Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104789 articles
Browse latest View live

DIVA ATUPIA PICHA YA KIFUA CHAKE INSTAGRAM

$
0
0
Hakika Mtandao wa Insta unazidi kushika kasi kwa Umaarufu kwa wadada kujianika Maungo yao ya mwili. sasa Imekuwa ndio fasheni kwa akina dada kutupia picha za mitego katika acount zao hizo. Leo hii Diva Lovenes Love Mtangazaji wa Clouds Fm naye ameingia kwenye list ya watu hao kwa Kutupia Mtupio Huu..
DIVA.....

MWANAMUZIKI LINA ADHIHIRISHA MAPAJA NA MIGUU YAKE NI MOTO WA KUOTEA MBALI

$
0
0

Week Kadhaa zilizopita Mwanadada Linah Alikaririwa akisema kwamba anapenda Paja na Miguu yake kwani ni mizuri sana...Kuna walio mbeza na kuponda...Sasa katoa picha mpya zikionesha vizuri miguu yake ....Amazing Legs Eeehh?

DIAMOND ATOBOA SIRI KUWA ANA MTOTO ALIPOKUWA ANAHOJIWA NA MTANDAO WA NIGERIA

$
0
0
Nani aliyekuwa anafahamu kuwa Diamond Platnumz ni baba? Well, hatujawahi kumsikia popote akisema kuwa ana mtoto lakini staa huyo wa ‘My Number One’ alikuwa mkarimu wa kutosha kuweza kuelezea ‘furaha ya kuwa mzazi’ kwenye mahojiano aliyofanya na mtandao maarufu wa Nigeria uitwao Lobatan Africa baada ya kwenda huko wiki kadhaa zilizopita alikoshirikishwa pia na mastaa wa huko wakiwemo Waje na Dr Sid.

Kwenye mahojiano hayo, mtandao huo ulimuuliza: What have you learnt about fatherhood, now that you’re a father (umejifunza nini kuhusu ubaba kwakuwa sasa wewe ni baba)

Diamond alijibu: Fatherhood is a great experience, very humbling. You learn a lot about your children and the kids and the kinds of things they love. For example, my baby loves this cartoon that has a catchy song, I think Ben10. Hahaha!! (Kuwa baba ni kitu kikubwa, kinavutia sana. Unajifunza mengi kuhusu watoto wako na vitu wanavyopenda. Kwa mfano ‘mwanangu’ anapenda katuni hii yenye wimbo unaogusa, nadhani Ben 10!

Kumbe Diamond ana mtoto tena mkubwa anayeweza kuangalia na kuelewa katuni? Swali ni kwanini hajawahi kusikika akisema ana mtoto? Hata hivyo September mwaka jana, moja ya magazeti ya udaku ya kampuni ya Global Publisher, yaliandika habari ya kuibuka kwa msichana aitwaye Sasha Juma aliyedai kuwa amezaa na Diamond.

Sasha akiwa na mtoto anayedai ni wa Diamond
Msichana huyo alidai kuwa likutana na Diamond Mlimani City jijini Dar es Salaam na akampenda kwakuwa anafanana na Wema Sepetu (kipindi hicho walikuwa wameachana. Gazeti hili lilisema wawili hao hawakuchukua muda na wakaanza uhusiano uliowafanya wakutane kimwili na kupelekea msichana huyo kushika ujauzito.

Lilidai asha alimpa taarifa staa huyo ambaye alimuomba asitoe mimba kwakuwa atamsomesha msichana huyo aliyefukuzwa shuleni na pia kuahidi kumlea mtoto huyo.

“Ni kweli nimezaa na Diamond. Mtoto ana miezi mitatu sasa. Unajua yeye ndiye alinikatisha masomo na kusema kuwa ataniendeleza na atamlea mtoto hivyo alivyokaa kimya sikuona tena sababu ya kumfuatilia kwa vile kwetu napata kila kitu,” gazeti hilo lilimnukuu Sasha.

Lilisema lilipomtafuta Diamond kwa simu ambaye kwa sasa yupo nchini Kenya, alijibu: Hahahaaa…mbona hiyo ishu ni kubwa sana kwangu! Ukweli huyo mwanamke simjui kabisa. Lete stori nyingine achana na hiyo.”

So kama Diamond ana mtoto, huenda aliamua kumkubali mtoto huyu na pengine ndiye mtoto huyu anayependa kuangalia katuni ya Ben 10!
Credits:Bongo5

TAARIFA KUHUSU AFANDE SELE KUACHANA NA MKE WAKE MAMA TUNDA

$
0
0
Taarifa ambazo alizi-amplify Soudy Brown April 15 ni kuhusu kutengana kwa Afande Sele na Mzazi Mwenzake aliyeishi nae kwa zaidi ya miaka 10 Mama Tunda,Afande Sele bahati mbaya alikosea ujumbe mfupi wa maandishi na kuituma kwa mhusika sikiliza hapa alichokiongea Afande Sele.
Sikiliza 88.0 Clouds Fm ukiwa Tabora.
Bonyeza play kusikiliza.

MAMA TUNDA"NILISHAMFUMANIA AFANDE SELE SANA NA HANA HESHIMA"

$
0
0
Kupitia You heard ya April 15 alisikika Afande Sele ambaye alikosea ujumbe mfupi wa maandishi kwa mhusika ambaye alikua Mama Tunda leo kapatikana na kazungumza pia kilichopo kati yao kama wazazi wa watoto wawili Tunda na Asante Sanaa.
96.0 inasikika Clouds Fm ukiwa Tanga.
Bonyeza play kusikiliza.

JANGA JINGINE..HII NDIO MELI ILIYOZAMA NA WATU 300 HAWAJULIKANI WALIPO

$
0
0
Zaidi ya watu 300 bado hawajapatikana baada ya meli kubwa iliyobeba watu 459 kuzama huko South Korea ambapo sehemu kubwa ya watu waliokuwemo kwenye meli hiyo ni wanafunzi na walikuwa wanasafiri kutoka kwenye bandari ya Incheon kwenda kwenye kisiwa cha Jeju.
Watu watatu wamesharipotiwa kufariki licha ya watu zaidi ya 300 kutoonekana na 13 wametolewa kama majeruhi huku uokoaji zikiendelea ambapo hadi habari hii inawekwa shughuli za uokoaji zinaendelea na watu wengi wanaokolewa kupitia madirisha huku chanzo cha ajali kikiwa hakijajulikana.


MWIGULU ASHAURI RAISI ATEGUE UTEUZI WA WAJUMBE WALIO SUSIA KIKAO CHA BUNGE

$
0
0
Ukawa walipanga njama tangu mda mrefu kukwamisha mchakato wa katiba ili wapate agenda za uchaguzi mwaka 2015. Fedha hizi tunazotumia zingewasaidia maskini kupata elimu, dawa na huduma zingine. Mwigulu anaomba muongozo kwa mwenyekiti, ili rais atengue uteuzi wa wajumbe aliowateua wa bunge la katiba ibaki wale wa kuchaguliwa ambao maamuzi yapo chini ya wananchi.

PICHA:AGNESS MASOGANGE AKIWA NA PACHA WAKE...SERIOUSLY ?

$
0
0
Agness Masogange Kapost Picha hiyo hapo juu.....Akisema yupo na Pacha Wake ....Ndio leo nasikia kuwa ana pacha ..na Nikiangalia kweli wanafanana Kinoma......Je ni kweli ana Pacha ama ni kufanana tu ?

MAMA AMTEMBEZA MUMEWE KAMA MBWA BAADA YA KUMFUMANIA NA MWANAMKE MWINGINE

$
0
0
Mapenzi muda mwingine yanakuwa na vituko vyake na vinapotokea huwashangaza na kuwaacha watu midomo wazi. Mama huyu alimfumania mmewe na mwanamke mwingine na mumewe alianza kuomba msamaha na ndipo mama huyu aliamua kumsamehe ila kwa kumpa adhabu mumewe na adhabu yenyewe ndiyo kama hiyo unayoiona ya kumtembeza mumewe kama mbwa kwa muda wa siku 3

Kama wewe unaweza kukubali kufanyiwa hivyo na wewe mwanamke unaweza kumfanyia hivyo mpenzi wako/mumeo?? toa maoni yako hapo chini

EDWIN MTEI ASIKITISHWA NA KITENDO CHA TUNDU LISSU KUMTUKANA BABA WA TAIFA

$
0
0
Nilimsikiliza Mheshimiwa Tundu Lissu na nasikitika kwamba sikubaliani naye jinsi alivyoeleza shutma juu na dhidi ya Mwalimu Julius Nyerere, Baba na Muasisi wa Taifa letu. 

Inajulikana na umma wa Watanzania, kwamba mimi binafsi, kama Waziri wa Fedha, nilitofautiana na Mwalimu, nikajiuzulu Uwaziri Decemba,1979, nikimwomba ateuwe Mtanzania mwingine atakayeshauri mambo ya Uchumi na Fedha. Lakini tuliendelea kuwasiliana kwa maelewano bila chuki, na hata aliniteuwa niwe Mwakilishi wa Tanzania na Afrika inayoongea Kiingereza katika IMF (Shirika la Fedha Duniani) chini ya miaka mitatu baadaye Novemba, 1972. 

Nimekuwa na mawasiliano na maelewano mazuri sana na Mwalimu hata baada ya kuasisi CHADEMA, Julai 1992 na tulipokamilisha Katiba na Sera za Chadema, nilimtembelea Nyumbani kwake Butiama nikampa azisome ajionee jinsi tulivyonuia kuwahudumia Wananchi wetu. Hata siku moja siwezi kumtusi Muasisi wa Taifa letu. Iwe ni mwiko pia kwa Chama cha Demokrasia na Maendeleo kumtusi Baba wa Taifa.

Ningewashauri uongozi wa Chadema na hasa Vijana wa M4C (Vuguvugu la Mabadiliko) tuendelee na uhamasishaji : kwa umakini, tukiwa na huruma kwa wanyonge maskini wa kutupwa, tukijiandaa kwa umakini na kiutaalamu Sera na Mikakati ya kuwakomboa toka katika umaskini wa kutupwa kwa kutumia nguvu ya umma (Peoples Power) tukitumia mikakati sahihi: kwani Hakuna Kulala Mpaka Kieleweke: 

Mikakati na Sera sahihi ikiwa ni kutumia misingi ya Uchumi na Miundombinu tulionayo licha ya uhalisia dhoofu tulioridhi; tukiwaenzi walioijenga na kuturidhisha kwa unyofu wao. 

Roho ya Julius Nyerere ilale mahala pema Peponi. Amen!

With all due respect to Hon. Tindu Lissu, this smacks BAD TASTE.


Edwin Mtei,

Founder Chairman of CHADEMA

JE INAWEZEKANA KUPATA MKE AMA MUME MZURI KUPITIA FACEBOOK?

$
0
0
Katika safari ya mapenzi wanandoa huwa wanakutana katika maeneo mbalimbali, wapo wanaokutana vyuoni,shuleni, kwenye nyumba za ibada, sokoni, kwenye daladala, kuunganishwa na mtu mwingine, au baada ya kusikia sauti kwenye simu, redioni, hotelini na sasa wengine kupitia mitandao ya kijamii kama facebook

Ukweli ni kwamba katika mitandao unapoanzisha uhusiano na mtu usiyemfahamu inawezekana ameona picha yako tu nakukuambia kuwa anakupenda na wewe ukiona picha yake ukaridhika naye mkaamua kuanzisha uhusino ni vyema kuonana kabisa ili kuwa na uhakika na uhusiano mnaotaka kuanzisha  kwani unahitaji kumfahamu zaidi  na ndipo utakapoweza kufanya maamuzi ya kukubali au kukataa.

Anaweza kuwa rafiki yako wa kawaida lakini uhusiano ukaja baada ya kuonana mkafahamiana zaidi, kwani ukikurupuka na kutaka kuoana haraka haraka na yule ambaye mna chat tu kwenye mitandao unaweza kujikuta unajuta baadaye kwa maamuzi yako ni vyema kufahamiana zaidi ya kuchat ili kuwa na uhakika na maamuzi yako....Je Wewe Unaonaje Kuhusu hilo?

DIAMOND AINGIA KWENYE NOMINATION CATEGORY MBILI MTV AFRICA MUSIC AWARDS

$
0
0
Nomination za MTV Africa music awards kwa mwaka 2014 zimetoka huku Mafikizolo,Uhuru na Davido wakiongoza kwa kupata nomination 4.
Watanzania wapo kwenye vipengele vitatu na moja ya vipengele hivyo vinasubiliwa kwa hamu kumjua mshindi kwasababu ni moja ya vipengele vikubwa kwenye awards hizo.
Best Male
Anselmo Ralph (Angola)
Davido (Nigeria)
“Diamond (Tanzania)“
Donald (South Africa)
Wizkid (Nigeria)
Best Female
Arielle T (Gabon)
Chidinma (Nigeria)
DJ C’ndo (South Africa)
Efya (Ghana)
Tiwa Savage (Nigeria)
Best Group
Big Nuz (South Africa)
Mafikizolo (South Africa)
Mi Casa (South Africa)
P Square (Nigeria)
Sauti Sol (Kenya)
Best New Act
Burna Boy (Nigeria)
Heavy K (South Africa)
Phyno (Nigeria)
Stanley Enow (Cameroon)
Uhuru (South Africa)
Best Live Act
2face (Nigeria)
Fally Ipupa (DRC)
Flavour (Nigeria)
Dr Malinga (South Africa)
Zakes Bantwini (South Africa)
Best Collaboration
Amani ft Radio and Weasel – ‘Kiboko Changu’ (Kenya/Uganda)
“Diamond feat Davido – ‘Number One’ (Remix) (Tanzania/Nigeria)“
Mafikizolo feat May D – ‘Happiness’ (South Africa/Nigeria)
R2bees feat Wizkid – ‘Slow Down’ (Ghana/Nigeria)
Uhuru feat DJ Buckz, Oskido, Professor, Yuri Da Cunha – ‘Y-tjukutja’ (South Africa/Angola)
Artist of the Year
Davido (Nigeria)
Mafikizolo (South Africa)
Mi Casa (South Africa)
P Square (Nigeria)
Uhuru (South Africa)
Song of the Year
Davido- ‘Skelewu’ (Nigeria)
DJ Clock feat Beatenberg – ‘Pluto’ (Remember Me) (South Africa)
DJ Ganyani feat FB – ‘Xigubu’ (South Africa)
DJ Kent feat The Arrows –‘Spin My World Around’ (South Africa)
Dr Sid feat Don Jazzy – ‘Surulere’ (Nigeria)
KCee – ‘Limpopo’ (Nigeria)
Mafikizolo feat Uhuru ‘Khona’ (South Africa)
Mi Casa- ‘Jika’ (South Africa)
P Square – ‘Personally’ (Nigeria)
Yuri Da Cunha -‘Atchu Tchu Tcha’ (Angola)
Best Hip Hop
AKA (South Africa)
Ice Prince (Nigeria)
Khuli Chana (South Africa)
Olamide (Nigeria)
Sarkodie (Ghana)
Best Pop
Danny K (South Africa)
Fuse ODG (Ghana)
Goldfish (South Africa)
LCNVL (South Africa)
Mathew Mole (South Africa)
Best Alternative
Gangs of Ballet (South Africa)
Michael Loman (South Africa)
Nakhane Toure (South Africa)
Parlotones (South Africa)
Shortstraw (South Africa)
Best Francophone
Arielle T (Gabon)
Espoir 2000 (Ivory Coast)
Ferre Gola (DRC)
Toofan (Togo)
Youssoupha (Congo)
Best Lusophone
Anselmo Ralph (Angola)
JD (Angola)
Lizha James (Mozambique)
Nelson Freitas (Cape Verde)
Yuri Da Cunha (Angola)
NON MUSIC CATEGORIES
Personality of the Year
Chimamanda Adiche (Nigeria)
Omotola Jalade Ekeinde (Nigeria)
Trevor Noah (South Africa)
Lupita Nyong’o (Kenya)
Yaya Toure (Cote d’Ivoire)
Transform Today by Absolut
Anisa Mpungwe (Tanzania)
Clarence Peters (Nigeria)
I See a Different You (South Africa)
Leti Arts (Ghana)
Rasty (South Africa)
Unaweza kuanza kupiga kura kupitia  www.mtvbase.com mwisho wa kupiga kura ni 4 June 2014.

UKAWA WASUSIA BUNGE, WATOKA NJE CHANZO NI HIKI HAPA

$
0
0
Dodoma. Mambo yamebadilika. Ukimya ulitawala jana katika Ukumbi wa Bunge mjini Dodoma, baada ya wabunge zaidi ya 200 ambao ni wanachama wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), kususia vikao vya Bunge hilo.

Ilikuwa ni saa 10:31 jioni baada ya Mjumbe wa Bunge hilo ambaye pia ni Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba alipohitimisha uchangiaji wake akisema: “Ukawa hatuwezi kuendelea kushiriki dhuluma dhidi ya wananchi kwa kupitisha Katiba ambayo ni kinyume cha matakwa yao.”

Baada ya kauli hiyo aliondoka akifuatiwa na Mwenyekiti wa Ukawa ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe, Mwenyekiti wa NCCR Mageuzi, James Mbatia na wajumbe wao kutoka nje ya Bunge.

Ukimya ulitawala takriban dakika mbili hivi na baada ya wajumbe hao kutoka, Makamu Mwenyekiti wa Bunge Maalumu, Samia Suluhu Hassan aliwaelekeza makatibu kuhesabu wajumbe ili kuona kama akidi imetimia ili waendelee na kikao.

Baadaye aliliambia Bunge kuwa makatibu wamemweleza hawahitaji akidi kwa kuwa kikao kilikuwa kinaendelea wakati Ukawa walipotoka nje ya ukumbi.

Hotuba ya Lipumba

Profesa Lipumba alianza kwa kunukuu Gazeti la Mwananchi la Aprili 14, mwaka huu katika sehemu inayosema; “Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, (Sera, Uratibu na Bunge) ameanza kampeni kanisani kwa kuwataka wananchi kupinga serikali tatu zilizopendekezwa na Tume ya Mabadiliko ya Katiba, vinginevyo nchi itatawaliwa na jeshi kwa kuwa serikali ya muungano itashindwa kuwalipa mishahara wanajeshi.”

Alisema yeye ni muumini wa dini ya Mwenyezi Mungu lakini anaafiki mapendekezo yaliyoletwa bungeni hapo na Tume ya Mabadiliko ya Katiba iliyoundwa na Rais.

“Hii ni kauli ya Waziri Lukuvi ndani ya Kanisa la Methodist wakati wa sherehe ya kumsimika Mchungaji Joseph Bundala kuwa Askofu na Waziri Lukuvi alikuwa anamwakilisha Waziri Mkuu.”

Alisema inasikitisha kwa sababu kauli hiyo inafanana na ya Rais Jakaya Kikwete aliyoitoa wakati akihutubia Bunge Maalumu.

Alisema kauli za Lukuvi zinatisha baada ya kusema Wazanzibari ambao wanataka kuwa na nchi yao hawawezi kujitegemea, bali wanataka wapate nafasi ya kujitangazia kuwa ni nchi ya Kiislamu.

“Waziri anaweza kusema hivyo ndani ya kanisa? Kawahamasisha mpaka yule kiongozi wa kanisa akasema ili kudumisha Muungano bora Katiba ya Zanzibar ifutwe ili iwepo moja ya nchi moja ambayo inadumisha Muungano,” alisema.

Alisema Lukuvi alikuwa akiwaaminisha kuwa mfumo wa serikali tatu ukipita kutakuwa na mapinduzi na nchi haitatawalika na hivyo watu watashindwa kwenda kusali makanisani.

“Kama ndugu zetu wa Zanzibar wangekuwa wanahitaji serikali moja tungekuwa na utaratibu mzuri tu, lakini siyo wanachama wa CUF, siyo wa CCM, Wazanzibari wote hawataki muungano wa serikali moja,” alisema.

Alisema Tume ya Mabadiliko ya Katiba imetoa mapendekezo ya serikali tatu kutokana na ukweli huo. “Hoja zilizoletwa hapa ni hoja za serikali moja, si hoja za serikali mbili lakini wenzetu moja hawataki, kwa hiyo tunahitaji Muungano ambao tutakuwa na maridhiano ya pande zote mbili,”

“Wengi wamenukuu makala niliyoitoa katika kituo cha TCD (Kituo cha Demokrasia Tanzania), ambayo iliunda Baraza la Katiba na mimi nilichambua mapendekezo ya Tume nikasema kwa mapendekezo yaliyomo ndani ya Rasimu ya Katiba hayatakidhi mapato ya shirikisho.”

Alisema wajumbe wanaomnukuu wanaishia hapo bila kwenda katika mapendekezo aliyoyatoa.

“Wamenisifu sana ni mchumi mahiri, basi waendeleze sifa hizo kwa mapendekezo niliyoyatoa ya mapato ya kukidhi uendeshaji wa serikali ya shirikisho.

“Nimeeleza katika hali halisi kuwa utaratibu mzuri ni mapato ya kila serikali kuchangia katika shirikisho na mambo haya yaandikwe katika Katiba. Katiba inaweza ikasema wazi asilimia 20 ya mapato yote yanayokusanywa Zanzibar au Tanganyika yataenda kwenye shirikisho.”

Alitaka pia kuwekwa kwa misingi mizuri ya kukusanya kodi na kutumia fedha za wananchi ndani ya katiba ya muungano ambayo ndiyo katiba mama.

“Lakini ndugu zangu mjadala wetu unavyokwenda utadhani kuwa Rasimu ya Katiba iliyoletwa imeletwa na CUF au na Chadema au na NCCR-Mageuzi, au Wapemba,” alisema.

Alisema ukurasa wa kwanza wa Rasimu ya Katiba unaeleza kuwa toleo hili la Rasimu ya Katiba lilichapishwa katika Gazeti la Serikali kwa mujibu wa Kifungu cha 20(2) ya Sheria ya Mabadiliko ya Katiba Sura ya 83.

Alisema hiyo ni rasimu ya Tume ya Rais na si rasimu ya Wapemba.

Hata hivyo, alisema mjadala unaoendelea bungeni umekuwa na utaratibu wa ubaguzi... “Watu wamebaguliwa humu na viongozi wakubwa wanapiga makofi, Bunge hili limekuwa kama Bunge la Intarahamwe. Hii ni hatari kwa nchi yetu. Wapemba, Waarabu, Wahindi, Wakongo,” alisema.

“Hii hatuhitaji, tunahitaji katiba ambayo itahakikisha kila mwananchi anapata haki yake wote tuwe sawa bila kujali rangi zetu, jinsia zetu, makabila yetu, huu ndiyo msingi aliotuachia Mwalimu Nyerere tuenzi msingi huo.”

Alilalamikia kile alichokiita kuwa ni ubaguzi ndani ya Bunge na kwamba kama Serikali haikutaka Katiba Mpya kwa nini imepeleka wabunge Dodoma? Pia alihoji ni kwa nini ilitumia Sh70 bilioni katika Tume ya Mabadiliko ya Katiba.

“Kwa nini mmetufikisha hapa? Jengo hili nimeambiwa limekarabatiwa kwa Sh8.2 bilioni hali hamuamini Rasimu ya Katiba ama ilikuwa ni utaratibu wa kupata hizo asilimia 10, ndiyo maana mmekarabati kwa gharama kubwa?” alisema.

“Tunataka CAG (Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali), akague matumizi ya fedha zilizotumika. Utatumiaje fedha nyingi wakati hiyo katiba iliyowasilishwa kumbe huitaki kabisa.

“Hakuna utaratibu wowote wa kupiga kura na kufanya maamuzi kuhusu sura hizi mbili. Tumechoka kusikiliza matusi. Tumechoka kudharau mawazo ya wananchi, tumechoka ubaguzi, hatuwezi kuwa sehemu ya kundi linalohamasisha ubaguzi ndani ya Tanzania hili hatukubali,” alisema.

BAADA YA KUSUSIA BUNGE WAJUMBE WAIMBA NYIMBO HIZI" UKOMBOZI NI SASA, VIJANA MSILALE BADO MAPAMBANO"

$
0
0
Nje ya Ukumbi wa Bunge, wajumbe hao kutoka Ukawa na baadhi ya wajumbe kutoka kundi la wajumbe 201 walioteuliwa na Rais, walitoka wakiimba “CCM Interahamwe”.

Pia walitumia falsafa maarufu ya Mchungaji Mtikila ya “Saa ya ukombozi ni sasa,” kuchagiza safari yao ya kutoka Ukumbi wa Bunge Maalumu la Katiba hadi Ukumbi wa Pius Msekwa uliopo eneo hilohilo la Bunge.

Wakiwa ndani ya ukumbi huo, wajumbe hao waliendelea kuimba nyimbo mbalimbali ikiwamo wimbo wa mshikamano (Solidarity forever) unaoimbwa na wafanyakazi kuonyesha mshikamano.

Pia waliimba: “Vijana msilale bado mapambano... Ukawa msilale bado mapambano.” Halikadhalika, wajumbe hao waliimba nyimbo mbalimbali za kumshutumu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, (Sera, Uratibu na Bunge), William Lukuvi na baadhi ya nyimbo hizo zilisikika “Lukuvi mbaguzi” na “Lukuvi mchochezi.”

Interahamwe ni kikundi cha wanamgambo wa Kihutu wa Rwanda ambacho kilichochea mbegu za ukabila na kusababisha mauaji ya halaiki ya Rwanda dhidi ya Watutsi.

Wajumbe hao walitoka nje ya ukumbi huo wa Bunge la Katiba wakiongozwa na viongozi mbalimbali wa kitaifa wa vyama vya siasa akiwamo Profesa Ibrahim Lipumba wa CUF na Freeman Mbowe wa Chadema.

Viongozi wengine wa kitaifa ni Emmanuel Makaidi wa NLD, James Mbatia wa NCCR-Mageuzi na Mchungaji Christopher Mtikila wa DP na viongozi wa vyama vingine ambao majina yao hayakupatikana.

Ndani ya Ukumbi wa Msekwa, Profesa Lipumba aliwashukuru wajumbe wote waliowaunga mkono wakiwamo baadhi kutoka kundi la 201 na kueleza kuwa kauli ya Lukuvi ndiyo kiini cha mgogoro huo mpya wa kisiasa. Alivitaja vyama vingine vya upinzani vilivyowaunga mkono kuwa ni NRA, Chauma na UDP.

“Imebidi tutoke… kwa namna tulivyokuwa tunakwenda ilikuwa hamna tija yoyote na hatuwezi na sisi kuungana nao (CCM na makundi yaliyobaki) kufanya maasi dhidi ya Watanzania,” alisema.

Profesa alipendekeza wajumbe wote wakutane leo saa 4:00 asubuhi kwenye Ukumbi wa Hoteli ya African Dreams ili kujadili na kuweka msimamo wa mwelekeo wa baadaye wa umoja huo.

Profesa Lipumba alisema baada ya kikao cha leo, watakwenda mapumziko ya Pasaka na hawatahudhuria tena mkutano huo wa Bunge la Katiba hadi mwafaka wa kisiasa utakapopatikana.

ZITTO KABWE "KITAKACHOVUNJA MUUNGANO SIO SEREKALI TATU"

$
0
0
Dodoma. Mjumbe wa Bunge la Katiba, Zitto Kabwe amesema kuandikwa kwa Katiba isiyokubaliwa na pande zote kutasababisha gharama kubwa kuliko zile zinazotajwa za serikali tatu.

Akichangia hoja kwenye Bunge hilo jana, Zitto alisema kuna kila sababu ya kukaa na kukubaliana ili kupata Katiba itakayokubalika pande zote.

“Muundo wa Muungano una hatari ya kuvunjika iwapo hakuna matakwa ya dhati ya watu kuungana... Maneno ya kusema Serikali tatu zitavunja Muungano ni ya siasa na hayana msingi wa kisayansi. Urusi ilivunjika sababu haikuwa na demokrasia na siyo sababu ya idadi ya Serikali,” alisema.

Zitto ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC), alisema hofu ya gharama inayotajwa katika uendeshaji wa muundo wa serikali tatu haina msingi wowote kwa kuwa hakuna ushahidi wa kitaalamu unaothibitisha gharama hizo.

“Nimesikia watu wanasema eti tutalazimika kujenga ikulu mpya, nani kasema lazima tuwe na marais watatu? Tunaweza kuwa na rais mmoja kwenye nchi na wakuu wa nchi washirika wawili… Ni jambo la makubaliano tu,” alisema.

Alisema bajeti ya mwaka huu ni Sh18 trilioni, kati ya hizo Sh5.3 trilioni ndizo zinazohudumia wizara za Muungano, lakini serikali ina uwezo wa kukusanya kodi zaidi ya Sh10 trilioni pamoja na mapato mengine.

“Kuna jumla ya Sh2.3 trilioni hatuzikusanyi kila mwaka kutoka kwenye kampuni kubwa, kwa uwezo wetu wa pato la ndani asilimia 17 tunao uwezo wa kuendesha serikali ya muundo wa idadi yoyote.

“Hofu ya Serikali ya Muungano kutokuwa na fedha ni sababu halisi, ni kweli kwamba ushuru wa bidhaa pekee yake hauwezi kutuendeshea serikali. Sasa nini kazi yetu, tunaingia hapa ili kuboresha hayo maeneo, kama hatuwezi tumekuja kufanya nini hapa?” alihoji.



SHILOLE: NILIPONASA SASA SIPINDUI-MAHABA NINYONGE

$
0
0
Na Denis Mtima
STAA wa filamu na mduara Bongo, Zuwena Mohamed ‘Shishi Baby’ amefunguka kuwa amenasa vilivyo katika penzi la msanii mwenzake, Nuhu Mziwanda hatarajii kuachika.

Akipiga stori na paparazi wetu, Shishi alisema yupo tayari kuolewa na Mziwanda kwani anampenda na ndiyo ubavu wake kutokana na vile ambavyo amekuwa akimwonesha mapenzi ya kweli tofauti na wapenzi wake wote waliopita.

“Huyu ndiye shemeji yenu, ndiye mume wangu mtarajiwa, ninampenda na yeye ananipenda kwa hiyo Mungu akijalia soon tutakamilisha taratibu za ndoa,’’ alisema Shishi Baby.
GPL

BABY MADAHA"WACHA NITENGENEZE CHAPAA KUOLEWA LABDA 2030"

$
0
0

Na Nyemo Chilongani
STAA wa muziki na filamu Bongo, Baby Madaha amesema hana papara na suala la ndoa kwani amejipanga kutimiza tendo hilo mwaka 2030.

Akizungumza na paparazi wetu, Baby alisema anachoomba ni uzima kwani suala la ndoa analiona halina umuhimu kwa sasa kwani ni kipindi cha yeye kusaka fedha kwa hali na mali.

“Sina haraka bwana, maisha haya yanahitaji kuyatengeneza, najipanga Mungu akipenda labda kwenye 2030 huko ndiyo nitafunga ndoa sasa hivi acha nitengeneze chapaa,” alisema Baby ambaye umri wake unakadiriwa kutopungua miaka 30. 
GPL

UKAWA RUDINI BUNGENI JAMANI TUENDELEE KUPATA UKWELI NA VIOJA

$
0
0
Kutokana na Bunge kupwaya sana baada ya UKAWA kutoka,ninawaomba warejee Mjengoni ili waendelee kutupa elimu ya Uraia ambayo tulikuwa tunaipata wakati session ikiendelea na sasa hatuipati.Tunaelewa kabisa kutoka na idadi yao kuwa ndogo mle ndani ni dhahiri kuwa hawawezi kushinda,lakini mioyoni mwa Watanganyika waliowengi nje ya jengo na Wazanzibari,hakika katiba hiyo haitapigiwa kura kutokana na halihalisi ya Rasimu ya Tume ya Warioba kuchakachuliwa.
Hivyo basi,Nawaomba  kuwasihi warejee mjengoni ili kukamilisha hatua hii ya Bunge la Katiba na kuendelea na kasi ileile ambayo inatusaidia sana Wajumbe tulio nje ya Jengo kufunguka na kupata uelewa halisi wa swala lenyewe.

MWANASHERIA MKUU WA ZANZIBAR NAE AUNGANA NA UKAWA ASEMA SEREKALI TATU NDIO MPANGO MZIMA

$
0
0
Katika hali ya kuonyesha kuwa ma-Interahamwe - ccm yanazidi kudhoofika kutokana na dhuluma yao kwa kufidhuli maoni na ukweli wa umma, Mwanasheria Mkuu wa Z'bar amewaumbua wanafiki wana-ccm wenzake na 201 waliobaki bungeni kuwa Serikali 3 ni ukweli uliopo wazi na ndivyo hata Katiba ya sasa inavyothibitisha, na hivyo ni ngumu sana kuufunika ukweli huo wakati Katiba ya sasa inazitaja wazi kuwa muungano wetu 'UNAUNDWA NA NCHI 2' na ni ngumu mno kuitaja Z'bar bila kuonyesha nchi ya pili ni ipi, kwa hivyo serikali 3 ni jambo lililosemwa hata ktk Katiba tuliyo nayo! Kauli liyowaacha CCM - interahamwe midomo wazi, kimyaaa na kwa aibu kubwa hawakuthubutu kumzomea, bali wameugulia mioyo, na kuguna kichinichini...unafiki na aibu! 
Source ITV News. 

My Take: TANGANYIKA ni TAIFA lisiloweza kuzuilika, Z'bar ni taifa lisiloweza kuzuilika, Serikali 3 ni mfumo usiozuilika na watawala waliojaa woga...! CCM wanaweweseka kila kukicha, wanaweka vikao vingi gizani na kusambaza fedha za udhalimu, za sembe, na dentals la nyara zetu ili kuendelea kutawala kidhalimu...lakini mkono wa Mungu unathibitisha ktk mwanga kuwa Watanganyika na Wazanzibar watawekwa huru...tena UHURU wa kweli na uliolindwa kwa mikono ya Mungu na Umma!

Naomba kuwasilisha!

KAULI YA MBOWE KUHUSU UKAWA KUSUSIA BUNGE

$
0
0
Leo katika kipindi cha KUMEPAMBAZUKA kinachorushwa hewani na kituo cha Radio cha RADIO ONE STERIO nimemsikia Kamanda Aikael Freeman Mbowe akitoa ufafanuzi wa UKAWA kutoka nje ya bunge maalumu la katiba na kutorudi tena bungeni bali kwenda kwa wananchi.

Mheshimiwa Mbowe ameeleza jinsi ambavyo bunge linavyoendeshwa kwa upendeleo mkubwa sana,Matusi makubwa ya nguoni kwa wajumbe wenye mawazo tofauti na ya serikali ya ccm,kutumia vitisho vingi,udhalilishaji na uonevu mkubwa .

Mheshimiwa Mbowe ametolea mfano kwamba Kama Lukuvi amekwenda kanisani na kuanza kuhutubia watu kwamba kama serikali 3 zitapita Jeshi litachukua nchi.Hivi ni vitisho ambavyo kwanza vinampunguzia umakini ama uwezo rais aliyepo madarakani na pia ni kuamsha hisia za jeshi kufanya hivyo hata leo.Kwa maneno mengine ni kuwapa mawazo ama maoni wanajeshi wetu kupindua serikali.

Inashangaza sana Mheshimiwa Lukuvi hawezi kuwajibika kwa kauli hii kwani mwaka 2009 Samson Mwigamba aliwahi kuandika makala fulani kwenye gazeti la TANZANIA DAIMA kuhusu jeshi lakini serikali ya ccm ikamfungulia mashtaka mahakamani kwamba ni mchochezi na analitaka jeshi LIASI TAIFA NA KUFANYA MAPINDUZI ( ARMY MULTINY AND REVOLUTION) na bahati nzuri sana kesi ile Mwigamba alishinda mwezi Fenruary 2014.Je serikali haioni kwamba Lukuvi ameamsha hisia na kufanya uchochezi jeshi kuasi????

Hata hivyo,mimi binafsi nadhani ccm wanakiinimacho wananchi.Wananchi wamesema Wanataka serikali 3 wao wanatoa vitosho vya Muungano kuvunjika,wanatoa vitisho kwamba nchi itaingia vitani,wanatoa vitisho kwamba fanya ufanyalo ni serikali 2 tu na mwingine akasema kwamba hata kama wananchi wanataka serikali 3 basi wasubiri yeye aondoke madarakani kwanza.

HIVI statements kama hizo zinaashiria dalili za nia njema kweli( GOOD POLITICAL WILL) ya kupata katiba mpya kweli???.Nina mashaka makubwa sana kama kweli katiba mpya inaweza kupatikana katika hali hii?
Viewing all 104789 articles
Browse latest View live




Latest Images