele, ambaye alikuwa wakili maarufu nchini kabla ya kuteuliwa kuwa mkuu wa wilaya, imeelezwa kuwa ameamua kujiuzulu kwa sababu binafsi.

Lakini, akizungumza  kwa simu jana, Mnyele alisema kwamba, “Ukiteuliwa, mamlaka husika inatoa taarifa, na ukiondoka katika nafasi hiyo mamlaka inatoa taarifa. Kwa hiyo mtafuteni Msigwa (Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu). Lakini sisi tuko huku tunaendelea na kazi.”

Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Aggrey Mwanri hakupatikana kuelezea kwa undani uamuzi huo, lakini gazeti hili limethibitishiwa na viongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Uyui kwamba Mnyele amejiuzulu na aliwaeleza hayo jana alipopita kuwaaga.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Uyui, Said Ntahondi alisema kwamba anawatakia kila la heri katika majukumu yao ya kazi. Alisema kwamba licha ya yeye (DC Mnyele) kuondoka, anatambua kuwa mapambano juu ya maendeleo ya Uyui, yataimarika kwa watumishi wote wa halmashauri hiyo.

Kwa mujibu wa taarifa yao, Mnyele alipita kila Idara za Halmashauri ya Wilaya hiyo kuaga akianzia na watumishi wa ofisi yake.

Taarifa za awali zinasema kuachia kwake ngazi ya ukuu wa wilaya imetokana na kutingwa na majukumu mengi binafsi aliyonayo, na kwamba imedaiwa kuwa mkuu huyo wa wilaya aliandika barua mwaka jana akiomba kujiuzulu nafasi hiyo, kwani ametingwa na majukumu mengine binafsi.

Taarifa zaidi zinasema baada ya kuandika barua ya kuutema ukuu wa wilaya, barua yake imejibiwa na amekubaliwa kuachia nafasi hiyo.

Mnyele alikuwa mmoja wa wakuu wa wilaya 139 walioteuliwa na Rais John Magufuli, Juni 26, 2016, ambao ilielezwa kuwa amezingatia mambo kadhaa, ikiwa ni pamoja na umri ambapo kwa wale ambao umri wao ni zaidi ya miaka 60 ameamua wastaafu.

Wizara ya Afya Kuhmia Dodoma Ndani ya Siku 14 Zijazo..!!!

$
0
0

WIZARA ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto itahamia Dodoma ndani ya siku 14 zijazo.

Waziri Ummy Mwalimu amesema tayari wizara yake imejiandaa kuhamia Dodoma, kutekeleza agizo la Rais John Magufuli la serikali kuhamia Dodoma kabla ya 2020.

“Tutahamia Dodoma ndani ya muda wa wiki mbili,” alisema Ummy wakati akifungua semina ya kitaifa ya afya mjini hapa juzi. Aliwatangazia wadau wa afya nchini kwamba atatangaza kabla ya kuhamia Dodoma ni huduma gani zitaendelea kutolewa Dar es Salaam na zile zitakazohamishiwa Dodoma.

Alithibitisha kwamba ofisi yake kama waziri, ya naibu waziri, na Katibu Mkuu wake wa wizara, hazitabaki Dar es Salaam, bali zitakuwa Dodoma.

Kuhamia kwa wizara hiyo Dodoma, itakuwa ni wizara ya tano, uhamisho huyo ulitanguliwa na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa aliyehamia Septemba mwaka jana na baadaye akafuata Waziri wa Nchi katika ofisi yake, Jenista Mhagama anayeshughulikia Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Walemavu.

Mawaziri wengine waliohamia Dodoma ni wa Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, George Simbachawene na msaidizi wake, Selemani Jafo pamoja na Waziri wa Katiba na Sheria, Dk Harrison Mwakyembe na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Angellah Kairuki.

Kutokana na ratiba iliyotangazwa na Waziri Mkuu mwaka jana, waziri mkuu na mawaziri wote pamoja na makatibu wakuu wa wizara, wanatakiwa kuwa tayari wamehamia Dodoma kufikia Februari 28, mwaka huu.

Ratiba hiyo inaonesha kati ya Machi na Agosti mwaka huu, watendaji wa wizara wanatakiwa kupanga na kutenga bajeti kwa maofisa wao kuhamia makao makuu ya nchi.

Watu 14 Akiwamo Mchina Wafukiwa Mgodini Geita

$
0
0

Watu 14 akiwemo Mchina, wanahofiwa kufa baada ya kufukiwa katika mgodi wa dhahabu wa Kampuni ya RZ Union Mining Ltd uliopo Kata ya Nyarugusu mkoani Geita.


Mkuu wa Mkoa wa Geita, Ezekiel Kyunga jana alisema watu hao wamefukiwa chini ya mgodi baada ya mlango wa kuingilia kwenye shimo la mgodi kumeguka udongo na kujiziba.


“Usiku wa kuamkia leo (jana) saa tisa kwenye mgodi huo unaoendeshwa na Wachina, mlango wa kuingilia mgodini mmoja ulimeguka na kujifunga watu 14 wakiwa ndani,” alisema Kyunga.


Kyunga alisema kwa mujibu wa kitabu cha orodha ya watu wanaojiandikisha kuingia mgodini, kuna majina ya Watanzania 12 na Mchina.


Aidha, alisema mbali na watu hao 13, pia kuna Mtanzania mmoja ambaye aliingia bila kujiandikisha na hiyo ni kwa mujibu wa watu walioshuhudia tukio hilo hivyo kufanya idadi ya watu waliofukiwa kuwa 14. 


Kyunga alisema tangu jana asubuhi jitihada mbalimbali za kuondoa udongo kuwaokoa watu hao zinaendelea wakitumia mitambo na wataalamu.


“Kwa kusaidiana na Kampuni ya Geita Gold Mine (GGM) na wataalamu wengine, jitihada zinaendelea ili kuhakikisha tunawaokoa watu hao,” alisema Kyunga. 


Alisema wakati huo huo wamefanikiwa kutoboa eneo jingine na kupitisha mabomba ya hewa ya oksijeni ili kuwafanya watu hao wasikose hewa.

Ajali
Viewing all 104709 articles
Browse latest View live


Latest Images