Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104414 articles
Browse latest View live

Mwanamuziki Chemical Amkataa Live Mwanamuziki Stereo...Adai Sio Type Yake

0
0
Hatimaye kipindi cha eNewz cha EATV kimetegua kitendawili cha endapo rapa wawili wa Bongo Stereo na Chemical watakuwa wapenzi, baada ya Chemical kumvulia uvivu na kutamka 'LIVE' kuwa Stereo siyo wa aina yake, huku akieleza jinsi alivyomkera

Kupitia kipindi cha eNewz, Chemical amesema kuwa kwa uchunguzi alioufanya, amejiridhisha kuwa kila kitu alichokifanya Stereo ilikuwa ni 'drama' na kwamba hakutegemea kama Stereo angefikia hatua hiyo kwa kuwa alikuwa akimuheshimu kama kaka yake ambapo amesema jambo lililomkera zaidi ni njia aliyoitumia ya kwenye kwenye vyombo vya habari badala ya kumtafuta yeye mwenyewe.

Amesema ana uhakika Stereo hatafuti kiki kupitia yeye, lakini amemkaribisha kama anahitaji kufanya kolabo na yeye, yuko tayari kwa hilo. "Sidhani kama Stereo alikuwa anatafuta kiki kwangu, maana yeye ni msanii mkubwa, halafu alisema eti hafahamu pa kupata namba zangu, siyo kweli, alikuwa ana uwezo wa kuzipata sehemu yoyote" Amesema Chemical

Amesema baada ya mambo hayo yote, alimpigia simu na kumuuliza kama alikuwa 'serious' au lah, ambapo majibu aliyopata yalionesha kuwa stereo hakuwa 'serious', huku akiweka wazi pia kuwa jambo hilo limempa wakati mgumu kwenye familia yake na hata shuleni kuwa bado ni mwanafunzi.
Kwa upande wake Stereo amesema yeye alichokifanya ni kueleza ukweli wake kwa kuwa anamchukulia Chemical kama msichana mwingine, na siyo kama msanii.

Tazama majibizano yalivyokuwa katika kipindi cha eNewz.

Kutana na Maalim Hussein Mtabibu wa Nyota za Binadamu Africa na Dunia Nzima,

0
0

Kutana na Maalim Hussein Mtabibu wa nyota za binadamu Africa na dunia nzima,
Anatoa TIBA MAENEO YOTE NCHINI, KWA WALE WENYE KUHITAJI TIBA ANATIBU YAFUATAYO,
Husafisha nyota na kutoa Pete za bahati na kwa wale walia sumbuka kwaajili ya matiba na hawakufanikiwa njoo ujionee muujiza wa papo kwa papo-humpa mtu jini la mali kwa yule anaetaka kumiliki mali bila masharti yoyote,
Anatibu magonjwa yalio shindikana-Mpenzi/MUME/MKE Aliekukimbia Anakurudishia Ndani ya saa 72 tu, Pia tunatoa dawa za Nguvu za KIUME na Kurefusha kwa saizi unayo Taka-Anatoa Dawa za BIASHARA NA MVUTO-Tunatoa Dawa za Uzazi kwa kina Mama kwa wale wenye Tatizo Sugu-Anatoa Zindiko ya Nyumba,Mwili, na Mvuto kazini- Tunamaliza kesi zilizo kaa muda Mrefu bila kumalizika, Tung'arisha Nyota na Cheo kazini. Tunarudisha Mali zilizopotea au Kuibiwa na Mengine Mengi ya Siri tuwasiliane kwa Simu-Whatsapp +255674835107
+255 629254849

Kamanda Sirro: Mbowe Jisalimishe Polisi; Masogange na Chid Mapenzi Tumewakuta na Madawa pia Wanatumia

0
0
Jeshi la Polisi Kanda Maalum Dar es salaam, limemtaka Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kujisalimisha Polisi mara moja kwa ajili ya Mahojiano yanayohusu vita vya dawa za kulevya baada ya juhudi za kumsaka katika makazi yake kushindikana huku simu yake ya mkononi ikiwa imezimwa

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es salaam Kamanda wa Polisi Kanda Maalum Simon Sirro amesema Bw. Mbowe aliahidi kwenda mwenyewe juzi tarehe 15, lakini hakwenda lakini jeshi la hilo lilimtafuta usiku na mchana katika makazi yake na kumpigia simu lakini simu yake ilizimwa

Aidha jeshi hilo limesema watuhumiwa watatu Agnes Masogange, Rashid Idd au Chid Mapenzi na Wallis Latif Nasher ambaye ni muuza magari katika eneo la mikocheni watapandishwa kizimbani Jumatatu kwa kosa la kukutwa na dawa za kulevya lakini pia walibainika wanaotumia dawa hizo baada ya kupelekwa kwa Mkemia Mkuu

Katika kupambana na Askari feki, jeshi limemtia mbaroni aliyekuwa askari Magereza wa cheo cha Koplo Peter Elias Msigwa aliyekuwa mtumishi katika gereza la keko, ambaye alifukuzwa kazi Desemba mwaka jana, lakini alikamatwa jana akiwa na mavazi ya kiaskari tena akiwa amejipandisha cheo kutoka koplo hadi Sajenti wa Polisi

Jeshi hilo pia limesema limewatia mbaroni watu 65 kwa kosa la kukutwa na dawa za kulevya pamoja na watuhumiwa 73 wa wizi na ujambazi wa kutumia silaha, mitambo mitano ya Gongo, lita 270 pamoja na Puli 250 za bangi.

Chanzo: Channel Ten

Hatarii..Mume wa Zari Afanya Kufuru Afrika Kusini,Agawa Dola Mitaani Kama Njugu,Yadaiwa ni Dongo kwa Diamond..!!!

0
0

Wakati staa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ akimwaga fedha za kutosha katika sherehe ya arobaini ya mtoto wake wa kiume, Nillan Nasibu ‘Chibu Junior’, aliyewahi kuwa mume wa mwandani wa jamaa huyo, Zarinah Hassan ‘Zari The Boss Lady’, Ivan Semwanga, amefanya kufuru ya aina yake nchini Afrika Kusini ‘Sauz’.

Chanzo makini kilichopo Sauz kilieleza kuwa, Ivan ameanzisha programu maalum kwa ajili ya kuonesha cheche zake za uwezo wa kifedha kwa kugawa fedha katika mitaa mbalimbali ili ateke hisia za wengi na kupotezea kufuatilia matukio ya Diamond ikiwemo arobaini hiyo ya mwanaye.

“Yaani jamaa ni kama anamjibu Diamond kwa kufanya hiyo sherehe ya arobaini. Ameamua kuwa anakusanya watu katika mitaa mbambali ya Sauz, anawapa fedha katika kiwango ambacho anakuwa amejisikia kwa siku husika.

“Unaambiwa hatoi fedha za Sauz, anawapa dola za Marekani. Kuna wakati anaweza kuwa anawapa dola mia kwa kila mtu. Lakini kuna wakati mwingine anafanya mia na hamsini.

“Mbaya zaidi kwa kiwango hicho cha fedha si kwamba anawapa watu labda ishirini au thelathini, yaani watu wanafika hata mia au zaidi, foleni inakuwa ndefu kwelikweli,” kilisema chanzo hicho.

Chanzo hicho kilizidi kumnasibu mume huyo wa zamani wa Zari kuwa, amekuwa akifanya vibweka hivyo kwa makusudi ili kumtambia Diamond kwamba asifikiri amewini kumpata Zari kwani yeye (Ivan) ndiye kila kitu.

“Kimsingi jamaa huwa anafikisha ujumbe kwa Diamond kwamba yeye anazo. Anamuonesha kwamba yeye ndiye baba wa watoto watatu (aliozaa na Zari) na muda mwingi yupo na Zari huko Sauz kuliko hata Diamond,” kilidai chanzo hicho.

Chanzo hicho kilizidi kutiririka kuwa, suala la kugawa fedha kwa Ivan ni endelevu kwani mwishoni mwa wiki iliyopita ndiyo alianza, mapema wiki hii aliendelea tena katika mitaa mbalimbali ya Jiji la Johannesburg wanakoishi.

“Unajua Ivan anafanya kama anavyojisikia. Anaweza akagawa siku ya kwanza, ya pili, ya tatu au akafanya hivyo hata wiki nzima. Kwa kweli watu wengi sana, wamekuwa na maswali juu ya utajiri wake, lakini hakuna anayejua ameupataje licha ya kuwa wengine wanamhusisha na mambo ya uganga,” kilisema chanzo hicho.

Risasi Jumamosi lilisaka mawasiliano ya Ivan ili kumdadadisi asili ya utajiri wake, lakini hadi tunakwenda mitamboni ilishindikana.

Hata hivyo, kupitia ukurasa wake wa Mtandao wa Instagram, Ivan amefunguka kuwa asichukuliwe vibaya kwani anatoa fedha hizo kwa ajili ya kurudisha fadhila kwa jamii hivyo  asiulizwe maswali mengi.

Baada ya Wafanyakazi wa Manji Kukamatwa,Ubalozi wa India Waibuka na Tamko Hili Zito kwa Serikali ya JPM..!!!

0
0

SIKU chache baada ya Idara ya Uhamiaji kukamata raia wa India kwa madai ya kufanya kazi bila vibali, Balozi wa India nchini, Sandeep Arya, ameingilia kati suala hilo na kusema tatizo lilikuwa mawasiliano kati ya mwajiri na Uhamiaji.

Akizungumza jana , Balozi Arya alisema anaendelea kufuatilia kwa karibu suala hilo na kudokeza kuwa jitihada za kumaliza sintofahamu hiyo, zinaendelea kwa njia ya mazungumzo kati ya mwajiri na Idara hiyo.

Akifafanua baada kumaliza kikao chake na wawakilishi wa kampuni 30 za kutengeneza dawa kutoka India zinazojiandaa kuwekeza nchini, Balozi Arya alisema baada ya kubaini tatizo kuwa mkanganyiko wa mawasiliano, ndiyo maana wameruhusu kampuni hizo kuwekeza nchini.

“Unajua zipo ajira za muda, zingine miaka miwili, hivyo udhaifu wa mawasiliano ulisababisha sintofahamu, hivyo taratibu za kufanya ukaguzi zinapaswa kuchukuliwa na vibali vitolewe maisha yaendelee,” alisema.

Balozi Arya alisisitiza kuwa jitihada za kumaliza sintofahamu hiyo, zinaendelea kwa njia ya mazungumzo na ofisi yake kwa kushirikiana na Serikali ya Tanzania, watahakikisha suala hilo linamalizika kidiplomasia bila kuathiri ushirikiano uliopo.

Ray C: Nilianza Mapenzi Nikiwa na Umri wa Miaka 16

0
0
Alikuwa akihojiwa kipindi cha Planet Bongo,
amezungumzia mambo mengi ikiwemo bifu za wasanii, kutoa albamu, alivyoanza mapenzi .
Amedai bifu ni nzuri sababu zinachangamsha muziki, alianza mapenzi akiwa na miaka 16 ila walaiachana kutokana na utoto na pia amedai watu wanamiss albamu kama zamani kwa kuwa siku hizi wasanii hawatoi tena, pia amesema sasa hivi ana nyimbo 8 tayari Mtazame Hapa:

Imefichukaa..Kumbe Mwalimu Nyerere Alikuwa Hajui Kuendesha Gari...!!!

0
0

KITABU chetu cha leo ni “Mlinzi Mkuu wa Mwalimu Nyerere,” kimeandikwa na Peter D. Bwimbo na kuchapishwa na kampuni ya Mkuki na Nyota. Kina nambari ISBN 9789987-753-32-1. Peter D. Bwimbo alikuwa afisa usalama wa taifa hivyo kuwa mlinzi mkuu wa Mwalimu Nyerere lilikuwa suala la utaratibu.

Mwandishi anatuachia kumbukumbu kuhusu maisha ya Mwalimu Nyerere na masuala ya ulinzi na usalama pamoja na maisha ya nyakati za ukoloni na baada serikali mpya ya Tanganyika (Tanzania) changamoto, mafunzo na maasi ya kijeshi ya mwaka 1964.

Kitabu hiki kinaeleza maisha ya makachero ama vyombo vya dola vinavyofanya kazi usiku na mchana kuhakikisha viongozi wetu wanaishi kwa amani na utulivu.  Pamoja na changamoto za kuwalinda wananchi nchini kuanzia Special Branch (Idara ya Usalama wa Taifa kabla ya ukoloni) ambayo baadaye ilibadilishwa na kuitwa TISS (Tanzania Intelligence and Security Service).

Matukio muhimu yanayotajwa ndani ya kitabu hiki, “Kwa hiyo kazi ya kuwaelemisha wananchi kwa njia ya mikutano ya hadhara kuhusu masuala ya siasa na faida ya kujitawala ilikuwa ngumu sana iliyohitaji Mwalimu Nyerere na wenzake kujitolea kusafiri kwa shida umbali mrefu na kwa njia mbaya vijijini na mijini wakati mwingine kwa miguu kuwafikia wananchi mahali walipo. Aidha, wananchi nao wakati mwingine waliogopa kuhudhuria mikutano hiyo kwa hofu ya uwezekano wa kukamatwa na vyombo vya serikali ya kikoloni hata kama mikutano hiyo kwa bahati ilipewa vibali,” (Uk. Uk. 24).

Mwandishi anasema kulikuwa na nyakati ngumu za kupigania uhuru na baada ya wakoloni kuondoka. Baadhi ya maofisa wa kizungu walichukizwa na kupatikana kwa uhuru wakaamua kutotoa mafunzo yoyote.

“Maofisa Wazungu katika Special Branch (Idara ya Usalama) kabla hawajarudi kwao kufuatia program ya Africanisation (neno hilo lilitumiwa hivyo hivyo katika Kiswahili kuwa frikanaizesheni), hawakutayarisha mwongozo wowote ingawa kitengo hiki walikianzisha wenyewe. Kwa hiyo, wakati nakabidhiwa kushika madaraka haya nilielezwa tu na Tim Hardy kwamba nitaongoza kitengo hiki cha ulinzi wa waziri mkuu Julius Nyerere kuanzia mwezi Agostia 1961,”(Utangulizi uk.XI).

Aidha, “Tanganyika ilipata serikali ya madaraka ya ndani tarehe 3 Septemba 1960, wakati huo mimi bado nikiwa masomoni Uingereza. Baada ya TANU kushinda katika uchaguzi na kupata idadi kubwa ya wajumbe katika Barazala la Kutunga Sheria (Legco) Mwalimu aliteuliwa na Gavana kushika wadhifa wa waziri mkuu (Chief Minister) Special Branch wakati huo ilikuwa chini ya Jeshi la Polisi,” (Uk. 29)

Hii ina maana kuwa kabla ya Uhuru kamili, Tanganyika ilianza kwa kupewa serikali ya madaraka ya ndani (Internal self Government). Kwenye suala la kuwalinda viongozi, anasema “Ulinzi wa Mwalimu Nyerere kwa ujumla haukuwa rahisi, ikilinganishwa na ulinzi wa viongozi wengine, kwa sababu alijiamini kuhusu maisha yake ya kisiasa kiasi cha kutokuwa na wasiwasi,” (Uk.33).

Nyerere alikataa sanamu yake kuweka katikati ya jiji. “Mara baada ya uhuru, Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam wakati huo walitaka sanamu yake itengenezwe ichukue nafasi ya ile ya asakri wa vita mwenye bunduki na singe katika maungano ya Mtaa wa Samora, Azikiwe na Makunganya, alikataa kata kata kwa maelezo kuwa sanamu kama hizo hazifai katika nchi zinazozingatia demokrasia na kuongozwa kwa utaratibu wa kupokezana madaraka muda unapokwisha,” (Uk.39).

Mnamo Januari 22, 1962, Mwalimu Nyerere alipotangaza kujiuzulu wadhifa wake wa uwaziri mkuu  kwa madai hakuwa akisikilizwa na serikali ya wakoloni. Baada ya kujiuzulu, alimteua Rashid Kawawa kuwa Waziri Mkuu (Uk.45).

Kuhusu maisha binafsi, kwa mfano, kabla ya uhuru palikuwa na Mwafrika mmoja tu nchini Tanganyika aliyekuwa na Digrii ya Masters aliyoipata mwaka 1952, miaka tisa kabla ya uhuru. Kulikuwa na madaktari Waafrika 12 pamoja na wahandisi Waafrika wawili wakati ambapo idadi ya watu wote nchini Tanganyika wakati huo ilikadiriwa kuwa milioni nne. Idadi hii ya wasomi nchini Tanganyika wakati huo alitajwa na Mwalimu Nyerere jijini Brasilia, Brazil tarehe 18 septemba 1996 katika hotuba yake aliyotoa kuhusu hali ya Afrika katika kipindi cha kuelekea karne ya 21. Mtu pekee Tanganyika aliyekuwa na digrii ya masters alikuwa yeye Mwalimu Nyerere lakini kwakuwa hakuwa mtu wa majivuno hilo hakulitaja,” (Uk.55).

Linalovuta hisia zangu ni hili, “Yeye mwenyewe Mwalimu Nyerere ameongoza nchi hii kwa muda mrefu lakini kadri ninavyofahamu, hakuweza kumiliki hata gari moja hadi anang’atuka kutoka ngazi ya urais wala hakujifunza kuendesha gari, bali alijua kuendesha Baiskeli,” (Uk.60).

Miujiza ya Shekh Sharifu Rashid Kutoka Bagamoyo , Anarudisha Mapenzi na Kusafisha Nyota

0
0

MIUJIZA YA SHEKH SHARIFU RASHID KUTOKA BAGAMOYO PWANI, (RUDISHA MAHUSIANO YAKO NDANI YA MASAA 48 TU) ASANTE KWA KUENDELEA KUMPIGIA SIMU SHEKH SHARIFU RASHID KWA WALE WENYE MATATIZO NA WALE WANAOTOA SHUKRANI:

SHEKH SHARIFU RASHIDI ni mtaalamu wa tiba mbalimbali za asili, anatumia kitabu cha quran, dawa za asili, dawa za kiarabu na majini, anazo dawa za mapenzi, nguvu za kiume, chango, ngiri maji na n.k, anakuvutia mpenzi alie kuacha au alie mbali, pia anatoa pete za bahati zilizoambatanishwa na jini mali kulingana na nyota yako, anaouwezo mkubwa wa kutumia jina la muhusika kwa kutatua tatizo lako, anaouwezo wa kumrudisha mtu aliepotea kimiujiza, pia anatibu kwa njia ya simu popote ulipo,

WASILIANA NAE KWA SIMU NA WHATSAPP NO: 0718-668347. 0685-224047, 0767-204308 au follow@shekh_sharifu_rashid, Email:shekhsharifurashid@gmail.com

Mwanamke Aishia Mikononi mwa Polisi Baada Ya Kukutwa Akifukua Maiti ya Mwanaye, Aliamini Atafufuka Baada ya Siku 3

0
0
Mwanamke aliyekuwa akiamini kuwa mtoto wake angefufuka siku ya tatu baada ya kufariki dunia Februari 15, jana alizua kizaazaa baada ya kufukua kaburi na kutoa maiti hiyo, hali iliyosababisha wananchi wafanye vurugu na kuichoma nyumba yake.

Mtoto huyo, Baraka Mwafongo (22), aliyefariki baada ya kuugua kwa muda mrefu, alizikwa siku iliyofuata lakini maiti yake ilifukuliwa usiku wa kuamkia jana na kuwekwa katika pagala ikiwa imevishwa suti kumsubiri mchungaji aifufue.

Mwanamke huyo, Ruth Segeleti (52), anayeishi Mtaa wa Shigamba, Mbalizi, hakutaka kuzika maiti ya mwanawe akieleza kuwa mtoto wake angefufuka baada ya siku tatu, kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Mbeya, Dhahiri Kidavashari.

Alisema polisi waliona kuwa huenda hana uwezo ndipo walipomsaidia kuzika, lakini usiku wa kuamkia jana alipata vijana wawili waliomsaidia kufukua kaburi na kuchukua maiti hiyo ambayo waliipeleka kwenye pagala na kuiweka ikiwa imevishwa suti.

Baada ya wakazi kubaini kaburi la mtoto huyo limefukuliwa, kundi la watu lilijitokeza makaburini na kusababisha polisi kufyatua mabonu ya machozi

Wananchi waligundua kuwa kaburi lilikuwa wazi majira ya saa 3:00 asubuhi baada ya majirani kumuona mwanamke ambaye walijua alikuwa na msiba wa mtoto wake Jumamosi akiwa na jembe mkononi na furushi la nguo akitokea makaburini.

“Nilipomsemesha, hakutaka kunijibu,” alisema mkazi wa mtaa huo, Mariam Mwakisepile ambaye ni jirani wa mwanamke huyo. 

“Nililazimika kuwaarifu majirani wengine ambao walikwenda makaburini ambako walikuta kaburi la Baraka likiwa limefukuliwa.”

 Shuhuda mwingine wa tukio hilo, Christina Nyopelo alisema walipiga simu kituo cha polisi cha Mbalizi na kuwaarifu.

“Baada ya muda mfupi polisi waliwasili na wakiwa makaburini waliona sanduku ndani ya kaburi, lakini mwili haukuwapo,” alisema Nyopelo.

 “Polisi kwa kushirikiana na wananchi waliamua kukagua maeneo ya makaburi na hatimaye walifanikiwa kuukuta mwili ukiwa umelazwa kwenye banda lililopo karibu na eneo hilo.” 

Habari hizo zilisambaa na kukusanya kundi la watu kutoka mji wa Mbalizi na kusababisha polisi kutumia mabomu ya machozi kuwatawanya.

Alisema baadaye polisi walikwenda nyumbani kwa mwanamke huyo na kumkamata, pia waliupeleka mwili wa Baraka, Hospitali Teule ya Ifisi kwa ajili ya kuuhifadhi.

Kamanda Kidavashari alisema mtuhumiwa alipelekwa Kituo cha Polisi Mbalizi kuhojiwa.

Umati wa watu pia ulijazana Mtaa wa Shigamba na kusababisha polisi walipue mabomu ya machozi ili kuwatawanya watu.

Jitihada hizo zilizaa matunda kwa muda mfupi, lakini ilipofika saa 8:00 mchana watu wasiofahamika waliichoma moto nyumba ya mwanamke huyo.

Katika kukabiliana na tukio hilo, polisi waliwatawanya wananchi kwa kupiga baadhi ya watu waliokutwa eneo la tukio. Kamanda Kidavashari alisema polisi wanawasaka watu waliohusika kuchoma moto nyumba ya mwanamke huyo.

Wawili Wapoteza Maisha Kwa Kukosa Dawa za Kulevya

0
0
Sunday , 19th Feb , 2017
Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Kuzuia na Kupambana na Dawa za Kulevya, Rogers Sianga amesema watu wawili wameripotiwa kupoteza maisha mkoani Mwanza kwa sababu ya kukosa dawa za kulevya mtaani kama walivyozoea.

Kamishna Sianga amesema taarifa hiyo ameipata kutoka kwa Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, hali inayomaanisha mafanikio ya mapambano ya dawa hizo, ambapo kwa sasa usambaaji wake umepungua mtaani kwa kiasi kikubwa.

"Nimeongea na Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, ameniambia kwamba kuna watu wwili wamefariki sababu walikuwa drug addict na sasa dawa hizo hazipo mtaani" Amesema Sianga

Sianga amesema mara baada ya kupokea kijiti cha mapambano kutoka kwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda, Mamlaka hiyo imeendelea na moto huo huo, na kwamba kwa hivi sasa timu yake hailali, ikiendelea na mapambano kila siku na kwamba hata leo, kuna mtuhumiwa mkubwa wa dawa za kulevya amekamatwa.

"Leo asubuhi tumemkamata mtuhumiwa mmoja mkubwa wa dawa kulevya, tupo naye tunaendelea kumuhoji, mengi yataibuka" amesema Kamishna Sianga

Kuhusu kuendelea kutumia mbinu iliyokuwa ikitumiwa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam paul Makonda ya kutaja majina hadharani,, Kamishna Sianga amesema hatatumia njia hiyo kwa kuwa kutaja majina ya watu hadharani kunaweza kuiingiza serikali katika matatizo maana kuna watu wengine wanaweza kutoa majina ya watu kwa sababu ya chuki binafsi.

Amesema njia anayoitumia ni kuwakamata na kuwahoji kimyakimnya na wakishajiridhisha hatua nyingine za kisheria zinafuata.

Katika hatua nyingine, Sianga amesema Tanzania iko makini katika kuwashughulikia wahusika wakubwa wa dawa za kulevya duaniani tangu miaka mingi iliyopita, akitolea mfano mtuhumiwa mmoja wa kike ambaye ni gwiji katika biashara hiyo au 'King Pin', ambaye hivi sasa amefungwa katika magereza ya Tanzania tangu mwaka 2010

"Tulimkamata mmoja kati ya watu waliokuwa wametajwa kama king pin wa dawa hizo nchini Marekani, alikuwa ameshindikana, na huko Marekani alikuwa na kesi zaidi ya 40, lakini alikamatwa hapa na amefungwa tangu mwaka 2010, yuko gerezani nafikiri kama siyo Keko, ni Segerea". Amesema Sianga.

Source:JF

SHILAWADU: Barnaba Kaongea Kuhusu Ugomvi na Mama Mtoto wake

0
0
Mwimbaji wa bongofleva Barnaba Boy yupo kwenye vichwa vya habari za burudani kwa zaidi ya siku 5 sasa hivi baada ya habari zinazodaiwa kwamba ameachana na Mama mtoto wake.

Barnaba amehojiwa na The weekend chat show na kusema hayo ni maneno ya watu tu ila yeye hajagombana na mama watoto wake Mama Steven japo kila mtu ana matatizo.

“Mimi na wife wangu hatuna matatizo, maneno hayo yanayoendelea uko nje achana nayo, Mimi sijawai kugombana na mama watoto wangu wala mama watoto hajawai kuondoka nyumbani na the Good Thing is mimi na familia yangu tupo karibu na Steven anaenda shule kama kawaida“

“Chukua hili neno kubwa sana MIMI NA MAMA WATOTO WANGU HATUNA MATATIZO, kila mtu anamatatizo lakini mimi sidhani kama matatizo yangu naweza kuyaleta hadharani  ila natanguliza samahani kwa watu wangu kwa sababu mimi sipendi kelele mbaya”

“kwenye muziki wangu, Mungu anisamehe huu mwezi umekuwa kama unaniandama kwa vitu vingi sana ila Namuamini Yesu na namwamini Mungu kilicho kibaya kilicho kizuri namuachia Mungu“

Download Application ya Udaku Special Blog Hapa Kutoka Play Store...

0
0


Download  Application ya Udaku Special Blog Kwenye Simu yako Kutoka Play Store Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi

Bonyeza Hapa CLICK HERE 


Au Kama Unayotayari Bonyeza Hapa Ku Update Uweze Kupata Ikiwa na Muonekano Mpya

Nimekuwekea Vyakula Vitano vya Wewe Kuala Ili Ujilinde Dhidi ya Ugonjwa wa Kansa na Magonjwa Mengine Makubwa..!!

0
0

LISHE bora ni jambo muhimu mno katika kuzingatia afya ya mtu. Chakula bora humwepusha mtu kukabiliwa na magonjwa kama kisukari, saratani na magonjwa ya moyo. Kwa faida ya afya ya mwili wako, hakikisha unapata vyakula hivi mara kwa mara.

NYANYA

Nyanya ina kemikali zinazoitwa flavonoids (anticarcinogenic) ambazo hupambana na visababisha saratani. Moja ya kemikali hiyo inaitwa lycopene ambayo hulipa tunda kama nyanya na tikiti rangi nyekundu. Lycopene ina nguvu kubwa katika kupambana na kuzuia saratani, hasa saratani ya tezi dume ( prostate cancer). Nyanya pia huchangia asilimia 38 ya vitamin C , asilimia 30 ya vitamin A na asilimia 18 ya vitamin K kwa matumizi ya kila siku.

BROCCOLI

Ni moja ya chakula kinachopatikana kwa wingi kwenye masoko ya vyakula. Mboga hii ina vitamin C mara mbili zaidi ya chungwa, madini mengi ya calcium kama maziwa, pia ina sifa ya kupigana na magonjwa kama saratani, kupambana na virusi, kutokana na wingi wa madini ya selenium. Kikombe kimoja cha mtori wa broccoli kitakupa mahitaji yako ya siku nzima ya Vitamin C na Vitamini K. Pia ni chanzo kizuri cha Vitamin A na Potasium. Faida nyingine ni kupambana na mashambulizi ya magonjwa, kusaidia usagaji wa chakula na kuondoa sumu mwilini. Inakulinda dhidi ya hatari ya kupata magonjwa ya moyo na inaimarisha mifupa na meno.

TANGO

Zamani tango lilikuwa linatumika katika kutibu maumivu ya kichwa. Juisi ya tango husaidia kusafisha ngozi na kuondoa uchovu kwenye macho. Maajabu haya ya tango yaliwafanya wanasayansi kuanza kutafiti juu ya tunda hili, zikiwemo mbegu zake na kubaini kuwa asilimia 90 ya tango ni maji ambayo yana Vitamini K na Vitamin C kwa ajili ya kupambana na maambukizi. Vitamini B ambayo husaidia mwili kuwa na nguvu, madini ya manganese kwa ajili ya kuimarisha mifupa, potassium na magnesium kwa ajili ya afya ya moyo.

Tafiti za hivi karibuni zinasema kuwa tango lina kemikali ya lignans ambayo hupatikana pia kwenye kabeji na vitunguu ikiwa na kazi ya kupunguza hatari ya kuugua magonjwa ya moyo, pia muungano wa lignin na bakteria wazuri walioko kwenye mfumo wa usagaji chakula husaidia kupunguza hatari ya kuugua badhi ya saratani ikiwamo ya matiti, kizazi na tezi dume.

PARACHICHI

Ukilinganisha na matunda mengine, hili lina virutubisho vingi zaidi hivyo hutakiwi kulikosa kwenye mlo wako wa kila siku, tunda moja la parachichi lina Vitamini K na vitamin B.

Parachichi lina kiasi kikubwa cha mafuta mazuri (god fats) ambayo husaidia kuweka mafuta yako ya mwili kwenye msawazo na hivyo kupunguza hatari ya kuugua magonjwa ya moyo na uzito mkubwa.

NAZI

Mafuta ya nazi hutumika katika kupikia vyakula mbalimbali.

Nazi husaidia kupunguza uzito kwani ina mafuta mazuri (medium chain fats) ambayo huweza kuvunjwa vunjwa kirahisi  ndani ya mwili  na hivyo kuweza kubadilishwa na ini kuwa nguvu moja kwa moja pasipo kuhifadhiwa kama mafuta kama ilivyo iwapo ukila wanga na sukari. Nazi ina uwezo mkubwa wa kupambana na bakteria, virusi na protozoa. Matumizi ya nazi pia yanasaidia ufanyaji kazi wa tezi ya thairodi, kuimarisha utendaji kazi wa ubongo na kuupa mwili kinga.

Mgombea wa Uholanzi Aahidi Kufunga Misikiti na Kuwazuia Waislamu..!!!

0
0

Mwanasiasa wa Uholanzi, Geert Wilders, anafanya mkutano wa mwanzo wa kampeni yake, na anahisi kuzuwia Waislamu kuhamia nchini humo, na kwamba atafunga misikiti.

Vilevile amawataja raia wa Morocco kuwa kashfa

Ulinzi mkali umewekwa katika mkutano huo karibu na Rotterdam.

Umebaki mwezi mmoja kabla ya uchaguzi, na kura za maoni zinaonesha kuwa chama cha bwana Wilders kina uongozi mdogo, ikilinganishwa na kile cha waziri mkuu, Mark Rutte.

Lakini katika majuma ya karibuni, wafuasi wa Bwana Wilders wamepungua.

Mwandishi wa BBC nchini Uholanzi, anasema kwa vile Bwana Wilders anamuunga mkono Donald Trump, inaonesha amepoteza baadhi ya wafuasi.

Chanzo: BBC

Zitto: Manji Anakomolewa, Sasa Anyang'anywa Hisa Zake za Tigo na Serikali..!!

0
0

Yanayoendelea dhidi ya Yusuf Manji yanashabikiwa na baadhi yetu kwa sababu wanadhani hayatawafika. Tabia ya kukomoa mtu ni tabia mbaya na ina madhara makubwa katika nchi. Ni dhahiri kuwa Manji sasa anaonewa na kudhalilishwa ili kumkomoa kwa sababu ambazo watawala wanazijua wenyewe. 

Wakati suala la kutumia unga lipo kortini, Serikali imeamua kumnyanganya hisa zake za Tigo. Sio kwamba Serikali itachukua hisa Hizo, la hasha. Ila Manji azikose tu. Unajiuliza, Serikali hii hii imeacha matapeli wa PAP kuitwaa IPTL na TANESCO inawalipa zaidi ya tshs 300m kila siku. Leo mpaka mahakama inatumia suo moto kurudisha suala la hisa za Manji kwenye Tigo ambalo halina maslahi yeyote ya Taifa. Kwanini Mahakama haikufanya suo moto kurudisha fedha za Tegeta Escrow? 

Watanzania wajue tu kuwa, mwaka 2004 Serikali iliachia hisa zake 20% kwenye Tigo kwa USD 750,000 ( vichekesho) kwa kuiuzia kampuni kutoka Luxembourg. Badala ya Serikali kuhangaika na maafisa wake walioachia hisa kutoka nje ya Tanzania wanahangaika na Mtanzania aliyezirudisha hisa Tanzania. 

Uhamiaji wanamwita kuhusu wafanyakazi wake wageni kana kwamba yeye Yusuf ni Afisa Rasilimali watu wa kampuni. Aliko Dangote hakuitwa uhamiaji kwa suala la wafanyakazi wake ila Manji anaitwa. 
Wakifanikiwa kwa Manji atatafutwa mwengine, Ni sawa na kula nyama ya mtu. Hutaacha. 

Manji anaweza kuwa ana madudu mengi Sana, ahukumiwe kwa haki kwa makosa yake. Asikomeshwe kwani ukomeshaji hautaishia kwake. Asionewe. Atendewe haki. 

Anyways Kama Mwana Simba, nawasihi Yanga achaneni na mambo ya mabango uwanjani. Hayasaidii lolote.

Fahamu Njia za Kupunguza au Kuondoa Kitambi Kabisa Bila ya Kunywa Dawa Wala Kufanya Mazoezi..!!!!

0
0

Uzito uliopitiliza ni upi?

Huu ni ule uzito ambao haufanani kiafya  na urefu wa mtu husika …

Njia rahisi ya kujua kama uko kwenye uzito sahihi ni hii.. mfano kama wewe una urefu wa sentimita 170.

Chukua 170 utoe 100 utapata 70. Kwa hiyo wewe hutakiwi kuzidisha kilo sabini.

Nb: 100 iliyotumika hapo ni costant.


 Zifutazo ni njia rahisi za kupunguza uzito

     Kunywa maji mengi kabla ya kula mlo wowote.

      Acha kula vitu vitamu sana vya kiwandani. Mfano, soda, pipi, biscuit na kadhalika.

     Usiingie kitandani kulala ukiwa umeshiba.

     Pata usingizi wa kutosha mfano  masaa nane na zaidi

     Weka chumvi kidogo sana kwenye chakula chako.

      Kula breakfast{chakula cha asubuhi} cha kutosha.

     Acha kula vyakula vinavyokaangwa na kuandaliwa haraka{fast foods}. Mfano chips, baga, saucage, vitumbua, maandazi, chapati na et.c

     Kula mboga za majani za kutosha i.e mchicha, Chinese, carrots, etc

   Kula matunda kwa wingi mfano apples, zabibu,

   Kula vyakula vyenye kamba{fibres} kwa wingi. Mfano kabechi, maembe, machungwa, machenza na etc

  jipangie ujazo maalumu mdogo wa chakula na ule ujazo huo kila siku, sio unakula huku unaongeza chakula ovyo.

   Punguza ulaji wa chakula aina ya wanga mfano ugali, mihogo, viazi vitamu,mikate na e.t.c

  Jipangie baadhi ya wiki unazimaliza bila kula nyama kabisa. mfano week moja kwa mwezi.

 Kula chakula aina ya protini kila mlo. Mfano maharage, karanga, soya, korosho, na kadhalika 

   Acha kushinda njaa kisha kula chakula jioni. Kula ata mara nne kwa siku ila kwa kiasi kidogo.

  Acha kunywa pombe kali eti  inakausha mafuta, hicho kitu hakipo na ni uongo mkubwa.

    Punguza unywaji wa bia i.e  kiafya mwanaume anatakiwa asinywe zaidi ya unit 4 za pombe  kwa siku na mwanamke anatakiwa asinywe zaidi ya unit 3 kwa siku.

Unit inapimwaje?

  Mfano bia moja  ina alcohol ya 8% ndani ya chupa lenye ujazo wa 500mils yaani nusu lita. Kwa hiyo ukinywa nusu ya bia{250mils} umefikisha unit nne tayari inabidi usinywe mpaka kesho tena kwa wewe mwanaume. Hivyo bia hiyo hiyo mwanamke hatakiwi kunywa  hata nusu yake.

   Kula chakula taratibu bila kua na haraka na hii husaidia mtu kula chakula kidogo na kuridhika. Mfano kula kwa dakika ishirini kila mlo.

Kwanini?

Mishipa ya fahamu ya tumboni inachukua dakika ishirini kugundua kama tumbo limeshiba hivyo na kutoa taarifa kwenye ubongo ili mtu aache kula. hivyo ukila ndani ya dakika tano ukamaliza, utahisi bado una njaa kwa sababu mishipa hiyo haijagundua kama umeshiba  hivyo utaongeza chakula kingine.kwa maelezo zaidi soma hapa

Kama Una Stress, Pitia Hapa! Usiache Kutupia na Wewe Maneno Yako!..!!

0
0

Kuna vijimisemo vifupi vimeibuka huku kwenye mitandao kwa sasa, yaani ni full burudani!
Ukivisomo mwisho lazima ubaki mdomo wazi au ucheke, baadhi ya niliyokutana nayo naweka hapa, pia karibuni kwa wenye zaidi tuburudike pamoja!

Leo kidogo nipigwe na MWANAMKE baada ya LIFTI kusimama...wakati tupo kwenye lift Nilikua nayaangalia MAZIWA yake akasema "Bonyeza Moja" mi si nikalibonyeza?
Yaani had sasa
bado najiuliza nilipokosea.

Hivi Utajisikieje Utakaposikia Rafiki Yako wa Karibu Hajaja Kwenye Mazishi Yako ???!
Nadhani Mimi Sitamwongelesha Tena !!!! 
I think nakaribia kupona

Nimenunua chips ili nile kwa bahat mbaya mtoto wa mama mwingine amekaa next to me akaanza kuzililia.
Imebidi nivae earphones. Napenda watoto, ila utoto ndio sipendi..

Jana nimepita njia ya mkato makaburini warembo wawili wakawa wananikimbilia wanatetemeka Eti tunaogopa kupita peke yetu na mm Nikawajibu hata mm nilivyokuwa hai nilikuwa naogopa sana . Wakazimia
Sipendagi kufatwa fatwa mm

Ex wangu leo kaupdate status yake ya watsap et "NILIOTEMBEA NAO WOTEMKAPIME" Saizi nipo apa pa fundi nguo pana foleni sanaHarusi sijui lini anapenda kushtukiza sana

Niliwahi kusikia kuwa maji na mafuta havichangamani, na pia mafuta huwa yanaelea juu ya maji... Basi jana mimi nikaamua kupaka mafuta mengi tu miguuni kisha nikaingia baharini ili niweze kutembea juu ya maji maana nilihisi ningeelea na kuweza kufanya chochote.
Sikumbuki nini kilitokea lakini nilijikuta nimelala mchangani watu wakiwa wamenizunguka huku wakisema niwashukuru sana wavuvi. Nadhani watakuwa wamenipa samaki wa bure.

Leo nimeenda kuchangia damu hospitalini,mara wananambia soda na biskuti zimeisha..!
Sa hii nipo zangu njiani na damu yangu kwenye blood bag naelekea nyumbani. Bora niwapelekee mbu take away..

Mwalimu kaniulizaa kama mtoto mdogo anaitwa mchanga... Je mtu mkubwa anaitwaje? ... Nikamjibu anaitwa kokoto..... Ameniitaa staff room labda atakuwa ameniitia chai

Huyu mwalimu ana roho nzuri sio kama mwl Msigwa

Stress ni nini??
Stress ni pale umeenda kijijini kwa bibi ako huku umebeba jeans zako tano zile ja mtindo wa kuchanika (chanika jeans) sasa siku ukazifua ukazianika ukaenda zako kutembea ile unarudi jioni unakuta bibi yako kazianua afu kazishona zote!

Utajiri wa Makonda Wawashtua Mashekhe,Habari Katika Vichwa vya Magazeti ya Leo 20/2/2017..!!

Kimenukaa Cuf...Maalim Seif Amtolea 'Povu' Prof Lipumba na Makundi Yake,Amchana Hadharani Juu ya Fitina Wanazofanya Cuf..!!!

0
0

KATIBU Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF), Maalim Seif Sharif Hamad, amewafunda wafuasi wake na kuwataka kuepuka fitna ambazo zitasababisha kukigawa chama chao.

Maalim Seif aliyaeleza hayo katika Kijiji cha Matele Jimbo la Chambani Wilaya ya Mkoani Mkoa wa Kusini Pemba alipoweka jiwe la msingi la tawi la chama hicho.

Alieleza kuwa wapo baadhi ya watu waliokuwa wabunge wa chama hicho, lakini baada ya kukataliwa na wanachama majimboni kwa sasa wamenuna na kuanzisha migogoro ndani ya chama hicho.

“Walidhani vile vyeo ni mali yao, sasa wamesahau kuwa wenye mamlaka ya kuteua mgombea ni wanachama, wanaanza kutaka kuharibu, lakini waambieni watajiharibu wenyewe na siyo chama hiki,” alieleza Maalim Seif.

Aliwaambia wanachama hao kuwa wakati huu ni vyema wakawa na umoja na kufanya kazi kwa pamoja katika chama ili kufikia malengo waliojiwekea.

“Wako watu wanajiita Mungiki, ambao wana nia mbaya na chama hiki, lakini tunawaambia nia zao zitawarejea wenyewe,” alieleza Maalim Seif ambaye ni Makamu wa Kwanza wa rais mstaafu wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ).

Alieleza kuwa kila mnafiki katika chama hicho atadhihirika na atatoka na kukiacha chama kikiendelea.

“Kwa hiyo ili kuwadhibiti hawa, ni vyema tukazidisha umadhubuti wa umoja wetu na kuwafagia wote ili chama kizidi kuwatia joto CCM na Seriklai zake,” alisema.

Alisema kuna watu kwa tamaa zao wamekubali kupokea hongo na kuanza kukihujumu chama chao huku akisema kuwa wamechelewa.

Maalim Seif alieleza kuwa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwa siku nyingi wamekuwa wakikiandama CUF kutokana na kuwa malengo ya kuwakomboa Wazanzibar na Watanzania, lakini wameshindwa kutokana na uimara walionao.

Aidha, alisema kuwa CCM wakiona chama cha upinzani kina dalili ya kuwaondoa madarakani, wanakifanyia kila aina ya hujuma ili kukimaliza na kudai kuwa hawana tena nguvu hiyo dhidi ya CUF.

“Wanatia migogoro katika vyama vya upinzani na kuwahujumu viongozi wake baada ya kuona wakati wowote madaraka yatawatoka,” alisema.

Naye Mkurugenzi wa Habari na Uenezi wa chama hicho, Salim Biman, alielza kuwa wasaliti wote ambao wamekisaliti chama hicho ni wale aliodai hawakuwa na machungu ya kuwakomboa Watanzania ambao tayari wameshachagua mabadiliko.

Aliwataka wanachama hao kutowapa nafasi wale aliodai mamluki kwani hawana nia nzuri kwa chama chao.

“Huu msukosuko unaopita kwenye chama chetu akipenda Mwenyezi Mungu utakwisha, licha ya kupata baraka za SMZ na SMT,” alieleza Biman.

Wakati huo huo Maalim Seif alizindua magari maalum kwa ajili ya kutoa huduma kwa Jimbo la Chambani ambayo yalitolewa na Mbunge wa jimbo hilo, Yusouf Salim Husein.

Wolper Afunguka Kulewa Pati ya Mtoto wa Diamond..Nillan

0
0

BAADA ya kuwa ‘topic’ kwenye sherehe ya 40 ya mtoto wa Nasibu Abdul ‘Diamond’, Nillan iliyofanyika hivi karibuni, Muigizaji Jacqueline Wolper  ameibuka na kusema katika maisha yake yote hajawahi kulewa.

Licha ya kuonekana kupoteza balansi hadi kufi kia hatua ya kutaka kuanguka alipokuwa akiwachana watu wanaomponda wifi  yake, Zarinah Hassan Zari ‘The Boss Hassan Zari ‘The Boss Lady’ kiasi cha watu kuamini hata maneno yaliyomtoka hakuyadhamiria bali ni pombe, Wolper alisema siku hiyo hakuwa amelewa na alichokiongea alimaanisha.

“Japo nakunywa lakini siku ile sikulewa na sijawahi kulewa. Niliyoyasema pale nilidhamiria maana watu wamekuwa wakimponda Zari kwa kuedit picha zake kitu ambacho si cha kweli na mimi lazima nimtetee yule ni mke wa bosi wa mume wangu,” alisema Wolper
Viewing all 104414 articles
Browse latest View live




Latest Images