Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104689 articles
Browse latest View live

Waliopasua Kidato cha Nne Gharama Yake Haikamatiki

$
0
0

“Usione vyaelea vimeundwa.” Huo ni msemo wa wahenga unaomaanisha kila mafanikio yana maandalizi yasiyo ya kubahatisha.

Msemo huo unaendana na kilichotokea katika matokeo ya mtihani wa kidato cha nne yaliyotangazwa wiki hii, ambayo katika shule 10 zilizofanya vizuri hakuna hata moja yenye maandalizi ya lele mama. Shule nyingi kati ya hizo ada zake ni kuanzia Sh8 milioni hadi 10 kwa mwaka.

Uchunguzi  umebaini kuwa shule hizo zote ni zenye majengo mazuri, walimu wazuri na wenye motisha, maabara zilizokamilika, sehemu nzuri za kulala na zinazotoza ada zaidi ya Sh2.5 milioni, mbali ya gharama nyingine za chakula, malazi na vitabu.

Shule 10 zenye watahiniwa zaidi ya 40 zilizoshika nafasi za kwanza ni Feza Boys (Dar es Salaam), St. Francis Girls (Mbeya), Kaizirege (Kagera), Marian Girls (Pwani), Marian Boys (Pwani), St Aloysius  Girls (Pwani), Shamsiye Boys (Dar es Salaam), Anwarite Girls (Moshi), Kifungilo Girls (Lushoto) na Thomas More Mashrina (Dar es Salaam).

Wanafunzi wa Sekondari Kaizirege Junior iliyoshika nafasi ya tatu, kila mmoja analipa Sh2.5 milioni za ada. Malipo hayo kwa baadhi ya shule hayahusishi gharama za malazi, chakula na vitabu.

 Shule ya Wasichana ya St. Francis ili mwanafunzi ajiunge nayo, anatakiwa kulipa Sh2.2 milioni za ada kwa mwaka, huku akitakiwa kulipa katika mikupuo minne mbali na mahitaji mengine.

Mwanafunzi wa Feza Boys ada ni Sh2.9 milioni, lakini ikijumlishwa na gharama za chakula, malazi na vifaa vya masomo, inafika zaidi ya Sh8 milioni.

Kuhusu Thomas More Machrine ada ni Sh3.6 milioni kwa kidato cha nne na cha sita. Hivyo, mwanafunzi akisoma kwa miaka minne anatakiwa kulipa Sh14.4 milioni.

Uchunguzi huo ulibaini mwanafunzi anayesoma shule za Marian Boys na Girls kidato cha kwanza hadi cha nne, anatakiwa kulipa Sh2.8 milioni.

Kwa wanafunzi wanaojiunga na shule hiyo kwa ajili ya kidato cha tano na sita, watalipa Sh2.7 milioni hiyo ina maana watatakiwa kulipa Sh5.4 milioni kwa miaka miwili.

Shule ya Anwarite ya Kilimanjaro ada yake ni Sh1.9 milioni,  hivyo kwa miaka minne mwanafunzi analazimika kulipa Sh7.6 milioni.

Mmoja na viongozi wa shule hizo ambaye hakuwa tayari kutajwa, alisema shule hizo zinatoa elimu bora na mazingira mazuri ya kuishi kwa mwanafunzi, hivyo badala ya kuonekana kero zingepewa ruzuku.

Askari 12 Waliotuhumiwa Kushirikiana na Wauza Unga Wasimamishwa Kazi

$
0
0
Mkuu wa Jeshi la Polisi IGP Ernest Mangu amewasimamisha kazi askari 12 waliotuhumiwa kujihusisha na madawa ya kulevya wakati uchunguzi ukiendelea.

IGP huyo amewaambia wanahabari, Jumamosi hii katika makao makuu ya Polisi huku akisema kuwa Polisi ndiyo chombo kinachoongoza mapambano juu ya madawa hayo, huku akisema kuwa hatua zitachukuliwa dhidi ya askari atakayetuhumiwa.

“Tumeamua kuwasimamisha kazi wote walioguswa moja kwa moja na sakata hili, pia Polisi itachukua hatua madhubuti ikiwemo kuwapeleka mahakamani wasanii waliotuhumiwa,” alisema.

Askari hao ni wale waliotajwa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Paul Makonda siku mbili zilizopita wakati akiwaambia wanahabari juu ya watu wanaotuhumiwa kujihusisha na biashara na matumizi ya madawa hayo.

Wasafi Hawaponi Sakata la Dawa za Kulevya- Afande

$
0
0
Baada ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam kutaja majina ya kadhaa ya wasanii na polisi mbalimbali ambao wanajihusisha huku wengine wakituhumiwa na matumizi na uuzaji wa madawa ya kulevya.


Afande Sele amefunguka na kusema kama jambo hili litafanywa kwa haki na umakini basi huenda hata wale wasafi wakaonekana  ni wachafu.

Afande Sele ameonyesha wasiwasi juu ya sakata hili la madawa ya kulevya ila amesisitiza kuwa kama kweli litafanyikwa kazi kwa umakini mkubwa basi kuna kundi kubwa la watu ambao wanaonekana ni wasafi kuchafuka kutokana na sakata hili.

"Katika hili sakata la MAPAPA na MAPUNDA ya unga kama kweli braza Paul yupo 'serious' na sio 'Matango Pori'kama tulivyoona katika masakata mengine, huenda hata wale WASAFI wakaonekana wachafu...kila la kheri Mr Paul....RiP dada Amina...wacha party ianzeee" aliandika Afande Sele 
Kauli hii ya Afande Sele imekuwa ni kauli tata na imeibuka mjadala kwa baadhi ya mashabiki katika kuitafsiri wengine wakisema Afande Sele amezungumzia wasanii ambao wapo chini ya label ya WCB Wasafi chini ya Diamond Platnumz huku wengine wakisema amezungumzia watu ambao wanaonekana ni wema katika jamiii kumbe si wema bali ni wachafu kwa matendo yao kwa kujihusisha na biashara za dawa za kulevya.

‘Aliyemwaga Mboga’ Mbele ya JPM Atiliwa Shaka..!!!

$
0
0

TAHARUKI iliyojitokeza juzi mbele ya Rais John Magufuli, kwa mkazi wa Tanga, Swabaha Shosi kudai kudhulumiwa mirathi ya mumewe, imeibua sintofahamu mpya baada ya waliojiita familia ya huyo mume, kujitokeza na kutangaza kutomtambua Swabaha.

Akizungumza jana Tanga na mwandishi , mwanafamilia aliyejitambulisha kuwa mtoto katika familia hiyo, Saburia Mohamed (37), alidai mara ya kwanza kumwona Swabaha, ilikuwa siku ya kumaliza msiba wa baba yake.

Juzi katika kilele cha Siku ya Sheria, Swabaha huku akilia mbele ya Rais Magufuli na uongozi wa juu wa Mahakama na Polisi, alidai kunyimwa haki ya mirathi ya mumewe na vyombo vya kutoa haki nchini.

Swabaha ambaye alifanikiwa kugonga vichwa vya habari juzi na jana, alitaja vyombo vilivyomnyima haki kuwa ni Polisi, Mahakama, Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashitaka (DPP) na Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG).

Lakini jana Saburia, aliyejitambulisha kwa mwandishi wa gazeti hili kama mwanafamilia, alidai kutomtambua na kueleza kuwa siku ya kwanza kumwona, ilikuwa ya kumaliza msiba wa baba yao.

Saburia alidai kuwa siku hiyo Swabaha alitambulishwa kama binamu yao kwa shangazi yao aliyeko Mombasa na alikuwa akitoka eda Dar es Salaam baada ya kufiwa na mumewe.  

"Yule mama sisi kwa mara ya kwanza tulitambulishwa siku ya kumaliza msiba wa baba yetu tukiwa kwenye kikao cha familia, alifika saa sita mchana, tukaambiwa kuwa ni mjomba wa marehemu baba na ametoka eda Dar es Salaam ya aliyekuwa mumewe naye alithibitisha hilo," alidai.

Hata hivyo, Saburia alidai kuwa wakili wa familia alipokuwa akisoma wosia wa marehemu, Swabaha alimnyang'anya wosia huo na kukimbia nao baada ya kuona jina lake halimo.

Mtoto huyo alidai kuwa mwaka 2012 ilifunguliwa kesi ambayo ilimalizika kwa kufutwa Desemba 15, mwaka juzi na mwaka huo huo familia ilipeleka maombi Mahakama ya Mwanzo, kumpendekeza Saburia awe msimamizi wa mirathi.

Alidai kabla ya kupewa usimamizi, Swabaha alijitokeza mahakamani na kupinga kwa madai kuwa anayependekezwa kusimamia mirathi hiyo si mtoto halali wa marehemu.

Saburia alidai kuwa mama huyo hakuwa sahihi kupeleka taarifa kwa Rais, kwani kesi yao bado inaendelea Mahakama Kuu, ambako inasikilizwa na Jaji Amour Said Khamis na bado hukumu haijatolewa.

Alidai kuwa yeye na familia yake hawana vitisho vyovyote kwa mama huyo na familia ilipatwa na butwaa aliposema anahitaji ulinzi kwa kuwa anatishwa.

Mtoto huyo alielezea masikitiko yake kuwa ameumia baada ya Swabaha kumtangaza mbele ya Rais kuwa anahusika na uuzaji wa dawa za kulevya, kitu ambacho si kweli na kwamba yuko tayari kufanyiwa uchunguzi wa jambo hilo.

"Mimi ni mfanyabiashara wa nguo na nina duka langu la nguo barabara ya 14, ameniumiza sana pamoja na familia yangu kwa kusema nauza dawa za kulevya. Naomba Serikali iliangalie hili, kwani niko tayari kufanyiwa uchunguzi wa tuhuma hizi," alidai.

Mbali na Saburia, mwandishi wa habari hii alizungumza na aliyetambulishwa kuwa mke mkubwa katika familia hiyo, Mariam Juma ambaye alidai kuwa hamfahamu Swabaha.

"Mimi ninamfahamu mama yake ambaye ni wifi yangu na anaishi Mombasa, yeye sijawahi kumwona. Sasa nilishangaa kubadilika na kusema kuwa ni mke wa marehemu na kudai ananyanyasika kwa kudhulumiwa mirathi," alisema Mariam.

Aliitaka Serikali iingilie kati suala hilo ili wapate haki zao yeye na familia yake, ambayo ina watoto tisa na wake wawili.

Juzi Rais Magufuli aliwaagiza Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Mkurugenzi wa Mashitaka, Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini na Mahakama kupitia Jaji Kiongozi, kushughulikia jambo hilo ikiwa ni pamoja na kuhamishia kesi hiyo Mahakama ya Juu ili uamuzi ufanyike.

Pitia Vichwa vya Magazeti ya Leo 5/2/2017..!!!

Ukawa Waunda Kamati ya Uda..!!!

$
0
0

MWENYEKITI wa Chadema, Freeman Mbowe, ameunda kamati ya watu watano kusaka mwafaka wa matumizi ya Sh bilioni 5.8 za uuzwaji wa hisa za Shirika la Usafiri Dar es Salaam (Uda) sambamba na mkakati wa kudumu wa kumaliza tatizo la usafiri Dar es Salaam.

Kamati hiyo iliundwa baada ya kumalizika kwa kikao kati yake na mameya, naibu mameya wa Jiji hilo pamoja na viongozi waandamizi wa vyama vinavyounda Ukawa, kilichofanyika kwenye ofisi za Kambi Rasmi ya Upinzani bungeni.

“Tulikutana si kujadili kiasi hicho cha fedha pekee, bali kutazama wajibu wa mamlaka ya  Jiji la Dar es Salaam kuwa waangalizi namba moja wa mifumo ya usafiri na haki za abiria jijini humo,” alisema Mbowe.

Alitaja wajumbe wa kamati hiyo kuwa ni Meya wa Jiji la Dar es Salaam, Isaya Mwita, Meya wa Ubungo, Boniface Jacob, Mbunge wa Kawe, Halima Mdee, Mbunge wa Kinondoni, Maulid Mtulia  na Naibu Meya wa Ilala.

Hivi karibuni kuliibuka mvutano kati ya Serikali na uongozi wa Jiji hilo linaloongozwa na Ukawa kuhusu kuidhinisha mabilioni hayo ya uuzwaji wa hisa asilimia 51 kati ya 100 kwa kampuni ya Simon Group.

Jumamosi iliyopita, Baraza la Halmashauri ya Jiji hilo chini ya Mwita kwenye kikao chake cha kawaida lilishindwa kufikia mwafaka wa kuzipangia matumizi fedha hizo kwa kilichoelezwa kuwa ni sawa na kubariki ufisadi wa uuzwaji wa hisa hizo ambazo wanaona ni kiasi kidogo.

Kikao hicho kilifanyika kutokana na agizo la Rais John Magufuli Januari 27 wakati akizindua mradi wa mabasi yaendayo haraka.

Katika agizo hilo Rais alitoa siku tano kwa uongozi wa Jiji kuhakikisha kiasi hicho cha fedha kinapangiwa matumizi.

“Tumelitazama hili kwa upana na kwa kina zaidi, tumekubaliana kuunda kamati ya watu watano ambayo itakuwa ikiripoti kwangu, itakwenda kuandaa mpango mkakati wa namna ya kuboresha usafiri wa Dar es Salaam,” alisema Mbowe.

“Mapendekezo ya kamati yakikamilika ndani ya wiki moja au mbili, tutayawasilisha serikalini na imani yetu watayapokea kwani Dar es Salaam ni ya wote, leo inaongozwa na Ukawa sijui kesho itaongozwa na nani. Tunapaswa kuweka kando siasa na kutanguliza maslahi ya Taifa.”

Anne Kilango Aisimulia Siku Aliyotimuliwa Ukuu wa Mkoa..!!!!

$
0
0

Anne Kilango Malecela, ambaye wiki iliyopita aliteuliwa na Rais kuwa mbunge, amezungumzia yaliyomsibu tangu Oktoba 25 mwaka juzi alipopoteza ubunge, kuteuliwa kuwa mkuu wa mkoa kisha kutimuliwa hadi aliporudishwa bungeni, akisema yote yalikuwa mpango wa Mungu.

Kilango, aliyejinasibisha kama mpambanaji wa ufisadi wakati wa Bunge la Tisa, alipoteza ubunge wa Jimbo la Same Mashariki katika Uchaguzi Mkuu uliofanyika Oktoba 25, 2015 baada ya kuliongoza kwa miaka 10.

Miezi mitano baadaye, alifarijika baada ya kuteuliwa na Rais John Magufuli Machi 13 mwaka jana kuwa Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga na kuapishwa siku mbili baadaye.

Lakini, alitumikia wananchi wa mkoa huo kwa siku 27 tu baada ya Rais Magufuli kutengua uteuzi wake Aprili 11 mwaka jana, baada ya Kilango kudaiwa kutoa takwimu za uongo kuhusu idadi ya watumishi hewa. Hata hivyo, baadaye Rais Magufuli akieleza sababu za kutengua uteuzi wake, aliahidi kumpangia kazi nyingine.

“Ndani ya nafsi yangu najua ule ulikuwa mpango wa Mungu,” alisema Kilango katika mahojiano maalumu.

“Wakati mwingine unaweza kuona jambo limekujia baya, kumbe ni Mungu anashusha nusura yake.”

Kilango alisema habari za kushindwa katika uchaguzi, kuteuliwa kuwa mkuu wa mkoa na kutenguliwa, alizipokea kwa kumshukuru Mungu akisema alijua kuna sababu ya hayo kutokea.

“Taarifa za kutenguliwa nilizipokea sawasawa na zile za kuteuliwa. Nilipoteuliwa nilimshukuru Mungu, vilevile, nilipotenguliwa nilimshukuru Mungu kwa sababu niliamini yote yaliyojiri yeye ndiye mhusika mkuu,” alisema.

“Mungu angetaka mpaka leo niwe mbunge wa Same Mashariki ningekuwa, angetaka pia niwe mkuu wa mkoa, Rais Magufuli asingenitengua.”

Historia ya Kweli:Kutana na Jambazi Msomi na Aliyefanikiwa Zaidi Katika Azma Yake..!!!

$
0
0

Mwaka 2021 ulimwengu utashuhudia mmarekani aliyefanikiwa zaidi kutekeleza matukio ya ujambazi akitoka gerezani baada ya kutumikia kifungo cha miaka 17 baada ya kufanikiwa kuishawishi serikali na mahakama kupunguza kifungo chake kutoka miaka mia moja kumi na tano (115) mpaka miaka hiyo 17.

Atakapotoka na kurudi uraiani atakuwa na miaka 69, jina lake anaitwa Carl Gugasian au maarufu kama 'The Friday Night bank robber'! Muhalifu aliyeiumiza kichwa FBI kwa miaka 30 akitekeleza matukio 50 ya kuvamia na kuiba benki pasipo kukamatwa kitendo kilichopelekea FBI na waendesha mashitaka wa marekani 'kumsifu' kuwa ndiye muhalifu mwenye akili na aliyefanikiwa zaidi katika historia ya marekani (the most prolific bank robber)

Kumekuwa na kelele nyingi kutoka kwa 'mashabiki' wakiitaka Hollywood watengeneze muvi kuhusu maisha ya 'the friday night bank robber'!

Jambo lililowashangaza wengi na ulimwengu wote ni jinsi gani binadamu mmoja aliweza kutekeleza matukio 50 ndani ya miaka 30 akiwa peke yake na FBI washindwe kujua identity yake wala kuwa na hata mbinu ya kuweza kumzuia au kumkamata.

Mbinu, weledi na nidhamu aliyokuwa nayo na kutumia kutekeleza matukio yake yalikuwa ni siri na kitendawili mpaka pale alipokamatwa na kuamua kuwasimulia FBI ili kujaribu kuwashawishi kumpunguzia adhabu ya kifungo.. Na hii ni historia yake 'kwa kifupi' tu

ALIWEKA DHAMIRA AWE "MUHALIFU MWELEDI"

Akiwa na miaka 15 Carl alitekeleza tukio lake la kwanza la ujambazi ambapo alijaribu kuiba fedha katika candy store bila mafanikio na alipigwa risasi tumboni na kukamatwa. Baada ya kukamatwa alipelekwa katika jela ya watoto ya Camp Hill kwa miezi 18.

Baada ya kutoka jela Carl alidhamiria sasa kuwa ni lazima awe muhalifu mwenye weledi wa hali ya juu kiasi kwamba atafanikiwa katika kila tukio na hatoweza kukamatwa na akadhamiria kama anataka kufanikiwa aibe fedha nyingi kwa wakati mmoja basi sehemu sahihi ya kuiba ni bank na kama anataka kweli awe muhalifu mweledi anatakiwa ajue namna sehemu hizo (majengo na mifumo) zinavyofanya kazi, afahamu namna ya kutumia silaha, ajue namna ya kujihami (self defense) na namna atakavyo toroka na fedha..

Baada ya kuweka dhamira hiyo Carl akachukua hatua ya kwanza na alichofanya ilikuwa ni kujiunga na Chuo kikuu cha Villanova ambapo alisomea Uhandisi wa umeme. Akiwa chuoni alitumia mwanya huo kujiunga na programu maalum ya jeshi la marekani kwa ajili ya kurecruit vijana walioko chuoni! Baada ya kumaliza Chuo akaenda kutumikia jeshi kwa muda mfupi kituo cha Fort Bragg na akiwa huko akapata mafunzo maalumu ya kijeshi (Special Forces and tactical weapons training)

Baada ya kupata mafunzo ya kijeshi Carl akarudi Chuo kusoma masters degree ya System Analysis na alipomaliza masters degree akafanya mafunzo ya awali kwa ajili ya shahada ya uzamivu katika Statistics.

Pia mtaani alipokuwa anaishi alijiunga na kituo cha kufundisha mafunzo ya kujihami (karate and judo) ambapo alifanikiwa kupata mkanda mweusi (third degree black belt)

Baada ya kufanikiwa kufanya maandalizi yote hayo na kupata kila aina ya mafunzo na uzoefu aliyohitaji ili kuwa 'muhalifu wa daraja la kwanza' sasa ulikuwa ni wakati kwake kupita kila benki kukomba hela na kuudhihirishia ulimwengu kuwa hakujapata kuwepo na itachukua miaka mingi kutokea muhalifu professional kama yeye Carl 'the Friday night bank robber'..

#1: MAANDALIZI KABLA YA TUKIO

Moja kati ya vitu vilivyomsaidia Carl kufanya matukio ya uhalifu kwa mafanikio ni uwezo wake wa kuweka mkakati wa utekelezaji jinsi gani atakavyofanikisha azma yake! Ni dhahiri kuwa mafunzo ya kijeshi aliyoyapata yalimsaidia sana kuwa mwanamkakati mzuri wa kiufundi wa matukio! Carl alikuwa anatumia had I miezi kadhaa katika kupanga utekelezaji wa tukio moja tu..

Kwanza kabisa Carl ali scout bank zilizopo katika miji midogo. Baada ya kupata orodha ya benki katika miji kadhaa midogo then Carl aliangalia kati ya bank hizo ni bank gani haziko katikati ya mji (kwa maana kwamba ziko pembezoni/nje ya mji). Kisha Carl aliichagua bank moja wapo kati ya hizo na bank ambayo inakuwa haiko karibu sana na makazi ya watu au iko karibu na msitu basi bank hiyo anaipa kioaumbele katika orodha yake..

Baada ya kuamua ni bank gani atafanya tukio, Carl alianza tafiti juu ya tukio lenyewe atakavyolitekeleza... Kwanza kabisa Carl alianza kwa kusoma mandhari yanayozunguka bank na interest yake kubwa inaelezwa kuwa alitafiti zaidi msitu ambao unakuwa karibia na bank.. Inaelezwa kuwa Carl angeutembelea msitu huo na kuukagua nukta baada ya nukta, haijalishi ni muda gani angetumia mpaka kumaliza kuukagua!

Inaelezwa kuwa lengo lake lilikuwa ni kujua ni maeneo gani ya msitu ambapo watu huwa wanamazoea ya kupita au kutembelea, ni eneo gani la msitu limejificha zaidi, ni upande gani wa msitu unakuwa rahisi kuifikia barabara, ni eneo gani la msitu lina umajimaji na eneo gani ni kavu na kadhalika na kadhalika.. Inaelezwa kuwa Carl angeutafiti huo msitu na kuufahamu kuliko hata wenyeji wa eneo hilo husika.. Angeufahamu msitu nukta kwa nukta!

Baada ya kuufanyia tafiti msitu, inaelezwa kuwa Carl alikuwa anageukia kuitafiti bank yenyewe na wafanya kazi wake.. Kuhusu bank, angetafiti je hiyo bank inafungwa na kufunguliwa saa ngapi, ni siku zipi huwa wanachelewa kufunga, ni siku gani wanakuwa na kiasi kikubwa cha fedha n.k! Kisha akimaliza hapo anageukia kuwatafiti wafanyakaxi wa bank husika.. Hapa alitafiti kuhusu 'shifti' zao za kazini, nanj ni teller, nani ni manager na pia kitu kingine cha msingi alijitahidi kuwasoma personality zao..

Baada ya kumaliza kufanya 'tafiti' zake Carl alienda hatua ya pili ya maandalizi ambapo ilikuwa ni kuandaa 'makazi na stoo' yake ya muda katika msitu uliopo karibu na bank ambapo alichimba handaki dogo kwa ustadi mkubwa na kulificha kabisa kwa juu mtu asiweze kujua kwa namna yoyote ile.. Moja ya wapelelezi ambao walihusika kufanikisha kumkamata Carl anaeleza Bw. Carr anaeleza kuwa siku ambayo walifanikiwa kugundua na kuliona handani mojawapo ambalo lilichimbbwa na Carl walistaajabu (kumbuka Carl alikuwa na zaidi ya mahandaki 30 sehemu tofauti tofauti za nchi ya marekani)! Inaelezwa kuwa kinachostaajabisha kuhusu mahandaki ya Carl ni jinsi yalivyo chimbwa kiustadi na kujengewa kwa ndani kwa vitofali vidogo vidogo.. Pia handaki lilikuwa linampangilio wa hali ya juu wa kiwango cha kijeshi (military precision). Ndani ya handaki kulikuwa na kila kitu ambacho angekihitaji, silaha, nyaraka za 'research', kifurushi cha kujikimu (survival kit), madawa ya dharura (first aid kit), vinyago vya kuficha sura (masks), fedha taslimu, majarida ya mazoezi ya kawaida na kijeshi na vitu vingine vingi..

Baada ya kumaliza maandalizi haya ya msingi Carl alijichimbia katika maktaba ya umma ya Philadelphia ambapo ndio alipafanya kama ofisi yake kwani inaelezwa kuwa alikuwa na mazoea ya kutumia muda mwingi hapo akifanya 'tafiti' na angekuwa hapo kwa wiki kadhaa ili ku-fainalize mpango wake na kufanya conclusion ya jinsi atakavyotekeleza tukio lenyewe..


#2: UTEKELEZAJI WA TUKIO

Matukio yote ambayo Carl aliyafanya alikuwa anayetekeleza mwezi October au November ambapo maeneo mengi yanakuwa yapo kwenye kipindi cha winter au autumn ambapo kunaambatana na baridi kali pamoja na jua kuzama mapema!

Pia matukio yake yote aliyatekeleza siku ya ijumaa na hii ndio iliyomfanya apewe jina la 'The Friday Night bank robber'..

Uchaguzi wake wa muda wa kufanya tukio ulimpa advantage kadhaa.. Kwanza kipindi cha winter na autumn jua linazama mapema kwa maana ya kwamba katika Masaa yale yale ambayo bank zinakuwa zinafungwa lakini katika kipindi hiki cha majira ya mwaka giza linakuwa limeanza kuingia hivyo inampa mwanya mzuri kufanya tukio.. Pia kufanya tukio ijumaa ilimaanisha kuwa ndio siku nzuri kwa bank kuwa na kiwango kikubwa cha Cash.. Lakini pia alitumia sababu ya kisaikolojia kuwa ijumaa wafanyakazi wanakuwa distracted kutokana na weekend kuanza hivyo umakini unakuwa mdogo..

Kwahiyo alichokifanya Carl kwanza ni kupaka 'harufu' kwenye nyumba zote zilizo karibu na bank ili kuwachanganya mbwa wa polisi wakija kujaribu kutafuta trail ya alikoelekea!

Now; siku ambayo Carl alikuwa anafanya tukio alivaa kinyago cha kutisha usoni ambacho kili-fit sawa sawa kabisa ili kuficha ngozi yake na! Pia alivaa manguo mengi ili kuleta muonekano kwamba ni mnene.. Na alikuwa akiingia ndani ya bank alitembea dizaini kama amechuchumaa mfano wa Kaa (crab)! Vitu vyote hivi alivyovifanya watu walihisi labda alikuwa na matatizo ya akili lakini hawakujua kuwa alivifanya kwa kusudi kabisa.. Alivaa kinyago cha kutisha ili kuleta effect ya kuogofya na kuficha tone ya ngozi yake, pia alivaa manguo mengi ili kuficha body size, na alitembea kama kaa akiwa kama amechuchumaa ili kuficha height!! Hii ilimsaidia sana kwani kwa miaka 30 FBI walishindwa kung'amua mtu wanayemtafuta alikuwa wa size gani, height gani au skin color ipi???


#3 KUVAMIA
Carl alikuwa anasubiri dakika 5 kabla bank haijafungwa ndipo alikuwa anavamia! Hii ilimpa possibility nzuri kuwa ndani kulikuwa na wafanya kazi pekee au Wateja wachache sana wamebakia..

Akishavamia bank alitoa bastola na kuamuru watu walale chini na wasimuangalie! Mashahidi wanaeleza kuwa kwa ustadi mkubwa (labda kutokana na mazoezi ya karate) Carl aliruka kutoka alipo mpaka kwenye droo za ma-teller na kuweka fedha zote alizozikuta humo kisha kwa ustadi ule ule aliruka tena mpaka upande wa wateja na kuwaamuru tena kwa msisitizo wasimuangalie na kabla hawajang'amua kinachoendelea Carl alikuwa tayari ashatoka nje ya bank na kutokomea katika msitu ulio karibu..

Inaelezwa kuwa katika matukio yake yote aliyatekeleza ndani ya muda usiozidi dakika mbili! Yani chini ya dakika mbili alikuwa tayari amevamia, amekomba hela na ameshatokomea msituni..

Carl anaeleza mwenyewe kuwa akiingia ndani ya msitu alikuwa anakimbia kwa dakika kadhaa kama kumi hivi mpaka mahala ambapo anakuwa ameficha baisikeli kisha anaendesha mpaka ndani ndani kabisa ya msitu kulipo na handaki lake, akifika kwenye handaki kila kitu anakiacha hapo; fedha alizoiba, masks, nguo, gloves etc kisha anavaa nguo nyingine za kawaida anaendesha baisikeli anaondoka! Carl anasema kuwa ataendesha baisikeli kwa muda wa kama dakika ishirini au zaidi mpaka upande wa pili wa msitu ambapo kuna barabara na hapo kunakuwa kuna gari amepaki linamsubiri.. then anawek baisikeli ndani ya gari anaendesha kama raia wa kawaida na kuelekea nyumbani..

Carl anasema alikuwa anacha wiki au miezi ipite mpaka stori kuhusu tukio la ujambazi zianze kufifia ndipo anarudi kwenye ule msitu na kuchukua 'hela zake'... Baada ya hapo maisha yanaendelea na anaanza 'tafiti' kwa ajili ya tukio linalofuata..


#4: KUKAMATWA NA MAZINGAOMBWE YA HUKUMU

Kukamatwa kwa Carl kulikuwa kwa bahati mbaya mno! Kuna watoto walikuwa wanacheza katika msitu uliopo karibu na nyumbani kwao! Wakiwa ndani ya huo msitu waliokota PVC tube/pipe iliyokuwa imefichwa.. Baada ya kuifungua ndani walikuwa ilikuwa na bastola na vitu vingine kadhaa vinavyotia shaka. Wale watoto wakawataarifu wazazi wao na wazazi wao wakashauri vipelekwe polisi! Baada ya vitu hivyo kupelekwa polisi, vikachunguzwa na kukakutwa ramani.. Polisi walipoifuatilia ile ramani ikawqpeleka moja kwa moja kwenye handaki dogo ndani ya msitu! Kutokana na vitu vilivyokutwa ndani ya handaki hilo polisi wakapata wasiwasi kuwa inawezekana wanadeal na ishu serious kuliko uwezo wao hivyo wakawataarifu FBI! Baada ya FBI kuwasili iliwachukua masaa kadhaa tu kung'amua kuwa vitu hivyo vinahusiana moja kwa moja na Jambazi wanayemtafuta kwa miaka 30, The Friday night bank robber.

FBI walitumia alama za vidole walizozikuta kwenye ile handaki na pia walitumia kijarida kidogo kinachohusu kituo cha mafunzo ya karate kumtrack down Carl mpaka wakampata.
Siku Carl anakamatwa alikutwa "ofisini kwake" Maktaba ya Philadelphia Free Library akiwa anafanya "tafiti"

Baada ya kukamatwa na kesi kufikishwa mahakamani ilikuwa ni dhahiri kuwa Carl atahukumiwa kifungo cha maisha au aghalabu miaka 115 pasipo uwezekano wa kupata parole kutokana na mashitaka yanayomkabili lakini mwisho wa siku Carl alikubaliana deal na FBI kuwa awaeleze nukta kwa nukta kuhusu matukio yote 50 aliyoyafanya, pia akubali kushirikiana na FBI kutengeneza programu maalum kuwasaidia maafisa wa FBI kutambua namna ya kuwabaini 'serial criminals', na pia awaelekeze kuhusu saikolojia ya ku-plan matukio ya uhalifu yaliyo perfect.! 

Carl akakubaliana na masharti yote haya na mahakama ikapunguza adhabu yake kutoka kifungo cha maisha mpaka kifungo cha miaka 17 bila parole..

Hivyo basi ikifika 2021 Carl Gugasian anarudi uraiani! Inaelezwa kuwa huko gerezani Carl ni mtu mnyoofu mno na ni mfungwa wa kuigwa na ameendeleza desturi yake ya kupenda mazoezi hivyo yuko katika afya njema sana na wengi wanaamini atafika 2021 akiwa salama salimini na naamini kabisa Hollywood wanaomba usiku na mchana atoke salama ili wamfanye celebrity na watupe bonge la muvi.!!

Mwisho..

Kampuni ya Mo Dewji, Lamada Hotel ni mdaiwa sugu wa kodi.....maofisa Ardhi wavamia ofisi, Watoa Notisi ya Siku 14

$
0
0
Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi imeanza oparesheni maalumu ya kukusanya Kodi ya Pango la Ardhi kutoka kwa wadaiwa sugu wa Makampuni, mashirika ya kiserikali na watu binafsi kwa kuwafuata katika maeneo yao.

Katika hatua ya kwanza Wizara kwa kushirikiana na Manispaa za  mkoa wa Dar es salaam imetoa notisi kwa wadaiwa sugu wa kodi ya pango la Ardhi wakiwemo Mohammed Enterprises anaedaiwa Shilingi milioni 73, Lamada  Hotel anaedaiwa Shilingi milioni 54, Mamlaka ya Maeneo Maalum ya Uzalishaji kwa Mauzo ya Nje (EPZA) anaedaiwa Shilingi milioni 144 na Tanganyika Motors anaedaiwa Shilingi milioni 22.

Makampuni hayo yamepewa notisi ya siku 14 ili kulipa kodi hizo wanazodaiwa na endapo hawatalipa watafutiwa umiliki au mali zao kwa kupigwa mnada ili kufidia gharama wanazo daiwa.

Serikali kwa kutumia kampuni ya Udalali ya Msolopa Investment imeendesha oparesheni hiyo kwa kufika katika ofisi za wamiliki wa viwanja na mashamba makubwa katika maeneo mbalimbali nchini.

Akiongea kwa kusisitiza, Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt. Yamungu Kayandabila amesema katika mwaka wa fedha 2016/17 Wizara imepanga kukusanya Sh. bilioni 111.77 kutokana na Kodi ya Pango la Ardhi.

Wizara haitaweza kufanikisha malengo hayo endapo itaendelea kuwaachia wadaiwa sugu ambao hawataki kulipa kodi. Kwani kwa miaka mingi sasa mapato mengi ya serikali yamekuwa yakiachwa kutokana na kushindwa kufuatilia wadaiwa sugu wa kodi ya pango la ardhi Kayandabila alisisitiza.

Rais Trump Apata Pigo.....Mahakama Yatengua Amri Yake

$
0
0
Jaji mmoja wa Marekani amesimamisha kwa muda utekelezaji wa amri ya Rais Donald Trump ya kuwazuia raia kutoka mataifa saba, yaliyo na raia wengi wa imani ya Kiislamu kuingia nchini Marekani.

Jaji wa Seattle alipuuzilia mbali sababu zilizotolewa na mawakili wa Serikali na kusema kuwa amri hiyo inaweza kusimamishwa mara moja huku kesi hiyo ikiendelea kusikilizwa mahakamani.

Serikali inatarajiwa kukata rufaa ya dharura dhidi ya uamuzi huo wa mahakama, ambao ni changa moto kubwa kwa utawala wa Trump.

Serikali ya Marekani inasema kuwa makumi ya maelfu ya visa zimefutiliwa mbali tangu rais Trump kutia sahihi amri ya kupunguza idadi ya watu wanaopaswa kuingia nchini Marekani juma lililopita.

Kutokana na hatua hiyo, Idara ya Forodha ya Marekani imeyaambia mashirika ya ndege kwamba waruhusu abiria kupanda ndege kuelekea Marekani abiria ambao walinyimwa ruhusa baada ya Rais Trump kutoa amri kwamba watu kutoka nchi saba zenye Waislamu wengi, wakataliwe kuingia Marekani.

Wakati huohuo waziri Mkuu wa zamani wa Norway, Kjell Magne Bondovik, alisema kuwa alizuiwa katika uwanja mmoja wa ndege mapema juma hili, katika tukio alilosema ni la uchokozi, kwa sababu eti alikuwa na visa ya Iran katika paspoti yake.

Sakata la Madawa ya Kulevya: Wema Sepetu Kawatoa Hofu Mashabiki Wake

$
0
0
Mwigizaji wa Tanzania Wema Sepetu ambaye mwishoni mwa wiki iliyopita alifika kwenye kituo kikuu cha Polisi kati Dar es salaam baada ya kutajwa kwenye orodha ya wanaotuhumiwa kufanya  biashara ya dawa za kulevya, amewatoa hofu Mashabiki zake.

Wema amesikika kwenye sauti aliyoiweka kwenye mitandao akisema: 'Nadhani natakiwa kusema kitu sababu najua nina mashabiki, nina watu wananipenda na kunifatilia…. nina watu wanani-support, nina watu wana hofu kuhusu mimi.

"Nina watu ambao wananijali sana na nina uhakika yani wana wasiwasi sana lakini nataka tu niwaambia kwamba msiwe na wasiwasi"

Msikilize hapo chini

Mwanamke wa Kitanzania Akamatwa na Cocaine India

$
0
0
Thelma Mkandawire (38) raia wa Zambia and Pamela Devid Kiritta (41) raia wa Tanzania baada ya kukamatwa na kilo nne za cocaine leo nchini India.

Wanawake wawili wamekamatwa jana Jumamosi na kilo nne za cocaine nchini India. Wanawake hao wametajwa kama Pamela Devid Kiritta mwenye umri wa miaka 41 raia wa Tanzania na Thelma Mkandawire mwenye umri wa miaka 38 raia wa Zambia.

Wanawake hao wamekamatwa ndani ya hoteli moja iliyoko kusini mwa jiji la New Deilhi baada ya maafisa husika kutonywa kuwa walikuwa wanapeleka mzigo huo wa cocaine kwa mtu fulani. Mwanamke wa Zambia alisafiri na ndege ya kampuni moja ya Ulaya akitokea Addis Ababa. Maafisa hao walianza kumfuatilia mara tuu alipotua kwenye uwanja wa kimataifa wa ndege wa IGI.

Baada ya kucheki out, Mzambia huyo alichukua teksi na kuondoka zake. Maafisa walimfuatilia mpaka kwenye hoteli moja iliyopo eneo la Mahipalpur ambapo partner wake Pamela alikuwa anasubiria mzigo. Wote wawili walikamatwa kabla ya kuondoka hotelini hapo. Ndani ya begi la Mzambia kulikuwa na mzigo wa kilo nne za cocaine ambazo zilikuwa zimefungwa kwa ustadi mkubwa sana kiasi kwamba machine za airport hazikuweza kugundua.

Alipohojiwa na maafisa hao, Pamela alisema alikuwa amepanga kwenye flat moja iliyoko Vasant Kunj tokea Januari 20 mwaka huu. Pamela amesema kuwa alikuwa anamfanyia kazi mwanaume mmoja wa Afrika ya Kusini. Pamela ameitembelea India mara tisa tokea mwaka 2006. Pia Pamela ameshatembelea nchini nyingine kama Ecuador, Afrika Ya Kusini na Kenya. Maafisa wa India wanahisi kuwa safari zake zinahusiana na biashara ya dawa za kulevya.

Kwa upande wa Mzambia (Thelma) alikamatwa Pakistani mwaka 2015 kwa tuhuma za kusafirisha dawa za kulevya. Pia ametemblea nchi za China na Hong Kong kwa biashara hiyo hiyo.

VIDEO: Alikiba alivyoimba LIVE na band yake Dodoma usiku wa kuamkia leo

$
0
0
Mwimbaji staa wa bongofleva Alikiba usiku wa February 4 2017 alikuwa makao makuu ya nchi Dodoma kwa ajili ya kutoa burudani kwa Watu wake huku akisindikizwa na mdogo wake AbduKiba pamoja na band yake ya live…. Hii video hapa chini ina tukio zima:

Muonekano Mpya wa Mtoto Aliyeokotwa Mtaani Nigeria Akiwa Mwenye Hali Mbaya

$
0
0
Sura ya furaha inaendelea kuonekana kwa mtoto Hope aliyechukuliwa mtaani nchini Nigeria wakati huo akiwa na miaka miwili baada ya kuachwa na Wazazi wake ikisemekana ni Mchawi.

Inasemekana alitelekezwa na familia yake kwa sababu walidhani yeye ni mchawi ambapo baadae akapatikana mtaani na kuchukuliwa na Mwanamke raia wa Denmark Anja Ringgren Loven aliyejitolea kumlea na kuishi nae.

Baada ya kuchukuliwa kutoka mtaani January 2016 picha mbalimbali zimekua zikitoka zikionyesha maendeleo ya Hope akionekana amenawiri kiafya na hata shule anasoma.
Hapa chini ni picha zake za kabla na baada ya kuokotwa…


Hii ni Kauli ya Vanessa Mdee Kufuatia Kutajwa Kwenye List ya Makonda...!!!

$
0
0

Iliwashangaza wengi baada ya Vanessa Mdee naye kutajwa kwenye orodha ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda ya mastaa wanaohusishwa na biashara ya madawa ya kulevya. Ni shutuma nzito, na hata kabla uthibitisho rasmi haujatoka, madhara ya kutajwa majina yao yameanza kuonekana katika maisha yao

Wito huo umemkutia Vee Money akiwa nchini Afrika Kusini anakoshoot tamthilia ya MTV Shuga, na bila shaka atalazimika kukatisha kwa muda na kurudi Tanzania kwenda kituo cha polisi central, anakotakiwa Jumatatu ya kesho.

Pamoja na hivyo, Vee ameonesha kuvuta pumzi ndefu na kuacha maisha yaendelee kama yalivyo. Kupitia Instagram, Vee amepost picha hizo juu na katika ile aliyokaa ameandika: The show must go on … bomb ass dress from @asos #FILA.

Kwenye hiyo black and white ameandika: The night is darkest before the dawn. #Breakthrough #Juu #CashMadame #SheKing.”

Kwenye picha hizo amezima comments ili kuepuka maneno ya kejeli kutoka kwa baadhi ya watu ambao tayari wamefanya hivyo kwenye picha zingine. Vee anaungana na mastaa wengine wakubwa wakiwemo Wema Sepetu, Mr Blue, TID na wengine kwenye orodha hiyo.

Amwua Binti Yake Kwa Kutopiga Mswaki...!!!

$
0
0

IRIS HERNANDEZ-RIVER (20) mwanamke mkazi wa Gaithersburg, Jimbo la Maryland, Marekani, alimwua binti yake, Nohely Alexandra Martinez Hernandez mwenye umri wa miaka minne kwa kutopiga mswaki.

Mama huyo alikasirishwa na kitendo hicho jana ambapo alimpiga teke la tumboni binti yake huyo na kusababisha binti huyo kudondoka na kugonga kichwa chake ukutani.

Ilimchukua Iris muda wa saa moja kupiga namba 911 ili binti yake apatiwe msaada ambapo Nohely alifikishwa hospitali akiwa mahututi na baadaye kufariki jana hiyo hiyo.

Prof Lipumba Afunguka Mazito Yaliyojificha Kati Yake na Maalim Seif..!!!

$
0
0

Mwenyekiti wa Chama cha wananchi (CUF), Profesa Ibrahim Lipumba amekanusha tuhuma za kuwa na ukaribu unaotia shaka kati yake na serikali na kutolea ufafanuzi ishu mbalimbali zinazoashiria ukaribu huo ikiwemo ya kuchepusha ruzuku ya chama.


Mwenyekiti huyo anayetambuliwa na Msajili wa Vyama vya Siasa amesema kinachodaiwa kuwa ni ukaribu wake na serikali, siyo sahihi kwa kuwa yeye huwa anaalikwa tu kwenye matukio mbalimbali ya kitaifa ambayo hawezi kukataa mwaliko.

"Kwa mfano ukikaribishwa kwenye shughuli ya serikai, labda Rais anazindua kitu, au sherehe za kitaifa na Rais yupo utakataaje" Amesema Lipumba.

RUZUKU

Suala la ruzuku ya chama hicho kuchepushwa pia ni jambo linalodaiwa kuwa ushahdi wa Prof Lipumba kuwa karibu zaidi na serikali, ambapo amesema ilikuwa ni lazima iwe hivyo kutokana na uamuzi wake kama Mwenyekiti wa chama wa kutengua uteuzi wa Mkurugenzi wa Fedha, ambaye ndiye aliyekuwa mtia sahihi katika masuala ya fedha.

Pia sababu nyingine ya kuchepusha fedha za ruzuku amesema ni mahitaji ya chama kwa kuwa kilikuwa kinaingia kwenye uchaguzi hivyo kilihitaji fedha kwa ajili ya shighuli mbalimbali.

" Kuhusu ruzuku, nilikuwa nimetengua uteuzi wa mkurugenzi wa fedha, bwana Bashange, kwahiyo hakuwa tena signatory wetu, kwa nafasi yangu kama mwenyekiti niliona hafai, tukajitahidi kufungua akaunti nyingine lakini haikuwezekana. Ikabidi Naibu Katibu Mkuu ambaye ndiye anayeshika nafasi ya Katibu Mkuu anapokuwa hayupo ofisini, aandike barua ya kuomba ruzuku kwa ajili ya mahitaji tuliyokuwa nayo" Ameeleza Lipumba 

Lipumba ameendelea kusema "Tukapeleka taarifa kuomba ruzuku. Kwahiyo Naibu Katibu Mkuu akaandika barua kwenda kwa Msajili kuwa tunaomba ruzuku na ipitie kwenye akaunti nyingine, na hilo likafanyika" 

MIKUTANO

Kuhusu yeye kuruhusiwa kufanya ikutano, huku Katibu Mkuu wake akizuiliwa, hususani tukio lililotokea mkoani Mtwara, Lipumba amesema hata yeye alipokwenda Mtwara hakuruhusiwa kufanya kilichokuwa kimempeleka, na badala yake aliishia kufanya mikutano ya ndani, huku akibainisha kuwa kilichomkwamisha Maalim Seif ni kwenda bila kutoa taarifa kwa kiongozi wa wilaya.

"Nimekwenda Mtwara, nilikaribishwa na viiongozi wa wilaya, kazi yangu ilikuwa ni kufungua matawi, lakini polisi wakanizuia kuwa sitakiwi kufanya mikutano ya nje, nikafanya mikutano ya ndani...Lakini Maalim Seif alikwenda bila kumtaarifu kiongozi wa wilaya". Amesema

ULINZI

Lipumba aliyekuwa katika mahojiano na kituo kimoja cha TV, amekanusha taarifa za kupewa ulinzi na serikali na kufafanua tukio la kupigiwa saluti na askari, akisema kuwa siku hiyo hakupigiwa yeye saluti bali diwani wa eneo ambalo yeye alishiriki kufanya usafi.

"Pale Buguruni, tulikuwa katika usafi, na tulikuwa na diwani wa eneo lile, askari walikuwa wakiangalia usalama, na alipotokea diwani wa eneo lile, askari walimpigia yeye kwa kuwa ndiye mkuu wa eneo lile, siyo mimi"

Katika hatua nyingine, amesema anaendelea kumtambua Maalim Seif kama Katibu Mkuu halali wa CUF,  huku akimtaka amfuate ili wamalize tofauti zao na kufanya kazi kwa pamoja.

Nape Amrushia Dongo Makonda Baada ya Kumtaja Wema Kuwa Anahusika na Madawa ya Kulevya,Amtaka Awe na Busara..!!!

$
0
0

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Nape Nnauye ameingilia kati na kutaka busara itumike katika zoezi la kutaja wasanii wanaohusika na dawa za kulevya linalofanywa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda

Nape ametoa ushauri huo leo Mjini Dodoma wakati akizungumza na wanahabari kuhusu sheria mpya wa huduma za habari, ikiwa ni siku nne tangu mkuu huyo wa mkoa aanze kutaja wahusika wa dawa za kulevya wakiwemo wasanii wa bongo fleva na filamu.

Baadhi ya waliotajwa na kutakiwa kuripoti polisi kwa mahojiano ni pamoja na Vanessa Mdee, Wema Sepetu, Nyandu Toz, Chidi Benz, TID, Tunda, Babuu wa Kitaa n.k

Nape baada ya kuulizwa swali na wanahabari kuhusu suala hilo amesema kuwa wizara yake inakiri kuwa tatizo hilo ni kubwa, na ilifikia hatua ya kuwasaidia baadhi ya wasanii kwenda kupata matibabu akiwemo msanii Ray C na kwamba wanaunga mkono jitihada zozote za kupambana na tatizo hilo.

Amesema tatizo lipo kwenye namna ya kuwaadhibu wanaogundulika kutumia dawa za kulevya, kwa maana ya sheria ipi itumike kuwashitaki, lakini pia tatizo lingine ni busara inayotumika kuwataja na kuwakamata watu ambao tayari wamekwisha athirika na dawa kulevya badala ya kuwasaidia.

Kwa mtazamo wake nape amesema hilo ni tatizo la jamii nzima, na kushauri jamii yote ya watanzania kushiriki katika kujenga maadili ya watoto.

Hatma ya Chege na Temba Sasa Hadharani..!!!

$
0
0

Msanii kutoka TMK Wanaume Family, Chege Chigunda amesema yuko mbioni kukata kiu ya mashabiki wa 'Chege na Temba' kwani bada ya kutoa ngoma yake ya Kelele za Chura, ngoma inayofuata ni yake na swahiba wake Mh. Temba kutoka familia hiyohiyo ya Wanaume.

Chege amelazimika kuweka wazi hatma ya Chge na Temba kutokana na kukumbana na maswali mengi ya watu mbalimbali wakitaka kujua ni lini wasanii hao watafanya tena kazi ya pamoja kutokana na temba kuwa kimya kwa muda mrefu.

Chege aliyekuwa akiitambulisha rasmi 'EXCLUSIVE' video yake ya 'Kelele za Chura' kwenye kipindi cha Friday Night LIVE cha EATV, alisema kwa sasa na yeye ameamua kutoa albam kwa kuwa anaamini albam zina soko, na kwa kutambua wabongo wame-miss albam kwa muda mrefu, sasa ameamua kukata kiu ya mashabiki.

Ameitaja albam yake kuwa itakwenda kwa jina la 'Sweet Sweet' na itakuwa na nyimbo 15, na kwamba kila kitu kimekamilika, na katikati ya mwezi huu itakua madukani

Mshiriki Miss Tanzania Akiri Kudanganya Umri..!!!

$
0
0

Aliyekuwa mshiriki wa mashindano ya urembo ya Miss Tanzania mwaka 2008, Nelly Kamwelu, amekiri kudanganya umri katika mashindano hayo wakati huo ili apate fursa ya kushiriki mashindano hayo.

Nelly ambaye aliingia katika fainali za Miss Tanzania baada ya kushika nafasi ya tatu katika Miss Ilala, amesema wakati huo umri wake ulikuwa ni miaka 15, lakini ilibidi ajikuze ili kukidhi vigezo na kuamua kuandika umri wa miaka 18.

Nelly amefunguka siri hiyo hivi karibuni akiwa kwenye kipindi cha Friday Night Live cha EATV ambapo amesema sababu kubwa ya kulazimisha kushiriki katika mashindano hayo ni ndoto aliyokuwa nayo tangu akiwa mdogo, lakini pia umbile lake lilikuwa linamruhuruhusu kwa kuwa alionekana kuwa na mwili mkubwa licha ya kuwa na umri mdogo.

Ukweli huo unaonesha jinsi ambavyo ni rahisi kwa warembo kudanganya umri wao katika mashindano hayo, pasipo kugundulika

Nelly mbali na kushiriki mashindano hayo ya Miss Tanzania ambayo hakuambulia kitu, anasema hakukata tama na hivyo kuingia katika mashindano mengine ya urembo ambayo yalikuwa ni Miss Universe Tanzania mwaka 2011 na kuibuka mshindi.

Hadi sasa anashikilia rekodi ya kuwa mrembo pekee ambaye ameiwakilisha Tanzania katika mashindano manne tofauti ya dunia ndani ya mwaka mmoja, kwani katika mwaka huo wa 2011, licha ya kuiwakilisha Tanzania katika Miss Universe nchini Brazil pia aliiwakilisha Tanzania katika mashindano ya Miss International mwaka 2011 nchini China na Miss Earth mwaka 2011 Manila, nchini Ufilipino ambapo katika mashindano hayo yote hakufanya vizuri.

Pia ndani ya mwaka huo huo w 2011 aliiwakilisha Tanzania katika mashindano ya Miss Tourism Queen International yaliyofanyika Xian, China na kufanikiwa kukamata nafasi ya 5.
Viewing all 104689 articles
Browse latest View live




Latest Images