Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104701 articles
Browse latest View live

Kutana na Baba Pamoja na Bintiye Wanaotamba Mitandaoni Kwa Kuonyeshana Mahaba Yanayohanikizwa na Urefu wa Nywele Zao za Asili..!!!

$
0
0



NI mwimbaji anayekuja juu, mwandishi wa nyimbo, mwanamitindo na baba wa aina yake, ambaye ni mkazi wa New York na Los Angeles nchini Marekani.

Baba huyu wa mtoto mmoja, Benny Harlem, kwa kipindi kifupi ameweza kuiteka mitandao kama vile Instagram, shukrani zikiendea aina ya nywele zake, kujivunia rangi ya ngozi yake nyeusi sambamba na bintiye mpendwa.

Harlem na bintiye mwenye umri wa miaka sita, Jaxyn daima wameonekana pamoja katika mitandao ya kijamii na hivyo kuwa kivutio kikubwa kwa wengi kwa namna ya mitindo yao inayoendana.

Ni hali iliyowafanya wajichotee mamia kwa maelfu ya wafuasi kutokana na haiba yao hiyo na kuonekana kana kwamba hawatenganishwi angalau kwa sekunde moja.

Jarida la Paper liliwahi kuzungumza naye kuhusu mvuto wao katika intaneti, wanavyolinda mwonekano wa misuli na ukakamavu wake pamoja na weusi wa ngozi yake katika Marekani ya leo na siri ya mafanikio ya nywele zake.

Baba huyu anasema hupenda kuonesha mfano mkubwa kwa msichana wake mdogo katika masuala ya kujiamini na kukumbatia asili yake.

Aidha, kutokana na uzoefu wake wa malezi aliyopitia nyuma, anataka kuelimisha jamii kwa vitendo hasa kwa wababa wenzake kuwapenda watoto wao na kuwapa mwongozo utakaowasaidia maishani.

Benny anasema kazi yake kama mzazi ni kumlinda na kumkuza mtoto wake huku akiwa na matumaini kuwa Jaxyn atakuwa msichana mwenye nguvu na kujiamini.

“Binti yangu ni mzuri na ninatarajia atakuwa mwanamke mrembo, lakini namfundisha ajipende yeye kwanza. Haelekezi macho kwa wanaume, au kuangalia televisheni au marafiki zake.”

Dogo Jaxyn anaonekana kuwa na imani na daima mwenye furaha kwa rangi ya ngozi yake, hivyo huwezi kukana kuwa babake anafanya vyema katika kazi yake ya uanamitindo.

Kuhusu siri ya nywele zao, anasema wanaziosha kila wiki, wanatengeneza shampoo na vitu kama hivyo kwa kutumia viungo vya asili kama vile mafuta ya nazi na kadhalika na kuwa hakuna kitu kikubwa zaidi ya hilo na matunzo mazuri.

Anasema binti yake Jaxyn anakumbana na wakati mgumu awapo shule, ambako wasichana hujaribu kuzishika nywele zake.

Kwa vile nyumba ameweka sheria ya kutoruhusu yeyote kugusa nywele zao, bintiye huyo anaendeleza utaratibu huo awapo shuleni, kitu ambacho mara nyingi ni changamoto mno kukizuia.

Anasema; “Watu wanatutazama na  kutuuliza iwapo kweli ni nywele zetu hasa zangu ni za asili au za kupandikiza. Jibu tunalowapa ni ndio. Kwa kweli wengi wameondokea kuzipenda pamoja na kuwa kuna wachache walio kinyume na hilo.

“Naona fahari ya kuwa hivi nilivyo.”

Hata hivyo, Harlem hajapitia mapenzi ya ubaba kama anayoonesha kwa bintiye, kiasi cha kuwa mfano kwa wababa wengi wanaomfuatilia mtandaoni.

Benny (27) ambaye alianza kukuza nywele zake tangu akiwa na umri wa miaka 15 anasema: “Binafsi sikuwahi kukutana na baba yangu hadi nilipokuwa na umri wa miaka saba. Wakati huo baba alikuwa kocha wa mpira wa miguu katika shule ya juu ya sekondari, hivyo mimi na familia yangu––yaani mama, shangazi na bibi yangu tulienda uwanjani na kusubiri hadi mpira ulipomalizika. Tuliingia kiwanjani na shangazi yangu akamwambia baba, ‘Hey! huyu ni mwanao.”

“Baba aliniangalia kwa sekunde 10 na kisha akasema, sina mtoto hapo. Ni kauli ninayoikumbuka sana na iliniuma sana kipindi kile” anasema taratibu kwa vituo kila baada ya maneno machache.

Anasema ni alihisi uchungu wa kukataliwa hasa ukiongeza namna alivyokuwa akiingiwa na wivu wa kuwaona watoto wenzake wakiwa wameshikwa mikono na baba zao matembezini na wanapopelekwa au kurudishwa nyumbani kutoka shuleni.

Baadaye, ili kuziba pengo hilo aliamua kuachana na hilo na kukubali hali halisi. “Nilijitegemeza zaidi kwa wanawake, ambao wametawala katika familia yetu. Nilikulia katika mazingira yenye wanawake watupu na mimi nilikuwa mwanaume pekee katika familia yetu licha ya kwamba nilikuwa na wajomba wachache mno.

“Kwa sababu hiyo niliwachukulia kina David Bowie (mwimbaji na mcheza filamu) na Tupac Shakuru (mwanamuziki wa rap ambaye ni marehemu) kama wababa wangu,” anasema Harlem, ambaye hakuna popote katika mitandao anakozungumzia mkewe au rafiki yake wa kike au kwa maneno mengine mama wa bintiye Jaxyn .

Wema Sepetu Afunguka Mazito Baada ya Jana Jina Lake Kuyajwa Kuwa Anahusika na Madawa ya Kulevya..!!!

$
0
0

Staa huyo ametoa kauli hiyo baada ya kuwepo kwenye orodha ya mastaa wanaotuhumiwa kubwia unga na walioamriwa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda kujisalimisha kituo cha polisi central jijini Dar, Ijumaa hii kwa mahojiano zaidi.

“Mimi kama Wema nimekuwa nikisemwa sana kuhusu kujihusisha na utumiaji wa madawa ya kulevya na hata kujihusisha katika kuuza madawa ya kulevya,” amesema Wema kupitia app yake.

“Sometimes wanasema nimefungwa, sometimes nimenyongwa, sometimes nimekamatwa hususan pindi ninaposafiri kwenda nchi mbalimbali, na sasa hivi nimeambiwa kwamba natumia madawa ya kulevya. Well, ni habari ambazo mheshimiwa mkuu wa mkoa amesema hana uthibitisho nazo lakini amelazimu kutaja majina kadha wa kadha ambayo ndio hivyo ameyataja mengine kwenye vyombo vya habari, na ameamuru twende tukaripoti kesho (leo Feb 3), ifikapo saa tano asubuhi,” ameongeza.

“Mi nasema hivi, nitaenda, nitaripoti, kwasababu ni wito ambao ametaja mkuu wa mkoa wangu kuona amefanya, unaambiwa kubali wito, usikatae neno. Kwahiyo tutaenda kesho, na ntamsikiliza yale ambayo anataka kuniambia, iwapo tukishajua which is true, which is not, then tutajua from there what to do, sasa hivi sina cha kusema, sina cha kufanya, because bado sijaonana naye, kwa sasa niacheni tu nirelat but I want to assure you one thing, I am not a drug addict, and I am not a drug abuser, and if I was nadhani we all know how drug addicts act, we all know how drug abusers wanakuwaga. I want you guys to relax, do not worry, everything is going to be fine.”

Mastaa wengine waliotajwa ni TID, Mr Blue, Chidi Benz, Recho na wengine.

Video: Makonda Atangaza Majina Mapya ya Watuhumiwa wa Dawa za Kulevya Wapo Askari 3 na Vanessa Mdee Ndani..!!!

$
0
0

Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Paul Makonda amemkabidhi Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Kamishna Simon Sirro majina mapya ya watu wanaotuhumiwa kuhusika kwenye mtandao wa biashara ya Madawa ya kulevya ambapo katika majina hayo wako askari 3, msanii wa muziki Vanessa Mdee pamoja na video queen ambaye pia alikuwa mpenzi wa rapper Young Dee, Tunda.

Aidha RC Makonda amesema wale walioitwa leo kituoni hapo bado wanaendelea kufanya nao mahojiano na kama kuna yeyote atakayekutwa na hatia sheria itachukua mkondo wake.

Akizungumza na waandishi wa habari Ijumaa hii, RC Makonda aliliagiza jeshi la polisi kuwakama wale ambao hawajaripoti leo kama walivyoagizwa jana huku akiwataka wale waliotajwa leo kuwasili Kituo Kikuu cha Polisi Dar es salaam Jumatatu.

Serikali Yatoa Kauli Juu ya Ulipaji wa Madeni ya Walimu..!!!

$
0
0

Serikali imesema kuwa suala la uhakiki wa madeni kwa walimu limekwisha ambalo lilikuwa changamoto sasa walimu hao wataanza kulipwa muda si mrefu.

Hayo yamesema Ijumaa hii mjini Dodoma na Naibu Waziri Ofisi ya Rais, Tamisemi, Utumishi na Utawala Bora, Selemani Jafo, kwa niaba ya Waziri wa TAMISEMI, alipokuwa akijibu swali la mbunge Benadeta Mshashu lililohoji, Je, serikali italipa lini madeni ya walimu? sambamba na mbunge huyo akitaka kutajiwa tarehe.

“Kama nilivyosema awali kwanza tuweke reference vizuri hapa na kumbukumbu vizuri katika kada ambayo serikali katika njia moja au nyingine imekuwa ikishiriki vizuri katika ulipaji wa madeni ni kada ya walimu. Ukiangalia miaka mitatu mfululizo trend ya madeni ya walimu tumekuwa tukizungumza hapa katika Bunge kila wakati, kwa kweli serikali inafanya kazi sana na ndio maana hata kwa kipindi cha sasa ukiangalia mwezi wa 11 huu uliopita kuna baadhi ya madeni ya walimu katika baadhi ya wilaya kwa mfano kuna halmashauri ya Temeke na halmashauri zingine kulikuwa na deni kama la bilioni 1 nalo lililipwa vilevile,” amesema waziri Jafo.

Ameongeza “Maana katika ulipaji wa madeni haya, haya madeni mapya mengine na ndio maana serikali ilikuwa inafanya zoezi hili zima la uhakika vizuri, ofisi ya TAMISEMI pamoja na HAZINA jambo hili limekamilika siwezi sema deadline lini hilo deni litalipwa, lakini kwasababu mchakato wa uhakiki umekamilika hili deni la shilingi bilioni 26 naamini muda si mrefu Hazina mchakato wa malipo utaanza kuanza. Naomba nikwambie mheshimiwa mbunge najua uko makini katika hili lakini amini serikali yako kwamba kwa vile zoezi la uhakiki lililokuwa changamoto limekamilika basi walimu hao wataanza kulipwa muda si mrefu.”

Wagonjwa 50,000 wa Saratani Hugundulika kila Mwaka

$
0
0

Takwimu zinaonesha kuwa kila mwaka duniani kote kunatokea wagonjwa wapya wa saratani wanaokadiriwa kufikia milioni 14.1, na kati ya hao zaidi ya wagonjwa milioni 8.2 hufariki dunia kutokana na ugonjwa wa saratani.

Takwimu hizo ni kwa mujibu wa Shirika za Kimataifa la Atomiki la Utafiti wa Saratani (IARC) na Shirika la Afya Duniani ambazo zimetolewa leo mjini Dodoma na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee, Watoto Mhe. Ummy Mwalimu ikiwa kesho ni siku ya Saratani Duniani na kusema kuwa kwa Tanzania tatizo la saratani limekuwa likiongezeka na kukua kila mwaka.

Amesema nchini Tanzania kila mwaka wagonjwa wapya wapatao 50,000 hugundulika na saratani za aina mbalimbali na kati ya hao ni wagonjwa 5,000 sawa na asilimia 10 ya wagonjwa wote ndiyo wanaofanikiwa kufika katika Taasisi ya Saratani ya Ocean Road ili kuweza kupata tiba, huku asilimia 70 ya wagonjwa wanaobahatika kufika katika taasisi hiyo na kupata huduma za tiba hufika wakiwa katika hatua za mwisho za ugonjwa.

Amesema tayari serikali imetoa shilingi bilioni tano kwa ajili ya ununuzi wa mashine mpya za mionzi ambazo zitasaidia kutibu wagonjwa wa saratani.

Fahamu Njia Tano Muhimu Zitakazo kusaidia Kumpa Mke Wako Ujauzito wa Mtoto wa Kiume..!!!

$
0
0

Uzazi wa mpango una mambo mengi sana.. sio kuzuia mimba tu ndio uzazi wa mpango ila hata kupanga idadi na jinsia za watoto ni moja ya njia za uzazi wa mpango..

Watu wengi wamekua wakitamani jinsia flani za watoto ili wazae watoto wachache ila kukosa kwa jinsia waliyoipanga hujikuta wakizaa watoto wengi wakati wakitafuta jinsia husika, mpaka familia hugombana na kutengana kwa sababu hizi.

Mara nyingi wazazi wa kiume hufikia hatua ya kuvunja ndoa kabisa hasa wanapokosa watoto wa kiume.

Leo ntamaliza kitendawili hiki kwa kutoa njia ambazo zinaweza kufanya mtu kupata mtoto wa kiume kwa asilimia nyingi…

Kitaalamu mbegu  zinazotoa mtoto wa kiume XY huenda kwa mwendo mkali sana kwenda kwenye mfuko wa uzazi lakini hufa haraka. lakini mbegu zinazotoa mtoto wa kike XX husafiri taratibu na huchelewa kufika na kufa  ndani ya mfuko wa uzazi kwani mbegu hizi huweza kuvumilia hali mbaya ya kimazingira ndani ya mfuko wa uzazi wa mwanamke, hivyo njia pekee ya kupata mtoto wa kiume ni kuhakikisha mbegu hizo za kiumeXY zinakutana na mayai ya kike kwenye mfuko wa uzazi haraka kabla ya kufa..

Zifuatazo ni njia hizo tano kali…

1.       Hakikisha unashiriki tendo la ndoa siku mayai ya mwanamke yanapokua yameshuka{ovulation}

  Ukishiriki tendo la ndoa siku hii ambayo yai linakua limeshuka    mbegu za kiume huweza kufika mapema na kujiunga na mayai ya kike  na kutengeneza mtoto{fertilization}hii ni siku ya 14 KABLA YA KUONA DAMU YA MWEZI UNAOFUATA SIO BAADA YA KUONA SIKU ZAKO..
                     Kama wewe mwanamke hujui siku yako ya ovulation fanya hivi.

 Pima joto lako la mwili: nunua kipima joto[thermometer} na kisha pima joto lako kila asubuhi , siku ukiona joto lako limeongezeka kidogo ujue umeanza ovulation na hiyo ndio siku muhimu ya kutafuta mtoto..

      Angalia maji maji ya uke: kawaida maji ya uke hua mazito na kuvutika kama maji ya mayai mabichi wakati mwanamke anapoanza ovulation..

2.       Wewe mwanaume ongeza idadi ya mbegu zako..{sperm count}

Mwanaume anatakiwa aongeze wingi wa mbegu zake hasa kwa kukaa siku mbili mpaka tano bila kushiriki tendo la ndoa wakati akisubiri mwanamke wake aanze ovulation.
Njia zingine za kuongeza mbegu ni

      a) weka korodani kwenye hali ya ubaridi:

  kawaida korodani hutengeneza mbegu nyingi wakati wa hali ya ubaridi kuliko joto  hivyo mwanaume anatakiwa kuepuka kuvaa nguo zilizobana sana, na  kuwekalaptop kwenye mapaja

   b) acha kuvuta sigara na kunywa pombe:wanaume wanaokunywa pombe na kuvuta sigara hua na mbegu kidogo sawasawa na wavutaji wa bangi..
 matumizi ya dawa za cancer pia husababisha uzalishaji wa mbegu kidogo sana.

3. Tumia style za ngono ambazo zinahamasisha muingilio mkubwa{deep penetration}

Hii huzipa faida mbegu za mtoto wa kiume{XY} kufika haraka na kufanya fertilization na upande mwingine, muingiliano mdogo{shallow penetration}husababisha mbegu kumwagwa mbali na mlango wa mfuko wa uzazi hivyo mbegu huweza kukutana na hali ya tindikali kwenye uke hivyo mbegu za mtoto wa kiume  kufa haraka na kuziacha mbegu zinazotoa mtoto wa kike.{XX}.

4. Hakikisha mwanamke anafika kileleni:

Mwanamke anapofika kileleni hutoa maji mengi ukeni ambayo hupunguza wingi wa tindikali ambayo ni adui wa mbegu  zote hasa mbegu za mtoto wa kiume XY ambazo hua haziwezi kuvumilia hali ngumu ya kimazingira.

5. Usifanye tendo la ndoa kabla na baada ya ovulation;

Kabla ya ovulation mbegu za mtoto wa kiume XY hufika haraka kwenye mfuko wa uzazi  kama kawaida na kukuta mayai ya mwanamke hayajafika na kufa vivo hivyo baada ya ovulation..
                     

Umeathirika na Punyeto Kiasi Huwezi Kufurahia 'Mechi',Usiogope Hii Itakusaidia kwa Haraka Mno,Ijaribu Leo...!!!

$
0
0

Karibuni ndugu wasomaji katika blog yetu katika muendelezo huu wa makala za kutujenga kiafya..makala mbili zilizopita niliongelea kuhusu madhara na jinsi ya kuacha punyeto, nilipokea simu nyingi sana za watu waliokiri wameathirika sana na tatizo hilo na wakataka kujua jinsi gani wataondokana na adha hiyo… 

Wengine niliwapa ushauri tu na wengine niliwapa matibabu ya chakula, mazoezi na dawa na kwa sasa wananipigia na kukiri kwamba wameacha punyeto na kupona kabisa madhara ya kupungukiwa nguvu za kiume yaliokua yakiwasumbua kutokana na tabia hiyo.

Hiyo ni furaha kwangu kuona kwamba kazi nayofanya inasaidia watu na nguvu zangu hazipotei bure, na ninamshukuru mungu sana kwa hilo. Leo ntaongelea matibabu ya nguvu za kiume kwa watu walioathirika na punyeto ili na wengine ambao hawakupata matibabu yangu wafaidike kama ifuatavyo.

Hakikisha umeacha punyeto kabisa: ili upone tatizo hili hutakiwi kua mtu wa kubadilika mawazo hovyo, kama umeamua kuacha basi acha kabisa na futa kichwani kwako. Jisemee moyoni kwamba mimi Fulani nimeacha tabia hii na sitarudi nyuma. Kama wewe ni mtu wa imani shika kitabu kitakatifu kabisa kulingana na imani yako.

Amsha mfumo wako wa fahamu na mzunguko wa damu sehemu za siri; hii tunaiita booster, kuna virutubisho tunatoa kwa mwezi mmoja ili kushtua nguvu za kiume zilizokua zimepungua kwa kuongeza msukumo wa damu nyingi kwenda sehemu za siri, kuongeza stamina, mbegu na nguvu za kiume maradufu kutokana na madhara haya ya punyeto kisha ataendelea staili ya maisha safi yaani chakula kinachoongeza nguvu za kiume kama karanga, korosho, kitunguu swaumu na ndizi mbivu, mazoezi angalau kuruka kamba na kukimbia mara tatu au nne kwa wiki na kua sawa kama zamani.. virutubisho hivyo ni vya asili havina kemikali hata kidogo.{unaweza kuwasiliana na mimi kwa namba yangu hapo chini kupata dawa hii  kama unahitaji, dozi ya mwezi mmoja bei yake 65000 ikiwa na tembe 60}.

Mazoezi: kama wewe ni mtu unayeishi bila mazoezi kabisa hutaweza kurudisha nguvu hizo, hivyo unahitaji kufanya mazoezi yeyote angalau nusu saa kwa siku. Inaweza kua kuruka kamba, push ups, kukimbia, kuogelea na kadhalika. Mazoezi haya ndio yanayofanya mzunguko wa damu ue mzuri na wewe usimamishe uume vizuri. Onyo: mazoezi yasiwe makali sana kwani yatakumaliza nguvu za kiume.

Kula chakula bora cha asili; vyakula vya viwandani vina kemikali nyingi sana na ndio vyakula vinaliwa sana kwenye kizazi chetu hichi cha sasa hivi ndio maana shida hizi zamani hazikuwepo ila siku hizi hata kijana mdogo analalamika kuishiwa nguvu za kiume. Kula ugali, maharage, viazi, maziwa mgando, karanga, korosho, mihogo na vyakula vyote vya asili unavyofahamu ila punguza ulaji wa nyama kwani hauna matokeo mazuri kwenye tiba hii.

Kunywa maji mengi sana; kusimama vizuri kwa uume kunategemea sana mzunguko mzuri wa damu mwilini hivyo kama mwili una maji mengi ni rahisi damu kwenda vizuri kwenye uume. Nikukumbushe kwamba ni wingi wa damu unaopelekwa sehemu za siri zako na kufanya uume wako usimame vizuri.. pia mwili unatoa kipaumbele vya damu nyingi kwa viungo vinavyotupa uhai kwanza kwa maana nyingine damu yako haiwezi kuacha kwenda kwenye ubongo, figo na moyo kwanza afu iende kwenye uume. Upe mwili sababu za kupeleka damu ya ziada kwenye uume wako kwa kunywa maji mengi

Pamoja na Jitihada Zote Aanzofanya,Wabunge Wamchambua na Kumshutumu Makonda kwa Haya..!!!!

$
0
0

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa imewashukia baadhi ya wakuu wa mikoa na wilaya ikisema wanatumia vibaya mamlaka waliyopewa kwa kuamrisha watumishi wa umma kuwekwa ndani kwa makosa yasiyostahili adhabu hiyo.

Akisoma taarifa ya shughuli za kamati hiyo kwa mwaka 2016/17, mjumbe wa kamati Ester Mahawe alisema, “Ipo mifano kadhaa ikiwa ni pamoja na mkuu wa mkoa mmojawapo nchini aliamuru daktari wa mkoa wake awekwe  rumande kwa sababu hakutangaza kuwapo kwa ugonjwa wa kipindupindu.”

Bila kutaja majina, alitoa mfano mwingine wa mkuu wa wilaya moja ya Mkoa wa Dar es Salaam aliyeamuru watumishi waliochelewa kazini wawekwe ndani na mwingine wa Mkoa wa Arusha aliyeamuru mwandishi wa habari wa kituo cha televisheni nchini awekwe ndani kwa kuandika habari kuhusu kero ya ukosefu wa maji, ambayo mkuu huyo wa wilaya alitafsiri kuwa ni uchochezi.

Mahawe alitoa mfano mwingine kuwa ni mkurugenzi wa halmashauri aliyeamuru mwalimu wa sekondari kudeki darasa mbele ya wanafunzi kwa sababu ni chafu.

“Mkuu wa mkoa kutumia lugha zisizofaa kwa watumishi kuwa ni wezi, wajinga wasiokuwa na akili timamu, hawa ndio vichaa tunaohangaika nao ni kudhalilisha utu wa mtu na kuvunja misingi ya Katiba,” alisema.

Alitoa ufafanuzi akisema Sheria ya Tawala za Mikoa ya mwaka 1997 sura ya 97 imeweka masharti muhimu kwa mkuu wa mkoa na wilaya ikiwa atahitaji kutumia mamlaka ya kuamrisha mtu akamatwe.

“Vifungu hivyo vinaeleza kwamba, itafanya hivyo pale tu ambako atakuwa amejihakikishia kuwa kosa lililotendwa na mhusika athari yake huwa ni kukamatwa na kushtakiwa,” alisema.

Alitaka viongozi wote na wabunge kuzingatia sheria, kanuni, miongozo na utaratibu uliopo na kwamba, kinyume na hapo watakuwa wameshindwa kutimiza wajibu wa kuwa mfano kwa wanaowaongoza.

Mbali na kamati, wabunge waliochangia mjadala wa taarifa hiyo walisema mambo yanayofanyika ni matumizi mabaya ya madaraka ya mamlaka waliyopewa.

Mbunge wa Kinondoni (CUF), Maulid Mtulia alisema watendaji wa Serikali wanashindwa kuelewa kauli zinazotolewa na Rais, jambo linalowafanya watekeleze maagizo tofauti na dhamira yake.

Mtulia, akitoa mfano wa kauli ya kutaka vyombo vya usafiri vitakavyopita katika barabara za mabasi ya mwendo kasi jijini Dar es Salaam kung’olewa matairi, alisema watendaji hawakumwelewa Rais kuwa alikuwa akimaanisha wachukuliwe hatua za kisheria.

 Mbunge wa Ukonga (Chadema), Mwita Waitara alimpongeza Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni kwa utaratibu alioufanya baada ya wilaya yake kutofanya vizuri kwenye mitihani ya kidato cha nne ya mwaka jana.

“Naomba tumpongeze DC wa Kigamboni (Hashim Mgandilwa) kwa hatua aliyoichukua ya kuitisha kikao cha idara husika na kuwapa nafasi ya kufanya utafiti kabla ya kuchukua hatua,” alisema Waitara.

Hata hivyo, aliwashutumu wakuu wa mikoa ya Dar es Salaam na Simiyu kwa kuwaweka ndani na kuwadhalilisha watendaji wanaokwenda kinyume na wanachotaka.

Mbunge wa Muheza (CCM), Adadi  Rajab alisema dhana ya madaraka kwa baadhi ya viongozi inakwenda vibaya na kwamba kuna haja ya kupata elimu.

Mbunge wa Nzega Mjini (CCM), Hussein Bashe alitaka Serikali kujenga uwezo wa taasisi badala ya kutegemea mtu ili kipindi chake cha uongozi kitakapopita taasisi iendelee.

Unakumbuka Ile Issue ya Wanajeshi Kumuua Kondakta Kwa Kipigo,Sasa Serikali Imechukua Hatua Hii Dhidi Yao..!!

$
0
0

ASKARI wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), Sajini John Komba na wenzake wanne wakiwemo mgambo na wanafunzi wa jijini hapa, wamefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Tanga kwa kosa la kusababisha kifo cha aliyekuwa kondakta wa daladala inayosafiri kati ya Nguvumali na Raskazoni, Salim Kassim (18) mkazi wa Mwamboni.

Wakili wa Serikali, Donata Kazungu akisoma shitaka hilo la mauaji linalowakabili watuhumiwa hao mbele ya Hakimu Mkazi Mfawidhi, Hilda Lyatuu alisema Januari 26, mwaka huu katika Kambi ya JWTZ iliyoko Kata ya Nguvumali jijini Tanga, Komba mwenye namba MT 69500 na wenzake watatu walimuua Kassim katika eneo la kambi hiyo.

Wakili Kazungu aliwataja washtakiwa wengine katika kesi hiyo ni Adam Juma (20), Sofia John (20) ambao ni mwanafunzi, Yohana Warioba na Bernard Nicholaus ambao ni wanamgambo wanaolinda katika kambi hiyo.

Hata hivyo, watuhumiwa hao hawakutakiwa kujibu chochote kutokana na mahakama hiyo kutokuwa na mamlaka ya kusikiliza kesi za mauaji. Aidha, upelelezi kuhusu kesi hiyo haujakamilika na hivyo itatajwa tena Februari 26, mwaka huu.

Tundaman Kayaandika Haya Baada ya ‘Tunda’ Kutajwa Kwenye List ya Makonda

$
0
0
Tunda Man ni msanii wa bongofleva ambaye makazi yake ni Dar es salaam ambapo February 3 2017 Mkuu wa mkoa Dar es salaam Paul Makonda alizungumza kwenye makao ya Polisi kituo cha kati na kusema miongoni mwa watu atakaowahitaji wakamuone Jumatatu kwa ishu ya dawa za kulevya ni pamoja na Tunda.

Kwa sababu mkuu wa mkoa hakutumia majina halisi ya kuzaliwa, watu mbalimbali walianza kumpigia simu msanii Tunda Man baada ya kuambiwa jina lililotajwa na Makonda ni Tunda.

Baada ya simu za kutosha Tunda Man aliamua kuandika Instagram kwamba sio yeye aliyetajwa bali aliyetajwa ndio huyo kwenye picha, akaambatanisha na picha ya Mrembo Tunda ambaye ameonekana kama video queen kwenye video za bongofleva.

Tundaman aliandika
‘Jamani Tunda aliyetajwa na Muheshimiwa @PaulMakonda ni huyu na sio mie maana simu zimekua nyingi, @Sudibrown na wewe hujui au umeamua kunipigia tu…

Wakuu wa Shule na Wakurugenzi Dar Watakiwa Kutoa Sababu za Shule Zao Kufeli..!!

$
0
0

Kufuatia Dar es Salaam kufanya vibaya katika mtihani wa kidato cha nne kwa mwaka 2016 kwa kuingiza shule 6 kati ya kumi zilizofanya vibaya, ofisi ya Elimu Mkoa imewaagiza wakuu wa shule na wakurugenzi kutoa taarifa za kina juu ya sababu zilizopelekea kufanya vibaya.

Akiongea na TBC, kaimu Afisa elimu mkoa, Janeth Nsunza, alisema bado wanaendelea na kikao kujadili tathmini ya matokeo hayo na wamesema watatoa taarifa kamili watakapomaliza majadiliano.

Alisema, “Kati ya shule 10 ambazo hazikufanya vizuri shule hizo ni Kitonga, Nyeburu, Mbopo, Mbondole, Somangila day na Kidete kufuatia shule hizo sita kutofanya vizuri mkoa wa Dar es Salaam, mkoa umepokea taarifa hizo kwa masikitiko makubwa kwani imekuwa ni kinyume cha matarajio yetu na serikali yetu kwa ujumla.”

“Kwakuwa matokeo yametanganzwA, hatua za kufahamu nini hali hiyo imejitokeza zimechukuliwa mara baada ya matokeo hayo kutangazwa ambapo wahusika wanaendelea kutoa maelezo yao, licha kwa kuwepo kwa viashiria katika mtihani wa Mock na wakurugenzi waliwaelekeza wakuu wa shule hizo kuondoa hali hizo mapema,” aliongeza Nsunza.

Dk Shein Kumbe Naye Anamipasho,Ona Hapa Alivyowapasha Huko Znz..!!!

$
0
0

RAIS wa Zanzibar, Dk Ali Mohamed Shein amesisitiza kauli yake ya kuwataka viongozi na watendaji katika sekta ya umma kuacha kufanya kazi kwa mazoea huku akieleza azma ya serikali ya kuwaongeza mshahara wafanyakazi wa kima cha chini ifikapo Aprili mwaka huu kuwa iko pale pale.

Aliyasema hayo kwenye Ukumbi wa Baraza la Wawakilishi la zamani, Mnazi Mmoja mjini Unguja wakati akifunga semina ya siku moja kwa viongozi na watendaji wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ) kuhusu umuhimu wa takwimu na matumizi yake.

Alisisitiza haja kwa kila kiongozi kuhakikisha anasimamia vyema kazi zake pamoja na kuwasimamia anaowaongoza katika sehemu yake ya kazi pamoja na kufanya kazi kwa bidii na kuachana na kufanya kazi kwa mazoea.

Alisema ni jukumu la kila kiongozi kubadilika katika utendaji wake wa kazi na kuwataka wajitahidi kufanya hivyo licha ya kuwa itachukua muda, lakini aliwasisitiza kuwa si busara kuendelea kufanya kazi kwa mazoea.

Dk Shein alisema moja kati ya tamko la Ilani ya Chama cha ASP katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 1963 ilikuwa ni kuwapa nafasi Waafrika wa Zanzibar kuongoza nchi yao na baada ya Mapinduzi ya Januari 12, 1964 chini ya uongozi wa Mzee Abeid Amani Karume hilo lilifanikiwa kwa kuanzia Wizara ya Afya na kuendelea kwa wizara nyingine ambapo wananchi wa Zanzibar walipata fursa ya kufanya kazi.

Mwanamke Ambae Natarajia Kumuoa Miezi 4 Ijayo Ananisaliti...Ushauri Wahitajika

$
0
0

Habari watanzania wenzangu
Nianze moja kwa moja kuna mkasa umenifika kama mwanaume ninayetarajia kufunga ndoa miezi minne ijayo lakini imetokea sintofahamu kubwa cn kwa mwenzangu kubadilika mm
Nafanya kazi dar na yy mkoani. mwenzangu katokea kubadilika kabisa ni ugomvi usioisha mpaka imefikia hatua tunashindwa kupanga vitu kuhusiana na ndoa yetu. Pia mahari kila kitu nilishatoa na mpaka ss hv pande zote mbili zinaendelea na vikao vy shughuri.

Mabadiliko haya yametokea gafla bila hata kutibuana wala kugombana ila kutokana na upelelezi hakinifu nimekuja kujuwa kaanza mahusiano na jamaa mmoja anafanya naye kazi nimefatilia kupitia system nilizonazo za cm za kila kitu nimejuwa kuwa ananisaliti na mpaka tarehe ya kunisaliti naijuwa kanisaliti tarehe 30 /1/2017 muda wa saa 4 usiku na pia tarehe 31/1/2017 tena kanisaliti muda kuanzia saa 3 usiku kalala kwa hyo jamaa
Imeniumiza sana nikifikiria kwa sasa tulipo hiki kitu kinatokea naumia naenda kazini sio mimi nimejaribu kutaka kuchukua maamuzi mazito moyo unasita najaribu kuuliza watu kupitia indirect way wanajibu inatakiwa kuwa na subira na kuwa na uvumilivu sana ila inauma sana.

Wanandugu naombeni ushauri nifanyeje kuhusiana na hili swala kwani nikiwa peke yangu nawaza sana inanibidi nijichanganye kupiga story kwa sana ili nijisahaulishe lakini jaman naomba ushauri nifanyeje
samahani kama nitakuwa nimewaudhimnisamehe.
Ni mm mwajamii mwenzenu.

Sakata la Unga,Harmorapa Aenda Central Kuhakiki Kama Jina Lake Lipo

$
0
0
Harmorapa ameonesha yeye sio mtu wa mchezomchezo linapokuja suala la afya ya akili na hasa maisha ya vijana wenzake.

Majira ya saa nane maeneo ya centrral police, Harmorapa alionekana kaunta akijaribu kuangalia kama kuna uwezakano wowote ule jina lake likawepo hapo either kama mtumiaji au punda, lakini kwa bahati nzuri anadai halikuwepo.

Akiongea na wahandishi wa habari baada ya kuthibisha jina lake halikuwepo ,Harmorapa amedai alipata maelfu ya sms kutoka kwa mashabiki wake ambao walitaka afatualie suala hilo polisi maana hawako tayari kumuona akipotea kwenye game na hasa kipindi hiki ambacho ameonekana kuziba ombwe la msanii anayetuwakilisha kimataifa.

pia msanii huyo amewaomba wasanii watumie muda mwingi studio na location na wajiatahidi kukaa mbali na maeneo ya Kinondoni hasa wanapokuwa na stress.

By Msaga Sumu

Wimbo Mpya wa Diamond Wazimwa na Wema Sepetu Sakata la Madawa ya Kulevya

$
0
0
Safari hii inaweza ikawa ni bad timing kwa mwanamuziki mashuhuli Africa, diamond platinum, baada ya hivi karibuni kuachia video ya wimbo wake mpya huitwao Marry me aliomshirikisha mwanamuziki Ne-yo kutoka marekani. Video hiyo inasemekana kufanyiwa fitina ya coincidence na mwana dada mwenye mvuto na umaarufu wa aina yake nchini, 

Wema sepetu ambapo scandal inayomkabili kwa sasa kuhusu utumiaji wa madawa ya kulevya kuvuta hisia kwa mashabiki zake na maadui zake, hali ambayo imefanya kila mmoja kuvutiwa na story ya mrembo hyo asiyekaukiwa na drama kuliko habari za msanii yeyote nchini kwa sasa (akiwemo diamond na zari). Wema kwa sasa amekuwa dhahabu kwa waandishi wa habari, 

Kila mtu anataka kuandika habari zake, nadhani ujio wake mpya pamoja na uzinduzi wake wa app yake bila kusahau scandal ya utumiaji madawa ya kulevya, vinatajwa kumuweka msanii huyo kwenye level za juu zaidi kuliko msanii yeyote kwa sasa.
By warumi

Serengeti Boys Yafuzu Kucheza Fainali za U -17 Kwa Bao la Mkono...!!!

$
0
0

Tanzania imefuzu kwa mara ya kwanza kucheza fainali za Mataifa ya Afrika kwa vijana U-17 zitakazofanyika Gabon mwaka huu.

Serengeti Boys ilifuzu baada ya kushinda rufaa yake dhidi ya Congo iliyomchezesha mchezaji aliyezidi umri.

Tanzania itaingia Kundi B ikichukua nafasi ya Congo kundi hilo lina timu za Niger, mabingwa watetezi Mali na Angola.

Timu nne zinazofanikiwa kuingia katika nusu fainali zitafuzu moja kwa moja  Kombe la Dunia la Fifa U17 litalofanyika India baadaye mwaka huu.

Waziri wa Michezo, Nape Nnauye aliandika kwenye akaunti yake ya twiter kuipongeza Serengeti Boys kwa kufikia hatua hiyo.

“Mungu Mkubwa! Tumefuzu kwenye fainali za Afrika chini ya umri wa miaka 17. Nia, uwezo na sababu za kuchukua kombe hili tunazo. Hongera TZ” aliandika Nape.

Miujiza ya Shekh Sharifu Rashid Kutoka Bagamoyo , Anarudisha Mapenzi na Kusafisha Nyota

$
0
0

MIUJIZA YA SHEKH SHARIFU RASHID KUTOKA BAGAMOYO PWANI, (RUDISHA MAHUSIANO YAKO NDANI YA MASAA 48 TU) ASANTE KWA KUENDELEA KUMPIGIA SIMU SHEKH SHARIFU RASHID KWA WALE WENYE MATATIZO NA WALE WANAOTOA SHUKRANI:

SHEKH SHARIFU RASHIDI ni mtaalamu wa tiba mbalimbali za asili, anatumia kitabu cha quran, dawa za asili, dawa za kiarabu na majini, anazo dawa za mapenzi, nguvu za kiume, chango, ngiri maji na n.k, anakuvutia mpenzi alie kuacha au alie mbali, pia anatoa pete za bahati zilizoambatanishwa na jini mali kulingana na nyota yako, anaouwezo mkubwa wa kutumia jina la muhusika kwa kutatua tatizo lako, anaouwezo wa kumrudisha mtu aliepotea kimiujiza, pia anatibu kwa njia ya simu popote ulipo,

WASILIANA NAE KWA SIMU NA WHATSAPP NO: 0718-668347. 0685-224047, 0767-204308 au follow@shekh_sharifu_rashid, Email:shekhsharifurashid@gmail.com

Maneno ya Afande Sele kwa Paul Makonda kuhusu Madawa ya Kulevya

$
0
0
Afande Sele ni miongoni mwa wasanii wa siku nyingi Tanzania ambao wamekua wakifatilia pia na ishu za siasa na mengine yanayoendelea ambapo leo hii ametumia time yake kuandika kwenye Facebook kuhusu ishu ya  dawa za kulevya iliyotangazwa na mkuu wa mkoa Paul Makonda.

Afande ameandika
‘Katika hili sakata la MAPAPA na MAPUNDA ya Unga kama kweli braza Paul yupo serious na sio ‘Matango Pori’kama tulivyoona ktk masakata mengine,huenda hata wale WASAFI wakaonekana wachafu…kila la kheri Mr Paul….RiP Da Amina…wacha parry ianzeee…..’

Pitia Vichwa vya Magazeti ya Leo 4/2/2017..!!!

Diamond Akwama Kurejea na Zari Bongo...!!!

$
0
0

Msanii wa muziki Bongo, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ amewaduwaza ndugu, jamaa na marafiki waliofika kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere kumpokea baada ya kutua kutokea Sauzi akiwa peke yake, tofauti na ilivyotarajiwa kuwa angerejea na mzazi mwenzake, Zarina Hassan ‘Zari’.

Awali zilivuja taarifa kuwa, Diamond amekwenda Sauzi kumchukua Zari na mtoto wao aliyezaliwa hivi karibuni, Nillan ili waje kufanya sherehe kidogo.

Kufuatia taarifa hizo, Jumatatu iliyopita, nyakati za jioni, watu wa karibu na Diamond walifika ‘airport’ kuwapokea lakini kilichowashangaza wengi ni kumuona anatoka mwenyewe na mabegi yake, jambo lililowafanya wahisi kuna kitu.

“Hee, mbona yuko peke yake sasa? Zari na watoto wako wapi sasa? Au wamezinguana?” alisikika akisema mmoja wa akinadada waliokuwa uwanjani hapo.

Mbali na dada huyo, wengi walionekana kunong’ona kuonesha kutoamini wanachokiona na kwa kuwa Diamond alijua kuwa kawaangusha kwa kutokuja na Zari, hakuwa na mbwembwe zaidi ya kwenda kwenye gari lililokuwa limeletwa na kijana aitwaye Q Boy, wakaondoka zao.
Viewing all 104701 articles
Browse latest View live




Latest Images