Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104694 articles
Browse latest View live

Gazeti la MwanaHALISI kumuanika Paul Makonda

$
0
0


Nyumba aliyokulia Paul Makonda, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam (Daudi Bashite)

KILA pembe ya kijiji cha Koromije, Wilaya ya Misungwi, pamoja na viunga vya jiji la Mwanza Paul Makonda, Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam anatajwa na kufahamika kama Daudi Albert Bashite, wanaandika Waandishi Wetu.


Wanaomtaja kwa jina hilo ni wanakijiji, ndugu zake, wanafunzi aliowahi kusoma nao pamoja na watu waliowahi kumshuhudia akifanya kazi kama kondakta.


Gazeti la MwanaHALISI baada ya uchunguzi wake wa kina uliohusishwa kutuma timu ya maripota wake jijini Mwanza, wanakuletea habari kamili inayofichua ukweli wa sakata hilo huku mama na baba wa Makonda, shangazi yake na wanafunzi waliowahi kusoma naye wakiwa wamehojiwa.

Shule ya Msingi aliyosoma Paul Makonda, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam

Chanzo: Mwanahalisi

Rais Magufuli Awaagiza Tanesco Kukata Umeme Ikulu...!!!

$
0
0

Rais wa Jamhuri ya Munngano wa Tanzania Mh Dr John Pombe Magufuli ametoa agizo kwa uongozi wa tanesco kukata umeme kwa Wizara au taasisi yoyote inayokwepa kulipa bili za umeme.

Mh Rais ameyasema hayo leo katika ziara yake ya kuzindua na kuweka jiwe la msingi katika mradi wa umeme wa msongo wa Kv 132 Mtwara " Tanesco pasitokee taasisi ama Wizara hata Ikulu isipolipa umeme we kata tu, hatuwezi kujiendesha kwa hasara wakati kuna watu wanakwepa kulipia gharama" wakati serikali inatoa ruzuku zake humu sasa ni wakati Tanesco ijiendeshe kwa faida.

Aidha Mh Rais ameonya tanesco kutoingia mikataba ya hovyo na makampuni ya nje yanayokuja kwa ujanja na alisema kampuni ikitaka kuja kuwekeza umeme nchini basi waje wazalishe umeme wao na wauze tanesco na wasitegemee umeme huu kufanya ujanja ili kutorudia mikataba mibovu kama symbion na makampuni mengine

Wema Sepetu Akutana na Lema, Afunguka Maneno Haya Mazito..!!!

$
0
0

Msanii wa filamu nchini Wema Sepetu ambaye hivi sasa amehamia Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) ametimiza hadi yake kwenda kuonana na Mbunge wa Arusha mjini Mhe. Godbless Lema ambaye amepata dhamani siku ya Ijumaa na kutoka gerezani.

Wema Sepetu juzi alisema atakwenda Arusha kuonana na Mbunge huyo ambaye amekaa ndani kwa zaidi ya miezi mitatu na kusema ni faraja kwao saizi kuona ametoka na kuja kuendeleza mapambano

"Ni faraja kwetu kwamba sasa umerudi mtaani kuendeleza mapambano, kwenye mapambano haya hautakuwa mwenyewe, mdogo wako Wema nitakuunga mkono mpaka kieleweke. For that sake, kesho (jana) i'll be in Arusha kuonyesha Solidarity" alisema Wema Sepetu 

Baada ya Wema Sepetu kufanikiwa kuonana na Mbunge wa Arusha Gobless Lema amefunguka na kusema saizi anajisikia furaha na amani kuwa ndani ya chama hicho

"Finally Met my brother, aisee Chadema inanipa furaha mimi. Nina amani ya moyo... Ona Venye nacheka .... It was A Good Day...." aliandika Wema Sepetu 

Harmorapa Azidi Kumganda Ali Kiba,Hii Hapa Kauli Yake Mpya...!!!!

$
0
0

Rapa ambaye amejizolea umaarufu sana kupitia mitandao ya kijamii Harmorapa amefunguka na kusema kwa Tanzania hii hajaona msanii wa kumfananisha na Alikiba na kusema hata ngoma yake ambayo amefanya na Juma Nature alitaka kufanya na Alikiba.

Harmorapa anasema kabla ya kurekodi ngoma yake hii mpya ambayo amefanya na mkongwa Juma Nature alijitahidi sana kumtafuta Alikiba ili aweze kufanya naye lakini jitihada zake ziligonga mwamba kutokana na ukweli kwamba Alikiba alikuwa na mambo mengi na kushindwa kumfikia kuzungumza naye jambo hilo.

"Kiukweli King Kiba kwa Tanzania hapa sioni wa kumfananisha naye, kwa hiyo nisema sijaona bado wa kumlinganisha naye sababu jamaa anafanya vizuri sana na anajua muziki sana, hata kabla ya kurekodi hii kazi yangu mpya nilifanya jitihada na watu wa karibu na Alikiba japo niweze kufanya naye kazi lakini sikuweza kufanikiwa kutokana na mambo yake kuwa mengi sana na watu pia ambao walikuwa wakinipa connection naye kuna vitu sikuweka sawa, na muda nikaona unazidi kwenda nikasema ngoja nifanye tu" alisema Harmorapa 

Jinsi Kesi ya Lema Ilivyoibua Mapinduzi ya Kisheria....!!!

$
0
0

Kesi ya tuhuma za uchochezi inayomkabili mbunge wa Arusha Mjini (Chadema), Godbless Lema, inaendelea, lakini inaweza kuwa imejenga misingi ya utoaji haki kwa vyombo vya Serikali, mawakili na mahakama.

Lema alipata dhamana Ijumaa baada ya kukaa mahabusu kwa siku 121 kutokana na sarakasi za kisheria baada ya ofisi ya Mwendesha Mashtaka wa Serikali kuweka pingamizi dhidi ya dhamana yake alipofikishwa kortini kwa mara ya kwanza.

Akitoa dhamana hiyo, Jaji Salma Maghimbi wa Mahakama Kuu Kanda ya Kaskazini alisema uamuzi wa Mahakama ya hakimu Mkazi wa Mkoa wa Arusha kumpa dhamana Lema, Novemba 11 mwaka jana ulikuwa sahihi na hakukuwa na sababu za kupinga.

Alisema DPP angekuwa na haki ya kupinga dhamana iwapo mshtakiwa asingetimiza masharti ya dhamana na si vinginevyo.

Jaji huyo alizielekeza mahakama za chini kusimamia mamlaka yake bila kuyaachia na kuzitaka ziheshimu misingi ya sheria.

Alikuwa akirejea kitendo cha Hakimu Mkazi wa Arusha kuacha kuendelea na masharti ya dhamana aliyompa Lema baada ya mawakili wa Serikali kumtaarifu kwa mdomo kuwa wana nia ya kukata rufaa kupinga dhamana hiyo.

Tangu wakati huo, dhamana ya Lema ilikuwa ikitegemea sarakasi hizo za kisheria zilizotinga hadi Mahakama ya Rufaa ambayo katika uamuzi wake iliweka bayana kuwepo kwa sintofahamu.

Lakini Februari 28 wakati wa kutoa uamuzi kuhusu pingamizi la dhamana lililowekwa na Serikali, Jaji Bernard Luanda, ambaye aliongoza jopo la majaji watatu wa Mahakama ya Rufaa, alionyesha kushangaa jinsi ofisi ya DPP ilivyoshughulikia suala hilo, ikiwa ni pamoja na kuondoa rufaa siku ya uamuzi,

Jaji Luanda alisema tabia ya wanasheria wa DPP inanajisi taaluma na hivyo kuitaka ifanye kazi kwa njia ambayo haitaonea wananchi.

Pia majaji hao walitupa mapingamizi mawili yaliyokuwa yamewasilishwa na ofisi ya DPP.

Kauli ya Jaji Maghimbi na ya majaji hao ni kama zimejenga msingi wa utoaji haki kwa vyombo hivyo.

“Ofisi ya DPP na Mwanasheria Mkuu wa Serikali zilipaswa kuwa ni watetezi wa haki, lakini zimebadilika na sasa zinatumika kukandamiza watu wakose haki zao,” alisema mbunge wa Tarime Vijijini (Chadema), John Heche.

“Leo mbunge amekaa miezi minne gerezani kwa kosa ambalo lina dhamana. Tujiulize ni Watanzania wangapi wanasota magereza kutokana na DPP na Mwanasheria Mkuu wa Serikali kushindwa kusimamia sheria?”

Alisema Serikali inatumia fedha nyingi kugharamia vyakula vya wafungwa, lakini uchunguzi wa kina ukifanyika itabainika wengi wapo jela kutokana na ofisi hizo mbili kutotimiza wajibu wao.

Mwanasheria wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu, Hamis Mkindi alisema kosa la kutoa lugha ya uchochezi lina dhamana, lakini kilichokuwa kinafanyika ni ukiukwaji wa sheria.

Mkindi alisema hata Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inaeleza wazi dhamana ni haki ya mtuhumiwa, lakini haki hiyo ilikuwa inachelewa kutokana na DPP kutumia vibaya mamlaka yake.

Mwanasheria wa Chadema, Peter Kibatala alisema tangu kuanza kwa shauri hilo walikuwa wanatetea haki na hadhi ya mahakama ambayo alidai iliporwa na DPP.

Kibatala, ambaye pia ni mmoja wa mawakili wa Lema, alisema wanashukuru kwa uamuzi wa Jaji Maghimbi kutoa dhamana.

“Jaji aliweka wazi kwenye uamuzi wake, mahakama za chini zinatakiwa kuheshimiwa na pia kuzuia DPP kuweka mapingamizi yanayokiuka haki,” alisema.

Mara baada ya Lema kutoka nje kwa dhamana, Mbunge wa Kawe (Chadema), Halima Mdee aliandika katika ukurasa wake wa Twitter akisema:

“Mhe Lema, karibu sana uraiani. Aliyeshinikiza unyimwe dhamana alidhani anakukomoa, kumbe anazidi kukuimarisha. Hongera sana Kamanda.”

Msanii wa filamu nchini aliyejiunga na Chadema hivi karibuni, Wema Sepetu naye aliandika katika ukurasa wa Instgram akimpongeza Lema na kwenda Arusha kumtembelea.

“Kwenye mapambano haya hautakuwa mwenyewe. Mdogo wako Wema nitakuunga mkono mpaka kieleweke,” aliandika msanii huyo.

Ofisa mmoja wa ofisi ya Mwanasheria Mkuu ambaye hakutaka jina lake litajwe gazetini alisema ofisi hiyo haipaswi kunyooshewa kidole cha lawama kwa sababu mahakama ilikuwa na uwezo wa kuingilia mapema na kutoa uamuzi inayoona unafaa.

“Hawakuwa na sababu ya kukaa kimya siku zote na kuja kutoa lawama hivi sasa,” alisema ofisa huyo.

Mrembo Diana Afunguka Dhuluma Aliyofanyiwa Miss World 2016 na Mkenya...

$
0
0

Hii ndiyo story nzima ya Miss world 2016.
Katika mashindano yale hawaangali urembo tu bali na lengo la Urembo yaani (BeautyWithaPurpose) na hivyo kila mshiriki anatakiwa atengeneze ya kwake ,hivyo mimi niliamua kutengeneza ya tofauti kidogo maana ni ngumu kupata video ya mtu anayekeketwa nikaamua kuonyesha kwa njia ya documentary , nikaiupload youtube mnamo tarehe 18 October 2016 kwa mara yakwanza na baadaye kuongeza baadhi ya maudhui katika ile documentary ya kwanza hii ilikuwa kwaajili ya maandalizi ya kwenda missworld, na baada ya hapo nikaipost tarehe 24 November 2016 .Nilipofika Washington nilikabidhi CD na pia tuliituma kwa njia ya email kwenda Miss World. Baada ya hapo tukaitwa usiku mmoja na tukaambiwa tunaoneshwa documentary zilizofanya vizuri na yangu iliingia kwenye 24 bora na ikasifiwa sana lakini siku baada ya kuoneshwa kesho yake asubuhi alikuja Miss Ghana katika chumba changu akiwa na hasira sana nkaamuuliza nini shida akasema Miss kenya anamuudhi ,na hapo kwa ajili hasira akaniambia Miss kenya kaenda kukushtaki kwa Mkuu wa MissWorld kuwa BWP yako hujaitengenezea nchini kwenu na yake ina maudhui mengi kuliko yangu.Nilipomjulisha Meneja hakutaka kuamini kuwa Taasisi kubwa kama Miss World haiwezi kuaminishwa kwa maneno ya mdomoni bila kufanya uchunguzi wa kina,lakini baada ya hapo muaandaji wa miss Kenya alikuwa ameshafika na akawa analalamika sana eti kwanini miss Kenya hafanyi vizuri akawa anashauriana naye vitu vingi.Baadaye tukatajiwa Top5 Kenya ikaingia ile hali haikuwepo katika orodha ya 24 Bora japo kwa kipindi chote hicho alikuwa hajaonesha documentary siku tulipotakiwa tukionesha documentary zetu.

Muandaaji wa Miss kenya alikuja wiki mbili kabla ya fainali na alikuwepo kwenye group la whatsapp la Miss world ambalo kimsingi lilikuwa ni group mahususi kwaajili ya washiriki tu na baadaye alijisahau akatuma meseji kumuuliza Evelyn kwanini havai hereni zenye kuitambulisha Kenya.Swali linakuja je alifuata nini kwenye group na aliingizwaje kwenye group la washiriki ambalo lilikuwa linajumuisha na viongozi wa MissWorld.

Barakah Da Prince na Naj vipi? Huu Ndio Ukweli wa Penzi lao 

$
0
0

Barakah Da Prince alikaa kitako na Mtangazaji wa ABM Radio ya Dodoma, DJ Rodger kuzungumzia status ya uhusiano wake na Naj.

Kwenye interview hiyo Barakah amedai kuwa bado mapenzi yao yapo moto moto ila wameamua kutopenda sana kupostiana kwenye mitandao ya kijamii kama zamani.

Ameongeza kuwa ukurasa wake wa Instagram sasa utaendelea kujikita katika kazi zake zaidi na sio mambo ya uhusiano.

Inasikitisha..Makonda Amwaga Chozi Kanisani Huku Familia Yake Ikimgeuka,Habari Katika Vichwa vya Magazeti ya Leo 6/3/2017..!!!


Sasa ni Rasmi Vodacom Tanzania Kuanza Kuuza Hisa Zake Kwa Wawekezaji

$
0
0

Kampuni ya simu za mkononi nchini Vodacom Tanzania itakuwa kampuni ya kwanza inayotoa huduma za mawasiliano kuuza hisa zake katika soko la hisa la Dar es Salaam maarufu kama DSE. Hii inafuatia rasimu ya waraka wa matarajio (Prospectus) na maombi yaliyotumwa kwenye Mamlaka ya Masoko ya Mitaji na Dhamana (CMSA) kukubaliwa. CMSA ndiyo mamlaka inayosimamia masoko ya mitaji na dhamana nchini.

Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya Vodacom Tanzania, Ian Ferrao
Uuzaji wa hisa za awali wa Vodacom Tanzania Limited PLC ni katika utekelezaji wa Sheria ya Posta na Mawasiliano iliyofanyiwa marekebisho na sheria ya Fedha mwaka 2016 ambayo inaagiza kampuni zote za simu za mikononi kuuza 25% ya hisa zao kwa umma.
Hisa za kampuni hiyo inayoongoza kwa kuwa na wateja wengi zaidi nchini, huenda sasa zikaanza kuuzwa muda wowote kuanzia wiki hii au wiki ijayo. Vodacom Tanzania inatarajia kuorodhesha asilimia 25 ya hisa zake katika soko la mitaji ambayo ni sawa ni hisa milioni 560 zitakazokuwa na thamani ya shilingi bilioni 476 huku kila hisa ikiuzwa kwa Tsh 850.
Hii ni hatua kubwa sana kwa Vodacom Tanzania ikizingatiwa kwamba kampuni nyingine za simu zinasuasua. Vodacom inatarajiwa kuwa miongoni mwa kampuni zitakazokuwa na mitaji mikubwa katika soko la DSE. Kampuni nyingine zenye mitaji mikubwa ni Acacia, EABL na TBL. Hadi hivi sasa DSE ina kampuni 25 zilizoorodheshwa ambapo kampuni za ndani ni 18 na zile zilizoorodheshwa kutoka masoko ya kigeni yakiwemo London na Nairobi ni 7.
Taarifa rasmi za mauzo ya awali ya hisa hizo milioni 560 lini zitaanza kuuzwa, na wawekezaji gani watakidhi vigezo zitatangazwa hivi karibuni. Tutazidi kukuletea taarifa hizi za uwekezaji kwa makampuni ya simu nchini.

Rais Magufuli: Hata Mkeo Anaweza Asikupende Siku Nyingine,,,,!!!

$
0
0

Rais Magufuli jana mkoani Mtwara wakati akiweka jiwe la msingi katika kituo cha kupooza umeme njia ya KV 132 amelipongeza Shirika la Umeme nchini Tanesco na kumpongeza Waziri wa Nishati na Madini, kwa juhudi zake katika kazi.

Rais Magufuli amesema aliamua kumteua Sospeter Muhongo kuwa Waziri kutokana na ukweli kwamba alikuwa anaona uchapaji wake wa kazi kipindi ambacho yeye ni Waziri wa Ujenzi. 

"Lengo lililokuwa kwenye ilani ya Uchaguzi kwa mwaka jana ilikuwa asilimia thelathini na kitu nyinyi mkafika mpka asilimia arobaini, na sasa hivi mko zaidi ya asilimia 46 sasa nisipowapongeza nitakuwa mtu mbaya wa moyo mbaya. Na mimi na moyo mzuri kweli ndiyo maana nawapongeza wizara pamoja na Tanesco haya matatizo mengine ambayo yanatokea ni kwa sababu tuliingia mikataba ya hovyo huko nyuma, ya kulipia capacity charges ninajua mnayashughulikia na tunajaribu kutafuta pesa za mikopo tulipe haya madeni twende na Tanesco mpya" alisema Rais Magufuli 

Mbali na hilo Rais Magufuli alimsihi Waziri wa Nishati na Madini Prof. Sospeter Muhongo 

"Nilipoteuliwa kuwa Rais sikuona mtu mwingine anayefaa kama Muhongo, nikamrudisha hapa hapa sababu mimi nilipokuwa nikihesabu kilometa za barabara yeye alikuwa anaesabu kilometa za nyaya, kwa hiyo nilifahamu kazi yake na saa zingine ukifanya kazi vizuri unakuwa kama hupendwi pendwi hivi, lakini kwa nini wakupende? Hata mke wako anaweza asikupende siku zingine, wewe chapa kazi" alisisitiza Rais Magufuli 

Rais Magufuli aliendelea kusisitiza kuwa katika maisha ya kila siku huwezi kupendwa na kila mtu 

"Hata ndugu yako anaweza asikupende, saa zingine hata baba yako au hata mdogo wako anaweza asikupende, huwezi ukapendwa na kila mmoja, hata mitume hawakupendwa na wote na wengine walisulubiwa pamoja na kwamba walifanya mazuri. Kwa hiyo Prof. Muhongo wewe fanyakazi tena usihangaike hata kusoma ile mitandao, mimi sisomagi hiyo mitandao achana nayo watandae huko huko wenyewe wewe chapa kazi" alisisitiza Mhe. Rais Magufuli.

JPM Akamilisha Ziara Mikoa ya Kusini, Atua Dar...!!!

$
0
0

Rais John Magufuli amewasili jijini hapa jioni ya jana (Jumapili) baada ya kukamilisha ziara ya kikazi ya siku nne katika mikoa ya Pwani, Lindi na Mtwara.

Rais Magufuli amewasili  katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JKIA) akitokea Mtwara.  

Mara baada ya kuwasili, Rais Magufuli alipokelewa na viongozi mbalimbali akiwemo Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Hashimu Mgandilwa.

Mchakato Awali Utafutaji Mafuta Kuchukua Miezi Mine Zanzibar...!!!!

$
0
0

Hatimaye kazi ya utafutaji wa mafuta na gesi asilia Visiwani Zanzibar inatarajia kuanza wakati wowote kuanzia sasa kwa kutumia ndege maalumu katika maeneo ya nchi kavu na bahari.

Akitoa taarifa ya Serikali jana kuhusu kuanza kwa kazi hiyo, Waziri wa Ardhi, Maji, Nishati na Mazingira wa Zanzibar, Salama Aboud Talib alisema kazi ya awali ya utafutaji itaanza kwa kitalu cha Pemba.

“Taarifa hii inakusudia kuwajulisha wananchi wote wa Unguja na Pemba kuwa hivi karibuni kazi ya awali ya itaanza,” alisema.

Waziri huo alibainisha kuwa utafutaji huo utafanywa na Kampuni ya Bell Geospace Enterprises ya Uingereza ikitumia ndege kukagua miamba iliyoko chini ya ardhi.

Salama alisema hatua ya kwanza ya utafiti itachukua miezi minne na Serikali inawaomba wananchi wasiwe na hofu wakati kazi hiyo ikiwa inaendelea kwa kuwa hakutakuwa na athari zozote.

Kuanza kwa kazi ya utafutaji wa mafuta na gesi asilia kunaanza baada ya Rais wa Zanzibar, Dk Ali Mohamed Shein kutia saini Sheria ya Utafutaji na Uchimbaji wa Mafuta na Gesi Asilia mwezi Novemba, mwaka jana.

Askofu Mokiwa Aaibnishwa Mbele ya Kanisa,Waraka wa Makosa Yake Wasambazwa Kila Usharika..!!!

$
0
0

Waraka wa Askofu Mkuu wa Anglikana nchini, Jacob Chimeledya umesomwa katika makanisa yote ya Dayosisi ya Dar es Salaam ukibainisha makosa yaliyofanywa na Askofu Valentino Mkokiwa na kumtaka kujiuzulu wadhifa wake.

Waraka huo umesomwa kanisa la Mtakatifu Albano leo na mjumbe wa halmashauri ya walei dayosisi hiyo, Helen Mkoma umebainisha kwamba Januari 28 mwaka huu, Askofu Chimeledya aliunda kamati ya kwenda kuzungumza na Askofu Mokiwa wakimtaka ajiuzulu kwa hiari ili kulinusuru kanisa hilo.

Hata hivyo, Askofu Mokiwa aliomba muda wa wiki mbili ili kutafakari suala hilo lakini wiki mbili zimekwisha hajatoa mrejesho wowote huku kukiwa na viashiria vya kwamba hayuko tayari kutii agizo hilo.

Wabunge Upinzani Wamtetea Mwenzao Aliyekosolewa na Rais Magufuli..!!!

$
0
0

Wabunge wa upinzani na wasomi wamekuwa na mawazo kinzani kuhusu maswali na kauli alizotoa Rais John Magufuli juzi mbele ya wananchi wa Somanga dhidi ya Mbunge wa Jimbo la Kilwa Kaskazini, Vedasto Ngombale (CUF).

Ilikuwa ni siku moja baada ya Ngombale kukataa ushauri wa Rais Magufuli wa kumtaka achangie angalau Sh15 milioni kutoka mfuko wa jimbo kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha afya.

Tukio hilo lilitokea eneo la Somanga Wilaya ya Kilwa wakati Rais Magufuli aliposimama kwa muda kuongea na wananchi baada ya kuanza ziara yake katika mikoa ya Pwani, Lindi na Mtwara.

Mhadhiri wa Sayansi ya Siasa, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Richard Mbunda alisema vita ya kupambana na upinzani kwa sasa imekuwa wazi na mwenyekiti wa CCM (John Magufuli) amekuwa akitumia kila nafasi anayoipata kuwamaliza wapinzani.

“Ni mentality (mtazamo) ya mwanasiasa yeyote, Rais Magufuli angetamani majimbo yote yawe ya chama chake, kwa hivyo akipata mwanya kama huo lazima awamalize,” alisema.

Hata hivyo, Mbunda alisema maendeleo ya wananchi hutekelezwa na halmashauri na mbunge kazi yake ni kuchochea wananchi kuanzisha na kushiriki miradi, ikiwamo kushawishi Serikali kupitia Bunge ili kushughulikia changamoto zilizopo.

“Lakini, fedha zilizotolewa na Rais Magufuli pamoja na mtumishi wa halmashauri zimetoka fungu gani?, wametoa mfukoni mwao au ni kodi za wananchi, wangetueleza ili tujue wazi kwa hivyo ni vita ya siasa tu inafanyika,”alisema Mbunda.

Mbunge wa Mikumi, Joseph Haule alisema Rais Magufuli anafahamu utaratibu wa sheria inayosimamia fedha hizo za majimbo, lakini alikuwa na lengo la kumharibia mbunge huyo aonekane hana msaada wowote kwa wananchi wake.

Alitoa mfano akisema katika jimbo lake mwaka 2015/16 alipokea Sh46 milioni ambazo aliwekeza kwenye kero ya mawadati. Licha ya kupunguza kero hiyo, alisema fedha hizo haziwezi kumaliza kero za wananchi katika kata 15 za jimbo lake.

“Fedha zinatolewa kwa kuangalia idadi ya watu na kiwango cha umaskini. Mwaka huu zimepunguzwa tena hadi Sh42milioni na kero bado ni nyingi. Kwa hivyo ni kweli Rais akiendesha siasa za namna hiyo inaweza kutuathiri kisiasa majimboni tukaonekana hatuna msaada wowote kwa wananchi. Lakini ni udhalilishaji ambao sitakubali utokee jimboni kwangu,” alisema Haule maarufu kama Profesa Jay.

Katika mkutano huo, Rais Magufuli alilazimika kuanzisha harambee ya ghafla huku akimtaka Ngombale kuchangia fedha hizo (Sh15 milioni) ambazo ni sehemu ya mfuko wa jimbo baada ya mkazi mmoja aliyepewa kipaza sauti kulalamika kuwa tatizo lao kubwa ni kituo cha afya.

Katika majibizano, mbunge huyo alisisitiza kutochangia kiasi hicho kwa kuwa tayari kamati ya mfuko wa jimbo ilishapanga bajeti katika kata zote 13, hivyo asingeweza kuweka ahadi asiyoweza kuitekeleza. Baada ya hapo Rais Magufuli aliamua kuchangia Sh20 milioni huku akimpiga kijembe mbunge huyo kwa wananchi.

Kutokana na mazingira hayo, Mbunge wa Iringa Mjini, Mchungaji Peter Msigwa alisema fedha hizo ni kidogo na hivyo CCM kupitia Serikali yake inaweza kutumia mwanya huo kujitafutia uhalali wa kisiasa kupitia matatizo ya wananchi majimboni.

“Ni kweli itakuwa ‘threat’ kwetu upinzani endapo ataendelea kufanya siasa hizo chafu, Rais anatumia mbinu hiyo apendwe na wananchi ili baadaye wananchi waone upinzani hatuna lolote,”alisema.

Katibu Mkuu wa zamani NCCR-Mageuzi, Samweli Ruhuza, alisema Serikali ndiyo ina wajibu wa kujenga zahanati na huduma za kijamii na siyo mbunge, hivyo alichokifanya Rais Magufuli ni kutumia udhaifu wa wananchi wasioelewa wajibu wa Serikali.

“Kwanza kauli ile ameitoa kama mwenyekiti wa CCM na siyo Rais, kwa hivyo alikuwa anafanya siasa za kumkomoa mbunge, kuonyesha wabunge wa upinzani hawawezi kusaidia lolote siyo siasa nzuri hata kidogo,” alisema.

Hata hivyo, Mbunge wa Misungwi (CCM), Charles Kitwanga alimtetea Rais Magufuli na kusema mbunge huyo alikuwa na nafasi ya kutoa ahadi kwa wananachi hao, kwa kuwa awamu ya pili ya fedha hizo za mfuko hazijatoka bado.

Alisema kwa kuwa ni mwenyekiti wa kamati ya mfuko wa jimbo, angeweza kutoa ahadi na baadaye kuishawishi kamati hiyo kupeleka fedha hizo Somanga.

“Wabunge wote bado hatujapata awamu ya pili kwa hivyo ajilaumu mwenyewe kukosa ushawishi,”alisema.

Hata hivyo, Kitwanga alisema fedha za jimbo bado haziwezi kumaliza kero za wananchi kulingana na wingi wa changamoto.

fedha za mfuko wa jimbo

Kwa mujibu wa Sheria ya Mfuko wa kuchochea maendeleo ya jimbo (CDCF) namba 16 ya mwaka 2009, fedha hizo hutolewa na serikali kuu katika jimbo kwa viwango tofauti kutokana na vigezo mbalimbali ikiwamo idadi ya watu na kiwango cha umaskini ndani ya jimbo husika.

Madhumuni ya sheria hiyo ni kuhamasisha maendeleo katika majimbo kwa kugharamia utekelezaji wa miradi ambayo imeibuliwa na wananchi katika maeneo yao, lakini haikupata fedha katika Bajeti za Halmashauri.

Kwa mfano, fedha hizo hutumika kukamilisha ujenzi wa shule, kisima au barabara kwa matumizi ya wananchi katika eneo hilo. Aidha, fedha hizo hutolewa kila mwaka katika awamu moja au mbili na huingizwa moja kwa moja katika akaunti ya mfuko inayoratibiwa na Halmashauri.

Kabla ya matumizi ya fedha hizo kupangwa, mbunge wa jimbo husika anaweza kufanya ziara katika Kata akikutana na Baraza la Maendeleo ya Kata (BMK), ambao wanatoa vipaumbele vyao ili kujua ataanzia wapi kugawanya fedha hizo.

Mohammed Ali wa Jicho Pevu Aastaafu Kufanya Habari za Uchunguzi na Kufichua Maovu..

$
0
0

Mwandishi Mahiri wa Habari za Uchunguzi, Mohammed Ali anayefahamika kwa Makala za Jicho Pevu ametangaza kujiuzulu kutoka taaluma ya kufichua maovu ya kiutawala na jamii na kujiunga na siasa.

Mohammed katika mtandao wake wa Twitter ameandika "Kwa miaka 10 mfululizo nimekuwa nikisimama nanyi kuzidisha sauti zenu za kuangaishwa. Sasa ni wakati wangu wa kuwauliza, msimame nami katika harakati zangu za kuwania ubunge wa Nyali kwa tiketi ya ODM". Ameahidi kuwa akitimiza ndoto hiyo atakuwa mshirikishi mkuu wa utawala wa haki kwa Wakenya wote bila ubaguzi.

Kauli ya Rais Magufuli kuhusu Watanzania waliofukuzwa Msumbiji

$
0
0

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli jana tarehe 05 Machi, 2017 amemaliza ziara yake ya kikazi ya siku 4 katika mikoa ya Pwani, Lindi na Mtwara.


Kabla ya kuondoka Mjini Mtwara na kurejea Jijini Dar es Salaam Mhe. Rais Magufuli alifanya mkutano wa hadhara katika Uwanja wa Mashujaa Mjini Mtwara ambapo alisema Serikali ya Awamu ya Tano imejipanga kuhakikisha inasukuma maendeleo ya Mtwara na Lindi kwa nguvu kubwa kwa manufaa ya wananchi.


Alisema Serikali imedhamiria kutilia mkazo juhudi za uendelezaji wa bandari ya Mtwara, ujenzi wa barabara, uimarishaji wa miundombinu ya nishati ya umeme, ujenzi wa viwanda vikubwa na usimamizi mzuri wa shughuli za kilimo ambavyo vitasaidia kukuza uchumi, kuzalisha ajira na kuboresha maisha ya watu.


Mhe. Rais Magufuli aliwapongeza viongozi na wananchi wa Mkoa wa Mtwara kwa mafanikio yaliyopatikana katika soko la korosho lililopita na ameagiza wale wote waliohusika kufuja fedha za wakulima wachukuliwe hatua.


Aidha, Mhe. Dkt. Magufuli alisema Tanzania itaendeleza uhusiano na ushirikiano wake mzuri na nchi jirani ya Msumbiji na ametaka suala la wahamiaji haramu wanaoondolewa nchini humo wakiwemo Watanzania lisikuzwe huku akisisitiza kuwaSerikali haiwezi kuwatetea watu wanaoishi katika nchi nyingine bila kufuata sheria.


Kuhusu Mkoa wa Mtwara kufanya vibaya kielimu, Mhe. Rais Magufuli amewataka wananchi wa Mtwara kubadilika kwani juhudi za Serikali kuwapelekea maendeleo hazitakuwa na maana kama wananchi watakuwa hawana elimu.


“Nimeambiwa hapa watu wanapenda sana disco na ngoma, watoto badala ya kusoma wanacheza disco, hapo tunakwenda pabaya” alisisitiza Mhe. Rais Magufuli.


Mkutano wa Mhe. Rais Magufuli Mjini Mtwara ulidhuriwa na viongozi mbalimbali wakiwemo Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. William Lukuvi, Waziri wa Nishati na Madini Prof. Sospeter Muhongo, Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Prof. Makame Mbarawa, Waziri wa Fedha na Mipango Dr. Philip Mpango, Wabunge na viongozi wa taasisi.



Gerson Msigwa

Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU

Sakata la Mama Wema Sepetu Kushikiliwa na Polisi Kwa Masaa 8 Kwa Madai ya Kutapeli

$
0
0

Mama mzazi wa msanii maarufu nchini, Wema Sepetu ametiwa mbaroni jijini hapa kwa madai ya kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu.


Mariam, ambaye ni mama mzazi wa mrembo huyo wa Tanzania 2006 alifikishwa Kituo cha Polisi cha Oysterbay Jumamosi hi kwa madai ya kujipatia fedha hizo kutoka kwa mfanyabiashara, Alex Msama.


Habari kutoka katika kituo hicho zinadai kuwa Mariam alifunguliwa jalada la taarifa ya polisi Na. OB/RB/3358/2017 na alishikiwa kuanzia saa nne asubuhi mpaka saa 12 jioni alipoandikisha maelezo na kudhaminiwa na watu wawili waliotajwa kwa majina ya Rose Moshi na Martha Mtiko.


Alipoulizwa kuhusu suala hilo, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, Suzan Kaganda alisema hana taarifa na kuahidi kuzungumzia suala hilo leo.


Inadaiwa kuwa Mariam ambaye hivi karibuni yeye na binti yake huyo waliihama CCM na kujiunga na Chadema, alikubali kumuuzia Msama nyumba iliyopo katika Kiwanja 663 Block E, maeneo ya Sinza kwa Sh125 milioni.


“Nyumba hiyo ilikuwa inatakiwa kupigwa mnada na benki ya TIB kwa sababu mama Sepetu alikuwa amemdhamini mtu aliyekuwa amekopa katika benki hiyo, yule mtu aliposhindwa kulipa, watu wa benki wakataka kuipiga mnada,” chanzo chetu kutoka Polisi Osyterbay kilisema jana jioni.


Katika maelezo ambayo yapo kituoni hapo, inadaiwa kuwa Mariam alikubali kumuuzia nyumba Msama ili apate fedha za kuilipa TIB, lakini kwa wakati huo Msama hakuwa na kiasi hicho.


Inadaiwa kuwa wakati Msama akiendelea na mchakato wa kutafuta fedha ikiwa ni pamoja na kufuatilia mkopo kwenye benki nyingine ili ainunue nyumba hiyo, Mama Wema alikuwa akipewa fedha kidogokidogo ambazo zilifika Sh14 milioni.


Hata hivyo inadaiwa kuwa baada ya mama huyo kuona mchakato huo unachelewa aliuza nyumba kwa mtu mwingine bila kumtaarifu Msama, ambaye alijulishwa na dalali.


Jana, wakati wa mahojiano na polisi inadaiwa kuwa Mariam alikiri kupewa Sh8 milioni ambazo zipo kimaandishi na hatambui kuhusu fedha nyingine.


Msama alipopigiwa simu jana usiku alikiri kumshtaki mama huyo Polisi Oysterbay na kusisitiza kuwa anachotaka ni kulipwa haki yake.


“Ni kweli suala hili lipo Polisi kama mlivyosikia, sipendi kulizungumzia sana,” alisema Msama ambaye pia ni mwandaji wa matamasha ya injili.


Mwanasheria Mkuu wa Chadema, Tundu Lissu alithibitisha kushtakiwa kwa kada huyo mpya wa chama chake na kusema aliandika maelezo kuhusu suala hilo na kuachiwa.

Umeshawahi Kufikiria Kupata Gari la Bure bila Kulipa Chochote, Basi hii Kampuni ya Cars From Japan Wanakupa Nafasi Hiyo ... 

Chakufanya ni Kubofya Link hapo chini na Ufate Maelekezo ya Jinsi ya Kuweza Kuwa Mshindi wa Gari hilo..

Imetosha Sasa, Mwacheni Makonda- Jacqueline Wolper

$
0
0

Muigizaji wa filamu nchini, Jacqueline Wolper amemkingia kifua mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda, akiwataka watu kuacha kumwandama kwa kashfa yake ya kufoji vyeti pamoja na kumtukana mtandaoni.


Kwa wiki kadhaa sasa, Makonda amekuwa akiandamwa mtandaoni kutokana na tuhuma kuwa jina analotumia si lake, na kwamba lake ni Daudi Bashite. Jumapili hii kumesambaa video mtandaoni ikimuonesha mkuu huyo wa mkoa akilia kwa uchungu kanisani baada ya kuzungumza na mchungaji akimbembeleza.


“Nimevaa kiatu chake kimenibana mpaka kinataka kunipasua kisigino,” ameandika Wolper kwenye Instagram.


“Jamani wa Tanzania tuwe na utu, acheni kumtukana huyu kaka daaaah hivi ni nani ambae yupo perfect mpk aanze kumtukana kaka wa watu jmn. Nimepost nikiwa km binadam wa kawaida ambae nina moyo!muhurumieni kaka watu acheni Mungu awe muhukumu basi,” ameongeza.

Umeshawahi Kufikiria Kupata Gari la Bure bila Kulipa Chochote, Basi hii Kampuni ya Cars From Japan Wanakupa Nafasi Hiyo ... 

Chakufanya ni Kubofya Link hapo chini na Ufate Maelekezo ya Jinsi ya Kuweza Kuwa Mshindi wa Gari hilo..

Breaking: Mbunge Tundu Lissu akamatwa na Polisi akitoka mahakamani

$
0
0

Jeshi la Polisi nchini linamshikilia Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu baada ya kuachiwa huru na Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu.


Lissu aliachiwa leo asubuhi na Hakimu Mkuu Mkazi, Huruma Shahidi baada ya upande wa Jamhuri ukiongozwa na Wakili Paul Kadushi kuwasilisha hati ya kuondoa shtaka hilo.


Kadushi aliwasilisha hati hiyo chini ya kifungua namba91 (1) cha makosa ya jinai akionyesha DPP hana haja ya kuendelea na kesi, mahakama ikaridhia na kumuachia.


Muda mfupi baada ya kuachiwa na kutoka nje ya mahakama alikamatwa tena na askari waliokuwapo mahakamani hapo na kupelekwa Kituo Kikuu cha Polisi.


Lissu alikuwa anashtakiwa kwamba Januari 11, mwaka huu katika kampeni za uchaguzi jimbo la Dimani aliwashawishi watu wasiridhike na wawe na nia ovu dhidi ya utawala.

Wema Sepetu Adai Kutishiwa Kuuawa

$
0
0

Mwigizaji  na mrembo wa taji la Tanzania mwaka 2006 Wema Sepetu, amedai anapokea vitisho vya kupotezwa kama ataendelea na msimamo wake wa kuitumikia Chadema.


Wema amesema yeye hatishwi na chochote, ameshaamua na hakuna mtu yeyote atakaebadili mawazo yake kwa kuwa anachohitaji ni amani ya moyo wake na kuwa huru kwani alikokuwa aliona nchi ilikuwa inaenda kubaya.


“Ninatishiwa sana, napigiwa simu na kutumiwa  ujumbe mfupi wa maneno kwenye akaunti zangu na kwenye mitandao ya kijamii.


“Mimi siogopi, nimeshaamua na hakuna wa kunizuia kwa hilo, kwani tangu nimeingia katika chama hiki nina amani ya moyo na ninahisi nimetua mzigo mzito  niliokuwa nimeubeba,” amesema Wema.


Amedai kuwa baadhi ya vitisho anavyopata ni matusi ya nguoni ambapo anaweza kupigiwa simu na kutukanwa, wengine kumtumia ujumbe mfupi wakidai watampoteza lakini anauhakika anayeweza kupoteza maisha yake  ni Mungu.


Amesema anajua amepata maadui ila anauhakika ni wachache sana kwani wengi wanamuunga mkono na ukizingatia watu wake wa karibu  wote wako naye bega kwa bega hivyo hana sababu za kuogopa na anauhakika yuko kwenye chama makini kinachojua nini maana ya demokrasia.


“Hakuna mtu muhimu kama mzazi wako kama anakupa sapoti ya kutosha basi hakuna mwingine atakayeweza kuzuia hilo, nashukuru wamejua nini ninakihitaji na ninataka kuonyesha nini nilichokuwa nacho ambacho nilikokuwa hawakukiona,”amesema Wema Sepetu.


Kwa sasa Wema  yuko katika ziara ya kutambulishwa  mikoa yote kwa wanachama na wapenzi wa Chadema na jana ameanzia Arusha kumtia moyo Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema, anayekabiliwa  na kesi ya uchochezi.
Viewing all 104694 articles
Browse latest View live




Latest Images