Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104664 articles
Browse latest View live

Trump Azidi Kukataliwa Uingereza,Spika a Bunge Asema Hataki Kuona Sura Yake Ndani ya Bunge Lake Tukufu..!!!!

$
0
0

Spika wa bunge la Uingereza John Bercow amepinga hatua ya Rais Donald Trump kuhutubia bunge la taifa hilo wakati wa ziara yake.

Hii ni kwa madai kwamba matamshi yake yamesababisha chuki huku mbunge mmoja akisema kuwa hayafai huku wengine wakidai hafai kupendelea upande mmoja.

Bercow alisema pingamizi dhidi ya ''ubaguzi wa rangi na ule wa kijinsia'' zinapaswa kuangaziwa sana na wanachama wa bunge hilo.

Akizungumza bungeni siku ya jumatatu, Bercow alisema kuwa anapinga Rais Trump kuhutubia mabunge yote kama ilivyo ada na viongozi wengine wa kimataifa na kuongeza kusema kuwa  kulihutubia bunge sio haki bali ni heshima anayopewa kiongozi wa kimataifa.

Kwa mujibu wa mwandishi wa BBC wa maswala ya kisiasa Eleanor Garnier, hilo ni pigo la kidiplomasia kwamba rais Trump hataruhusiwa kuhutubia bunge la nchi hiyo.

Kweli Kufa Kufaana,Ray C Aamua Kuja na Kmapeni Hii Wakati Wema na Wenzake Wakiwa Ndani Kwa Kuhusishwa na Madawa ya Kulevya..!!

$
0
0

MSANII wa Bongo Fleva, Rehema Chalamila maarufu kama‘Ray C’ Kiuno Bila Mfupa, amejitokeza kumuunga mkono Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda kwa kuweka video mtandaoni ikimuonesha mtu aliyepoteza maisha kwa madawa ya kulevya huku akiandika: “SAY NO TO DRUGS”

Aidha Ray C ambaye anatajwa kama nimhanga wa madawa hayo aliwahi kupewa huduma vituo mbalimbali vinavyotoa huduma kwa waathirika wa madawa ya kulevya ‘Sober House’ na baada ya muda anaonekana kurudia hali ya kudhoofu na kuwa kama mhanga wa madawa hayo.

Ray C amewahamasisha watu wengi kupitia video aliyoiweka katika mtandao na imewagusa Watanzania wengi kwa kuchangia maoni yao juu ya athari mbaya za madawa ya kulevya na sakata la linalonguruma kwa sasa nchini.

Mwanafunzi wa Sekondari Atiwa Mbaroni Akiwa na Kete 24 za Cocaine..!!!

$
0
0

Polisi mkoani Mbeya wametangaza kumkamata mwanafunzi anayesoma sekondari akiwa na kete 24 za cocaine eneo la Mbalizi mkoani Mbeya.

Kamanda wa polisi mkoa, Dhahir Kidavashari amesema Jumanne hii kuwa polisi wamemkamata mwanafunzi huyo akiwa anaziuza dawa hizo kwa watu mbalimbali na kwamba upelelezi wa kuwadaka mapapa unaendelea.

Kukamatwa kwa kijana huyo kunatokea siku moja baada ya Rais John Magufuli kuunga mkono kazi ya Makonda huku akiwaagiza wakuu wa vyombo vya ulinzi na usalama kuwashughulikia wote wanaojihusisha na dawa za kulevya bila kujali huyu ni nani.

Kidavashari amesema kwamba vita dhidi ya dawa za kulevya ilikuwa ikiendelea, lakini sasa imepata msukumo mpya ambao unalenga kuukata mnyororo mzima wa mtandao unasambaza dawa hizo.

AY Afunguka kuhusu msanii mwenzake wa East Coast Team kutumia madawa ya kulevya

$
0
0
Wiki hii nzima habari iliyomake headline ni kuhusu ishu ya madawa ya kulevya ambapo wasanii mbalimbali pamoja na watu wengine wamefikishwa polisi na wengine mahakamani kutokana na madawa ya kulevya.

Baada ya kuibuka kwa swala hili tumekuja kugundua kua kumbe kuna wasanii wengi wamehusishwa na utumiaji wa madawa ya kulevya. Msanii AY alipoulizwa kuhusiana na mmoja wa wasanii ambao walikua wakiunda kundi la East Cost Team kua ni mtumiaji wa madawa ya kulevya alifunguka haya.. Unaweza tazama video nzima hapa chini

Kutoka Mahakamani..Wema Sepetu na Wenzake Wapewa Dhamana na Masharti Haya Matatu Mahakamani...!!!

$
0
0

Hatimaye wale watuhumiwa wa madawa ya kulevya ambao pia ni wasanii wa filamu na muziki pamoja na wafanyabiashara nchini wamefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu na kupewa dhamana Iliyoambatana na Masharti Matatu.

Waliopanda kizimbani leo muda mfupi uliopita  ni Johan (muongozaji), Babuu, Dogo Hamidu, TID, Recho (wanamuziki), Tunda (muigizaji), Rajabu ambaye ni kaka yake Dogo Hamidu na Dj Rommy Jones.

Akisoma masharti hayo, Hakimu wa Mahakama ya Kisutu, Huruma Shaidi alisema kwamba watuhumiwa hao watatakiwa kufanya vitu vitatu mara tu watakapotoka mahakamani hapo.

Kila mmoja alitakiwa kuweka bondi ya shilingi milioni kumi, kuripoti katika Kituo Kikuu cha Polisi, Dar mara mbili kwa mwezi kwa mwaka mzima huku pia wakitakiwa kuwa chini ya uangalizi wa mahakama kwa miaka mitatu mfululizo.

Kwa upande wa serikali katika kesi hiyo ilisimamiwa na Wakili Nassoro Katuga huku upande wa utetesi ukiwakilishwa na Wakili Albert Sando.

Pichaaa: Harmorapa Amtembelea P-Funk Majani..!!!

$
0
0

Rapper mchanga Harmorapa Jumatatu hii alimtembelea producer mkongwe wa Bongo Record, P-Funk Majani nakuzungumza naye mambo kadhaa kuhusu muziki.

Hivi karibuni mtayarishaji huyo mkongwe alionyesha kupendezwa na harakati za rapper huyo ambaye amekuwa akizungumziwa kila kukicha.

Rapper huyo baada ya kutembelea studio hapo na kukutana na mkongwe huyo alionyesha kufurahishwa huku akiwataka watu kuacha kuongea.

“Dreams are brighter days!! Nikiwa na legend producer Majani. Ya leo siyo ya jana hatuongei ongei tu #shout out,” aliandika rapper huyo Instagram.

Kwa upande wa Majani alipost picha aliyopiga na rapper huyo na kuandika :Harmorapa payed us a visit today.

Imefichukaaa...Hii Ndio Sababu ya Wema Sepetu Kunyimwa Dhamana Wakati Wenzake Wakiondoka Mahakamani Leo

$
0
0

Watuhumiwa wa biashara na matumizi ya dawa za kulevya waliotajwa hivi karibuni na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaamm, Paul Makonda, Jumanne hii, February 7, 2017 wamefikishwa katika mahakama ya Kisutu jijini Dar es Salaam kujibu tuhuma zinazowakabili.

Mastaa hao wakiwemo TID, Nyandu Tozi, Babu wa Kitaa, Romy Jones, Tunda, na wengine, wameachiwa kwa sharti la dhamana ya shilingi milioni 10 kila mmoja na watakuwa wakiripoti kwa mwezi mara mbili huku wakiwa katika uangalizi wa jeshi la polisi kwa kipindi cha mwaka mmoja.

Hata hivyo watuhumiwa wengine wakiwemo Petit Man, Said Alteza, Lulu Diva na wengine wametakiwa kuweka dhamana ya shilingi milioni 20 na watakuwa chini ya uangalizi kwa kipindi cha miaka mitatu. Iwapo watuhumiwa hao watashindwa kufuata masharti hayo watarudishwa tena mahakamani.

Hali imekuwa tofauti kwa Wema Sepetu ambaye ameendelea kukaa rumande baada ya msako kubaini msokoto wa bangi nyumbani kwake na hivyo kuongezwa kosa jingine zaidi ya lile la awali, ambapo sasa inasubiriwa uchunguzi kukamilika.

Wabunge wa upinzani Walivyosusa na kutoka nje kisa kukamatwa kwa Tundu Lissu

$
0
0
Wabunge wote wa vyama vya upinzani waliokuwa bungeni katika kikao kinachoendelea jioni hii wametoka nje ya Bunge, wakipinga wenzao kufukuzwa bungeni pamoja na kitendo cha Mbunge Tundu Lissu kukamatwa.

Wabunge waliokuwa wameamuliwa kutoka nje ya ukumbi wa Bunge na Naibu Spika Dkt Tulia Ackson ni pamoja na mbunge wa Kawe Halima Mdee, Mbunge wa Bunda Mjini Ester Bulaya na Mbunge wa Serengeti Marwa Ryoba.

Wabunge hao watatu wamedaiwa kupinga uamuzi wa Naibu Spika kuhusu muongozo ulioombwa na mbunge wa Kigoma Mjini Zitto Kabwe, kuhusu utaratibu uliotumika kumkamata mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu.

Mara baada ya Naibu Spika kutoa maamuzi ya kuwaondoa wabunge hao watatu bungeni, ndipo wabunge wengine wa upinzani pia wakaamua kutoka kama ishara ya kupinga maamuzi hayo, pia ikiwa ni ishara ya kupinga utaratibu wa kukamatwa kwa mbunge Tundu Lissu.

Nje ya ukumbi wa Bunge, Mbunge wa Kigoma Mjini Zitto Kabwe , amesema wamefikia hatua hiyo kuonesha kuwa uataratibu unaotumiwa kukamata wabunge wakiwa bungeni siyo sahihi, na kwamba kesho wataendelea na vikao vya bunge lakini mapambano yataendelea.

"Kesho tunarudi bungeni, lakini mapambano yataendelea, tunataka kuonesha kuwa utaratibu huu wa kuvizia wabunge kwenye milango ya bunge bila taarifa rasmi ya Spika na bila kuwaeleza wabunge sababu za kukamatwa kwao siyo sawa. Tukilifumbia macho litakuja kumtokea mbunge yoyote hata wa CCM" Amesema Zitto.

Video..Diamond na Zari Wala Raha Mbele ya Mama Diamond Huku Akiwatazama Kwa Aibu..!!!

Baada ya Iyobo Kumuita Nyani Hamorapa,Dada Yake Dimaond Aibuka na Kumchana Hamorapa kwa Staili Hii..!!!

$
0
0

MWANAMUZIKI anayefanya vizuri kwenye tasnia ya Muziki wa Bongo Fleva akiwa chini ya Lebo ya WCB,  ‘Queen Darleen’  hivi karibuni ameonyesha kushangazwa na kitendo cha mwanamuziki chipukizi Hamorapa kujifananisha na Hermonize.

Akipiga stori na Uwazi Showbiz, hivi karibuni na kutakiwa kuzungumzia kauli aliyoitoa Dancer Mose Iyobo ambaye yupo kwenye Lebo ya WCB kuwa Hamorapa anafanana na sokwe alisema hamjui msanii huyo kivile na anamshangaa kujifananisha na Harmonize.

“Hata kama nilishamuona sijamtilia maanani, simjui kabisa na sidhani kama anafanana na Harmonize, lakini  pia siwezi kuzungumzia lolote juu ya kauli ya Iyobo,” alisema Queen Darleen

Soma Kimya Kimya..Fahamu Faida za Kula Pweza..!!!

$
0
0

Samaki aina ya Pweza amejawa na wingi wa virutubisho ambavyohusaidia mwili kujikinga dhidi ya magonjwa kama vile saratani vile saratani ya mdomo, utumbo mkubwa, tumbo, matiti, shingo ya kizazi na pia kansa ya mapafu.

Pweza amejawa na virutubisho vinavyosaidia kuongeza ashki (hamu) na kuboresha tendo la ndoa. Hii ni kutokana na uwepo wa virutubisho aina ya protini na madini ya selenium.

Aidha Pweza humsaidia mwanamke kuwa na sifa halisi za ukike na pia mwanaume kuwa mwanaume wa shoka. Kwa mwanaume humsaidia kuwa na misuli iliyojengeka vizuri na hivyo kuweza kumtofautisha mwanaume na mwanamke.

Faida ya nne ni kuwa pweza ina virutubisho vinavyosaidia  kuukinga mwili dhidi ya  kupungukiwa na uwezo wa ubongo hasa kwa wenye umri mkubwa. Kitaalamu tatizo hili huitwa Alzheimer.

Pweza huwasaidia walaji kujikinga dhidi ya ugonjwa wa Pumu . Wataalamu wamegundua kuwa mlaji wa pweza yupo katika hatari ndogo ya kuugua ugonjwa wa pumu. Hata wenye ugonjwa huo huweza kupata virutubisho vya kupunguza athari za ugonjwa.

Pweza husaidia mwili kufanya kazi zake vizuri ikiwamo mmeng’enyo wa chakula, upumuaji na hata mzunguko wa damu.

Minofu ya pweza huusaidia mwili kuzalisha Haemoglobin ambazo ni muhimu katika damu. Hii ni kwa sababu pweza ana madini aina ya shaba ambayo ni muhimu kwa kazi hiyo.

Kwa upande wa kina mama, pweza husaidia katika uzalishaji wa maziwa pindi wanapojifungua .
Faida nyingine waipatayo watumiaji wa supu na minofu ya pweza ni kuwa huongeza madini joto mwilini.

Virutubisho vilivyomo ndani ya pweza husaidia kupunguza athari za maradhi ya moyo kwa kuwepo mafuta ya omega-3 fatty acid.

Habari Picha..,Hivi Ndivyo Obama Alivyokuwa Akijirusha Baharini na Rafiki Yake

$
0
0

Rais Barack Obama akiwa mapumzikoni na rafiki yake, Richard Branson baada ya kumaliza miaka minane ya utumishi kama Rais wa Marekani.




Baada ya Maneno Kuwa Mengi,Ommy Dimpoz Avunja Ukimya,Amaunika Mchumba Wake...!!!

$
0
0

Msanii Ommy Dimpoz ambaye anafanya vyema na wimbo wake 'Kajiandae' wiki kadhaa zilizopita alifunguka na kusema ikifika wakati ataweka wazi suala la mahusiano yake kwa jamii, na kumuweka wazi mchumba wake ili watu wajue.

Ommy Dimpoz alisema hayo kwenye kipindi cha eNewz cha EATV wiki kadhaa zilizopita, Ommy alifunguka na kuthibitisha kuwa kwa sasa yupo kwenye mahusiano na raia wa China., ambaye watu wengi hawamjui.

Juzi Ommy Dimpoz ametupia Instagram picha ya pamoja akiwa na binti huyo mwenye asili ya China kisha akaweka 'emoji' yenye ishara ya love, akiashiria 'Mapenzi bampa 2 bampa'.

Ingawa Ommy Dimpoz hakutaka kufungua mjadala kwenye picha ile kwa kuamua kufunga uwanja wa comment ili watu wasiweze kuzungumza wala kujadili katika picha hiyo. Lakini ukweli ni kwamba picha ile inazungumza mambo mengi kwa kila anayeiangalia.

Video..Mzungu Awachana Watanzania Wanaolialia Njaa ,Awaambia Wale Majani..!!!

Kaibuka..Mrema Aibua Mapya Issue ya Madawa ya Kulevya,Awataja Wengine Wanaohusika...!!!

$
0
0

Mwenyekiti wa Taifa wa Bodi ya Parole, Augustino Lyatonga Mrema ameibuka na kusema kuwa wapo baadhi ya polisi wanagawa na kusambaza dawa za kulevya pia wanawasaidia baadhi ya waathirika wa dawa hizo waliopo magerezani kuzipata.

Augustino Mrema anasema vita ya dawa za kulevya inawezekana kumalizika kama watawatumia watumiaji na wauzaji wadogo wadogo kuwapata wale wauzaji wakubwa ambao ndiyo tatizo zaidi katika jamii.

"Vita hivi vitawezekana kumalizika kama tutatumia hawa wadogo wenye kete mbilimbili, na siyo kuwapeleka magerezani, wamenionesha na njia wanazotumia kuwapa dawa waathirika waliopo magerezani, tusitumie nguvu nyingi kuwakamata hawa dagaa wadogo wadogo, bali tuwatumie hawa tupate chain nzima, kwa njia hiyo tutapeleka watu wanaostahili magerezani" alisema Augustino Mrema

Mbali na hilo Augustino Lywatonga Mrema anasema kama polisi walikuwa wanasambaza na kugawa madawa ya kulevya hivyo basi wao ndiyo walikuwa wakiendesha hivyo vijiwe na kuwajua wahusika wa madawa ya kulevya.

"Sasa kama polisi ndiyo anasambaza na kugawa madawa kwa hiyo vijiwe vile vilikuwa vinaendeshwa na wao, hivyo wanawajua wanaogawa, na wanaotumia sasa huu mtandao ukikamatwa hii nchi itapona" alimalizia Mrema.

Huyu Ndiye Mbunge Anayemkomalia Makonda Bungeni,Adai Makonda ni Mshirika Mkubwa wa Madawa ya Kulevya Ataka Akamatwe Haraka Sana...!!

$
0
0

Mbunge wa Geita Vijijini (CCM), Joseph Kasheku ameendeleza ‘vita’ yake dhidi ya Paul Makonda, akisema yupo tayari kusaidia vyombo vya dola kukamata vigogo wa dawa za kulevya na kuhoji ukimya wa mawaziri watatu dhidi ya kile alichodai utajiri wa mkuu huyo wa Mkoa wa Dar es Salaam.

Awali, Kasheku ambaye ni maarufu kwa jina la Msukuma, alitoa tuhuma dhidi ya Makonda juzi, alipotaka kujua wafadhili wa safari za mkuu huyo wa mkoa nje ya nchi na sababu za kubagua watuhumiwa wa biashara ya dawa za kulevya kwa kutaja baadhi na kuwaacha wengine, huku mawaziri wakisita kuchukua hatua.

Alitoa tuhuma hizo bungeni baada ya Makonda kuagiza watu 12, wakiwemo wasanii maarufu wa muziki na filamu, kuripoti Kituo Kikuu cha Polisi cha Dar es Salaam, akiwatuhumu kuhusika na utumiaji au biashara ya dawa za kulevya.

Jana, Msukuma aliibuka na hoja nzito zaidi akihoji sababu za mawaziri kutochukua hatua na pia kutaja baadhi ya mali alizopata Makonda katika kipindi kifupi alichoshika madaraka ya mkuu wa mkoa baada ya kuwa mkuu wa Wilaya ya Kinondoni pia kwa muda mfupi.

Mbunge huyo alitoa tuhuma hizo nzito muda mfupi baada ya kumalizika kwa kipindi cha maswali na majibu, wakati alipotumia kanuni ya 68 (7) kuomba mwongozo kutoka kwa Naibu Spika, Tulia Ackson.


Wasanii 13 Wawekwa Chini ya Uangalizi, Wema Aendelea Kusota Rumande..!!!

$
0
0

Wakati wasanii 13 wakipandishwa kizimbani katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kwa nyakati tofauti na kuweka chini ya uangalizi, wenzao wawili, Wema Sepetu na Omari Micheri wameendelea kusota rumande kwa zaidi ya saa 120.

Wema na Omari ndiyo pekee katika kundi la wasanii waliojisalimisha katika Kituo Kikuu cha Polisi tangu Ijumaa iliyopita kwa tuhuma za ama kutumia au kuuza dawa za kulevya waliodaiwa kukutwa na vielelezo.

Wakati Wema akidaiwa kukutwa na misokoto ya bangi, Omari anadaiwa kukamatwa na kete nne za dawa za kulevya ambazo hazijafahamika.

Juzi, Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Simon Siro alisema wasanii hao wangepelekwa mahakamani juzi pamoja na wenzao, lakini wawili hao hawakupelekwa hadi jana.

Baada ya kufikishwa mahakamani, wasanii watano kati ya 13 waliwekwa chini ya uangalizi wa mahakama kwa miaka mitatu huku wenzao wanane wakiwekwa chini ya uangalizi wa mahakama wa mwaka mmoja.

Waliowekwa chini ya uangalizi wa miaka mitatu na Hakimu Mfawidhi, Cyprian Mkeha na kutakiwa kuripoti polisi mara mbili kwa mwezi ni Ahmed Hashim maarufu kama Petitman, Said Masoud Linnah maarufu kama Said Alteza, Nassoro Mohamed Nassoro, Bakar Mohamed Khelee na Lulu Abbas Chelangwa maarufu kama Luludiva.

Pamoja na Kwamba Amekamata,Lissu Awashawishi Wabunge wa Upinzani Kutoka Bungeni Jana..!!!

$
0
0

Wabunge wa upinzani jana walisusia kikao cha Bunge mjini hapa, wakipinga kile walichodai ni mhimili huo wa dola kudhalilishwa na kushushiwa hadhi yake na Jeshi la Polisi.

Tafrani hiyo iliibuka saa 10:22 jioni baada ya Naibu Spika, Dk Tulia Ackson kukataa hoja ya Mbunge wa Kigoma Mjini (ACT -Wazalendo), Zitto Kabwe aliyetaka Bunge lijadili na kuweka azimio la kadhia hiyo.

Wakizungumza katika viwanja vya Bunge baada ya kutoka ukumbini, wabunge hao walisema vita hiyo wataiendeleza leo asubuhi, hadi kiti cha Spika kitakapotoa msimamo wa kulinda hadhi ya mhimili huo.

Kilichowasukuma zaidi wabunge hao kutoka ni hatua ya Naibu Spika, kuwaamuru askari wa Bunge kumtoa Mbunge wa Serengeti (Chadema), Marwa Ryoba aliyekuwa akipinga uamuzi wa kiti.

Baada ya uamuzi wa Naibu Spika kukataa Bunge lisijadili hoja ya Zitto na kuweka azimio, wabunge wa upinzani walionekana kupinga kwa kupaza sauti zao akiwamo Ryoba.

“Mheshimiwa Ryoba naomba utoke mwenyewe. Mheshimiwa Ryoba naomba utoke mwenyewe,” alisikika Naibu Spika akisema huku Ryoba akisema hatoki ndipo Tulia akaagiza polisi wamtoe.


Hata hivyo, wabunge wa upinzani kwa umoja wao ndipo wakaamua kutoka ukumbini na kuwaacha wa CCM wakiendelea na kikao cha Bunge cha jioni.

Kiini cha sakata hilo ni hatua ya polisi kumkamata Mbunge wa Singida Mashariki, (Chadema) Tundu Lissu, juzi jioni wakati akitoka bungeni na jana ilidaiwa polisi walikuwa wakimwinda Zitto.

Baada ya Danadana Nyingi..Hatiaye Serikali Imekiri Hali ya Uchumi Kuwa Mbaya ..!!!

$
0
0

Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Philip Mpango amesema licha ya uchumi wa Tanzania kukua kwa asilimia saba kwa zaidi ya muongo mmoja, bado hali ya uchumi ni mbaya Kusini mwa Jangwa la Sahara.

Akizungumza katika ufunguzi wa mkutano wa kimataifa wa takwimu jijini Dar es Salaam jana, Dk Mpango alisema ili kupambana na umaskini, Serikali imejikita kwenye ujenzi wa viwanda kwa ajili ya kuongeza ajira.

Alitaja takwimu za Benki ya Dunia (WB) za mwaka 2013 akisema asilimia 10.7 ya watu wote duniani ambao ni bilioni 7.1 walikuwa wakiishi chini ya Dola 1.90 za Marekani kwa siku ikilinganishwa na asilimia 12.4 mwaka 2012.  “Mbali na takwimu hizo kuonyesha umaskini kushuka kwa kasi ndogo, mafanikio hayo hayaonekani waziwazi kwa baadhi ya nchi zinazoendelea ikiwamo Tanzania,” alisema.

Alisema hali hiyo inatokana na ukuaji wa uchumi  kutokana na sekta zinazoajiri watu wachache na nyingi zikijikita mijini na kuwapo kwa kasi ya ongezeko la watu.

Kutana na Maalim Hussein Mtabibu wa Nyota za Binadamu Africa na Dunia Nzima,

$
0
0

Kutana na Maalim Hussein Mtabibu wa nyota za binadamu Africa na dunia nzima,
Anatoa TIBA MAENEO YOTE NCHINI, KWA WALE WENYE KUHITAJI TIBA ANATIBU YAFUATAYO,
Husafisha nyota na kutoa Pete za bahati na kwa wale walia sumbuka kwaajili ya matiba na hawakufanikiwa njoo ujionee muujiza wa papo kwa papo-humpa mtu jini la mali kwa yule anaetaka kumiliki mali bila masharti yoyote,
Anatibu magonjwa yalio shindikana-Mpenzi/MUME/MKE Aliekukimbia Anakurudishia Ndani ya saa 72 tu, Pia tunatoa dawa za Nguvu za KIUME na Kurefusha kwa saizi unayo Taka-Anatoa Dawa za BIASHARA NA MVUTO-Tunatoa Dawa za Uzazi kwa kina Mama kwa wale wenye Tatizo Sugu-Anatoa Zindiko ya Nyumba,Mwili, na Mvuto kazini- Tunamaliza kesi zilizo kaa muda Mrefu bila kumalizika, Tung'arisha Nyota na Cheo kazini. Tunarudisha Mali zilizopotea au Kuibiwa na Mengine Mengi ya Siri tuwasiliane kwa Simu-Whatsapp +255674835107
+255 629254849
Viewing all 104664 articles
Browse latest View live




Latest Images