Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104698 articles
Browse latest View live

Pichaa..Thea Atinga Ofisini kwa Kamishna wa Madawa ya Kulevya Leo

$
0
0

Msanii mkongwe wa filamu Thea ameibua maswali kwa wadau wa mambo baada ya kuonekana mchana huu akiwa ofisi ya Kamishna wa operesheni wa mamlaka ya kupambana na kuzuia dawa za kulevya iliyopo Upanga jijini Dar es salaam.

Hivi karibuni wasanii mbalimbali wa filamu na muziki wamekuwa wakitajwa kuhusika katika sakata la biashara haramu ya madawa ya kulevya.

Issue ya Masogange Kushikiliwa na Polisi ka Kuhusika na Madawa ya Kulevya, Uwoya Amlipua Wema...!!

$
0
0

Lile sakata la masogange kuwekwa ndani kwa shutuma za madawa ya kulevya, limeingia ukurasa mpya baada ya hivi karibuni rafiki wa masogange ambaye pia ni staa wa filamu aitwaye Irene uwoya, kumjia juu wema sepetu baada ya kumtaja masogange kuwa mi miongoni mwa ma staa wanaotumia na kuuza madawa ya kulevya, staa hyo alitumia tafsida kufikisha ujumbe kwa wema sepetu kuwa alichokifanya sio ustaarabu ,alimtaka staa hyo kujifunza kutatua matatizo yake bila kumshirikisha mtu. 

Wema na uwoya ni mastaa ambao inasadikiwa wako kwenye bifu la chini kwa chini kwa muda mrefu, uenda sakata hili linaweza kuibua ugomvi mkubwa kwa mastaa hao wawili wenye mvuto wa aina yake

Mwakyembe: Masogange Aliniletea Nyodo...!!!

$
0
0

Dkt. Harrison Mwakyembe Waziri wa Sheria na Katiba ameendelea kufunguka changamoto zilizomkwamisha kudhibiti upitishwaji wa dawa za kulevya katika Uwanja wa Ndege wa Dar es Salaam wakati alipokuwa Waziri wa Uchukuzi hadi kuzidiwa kete na Agnes Masogange

Kupitia kipindi cha Breakfast cha East Africa Waziri Mwakyembe amesimulia kilichotokea wakati alipotaka kumdhibiti binti mmoja aliyedaiwa kupitisha masanduku matano ya ‘materials’ za kutengenezea dawa za kulevya aliyekamatwa nchini Afrika Kusini akitokea Tanzania.

Amesema baada ya kufuatilia sakata lile mbali na kuchukua hatua kwa watu waliomsaidia kupitisha mzigo uwanja wa ndege, aliamua kufanya jitihada za kumkamata binti huyo ili achukuliwe hatua, lakini muda mfupi baada ya binti huyo kurejea nchini, yeye alihamishwa wizara, hivyo kukosa nguvu ya kumshughulikia, hatua iliyofanya binti huyo kumfanyia “nyodo”.

Kumbukumbu zinaonesha kuwa binti ambaye alikamatwa nchini Afrika Kusini wakati huo kwa madai hayo, na kisha Waziri Mwakyembe kumfuatilia hadi kutimua baadhi ya watumishi wa uwanja huo Mwezi Agost mwaka 2013 alikuwa ni ‘video queen’ maarufu nchini, Agnes Geral d ‘Masogange’.

Aidha Mwakyembe amesema kijana wake mmoja anayefahamika kwa jina la Jingu ambaye yuko gerezani, anapaswa kuongezewa ulinzi kwa kuwa yeye ndiye aliyekuwa jemedari wa kudhibiti dawa za kulevya uwanjani hapo, lakini baadaye aliundiwa kesi na sasa huko gerezani anakutana na watu ambao wanaweza kumdhuru kutokana na kwamba yeye ndiye aliyesababisha wafungwe.

Baada ya Kumuita Nyani, Iyobo Amvaa Tena Harmorapa...!!!!

$
0
0

KIONGOZI wa madansa ambaye ni dansa tegemezi wa Wasafi Classic Baby (WCB) Mose Iyobo amefunguka kuwa yeye hana imani na Harmorapa na anashangaa anavyotajwa kila mahali kwani yeye hajawahi kusikia kazi yake yoyote hivyo hajui uwezo wake kimuziki.

Iyobo aliendelea kwa kutoa povu kuwa yeye anamchukulia Harmorapa kama mtu aliyekurupuka kwenye muziki na hajui ni nini anachotakiwa kufanya.

Kupitia eNewz ya EATV Iyobo alifunguka hayo huku akikazia kuwa muziki si jambo la mchezo mchezo bali unahitaji kujipanga.

“Mimi ni mtu ambaye nipo kwenye muziki muda mrefu, kila siku nyimbo mpya zinapotoka ziwe za watu maarufu hata wasio maarufu nazisikia lakini mimi sijawahi kusikia kazi yoyote ya Harmorapa, kwa hiyo sina cha kumshauri ila hiyo kazi anayofanya inahitaji mtu makini, anayekwenda na wakati na siyo kukurupuka tu na kufanya ghafla sababu hiyo kazi ina pesa nyingi na inatia umasikini kwa haraka sana kama hufanyi vile inavyotakiwa,” alisema Mose Iyobo

Nuh Mziwanda Akesha Akiomba Mapacha

$
0
0

MSANII wa muziki Bongo, Naftal Mlawa ‘Nuh Mziwanda’ amefunguka kuwa anakesha kila siku akimuomba Mungu amjaalie mke wake Nawal ambaye sasa ana mimba ya takriban miezi minne ajifungue watoto mapacha.

Akizungumza na Ijumaa hivi karibuni, Nuh alisema kuitwa baba wawili imekuwa ni ndoto yake ya muda mrefu na anaomba itimie kwa mkewe huyo kipenzi. “Niseme tu wazi kwamba natamani sana mke wangu ajifungue mapacha.

Naamini furaha yangu itakuwa zaidi ikiwa hivyo lakini hata akiwa mmoja pia nitashukuru. Kikubwa naomba mke wangu ajifungue salama ili na sisi tuingie kwenye ulimwengu wa wazazi,” alisema Nuh.

Nuh alifunga ndoa na Nawal mwishoni mwa mwaka jana na ilielezwa kuwa, wakati mwanadada huyo akiolewa alikuwa tayari ameshanasa mimba.

Video..Tazama Wimbo wa 'Am Sorry Jk' wa Nikki Mbishi Uliofungiwa na Basata..!!!!

Uwoya ni Gusa Unate..!!!!

$
0
0

Msanii maarufu wa filamu Bongo, Irene Uwoya (pichani)  anatajwa kuwa kati ya mastaa wa kike Bongo aliyewahi kutoka na mastaa na vigogo mbalimbali huku ikidaiwa kuwa, kila aliyekuwa naye alimuacha yeye na si kuachwa. Kwa mujibu wa rafiki wa karibu wa Uwoya aliyeomba hifadhi ya jila lake, staa huyo mwenye shepu na mvuto wa kudatisha kimahaba amekuwa akipapatikiwa sana na wan aume lakini mwisho wa siku huishia kuwaliza kwani yeye ndiye anayeamua kuendelea na wewe au akuache.

“Uwoya namjua vizuri sana, yule ni hatari kwa wanaume. Kwanza anajijua kuwa ni mzuri hivyo amekuwa akiwadenguliwa wanaume wengi sana na orodha ya wanaomtokea kila siku ni kubwa.

“Lakini akitokea kukupenda atakupenda kweli hadi unaweza kuona kero. Kwa kifupi anajua kupenda, kujali na kubembeleza kiasi kwamba ukinasa kwake ni vigumu kutoka ndiyo maana wapo wanaosema kwamba, Uwoya ni gusa unate!

“Ila sasa, anaweza kukuchanganya kwa mahaba mazito lakini siku akiamua kukuacha, anakuacha na si mtu anayependa sana kudumu na mwanaume mmoja kwa muda mrefu, fuatilia utagundua hili.

UWOYA ALIWAHI KUKIRI HILO

Katika moja ya mazungumzo na mwandishi wetu, staa huyo aliwahi kukiri kuwa, hapendi kugandwa sana na mwanaume mmoja kwa muda mrefu. “Yaani mimi kukaa muda mrefu na mwanaume sipendagi kabisa na sina mzuka huo. Ndiyo maana mtu nikiamua kumbwaga anahaha na wengine watabembeleza weee lakini wala sina tabia ya kurudi nyuma, kwa kifupi sipendi kudumu na mpenzi,” aliwahi kusema Uwoya.

KUMBUKUMBU ZINAONGEA

Hata hivyo, kumbukumbu zinaonesha kuwa, wanaume wengi waliowahi kutoka na staa huyo ukiacha mumewe, Hamad Ndikumana ambaye alionekana kufa na kuoza kwake kiasi kwamba hakukubali kirahisi kuachwa, wengi wao walioonja penzi lake ilikuwa vigumu kutoka hadi walipoachwa.

UWOYA ANASEMAJE?

Kufuatia ripoti hiyo, mwandishi wetu alimtafuta Uwoya ili kuzungumzia siri ya kugandwa na wanaume hadi kufikia hatua ya kuitwa gusa unate ambapo alikuwa na haya ya kusema: “Kwanza ujue mimi ni mwanamke ambaye sipapatikii mwanaume, anayetokea na kuonesha kunipenda, nikazungumza na moyo wangu ukakubali kumpa nafasi, namkubalia lakini ujue siku moyo wangu ukisema basi, hakuna mjadala, nakuacha. “Lakini lingine ni kwamba, moja ya sifa ya mwanamke ni kujua kumshika mwanaume, kwamba akiwa na wewe ujue kumfanya asifikirie kukuacha, ufanye kila unaloweza anase kwako, kwa hiyo utundu na ubunifu ndiyo siri yangu.”

HISTORIA YAKE!

Uwoya katika maisha yake ya kimapenzi amewahi kutoka kwa siri na vigogo pamoja na mastaa mbalimbali akiwemo pedeshee mmoja aliyekuwa akifahamika kwa jina la Ababuu, Nasibu Abdul ‘Diamond’, Hamis Baba ‘H-Baba’, Jovann Msami na wengineo.

Manati Kubwa ya Kurusha Madawa ya Kulevya Kutoka Mexico Mpaka Marekani Yakamatwa

$
0
0

Maafisa wa Marekani wanaoshika doria mpakani, wamegundua manati kubwa iliyokuwa inatumika kurushia dawa za kulevya kutoka Mexico- via BBC

Ubuyu wa Moto Moto...Zari, Wema Kuigiza Kwenye Film Pamoja.....!!!

$
0
0

Za chini kwa chini tunaambiwa kuna producer wa Filamu Bongo anataka kuwakutanisha Zari na Wema Sepetu katika movie moja matata na yupo tayari kuwapa mkwanja watakaohitaji kupitia sponsor but ugumu upo kwa mafahari hao wawili kukubali kuigiza pamoja

Kama Ulikuwa Unajiuliza Agness Masogange Kapata Wapi Ule Msambwanda Jibu Hili

$
0
0
Ndugu wa Agness Masogange Wakiondoka Mahakamani baada ya Masogange kutopandishwa mahakamani kwa kesi ya Madawa ya kulevya.. Kama ulikuwa unajiuliza Agness kapata wapi Msambwanda ule basi angalia picha........... Ila mpiga picha Mungu anakuona

Hali ya Afya ya Manji Yazidi Kudorora,Akimbizwa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete..!!

$
0
0

BAADA ya kupata dhamana ya Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu juzi, mfanyabiashara maarufu nchini, Yusuf Manji, amelazwa tena kwenye Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) iliyoko katika Hospitali ya Taifa Muhimbili.

Kwa mujibu wa taarifa zilizothibitishwa na Ofisa Uhusiano wa Taasisi hiyo jana, Anna Nkinda, Manji alifikishwa hospitalini hapo juzi jioni ikiwa ni muda mfupi baada ya kupata dhamana dhidi ya kesi ya kutumia dawa za kulevya aina ya heroin inayomkabili.

“Ni kweli Manji yupo hapa, aliletwa jana jioni (juzi) kwa matibabu ambapo hadi leo (jana) ninavyoongea na wewe bado yupo hapa amelazwa anaendelea na matibabu kama kawaida,” alisema Anna.

Hii ni mara ya pili kwa Manji ambaye pia ni Diwani wa Kata ya Mbagala Kuu, kulazwa kwenye taasisi hiyo.

Mara ya kwanza ilikuwa ni Februari 12, mwaka huu alipolazwa hapo akitokea katika Kituo Kikuu cha Polisi Dar es Salaam, alipokuwa ameshikiliwa tangu Februari tisa akifanyiwa mahojiano.

Mfanyabiashara huyo alifika mwenyewe kwenye kituo hicho cha polisi kutokana na wito uliotolewa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda, aliyetaja majina 65 ya watu aliodai wanajihusisha na biashara ya dawa za kulevya.

Mbali na Manji, baadhi ya watu wengine waliotajwa na Makonda na kutakiwa kufika kituoni hapo ni Mchungaji wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima, Mbunge wa zamani wa Kinondoni, Idd Azzan ambao tayari wamehojiwa polisi huku Mbunge wa Hai, Freeman Mbowe, akiwa bado hajahojiwa licha ya kutajwa kwenye orodha hiyo.

Juzi Alhamisi, Manji alifikishwa kwenye Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, ambapo shauri lake lilisikilizwa na Hakimu Mfawidhi wa Mahakama hiyo, Cyprian Mkeha.

Karani wa mahakama hiyo, Sarah Mulokozi, alimsomea mshtakiwa shtaka lake ambapo alidai kuwa kati ya Februari 6 na 9, mwaka huu eneo la Upanga Sea View jijini Dar es Salaam, Manji alitumia dawa za kulevya aina ya heroin.

Mtuhumiwa huyo alikana shtaka hilo na Mkurugenzi wa Mashtaka Msaidizi (ADPP), Osward Tibabyekomya, alidai kuwa upelelezi wa kesi hiyo bado haujakamilika na kuiomba Mahakama kupanga tarehe nyingine ya kutajwa.

Upande wa mawakili wa utetezi ambao ni Alex Mgongolwa na Hudson Ndusyepo, waliiomba Mahakama kumpa mshtakiwa dhamana  kwa sababu ya mashtaka yanayomkabili yanadhaminika.

Hakimu Mkeha alisema mshtakiwa atakuwa nje kwa dhamana kwa kutakiwa kusaini hati ya dhamana ya Sh milioni 10 pamoja na mdhamini mmoja wa kuaminika ambapo Katibu Mkuu wa Klabu ya Yanga, Charles Mkwasa, alimdhamini Manji, ambaye aliachiwa kwa dhamana hadi Machi 16.

Mara baada ya kupata dhamana, Manji aliondoka mahakamani hapo saa 9:40 akiwa kwenye gari yenye namba T670 BBX aina ya Hummer.


Sony Music Wampa Tuzo Alikiba kwa Wiews Milioni 5 za Video ya Aje

$
0
0
Label ya Sony Music Africa, imemtunuku tuzo Alikiba baada ya video ya wimbo wake Aje kufikisha views milioni 5 kwenye mtandao wa Youtube.

Amepewa tuzo hiyo Ijumaa hii jijini Johannesburg, Afrika Kusini kwenye makao makuu ya Sony Music Africa.

“What an incredible start to 2017! One month in and we’ve had the honour of presenting @officialalikiba an award for 5 million views of #AJE! 👏🏾 it was awesome having you with us today 🙏🏾 #KingKiba fans, #AJERemix is out today! Go watch the official music video on the AlikibaVEVO @youtube channel,” wameandika Sony kwenye Instagram.

Alikiba anajipanga kuanza ziara yake ya kwanza nchini humo.

TID: Nisingejiingiza Kwenye Kutumia Dawa za Kulevya Ningekuwa Tajiri Sana

$
0
0
Khalid Mohamed aka TID Mnyama, amekiri kuwa kujihusisha kwenye utumiaji wa dawa za kulevya kumemrudisha nyuma kiuchumi.

Akiongea kwenye kipindi cha XXL, kupitia Clouds FM Ijumaa hii, Mnyama ambaye alikiri hadharani kuwa mmoja wa mastaa walioathirika na matumizi ya dawa hizo, alisema hadi sasa angekuwa na utajiri wa kushangaza. Anasema dawa hizo zina gharama kubwa.

“Nadhani ningekuwa nimenunua kama magari mengine manane, ningekuwa nimefanya video za muziki kadhaa zenye kiwango kikubwa. Lakini nilitumia hela nyingi sana hasa pale ninapoenda kujirusha ningetumia hela nyingi sana,” alisema TID.
“Lakini hii imefikia mwishoni,” alisisitiza.
Staa huyo amedai kuwa dawa zilimfanya awe na mtazamo tofauti katika vitu vingi ambavyo alivichukulia rahisi rahisi.

“When you are high you think you are on top, nobody can touch you sababu you are under influence unaanza kugombana na watu, ukawajibu watu vibaya, but when you are clean unaweza ukafanya vitu, you can save a lot of money, you can be a better person, you can even marry a good girl, you can fall in love,” amesema Mnyama ambaye amejitolea kuwa balozi wa vita dhidi ya matumizi ya dawa za kulevya.

“It’s over now.”

Kwenye show hiyo TID aliachia wimbo mwingine uitwao Woman ambao amedai kuwa remix yake atamshirikisha Diamond.

Rapper AKA na Mtangazaji Bonang Matheba Wamwagana

$
0
0
Rapper AKA ametangaza kupitia Twitter kuwa yeye na mtangazaji wa redio na TV, Bonang Matheba wameachana.

Wawili hao walirejea kutoka kwenye mapumziko nchini Thailand wiki chache zilizopita na siku moja tu iliyopita walikuwa wakioneshana mahaba kwenye mitandao ya kijamii.

“Sad to announce that myself and Bonang have broken up. We tried guys,” alitweet AKA.

Hii ni mara ya pili AKA anatweet kuhusu kuachana na Bonang. Mwaka jana alisema hivyo pia lakini aliifuta post dakika chache baadaye, akisema kuwa waligombana na kisha kuachana.

Bonang bado hajazungumza chochote kuhusu kuachana kwao. Katika msimu wa sikukuu mwishoni mwa mwaka jana, AKA alimkunisha Bonang na ndugu zake.

VIDEO: Polisi Yaongea Kwanini Diamond Platnumz Hakufikishwa Mahakamani Kama Wale wa Singida

$
0
0
Mohamed Mpinga ni Mkuu wa kikosi cha usalama barabarani Tanzania na amekubali kukaa kwenye Exclusive Interview na AyoTV kujibu baada ya watu ku-comment kwenye mitandao ya kijamii baada ya kuona Diamond amepost picha akiwa na Kamanda na hakupelekwa Mahakamani.

Kamanda Mpinga ameeleza kwanini Mwimbaji Diamond Platnumz hakupelekwa Mahakamani baada ya video yake kusambaa akiendesha gari huku akiimba na kucheza wakati kuna wale wa Singida walipelekwa mpaka Mahakamani kwa kosa hilohilo……

TAZAMA HII VIDEO HAPA CHINI

Makonda Kuchunguzwa, Endapo Malalamiko Yakipelekwa Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma

$
0
0
SEKRETARIETI ya Maadili ya Viongozi wa Umma imesema ipo tayari kuhakiki mali za Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda, endapo watapokea malalamiko kutoka kwa wanaomtilia shaka.

Hivi karibuni wakati akitangaza orodha ya watu wanaotuhumiwa kuuza, kuagiza na kutumia dawa za kulevya,  Makonda alijikuta akiingia katika vita ya maneno na wabunge.

Msingi wa vita yenyewe ni hatua ya baadhi ya wabunge kupinga utaratibu alioutumia Makonda kuwataja kwa majina watuhumiwa hao na hata kwenda mbali zaidi wakimtuhumu na kuhoji alikopata utajiri wa ghafla.

Hatua ya kuhoji mali za Makonda ilichochewa na kauli ya Mkuu huyo wa Mkoa ambaye alionekana kukerwa na ukosoaji wa wabunge hao na hivyo kuwatuhumu wawakilishi hao wa wananchi kulala bungeni na kuitikia kila kitu ndiyoooo.

Akizungumza na MTANZANIA Jumamosi lililotaka kupata ufafanuzi kwa upande wa sekretarieti hiyo juu ya madai hayo ya utajiri wa Makonda na iwapo aliziorodhesha kama sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma ya 1995 inavyoelekeza, Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano wa sekretarieti hiyo, Joseph Ishengoma, alisema chombo hicho kipo tayari kufanya uhakiki endapo watapokea malalamiko rasmi kutoka kwa wananchi au wabunge waliosikika hivi karibuni wakizungumzia suala hilo bungeni.

Alisema kinachotakiwa ni kufuata utaratibu ambao ni kupeleka malalamiko kwa sekretarieti hiyo kuomba kufanyika kwa uhakiki wa mali za kiongozi huyo kutokana na tuhuma walizozitoa.

Kauli hiyo ya sekretarieti imekuja ikiwa imepita takribani wiki moja sasa tangu wabunge na Makonda washambuliane kwa maneno.

Miongoni mwa wabunge walioonekana kukerwa na kauli pamoja na utaratibu alioutumia Makonda na hata kutaka naye achunguzwe ni Mbunge wa Rombo (Chadema), Joseph Selasini,  ambaye alikwenda mbali na kutaja mali zinazodaiwa kumilikiwa na Mkuu huyo wa Mkoa wa Dar es Salaam.

Akichangia taarifa za Kamati za Bunge  za Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge na Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama, Selasini alisema Makonda amenunua jengo (apartment) lenye thamani ya shilingi milioni 600.

“Makonda amenunua apartment pale Viva Towers kwa shilingi milioni 600, Makonda amempa mke wake gari aina ya Mercedez Benz lenye thamani ya  Dola 250 za Marekani (shilingi milioni 550) kama zawadi ya birthday,” alisema Selasini.

Siku moja kabla ya Selasini kusema hivyo, Mbunge wa Geita Vijijini, Joseph Rushaku (Msukuma), naye aliibuka na tuhuma nyingine nzito dhidi ya Makonda na kutaka vyombo husika vimchunguze.

 “Mheshimiwa Spika, nasimama kwa kanuni ya 68(7) kuhusu jambo lililojitokeza jana (juzi) wakati wa mjadala wa Bunge…naomba mwongozo wako.

“Mimi binafsi naunga mkono jitihada za Rais kukamata wauza dawa za kulevya, lakini dalili ya kwanza ya kuanza kumhisi mtu kama anajishughulisha na biashara ambazo hazieleweki, kwanza ni mwenendo wa mtu yeyote…si mbunge wala si nani.
 “Anatumia Lexus ya petroli ya Sh milioni 400, lakini imekarabatiwa ofisi (yake) ya RC Dar es Salaam kwa zaidi ya Sh milioni 400 bila kufuata utaratibu wa manunuzi wa Serikali.
“Ana ma-V8 na Mwanza amejenga jengo la ghorofa…ni kina nani wanaotakiwa kujadiliwa na kufanyiwa uchunguzi? Na hawa mawaziri tulionao humu kwanini wamepigwa ganzi? Utawala bora, Mambo ya Ndani na Waziri wa Sheria…kwanini mmepigwa ganzi?”

Msukuma pia alihoji anakopata fedha Makonda za kwenda Paris na Marekani na kukaa siku 21 hasa ikizingatiwa kuwa tiketi moja ni Dola za Kimarekani 14,000 huku yeye na mkewe jumla ikiwa ni dola za Kimarekani 28,000.

Kutokana na hilo, Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano wa Sekretarieti hiyo, Ishengoma, alisema wabunge hao baada ya kutoa malalamiko ya kutilia shaka mali za Makonda, wanatakiwa kulipia kiasi cha shilingi 1,000 na kisha watapewa faili kwa ajili ya kuangalia na kujiridhisha mali ambazo Makonda alizitaja kwao.

Alisema na hiyo ni kwa mujibu wa Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma namba 13 ya mwaka 1995.

Alisema kwa kuzingatia Katiba na sheria hiyo, Sekretarieti itakuwa na wajibu wa kupokea hati za tamko rasmi zinazohitajika kutolewa na viongozi wa umma kwa mujibu wa Katiba au sheria nyingine yoyote.

Alisema kifungu cha 18 (b) kinaeleza kuwa; Sekretarieti itapokea malalamiko na taarifa za ukiukwaji wa sheria ya maadili ya viongozi wa umma kutoka kwa wananchi.

Kifungu cha 18 (c) Sekretarieti itachunguza tuhuma yoyote ya kuvunjwa kwa sheria ya maadili ya viongozi wa umma na viongozi wote wa umma wanaopaswa kuwajibika chini ya sheria hiyo.

Alisema pia sekretarieti katika kutekeleza majukumu yake kwa mujibu wa vipengele hivyo, itakuwa na mamlaka  ya kupokea na kusikiliza malalamiko yote kuhusu kiongozi yeyote wa umma yawe kwa mdomo au kwa maandishi kutoka kwa si tu wabunge hao bali kwa mwananchi yeyote bila kuuliza majina na anwani za watu waliopeleka malalamiko hayo.

Kwa mujibu  wa sheria ya maadili ya mwaka 1995 (23) (1) endapo mtu mwenye wadhifa wa waziri au wa mkuu wa mkoa amekiuka miiko hiyo malalamiko yanaweza kuwasilishwa kwa rais na mtu yeyote kwa maandishi yaliyotiwa saini, anwani na jina la mlalamikaji.

Zaidi, Ishengoma alisema taarifa ya mali za Makonda pamoja na viongozi wengine ziliwasilishwa katika ofisi yao Desemba 31, mwaka jana kwa mujibu wa sheria.

Alisema pamoja na hayo hatamzuia mtu kupeleka kile anachokijua ili waweze kufanyia kazi.

“Sheria hii yenyewe inampa mtu ‘Comsumption’ kama Kamishna wa Tume ya Maadili ataangalia kama mali zake zina ushahidi na ofisi inaweza kufanya uhakiki wa kupata taarifa sahihi kama alificha hizo mali hapo awali au la na hatua ya kwanza atapewa kubadilisha.

“Na kama Kamishna akiridhia kuwa amedanganya basi atapelekwa katika Baraza la Maadili na anayelalamika  anakuwa ni miongoni mwa mashahidi na kitakachofuata atajitetea na chombo hicho kitatoa mapendekezo,” alisema Ishengoma.

SELASINI ANENA TENA

Akizungumza kwa njia ya simu jana na gazeti hili lililotaka kujua iwapo atapeleka malalamiko katika Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kutaka kuhakiki mali za Makonda kama alivyomtuhumu bungeni, Selasini ambaye yupo jimboni kwake Rombo alisema hawezi kupeleka malalamiko kwa kuwa viongozi wengi ni waongo.

Katika hilo wao wamekwishataja na kilichobaki ni vyombo vya uchunguzi kufanya kazi hiyo.

“Watu wamejaza mali zao majina ya shemeji zao, wake zao, watoto wao, mahawara zao hivyo kupeleka malalamiko sisi ni kujidanganya tu.

“Sisi tumeshasema na si lazima tupeleke malalamiko, hapa kinachotakiwa ni vyombo vya uchunguzi vifanye kazi zake, kwani havina watu wa kuchunguza kuanzia safari ya Ufaransa siku 21 kwa kwenda Airport kuchunguza alivyoondoka,” alihoji Selasini.

Alisema hakuna haja ya vyombo vya uchunguzi kutupia aliouita mzigo kwa watu wengine huku akisema endapo atapeleka malalamiko shahidi atatakiwa awe yeye mwenyewe na hana muda wa kupoteza katika hilo.

Alisema siku ambayo alimtuhumu Makonda kumiliki mali hizo alipomaliza tu na kutoka alifuatwa na mtu aliyemtaja kuwa wa usalama na kumweleza kuwa Makonda Dodoma ana viwanja 19 na vipo kwa jina lake.

“Hilo nalo watataka tupeleke malalamiko, hapana wanatakiwa kufika tu Ardhi Dodoma na kuangalia jinsi ambavyo alivyoviandikisha vyote kwa majina yake, lakini kwa kupeleka malalamiko hatutafika katika hili na hutampata mtu, vyombo vya uchunguzi vifanye kazi yake tu,” alisema Selasini.

Alisema kuundwa kwa chombo hicho lengo lake nikuwa na viongozi wenye maadili hivyo kama watashindwa kufanya hivyo itakuwa ni kwa sababu ya kuingia katika siasa.

MSUKUMA

Alipotafutwa Msukuma kuelezea kama ana nia ya kupeleka malalamiko, alisema hiyo si kazi yake.

“Hizo ni kazi za Spika wa Bunge yeye ndiye anatakiwa kunipigia simu na kuniambia nipeleke malalamiko au wanipe maelekezo nifanye hivyo na si mwandishi,” alisema na kukata simu ghafla.


Utajiri wa Makonda Kuchunguzwa...!!!

$
0
0

SEKRETARIETI ya Maadili ya Viongozi wa Umma imesema ipo tayari kuhakiki mali za Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda, endapo watapokea malalamiko kutoka kwa wanaomtilia shaka.

Hivi karibuni wakati akitangaza orodha ya watu wanaotuhumiwa kuuza, kuagiza na kutumia dawa za kulevya,  Makonda alijikuta akiingia katika vita ya maneno na wabunge.

Msingi wa vita yenyewe ni hatua ya baadhi ya wabunge kupinga utaratibu alioutumia Makonda kuwataja kwa majina watuhumiwa hao na hata kwenda mbali zaidi wakimtuhumu na kuhoji alikopata utajiri wa ghafla.

Hatua ya kuhoji mali za Makonda ilichochewa na kauli ya Mkuu huyo wa Mkoa ambaye alionekana kukerwa na ukosoaji wa wabunge hao na hivyo kuwatuhumu wawakilishi hao wa wananchi kulala bungeni na kuitikia kila kitu ndiyoooo.

Akizungumza ili kupata ufafanuzi kwa upande wa sekretarieti hiyo juu ya madai hayo ya utajiri wa Makonda na iwapo aliziorodhesha kama sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma ya 1995 inavyoelekeza, Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano wa sekretarieti hiyo, Joseph Ishengoma, alisema chombo hicho kipo tayari kufanya uhakiki endapo watapokea malalamiko rasmi kutoka kwa wananchi au wabunge waliosikika hivi karibuni wakizungumzia suala hilo bungeni.

Alisema kinachotakiwa ni kufuata utaratibu ambao ni kupeleka malalamiko kwa sekretarieti hiyo kuomba kufanyika kwa uhakiki wa mali za kiongozi huyo kutokana na tuhuma walizozitoa.

Kauli hiyo ya sekretarieti imekuja ikiwa imepita takribani wiki moja sasa tangu wabunge na Makonda washambuliane kwa maneno.

Miongoni mwa wabunge walioonekana kukerwa na kauli pamoja na utaratibu alioutumia Makonda na hata kutaka naye achunguzwe ni Mbunge wa Rombo (Chadema), Joseph Selasini,  ambaye alikwenda mbali na kutaja mali zinazodaiwa kumilikiwa na Mkuu huyo wa Mkoa wa Dar es Salaam.

Akichangia taarifa za Kamati za Bunge  za Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge na Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama, Selasini alisema Makonda amenunua jengo (apartment) lenye thamani ya shilingi milioni 600.

“Makonda amenunua apartment pale Viva Towers kwa shilingi milioni 600, Makonda amempa mke wake gari aina ya Mercedez Benz lenye thamani ya  Dola 250 za Marekani (shilingi milioni 550) kama zawadi ya birthday,” alisema Selasini.

Siku moja kabla ya Selasini kusema hivyo, Mbunge wa Geita Vijijini, Joseph Rushaku (Msukuma), naye aliibuka na tuhuma nyingine nzito dhidi ya Makonda na kutaka vyombo husika vimchunguze.

 “Mheshimiwa Spika, nasimama kwa kanuni ya 68(7) kuhusu jambo lililojitokeza jana (juzi) wakati wa mjadala wa Bunge…naomba mwongozo wako.

“Mimi binafsi naunga mkono jitihada za Rais kukamata wauza dawa za kulevya, lakini dalili ya kwanza ya kuanza kumhisi mtu kama anajishughulisha na biashara ambazo hazieleweki, kwanza ni mwenendo wa mtu yeyote…si mbunge wala si nani.

 “Anatumia Lexus ya petroli ya Sh milioni 400, lakini imekarabatiwa ofisi (yake) ya RC Dar es Salaam kwa zaidi ya Sh milioni 400 bila kufuata utaratibu wa manunuzi wa Serikali.



“Ana ma-V8 na Mwanza amejenga jengo la ghorofa…ni kina nani wanaotakiwa kujadiliwa na kufanyiwa uchunguzi? Na hawa mawaziri tulionao humu kwanini wamepigwa ganzi? Utawala bora, Mambo ya Ndani na Waziri wa Sheria…kwanini mmepigwa ganzi?”

Msukuma pia alihoji anakopata fedha Makonda za kwenda Paris na Marekani na kukaa siku 21 hasa ikizingatiwa kuwa tiketi moja ni Dola za Kimarekani 14,000 huku yeye na mkewe jumla ikiwa ni dola za Kimarekani 28,000.

Kutokana na hilo, Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano wa Sekretarieti hiyo, Ishengoma, alisema wabunge hao baada ya kutoa malalamiko ya kutilia shaka mali za Makonda, wanatakiwa kulipia kiasi cha shilingi 1,000 na kisha watapewa faili kwa ajili ya kuangalia na kujiridhisha mali ambazo Makonda alizitaja kwao.

Alisema na hiyo ni kwa mujibu wa Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma namba 13 ya mwaka 1995.

Alisema kwa kuzingatia Katiba na sheria hiyo, Sekretarieti itakuwa na wajibu wa kupokea hati za tamko rasmi zinazohitajika kutolewa na viongozi wa umma kwa mujibu wa Katiba au sheria nyingine yoyote.

Alisema kifungu cha 18 (b) kinaeleza kuwa; Sekretarieti itapokea malalamiko na taarifa za ukiukwaji wa sheria ya maadili ya viongozi wa umma kutoka kwa wananchi.

Kifungu cha 18 (c) Sekretarieti itachunguza tuhuma yoyote ya kuvunjwa kwa sheria ya maadili ya viongozi wa umma na viongozi wote wa umma wanaopaswa kuwajibika chini ya sheria hiyo.

Alisema pia sekretarieti katika kutekeleza majukumu yake kwa mujibu wa vipengele hivyo, itakuwa na mamlaka  ya kupokea na kusikiliza malalamiko yote kuhusu kiongozi yeyote wa umma yawe kwa mdomo au kwa maandishi kutoka kwa si tu wabunge hao bali kwa mwananchi yeyote bila kuuliza majina na anwani za watu waliopeleka malalamiko hayo.

Kwa mujibu  wa sheria ya maadili ya mwaka 1995 (23) (1) endapo mtu mwenye wadhifa wa waziri au wa mkuu wa mkoa amekiuka miiko hiyo malalamiko yanaweza kuwasilishwa kwa rais na mtu yeyote kwa maandishi yaliyotiwa saini, anwani na jina la mlalamikaji.

Zaidi, Ishengoma alisema taarifa ya mali za Makonda pamoja na viongozi wengine ziliwasilishwa katika ofisi yao Desemba 31, mwaka jana kwa mujibu wa sheria.

Alisema pamoja na hayo hatamzuia mtu kupeleka kile anachokijua ili waweze kufanyia kazi.

“Sheria hii yenyewe inampa mtu ‘Comsumption’ kama Kamishna wa Tume ya Maadili ataangalia kama mali zake zina ushahidi na ofisi inaweza kufanya uhakiki wa kupata taarifa sahihi kama alificha hizo mali hapo awali au la na hatua ya kwanza atapewa kubadilisha.

“Na kama Kamishna akiridhia kuwa amedanganya basi atapelekwa katika Baraza la Maadili na anayelalamika  anakuwa ni miongoni mwa mashahidi na kitakachofuata atajitetea na chombo hicho kitatoa mapendekezo,” alisema Ishengoma.

SELASINI ANENA TENA

Akizungumza kwa njia ya simu jana na gazeti hili lililotaka kujua iwapo atapeleka malalamiko katika Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kutaka kuhakiki mali za Makonda kama alivyomtuhumu bungeni, Selasini ambaye yupo jimboni kwake Rombo alisema hawezi kupeleka malalamiko kwa kuwa viongozi wengi ni waongo.

Katika hilo wao wamekwishataja na kilichobaki ni vyombo vya uchunguzi kufanya kazi hiyo.

“Watu wamejaza mali zao majina ya shemeji zao, wake zao, watoto wao, mahawara zao hivyo kupeleka malalamiko sisi ni kujidanganya tu.

“Sisi tumeshasema na si lazima tupeleke malalamiko, hapa kinachotakiwa ni vyombo vya uchunguzi vifanye kazi zake, kwani havina watu wa kuchunguza kuanzia safari ya Ufaransa siku 21 kwa kwenda Airport kuchunguza alivyoondoka,” alihoji Selasini.

Alisema hakuna haja ya vyombo vya uchunguzi kutupia aliouita mzigo kwa watu wengine huku akisema endapo atapeleka malalamiko shahidi atatakiwa awe yeye mwenyewe na hana muda wa kupoteza katika hilo.

Alisema siku ambayo alimtuhumu Makonda kumiliki mali hizo alipomaliza tu na kutoka alifuatwa na mtu aliyemtaja kuwa wa usalama na kumweleza kuwa Makonda Dodoma ana viwanja 19 na vipo kwa jina lake.

“Hilo nalo watataka tupeleke malalamiko, hapana wanatakiwa kufika tu Ardhi Dodoma na kuangalia jinsi ambavyo alivyoviandikisha vyote kwa majina yake, lakini kwa kupeleka malalamiko hatutafika katika hili na hutampata mtu, vyombo vya uchunguzi vifanye kazi yake tu,” alisema Selasini.

Alisema kuundwa kwa chombo hicho lengo lake nikuwa na viongozi wenye maadili hivyo kama watashindwa kufanya hivyo itakuwa ni kwa sababu ya kuingia katika siasa.

MSUKUMA

Alipotafutwa Msukuma kuelezea kama ana nia ya kupeleka malalamiko, alisema hiyo si kazi yake.

“Hizo ni kazi za Spika wa Bunge yeye ndiye anatakiwa kunipigia simu na kuniambia nipeleke malalamiko au wanipe maelekezo nifanye hivyo na si mwandishi,” alisema na kukata simu ghafla.

Pendeza Kwa Kutumia Bidhaa zilizotengenezwa Kwa Asili Kutoka Markson Beauty Products

$
0
0

MWAKA MPYA NA
MAMBO MAPYA

Katika kusherehekea miaka kumi na saba (17) MARKSON BEAUTY tumezindua bidhaa mpya za mwaka 2017 kwa mafanikio makubwa.
Bidhaa mpya zimeboreshwa mara 3 zaidi hivyo zina matokeo ya haraka sana. Bidhaa zetu zimetengenezwa kwa mimea na matunda na kuthibitishwa ktk mamlaka husika. (NO SIDE EFFECTS).

BIDHAA MPYA NA BEI:-
1.Kerefusha nywele na kuzuia kukatika ovyo @120,000/=
2.Kuongeza shepu (hips na makalio) kwa (a)Dawa ya kunywa au kupaka @150,000/=
(b)Vidonge @170,000/=
3.Kuwa mweupe na softi mwili mzima kwa :- (a)mafuta @120,000/=
(b)Vidonge @150,000/=
4. Kupunguza unene, uzito na manyama uzembe @150,000/=
5. Kuongeza uume pamoja na nguvu za kiume kwa :-
(a)Gely ya kupaka @120,000/=
(b)Vidonge @120,000/=
(c)Mashine original ya HANDSOME UP @180,000/=
6.Kuondoa mvi milele zisiludi tena @120,000/=
7.Kuongeza hamu ya kula, unene na uzito wa mwili mzima @120,000/=
8.Kupunguza tumbo (kitambi) na nyama za pembeni kwa :-
(a)Dawa ya kunywa au kupaka @ 120,000/=
(b)Mkanda (corset) 150,000/=.
9.Kubust maziwa na kuyasimamisha @100,000/=
10.Kushepu miguu na kuwa minene @120,000/=
11. Kuondoa mipasuko mwilini (michirizi) @100,000/=.
12.Kurudisha usichana (bikra) @120,000/=
NB. HAKIKISHA UNAPATA RISITI YENYE MUHURI HALISI WA MARKSON CO PAMOJA NA GARANTII ILI KUKUHAKIKISHIA KUFANIKIWA KWAKO.
Popote ulipo duniani
Wasiliana nasi kwa (+255) 0767447444 au 0714335378. Utapata huduma zetu.
(Google seach MARKSON BEAUTY) or
Follow us
@Markson_beauty_pr @Markson_beauty_pr @Markson_beauty_pr @Markson_beauty_pr @Markson_beauty_pr @Markson_beauty_pr @Markson_beauty_pr @Markson_beauty_pr

Wafanyakazi Wawili wa TRA Mbaroni Kwa Kujihusisha na Biashara ya Madawa ya Kulevya

$
0
0

Jeshi la Polisi lawashikilia watumishi wawili wa TRA kwa tuhuma za kuhusika kupitisha viuatilifu vya kutengeneza Dawa za Kulevya.

Aidha watumishi wengine wawili wanafuatiliwa nyendo zao kabla ya kutiwa nguvuni kwa ajili ya mahojiano.

Taarifa hiyo imetolewa na Kamishna wa Intelijensia wa Tume ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya.

Mwanamke Aelezea Jinsi Askari Walivyombaka Msumbiji

$
0
0


Wakati Serikali ikiahidi kufanya uchunguzi wa vitendo vya ukiukwaji wa haki za binadamu katika kutimua Watanzania nchini Msumbiji, mwanamke mmoja amesema alibakwa na askari watatu kabla ya kuwekwa mahabausu ambako alikaa siku tatu bila kula.

Mwanamke huyo, aliyejitambulisha kwa jina la Halima (si jina lake halisi) ni mmoja kati ya zaidi ya Watanzania 180 ambao wamekuwa wakitimuliwa nchini Msumbiji tangu mwanzoni mwa wiki na wengi wakidai wana hati halali za kuishi nchi hiyo jirani na wengine kulalamikia vitendo vya ukiukwaji haki wakati wa utekelezaji wa operesheni hiyo.

Tayari Serikali imesema kuwa itafanya uchunguzi wa madai hayo, ambayo yanaweza kuharibu uhusiano wa muda mrefu wa Tanzania na Msumbiji.

Halima anasema walianza kufukuzwa usiku wa Jumamosi ya Februari 11, muda ambao askari hao waliutumia kumfanyia kitendo hicho.

Halima anasema kuwa alisikia watu wakivunja geti la nyumba waliyokuwa wakiishi na kudhania ni majambazi, kumbe walikuwa ni askari ambao waliwalazimisha kutoa nyaraka zao zote za kuishi Msumbiji pamoja na pesa.

“Niliwasikia wakivunja geti nikamwambia mume wangu watakuwa ni majambazi kumbe askari, mume wangu akajificha chini ya uvungu, lakini wakamtoa na baadaye kututoa ndani na kuanza kutupiga.”

Anasema baada ya kipigo walilazimishwa kuzoa mali zao kutoka ndani na zikawekwa kwenye gari la polisi na kisha kuwafunga mikono na baadaye kuwapeleka mahabusu.

“Cha kushangaza tulibebeshwa vitu wenyewe kuweka kwenye gari pasipo kuelezwa sababu baada ya hapo askari akanivuta nyuma ya nyumba na kuniingilia kimwili. Nikajua ni mmoja, lakini waliendelea hadi wakafikia watatu,” alisema.

“Ninaona aibu walinibaka kwa njia ya kawaida tofauti na taarifa za wengine wanaosema tulibakwa kinyume na maumbile, si kweli. Nawaomba waelewe hatukubakwa kinyume na maumbile kama wanavyosema ilikuwa kawaida.”

Hata hivyo anaeleza baada ya hapo waliwekwa mahabusu kwa siku tatu pasipo kula, hali iliyowalazimu kunywa maji yaliyokuwa yamewekwa chooni.

“Tulikaa mahabusu siku tatu, hamna kula wala kunywa, chooni tulienda kwa mtutu tukalazimika kunywa maji ya chooni kwa sababu hakukuwa na jinsi na njaa ilizidi. Kwa hiyo inabidi useme unakwenda chooni ili ukanywe maji,” alisema Halima.

Kutokana na hali hiyo, Halima anashangazwa na kauli ya Naibu Waziri wa Mambo ya Nje, Dk Susan Kolimba kwamba waliorudishwa hawakuwa na nyaraka huku kaimu balozi wa Tanzania nchini Msumbiji akiwatangazia wengine kuondoka ndani ya siku tano.

“Kweli mtu utathubutu vipi kuishi nchi ya watu bila kibali? Hata kaimu balozi na yeye anatukana, kwamba hatujaingia na documents (nyaraka)? Ilibidi atutetee lakini katukana. Mungu atatulipia,” alisema.

Mwanamke mwingine aliyewekwa mahabusu kabla ya kurudishwa nchini, Mary Makundi anasema askari wa kiume walimwambia awape fedha na alipowajibu kuwa hana, walimpekua na kuzikuta.

Anasema walizichukua fedha hizo pamoja na simu kabla ya kumpiga na kutaka kumbaka.

“Walivunja mlango wakanikuta. Wakaniambia niwape nyaraka zangu. Nikawapa nikijua wanazikagua tu na kuniacha, lakini cha kushangaza walizichana mbele yangu na kunitaka niwape pesa na simu. Nikawaambia sina wakanipiga na kunikagua hadi sehemu za siri na kuchukua pesa na simu,” alisema Mary.

“Baada ya hapo walinipiga kwanza kabla ya kunifunga mkono. Askari mmoja akataka kunibaka, nikamwambia kuwa hata kama hawatutaki nchini kwao, hawawezi kuniingilia bila kinga.

“Nilipoona hali imekuwa mbaya, nilisema wacha nigombane nife kwa silaha, lakini si kubakwa.”

Mtanzania mwingine Mohamedi Said ni mmoja wa wafanyabiashara walioambiwa waondoke pasipo kuchukua chochote na anadai kuacha mali zake zote pamoja na nyumba aliyojenga.

“Polisi walikuja ghafla wakatuambia wageni wote tunatakiwa tuondoke. Hapa nina vibali vyote mpaka leseni ya biashara, lakini imebidi niondoke kwa sababu ya usalama wangu,” alisema Said.

“Hakuna anayejua sababu mpaka sasa. Nimekuja nyumbani kufuatilia haki yangu kwa sababu mpaka kibali cha kujengea ninacho.

“Mpaka sasa amekuja kaimu balozi kutoka ubalozi wa Tanzania na amesema kwa ripoti aliyopewa ametupa siku tano tuondoke. Hatujui kwanini siku tano. Utahamishaje vitu kwa siku tano au kumtafuta mnunuzi wa nyumba kwa siku tano kwa sababu imenibidi niache duka kubwa na gari,” alisema Said.

Akizungumzia tukio hilo, mwenyekiti wa Kijiji cha Kilambo kilichopo mpakani na Msumbiji, Mohamed Mkama alisema wananchi wa kijiji chake wamekuwa wakishirikiana na wanakijiji wa vijiji jirani vya Msumbiji, lakini tukio hilo limewashangaza.

Amesema mara nyingi wamekuwa wakitembeleana na hata wengine kutoka upande wa Msumbiji kuja kutibiwa Tanzania kutokana na ujirani mwema uliopo.

“Kijiji changu kina vitongoji vitano ambavyo tumekuwa tukishirikiana na kijiji cha upande wa pili kwa muda mrefu na wengine wana vitambulisho vya uraia mwema, lakini tunashangaa kwanini wanarudishwa pasipo kuelezwa sababu,” alisema Mkama.

Ofisa uhamiaji Mkoa wa Mtwara, Rose Mhagama alisema idadi ya Watanzania waliorudi na kusajiliwa katika mpaka wa Kilambo ni watu 221 hadi kufikia jana mchana.
Viewing all 104698 articles
Browse latest View live


Latest Images