Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104789 articles
Browse latest View live

‎'Help, I Want To Cheat On My Husband'

$
0
0
I am so confused and didn't know where else to go with such a tough decision! I will just give you the main details and maybe you could help me out.

I have been married for almost 2 years to a perfect husband. I trust him with all my heart. He does almost everything a wife wants. We do have some difference in some areas in our marriage but other than that all is perfect. My husband and I also share 3 children together.

My husband has a good friend I will call 'Jim'. I have known Jim ever since I met my husband. About 2 years ago I started feeling an attraction towards him but never revealed it to anybody. Some time ago, we were all out together and Jim and I both had too much to drink and began to discuss this mutual attraction. After that night nothing more was ever really said.

Last weekend, we were all hanging out again and Jim and I started talking about our feelings again. Saying that maybe we should just sleep together and then maybe the whole thing would go away since we will know what it would be like, (to make matters worse, he is also married with children). We continued to joke about this throughout the night.

Yesterday he stopped by to see my husband but he wasn't here so we started talking. We discussed how if nobody knows, then nobody can get hurt. We also discussed consequences and many other things. I know it would be immoral for me to cheat on my husband, but what do I do with these feelings?

I am not a bad person, I have never been a cheater! We made plans for a 'date' today while my husband is with his family. The more I have been running this through my head the more I realize how much is at stake.

Should I do it once and then maybe that will kill the curiosity? Or just tell Jim that we just can't do it?

I guess I know what I SHOULD do, but honestly tell me what you would do in this situation.

Tundu Lissu Abaini Mbinu Chafu kwa Chama Fulani Kuweka Mgombea Urais TLS..!!!

$
0
0

Mwanasheria Mkuu wa Chadema na mbunge wa Singida Mashariki kupitia chama hicho, Tundu Lissu amezungumzia hatua yake ya kujitosa kuwania urais wa Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS).

Mosi, Lissu amesema amepata msukumo kutokana na kauli ya rais John Magufuli kuwa kuna kampeni zimeanza za kumuondoa rais wa sasa wa TLS na zinaendeshwa na chama fulani ambacho kimeweka mgombea wake.

Pili, akasema Lissu ni kauli kuwa mawakili wanaotetea wauza dawa za kulevya nao wakamatwe wawekwe ndani.

“Sikuwa na mpango wa kugombea lakini the moment (wakati) aliposema, nikasema sasa nitagombea urais wa TLS,” amesema mbunge huyo.

Rais alitoa matamko hayo katika sherehe za maadhimisho ya Siku ya Sheria iliyofanyika mapema mwezi huu kwenye uwanja wa Mahakama Kuu jijini Dar es Salaam.

Lissu amesema TLS imepoteza mwelekeo na nafasi yake katika jamii kwenye masuala ya kisheria, hasa kushindwa kukemea vitendo vya uvunjifu na ukiukaji wa Katiba na sheria unaofanywa na viongozi.

“Chama cha wanasheria kinatakiwa kiwe cha kwanza kupiga kelele sheria za hovyo zinapotungwa, kinatakiwa kuwa mstari wa mbele kukemea vitendo vya ukiukaji wa Katiba na sheria vinavyofanywa na watu wenye mamlaka lakini Law society ya kwetu imekaa kimya,” amesema.

Kuhusu msimamo wake wa kisiasa na chama hicho endapo atapata nafasi hiyo, Lissu amesema masuala ya kisheria hayana uhusiano na vyama vya kisiasa na kwamba chama hicho kipo kwa ajili ya kulinda na kusimamia utawala wa sheria.

Pia, amesema kama chama chake kitakuwa na msimamo sawa na misingi ya chama hicho katika kutetea utawala wa kisheria, si tatizo na kwamba, ikiwa kitakuwa na msimamo tofauti katika mambo ya msingi, hakina budi kukosolewa.

“Sigombei ili kuipeleka Chadema ndani ya TLS. Masuala haya yanatuhusu sisi wote kujua mambo yanapoharibika, kuona sheria zinapokiukwa na kuona sheria mbovu zinapotungwa,” alisema.

Ofisa Maboresho ya Sheria wa TLS, Mackphason Buberwa amesema mchakato wa kupata wagombea umeshakamilika na waliopitishwa na kamati ni watano.

“Taratibu zimekamilika, kilichobaki ni wagombea kuandaa kampeni zao kabla ya Machi 18 siku ambayo uchaguzi utafanyika mjini Arusha,” amesema Buberwa.

Wagombea wengine ni Francis Stola, Lawrance Masha, Victoria Mandali na Godwin Mwapongo. Uchaguzi huo umepangwa kufanyika Machi 18 jijini Arusha ambako zaidi ya mawakili 6,000 wanatarajiwa kuhudhuria.

Jaji Chande Apewa Kazi Umoja wa Mataifa..!!

$
0
0

Jaji Mkuu mstaafu Othman Chande ameteuliwa kuongoza jopo la wataalamu watakaochunguza mazingira yaliyosababisha ajali ya ndege iliyomuua aliyekuwa katibu mkuu wa umoja huo, Dag Hammarskjold.

Uteuzi huo wa jaji mkuu mstaafu umefanywa na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa (UN), Antonio Guterres.

Hammarskjold alipoteza maisha katika ajali ya ndege iliyotokea Zambia mwaka 1961 wakati akitokea Congo ambayo ndiyo kwanza ilikuwa imepata uhuru.

Hammarskjold alikuwa nchini humo kwa ajili ya ujumbe wa amani.

Naibu msemaji wa UN, Farhan Haq amesema Chande ataongoza jopo hilo ambalo litakuwa na kazi kupitia taarifa zilizoandaliwa na wachunguzi waliopewa jukumu na katibu mkuu mstaafu, Ban Ki-moon.

Uchunguzi huo unafuatia azimio la Umoja wa Mataifa lililopitishwa na Baraza Kuu ambalo lilipendekezwa kufanyika uchunguzi wa kina kubaini mazingira ya ajali hiyo.

Awali, kulikuwa na ripoti kuwa Uingereza na Marekani zilikuwa zimegoma kutoa baadhi ya taarifa muhimu kuhusu tukio hilo, huku Afrika Kusini ikilalamikiwa kwa kushindwa kutoa majibu kwa baadhi ya hoja.

Ripoti iliyotolewa na wataalamu huru waliochunguza ajali hiyo inaeleza kuwa Hammarskjold aliuawa baada ya kunusurika kwenye ajali hiyo. Kumekuwa na taarifa kuwa ndege hiyo ilishambuliwa.

Jopo hilo linaloongozwa na Chande linatarajia  kuanza kazi mara moja na kwamba litakuwa na jukumu la kupitia nyaraka zote, ikiwamo ripoti ya kurasa 99 iliyoandaliwa na wataalamu wa awali waliochunguza mazingira ya ajali hiyo.

Vita Dhidi ya Madawa ya Kulevya..Wanawake Wawili Wadakwa na Kilo 114 za Bangi..!!

$
0
0

Wanawake wawili ni miongoni mwa watu zaidi ya 15 waliokamatwa kwa tuhuma za kukutwa na dawa za kulevya mkoani Mwanza

Watu hao wamekamatwa wakijihusisha nadawa hizo ndani ya wiki moja kuanzia Febuari 6.

Habari zinasema wanawake hao wamekamatwa wilayani Magu wakiwa na kilo 114.

Hata hivyo, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Ahmed Msangi amesema watuhumiwa 11 wamekamatwa wilayani Nyamagana na Ilemela na kilo 57 za dawa za kulevya aina ya miraa na kete mbili zinazodaiwa kuwa ni heroin.

“Mtuhumiwa mwingine ambaye ni mfanyabiashara wa vipuri vya magari, alikamatwa eneo la Butimba akiwa na kete 240 ya dawa za kulevya zinazodaiwa kuwa ni  heroin na ndunga mbili,” amesema.

Msangi amesema mtuhumiwa huyo alitaka kuzitumbukiza  chooni dawa hizo ili kupoteza ushahidi, lakini polisi waliwahi kukata bomba.

Lissu Afunguka Kasoro za Kisheria Alizofanya Makonda Wakati wa kutangaza Wahusika wa Madawa ya Kulevya,Adai Huenda Kesi Ikamgeukia Yeye Mwenyewe..!!!

$
0
0

Mbunge wa Singida Mashariki Tundu Lissu ametaja kasoro kadhaa katika zoezi la vita ya dawa za kulevya lililoanzishwa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Paul Makonda. 

Amesema, Kwanza, Mkuu wa Mkoa hana mamlaka yoyote ya kuelekeza watu kwenda kuripoti polisi. Hii ni licha ya mamlaka yake kama Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa na mamlaka yake ya kipolisi yapo chini ya Sheria ya Tawala za Mikoa. 

Pili, kwa mujibu wa Sheria ya Mwenendo wa Jinai, kila mtu ana wajibu wa kutoa taarifa ya kosa la jinai analoona limetendeka kwa polisi. Hii ni ile inayoitwa kufungua RB. Mkuu wa Mkoa Makonda alitakiwa afungue RB kwa wote anaowatuhumu kufanya biashara ya madawa. Hajafanya hivyo na ni kosa la jinai kutokufanya hivyo.

Tatu, kwa kutumia mamlaka yake ya kipolisi, Mkuu wa Mkoa Makonda alikuwa na uwezo wa kuamuru wale wote anaowatuhumu kufanya biashara ya madawa kukamatwa na kuwekwa kizuizini kwa masaa 48 na baadae kufikishwa mahakamani. Badala ya kuamuru 'wahalifu' hawa wakamatwe, Mkuu wa Mkoa Makonda aliwaelekeza wajipeleke polisi kwa mahojiano.

 Nne, kwa kuzingatia hatari kubwa ya madawa ya kulevya kwa jamii yetu, sheria husika za nchi zimeweka adhabu ya chini kabisa ya kifungo cha miaka 20 kwa wanaothibitika na mahakama kuhusika na biashara hiyo. Aidha, makosa ya madawa ya kulevya hayana dhamana kisheria. Iweje wale wote waliotuhumiwa na Mkuu wa Mkoa Makonda wamepelekwa mahakamani lakini wote wamepewa onyo tu au wamepewa dhamana Mahakamani. 

Kati ya mapolisi 11 waliotuhumiwa, hakuna hata mmoja aliyepelekwa mahakamani na kushtakiwa kwa tuhuma hizi. Badala yake, tunaambiwa wamesimamishwa kazi kupisha uchunguzi wa polisi dhidi yao. Kwa mujibu wa Sheria zetu za ajira, mtumishi anayesimamishwa kazi analipwa mshahara kamili kwa muda aliosimamishwa 

Tano, kitendo cha kuwatangaza watuhumiwa kwa namna alivyofanya Mkuu wa Mkoa Makonda, kesi yoyote itakayofunguliwa dhidi yao itaharibika. Kila mtuhumiwa atajitetea kwamba amekamatwa na kushtakiwa kwa sababu za kisiasa na kwa amri haramu za Mkuu wa Mkoa. Kila mtuhumiwa atajitetea kwamba hakuna RB yoyote iliyofunguliwa dhidi yake na kila wakili wa utetezi atataka Mkuu wa Mkoa Makonda aitwe mahakamani kwa ajili ya kuhojiwa. Makonda ataliwa nyama na mawakili kwenye cross-examination. Kwa kifupi, hii sio vita dhidi ya wauza 'unga', hii ni political charade na character assassination inayofanywa kwa mbinu za ovyo kabisa bila kufuata sheria Haitafika popote.

Askofu Josephat Gwajima: Dk Slaa Amenitumia Meseji Baada ya Kutoka Sentro

$
0
0

 AKIONGOZA ibaada katika Kanisa lake la Ufufuo na Uzima, Askofu Josephati Gajima leo Jumapili, Feb. 12, 2017 amesema kuwa amemtumiwa ujumbe na aliyewahi kuwa Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Wilbroad Slaa akimpa pole mchungaji huyo na kuonesha kusikitishwa kwake na kuhusishwa na biashara ya madawa ya kulevya.

MAHUBIRI YALIVYOKUWA; IBAADA YA ASKOFU JOSE PHAT GWAJIMA KATIKA KANISA LAKE LA UFUFUO NA UZIMA;

Kwaya wamemaliza kuimba mzee wa kanisa anawapongeza na kusema “Kama Gwajima angeendelea kuwa ndani na wauza madawa kuendelea kutanua mtaani basi hii kwaya leo ingekuwa inamalizia kurekodi album yake pale central”

Gwajima ameingia madhabahuni ananena

“Mheshimiwa rais anapigana peke yake, kama kuna mtu ana mpango wa kunitenganisha na rais, atashindwa, huwezi kunitenganisha na rais.

Gwajima amewaombea Rais Dkt John Pombe Magufuli,  Makam wa Rais, Bi Samia Suluhu, Waziri Mkuu Kassim Majaliwa na baadaye akamuombea Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda.

Gwajima: Nimeandikiwa meseji na DK Slaa

Askofu Gwajima baada ya kumaliza kuwaombea viongozi wakuu wa taifa amesema kuwa amandikiwa ujumbe kwa njia ya simu na aliyekuwa Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Willbroad Slaa.

“Baada ya kutoka polisi, viongozi wengi wa dini na serikali wamenipigia simu wakinipa pole lakini miongoni mwao ni Dk Slaa ambaye ameniandikia meseji.

“Sijajua yuko wapi, lakini ameniandikia ujumbe na nitausoma mbele ya waumini wote na Watanzania wasikie, sisomi huu ujumbe kwa ajili ya mambo ya kisiasa, la hsha nausoma ili kila niwaoneshe alichokisema Dk Slaa.”

UJUMBE WENYEWE

DK Slaa: Baba pole sana, pamoja na mengine yote, kwa hilo la madawa ya kulevya wamekuonea, hata kwa mali zako pia wanakuonea na kukudharirisha tu.

GWAJIMA: Nashukuru, nimepata meseji  yak leo baada ya kuachiwa.

Dk Slaa: Mungu yuko pamoja nawe kwenye kweli, nilisema nitasimamia ukweli, na siyumbishwi, nipo tayari kukutetea. Mwisho wa kunakili.

Yanga Waibabua 5 -1 Ngaya ya Comoro

$
0
0

KLABU ya Yanga imefanikiwa kuibuka na ushindi wa bao 5-1 dhidi ya Klabu ya Ngaya ya Visiwani Comoro.

Magoli ya Yanga yamepachikwa na Zulu dakika 43, Simon Msuva dakika ya 45, Chirwa dakika ya 59, Amis Tambwe dakika ya 65 na Thaaban Kamusoko dakika ya 7. Huku upande wa Ngaya, bao lao la kufutia machozi limepachikwa na Said Khalfan dakika ya 66

Uchokozi: Korea Kaskazini Yaifyatulia Kombora Japan

$
0
0

Korea Kaskazini kwa mara nyingine tena imefyatua kombora na kulielekeza upande wa Pwani ya Japan. Maofisa wa kijeshi kutoka Korea Kusini wamekadiria kombora hilo limesafiri umbali wa takribani kilomita 500 huku serikali ya Korea Kusini sasa imeitisha kikao cha kiusalama mjini Seoul .

Maafisa wa Pentagon nchini Marekani nao wamesema wamelifuatilia tukio hilo na kuongeza kuwa wamebaini ni kombora la masafa ya kadri.

Waziri wa mambo ya nje wa Korea Kusini amesema vitendo kama hivyo vya uchokozi unaoendelezwa na Korea Kazkazini vinaonyesha dhahiri jinsi utawala jirani yao huyo usivyo na makini huku wakipania kuwa na zana za Nuclear.

Waziri mkuu wa Japan, Shinzo Abe ambaye angali ziarani Marekani, ameshtumu ufyatuaji huo wa Kombora huku Rais Trump akimhakikishia Abe kuwa anamuunga mkono asilimia 100.

Harakati hizo za ufyatuaji wa kombora zimekuja siku moja tu baada ya mazungumzo kati ya rais wa Marekani Donald Trump na waziri mkuu wa Japan Shinzo Abe mjini Washington, ambako wamekubaliana kulipa kipa umbele swala la jinsi ya kukabiliana na vitisho vya zana za kinuklia kutoka Korea Kazkazini..

Baada ya Makonda Kulianzisha ,Rais Magufuli Amkabidhi Jukumu la Kupambana na Madawa ya kulevya Waziri Mkuu..!!

$
0
0

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli amemkabidhi Waziri Mkuu, Mhe. Kassim Majaliwa kazi ya kuzuia na kupambana na dawa za kulevya akiwa kama Mwenyekiti wa Tume ya Kudhibiti Dawa hizo nchini.

Rais Magufuli ameyasema hayo leo Ikulu Jijini Dar es Salaam wakati akiwaapisha Kamishna Jenerali wa Jeshi la Uhamiaji, Anna Peter Makakala, Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Kuzuia na Kupambana na Dawa za Kulevya, Rogers William Sianga pamoja na mabalozi watatu Mhe. Omary Yusuph Mzee, Mhe.Joseph Edward Sokoine pamoja na Mhe. Grace Aron Mgovano aliowateua hivi karibuni.

Dkt. Magufuli amesema kuwa Waziri Mkuu anatajwa kwenye Sheria Na.5 ya mwaka 2015 kuwa ni Mwenyekiti wa Tume hiyo ambapo Wajumbe wake ni Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Waziri wa Mambo ya Ndani, Waziri wa Elimu ana Mafunzo ya Ufundi, Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Waziri wa Fedha na Mipango, Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto pamoja na Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi.

“Nalipongeza sana Bunge la kipindi cha mwaka 2010 – 2015 chini ya Spika mstaafu, Mhe. Anne Makinda lililopitisha Sheria hii baada ya kuona sheria za mwanzo za kupambana na dawa za kulevya hazina nguvu hivyo Wabunge wa wakati ule walisimama kwa pamoja bila kujali itikadi za vyama vyao wakapitisha sheria hii,” alisema Dkt. Magufuli.

Aidha, Dkt. Magufuli amempongeza Rais Mstaafu Dkt. Jakaya Kikwete kwa kusaini sheria hiyo haraka mara baada ya Bunge hilo kuipitisha kwa sababu alijua madhara ya dawa za kulevya katika nchi yetu.

Amefafanua kuwa sheria imeeleza wazi katika kifungu cha 10 cha Sheria Na.5 ya mwaka 2015 kuwa jukumu la kupambana na dawa za kulevya linasimamiwa na Serikali pekee yaani Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Makamo wa Rais, Waziri Mkuu, Mawaziri, Wakuu wa Mikoa na Wilaya pamoja na Wakurugenzi wa Halmashauri za Wilaya au mtu yoyote atakayekuwa amepewa mamlaka ya kusimamia Serikali.

Kwa upande wake Waziri Mkuu, Mhe. Kassim Majaliwa amesema kuwa Taifa limeendelea kushuhudia kizazi chetu kikiendelea kudidimia kwa sababu ya matumizi ya dawa za kulevya na Serikali kwa mipango yake imeendelea kukemea, kudhibiti na kuchukua hatua mbalimbali dhidi ya wazalishaji, wasambazaji, wauzaji na watumiaji wa dawa hizo.

“Jambo hili limeleta athari kubwa sana kwani vijana wetu wengi wamepoteza uwezo wa kujisimamia katika shughuli zao za maendeleo kwa sababu baada ya matumizi tumeona athari kadhaa zikiwezo za kudhoofishwa kwa mwili, uwezo wa kutafakari pamoja na kutoweka kwa uwezo wa kufanya kazi,”alisema Waziri Mkuu Majaliwa.

Waziri Mkuu Majaliwa ameongeza kuwa Taifa hili la Watanzania kwa kiasi kikubwa linawategemea vijana waweze kuleta msukumo wa maendeleo ndani ya nchi hivyo jambo hili likiachiwa linaweza kuleta athari kubwa katika ukuaji wa uchumi na maendeleo yetu kwa ujumla wake.

Alisisitiza kuwa vita hii ilianza, inaendelea na itaendelea kupiganwa hadi imalizike hivyo Watanzania hawana budi kuunga mkono jitihada zozote zinazofanywa na Serikali kuhakikisha wanatokomeza uzalishaji, usambazaji, uuzaji na matumizi yake kwa namna yoyote ile, kila mmoja anatakiwa kushiriki kikamilifu ili kubaini matumizi ya dawa za kulevya ndani ya nchi hii.

Wenzetu Wanateseka Magerezani- Tundu Lissu ..!!!

$
0
0

Mbunge wa Singida Mashariki kwa tiketi ya CHADEMA Mhe. Tundu Lissu baada ya kufanikiwa kupata dhamana jana amefunguka na kuwashukuru watanzania huku akisema si jambio la kufurahia sana kwani bado wenzao wanapata mateso magerezani.

Mhe. Tundu Lissu ameyasema hayo kupitia mtandao wake wa twitter 

"Asanteni Watanzania kwa maombi yenu hatuwezi kushangilia kama bado wenzetu wanateseka Magerezani" alindika Tundu Lissu 

Mwanza: Ashikiliwa na Polisi kwa Kumuingilia Kimwili Mbuzi Jike..!!!

$
0
0

Wakazi wa Mwanza wameshuhudia kituko baada ya mkazi wa jiji hilo, Jumanne Nasibu kumuingilia kimwili mbuzi jike. Tukio hilo lilitokea baada ya mmiliki wa mbuzi hao kuwafunga malishoni wakiwa sita na baadae kuwakuta wakiwa watano na kuanza kumsaka mmoja kwa hofu ya kuibiwa ndio alipokumbana na mkasa huo.

Kamanda wa polisi mkoa wa Mwanza, amewataka wananchi kuripoti ili sheria zichukuliwe dhidi yao.

Video..Agizo la Rais Magufuli Kuhusu Madawa ya Kulevya kwa Vyombo vya Ulinzi..!!!

Manji Kachukuliwa na Gari la Wagonjwa (Ambulance) Kutoka Kituo cha Polisi Kati....!!!

$
0
0

Mfanyabiashara Yusuph Manji amekimbizwa kutoka kituo cha polisi na gari la wagonjwa alikoenda kwa mahojiano tangu Alhamisi. Gari lililombeba limeonekana kuishia kituo cha dharura kwa wagonjwa cha hospitali ya Taifa Muhimbili.

Zifahamu Dawa 5 Zinazotumika Kuwaachisha Watu SigaraI...!!!

$
0
0

moja ya vitu vigumu zaidi kuacha duniani ni sigara, ni watu wachache sana wenye juhudi kubwa hufanikiwa kuacha sigara kutokana na kiasi cha kemikali ya nicotine kilichoko ndani ya sigara ambacho kinamfanya mtumiaji apate kiu kali ya kutaka kuvuta sigara pale anapojaribu kuacha. ukiwa unaanza kuvuta sigara huwezi ukajua kua ipo siku utakuja kua mtumwa wa sigara lakini baada ya miaka kadhaa ndio utagundua kwamba umekua mtumwa na kuacha huwezi..

watafiti wamejitahidi kutafuta suluhisho la sigara na kugundua baadhi ya dawa , pamoja na kutumia dawa hizi mtumiaji lazima pia atumie njia kadhaa za kuacha ambazo sio za dawa kama kuamua moyoni kwamba ameamua kuacha, kukaa mbali na wavutaji sigara, kuanza mazoezi yeyote ya mwili ambayo kimsingi husaidia sana kuponya addiction, kula vizuri na kupumzika, kuepuka kutumia vilevi vyovyote ambavyo vitamrudisha huko na hata kuonana uso kwa uso na mshauri wa afya.
dawa zifuatazo zimesaidia baadhi ya watu kujikomboa na uvutaji wa sigara

bupropion; hii ni dawa ya mgandamizo wa mawazo ambayo pia hutumika kutibu watu wanaotaka kuacha sigara, hufanya kazi kwa kuondoa kiu kali ambayo huipata pale tu anapoacha sigara. mgonjwa hutumia dozi ya 100mg kutwa mara tatu huku akiendelea kuvuta sigara kisha wiki ya pili mgonjwa huacha sigara na kuendelea na dawa hizi angalau kwa muda wa wiki saba.

nicotine; hii ni kemikali inayopatikana ndani ya sigara ambayo inamfanya mtumiaji wa sigara ashindwe kuacha, hivyo wataalamu wameichukua kemikali hii na kuiweka kwenye jojo au big g ili mtumiaji aweze kuila kwa kutafuna jojo hizi kama mbadala wa sigara na baada ya muda fulani apunguze dozi ya jojo hizi mpaka pale atakapokua ameacha kabisa na mwili kuzoea kuisha bila nicotine. hutakiwi kutumia zaidi ya jojo 20 kwa ndani ya saa 24.

clonidine; hii ni dawa inayotumika kutibu presha ya kupanda lakini pia imethibitika kwamba inasaidia watu kuacha kuvuta sigara, matumizi yake ni kidonge kimoja kutwa mara mbili....unaweza kuanza kutumia dawa hii siku ya kuacha au siku tatu kabla ya kuacha na kuendelea nayo huku ukipunguza dozi kwa siku nne mpaka tano. hutakiwi kuacha dawa hii ghafla kwani huweza kupandisha presha ghafla.

varenicline; baadhi ya watafiti wanahisi dawa hii inafanya kazi kuliko dawa nyingi za kuacha sigara, hufanya kazi kwenye ubongo kwenye sehemu inayoitwa kitaalamu kama nicotine receptors kwa kumfanya mtumiaji asione raha kuvuta sigara lakini pia huondoa ile kiu mtumiajia anayoipata pale anapokosa kuvuta sigara. matumizi yake ni wiki mbili kabla ya kuacha sigara na kidonge kimoja humezwa na maji mengi baada ya kula. dawa hii huendelea kutumika mpaka wiki 12 na zaidi ili kumsaidia mtumiaje aache kabisa.

notriptyline; hii ni dawa inayotumika kutibu mgandamizo wa mawazo, ambayo pia husaidia kutuliza ile kiu mtu anayoipata anapokosa sigara. huanza kutumiaka siku 10 mpaka 28 kabla ya kuacha kuvuta sigara..dawa hii hupunguza uwezo wako wa kutumia mashine yeyote ya moto kwa kipindi hiko.. ni vizuri usitumie mashine yeyote ya moto au kuendesha gari.

mwisho; dawa hizi zina madhara madogo madogo na makubwa kama ilivyo kwa dawa zingine, ni vizuri kabla ya kuanza kuzitumia au kuzinunua uonane na daktari ili ujue kama wewe zinakufaa kwani kuna baadhi ya dawa hazifai wagonjwa fulani fulani kama wa moyo, kisukari au madonda ya tumbo. bahati mbaya hata kuzipata hapa nchini kwetu ni changamoto kidogo lakini kwa watanzania walioko nje wanaweza kuzipata hata watanzania wa ndani ya nchi wanaweza kuagiza nje kama wanaweza.

JPM: Hata Waziri Mkuu Hakulijua Hili..!!!

$
0
0

Rais John Magufuli amesema Waziri Mkuu Kassim Majaliwa  alikuwa hajui kama yeye ni Mwenyekiti wa Baraza la Kudhibiti Dawa za Kulevya kama ilivyobainishwa kwenye sheria.

Rais Magufuli amesema hayo wakati akiwaapisha viongozi mbalimbali, Ikulu na kuagiza wakachape kazi bila kumuogopa mtu yeyote.

“Kama anajua, amejua jana au leo. Nina uhakika hata mawaziri wake ambao ni wajumbe wa baraza hilo walikuwa hawana taarifa na hakuna aliyewakumbusha,” amesema Rais na kuongeza: “Hata mimi sikuletewa mapendekezo ya kumteua kamishna mkuu wa mamlaka hii (ya Kuzuia na Kupambana na Dawa za Kulevya, Rogers Sianga). Nilimteua kwa sequence (utaratibu) niliyonayo mwenyewe. Lazima tuwe wa kweli, tusijifanye malaika kwa kuficha ukweli,” alisema Rais Magufuli.

Pia, ameeleza kuchukizwa na kitendo cha watu kwenda Kituo Kikuu Polisi (Central) na kuanza kuosha gari la mtuhumiwa huku wengine wakienda na kwaya katika eneo hilo.

Tukio hilo lilitokea Alhamisi iliyopita wakati mwenyekiti wa Klabu ya Yanga, Yusuf Manji alipokwenda kuripoti polisi na baadhi ya mashabiki wake kuosha gari lake lililokuwa limeegeshwa katika kituo hicho.

Wengine wanaoaminika kuwa ni wanakwaya wa Kanisa la Ufufuo na uzima linaloongozwa Askofu Josephat Gwajima walifika eneo hilo wakati kiongozi wao alipokwenda kuhojiwa huku wakiimba nyimbo mbalimbali.


“Sitaki kuona tena wananchi wanajazana kituo cha polisi watuhumiwa wanapohojiwa. Lazima tujenge nidhamu, mbona hawakwenda Lugalo kwa CDF (Mkuu wa Majeshi) kuimba kwaya?” amesema Rais Magufuli huku akimuagiza Kamishna wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Simon Siro.



Wabunge Waingilia Kati Sakata la Tanesco la Kulipa Deni la Bilioni 300...!!!!

$
0
0

Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) imeahidi kujadili deni linalodaiwa Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) linalofikia Sh300.6 bilioni.

Tanesco inadaiwa deni hilo na Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) kutokana na mradi wa bomba dogo la gesi.

Mwenyekiti wa PAC, Naghenjwa Kaboyoka amesema wameipokea ripoti ya TPDC na kutokana na umuhimu wake, kamati hiyo itakaa kujadili na kutoa uamuzi.

“Kama unavyoona, shirika hili limepewa jukumu kubwa la kuhakikisha linasambaza gesi kwa Watanzania ili kuwezesha utunzaji wa mazingira. Ni lazima tuwasaidie waweze kupata fedha za maendeleo,” alisema.

Awali, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Tanesco, Dk Tito Mwinuka amesema deni hilo linaendelea kulipwa kidogokidogo na kwamba hata wiki iliyopita walipunguza.

Akizungumza katika mkutano wa TPDC na PAC, Mwenyekiti wa bodi wa shirika hilo, Profesa Sufian Bukurura amesema  pia wanaiomba kamati hiyo kuwasaidia ili wapate fedha za maendeleo ambazo Serikali iliahidi kuzitoa kama njia ya kukuza mtaji.


“Tungezipata hizo fedha tungeweza kulipa deni la Sh100 bilioni tunalodaiwa na taasisi mbalimbali,” amesema.


SMZ Yachachamaa Matokeo Mabaya Shuleni..!!!

$
0
0

Serikali ya Mapinduzi Zanzibar imesema kuna tatizo katika usimamizi wa elimu visiwani humo kiasi cha kusababisha kuwapo kwa matokeo mabaya kila mara.

Hayo yamesema na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Balozi Seif Ali Iddi alipokutana na viongozi wa shule na Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali katika Wilaya ya Kaskazini ‘B’ Unguja.

Balozi Idi amesema kamati za shule zina jukumu la kuondoa hali hiyo kwa kuwabana walimu kila wanafunzi wanapofanya vibaya ili waweze kupandisha kiwango cha ufaulu.

Amesema, kamati hiyo zinatakiwa kuwaita walimu na kuwaweka ‘kitimoto’ waeleze sababu badala ya kuwaangalia wakati jahazi la elimu linaporomoka.

Makamu huyo wa Rais wa Zanzibar amesema matokeo mabaya ya mitihani ya wanafunzi yanadhihirisha usimamizi mdogo wa walimu shuleni ikilinganishwa na miaka ya nyuma.

Hata hivyo, Waziri wa Elimu, Riziki Pembe Juma amesema pamoja na kuwapo kwa mikakati mbalimbali ya kiserikali kuinua elimu, wazazi wana nafasi yao kufanikisha suala hilo na kwamba, walimu peke yao hawawezi kufanikisha.


Riziki amewahamasisha wazazi na walezi kila mara wajitahidi kufuatilia mienendo ya watoto wao kuanzia shuleni hadi majumbani.

Walimu Waikomalia Serikali Madai Yao..!!!

$
0
0

Mwenyekiti wa Chama cha Walimu Tanzania (CWT) Mkoa wa Mara, Livingstone Gamba amesema licha ya walimu kupiga kelele kila mara, Serikali imekaa kimya kuhusiana na malimbikizo ya madai wanayoidai.

Gamba amesema wataendelea kupiga kelele bila kuchoka kwa kuwa wanachodai ni haki yao ya msingi na kwamba, jasho lililowatoka ndilo wanalolipigania.

Wakati kigogo huyo akisema hayo, Chama cha Walimu Tanzania (CWT) wilayani Tarime kimetangaza ‘mshiko’ wanaoidai Serikali umefikia Sh399 milioni.

Akizungumza kwenye mkutano wa kamati tendaji ya chama hicho wilayani Tarime, Mwenyekiti wa CWT wa wilaya hiyo, Shirikisho Nyagoseima amesema madai hayo ni matibabu (Sh30 milioni), likizo (Sh20. 6 milioni), masomo (Sh22.7 milioni), uhamisho (Sh183.8 milioni), mazishi (Sh6.3 milioni), usafirishaji mizigo (Sh20 milioni) na mishahara yanayofikia Sh245.3 milioni.

 “Tunaitaka Serikali kulipa stahiki hizi ili walimu wafanye kazi kwa kiwango kinachotakiwa ifikapo Machi Mosi ili tusiingie kwenye mgogoro,” amesema Nyagoseima.

Tayari Rais wa CWT ngazi ya Taifa, Gratian Mkoba ametangaza kuwa chama hicho kinatarajia kutangaza mgogoro na Serikali ifikapo mwezi ujao iwapo malimbikizo ya madai ya walimu yatakuwa hayajalipwa.

Magufuli Amuumbua Makonda,Katika Vichwa vya Magazeti ya Leo 13/2/2017..!!!

Nyasi za Tanzania Zinavyoinufaisha Australia..!!!

$
0
0

Ofisa Mtendaji Mkuu wa Kituo cha Mpango wa Kuendeleza Kilimo Ukanda wa Kusini mwa Tanzania (Saggot), Geoffrey Kirenga amesema kama kuna jambo linaloumiza ni Australia kutumia nyasi kutoka Tanzania kwa ajili ya malisho na kisha kurejesha maziwa na nyama kutuuzia hapa nchini.

Kirenga amesema hayo wakati akizungumzia namna Tanzania ilivyo fursa nyingi ambazo zimeachwa bila kuendelezwa au kushughulikiwa na wananchi ili kuwezesha Taifa kuendelea.

“Lakini cha kushangaza, Australia wanatumia nyasi za Tanzania kulisha ng’ombe wao halafu wanakuja kutuuzia nyama na maziwa,” amesema.

Ameongeza kuwa,“vilevile tuna tatizo la kuhifadhi chakula, mahindi yanayozalishwa nchini kwa mwaka ni kati ya tani milioni 6 hadi 7, lakini yanayohifadhiwa kwa njia za kisasa ni kati ya tani milioni moja hadi mbili yaliyobaki yanahifadhiwa kwa njia za kienyeji, yanaishia kuharibika. Ipo haja kwa Serikali ikatengeneza maghala katika maeneo ya uzalishaji.”  

Kirenga akasema katika ukanda wa Afrika Mashariki na Kati, Tanzania ina fursa nyingi za kilimo lakini tatizo ni  kukosa uthubutu na taarifa za uhakika.

 Naibu Ofisa Mtendaji Mkuu wa Saggot, Jennifer Baarn amesema wanaangalia matatizo yanayorudisha nyuma sekta ya kilimo na namna ya kuyatatua ili kuhakikisha mnyororo wa kuongeza thamani ya mazao unaleta tija kwa wakulima, hasa wadogo.
Viewing all 104789 articles
Browse latest View live




Latest Images