Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104789 articles
Browse latest View live

Kamishna Mpya Dawa za Kulevya Afunguka

$
0
0



Dar es Salaam. Rais John Magufuli amemteua Rogers Sianga kuwa kamishna mkuu wa Mamlaka ya Kuzuia na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA).

Baada ya kuteuliwa Sianga alizungumza na Mwananchi na kusema kwanza anamshukuru Mungu kwa uteuzi huo na akaahidi kushughulikia kwa karibu kesi za vinara wa ‘unga’.

Taarifa iliyotolewa na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais jana, Gerson Msigwa ilisema Sianga atasaidiwa na Mihayo Msikela atakayekuwa Kamishna wa Operesheni na Fredrick Kibuta atakayekuwa Kamishna wa Intelijensia.

Uteuzi huo umekuja siku chache baada ya Mbunge wa Bunda Mjini, Ester Bulaya (Chadema) kumtaka Rais Magufuli kuteua kamishna mkuu wa tume hiyo, ambayo imekaa bila kiongozi tangu Sheria ya Kupambana na Kudhibiti Dawa za Kulevya ilipotungwa mwaka 2015.

“Tusifanye siasa kwenye vita hii ya madawa ya kulevya, tusimwongopee Rais kwa kutaka kuhakikisha vyeo vyetu tumwambie ukweli.

“Ili kumsaidia Rais anapaswa kumteua kamishina wa hii tume maana tangu tulipopitisha sheria hiki chombo hakina kamishna, tutakapohakikisha hicho chombo kinapata kamishna kwa kumsaidia Rais tutakamata wale wanaoingiza dawa za kulevya, wale mapapa na si hao wanaokamatwa sasa hivi,” alisema Bulaya.Mbali na Bulaya, Mbunge wa Kawe, Halima Mdee alishauri bungeni kuwa mapambano ya dawa za kulevya hayatafanikiwa bila kuiwezesha tume hiyo kifedha.



Sianga afunguka

Akizungumza na Mwananchi Sianga alisema kwanza anashukuru Mungu kwa uteuzi huo, akaahidi kushughulikia kwa karibu kesi za vinara wa ‘unga’.

Kuhusu vigogo na wafanyabiashara maarufu walitajwa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda, Sianga aliyekuwa Moshi mkoani Kilimanjaro, alisema akifika Dar es Salaam atakutana na watendaji wengine waangalie cha kufanya.

“Ndiyo kwanza nimeteuliwa bado nipo Moshi nikifika Dar es Salaam, nitazungumza na wenzangu naamini tutashirikiana na tutashughulikia kwa msingi wa sheria.

Pia, alitoa onyo kwa watu wanaolima mirungi au bangi nchini.

“Dawa hizo nyingine za kulevya ni ghali na zinaletwa kutoka nje ya nchi, lakini mirungi na bangi tunajua inalimwa nchini hao wakulima waache walime mazao ya vyakula, maana dawa hizo zinaleta madhara makubwa kwa maendeleo ya taifa,” alisema.Uteuzi huo umekuja ikiwa pia ni siku chache baada ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda kuanza kutangaza majina ya watu anaotaka waripoti polisi kuhusiana na vita hiyo.

Huku kukiwa na maoni tofauti kuhusu hatua hiyo, Makonda ameahidi kutangaza orodha nyingine ya tatu ikiwa ni sehemu ya mapambano yake ya dawa za kulevya.

Washukiwa hao wamekuwa wakiripoti katika kituo kikuu cha Polisi cha Kanda Maalumu ya Dar es Salaam kwa ajili ya mahojiano kabla ya kupelekwa mahakamani.

Mbali na uteuzi huo, Rais Magufuli pia amemteua Dk Anna Makakala kuwa kamishna mkuu wa idara ya Uhamiaji.

Kabla ya uteuzi huo, Dk Makakala alikuwa mkuu wa chuo cha Uhamiaji mkoani Kilimanjaro.

Taarifa hiyo imesema wateule hao wataapishwa kesho Ikulu ya Dar es Salaam.

Kenya Yasalimu Amri..Rais Kenyatta Atangaza Janga la Ukame na Ukosefu wa Chakula

$
0
0

KENYA: Rais Uhuru Kenyatta jana alitangaza hali ya ukame kuwa ni janga la kitaifa baada ya kuyakumba majimbo 23 katika muda wa miezi 6.

Rais Kenyatta aliwaonya watu wanaosambaza chakula cha misaada kutouza chakula hicho ili watajirike.

Shirika la kimataifa la Msalaba Mwekundu limeonya kuwa takribani watu 11 kutoka Kenya, Ethiopia na Somalia wako katika hatari ya kufa njaa.

Madaha Ajikosha, Ampa Tano Makonda..!!!

$
0
0

MWANAMUZIKI Baby Joseph Madaha amefungukia uamuzi wa Mkuu wa Mkoa wa Dar, Paul Makonda wa kuanza kudili na wauzaji na watumiaji wa madawa ya kulevya akisema kuwa, huenda ikasaidia mastaa wengi kubadilika. Akipiga stori na Ijumaa

hivi karibuni, Baby Madaha ambaye naye aliwahi kukwaa skendo ya kudaiwa kusafi risha unga kwenda Uarabuni, alisema kuwa anajua kweli mastaa wengi ni watumiaji na wasafi sharisha wa unga hivyo kitendo cha baadhi yao kutaitiwa, kinaweza kuwa mwanzo mzuri.

“Niliwahi kudaiwa kusafi risha unga lakini haikuwa kweli. Wanaouza na kutumia wanajulikana, hivyo mimi nimpe tu tano Makonda kwa hatua hii nzuri, naamini huko tuendako jitihada hizi zitazaa matunda,” alisema Madaha

Makubwa Haya..Dada Yake Diamond Azuiwa Kumuona Zari,Aaambiwa Akitaka Kumuona Akachukue Barua ya Utambulisho Serikali za Mitaa..!!

$
0
0


Ukistaajabu ya Musa Utaona ya Firauni, hivyo ndivyo unavyoweza kusema kufuatia mzazi mwenza wa mkali wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’, Zarinah Hassan ‘The Boss Lady’ kuwa na masharti magumu ya kumfikia pale uwapo na hitaji la kuonana naye baada ya kutua nyumbani kwa Diamond, Madale jijini Dar.

Hivi karibuni dada wa aliyejitambulisha kuwa ni wifi wa Zari alijikuta kwenye simanzi baada ya kupewa masharti ya aina yake na mlinzi wa getini nyumbani kwa Diamond alipokuwa amekwenda kumtembelea.

Aliambiwa ili aweze kumuona Zari, anatakiwa kuwa na barua kutoka serikali ya mtaa ili kumtambulisha kabla ya kupata ruhusa ya kuonana na mama huyo raia wa Uganda au uwe umewasiliana na Diamond mwenyewe na akakiri kukutambua.

Kamera za makachero wa Oparesheni Fichua Maovu ya Global Publishers (OFM) zilifanikiwa kulinasa tukio zima baada ya wifi huyo aliyedai ametokea Tandale nyumbani alipokulia Diamond, kuwaomba OFM wampe kampani alipokuwa anaenda Madale. “Nimeambiwa nyinyi OFM mnapajua vizuri kwa Diamond sasa naomba mnipeleke nikamuone wifi yangu maana nimejaribu kutafuta mawasiliano ya Diamond bila mafanikio.

Unajua Diamond tumekua naye Tandale sasa japo si ndugu yangu wa damu  lakini Zari ndiye wifi yetu kutokana na ukaribu tuliokuwa nao,” alisema wifi huyo.

OFM iliongozana na dada huyo hadi nyumbani kwa Diamond lakini bahati haikuwa yake maana alikutana na vizingiti vya hali ya juu getini:

Wifi: Habari zako.

Mlinzi: Poa nikusaidie nini?

Wifi: Naitwa (anataja jina lake) naishi Tandale ni dada yake na  Diamond wa hiyari, nimekuja kumsalimia wifi yangu Zari.

Mlinzi: Iko wapi barua ya serikali ya mtaa?

Wifi: Kwani kuja kumsalimia wifi yangu hadi niwe na barua kutoka serikali ya mtaa ndiyo utaratibu gani huo?

Mlinzi: Huo ndiyo utaratibu na ni vizuri ukatambua utaratibu uliowekwa na wahusika wa mji huu, bila barua kutoka serikali ya mtaa unakotokea huwezi kuingia ndani na siyo wewe tu huu ni utaratibu ni wa kila mtu.

Hadi OFM wanaondoka nyumbani hapo, wifi huyo alishindwa kuingia baada ya kusema hawezi kwenda serikali ya mtaa kwa ajili ya jambo hilo.

Mbunge Mwingine Aibuka na Kutaja Mali Hizi Nyingine za Kutisha Anazomiliki Makonda,Amtaka Aeleze Wapi Alikozipata..!!!

$
0
0

Sakata la mali zinazodaiwa za Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda limeendelea kulitikisa bunge baada ya Mbunge wa Rombo, Joseph Selasini (Chadema) kuongeza nyingine.

Akichangia taarifa za Kamati za Bunge za Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge na ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama, Selasini alisema Makonda amenunua jengo (apartment), lenye thamani ya Sh600 milioni.

“Makonda amenunua apartment pale Viva Towers kwa Sh600 milioni. Makonda amempa mke wake gari aina ya Mercedes Benz lenye thamani ya Dola 250,000 za Marekani (Sh550 milioni) kama zawadi ya ‘Birthday’,” alisema Selasini.

Suala la utajiri wa Makonda, liliibuliwa bungeni kwa mara ya kwanza Februari 6 na Mbunge wa Geita Vijijini (CCM), Joseph Msukuma akitaka mteule huyo wa Rais achunguzwe kwa kujilimbikizia mali.

Kiini cha mbunge huyo kumshukia Makonda ilitokana na hatua yake ya kutangaza majina ya watu aliodai wanajihusisha na biashara ya madawa ya kulevya, huku akidai utajiri wake una shaka.

Msukuma Februari 7, mwaka huu aliomba mwongozo kwa Spika, akitaka Bunge litoe mwongozo kuhusu utajiri huo wa Makonda ndani ya muda mfupi.

Msukuma alisema kuwa katika kipindi cha mwaka mmoja tu wa wadhifa wake kama mkuu wa mkoa, Makonda amejilimbikizia mali likiwamo gari aina ya Lexus, lenye thamani ya Sh400 milioni.

Mbali na mali hizo Msukuma alisema Makonda anamiliki magari mengine ya kifahari aina ya V8, anajenga maghorofa jijini Mwanza na amekarabati ofisi yake kwa Sh400 milioni bila kutumia utaratibu wa sheria ya manunuzi.

Mbali na hilo, Selasini alisema utaratibu unaotumiwa na Makonda kushughulikia tatizo la dawa za kulevya, umetoa mwanya kwa wafanyabiashara wakubwa wa dawa hizo kukimbilia nje ya nchi.

“Kama unawatangaza watu kwa utaratibu huu. Ni mfanyabiashara gani wa dawa za kulevya mjinga amebaki katika hii. Makonda amesaidia kuwakimbiza labda anashirikiana nao,” alisema.

Wakati huo huo Mbunge wa Ukonga, Mwita Waitara (Chadema), ameliomba Bunge kutoa mwongozo kwa kile alichodai ni hatua ya katibu wa Bunge, Dk Thomas Kashililah kupingana na maazimio ya Bunge.

Pamoja na Kumuhusisha na Madawa ya Kulevya,TID Amfuata Makonda Hadi Nyumbani Kwake,Haya Ndiyo Aliyomueleza..!!!

$
0
0

Mapema jana Mwanamuziki Khalid Mohamed maarufu kama "Top In Dar" (TID) ambaye alikuwa miongoni mwa watu wa kwanza kuitwa polisi kwa mazungumzo ya tuhuma zake kuhusu anavyohusika na madawa ya kulevya, alifika nyumbani kwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Paul Makonda kwa ajili ya kumsalimia na mazungumzo ya kawaida 

Kwa muda wote ambao wawili hao walipokuwa pamoja walionekana kufurahia mazungumzo yao, wakiwa wamekaa kama marafiki. Mkuu wa Mkoa akitumia muda wa mazungumzo hayo kumshauri TID kuhusu maisha kwa ujumla na umuhimu wa kumtegemea Mungu katika kila jambo analofanya 

Kwa upande wake TID yeye alitumia muda huo kumweleza Paul Makonda kuhusu maisha ya kawaida na yale ya muziki, Aidha, mazungumzo ya wawili hayo yaligusa kuhusu namna wanavyoweza kuokoa vipaji vya wasanii 

Aidha, TID amenukuliwa akisema "Muziki bila madawa ya kulevya inawezekana... This is the turning Point kwangu mimi na kizazi cha muziki huu wa kizazi kipya, nikiwa na Mhe. Makonda leo tukijadili jinsi ya kuokoa vipaji na sanaa kwa ujumla, Mungu ibariki bongo fleva, Mungu ibariki Tanzania".

Naye Makonda kupitia ukurasa wake wa Instagram ameandika "Mungu wetu hajalala na siku zote anampenda amtafutae, karibu tena nyumbani TID".

Huu Ndio Ujumbe Alioandika Askofu Gwajima Akiambatanisha na Picha ya RC Makonda..!!!!

$
0
0

"Mchana na usiku huzunguka kutani mwake; Uovu na taabu zimo ndani yake; Tamaa mbaya zimo ndani yake; Dhuluma na hila haziondoki mitaani mwake. Kwa maana aliyetukana si adui; Kama ndivyo, ningevumilia. Aliyejitukuza juu yangu siye anichukiaye; Kama ndivyo, ningejificha asinione. Bali ni wewe, mtu mwenzangu, Rafiki yangu, niliyejuana nawe sana. Tulipeana shauri tamu; na kutembea Nyumbani mwa Mungu pamoja na mkutano."

ZAB. 55:10‭-‬14 SUV

Serikali Imuunge Mkono Askofu Dr. Gwajima Katika Mpango wa Kununua Treni ya Mwendo Kasi..!!!

$
0
0

Baba Askofu Dr. Gwajima, ameanza mchakato wa kunua Treni ya mwendo kasi ambayo itakua inatoka Dar hadi Morogoro. Katika usajili bado anawekewa Zengwe, ila nia yake ni nzuri kabisa.

Katika Tanzania ya Viwanda, hatuwezi kufanikiwa Tanzania ya viwanda kama hatuna Usafiri wa Uhakika wa kutoka sehemu moja hadi nyingine.

Tayari kashafanikisha Mpango wa kujenga chuo cha Urubani, anasubiri ruksa ya Rais Magufuli. Dr Gwajima alishampeleka Mkufunzi wa mambo ya ndege kusomea kufundisha mambo ya ndege. Kwa Tanzania watu wengi wanapenda Urubani lakini garama za masomo ni kubwa. Hivyo kampeleka Kaka John kusomea Ualimu wa ndege. Nadhani wote mnamjua John wa Ufufuo na uzima. Ni kijana mwenye akili sana.

Hadi sasa Dr Gwajima kushirikiana na Msukuma(Mbunge) wameshaanza mchakato wa kumuona Rais ili awape sehemu ya kujenga chuo cha Urubani.

Vilevile ameshaagiza Chopa tatu kwaajili ya wanafunzi.

Wito wangu
Naomba Serikali isilete siasa katika hili Swala kwani lina manufaa kwa Watanzania. Tutawanyanyasa wawekezaji lakini Kenya ikiwachukua tunaanza kulalamika.

Askofu Dr Gwajima kwa wasiomjua, ni Askofu wa Makanisa ya Ufufuo na Uzima ambayo ni Zaidi ya Makanisa mia nne(400) Dunia. Vilevile ana makampuni mengi kama makanisa mengine yalivyo na mabank mfano Mkombozi, Efatha Bank nk.

Dr Gwajima ni Mwalimu ambaye Hulipwa zaidi ya dola 1,000/= kwa saa. Anafundisha Mambo ya Kiroho Duniani na huwa anaalikwa kufundisha hata kwa miezi mitatu.

Kwa sasa anamiliki ndege ambayo humuwezesha kuhudumia Ibada katika Makanisa Matatu Tofauti mikoa tofauti kwa siku.

Watanzania tuache wivu na kijicho cha roho mbaya, bali tuwaunge mkono Watanzania wenzetu ambao Mungu Kawainua. 


Mwigulu Nchemba Afunguka Ukimya Juu ya Sakata la Madawa ya Kulevya

$
0
0

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu Nchemba alisimama Bungeni juzi, February 10, 2017 kuzungumza vitu mbali mbali vianavyohusu wizara yake ambapo aligusia kuhusu maswali anayokutana nayo kwamba kwanini hajaonekana akiongelea sakata la dawa za kulevya toka limeibuka Dar es Salaam.

Waziri Mwigulu alizungumza yafuatay:

“Lililoongelewa sana ni hili la dawa za kulevya, vita ya dawa za kulevya ni vita ya kila Mtanzania na haijaanza sasa, mimi tangia nilipofika nilikuta tayari Mh. Kitwanga ameshakamata Mapapa Wakubwa tu na tulivyotoka pale tumeendeleza.

“Ninachowaambia Waheshimiwa Wabunge tunaweza kutofautiana mtazamo kwenye approach na nyinyi kama Wabunge na Washauri wetu mkitushauri njia nzuri za kufanikisha jambo hili sisi mara zote tutakua tunapokea ushauri huo sababu vita hii ni yetu sote.

“Jambo moja tu ambalo nawahakikishia na ambalo nawaomba wote tuwe nalo, tusibadili lengo… na kuna watu wengine walikua wanasema mbona Waziri hujasema? ……..nimeshazunguka mikoa yote kasoro Njombe, Ruvuma, Singida na Songwe, kwenye mikoa yote huko nimetoa maelekezo ya kufanyiwa kazi, mojawapo ni dawa za kulevya.

“Nikishatoa maelezo kama hayo sibinafsishi tena hiyo shughuli, Mtanzania ambaye inamuhusu popote alipo lazima tusimamie mambo haya kwa upana wake, Waheshimiwa Wabunge katika maswala haya ya kitaifa tushirikiane wote, watu huwa hawagombani kwa ajili ya kazi watu huwa wanasaidiana kazi.” Alisema Mwigulu.

Sasa Kukamata Wabunge Hovyo Hovyo Mwisho- Zitto...!!

$
0
0

Mbunge wa Kigoma mjini Zitto Kabwe amefunguka na kusema ile hali ya polisi kuwakamata wabunge hovyo sasa mwisho baada ya jana Ndugai kutoa uamuzi kuwa Afisa yoyote wa Serikali ambaye atakuwa akimuhitaji mbunge ni lazima kwanza atoe taarifa kwa spika

Hali hii imefikia baada ya Jumatano bunge kupitisha azimio la kutaka kwanza ruhusa ya spika wa bunge pale vyombo vya dola kama polisi wanapokuwa wanamuhitaji mbunge yoyote kwa jambo lolote.

"Leo (jana) Spika wa Bunge ametoa uamuzi wa Spika kwamba Afisa wa Serikali anapomtaka mbunge kwa jambo lolote lile lazima kwanza kupata kibali chake. Mabunge yote ya Jumuiya ya Madola hulinda kwa wivu mkubwa hadhi yake kama mhimili.

Sasa kukamata kamata wabunge hovyo mwisho. Lazima mihimili iheshimiane. Sasa tuone kama Sirro atamfuata Mbunge wa Hai kama alivyosema" alisema Zitto Kabwe

Mbali na hilo Mhe. Zitto Kabwe ametoa pongezi kwa wabunge wote pamoja na Spika wa bunge kwa kuonyesha msimamo na kupigania heshima ya bunge

"Nawapongeza wabunge wote kwa kuonyesha msimamo katika jambo hili na ninampongeza sana Spika Ndugai kwa kusimamia heshima ya bunge lake" Alimalizia Zitto Kabwe

Pitia Vichwa vya Magazeti ya Leo 12/2/2017..!!!!

Rais John Pombe Magufuli Awapangia Vituo vya Kazi Mabalozi 3 Aliowateua...!!

$
0
0

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli amewapangia vituo vya kazi Mabalozi wapya watatu ambao aliwateua tarehe 03  Desemba 2016.

Mabalozi hao waliopangiwa vituo ni Mhe. Joseph Sokoine anayekuwa Balozi wa Tanzania nchini Ubelgiji, Mhe. Omar Yussuf Mzee anayekuwa Balozi wa kwanza wa Tanzania nchini Algeria na Mhe. Grace Mgavano anayekwenda kujaza nafasi iliyoachwa wazi na Mhe. Dkt. Ladis Komba nchini Uganda ambaye alistaafu kwa mujibu wa Sheria.

Balozi Sokoine ambaye anakwenda kujaza nafasi iliyoachwa wazi na Mhe. Deodorus Kamala ambaye kwa sasa ni Mbunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kabla ya uteuzi huo alikuwa Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki.

 Balozi Mzee kabla ya kuteuliwa kushika nafasi hiyo alishawahi kushika nafasi mbalimbali katika Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar na nafasi ya mwisho alikuwa Waziri wa Fedha wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar katika awamu ya kwanza ya Mhe.  Rais Dkt. Ali Mohammed Shein.

Kwa upande wa Balozi Mgavano kabla ya kuteuliwa kushika wadhifa wa Ubalozi alikuwa Afisa Mwandamizi katika Ofisi ya Rais, Ikulu.

Mabalozi wote waliopangiwa vituo vya kazi wataapishwa na Mhe. Rais Ikulu jijini Dar Es Salaam leo  Jumapili tarehe 12 Februari 2017 saa tano asubuhi.

Makonda Afunguka Kuitwa na Bunge...!!!

$
0
0
MKUU wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda amesema hawezi kufika mbele ya Kamati ya Haki, Kinga na Madaraka ya Bunge kuhojiwa kwa kuwa hajapokea barua ya kuitwa.

Akizungumza  jana jijini Dar es Salaam, Makonda alisema hatoweza kwenda mbele ya kamati hiyo bila barua rasmi iliyomtaka kufanya hivyo.

Bunge lililokuwa likiendelea na vikao vyake Dodoma kabla ya kuahirishwa juzi, lilipitisha uamuzi wa kuwataka Makonda na Mkuu wa Wilaya ya Arumeru, Alaxander Mnyeti, kufika mbele ya kamati hiyo na kuhojiwa kutokana na kauli walizozitoa, zinazodaiwa kuudharau mhimili huo wa dola.

Lakini Makonda alisema jana “hilo suala la mimi kuitwa kwenye kamati nalisikia na kulisoma kwenye magazeti."

"Sina uhakika ni lini wamefikia uamuzi huu wa kuniita na hata kama wamefikia uamuzi huo, sijaletewa barua rasmi.”


Baada ya Bunge kupitisha uamuzi huo wa kuitaka Ofisi ya Bunge iwaandikie barua viongozi hao, juzi baadhi ya wabunge walihoji kauli ya Katibu wa Bunge, Dk. Thomas Kashililah, kwamba azimio la chombo hicho cha kutunga sheria kumtaka Makonda kufika mbele ya kamati kujieleza kuhusu tuhuma za kuudharau mhimili huo, halikufuata utaratibu.

Hatua hiyo iliamsha hasira kwa baadhi ya Wabunge na kuomba mwongozo kuhoji kwa nini Katibu wa Bunge ametoa kauli ambayo inakinzana na makubaliano ya Bunge.

Mbunge wa Ukonga, Mwita Waitara na mwezake wa Iringa Mjini Mchungaji Peter Msigwa (wote Chadema) walihoji kuhusu kauli ya Dk. Kashililah.

Waitara alisema, “Asubuhi ya leo ( juzi) nimetumiwa ‘clip’ ya sauti ya Katibu wa Bunge akikosoa uamuzi wetu hapa na pia gazeti la Habari Leo, Ukurasa wa 25, kuna habari imeandikwa.

Katika taarifa hii, Katibu wa Bunge anasema maazimio ya Bunge yalikosewa na hayakufuata utaratibu,” alisema na kuongeza kuwa: “ Kwa maana nyingine, hatatekeleza kile tulichokubaliana.”

Mchungaji Msigwa wakati akichangia taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama, alieleza kuwa hajafurahishwa na kauli ya Katibu wa Bunge.

Alisema Katibu wa Bunge amekosea kwenda katika vyombo vya habari na kudai chombo hicho cha kutunga sheria kimekosea kwa kuwa anafanya kazi ya Bunge na kwamba hajaajiri wabunge na anapaswa kufuata maagizo yao.

Hoja ya kutaka kina Makonda washughulikiwe iliwasilishwa na Mbunge wa Ukonga, Mwita Waitara (Chadema) katikati ya wiki na ilijadiliwa na kuungwa mkono na wabunge wote, wakiwamo mawaziri kwa kusema ‘ndiyo’.

Majaliwa Afunguka Issue ya Madawa ya Kulevya Inayoratibiwa na Makonda..!!!!

$
0
0

JUMLA ya Watanzania 578 wamekamatwa na kufungwa katika magereza ya nchi mbalimbali kwa makosa ya kujihusisha na biashara ya dawa za kulevya.

Akiahirisha mkutano wa sita wa Bunge la 11 mjini Dodoma juzi, Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, alitaja nchi ambazo Watanzania hao wamefungwa kuwa ni pamoja na China (200), Brazil (12), Iran (63), Ethiopia (7) na Afrika ya Kusini (296).

Majaliwa pia alisema vita inayoendelea nchini dhidi ya dawa za kulevya inapaswa kuungwa mkono.

Alisema madawa ya kulevya huingia zaidi kutumia kwa njia za bandari bubu kupitia Bahari ya Hindi na mipakani kwa njia ya magari binafsi na mabasi yatokayo Kenya, Uganda na Zambia.

“Lengo la serikali ni kuwasaidia walioathirika na dawa za kulevya na kuwachukulia hatua kali wale waliowaathiri - wauzaji na wasambazaji," alisema Majaliwa.

Kutana na Maalim Hussein Mtabibu wa Nyota za Binadamu Africa na Dunia Nzima,

$
0
0

Kutana na Maalim Hussein Mtabibu wa nyota za binadamu Africa na dunia nzima,
Anatoa TIBA MAENEO YOTE NCHINI, KWA WALE WENYE KUHITAJI TIBA ANATIBU YAFUATAYO,
Husafisha nyota na kutoa Pete za bahati na kwa wale walia sumbuka kwaajili ya matiba na hawakufanikiwa njoo ujionee muujiza wa papo kwa papo-humpa mtu jini la mali kwa yule anaetaka kumiliki mali bila masharti yoyote,
Anatibu magonjwa yalio shindikana-Mpenzi/MUME/MKE Aliekukimbia Anakurudishia Ndani ya saa 72 tu, Pia tunatoa dawa za Nguvu za KIUME na Kurefusha kwa saizi unayo Taka-Anatoa Dawa za BIASHARA NA MVUTO-Tunatoa Dawa za Uzazi kwa kina Mama kwa wale wenye Tatizo Sugu-Anatoa Zindiko ya Nyumba,Mwili, na Mvuto kazini- Tunamaliza kesi zilizo kaa muda Mrefu bila kumalizika, Tung'arisha Nyota na Cheo kazini. Tunarudisha Mali zilizopotea au Kuibiwa na Mengine Mengi ya Siri tuwasiliane kwa Simu-Whatsapp +255674835107
+255 629254849

Wakati Party ikiendelea, Zari Aficha Funguo za Nyumba yake

$
0
0
Katika hali ya kuonyesha kuwa hana imani na wageni waalikwa walioudhuria Party ya mwanae, mjasiriamali zari ameamua kubeba kabisa funguo za nyumba yake mkononi jambo lililozua minongono kwa baadhi ya waalikwa wakidai Zari hataki Upuuzi kabisa anaogopa kuibiwa dhahabu zake.
By warumi

40 ya Nillan: Wolper Achafua Hali ya Hewa, Atoa Povu Hadharani Mbele ya Wageni

$
0
0
WAKATI sherehe ya kutimiza 40 kwa mtoto wa Diamond na Zari, Nillan ikiendelea, staa wa Bongo Movies, Jackline Wolper Massawe amekerwa na wanaomsema vibaya Zari na kuamhua kuwafungukia hadharani akitoa povu lake mbele ya wageni waalikwa.
Tazama Video:

Application ya Udaku Special Blog Imefanyiwa Marekebisho ..Fanya Hivi Ku Update

$
0
0

Kwa wenye kupata habari zetu kupitia Application yetu ya Udaku Special Blog kutoka Android tunapenda kuwaambia kuwa kuna Marekebisho kidogo tumefanya, Bonyeza HAPA ku Update

Au kama Huna Bonyeza HAPA Kuinstall

Baada ya Kutoka Selo Kwa Dhamana Hii Ndio Post ya Kwanza Aliyoandika Wema Sepetu Instagram

$
0
0
Inawezekana kama wewe ni shabiki wa Wema Sepetu ulikua na hamu sana ya kujua post yake ya kwanza kwenye mitandao ya kijamii itahusu nini baada ya kuachiwa kwa dhamana na Mahakama kufuatia sakata la dawa za kulevya lililomfanya alale Polisi.

Post ya kwanza ya Mwigizaji huyu haijahusu chochote kuhusu kesi yake ama alichokipitia wiki iliyoisha bali imemuhusu dada yake ambaye leo ni siku yake ya kuzaliwa kama inavyoonekana hapa chini.



Wema Sepetu atarudi tena Mahakamani mwishoni mwa mwezi huu baada ya kupata dhamana Alhamisi ya wiki iliyopita kwenye Mahakama ya hakimu mkazi Kisutu Dar es salaam.

Magufuli Awaita Mabalozi Dodoma...!!!!

$
0
0

RAIS John Magufuli juzi aliwaeleza rasmi mabalozi na wawakilishi wa mashirika ya kimataifa azma ya serikali kuhamishia Makao Makuu mjini Dodoma katika kipindi cha miaka mitano ya utawala wake na kuwaomba nao waanze mchakato wa kuhamia Dodoma.

“Mwaka jana wakati nakabidhiwa uenyekiti wa Chama cha Mapinduzi niliahidi ndani ya miaka mitano serikali itahamia Dodoma," taarifa ya Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki ilisema juzi.

"Tayari Waziri Mkuu na baadhi ya wizara zipo Dodoma. Nawaomba mabalozi nanyi muanze kufikiria kuhamia Dodoma kwani serikali imekwishatenga viwanja kwa ajili yenu."

Kwa upande wake, taarifa ya Wizara ilisema juzi, Kaimu Mkuu wa Mabalozi ambaye pia ni Balozi wa Zimbabwe nchini, Edzai Chimonyo alisema Jumuiya ya Mabalozi inaunga mkono wazo hilo na wapo tayari kuhamia Dodoma kama ilivyopangwa.

Taarifa hiyo ya Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki ilisema Rais Magufuli alitoa taarifa hiyo wakati wa hafla ya kuukaribisha mwaka mpya.

Hafla hiyo, imeelezwa, ilifanyika Ikulu, Dar es Salaam kati ya Rais, mabalozi na wawakilishi wa mashirika ya kimataifa yaliyopo nchini.

Rais Magufuli, imeelezwa pia, alitumia hafla hiyo kuwashukuru mabalozi na wawakilishi wa mashirika ya kimataifa kwa ushirikiano na mchango wao kwa serikali ambao umesaidia kufikia malengo ya mwaka uliopita.

Aidha, Rais Magufuli amewasihi mabalozi hao kuendelea kuisaidia Serikali ili kufikia malengo iliyojiwekea kwa mwaka huu.

Katika hotuba yake, imeelezwa, Rais Magufuli alisema mwaka 2016 ambao ulikuwa mwaka wake wa kwanza madarakani umekuwa wa mafanikio makubwa ambapo nchi imendelea kudumisha amani, mshikamano, umoja na muungano umeimarika.

Aidha katika mwaka huo, taarifa ya Wizara ilisema, Rais Magufuli alisema serikali imeongeza jitihada za kuimarisha demokrasia, kupiga vita rushwa, ujangili na ufisadi.

Akizungumzia suala la ukusanyaji mapato, Rais Magufuli alisema serikali inasimamia kikamilifu ambapo kwa sasa kiwango cha ukusanyaji wa mapato kimeongezeka kutoka Sh. bilioni 850 hadi kufikia Sh. trilioni 1.2 kwa mwezi, taarifa ilisema.

Kuhusu Mpango wa Maendeleo wa Miaka Mitano 2016-2021, taarifa ilisema Rais Magufuli aliwaeleza mabalozi kuwa mpango huo unalenga kujenga uchumi wa viwanda ili kuiwezesha nchi kuwa ya uchumi wa kati ifikapo mwaka 2025 kama Dira ya Maendeleo ya Taifa inavyoelekeza.

Rais Magufuli alisema kwenye hafla hiyo kuwa katika kutekeleza mpango huo, Sh. trilioni 107 zinahitajika na kati ya hizo serikali itatoa Sh. trilioni 59 ambazo ni wastani wa Sh. trilioni 11.8 kila mwaka, kwa kipindi cha miaka mitano ijayo.

Taarifa ilisema Rais aliwaambia wageni wake kuwa utekelezaji wa mpango huo umeshaanza ambapo serikali katika bajeti yake ya mwaka 2016 imetenga kiasi cha Sh. trilioni 29.5, sawa na asilimia 40 ya bajeti ya serikali, kwa ajili ya maendeleo.

Ni kiwango cha juu zaidi kuwahi kutengwa kwenye bajeti ya maendeleo katika historia ya Tanzania.

Fedha hizo, alisema Rais Magufuli, zimeelekezwa kwenye ujenzi wa miundombinu wezeshi kwa ajili ya uwekezaji wa viwanda kama vile nishati, barabara, reli na maji.

“Hii imetuwezesha kuendelea au kuanza utekelezaji wa miradi mikubwa ya usafiri ikiwemo reli, barabara, anga, maji pamoja na miradi ya umeme," taarifa ya Wizara ilimnukuu Rais. "Tuliweza pia kununua ndege mpya sita ambazo bila shaka zitasaidia kukuza sekta ya utalii nchini.”
Viewing all 104789 articles
Browse latest View live




Latest Images