Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104416 articles
Browse latest View live

U HEARD: Irene Uwoya afafanua ishu ya kupenda wenye sura mbaya

0
0
Baada ya mwigizaji Irene Uwoya kusema kuwa anapendelea zaidi kuwa na wanaume wenye sura mbaya, leo kupitia XXL ya clouds FM, Soudy Brown amepiga naye stori na ameifafanua zaidi kauli kauli.

‘Nawapenda wanaume wenye sura mbaya kwa sababu wanajua mapenzi na wanaogopa kuachwa, mtu mwenye muonekano mzuri yuko busy na kujitengeneza lakini mbaya yeye mkiwa sehemu akili inakuwa pale’;-Iren Uwoya

Bonyeza play hapa chini kusikiliza Full Stori:

Miujiza ya Shekh Sharifu Rashid Kutoka Bagamoyo , Anarudisha Mapenzi na Kusafisha Nyota

0
0

MIUJIZA YA SHEKH SHARIFU RASHID KUTOKA BAGAMOYO PWANI, (RUDISHA MAHUSIANO YAKO NDANI YA MASAA 48 TU) ASANTE KWA KUENDELEA KUMPIGIA SIMU SHEKH SHARIFU RASHID KWA WALE WENYE MATATIZO NA WALE WANAOTOA SHUKRANI:

SHEKH SHARIFU RASHIDI ni mtaalamu wa tiba mbalimbali za asili, anatumia kitabu cha quran, dawa za asili, dawa za kiarabu na majini, anazo dawa za mapenzi, nguvu za kiume, chango, ngiri maji na n.k, anakuvutia mpenzi alie kuacha au alie mbali, pia anatoa pete za bahati zilizoambatanishwa na jini mali kulingana na nyota yako, anaouwezo mkubwa wa kutumia jina la muhusika kwa kutatua tatizo lako, anaouwezo wa kumrudisha mtu aliepotea kimiujiza, pia anatibu kwa njia ya simu popote ulipo,

WASILIANA NAE KWA SIMU NA WHATSAPP NO: 0718-668347. 0685-224047, 0767-204308 au follow@shekh_sharifu_rashid, Email:shekhsharifurashid@gmail.com

Miezi Kadhaa Toka Ndege Zianze Kufanya Kazi,Majaliwa Aibua Madudu Haya Kwenye Shirika la Ndege la Tanzania..!!!

0
0

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ameagiza Shirika la Ndege Tanzania (ATCL), kujiridhisha na kiwango cha mapato linayokusanya kwa usafirishaji mizigo iwapo kiko sahihi.

Majaliwa amesema hayo alipotembelea makao makuu ya ATCL jijini Dar es Salaam kujionea utendaji tangu lilipoboreshwa mwaka jana kwa kununuliwa na Serikali ndege mpya mbili.

Waziri Mkuu amemtaka Kaimu Mkurugenzi wa Fedha na Utawala wa ATCL, Witness Mbaga kuhakikisha anatekeleza suala hilo.


Pia, ametakaka viongozi wa shirika hilo kuhakikisha wanazingatia ratiba za njia na muda wa safari ili wasipoteze wateja.

Vievile amesema ataagiza uchunguzi ufanywe na Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) utakaolenga kujua ukusanyaji mapato katika kipindi hicho.

Waziri Mkuu akasema Serikali haitakuwa tayari kushuhudia shirika hilo linakufa tena na kuwataka viongozi wahakikishe linaendeshwa kwa faida kwa manufaa ya Taifa.

Makonda Apingwa Kila Kona,Wabunge Waungana na Mawaziri Kumuwajibisha Ipasavyo..!!!

0
0

SIKU chache baada ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda, kutaja watuhumiwa 65 katika vita dhidi ya dawa za kulevya, Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), kimesema haki zimekiukwa katika utajaji majina.

Mbali na LHRC baadhi ya wanaharakati wameungana na kituo hicho kukosoa utaratibu uliotumiwa na Makonda.

Akizungumza na gazeti hili jana, Mkurugenzi wa LHRC, Dk Hellen Kijo-Bisimba alisema kutangaza majina ya watu kwa kuwahusisha na dawa za kulevya bila uchunguzi, ni kinyume na  haki za binadamu na kuchafua majina yao kwa vile hakuna  uthibitisho wa kuwahusisha na tuhuma hizo.

Alisema hayo baada ya mwandishi wa habari hizi kumtaka azungumzie mazingira ya kutaja majina ya watuhumiwa kwa kulinganisha na misingi ya haki za binadamu.

Dk Bisimba alisema majina ya watu yalipaswa kutajwa kama Jeshi la Polisi nchini lingefanya uchunguzi wa awali na kupata uthibitisho na  Mahakama ndiyo yenye jukumu la kutoa haki kwa kutafsiri sheria na si kiongozi.

“Kama uchunguzi wa awali ungefanyika, suala la kutaja majina lingekuwa  sahihi, lakini  kutangaza bila upelelezi ni kinyume na sheria,” alisema.

Alisema Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Simon Sirro aliwahi kunukuliwa na vyombo vya habari akisema walipata kupokea majina ya uongo, hivyo ni hatari kutangaza jina la uongo kisheria.

Wakili wa Kujitegemea, Nassor Kitugulu alisema ni jambo la kushangaza mtu kutaja mbinu za adui, hiyo ni dalili kuwa vita hiyo ni ngumu bila ushirikiano.

Alisema iwapo Serikali imedhamiria kupambana na dawa za kulevya nchini baada ya kutambua njia zinazotumiwa, ilipaswa kuweka mitego ya kunasa watuhumiwa.

“Tunajua kuwa dawa za kulevya zinapoteza nguvukazi, lakini utaratibu wa kutangaza bila uthibitisho wa tuhuma ni kuchafua sifa ya mtu kwenye jamii,” alisema.

Naye Fidelis Butahe anaripoti kutoka Dodoma, kwamba Bunge juzi usiku liliweka historia kwa kupitisha maazimo manne, yakiwamo ya kumtaka Makonda na Mkuu wa Wilaya ya Arumeru, Alexander Mnyeti kuhojiwa na Kamati ya Bunge ya Haki, Kinga na Madaraka ya Bunge na ikibainika wana makosa mamlaka zao za uteuzi ziwawajibishe.

Wateule hao wa Rais wanadaiwa kutoa kauli za kudharau Bunge takribani siku tatu zilizopita na kuamsha hisia za wabunge waliotoa kauli za kuwakemea bungeni.

Kwa sakata hilo, Mbunge wa Ukonga, Mwita Waitara (Chadema) aliwasilisha hoja ya kutaka washughulikiwe, ambayo ilijadiliwa kuanzia saa 1.30 usiku hadi saa 2.15 usiku na kuungwa mkono na wabunge wote, wakiwamo mawaziri kwa kusema “ndiyo”.

Wakati wa mjadala wa hoja hiyo, Mbunge wa Bunda, Esther Bulaya (Chadema) alieleza jinsi Makonda alivyompigia simu kumweleza kuwa atawashughulikia wabunge, kwa sababu yuko karibu na ‘Bwana mkubwa’, huku Joseph Msukuma (Geita Mjini-CCM) akitangaza vita na Mkuu huyo wa mkoa.

Ilikuwa kama sinema bungeni, kutokana na wawakilishi hao wa wananchi kuonekana kama wabunge wa chama kimoja, walipotoa hoja zao kupinga kauli hizo, huku Mwenyekiti wa Bunge, Andrew Chenge akiwaongoza kufuata kanuni za chombo hicho katika mjadala huo.

Maazimio hao ni; Makonda na Mnyeti kuitwa mbele ya Kamati, Waziri wa Tamisemi kutoa maelekezo kwa wakuu wa mikoa na wilaya namna ya kufanya kazi zao bila kuingilia mihimili mingine.

Pia, mamlaka nyingine zikimhitaji Mbunge kwa mashitaka ya aina yoyote lazima zimjulishe Spika wa Bunge na mamlaka ya kinidhamu kuwawajibisha wateule hao wa Rais ikibainika wametenda kosa la kudharau chombo hicho.

Ilivyokuwa

Akiwasilisha hoja hiyo usiku baada ya kipindi cha asubuhi kutoruhusiwa na Chenge kwa maelezo kuwa alitaka kujiridhisha kama Mbunge huyo alizingatia kanuni, Waitara alisema Mnyeti ameonekana katika mitandao ya kijamii akisema wabunge hawajielewi.

“Haya mambo ndiyo yamejirudia wakati nikiangalia televisheni ya Clouds, Makonda akionekana akisema sisi humu bungeni tunasinzia,” alisema Waitara.

Alibainisha kuwa kwa mujibu wa Katiba ibara ya 63(2), Bunge ndicho chombo kikuu kwa niaba ya wananchi, kuisimamia na kuishauri Serikali na linapitisha bajeti inayotumiwa na wateule hao wa Rais.

Alisema si sawa kwa wakuu wa mikoa na wilaya kuwaweka rumande wabunge, madiwani na watumishi wa Serikali.

“Bunge linaingia katika majaribu makubwa ya kudharauliwa. Tunakula kiapo humu, tuamue kwa niaba ya Watanzania, lakini Mkuu wa Wilaya anasema hawa ni wapuuzi na Mkuu wa Mkoa anasema hawa wanalala tu,” alisema.

Baada ya hoja hiyo, Waitara alitaka ijadiliwe na Bunge na kutoa maazimio ili kurejesha heshima ya chombo hicho, hoja ambayo Chenge aliipokea na kutoa nafasi kwa wabunge wanne, kujadili kutokana na ufupi wa muda.

Mbunge wa Ulyankulu (CCM), John Kadutu alisema: “Nimehuzunika sana  wabunge tunafika mahali tunadharauliwa, halafu watu tunaangalia tu. Haya ambayo yametokea kwa Makonda na Arumeru, pia yametokea Manispaa ya Dodoma. Mkurugenzi anaongea na wabunge kama watoto.

“Mimi nadhani hata ile sheria ya Marekani wenzetu wanaoteuliwa kwa ngazi za juu lazima wapelekwe bungeni, hapa kwetu ingefaa kuletwa ili watu wa aina hii tuweze kuwamaliza hapa hapa. Wapo wanaodhani wako juu yetu.”

Alisema ni jambo la hatari kujenga Serikali yenye kiburi na kusisitiza: “Unapotaka kutoa pepo halibembelezwi. Unataka kupunga majini huwezi kubembeleza. Lazima ukazane kupunga jini litoke. Hatuwezi kutoa pepo kwa lugha nyepesi nyepesi (akipunguza sauti) pepo toka, haiwezekani. Kama ni pepo tulikemee litoke.”

Bulaya alibainisha jinsi Makonda alivyompigia simu na kutamba kushughulikia wabunge kwa kuwa yeye yuko karibu na ‘Bwana mkubwa’, huku akisisitiza kuwa Mkuu huyo wa Mkoa hakutengezwa kuwa kiongozi.

“Makonda alinipigia simu na kunitisha kwamba yeye yuko karibu na Bwana mkubwa, atatushughulikia wabunge. Alisema ataanza na Msukuma, Halima Mdee (Kawe-Chadema), Esther Matiko (Tarime Mjini-Chadema), Sugu (Joseph Mbilinyi-Chadema Mbeya Mjini) na Msigwa (Mchungaji Peter-Iringa Mjini-Chadema),” alisema.

Mbunge wa Ubungo (Chadema), Saed Kubenea alisema: “Ni lazima heshima ya Bunge ilindwe kwa gharama yoyote. Makonda anawapigia simu wabunge akitaja mmoja wa mawaziri kuwa ndiye anatuma wabunge wamtukane.”

Naye Msukuma alisema haiwezekani Makonda afanye kazi ya polisi na kuhoji aliko Mkuu wa Jeshi la Polisi, makamanda na makamishna wake.

“Makonda ni nani katika hii nchi? Kama Jairo (David-aliyekuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini) alitoka kwa azimio la Bunge, Makonda ni nani? Mimi niko tayari kupambana na Makonda,” alisema Msukuma.

Hoja hiyo pia ilitolewa ufafanuzi na Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG), George Masaju na Waziri Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Uratibu na Bunge, Kazi, Vijana na Watu wenye Ulemavu, Jenista Mhagama, wakitaka wahusika hao wasikilizwe kwanza na kuachia ngazi zingine iwapo watabainika kutenda kosa.

Chenge  

Baada ya wabunge kuchangia, Chenge alitoa nafasi kwa Waitara ambaye alihitimisha hoja hiyo na kutoa maazimio manne ambayo Mwenyekiti huyo wa Bunge aliyafafanua na kupitishwa.

“Ni kwamba Waziri wa Tamisemi atoe waraka kwa wahusika (wakuu wa mikoa na wilaya) kuwaeleza namna ya utekelezaji wa majukumu yao. Pili, wahusika waitwe kwenye Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge,” alisema Chenge.

“Endapo itaridhika, baada ya Kamati kuwasilisha taarifa bungeni na Bunge kuridhia kwamba kuna jinai, hasa sheria yetu ya Bunge inatoa madaraka kwa AG kufuatilia na vyombo vingine vya Dola,” alisema Chenge.

Alisisitiza: “Sisi hatuwezi kufika huko tunaishia katika haya yatakayoletwa na Kamati na suala la uwajibikaji linakwenda sambamba na hayo yatakayoletwa na Kamati.”

Alipolihoji Bunge kama linakubaliana na hoja hiyo, hali ilikuwa hivi; “mnaokubali hoja hii semeni ndiyo.” Wabunge wote waliitika “ndiyo” na aliposema wasiokubaliana na hoja hiyo waseme “siyo”. Bunge lilibaki kimya.

Baada ya Prof Lipumba Kumtaka Wayamalize,Maalim Seif Amjibu Lipumba Kwa Staili Hii...!!!

0
0

KATIBU Mkuu wa CUF, Maalim Seif Sharif Hamad, amesisitiza kuwa haoni sababu ya kukutana na Profesa Ibrahim Lipumba kuzungumzia mambo ya chama kwa kuwa si mwanachama halali wa CUF hivi sasa.

Taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari Dar es Salaam jana, ilisema Maalim Seif alitoa kauli hiyo kwenye ziara ya siku nne kwenye wilaya saba za mikoa mitatu ya Unguja.

Maalim alisema ataendelea kufuata taratibu za kisheria ili kuhakikisha chama kinamaliza moja kwa moja mgogoro aliodai umepandikizwa na CCM kupitia kwa Lipumba.

Alitaka wapenzi na wanachama wa CUF kuunga mkono jitihada   zinazofanywa na chama kupigania demokrasia ya kweli nchini.

Aliwataka wanachama wa CUF kushirikiana na viongozi wakuu wa CUF wanaotambuliwa na Baraza Kuu la Uongozi kujenga na kuimarisha chama hicho.

Alifafanua kuwa wakati anaendelea kuimarisha chama kupitia viongozi halali, ni vema wasiwe na wasiwasi na uamuzi walioufanya kwenye uchaguzi mkuu wa Oktoba 25 mwaka juzi kwa kuipa CUF ushindi wa urais wa Zanzibar kuwa hautapuuzwa.

Aliwataka kuendelea kuwa watulivu na kuwahakikishia kuwa siku chache zijazo haki yao itapatikana. "Nawahakikishia, tumepigana vya kutosha katika kudai haki yetu na tumefikia hatua nzuri za kupata haki yenu.

“Hatua ya wananchi wa Zanzibar ya kuipa ushindi CUF ni kutokana na CCM kushindwa kuongoza Wazanzibari kwa misingi ya haki, usawa na demokrasia,” alisema.

Alifafanua kuwa mgogoro wa uongozi ndani CUF uliotokana na hatua ya Profesa Lipumba kuamua kurudi katika nafasi ya uenyekiti wa chama hicho na kusema watahakikisha wanapata ushindi.

“Lipumba alijiuzulu mwenyewe hivyo hakuna hoja yoyote ya kisheria inayomwezesha kurudi tena katika nafasi hiyo,” alisema.

Maalim Seif ataendelea na ziara hiyo katika Wilaya ya Magharibi ‘A’, ‘B’ kisiwa cha Unguja, Pemba hadi Februari 24.

Pamoja na kufanya ziara hiyo na kuzungumza na viongozi wa chama na jumuiya zake, Katibu atafanya uzinduzi na uimarishaji wa waratibu wa chama.

Breaking News..Mbowe Atumbua Jipu la Madawa ya Kulevya ,Awataja Wahusika Wakuu Huku Akimwambia Makonda Asimchezee Ovyo(video)..!!!

0
0

Freeman Mbowe amesema hatafika polisi kwa kuitwa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda.
Amekanusha vikali tuhuma za kuhusika na biashara au kutumia madawa ya kulevya.

Anasema wao kama chama wanaunga mkono jitihada za mapambano dhidi ya dawa za kulevya.


Askofu Gwajima Afunguka Chanzo cha Utajiri Wake,Adai Analipwa Milioni 2.4 kwa Saa ..!!!

0
0

Mchungaji Josephat Gwajima ni mmoja wa watu waliotengeneza vichwa vya habari wiki hii baada ya kutajwa kwenye orodha ya pili ya mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam ya watu wanaotuhumiwa kuhusika kwenye biashara ya madawa ya kulevya.

Gwajima anafahamika kwa utajiri mkubwa kiasi cha kumiliki ndege, helikopta na kudai kuwa na mpango wa kununua treni. Utajiri wake umekuwa ukizusha maswali mengi na kupitia mkutano wake na waandishi wa habari Alhamis hii uliofanyika kanisani kwake, Gwajima alielezea vyanzo vyake vingine vya mapato.

“Cha kwanza mimi ni daktari wa philosophy, ni lecturer peke yake Tanzania kwa malecturer wa kidini ambaye husafiri kwenda kulecture nje ya nchi,” alisema.

“Lecture yangu moja nalipwa dola elfu moja, ambayo ni sawa sawa na milioni 2 na laki kama nne, moja ya saa moja. Nikienda kulecture Japan naweza kulecture miezi mitatu na mimi sijawahi kusafiri na hela mfukoni, hela zote zinakuja kwa benki mpaka hapa. Chini ya kanisa letu kuna kampuni zinaitwa Mahanai Organisations, ni makampuni makubwa.”

Gwajima ametii agizo la kwenda kuhojiwa kwenye kituo kikuu cha polisi jijini Dar es Salaam.

Imemfikia..na Haya Ndio Majibu:Diamond Afunguka Juu ya Mwanaume Aliyekuwa Anamsumbua Zari,Anasema Alimfanya Hivi Ili Kumkomesha..!!!

0
0

Pamoja na kumweka ndani na kumzalisha watoto wawili, Tiffah na Nillan, Diamond bado anakumbana na upinzani toka kwa wanaume vichwa nguvu wanaoendelea kujaribu bahati zao ili kumnasa Zari.

Akiongea kwenye kipindi cha Leo Tena cha Clouds FM Alhamis hii, Diamond alisema baada ya kuona mtu huyo amezidi, alimwambia Zari amchinjie baharini na kudai kuwa hakuwa na uzito wa kumfanya ‘apige simu Kigoma.’

“Kulikuwa na nyendo za mtu mmoja nilishasikia nikasema sasa mambo ya kusumbuana kupiga simu Kigoma tena ya nini. Zari akamblokia zake mbali,” alisema.

“Mwanzo kulikuwa na watu wanaojifanya wao wako karibu sana, kujifanya wao ndio wanamwelekeza ‘Diamond anafanya hivi na hivi.’ Yaani unajua kuna watu wengine wana mambo ya ushamba wanahisi wakikumaliza wanatengeneza nafasi zao. Lakini nikakaa nikasema, kwa suala hili dogo tena mtu mmoja tuanze kupiga simu Kigoma haitakuwa vizuri,” aliongeza.

Hata hivyo Zari na Diamond wamesema wamekubaliana kutoshika simu zao kwakuwa husababisha malumbano makubwa kutokana na wao kuwa watu maarufu.

Young Dee Avamiwa na Kuibiwa Simu na Pochi, Amtuhumu Van Dame

0
0
Msanii wa muziki wa hip hop, Young Dee amefunguka kwa kudai kuwa usiku ya juzi alivamiwa na mtu anayedaiwa kuwa ni Van Damme wa Sinza ‘Damme’ na kuporwa simu pamoja na pochi yake ambayo ndani ilikuwa na vitambulisho mbalimbali.


Rapper huyo ambaye anafanya vizuri na wimbo ‘Young Daddy’ ameomba kwa yeyote atakaye okota kitambulisho chake atoe taarifa.

Usiku Wa kuamkia juzi, tulivamiwa na jamaa anaesemekana ni Dame Wa sinza, nikiwa nimekesha studio maeneo ya sinza palestina kwa Mr T Touch,” aliandika Young Dee Instagram.

Aliongeza,
“Sasa juhudi za kumpata zimekua ngumu maana amekua na matukio ya hivo mara kwa mara juzi kaiba simu mbili moja ni yangu (iphone6s+) na Samsung na wallet yangu iliyokua na vitambulisho vyangu pamoja na Card ya bank, Sasa kwa yoyote ataepata taharifa itayoweza kunisaidia naomba anifate Dm tafadhari! 🙏 Tag wana wote Wa sinza tusaidiane kwa hili!,”

Ubuyu wa Moto Moto..Masogange Afunguka A to Z Juu ya Kupangiwa Mjengo na Makonda…

0
0

ISHU hot iliyotrendi wiki hii ni kuhusu kigogo mmoja kudaiwa kumpangishia Video Queen maarufu Bongo, Agnes Gerald ‘Masogange’ mjengo wa maana uliopo Makongo Juu jijini Dar ambapo Ijumaa limechimba ili kujua ukweli wa mambo.

Madai hayo yaliibuka juzikati baada ya watu kibao wakiwemo mastaa kuhoji kwa nini modo huyo hakutajwa kwenye listi ya mastaa wa unga wakati aliwahi kunaswa akisafirisha ‘mzigo’ nchini Afrika Kusini na sasa anaishi maisha bomba.

“Unajua kati ya mastaa wanaoishi kwenye nyumba za kifahari Masogange yumo, watu wanasema anauza madawa lakini ninachojua mimi ni kwamba kapangishiwa bonge la jumba kule Makongo juu, ukifika pale utadhani anaishi bosi f’lani.

“Kapangishiwa na kigogo mmoja na huyo ndiye anampa jeuri mjini, sasa jaribuni kufuatilia mtaujua ukweli ila mimi msinitaje, msije mkanitafutia matatizo,” alidai mtoa ubuyu huyo.



Kufuatia madai hayo, Ijumaa lilifanya jitihada za kufahamu ilipo nyumba hiyo ambapo, kwa kuwatumia watu wanaomjua vizuri lilifanikiwa kufika Makongo Juu na kushuhudia nyumba hiyo ya kihafari.

Katika ‘kunyapianyapia’ ili kujua kama staa huyo alikuwemo ndani, paparazi wetu aligonga geti muda mrefu lakini halikuweza kufunguliwa wala kuonekana mtu yeyote.

Ijumaa laamua kumpigia simu

Waandishi wetu wakiwa wamekaa nje ya nyumba hiyo huku wakiangaza huku na kule, waliamua kumpigia simu Masogange na bahati nzuri alipokea na alipoambiwa wako nje kwake, alijibu kuwa hakuwepo hapo nyumbani.

“Sipo, niko mbali kidogo,” alisema mdada huyo mwenye figa matata.

Alipotakiwa kufungukia madai kuwa, nyumba hiyo anayoishi amepangiwa na kigogo mmoja maarufu na ndiye anayempa ujanja wa kuishi mjini, Masogange alisema kuwa ni kweli amepangiwa nyumba hiyo lakini siyo na kigogo kama inavyodaiwa.

“Watu wanasema eti nimepangiwa nyumba na kigogo, ukweli naujua mwenyewe. Nina mpenzi wangu na ndiye aliyenipangishia nyumba hii na hili suala lipo wazi kabisa kwani watu wangu wa karibu wanamjua,” alisema Masogange.

Aidha, katika muendelezo wa madai ya Masogange kupangiwa mjengo na kigogo, juzikati ilivuja clipu iliyodaiwa ni ya staa Wema Sepetu akihoji sababu za Masogange kutotajwa kwenye listi ya mastaa wa unga.

Hata hivyo, juzi kwenye mkutano wa Mkuu wa Mkoa wa Dar, Paul Makonda  na waandishi wa habari, mmoja wa mapaparazi alimuuliza sababu za Masogange kutotajwa kwenye listi hiyo kama alivyodaiwa kuhoji Wema ambapo mheshimiwa huyo aliyedhamiria kupambana vilivyo na biashara ya madawa ya kulevya katika Jiji la Dar alijibu:

“Kwanza ni kosa kisheria mtu anapokuwa anashikiliwa na jeshi la polisi kushika simu, sasa kama una jambo unataka kulisema na uko polisi, kwa nini usiliseme badala yake u.”

Vita dhidi ya Dawa za Kulevya: Iddi Azzan, Hussein Pamba Kali na Bosi wa Sea Cliff Watua Central Polisi

0
0

Aliyekuwa mbunge wa Kinondoni Iddi Azzan, bosi wa Sea Cliff pamoja na watuhumiwa wengine wa sakata la biashara ya Madawa ya kulevya wamefika polisi kituo cha kati kutii wito wa Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Paul Makonda.

Watuhumiwa 65 wa biashara ya Madawa ya kulevya katika list ya pili ya Mkuu huyo wa mkoa wa Dar es salaam Walitakiwa kuripoti central polisi Ijumaa hii.

Hata hivyo kati ya watuhumiwa hao, Manji pamoja na Askofu Gwajima waliripoti kituoni hapo jana na taarifa ambazo zilizagaa mitandaoni walipelekwa kwa mkemia mkuu kupimwa.

Mzee wa Upako Kashusha Nyundo Hizi Baada ya Gwajima Kutajwa Sakata la ‘Unga’...!!!

0
0

Mchungaji wa Kanisa la Maombezi (GRC), Anthony Lusekelo ‘Mzee wa Upako’ ameshauri kuwapo kwa utaratibu maalumu wakati wa kuwaita kwa mahojiano watu wanaoitwa kwa mahojiano kuhusu dawa za kulevya.

Mzee wa Upako alisema hakukuwa na umuhimu wa vyombo vya habari kuhusika katika kuwataja watu hao hasa viongozi wa dini, bali wangeitwa kwa barua maalumu. Alisema inapotokea wachungaji wakahusishwa na dawa za kulevya ni muhimu kuwapo na ushahidi wa kutosha kinyume na hapo, itawavunjia heshima yao.

Mzee wa Upako alisema anaunga mkono kwa asilimia zote vita dhidi ya dawa za kulevya ila hajafurahishwa na namna suala hilo linavyofanyiwa kazi hali inayoweza kuwaharibia watu heshima.

Mchungaji wa Kanisa la Maombezi (GRC), Anthony Lusekelo ‘Mzee wa Upako’ ameshauri kuwapo kwa utaratibu maalumu wakati wa kuwaita kwa mahojiano watu wanaoitwa kwa mahojiano kuhusu dawa za kulevya.

Mzee wa Upako alisema hakukuwa na umuhimu wa vyombo vya habari kuhusika katika kuwataja watu hao hasa viongozi wa dini, bali wangeitwa kwa barua maalumu. Alisema inapotokea wachungaji wakahusishwa na dawa za kulevya ni muhimu kuwapo na ushahidi wa kutosha kinyume na hapo, itawavunjia heshima yao.

Mzee wa Upako alisema anaunga mkono kwa asilimia zote vita dhidi ya dawa za kulevya ila hajafurahishwa na namna suala hilo linavyofanyiwa kazi hali inayoweza kuwaharibia watu heshima.

Sugu Alaani Uamuzi wa TCRA Kuzizuia TV za mtandaoni..Adai Tunakuwa Kama North Korea Kwa Spidi ya Ajabu

0
0
Mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph ‘Sugu’ Mbilinyi amelaani kitendo cha mamlaka ya mawasiliano nchini, TCRA kuzizuia online TV kuendelea kufanya kazi kama TV za kawaida hadi pale itakapotolewa muongozo na sheria za kuziendesha.


Katazo hilo itaziathiri baadhi ya TV za mtandaoni zenye umaarufu ikiwemo Ayo TV ya Millard Ayo. Akiongea bungeni leo mjini Dodoma, Mbilinyi amedai kuwa uamuzi huo unaliingiza taifa gizani.

“Tunakuwa North Korea kwa spidi ya ajabu sana,” amesema.

“Tunaonekana wa ajabu kwenye international community kwa maamuzi kama haya. Kwasababu wananchi wana haki ya kupata habari kutoka upande wa pili, mfano jana Askofu Gwajima na mfanyabiashara Manji walipata nafasi ya kujibu kwa haraka sana tuhuma dhidi yao zilizotangazwa kwenye TV pendwa za serikali lakini wao wasingeweza kupata nafasi ya live kusingekuwa na online TV wakaweza kujitetea kwa haraka sana,” ameeleza.

“Wananchi sasa wamekuwa wakitegemea online TV kupata habari za bunge kwahiyo ni wazi suala la kuzuia kwa namna yoyote online TV ni mwendelezo wa kuzuia wananchi kupata habari za bunge, ni mwendelezo wa kuliweka taifa gizani.”

Sugu amependekeza kazi za online TV ziendelee hadi pale sheria hizo zitakapotungwa kwasababu uwepo wake hakuvunji sheria yoyote.

Jeshi la Polisi Dar Lamjibu Mbowe..Lasema Kama Hataripoti Polisi, Basi Litamfuata Popote Alipo.

0
0

Jeshi la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam limesema kama Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe hataripoti bila kutoa taarifa yoyote ya udhuru atafuatwa kwa kuwa jeshi hilo linahitaji  kumhoji.

Kamanda wa kanda hiyo, Simon Sirro amesema hayo leo muda mfupi baada ya Mbowe kueleza kuwa hataripoti polisi kutokana na wito wa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda.

Amesema operesheni dhidi ya mihadarati bado inaendelea na kuanzia sasa hawataruhusu tena mkusanyiko wa watu katika kituo cha polisi kati na wale watakaoonekana watashughulikiwa hivyo asije kulalamika mtu kwani taarifa imeshatolewa.

Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe ametangaza rasmi kutofika kituoni hapo kwa madai kuwa hawezi kwenda polisi kwa wito wa Mkuu wa Mkoa, Paul Makonda isipokuwa pale tu taratibu za kisheria zitakapofuatwa.

Hivyo Joti amkana Gigy money mchana kweupee!!!!

0
0

Baada ya Mtangazaji wa ChoiceFM, Gigy Money kuonekana akimpost mchekeshaji Joti na alipoulizwa na Soudy Brown kwenye U heard iliyopita alikiri kuwa mapenzini na Joti.

Sasa leo kupitia XXL ya clouds FM, Mtangazaji Soudy Brown kwenye U heard amepiga stori na Joti ili kuujua ukweli, haya yalikuwa majibu yake. ‘Mimi kwa heshima ambayo nimeitengeneza na watu wangu ninaofanya nao kazi  halafu wewe unataka kuiharibu kwa mara moja, huyo Gigy unayemzungumzia picha ambazo amepost umeona picha ambayo mimi nafanya nae mapenzi?”

“Mimi siilewi…………mimi nina mke wangu, nina familia yangu, mbona unataka kuniweka kwenye maisha ambayo wanaishi watu, mimi siishi huko’ – Joti
.l

Kamanda Sirro Asema Manji na Gwajima Bado Wapo Lupango, Aeleza Walioripoti Leo ..!!

0
0

Kamanda Sirro amesema  bado wanamshikilia mwenyekiti wa Yanga, Yusuph Manji pamoja Askofu wa kanisa la Ufunuo na Uzima, Josephat Gwajima kwa tuhuma za kujihusisha na biashara ya kulevya.

Watuhumiwa hao wawili waliripoti kituoni hapo jana mchana na siyo leo kama walivyoagizwa na RC Paul Makonda. 

Kamanda Sirro amesema atatoa taarifa Jumatatu kueleza nini kinaendelea kuhusu watuhumiwa hao. 

Mpaka wakati anazungumza na waandishi wa habari kamanda huyo alisema walioripoti kituoni hapo ni watuhumiwa 4 kati ya 65 . 

Walioshuhudiwa na waandishi wa habari wakiripoti kituoni hapo ni Iddi Azzan, Hussain Pamba Kali pamoja na bosi Sea Cliff.

Baada ya Kukataa Wito wa Polisi,Mbowe Aamua Kumpeleka Makonda Mahakamani,..!!

0
0

Mwenyekiti wa Chadema Taifa, Freeman Aikael Mbowe (MB) leo tarehe 10 February 2017 amefungua kesi ya kikatiba dhidi ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salam, Mkuu wa Upelelezi wa Kanda Maalumu DSM na Kamanda wa Polisi wa Kanda Maalumu Dsm.

Kesi hiyo ilisajiliwa kama Kesi ya Kikatiba namba 1 ya 2017 imefunguliwa kwenye Mahakama ya Kuu masijala ya Katiba (Masijala Mkuu).

Kwenye Kesi hiyo Mbowe anaomba Mahakama Kuu itamke na kuwa Mkuu wa Mkoa hana mmalaka ya kudharilisha, na kukamata.

Mbowe pia ameiomba mahakama itengue vifungu vya 5&7 vya Sheria ya Tawala za Mitaa kwakua ni batili na vinakiuka haki za kikatiba.

Katika kesi hizo Mbowe atawakilishwa na Mawakili toka Kurugenzi ya Katiba Sheria na Haki za Binadamu ya CHADEMA.

Messi Afanya Kufuru.. Anunua Nyumba ya Jirani Yake Baada ya Kukerwa na Kelele

0
0

Mshambuliaji wa Barcelona, Lionel Messi (29) amenunua nyumba ya jirani yake katika eneo la Castelldefels, mjini Barcelona anapoishi kwa sababu walikuwa wakimsumbua kwa kelele.

Taarifa hizo zimeelezwa na mchezaji mwenzake wa Barca, Ivan Rakitic aliyesema kuwa Messi amekuwa akikerwa na kelele za jirani yake huyo hivyo kuamua kuinunua nyumba hiyo ili jirani aondoke na kuamuachia yeye na familia yake.

Vita Dhidi ya Madawa ya Kulevya..Rais magufuli Amuongezea Nguvu Makonda ..!!!

Mkude Atoa Kauli Tata Simba..!!!

0
0

WAKATI kikosi cha Simba, kesho Jumamosi kikitarajiwa kushuka uwanjani kucheza dhidi ya Prisons ya Mbeya katika Ligi Kuu Bara kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, nahodha wa Simba, Jonas Mkude ametoa kauli kuhusu nidhamu yake.

Mkude amesema kuwa yeye siyo mtovu wa nidhamu kama anavyodaiwa kauli ambayo inaweza kupokelewa kwa hisia tofauti na wenzake na mashabiki wa soka ambao mara kadhaa wamekuwa wakimlaumu kuwa ni mtovu wa nidhamu.

Kauli hiyo imekuja baada ya taarifa kuwa kuna baadhi ya wachezaji wenzake wa Simba wamemuomba kocha mkuu wa timu hiyo, Mcameroon, Joseph Omog kumpokonya Mkude unahodha kutokana na nidhamu yake kuwa mbaya.

Mkude hakusafiri na timu yake kwenda Songea kucheza dhidi ya Majimaji na inaelezwa kuwa wenzake hawakufurahishwa na kitendo hicho.

“Mimi siyo mtovu wa nidhamu kama inavyodaiwa na sijui ni kwa nini nimekuwa nikiandamwa na tuhuma hizo kila wakati.

“Ninapokuwa sionekani katika timu siyo kwamba ninafanya kusudi ila ninakuwa na matatizo na huwa natoa taarifa kwa viongozi wangu ambao nawajibika kwao kila siku ambao ni kocha pamoja na meneja, lakini haya ambayo yamekuwa yakisemwa kuwa sina nidhamu ninafanya mambo kwa kujiamulia siyo kweli.

“Kama kuna jambo lolote baya ambalo nililifanya na halikuwapendeza na hiyo ndiyo ikawa sababu ya kusemwa vibaya kila simu basi naomba wanisamehe,” alisema Mkude.
Viewing all 104416 articles
Browse latest View live




Latest Images