Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104712 articles
Browse latest View live

Julius Mtatiro na Lupumba Katika Vita Nyingine CUF

$
0
0

Mwenyekiti wa kamati ya uongozi CUF, Julius Mtatiro amesema Prof. Lipumba hana uwezo wa kumteua Katibu Mkuu hata kama nafasi hiyo angekuwa nayo kama zamani.
Pia amedai hawezi kufukuza Wakurugenzi kwani hutenguliwa na Mwenyekiti kwa kushauriana na Naibu Mwenyekiti na wote hao hawapo CUF kwa sasa.

CUF ya Maalim Seif Kuiburuza CUF ya Prof.Lipumba Mahakamani..!!!!

$
0
0

Bodi ya Wadhamini ya Chama cha Wananchi (CUF ), imefungua kesi ya madai dhidi ya wanachama wake nane akiwemo Naibu Katibu Mkuu, Magdalena Sakaya

Kesi hiyo imefunguliwa jana katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu ikitaka wanachama hao wasijihusishe na harakati  zozote za chama hicho.

Mbali ya Sakaya ambaye pia ni mbunge wa Kaliua mkoani Tabora, wadaiwa wengine ni Thomas Malima, mbunge wa Mtwara Mjini,Mafta Nachumu, Omar Mhina Masoud, Abdul Kambaya, Salama Masoud, Zainabu Mndolwa na Jafari Mneke.

Maombi hayo mbayo yametajwa mbele ya Hakimu Mkazi, Wilbard Mashauri yamewasilishwa na Wakili wa bodi, Hashim Mziray na yamepangwa kusikilizwa kesho.

Katika maombi hayo yaliyopewa namba 1 ya mwaka 2017, bodi inaiomba mahakama kutoa zuio kwa wadaiwa kutojihusisha katika masuala yeyote yanayohusiana na chama hicho.

Mbali ya maombi hayo, pia Wakili Mziray amewasilisha maombi madogo ya kuiomba mahakama kuwaamuru wadaiwa wasijihusishe na mikutano ya chama hicho.

Aidha, Mziray aliomba maombi yao madogo yasikilizwe kwa upande mmoja wa wadai tu kwa kuwa wamechelewa kuwapatia nyaraka za madai yao wadaiwa.

"Mheshimiwa tunaomba tusikilizwe upande mmoja ukizingatia maombi yameletwa chini ya hati ya dharula na kwa mujibu wa sheria mahakama hii... inayo mamlaka ya kufanya hivyo".

Hakimu Mashauri alisema anakubaliana na upande wa wadai na maombi hayo yatasikilizwa kesho mahakamani hapo.

Hatua ya Bodi ya CUF, kukimbilia mahakamani inakuja ikiwa ni siku moja baada ya upande unaomuunga mkono Katibu Mkuu wa chama hicho, Maalim Seif Shariff Hammad kupinga uteuzi wa Mwenyekiti wa chama hicho, Profesa Ibrahim Lipumba.

Uteuzi wa Profesa Lipumba ambao unapingwa ni ule alioufanya Machi 6, mwaka huu baada kuwaondoa katika nafasi zao, Mkurugenzi wa Mipango na Uchaguzi, Omar Ali Shehe.

Mkurugenzi wa Habari, Uenezi na Mahusiano na Umma, Salim Abdull Bimani, Mkurugenzi wa Fedha na Uchumi, Abdullah Bakar Hassan.

Wengine ni Pavu Juma, Naibu Mkurugenzi wa Haki za Binadam na Sheria, Mahmoud Ali Mahindo na Katibu wa Jumuiya ya Vijana, Yusuph Salim.

Mashabiki Wamtaka Tunda Kuheshimu Ujauzito..!!!

$
0
0

Muuza nyago kwenye video za mastaa wa Bongo Fleva, Tunda Sebastian ambaye amekuwa gumzo baada ya jina lake kuwa katika orodha ya awamu ya pili ya wafanyabiashara, watumiaji na wasafirishaji wa unga iliyotwaja na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda, anadaiwa kuwa mjamzito na hajisitiri.

Mashabiki wamemtaka staa huyo ajisitiri kwani mavazi yake kwa sasa yanalionesha tumbo lake ambalo limeanza kuwa kubwa.

“Hatukatai kama Tunda ni staa na tunamfatilia sana ila ajisitiri sana bwana kitumbo ndiii”, alimaliza shabiki huyo huku akiomba kutoandikwa jina lake

Donald Trump Kufanya Mazungumzo na Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta...!!!

$
0
0

Rais Donald Trump atazungumza na Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta hivi karibuni kwa njia ya simu. Mazungumzo yao yatakuwa ya kwanza tangu rais huyo wa Marekani apate ushinda katika uchaguzi mkuu uliofanyika mwishoni mwa mwaka jana.

Uhuru Kenyatta atakuwa rais wa nne wa Afrika kuzungumza na rais huyo kutoka Marekani, Taifa lenye uwezo mkubwa duniani.

Kati ya marais wa Afrika aliozungumza nao kwa njia ya simu ni Rais wa Misri Abdel Fatah al Sisi, Rais wa Afrika Kusini Jacob Zuma na Rais wa Nigeria Muhammadu Buhari .

Miongoni mwa maswala wanayotarajiwa kugusia ni swala la usalama, Somalia na ukame unaendelea kukumba eneo zima la Afrika Mashariki.

Ngoma Huyoo Msimbazi,Wakala Wake Afunguka Mchezo Mzima Jinsi Ulivyo..!!!

$
0
0

HII unaweza ukaihesabu kama ni vita mpya baina ya mahasimu wa soka nchini, Simba na Yanga.

Hali hiyo inaletwa na mkakati wa siri ambao Dimba imeugundua ambapo vigogo wa timu ya Simba wameamua kuingia vitani kumshawishi na kisha kumsajili mshambuliaji wa kimataifa wa Yanga, Donald Ngoma, muda mfupi baada ya kumaliza mkataba wa kuitumikia timu hiyo ya Jangwani.

Ngoma, ambaye ni raia wa Zimbabwe, anamaliza mkataba wake sambamba na kuhitimishwa kwa michuano ya Ligi Kuu Tanzania Bara Mei, mwaka huu.

Habari za uhakika ambazo Dimba limezipata kutoka kwa mmoja wa viongozi waliokuwamo katika kamati ya usajili zilisema kwamba, mchezaji huyo anapigiwa mahesabu na klabu hiyo ya Msimbazi kutokana na uwezo wake anaoendelea kuuonyasha katika klabu ya Yanga.

Mjumbe huyo alibainisha kuwa, hata hivyo, klabu yake inamtaka straika huyo siyo kwa ajili ya kucheza michuano ya Ligi Kuu, bali wanamtaka kwa ajili ya kuiongezea nguvu timu hiyo katika michuano ya kimataifa, ambapo wenyewe Simba wanaamini watatwaa ubingwa msimu huu na hivyo watakuwa wakishiriki michuano hiyo hapo mwakani.

Mjumbe huyo amekwenda mbali zaidi na kudai kwamba, tayari dau la mshambuliaji huyo limeshawekwa mezani ambapo Wekundu hao wa Msimbazi watatakiwa kulipa kiasi cha Dola za Kimarekani 150,000, sawa na Sh milioni 300 za Kitanzania ili kuweza kumnasa Mzimbabwe huyo.

“Kiasi hicho tunaweza kutoa, lakini hii itawezekana endapo tutapata nafasi ya kushiriki michuano ya kimataifa hapo mwakani,” alisema.

Wakala wa mchezaji huyo, Jonas Tiboroha, alikiri kupigiwa simu na kigogo mmoja wa Simba, ambaye hakutaka kuweka wazi jina lake na kuomba taratibu za kumsajili mchezaji huyo.

Tiboroha alisema, licha ya Simba, pia klabu za Mamelodi Sandown, Malaga FC za Afrika Kusini, Zesco ya Zambia, Al Ahly ya Misri zimeonyesha nia ya kumhitaji mshambuliaji huyo, lakini pia klabu yake ya sasa, Yanga nao wameshaonyesha nia yao ya kumbakiza mshambuliaji wao huyo ambaye hadi sasa ameshaipachikia timu yake hiyo mabao 8 katika michuano ya Ligi Kuu.

Alisema, Yanga wameweka ofa ya Sh milioni 120, kwa ajili ya mkataba mpya wa Mzibambwe huyo baada ya ule wa kwanza kumalizika.

Katika hatua nyingine, vigogo karibu wote wa klabu ya Simba wiki iliyopita walikutana kwa siri katika sehemu nyeti inayofahamika kwa jina la Pentagoni, iliyopo maeneo ya daraja la Salenda, katikati ya jiji la Dar, ambapo pamoja na mambo mengine, walijadili na kuweka mikakati mbalimbali ya kuhakikisha wanachukua pointi zote 18 zilizobaki ili waweze kuchukua ubingwa msimu huu.

Vigogo hao wa kamati ya utendaji pamoja na wadau wengine, wakiongozwa na Rais wa klabu hiyo, Evance Aveva, wamekuwa wakikutana mara kwa mara katika kipindi hiki ambacho timu yao iko kileleni katika msimamo wa ligi, huku wakielekea kusafiri kwenda kanda ya ziwa kwa ajili ya kucheza mechi tatu ambazo ndizo zitakazotoa mwanga wa timu hiyo kutwaa ubingwa au la.

Hata hivyo, Aveva aliliambia Dimba kwamba, kukutana kwao ni kawaida kama viongozi na wadau kwa ajili ya kujadili maendeleo ya timu yao, lakini bado kikosi chao hicho kitakuwa na mikakati ya kifundi inayoendelea kuandaliwa na benchi la ufundi chini ya kocha wake mkuu, Joseph Omog.

“Kocha ndiye anayejua masuala ya ufundi, ukisikia sisi tukikutana ujue tunapanga mikakati mingine, maana klabu si wachezaji pekee, bali na viongozi pia wana majukumu ya kuhakikisha mambo yanakwenda sawa.

Naye Kocha Mkuu wa Simba, Joseph Omog, amesema katika wakati wowote aliokuwa akiifundisha Simba, kipindi hiki ndicho kinachomuweka katika wakati mgumu, hasa kutokana na umuhimu wake.

Kocha huyo aliliambia Dimba kwamba, anafahamu mechi zilizobaki ni ngumu, hivyo miongoni mwa mambo muhimu anayotakiwa kuyahakikisha ni kuwaweka vijana wake katika hali ya tahadhari ili wasijiachie wakadharau mechi zilizosalia.

Endapo ratiba haitabadilika Simba itakipiga na Kagera Sugar Aprili 4, mwezi ujao na kisha itakwenda jijini Mwanza kukipiga na Toto Africans na kisha itacheza na Mbao, mechi ambazo kocha huyo alisema ni ngumu na zinazohitaji mikakati ya nguvu.

Mpaka sasa Simba ndiyo inayoongoza Ligi Kuu ikiwa na pointi 55, ikifuatiwa kwa karibu na watani wao wa jadi, Yanga, iliyofikisha Pointi 53, huku zote zikiwa zimeshacheza michezo 24.

Credit - Dimba

Za Kunyapia Nyapia... Wema Sepetu ni Mjamzito,Adaiwa Kuifanya Siri Lakini Ubuyu Wote Waanikwa Hadharani...!!!

$
0
0

STAA wa filamu za kibongo, Wema Sepetu ambaye alikuwapo mkoani Arusha kwa ajili ya kumsabahi Mbuge wa Arusha Mjini, Godbless Lema, anadaiwa kuwa mjamzito kwa sasa.

Uvumi huo umeanza baada ya kuzagaa picha za mrembo huyo aliyewahi kutwaa taji la Miss Tanzania mwaka 2006 kwenye kurasa mbalimbali za mitandao ya kijamii.

Picha hizo ambazo zilimwonyesha Wema akiwa na tumbo lenye ukubwa kiasi, zilizua shangwe kwa mashabiki wake wakiamini mrembo huyo huenda akawa na ujauzito.

Pamoja na maswali mengi ya mashabiki wake, Wema hakuweza kujibu chochote kuhusu madai hayo na kuwafanya wale wote wanaomuunga mkono, yaani ‘Team Wema’ kuendelea  wakizituma picha hizo kwenye kurasa zao za mitandao ya kijamii.

Lakini jambo kubwa lililozidi kuwachanganya mashabiki wake ni ujumbe tata wa Idrisa Sultan ambaye ni mpenzi wa zamani wa Wema ambaye aliandika: “Pigo moja tu, mbuyu chini.” Ujumbe uliozidi kuwaweka njiapanda mashabiki wa mkali huyo wa filamu.

Wema amekuwa kwenye kilio cha muda mrefu kutafuta mtoto, ambapo amewahi kubeba ujauzito wa mapacha wawili lakini haukuweza kudumu baada ya kutoka.

Alikiba na Kolabo ya Justin Bieber, Amefumguka haya..

$
0
0


Muimbaji mahiri wa muziki Alikiba amefunguka kwa kukanusha taarifa ambazo zilizagaa kwenye mitandao ya kijamii kuwa ana mpango wa kufanya kolabo na Justin Bieber.


Akiongea na mtangazaji wa JEMBE FM JJ akiwa Las Vegas Marekani, Alikiba alidai taarifa za kwamba ana mpango wa kufanya kolabo na Justin Bieber zilitungwa na mashabiki wake wa muziki.


“Ni mashabiki waliamua kuzusha, kwa hiyo ni vitu vya uzushi havina maana,” alisema Alikiba.


Pia muimbaji huyo alidai hana mpango wakufanya kolabo na Wizkid kwa sasa lakini ukifika muda na akipata nafasi anaweza kufanya hivy

Joket Atoa ya Moyoni Baada ya Ali Kiba Kumkana Hadharani...!!!

$
0
0

SIKU chache baada ya msanii wa kizazi kipya, Ali Kiba, kudai kuwa anamchukulia mwanamitindo Jokate Mwegelo kama rafiki yake, mrembo huyo ameibuka na kusema huenda aliteleza kutoa kauli hiyo.

Jokate alitoa kauli hiyo mwishoni mwa wiki hii alipokuwa anahojiwa kwenye kipindi cha Clouds 360 kinachorushwa na Clouds Tv, ambapo mrembo huyo alisema kauli hizo huenda zimetolewa kimakosa.

“Sifikirii sana maana mimi ni mtu ‘positive’ nataka niamini hawakumaanisha, sasa sijui waliteleza au walikosea,” alisema mrembo huyo aliyewahi kushika nafasi ya pili kwenye shindano la Miss Tanzania mwaka 2006.

Mrembo huyo alikwenda mbali kwa kusema: “Unajua katika maisha huwezi kumlazimisha mtu kuona thamani yako, wanasema tenda wema nenda zako mengine ni matokeo na sipendi kulizungumzia sana maana siku hizi watu wanapenda sana kuokota maneno wanayatengeneza wanavyojua wao.”

Kiba na mama yake walimkana Jokate kwenye sherehe ya kumpongeza msanii huyo baada ya kurudi kutoka Afrika Kusini na tuzo ya MTV.

Tuzo hiyo ambayo awali alitangazwa Wiz Kid kwamba ndiye aliyeshinda lakini baadaye uongozi wa MTV wakakiri mshindi halali alikuwa ni Ali Kiba na kuahidi kumpa tuzo yake nchini Afrika Kusini.

Duh..Noma Sana ... Diamonda Afanya Kufuru Nyingine,Baada ya Marry Me ya Neyo,Mzigo Huu Ndio Unaofuata..!!!!

$
0
0

NYOTA wa muziki wa kizazi kipya nchini, Nassib Abdul ‘Diamond Platinum’, amesema wakati wowote kuanzia sasa ataachia albamu yake mpya inayokwenda kwa jina la ‘Nothing But Bongo Fleva’.

Diamond ambaye kwa sasa anatamba na kibao chake kipya cha ‘Marry Me’ alichoshirikiana na staa wa Marekani, Neyo amesema albamu yake hiyo itakua na nyimbo zaidi ya 10 ikijumuisha mpya na zile za zamani.

Katika hatua nyingine, Diamond amesema wanaandaa kolabo ya pamoja na wasanii wote wa kundi la Wasafi ambayo itatoka hivi karibuni.

Barnaba Afunguka Juu ya Kumfunika Diamond Kwa Show za Nnje ya Nchi..!!!

$
0
0

Muimbaji wa muziki Barnaba, amedai hana mpango wa kufanya kolabo na msanii wa nje kwa sasa kwa kuwa bado anajipanga vizuri kisanaa huku akidai yeye ni mwanamuziki anayeongoza kwa kufanya show nyingi za nje ya nchi.

Alisema si kwamba anaogopa ila kwa upande wake anaona bado anahitaji kujipanga zaidi ili atakapoamua kufanya kolabo yoyote iwe kubwa kama alivyorekodi na msanii wa Uganda, Jose Chameleone.

“Muziki hautaki kubahatisha, mimi ni mwanamuziki ninayeongoza kwa kufanya shoo nyingi nje ya nchi, lakini sijataka kumshirikisha msanii yeyote wa nje kwa kuwa muziki wangu bado nauandaa, unaenda kidogo kidogo na nikiona umefika ninakotaka nitafanya hivyo,” Barnaba aliliambia gazeti la Mtanzania.

Alisema kufanya hivyo hakumaanishi yeye ni msanii mdogo, ila katika maisha kila kitu lazima ufanye kwa malengo na baada ya wimbo wa ‘Love boy’ anatarajia kuachia wimbo wake mpya wa ‘Alone’

Lema Kuachia Waraka Mzito kwa Rais Magufuli..!!!!

$
0
0

Waraka wa Mbunge wa Arusha Mjini (CHADEMA), Godbless Lema kuachiwa juma lijalo. Waraka huo, niliopata bahati ya kuuchungulia, unabeba mambo muhimu yahusuyo hasa haki za binaadamu. Mambo hayo yalionwa na kusikiwa na Lema alipokuwa Mahabusu Kisongo kwa takribani miezi minne.

Waraka huo maalum kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania pamoja na viongozi wengine,unaibua pia njama mbalimbali zinazofanywa na wakandamizaji wa haki za binaadamu. Lema pia anaanika simulizi zenye kuliza za mahabusu wanaopigwa danadana kwenye kesi zao na kuwafanya wasitendewe haki.

Lema ameandika. Lema anataka Rais ajue. Anataka ujumbe umfikie Rais na marekebisho yafanyike. Lema ameapa kuendelea kusema ukweli na kuusimamia kwa namna yoyote iwezekanayo. Lema hatanii, anasema na kufanya kweli. Kaeni mkao wa kula kwa Waraka huo wa Mbunge Lema kwenda kwa Rais.

RC Makonda Ameyasema Haya Leo March 8

$
0
0

RC Makonda ameyasema haya leo March 8

Kupitia ukurasa wake wa Instaram Makonda yafuatayo...

"Asilimia kubwa ya WANAWAKE ni aina ya watu waliokuza watoto wao katika mazingira magumu, mateso, machungu na kunyanyasika kwa hali ya juu mara nyingine, na walikubali kupitia hayo ili tu MTOTO ASIMAME na kuwa mtu atakaejitegemea na kutegemewa siku moja, LAKINI kuna kundi kubwa lililodhamiria kwa makusudi kabisa kuwarudisha nyuma kwenye mategemeo yao hayo, kundi lililopanga kwa makusudi kabisa kuangamiza vijana wao kwa ajili ya maslahi yao binafsi, kundi lisilojali kwa namna yoyote struggle za kina MAMA hawa katika kuwakuza watoto wao, kundi linalowaharibu huku wakiwa WANAJUA kabisa athari kwa TAMAA TU ya mali za haraka. Kundi la WAUZAJI WA MADAWA YA KULEVYA.


Siku ya leo tunapoadhimisha SIKU YA WANAWAKE DUNIANI napenda kuchukua fursa hii kuwahakikishia kina MAMA wote na wananchi wa mkoa wangu wa DAR ES SALAAM kuwa sitakubali watoto mliowabeba matumboni mwenu miezi tisa na kuwalea kwa tabu wafe kwa MATUMIZI YA MADAWA YA KULEVYA. Naomba tuungane na Muheshimiwa Rais wetu Magufuli kuhakikisha tunashinda dhudi ya wauaji na wanyinyaji wanaofanya biashara haramu ya madawa ya kulevya. Kama uliweza kumtunza tumboni miezi tisa basi usikubali mtoto wa mwingine akakarisha matumaini yako, mlinde mwanao ili ule matunda ya uzao wako.."

Nape Aviambia Vyombo vya Habari Kutohofia Kuikosoa Serikali

$
0
0

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nnauye, amevitaka vyombo vya habari kuwa huru huku akisema kuwa serikali haina uadui hivyo vyombo hivyo havipaswi kuigopa kwa sababu imebeba dhamana kubwa ya kuliongoza taifa.

Amezungumza hayo katika mkutano na wahariri na wamiliki wa vyombo vya habari Dar es Salaam Jumanne hii na kusema vyombo vya habari vinatakiwa kuwaleta pamoja Watanzania katika uchumi wa viwanda ili kufikia malengo ya Dira ya Taifa ya Maendeleo.

“Serikali ni rahisi sana kujisahau, ama inaweza ikaziba masikio, hivyo ni lazima pawepo na ‘very strong media’ zitakazofanya kazi ya kuiambia serikali kwa namna fulani ya heshima, lakini ujumbe unafika.”

“Najua kuna hofu na lazima tuchukue hatua tuiondoe, kwa sababu ikiendelea kuwepo watu watabaki na mafundo fundo na si vizuri katika nchi. Hivyo muwe huru, Serikali si adui, nguvu yenu ni kubwa na msiposhiriki kikamilifu tutawaacha Watanzania wengi nyuma,” alisema Nape.

Flora Mbasha Adaiwa Kupigwa Mimba

$
0
0
WAKATI vikao vya harusi yake vikiwa vinaendelea kusubiri kufunga ndoa Aprili mwaka huu, nyota mkubwa wa nyimbo za Injili, Madame Flora, ambaye ni maarufu zaidi kama Flora Mbasha, anadaiwa kupata ujauzito, Risasi Mchanganyiko limetonywa.


Flora Mbasha
Chanzo makini kilicho karibu na mwimbaji huyo ambaye ndoa yake ya kwanza na mumewe Emmanuel Mbasha ilivunjwa na mahakama hivi karibuni, kilisema tayari ana ujauzito unaokadiriwa kuwa na umri kati ya miezi miwili au mitatu, ambao umeanza ‘kumsumbua’ kiasi cha kushindwa kufanya shughuli zake vyema.

“Hivi mnajua kama Flora (Mbasha) ni mjamzito? Basi kwa taarifa nilizonazo ni kuwa wakati vikao vya ndoa yake inayotarajiwa kufungwa mwezi ujao vikiendelea, imebainika kuwa ni mjamzito, jambo ambalo limezua minong’ono kwa baadhi ya waimbaji wenzake wakihoji imekuwaje mtumishi huyo wa Mungu kubeba mimba kabla ya ndoa?” kilisema chanzo hicho.


Flora Mbasha
Kuhusu ndoa yake hiyo, chanzo hicho kilisema hakuna mabadiliko juu ya shughuli hiyo, isipokuwa gumzo kubwa miongoni mwa waimba Injili ni suala hilo la ujauzito. Risasi Mchanganyiko lilimtafuta mwimbaji huyo ambaye alipopatikana na kuulizwa juu ya suala hilo, hakukataa wala kukubali, isipokuwa alisema kama ni kweli jambo hilo lipo, basi ni kitu cha kheri.

“Mimi sijui unachokizungumzia kinaanzia wapi, lakini kama ni kweli hivyo unavyosema, basi ni jambo la kheri kwa sababu siku zote watoto ni Baraka,” alisema kwa kifupi na kumwambia mwandishi ni vyema kama wataongelea kuhusu albamu yake ijayo.

“Nipo katika maandalizi ya mwisho ya albamu yangu mpya, nategemea kuizindua wakati wa Pasaka mwaka huu, hii itakuwa ni albamu yangu ya sita ambayo itakuwa tayari wakati wowote kuanzia sasa,” alisema.

Baada ya kuachana na Emmanuel Mbasha, Madame Flora alikuwa akitoka kimapenzi na kijana anayejulikana kwa jina moja la Peter anayedai kuzaa mtoto na mwimbaji huyo. Hata hivyo, uhusiano huo ulivunjika siku chache zilizopita ndipo zilipopatikana habari za kutaka kuolewa na mwanaume mwingine anayetajwa kwa jina la Daudi inayotarajiwa kufungwa Aprili 30, mwaka huu.

Vanessa Mdee Akamatwa na Polisi, Apelekwa kwa Mkemia Mkuu

$
0
0
Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam linamshikilia mwanamuziki Vanessa Mdee maarufu Vee Money kwa tuhuma za kujihusisha na biashara haramu ya dawa za kulevya.

Akizunguzumzia taarifa hiyo, Mwanasheria wa mwanamuziki huyo, Amin Tenga amethibitisha kutokea kwa tukio hilo ambapo amesema kuwa Vanessa alijisalimisha mwenyewe katika kituo cha polisi kama alivyoagizwa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam wakati akitaja majina ya watuhumiwa wa dawa hizo mapema mwezi uliopita.

Vanessa ni miongoni mwa watu waliotajwa katika orodha ya watuhumiwa wa dawa za kulevya, lakini hakuweza kuripoti kwa wakati sababu alikuwa nchini Afrika Kusini kikazi.

Baada ya kujisalimisha, Jeshi la Polisi lilifanya upekuzi nyumbani kwake kabla ya kumpeleka kwa Mkemia Mkuu wwa Serikali kwa ajili ya uchunguzi zaidi.

Jeshi la Polisi hadi sasa halijatoa taarifa kuhusu tukio hilo na kama walikuta ushahidi wowote nyumbani kwa mwanamuziki huyo.

Historia ya Paul Makonda Iwasisimue Vijana Wanaokutana na Changamoto Katika Maisha

$
0
0

Rai yangu, Historia ya Paul Makonda Iwasisimue (inspire)Vijana wanapokutana na changamoto kwenye maisha na kujifunza namna ya kushinda.

Juzi hivi nilipata kumsikiliza Mh Paul Makonda akielezea historia ya maisha yake iliyojaa changamoto nyingi. Clip hiyo ikanikumbusha maneno aliyoniambia Paul Makonda mwaka 2009 wakati tunakwenda Dodoma. Alivyoeleza kwenye clip ndivyo alivyonisimulia siku ile tukiwa safarini kwenda Dodoma. Siku ile alipokuwa akinisimulia aliishia kulia kwa uchungu. Pia niliumia sana.

Alipokuwa akinisimulia, mara kwa mara Paul Makonda alisema "lakini sikukata tamaa niliendelea kumtumaini Mungu". Hakukata tamaa na ndiyo sababu ya yeye kufika alipofika.

Kuna picha inaonyeshwa na kudaiwa hapo ndipo alipozaliwa. Sehemu duni. Kuna picha zinaonyeshwa Paul akiwa kwenye mazingira duni, kuna picha zinamwonyesha akilia, lengo ni kumdhalilisha.
Rejeeni historia za watu maarufu duniani leo, wengi walikuwa watu wa kawaida na huenda duni lakini walikabiliana na changamoto bila kukata tamaa na wakashinda. Mmoja ni Baraka Obama.

Obama kwao ni Kenya. Na alipokuwa anagombea mara ya kwanza republicans walitoa picha ya Obama akiwa na bibi yake kijijini kwenye nyumba duni, lengo wamdhalilishe. Obama hakukata tamaa na hatimae akawa rais wa Marekani ambayo yalikuwa makusudi ya Mungu.

Hakuna binaadam amayepanga azaliwe wapi na wazazi wapi. Watu wengi, kwa kukabiliana na changamoto katika maisha hufanikiwa kubadili maisha yao na kufikia mafanikio makubwa, hasa kwa kutokata tamaa na kumtumaini Mungu. Vijana nilidhani mngejifunza hilo kwa Paul Makonda badala ya kukejeli.

Kingine ambacho nimeona nikiandike, mimi ukweli nashangaa kuona wengi wanaomdhihaki Paul Makonda siyo wapagani. Ni watu wenye dini, tena dini maarufu. Inasikitisha sana.

Kuwa na dini na kumjua Mungu ni vitu viwili tofauti. Unaweza kuwa kiongozi wa dini lakini humjui Mungu wa Kweli. Tabia moja kuu ya Mungu ni upendo. Mungu ni pendo. Pendo huvumilia, hustahimili, nk. Hivyo, tabia hii inatakiwa kudhihirika kwa watumishi wa Mungu.

Yesu Kristo alimfunua au alidhihiridha upendo wa Mungu alipokuwa msalabani akiteseka ili aukomboe ulimwengu. Akiwa msalabani alisamehe, hakulaani. Alipnyesha upendo wa Mungu. Alipotukana na kudhihakiwa hakurudidha mashambulizi bali alibariki. Aliposingiziwa, hakuwatisha waliomsingizia bali aliwaombea. Yesu Kristo alitoa pepo na kuyaelekeza apepo yaende kwa nguruwe, hakuyapeleka kwa binaadamu aliokuja kuwaokoa.

Lakini hali inavyoonekana sasa inasikitisha. Hilo nalo tujifunze.

Vijana wengi wanaangamia kwa kutumia madawa ya kulevya. Bila hatua madhubuti kuchukiliwa, ninahofu inawezekana Tanzania ikatawaliwa tena. Tena kirahisi tu. Hapatakuwa na rasilimali watu wenye kuwajibika na kulilinda Taifa hili.

Paul Makonda kathubutu, vijana na watanzania kwa ujumla, tuache itikadi ya vyama vya siasa tuunge mkono juhudi za kupiga vita madawa ya kulevya kwani madawa ya kulevya yanalingamiza taifa.

Ikiwa Leo ni Siku ya Wanawake Duniani:Wanawake Mombasa Watembea Uchi Kuhinikiza Jambo Hili..!!!

$
0
0

WAKATI dunia ikiadhimisha Siku ya Wanawake leo, akina mama katika Kaunti ya Mombasa, wametishia kuandamana uchi iwapo Naibu Gavana, Hazel Katana, ataendelea kutoheshimiwa.


Wamesema Katana anakandamizwa na watu wasiojulikana walioko katika Serikali ya Kaunti ya Mombasa kwa vile ni mwanamke.
Zaidi ya kina mama 200 waliandamana juzi katika bustani ya Uhuru wakimtaka Rais Uhuru Kenyatta aingilie kati siasa za Mombasa.


“Katika kipindi hiki cha kuelekea Siku ya Kimataifa ya Wanawake, tutaandamana uchi wa mnyama, hatuwezi kukubali mama yetu aendelee kudharauliwa eti ameiba viti vilivyozeeka. Kama alikuwa anataka kuiba angeiba vitu vya maana,” alisema Asha Mwidani.
Walisema tangu mwenzao ajiengue kutoka Chama cha ODM na kwenda Jubilee ambako atawania kiti cha useneta, amekuwa akikumbwa na misukosuko na dharau kutoka kwa wafanyakazi wa kaunti kutokana na jinsia yake.


Wakibeba mabango yanayomtaja Katana, kina mama hao walisema wanasiasa wanawake wanapaswa kuheshimiwa na wanaume.
“Katana anapaswa kuheshimiwa kama viongozi wengine wa kiume. Kama gavana hayupo, Katana anapaswa kuchukua nafasi yake ya usimamizi wa shughuli za kaunti, lakini katika Serikali hii hilo ni ndoto,” alisema mama huyo mkazi wa Kingorani.


Alidai watu kadhaa katika kaunti hiyo ambao hakuwataja, walibeba viti kisha baadaye wanamlaumu Katana.
“Kiti anachokalia Katana ni moto sana, joto la siasa limejaa, siasa si uadui jamani. Tutatembea uchi mpaka kieleweke, iwe mara ya mwisho mama yetu kudhulumiwa,” aliongeza Fatuma Atemi.


Hata hivyo, Mkurugenzi wa Mawasiliano wa kaunti hiyo, Richard Chacha, alisema suala hilo linachunguzwa na vyombo vya usalama.

Hivyi Ndivyo Wabunge wa Tanzania, Kenya na Msumbiji Wavamiwa na Majambazi Nchini Afrika Kusini...!!!!

$
0
0

Wabunge wa bunge la Afrika kutokea mataifa ya Tanzania, Kenya na Msumbiji walivamiwa na majambazi walipokuwa wakitoka uwanja wa ndege wa OR Tambo mjini Johannesburg wakielekea hotelini 

Mmoja wa wabunge hao kutokea Kenya alipigwa vibaya na majambazi hao alipokuwa akijaribu kuzozana nao wasiwaibie 

Wabunge wengi wanasema wakati sasa umefika kwa Bunge hilo la Afrika kuhamishiwa kutoka Afrika Kusini kwa sababu hakuna usalama wa kutosha nchini humo. 

Shinda Gari ya Bure Kabisa Kutoka Kampuni ya Magari Japan

$
0
0
Umeshawahi Kufikiria Kupata Gari la Bure bila Kulipa Chochote, Basi hii Kampuni ya Cars From Japan Wanakupa Nafasi Hiyo ... 

Chakufanya ni Kubofya Link hapo chini na Ufate Maelekezo ya Jinsi ya Kuweza Kuwa Mshindi wa Gari hilo..


Kisha Jisajili kwa Kuweka Jina na Email Yako... USIWE NA WASIWASI HUDUMA HII NI SALAMA KABISA..

Jinsi ya kujiunga:

Bofya hayo maandishi ya rangi ya blue kisha itafunguka kurasa ambayo itakuwa iko hivi.

Kisha Bofya neno APPLY NOW kisha itafunguka hivi.


Kisha utajaza Form hii kisha utaBofya neno NEXT itafunguka kurasa ingine nayo ufate maelezo yake..

Mwisho wa Kujisajili ni 22 / 3 / 2017

Wema Afanya Jambo Siku ya Wanawake Duniani..!!!

$
0
0

Katika kuadhimisha siku ya wanawake duniani Miss Tanzania 2006 Wema Sepetu ameshiriki kwa kupanda miti katika vyanzo vya maji vya Mbogo na Nukutu katika milima ya Uluguru, Manispaa ya Morogoro.

Wema aliyeungana na Mbunge wa Viti Maalum mkoa wa Morogoro kupitia CHADEMA, Devotha Minja, Diwani wa kata hiyo pamoja na wenyeviti wa serikali za mitaa, wamefikia hatua hiyo kwa lengo la kuhifadhi vyanzo vya maji ambavyo vimekuwa vikiharibiwa kwa kiasi kikubwa katika maeneo hayo, hali inayotishia maisha ya viumbe pamoja na wakazi wanaotegemea vyanzo hivyo.

Mrembo huyo ambaye pia msanii wa filamu nchini, amesema kuwa ameamua kuunga mkono jitihada hizo za kuhifadhi vyanzo vya maji ili kuondoa kero za maji ambazo wanawake hukumbana nazo, huku akitoa somo kuwa faida na manufaa ya miti hiyo zitaonekana baadaye.

"Leo ni siku ya wanawake duniani, nikaonelea nijiunge na wanawake wenzangu wa Mkoa wa Morogoro siku ya leo katika upandaji wa miti ambao utakuja kuwa na tija kwetu na kupunguza kero kubwa inayotukabiri ya maji, wote tunajua kuwa mwanamke ndiyo anakerwa zaidi katika upatikanaji wa maji labda haittusaidia leo wala kesho lakini itakuja kusaidia vizazi vyetu vya baadae". Amesem Wema Sepetu.

Wema ambaye hivi karibuni ametangaza kujiunga na CHADEMA akitokea CCM, amesema ameongeza kuwa mazingira hayana itikadi wala vyama na kwamba yanamgusa kila mtu hivyo yampasa kila mmoja kupanda miti ili kuweza kulinda vyanzo vya maji.

Kwa upande wake Mbunge Devotha Minja ambaye kabla ya kuwa mbunge amekuwa akiripoti habari nyingi kuhusiana na uharibifu wa mazingira kupitia kazi yake ya uandishi wa habari, amesema ameamua kuchukua hatua kwa vitendo kama kiongozi ili kuwa mfano kwa jamii nzima ya watanzania hususani wakazi wa Morogoro, kuhusu umuhimu wa kuhifadhi mazingira na vyanzo vya maji.
Viewing all 104712 articles
Browse latest View live




Latest Images