Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104775 articles
Browse latest View live

MCHUANO Mkali Waibuka Kati ya Mawakili wa Chadema na Serikali..Kisa Hichi Hapa

$
0
0

Mvutano mkali wa kisheria umeibuka baina ya mawakili wa serikali na mawakili mwenyekiti wa chama cha demokrasia na maendeleo – Chadema Freeman Mbowe katika kesi ya kikatiba iliyofunguliwa katika mahakama kuu na mwenyekiti huyo wa chadema dhidi ya mkuu wa mkoa wa dar es salaam Paul Makonda na wenzake wawili.

Mwenyekiti wa Chadema Freeman Mbowe alifungua shauri la kikatiba No 1 mwka 2017 sambamba na hilo alifungua maombi ya kuimba makahama itoe amri ya zuio la kukamatwa, kushikilia na kuhojiwa kufuatia tuhuma zilizoelekezwa kwake na mkuu wa mkoa Paul Makonda za kujihusisha na dawa za kulevya.

Washtakiwa wengine kwenye kesi hiyo ni kamanda wa polisi kanda ya dar es salaam kamishna Simon Sirro, na mkuu wa upelelezi wa mkoa wa dsm.

Awali akisoma hoja tano ambazo ziliwasilishwa na wapelekea maombi mbele ya jopo la majaji watatu wakiongozwa na jaji Sekieti Kihiyo, Pelegia Kadai na Lugano Mwandambo wakili wa serikali mkuu Gabriel Malata aliiomba mahakama kuu kutupilia mbali maombi hayo na kuyaita kuwa ni batili kutokana na kuwa mahakama hiyo haina uwezo wa kusikila kesi hiyo ambayo ameitaja kuwa ni ya kijanai wakati mahakama hiyo ina uwezo wa kusikiliza kesi za madai.

Hoja za mawakili hao wa serikali zinadai kwamba kisheria mahakama hiyo haina uwezo wa kutoa zuio kwenye vyombo vya dola kwani maofisa wa jeshi la polisi wanatekeleza majukumu yao kwa mujibu wa sheria huku kikunukuliwa kifungu cha sheria y bunge kifungu namba 7 ambacho kinatoa malmlaka kwa mkuu wa mkoa
kumkamata na kumweka kizuizini mtu yeyote inapobidi.

Mawakili wa Bwan Mbowe wakiongozwa na Tundu Lissu na Peter Kibatala wamepingana na hoja za mawakili upande wa serikali na kudai kwamba mahakama kuu ndio yenye mamlaka ya kusikiliza kesi zinazohusiana na ukiukwaji wa haki za bianadamu hivyo walikuwa sahihi kuleta maombi hayo katika mahakama hiyo.

MARCHI 2 mwaka huu mahakama kuu itatoa maamuzi ya mapingamizi ya mawakili wa serikali dhidi ya mlalamikaji .

Wakati huo huo ameonekana akiwa miongoni mwa wapenzi wa karibu walioongozana na bwana Mbowe mahakama hapo huku kukiwa na taarifa kwamba anatarajiwa kujiunga na chama hicho kama anavyoeleza afisa habari wa chadema Tumaini Makene.

MKE Wa Bilionea Msuya Aachiwa Huru Na Kukamatwa Tena

$
0
0

Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imemuachia huru mke wa marehemu bilionea Erasto Msuya, Miriam Mrita na mwenzake Revocatus Muyela wanaokabiliwa na kesi ya mauaji ya Aneth Msuya.


Hata hivyo washtakiwa hao walikamatwa tena na jeshi la polisi.


Hakimu Mkazi Mkuu, Godfrey Mwambapa leo amewaachia huru washtakiwa hao baada ya upande wa mashtaka kushindwa kutimiza amri yake iliyowataka kufanyia marekebisho ya hati ya mashtaka


Washtakiwa hao walikuwa wanakabiliwa na kesi ya mauaji ya kukusudia.


Uamuzi wa mahakama kuifuta kesi hiyo umefikiwa leo baada ya jalada la kesi hiyo lililokuwa limeitwa Mahakama Kuu kurejeshwa mahakamani hapo.
 

Februari 20, mwaka huu, Hakimu Mwambapa aliupatia upande wa mashtaka muda wa siku tatu kurekebisha hati ya mashtaka.


Lakini mpaka siku hizo tatu zinaisha hawakuwa wamefanyia bali  Wakili wa Serikali, Hellen Moshi aliiambia mahakama kuwa baada ya ofisi yao kutafakari kwa kina wameamua kuwa hawana cha kubadilisha kwa hati hiyo ya mashtaka


Wakili wa utetezi,  Peter Kibatala alidai kuwa upande wa mashtaka licha ya kupewa muda wa kutosha kufanyia marekebisho hati hiyo lakini wamekaidi amri hiyo.


Kibatala aliiomba mahakama kuwaachia washtakiwa huru kwa kuwa amri ya mwisho ya mahakama ilisema kama wasipofanya marekebisho itachukua hatua  na pia hakuna rufaa yoyote iliyokatwa na Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) kupinga uamuzi huo.


Hakimu Mwambapa amesema,kweli mahakama imeamuru upande wa mashtaka kufanyia marekebisho hati ya mashtaka pindi ilipoona inamapungufu lakini hawakufanya hivyo, akawaongezea muda hawakufanya hivyo, Ila leo wamekuja na maelezo ya kuwa hati ya mashtaka ni sahihi.


"Hati ipi ambayo ipo sahihi wakati mahakama ilisema haipo sahihi, nawaachia huru washtakiwa", amesema Mwambapa.


Awali ndugu wa marehemu waliwasilisha barua mahakamani hapo na Kwa mujibu wa barua hiyo walikuwa wanataka Hakimu huyo ajitoe kwa sababu hawana imani naye.


Hakimu Mwambapa alikuwa atoe uamuzi juu ya hoja zilizowasilishwa na upande wa utetezi pamoja na upande wa mashtaka ambapo Wakili John Malya aliomba washtakiwa hao waachiwe huru kwa sababu   hakuna hati ya mashtaka inayowashikilia washtakiwa hao mahakamani hapo.


Wakili wa Serikali Mwandamizi, Kishenyi Mutalemwa yeye aliiomba mahakama iwape muda ili waweze kutekeleza amri ya mahakama iliyotolewa Januari 9, mwaka huu


Washtakiwa Miriam na Revocutus  wanadaiwa kumuua kwa makusudi Aneth Msuya, kwa kumchinja, nyumbani kwake Kigamboni jijini Dar es Salaam.


Miriam  ambaye ni mshtakiwa wa kwanza katika kesi hiyo alikuwa mke wa aliyekuwa kaka wa Aneth, marehemu Erasto Msuya, maarufu kama bilionea Msuya.


Erasto Msuya, ambaye alikuwa mfanyabiashara bilionea wa madini ya Tanzanite, pia aliuawa kwa kupigwa risasi, Agosti, 2015 eneo la Mijohoroni,  kando ya barabara ya Arusha – Moshi wilayani Hai mkoani Kilimanjaro.


Hata hivyo washtakiwa hao walikamatwa tena na kuondoka na gari la polisi.

KUTOKA Mahakamani: Mbowe Kuendelea Kutokamatwa na Polisi Wala Kuwekwa Kizuizini

$
0
0

Mwanasheria wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA Tundu Lissu ameongea na waandishi wa habari jioni hii  baada ya kutoka Mahakamani  kwenye kesi iliyofunguliwa na Freeman Mbowe dhidi ya Mkuu wa Mkoa w Dar Paul Makonda  na Kamshna Sirro.


Lissu amesema Amri ya kuzuia Freeman Mbowe asikamatwe na wala kuwekwa kizuizini na Polisi inaendelea isipokua wanaweza kumuita kwa Mahojiano ambapo pia Mahakama itatoa maamuzi Tarehe 2, March  2017

Miujiza ya Shekh Sharifu Rashid Kutoka Bagamoyo, Anarudisha Mapenzi na Kusafisha Nyota

$
0
0

MIUJIZA YA SHEKH SHARIFU RASHID KUTOKA BAGAMOYO PWANI, (RUDISHA MAHUSIANO YAKO NDANI YA MASAA 48 TU) ASANTE KWA KUENDELEA KUMPIGIA SIMU SHEKH SHARIFU RASHID KWA WALE WENYE MATATIZO NA WALE WANAOTOA SHUKRANI:

SHEKH SHARIFU RASHIDI ni mtaalamu wa tiba mbalimbali za asili, anatumia kitabu cha quran, dawa za asili, dawa za kiarabu na majini, anazo dawa za mapenzi, nguvu za kiume, chango, ngiri maji na n.k, anakuvutia mpenzi alie kuacha au alie mbali, pia anatoa pete za bahati zilizoambatanishwa na jini mali kulingana na nyota yako, anaouwezo mkubwa wa kutumia jina la muhusika kwa kutatua tatizo lako, anaouwezo wa kumrudisha mtu aliepotea kimiujiza, pia anatibu kwa njia ya simu popote ulipo,

WASILIANA NAE KWA SIMU NA WHATSAPP NO: 0718-668347. 0685-224047, 0767-204308 au follow@shekh_sharifu_rashid, Email:shekhsharifurashid@gmail.com

Utawala Wako Binafsi Unavyoweza Kukufanya Tajiri au Maskini

$
0
0
Utawala binafsi ni vile mtu anaweza kuishi katika maagano na malengo yake kwa kuzingatia muda,mahitaji na nguvu aliyonayo katika kukamilisha jambo hilo. Kwa tafsiri yangu mtu akiweza kuishi katika hayo anakuwa ameweza kujitawala vizuri.

Katika uongozi wa nchi huu ni utawala wa tano kuwepo tangia Tanzania imepata uhuru,ukianzia kwa mwalimu Nyerere,Mwinyi,Mkapa,Kikwete na hatimaye Rais Magufuli. Katika awamu zote hizo zilizopita watu walihusisha matatizo yao ya kiuchumi na mfumo wa maisha kwa ujumla na utawala uliokuwepo!

Mfano wakati wa Mkapa kuna kipindi umaskini au ukosefu wa pesa uliitwa ukapa,kipindi cha Jakaya Kikwete vivyo hiyvo watu walihusisha umaskini na ukosefu wa pesa na utawala wa Kikwete. Muda huu tukiwa chini ya Rais wa awamu ya tano Dkt JPM, utawala wake bado unalaumiwa kwa kuwa chanzo cha watu kukosa pesa. Natabiri hata utawala wa awamu ya sita hali itakua hivyo hivyo.

Lengo langu sio kukataa kuwa kama serikali na viongozi wake hawana la kulaumiwa katika haya la hasha! Lengo langu ni kusema kumbe inaonekana pengine ndiyo hali halisi ya viongozi wetu kushindwa kukidhi mahitaji yetu tunayodhani wanaweza kututatulia. Kumbe hili ni tatizo sugu kwa Afrika na pengine lisije kuisha mpaka pumzi yako ya mwisho itakapokata! Kwahiyo utaendelea kuishi ukilaumu tawala zote zimepita kuwa ndo sababu ya wewe kutofanikiwa?

Vipi kuhusu utawala wako wewe binafsi? Ni kweli unaishi katika malengo uliojiwekea? Ni kweli matumizi ya rasimali zako unazomiliki unazitumia sawa sawa na inavyotakiwa?

Vipi muda unaotumia katika kufanikisha ndoto na malengo ulojiwekea maishani? Au unasubiri rais na utawala wa awamu ya sita ndo uje kua suluhisho la matatizo yako?

Katika kipindi ambacho wewe unalalamikia utawala kuna wenzio wanaingiza pesa,katika awamu ulizoishi za uongozi kuna wengine wamepata utajiri na huku wakiishi katika tawala hizo hizo unazolalamikia wewe kuwa hazisaidii wananchi kufanikiwa kuishi maisha yaliyo bora.

Amini utawala wako. Ni kichwa chako ukiweza kuishi katika mipango,nidhamu,ubunifu na kufanya kazi kwa bidii hata ikulu kukiwa kuna jiwe utatusua. Wakati tukiendelea kupigania misingi iliyo imara na yenye kumwezesha mwananchi kufanya shughuli zake katika ustawi mzuri kwa maana ya kuhakikisha utawala wa nchi unawanufaisha wananchi lazima uhakikishe utawala wako mwenyewe unafanya kazi kwa kadri na kiwango kinachotakikana.

Na Eliezer Gibson ‘greencitynative

SIRI IMEVUJA! Maongezi ya Mama Wema na Steve Nyerere Kuhusu Vigisu Walizozifanya Bungeni ili Wabunge Wamtete Wema Sepetu

$
0
0
Maongezi ya Mchekeshaji Steve Nyerere na Mama Sepetu yamevuja wakijadili issue ya Wema Sepetu Kuwekwa ndani kuhusu Madawa ya Kulevya Pamoja na Mikakati yao kumtumia Wema ili wapige pesa kutoka Chadema na CCM....

Bonyeza Play Kusikiliza:

FULL VIDEO: Wema Sepetu Pembeni ya Freeman Mbowe Mahakamani

$
0
0
Mwigizaji Wema Sepetu ameungana na viongozi wa Chama cha Demokrasia na maendeleo CHADEMA Mahakama kuu Dar es salaam Tanzania ambapo muda mfupi baada ya kuonekana pamoja, Msemaji wa CHADEMA amethibitisha kuwa wanatarajia kumtangaza kama Mwanachama mpya…

 TAZAMA KWENYE HII VIDEO HAPA CHINI:

KRC Genk Inayochezewa na Mbwana Samatta Inaungana na Man United 16 Bora ya Europa League

$
0
0
Usiku wa February 23 2017 mtanzania Mbwana Samatta akiwa na timu yake ya KRC Genk ya Ubelgiji aliingia kwenye headlines baada ya kufanikiwa kufuzu kucheza hatua ya 16 bora ya Europa League kwa kuitoa FC Astra ya Romania.

Samatta akiwa na KRC Genk waliikaribisha FC Astra ya Romania katika mchezo wao wa pili wa marudiano wa Europa League, katika uwanja wa Luminus Arena ikiwa ni wiki moja imepita toka watoke sare ya 2-2 ugenini.

Katika game hiyo ya marudiano iliyochezwa na KRC Genk kupata ushindi wa goli 1-0 lililofungwa na Pozuelo kwa faulo dakika ya 67, wameiondoa FC Astra kwa jumla ya goli 3-2, hivyo Genk wanaungana na timu nyingine 15 kucheza hatua 16 bora ya Europa League ikiwemo Man United.

HABARI Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya February 24

$
0
0

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya February 24

Bill Nas Aijibu Kauli ya Dayna Nyange Kuwa Mastaa wa Kibongo Hawajui Kutongoza

$
0
0
Bill Nas ameijibu kauli ya Dayna Nyange kuwa mastaa wa Kibongo hawajui kutongoza.

Dayna aliiambia Bongo5 kuwa hiyo ndio sababu moja wapo ya kwanini hana uhusiano na staa mwenzake. Lakini Bill ambaye ameshirikishwa kwenye wimbo wa Dayna, Komela, ameipinga vikali kauli hiyo.

“Hapaswi kujumuisha wasanii wote wa Bongo Flava, kama kuna washkaji wawili watatu wamewahi kumtongoza au watano, bado umma wa Bongo Flava ni mkubwa sana,” Bill Nas alikiambia kipindi cha Amplifaya cha Clouds FM, Jumatano hii.

“Kama kuna watu wawili watatu, aseme hao hao asijumuishe watu wengine,” ameongeza rapper huyo na kudai kuwa kwakuwa yeye hajawahi kutoka na msichana wa Bongo Flava, hawezi kuhitimisha kuwa hakuna msichana anayemvutia.

Awali kwenye interview ya Bongo5, Dayna alisema, “”Sijawahi kudate na staa na si kwamba wakaka wazuri hawapo, na sio kwamba hawanitokei, labda hawajui kutongoza vizuri. Kwa sababu sijawahi kushawishika kutembea na staa na sipendi kutembea na staa, so wakati mwingine unaweza ukawa haupendi kitu lakini ukashawishika kuingia lakini mimi bado hajatokea.”

VIDEO MPYA ya Mdogo wake Vanessa Mdee ‘Mimi Mars’ inaitwa ‘shuga’

$
0
0
Marianne Mdee, kwenye BIO yake katuandikia ana uwezo wa kuimba, kuandika nyimbo na kufanya utangazaji ambapo leo ndio siku rasmi ameamua kutuonyesha upande mwingine wa kipaji chake ambacho ni mziki, ukishamaliza kuitazama video yenyewe usisahau kuachia comment yako…

MREMBO Jack Wolper Amtema Rasmi Mwanamuziki Harmonize

$
0
0
DAR ES SALAAM: Msanii wa sinema za Bongo, Jacqueline  Wolper amefunguka kuhusu kuachana rasmi na mpenzi wake ambaye ni msanii wa muziki kutoka Kundi la Wasafi Classic Baby ‘WCB’, Rajabu Ibrahim ‘Harmonize’.

Akizungumza na mwandishi wetu jana, Wolper alikiri kwamba, yeye na Harmonize, mapenzi yao yamekwisha kabisa.

“Yah! Ni kweli, nimeamua tu kuachana naye. Unajua katika uhusiano kuna kugombana, tumekoseana na kusameheana mara nyingi, sasa tumeamua kila mtu aendelee na maisha yake. Kwangu ni fursa nzuri kwani nitakuwa na amani ya moyo. Maisha yatasonga na nitajikipu ‘bize’ na kazi zangu. “Siwezi kujutia uamuzi huu na moyo wangu umeshazoea, kanikuta nikiwa Wolper na tumeachana nikiwa Wolper labda kama angekuwa amenikuta Fatuma na kunifanya kuwa Wolper.

“Harmonize nimedumu naye kwenye mapenzi kwa mwaka mmoja tu. Nilimkosea, akanikosea kanikosea tena, siwezi kuongelea kitu halisi alichonikosea lakini jua hilo.

“Wakati tukiwa kwenye uhusiano wetu hatujawahi kuchiti (kusaliti) au inawezekana tulichiti na tukasameheana ila kwangu ni rahisi kusamehe kwa kuchiti kuliko kukusamehe kwenye kosa dogo ambalo wewe unaliona ni la kawaida lakini kwangu nikahisi kama unanishusha thamani, na ninapoingia kwenye uhusiano huwa nasema vitu ambavyo sivipendi kukosewa, na nikiona unakosea mara kwa mara najua hiyo ndiyo tabia yako,” alisema Wolper na kuongeza:

“Hata sikumbuki mara ya mwisho niliongea naye lini ila neno lake la mwisho kwangu lilikuwa ni samahani ambalo sijalikubali.” Juhudi za kumpata Harmonize zinaendelea baada ya jana kutokupatikana hewani.

WAZIRI Mahiga Abainisha Kisa cha Watanzania Kutimuliwa Msumbiji

$
0
0
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Philip Mahiga amesema kuwa Watanzania waliokuwa nchini Msumbiji wamefukuzwa kutokana na kukiuka taratibu na sheria za kuishi nchini humo.

Mahiga amesema kuwa Watanzania hao wamefukuzwa Msumbiji baada ya kubainika kuwa wanaishi nchini humo bila kuwa na pasipoti za kusafiria, vibali vya kuishi na kutofuata vigezo walivyokuwa wamepewa na mamlaka husika ya nchi hiyo.

Hayo ameyasema wakati alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari kuhusu ugeni unaotarajiwa kuwepo nchini Tanzania wa Rais wa Uganda, Yoweri Museveni anayetarajiwa kufanya ziara ya siku mbili ya Kitaifa nchini Februari 25 na 26, 2017.

Rais wa Visiwa va Shelisheli, Mhe. Dannu Faure naye atawasili Tanzania kwa ziara ya siku mbili kuanzia Tarehe 27-28, februari mwaka huu.

FEZA Kessy 'Napenda Mwanaume Ambaye Havai Skini Jinzi na Ambaye Sio Chips Mayai'

$
0
0
HII ikufi kie wewe mpenda burudani na ubuyu wa town! Msanii wa Bongo Fleva, Feza Kessy amepigwa kibuti siku kumi kabla ya kufi kia Sikukuu ya Wapendanao ‘Valentine’s Day’.

Akizungumza na E’bana Dah hivi karibuni ndani ya Ukumbi wa Club Next Door uliopo Masaki jijini Dar, Feza ambaye pia alikuwa mshiriki wa Shindano la Big Brother Africa 2013 ‘The Chase’ alisema, kwa sasa ameamua kupumzika kidogo mpaka moyo utulie.

“Tangu niachwe kabla ya valentine nipo singo sasa hivi kimyakimya na bado nina maumivu labda hapo baadaye,” alisema Feza. Alipobanwa ni mwanaume wa aina gani anampenda alisema:
“Napenda mwanaume ambaye havai skini jinzi, nataka mwanaume apige timba (viatu aina ya mabuti) na tisheti. Siyo mwanaume anakula chipsi mayai. Sitaki awe milionea, pesa kidogo ya kutumia inatosha, kikubwa aniheshimu na asiwe mshamba wa mademu wa kutaka achepuke wakati yupo na mimi.”

BREAKING News: Tetemeko la Ardhi Lenye Ukubwa wa 5.7 Latikisa Zambia na Tanzania

$
0
0
Tetemeko la ardhi ya ukubwa wa 5.7 kwenye vipimo vya Richter limekumba maeneo ya Ziwa Tanganyika mapema Ijumaa.

Tetemeko hilo lilitikisa maeneo ya kaskazini mwa Zambia na mitetemeko hiyo ikasikika maeneo ya kusini magharibi mwa Tanzania.

Kitovu cha tetemeko hilo, kwa mujibu wa Shirika la Utafiti wa Jiolojia la Marekani, kilikuwa kilomita 10 chini ya ardhi umbali wa kilomita 45 kutoka mji wa Kaputa nchini Zambia.

Mji huo unapatikana katika mpaka wa nchi hiyo na Tanzania na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.

Tetemeko hilo lilitokea mwendo wa saa tisa na dakika thelathini na mbili usiku (0032 GMT).

Tetemeko la ardhi la ukubwa kama huo huchukuliwa kuwa la kadiri lakini wataalamu wanasema kutokana na hali kwamba kitovu chake chakikuwa chini sana ndani ya ardhi, huenda hilo lilisababisha mitikisiko kuwa mikubwa.

Desemba mwaka 2005, tetemeko kubwa la ardhi lilitokea eneo la Ziwa Tanganyika.

Tetemeko hilo la nguvu ya 6.8 lilitikisa majumba katika miji maeneo ya Afrika mashariki na kati.

Sehemu kubwa ya maeneo ya Afrika Mashariki huwa katika Bonde la Ufa, bonde kubwa lililoundwa kutokana na kuhama kwa maeneo makubwa ya ardhi na milipuko ya volkano.

Hilo huyafanya kuwa hatarini ya kukumbwa na mitetemeko ya ardhi.

Septemba mwaka 2016, tetemeko jingine la ardhi lililotokea eneo la Bukoba, mkoani Kagera kaskazini mwa Tanzania.

Watu 16 walifariki na wengine 250 kujeruhiwa kutokana na tetemeko hilo. Mamia wengine walibaki bila makao.

Tetemeko hilo la ukubwa wa 5.7 kwenye vipimo vya Richter, lilitajwa kuwa mbaya zaidi kuwahi kukumba taifa hilo la Afrika Mashariki katika kipindi cha zaidi ya mwongo mmoja.

HELA Wanazotuhumiwa Kupewa Kina TID Zilitolewa na Nani na Kutoka Fungu Gani?

$
0
0

Clip iliyosambaa toka jana katika mitandaoni ya kijamii akisikika Mama Wema Sepetu na Steve Nyerere imezua Maswali mengi ikiwemo haya hapa chini:


1.Hiyo milioni mbili inayotajwa kuwa TID kapewa imetolewa na nani?

2.Kama kweli baadhi ya walionekana kwenye vyombo vya habari watakuwa wamepewa hela, itakuwa wamepewa jumla ya shilingi ngapi?

3.Inawezekana mtu akatoa hela hizo zote kutoka mfukuoni mwake?

4.Kama kuna kikundi au taasisi ndio imehusika kutoa hizo fedha,watatoa tu hela zao hivi hivi bila kuwa na maslahi?

5.Kama kuna maslahi,yatakuwa ni maslahi gani?

6.Kwasababu zoezi hili lilikuwa likiratibiwa na serikali,inawezekana kuna mkono wa serikali?

7.Kama kuna mkono wa serikali,ni afisa gani kahusika na amezitoa katika fungu gani?

8.Kama hizi "clip" ni fake,kuna yoyote miongoni mwa wanaotajwa amejitokeza kukana yanayosemwa?

9.Mama Sepetu na Steve Nyerere kuna yoyote kati yao amejitokeza kuzikana hizo clip mpaka sasa?

10.Kama hizi clip ni za kweli, Mama Sepetu na Steve Nyerere hawatashili kuhojiwa na vyombo husika?

11.Swala hili likipita pasipo wahusika kuhojiwa au likaishi tu kimya kimya,itakuwa ni hivi hivi tu?

12.Wote wanaotajwa kama kweli wanasingiziwa, ina maana wote mpaka muda huu wameshindwa kutumia hata mitandao ya kijamii kukanusha /kutolea ufafanuzi?

Kama kina TID walipewa/hawakupewa hizo hela basi tunaomba kina TID na hao wenzake wajitokeze hadharani wakanushe au wakiri kupewa hizo fedha lakini wakikiri watuambie walipewa na nani.

Mwisho kama ni taasisi ya serikali ikihusika bila shaka taratibu zilifuata hivyo tutaomba kuona document za malipo hayo.

Ukiona giza linazidi,ujue ndio kunakaribia kukucha.

By Salary Slip

RICH Mavoko Atoa Povu Kwa Wanaosema Amekosea Kujiunga na Lebo ya Diamond WCB

$
0
0
Muimbaji wa Kokoro, Rich Mavoko amedai kuwa kama bado kuna watu wanaona uamuzi wake wa kusainishwa na label ya Diamond, WCB ni kujishusha sababu yeye ni msanii mkubwa, hawaijui biashara yake.

“Mimi nakutana vitu vingi, mtu mwingine nyuma ya pazia haoni,” muimbaji huyo alikiambia kipindi cha Ngaz Kwa Ngaz cha Salama Jabir.
“Tunashoot, tunatoa video, tunarelease ngoma inahit, mimi ndo nakuwa napata tabu.Mtu anayesema nimejishusha kimuziki kujiunga WCB anakuwa hajui biashara yangu,” aliongeza.

Rich alisainishwa na WCB mwaka jana na kuachia wimbo wake wa kwanza, Ibaki Story.

Kwa upande mwingine, Rich alidai kuwa asipofanya muziki atakuwa akiwaandikia watu wengine mashairi na kwamba Tanzania ina upungufu mkubwa wa waandishi wa Bongo Flava.

MZEE wa Upako Amuonya Nay wa Mitego Baada ya Kudai Anakuja na Kanisa lake

$
0
0
Baada ya hivi karibuni msanii wa hip hop, Nay wa Mitego kutangaza kuwa atafungua kanisa lake ambalo litakuwa si la biashara bali ni la kumuabudu Mungu aliye hai, Mchungaji maarufu nchini, , Lusekelo Anthony aka Mzee wa Upako amemuonya kutomchezea Mungu.

Mzee wa upako ameyasema hayo alipotafutwa na E-News ya EATV baada ya kuulizwa maswali juu ya kauli hiyo.

“Kama unakuja kanisani kwa maana kuna biashara, nakupa miaka hii mitatu sio utatembelea ndala utatembelea kucha, ni mtoto mdogo sana hana akili. Mungu hataniwi, anafanya kufuru, kama ana mama yake amemzaa amuonye. Mimi biblia nimesoma na hizo lugha zake nyepesi zitamtokea puani, asithubutu kufanya kanisa kama biashara. Baada ya miaka hii mitatu atajua kwamba kuongoza watu sio kama kuongoza ngo’mbe hakuna jambo gumu kama kuongoza watu wenye akili kama wewe wenye ufahamu kama wewe, wapo watu wengi walianzisha makanisa kwanini walifunga, ujinga hujui ni ujinga ni utoto,” Alisema Mzee wa Upako.

Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) Chaipinga TCU, Chasema Hakijawahi Dahili Wanafunzi Vilaza

$
0
0
Siku moja baada ya Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU) kutangaza utata wa udahili wa wanafunzi wa vyuo vikuu, wadau wakubwa wa elimu, wamejitokeza kupinga hatua hiyo. Wadau hao ni pamoja na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) .

UDSM kimeeleza kwamba hakuna mwanafunzi hata mmoja aliyedahiliwa chuoni hapo, ambaye hana sifa za kujiunga na chuo hicho.

Naibu Makamu Mkuu wa Chuo hicho, Profesa Florens Luoga alisema jana kuwa chuo hicho kimeweka utaratibu ambao unaweza mwanafunzi yeyote anayedahiliwa chuoni hapo, awe na sifa zinazohitajika kwa kuwa hawafanyi biashara.

“Sisi hapa ni wakali kuhusu jambo hilo, tukibaini kuwepo kwa mwanafunzi ambaye hana sifa tunamfukuza. Hatusubiri TCU iseme...hata tukibaini kuwa mtu alifanya udanganyifu na alishamaliza chuo, lakini hakuwa na sifa, tunamnyang’anya digrii tuliyompa,” alisema Profesa Luoga na kuongeza:

“Hiki ni chuo, hatufanyi biashara, sisi kazi yetu hapa ni kuandaa wataalamu na ndio maana tunakuwa wakali na makini kuhakikisha wanafunzi tunaowachukua, wote wanakuwa na sifa stahiki”, alisema

 Profesa Luoga alisema uhakiki ambao umefanywa na TCU na kutoa idadi ya wanafunzi 224 wanaosoma chuoni hapo, kuhakikisha wanawasilisha ushahidi wa nyaraka zao, wanaufanyia kazi, kwani kuna uwezekano tume hiyo haina taarifa kuhusu programu zinazoendeshwa na chuo hicho.

Alifafanua kuwa kuna baadhi ya programu maalumu, ambazo Serikali ya Tanzania imeingia na nchi nyingine kwa ajili ya kuendesha programu maalum.

Alisema kozi hizo zimekuwepo chuoni hapo kwa muda wa miaka 40 sasa na zinafanywa kutokana na makubalino ya Serikali ya Tanzania na nchi husika.

Alisema chuo hicho kikongwe Tanzania, kutokana na kuwepo makubaliano hayo kimekuwa kinapokea baadhi ya wanafunzi ambao wanatoka nje ya nchi na akasisitiza kuwa yawezekana ndio hao ambao TCU imeshindwa kupata nyaraka zao.

“Yawezekana kuna taarifa ambazo hazijakaa sawa, tumepokea taarifa ya TCU sisi kama chuo ni jukumu letu kuitekeleza,” alieleza Profesa Luoga.

Diamond Platnumz Aingia Top 20 ya New Artists Marekani Kupitia Wimbo wa Marry you

$
0
0
Nyota wa Africa diamond platnumz ameweka record mpya kwenye mziki wake baada ya kuingia 20 ya wasanii wapya nchini marekani kwa video take ya marry you kupitia mtandao wa Vevo
Video ya marry you imeendelea kufanya vizuri kupitia a/c hiyo mpya ya Diamond ikiwa na views milioni 3.7 ndani ya wiki 3.
Viewing all 104775 articles
Browse latest View live




Latest Images