Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104776 articles
Browse latest View live

Kutana na John Ferraro..Mtu Mwenye 'Kichwa Nyundo' Anauwezo wa Kupigilia Misumari kwa Kichwa..!!!

$
0
0

MWANAMUME mmoja mburudishaji amewashangaza wengi kwa uwezo wake wa kugongelea misumari kwenye mbao akitumia kichwa chake mithiri ya nyundo.

Video na picha zilizowekwa kwenye tovuti ya asasi ya rekodi za dunia cha Guinness, zilionyesha umati ukishangazwa na jamaa huyo mkazi wa Boston nchini Marekani, John Ferraro.

Maelezo ya wataalamu wa afya yanasema fuvu lake la kichwa ni karibu mara tatu kwa uzito ikilinganishwa na binadamu wa kawaida.

Katika moja ya matukio alishuhudiwa akigongelea misumari 38 ya inchi tisa katika mbao kwa dakika mbili tu, akilenga kuvunja rekodi ya dunia kuhusu misumari mingi zaidi iliyogongelewa kwa kutumia kichwa kwa dakika chache zaidi.

Inasemekana mbali na kipaji hicho kisicho cha kawaida, jamaa huyu ni mwanamieleka.

Ferraro si tu ana uwezo wa kupigilia misumari kwa kichwa bali pia anaweza kustahimili tofali zito kuvunjwa kichwani mwake kwa kutumia mipira mizito ya mchezo wa kuviringisha tufe (bowling).

Kana kwamba hiyo haitoshi, Ferraro huruhusu watu kuvunja matofali katika kichwa chake.

Ferraro ambaye ni mkazi wa Boston mara ya kwanza alijigundua kuwa na kipaji akiwa mvulana wakati alipojigonga kichwa kwa kishindo kikubwa katika mlango wao mzito uliotokana na mwaloni wakati akimkimbiza kaka yake.

Mwenyewe anasema: “Nikiwa bado mdogo wakati namkimbiza kaka yangu ulipotokea ugomvi, alifunga mlango kwa nyuma ili kunikwepa. Kwa bahati mbaya sikuwa na hili wala lile nilijikuta nikiugonga kwa kishindo kwa kichwa kwa bahati mbaya na kusababisha ulegee bawaba zake na fremu zake.

“Wakati  nilipokuwa mkubwa nilitumia kila aina ya mbinu kukuza kipaji changu kupitia usomaji wa vitabu vya zamani na makala kisha kufanyia mazoezi niliyojifunza pamoja na mbinu za mafunzo.

“Maandalizi, mafunzo na dhamira ya kufikia lengo viliniwezesha kujiamini juu ya uwezo wangu. Wakati muda wa kufanya onesho huwa nafanya kweli na kutoa burudani itakiwayo.

“Wakati wa maonesho haya ya kugongelea misumari, kupasua tofali kichwani kwa kutumia mpira mzito, 'maumivu huwa si kitu hata kidogo, nguvu ya akili na moyo ndivyo vinavyoniongoza. Inapobidi kutoka damu kwa ajili ya sanaa niioneshayo, hutoka damu. Ni kitu cha kukufanya uweze kujiamini mwenyewe,” anasema.

Anasema kuwa unachotakiwa ni kujiamini kwamba una nguvu na kitu kitapinda, kuharibika au kuvunjika.

Kitabibu, fuu la mburudishaji huyo ni karibu mara tatu ya wastani wa kawaida wa binadamu, likipimika kwa unene wa milimita 16 kulinganisha na wastani wa milimita 6.5 wa kawaida.

Ferraro alifanyiwa vipimo vya scan ya MRI katika shule ya Utabibu Harvard mjini Boston na wataalamu wa nyolojia na maradhi ya ubongo.

Ilifichua kwamba hana tatizo lolote la kiafya katika fuu lake na kumfanya Ferraro aamini ni zawadi toka kwa Muumba.

Kupitia uchunguzi wa kina wa x-ray, wataalamu wa afya walibainisha kuwa ubongo wa mburudishaji huyo uko vizuri licha ya kukumbana na vipondo karibu kila siku wakati akifanya maonesho.


Anasema: “Kamwe sijawahi kuumia au kupata athari kichwani au ubongoni kutokana na nguvu kubwa ya vipondo kichwani. Madaktari wanashangazwa kwamba niko vile vile kiafya bila kuumia kutokana na shughuli pevu ya gongagonga inayokabili kichwa.

Farraro kwa sasa ameshaweka rekodi mbili katika Kitabu cha Rekodi za Dunia, Guinness World Records moja ikihusu kuvunjwa kwa tofali kwa kutumia mpira mzito wa bowling wenye uzito wa lb 16 sawa na kilo saba kutokea umbali wa futi 10 juu ya kichwa chake. Nyingine ya kupigilia msumari katika mbao kwa kutumia kichwa.

Hiki ndicho Alikiba Alichowaambia Sony Music Kuhusu Mashabiki Wake

$
0
0


Alikiba ameyasikia malalamiko ya mashabiki wake kuhusu ukimya wake wa hapa na pale na amekiri huumia sana kuona wakimrushia lawama.


Kutokana na ukweli huo, hitmaker huyo wa Aje amedai kuwa amelazimika kuwaambia mabosi wa Sony kuwa wajipange vyema ili kuhakikisha kuwa mashabiki wake wanaridhika.


Kwenye interview na millardayo.com, Alikiba amedai kuwa CEO wa Sony Music Africa, Sean Watson, ameiambia bodi ya label hiyo jinsi Alikiba alivyo na mashabiki wengi nyuma ambao panapotokea kuchelewa kwa lolote, ‘hung’ata kama nyuki.’


“Kwahivyo they have to make sure kila kitu kinaenda on point, kila kitu hakitakiwi kudelay, kila kitu kinakwenda sawa,” amesema Kiba.

Siwema: Nay Alinitapeli Mil. 7 Hivi Hivi Najiona..

$
0
0

MZAZI mwenzake na staa wa Hip Hop Bongo, Emmanuel Elibariki ‘Nay wa Mitego’, Siwema ameibuka na kutoa simulizi yake ya nyuma na kusema kamwe hatasahau mzazi mwenzake huyo alivyomuongopea na kumpiga shilingi milioni 7 taslimu.

Siwema aliivujisha ishu hiyo hivi karibuni wakati mwanahabari wetu alipomtaka aseme kitu gani ambacho hatakisahau kutoka kwa mpenzi wake huyo wa zamani ndipo mrembo huyo alipofunguka hayo lakini akasema hata hivyo, alishasamehe kwa sababu yalitokea kwenye kipindi ambacho penzi lilikuwa motomoto.

“Si unajua tena mtu ukikolea, kuna kipindi aliniambia ametaitiwa polisi, zinahitajika hela, nilipata mshtuko kweli, ikabidi niende benki haraka, nikamtumia. Nilishasamehe maana tuliyazungumza na tukiwa kama wapenzi yaliisha, ila sitasahau aisee,” alisema Siwema.

Alipotafutwa Nay ili kumsikia kama ana lolote kuhusu ishu hiyo, simu yake iliita kwa nyakati tofauti bila kupokelewa kwa takriban wiki tatu mfululizo.


Masikini Ndugu wa Masogange…

$
0
0

Video Queen mwenye umbo ‘matata’ Bongo, Agnes Gerald ‘Masogange’, amesoteshwa rumande na Jeshi la Polisi kufuatia kuendelea kumshikilia katika Kituo Kikuu cha Polisi Dar es Salaam ‘Central’ kwa msala wa madawa ya kulevya huku ndugu zake nao wakisota kwenye Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu wakisubiri apandishwe kizimbani bila mafanikio.

Februari 16, mwaka huu, Jeshi la Polisi kupitia kwa Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, CP Simon Siro, lilithibitisha kumshikilia mrembo huyo kwa mahojiano na vipimo juu ya tuhuma za kujihusisha na utumiaji na usafirishaji wa madawa ya kulevya huku likiahidi kumfikisha mahakamani jana lakini likagonga mwamba.

Mapema jana, Risasi Jumamosi liliweka kambi mahakamani hapo likimsubiria Masogange endapo atafikishwa na kupandishwa kizimbani kusomewa mashitaka yake lakini hadi mawio, mrembo huyo hakufikishwa kwa madai ya kutokamilika kwa upelelezi wa mashitaka yake.

Ndugu, jamaa na marafiki wa Masogange walijitokeza mahakamani tangu asubuhi wakisubiria kama ndugu yao huyo atafikishwa mahakamani hapo lakini hakuweza kufikishwa hivyo wakajikuta wakikata tamaa baada ya kusota kwa muda mrefu hivyo kuondoka eneo hilo kwa huzuni na kulengwalengwa na machozi.

Wakiwa kwenye banda la kusubiria, ndugu hao wa Masogange, muda mwingi walisikika wakinung’unika kutokana na ndugu yao kukawizwa kufikishwa mahali hapo kiasi cha wengine kuamua kwenda Central kuulizia kama uwezekano wa kumleta utakuwepo.

Baadhi ya waliokwenda Central waliulizia kwa askali waliokuwepo kituoni hapo na kujibiwa kuwa hataweza kufikishwa mahakamani jana  kufuatia majibu ya Mkemia Mkuu wa Serikali kukawia kufika polisi.
Baada ya hali kuwa hivyo, waliporudi Kisutu walikusanyana pamoja na kuamua kuondoka mahakamani hapo huku wakilalama kuwa, ni kwa nini kama polisi walifahamu wazi kwamba jana hawatamfikisha, wangewaambia ili waendelee na shughuli zao.

“Hatujapendezwa kabisa na hali hii, maana kama walijua hawataweza kumfikisha mahakamani leo (jana) hapakuwa na sababu ya kutuficha, maana tungewaona wema kama wangesema tukaendelea na shughuli zetu.

“Hebu ona sasa hawajamleta na leo (jana) ni Ijumaa, kama siyo usumbufu ni nini? Kutomleta maana yake si watamuweka hadi Jumatatu?,” walisikika wakilalama baadhi ya ndugu hao.

Hadi Risasi Jumamosi linaondoka mahakamani hapo majira ya saa 10:00 jioni, Masogange alikuwa hajafikishwa kwa madai ya kutokamilika kwa baadhi ya nyaraka za upelelezi wa kesi yake hiyo.

Hivi Ndivyo Uzuri wa House Girl Ulivyomponza Mke wa MTU Mpaka Akaambukizwa Ukimwi

$
0
0

Inasikitisha sana. Fuatilia mkasa huu mwanzo mwisho....

Mke alimhisi mmewe kuwa anatembea na housegirl wao kutokana na ukweli kuwa, housegirl alikuwa mzuri mno kimuonekano, kiumbo na kwa sura. Alifikiri kumfukuza ila mme aligoma kutokana na uchapakazi wa binti yule. Hivyo, hakuona sababu ya msingi ya kumfukuza. Hakika housegirl alikua akizidi kumnyima usingizi mke wa boss. Kadri siku zilivyozidi kwenda, housegirl alizidi kumeremeta. Kila nguo aliyovaa ilimpendeza. Kila mkao aliokaa alionekana ni wa kimitego na hofu iliendelea kutanda kwa mke wa boss.

Mke alizidi kuhisi na mbaya zaidi kila siku usiku wakati mmewe akiaga kuwa anaenda kuangalia mpira sebuleni baada ya muda mfupi mke alikuwa anasikia miguno chumba mwa housegirl hivyo akajua itakua tu ni mmewe huwa ananyata na kumuingilia housegirl wao ndio maana mme shughuli chumbani siku za karibuni ilionekana kumshinda kwa kuchoka haraka mno.

Jumamosi moja aliamua kumtuma housegirl kijijini kwa safari ya siku mbili bila kumjulisha mmewe wala mtu yeyote pale nyumbani. Usiku ule wa Jumamosi mme alimwambia mkewe utaratibu wake wa kawaida kuwa anaenda kuangalia mpira kwenye tv ya sebuleni. Kama kawaida, mke alikubali na mme akaenda sebuleni. Mke taratibu aliingia chumbani kwa housegirl akajilaza kitandani uchi kama alivyozaliwa. Kama kawaida alisikia mlango ukifunguliwa taratibu akaingia mtu akapanda kitandani na bila kuuliza akavua nguo akaanza kula tunda. Baada ya goli la 5, mke alisema, *_"INATOSHA. LEO NIMEKUKAMATA. KUMBE HIVI NDIVYO HUWA UNAFANYA NA HOUSEGIRL WAKATI UKIWA NA MIMI GOLI MBILI TU UNASEMA UMECHOKA? MCHEZO WAKO HUU NDIYO UNAKUMALIZA NGUVU NA UKIJA CHUMBANI KWANGU UNASEMA UMECHOKA WAKATI HAPA TAYARI MABAO MATANO NA UNATAKA UENDELEE?_*"

Kwa MSHTUKO, ghafla mme alijibu, "SAMAHANI mke wa boss sikujua kama ni wewe. Mimi ni houseboy wenu mkata majani; nisamehe tafadhali!"

Mke alishtuka akapiga kelele kwa kupaniki maana alimjua houseboy wao alivyo mwathirika hata kumuajiri pale kwao ilikuwa ni kwa kumsaidia maana yeye na mme wake wanamjua ni kijana yatima aliyekuwa amezaliwa na UKIMWI kwani wazazi wake walipofariki alitengwa na ndugu ndipo wakamsaidia wakamuajiri kuwa houseboy wao ili akate majani, kuzibua vyoo n.k.

Kelele alizopiga mama zilimkurupusha mmewe sebuleni na kuwasha taa za nyumba nzima kisha akaelekea chumba cha housegirl kujua nini kimemsibu mkewe. Alipoingia hakuamini macho yake kwa kumwona MKEWE AKIWA UCHI WA MNYAMA KITANDANI NA HOUSEBOY WAO AKIMBEMBELEZA UCHI KAMA WALIVYOZALIWA.

*_WIVU MBAYA JAMANI!!!_*

Ama kweli umdhaniaye ndie siye, na usilolijua ni usiku wa giza. Maskini mama mwenye nyumba kajiponza kisa wivu. Alijua mmewe anatembea na housegirl kumbe baba wa watu hana shida na mtu yuko busy na mambo yake. Sasa yamemkuta makubwa mama huyu aibu hii atamuelewa nani mbaya zaidi houseboy ni mwathirika. Je, kama ameambukizwa UKIMWI itakuwaje? Hakika, familia na nyumba nzima imekumbwa na giza nene. NAAMINI WENYE TABIA ZA KUHISI NA KUAMINI TETESI BILA KUTHIBITISHA MTAKUA MMEJIFUNZA KITU.

JE! UNGEMSHAURI MME ACHUKUE MAAMUZI GANI?

Usiku mwema na Mungu awabariki na kuwalinda!!!

Mke wa Mugabe Asema ''Mugabe Anaweza Kupigiwa Kura Akiwa Maiti''

$
0
0

Grace Mugabe na mumewe rais wa Zimbabwe Robert Mugabe

Mke wa Rais mkongwe wa Zimbabwe, Robert Mugabe, amesema kuwa mumewe ni mashuhuri sana hivi kwamba anaweza kupigiwa kura hata akiwa maiti.

Bwana Mugabe, ambaye atakuwa na umri wa miaka 93 mnamo Jumanne, ametangaza mara kadhaa kuwa atagombea kiti cha Urais katika uchaguzi mkuu wa mwaka ujao.

Grace Mugabe ana miaka 40 mchanga kwa mumewe.

Aliambia mkutano wa chama tawala cha ZANU-PF kuwa hata mumewe akifariki, bado jina lake litawekwa kwenye karatasi za kupiga kura.

Alisema watu wa Zimbabwe wanampenda Rais wao sana, hivi kwamba wangempigia kura hata akiwa maiti.


Bi Mugabe amekuwa mkosoaji mkuu wa wakosoaji wa mumewe na kwa wale walio na tamaa ya kumrithi.

Inadhaniwa kuwa alikuwa mstari wa mbele wa kumwachisha kazi aliyekuwa makamu wa rais, Joice Mujuru mwaka 2014.

Bwana Mugabe, ambeye siku hizi haonekani sana hadharani, ametawala Zimbabwe tangu taifa hilo kuwa huru miaka 37 iliyopita.

Duh..Noma Sana ...Kocha Afukuzwa kwa Kukataa Kuroga..!!!

$
0
0

KOCHA wa timu ya Mzimuni FC ya Sarawak mkoani Pwani, Ally Yusuf ‘Ostadh’, hivi karibuni alijikuta kwenye wakati mgumu baada ya kutimuliwa kikosini kisa kikitajwa ni kukataa kukubali kuroga kabla ya mechi.

Ostadh ambaye alikuwa akikiandaa kikosi chake kukabiliana na Sunderland FC kwenye michuano ya Kombe la Jezi, alipotakiwa na uongozi wa timu hiyo kukubali kuroga ili washinde kirahisi, alikataa kwa kusema imani yake ya dini haimruhusu kufanya hivyo.

Ostadh alisema: “Unajua tangu mwanzo tulikuwa tukishinda bila hata ya kufanya hivyo, lakini baada ya kuona tumefika hatua ya nusu fainali halafu tunakutana na timu ngumu, wakasema tukaroge, nikakataa kwa sababu dini yangu hairuhusu mambo hayo, wakanitimua, lakini kichapo walichokutana nacho cha mabao 3-0 kimekuwa fundisho kwao.”

Makubwa Haya..Ray C Afunguka Kumpenda Rayvanny,Adai Anatamani...!!!

$
0
0

Msanii mkongwe wa Bongo Fleva mwenye sauti ya kumtoa nyoka pangoni, Ray C amedai kuwa anamkubali zaidi Rayvanny kutoka lebo ya WCB.

Ray C amesema kuwa amesikia msanii huyo amewaandikia wasanii wengi nyimbo hivyo na yeye anatamani siku moja aje kufanya naye kazi.

“Nampenda sana yule mtoto Rayvanny. Anaandika sana mashairi, nasikia anaandikia wasanii wengi nyimbo hata mimi natamani kufanya naye kazi,” Ray C amekiambia kipindi cha Planet Bongo cha EA Radio.

Mbali na hilo msanii huyo ameongeza kuwa anamheshimu sana Diamond Platnumz kutokana na kule alipofika kwakuwa muziki wake umefika sehemu ambayo wao hapo mwanzo hawakuwahi kufika.

Baada ya Sekeseke la Madawa ya Kulevya Kutulia,TID Aamua Kumtaja Tena Diamond..!!!

$
0
0

Kwa sasa msanii TID Mnyama anahakikisha anarudisha makali yake ya zamani kwenye muziki. Muimbaji huyo amewaahidi mashabiki wake kufanya kazi na Diamond hivi karibuni.

Akiongea kwenye kipindi cha XXL, kupitia Clouds FM Ijumaa hii, Mnyama amesema kuna nyimbo anayofikiria kumshirikisha Diamond ambaye taarifa hizo tayari ameshazipata.

“Nina ngoma nafikiri itafaa zaidi nikimshirikisha Diamond. Diamond ameshapata habari nafikiri tutaifanya ngoma hiyo soon as possible,” amesema TID.

Kwa sasa msanii huyo ameachia wimbo wake mpya aliomshirikisha rapper Fid Q unaojulikana kama ‘Maisha ya Jela’ pamoja na mwingine uitwao Woman.

Binadamu Kuanza Kuwekewa Moyo wa Plastiki,Soma Hapa Kujua Utakavyofanya Kazi...!!!

$
0
0

NCHINI Marekani kila baada ya dakika 10 mtu mmoja huwekwa kwenye foleni ya watu wanaosubiri kuwekewa moyo mpya ili kuweza kuendelea kuishi. Hali hii hotokea baada ya moyo wa mgonjwa kuonekana hauwezi kufanyiwa matibabu na hivyo njia pekee ya kuokoa maisha yake ni kupata moyo mpya ambao huwekewa kwa njia ya upasuaji (transplant).

Shirika la Umoja wa Kuchangia Viungo, linasema kuwa takribani watu 22 hufariki dunia kila siku nchini Marekani wakiwa katika foleni ya kusubiri mtu wa kujitolea moyo kwa ajili ya kuokoa maisha yao. Hata hivyo, wagonjwa wa aina hii sasa wanaweza kufurahia baada ya ugunduzi wa moyo wa bandia ambao inawezekana wakautumia kwa maisha yao yote (Total Artificial Heart)TAH).

Mtu anayechangia moyo (donor) anaweza kuwa ni mtu ambaye tayari ubongo wake umekufa lakini mwili bado una uhai na hivyo moyo wake kuwa mzima. Mgonjwa wa aina hii hawezi kupona. Mgonjwa yeyote ambaye ana hali mbaya lakini ugonjwa wake hauhusiani na moyo na ambaye hawezi kupona pia anaweza kujitolea moyo. Mtu aliyefariki pia anaweza kutolewa moyo na kusaidia wenye uhitaji lakini mara nyingi hii huwa ni kwa ridhaa yake kabla hajafariki.

Ukiwa umegunduliwa kwa mara ya kwanza takribani miaka 60 iliyopita, moyo wa bandia wa wakati huo uliwawezesha wagonjwa waliokuwa wakisubiri kupata mtu atakayejitolea kupatikana na uliweza kumsaidia mgonjwa kwa muda tu. Ugunduzi huu mpya, unaweza kutoa suluhisho la kudumu kwa kuwa moyo huo unalenga kumwezesha mgonjwa kuishi maisha yake yote.

Historia inaonyesha kuwa, kipindi kirefu ambacho mgonjwa ameweza kuishi kwa msaada wa teknalojia ya moyo wa bandia uliojulikana kitaalamu SynCardia temporary TAH ni miaka minne.

Katika kile ambacho kinaelezwa kama hatua nzuri ya ugunduzi, Kampuni inayohusika na matatizo ya moyo ya nchini Marekani inayojulikana kama SynCardia Systems Inc inaendesha utafiti na kufanya uchambuzi wa kina kuona kama TAH inaweza kuwa suluhisho la kudumu kwa wagonjwa wanaohitaji kubadilishiwa moyo na kushindwa kuupata kwa wakati kutokana na kuongezeka kwa mahitaji.

“Mwishoni mwa miaka ya 1960 wakati wagonjwa walipoanza kuwekewa mioyo mipya kutoka kwa binadamu wengine, upatikanaji wa kiungo hicho muhimu kwa maisha ya binadamu ulikuwa mkubwa. Upatikanaji wake ulikuwa mkubwa kuliko mahitaji lakini kwa sasa mahitaji yameongezeka zaidi na upatikanaji umepungua,” anasema Danald Isaacs ambaye ni Makamu wa Rais wa SynCardia, akiliambia Shirika la Habari la Fox.com.

Idara ya Afya na Huduma za Binadamu ya Marekani inakadiria kuwa watu 4,000 husubiria kupata moyo mpya ili waweze kuendelea kuishi kila siku wakati mioyo 2,300 ikiwa inatolewa.

Ugonjwa wa moyo ni chanzo namba moja cha vifo nchini Marekani ukigharimu maisha ya watu 611,000 mwaka 2015, hii ni kwa mujibu wa Kitua cha Kupambana na Kuzuia Magonjwa cha nchi hiyo (CDC)

Wakati wa kumwekea mgonjwa moyo wa bandia au TAH, daktari huondoa kwa njia ya upasuaji ventrikali ya kulia pamoja na valvu nne kama ambavyo hufanyika wakati mgonjwa akiwekewa moyo ambao hutolewa na binadamu mwingine ambapo huwekwa wa bandia badala yake.

“Asilimia 96 ya mfumo wa kuweka moyo bandia ni ule wa SynCardia Temporary TAH ambao hutoa suluhisho la muda tu,” anasema Isaacs. Takwimu za SynCardia zinaonyesha kuwa wagonjwa 1,123 wamewekewa mfumo huo ambao ni modeli 70cc.

John Beckingham, mwenye umri wa miaka 58 ambaye ni mhandisi mstaafu anayeishi katika eneo la Rochester jijini New York alifanyiwa upasuaji uliofanikisha kuwekewa moyo mpya katika hospitali ya Cleverland, Oktoba mwaka 2015 baada ya kukaa miezi sita kwenye foleni ya kusubiria. Wakati akisubiria alikuwa akitumia mashine maalumu ambayo ilikuwa ikitumia betri  na ambayo ufanisi wake haukuwa sawa na teknalojia hii mpya.

Kudadadeki..Hivi Ndivyo Mbowe Alivyofanikiwa Kuwatoroka Polisi Mchana Kweupe Wakati Wakimtafuta..!!!

$
0
0

Jeshi la Polisi Kanda Maalum Dar es salaam, limemtaka Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kujisalimisha Polisi mara moja kwa ajili ya Mahojiano yanayohusu vita vya dawa za kulevya baada ya juhudi za kumsaka katika makazi yake kushindikana huku simu yake ya mkononi ikiwa imezimwa 

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es salaam Kamanda wa Polisi Kanda Maalum Simon Sirro amesema Bw. Mbowe aliahidi kwenda mwenyewe juzi tarehe 15, lakini hakwenda lakini jeshi la hilo lilimtafuta usiku na mchana katika makazi yake na kumpigia simu lakini simu yake ilizimwa 

Aidha jeshi hilo limesema watuhumiwa watatu Agnes Masogange, Rashid Idd au Chid Mapenzi na Wallis Latif Nasher ambaye ni muuza magari katika eneo la mikocheni watapandishwa kizimbani Jumatatu kwa kosa la kukutwa na dawa za kulevya lakini pia walibainika wanaotumia dawa hizo baada ya kupelekwa kwa Mkemia Mkuu 

Katika kupambana na Askari feki, jeshi limemtia mbaroni aliyekuwa askari Magereza wa cheo cha Koplo Peter Elias Msigwa aliyekuwa mtumishi katika gereza la keko, ambaye alifukuzwa kazi Desemba mwaka jana, lakini alikamatwa jana akiwa na mavazi ya kiaskari tena akiwa amejipandisha cheo kutoka koplo hadi Sajenti wa Polisi 

Jeshi hilo pia limesema limewatia mbaroni watu 65 kwa kosa la kukutwa na dawa za kulevya pamoja na watuhumiwa 73 wa wizi na ujambazi wa kutumia silaha, mitambo mitano ya Gongo, lita 270 pamoja na Puli 250 za bangi. 

Mbeya : Mama Afukua Kaburi la Mwanae,Kisa Kamili Hiki Hapa...!!!

$
0
0

Katika hali isiyo ya kawaida mama mmoja mwenyeji wa mkoa huu wa mbeya mji mdogo wa mbalizi, usiku wa kuamkia leo alienda kaburini alikokua kafukiwa mwanae aliyefariki dunia Siku ya jumatatu na kuzikwa jumanne ya wiki Hii na kufukua kaburi hilo na kuitoa maiti 

Kwa mujibu wa mama huyo maarufu Kama mama vumi anadai aliambiwa na mchungaji kuwa mwanae hajafa Bali Kuna sehemu anafanya kazi hivo aende akaitoe ile maiti kaburini ili iombewe irudi kuwa binadam wa kawaida,

Jana usiku yule mama ndio akaenda kuifanya kazi aliyotumwa na mchungaji wake ambapo leo asubuhi ndio raia wakagundua ishu na kwenda kukinukisha kwa yule mama, polisi walifika eneo la tukio na kumuokoa yule mama toka kwenye mikono ya wananchi wenye hasira Kali na kuondoka nae pamoja na maiti ya mtoto

Mbunge Mwingine wa Chadema Akiuka Maagizo ya Mbowe,Aisifia Serikali ya Magufuli Hadharani...!!!

$
0
0

MBUNGE wa Simanjiro, James ole Millya (Chadema) amepongeza viongozi wa Serikali kwa jinsi wanavyojali na kuhudumia wananchi.

Alitoa pongezi hizo juzi kwenye mikutano miwili ya hadhara Orkesumet na Mirerani wilayani hapa, baada ya kupewa nafasi kusalimia wananchi kabla Waziri Mkuu Kassim Majaliwa hajazungumza nao.

“Serikali hii ina viongozi wachapakazi akiwemo Waziri Mkuu. Kwa mara ya kwanza katika jimbo hili, wananchi watapata maji safi kupitia mradi wa maji kutoka Mto Ruvu unaoendelea kujengwa sasa,” alisema akiwa Orkesumet.

Alitumia fursa hiyo kumwomba Waziri Mkuu afuatilie ujenzi wa hospitali ya wilaya, kwani sasa wanategemea kituo cha afya na hali ikibadilika inabidi mgonjwa apelekwe Arusha Mjini  umbali wa kilometa 150 kutoka hapo yalipo makao makuu ya wilaya.

Pia aliomba ijengwe barabara ya lami kuunganisha wilaya hiyo wilaya za Hai na Kiteto.

Akiwa Mererani, Ole Millya aliipongeza Serikali kwa kujenga barabara ya lami kutoka uwanja wa ndege wa Kilimanjaro (KIA) hadi Mererani. Hata hivyo, aliiomba Serikali iongeze juhudi ili barabara hiyo iweze kufika Mirerani na Orkesumet.

Akijibu maombi hayo, Waziri Mkuu Majaliwa alimpongeza Mbunge huyo kwa uungwana wake wa kutambua juhudi za Serikali kwa wananchi wa jimbo lake.

Waziri Mkuu ambaye alikuwa katika siku ya pili ya ziara yake mkoani Manyara, aliwaambia wakazi hao kwamba Serikali itaendelea kufanya nao kazi bila kubagua kwa itikadi za kisiasa.

Rasmi..Flora Mbasha Achumbiwaaa.Abadilisha Jina la Mbasha Sasa Anataka Aitwe Jina Hili..!!!

$
0
0

Baada ya wanandoa ambao ni wanamuziki maarufu wa nyimbo za Injili, kuingia katika mzozo miaka minne iliyopita, mmoja wao Flora Mbasha amechumbiwa na anatarajiwa kufunga ndoa ya pili hivi karibuni mkoani Mwanza.

Sakata hilo linaweza kuibua mjadala miongoni mwa waumini wa dini ya Kikristo ambayo pamoja na kuruhusu ndoa kuvunjika, ni nadra sana kwa makanisa kuidhinisha suala hilo.

Habari za kuaminika  zinasema vikao vya maandalizi ya harusi hiyo vimeshaanza baada ya Flora kufanikiwa kupata talaka aliyoidai Mahakama ya Wilaya ya Kinondoni jijini hapa.

Flora, ambaye ni mjukuu wa aliyekuwa muhubiri maarufu nchini, Askofu, Moses Kulola (sasa marehemu), tayari amevishwa pete ya uchumba na amebadili jina la kisanii akitaka mashabiki wake wamtambue kama “Madame Flora” badala ya jina aliloibukia la Flora Mbasha.

Asili ya neno “madame” analotumia Flora ni Ufaransa na linamaanisha mwanamke aliyeolewa.

“Kwa sasa siwezi kukwambia chochote kuhusu hilo. Sijui, labda ifikapo Machi naweza kuzungumza,” amesema Flora, ambaye alitamba na kibao cha “Jipe Moyo”.

Zijue Namba Maalum za Magari ya Viongozi, Serikali na Taasisi za Umma kwa Ujumla..!!!

$
0
0

Ukiona mtaani gari zimeandikwa ktk plate number kama ifuatavyo usiumize kichwa jua ni hivi:

1. Ngao-Rais, makamu wa rais na waziri mkuu

2. S-Spika wa bunge

3. JM- Jaji mkuu

4. JR- Jaji wa mahakama ya rufaa

5. JK- Jaji Kiongozi

6. J- Jaji wa mahakama kuu

7. XXXX-Mkuu wa majeshi(CDF)

8. CAG-Mdhibiti na mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali

9. CS- Katibu mkuu kiongozi

10. W mwanzoni inaashiria waziri kisha kifupi cha wizara yake hufuata

11. NW-Naibu waziri

12. DFP-Donor's Fund project

13. ST-Serikali ya Tanzania kisha herufi nyingine hufuata

14. SMZ-Serikali ya mapinduzi ya Zanzibar

15. PT-Police of Tanzania

16. SM-Serikali za mitaa

17. CD- Magari ya ubalozini

18. SU-Shirika la umma.

19. gari za jeshi pia zina namba zake ambazo zina vifupi vya JW

20. MT-Magereza Tanzania

21. CGP-Commissioner General of Prison(Mkuu wa Magereza)

22. Gari nyingine za umma zina namba zaidi ya moja kwa kazi maalum

NYONGEZA:
Gari za biashara zina plate number nyeupe na zile za matumizi binafsi plate number ya njano.


Wabunge Wamchochea Spika Ndugai Kwa Makonda..Habari Katika Vichwa vya Magazeti ya Leo 19/2/2017..!!

Haya ndio Mataifa Matano Yanayopinga Uwepo wa Mungu

$
0
0
Utafiti Unaonesha kwamba 63% ya watu duniani wanaamini uwepo wa Mungu, yafuatayo ni Mataifa 5 yanayoongoza kwa idadi kubwa ya watu wasiyoamini uwepo wa Mungu (Atheism).

1. China. 
Ikiwa na wapagani asilimia 30%, huku asilimia 47% ya watu hawaamini kabisa kama Mungu yupo.

2. Japan.
Ikiwa na asilimia 31% ya wapagani, huku asalimia 31% ya wajapani hawaamini kabisa kama Mungu yupo.

3. Czech Republic. 
Ikiwa na 48% ya wapagani, huku asilimia 30% ya wananchi wanasema kwamba Mungu hayupo.

4. France. 
Asimilia 29% ya wafaransa hawaamini kabisa kama Mungu yupo.

5. Korea Rep (South).
Ikiwa asamilia 15% watu wasioamini kwamba Mungu yupo.

VIDEO: Mwingine aliyeza na Nay Wa Mitego aibuka

$
0
0
Soudybrown alipowagonganisha Kwa simu Sista Fey anae dai kutelekezwa na Mtoto matunzo Wala Ada Za Shule huku "Nay Wa Mitego" aki tambulisha wanae wengine bila kum'hesabu wa Sista Fey.

Alikiba Ampagawisha Waziri Nape Nnauye

$
0
0
Msanii Alikiba ambaye leo ameachia remix ya wimbo wake wa 'Aje' ameonesha kumkosha Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mh. Nape Nnauye kiasi cha Waziri huyo kusema kuwa Alikiba ni kati ya wasanii wanaofanya ajisikie fahari kuwa Waziri

Mhe. Nape Nnauye amesema hayo leo baada ya msanii huyo kukabidhiwa tuzo yake katika kituo kimoja cha Television nchini Afrika Kusini na kuachia kazi yake mpya ambayo imeonesha kuwakosha watu wengi.

"Kiba! Big Up! Am so proud of you! we ni mmoja wa wasanii wanaonifanya nijisikie fahari kuwa Waziri wa Sanaa Tanzania! May allah bless you!" aliandika Nape Nnauye 
Msanii Alikiba ni kati ya wasanii wachache kutoka Tanzania ambao wanaiwakilisha vyema nchi kupitia muziki wao.

Wanaokiri Kutumia Dawa za Kulevya Kusamehewa?

$
0
0
Waziri wa Sheria na Katiba Dkt. Harrison Mwakyembe amesema licha ya sheria kuweka adhabu ya kifungo kwa watu wanaotumia dawa za kulevya, bado kuna nafasi ya watu wa aina hiyo kusamehewa endapo watajitokeza mapema, kukiri na kuahidi kuacha.


Dkt. Mwakyembe amesema hayo wakati akitoa elimu juu ya sheria mpya ya kupambana na kudhibiti dawa za kulevya, kupitia kipindi cha East Africa Breakfast cha EA Radio, na kutolea mfano baadhi ya wasanii ambao walitajwa hivi karibuni na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaa, ambao baadha ya kuhojiwa walikiri kutumia na kuahidi kuacha.

Amesema kama mtu anatumia, halafu akawa anakataa kiasi cha kulazimu uchunguzi hadi kufikishwa mahakamani, huyo atapelekwa mbele ya sheria ichukue mkondo wake.

Msanii TID alipowaomba radhi watanzania na kutangaza kuacha matumizi ya dawa za kulevya
Baadhi ya wasanii ambao walikiri kutumia dawa hizo, na kuwekwa chini ya uangalizi wa mahakama kwa mwaka mmoja na wengine miaka miwili ni pamoja na TID, Tunda, Petit Man na wengine.
Kwa mujibu wa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, sheria imetoa adhabu kwa mtumiaji wa dawa hizo kufungwa gerezani miaka mitatu.
Huyu hapa Dkt. Mwakyembe Tazama Video:
Viewing all 104776 articles
Browse latest View live




Latest Images