Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104780 articles
Browse latest View live

Hatariii..Waziri Mwakyembe Akiri Kushindwa Vita Dhidi ya Madawa ya Kulevya,Asimulia Jinsi Alivyoteseka Nayo..!!!

$
0
0

Waziri wa Sheria na Katiba Dkt. Harrison Mwakyembe, amepongeza jitihada za Rais Magufuli za kupambana na dawa za kulevya huku akisimulia alivyoshindwa vita hiyo wakati alipokuwa Wazri wa Uchukuzi, hususan katika Uwanja wa Ndege wa Dar es Salaam

Amesema alipata taarifa za kichunguzi kuhusu jinsi dawa za kulevya zinavyopitishwa katika uwanja wa ndege wa Dar es Salaam, na akaamua kutangaza vita akisaidiana na mtu ambaye hajamuweka wazi, lakini mwisho mtu huyo aliyekuwa akiongoza vita hiyo, aliishia kufungwa gerezani mpaka leo.

Mwakyembe amesema hata baada ya yeye kutumia nguvu zake kumtoa gerezani ameshindwa, jambo ambalo linaonesha kuwa vita dhidi ya dawa za kulevya ni ngumu kuliko kawaida, huku akionesha matumaini kuwa katika awamu hii, serikali itashinda.

Dk. Mwakyembe amezungumza hayo  jijini Dar es Salaam, alipokutana na wahadhiri na wanafunzi kutoka Shule Kuu ya Sheria ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, kwa lengo la kupokea mapendekezo ya kanuni ya kusimamia sheria mpya ya msaada wa kupata msaada wa kisheria iliyopitishwa na Bunge hivi karibuni.

Noma Sanaaa..Iddi Azzan Afurahi Kutajwa na Makonda Kuwa Anahusika na Madawa ya Kulevya..!!!!

$
0
0

Mbunge wa zamani Kinondoni, Iddi Azzan amezungumzia sakata lake na Jeshi la Polisi baada ya kukaa mahabusu kwa siku mbili alikokuwa akihojiwa kuhusu kuhusishwa kwake na masuala ya dawa za kulevya.

Mapema jana akiwa katika Kituo Kikuu cha Polisi Dar es Salaam, Azzan alisema aliingia katika orodha ya watuhumiwa kwa kuwa amekuwa akisemwa katika mitandao ya kijamii kwa muda mrefu.

Hata hivyo, alisema alifurahishwa na kitendo cha kutajwa kwenye orodha ya wanaojihusisha na biashara hiyo akiamini kwamba hatimaye suala hilo litafikia mwisho.

“Bora nilivyotajwa huenda suala hili litaisha kwa kuwa nimeanza kusemwa tangu mwaka 2011. Cha ajabu ni kwamba awali nilituhumiwa kujihusisha na biashara sasa hivi napimwa kuona kama natumia.

Mbunge huyo pamoja na Askofu Josephat Gwajima walitoka polisi saa 10:28 baada ya kuitukia wito uliowataka kuripoti hapo jana saa nane mchana.

Wakati Azzan aliondoka kituoni hapo kwa gari aina ya Toyota Rav 4 ‘short chassis’, Askofu Gwajima aliondoka kwa teksi.

Barcelona Waisoma Namba Ufaransa..!!!

$
0
0

Miamba wa soka wa Hispania Fc Barcelona wameanza vibaya hatua ya kumi na sita bora baada ya kukubali kichapo cha mabao 4-0 ugenini dhidi ya Psg ya Ufaransa.

Angel di Maria alianza kuwaandika Pgs goli kwa mpira wa adhabu uliokwenda moja kwa moja nyavuni, katika dakika ya 40 mshambuliaji mpya wa Wafaransa hao Julian Draxler akaongeza bao la pili.

Dakika ya 55 Angel di Maria tena akawachapa Barca bao la tatu, kabla ya Edinson Cavan kuhitmisha shughuli kwa bao la nne .

Katika mchezo mwingine Benfica ya Ureno wameibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Borrrusia Dotmund ya Ujeruman kwa bao la Konstantinos Mitroglo.

Ligi hiyo itaendlea tena leo kwa michezo miwili Bayern Munich wakiwalika Arsenal nao Real Madrid wakiwa wenyeji wa Napoli.

Lissu ni Shiidaaha.. Amnyoosha Kamanda wa Polisi Mahakamani..!!!

$
0
0

Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu na kamanda wa polisi wa Mkoa wa Ilala, Salum Hamdani wamechuana mahakamani katika kesi ya uchochezi inayomkabili mbunge huyo na wahariri wa gazeti la Mawio.

Hata hivyo, Hakimu Mkazi Mkuu Thomas Simba leo atatoa uamuzi wa kama Hamdani aeleze anachokifahamu juu ya Katiba ya Zanzibar na kama Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi  Zanzibar (ZEC), Jecha Salim Jecha anaweza kufuta matokeo ya uchaguzi.

 Hiyo ilikuwa ni baada ya Lissu kumtaka Hamdani, ambaye ni shahidi wa upande wa mashtaka, aeleze anachokifahamu kuhusu Katiba ya Zanzibar na kama Jecha anaweza kufuta matokeo ya uchaguzi.

Hakimu Simba alifikia uamuzi huo baada ya wakili wa Serikali, Paul Kadushi kupinga shahidi huyo kujibu swali hilo kwa sababu si mtaalamu wa sheria wala katiba hivyo hawezi kutoa tafsiri ya Katiba ya Zanzibar na kwamba Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu haina mamlaka ya kusikiliza masuala ya kikatiba.

Lissu alimhoji Hamdani maelezo yake yaliyo polisi aliyaandika kama nani? Mahojiano yao yalikuwa kama ifuatavyo:

Hamdani: Niliandika maelezo yangu kama mlalamikaji na kwamba mikusanyiko hiyo haikuwa haramu, ilikuwa halali kisheria.

Lissu: Mweleze mheshimiwa kama mihemko kisheria inakatazwa ama la?

Hamdani: Haikatazwi.

Wamempingaaah..Wenye Maduka ya Kubadili Fedha Dar Watoa Kauli Hii Nzito Juu ya Makonda..!!

$
0
0

 Baada ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda kueleza kuwa kuna maduka mengi ya kubadili fedha (Bureau de Change) ambayo yanatumika kutakatisha fedha za dawa za kulevya, wasimamizi wa maduka hayo wameeleza kutoshiriki, bali wanafuata utaratibu uliowekwa na Benki Kuu ya Tanzania (BoT).

Kwa nyakati tofauti wamesema kabla ya kuuza au kununua fedha za ndani na nje ya nchi, hupewa utaratibu ambao ni lazima waufuate.

Akizungumza juzi wakati wa kukabidhi majina 97 ya watuhumiwa wa uuzaji wa dawa za kulevya, Makonda amesema jijini Dar es Salaam kuna maduka ya kubadilishia fedha takriban 220 na nchi nzima yapo zaidi ya 400, hivyo utitiri wa maduka hayo unarahisisha kuingiza fedha za dawa za kulevya kwenye mzunguko na kusaidia kutakatisha fedha haramu.

Meneja wa duka la kubadilishia fedha la TK, Tukuza Amri amesema ndiyo kwanza amesikia tuhuma hizo kwa sababu wao hufuata kanuni na utaratibu wa BoT.

Hivi Ndivyo Madawa ya Kulevya Yalivyomnufaisha Makonda Ndani ya Kipindi Kifupi Tu..!!!

$
0
0

Baada ya kuja na operesheni ya kupambana na dawa za kulevya, jina la Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda linaweza kuwa ndilo lililotajwa zaidi katika mkutano wa Bunge uliomalizika wiki iliyopita na kwenye mitandao ya kijamii kwa wiki ya pili sasa.

Makonda alianza kuwa mjadala ndani na nje ya nchi baada ya kutaja orodha ya kwanza na ya pili ya watu maarufu wakiwamo wasanii, wanasiasa na viongozi wa dini na kuagiza wafike Kituo Kikuu cha Polisi, Dar es Salaam wahojiwe kuhusu dawa za kulevya.

Kasi ya kutajwa kwa jina lake iliongezeka zaidi Jumatano iliyopita baada ya kumtaja Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani bungeni, Freeman Mbowe, Askofu Josephat Gwajima na mfanyabiashara Yusuf Manji.

Hata hivyo, Mbowe, Gwajima na Manji wamekanusha vikali kuhusika na biashara hizo na kuahidi kumshtaki Makonda kwa kashfa. Gwajima na Manji wameshahojiwa polisi.

Katika mtandao wa kijamii wa JamiiForums, hadi kufikia juzi saa 8:00 mchana, kulikuwa na kurasa 49 ambazo jina la Makonda lilikuwa limetajwa mara 961 katika mijadala iliyokuwa ikiendelea.

Mijadala hiyo ilikuwa ikihusu kama Makonda yuko sahihi au la katika utaratibu alioutumia na kama ana mamlaka ya kuagiza watu kuripoti polisi.

Spika Ndugai Ampuuza Makonda,Habari Katika Vichwa Vya Magazeti ya Leo 15/2/2017..!!!

Ulinzi Waimarishwa Taasisi ya Moyo Muhimbili Ambako Yusuf Manji Amelazwa..!!!

$
0
0

Hali ya ulinzi imeimarishwa katika Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) alikolazwa mfanyabiashara Yusuf Manji baada ya kuugua ghafla akiwa polisi alikokuwa akihojiwa.

Manji aliyekuwa akihojiwa katika Kituo Kikuu cha Polisi jijini hapa alipelekwa hospitalini hapo juzi jioni akiwa ndani ya gari la wagonjwa aina ya Toyota Land Cruiser lenye nembo ya Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi (UNHCR) huku gari lake aina ya Range Rover likifuata kwa nyuma.

Askari wenye sare na wengine wakiwa na mavazi ya kiraia nje ya wodi aliyolazwa mwenyekiti huyo wa klabu maarufu nchini ya Yanga walionekana wakiimarisha ulinzi.

Ilipofika saa 4:13 asubuhi mfanyabiashara huyo alitoka kwenye chumba hicho na kuongozwa kuelekea upande mwingine wa jengo hilo.

Akiwa amevalia nguo za wagonjwa zenye rangi ya kijani, Manji alitembea taratibu kuelekea upande aliokuwa akielekezwa.

Alipoulizwa kuhusu uwapo wa Manji hospitalini hapo, Mkurugenzi Mtendaji wa JKCI, Profesa Mohamed Janabi alisema hawezi kuzungumzia taarifa za mgonjwa.

Februari 8, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda alitoa orodha ya watu 65, akiwamo Manji ambao aliwataka wafike Polisi kwa ajili ya mahojiano kuhusu masuala ya dawa za kulevya.


Hii ni kwa Wale Wanaokurupuka Kutoka Asubuhi Bila Kunywa ChaI,Soma Hapa Ujue Faida za Kunywa Chai Asubuhi..!!!!

$
0
0

Je, ni mara ngapi umekuwa ukiondoka kwako asubuhi bila kunywa chai? naamini inaweza kuwa ni mara kadhaa lakini wengine ikawa ndio desturi yao kabisa kutokunywa chai asubuhi wanapotoka nyumbani kuelekea kwenye mishughuliko au masomo yao.

Sasa leo ninazo hizi faidia kadhaa za kunywa chai wakati wa asubuhi kabla hujatoka kwako.

1. Husaidia kuongeza uwezo wako wa kufikiriwa chai  zaidi ya vile ambavyo utatoka bila kunywa chai asubuhi. Hivyo kama wewe ni mwanafunzi au mfanyakazi ni vyema kuzingatia unywaji wa chai kabla ya kuanza shughuli zako za siku husika.

2. Unapokunywa chai unajipunguzia hatari ya kuzongwa na magonjwa mbalimbali hususani yale ambayo si ya kuambukiza.

3.Pia unapokunywa chai asubuhi husaidia kuboresha mahusiano mazuri kati yako na familia yako. Kwa sababu unapoamka na kukaa meza moja na watoto au mke au ndugu na kunywa chai huwezesha wanafamilia kujuzana machache kuhusu siku hiyo kabla ya upilika 'ubuys' wa siku hiyo kuanza.

Mwanamke Huyu wa Marekani Ametembelea Nchi Zote 196 na Kuweka Rekodi ya Dunia..!!

$
0
0

Wakati ambapo wewe hujawahi kufika katika kila mkoa hapa Tanzania, kuna mwanamke wa Marekani ambaye amefika kwenye kila nchi duniani.

Kama haitoshi, ameweza kufika katika nchi zote 196 ndani ya miezi 18 na siku 26. Cassie De Pecol amevunja rekodi ya Guinness World iliyokuwepo mwanzo.

Mwanamke huyo alianza safari yake July 2015, akipigia debe utalii endelevu kama balozi wa taasisi ya International Institute of Peace Through Tourism.

Jumla, De Pecol ametumia bajeti ya $198,000 kuizunguka dunia.

Tembelea Tovuti Pendwa ya ASILI ZETU inayohusiana na Masuala ya Tiba Asilia Kama Kusafisha Nyota na Kumvuta Mpenzi

$
0
0
Tembelea  tovuti  pendwa  ya ASILI ZETUinayohusiana na masuala ya tiba asilia, kusomewa dua na visomo, kusafisha nyota,  kumvuta mume au mpenzi aliyekuacha, tiba ya magonjwa mbalimbali yaliyoshindikana,  mvuto wa biashara.

Pia tunatoa dawa za uzazi kwa wale kina mama wenye matatizo ya uzazi walio angaika kwa muda mrefu bila kupata mafanikio yoyote, kupandishwa cheo kazini, mali isiyohuzika kama vile kiwanja, shamba, nyumba, gari n,k.

Bonyeza Hapa: https://asilizetu.wordpress.com

Zilizotufikia Hivi Punde..Masogange Ndaniii Akamatwa na Polisi Sakata la Madawa ya Kulevya..!!!

$
0
0

TAARIFA zilizotufikia, zinaeleza kwamba video queen maarufu Bongo, anayefahamika kutokana na shepu yake matata, Agness Gerald almaarufu Masogange, anashikiliwa na Jeshi la Polisi, Kituo Kikuu (Central) akituhumiwa kuhusika na biashara na matumizi ya madawa ya kulevya.

Masogange alikamatwa na polisi jana usiku na taarifa zinaeleza kwamba, mpaka muda huu bado anashikiliwa central. Mwanadada huyo anaingia kwenye orodha ya wasanii wengine na watu maarufu Bongo, walioshikiliwa na wanaoendelea kushikiliwa wakihusishhwa na ishu ya matumizi na biashara ya madawa ya kulevya, katika vita kali inayoongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda.

Taarifa zaidi kuhusu kukamatwa kwa Masogange na kinachoendelea, zitaendelea kukujia kupitia hapahapa, endelea kufuatilia mtandao huu na pia kufuatilia Udaku Special Blog

BARUA NZITO: Salamu Zangu Kwako Mkuu wa Mkoa wa Dar, Paul Makonda...!!!

$
0
0

BILA shaka u-mzima wa afya, kaka yangu, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda. Pole kwa shughuli nzito ya ujenzi wa Taifa uliyonayo. Mimi ndugu yako ni mzima wa afya, namshukuru Mungu. Naendelea kupambana kwenye eneo langu, 

Ndugu yangu leo nimekukumbuka kwa barua. Nimeona si vyema vuguvugu hili la madawa ya kulevya likapita hivihivi bila mimi kuzungumza jambo na wewe. Kwanza nakupongeza. Umeonesha uthubutu wa hali ya juu.

Kwa vijana wa mtaani wanasema umejilipua. Si siri inahitaji ujasiri mkubwa sana kufanya jambo unalolifanya, ndiyo maana wengi wetu tumekuwa tukiishia kusema tu chinichini kwamba fulani anauza, fulani anatumia madawa ya kulevya lakini si hadharani.

Ndugu yangu mimi naona kwa ulichokifanya, kinapaswa kuungwa mkono na mtu yeyote kwa kuwa dhamira yako ilikuwa njema. Hata kama watu wameibuka na kukupinga, kuibua ‘madudu’ wanayoyajua lakini mwisho wa siku lazima tukubaliane tu, wewe umeonesha kwa vitendo kwamba unapaswa kuwa kiongozi.

Vita uliyoiingia, imewashinda wengi. Hawa ambao wanaibuka sasa hivi na kukosoa mfumo unaotumia, wengi wao walikuwa wanafahamu madhara ya madawa ya kulevya lakini kwa sababu wanazozijua, walifunga midomo yao. Mbunge wa Geita vijijini, Joseph Kasheku Msukuma (CCM) yawezekana alikuwa na hoja zake za msingi katika kukukosoa, lakini niliona ni vyema nguvu zake angezielekeza zaidi kwenye kukushauri na si kuibua yale ya utajiri wako na mambo mengine.

Niliona ni busara hayo ya utajiri, pengine angeyaibua kabla au hata baada ya sakata hili kupita kuliko kuliibua katika kipindi ambacho wewe unatupa silaha zako katika kupambana na madawa ya kulevya. Ongeza nguvu zaidi kaka, tuko nyuma yako.

Wewe umefanya, wengi wao wametutoa kwenye hoja ya msingi na kutupeleka kwenye hoja binafsi.  Wanataka kutulisha mambo binafsi,

tusahau tatizo la msingi. Nikwambie tu mkuu wangu wa mkoa, usikate tamaa, songa mbele. Pale ambapo unaona kunatolewa ushauri wa msingi kuhusu vita hii, ni vyema ukauchukua na kuufanyia kazi.

Tunakubaliana kwamba katika kusaka suluhu ya jambo, si rahisi kusikiliza kila mtu lakini kwa kuwa nawe ni kiongozi, hakika unao upeo wa kutosha wa kung’amua mambo.

Tangu sakata hili limeanza, nimejaribu kufuatilia, wapo watu wengi sana ambao wamekuwa wakishauri mambo ya msingi ambayo hata mimi naamini ukiyasikiliza, bado yataongeza tija. Mfano ni lile suala la kuwashughulikia kimyakimya, linaweza likatoa majibu chanya pia.

Kaka, una jeshi la polisi ambalo lipo chini yako, endelea kulimulika nalo kwani maneno ya kwamba wao ndiyo sehemu kubwa ya tatizo yanasemwa sana huku mtaani. Ni lazima uwe na askari juu ya askari. Wachungazane wenyewe kwa wenyewe, usimuamini mtu mmoja. Tuwe na askari waaminifu, watakaoweza kweli kutokomeza vijiwe vyote vya mitaani ambavyo vinajulikana hata kwa watoto wadogo kwamba sehemu fulani kunauzwa unga. Doria zifanyike mara kwa mara, wenyeviti wa mitaa kweli washiriki kikamilifu katika vita hii maana wao wanawajua watu wao.

Lengo letu ni moja, sidhani kama unaweza kukataa kupokea ushauri ambao nao una lengo la kujenga. Tunaamini kwa gia yako ya awali, unaweza pia kubadili gia ya pili kama hiyo ya kimyakimya na mambo yakaenda vizuri. Ni matumaini yangu utakuwa umenielewa na nikutakie kila la kheri katika mambo haya mazito ambayo umeyaanzisha.s

Mimi kama kijana mwenzio, nakuombea kwa Mungu, akupe ulinzi wake na uweze kutekeleza vyema wajibu wako hapa duniani kwa nafasi ambayo Mungu amekupa. Mimi ni ndugu yenu;

Erick Evarist

Gigy Money ..Waliohusika na Madawa ya Kulevya Wameniiga Mimi..!!!

$
0
0

WAKATI baadhi ya mabinti wanaohusika kama video queens kutajwa katika sakata la madawa ya kulevya hivi karibuni, Gift Stanford ‘Gigy Money’ ameibuka na kusema baadhi yao wanaponzwa na kuiga aina ya maisha anayoishi, hivyo kujikuta wakijihusisha na ishu hiyo.

“Naona wanapenda kuniiga maisha yangu sana, sijawahi kubeba au kutumia unga na sina hofu kabisa ya kutajwa maana huwa nafanya kazi halali, hao video queen wanaoiga na kutaka kuwa juu kama mimi hawajui kwamba siri ya mafanikio yangu ni kufanya kazi,” alisema msanii huyo ambaye licha ya kuwa video queen, pia ni mtangazaji wa redio.

Katika vita alivyoanzisha vya kupambana na madawa ya kulevya, Mkuu wa Mkoa wa Dar, Paul Makonda alitaja majina ya watu mbalimbali wanaotuhumiwa kujihusisha nayo, wakiwemo video queens, Lulu Abbas ‘Lulu Diva’ na Tunda Sebastian ambao walifikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi, Kisutu na kuachiwa kwa dhamana.

Natamani Kudate na Alikiba – Diva The Bosslady..!!!

$
0
0

Mtangazaji wa kipindi cha Ala za Roho cha Clouds FM, Diva The Bosslady amefunguka kwa kudai kuwa katika mastaa wa muziki Alikiba ndiye msanii ambaye anatamani kudate naye.

Diva ambaye kwa sasa anatoka kimapenzi na muimbaji Heri Muziki, alikuwa host wa show ya Valentine’s Day iliyofanyika Jumatano hii katika ukumbi wa Next Door na kuhudhuriwa na mastaa mbalimbali.

Akiongea na waandishi kabla ya kwenda kusherehesha show hiyo iliyoandaliwa na Irene Uwoya, Diva alidai Alikiba ndiye msanii ambaye anatamani kudate naye.

“Alikiba ndiyo msanii au staa ambaye natakamani kudate naye,” Diva alisema baada ya kuulizwa ni staa gani ambaye anatamani kudate naye. “Sijawahi kutoka naye kimapenzi, pia sasa hivi mimi nipo kwenye mahusiano na mtu mwingine,”

Mtangazaji huyo alidai yeye wanaume wake wengi wanawapata kupitia kipindi chache la Ala za Roho ambacho uchambua mambo mbalimbali kuhusu mahusiano.

Naibu Waziri wa Afya kuweka hadharani majina ya mashoga Dar es Salaam

$
0
0
Naibu Waziri Wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto, Dkt. Hamis Kigwangalla amesema kuwa atawaweka hadharani wanaume wote wanaojihusisha na mapenzi ya jinsi moja (mashoga) ambao hufanya biashara hiyo kupitia mitandao ya kijamii.

Naibu Waziri aliyasema hao jana usiku kupitia ukurasa wake wa Twitter ambapo alieleza kuwa yupo katika ziara jimboni kwake na mara atakaporejea jijini Dar es Salaam kabla ya kuhamia Dodoma rasmi ataiweka orodha hiyo hadharani.

Aidha, amesema kuwa wale wote wanaodhani kuwa vita dhidi ya wanaume wanaojihusisha na mapenzi ya jinsia moja ni mzaha, wataona hali itakavyokuwa kwani vita hiyo ni kubwa sana na wataishinda.

Kigwangalla ambaye pia ni mtaalamu wa afya alisema kuwa suala la mtu kuwa shoga si suala la kibaolojia (asili) bali ni watu tu kujiendekeza na hivyo watakahikikisha wanalikomesha.

Sheria ya ndoa ya Tanzania inapinga watu wa jinsia moja kujihusisha na mahusiano ya kimapenzi, lakini pia ni kitu kilichozuiliwa katika vitabu vitakatifu vya dini.


Dr. Kigwangalla,
Uchunguzi dhidi ya watuhumiwa wa ushoga unaendelea. Watakamatwa kimya kimya! Serikali ina mkono mrefu. Wakipatikana watatusaidia wenza wao!

 Dr. Kigwangalla, 
Kuna watu wanadhani vita dhidi ya ushoga ni ya mzaha, ni vita kubwa na tutaishinda. Mtandao ni mrefu na nitaendesha operation kamata kamata!

 Dr. Kigwangalla, H.
Namalizia ziara jimboni. Nikirudi Dar, kabla ya kuhamia rasmi Dodoma, nitaweka wazi orodha ya watuhumiwa wa ushoga wanaojiuza mitandaoni!

 Dr. Kigwangalla, H.
Kuna nchi marafiki zetu zinafanya jitihada za kupenyeza ushoga Tanzania na kudai ni haki ya binadamu kuchagua ampendaye, sisi tunasema NO!

 Dr. Kigwangalla, H.
Ushoga hauna addiction wala siyo wa kuzaliwa nao, wanaofanya hivyo wanajiendekeza tu! Ushoga siyo biological. Mashoga wote waache mara moja

Wastara Asema Anaweza Kumuacha Mpenzi Wake Bond Muda Wowote

$
0
0
Msanii wa bongo movie Wastara amemchana mpenzi wake wa sasa Bond kwamba asipojirekebisha baadhi ya tabia zake atamuacha na akimwacha hatarudi tena kwake.

Hata hivyo Wastara amesema anaweza kuvumilia shida anazopata kwa Bond lakini anaweza kumuacha muda wowote kwani hahitaji 'stress' za kimapenzi huku akiweka wazi kuwa amejitahidi na amefanikiwa kumrekebisha kwa 80 % na endapo ataendelea na mambo yake ya zamani zamani ataachana naye.

Akiongea kupitia eNewz ya EATV, Wastara amesema
"Niseme tu ukweli kwamba kwa Sajuki hakuna mtu anayeweza kufikia upendo wetu kwa kuwa Sajuki alikuwa anajali kila kitu ambacho nilikuwa nakipenda, kitu ambacho mpaka sasa sijapata ni mtu ambaye amefikia hatua za Sajuki ". Alisema Wastara.

Alichosema Kikwete Kuhusu Sakata la Dawa za Kulevya

$
0
0
Mbunge wa Jimbo la Chalinze Mkoani Pwani Ridhiwani Kikwete, amefunguka kuhusu sakata la dawa za kulevya na kuipongeza serikali hususani Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda kwa kuanzisha vita hiyo na kutaka wahusika wachukuliwe hatua.

Kikwete amefunguka hayo leo katika kipindi cha East Africa Breakfast cha EA Radio, kinachoruka kila siku saa 11:00 alfajiri hadi saa 3:00 asubuhi.

Ametumia nafasi hiyo kuishauri serikali kuifikisha mwisho vita hiyo, ili kulimaliza kabisa tatizo hilo kwa kuwa limepoteza vijana wengi wenye uwezo mkubwa na mchango katika taifa, huku akitolea mfano uwezo wa msanii wa Bongo Fleva, Langa ambaye kwa sasa ni marehemu ikidaiwa kuwa alipoteza maisha kutokana na dawa hizo, pamoja na shida alizokuwa akizipata msanii Ray C, za kutafuta dawa hizo hata usiku wa manane.

Ameitaka mamlaka mpya wa dawa za kulevya kuwachunguza watu 97 ambao majina yake yamekabidhiwa hivi karibuni na mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda, na yeyote atakayethibitika kuhusika, achukuliwe hatua, huku akionesha imani kubwa kwa Kamishna Mkuu wa Mamlaka hiyo, Dkt Rogers William Sianga.

Aunt Ezekiel Aeleza Kitu Ambacho Kilimuumiza Sana Kwenye Mahusiano yake na Mose Iyobo

$
0
0
Msanii wa filamu ambaye ni mama wa mtoto mmoja, Aunt Ezekiel katika usiku wa siku ya wapendanao alifunguka na kuzungumzia kitu ambacho kilimuuza katika mahusiano yake na Mose Iyobo.


Akiongea na Bongo5 usiku wa jana katika show ya Valentine’s Day iliyoandaliwa na Irene Uwoya, Aunt amedai kitu ambacho kilikuwa kinamsumbua ni kuambiwa anatoka na mkata viuno.

“Kusema kweli kuna mambo mengi yanatokea kwenye mahusiano lakini mimi hakuna kitu ambacho kilikuwa kinaniumiza kama watu kuniambia natoka kimapenzi na mkata viuno, nilikuwa naumia sana kusema kweli,” alisema Aunt Ezekel “Lakini baadaye nikawa nashangaa wao ambao wanadai natoka na mkata viuno wakaanza kumtumia meseji Mose kwamba wanamtaka,lakini nashukuru sikukata tamaa mpaka sasa nipo na Mose na tunapendana sana,”

Muigizaji huyo amedai amevumilia vingi mpaka sasa ambapo anafurahia maisha yake akiwa Mose Iyobo ambaye ni dansa ya Diamond Platnumz.

Alichokipost Diamond Baada ya Kukamatwa na Polisi Kwa Kuendesha Gari Bila Kufunga Mkanda..!!!

$
0
0
Viewing all 104780 articles
Browse latest View live




Latest Images