Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104431 articles
Browse latest View live

Jitihada za Kuendelea Kuokoa Waliofukia Mgodini Zaendelea..!!!

0
0

Jitihada za kuwatafuta wachimbaji wadogo 14 wa mgodi wa dhahabu wa RZ uliopo Nyarugusu mkoani Geita waliofukiwa na kifusi baada ya udongo kuporomoka mpaka usiku zilikuwa zikiendelea.

Wachimbaji hao wamefukiwa kwenye shimo lenye urefu wa mita 38 walimokuwa wanachimba dhahabu .

Tukio la kuporomoka kwa shimo hilo lilitokea saa tisa usiku wa kuamkia jana na wachimbaji 13 raia wa Tanzania na mmoja mwenye asili ya China walikuwa ndani.

Akielezea tukio hilo, msemaji wa kampuni ya RZ, Francis Kiganga alisema shimo lililofukiwa na udongo licha ya kuwa na urefu wa mita 38 kwenda chini, pembeni lina njia yenye urefu wa mita nyingine 38.

Alisema sababu za udongo kuporomoka na kuziba njia ni eneo hilo kuwa na mashimo mengine yaliyochimbwa na wakoloni miaka ya 60 iliyopita na kusababisha udongo kutitia.

Mmoja wa wachimbaji aliyeshuhudia tukio hilo, Lucas Misalaba  alisema saa nane usiku waliona shimo likititia ndipo walitoa taarifa kwa wenzao walioko chini kusogea na kukaa pembeni na baada ya muda kidogo shimo lote lilifukiwa na udongo.

Akizungumza baada ya kutembelea eneo hilo, Mkuu wa Mkoa wa Geita, Ezekiel Kyunga alisema yapo matumaini kwamba wachimbaji hao watakuwa hai na kuitaka idara ya madini mkoa kuongeza nguvu za uokoaji ili kuwanusuru wachimbaji hao.

Watanzania 8 Waliokamatwa Malawi Kujadiliwa..!!!

0
0

TUME ya Ushirikiano wa Pamoja ya Kudumu (JPCC) kati ya Tanzania na Malawi, inatarajia kukutana nchini humo kwa ajili ya kujadili masuala mbalimbali, ikiwemo la Watanzania nane kukamatwa nchini humo kwa tuhuma za kuingia eneo la migodini bila kuwa na kibali.

Mbali na kujadili suala la Watanzania hao, lakini pia tume hiyo itajidili mgogoro wa mpaka uliopo baina ya nchi hizo mbili katika Ziwa Nyasa.

Mkutano huo unatarajiwa kuanza Februari 3 hadi 5 mwaka huu nchini Malawi.

Akizungumza Dar es Salaam, Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mindi Kasiga alisema tume hiyo ilikuwa haijakutana kwa muda mrefu, jambo ambalo limesababisha watu kuwa na sintofahamu kati ya ushirikiano wa nchi hizo mbili.

Kasiga alisema mkutano wa tume hiyo, mara ya mwisho ulifanyika mwaka 2003 jijini Dar es Salaam, hivyo kuwa kimya kwa muda mrefu kuna baadhi ya watu walidhani kuwa ushirikiano wa nchi hizo mbili si mzuri.

“Kikao kama hiki kilikaa miaka mingi kidogo… kuna masuala yaliyochelewa kutekelezwa kutokana na kukaa kwa kikao hiki, lakini kwa sasa yatatekelezwa kupitia vikao hivyo,” alisema Kasiga.

Aliongeza kuwa kwa mara ya kwanza, vikao hivyo vitashirikisha wafanyabiashara kutoka mikoa ya Njombe na Ruvuma, pia wavuvi kutoka katika mikoa hiyo ambao wataeleza namna wanavyofanya shughuli zao kwa kushirikiana na wenzao wa Malawi bila kuingilia.

Mindi alisema katika kikao hicho, ujumbe wa Tanzania utaongozwa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Dk Augustine Mahiga; na mbali na kujadili mgogoro wa mpaka wa Ziwa Nyasa na Watanzania waliokamatwa, pia utajadili masuala mbalimbali katika sekta za biashara, elimu, kilimo pamoja na sekta zingine.

Kasiga pia alikabidhi tuzo za Mamlaka ya Usimamizi na Udhibiti wa Sekta ya Hifadhi ya Jamii (SSRA) pamoja na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) walizoshinda kutoka Umoja wa Afrika (AU). SSRA ambayo imekuwa wa kwanza katika Tuzo za Ubunifu Katika Sekta za Umma Afrika (AAPSIA), ilikabidhiwa kikombe pamoja na cheti cha ushindi.

Ushindi huo wameupata kupitia mradi wao wa Mradi wa Kanzidata ya Taifa ya Sekta ya Hifadhi ya Jamii.

Pitia Vichwa vya Magazeti ya Leo 27/1/2017..!!!

CHADEMA- Jengo la Makao Makuu ya Chama Ni Letu,Hakuna wa kutupa Notisi ya Kuhama..!!

0
0

CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimesema nyumba iliyopo Mtaa wa Ufipa katika Manispaa ya Kinondoni jijini Dar es Salaam, inamilikiwa na chama hicho kupitia Baraza la Wadhamini.

Chadema imetoa ufafanuzi kutokana na taarifa zilizosambaa katika mitandao ya kijamii kuwa wamepewa notisi ya siku 14 na mmiliki wa jengo hilo, wanalotumia kama ofisi na Makao Makuu ya chama hicho, kuhama kutokana na kukiuka mkataba wa malipo na upangishwaji.

Ofisa Habari wa Chadema, Tumaini Makene akijibu uvumi huo, alisema chama hicho ni mmiliki halali wa jengo la Makao Makuu lililo chini ya Baraza la Wadhamini.

“Kama kuna mmiliki wa jengo hilo ajitokeze, lakini nawahakikishia hakuna hivyo puuzeni habari zinazozagaa,” alisema Makene na kuongeza kuwa kuna hati ya jengo hilo, iliyoandikwa mmiliki wa jengo hilo ni Chadema. Alisisitiza watu wapuuzie propaganda hizo, zinazopanga kuwahadaa wanachama na Watanzania kwa ujumla.

Baada ya Kimya Kirefu,Makonda Aibuka na Hili Jipya ..!!!

0
0

KATIKA kuboresha huduma ya usafiri wa teksi mkoani Dar es Salaam, Mkuu wa Mkoa huo, Paul Makonda amewataka madereva wa usafiri huo kuhakikisha wanakaa na kujadili mfumo bora wa uendeshaji wa biashara zao kwa manufaa yao na abiria.

Makonda alitoa kauli hiyo wakati akizungumza na madereva teksi wa mkoa huo ili kuzungumza namna bora ya kuboresha huduma hiyo na kuwa ya tofauti.

“Nawapa wiki moja mkae mjadiliane na mkija hapa mje na majibu ya kutatua kero zenu pamoja na namna bora ya kuendesha biashara zenu bila bugudha,” alisema Makonda.

Alisema katika kuboresha huduma hiyo ni lazima kiwepo mfumo mzuri ambao utakuwa na manufaa kwa madereva hao pamoja na watumiaji hivyo anataka mfumo wa ukadiriaji wa gharama za usafiri wa teksi uondoke katika mkoa huo na abiria wasikadiriwe gharama badala yake anapaswa kujua gharama

. “Azma ya Serikali ni kuboresha huduma za usafiri na kuwa wa kipekee ili kukamilisha hilo nataka teksi zote kuanza kutumia vifaa maalumu vitakavyoonesha umbali wa eneo analokwenda abiria kuondoa gharama za ukadiriaji kwani kwa kufanya hivyo kutaisaidia Mamlaka ya Mapato (TRA) kuwatoza kodi stahiki kulingana na magari yenu,” alisema Makonda.

Aidha Makonda alisema serikali yake imejipanga kuziondoa teksi bubu zote, na utaratibu wa kuweka rangi na namba kwenye magari utarudi ili magari yatambulike.

“Tutaziondoa teksi bubu zote na yeyote atakayetumia akumbuke akikumbwa na tatizo hakuna atakayemsaidia, tutaendeleza mfumo wa kupaka rangi na kutoa namba kwa teksi zote ili kuhakikisha huduma zinakuwa bora, “ aliongeza.

Kwa upande wake, Makamu Mwenyekiti wa madereva wa teksi Ilala, Jacob Anyandwile, alimuelezea Makonda changamoto mbalimbali wanazokutana nazo kuwa ni pamoja na kutozwa kodi kubwa na TRA pamoja na uwepo wa huduma ya teksi kwa njia ya mtandao unafanywa na kampuni ya UBA aliyodai pia kuwa wanatumia pia teksi bubu jambo ambalo ni kinyume cha sheria.

Hali si Hali,Serikali Yahaha Kutafuta Trilioni 1.7 za Kutekeleza Miradi Yake..!!!

0
0

SERKALI ipo katika mazungumzo na Benki ya Dunia kwa ajili ya kusaidia miradi ya maendeleo inayoandaliwa kwa mwaka ujao wa fedha itakayogharimu dola milioni 785 ambayo ni sawa na Sh trilioni 1.747.

Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Philip Mpango ameyasema hayo jana jijini Dar es Salaam wakati akizungumza na waandishi wa habari baada ya kuzungumza na Makamu wa Rais wa Benki ya Dunia anayeshughulikia Kanda ya Afrika, Makhtar Diop.

Dk Mpango alisema kwa upande wa kuboresha Bandari ya Dar es Salaam, mradi mzima ulikadiriwa utahitaji dola milioni 600, lakini kwa awamu ya kwanza ambayo Benki ya Dunia wamekubaliana watakwenda kuharakisha mchakato na kutoa dola milioni 305 ili kazi ianze mapema.

Alisema ipo miradi mingine ambayo ni ya kisera ambayo ni kwa ajili ya kuboresha mazingira ya kufanya biashara ambayo ina thamani ya dola milioni 80 na kuna miradi mingine ambayo baada ya kumaliza majadiliano itatekelezwa.

Akitolea mfano, alisema kuna mradi wa elimu ambao utagharimu dola milioni 100, mradi wa kusaidia kuimarisha menejimenti ya bajeti na uwazi katika masuala ya bajeti ambao ni dola milioni 80, mradi wa awamu ya pili ya maji ambao ni dola milioni 100.

Dk Mpango alisema miradi hiyo inatekelezwa kwa awamu na mingine ipo kwenye maandalizi ambapo kwa upande wa makutano ya barabara uya Ubungo alisema kuwa bado hawana makubaliano ila haitapungua dola milioni 60.

Pia alisema wamelenga kuboresha sera na kufanya kuwa sehemu nzuri ya kufanyia biashara, na wamekubaliana kuongeza uwezo katika miradi ya ubia kati ya sekta ya umma na sekta binafsi (PPP) na kusaidia kuongeza uwezekano wa kupata wabia.

Amuua Mkewe Kisa Tsh 200 tu...!!!

0
0

 MKAZI wa kijiji cha Mwamgongo mkoani hapa Zubeda Said (33) anadaiwa kupigwa na mumewe hadi kuuawa baada ya kupoteza Sh 200.

Akizungumza na waandishi wa habari mjini hapa jana, dada wa marehemu, Siwema Masoud alidai kuwa awali ndugu yake huyo alimpigia simu kuwa Januari 19 usiku alipigwa na mumewe kwa kupotea Sh 200.

Alisema siku moja kabla alimpa mtoto wa kaka yake mwenye umri wa miaka mitano Sh 200 akanunue maandazi, lakini mtoto huyo aliporwa fedha hiyo na wenzake, akashindwa kurudi nyumbani kwa siku mbili, akarudi siku ya ugomvi wa wawili hao na mumewe kukasirika. 

Alidai kuwa mume huyo, Kunduwenda Kiza (37) akimfokea mtoto huvyo mama mtu kuamua kumwomba radhi mumewe huyo lakini bila mafanikio kwani katika hali ya kushangaza mumewe alimpiga mpaka kupoteza fahamu.

Siwema asilimulia kuwa kesho yake saa 9.45 alfajiri hali ya Zubeda ilibadilika na  kutokwa damu sehemu mbalimbali zilizo wazi mwilini mwake, mumewe akamkimbiza kwenye zahanati ya kijiji hicho na Januari 20, alipewa rufaa kwenda hospitali ya mkoa ya Maweni.

Alisema  Januari 21, saa 12.45 Zubeda alipoteza maisha hali iliyowapa mashaka na kufikisha taarifa Polisi  kwa uchunguzi maiti lakini walipokwenda na askari hospitalini wakaambiwa jalada halionekani.

Hata hivyo, mganga aliyetambuliwa kwa jina la Dk Muganyizi alijitolea na kuufanyia uchunguzi mwili huo na baada ya uchunguzi maiti alibaki mochari.

Lakini wakati ndugu wakijiandaa kwenda kuchukua mwili walishangaa kukuta umeondolewa, na kwa msaada wa polisi waliukamata ukisubiri kusafirishwa kinyemela.


Mwandishi alifika Maweni na kugundua kuwa kabla ya kifo alilazwa wodi 2(b) ya wanawake huku jalada lenye taarifa zake likiwa limetoweka huku uchunguzi wa Mganga ukibaini kuwa na majeraha ndani ya mwili yaliyosababisha kuvuja damu kulikochangia kifo hicho.


Kamanda wa Polisi wa Mkoa, Ferdinand Mtui  alikiri kupokea taarifa za kifo cha kutatanisha cha Zubeda.

Kamanda Mtui alisisitiza kuwa mshukiwa Kiza anashikiliwa na Polisi   kwa upepelezi na ikibainika ametenda kosa hilo, atafikishwa mahakamani.

CUF Waipa CCM Onyo Juu ya Matumizi ya Dola..!!!

0
0

 WAKATI CUF leo ikiadhimisha miaka 16 ya kumbukizi ya mauaji na ukiukwaji wa haki za binadamu, imeihadharisha CCM na Rais John Magufuli kutofanyia mzaha matumizi makubwa ya nguvu za Dola kuendesha shughuli za kidemokrasia na uchaguzi nchini.

Taarifa iliyotumwa jana kwa vyombo vya habari na Naibu Mkurugenzi wa Haki za Binadamu na Sheria wa CUF,  Pavu Abdallah Juma, ilisema wanalaani mauaji ya raia wasio na hatia na vitendo vyote vya ukiukwaji wa haki za binadamu vilivyofanywa na Serikali ya CCM.

“Jeshi la Polisi limeshindwa kutekeleza wajibu wake kwa misingi ya haki, sheria na uadilifu,  badala yake  linatumika kama mkono wa kulazimisha ushindi wa CCM katika uchaguzi na kufanya kazi zake kisiasa zaidi, badala ya kutanguliza uzalendo na weledi,” alisema Juma kwenye taarifa hiyo.

Aidha, iliitaka Serikali kutambua kuwa wananchi wamechoka uonevu na ukiukwaji wa haki za binadamu na wamechoka kunyanyaswa na kushindwa kuheshimiwa kwa mfumo wa siasa za vyama vingi nchini, misingi ya demokrasia na uchaguzi huru na wa haki.

Iliionya Serikali ya CCM na vyombo vya Dola kutoirejesha nchi kwenye matukio ya Januari 26 na 27, 2001 ambayo yalisababisha umwagaji wa damu na mauaji ya raia wasio na hatia. 

Alisema CUF itaendeleza juhudi za kuhakikisha migogoro ya kisiasa inapata ufumbuzi kwa njia ya kidemokrasia na amani, na kuunganisha Wazanzibari na Watanzania kwa  kuwa kitu kimoja na kutanguliza maslahi mapana ya nchi.

Aidha, ilitoa shukrani kwa viongozi, wanachama, wapenzi na wananchi wakazi wa Zanzibar kwa  uvumilivu ambao unadhihirisha ukomavu wa hali ya juu wa kisiasa, licha ya hujuma, mauaji, uchokozi na usumbufu wa makusudi uliofanywa na Jeshi la Polisi na vyombo vya Dola na vikosi vya ulinzi.

Taarifa ilieleza kuwa CUF itaendelea kushirikiana na vyama vingine vya siasa, wadau wanaounga mkono kuheshimiwa kwa demokrasia na misingi ya utawala bora ili kuhakikisha Serikali ya CCM inaheshimu  demokrasia na Watanzania wanapata tume huru za uchaguzi na Katiba inayotokana na ridhaa yao.

Ilibainisha, kwamba madai hayo yanaungwa mkono na jumuiya ya kimataifa ambayo ilishiriki kwenye uangalizi wa uchaguzi mkuu wa Oktoba mwaka juzi,  ambapo katika ripoti ya waangalizi wa Jumuiya ya Ulaya walipendekeza hadi 2020 matatizo yaliyopon yawe yamefanyiwa kazi.

Mwaka 2001 wanachama na wafuasi CUF walijitokeza kwenye maandamano ya kupinga matokeo ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2000 na kudai Katiba mpya na tume huru za uchaguzi.

aada ya Harmorapa, Sasa Aibuka Chiburapa,Anafanana Kila Kitu na Diamond..!!!

0
0

MWEZI Januari mwaka huu katika mitandao ya kijamii aliibuka msanii chipukizi wa Bongo Fleva anayefanana sana kwa sura na msanii kutoka Wasafi Classic Baby (WCB) aitwaye Harmonize kiasi mashabiki  walimbatiza jina la ‘Pacha wa Harmonize’ au Harmorapa.  Mwanzoni mwa wiki hii ameibuka msanii mwingine anayefanana na Diamond Platnumz naye kupewa jina la Chibu Rapa. 

Katika mitandao ya kijamii msanii kutoka WCB ‘Harmonize ‘ alimuanika na baadae kumtoa kijana huyo aliyefanana na Diamond huku mashabiki wakifunguka kwa kuachangia hoja na wengi walikubaliana na Harmonize kuwa ni kweli kijana huyo amefanana kwa muonekano na  na Diamond Platnumz.
Aidha bado haijafahamika kama kijana huyo naye anafanya sanaa ya muziki au laa.

Trump Afanya Ziara ya Kwanza kwa Kutumia Air Force One,Tazama Hapa Pichaazz..!!!

0
0


Rais wa 45 wa Marekani, Donald Trump amefanya safari yake ya kwanza akiwa rais kwa kutumia ndege ya  Rais, Air Force One  na helkopta ya Rais, Marine One Januari 26.
Trump amefanya safari akitoka Ikulu iliyopo Washington DC na kwenda Jimbo la Philadelphia umbali wa takribani maili 150, jana Alhamisi alipokwenda wenye mkutano wa mwaka na baadaye majira ya mchana kurudi tena Washington DC.

Wiki iliyopita Trump alitumia Air Force One wakati akitoka New York kwenda Washington DC kwa ajili ya kuapishwa kuwa rais wa nchi hiyo.

Rayvany: Sijamtundika Mimba Faima Ila…

0
0

Msanii kutoka Wasafi Classic Baby (WCB), Raymond ‘Rayvany’ amekuwa akitajwa kutoka kimapenzi na modo wao anayefahamika kwa jina la Faima na taarifa zikavuja  kuwa ‘mtoto’ huyo mzuri sasa ana ‘kibendi’ chake.

Ikadaiwa na chanzo kilicho karibu na wawili hao kuwa, uhusiano wao umekuwa wa siri sana na wa muda mrefu licha ya wakati mwingine kushindwa kujizuia kuanika hisia zao mtandaoni.

Kufuatia madai hayo, Gazeti la Ijumaa lilimtafuta Rayvany ili kuweka wazi ishu ya kumpa mimba Faima ambapo alifunguka: “Kwanza mimi sina uhusiano na Faima na sijampachika mimba kama wanavyosema ila yeye ni mtu wangu wa karibu sana. Yale ninayofanya kule mtandaoni, nafanya kama mshikaji wangu.”

Hata hivyo, licha ya yeye kukana kuwa na uhusiano naye, Ijumaa lilimtafuta Faima kupitia simu yake kuzungumzia madai ya kuwa mjamzito bila mafanikio lakini aliwahi kukiri kuwa Rayvany ni baby wake na wala hawezi kuficha.

Huddah Akiri Kubanjuka na Wizkid,...!!!

0
0

MODO na mshiriki wa Shindano la Big Brother Africa Season 8, Huddah Monroe ameweka wazi kuwa alishawahi kubanjuka kimapenzi na staa wa muziki kutoka Nigeria, Ayo Balogun ‘Wizkid’.

Huddah aliyasema hayo baada ya kuachia kipande cha video katika mitandao ya kijamii kikimuonesha akiimba moja ya nyimbo za Wizkid na kusema kuwa amekuwa ni mwanamuziki wake wa muda wote;

“Mungu mjalie maisha marefu Wizkid kwa sababu siwezi ishi bila muziki wake. Nimekuwa nikisikiliza kila wimbo wake. Wizkid amenipa kila hali ya kujisikia raha.”

Baada ya kuandika hivyo, wapo walioungana naye na wengine wakamshambulia kuwa anajigonga kwa Wizkid ampende ndipo povu lilipoanza kumtoka;

“Hata mkisema vipi tayari nimeshabanjuka naye. Hata ninachoongea kuhusu muziki ni kweli yupo juu.”

Waziri Nape Aufungua Tena Uwanja wa Taifa kwa Mechi za Ligi Kuu

0
0

Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia kwa Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo, Nape Nnauye wametangaza kuufungua tena uwanja wa taifa baada ya kuufunga mwezi Oktoba mwaka jana kwa shughuli zozote.

Uwanja huo ulifungwa kutokana na uharibifu uliotokea wakati wa vurugu zilizotokea uwanja huo wakati wa mechi ya watani wa jadi Simba na Yanga iliyochezwa Oktoba 1 mwaka jana. Uwanja huo utaanza kutumika katika mechi ya Simba na Azam itakayochezwa Jumamosi hii.

Soma taarifa hiyo zaidi hapa chini.

Rais Adam Barrow Arudi Gambia Kuliongoza Taifa Lake..!!!

0
0

Rais mpya wa Gambia Adama Barrow, amewasili nchini humo kuchukua hatamu za uongozi, kufuatia kuondoka madarakani kwa rais wa mda mrefu Yahya Jammeh

Barrow aliapishwa wiki iliyopita nchini Senegal wakati viongozi wa kieneo walipokuwa wakimshawishi Jammeh kuondoka madarakani.

Maelfu ya watu walifurika katika barabara za mji mkuu wa Gambia Banjul kumlaki rais huyo mpya.

Taarifa zinasema Barrow atakaa katika makaazi yake wakati ukaguzi ukifanywa katika ikulu kutambua hatari yoyote kufuatia kuondoka kwa Yahya Jammeh kwenda uhamishoni Guinea ya Ikweta.

Maelfu kadhaa ya wanajeshi wa mataifa ya Afrika magharibi wanasalia Gambia wakati kukiwa na taarifa kuwa wafuasi waovu wa Jammeh wamo miongoni mwa vikosi vya usalama nchini.

Video: Harmonize Amlilia Wolper Kupitia ‘Ibaki Stori’ ya Rich Mavoko

0
0

Mapenzi ni kidonda ukiwaza utakonda. Harmonize ameonyesha bado anamhitaji Jacquline Wolper kwenye himaya ya moyo wake baada ya kupigwa kibuti.

Baada ya kusambaa kwa taarifa kuwa wawili hao wamemwagana tena huku Wolper akipigilia msumari kuwa jambo hilo ni ukweli mtupu japo Harmo alikuwa akilificha, sasa muimbaji huyo ameanza kuonyesha kuwa jambo hilo ni kweli.

Harmonize ameonekana katika kipande cha video alichokiweka Wolper katika mtandao wake wa Instagram akimuimbia mpenzi wake huyo wa zamani wimbo wa ‘Ibaki Stori’ wa Rich Mavoko kama njia ya kumshawishi mrembo huyo asahau yaliyopita.

Inahuzunisha Sana..Mke Ammwagia Mafuta ya Moto Mume na Mtoto Baada ya Kupewa Talaka (Video)

0
0

Mohamed Maulid mkazi wa Pugu Kinyamwezi ambaye ni mfanyakazi wa Tanesco na mtoto wake Sumaiya Mohamed (3), wamemwagiwa mafuta ya moto na mke wake (Severine) baada ya mke huyo kupewa talaka siku mbili kabla ya tukio hilo.

Maulid alisema baada ya kumpa mwanamke huyo talaka alikuwa anampiga tu tarehe kuwa ‘ntaondoka kesho, ntaondoka kesho.’ “Na nilivyokuwa naenda kazini nilimuuliza utaondoka saa ngapi akasema ataondoka jioni, nikahisi kwamba anaona aibu kuondoka mchana ataondoka jioni,” amesimulia.

“Nilikuwa nimelala nikasikia kama moto umelipuka, nilikuwa nimelala fofoFo, nikashtuka nikaanza kupiga kelele nimemwagiwa maji ya moto nikapiga kelele majirani wengine wakanisikia wakatoka nje, wakaenda kumuangalia na mtoto wakakuta na mtoto naye kaungua sana na yupo kule wodi ya watoto.”

Baadaye majirani wakanisaidia wakamuita dereva taksi nikawaambia nikimbizeni hospitali kwa uzima wangu. Mimi nilipomwagiwa mafuta yale, nilikurupuka nikakuta mlango upo wazi na wakati mlango nilikuwa nimefunga nimefunga na misumari kwasababu nilikuwa simuamini tena kwanini hataki kuondoka, nikakuta mlango ule umefunguliwa na wa nyuma umefunguliwa na mtoto wangu alimwagiwa mafuta kichwani nilimuona.”


Jirani yao aliyejulikana kwa jina la Sofia Ngumbali alisema, “usiku mwanamke huyo alienda jikoni kuchemsha mafuta na akapanga viti akarukia chumba cha mumewe kufika pale mlangoni kwa kuwa funguo alikuwa hajaichomoa akafungua mlango na akachukua mafuta akaja kuwamwagia yeye na mwanae waliokuwa wamelala pamoja.”

“Yule mwanaume alivyokurupuka akapiga kelele majirani tulijua mwizi kukurupuka tukamkuta anagalagala nje anasema kuwa mkewe amemmwagia mafuta, na sisi tulikuwa tunaona wanaishi kwa amani wakitoka wanatoka wote na kurudi wote kwahiyo ya ndani mtu huwezi kujua yaliyopo ndani ya ndoa,” aliongeza jirani huyo.

Kwa upande wake mama wa mtuhumiwa huyo akiwa na mjukuu wake katika hospitali hiyo aligoma kutoa ushirikiano alipokuwa akihojiwa na waandishi.

Auawa kwa Kuiba Kuku..!!!

0
0

Mtu mmoja aliyejulikana kwa jina la Safari Bungate, miaka 51, mkazi wa Usagara, wilayani Misungwi mkoani Mwanza ameuawa na kundi la watu kwa kupigwa mawe na fimbo kwa madai ya kuiba kuku nyumbani kwa mtu. 


Taarifa ya jeshi la Polisi Mkoa wa Mwanza imesema kuwa tukio hilo limetokea tarehe 26.01.2017 majira ya saa 10 usiku katika kijiji cha Kanyelele, wakati mwenye nyumba bwana Tetema Mathias akiwa amelala  na familia yake.

Inadaiwa kuwa marehemu huyo alifika katika nyumba hiyo akaingia ndani kupitia dirishani na kuiba kuku mmoja, ndipo wakati alipokuwa anataka kuondoka mwenye nyumba huyo alimuona na kuanza kupiga yowe ya mwizi akiomba majirani wamsaidie kumkamata huku akimkibiza barabarani.

Inasemekana kuwa majirani waliamka na kufanikiwa kumkamata  marehemu akiwa na kuku amemshikilia kisha wakaanza kumpiga  kwa mawe na fimbo sehemu mbalimbali za mwili wake  kitendo kilichopelekea marehemu  kupoteza fahamu na baada ya muda mchache  alifariki dunia.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza Ahmed Msangi amesema kuwa raia wema walitoa taarifa polisi ndipo askari walifika eneo la tukio na kukuta mtuhumiwa wa wizi akiwa tayari amefariki dunia.

Amesema mwili wa marehemu tayari umefanyiwa uchunguzi na daktari na kukabidhiwa kwa ndugu wa marehemu kwa ajili ya mazishi na kwamba mwenye nyumba Bwana Tetema Mathias anashikiliwa na jeshi la polisi kwa mahojiano zaidi

Pesa Kupotea Mitaani… Machangudoa Watoa Kilio Chao kwa JPM

0
0


Dar es salaam:  Kufuatia hali ngumu ya kimaisha kutokana na pesa kutopatikana kirahisi kama ilivyokuwa awali, akinadada wanaofanya biashara haramu ya kuuza miili yao ‘machangudoa’ katika Jiji la Dar wametoa kilio chao kwa Rais John Magufuli ‘kulegeza’ kidogo kwani wanakufa njaa.

Machangu hao waliamua kufunguka hivyo hivi karibuni baada ya kuhojiwa na mapaparazi wa OFM waliokuwa wakifanya uchunguzi kuhusiana na biashara hiyo katika kipindi hiki ambacho kila mtu analia akisema ‘pesa imekauka mifukoni’.



Hali ikoje?

Katika utafiti huo uliofanyika katika maeneo ya Sinza Afrikasana, Kinondoni Makaburini na Buguruni jijini Dar, biashara hiyo imeonekana kudoda huku wengi wakieleza kuwa, hali hiyo imetokana na ugumu wa maisha.

Akizungumza na paparazi wetu, dada mmoja aliyejitambulisha kwa jina la Pili, Mkazi wa Buguruni jijini Dar anayefanya biashara hiyo maeneo ya Sinza Mapambano alisema:

“Kiukweli hali ni mbaya sana, unajua wateja wetu wengi walikuwa wale ambao walikuwa wakipata pesa za kimagumushi, sasa baada ya Magufuli kubana, watu wamekuwa makini sana na pesa zao.

“Matokeo yake sasa, wateja wamekauka, unaweza kuja kijiweni, ukapigwa na baridi wee bila kupata mwanaume, ukarudi nyumbani mikono mitupu, kwa kweli hali ni mbaya.”

Naye Betty anayejiuza maeneo ya Sinza Mori jijini Dar alisema; “Kwa kweli itafika wakati inabidi tukalime, nimefanya biashara hii kwa muda mrefu lakini sijawahi kukumbana na ukata kama huu.

“Kuna miezi ambayo tunajua watu hawana pesa lakini kuna ile ambayo tunajua biashara itakuwa poa ila sasa hivi wateja hakuna mwanzo mwisho, yaani Magufuli ni noma, angelegeza kidogo.”

Hata hivyo asilimia kubwa ya machangu waliozungumza na OFM na kuulizwa kwa nini wang’ang’anie biashara hiyo hatarishi walisema, eti ndiyo ambayo imekuwa ikiwasaidia katika kuendesha maisha yao kwa muda mrefu.

“Wewe unadhani mimi nitakwenda kufanya nini, sijasoma wala sina ujuzi wowote, nimefanya biashara hii kwa muda mrefu, nimeichukulia kama ajira kwangu, sasa hali ikiwa mbaya hivi nikalie wapi? Watoto nitawasomesha na nini? Pango nitalipa na nini?” alisema dada mmoja aliyegoma kutaja jina lake.

Biashara kwa promosheni sasa

Katika maeneo ambayo OFM walitembelea, wasichana hao wakiwa wamevalia nguo za kihasara walionekana kugombea kila mteja aliyekatiza mbele yao na wakati mwingine kufikia hatua ya kupigana.

Aidha, tofauti na kipindi cha nyuma ambacho ukikutana na dadapoa anakupa bei ya kwenda kulala naye na ya ‘short time’, sasa hivi ni kwa promosheni na unaulizwa una shilingi ngapi, kiasi utakachotaja ni ngumu kukataliwa.

Wamepagawa

Kufuatia ukata huo, wadada wengi wanaofanya biashara hiyo wanaonekana kudata, ambapo wengi wamekuwa wakivuta bangi na kulewa sana kiasi kwamba ukikutana naye uso kwa uso, utaona dhahiri ni mtu aliyekata tamaa.

Wizi umeongezeka

Uchunguzi wetu umebaini kuwa, kutokana na wateja kupungua baadhi ya dadapoa hao wameanzisha tabia ya kuwaibia watu simu na pesa hasa katika maeneo ya Kinondoni na Buguruni.

Freeman Mbowe Atembelea Shamba Lake Lililopigwa Marufuku na Serikali ..!!!!

0
0

Mwenyekiti wa Chadema ambaye pia ni Mbunge wa  Hai, Freeman Mbowe ametembelea shamba lake la kilimo cha kisasa cha mboga mboga (Green House) yaliyopo Hain na kuwajulia hali wafanyakazi pamoja na wataalam wake leo Ijumaa.

Pia, Mbowe amepata wasaa ya kuzungumza na baadhi ya wafanyakazi ambao walimweleza hofu kubwa waliyoingiwa  nayo ya kupoteza ajira zao wanazozitegemea katika kuendesha maisha yao ya kila siku.

Hali hiyo imekuja baada ya Mkuu wa Wilaya ya Hai, Gellasiu Byakanwa kupiga marufuku shughuli za kilimo zinazoendeshwa na shamba la Kilimanjaro Veggies linalomilikiwa na Mbowe.

Byakanwa alitoa amri hiyo baada ya kutembea shamba hilo lenye ukubwa wa hekari mbili akisema kilimo hicho ni kinyume cha sheria kwani shamba hilo lipo ndani ya mita 60 kutoka mto Weruweru.

Hivi ni Kwanini Wanawake Wengi Hujivunia Sana Makalio Yao?

0
0
Angalia hata picha wanazopiga wanawake utaona jinsi wanavyojibinua ili wanaonekane wana makalio makubwa.

Hata wakati wa kutembea pia wengine hutembea tofauti ili kuhakikisha kuwa makalio yake yanatikisika na ndio maana hata wengine hudiriki hata kutumia dawa za mchina ili kukuza makalio yao na hata baadhi yao wakati mwingine hujigamba kuwa eti wanamshukuru Mungu kwa kuwapa hips kubwa na wakati mwingine husikika wakisema eti mwanamke inye. 

Hivi nyie wanawake hususani wasichana ni kwanini mnapenda sana kujivunia na kuringia makalio yenu? Ina maana katika miili yenu kitu mnachokiona ni cha thamani ni makalio pekee? Badilikeni bwana maana kujivunia makalio badala ya akili ni ujinga wa kiwango cha lami
Viewing all 104431 articles
Browse latest View live




Latest Images