Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104414 articles
Browse latest View live

Harmo Rapper: Hata Kwa Dau Gani Kamwe Siwezi Kujiunga na Wasafi

0
0
Msanii anayejifananisha na Harmonize Harmo Rapper alikuwa akihijiwa kwenye kipindi cha Planet Bongo Cha East Africa Radio na kusema kwa sasa yeye ni msanii mkubwa wa level za akina Fid Q na hawezi kujiunga na Wasafi hata kwa dau kubwa kiasi gani....

Rais Magufuli Amjibu DC Aliyeomba Kujiuzulu

0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania amemjibu Mkuu wa Wilaya ya Uyui mkoani Tabora aliyeomba kujiuzulu wadhifa huo.

Katika majibu yake Rais Magufuli ameridhia uamuzi huo na kwamba uteuzi wa mtu mwingine atakayejaza nafasi hiyo utafanyika baadaye.

Taarifa iliyotolewa na Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu bwana Gerson Msigwa imesema "Ombi la Bw. Gabriel Simon Mnyele aliyeomba kujiuzulu wadhifa wake wa Mkuu wa Wilaya ya Uyui Mkoani Tabora limekubaliwana Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli. Nafasi ya Mkuu wa Wilaya ya Uyui Mkoani Tabora itajazwa baadaye."

Taarifa za kujiuzulu kwa Mkuu huyo wa wilaya zilianza kusambaa jana zikidai kuwa Mkuu huyo wa Wilaya aliaga katika Kamati ya Madiwani wa CCm, pamoja na kutoa taarifa kwa Mwenyekiti wa halmashauri kuwa ameamua kuchia ngazi, bila kueleza sababu sababu za uamuzi huo.

Hata hivyo baadaye kulitokea utata baada ya kusambaa kwa taarifa za yeye kukanusha kufanya uamuzi huo, lakini sasa ni dhahiri kuwa Bw. Gabriel Simon Mnyele siyo mkuu wa wilaya hiyo ten

Al-Shabab Washambulia kambi ya Wanajeshi wa KENYA Nchini Somali na Kuwaua 57

0
0
Kundi la al-Shabab nchini Somalia limesema wapiganaji wake wameshambulia kambi ya wanajeshi wa Kenya wanaohudumu chini ya kikosi cha Umoja wa Afrika (Amisom)nchini Somalia.

Wapiganaji hao wanadai kuwaua wanajeshi wengi kwenye shambulio hilo katika kambi ya Kulbiyow kusini mwa Somalia karibu na mpaka wa nchi hiyo na Kenya.

"Mujahideen (wapiganaji) wawili walivurumisha magari yaliyokuwa na mabomu na kuyalipua kwenye lango la kambi hiyo ya mji wa Kulbiyow kabla ya wapiganaji wengine kuingia. Baada ya makabiliano makali, tumefanikiwa kuiteka kambi," mmoja wa wasemaji wa al-Shabab Sheikh Abdiasis Abu Musab ameambia shirika la habari la Reuters.

Msemaji huyo amedai kundi hilo limewaua wanajeshi zaidi ya 57 na kutwaa magari na silaha za wanajeshi hao, taarifa ambazo msemaji wa majeshi ya Kenya amekanusha.

Kanali Paul Njuguna ameambia Reuters: "Ni uongo. Operesheni ya kijeshi inaendelea. Tunaendelea kupokea taarifa."

Al-Shabab wamekuwa wakipigana dhidi ya serikali  inayoungwa mkono na mataifa ya magharibi na jamii ya kimataifa.

Wanajeshi wa Kenya pamoja na wanajeshi kutoka Djibouti, Uganda na Ethiopia, chini ya Amisom, wamekuwa wakisaidia serikali hiyo yenye makao yake Mogadishu.

Januari mwaka uliopita, wapiganaji wa al-Shabab walishambulia kambi ya majeshi ya Kenya el-Adde na kuua wanajeshi wengi.

Al-Shabab walisema waliua zaidi ya wanajeshi 100. Jeshi la Kenya halijatangaza idadi kamili ya wanajeshi waliouawa hadi wa leo.

Chanzo: BBC

Kutana na Maalim Hussein Mtabibu wa Nyota za Binadamu Africa na Dunia Nzima,

0
0

Kutana na Maalim Hussein Mtabibu wa nyota za binadamu Africa na dunia nzima,
Anatoa TIBA MAENEO YOTE NCHINI, KWA WALE WENYE KUHITAJI TIBA ANATIBU YAFUATAYO,
Husafisha nyota na kutoa Pete za bahati na kwa wale walia sumbuka kwaajili ya matiba na hawakufanikiwa njoo ujionee muujiza wa papo kwa papo-humpa mtu jini la mali kwa yule anaetaka kumiliki mali bila masharti yoyote,
Anatibu magonjwa yalio shindikana-Mpenzi/MUME/MKE Aliekukimbia Anakurudishia Ndani ya saa 72 tu, Pia tunatoa dawa za Nguvu za KIUME na Kurefusha kwa saizi unayo Taka-Anatoa Dawa za BIASHARA NA MVUTO-Tunatoa Dawa za Uzazi kwa kina Mama kwa wale wenye Tatizo Sugu-Anatoa Zindiko ya Nyumba,Mwili, na Mvuto kazini- Tunamaliza kesi zilizo kaa muda Mrefu bila kumalizika, Tung'arisha Nyota na Cheo kazini. Tunarudisha Mali zilizopotea au Kuibiwa na Mengine Mengi ya Siri tuwasiliane kwa Simu-Whatsapp +255674835107
+255 629254849

Hali ni Tete Waliofukiwa Mgodini Geita

0
0

HALI bado ni tete katika kazi ya uokoaji wa watu 14 waliofukiwa na kifusi katika Mgodi wa Dhahabu wa Kampuni ya RZ Union Mining Ltd uliopo Kata ya Nyarugusu mkoani Geita, kutokana na hadi jana kutookolewa mtu yoyote.

Hata hivyo pamoja na sintofahamu hiyo juhudi za uokoaji zinaendelea kwa kasi, huku Mkuu wa Mkoa wa Geita, Ezekiel Kyunga akisema bado anayo imani kuwa watu hao wataokolewa wakiwa hai.

Mkuu huyo wa Mkoa alisema moja ya kazi iliyoendelea jana ilikuwa ni kwa vikosi vya uokoaji kuendelea kuchimba kifusi ili kutafuta njia ya kuwafikia waathirika huku mipira zaidi ya Oxygen ikiingizwa chini ya mgodi waliko watu hao ili kuwaongezea hewa.

Watanzania 13 na raia mmoja wa China walifukiwa na kifusi juzi usiku baada ya udongo kukatika na kuziba mlango waliokuwa wakitumia kuingia na kutoka. Mkuu wa Mkoa aliliambia gazeti hili jana kuwa hadi jana walikuwa bado hawajafanikiwa kuwafikia watu hao lakini kazi ya kuwafuata waliko inaendelea kwa kasi.

Akizungumza akiwa eneo la tukio, Kyunga alisema vyombo mbalimbali vya uokoaji kwa kushirikiana na wananchi walikuwa wanaendelea kuchimba kifusi ili kuwasaka mahali walipo mgodini.

“Kutokana na uzoefu wa kazi na matukio kama haya yaliyowahi kutokea tuna matumaini makubwa ya kuwaokoa wakiwa hai kutoka na mlango ndiyo uliojiziba na udongo na watu hao wako katika mtaro wa mlalo hivyo kwa kutumia Oxygen tunayoingiza kwa mipira tutawakuta wakiwa hai,” alisema.

Kyunga alieleza kuwa watu wengi wapo katika eneo hilo wakiwemo ndugu wa waliofukiwa lakini kwa juhudi wanazoziona za uokoaji wametulia na kufuata maelekezo wanayopewa ikiwemo kukaa mita 500 kutoka eneo la tukio.

Alisema wametakiwa kukaa mbali na eneo hilo la uokoaji ili wasisongamane na watu wanaoendelea na uokoaji ili kuwapa fursa nzuri ya vikosi vyote kujadiliana namna ya kufanywa kwa ajili ya kufanikisha uokoaji huo.

Kwa upande wake Kamanda wa Polisi Mkoa wa Geita, Latson Mponjoli alisema juhudi za uokoaji zinaendelea kwa ushirikiano wa vikosi vya uokoaji vya Kampuni ya Geita Gold Mine (GCM), Jeshi la Zimamoto na Polisi pamoja na kikosi cha ukoaji cha Sekta ya Madini. Alisema hali ni shwari katika eneo hilo na wana matumaini ya kuwafikia watu hao wakiwa hai.

Kampuni inayoendesha mgodi huo imesema kutokana na kitabu cha orodha ya watu wanaojiandikisha kuingia mgodini, kuna majina ya Watanzania 12 na Mchina mmoja waliofukiwa kifusini. Ilielezwa kuwa watu pia waliomshuhudia Mtanzania mmoja akingia mgodini humo bila kujiandikisha na hivyo kufanya waliofukiwa kufikia 14.

Agizo la Magufuli Lazua Mtafaruku Chadema..!!!

0
0

Agizo la Rais John Magufuli la kutaka Baraza la Madiwani la Jiji likutane kuamua matumizi ya fedha zilizolipwa kununua hisa za Shirika la Usafiri Dar es Salaam (Uda), limesababisha makada wawili wa Chadema kugombana kikaoni.

Kampuni ya Udart, inayoendesha mradi wa mabasi yaendayo kasi, ililipa Sh5.8 bilioni kukamilisha ununuzi wa hisa za Uda na hivyo Rais kuamua madiwani wakutane kujadili matumizi yake.

Jana, baraza hilo lilikutana na ndipo kasheshe hiyo ilipoibuka.

Upande mmoja ulitaka baraza la madiwani lisipitishe uamuzi wa kutumia fedha hizo kwa madai kuwa mchakato wa uuzaji wa hisa hizo kwa Udart, inayoendesha mradi wa mabasi yaendayo kasi, haukufuata sheria wala taratibu, wakati upande mwingine ukitaka zitumike.

Wajumbe hao wa Chadema, Boniface Jacob, ambaye ni Meya wa Ubungo na Patrick Assenga (Diwani, Tabata) walishikana mashati kwenye kikao cha pembeni cha madiwani wa Chadema kilichofanyika baada ya mkutano wa Baraza la Madiwani.

Madiwani hao wa Chadema walienda ofisi ya Meya wa Jiji, Isaya Mwita kuzungumzia suala hilo na katika mazungumzo walipishana kauli kutokana na kile kilichoonekana ni kutosimamia msimamo wa chama wa kutokubali fedha hizo zitumike kwa kuwa wanaamini mchakato wa kuuzwa kwa hisa hizo haukufuata sheria na taratibu zinazotakiwa.

Kipigo cha Wanajeshi cha Sababisha Kifo cha Konda wa Daladala..!!

0
0

Kondakta wa daladala linalofanya safari zake kati ya Nguvumali hadi Raskozone, Salim Kassim amefariki dunia baada ya kudaiwa kushambuliwa ndani ya kambi ya jeshi jijini hapa.

Kwa mujibu wa habari zilizopatikana na kuthibitishwa na Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Tanga, Benedict Wakulyamba, kondakta huyo alikufa wakati akipelekwa katika Hospitali ya Mkoa ya Bombo na chanzo cha kifo bado kinachunguzwa.

Mwananchi ilielezwa kuwa tukio hilo lilitokea juzi usiku, ambapo mashuhuda walidai kuona kondakta huyo akichukuliwa na wanajeshi na kuingizwa kambini na baadaye alitolewa akiwa hajitambui

Akizungumzia tukio hilo, Khalid Juma mkazi wa Nguvumali jijini hapa alisema askari hao wamekuwa na desturi ya kuwapiga wananchi bila kuchukuliwa hatua zozote za kisheria.

“Tumekuwa tukipata vipigo kila wakati, licha ya viongozi kupata taarifa za matukio hayo wamekaa kimya na hili tukio ni la tatu kutokea hapa,” alidai Khalid.

Diwani wa Kata ya Nguvumali ambaye pia ni Meya wa Jiji la Tanga, Alhaji Mustapha Selebosi alisema sababu za kipigo hicho ni mwanafunzi wa shule moja jijini Tanga ambaye ni mtoto wa ofisa wa JWTZ kuzozana na kondakta.

Mwanamke Asimulia Alivyokuwa Akimshushia Kipigo Mumewe kwa Miaka 30 Mfululizo..!!

0
0

Mara nyingi vitendo vya ukatili na unyanyasaji kijinsia vimezoeleka kufanywa na wanaume dhidi ya wanawake na watoto.

Hata hivyo, kampeni ya “Tunaweza” inayoratibiwa na shirika lisilo la kiserikali la Kivulini jijini Mwanza kwa lengo la kutokomeza ukatili na unyanyasaji wa kijinsia, imebaini kuwa vitendo hivyo pia hufanyika dhidi ya wanaume.

Mkazi wa Mtaa wa Mwananchi, Kata ya Mahina jijini Mwanza, Ernest Kibinzaroya (78) ni mfano wa ukatili unaofanywa na wanawake dhidi ya wanaume. Yeye pamoja na mkewe, Maria Kibinzaroya (57) wamejitokeza hadharani kueleza walivyopitia maisha hayo.

Inaelezwa kwamba Maria alikuwa akimpa kipigo cha mara kwa mara mumewe kabla ya ‘kuokoka’ na kuwa mke mwema.

‘Wokovu’ huo ni baada ya kampeni hiyo inayofanyika katika wilaya za Ilemela, Nyamagana, Magu, Misungwi, Sengerema mkoani Mwanza kuwafikia wanadoa hao na wote hivi sasa wana mabadiliko na wanapiga vita ukatili na unyanyasaji wa kijinsia.

Akizungumza mbele ya mumewe wakati wa mahojiano maalumu nyumbani kwao, Maria anasema miaka zaidi ya 30 ya ndoa yao imekuwa ya mateso, manyanyaso na misukosuko iliyoambatana na kipigo alichokuwa akimpa mumewe.

“Kabla ya kupata elimu kuhusu vita dhidi ya ukatili na unyanyasaji wa kijinsia, nilikuwa nampiga mume wangu mara kwa mara,” anasimulia Maria.

Huku mume wake akitikisa kichwa kuonyesha kukubaliana na maelezo ya mkewe, Maria anasema vitendo hivyo viliambatana wakati mwingine na kugoma kupika chakula, vimemfanya mumewe kupata shinikizo la damu.

Samia Aishukuru India kwa Kufadhili Miradi ya Maji Nchini..!!!

0
0

MAKAMU wa Rais Samia Suluhu Hassana ameishukuru Serikali ya India kwa ufadhili wake wa miradi ya maji katika miji 17 nchi ambayo inalenga kupunguza tatizo la maji kwa wananchi wengi nchini.

Samia alitoa kauli hiyo jijini Dar es Salaam jana katika hafla ya Maadhimisho ya miaka 68 ya Siku ya Kitaifa ya Jamhuri ya India, iliyoambatana na uzinduzi rasmi wa majengo ya ofisi mpya ya Ubalozi wa India nchini.

Samia alisema ufadhili wa miradi ya maji na miradi mingine unaofanywa na Serikali ya India kwa Tanzania Bara na Zanzibar unadhihirisha wazi uhusiano mzuri uliopo ulioasisiwa na Mwalimu Juliu Nyerere na Mahatma Gandhi wa India.

Alisema kwa miaka mingi sasa uhusiano wa kindugu umekuwa ukiimarika katika sekta mbalimbali ikiwemo kisiasa, kidiplomasia, kibiashara, masuala ulinzi, utamaduni na mwingiliano wa watu na watu.

Aidha Makamu wa Rais pia aliishukuru Serikali ya India kwa msaada wake wa Sh milioni 500 alioutoa kwa wananchi wa Mkoa wa Kagera ambao walikumbwa na tetemeko la ardhi mwaka jana.

Katika hafla hiyo, Makamu wa Rais kwenye hotuba yake alitoa salamu za rambirambi kwa Serikali ya India kufuatia ajali ya treni iliyotokea katika Jimbo la Andhra Pradesh na kusababisha vifo vya watu 30 na kujeruhi wengine.

Kwa upande wake, Balozi wa India nchini Sandeep Arya alimhakikishia Makamu wa Rais Samia kuwa Serikali ya India itaendelea kudumisha na kuendeleza uhusiano mzuri uliopo kwa ajili ya manufaa ya wananchi wa pande zote mbili.

Pitia Vichwa vya Magazeti ya Leo Jumamosi 28/1/2017..!!!

Wanasayansi Wagundua Jiwe Lenye Thamani ya Dunia na Zaidi,Linathamani ya Quadrilion 10,000

0
0

WANASAYANSI wa Kituo cha Anga cha Marekani (NASA), wamegundua jiwe kubwa lenye utajiri wa kutisha wa madini ya aina mbalimbali linaloelea angani.

Thamani ya utajiri wa madini yaliyopo katika jiwe hilo, unaelezwa kuwa ni zaidi ya uchumi wa dunia nzima.

Kutokana na ugunduzi huo, NASA wanapanga kuruka maelfu ya kilomita angani mwaka 2023 kwenda kwenye jiwe hilo ambalo kama litafanikiwa kurudishwa duniani, linaweza kuleta utajiri wa kufuru.

Likiwa katikati ya Sayari ya Mars na Jupiter, jiwe hilo linaaminika ni kiini cha ndani cha moja ya sayari zilizokufa.

Kwa mujibu wa wanasayansi, jiwe hilo ni la kipekee na limeundwa kwa madini ya metali kwa asilimia 100.

Jiwe hilo lenye umbo la duara lina urefu wa kilomita 200 na lina madini kama chuma, nickel na wanasayansi wanasema upo uwezekano mkubwa wa kuwa na madini adimu duniani kama dhahabu, platinamu na cobalt.

Jiwe hilo ambalo ni sayari mfu, lina thamani ya fedha nyingi mno, chuma peke yake kilichopo katika jiwe hilo, kinaweza kuwa na thamani ya Dola za Marekani 10,000 quadrillion, hii ni kwa mujibu wa mchunguzi mkuu wa jiwe hilo, Profesa Lindy Elkins-Tanton.

Uchumi wa dunia kwa jumla hivi sasa una thamani ya dola za Marekani 73 trilioni.

“Kwa sasa, kwenda kwa NASA katika anga za juu kunaleta dhana halisi ya ugunduzi. Safari hiyo, itawezesha kufika katika sehemu yenye kitu ambacho hakijawahi kuonekana wala kujulikana. Itatoa nafasi kwa wanasayansi kuona kitu ambacho kilikuwa kinafikirika hadi kufikia hivi sasa.

“Bado hatujaweza kufahamu mambo mengi, lakini tunadhani jiwe hili ni kiini cha metali ya sayari ndogo iliyoharibiwa kutokana na nishati kubwa, mwendo kasi wa dunia,” anaeleza  Elkins-Tanton

Mpango huo wa kufika katika anga lililopo jiwe hilo, unatarajiwa kuzinduliwa mwaka 2023 na hadi kufikia mwaka 2030 chombo cha anga za juu kitakuwa kimefika eneo lililopo.

Wanasayansi ambao wametumia muda mwingi kulichunguza jiwe hili wanasema ndiyo jiwe kubwa la metali kwenye mfumo wa jua lililopo umbali wa kilomita 300 na inaaminika kuwa na kiasi kikubwa chuma na nickel.
Jiwe hilo kwa mara ya kwanza aliliona mwanaanga wa Kitaliano Annibale de Gasparis mwaka 1852 na kupewa jina la mungu wa roho wa Kigiriki Cupid.

Mwanzoni, ilidhaniwa kuwa ni jiwe la barafu lakini miaka ya 1980 wanaanga walishangazwa kuona rada ikisoma kuwa jiwe hilo lilikuwa linaundwa na metali.

Wanasansi wanaamini kuwa, jiwe hilo limepoteza ganda lake la nje, kutokana na msuguano na msukumano ambao umefanyika kwa mamilioni ya miaka.

Ili kupata ukweli zaidi kuhusiana na ugunduzi ambao bado unaacha maswali mengi, NASA itapeleka chombo chake katika eneo lililopo kwa ajili ya uchunguzi zaidi wa kisayansi ambao unatarajiwa kuchukua muda mrefu.

Hii ni nafasi ya ugunduzi wa aina mpya ya dunia ambayo haijawahi kuonekana, si mwamba wala jiwe la barafu bali ni metali tupu,” anasema Elkins-Tanton ambaye ni Profesa katika chuo Kikuu ha Arizona nchini Marekani.

Anaongeza: "Jiwe hili ni aina pekee ya umbo ambalo limeweza kugundulika kwenye mfumo wa jua, ni njia pekee ya binadamu kuona shehemu ya kiini cha sayari iliyokufa. Mara nyingi tumekuwa tukijifunza sehemu ya ndani au kiini kwa kutembelea na kutizama sehemu za juu.

Chombo kitakachokwenda katika anga lililopo jiwe hilo, kitachukua miaka saba kufika. Pia kitakaa kwenye jiwe hilo kwa miezi sita kikijaribu kurekodi vitu mbalimbali kama muonekano, usumaku na vitu vilivyomo ndani yake.

Mpango huo ni sehemu ya mpango wa ugunduzi wa NASA utakaogharimu dola za Marekani milioni 450 wenye lengo la kujifunza kuhusu mfumo wa jua miaka milioni 10 tangu kuzaliwa kwa jua.

Mpango wa pili utazinduliwa mwaka 2021 ambao utalenga kuchunguza mabaki ya maombo ambayo yapo jirani na sayari ya Jupiter.

Daktari Feki Akamatwa Akitoa Huduma Hospitali ya Mnazi Mmoja..!!!

0
0

WATU saba, akiwamo mmoja anayedaiwa kuwa daktari bandia, wanashikiliwa na Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam kwa madai ya kutengeneza kadi bandia za chanjo ya homa ya manjano na kuziuza kwa watu wanaofika hospitali ya Mnazi Mmoja kwa ajili ya kupata huduma hiyo.

Chanjo hizo ni zile ambazo hutolewa kwa watu ambao wanasafiri nje ya nchi kama kinga kwa ajili ya homa manjano.

Kamishna wa Kanda hiyo, Simon Sirro, akizungumza jana na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, alimtaja aliyejifanya daktari kuwa ni mfanyabiashara Salum Natali (47), mkazi wa Chanika Magengeni.

Kamanda Sirro aliwataja watuhumiwa wengine ni walinzi watatu ambao ni Aisha Hassan (29) mkazi wa Vingunguti Mikoroshini, Yakobo Msenga (42) mkazi wa Chanika na Junith Dunstan (23) mkazi wa Kiwalani.

Wengine ni Oliver Bwegege (58) mkazi wa Kigogo Mkwajuni, mjasiriamali Fredy Nyomeye (44) mkazi wa Chang’ombe na fundi umeme Mohamed Bwanga (59) mkazi wa Majohe Gongo la Mboto.

Alisema watu hao walikamatwa Januari 16, mwaka huu majira ya saa 11:00 asubuhi baada ya mtoa taarifa (jina linahifadhiwa) kufika hospitalini hapo na kutakiwa kutoa fedha na mmoja wa watuhumiwa hao ili kupatiwa kadi hiyo ya chanjo ya homa ya manjano.

“Katika mahojiano, watuhumiwa hao walikiri kufanya kosa hilo la kughushi na kutoa kadi hizo za chanjo pasi na mtu kuchomwa sindano yenyewe ya chanjo,” alisema.

Kamishna Sirro alisema Natali alikuwa akijifanya kuwa ni daktari aliyekuwa akiwachoma watu sindano.

Alisema uchunguzi wa tukio hilo bado unaendelea ili kuwabaini washiriki wengine katika mtandao huo wa utoaji wa kadi hizo bandia za chanjo bila kutoa chanjo yenyewe husika.

Katika tukio lingine, watu wawili wanaodaiwa kuwa majambazi wameuawa na polisi baada ya kudaiwa kuhusika kwenye tukio la mauaji Boko Basihaya, jijini Dar es Salaam.

Sirro alisema inadaiwa kuwa watu hao walihusika kwenye kifo cha mlinzi wa duka la pombe (Grocery) aliyetajwa kwa jina la Marwa. Alisema watu hao wanadaiwa kumpiga risasi kichwani mtu huyo na kupora Sh. milioni 1.3.

“Baada ya tukio hilo Jumatatu ya wiki hii polisi walimkamata mwendesha bodaboda, Nathan Mathias akiwa kwenye baa iitwayo PK eneo la Kawe, ambaye alikiri kuhusika na tukio hilo na alimtaja Hamis Daudi mkazi wa Boko njia panda Magereza kushirikiana naye.

“Polisi walifanya upekuzi nyumbani kwa Daudi na kuipata silaha aina ya Shotgun Pump Action yenye namba P. 918884 na TZCAR 76475 ikiwa na risasi mbili,” alisema.

Alisema watuhumiwa hao waliwaeleza polisi kuwa bunduki nyingine wameificha maeneo ya Ununio kwenye mabwawa ya chumvi kando ya Bahari ya Hindi hivyo askari walikwenda nao huko kwa ajili ya kuzichukua.

Serikali Yapiga Marufuku Wanafunzi kufundishwa Somo la Dini ya Kiislamu Mashuleni..!!!

0
0

 SERIKALI nchini Swaziland imeziagiza shule zake kufundisha somo la dini ya Kikristo pekee, hatua iliokosolewa na wadau mbalimbali kwa kuwa haiheshimu dini nyengine.

Agizo hilo lilitolewa wiki iliyopita na Wizara ya Elimu nchini humo, ambapo ilipita shuleni ikiwaagiza walimu wakuu wote kuhakikisha mtaala hautaji dini nyingine zaidi ya Kikristo.

Sahid Matsebula, ambaye ni Muislamu anayefanya kazi msikitini karibu na Mji Mkuu wa Mbabane, alinukuliwa akisema kwamba sera hiyo huenda ikazua wasiwasi wa kidini katika ufalme huo.

''Serikali ina mpango gani kwa watoto wetu ambao si Wakristo? Ambao licha ya kujifunza wakiwa nyumbani, mambo mengine wanapaswa wajifunze wakiwa shuleni,” alisema.

Sera hiyo mpya imekuja baada ya raia kulalamika kuhusu wahamiaji wa Bara la Asia na wale wa Kiislamu kwamba wamekuwa wakiingia nchini humo hatua iliyolazimu Bunge kuunda kamati ya kuchunguza tukio hilo.

Wahamiaji wengine tayari wamerudishwa makwao na Waziri wa Biashara, Jabulani Mabuza ameliambia Bunge kwamba wameanza kutunga sheria itakayowazuia wahamiaji kuanzisha biashara nchini Swaziland.

Rais wa Baraza la Makanisa nchini humo, Stephen Masilela ameunga mkono mtaala huo mpya.

''Ukristo ndio msingi wa kujengwa kwa taifa hili,” alisema.

Hata hivyo, Taifa la Swaziland linaloongozwa na Mfalme Mswati wa tatu tangu mwaka 1986, lina idadi ndogo ya waumini wa Kiislamu.

Sera hiyo ya kufundisha dini ya Kikristo pekee shuleni, pia imekosolewa na mwandishi Nomsa Mbuli wa gazeti la Times of Swaziland.

“Kinachoinua dini moja juu ya nyengine ni nini wakati ambapo Katiba inaagiza usawa wa kidini?” alihoji.

Chuchu: Mtoto Ameongeza Mahaba kwa ‘Baby’..!!!

0
0

MUIGIZAJI wa sinema za Kibongo, Chuchu Hans ambaye hivi karibuni alijifungua mtoto wa kiume (Jayden), amesema mtoto huyo ameboresha mahaba niue kwa mpenzi wake, Vincent Kigosi ‘Ray’.

Akizungumza na Mikito Nusunusu, Chuchu alisema mtoto huyo amekuwa ni faraja kwao wote na mapenzi yameongezeka baina yake na mpenzi wake huyo kitu ambacho anamshukuru Mungu. 

“Jamani mwacheni Mungu aitwe Mungu, mahaba yamezidi asilimia ni jambo la kumshukuru sana aliye juu maana bila yeye kusingekuwa na kitu kabisa na ninamuomba atimize mambo mengine makubwa zaidi,” alisema Chuchu.

Breaking News: Kiongozi wa Walinzi wa Ikulu ya Gambia Atoroka

0
0

Kamanda wa Polisi wa Jeshini (MP) katika ikulu ya Gambia, Luteni Nuha William Jammeh, yasemekana yupo mafichoni. Inasemekana alitoroka Gambia siku chache zilizopita. Kamanda huyu alitoa amri ya kukamatwa kwa maafisa kadhaa wa jeshi la nchi hiyo walioonekana kumpinga Rais aliyemaliza muda wake, Yahya Jammeh.

Kwa sasa Luteni Nuha Jammeh hajulikani alipo. Amekimbia mji mkuu wa Banjul na inaaminika kuwa amekimbilia nchini Senegal. Namba yake rasmi ya simu inayojulikana inaonesha kuwa yupo nchini Senegal ingawa simu yake imezimwa.

Akimzungumzia Nuha Jammeh, mtu aliyewahi kusoma nae darasa moja alisema: ” Alikuwa mkimya sana na anayependa sana dini. Ilikuwa ni rahisi sana kuzoeana naye kipindi kile. Baada ya kukutana na Yahya Jammeh, huwezi jua, kwa maana yule dikteta alikuwa na uwezo wa kugeuza watu wazuri kabisa kuwa mashetani.”

Ni Funzo Kubwa…. Liruhusu Likae Moyoni Mwako

0
0
nomaKuna jamaa alikuwa masikini sana mkoani Kigoma. Alikuwa akiishi na mke wake huku wakiwa na mtoto wao mdogo. Kutokana na maisha kuwa magumu, akaamua kuwa mkulima. Akalima na kulima lakini hakufanikiwa. Akakata tamaa hivyo kuamua kujiingiza kwenye uuzaji wa mafuta ya mawese.

Alihisi kwamba mambo yangebadilika lakini baada ya yeye kuanza biashara hiyo, soko la mafuta ya mawese likashuka kwa kasi ya ajabu hivyo hakufanikiwa. Maisha yaliendelea kumtesa, umasikini ulimtafuna yeye na familia yake.

Kikafika kipindi akachoka, hakutaka kuona akiteseka na familia yake hivyo kumwambia kwamba ni lazima aondoke na kwenda nchini Kongo kuchimba dhahabu, labda bahati yake ilikuwa huko. Mkewe alipinga lakini akamshawishi kwa kipindi kirefu na hatimaye akakubaliana naye.

Baada ya kutafuta fedha za kuungaunga, akaelekea huko. Alipofika, alikaa kwa miaka saba ndipo akafanikiwa kupata dhahabu kubwa, nzito ambayo aliamua kuibeba katika begi lake na kurudi Kigoma kwa meli.

Ndani ya meli kulikuwa na watu wengi, hasa Wazungu ambao walikwenda huko kufanya utalii. Wakati meli ikiwa imefika katikati ya ziwa Tanganyika, ikaanza kuzama. Watu walipiga kelele sana, kwa jamaa hakukuwa na tatizo kwani alijua sana kuogelea, hivyo akawa anapiga mbizi na wakati mwingine kuelea juu ya maji.

Wakati watu wengi wamekufa, akasikia sauti ya msichana mmoja mdogo akilia, alikuwa mtoto wa Kizungu, wa kike aliyekuwa akiomba msaada. Jamaa alimuona mtoto yule wa miaka kumi na tano, akaamua kumfuata na kumbeba, kitu cha ajabu kabisa ambacho hakujua ilikuwaje, akaanza kuzama kutokana na uzito.

Kulikuwa na mambo mawili makubwa, alitakiwa kufanya moja ili anusurike. La kwanza lilikuwa ni kumuacha mtoto yule afe na yeye aondoke zake, au kuiacha dhahabu ile ili amnusuru yule mtoto. Ulikuwa mtihani mkubwa mno kwake. Aliondoka nyumbani miaka saba iliyopita, alimwambia mkewe kwamba anakwenda kutafuta utajiri nchini Kongo.

Alifanikiwa kwa kupata dhahabu kubwa ambayo aliamini ingemfanya kuwa bilionea. Sasa iweje aiache dhahabu kwa ajili ya mtoto asiyemjua ambaye wazazi wake walikufa? Moyo wake ukagawanyika, upande mmoja ukamwambia aachane na mtoto kwani hata angemuokoa, angeishi naye wapi?

Angemsaidia nini na wakati hawakujuana? Ukamkumbusha maisha aliyokuwa amepitia, maisha ya kimasikini, yaliyomuumiza, yakamletea picha ya mkewe na mtoto wake walivyokuwa wakiteseka kwa kupigwa na umasikini.

Upande mwingine ukamwambia lilikuwa jambo jema kumsaidia mtoto yule. Utajiri hauna kitu mbele ya utu. Ilikuwa ni lazima amsaidie mtoto yule kwani hata kama angepata fedha, bado angekufa baadaye, ni wangapi walikuwa na fedha ila wamekufa na kuziacha fedha hizo?

Moyo wake ukawa mgumu kufanya maamuzi lakini mwisho wa siku akaitupa dhahabu kubwa majini. Moyo ulimuuma sana lakini hakuwa na jinsi. Akambeba msichana yule wa Kizungu na kuanza kuogelea naye, saa moja mbele, wakaokolewa na meli nyingine.

Mtoto yule akasaidiwa na Umoja wa Mataifa kurudishwa Marekani alipokuwa akiishi huku nyuma jamaa alipofika nyumbani na kumuhadithia mkewe kilichotokea, alimtukana sana na kumuona mjinga, iweje atupe dhahabu na wakati alipoteza miaka saba kuitafuta? Majirani wakamcheka, wakamdharau na mkewe akaamua kuondoka kurudi kwao kwani asingeweza kukaa na mwanaume mpumbavu kama yeye.

Jamaa akaanza upya, maisha yakaanza kumpiga tena. Alilia sana, alichekwa kila kona. Alitamani kurudi Kongo kutafuta tena dhahabu lakini hakuwa na fedha. Akawa ombaomba, kila kona mkoani Kigoma alikuwa akipita kuomba, kuanzia Ujiji, Mwanga, Mwembetogwa, Mji Mwema, Bangwe na kila sehemu alikuwa akiombaomba.

Baada ya miaka mitano, wakati akiwa amepigwa sana na maisha, ghafla akamuona msichana wa Kizungu akija mbele yake. Hakumjua, msichana yule alipiga hatua mpaka kule nyumbani kwake alipokuwa. Alipofika, akamsalimia huku akiwa na Mkalimani wake. Akamuuliza kama alimkumbuka, jamaa akasema hamkumbuki ndipo yule msichana akasema kwamba yeye ndiye yule binti wa miaka kumi na tano aliyekuwa amemuokoa kipindi cha nyuma.

Jamaa alifurahi kumuona, akamkumbatia. Msichana yule akamwambia kwamba alikuwa akimkumbuka kila siku kwa wema aliomuonyeshea. Kipindi hicho, msichana huyo alifanikiwa sana, alikuwa mfanyabiashara mkubwa Marekani, mwenye kampuni nyingi kwani wazazi wake walimuachia utajiri mkubwa.

Jamaa akamwambia kila kitu kilichotokea katika miaka mitano ya mateso. Msichana yule akahuzunika sana, alichokifanya ni kumwambia jamaa kwamba alikuja Kigoma kwa ajili ya kumchukua yeye na familia yake kwenda kuishi nchini Marekani kama fadhila kwake. Ila kwa sababu mkewe aliondoka na mtoto na hakujua walipokuwa, basi aondoke naye tu.

Jamaa akafurahi. Huo ndiyo ukawa mwisho wa kuishi Tanzania. Akaondoka na kuelekea Marekani, kama alivyokuwa msichana yule, naye akawa mfanyabiashara mkubwa. Ameoa huko na maisha yake yanaendelea kama kawaida.

FUNZO: Unapotakiwa kutenda wema, wewe tena pasipo kujali itakugharimu kiasi gani. Inawezekana jamaa angeona dhahabu ni mali, angekufa njiani au ingepotea. Kwa kumsaidia msichana yule, Mungu akaileta meli. Kwa kumuokoa msichana yule, leo hii yupo nchini Marekani akila maisha.

Alisubiri kwa miaka mitano, kama kukata tamaa angekata mapema sana. Msichana hakumsahau, aliendelea kumkumbuka, aliukumbuka wema wake na kurudi Tanzania kutoa fadhila.

E.J SHIGONGO.

Kimenukaa..!! Iyobo Afichua Michepuko ya Aunt Ezekiel,Adai Atashindwa Kumvumilia Endapo...!!!!

0
0

DANSA maarufu wa Kundi la Wasafi  Classic Baby (WCB), Moses Iyobo amefunguka kuwa kamwe hawezi kumnunulia gari mzazi mwenziye, Aunt Ezekiel kwa kuwa anaogopa atapandisha michepuko yake.

Iyobo alifunguka hayo juzikati alipokuwa akipiga stori mbili tatu na Global Publishers ambapo alisema kwa sasa anajipanga kumnunulia nyumba mpenzi wake huyo lakini siyo gari maana anaweza kuwapandisha ‘michepuko’ wake kitu ambacho kitamuumiza bora nyumba mtu hawezi kukanyaga.

“Hapa mimi najipanga nimnunulie nyumba lakini gari hapana nimeshakataa, akipandisha ‘mababy’ zake je? Bora nyumba hakuna mtu atakayekanyaga kabisa,” alisema Iyobo.

Wowowowo..Wema Sepetu Aibuka Upya Instagram ...!!

0
0

MREMBO asiyeishiwa matukio kila kukicha Bongo, Wema Isaac Sepetu hatimaye ameibuka kwa mara nyingine Instagram baada ya kuitelekeza akaunti yake kwa muda ambapo alifuta picha zake zote za zamani na kubakiza maswali mengi kwa mashabiki wake ambao hawakuweza kupata majibu.

Kabla ya kufuta kila kitu kwenye akaunti yake hiyo, Wema alikuwa na zaidi ya followers milioni mbili na nusu, ambao wameendelea kumvumilia hadi jana jioni aliporejea na kuanza kuweka picha mpya kwenye profile yake kisha akaipost upya kwenye akaunti yake hiyo.

Hadi muda huu, Wema bado hajatoa sababu ya msingi iliyomfanya aamue kufuta posti zake hizo pamoja na kuwa na maswali mengi kutoka kwa mashabiki wake wakimtaka awafafanulie kilichomfanya kuchukua uamuzi huo.

Wema ameandika yafuatayo kwenye akaunti yake:

Happy 2017… and am excited.. how Many Likes?? Share from
This one and am gonna Tell You something to Celebrate for the whole Year…. #WSSoCloseToYou #WSladieschoice #WSyourAddiction
#unataka kusikia jambo zuri kutoka kwangu kwa mwaka 2017? Gonga Likes za kutosha and nitarudi kukung’ata sikio… This be your First Image…. There is plenty of these Just for You…. I missed You too…. @ossegrecasinare You are Life….

Ommy Dimpoz Afunguka Mapya Juu ya Wasanii wa Label ya WCB ya Diamond..!!!

0
0

Msanii Ommy Dimpoz ambaye kwa sasa anafanya vyema na wimbo wake 'Kajiandae' akiwa na Alikiba amefunguka na kusema hata yeye anaweza kufanya collabo na msanii yoyote yule kutoka WCB. 

Ommy Dimpoz alisema hayo kupitia kipindi cha eNEWz cha (EATV) na kusema kwenye muziki kuna wakati unaweza kupata wimbo ambao unahitaji collaboration na msanii fulani ili uweze kuwa bora zaidi hivyo inapotokea hivyo ni lazima ufanye mawasiliano na msanii huyo ili ufanye naye hata kama yupo WCB au sehemu nyingine.

"Siyo tu Nedy hata mimi naweza kufanya kazi na msanii kutoka WCB siyo tatizo, kwa sababu huu ni muziki pia ni biashara na lazima uangalie wimbo huu naotaka kufanya nikifanya na msanii fulani kutakuwa na hiyo combination nzuri? Kwa hiyo haijalishi kikubwa wote tunafanya muziki na kufanya biashara na kuangalia nikifanya na msanii huyu kazi yangu itakuwa na impact gani kwa hiyo hivyo vitu vyote vinawezekana" alisema Ommy Dimpoz

Mbali na hilo Ommy Dimpoz ameweka wazi kuwa kwa mwaka huu ataachia kazi nne, mbili zikiwa na kazi za kushirikiana na kazi mbili atakuwa amefanya yeye mwenyewe 

Wastara Aweka Wazi Sababu ya Kuacha Wanaume

0
0

Msanii wa filamu, Wastara Juma ameweka wazi sababu kubwa ambayo ilimpelekea kuachana na aliyekuwa mpenzi wake Bondi Bin Salim na kwenda kuolewa na Mbunge wa jimbo la Donge, Sadifa Khamis Juma kisha kuachana naye na kurudiana tena na mpenzi wake 

Akiongea kwenye kipindi cha Friday Night Live cha (EATV) Wastara anasema aliamua kuachana na Bond kutokana na tabia yake ya matumizi ya dawa za kulevya aina ya mirungi na pombe pamoja na tabia zingine ambazo yeye alishindwa kuvumilia na kuamua kuachana naye.

"Ukweli ni kwamba kuna issue nzito ilitokea kati ya mimi na Bond mpka Bond mwenyewe aliamua kutoa ushuhuda na kutubu juu ya matumizi ya dawa za kulevya aina ya mirungi, mpka aliamua kuondoka mwenyewe kwenda mbali na mazigira ambayo mimi nilikuwa naishi, alikuwa anatafuta njia ya kujisaidia ili aache vile vitu ambavyo binafsi nilikuwa sivipendi, kwanza kwenye mahusiano kulikua hakuna uaminifu kabisa, ilifikia hatua mpka kuna watoto wengi sana walikuwa wanaletwa wengine ni kweli wengine wa uongo vile vitu binafsi kama mwanamke vilikuwa vinaniumiza" alisema Wastara 

Mbali na hilo Wastara anasema baada ya hapo familia yake ilimshawishi aweze kuolewa na Mbunge huyo Sadifu ambaye alikuwa anahitaji kuwa naye na kusema aliwasikiliza sababu siku zote familia yake huwa inaiweka mbele na kuwasikiliza na kuamua kwenda kuolewa na Mbuge lakini anasema baada ya kuingia huko alikutana na matatizo mara kumi ya alipotoka hivyo ndoa hiyo ilimshinda ndani ya siku sabini na kitu  na kuamua kuachana naye.

Wastara alizidi kuelezea kuwa baada ya hapo Bond alirudi toka reharb akiwa ameachana na tabia zake zile na alijiridhisha kuwa sasa amebadilika hivyo akarudiana naye na wanaendelea kuishi pamoja mpka sasa kama wapenzi. 

Viewing all 104414 articles
Browse latest View live




Latest Images