Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104709 articles
Browse latest View live

MWANAMUZIKI ALIYEJIKATA UUME YABAINIKA ALITUMIA MADAWA YA KULEVYA HATARI

$
0
0
Rapper wa Marekani, Andre Johnson aliyejaribu kujiua kwa kujikata uume wake aliwashangaza wengi kwa kuwa kitendo hicho sio cha kawaida na wengi walitaka kufahamu sababu hasa iliyompelekea kufanya jaribio hilo.

Kwa mujibu wa E! News, chanzo cha kuaminika kimeeleza kuwa rapper huyo alitumia madawa hatari ya PCP ambayo yanajulikana kama Phencylidine au Angel Dust kabla ya kufanya tukio hilo na kujaribu kujirusha kutoka kwenye balcony baada ya polisi kufika na kumuomba ashuke aongee nao.

PCP yanatajwa kuwa moja kati ya madawa ya kulevya hatari zaidi na humfanya mtu kuwa na hasira na kufanya uharibifu na hupelekea watu kujifanyia mambo ya hatari zaidi.

Japokuwa rapper huyo alilkubali ombi la polisi hao, alijiachia ghafla hadi chini. Polisi walipoingia ndani ya nyumba walikuta kipande cha sehemu ya uume wa rapper huyo.

Kutokana na hali mbaya aliyokuwa nayo, alikimbizwa hospitalini ambapo alipewa huduma.

Hata hivyo, madaktari walishindwa kabisa kuunganisha uume wake.

DRAKE AMNUNULIA RIHANNA PETE YENYE THAMANI YA SHILINGI MILION 68

$
0
0
Drake na Rihanna wanaendelea kushibana na penzi lao linachanua huku wakiripotiwa kuwa na mpango wa kuishi pamoja.

Kwa mujibu wa gazeti la Daily Star, chanzo kimoja kimeeleza kuwa Drake amemnunulia Rihanna zawadi ya pete ya almasi yenye rangi ya njano yenye thamani ya $42,000 (sawa na 68,712,000/-).

Hata hivyo imeelezwa kuwa pete hiyo sio ya uchumba.

“Rihanna aliikubali zawadi hiyo kama ishara ya mapenzi ya Drake. Sasa hivi (Drake) anabadili hata ratiba zake ili atumie muda mwingi ipasavyo kuwa na Rihanna.” Kilieleza chanzo hicho.

Drake na Rihanna wanaonekana kuwa karibu zaidi kadiri siku zinavyozidi kwenda, na hata Jumapili katika MTV Movie Awards walionekana wakiwa wameshikana mikono muda mfupi baada ya Drake kuperform

KUMBE RAISI HANA UWEZO WA KUWAFUKUZA UKAWA BUNGE LA KATIBA NA KULETA WENGINE

$
0
0
Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Jaji Frederick Werema amesema Rais Jakaya Kikwete hana uwezo kisheria wa kuwafukuza au kutengua uteuzi wa wajumbe wa Bunge Maalumu la Katiba.

Jaji Werema alisema Sheria namba 8 ya Mabadiliko ya Katiba ya 2011, ipo kimya kuhusu suala hilo na kwamba kwa maana hiyo Rais hana mamlaka ya kutengua hata ubunge wa wale aliowateua kupitia kundi la wajumbe 201.

“Umesoma Sheria ya Mabadiliko ya Katiba? Kaisome maana ili mtu afukuzwe ubunge lazima apungukiwe sifa za nafasi hiyo, lakini kama sheria iko kimya maana yake ni kwamba hana (Rais) uwezo wa kuwafukuza,” alisema Jaji Werema.

Jaji Werema alikuwa akijibu maswali ya gazeti hili kuhusu hatima ya wajumbe ambao ni wanachama wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) ambao Jumatano jioni waliondoka bungeni kwa madai ya kutoridhishwa na uendeshaji wa Bunge Maalumu.

Wajumbe waliotoka nje ni wanaotokana na vyama vya CUF, Chadema, NCCR Mageuzi, NRA, NLD na baadhi kutoka kundi la 201. Alhamisi asubuhi, Mwenyekiti wa Bunge Maalumu, Samuel Sitta alisema utafiti uliofanywa na ofisi yake ulibaini kuwa katika kundi la 201, ni wajumbe 25 tu ambao walitoka nje pamoja na Ukawa.

Baada ya wajumbe hao kutoka nje, Mjumbe wa Bunge hilo, Mwigulu Nchemba ambaye ni Naibu Katibu Mkuu wa CCM Bara, aliomba mwongozo akihoji iwapo Ofisi ya Mwenyekiti wa Bunge Maalumu haiwezi kumwandikia Rais Kikwete ili ateungue uteuzi wa wajumbe katika kundi la 201 ambao waliungana na Ukawa kususia vikao.

“Ningependa Rais atengue hadhi zao ili kuingiza watu wengine ambao wako tayari kufanya kazi hata bure, sisi tunalipwa fedha nyingi, lakini tunaleta mzaha, watu hawana maji, dawa, madawati, ada za elimu ya juu watu wamekosa, hizi fedha zingetumika huko,” alisema Nchemba mwenye wadhifa mwingine wa Naibu Waziri wa Fedha.

Matakwa ya Sheria

Jaji Werema alisema: “Ili mtu aondolewe katika nafasi yake ni lazima akose sifa za kuwa mjumbe, mathalan kuugua ugonjwa wa akili au kichaa, kuumwa muda mrefu kiasi cha kushindwa kutimiza majukumu yake na kadhalika, lakini sifa hizo kama hazipo kwenye sheria sasa unaanzia wapi?”

Sheria ya Mabadiliko ya Katiba ya 2011 pamoja na marekebisho yake ya 2012 na 2013 inawataja Wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi kuwa Wajumbe wa Bunge Maalumu la Katiba kwa mujibu wa nafasi zao.

Kadhalika sheria hiyo inampa Rais mamlaka ya kufanya uteuzi wa wajumbe 201 kutoka makundi mbalimbali, lakini haitaji sifa wanazopaswa kuwa nazo wajumbe hao.

Jaji Werema alisema hata kama sheria ingekuwa inaruhusu kufukuzwa au kusitishwa kwa ujumbe wa wabunge hao, hakuna sababu ya msingi ya kuwachukulia hatua hiyo.

ONE MINUTE WOMAN....NAFIKA KILELENI HARAKA SANA KABLA MPENZI HAJARIDHIKA

$
0
0
Napata wakati mgumu sana tuwapo kwenye 6x6 kwani nawahi sana kufika Kileleni, Yaani within 1min tayari nakuwa nimefika na nikishafika nakosa hamu kabisa ya kuendelea na kumsukuma boyfriend wangu Pembeni


Hata mpenzi akiniandaa upya nashindwa na sijisikii raha yoyote hata akiendelea. Hamu huja tena mpaka nilale na kupitiwa usingizi nikiamka ndio naweza kunyegeka tena.

Hata ikitokea nikachelewa kufika haizidi dakika 5. Hali hii inaninyima raha sana sana kwani sipati raha ya kushiriki mapenzi kwa muda mrefu.


Mpenzi wangu anateseka sana mara nyingi humuacha akiwa hajafika hufikia hatua hulia.

Nahofu ipo siku atachoka na hii hali na kutafuta mtu mwingine kwa sababu amevumilia hii hali kwa miaka mingi, pia najihisi na kuona aibu napokuwa nae kwani tunaishi mbali mbali kukutana ni mara chache mfano kila baada ya miezi 3 lakini bado simridhishi.

Nakuwa na hamu sana sana ya kufanya mapenzi ila tukianza tu nafika.

NISAIDIENI..

KAKOBE "TANGANYIKA HURU LAZIMA IPATIKANE....NYERERE SIO MUNGU NAYE ALIKUWA NA MAPUNGUFU YAKE"

$
0
0
Amesema Tanganyika huru lazima ipatikane ni
suala la muda tu
Nchi yetu imekuwa katika laana kwa muda mrefu
kwa sababu tumeshindwa kuilinda mipaka yetu
Moto wa kudai Tanganyika umewaka na hamna
mtu awezaye kuuzima. Awaonya watawala kusoma
alama za nyakati na amewataka kuiepusha nchi
kuingia katika machafuko kwa kuridhia Serikali ya
Tanganyika.
Pia amesema Nyerere sio Mungu naye ana
mapungufu yake wanaomuabudu wanakosea.
Kosa alilolifanya Nyerere ni kuruhusu kuunda
serikali hewa ya Tanzania bara ambayo kimsingi
haipo ukiliganisha na Zanzibar.
Amewaonya viongozi wanaopinga kurejeshwa
kwa Tanganyika kuwa wataitumbukiza nchi katika
machafuko.
...Hizo zilikuwa salamu za Pasaka alizozitoa leo
katika kanisa la FGBF Dar es salaam.

HIVI ZITTO KABWE NAE PIA ANASHIRIKI KATIKA HARAKATI ZA UKAWA?

$
0
0
Wadau hivi Zitto Kabwe  pamoja na kuonekana ni mamluki na ukizingatia mmgogoro uliopo kati yake na CHADEMA ,Vipi hali yake kwenye hii movement ya UKAWA .. au wamemtenga na huku . ?? Kwa Anaye Jua Atujuze

VIDEO YA IZZO B ILIYOFANYWA NA DIRECTOR NICK DIZZO YACHEZWA CHANEL O

$
0
0
Harakati za kuuvusha muziki wa Tanzania nje ya mipaka ya Tanzania ni pamoja na kupata airtime kwenye vituo vya kimataifa ambapo Channel O ni kituo mojawapo kati ya vituo vinavyoaminika kwa kusambaza upendo na kuonyesha wanachofanya Waafrika.
Imekua ni sherehe au furaha kubwa sana pale Mtanzania anapopata nafasi ya video yake kuchezwa Channel O ambapo baada ya Weusi na yao ya ‘nje ya box’ sasa ni staa kutoka 87.8 Mbeya ndio anaichukua headline.


MANENO YA LUKUVI YATIMIA CHADEMA NAYO IMEINGIA KATIKA MTEGO MZITO

$
0
0
Hapa kuna ajenda za siri ukweli mchungu ni huu hapa na nitaendelea kuwaletea siku hadi siku hata kama ni mchungu lakini ndio dawa sasa. UKAWA sasa imeingia kwenye mtego mzito wa UAMSHO na upande wa pili kuna taarifa za siri mtoto wa Sultan wa Oman alikutana mara kwa mara na Sharif Hamad Uingereza kuhusu kuipa Zanzibar mamlaka kamili na ameapa kuisaidia kifedha na kimbinu na pia wameahidiwa mengine mengi, hapa ni pakuchunguza sana tena kiintelejensia haswa. 

Hapa sasa picha kamili inaonekana bila chenga kabisa hebu weka ushabiki pembeni alafu mtanielewa kwanza kumbukeni Lukuvi ni kiongozi wa juu kabisa wa serikali ukiachana na ujumbe wake ndani ya bunge maalumu la Katiba sasa kama ni taarifa za kiintelejensia atakua ameshazipata siku nyingi sana na ndio maana yeye kama mjumbe alitoa maoni yake kikamilifu na akaligusia hilo na kulifafanua bila uwoga kabisa maana hata ukimuuliza hana wasiwasi na anakuhambulia kimoja kimoja. 

Napata mashaka hapa ya kiusalama katika taifa hili changa kuna watu wana yao ila wanatumia UKAWA kama kivuli tuu cha kutetea wanyonge na tatizo jingine lililojitokeza ni hiki chama kikuu cha upinzani CHADEMA kujiunga na marafiki asiowajua kiundani sasa sina budi na yeye nimweke kundi hilohilo na ajenda hizohizo kwasababu wote ni UKAWA. 

Maswala madogo na marahisi ya kujiuliza ni haya hapa kwanini vuguvugu lao lianzie Zanzibar kule kwenye UAMSHO.? 

Je walipokua Zanzibar hawa viongozi wa UKAWA tuna uhakika gani kama hawakukutana na UAMSHO.? Maana hapa kuna shutuma za CUF kua na uhusiano na UAMSHO.

Shutuma alizozitoa Lukuvi zina ukweli wowote? Maana Lukuvi ana kofia mbili huyu ya uwaziri na ujumbe sasa kama ni taarifa za kiintelejensia atakua nazo tu bila shaka.

Wameshindwa plan A je plan B watafanyaje au watakua ni kikundi cha waasi.?

Kuhusu kurudi kwa Sultan wa Oman vipi wameshakutana na Sharif kujadili.? Pia kuna taarifa za chini kwa chini kua hata PEMBA na UNGUJA zinavuguvugu la kujitenga kila mmoja kivyake, hata Nyerere aliliona na alishalionya mapema kama naongopa nikosoe. Pia kuna kauli fulani za wanzanzibar bungeni kama "Ya wazanzibar tuachie wenyewe tunajuana" hii kauli ni pana sana na ina maana kubwa.

CHADEMA ameungana rafiki asiomjua kiajenda aachane nao haraka sana hapo ni WORKING TIME BOMB.

Ushauri wangu kikundi cha UKAWA kifutwe tu nina wasiwasi kitakua kikundi kamili cha waasi kwanza siyo rasmi na wakiendelea na hujuma zao wachukuliwe hatua kali kabisa na kiitwe rasmi ni kikundi cha waasi

NDUGU WANAOKULA NYAMA ZA MAITI WAKAMATWA TENA

$
0
0
Watu wawili wanaotuhumiwa kula nyama za binadamu wamekamatwa baada ya kichwa cha mtoto wa miaka mitatu, kukutwa katika nyumba wanayoishi nchini Pakistan.

Polisi waligundua tukio hilo la kutisha na kuwakamata watuhumiwa Mohammad Arif Ali (35) na mdogo wake Mohammad Farman Ali mwenye miaka 30.

Kwa mujibu wa gazeti la mtandaoni la Dailymail, wanandugu hao wanaotoka katika mji mdogo wa Darya Khan wamewahi kuhukumiwa kifungo cha miaka miwili jela, baada ya kutiwa hatiani kwa makosa ya kula nyama za binadamu. Waliachiwa huru baada ya kumaliza kutumikia adhabu hiyo mwaka jana.

Arif na Farman walikamatwa na kuswekwa rumande wakati uchunguzi ukiendelea, baada ya tukio hilo lililowavuta wengi na kutikisa tena eneo hilo.

Miaka mitatu iliyopita ndugu hao walifukua zaidi ya miili 100 ya maiti katika makaburi yaliyopo karibu na kijiji chao kisha kuzitumia maiti hizo kama asusa.

Mkuu wa Polisi katika eneo hilo, Ameer Abdullah alisema maofisa wake wa polisi waliamua kuvamia na kufanya upekuzi katika eneo hilo, baada ya majirani kulalamika kwamba kuna harufu mbaya ambayo imekuwa ikitoka katika nyumba waliyokuwa wakiishi.

“Wakazi hao waliifahamisha polisi baada ya kusikia harufu mbaya ikitokea katika nyumba waliyokuwa wakiishi watu hawa,” alisema Abdullah.

Abdullah alisema: “Tulifika katika nyumba hiyo siku ya Jumatatu asubuhi na kufanya upekuzi kabla ya kukiona kichwa cha mtoto wa miaka mitatu.

“Baada ya kugundua kitu hicho kinachotisha, tulimkamata mmoja wa ndugu hawa Mohammad Arif na alitupatia ushirikiano hadi tulipomweka kizuizini ndugu yake,” alisema Abdullah.

Alisema jeshi la polisi bado linaendelea na uchunguzi ili kung’amua iwapo kuna makaburi mengine yamechimbwa na watu hao kijijini hapo au katika vijiji vya jirani.

Baada ya kuulizwa maswali mengi na polisi, ndugu hao walikiri kula nyama za watu na kueleza ukweli namna walivyokuwa wakitengeneza mlo huo. Kwa kuwa Pakistan haina sheria zinazohusu ukatili wa maiti, huenda haitakuwa rahisi kwa wawili hao kufungwa jela maisha.

MAASKOFU 32 WAUNGA MKONO RASIMU YA WARIOBA KAMA ILIVYO

$
0
0
Katika salama za pasaka viongozi wa dini wa katoliki 32 wamesema maoni ya wananchi katika rasimu ndio msingi wa katiba hivyo wamewataka wajumbe wa bunge la katiba wa yaheshimu kama yalivyo wasilishwa na jaji warioba bungeni,wamesema wajumbe wa tume waheshimiwe kwakua taasisi zote,mtu mmoja mmoja na makundi mbali mbali ya kijamii yalipata nafasi kupeleka maoni yao mbele ya tume ya warioba,hivyo wanapashwa kuheshimu rasimu hiyo iliyo beba maoni ya wananchi hakuna haja ya wakuidharau tume iliyo undwa na watu makini na wanao heshimika katika taifa letu

TID, RECHO THT WADAIWA NI WAPENZI

$
0
0
MALOVEE? Bosi wa Top Band, Khaleed Mohamed ‘TID’ au ‘Mzee Mnyama’ na mtoto mzuri kutoka Jumba la Vipaji Tanzania (THT), Winfrida Josephat ‘Recho THT’, wanadaiwa kuwa na uhusiano uliotafsiriwa ni wa kimapenzi, Ijumaa Wikienda limeinusa.

Kwa mujibu wa chanzo makini, wawili hao wamekuwa wakionekana pamoja sehemu mbalimbali huku wakidaiwa kupiga ‘mitungi’ kiasi cha kushindwa kuzificha hisia zao.

“Mbona ipo wazi, TID na Recho siku hizi hawafichi kitu, tena wanapopiga mitungi ndiyo kabisa, mfano mzuri ni juzikati walikuwa pamoja mjini Dodoma, waliponda raha kinomanoma,” kilitiririka chanzo hicho.
Kama ilivyo ada, wanahabari wetu waliingia mzigoni kwa kuanzia nyumbani kwa Recho, Kinondoni, Dar, wakamkosa lakini badala yake, walipatikana mashosti zake wa karibu.

“Recho kwa sasa anatoka na Mnyama na hapa tunavyoongea yupo Njombe ambapo ametimka baada ya taarifa za yeye kutoka na TID kuzagaa mtaani, halafu pia Recho siku hizi anapombeka sana na tunahisi hata ‘mambo meupe’ anatumia,” alisema shosti huyo.

Baada ya kushibishwa data hizo, waandishi wetu walitinga ofisini kwake THT, Kinondoni ambapo wanamuziki wenzake walisema staa huyo ana muda mrefu hajafika kazini hapo pasipo kutoa sababu za msingi.

Ijumaa Wikienda lilimpigia simu Recho, akafunguka: 
“Kweli nakunywa pombe lakini si kiivyo watu wanavyonisema. TID ni mtu wangu kikazi wala siyo kimapenzi. Watu wamekuwa wakinishutumu kila ninapokuwa na mwanaume wanasema ni bwana’ngu kitu ambacho si cha kweli kama wanavyonizushia kuvuta bangi.

“THT siendi kwa sababu nimesafiri, hapa ninapoongea nipo Njombe. Nimekuja kutulia huku kutokana na maneno kuzidi na watu kunipakazia uongo,” alisema Recho.

Kwa upande wake TID, alipopigiwa simu, alijitetea kwa kusema kuwa yupo na Recho kikazi na wala si vinginevyo.

“Dah...! Ebwana naomba uachane na hizo habari za mapenzi, mimi ni mtu mzima nina mengi ya maendeleo ambayo natakiwa nifanye,” alisema TID.
GPL

BABY MADAHA AJIBU MAPIGO KWA STEVE NYERERE

$
0
0
Stori: Nyemo Chilongani

VITA ni vita! Mwanadashosti anayesukuma maisha laifu kupitia filamu na muziki Bongo, Baby Joseph Madaha amesema anamshangaa Mwenyekiti wa Klabu ya Bongo Movie Unity, Steve Mengere ‘Steve Nyerere’ kwa kauli aliyoitoa dhidi yake kuwa hayupo sehemu yoyote ile.

Akifafanua kuhusiana na kauli hiyo aliyoitoa mwenyekiti huyo wiki iliyopita, Baby alijibu mapigo kuwa kiongozi huyo alipotosha umma kwani yeye ni memba halali wa Bongo Movie Unity.

“Steve anasema hajui nipo wapi, hivi ni kweli mwenyekiti hawajui watu waliokuwa na kadi ya uanachama? Mimi nipo kotekote, nipo Bongo Movie, nipo hata Bongo Fleva, kama akitaka kadi aseme nimwoneshe, sionekani sana kwani muda mwingi nakuwa Kenya,” alisema Baby Madaha, alipotafutwa Steve, hakuwa tayari kufafanua ishu hiyo.

RIYAMA NJIA PANDA KWA MITUNGI

$
0
0
Stori: Erick Evarist

Mh! Mwigizaji wa sinema za Kibongo, Riyama Ally, amejikuta akiwa njia panda baada ya kutakiwa kunywa pombe ya kienyeji aina ya ugimbi ambayo hajawahi kunywa maishani mwake.

Riyama aliingia kwenye mtihani huo juzikati pande za Songea alipokuwa amekwenda kikazi ambapo alitakiwa kunywa pombe hiyo kutokana na matakwa ya filamu lakini akashindwa.

“Ulikuwa mtihani kwa kweli, ili kuleta uhalisia ilitakiwa ninywe pombe hiyo lakini kiukweli nilishindwa kwa kuwa sijawahi kunywa hata siku moja, ilibidi nizuge na kopo tupu,” alisema Riyama ambaye ni mkali wa kuzitendea haki sini za siriasi.
GPL

WEMA, PENNY WAIPASUA FAMILIA YA DIAMOND

$
0
0
Stori: GLADNESS MALLYA NA CHANDE ABDALLAH

BOOOM! Katika hali ya kushangaza, mastaa wawili Bongo, mwigizaji Wema Isaac Sepetu na mtangazaji wa DTV, Penniel Mungilwa ‘Penny’ wanadaiwa kuipasua familia ya kinara wa Bongo Fleva, Nasib Abdul ‘Diamond Platnumz’, Ijumaa Wikienda lina ripoti kamili.

Kwa mujibu wa chanzo makini ambacho ni mtu wa karibu na familia hiyo kuna mgawanyiko ambao umesababisha mpasuko unaofanya familia hiyo kuwa na makundi mawili yasiyoelewana juu ya uhusiano wa Diamond na warembo hao.

Kwa sasa Diamond anatoka kimapenzi na Wema baada ya kumwagana na Penny lakini mtangazaji huyo anadaiwa kuendelea kwenda katika familia hiyo kwani asilimia kubwa inaonesha anakubalika zaidi ya wengine wote.


TEAM PENNY VS TEAM WEMA
Habari zilidai kuwa mpasuko huo ni mkubwa kwani kundi moja linalojiita Team Penny linamkubali zaidi Penny na lingine ambalo lina watu wachache Team Wema linamkubali Wema. Imefahamika kwamba kundi linalomkubali Penny na kumuona ndiye mwanamke sahihi kuwa na Diamond japokuwa wameshaachana ni Mama Diamond mwenyewe, Sanura Kassim ‘Sandra’, dada zake Esma Platnumz, Queen Darleen, Anko na dada wa hiyari wa Diamond, Halima Haroun ‘Kimwana’


Ilidaiwa kwamba kundi hilo limekuwa likitoa ushirikiano wa karibu mno kwa Penny na sehemu nyingi wanakuwa wote ikiwemo kwenye sherehe na viwanja vya starehe, yaani ni fulu kujiachia.
Habari hizo zilidadavua kuwa hata dada wa Diamond, Esma anaishi nyumba moja na wifi yake huyo wa zamani.

“Familia ya Diamond imegawanyika katika makundi mawili, kundi kubwa linamkubali sana Penny japokuwa alishaachana na Diamond. Ilisemekana kuwa si familia tu kwani hata madansa wa Diamond wanampenda sana Penny kuliko Wema,” kilisema chanzo.


TEAM WEMA HII HAPA
Uchunguzi wa wanahabari wetu ulibaini kuwa ndani ya kundi linalomtaka Wema kuna watu wachache akiwemo Diamond mwenyewe, baba yake, Abdul Jumaa ambaye kwa upande wake alitamka wazi: “Wema ndiye mkwe wa ukweli kabisa.”

Baba huyo alikwenda mbali na kusema anamkubali Wema kwa sababu ana nyota kali na ana roho nzuri hivyo akiendelea kuwa na mwanaye atakuwa na mafanikio tofauti na alivyokuwa na Penny.
Pia ilijulikana kuwa kundi hilo lina mtu mwingine, ndugu wa Diamond aitwaye Rommy Jones ambaye amekuwa akionekana na Wema mara kwa mara hasa wakati msanii huyo akiwa amesafiri.

HALIMA KIMWANA AITWA KIGEUGEU
Taarifa nyingine zilidai kwamba katika sakata hilo, Halima kimwana amekuwa akiitwa kigeugeu kutokana na kutokuwa na upande anaosimamia. “Mara utamuona na Wema ghafla unamuona tena na Penny, yule hata haeleweki. Anajichetua sana,” kilisema chanzo chetu.

MAMA DIAMOND ANASEMAJE?
 “Mimi siwezi kumchagulia Diamond mwanamke wa kuwa naye, yeye mwenyewe ataamua kwa sababu ni mtu mzima kwa hiyo siwezi kumpangia au kumchagulia mwanamke wa kuwa naye,” alisema mama Diamond bila kukanusha kuwa na ukaribu zaidi na Penny.

MSIKIE HALIMA KIMWANA
Baada ya kuwatafuta Diamond, Wema na Penny bila mafanikio, Ijumaa Wikienda lilizungumza na Halima Kimwana ambaye alikuwa na haya ya kusema:
“Sisi tuko karibu na Penny kwa sababu anapenda kujichanganya na sisi hivyo hata Wema akija kutuchukua na kutaka twende naye klabu hatukatai kwa sababu wote ni mawifi zetu.
“Hatubagui kwani hakuna siku ambayo Wema alishataka kuwa na sisi tukamkatalia.”

MASWALI
Hivi karibuni picha za Penny akiwa na mawifi zake kwenye shughuli ya kumtoa mtoto wa ndugu yao zilivuja ambapo ndani ya sherehe hiyo pia Diamond alikuwepo akiwa anacheza dufu lakini Wema hakuonekana, jambo lililozua maswali.
GPL

WEMA SEPETU NDIYE IJUMAA SEXIEST GIRL

$
0
0
STAA wa filamu Bongo, Wema Isaac Sepetu ameibuka mshindi katika shindano la Ijumaa Sexiest Girls akiwabwaga Elizabeth Michael ‘Lulu’, Nelly Kamwelu, Jacqueline Wolper na Jokate Mwegelo usiku huu ndani ya Dar Live.

Shindano hilo lilikuwa linaendeshwa kupitia Gazeti Pendwa la Ijumaa linalochapishwa na kampuni ya Global Publishers Ltd.

KUMBE WEMA SEPETU NA GLOBAL PUBLISHERS NI DAMU DAMU

$
0
0
Juzi tu Wema Alienda Ofisi za Global Publishers na kuanzisha Timbili la Haja kwa kudai kuwa wanamfuatilia sana na kumwandika Sana kwenye Magazeti yao..Nikiamini Wema Sepetu na Global Publishers ni Maadui wa Kutupwa ....Lakini Jana Wema Sepetu Kaudhuria Shindano la Global Publishers na Kutunikiwa Ijumaa Sexiest Girl kama Sikosei...Najaribu kuwaza tu kwa sauti  Je walikaa chini na Kumaliza Tofauti zao ? Au kummpa Ushindi huo wa Sexiest Girl Basi Wema Ndio Kasahau Kila Kitu .....?????

DAVID MOYES KUACHISHWA KAZI MUDA WOWOTE KUANZIA LEO

$
0
0
Vyombo vya habari vya Uingereza, likiwemo Mail on Sunday vimeripoti kuwa David Moyes ataachishwa kazi wiki chache zijazo na kwamba anaweza kuachiswa hata leo au kesho

Wamiliki wa timu hiyo, familia ya Glazer wanadaiwa kuishiwa uvumilivu kwa kocha huyo ambaye tangu aanze kuinoa imeendelea kufanya vibaya na sasa ikiwa nafasi ya saba kwenye msimamo wa Barclays Premier League. Jana Man United ilifungwa mabao 2-0 na Everton.

Uongozi wa juu wa klabu ulikuwa umepania kumpa muda kocha huyo lakini umeona ni ngumu kuona mabadiliko kwakuwa hata wachezaji hawamwamini tena kocha wao. Ripoti hizo zinadai kuwa nafasi yake inaweza ikachukuliwa kwa muda na Ryan Giggs huku makocha wanaowaniwa kuchukua nafasi ya muda wote wakitajwa kocha wa Dortmund, Jurgen Klopp, kocha wa Uholanzi, Louis van Gaal na kocha wa Real Madrid, Carlo Ancelotti.

WASANII AFRICA MASHARIKI WAJIPANGA KUZISUSIA TUZO ZA MTV AFRICA MUSIC AWARDS

$
0
0

Website ya Nairobi News imeripoti kuwa wasanii wa Afrika Mashariki wanapanga kuzisusia tuzo za MTV Africa Music Awards, MAMA.

Wasanii hao wanazishutumu tuzo hizo kwa kutozitendea haki nchini za Afrika Mashariki mwaka huu na kwa kuwapendelea wasanii wa Afrika Kusini na Nigeria zaidi. “Uganda imeumia zaidi kwasababu kutajwa kwao pekee ni kwa collabo na Amani,” msanii mkubwa wa Kenya ambaye hakutaka kutajwa jina lake aliuambia mtandao huo.

Umeandika kuwa wasanii waliotarajiwa kutajwa kwenye tuzo hizo ni AY, Ommy Dimpoz na Lady Jaydee, Tanzania, P-Unit, STL, Elani na Wyre wa Kenya na Jose Chameleone na Navio wa Uganda. Mtandao huo umeripoti kuwa wasanii wengi zaidi wanapanga kutoshiriki kwenye show za utangulizi za Road to Mamas zitakazofanyika Dar es Salaam kwa Afrika Mashariki.

MANCHESTER UNITED YAMTIMUA NA KUMRUSHIA VIRAGO DAVID MOYES

$
0
0

Kocha David Moyes ameondolewa rasmi kwenye majukumu yake ya ukocha katika klabu ya Manchester United. Taarifa rasmi ya klabu hiyo imetolewa kupitia mtandao wa Twitter unaweza kuicheki hapo chini……

BAADA YA DAVID MOYES KUFUKUZWA MAN U HUYU NDIO KOCHA MPYA

$
0
0
Kutokana na kutofanya vizuri chini ya uongozi wake David Moyes hatimaye leo April 22 Manchester United wamemtangaza Mchezaji wa siku nyingi wa Manchester United Ryan Giggs kukabidhiwa  kwa muda mikoba ya David Moyes aliyetimuliwa kazi leo
Viewing all 104709 articles
Browse latest View live




Latest Images