Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104775 articles
Browse latest View live

Kazi Imeanza...Wawili Wapoteza Maisha kwa Kukosa Dawa za Kulevya..!!!!

$
0
0

Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Kuzuia na Kupambana na Dawa za Kulevya, Rogers Sianga amesema watu wawili wameripotiwa kupoteza maisha mkoani Mwanza kwa sababu ya kukosa dawa za kulevya mtaani kama walivyozoea.

Kamishna Sianga amesema taarifa hiyo ameipata kutoka kwa Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, hali inayomaanisha mafanikio ya mapambano ya dawa hizo, ambapo kwa sasa usambaaji wake umepungua mtaani kwa kiasi kikubwa.

"Nimeongea na Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, ameniambia kwamba kuna watu wwili wamefariki sababu walikuwa drug addict na sasa dawa hizo hazipo mtaani" Amesema Sianga

Sianga amesema mara baada ya kupokea kijiti cha mapambano kutoka kwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda, Mamlaka hiyo imeendelea na moto huo huo, na kwamba kwa hivi sasa timu yake hailali, ikiendelea na mapambano kila siku na kwamba hata leo, kuna mtuhumiwa mkubwa wa dawa za kulevya amekamatwa.

"Leo asubuhi tumemkamata mtuhumiwa mmoja mkubwa wa dawa kulevya, tupo naye tunaendelea kumuhoji, mengi yataibuka" amesema Kamishna Sianga

Kuhusu kuendelea kutumia mbinu iliyokuwa ikitumiwa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam paul Makonda ya kutaja majina hadharani,, Kamishna Sianga amesema hatatumia njia hiyo kwa kuwa kutaja majina ya watu hadharani kunaweza kuiingiza serikali katika matatizo maana kuna watu wengine wanaweza kutoa majina ya watu kwa sababu ya chuki binafsi.

Amesema njia anayoitumia ni kuwakamata na kuwahoji kimyakimnya na wakishajiridhisha hatua nyingine za kisheria zinafuata.

Katika hatua nyingine, Sianga amesema Tanzania iko makini katika kuwashughulikia wahusika wakubwa wa dawa za kulevya duaniani tangu miaka mingi iliyopita, akitolea mfano mtuhumiwa mmoja wa kike ambaye ni gwiji katika biashara hiyo au 'King Pin', ambaye hivi sasa amefungwa katika magereza ya Tanzania tangu mwaka 2010

"Tulimkamata mmoja kati ya watu waliokuwa wametajwa kama king pin wa dawa hizo nchini Marekani, alikuwa ameshindikana, na huko Marekani alikuwa na kesi zaidi ya 40, lakini alikamatwa hapa na amefungwa tangu mwaka 2010, yuko gerezani nafikiri kama siyo Keko, ni Segerea". Amesema Sianga.

Za Chini ya Kapeti...Diamond Hana Furaha na Zari,Makubwa Yaanikwa Juu ya Maisha ya Wawili Hao Ndani ya Nyumba..!!!!

$
0
0

Taa nyekundu inamuwakia staa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ baada ya kubainika kuwa hana furaha na mpenzi wake wa sasa, Zarinah Hassan ‘Zari The Boss Lady  ’, twende pamoja hapa chini.

RAFIKI AMWAGA UBUYU

Mmoja wa wanafamilia wa Diamond (jina tunalo), ameibuka na kuvujisha ubuyu wa motomoto kwa Wikienda kuwa, jamaa huyo hana furaha na Zari kwani ameanza kuona kuwa huko tuendako uhusiano wao hauna mwisho mzuri.

AMEANZA KUSHTUKIA?

Mtu huyo wa karibu zaidi na Diamond ameeleza kuwa, staa huyo naye ameanza kuhisi kwamba huenda Zari hakumpenda kama alivyo na zaidi alifuata ‘chapaa’ ambapo anaweza kusepa zake muda wowote endapo fedha zitampiga chenga staa huyo wa Wimbo wa Marry You aliomshirikisha Ne-Yo wa Marekani. “Iko hivi, Diamond mwanzoni alikuwa anachukulia poa lakini nafikiri sasa hivi inafikia wakati hata yeye kengele ya hatari imeanza kugonga. Nafikiri ni kwa sababu sisi tunavyomshtuashtua  kwamba awe makini naye maana anaonekana ni mjanjamjanja sana.

“Kwa taarifa tulizozipata, hata kule Afrika Kusini, inaonekana alimwagana na yule mumewe (Ivan Semwanga) kwa sababu ya kuvuna alichokuwa amekitaka, hivyo mara nyingi sana hata mimi nimekuwa nikimueleza Diamond awe makini sana katika eneo hili,” alisema mwanafamilia huyo.

WEMA NDO’ MPANGO MZIMA

Chanzo hicho kilizidi kutiririka kuwa, Diamond alikuwa sahihi alivyokuwa kwenye uhusiano na mlimbwende matata Bongo, Wema Isaac Sepetu ‘Madam’ kwani ni mtu ambaye alikuwa anamfahamu vizuri historia yake na mwenye mapenzi ya dhati. “Si unajua Wema akipenda huwa anapenda kweli? Ndo’ maana licha ya kuwa miaka ya karibu minne imepita  sasa tangu waachane, lakini Diamond bado anaonekana kulikumbuka sana penzi la Wema.

“Anauona upendo wa kweli kwa Wema licha ya kuwa walipishana kwa namna moja au nyingine. Wema hakuonesha kwamba anamhitaji kwa ajili ya fedha. Ndiyo maana alianza na Diamond hata akiwa bado fedha hazimchanganyia kivile,” alisema ndugu huyo.

USHAURI WA BURE

Jamaa huyo alisema kuwa, wao kama familia, ingawa si busara sana kumshauri mtu kuhusiana na suala zima la mapenzi, lakini wameona si vibaya kama watampa tahadhari ili aweze kuchuja mbivu na mbichi. “Tunataka ajue kama anaendelea kuishi naye, aishi naye kwa staili gani ili asiumbuke baadaye itakapotokea ameshuka kimuziki.

“Hatumwambii amuache, lakini  tunataka ajue kwamba tunasikia mengi yanayomhusu. Inasemekana Zari suala la kumzalia mwanaume ili aweze kutimiza matakwa yake siyo ishu.

‘ALIMPIGA’ IVAN?

“Kwa Ivan (mume wa zamani wa Zari) alikuwa mpole. Akavuna mkwanja wa kutosha ambao ulimwezesha kufungua maduka na kumiliki shule na vyuo Afrika Kusini ikiwemo na kuweka makazi katika nchi ambayo si yake.

“Nini hawa watoto wawili wa Diamond? Ivan alimzalia watoto watatu. Na ninasikia jamaa (Ivan) kuna wakati mambo hayakwenda vizuri, wakamwagana. Huku na huku ndiyo akajitokeza Diamond. Kipindi hicho Diamond ndiyo alikuwa ameanza kulishika soko la muziki Afrika Mashariki na mshiko nao ulikuwepo.

NI MJANJAMJANJA?

“Ukitazama kwa makini utaona namna ambavyo Zari ni mjanjamjanja, alichungulia Bongo, akaona anaweza kumtumia Diamond kupiga hela. Akaja na wazo la Zari All White Party, akaona isingekuwa rahisi kwa mtu mgeni kama yeye kuja kufanya tamasha nchini, akamtumia Diamond, akapiga mkwanja. Akatambaa,” alisema jamaa huyo.

NI KATILI?

Rafiki huyo alizidi kuweka bayana kuwa japo wao hawawezi kuhukumu moja kwa moja lakini kupitia matukio hayo, wanashindwa kumuwekea asilimia mia moja kwamba si mkatili. “Sisi tuko naye karibu. Tunamuona hata macho yake yanasema nini lakini hatuwezi ‘kujaji’ moja kwa moja ila kuna vitu tunaviona.

Mfano mdogo sana, kwenye ile Arobaini ya Nillan (mtoto wa pili wa Diamond), kuna jambo Zari alilifanya, tulishangaa sana. “Lilikuwa na viashiria fulani vya ukatili maana alimyakua Nillan kama vile ameshika bawa la kuku. Kitendo kile kilizua minong’ono sana kiasi ambacho wengi walitafsiri kwamba ni kitendo cha ukatili,” alisema rafiki huyo.

ZARI ANASEMAJE?

Wikienda lilifanya jitihada za kumsaka Zari bila mafanikio kwa kwenda nyumbani kwa Diamond zaidi ya mara tatu lakini walinzi walikataa kuruhusu mzazi mwenziye huyo wa Diamond kufanya mahojiano.

ALIWAHI KUFUNGUKA…

Hata hivyo, huko nyuma Zari alishafikishiwa habari kwamba Wabongo wamemshtukia kwamba ni mpigaji ambaye anatumia kigezo cha uhusiano kama silaha ya kuvuna fedha (gold digger) ndipo mama huyo wa watoto watano alipofunguka kupitia ukurasa wake wa Instagram: “When people call you a gold digger show them how you dig, too much money out there for all of us. Why hate? Stop BITCHCRAFTY it’s the 21st century,” aliandika hivyo akiwa anamaanisha kuwa hajali kuitwa mwizi wa mapenzi na kama akiitwa hivyo, anawaonesha kwa matendo namna gani anavuna fedha kwa ajili yao wote hivyo watu waache kupiga majungu katika karne hii ya 21.

Alipotafutwa Diamond kuhusiana na ushauri huo aliopewa, aliomba yeye asiwe mzungumzaji kwa sasa. KUMBUKUMBU Diamond kabla ya kutua kwa Zari, alishawahi kuwa na uhusiano na warembo wakali Bongo akiwemo mwanamitindo Jokate Mwegelo na Mtangazaji Penniel Mungilwa ‘Penny’ ambao wote walizidiwa nguvu ya umaa rufu na uhusiano wake na Wema.

Makonda na Sirro Waitwa Mahakamani Leo

$
0
0

MKUU wa Mkoa wa Dar es Salaam (RC), Paul Makonda, Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu Dar es Salaam (ZPC), Kamishna Simon Sirro na Mkuu wa Upelelezi wa kanda hiyo (ZCO), Camilius Wambura, wamepelekewa barua za mwito za kuwataka wafike Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam leo.

Viongozi hao wamepelekewa mwito huo kutokana na kesi ya Kikatiba iliyofunguliwa na Mwenyekiti wa Chadema Taifa, Freeman Mbowe dhidi yao.

Mbowe amefungua kesi hiyo kupinga Makonda kumtaja katika orodha yake ya watuhumiwa 65 wanaojihusisha na dawa za kulevya katika awamu ya pili na kumtaka afike katika Kituo Kikuu cha Polisi, Februari 10 mwaka huu, kwa ajili ya mahojiano.

Katika kesi hiyo Namba Moja ya Mwaka 2017, Mbowe pamoja na mambo mengine, anapinga mamlaka ya RC kumkamata kwa kile anachokiita kudhalilisha watu.

Kesi hiyo imepangwa kutajwa leo na itasikilizwa na jopo la majaji watatu, Sekieti Kihiyo ambaye ni kiongozi wa jopo hilo, akisaidiana na Jaji Lugano Mwandambo na Jaji Pellagia Kaday.

Mbowe anaiomba mahakama hiyo itamke kuwa vifungu vya Sheria ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa vinavyowapa mamlaka wakuu wa mikoa na wakuu wa wilaya kuwakamata watu na kuwatia mbaroni viko kinyume cha Katiba.

Aidha, Mbowe ambaye pia ni Mbunge wa Hai mkoani Kilimanjaro na Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni, jana alifungua maombi mahakamani hapo akipinga kusudio la Kamanda Sirro la kumkamata kama hatajisalimisha katika kituo cha polisi kwa mahojiano.

Mahakama hiyo imetoa hati za mwito wa kufika mahakamani hapo kwa wadaiwa hao ambao ni Makonda, Sirro na Wambura. Hata hivyo, inadaiwa Kamanda Sirro alikataa kupokea mwito huo akielekeza kuwa hati hiyo ya mwito ipelekwe kwa Wambura.

Wadaiwa kukataa kusaini Kwa mujibu wa Ofisa wa mahakama, Yusuph Juma ambaye alipeleka mwito huo, alidai kuwa baada ya kuelekezwa na Kamanda Sirro kuwa ampelekee mwito huo Wambura, alipokwenda kwa Wambura, hakumkuta.

Juma alidai hati ya mwito wa mkuu wa mkoa alipoupeleka hakumkuta na kwamba wasaidizi wake nao walikataa kuusaini mwito huo.
#HabariLeo

Majibu ya Ommy Dimpoz Baada ya Kudaiwa Kupangishiwa Nyumba na Bilionea

$
0
0
DAR ES SALAAM: Madai mazito! Hivi karibuni taarifa imevuja kuwa msanii mkali kwenye gemu la Bongo Fleva ambaye kwa sasa anatamba na ngoma iitwayo Kajiandae kwamba nyumba ‘kali’ anayotamba nayo sasa, amepangiwa na bilioneaa kijana ambaye ni mmoja wa wamiliki wa kampuni moja kubwa jijini.

Habari chengachenga zinaendelea kudai kuwa, mbali na kumpangishia mjengo mkali huyo wa Bongo Fleva, bilionea huyo kijana ndiye kila kitu kwenye maisha yake, anamsapoti kwenye muziki na mambo mengine mengi ikiwemo kumlipia sehemu ya kufanyia mazoezi yaani gym.

Mtoa habari huyo anaendelea kudai, Dimpoz na bilionea huyo wapo karibu sana kiasi kwamba wanawafanya watu kuwa na wasiwasi nao na kama ingekuwa ukaribu wao ni wa mwanaume na mwanamke wangehusishwa kutoka kimapenzi!

“Nakwambieni kweli kuna kitu kinaendelea kati ya Ommy na bosi huyo wa …(anaitaja kampuni), haiwezekani ampangishie nyumba, amlipie gmy na kumsapoti katika kazi zake za muziki. Lazima kuna kitu kinaendelea kati yao,” alisema mtoa habari huyo. UWAZI: Sasa wewe unahisi nini kinaendelea kati yao, si ni washikaji tu?

MTOA HABARI (MH): Hakuna cha ushikaji, ushikaji gani huo, sasa ngoja nikupe siri, mshikaji wake mkubwa na huyo kigogo ni MwanaFA, sasa kwa nini hayupo karibu zaidi ya MwanaFA na yupo na Dimpozi? Huwezi kujiuliza?

UWAZI: Ha Haa haaa! Povu linakutoka sana mzee, kwani hiyo nyumba aliyopangishiwa Dimpoz wewe unajua ipo wapi na analipiwa shilingi ngapi?

MH: Nyie mfanye uchunguzi, wewe unataka kila kitu nikusafishie picha, haya ni hivi, nyumba ipo Mbezi Beach, analipiwa shilingi ngapi, anaishi vipi, kazi kwako na wewe kusafisha picha!

UWAZI: Naona unapaniki mzee, twende taratibu vipi kuhusu hiyo gym anayolipiwa na huyo kigogo, ipo wapi na analipiwa shilingi ngapi?

MH: Aisee una maswali sana, ninachojua gym inaitwa Colosseum halafu siyo Ommy Dimpoz tu, mastaa wengi tu wanafanyia mazoezi pale.

UWAZI: Hao pia wanalipiwa na huyo kigogo?

MH: Sijui kaka, mimi nakupa habari hiyo tu kwa leo (akakata simu).

OMMY DIMPOZI HUYU HAPA

Alipotafutwa Dimpoz kwenye anga zake ili aweze kuanika ukweli kuhusu tuhuma hizo. Dimpoz alipopatikana na kusomewa mashitaka yake ilikuwa hivi;

DIMPOZ: Sasa ndugu yangu hivi ni kila mtu huwa anatafutwa na kuulizwa anapoishi, anaishi vipi, nani anamlipia pango au ni mimi tu?

UWAZI: Aaaa! Watu wanaulizwa hasa mastaa, we eleza ukweli tu mzee.

DIMPOZ: Umesema hiyo nyumba ninayodaiwa kupangiwa ipo wapi?

UWAZI: Eti inasemekana ni Mbezi Beach kaka.

DIMPOZ: Dah! Unaona sasa, mimi naishi kwangu Kigamboni kwa hiyo hayo madai hayana ukweli.

UWAZI: Na unahisi ni kwa nini huo ukaribu wako na huyo kigogo unatiliwa mashaka na watu, na ni kweli kuwa kakulipia gym na anakusapoti kwenye shughuli zako zingine za kimuziki.

DIMPOZI: Kaka naingia benki, siwezi kuzungumza lingine lolote. Dimpozi alikata simu.

Miujiza ya Shekh Sharifu Rashid Kutoka Bagamoyo , Anarudisha Mapenzi na Kusafisha Nyota

$
0
0

MIUJIZA YA SHEKH SHARIFU RASHID KUTOKA BAGAMOYO PWANI, (RUDISHA MAHUSIANO YAKO NDANI YA MASAA 48 TU) ASANTE KWA KUENDELEA KUMPIGIA SIMU SHEKH SHARIFU RASHID KWA WALE WENYE MATATIZO NA WALE WANAOTOA SHUKRANI:

SHEKH SHARIFU RASHIDI ni mtaalamu wa tiba mbalimbali za asili, anatumia kitabu cha quran, dawa za asili, dawa za kiarabu na majini, anazo dawa za mapenzi, nguvu za kiume, chango, ngiri maji na n.k, anakuvutia mpenzi alie kuacha au alie mbali, pia anatoa pete za bahati zilizoambatanishwa na jini mali kulingana na nyota yako, anaouwezo mkubwa wa kutumia jina la muhusika kwa kutatua tatizo lako, anaouwezo wa kumrudisha mtu aliepotea kimiujiza, pia anatibu kwa njia ya simu popote ulipo,

WASILIANA NAE KWA SIMU NA WHATSAPP NO: 0718-668347. 0685-224047, 0767-204308 au follow@shekh_sharifu_rashid, Email:shekhsharifurashid@gmail.com

Wachungaji wa MAKANISA Wanajua Biashara Sana..Wanacheza na Mahitaji ya Soko - Nikki wa Pili

$
0
0

Rapa Nikki wa Pili kutoka katika kundi la Weusi ameungana na rapa Nay wa Mitego kusema kuwa baadhi ya wachungaji wa makanisa hivi sasa wamefanya makanisa kama biashara na kujiingizia kipato.

Kwa upande wake Nikki wa Pili anasema wachungaji wanajua sana biashara kwa kuwa wanajua mahitaji ya watu kulingana na wakati jambo ambalo huwafanya wachungaji hao kuja na maombi ya kitu ambacho huenda wakati huo ndiyo hitaji kubwa kwa walio wengi hivyo ni lazima watu wenye hitaji hilo waweze kufika katika madhehebu hayo.

"Maombi ya kuombea waliokosa waume..wachungaji wanajua biashara sana..wanacheza na mahitaji ya soko" aliandika Nikki wa Pili 

Mbali na hilo Rapa Nikki wa Pili amefunguka na kusema katika muziki hakuna kitu kinaitwa kubebwa bali unatakiwa kufanya kazi kwelikweli ili kuendelea kuwa katika ramani ya muziki kwa muda mrefu, kwani yeye anakaribia kufikisha miaka 10 na hiyo ni kutokana na jitihada zake na kufanya kazi kwa kujituma zaidi.

"Januari mpaka sasa nimesharekodi zaidi ya nyimbo 10, G Nako Warawara amerekodi zaidi ya nyimbo 20 labda ndiyo sababu nakaribia kufikisha miaka 10 kwenye game, muziki hauna bahati wala kubebwa fanya kazi" alisema Nikki wa Pili 

Tundu Lissu: Serikali Ina Hofu Na Mimi TLS

$
0
0
Mwanasheria Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo(CHADEMA), Tundu Lissu, amesema ameanza kuogopwa na viongozi wa serikali  baada ya jina lake kuwa miongoni mwa majina matano bora ya wagombea wa nafasi ya urais katika Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS) kutokana na misimamo yake ya kuitetea Katiba ya Tanzania.

Akizumgumza na waandishi wa habari  Mwanza jana, Lissu alisema  tangu atangaze nia yake ya kugombea urais wa TLS ameanza kuogopwa  kutokana  na kujulikana kwa   misimamo yake kuhusu  masuala ya   sheria,  siasa na  katiba ya nchi hii.

Alisema TLS ina majukumu makubwa katika nchi ya kulinda utawala wa sheria na wanasheria ndiyo wanaojua kuliko mtu yeyote  zinapotungwa sheria mbovu na zile za kikandamizaji, pia wao ndiyo wanapaswa kuwa wa kwanza kuanza kuzipigia kelele sheria hizo.

“Kwa miaka mingi  TLS imeongozwa  na watu ambao hawafikiri kwamba wajibu wao wa kwanza kulinda utawala wa sheria,  wao wanafikiri wajibu wao wa kwanza ni kuwapendeza  wanasiasa na matokeo yake TLS imepotea, wanachoogopa  ni kwamba hii raha ambayo wameipata miaka yote hii wakati  wanasheria wa  TLS wakiwa  usingizini akija huyu Lissu itaisha,” alisema Lissu.

Alisema aligombea nafasi hiyo  baada ya kumsikia Rais Dk. John Magufuli akizungumza mbele  ya watanzania kwamba wakili  yeyote  atakayewatetea  watuhumiwa wanaokutwa na  dawa ya kulevya au nyara za serikali wakamatwe na kuwekwa ndani.

Alisema aliposikia kauli hiyo alicheka na kusema sasa ni wakati wa yeye kuwa rais wa TLS ili kauli za aina hiyo zikome na siku mbili kabla ya Rais Dk. John Magufuli kutoa kauli hiyo,  Bunge lilipitisha sheria ya msaada wa sheria.

“Sheria hiyo inasema mtu yeyote anayefunguliwa kesi ya jinai, au madai kama ni maskini hana uwezo wa kumlipa wakili atapatiwa huduma hiyo na wakili atalipwa  na  mtendaji mkuu wa mahakama.

“Sheria hiyo inampatia haki  mwananchi yeyote atakayekuwa  na kesi ya mauaji, pembe za ndovu au dawa za kulevya  kupata wakili atakayelipwa na serikali.

“Siku mbili baadaye Rais anakinzana na sheria hiyo nilishangaa kweli.  Tayari sheria hiyo imetungwa  ni jambo muhimu kweli kwa sababu katika  nchi hii watu wanasingiziwa sana, kwenye maegereza nyingi   nchini wamejazana wananchi ambao hawana hatia na wapo huko kwa sababu hawakuwa na mawakili wa kuwatetea,” alisema Lissu.

Lissu alisema  endapo atachaguliwa kuwa rais wa TLS atahakikisha sheria ya msaada wa  sheria  inatekelezwa.

Kuhusu hoja ya  Waziri wa katiba na  Sheria, Dk. Harrison Mwakyembe ya kutishia kukifuta chama hicho hicho kwa kuwa kimeanza kujiingiza katika masuala ya siasa, Lissu alisema wanaoleta hoja za kutaka kukifuta chama hicho kama ni wanasheria ujuzi wao wa sheria ni wa shaka lakini kama ni wasiojua sheria wanasamehewa.

Alisema  sheria ya iliyoanzisha TLS inasema mwanachama yeyote aliyekidhi vigezo  vya chama hicho ana haki ya kuwa mgombea wa nafasi yoyote ya uongozi na haijasema  ukiwa mwanachama wa chama chochote cha siasa unapungukiwa sifa  ya kugombea.

“Watu wanazungumza   kana kwamba ni makosa mwanasheria kuwa mwanasiasa, katika nchi hii katiba imeruhusu  siasa za vyama vingi, kuwa wanachamaau  kiongozi wa chama.

“Kuwa tu mwanachama una kuwa na fursa ya kugombea nafasi mbalimbali za uongozi serikalini lakini sasa watu wanataka kuaminishwa kuwa ukiwa mwanasiasa huna haki,” alisema

CCM Yamweka Kiporo Yusuf Manji

$
0
0
Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Temeke, kimesema hakitamjadili Diwani wa Kata ya Mbagala Kuu, Yusuph Manji, hadi kesi yake kuhusu madai ya kutumia dawa za kulevya itakapomalizika mahakamani.

Msimamo huo umetolewa baada ya kuwapo  taarifa kwamba chama hicho kimepanga kumjadili Manji kuhusiana na tuhuma zinazomkabili.

Taarifa hizo zilieleza kuwa diwani huyo atajadiliwa vikaoni ili afukuzwe uanachama kwa kuwa chama hicho hakitaki wanachama wenye tuhuma na wanaovunja amri za nchi.

“Kikao cha kamati ya utendaji ya chama kitaitishwa mapema mwezi huu kutekeleza maazimio ya vikao vilivyokwisha kufanyika kuanzia tawi hadi kata ambavyo vilikuwa na agenda ya kumjadili Manji kuhusu tuhuma zake,” ilisema sehemu ya taarifa hiyo.

Jana, Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Temeke, Yahaya Sikunjema, alisema hawawezi kuingilia suala ambalo bado liko kwenye vyombo vya sheria.

“Wakati utakapofika na ikaonekana ipo sababu baada ya vyombo husika vya sheria kama mahakama kumtia hatiani.

“Kama chama tutakaa tuangalie katiba yetu inatuelekeza vipi na hapo ndipo tutachukua hatua,” alisema Sikunjema.

Wiki iliyopita Manji ambaye pia ni Mwenyekiti wa Klabu ya Yanga, alipandishwa kizimbani katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu akidaiwa kutumia dawa za kulevya.

Manji alikana shtaka hilo na kuachiwa kwa dhamana.

Mbwa Wakamata 20 Dawa za Kulevya...!!!

$
0
0

WATU 20 wamekamatwa kwa msaada wa mbwa wa polisi mkoani hapa katika wiki moja iliyopita, wakituhumiwa kujihusisha na dawa za kulevya.

Watu hao walikamatwa baada ya Jeshi la Polisi kuanza kutumia mbwa maalumu ili kusaka watuhumiwa wa madawa hayo, kwenye mabasi yanayopita barabara kuu zinazoingia na kutoka mkoani Singida.

Kamanda wa Polisi wa Mkoa, Debora Magiligimba alisema njia hiyo imesaidia kukamata watuhumiwa 20 ambao walikutwa na zaidi ya misokoto 7,000 ya bangi, 'unga' aina ya heroine na mirungi. Alisema kuwa zoezi hilo litakuwa endelevu ili kukabiliana na wauzaji na watumiaji wa madawa ya kulevya.

Kamanda Debora alisema wauzaji na watumiaji wamekuwa wakibuni njia mpya kila siku kwa ajili ya kufanikisha "shughuli zao haramu".

Vita dhidi ya dawa za kulevya nchini imepata msukumo mpya tangu Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda ataje watu 65 waliotakiwa kuisaidia polisi kuhusu biashara ya mihadarati wiki mbili zilizopita.

Kabla ya kutaja orodha hiyo iliyokuwa na viongozi wa dini, wafanyabiashara na wanasiasa, Makonda alikuwa ametoa orodha ya polisi 12 na wasanii kadhaa ambao walitakiwa pia kufika Kituo Kikuu cha Polisi, Kanda Maalumu ya Dar es Salaam kwa mahojiano.

Vita hiyo ikaongezwa nguvu na Inspekta Jenerali wa Polisi (IGP), Ernest Manguvita ambaye naye aliamuru katika taarifa Makamanda wa mikoa yote nchini waongeze nguvu.

Tangu hapo, zaidi ya watu 500 wamekamatwa katika mikoa mbalimbali nchini wakihusishwa kwa namna moja au nyingine na biashara ya dawa za kulevya.

Katika matukio yote hayo ya ukamataji, hata hivyo, makamanda wa polisi wa mikoa walielezea kukamata watuhumiwa bila ya kuhusisha mbwa waliopewa mafunzo maalumu ya kugundua mihadarati.

Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Injinia Hamad Masauni alikabidhiwa na Kaimu Balozi wa Marekani nchini, Virginia Blaser mbwa maalumu wa kubaini madawa ya kulevya na pembe za ndovu mwaka jana, tukio lililofanyika kwenye Bandari ya Dar es Salaam.

ZOEZI ZURI

Abiria wa mabasi yaliyofanyiwa upekuzi kwa kutumia mbwa wa polisi na kuzungumza na Nipashe, walieleza kufurahishwa na zoezi hilo kwa madai kuwa litaondoa uwezekano wa kusambazwa ovyo kwa madawa hayo.

"Zoezi hili ni zuri sana, naomba liendelee ili kupiga vita uuzaji na matumizi yake," alisema, Keneth Paul, abiria raia wa Marekani, aliyesafiri na moja ya basi kutoka Arusha kwenda mikoa ya Kanda ya Ziwa.

"Mimi nilikuwa mtumiaji sana, lakini niliachana nayo na sasa nahubiri injili. Awali akizungumza zaidi, Kamanda Debora alisema mtuhumiwa mmoja aliyekamatwa na kete moja ya heroine, baada ya upelelezi alibainika kuwa ni mtumiaji, lakini anaendelea na mahojiano zaidi ili kubaini alikoinunua.

Alisema baada ya upelelezi kukamilika watuhumiwa wote watapandishwa kizimbani kujibu tuhuma zinazowakabili.

Kamanda huyo wa polisi wa mkoa aliwataka wakazi wa mkoa wa Singida kuendelea kushirikiana na jeshi lake ili kuunga mkono jitihada za serikali ya awamu ya tano katika kutokomeza madawa ya kulevya nchini.

Rais wa tano, John Magufuli ameshaagiza vita hiyo isiache mtu yeyote. “Hakuna mtu maarufu, mwanasiasa, waziri au kiongozi yeyote au mtoto wa fulani, askari ambaye anajihusisha na dawa za kulenya aachwe, hata awe mke wangu Janeth... kamata wote weka ndani,” alisema Rais Magufuli mwanzoni mwa mwezi.

Aidha, Rais Magufuli pia ameshamteua Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Kuzuia na Kupambana na Dawa za Kulevya na kuweka msimamo wa Serikali yake juu ya zaidi ya Watanzania 1,000 waliofungwa au kuhukumiwa kunyongwa katika magereza mbalimbali duniani.

Rais Magufuli amesema serikali haitajishughulisha na Watanzania waliokamatwa ughaibuni na kuhukumiwa kunyongwa kutokana na kujihusisha na biashara ya dawa za kulevya.

Mbowe Aaachiwa Huru Polisi,Asisitiza Lazima Makonda Aisome Namba Mahakamani Leo..!!!

$
0
0

Hatimaye Jeshi la Polisi nchini limemwachia Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe baada ya kumshikilia kwa saa 10.

Ofisa Habari wa chama hicho Tumaini Makene, amethibitisha kuachiwa kwa Mwenyekiti huyo ambapo pia amesema polisi wamemtaka kuripoti katika Kituo Kikuu cha Polisi (Central) kesho Jumatano.

Mbowe aliachiwa saa saba usiku wa kuamkia leo baada ya kufanyiwa upekuzi nyumbani kwake na kukutwa ambako polisi hawakukuta dawa za kulevya zaidi ya nyaraka mbalimbali za chama zikiwamo Hati moja ya Chadema-Chaso kwenda kwa Mwenyekiti ya Julai 16, mwaka 2013, picha mbalimbali nane za matukio ya uhalifu, hati moja ya Rasimu ya Kwanza ya Chadema kuhusu uundwaji wa Red Brigade na hati moja ya kurasa 13 inayoongelea mambo ya Muungano.

Hata hivyo, pamoja na Mbowe kuachiwa na polisi Makene amesisitiza kwamba kesi yake aliyomfungulia Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda kumtaja katika orodha ya wahusika wa dawa za kulevya iko pale pale.

Idris Sultan Asema Amekoma Kuweka Wazi Mkwanja Anaoingiza Kwenye Deal Anazosaini

$
0
0
Mchekeshaji Idris Sultan amefunguka kwa kusema kuwa sasa hivi hatoweka wazi tena kiasi cha pesa ambacho atakuwa anaingiza kwenye deal mbalimbali anazosaini.

Mshindi huyo wa BBA 2014 ambaye hivi karibuni alisaini deal ya balozi wa amani Tanzania, amedai baada ya wananchi kujua pesa ambazo aliingiza kupitia BBA kulisababisha mambo mengi kutokea.

“Kusema kweli siwezi kuweka wazi hela ambazo naingiza kwenye deal ya ubalozi lakini ni pesa nzuri sana, ningependa watu wanifuatilie mimi, hizi ishu nyingine waachane nazo kwa sababu ile ishu ya BBA ilizungumziwa sana. Yaani baada ya watu kujua napewa kiasi gani ilikuwa tatizo sana,” alisema Idris.

Fahamu Sifa za Mwanamke Asiyefaa Kuolewa Asilani

$
0
0
SUALA la kuoa lipo tu licha ya kwamba wapo wanaochelewa kuingia kwenye maisha hayo wakihisi inaweza kusitisha furaha ya maisha yao. Nasema hivyo kwa kuwa najua wapo wanaoamini kuoa ama kuolewa ni kujiingiza kwenye matatizo.

Dhana hiyo haina mashiko kiviile, asikuambie mtu unapoingia kwenye ndoa na mtu anayekupenda na wewe unampenda kwa dhati, karaha hakuna licha ya kwamba kugombana kwa hapa na pale hakuwezi kukosekana.

Hata hivyo, nikiri tu kwamba, zipo ndoa ambazo ni ndoano. Yaani unakuta mtu kaingia kwenye ndoa na mtu ambaye hakuwa amedhamiria, matokeo yake kadiri siku zinavyokwenda anahisi ameingia chaka na anaishia kuomba ndoa isiwepo.

Leo nataka kuwazungumzia wanawake ambao ni majanga na ukijichanganya ukaingia nao kwenye maisha ya ndoa, utakiona cha mtemakuni.

10. Asiyeridhika na penzi unalompa
Wapo wanawake ambao wewe unaweza kujitahidi kumpatia mapenzi kadiri unavyoweza lakini yeye hatosheki. Anakuchukulia wewe ni dhaifu sana na wakati mwingine kuhisi yupo mwingine anayeweza kumpa zaidi ya kile unachompa, huyu ni tatizo.

9. Wivu kupindukia
Hatukatai, wivu ni muhimu sana kwenye suala la mapenzi lakini kuna ule wivu uliopindukia kiasi cha kuwa kero. Walio kwenye ndoa wananielewa namaanisha nini.

Kwa kifupi mtu mwenye mapenzi ya dhati na mwenziye lazima awe na wivu lakini ukiwa na ule wa kupinduki ni tatizo linaloweza kuitibua ndoa.

8. Anaona unamsaliti kila mara
Huku kunatokana na kutokujiamini tu. Ukioa mwanamke ambaye kila wakati unapokuwa mbali naye anahisi unamsaliti, huyo hakuamini na kamwe hamuwezi kudumu. Mara kadhaa mtakuwa mkigombana akihisi una mwingine kumbe hakuna ukweli katika hilo.

7. Anahisi amekosea kuwa na wewe
Wapo wanawake ambao wanapoingia kwenye ndoa baada ya muda wanahisi wamekosea kuolewa na mwanaume huyo. Unakuta mke wa mtu anahisi fulani ambaye zamani alikuwa kwenye uhusiano naye angekuwa sahihi zaidi baada ya kuona upungufu fulani kwa huyo aliyemuoa.

6. Yuko kimasilahi zaidi
Kuna wanawake ambao ukiwaoa wanakuwa na furaha na wewe ukiwa unazo tu, ukiishiwa wanaanza kununa na kuleta visirani vya hapa na pale. Hawa ni tatizo, mwanamke wa kweli ni yule anayeridhika kuwa na wewe kwenye shida na raha

5. Yuko tayari kuachana na wewe
Hivi hujawahi kumsikia mke wa mtu akimwambia mumewe; ‘Kama vipi tuachane, kwanza kwetu sijafukuzwa na nilikuwa nakula, nalala, navaa.” Mwanamke anayeweza kumtamkia mume wake maneno haya, huyo si mke na kamwe hawezi kukufanya uwe na furaha.

4. Hapendi ndugu zako
Waswahili wanasema ukipenda boga, penda na ua lake. Kama utatokea kuoa mwanamke ambaye anakupenda wewe tu lakini akija ndugu, rafiki au mtu mwingine wa karibu yako anabadilika, huyo ana matatizo kwani atakufanya utengwe na jamii yako.

3. Anajali mafanikio binafsi
Siku zote wawili waliotokea kupendana wakioana wanakuwa mwili mmoja hivyo lazima watakuwa wanawaza na kufanya maamuzi pamoja.

Ogopa sana mwanamke anayependa kutumia kipato chake kufanya mambo binafsi tena kwa siri. Kwa mfano kusaidia kwao, kujenga nyumba kwao, kuanzisha miradi yake bila kukushirikisha.

2. Eti akizaa utamzeesha
Hili kwa wale wanaopenda kuoa masistaduu. Wapo ambao wakitajiwa suala la kuzaa mara baada ya kuingia kwenye ndoa wanagoma wakidai eti watazeeshwa hivyo waachwe kwanza wale ujana. Wakati huo unaweza kukuta mwanaume anataka mtoto ili apate ile heshima, mke anagoma kwa sababu hiyo isiyo na msingi, hili ni tatizo.

1. Anataka awe na sauti
Mwanaume siku zote atabaki kuwa kiongozi wa familia lakini wapo baadhi ya wanawake hawataki kukubaliana katika hilo. Wengi wanalazimisha usawa na wengine wakitaka wao ndiyo wawe na sauti kuliko wanaume zao

Kusaga Aonjesha Ujio wa Station Mpya ya redio 103.3 Dar

$
0
0
Station mpya ya redio imetua jijini Dar es Salaam. Inapatikana kwenye masafa ya 103.3 (zamani yalikuwa yakitumiwa na BBC).

Kwa mujibu wa poster iliyowekwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Clouds Media Group, Joseph Kusaga, station hiyo inaonekana kuwa ya muziki peke yake na tayari imepewa sifa za kuwa ‘Africa’s Number 1 Hits Station.’ Ni wazi kuwa inamilikiwa na kampuni hiyo ambayo hadi sasa ina redio mbili, Clouds FM na Choice FM. Bado haijajulikana itatumia jina gani.

Kwa sasa inapiga muziki peke yake.

VIDEO: Irene Uwoya Aongea Kwanini Hakupost Chochote Baada ya Wema Sepetu Kukamatwa

$
0
0
Kwenye hii Exclusive Interview Mwigizaji staa wa Tanzania Irene Uwoya amekaa na Mtangazaji Millard Ayo na kuelezea ishu mbalimbali ikiwemo kwanini hakupost chochote baada ya Mwigizaji mwenzake Wema Sepetu aliposhikiliwa kwa tuhuma za dawa za kulevya.

Pamoja na hayo, Irene amezungumzia ishu mbalimbali za ndoa yake iliyovunjika pamoja na ishu mbalimbali za maisha yake, bonyeza play kwenye hii video hapa chini:

Mzee wa Upako: Sinywi Pombe, ila Nakunywa Wine

$
0
0
Mchungaji Anthony Lusekelo maarufu kama ‘mzee wa upako’ amefunguka kuhusu tuhuma za yeye kunywa pombe, na kuweka wazi kuwa hanywi pombe bali anakunywa ‘wine’ isiyo na kilevi, huku akisema kuwa amewasamehe waandishi aliwowatabirian kifo.

Amefunguka hayo kwenye kipindi cha KIKAANGONI cha EATV, na kuweka wazi kuwa wanaomtuhumu kuwa yeye anakunywa pombe wanapaswa kutoa ushahidi juu ya tuhuma hizo, na kwamba unywaji pombe unaweza kuwa dhambi ama usiwe dhambi kulingana na imani na dini ya mtu. “Hao wanaotuhumu kuwa nakunywa pombe, waeleze ni pombe gani nakunywa, nilikuwa nakunywa wapi na aliyeniona ni nani, kuna sehemu nyingine pombe siyo dhambi, dini nyingine mpaka kanisani kuna bar.”

Alipoulizwa Je, kunywa bia kiasi bila kulewa ni dhambi au siyo dhambi? alijibu kuwa “Inategemea na makanisa, kuna mengine hata kunywa soda ni dhambi. Dhambi ni makubaliano yenu kwenye dini yenu. Biblia inasema kula kitu chochote hata chakula kama ukila kupitiliza ni dhambi, hata unywaji wa pombe ukinywa ukapitiliza ni dhambi. Biblia haijaandika moja kwa moja kwamba msinywe pombe, imesema msilewe kwa kuwa ndani ya ulevi kuna ufisadi, cha msingi mbadilishe ulevi wenu uwe ni roho mtakatifu”

Aidha mzee wa upako alipoulizwa kuhusiana na ahadi yake hiyo ya kuwatabiria vifo waandishi walioandika habari iliyohusisha kurushiana maneno na jirani zake ambapo baada ya hapo vyombo vya habari hasa magazeti yaliripoti tukio hilo kwa namna ambayo Mzee wa Upako hakuipenda, na hata kufikia hatua ya kuwatabiria kifo waandishi walioandika habari hiyo, amesema:

“Tulisema hatuwezi kutumia nguvu kubwa sana kuwaombea watu kifo, kwa sababu sisi ni wanadamu, na wanadamu tuna mapungufu kwahiyo nikaona ni bora kumuachia Mungu. Uwezo huo wa kuwaombea watu wakafa, mimi ninao, lakini nikaona inasaidia nini mtu kumuombea mabaya, kwahiyo nikaamua kusamehe.”

Source: Eatv.

Kimenukaaa..Kamishna wa Madawa ya Kulevya Amkosoa Makonda,Adai Hakufuata Sheria Kuwaita Kina Wema Sepetu Kienyeji Enyeji.....!!!!

$
0
0

KAMISHNA Mkuu wa Mamlaka ya Kuzuia na Kupambana na Dawa za Kulevya nchini, Rogers Siyanga amesema mfumo uliotumika na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda hivi karibuni kutaja majina ya watuhumiwa wa dawa hizo ni tofauti na utaratibu wa utendaji kazi wa kamisheni yake, akieleza watajikita katika kufanya kazi kwa kuzingatia weledi na sheria.

Aidha, Siyanga amesema licha ya kukabidhiwa majina 97 na mkuu huyo wa mkoa katika jalada lililosomeka, ‘majina 97 ya wauzaji dawa za kulevya wakubwa’ yeye atawachunguza watu hao na kufuata taratibu zote za kisheria katika kuwachukulia hatua, lakini wanasheria wamesema Makonda anaweza kusababisha Serikali kushtakiwa.

“Kutangaza majina si kipaumbele chetu sisi tunazingatia uchunguzi na mahojiano ambayo yanaweza kutupatia taarifa zaidi za wahusika kwani huu ni mtandao wa kidunia,”alisema.

Kauli hiyo ya Siyanga inaweza kutafsiriwa kuwa ni kumkosoa Makonda kwa kutaja majina ya watu 65 akiwahusisha na dawa za kulevya, jambo linalotajwa pia kuwa kinyume cha sheria.

Alisema kimsingi mapambano ya dawa za kulevya yalikuwa yakitaribiwa wa Tume ya Kudhibiti Dawa za Kulevya na sheria husika ilitoa nafasi pia kwa mamlaka mbalimbali kujihusisha na operesheni hiyo hadi kufikisha watuhumiwa mahakani.

Kamishna huyo alisisitiza kuwa kwa mujibu wa Sheria ya mwaka 2015 wanayoisimamia, kutaja majina si kipaumbele kikuu kwao na kwamba wanazingatia uchunguzi zaidi ili kubaini mtandao mzima wa dawa za kulevya.

Alisema kupambana na dawa za kelevya si jambo rahisi na kuwa wanaohusika na biashara hiyo ni watu ambao kwenye jamii wanaonekana wasafi hivyo ni vema kujipanga.

Alisema suala la watu wanaodaiwa kutumia dawa za kulevya kufikishwa mahamakani limejikita katika pande mbili ambazo ni baada ya mhusika kukataa kutumia, lakini pia inaweza kuwa ni sehemu sahihi ya kumtaka mhusika kuacha na huwekwa katika uangalizi.

Siyanga alitoa wito kwa watumiaji wa dawa za kulevya kutoa ushirikiano ili waweze kuwasaidia kwani ni moja ya majukumu yao.

Kesi ya Manji

Alipotakiwa kueleza ni kwa nini Manji alipelekwa mahakamani alisema kimsingi kesi hiyo haiwahusu kwa sababu ilianza kupitia mamlaka nyingine kabla ya mamlaka yake kuanza kazi.

Mapapa wa dawa za kulevya

Kwa upande mwingine, Siyanga alisema mamlaka yake inatarajia kuzunguka katika magereza mbalimbali duniani na kuzungumza na Watanzania ambao wamehukumiwa kunyongwa na vifungo vya maisha ili waweze kuwataja watu ambao wanawatuma kufanya biashara hiyo.

Alisema kupitia utaratibu huo wanaweza kukabiliana na tatizo hilo huku akibainisha kuwa akitolea mfano mfanyabiashara mkubwa ambaye ni mwanamke amehukumiwa kifungo jela, baada ya wafungwa zaidi ya 40 nchini Ujerumani, kubainisha kuwa yeye ndiye aliwatuma.

Kamishna Siyanga alisema pia mfanyabiashara mwingine mkubwa mwanaume, amehukumiwa kwenda jela mwaka 2010 baada ya kubaini mtandao mzima wa tatizo hilo na kuwa mkakati wao ni kumaliza mtandao zaidi.

“Huyu mwanamke yupo gerezani kati ya Segerea au Keko. Huyu mwanaume pia yupo katika magereza yetu,”alisema.

Alisema Tanzania imekuwa ikikamata hadi tani 1.5, kilo 800, 200, 100, 50 hivyo wapo katika mapamano ya kuhakikisha kuwa hali hii inakabiliwa.

Wanasheria wanena

Wakati Siyanga akieleza hayo, wanasheria wameeleza kwa kuandika ‘majina 97 ya wauzaji wa dawa za kulevya wakubwa, Makonda anaweza kusababisha Serikali kushtakiwa wakisema inawezekana hakuwa anajua anachokifanya.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti, wanasheria hao walisema kilichofanywa na Makonda kuandika watu hao ni wauzaji, kisheria ni kosa kwani tayari alikuwa amewahukumu wakati yeye hana mamlaka hayo.

“Sijui alitoa wapi uwezo wa kuandika kwamba hao watu 97 ni wauzaji wakati bado hata hawajapelekwa mahakamani, achilia mbali kukamatwa. Nafikiri hakuwa anajua nini anakifanya ile kwenye sheria ndiyo tunaita ‘defamation’ yaani unampa mtu hukumu hata kabla ya kumfikisha Mahakamani:

“Hakuna mahali popote kwenye Katiba ya Tanzania inayompa mtu mamlaka hata Rais ya kumhukumu mtu tofauti na mahakama, hiki ndio chombo kinachoweza kusikiliza kesi, kuitolea ufafanuzi na kutoa hukumu tofauti na hapo unaweza baadaye kushtakiwa kwa kuchafua majina ya watu,”alisema Joseph Kiwanga wa Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM).

Kauli hiyo iliungwa mkono na Wakili James Marenga ambaye alisema sheria ipo wazi kuwa chombo pekee chenye uwezo wa kuhukumu nchini ni Mahakama na siyo Bunge, Baraza la Wawakilishi wala Serikali Kuu.

“Kilichofanywa na Makonda ni kinyume na sheria na endapo watu hao wakihojiwa na kukosekana na hatia wanaweza kufungua kesi ya madai. Katiba yetu inasema vizuri kabisa katika ibara ya 107 A kifungu kidogo cha kwanza kwamba mahakama ndio yenye mamlaka kisheria ya kusikiliza kesi na kumtia mtu hatiani au baada ya kumkosa na hatia hapo mtu huyo anakuwa hana kosa lolote lililothibitika.

“Sheria ilivyo hata kama polisi wamekamata kundi la mateja wanaotumia dawa za kulevya, au wamefanikiwa kuyakamata majambazi bado hawawezi kukupeleka moja kwa moja Segerea au Ukonga japo wana ushahidi hadi upelekwe mahakamani, upelelezi ufanyike ndio mahakama iseme kama imemkuta na hatia, tofauti na hapo unatuhumiwa tu,”alisema Marenga.

Wakili Marenga alisema kifungu cha 13 cha Katiba kinatoa haki ya mtuhumiwa kusikilizwa kwanza kabla ya kuhukumiwa na kuongeza kuwa kama watu hao hawatokutwa na hatia wanaweza kuidai fidia Serikali, jambo ambalo linaweza kulisabishia hasara Taifa kwa kulipa kundi kubwa la watu.

Kwa upande wake Mhadhiri wa UDSM, Dk James Jesse alisema kilichofanywa na Mkuu wa Mkoa ni makosa kwani alihukumu kabla ya kuwapeleka mahakamani na kwamba kama hana ushahidi wa kutosha dhidi ya watu hao ni rahisi kufunguliwa kesi ya kuchafua majina yao.

Hata hivyo, upande wake Wakili Ufforo Mangesho kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), alisema inawezekana Makonda alikuwa na lengo tofauti na ndiyo sababu ya kuyaita majina hayo ‘wauzaji’ badala ya watuhumiwa huku akijua hana uhalali wa kisheria wa kumhukumu mtu.

“Inawezekana kulikuwepo na kingine nyuma ya vita ya dawa za kulevya kwa sababu ninachoamini Makonda alikuwa anajua kabisa kwamba anavunja sheria kwa kuhukumu majina ya watu hadharani ilihali mahakama zipo na ndio zenye wajibu kikatiba wa kushughulikia kesi na kutoa hukumu,”alisema Mangesho.

Februari 13, Mwaka huu wakati akitangaza awamu ya pili ya kile anachokiita vita dhidi ya dawa za kulevya Mkuu huyo wa Mkoa alimkabidhi jalada hilo kamishna Sianga huku likiwa limeandikwa kwamba ni majina ya ‘wauzaji ’ wa mihadarati hiyo jambo ambalo lilileta tafsiri tofauti miongoni mwa wanasheria wakihoji uhalali wa Makonda kuhukumu.

A to Z...Simulizi 'Mzungu wa Unga' Alivyopekuliwa...!!!

$
0
0

SHAHIDI wa tatu, Konstebo wa Polisi (PC), Juliana Moses (31), ameieleza mahakama kuwa aliwapekua mshtakiwa Mwanaidi Mfundo, maarufu kama Mama Leila, na Sara Munuo katika vyumba vyao vya kulala na kupata pakiti nne za unga uzaniwao kuwa dawa za kulevya, fedha na hati tatu tofauti za kusafiri.

Aidha, PC Moses alidai kuwa kabla ya upekuzi huo alifika nyumbani kwa Mama Leila Mei 31, 2011 kati ya saa mbili na saa tatu usiku akiwa na polisi wenzake pamoja na mkuu wake, Kapufi, na kufanikiwa kuwaweka chini ya ulinzi washtakiwa wanane.

PC Moses alitoa madai hayo jana wakati akitoa ushahidi katika kesi ya kuingiza nchini dawa za kulevya zenye thamani ya sh. milioni 225, mbele ya Jaji Isaya Arufani.

Upande wa Jamhuri uliongozwa na Wakili wa Serikali Mkuu, Edwin Kakolaki, Wakili wa Serikali Mwandamizi, Joseph Maugo na Wakili wa Serikali, Paulina Mwangamila.

Akiongozwa na Kakolaki, shahidi alidai kuwa siku ya tukio aliambatana na askari wenzake wakiongozwa na kiongozi wao Kapufi kwenda kwenye kazi maalum.

"Afande alisema tunakwenda Mbezi Beach kwenye tukio, tulipofika tukaacha magari tukatembea hadi kwenye nyumba ya mshtakiwa wa kwanza," alisema PC Moses na kueleza zaidi:

"Tulifanikiwa kuizunguka nyumba kuiweka kwenye usalama, afande Kapufi aligonga mlango akajitambulisha ni askari lakini tulisubiri muda wa nusu saa bila kufunguliwa mlango.

"Tulipochungulia ndani tuliona watu wakizunguka huku na kule ndipo afande akagonga na kuwaarifu wasipofungua atavunja mlango.

"Mlango ulifunguliwa na mwanamke aliyejitambulisha kwa jina la Mwanaidi ama Mama Leila; aliwekwa chini ya ulinzi na wote waliokuwa ndani ya nyumba ile."

Akifafanua zaidi, alidai kuwa waliamrisha wote walioko ndani watoke nje, wakatoka watu wanane akiwamo Mama Leila.
Ifuatayo ni sehemu ya mwongozo kati ya wakili wa Jamhuri na shahidi:

Wakili: Baada ya kuwaweka chini ya ulinzi nini kilifuata?

Shahidi: Afande Kapufi alimtaka Mama Leila kumwelekeza makazi ya mjumbe wa eneo hilo kwa ajili ya kushuhudia upekuzi.

Hata hivyo, Mama Leila aligoma kutoa maelekezo kwa madai kuwa miongoni mwa wale walioko chini ya ulinzi atakuwa shuhuda wake.
Wakili: Kwanini aligoma?

Shahidi: Mama Leila alisema anaepuka aibu kwa majirani, lakini afande alikataa utetezi wake ndipo akakubali kutoa maelekezo.

Afande aliwaagiza askari wawili kati yetu, kwenda kwa mjumbe lakini walirejea wakiwa na wajumbe wawili wa jirani, baada wa yule anayehusika na eneo lile kudaiwa kuwa ameingia kazini usiku.

Wakili: Je, nini kilitokea?

Shahidi: Afande alijitambulisha kwao na kuwaeleza nia na madhumuni ya kuwaita ni kutaka wasimamie upekuzi wa nyumba ile.
Wakili: Mlipekua?

Shahidi: Ndiyo, afande alimtaka Mama Leila kutuelekeza chumba chake cha kulala, mimi, wajumbe na mwenyewe bosi, alikubali kutuongoza nikaanza kumpekua.

Wakili: Ulifanikiwa kupata chochote?

Shahidi: Ndiyo, kitandani kwake Mama Leila, kati ya godoro na chaga nilikuta pakiti mbili zilizokuwa zimeandikwa 'Coffee Care Orginal' zilizokuwa na unga uzaniwao dawa za kulevya, hati moja ya kusafiria, fedha za Kitanzania, Kenya na dola za Kimarekani.

Pia, nilimpekua Munuo chumbani kwake; nilifanikiwa kupata pakiti moja kwenye kabati la nguo, nyingine ya pili chooni ndani ya sinki la kusukumia maji zenye unga uzaniwao kuwa dawa za kulevya, hati mbili za kusafiria, ikiwamo ya Kenya.
Kesi hiyo inaendelea na ushahidi wa upande wa Jamhuri leo.

Mapema mahakamani hapo, shahidi wa kwanza Mkemia Mkuu Daraja la Kwanza, Bertha Mamuya alidai kuwa alipofanyia uchunguzi pakiti mbili zilizokuwa na maandishi ya 'Coffee Care Orginal' na ile pakiti iliyotolewa chooni zilikuwa na dawa za kulevya aina ya heroin na ile pakiti moja iliyotolewa kwenye kabati la mshtakiwa Munuo ilikuwa na dawa za kulevya aina ya cocaine.

Mbali na Mama Leila na Munuo, washtakiwa wengine ni, raia wa Kenya Anthony Karanja na Ben Macharia, na Almas Said, Yahya Ibrahim, Aisha Kungwi, Rajabu Mzome na John William.

Katika kesi ya msingi, washtakiwa hao wanadaiwa kuwa mwaka 2011, wanadaiwa kuingiza nchini dawa za kulevya aina ya cocaine zenye thamani ya sh. milioni 225.

Mahakama Yamkingia Kifua Mbowe,Yatoa Amri ya Kutokamatwa Kwake,Aaagizwa Pia Amfungulie Kesi Mwanasheria Mkuu wa Serikali...!!!

$
0
0

MAHAKAMA Kuu Kanda ya Dar es Salaam, imetoa zuio la muda kwa Jeshi la Polisi kuacha kumkamata Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe hadi maombi yake ya kupinga kukamatwa aliyowasilisha mahakamani hapjana yatakaposikilizwa Ijumaa Februari 24, mwaka huu, saa saba mchana.

Aidha mahakama hiyo pia imemtaka Mbowe kurekebisha hati ya mashtaka na kumwingiza Mwanasheria Mkuu wa Serikali, katika kesi yake ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda, Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Kamishna Simon Sirro na Mkuu wa Upelelezi wa kanda hiyo, Camilius Wambura aambapo ametakiwa kuyawasilisha Jumatatu, Februari 26, mwaka huu.

Wakati kesi hiyo ikiendelea katika chemba namba 64, mahakamani hapo, Kamanda Wambura pekee kati ya walalamikiwa waliotajwa katika kesi hiyo ndiye aliyeonekana mahakamani hapo na kupotea ambapo haikufahamika mara moja alikwenda wapi.

Kesi hiyo itasikilizwa tena Machi, 8 mwaka huu. Katika kesi hiyo, Mbowe anasimamiwa na mawakili Peter Kibatala, Tundu Lissu, Albert Msando, na John Mallya.                       

Msuva Afunguka Jinsi Anavyojuta Kuichezea Yanga...!!!!

$
0
0

WINGA wa Yanga, Simon Msuva, amesema katika maisha yake ya soka hatasahau mwaka 2015 alivyozomewa na mashabiki wa klabu yake hiyo baada ya kukosa penalti dhidi ya Simba, ambapo walifunga bao 1-0 mpaka akajuta kuichezea timu hiyo lakini sasa mambo yako poa.

Msuva ambaye kwa sasa ana mabao 10 akiongoza kwenye msimamo wa wafungaji, alisema baada ya kukosa penalti hiyo mashabiki walishindwa kuvumilia wakaanza kumrushia maneno mazito huku wengine wakifikia hatua ya kumtaka aondoke.

“Maisha ya mpira wa miguu hasa unapochezea hizi timu mbili za Simba na Yanga yanataka uvumilivu sana, kwani bila hivyo unaweza ukaamua kuondoka kutokana na baadhi ya mashabiki kuwa na maneno makali.

“Nakumbuka msimu wa mwaka 2015 ilitokea penalti upande wetu nikachukua uamuzi wa kuipiga, lakini bahati mbaya sikufanikiwa kufunga nikatukanwa sana mpaka nikajua, mchezo huo ulimalizika kwa sisi kupoteza tukifungwa bao 1-0,” alisema.

Anasema tangu kukosa penalti hiyo alikosa raha kwani mashabiki walikuwa wakimzomea sana huku wengine wakiutaka uongozi kutomwongezea mkataba mpya, lakini hata hivyo alijipa moyo na yote hayo yakapita.

Kuelekea Mechi ya Watani wa Jadi...SIMBA Wamelishwa Nini?

$
0
0

SIMBA wamelishwa nini? Hilo linaweza kuwa swali sahihi kwa mashabiki, wanachama na viongozi wa timu hiyo kutokana na mzuka walionao kuelekea pambano la kukata na shoka dhidi ya watani wao wa jadi, Yanga.

Japo katika soka kuna matokeo ya aina tatu, yaani ushindi, sare na kufungwa, lakini watu wa Simba wamekuwa na uhakika wa asilimia 100 wa kuwafunga Yanga Jumamosi katika mchezo wa marudiano wa Ligi Kuu Tanzania Bara, utakaopigwa kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Japo Simba wanafahamu kuwa Yanga ndio mabingwa watetezi wa ligi hiyo ambao wameonekana kuwa ngangari, wakiwa wamepigwa tafu na ushiriki wao wa mashindano ya kimataifa, lakini kwa Wekundu wa Msimbazi hao, hayo hayawasumbui kichwa wakiamini ‘Yeboyebo’ lazima ikatike siku hiyo.

Kinachowapa jeuri Simba, si kama wamenyweshwa ‘kizizi’ au vinginevyo, bali ni kutokana na imani ya ubora wa kikosi chao kinachoundwa na wachezaji wenye uwezo wa kiwango cha juu, hasa wale wanaounda safu ya kiungo.

Lakini pia, safu ya ulinzi inayoongozwa na Method Mwanjali na ile ya ushambuliaji ‘iliyofufuka’ baada ya Laudit Mavugo na Ibrahim Ajib kuunda upacha wa aina yake, wakitarajiwa kushirikiana na fundi Mohammed Ibrahim ‘Mo’, ndivyo vinavyowapa kichwa watu wa Simba kuelekea ‘Super Saturday’, yaani Jumamosi.

Katika kukoleza hayo, Simba imeweka mikakati kabambe ikiwamo Rais wao, Evans Aveva, kukutana na viongozi na wanachama wa matawi yao yote ya Dar es Salaam kujipanga kuhakikisha Yanga hatoki siku hiyo.

Katika kikao hicho kilichofanyika Ijumaa iliyopita, pamoja na mambo mengine walijadili juu ya pambano la Jumamosi dhidi ya Yanga, lakini pia mbio za ubingwa.

Tayari Simba wameweka kambi visiwani Zanzibar, lakini kukiwa na usiri mkubwa wa nini kinaendelea huko.

Meneja wa Simba, Mussa Hassan ‘Mgosi’ ambaye kwenye kurasa zake mbalimbali za mitandao ya kijamii amekuwa akiandika ujumbe tata kama ‘Walete Walete Watufungulie Njia za Ubingwa,’ amedai kuwa mechi yao na Yanga ni kama mechi nyingine tu.

“Ni muhimu kwetu sana kwa sababu tukishinda hapa, mbio za ubingwa zinazidi kukolea lakini kila mpinzani wetu tunampa uzito mkubwa ila ushindi kwetu utatusaidia kurejea kuongoza,” alisema.

Simba wapo kileleni mwa msimamo wakiwa na pointi 51 katika michezo 22 waliokwishakucheza mpaka sasa, huku Yanga wakiwa nafasi ya pili na pointi 49 wakicheza michezo 21 ambapo timu itakayoshinda itakuwa na nafasi nzuri ya kusimama kileleni.
Viewing all 104775 articles
Browse latest View live




Latest Images