Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104428 articles
Browse latest View live

STEVE Nyerere Kakerwa na Kitendo cha Kurekodiwa na Mama yake Wema Sepetu..Kasema Wema Sepetu Hadai Chochote CCM

0
0
Baada ya sauti zilizosambaa zikimuhusisha Mwigizaji Steve Nyerere na Mama wa mwigizaji Wema Sepetu wakizungumza huku akitaja baadhi ya viongozi mbalimbali aliodili nao kwenye sakata la Wema kushikwa na Polisi, leo Steve Nyerere ameita Waandishi wa habari na kuongea nao.

Steve Nyerere amesema kuwa hakuna msanii hata mmoja ambaye anakidai Chama Cha Mapinduzi (CCM) na kusema mambo ambayo anasema Weme Sepetu kuwa anakidai chama hicho ni uongo na uzushi mtupu.

Amesema katika wasanii mbalimbali ambao huenda walilipwa pesa nyingi zaidi ni Wema Sepetu pamoja na yeye na kusema wao pamoja na wasanii waliokuwa wanaendesha kampeni ya 'Mama ongea na mwanao' ni wasanii ambao walilipwa vizuri sana na Chama Cha Mapinduzi kuliko wasanii wengine wowote wale.

Steve Nyerere anasema katika mkataba walioingia na Chama Cha Mapinduzi hakuna sehemu mkataba huo unasema ukikamatwa na madawa ya kulevya, bangi  chama hicho kitakuja kukusaidia.

Pia Steve Nyerere anakiri wazi kuwa sauti ambayo inazunguka kwenye mitandao ya kijamii ni kweli ni sauti yake na alikuwa akiongea vile ili kumridhisha mama yake na Wema Sepetu kwani wakati huo jambo hilo lilikuwa ngumu kwake.

==> Fuatilia maongezi yake ya moja kwa moja hapo chini

1.Nimewaiteni hapa kama msanii wa tasnia ya filamu pia kama kada wa chama cha mapinduzi

2.Kulikuwa na maongezi ya simu kati ya mimi na mama Sepetu, mimi ndio nilikuwa naogea na mama Sepetu yasipindishwe

3.Nilichofanya ni kutumia sanaa yangu na ujuzi kumtoa mama kwenye hali ambayo anasema anataka kujitoa hata kwenye chama"

4.Mama alikuwa anaamini naweza kumtoa Wema, nilikuwa natumia ujuzi wa akili yangu kumlidhisha mama, kumbe yeye ananirekodi

5.Kwenye kampeni tulilipwa hakuna aliyefanya kazi bila kulipwa, kundi la mama ongea na mwanao mimi ndio nilikuwa mwenyekiti

6.Maneno niliyoyasema ktk simu na Mama Wema na kutaja viongozi ni UONGO, ilibidi nifanye hivyo maana sikuwa na jinsi...

7.Uwezo wa kuwaambia Wabunge au kuwaelekeza cha kufanya sina, sina ujanja huo.... namuomba radhi Spika Job Ndugai"

8.Mimi na Wema ndio tuliwafuata CCM kwamba tuna wazo la mama ongea na mwanao, na tukalipwa

9.Namuomba radhi Rais Magufuli na Chama changu cha CCM, yanaongelewa mengi ninayasikia, naomba radhi familia pia, niliteleza

10.Nia yangu haikua mbaya, wakati naongea na Mama niliamini ni mama mzazi... ile audio ina siku 5, kwanini iachiwe juzi?

11.fikifria ile audio ina siku tano, inakuja kutolewa juzi na watu wamehama tayari chama, nafikiri walifanya hivyo kunichafua

12.Ile audio imekuja kuachiwa juzi wakati watu wanahama chama, kwanini nirekodiwe? naamini wamefanya hivyo makusudi

13.Nimetaja viongozi ktk ile audio alafu unakuja kuisambaza nimetaja viongozi wa Nchi, Mama alichofanya kuisambaza ni mauaji

14.Si kweli nilishinkiza wabunge wamjadili Wema, mtoto anapotaka kuchomwa Sindano kuna vitu anaambiwa, ndio hivyo nilivifanya

15.Watanzania wenzangu usimuamini binadamu yeyote, Mama Wema alitaka kuniharibia maisha yangu, Mama kanikosea.. namuachia Mungu

16.Mimi na Makonda hatujawahi kwenda alikokutaja Mama, ilibidi niitikie kama zoba, Waandishi naomba mkaseme NAOMBA RADHIII

17.Sina ugomvi na Makonda na ninamuomba msamaha na hakuna ukweli kwamba siongei nae.... Paul ni kaka yangu, tunawasiliana

18.Naliomba radhi bunge tukufu na Spika Ndugai kwa kauli ya kusema nimeshinikiza bunge, nilifanya hivyo kutaka asitoke ndani ya CCM

19.Uwezo wa kuwashinikiza wabunge sina na wala mamlaka hiyo sina

20.Hii kesi kila mtu alirudi nyuma.. ni maulizo tu inaendeleaje? tunamuombea kwa Mungu tu, CCM ni kama bahari wametoka wangapi?

21.Mimi kama mtu wa karibu na familia nilitakiwa nitoe maneno matamu na ndio hayo

22.Kwenye project ya kampeni ya uchaguzi mkuu 2015 MAMA ONGEA NA MWANAO hatuidai CCM hata senti tano

23.Alichofanya mama kunirekodi huo ni uuaji, kuna watu wananitegema nyuma ya Steve alitaka anigombanishe na marafiki

RC Makonda Agoma Kuzungumzia Kughushi vyeti

0
0
Licha ya kuandamwa na tuhuma za kughushi vyeti, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda amesema hawezi kuzungumzia suala hilo kwani majibu yake yapo mtandaoni sakata lilipoanzia.

Makonda amesema hayo leo (Ijumaa) alipoulizwa swali na wanahabari kuhusu uhakika wa taarifa zinazosambaa mitandaoni kuwa alinunua vyeti na kutumia jina lisilo lake.

"Maswali ya mitandaoni yanaishia mitandaoni siko hapa kupoteza focus (mwelekeo). Ukiona maneno mengi yanaibuka kwenye ishu ya dawa za kulevya ndiyo ujue vita imefika penyewe," amesema Makonda.

 Chanzo: Mwananchi

Kauli ya TFF Kuhusu Watu Wanaotaka kuchoma Kadi za Chama Flani cha siasa Uwanja wa Taifa Leo

0
0
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania limeonya vikali na kupiga marufuku watu kuingiza siasa katika mchezo wa leo kati ya Simba na Yanga

Akiongea leo na waandishi wa habari,Afisa Habari wa TFF, Alfred Lucas amesema kuwa wamepata taarifa kuna watu fulani leo wanataka kuchana kadi za chama fulani, wengine wanataka kuchoma bendera za chama fulani kupitia mchezo wa leo kati ya Simba na Yanga, hivyo wameonya vikali watu wasijaribu kuingiza siasa zao kwenye michezo na kusema kwa yoyote atakayejaribu yatakayompata asije kuwalaumu TFF

"Kuna watu tumesikia na kuthibitishiwa kwamba kuna watu leo wanataka kuchana kadi za chama fulani cha siasa uwanja wa Taifa mbele ya mashabiki wa Simba na Yanga.

"Kuna wengine wamepanga kuzichoma moto, wako wale wengine wamepanga kuchoma hata bendera za chama hicho, wengine wanasema watafanya ndani ya uwanja wengine nje ya uwanja.

"Nitumie nafasi hii kuwaambia kwamba taarifa tunazo na tunatoa onyo kali kwa yoyote atakaye thubuti kufanya hayo wanayotaka kufanya kwani litakalo mtokea lisijekuwa lawama kwa TFF" alisema Alfred Lucas.

IKULU Yakanusha taarifa FEKI Inayosambazwa Mitandaoni kuhusu Rais Magufuli

0
0
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu, Gerson Msigwa ametahadharisha umma kuhusu habari hii bandia inayosambazwa kwenye mitandao ya kijamii.

Msigwa ameandika kupitia ukurasa wake wa Twitter kuwa taarifa hiyo si ya Ikulu na kuwa imetengenezwa na wahalifu wa mitandao hivyo kwa kuwataka wananchi kuipuuza.

Hii ndo Taarifa ya uongo inayosambazwa

MUME Amuua Mke Wake, Ajinyonga na Kuacha Ujumbe Mzito

0
0


Dar/Sumbawanga. Mfanyabiashara Mohammed Mohammed (46), mkazi wa Boko Chama jijini Dar es Salaam amemuua mkewe Sophia (36) kisha kujiua akiacha ujumbe wenye kurasa 80 uliobeba sababu za kufanya tukio hilo.

Katika ujumbe huo ambao upo katika nakala sita ambazo alielekeza watu wanaopaswa kukabidhiwa, aliomba mtu yeyote asihusishwe na mauaji hayo.

Ametaka nakala hizo zipelekwe Polisi, kwa mwanaye wa kiume anayeishi Masasi, mjomba wake, baba mwenye nyumba, baba mkwe na nyingine kwa majirani.

Katika ujumbe uliomo kwenye waraka huo, Mohamed alieleza kwamba uamuzi huo ulikuwa katika nafsi yake akisema umetokana na mgogoro wa kimapenzi muda mrefu kati yake na mkewe.

Imedaiwa kwamba katika tukio hilo, Mohammed alimpiga mkewe kwa nyundo kichwani, kumchoma kisu ubavuni na kumchinja kwa kutumia kisu kilichoonekana kuwa kipya.

Akizungumzia tukio hilo jana, Mjumbe wa Shina Namba 2 Mtaa wa Boko Chama Msikitini, Abdallah Kassim alisema marehemu alionekana kupanga kutekeleza tukio hilo kwa muda mrefu kutokana na baadhi ya vitu walivyoona akidokeza kuwa inawezekana maandalizi yake yalifanyika kwa zaidi ya mwezi mzima.

“Tumekuta chumbani kwake barua yenye kurasa nyingi. Ina michoro ya kisu, nyundo na maandishi yameandikwa na kuchorwa kwa kutumia kompyuta jambo ambalo haliwezi kufanyika hata ndani ya wiki moja,” alisema Kassim.

Alisema hata vifaa alivyotumia katika kutekeleza tukio hilo vinaonekana kuwa vipya na vilikuwa vimeandaliwa maalumu kwa kazi hiyo. Shuhuda huyo alisema katika barua hiyo, mume huyo aliandika kuwa mwanamke huyo amekuwa akidai kuwa watoto waliozaa naye siyo wa kwake, huku akimtuhumu kutumia dawa za kishirikina kumfanya kuwa kama mpumbavu na kuchukua fedha zake (mume) na kwenda kujenga kijijini kwao.

Kassim alisema mwishoni mwa ujumbe huo, marehemu Mohammed amewausia wanawake kuwa makini katika maisha yao ya ndoa na wasipende kuwa na marafiki wanafiki.

Mwenye nyumba waliyokuwa wakiishi marehemu hao, Mwinyi Ramadhani alisema Mohammed alikuwa mtulivu asiyependa makundi na hata siku moja hawajawahi kusikia akigombana na mkewe na kwamba tukio hilo limewashangaza.

“Mohammed ameishi katika nyumba yangu zaidi ya miaka mitatu. Hata siku moja sijawahi kusikia akigombana na mkewe wala kupokea kesi yoyote kutoka kwake au wapangaji wenzake wakimshtaki. Mambo yake alikuwa akimaliza mwenyewe,” alisema Ramadhani.

Hata hivyo, alisema marehemu Mohammed ambaye ameacha watoto wawili, mmoja wa kike na mwingine wa kiume ambao wamechukuliwa na ndugu, alikuwa mtu wa kulalamika kuwa wanawake ni watu wenye matatizo lakini hakuwa mtu wa kuhitaji msaada wa mawazo kwa wengine.

Mpangaji mwenzake, Helen Zacharia alisema walikuwa wakiishi vizuri na marehemu Sophia na mumewe na hakuwahi kuwasikia wakilalamika juu ya kutokuelewana.

“Kwa jinsi walivyokuwa wakiishi, hatukuwahi kuwaza kama kitu kama hiki kitaweza kutokea kwani hatukuwahi kusikia hata siku moja wakigombana,” alisema.

Michael Robert ambaye alijitambulisha kuwa ni mdogo wa marehemu Mohammed, alisema kuwa wameelezwa na polisi kuwa uchunguzi wa suala hilo haujakamilika na kwamba leo watapata kauli ya jeshi hilo kauli ambayo ilithibitishwa na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kipolisi Kinondoni, Suzan Kaganda ambaye alisema upelelezi unaendelea ili kujiridhisha kama ni kweli marehemu Mohamed ndiye aliyetekeleza tukio hilo.

Watatu wa familia moja wauawa

Wakati mauaji hayo yakitokea Dar es Salaam, watu watatu wa familia moja, wakazi wa Kijiji cha Kipa, Sumbawanga wameuawa kwa kukatwa mapanga na watu wasiojulikana kwa tuhuma za ushirikina.

Tukio hilo lilitokea Jumatano iliyopita saa 2:45 usiku katika Kijiji cha Mfinga na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Rukwa, George Kyando aliwataja waliouawa kuwa ni Joachim Kayanda (60), Everina Mwanakatwe (47) na Emmanuel Kayanda (27) ambao imeelezwa kwamba walikwenda Mfinga kwa shughuli za kilimo.

Kamanda Kyando alisema wanafamilia hao waliuawa walipokuwa wakijiandaa kulala ambako kundi la watu lilivunja mlango na kuwavamia likiwatuhumu kuwa ni wachawi.

Alisema watu watano wanahojiwa kutokana na mauaji hayo na alitoa rai kwa wananchi kuachana na imani potofu za kishirikina ambazo zimekuwa zikisababisha mauaji ya kujichulia sheria mkononi mara kwa mara.

MARTIN Kadinda afunguka Kinachomponza Wema Sepetu

0
0


MWANAMITINDO Martin Kadinda, amefunguka kuwa kinachomponza Wema hadi ajikute anaingia kwenye misala mbalimbali ya kipolisi ni watu wanaomzunguka.

Kadinda ambaye pia ni meneja wa msanii huyo, alisema ili Wema aweze kufanikiwa maishani, hana budi kuwaweka pembeni baadhi ya marafi ki ambao wana tabia chafu kwani mara nyingi wamekuwa wakimsababishia matatizo mbele ya jamii.

“Siwezi kuwataja majini lakini Wema mwenyewe naamini anawajua marafi ki zake ambao si wazuri, wanaomwingiza kwenye majanga mara kwa mara, ni vyema akaachana nao ili ‘kumaintain’ heshima ya jina lake,” alisema Kadinda

BODA BODA Dar es Salaam Mwisho Saa 6 Usiku

0
0



Jeshi ya Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam limetoa wito kwa madereva bodaboda katika Jijini la Dar es salaam, kuacha kufanya shughuli hiyo ifikapo majira ya saa 6 usiku ili kupunguza uhalifu.


Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam Kamishna Simon Sirro, amesema kuwa jeshi hilo limebaini wahalifu wengi hutumia mwanya katika muda huo kutenda uhalifu ikiwa ni pamoja na kuwadhuru waendesha pikipiki.


Aidha, Kamanda Sirro, amesema, kuanzia Februari 18 hadi 23 Jeshi la Polisi Usalama Barabarani limefanikiwa kukusanya kiasi cha shilingi milioni 460 kutokana na makosa mbalimbali ya barabarani pamoja na kukamata pikipiki 1,280 kati ya hizo pikipiki 30 zimekamatwa kutokana na kupita katika njia ya mabasi yaendayo haraka huku madereva 27 wakifikishwa mahakamani.


Kuhusu suala la dawa za kulevya, Sirro aliwaambia waandishi wa habari jana kuwa mpaka sasa limefanikiwa kukamata jumla watuhumiwa 257 pamoja na kete za dawa za kulevya 1,526, puli 112 na misokoto ya bangi 247 kutokana na oparesheni inayoendelea.


Alisema baadhi ya watuhumiwa bado awajafikishwa mahakamani kwani upelelezi bado haujakamilika na mara baada ya upelelezi kukamilika watafikishwa mahakamani kujibu tuhuma zinazowakabili

NAPE: Hata Kwa Goli la Mkono Lazima Tuibuke Washindi Gabon

0
0

WAZIRI wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nnauye amesema hata kwa goili la mkono ni lazima Serengeti Boys warejee nyumbani wakiwa ama na kombe  au wakiwa wamefuzu  kushiriki kombe la dunia kwa kuwa moja ya timu mbili zinazohitajika.


Kauli ya Waziri Nape ameitoa leo asubuhi wakati akifungua mashindano ya Kombe la Standard Chartered 2017 safari kuelekea Anfield ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 100 tangu benki hiyo kuanzishwa mwaka 1917 yaliyoanza kutimua vumbi katika viwanja vya JK Park Kidongo Chekundu, Gerezani.


Alisema haiwezekani taifa hili kuwa na Waziri mjanja kama Nape halafu Serengeti Boys inakosa kombe huko Gabon na nafasi ya ushiriki Kombe la dunia.


Pamoja na kauli yake hiyo Waziri Nape aliiomba Benki ya Standard Chartered kushiriki katika jukumu la kuhakikisha kwamba Serengeti Boys  ama inarejea na kombe au inafuzu miongoni mwa timu mbili zitakashiriki Kombe la Dunia.

KICHUYA Kiboko Yao...Yanga Apakatwa na Simba Vilivyo...

0
0

WINGA Shiza Ramadhani Kichuya, kwa mara nyingine leo ameibuka shujaa wa Wekundu wa Msimbazi baada ya kutokea benchi na kuisaidia Simba kushinda 2-1 dhidi ya mahasimu, Yanga katika mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara.

Kichuya aliyempokea beki Novatus Lufunga dakika ya 55, kwanza alimsetia mshambuliaji Mrundi, Laudit Mavugo kuifungia bao la kusawazisha Simba dakika ya 66 kabla ya yeye mwenyewe kufunga la ushindi dakika ya 81.

Ikumbukwe Kichuya ndiye aliyeifungia Simba bao la kusawazisha dakika ya 86 Oktoba 1, mwaka jana timu hizo zikitoka sare ya 1-1 baada ya Amissi Tambwe kutangulia kuifungia Yanga dakika ya 26 kwa makosa ya Lufunga tena.

Na leo Yanga SC walitangulia kwa bao la mapema tu dakika ya tano la Simon Msuva kwa mkwaju wa penalti, baada ya kiungo Mzambia, Obrey Chirwa kuangushwa kwenye boksi na Lufunga.

Refa asiyejiuliza mara mbili katika maamuzi yake, Methew Akrama wa Mwanza alimtoa nje kwa kadi nyekundu beki Mkongo wa Simba, Janvier Besala Bokungu dakika ya 55 baada ya kumuonyesha kadi ya pili ya njano kufuatia kumchezea rafu Chirwa.

Akrama alikuwa mwiba kwa timu zote mbili leo kutokana na maamuzi yake ya kufuata sheria 17 za soka bila kusita pale tu linapotokea kosa, hali ambayo ilisababisha wachezaji wenyewe waamue kuwa na nidhamu uwanjani.

Yanga ndiyo waliuanza vizuri mchezo huo wakitawala sehemu ya kiungo, iliyokuwa ikiundwa na wageni watupu, Mnyarwanda, Haruna Niyonzima, Mzimbabwe Thabani Kamusoko na Mzambia Justin Zulu.

Na Simba iliyonza na washambuliaji watatu, Mavugo, Juma Luizio na Ibrahim Hajib ikajikuta imeelemewa mno katika dakika 30 za mwanzo za mchezo.

Yanga watajilaumu wenyewe kwa kucheza mchezo wa ‘kibishoo’ zaidi, wakigongeana pasi zisizo na tija badala ya kusaka mabao moja kwa moja.

Kibao kilianza kuigeukia Yanga baada ya kocha Joseph Omog kumpunguza mshambuliaji mmoja, Luizio na kumuingiza kiungo Said Hamisi Ndemla dakika ya 27 aliyekwenda kuipa uhai timu yake.

Na Yanga ikapata pigo baada ya kiungo wake tegemeo, Kamusoko kuumia na kumpisha Said Juma ‘Makapu’.

Kipindi cha pili, Simba SC ilirudi na maarifa mapya na pamoja na mabadiliko mengine yaliyofanywa na Omog, akiwatoa Lufunga na Mohammed Ibrahim na kuwaingiza Mkude na Kichuya mambo yakawa mazuri upande wao.

Pamoja na kumpoteza Bokungu aliyetolewa kwa kadi nyekundu, lakini Simba wakatoka nyuma na kushinda 2-1.

Kikosi cha Yanga kilikuwa; Deogratius Munishi ‘Dida’, Juma Abdul, Mwinyi Haji, Andrew Vincent, Kevin Yondan, Justine Zulu/Juma Mahadhi dk78, Simoni Msuva, Thabani Kamusoko/Said Juma ‘Makapu’ dk45, Amisi Tambwe/Deus Kaseke dk70, Obrey Chirwa na Haruna Niyonzima.

Simba SC; Daniel Agyei, Janvier Bokungu, Mohammed Hussein ‘Tshabalala’, Novaty Lufunga/Shiza Kichuya dk51, Abdi Banda, James Kotei, Ibrahim Hajib, Muzamil Yassin, Juma Luizio/Said Ndemla dk27, Laudit Mavugo na Mohammed ‘Mo’ Ibrahim/Jonas Mkude dk57.

STEVE Nyerere : Naomba radhi kwa viongozi wote niliowataja kwenye mazungumzo yangu na mama sepetu.

0
0

Msanii wa Filamu na Muigizaji mahiri hapa nchini Steve Nyerere, akizungumza mbele ya Waandishi wa habari mapema leo jijini Dar kuhusiana na mambo mbalimbali yaliyotokea hivi karikuni ,likiwe suala la ujumbe wa sauti ambao umekuwa ukisambazwa katika mitandano ya kijamii ukimuhusisha yeye Steve pamoja na Mama Wema Sepetu.

Katika Mkutano huo STEVE NYERERE amesisitiza kuwa kilichosemwa na WEMA SEPETU kuwa anaidai CCM fedha ni uongo, kwani walilipwa huku akisema Msanii aliyelipwa fedha nyingi katika kazi hiyo ni Wema Sepetu, hivyo anashangaa kusikia akidai kuwa hajalipwa.

Mradi wa Mama Ongea na Mwanao uliratibiwa na Steven Nyerere huku akisaidiwa na Wema Sepetu na kazi yake ilikuwa ni kutoa elimu kwa wazazi kuwa karibu zaidi na vijana wao wakati wa Kampeni za Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015.

Hata Hivyo, Steve Nyerere, ametumia mkutano huo kukiri kuwa Sauti iliyotumwa kwenye Mitandao ya Kijamii inayohusisha mazungumzo yake na Mama yake Wema Sepetu ni ya kwake, hivyo amewaomba radhi viongozi wote aliowataja katika mazungumzo hayo.

'Kulikuwa na maongezi ya simu kati ya mimi na mama Sepetu, mimi ndio nilikuwa naogea na mama Sepetu yasipindishwe,"Ile Sauti imekuja kuachiwa juzi wakati watu wanahama chama, kwanini nirekodiwe? naamini wamefanya hivyo makusudi" ,alisema Steve Nyerere

"Namuomba radhi Rais Magufuli na Chama changu cha CCM, yanaongelewa mengi ninayasikia, naomba radhi familia pia, niliteleza,Nimetaja viongozi katika ile sauti halafu mtu anakuja kuisambaza nimetaja viongozi wa Nchi, Mama alichofanya amenikosea sana,Lakini namuachia Mungu"alimaliza kusema

Corner Bar yafungiwa baada ya kudaiwa kukiuka maadili

0
0

Baada ya malalamiko kuzidi kutokana na kuwapo biashara zisizo rasmi katika baa maarufu ya Corner, sasa baa hiyo imeamriwa kufungwa.

Akiwa katika ziara ya kawaida leo (Jumamosi) mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Ally Hapi amemuagiza Ofisa Biashara wa Kinondoni, Mohamed Nyasama kuifunga baa hiyo.

“Hatuwezi kuvumilia vitendo hivi vikaendelea kufanyika huku tukiwa kimya…natoa agizo kesho.nendeni kaifungieni hiyo baa kwa kuwa inakiuka maadili,”amesema Hapi.

Hata hivyo Nyasama amesema walishaitoza baa hiyo faini ya Sh 300,000 kwa kosa hilo.

“Mkuu hii baa ni sugu, nimewahi hata kuipiga faini na bado imeendelea na utaratibu huo huo wa kuruhusu kina dada kujiuza.Kwa amri yako mkuu naanza taratibu za kuifungia leo, hadi kufikia kesho itakuwa tayari,” amesema.

Rais Magufuli Atoa Mkwala Mzito Kwa Wanaojenga Bomba la Mafuta Kutoka Tanga Hadi Uganda..

0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr.John Pombe Magufuli amesema hatavumilia uzembe wa aina yoyote katika ujenzi wa bomba la mafuta kutoka Tanga hadi Hoima nchini Uganda bali anataka ujenzi wa bomba hilo ufanywe katika hali inayotarajiwa ili wananchi wa Uganda na Tanzania wanufaike nalo.

Dr.Magufuli ametoa onyo hilo Ikulu jijini Dar es salaam  mara baada ya kushuhudia utiaji saini wa mkataba wa ushirikiano baina ya Tanzania na Uganda uliofanyika mbele yake na Rais wa Uganda Yoweri Kaguta museveni ambaye yupo nchini kwa ziara ya kikazi ya siku mbili.

Aidha Rais DKt.magufuli amemweleza mgeni wake Rais Museveni kuwa Tanzania imeanza kujenga reli kutoka Dar es Salaam hadi mkoani Mwanza kwa kiwango cha kisasa yaani Standard Gauge ambapo itakapofika mkoani Mwanza atajenga bandari kavu maalum kwa ajili ya kuhudumia wafanyabiashara wa Uganda pekee.

Naye Rais Museveni amesema nchi ya Uganda inaitambua Tanzania kama rafiki wa kweli na kwamba atashirikiana na Rais Dr.Magufuli katika nyanja zote lengo kuu likiwa ni kuwafanya watanzania na waganda waweze kuishi maisha bora zaidi ya hivi sasa.

Baadhi ya nyanja ambazo Tanzania na Uganda wamekubaliana ni kuimarisha biashara miongoni mwao,kushirikiana katika usafiri wa anga,mawaziri wa mambo ya nje kukutana mara kwa mara na kujadiliana jinsi ya kuboresha uhusiano baina ya mataifa.

Picha 8 za Mbowe, Lowassa , Nape na Wema Sepetu Walivyoshuhudia Yanga Ikitandikwa Mabao Mawili na Simba

0
0
Baadhi ya Viongozi wa Serikali na Siasa leo walikuwa miongoni mwa watu walioshuhudia mpambano kati ya watani wa jadi Simba na Yanga katika Uwanja wa Taifa Jijini Dar es Salaam, ambapo mnyama Simba ameibuka kidedea kwa kuibamiza Yanga goli 2-1 licha ya kuwa pungufu kwa muda mrefu.

Viongozi hao ni pamoja Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe, Mjumbe wa Kamati Kuu Chadema na Aliyekuwa Waziri Mkuu, Edward Lowassa, Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nnauye, Rais wa Shirikisho la Soka Nchini (TFF), Jamal Malinzi na Mbunge wa Chalinze, Ridhiwani Kikwete.

Rais Magufuli Ateua VIGOGO Wapya Mamlaka ya BIMA, NHC

0
0
Rais Magufuli Ateua VIGOGO Wapya Mamlaka ya BIMA, NHC

Ridhiwani Kikwete Akutana na Edward Lowassa, Asema Amejifunza Mengi Kutoka Kwake, na Bado Atajifunza

0
0
Baada ya Jana Ridhiwani Kikwete Kukutana na Edward Lowassa Uwanja wa Taifa na Kupiga nae Stori kidogo amefunguka haya kwenye ukurasa wake wa Twitter:

"Siasa ni Shule ambayo haina kikomo. Tusichoke kujifunza. Mimi nahisi bado niko shule ya Msingi na ninaendelea kujifunza.#siasasivita" Ridhiwani

FULL VIDEO: Steve Nyerere Atokwa Machozi, Aongelea Simu ya Mama Wema Sepetu

0
0
Mwigizaji wa Tanzania Steve Nyerere amezungumza na Waandishi wa habari kuelezea sakata lake sauti yake iliyosambaa ya mazungumzo ya simu kati yake na Mama wa Mwigizaji Wema Sepetu… hii video hapa chini ina kila kitu.

 VIDEO:

Kutana na Maalim Hussein Mtabibu wa Nyota za Binadamu Africa na Dunia Nzima,

0
0

Kutana na MAALIM HUSSEIN Mtabibu wa Nyota za Binadamu Mwenye uwezo wa Kurudisha Mahusiano ndani ya siku 4 tu.

MAALIM HUSSEIN Anaupeo wa Kubaini Tatizo lako Kupitia Wasaa Punde Utakapo Fanya Mawasiliano
Kwa wale wenye MATATIZO kupitia UWEZO na KUBRI Alionayo"INSHALLAH YATATUKUKA"

MAALIM HUSSEIN Anauzoefu wa Zaidi ya miaka 19 Katika kutoa huduma ya UTABIBU WA NYOTA NA TIBA ASILI KATIKA NCHI 37.

MAALIM HUSSEIN HUTIBU KUPITIA VITABU VYA QUR-AN, Dawa za Asili ya Africa, DAWA ZA KIARABU NA MAJINI... Kwa Matatizo Yafuatayo》》☆☆
☆Kutafsiri Ndoto
☆Mfarakano wa Ndoa
☆Kufungua Kizazi(kwa walifungwa kwa njia ya Kishirikina)
☆Nguvu za Kiume
☆Kusafisha NYOTA
☆BAHATI NASIBU(Kubashiri Timu za Kushinda)
☆Pete za Bahati
☆Kinga ya Mwili & Biashara
☆Zindiko ya Nyumba & Kiwanja
☆ Humaliza Kesi za muda mrefu
☆Hurudisha MALI ILIOPOTEA
☆Humaliza tatizo la CHUMA ULETE
Na DUAH MAALUM KWA WAHITAJI WOTE
  (Na Mengine Mengi ya Siri)
Kwa Ushauri na Tiba Whatsapp/Calls
      +255 674835107

Ishu ya Kujaladia Makalio Yamtoa Povu Aunti Ezekiel

0
0

BAADA ya watu kumuandama mitandaoni kuwa anatumia ‘makalio ya dukani’ kuongeza muonekano mzuri wa mwili wake, muigizaji wa sinema za Kibongo, Aunt Ezekiel, ameibuka na kusema aachwe kwani kama anatumia ni yeye.

Alisema wanaomkosoa hivyo hawana hoja kwani vitu hivyo vimewekwa kwa ajili yao madukani ndiyo maana vinauzwa hivyo hajali wanaomkosoa.

“Niwe natumia makalio sinema za Kibongo, Aunt Ezekiel, ya kujaladia, niwe situmii, ni mimi. Waniache, kwani nikitumia kuna tatizo? Kwani madukani  yamewekewa kina nani?,” alisema Aunt alipozungumza na mwanahabari wetu kuhusiana na suala hilo

Shamsa Ford : Matatizo Yamenifunza

0
0


Msanii wa filamu nchini Shamsa Ford ambaye siku za karibuni muwewe alipatwa na maswahibu na kujikuta chini ya mikono ya polisi kwa tuhuma za kujihusisha na matumizi au kufanya biashara ya madawa ya kulevya.

Inawezekana kufuatia matatizo aliyopata muwe wake, Shamsa Ford amepata kujifunza kuwa siku zote watu ambao wewe unaweza kuwaona ni marafiki wakawa ndiyo maadui wakubwa katika maisha yako. Shamsa Ford anasema muda mwingine inawezekana mtu ambaye huna hata muda naye pengine ndiye mwema kwako kuliko hao unaokuwa nao karibu kila wakati.

"Mtu anayekupenda na mwema kwako ni ngumu kumjua, ukute hata huwa hakuongeleshi na hana time na wewe. Ila ukipatwa na shida ndo utamjua ila wale ambao kutwaa uko nao, unacheka nao, unawaamini hao ndiyo maadui zako wa kwanza. Ukidondoka kimaisha au mkigombana kidogo ndiyo wa kwanza kutangaza siri zako, kuwa makini na binadamu kwani binadamu wa sasa hata usipomkosea atakuadhibu tu" aliandika Shamsa Ford

Nitakubali Utetezi wa Steve Nyerere Endapo Nitajibiwa Maswali haya

0
0
Maswali niliyoyapata baada ya utetezi wa Steve kuhusu kukana matamshi yake aliyorekodiwa kwamba alikuwa anatania;

1. Aliyeonekana Dodoma napo hakuwa yeye?

2. Nape, Msukuma na Mwigulu walipata wapi Namba ya simu kumpigia Mama sepetu?

3. Nani aliyesababisha Nape kutoa kauli yake?

4. Nani aliyetoa siri za Mali ya makonda?

5. Je wana utani na mama Sepetu? Kwanini awaingize viongozi na mawaziri (Nape, Msukuma, Mwigulu) na si wengine kama hakuna ukweli?

6. Kwanini hakufika central police kumsindikiza dadake kama Hakupigwa marufuku kukanyaga na RC?

7. Kwanini simu yake alizima wakati Wema Sepetu alipokamatwa?

8.Kwanini kajibu tuhuma za Audio punde tu baada ya kutoka police?

9. Yupo tayali kukabiliana na ushahidi utakaotolewa na Mama Sepetu?

10. Ni kipimo gani kitaonyesha maneno aliyosema mbele ya waandishi yaaminiwe kuliko aliyoyasema kwenye Audio huku akithibitisha Kwa vitendo?

VINGINEVYO UTETEZI WAKE NI WA KUPUUZWA

By Mswangilishi/Jamii Forums



Viewing all 104428 articles
Browse latest View live




Latest Images