Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104670 articles
Browse latest View live

Breaking News..Askofu Gwajima Amjibu Makonda kwa Ujumbe Huu ..!!!

$
0
0

Saa chache baada ya kutakiwa kufika polisi na mkuu wa mkoa kwa kutoa taarifa juu ya madawa ya kulevya,Askofu Mkuu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima,Josephat Gwajima Amepost Ujumbe picha huu ambao wataalamu wa mambo wanadai kuwa ni kama jibu kwa Mhe Makonda.



Rasmi...Dj Majizzo na Bosi wa Radio ya EFM Amekamatwa na Polisi kwa Tuhuma za Madawa ya Kulevya,Makonda Amethibitisha..!!!

$
0
0

Kwenye mkutano kati ya RC Makonda na waandishi wa habari aliulizwa swali kama ni kweli Majizzo(C.E.O wa E-FM/TV-E)? Mh Makonda alijibu ni kweli anashikiliwa kwa mahojiano.

Taarifa ni kwamba Dj Majizzo alikamatwa juzi nyumbani kwake na kupekwa kituo cha kati kwa mahojiano.
Kwa wale wasio mfahamu vyema Majizzo ni yule kijana anaye miliki kituo cha E Fm cha Jijini Dar Es Salaam

Kisa cha Kweli:Rafiki Aliyefungwa Miaka 30 kwa "Kubaka",Daftari la Wageni NECTA Likamuokoa Kifungoni..!!!

$
0
0

Huyu ni Rafiki yangu toka udogo,tukiwa shule ya Msingi mpaka Sekondari.Tulikaa pamoja na kusoma pamoja.Namzungumzia rafiki wa kufa na kuzikana.

Duniani kuna visa wakuu,visa hivi visikie kwa jirani lakini visikukute wewe au mtu wako wa karibu.Miaka 10 iliyopita,mwezi kama huu,huyu ndugu yangu alianza taratibu za kukata rufaa ili shauri lake liweze kusikilizwa tena.

Alifungwa kifungo cha miaka 30 gerezani.Kesi yake ilikuwa ya kutungwa na kubambikiwa.Pesa ilitembea na wakubwa wakaisimamia kesi yake.Nakumbuka alivyolia kwa kilio cha nguvu,siku Jaji alipogonga meza baada ya kumuhukumu kutumikia miaka 30 behind the bars!!

Kosa la kusingiziwa kubaka lisikie tu,kweli sio wote walio garezani wana hatia,wengine ni kesi za kusingiziwa.

Kila nilipoenda kumcheki gerezani jamaa alikuwa analia sana.Aliamua kuwa muhubiri na mwimba kwaya wa gerezani,katekista na muongoza ibada mbalimbali mle gerezani.Aliamini ipo siku atatoka,maana alimlilia Mungu wake,toka mawio ya jua mpaka machweo yake.

Baada ya miongozo ya watu wa gerezani(Wafungwa wengi hujua sana taratibu za sheria na namna ya kukata rufaa) jamaa aliamua kukata rufaa.Hoja kubwa ikiwa,siku na tarehe aliyoshutumiwa kutenda kosa,ndio siku na tarehe aliyokuwa Dsm,eneo la baraza la Mitihani akifuatilia "result slip" yake.

Huu ndio ulikuwa ushahidi mkubwa,kitabu cha wageni cha baraza la mtihani,kilionyesha mnamo terehe hiyo,siku hiyo,majira fulani mshitakiwa aliandika jina lake na sahihi yake ktk kitabu cha wageni kwenye lango la Baraza la Mitihani-Dsm.

Kitabu kile kilithibitishwa na Baraza la Mitihani kuwa ni sahihi,na baraza likathibitisha kuwa,tarehe tajwa,na siku tajwa ya mwezi tajwa,majira ya mchana,kitabu kinachoonyesha kuidhinishwa na kutolewa kwa "result slip" kilikuwa na sahihi ya afisa wa NECTA na mchukuaji wa "result slip" ambaye ndio mtuhumiwa.

Ndugu mwema alishinda kesi,sahihi na jina ktk vitabu vya NECTA vilmuokoa kuendelea kutumia miaka 29 iliyobaki baada ya kuwa tayari ametumikia mwaka mmoja jela.Ilikuwa ni siku ya ajabu,ikawa kama ndoto,ilikuwa ni siku ambayo majina na utukufu wote wa Mungu ulitajwa.Siku hii,kwa sahibu wangu,haikuhitaji muujiza wa kuhamisha mlima toka uwanda mmoja kwenda mwingine.Rufaa ile iliyoambataba na ushindi,ulikuwa ni muujiza tosha.

Pesa hudunisha utu,pesa hununua haki na pesa hubadili haki kuwa batili na batili kuwa haki.Sio wote walio gerezani wana hatia,na sio wote hawana hatia.

Sasa ni baba wa watoto watatu,ni miaka kumi na ushee sasa imepita.Kama ilivyo kwa wengine kukumbuka siku yao ya kuzaliwa,kwa ndugu yangu hii ndio siku kubwa ya kukumbukwa maishani mwake.Kila ifikapo,huandaa ibada na sadaka...Kumwambia Mungu...WEWE NI MUNGU WA HAKI.

Imebaki kuwa simulizi,itakuwa historia na baadae hadithi.Kimoja na kikubwa,huwa hatamani kuisimulia hii kwa mke wake,na hadhani kama atakuja kuisema kwa watoto wake.Imebaki kuwa fundo la siri katikati ya mifupa ya kifua chake.

Hii ni habari ya rafiki kipenzi,mjelajela wa kubaka!Ambaye hata kwa uso na sura yake,hudhani kuwa anaweza kutamani kubaka, achilia mbali hata kubaka kwenyewe.Haki mbinguni,duniani ni ubatili.

Video..Zari na Diamond Wajirekodi Video Wakipeana Mapenzi Mubashara Mchana Kweupee..+18

Miujiza ya Shekh Sharifu Rashid Kutoka Bagamoyo , Anarudisha Mapenzi na Kusafisha Nyota

$
0
0

MIUJIZA YA SHEKH SHARIFU RASHID KUTOKA BAGAMOYO PWANI, (RUDISHA MAHUSIANO YAKO NDANI YA MASAA 48 TU) ASANTE KWA KUENDELEA KUMPIGIA SIMU SHEKH SHARIFU RASHID KWA WALE WENYE MATATIZO NA WALE WANAOTOA SHUKRANI:

SHEKH SHARIFU RASHIDI ni mtaalamu wa tiba mbalimbali za asili, anatumia kitabu cha quran, dawa za asili, dawa za kiarabu na majini, anazo dawa za mapenzi, nguvu za kiume, chango, ngiri maji na n.k, anakuvutia mpenzi alie kuacha au alie mbali, pia anatoa pete za bahati zilizoambatanishwa na jini mali kulingana na nyota yako, anaouwezo mkubwa wa kutumia jina la muhusika kwa kutatua tatizo lako, anaouwezo wa kumrudisha mtu aliepotea kimiujiza, pia anatibu kwa njia ya simu popote ulipo,

WASILIANA NAE KWA SIMU NA WHATSAPP NO: 0718-668347. 0685-224047, 0767-204308 au follow@shekh_sharifu_rashid, Email:shekhsharifurashid@gmail.com

Jifunze Zoezi Lenye Kuufanya Uume Usimame kwa Muda Mrefu na Kuchelewa Kukojoa Wakati wa Kufanya Mapenzi..!!

$
0
0

Misuli inayohusika na nguvu za kiume na kuwahi kumaliza wakati wa tendo la kufanya mapenzi huitwa ”puboccugeous Muscle” maarufu inajulikana kama Pelvic Muscle. Misuli hii inapokuwa dhaifu,uwezo wa kusimamisha uume kwa muda mrefu na kuchelewa kukojoa wakati wa kufanya mapenzi huwa mdogo.

Zoezi lenye uwezo wa kuongeza nguvu ya misuli ya uume ,linaloweza kuufanya uume kusimama kwa muda mrefu,bila kusinyaa wala kuchoka,hili ni zoezi kama mfano wa zoezi lolote la kunyanyua vyuma vizito ambalo husaidia misuli kuinuka ,kukua na kuongezeka ukubwa na nguvu.

ZOEZI LA KWANZA
Wataalam wa mambo ya mapenzi wamethibitisha zoezi la misuli ya uume liitwalo ”physiotherapy”ndiyo hurudisha uwezo wa nguvu za kiume za asili,zoezi hili halina madahara yoyote kiafya na linaweza kufanyika wakati wowote.

JINSI YA KUFANYA ZOEZI HILI
Ukiwa umekaa popote fanya zoezi hili asubuhi na jioni na hali ya kuwa hauna mkojo kabisa(yaani kojoa kwanza)

Ukiwa umekaa anza kujibinya kama mtu aliyebanwa na mkojo halafu choo kipo mbali,bana ili mkojo usikutoke kwa kukaza misuli hiyo ya sehemu nyeti,fanya mara 20>25 asubuhi na jioni kila unavyobana hesabu 3 mpaka 5 kisha unaachia,unabana tena hivyo hivyo.

Endelea na zoezi hilo kiasi cha wiki,baada ya wiki mbili ongeza ubanaji zaidi kutoka mara 20 mpaka 70. Endelea kufanya zoezi hili kwa wiki 6 na matokeo mazuri huanza kuonekana wiki ya 4 mpaka 6

FAIDA YA ZOEZI HILI
1.Husaidia mzunguko wa damu kuingia kwenye uume na kuufanya uume utanuke na kuwa mgumu zaidi

2. Misuli ya uume itakuwa imara na kuweza kuzuia shahawa na hivyo kukuwezesha kumridhisha mwenza wako kila mara

3. Litakuwezesha kujibana kila unapotaka kukojoa huwapo kwenye tendo la ndoa(usingoje mpaka utamu umezidi utashindwa)jibane kama unajizuia kukojoa mkojo wa kawaida lakini usikate kiuno wakati mwenzio anaendelea kutingisha nyonga.

Ikiwezekana hata fikra za utamu huo zihamishe kwa sekunde kadhaa mpaka hali hiyo ya kutaka kukojoa ikiondoka zirudishe fikra ili kuendelea na mwenzio kwa pamoja katika game hilo la kiutu uzima.

Kasi iendelee na utaendelea hivyo mpaka uhakikishe mwenzio amekojoa ,na anaweza kukojoa hata mara 3,yaani ukiridhika kuwa mwenzio ameridhika au ukiskia ile sauti “”inatoosha” ndyo sasa nawe ukojoe hapo mwenzio atapata raha zaidi.

ZOEZI LA PILI
Uinue juu na kuushusha uume wako,uchezeshe juu chini,chini juu mara 5 mpaka 10,fanya mara mbili tatu huku unapumzika kidogo,uwe unaminyaminya kidogo wakati huohuo unavuta hewa kwa pua na kuitoa kwa mdomo.
fanya zoezi hili mara kwa mara japo mara 3 kwa wiki linaweza kukusaidia kuimarisha misuli yako ya uume.

ZOEZI LA TATU
Ufanyaji wa tendo la ndoa mara kwa mara huimarisha moyo,ubongo na misuli ya uume ,wanasayansi wamelithibitisha hili kuwa ufanyaji wa mara kwa mara husaidia uume kupata nguvu(zipo tofauti kati ya uwezo wa mwanamme mwenye mke mmoja na mwenye wake wengi)

Mwenye wake wengi anaongeza nguvu zaidi, Mwenyez Mungu anataka wanaume wa kiislam waimarishe misuli hii kwa kutoa fursa ya kufanya tendo la ndoa mara kwa mara pale alipowaamrisha waoe kuanzia wake wawili mpaka wanne wakiweza.

Kadri unavyoongeza mke ndivyo unavyojiongezea uwezo kwa aliyeoa wake wawili na zaidi,pima uwezo uliokuwa nao ulipokuwa na mke mmoja kisha zitazame nguvu hizo baada ya kuongeza mke wa pili watatu na wanne

Ndiyo maana utakuta mtu mwenye wake wawili akifiwa na mmoja huongeza mke ili kuziba pengo hilo. 

Lissu Agoma Kula Hadi Afikishwe Mahakamani..!!

$
0
0

Wakati Mbunge wa Singida Mashariki (Chadema), Tundu Lissu akigoma kula hadi afikishwe mahakamani, wakili wake amepeleka maombi Mahakama Kuu kuomba apewe dhamana baada ya polisi kuendelea kumshikilia kwa siku ya tatu.

Wakili wa mbunge huyo, Peter Kibatala alisema mteja wake amefikia hatua hiyo, baada ya Jeshi la Polisi linalomshikilia kumnyima dhamana bila sababu.

“Hakuna sababu za msingi za kumnyima dhamana na tangu jana Lissu hajala na amesema hatakula hadi afikishwe mahakamani,” alisema Kibatala na kuongeza:

“Kosa analodaiwa kulifanya lilifanyika Januari 4 na hadi Februari 6 ni mwezi, kama ni muda wa kuchunguza kosa hata hati ya mashtaka ingekuwa tayari,” alisema Kibatala.

Alisema mteja wao (Lissu) analalamikia kuanzia ukamatwaji wake ulipoanza, alipokamatwa eneo la Bunge bila Spika kuwa na taarifa.

Kibatala alisema polisi waliokwenda kumkamata aliwatambua njiani na alikamatwa bila kuwapo kibali cha kukamata (arrest warrant).

Tumbua Tumbua ya JPM Yarudi Tena,Safari Hii Amemtum,bua Kigogo Huyu wa Wizara ya Fedha..!!!

$
0
0

Rais John Magufuli amemsimamisha kazi Kaimu Katibu wa Tume ya Mipango (Wizara ya Fedha), Florence Mwanri aliyeidhinisha kuanza kwa awamu ya pili ya ujenzi wa jengo jipya la Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) (Terminal 3) kabla ya kumalizika kwa awamu ya kwanza.

Rais Magufuli alifikia uamuzi huo baada ya kufanya ziara ya kushtukiza katika mradi wa ujenzi wa jengo jipya na kuagiza shughuli za ujenzi wa uwanja huo ziendelee kuanzia leo.

Katika ziara aliyoifanya jana ilielezwa kuwa mkandarasi anayejenga uwanja huo,  kampuni ya BAM International alitangaza kusitisha ujenzi kuanzia jana kutokana na kutolipwa madai yake. Hata hivyo, Rais Magufuli ameahidi kulipa fedha hizo haraka.

Taarifa iliyotolewa jana na Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu, Gerson Msigwa ilieleza kuwa Rais Magufuli alisikitishwa na namna mradi huo unavyotekelezwa, ikiwamo Serikali kukubali gharama kubwa za mradi ambazo ni Sh560 bilioni kiwango ambacho ni kikubwa ikilinganishwa na jengo linalojengwa.

“Hivi kulikuwa na sababu gani za ninyi wataalamu wa Serikali kukubali gharama kubwa namna hii, hivi hili jengo linafanana na Sh560 bilioni? 

“Halafu mlikuwa na haraka gani kuidhinisha kuanza awamu ya pili ya ujenzi kabla ya kumaliza awamu ya kwanza?” alihoji Rais Magufuli.


Alimuagiza Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa kuunda timu ya wataalamu watakaofanya tathmini ya utekelezaji wa mradi huo ikiwa ni pamoja na kuzungumza na mkandarasi anayejenga uwanja huo na mhandisi mshauri ambao wamekubali kupunguza gharama za ujenzi wa mradi huo.

Lema Azidi Kukwamishwa Gerezani,Mahakama Yakomalia Pingamizi Lake..!!!

$
0
0

Mahakama ya Hakimu Mkazi Arusha, imetupa pingamizi la mawakili wa Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema la kuitaka isisikilize kesi ya kuhamasisha maandamano ya Ukuta, bali kwanza ifikishwe Mahakama ya Katiba.


Lema, ambaye ni mbunge kupitia Chadema, anakabiliwa na kesi hiyo akidaiwa kuhamasisha maandamano hayo ya chama chake yaliyokuwa yamepangwa kufanyika Septemba Mosi, mwaka jana.

Mawakili wa Lema, John Mallya na Sheck Mfinanga,  waliwasilisha ombi mahakamani hapo wiki iliyopita wakitaka kesi hiyo isikilizwe Mahakama ya Katiba kwa kuwa kuna hoja za kikatiba ambazo zitahitaji kutolewa maelezo na majaji watatu wa Mahakama hiyo.

Katika kesi hiyo, Lema anadaiwa kuhamasisha maandamano kwa njia ya mtandao wa kijamii (audio clip) aliyoitengeneza na kujirekodi ujumbe mfupi wa sauti na kisha  kusambaza  Agosti Mosi hadi 26, mwaka  jana katika mitandao ya kijamii ya WhatsApp.

Hakimu Bernard Nganga alisema kosa alilofanya Lema siyo la kikatiba na hoja za kutaka kuhamishiwa shauri hilo Mahakama ya Katiba hazina mashiko kisheria.

Alisema sheria ipo wazi, kuwa mtu yeyote akihusika na kushawishi utendaji wa kosa hata kama halina madhara, muhusika ana makosa na adhabu yake ni kifungo cha miaka miwili au kulipa faini.


Hakimu Nganga alisema pingamizi za utetezi zimetupwa na shauri litaendelea kusikilizwa.

Baada ya Mbowe na Lissu Kukumbwa na Kashkashi.Chadema Watoa Tamko Hili..!!!

$
0
0

Chama cha Demokrasia na Maendeleo(Chadema) kimesema muendelezo wa kukamatwa kwa viongozi wa chama hicho hakuwayumbishi bali kunawajenga kisiasa.

Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Vicent Mashinji amezungumza na waandishi wa habari  na kueleza kuwa suala hilo halitachukua muda mrefu kwenye utekelezaji.

"Hapa tunapoongea Mwenyekiti wa Halmashauri ya Tarime, Misiwa ameshikiliwa na jeshi la polisi," amesema Dk Mashinji.

Amesema Watanzania wanapaswa kukemea suala hilo kwa kupaza sauti zao zifike mataifa mbalimbali wafahamu ukiukwaji wa sheria.

Wabunge Wapinga Mbowe Kutajwa na Makonda,Zitto Kabwe Atoa Povu Hili..!!!

$
0
0

Hatua ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda kumtaja Kiongozi wa Upinzani bungeni, Freeman Mbowe kufika katika Kituo Kikuu cha Polisi jijini hapo kesho kuhojiwa, imewachefua baadhi ya wabunge.

Wabunge waliohojiwa mjini Dodoma jana, walisema kinachoendelea ni siasa badala ya uhalisia.

Mbunge wa Kigoma Mjini, (ACT – Wazalendo), Zitto Kabwe alisema kinachoendelea ni siasa za kuchafuana na kwamba Makonda ajiandae kubeba msalaba wake katika jambo hilo.

“Juzi hapa nililalamika bungeni kwamba leo wanakamatwa wasanii, kesho watakamatwa wabunge. Mmeona leo Makonda amemtaja Mbowe. Kinachoendelea ni siasa za kuchafuana. Kitendo cha Makonda kumtaja Mbowe maana yake ni kwamba kazi anayoifanya si yake, ni kazi ambayo ametumwa na wakubwa wake na ndiyo maana wanamuunga mkono,” alisema.

Zitto aliwataka wabunge wa upinzani bila kujali tofauti zao za vyama, kuliona suala la Mbowe kuwa si shambulio kwa mbunge huyo wa Hai pekee yake, bali ni mashambulizi dhidi ya wabunge wa upinzani. “Tukiliacha bila kulisemea maana yake kesho na keshokutwa kila mbunge wa upinzani anaweza kuonekana ni muuza dawa”.

Hata hivyo, Mbunge wa Muheza (CCM), Balozi Adadi Rajabu alisema anaamini hadi Makonda kuamua kumtaja Mbowe na watu wengine, atakuwa na ushahidi kwa sababu hawezi kufanya hivyo pasipo ushahidi. Balozi Adadi ambaye aliwahi kuwa Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI), alisema anaamini kabla ya kutangaza majina hayo, aliwasiliana na Jeshi la Polisi kwanza.

Lakini Mbunge wa Kawe (Chadema), Halima Mdee alisema wameamua kumchukulia Makonda kama mtu anayetumwa, huku akisema Jeshi la Polisi limemwachia mkuu huyo majukumu yake.

Kimenuka Bungeni..Wabunge Washindwa Kumvumilia Makonda Wapitisha Azimiio la Kumwita Bungeni Ili na Yeye Akahojiwe Mbele ya Bunge..!!!

$
0
0

Bunge limepitisha kwa kauli moja, azimio la kuitwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul  Makonda na Mkuu wa Wilaya ya Arumeru, Alexander Mnyeti ili kuhojiwa na Kamati ya Haki, Kinga na Madaraka ya Bunge.

Azimio hilo lililopitishwa leo lilitokana na hoja iliyowasilishwa na Mbunge wa Ukonga, Mwita Waitara akisema wateule hao wa Rais wametoa kauli zinazodhalilisha hadhi ya mhimili huo wa Dola.

Akijibu swali kuhusu tuhuma dhidi yake zilizoibuliwa na wabunge kuhusu chanzo cha mali zake, Makonda aliwaambia waandishi wa habari kuwa wakati mwingine watunga sheria hao hulala bungeni kwa kukosa cha kuzungumza.

Kutokana na wabunge kukerwa na kauli ya Makonda, mbunge wa Mkuranga (CCM), Abdallah Ulega aliomba mwongozo kuhusu suala hilo.

Mkuu wa wilaya, Mnyeti anadaiwa kuandika kwenye ukurasa wake wa Facebook kuwa wabunge ni wapuuzi kutokana na michango yao wakati walipohoji hatua ya Ma-DC na Ma-RC kutoa amri za kuwaweka mahabusu viongozi wa kisiasa.

Pitia Vichwa vya Magazeti ya Leo 9/2/2017..!!!

Daktari wa Macho Atoa Ushahidi Mzito ‘Kesi ya Scorpion Mtoboa Macho’...!!!

$
0
0

Shahidi wa nne katika kesi ya unyang’anyi wa kutumia silaha na kujeruhi inayomkabili Salum Njwete, ameieleza Mahakama kuwa mtu aliyehusika kumtoa macho Said Mrisho alikuwa ni mzoefu wa vitendo hivyo  na siyo wa kawaida.

Shahidi huyo, Dk Christine Mataka (52) ambaye ni daktari  bingwa  wa macho kutoka Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH), alitoa maelezo hayo katika Mahakama ya Wilaya ya Ilala alipotoa ushahidi dhidi ya mshtakiwa Njwete (34) katika kesi iliyopata umaarufu wa ‘kesi ya Scorpion’ kutokana na maelezo kwamba aliyefanya uhalifu huo ni Scorpion.

Akiongozwa na Wakili Mwandamizi wa Serikali, Nassoro Katuga, Dk Mataka kutoka kitengo cha macho alidai ilikuwa mara yake ya kwanza kuona mgonjwa aliyepelekwa Muhimbili akiwa hana vipande vya gololi za macho yote mawili.

Dk Mataka alidai mlalamikaji Said aling’olewa macho kwa kutumia kitu kikali kilichojikunja mbele ambacho kinaweza kutoa mboni ya jicho nzima bila kubaki kitu chochote.

Mbele ya Hakimu Mkazi, Flora Haule alidai kwa kawaida wagonjwa wanaopasuka jicho huwa wanakuwa na mabaki  au vipande vya gololi ya macho.

Wachezaji wa Simba Wakerwa Na Mapozi Ya Jonas Mkude,Waamua Kumchana Live Mbele ya Omog..!!!

$
0
0

Huku kikosi cha Simba, leo hii kikitarajia kuingia kambini kujiandaa na mechi yake ya Jumamosi dhidi ya Prisons ya jijini Mbeya, balaa jipya limeibuka ndani ya kikosi hicho linalomhusu nahodha wa timu hiyo, Jonas Mkude.

Baadhi ya wachezaji wa timu hiyo wanadaiwa kumtaka kocha mkuu wa timu hiyo, Mcameroon, Joseph Omog kumpokonya Mkude cheo cha unahodha wa klabu hiyo kutokana na vitendo vyake vya utovu wa nidhamu ambavyo amekuwa akifanya kila wakati klabuni hapo.

Wachezaji hao wamefikia hatua hiyo baada ya kutofurahishwa na kitendo cha Mkude cha kutojiunga na timu hiyo katika safari ya kwenda mkoani Songea kwa ajili ya mechi ya Ligi Kuu Bara dhidi ya Majimaji pasipo kuwa na sababu zozote za msingi.

Habari za kuaminika kutoka ndani ya Simba ambazo  zimedai kuwa kutokana na hali hiyo Omog amewataka wachezaji hao kutulia na kuwahakikishia kuwa atalifanyia kazi suala lao hilo na kwa kuanza kumpa nafasi ya kucheza dhidi ya Prisons siku ya Jumamosi kwenye Uwanja wa Taifa, jijini Dar es Salaam.

“Wachezaji wengi hawafurahii kabisa tabia ya Mkude kwani hata leo hii (jana) katika mazoezi yaliyofanyika kwenye Uwanja wa Chuo Kikuu cha Polisi, Kurasini ameelezwa.

“Wamemwambia kuwa hawafurahii kuendelea kuongozwa na nahodha ambaye ndiye kinara wa utovu wa nidhamu ambaye amekuwa hana uchungu na timu na wakamkumbishia matukio yote kama hilo kukacha kwenda Songea pasipo sababu yoyote ya msingi lakini pia alifanya hivyo wakati tulipokuwa tunakwenda Zanzibar katika michuano ya Kombe la Mapinduzi.

“Hakuambatana na timu na kuja siku iliyofuatia peke yake jambo ambalo lilimfanya kocha ampige benchi katika mechi ya kwanza ya michuano hiyo,” kilisema chanzo hicho cha habari.

Alipotafutwa Omog ili aweze kulizungumzia suala hilo hakupatikana kutokana na simu yake ya mkononi kuita bila ya kupokelewa.

Afande Sele: Tafsiri ya Wasafi Wataonekana Wachafu Imeonekana Kwenye List Mpya ya Makonda...!!!

$
0
0

Msanii wa muziki wa hip hop kutoka Morogoro Afande Sele amesema leo tafsiri ya msemo wake ‘wasafi wataonekana wachafu’ ambayo aliitoa siku za karibuni baada ya mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Paul Makonda kutangaza awamu ya kwanza ya majina ya watu ambao wanatuhumiwa kujihusisha na matumizi ya Madawa ya kulevya.

Kauli hiyo ilitafsiriwa vibaya na mashabiki wa Diamond wengi wakidhani mkongwe huyo naye naamini kwamba WCB wapo kwenye sakata hilo.

Kupitia list mpya ya RC Makonda ambayo ameitoa leo na kutaja majina ya watu wakubwa akiwemo Yusuph Manji, Mchugaji Mwajima, Iddi Azzan na wengine, Afande Sele ameweka bayana nini alikuwa anakimaanisha kwenye kauli yake hiyo.

“Juzi kati niliposema kuwa kwenye hili sakata la MAPAPA na MAPUNDA wa’Unga’kama kweli braza Paul yupo’serious’….basi hata wale WASAFI wataonekana WACHAFU….wenye akili zao timamu walinielewa vyema….lkn vibichwa panzi walitafsiri kiudaku na kichonganishi tu wakimaanisha neno wasafi na wale wasafi wao wa mbagala…nadhani sasa tumeanza kuelewana…..NAONA MBALI KWA DARUBINI KALI…..wacha ‘parry’iendelee,” aliandika rapper huyo Instagram.

Hivi Ndivyo 50 Cent Alivyoipaisha Video ya Diamond Platnumz na Ne-Yo...!!!

$
0
0

Tovuti ya thisis50.com ilianzishwa na idara mpya ya habari iliyo chini ya Rapper maarufu wa Marekani 50 Cent mwaka 2007 kwa lengo la kuendeleza na kusambaza habari za utamaduni wa pop na hiphop

Mwimbaji Mtanzania Diamond Platnumz ameingia kwenye rekodi ya kuwa msanii wa kwanza Mtanzania video yake kuwekwa kwenye tovuti hiyo kupitia single yake mpya aliyomshirikisha Mmarekani Ne-Yo ‘Marry You”

Dogo Ahaha Kumuokoa Wema Polisi,Adai Yuko Tayari Kwa Lolote kwa Kuwa Anamahaba Naye..!!!!

$
0
0

Wakati hali ikiwa bado tete kwa Miss Tanzania 2006, Wema Sepetu ambaye anashikiliwa katika Kituo Kikuu cha Polisi Kati jijini Dar, dogo mmoja anayekadiriwa kuwa na umri wa miaka kati ya 12-16, aliyejitambulisha kwa jina la Hamisi Bruno, ameonekana akihaha vibaya kituoni hapo akitaka kumuokoa muigizaji huyo nyota aliyedai ni rafiki yake, Risasi Mchanganyiko lina mkanda mzima.

HIVI NDIVYO ILIVYOKUWA

Juzi Jumatatu, timu ya waandishi wetu ilipiga kambi katika kituo hicho tangu alfajiri, kwa ajili ya kutaka kushuhudia wasanii wengine waliotajwa na Mheshimiwa Paul Makonda, kwa kudaiwa kujihusisha na madawa ya kulevya wakiwasili kituoni hapo kwa ajili ya kuhojiwa.

Waliotarajiwa kuwasili ili kuhojiwa ni msanii wa Bongo Fleva, Winfrida Josephat ‘Recho’, Video Queen Tunda na staa mwingine mkubwa, Vanessa Mdee maarufu kama Vee Money.

Lakini baada ya kuwashuhudia Recho na Tunda wakiwasili kituoni hapo mapema asubuhi, kila mmoja akitegemea kumuona Vee Money, majira ya saa sita mchana, dogo huyo, alionekana kuingia kituoni hapo na kuvuta hisia za watu wengi.

ASIMAMISHWA, AWAIMBISHA POLISI

Akiwa ameweka mikono yake mifukoni na akitembea taratibu kulifuata lango la kuingilia sentro, dogo huyo alijikuta mikononi mwa polisi, waliotaka kujua wapi anakwenda na kufanya nini.

Dogo huyo aliwaambia polisi hao ambao walikuwa wameweka ulinzi mkali, kuwa alikuwa anahitaji kumuona na kumsalimia rafiki yake, Wema Sepetu na kwamba alitaka pia kuangalia uwezekano wa kumsaidia kutoka kwenye sakata hilo.

“Duu yaani huyu dogo wala hana wasiwasi, maana kuna wengine hapa watu wazima kabisa lakini hawana uthubutu kabisa wa kusogea hata pembeni ya polisi lakini yeye kaenda kukabiliana nao,” alisikika akisema mmoja wa watu waliokuwa wamejazana kituoni hapo.

ARUHUSIWA, AINGIA NDANI

Baada ya kujieleza, polisi waliokuwa wameimarisha ulinzi eneo la sentro hawakuwa na hiyana, walimruhusu kuingia mapokezi, ambapo alipoeleza pia shida yake, aliruhusiwa kwenda kumuona muigizaji huyo nyota ambaye kwa siku tano sasa, amesota rumande akituhumiwa kujihusisha na madawa hayo ya kulevya yanayomaliza nguvu kazi kubwa ya vijana wa Kibongo.

ATOKA NA CHUPA YA SODA

Dakika kumi baada ya kuwa ameruhusiwa kwenda kumsalimia rafiki yake huyo, mtoto Hamisi alitoka nje ya kituo hicho akionekana kuwa na uso wenye bashasha, huku mkononi mwake akiwa amebeba chupa tupu ya soda.

Katika hali ya kufurahisha zaidi, mtoto huyo alikataa kuzungumza, akiwapa watu ishara ya kuomba njia ili aende anakojua mwenyewe.

AREJEA…

Baada ya muda kidogo, kijana huyo aliyegeuka kuwa kivutio kituoni hapo, alirejea akiwa amebeba soda kwenye mkoba na haikuweza kufahamika ni ya aina gani, akaingia zake ndani.

ATOKA, RISASI LAMBANA

Baada ya kuingia kituoni kwa mara nyingine kwa ajili ya kupeleka soda hiyo, Risasi Mchanganyiko lilimsubiri alipotoka akiwa ameongozana na shoga mpya wa Wema Sepetu, Jike Shupa na kumtaiti, likitaka kupata mawili matatu kutoka kwake.

“Ninashukuru sana kupata nafasi ya kuonana na Wema, tena bila kipingamizi chochote, kwa kuwa ni rafiki yangu tangu 2016.

“Yaani japokuwa nina majonzi makubwa, lakini namshukuru sana Mungu, kuweza kumuona na nimempelekea soda aliyokuwa ameitaka na bado naendelea kumuombea ili aweze kutoka kwa sababu tangu akamatwe mimi sina raha kabisa,”alisema dogo huyo.

Meya wa Ubungo Amtaka Mbowe Kuwaruhusu Bavicha Kupambana an Polisi na Watawala,Amwambia Mbowe Wanangoja Amri Yake Tu Waanze Kazi..!!!

$
0
0

Dear 
Freeman Aikael Mbowe.

Salaamu na baada ya salamu,pole na mapambano ya kutufikisha "Canaan" kupitia ukombozi wa pili wa Taifa hili... Najua fika ujasiri na uimara wako wakati wote,sitishwi wala sijawahi kuwa na wasiwasi juu ya maamuzi na kila hatua unayopiga kuelekea mbele.

Ndiyo maana nipokuwa upande mmoja na wewe sitishwi na upepo wa kisulisuli,wala mvua za mabarafu,kwa kuwa najua ulivyosimama imara dhidi ya dhoruba na vimbunga,vya kusi na tonadozi

Walipokupokonya vitega uchumi vyako ulicheka huku mikono umeweka mifukoni,ukatuduwaza na kutuacha tukibubujikwa na machozi,walipokuja kujachufua hotel yako na ukwepaji kodi,ulituambia umechoka kuonewa huruma na kama hayupo tayari kukutana na haya tuachane na siasa za upinzani Africa,wiki baadae tunaona wamekufuata mpaka kwenye bustani za mchicha na nyanya,

Mimi na vijana wenzangu tulinyamaza kimya safari hii tukiogopa kufokewa tena na wewe,na baadae tulikumbuka maneno yako ambayo ulikuwa ukitusisitiza kuyakumbuka wakati wote. "Ni kweli wanaotutesa si wengi kama sisi tunaoteswa,ila kuingiza nguvu wakati huu no kihatarisha maisha ya wanyonge walioupande wetu,kwa nini tusisubirie watesi wetu wakiwa mahala salama kwetu,kuepusha maafa"

Na kwamba jeshi zuri si lile linaloshinda vita tuh,bali ni lile linaloshinda vita bila umwagaji damu na upotevu wa rasilimali zake nyingi,ingawa siku zote vita huacha wahanga.

Dear Freeman Aikael Mbowe,nasubiria kwa hamu command yako ya kusongambele,na nijaua si mimi tuh,nakuhakikishia vijana wenye utayari ni zaidi ya mamillioni,waona jeshi la adui lipo nje ya geti letu je na kuanza kuitikisa ngome yetu? Tuendelee kusubiria sauti yako kuu dhidi yao?

Vijana wako tupo tayari kukulinda kwa gharama yoyote hata kama ni damu na uhai wetu,ili makusudio ya ukombozi wa Taifa hili yafikie kama ilivuokusudiwa.

Marehemu mawazo,alipata kusema "wanaotudhalilisha na kututesa sana wanatuharakisha sana,kufika tunapo elekea"

Tabia za vyombo vya dolla ni zilezile tuh,kizazi na kizazi avitoamka na kuwa upande wetu milele

Je tuendelee kusubiria lingine zaidi ya hili au wakati ni sasa,? Askari wako Mtiifu
BONIFACE JACOB
senior councillor UBUNGO
MJUMBE KAMATI KUU CHADEMA

Breaking News..Wema Sepetu Afikishwa Mahakamani na Kupewa Dhamana..!!!

$
0
0

Hatimaye wema sepetu apata dhamana kwa mashtaka yaliyomfikisha kisutu mbele ya mh. Simba.

Wema alikua akiwakilishwa na wakili Msando.

Kesi imepangwa kwa kutajwa tarehe 22/2
Viewing all 104670 articles
Browse latest View live




Latest Images