Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104415 articles
Browse latest View live

Mchepuko Wangu Unanipigisha PUNYETO Hataki Kunipa Pale Kati

0
0
Nimekuwa nae sasa kwa takrini miezi 2 na nusu sasa ila chakushangaza kila ninapohitaji mzigo anakuwa Oky, sasa ananiambia tuanze maandalizi ndipo bi mdada anapoanza kunishughulisha kwa kunipigisha NYETO hadi nafika goli 2-3 na mwisho uume wangu unakosa nguvu na siwezi tena kula mzigo sasa mnanishaurije kwa huyu mchepuko hawezi kunimalizia uwezo wangu wa nguvu za kiume kweli?

Vodacom Yawapiga Msasa Mawakala Watakaokusanya Fedha za Hisa

0
0
Mawakala wa kuuza hisa za Kampuni ya mawasiliano ya Vodacom Tanzania PLC, wamepatiwa mafunzo elekezi ya siku moja yaliyokuwa na lengo la kuwaelimisha jinsi ya kukusanya fedha wakati wa zoezi la kuuza hisa za kampuni hiyo litakapoanza hivi karibuni tukio ambalo limekuwa likisubiriwa kwa hamu kubwa na watanzania walio wengi.

Mkurugenzi Mtendaji wa Vodacom Tanzania PLC, Ian Ferrao akifafanua jambo  kwa mawakala (hawapo pichani )wakati alipokuwa akitoa mafunzo elekezi ya siku moja jijini Dar es Salaam leo  juu ya ukusanyaji wa  fedha wakati wa zoezi la kuuza hisa za kampuni hiyo litakaloanza hivi karibuni.

Semina hiyo ilifanyika jijini Dar es Salaam katika ukumbi wa Mlimani City ambapo Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni hiyo, Ian Ferrao alisema “Tunawashukuru kwa ushirikiano wenu tangia tulipoanza mchakato wa maombi ya kuuza hisa kwa umma hadi kufkia sasa ambapo tayari tumepata kibali cha kutekeleza zoezi hili kutoka serikali kupitia Mamlaka ya Dhamana Masoko na Mitaji (CMSA) na mkiwa wabia wetu katika mchakato huu tumewaita kwa ajili ya kubadilishana mawazo jinsi tutakavyofanikisha matarajio yetu tuliyokusudia na kuwa tayari kwa kazi iliyosubiliwa kwa muda mrefu”.

Ferrao alieleza kuwa Vodacom inatarajia  kuuza asilimia 25% ya hisa zake kwa umma  zenye thamani ya shilingi Bilioni 476/-na kila hisa itauzwa kwa shilingi 850/-
Vodacom Tanzania PLC,imekuwa ya kwanza kutekeleza  sheria ya Electroniki na Mawasiliano ya Posta (EPOCA) na sheria ya fedha ya mwaka 2016 inayoyataka makampuni kumilikisha asilimia 25% ya hisa zake kwa umma kupitia Soko la Hisa la Dar es Salaam.
Kwa mujibu wa Ferrao, wananchi wataweza kununua hisa za zao katika matawi ya Benki ya NBC na mawakala wa Soko la Hisa la Dar es Salaam (DSE) waliopo nchini kote.
Wakati zoezi la uuzaji hisa za Vodacom linatarajiwa kuanza rasmi hivi karibuni,wawekezaji na wananchi wamekuwa wakisubiri kwa shauku kubwa ambapo wamekuwa wakifuatilia kwa karibu jinsi zoezi hili linavyoendelea ili waweze kujipatia fursa ya kumiliki hisa katika kampuni kinara ya mawasiliano nchini.

Sehemu ya Mawakala  watakaouza hisa za Kampuni ya mawasiliano ya Vodacom Tanzania PLC, wakimsikiliza Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni hiyo,Ian Ferrao(hayupo pichani) wakati alipokuwa akitoa mafunzo elekezi ya siku moja jijini Dar es Salaam leo  juu ya ukusanyaji wa  fedha wakati wa zoezi la kuuza hisa za kampuni hiyo litakaloanza hivi karibuni.



Baadhi ya Mawakala  watakaouza hisa za Kampuni ya mawasiliano ya Vodacom Tanzania PLC, wakimsikiliza Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni hiyo,Ian Ferrao(hayupo pichani) wakati alipokuwa akitoa mafunzo elekezi ya siku moja jijini Dar es Salaam leo  juu ya ukusanyaji wa  fedha wakati wa zoezi la kuuza hisa za kampuni hiyo litakaloanza hivi karibuni.

VIDEO: Mafuriko yaliyotokea leo DSM yamesababisha kifo cha mtu mmoja

0
0
Mvua ya takribani saa tatu iliyonyesha leo March 8 2017  jijini Dar es salaam na kusababisha mafuriko katika baadhi ya maeneo ya Jiji, Tabata na Jangwani ndio maeneo yanayoripotiwa kuathirika zaidi na Mvua hiyo ambapo taarifa zimedai kuwa mtu mmoja amepoteza maisha kutokana na mafuriko hayo.

Bonyeza play hapa chini kutazama.

Fahamu Sifa za Wanawake Wanaopenda Sana Pesa

0
0

Hongereni wanawake kwa siku yenu. Tunawapenda Sana kwani ninyi ndio furaha yetu, amani yetu, utulivu wetu. Bila ninyi dunia hatujui ingekuwaje.

Basi baada ya machache hayo nirejee kunako mada.

Siku hizi kumekuwa na ongezeko kubwa la mamilioni ya wanawake wanaopenda Sana pesa kuliko kitu chochote. Jambo hili lilianza Kama mzaha lakini kwa sasa hakuna wakuuzima moto huu.
Kupenda pesa sio vibaya Bali kuipenda Sana kiasi kwamba mtu yupo radhi auze utu wake na kuudharau kabisa uanamke wake. Kama hiyo haitoshi wanawake wengi wanaopenda pesa ndio huwa chanzo cha maangamizi katika familia.

Zifuatazo ni sifa bainifu za wanawake wanaopenda Sana pesa;-

1. Huwa na tamaa ya mambo yasiyo ya lazima.
Wanawake wengi wapendao pesa huwa na tamaa ya mambo yasiyo ya lazima, mambo ambayo hayagusi maisha moja kwa moja. Hata nilipokuwa chuo wanawake wengi waliokuwa wanapenda pesa Sana walikuwa na tamaa za kusikitisha ambazo zilipofusha fahamu zao. Unakuta mwanamke anaomba laki tano kwaajili tuu ya kununua Simu nyingine kubwa wakati akiwa bado na simu mpya. 
Katika maisha ni bora uingie jehanam kuliko kukutana na mwanamke mpenda pesa kwani utateseka Sana kwa ajili yake na bado hata ona msaada wako.

Sio rahisi kujenga familia bora na mwanamke mpenda pesa.

2. Wengi hutoka familia masikini.
Wanawake wengi Kama sio wote ambao hupenda pesa kuliko utu wao hutoka familia kame Sana. Ukame wa kiuchumi mpaka kiakili. Wengi wao huweza kutoa hata rushwa ya ngono ili tuu wapate pesa wasijue miili yao inathamani zaidi ya zile karatasi.
Hata humu jukwaani wapo wengi Sana na comments zao zinajulikana.
Wengi huweka matamanio yao hapa jamvini matamanio waliyoyakosa. Mtu ni masikini unandoto za kuwa na mwanaume mwenye pesa nani alikuambia wenye pesa wanataka masikini. 
Umasikini wako usikufanye ujidharau au mtu akudharau. Ndio maana wanawake pamoja na mchango wenu katika dunia hii lakini bado mpaka wanyama hawawaheshimu.
Lipo kundi dogo la wanawake wanaojitahidi kutetea thamani ya jinsia yao lakini wengi wao ni wakuonewa huruma tuu.

3. Wengi wao hawana elimu ya kutosha.
Mwanamke aliesoma akaelimika hawezi hangaika na pesa ya mtu. Ndio maana wanawake wachache huhangaika kwajili ya kujitegemea na sio kumtegemea mwanaume. Wanawake wengi wenye elimu na vipato vizuri huwezi msikie akiongelea pesa Kama kigezo muhimu kwa mwanaume anayemuhitaji awe mume wake. Wengi wa wanawake humu jamvini ambao hujipa matumaini na comments zao za kujiliwaza iwe wanakazi zenye mishahara duni au elimu ndogo sambamba la kutelekezwa na wanaume kwa ukame wao wa akili.

4. Ni wavivu na wasio na mawazo.
Wanawake wote wanaopenda pesa ni wavivu kupita kiasi. Uvivu wao umeanzia akilini kiasi kwamba hawana mawazo ya maendelo. Utakuta mwanamke anawaza mambo mepesi kabisa Kama urembo, nguo, mtoko, n.k.
Wanawake wapenda pesa ni hatari kwa ustawi wa familia.
Huwezi kuwa na familia kubwa ukiingia katika bahari ya viumbe hawa.

5. Hawana shukrani wala uvumilivu.
Wanawake wapenda pesa huwezi msikia akikushukuru zaidi ya kujichekesha tuu na kubinua makalio.
Kwa mfano amekuomba milioni moja then ukampa laki tano basi utamsikia akisema sasa hii nitafanyia nini, au niongezee tena mume wangu huku akikushika kifua au ndevu. Wanawake wenye hekima hushukuru mpaka mwanaume anasikia aibu.
Suala la uvumilivu halipo kwa hawa viumbe. Shida ikitokea ukishindwa kuitatua kwa wakati huo basi hesabu umeliwa. Yaani kwao kukusaliti ni jambo lisilo na mashaka.

Babu aliwahi kunambia;
Usimpe mwanamke pesa yote aombayo.

Wenye wake mmenielewa.

Mapenzi Matamu Sana..Mdada Fahamu Njia 18 za 'Kumshika' Kidume Yeyote Yule Ulimwenguni....!!!

0
0

I was single once, but now i'm a wife and a mother. Nimekaa nikaona sio vibaya iwapo nta-share tips kadhaa zilizonisaidia kumuweka baba watoto sawa na mpaka leo hii sijawahi kuhisi wala kugundua kwamba anatoka nje ya ndoa yetu, japo matatizo ya hapa na pale hayakosekani ila tumedumu na bado tunaendelea na safari.
Unapokutana na mwanaume akakutongoza/mwanamke akakukubalia kuna uwezekano mkubwa kuwa amevutiwa na wewe kweli au kakutamani tu. Kitu ambacho watu hua wanasahau ni kwamba hata mtu aliyekutamani tu unaweza ukampa mwongozo/sababu mpaka mwenyewe akajikuta anakupenda kuliko ambavyo angeweza kutarajia kwamba angewahi kupenda. Ndio maana hata wale waitwao 'bad girls/boys' hua wanajikuta wamenaswa na kunasika at some point.

1. Usiigize.
Maigizo waachie wasanii wetu, kuwa vile ulivyo kweli kimaisha/kitabia (isiwe mbaya)/mazoea n.k

2. Don't move too fast/act desperate.
Usitumie ule muda wa mwanzo kabisa wa mahusiano yenu kutaka kujua "una malengo gani na mie?""utanioa?""Kanitambulishe/nataka nikakutambulishe." n.k Mpe nafasi ya kukusoma na kupata kujua wewe ni mtu wa aina gani, je unafanania na mwanamke ambae angependa kuwa nae kwa muda mrefu, possibly hata ndoani? Na wewe nawe tumia muda huo kufanya kitu hicho hicho.

3.Don't be too demanding.
Huyo sio baba yako wala sio mume just yet, hivyo chochote atakachokufanyia kinatokana na yeye kutaka/kupenda kufanya hivyo na sio kwakulazimika. Haki hiyo hauna.

4. Kuwa na shukurani.
Learn to appreciate all that he does for you, that way ataona umuhimu wa hayo anayokufanyia, yawe makubwa au madogo.

5. Be real.
Badala ya kufika kwake na kuanza kushangaa anaishije bila ya mfanyakazi wa ndani huku ukitamba kuwa wewe huwezi, shangaa anawezaje weka nyumba yake katika hali nzuri mwenyewe bila ya msaada. Hii itaonyesha fika wewe utakua mke wa aina gani hapo baadae, kama ni wale wakukaa miguu juu huku wakiagiza hata maji waliyoombwa na mume au la.

6. Learn to cook if you don't know how to.
Waliosema "the way to a man's heart is through his stomach" hawakukosea. Ukiachilia mbali wale watu wachache wanaokula ili kushiba wengi hua wanajali ladha. Hiyo ndio hua inawaongezea hamu ya kula na kuwarudisha nyumbani mapema pia kuwafanya wakumiss pale inaposhindikana kula chakula chako . Kwakumwonyesha mwanaume kwamba hata tumbo lake unaweza kuliridhisha unamwongezea sababu za kukuweka kwenye maisha yake.

7. Mheshimu.
Mpe heshima yake kama mwanaume wako ila usimwogope. Wengine wote usiwape nafasi kumfanya ajisikie kwamba haheshimiki.

8. Kuwa ngao yake.
Inapotokea anakumbwa na matatizo yoyote yale onyesha utayari wa wewe kuwa pamoja naye kwa hali na mali mpaka yatakapoisha. Pia usikose kumjali kumpa moyo pale unapoona inahitajika.

9. Kuwa muwazi.
Kama kuna mambo ambayo unajua moja kwa moja yatakuwa sehemu ya mahusiano yenu (watoto/X mkorofi .nk) mweleze mapema ili aamue kama yuko tayari kudeal nayo au la.

10. Usiwe na chuki.
Kikifika kipindi cha yeye kukutambulisha kwa ndugu na rafiki zake onyesha ushirikiano. Usionyeshe chuki wala kujiona kana kwamba wewe ndio wewe.

11. Give your all.
Kama na nyie mtaamua kuonjeshana tunda kabla (kama ambavyo wengi wanafanya karne hii) basi kuwa mbunifu, mtundu na usiwe mvivu.

12.Pendeza.
Vaa/onekana vizuri unapokuwa nje hata ndani pia. Usisahau kuzingatia/jali hisia zake kuhusu mavazi 
yako.

13. Onyesha interest kwa yale ayapendayo yeye.
Usiwe mbinafsi kila siku unataka kusikilizwa wewe tu na story/mambo utakayo wewe. Uliza/jua kuhusu yale anayopenda yeye mf. mpira/siasa.

14.Kuwa mtulivu.
Usiwe mtu ambae kila saa simu yako inapigwa pigwa na wanaume wasio ndugu wala marafiki wakaribu na wanaoeleweka. Discpline ni muhimu sana.

15.Usimzonge.
Usiwe mmoja wa wale watu wanaofuatilia wenzi wao masaa yote wanapokuwa hawapo pamoja. Mpe nafasi ya kuwa na marafiki zake bila kuhitaji kuzima simu ama ku-ignore simu/text zako.

16. Mfurahishe/chekeshe.
Joke around sio muda wote yeye ndio awe wakukufurahisha wewe.

17. Jifunze kusamehe.
Mambo madogo madogo yanapoombewa msamaha samehe na uache yapite.

18. Mshirikishe Mungu wako.
Ukishaona kwamba huyo ndie basi mshirikishe yule unayemwamini ili upate mwongozo wa kiroho.

Hii Hapa Sababu Kubwa Inayowafanya Wanawake Kupiga Kelele Wakati wa Tendo la Ndoa

0
0

Kumekuwa na tabia au hali ya wanawake wengi kupiga kelele au unaweza kusema kutoa sauti wakati wakishiriki tendo la ndoa. Hali hii imeacha maswali kama kutoa huko sauti ni jambo la asili au ni mwanamke mwenyewe anaamua hapa atoe sauti na kwingine asitoe.

Mwaka 2011 watafiti wawili mmoja kutoka Chuo Kikuu cha Lancashire na mwingine kutoka Chuo Kikuu cha Leeds wote wa nchini Uingereza walichapisha utafiti wao walioufanya uliokuwa ukihusu utoaji wa sauti wa kati wa kujamiina. Walitaka hasa kujua kwanini wanawake hutoa sauti hizo.

Katika utafiti huo, waliwahoji wanawake 71 wenye umri kati ya miaka 18 na 48 ambao hushiriki mapenzi mara kwa mara juu ya utoaji wa sauti wakati wa kujamiiana.

Katika utafiti huo ulibaini kuwa wanawake wengi huto sauti hizo lakini sio pale tu wanapokuwa wamefika kileleni. Asilimia 66 walisema kuwa hutoa sauti wakati wa kujamiina ili  kuwasaidia wenza wao kufika kileleni haraka, wakati asilimia 87 walisema kuwa hutoa sauti hizo ili kuwaongezea wenza wao kujiamini kwa kile wanachokifanya kuwa wapo sawa.

Wanawake walieleza kuwa mara nyingi hutoa sauti wakati wenza wao wanapofika kileleni. Baadhi pia walieleza kuwa sauti hizo huwasaidia kuwaondolea uoga walionao, hali ya kutojisikia kuwa sawa, wakati mwingine kuondoa maumivu lakini pia kama njia ya kufurahia raha anayokuwa anaipata.

Aidha, wataalamu hao walisema kuwa kwa vile wanaume wengi huhusisha utoaji wa sauti na mwanamke kufika kileleni, basi baadhi ya wanawake hutoa sauti hizo kwa uongo ili tu kuwaridhisha wenza wao waone kila kitu kipo sawa.

Kwa upande mwingine, imegundulika kuwa wanawake si jamii ya wanyama pekee ambao hutoa sauti wakati wa kujamiiana kwani hata nyani (baboons) wana aina zao za sauti ambazo huzitoa wakati wakijamiiana.

Imeelezwa kuwa wakati mwingine huwa ni vigumu sana kuelezea kila kinachotokea wakati wa kijamiiana kwa sababu kila mtu huwa na utashi wake. Lakini kitu wataalamu walichokubaliana ni kuwa sauti hizo zinaweza kumsaidia mwenza kujua kama anachofanya ni sasa hivyo aendelee au aache, aongeze au apunguze.

Andika Maoni yako Hapo Chini Utuambie nini Kinamfanya Mpenzi Wako Apige Kelele Wakati wa Kuhondomola au Kama Wewe ni Mwanamke Tueleze Sababu ya Nini Kinapelekea Hadi mnapiga kelele wakati wa game,Zingatia Lugha yenye tafsida isiyokuwa na matusi.

Thomas Ulimwengu Apewa Mazoezi Ya Ziada Ulaya

0
0


MSHAMBULIAJI wa kimataifa wa Tanzania, Thomas Ulimwengu amesema kwamba amekuwa anapewa mazoezi ya ziada katika klabu yake mpya, AFC Eskilstuna ya Sweden ili awe fiti zaidi, kwa sababu alijiunga na timu hiyo akitoka kuuguza maumivu ya mguu.

Akizungumza  Online leo, Ulimwengu amesema kwamba alijiunga na AFC Eskilstuna baada ya kuwa nje kwa takriban miezi mitatu kutokana na maumivu ya mguu.

“Ninapewa mazoezi ya ziada hapa kwa sababu nilikuja katika hii timu baada ya kuwa nje kwa miezi kama mitatu kwa sababu ya maumivu ya mguu. Hivyo sikuwa fiti kiasi cha kutosha,”amesema.

Ulimwengu amesema kabla ya mazoezi ya pamoja na wenzake, amekuwa akifanyishwa mazoezi maalum ya kumuweka fiti zaidi na kwa ujumla anaendelea vizuri. 

Ulimwengu alijiunga na Eskilstuna ambayo awali ilikuwa inajulikana kama FC Cafe Opera na Vasby United Januari mwaka huu kwa mkataba wa miaka miwili akitokea TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC).

Ulimwengu aliyezaliwa Juni 14, mwaka 1993 aliibukia katika taasisi ya soka Tanzania (TSA) mwaka 2008, kabla ya mwaka 2009 kwenda kuanza kukomazwa Ligi Kuu katika klabu ya Moro United alikokuwa akicheza kwa mkopo hadi mwaka 2010 alipokwenda akademi ya AFC Eskilstuna ya Sweden, alikocheza hadi 2011 TP Mazembe alipochukuliwa na timu ya vijana ya Mazembe.

Alicheza U-20 ya Mazembe kwa msimu moja kabla ya kupandishwa rasmi timu ya wakubwa mwaka 2012 na moja kwa moja kuwa mchezaji wa kikosi cha kwanza hadi anamaliza Mkataba wake Oktoba mwaka jana.

Ulimwengu anajivunia kushinda mataji makubwa akiwa na  Mazembe kama Ligi ya Mabingwa Afrika, Super Cup ya Afrika na pamoja na kucheza Klabu Bingwa ya Dunia.

Ulimwengu tayari ameanza kuichezea timu yake mpya nchini Sweden

Only in TZ...Aliyetangazwa Kuwa Mtuhumiwa wa Madawa Kukaribishwa Kukaa na Viongozi wa Wakubwa Serikalini

0
0


Ni Tanzania pekee, mtu aliyetangazwa kuwa mtuhumiwa wa biashara ya dawa za kulevya, anaweza kukaribishwa jirani na viongozi wakubwa wa Serikali, wanapiga stori, wanacheka mpaka kugonganisha mikono.

Hapa Mbunge wa Hai (Chadema), Freeman Mbowe, ambaye ni Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni, akiwa na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa.

Katika picha hizo, Mbowe anaonekana kwa ukaribu pia na Rais mstaafu, Dk Jakaya Kikwete, Waziri Mkuu mstaafu, Mizengo Pinda, vilevile Waziri wa zamani wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe.

Picha hizi zimepigwa leo kwenye msiba wa mama mdogo wa Rais Kikwete, Nuru Khalfan Kikwete, aliyefariki dunia usiku wa kuamkia jana kisha kuzikwa leo Bagamoyo.

KUMBUKA

Mbowe alituhumiwa mbele ya kadamnasi na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda kuwa anahusika na biashara ya dawa za kulevya.

Makonda aliagiza Mbowe aripoti polisi kwa mahojiano. Baadaye Mbowe aliripoti polisi na kuachiwa. Mbowe pia alimfungulia mashitaka ya kikatiba Makonda kuwa maagizo aliyotoa yanakinzana na Katiba ya Tanzania.

MUUZA UNGA KWELI?

Duniani kote mtuhumiwa wa dawa za kulevya ni najisi, hata kama hakuna ushahidi wa kumtia hatiani, hutakiwa awe mbali na viongozi wa nchi maana anaweza kuwanajisi.

Kwa hiyo, Mbowe kupitia tuhuma za Makonda, hatakiwi kuwa karibu na viongozi wa nchi. Hakupaswa kuonekana karibu na Waziri Mkuu.

Hii nchi ina Usalama wa Taifa, maofisa wake ambao walikuwepo kwa wingi leo msibani, waliruhusi vipi Mbowe (mtuhumiwa wa dawa za kulevya) awe karibu na Waziri Mkuu pamoja na Rais Mstaafu?

Je, Usalama wa Taifa walishaziona tuhuma za Makonda ni famba? Kwa hiyo wanaona Mbowe ni mtu safi kuwa karibu na viongozi hao?

TAFSIRI YANGU

Tuhuma za Makonda kuhusu watuhumiwa wa dawa za kulevya haziingii akilini kwa Waziri Mkuu, Usalama wa Taifa, JK, Pinda na Membe ndiyo maana Mbowe leo alikuwa pamoja na viongozi msibani na kupewa heshima kama kiongozi.

Maana kama viongozi hao pamoja na Usalama wa Taifa, wangekuwa wanamchukulia Mbowe kama Makonda alivyomtangaza, leo asingepewa nafasi ya kiitifaki msibani. Zaidi asingeruhusiwa kumkaribia kiongozi mkubwa kama Waziri Mkuu.

Ndimi Luqman MALOTO

Naomba Nitoe Hukumu ya Gwajima Vs Makonda

0
0


Makonda hakuwa sahihi kumtaja Gwajima kuwa anahusika na dawa za kulevya wakati hakuwa na ushahidi angalau wa asilimia 90. Kitendo cha Gwajima kutofunguliwa mashitaka, maana yake alimtaja bila ushahidi.

Gwajima hapaswi kuendesha vita yake binafsi na Makonda kupitia Kanisa. Ni kama ambavyo Makonda hakuwa sawa kutumia cheo chake kumpa Gwajima tuhuma nzito za dawa za kulevya.

Tafsiri ni kuwa Makonda alitumia ofisi yake vibaya, naye Gwajima ametumia madhabahu yake vibaya. Kwa msemo wa mtaani, hiyo wanaita “mbwa kala mbwa! Yaani mechi sare. Kwamba ngoma droo.

Wanasheria wanapokuwa wakitekeleza majukumu yao katika kesi, hufanya marejeo ya kesi za nyuma zenye mfanano na kesi husika ili kuzipa uzito hoja au hukumu, wenyewe huita legal citation.

Kwa kesi hii, ‘legal citation’ ambayo naitumia ni tukio la miaka nane iliyopita, pale mfanyabiashara Reginald Mengi alipotangaza wafanyabiashara watano kuwa ndiyo mafisadi papa. Aliwataja kuwa ni Rostam Aziz, Yusuf Manji, Tanil Somaiya, Jeetu Patel na Subhash Patel.

Rostam alimjibu Mengi kwa kumtaja kuwa ni fisadi nyangumi. Baada ya hapo mzee Mengi alikwenda mahakamani, akituhumu kuchafuliwa jina lake.

Swali likawa, je, kwani wakati yeye anataja mafisadi papa, alidhani Rostam angechekelea na asingeumia? Kila nafsi ina nyama na damu, kinachokuumiza wewe, na mwenzako akitendewa kitamuumiza.

Kama ambavyo Makonda anaumia na hata kutoa machozi kwa sababu ya mjadala wa cheti, ndivyo na Gwajima aliumia sana kutajwa kuhusika na biashara ya dawa za kulevya. Zaidi Gwajima alilala mahabusu, akapelekwa nyumbani kupekuliwa kisha kupimwa kwa Mkemia Mkuu wa Serikali. Gwajima hakulia ila aliumia.

Kinachotokea kati ya Makonda na Gwajima, ni ile dhana kuwa ukichezewa rafu uwanjani kisha ukarudisha, wewe unakuwa umekosea zaidi. Hata hivyo ukweli usiopingika ni kuwa anayetumia mamlaka ya nchi kumkabili raia isivyofaa, anapaswa kuwa mkosefu zaidi.

Kwa msingi huo, watu wanaomlaumu Gwajima kutumia uwanja wa taasisi yake ya kidini kumkabili Makonda, wanatakiwa kuwa wakali zaidi kumsema Makonda kutumia ofisi ya umma kuzushia watu kashfa na kuwachonganisha na jamii

By @luqmanmaloto

Zaidi ya Watu 30 Wanahofiwa Kuuawa Afghanstan

0
0

Zaidi ya watu 30 wameuawa, kulinga na maafisa, lakini baadhi ya ripoti zinasema kuwa idadi ya vifo huenda ikawa kubwa zaidi.

Makamanda wa Afghanstan tayari wametua kwenye paa la hospitali hiyo ya Sardar Daud na sasa wanapigana na wanamgambo.

Kundi la Islamic State(IS) limedai kuhisika na shambulio hilo.

Taleban wamekanusha kuhusika, kulingana na ripoti ya vyombo nchini humo.

Rais Ashraf Ghani amesema kuwa shambulio hilo kwenye hospitali ya Sardar Daud hospital yenye uwezo wa kuwalaza wagonjwa 400 ni "uvunjaji wa maadili yote ya binadamu".

" Katika dini zote, hospitali inachukuliwa kama mahala penye kinga na kuishambulia ni kuishambulia Afghanstan nzima ," alisema .

IS wamekuwa wakiendesha harakati zao nchini Afghanistan tangu mwaka 2015 na tayari wamekwisha tekeleza mashambulio kadhaa nchini humo.

Ilidai kuwajibika na ulipuaji wa mashambulio ya kujitoa muhanga katika mahakama kuu ya mjini Kabul mwezi uliopita ambapo watu 22 waliuawa.

Kundi linalojiita jimbo la Khorasan, ambalo linaunganisha mataifa ya Afghanistan na Pakistan, hivi karibuni limeanza harakati zake katika mataifa yote mawili.

Wapiganaji wa Taleban pia wamekuwa wakiendesha mashambulio yaliyowauwa watu 16 mjini Kabul katika mashambulio yaliyokuwa ya kujitolea muhanga.

Shambulio lilianza saa tatu unusu kwa saa za Aghanstan wakati mwanamgambo alipojilipua katika lango moja la upande wa kusini mwa hospitali- ambayo iko karibu na ubalozi wa Marekani- halafu washambuliaji wengine watatu wa wakaingia ndani ya mazingira ya hospitali hiyo.

Wakaingia katika ghorofa la pili na la tatu huku wakiwa na silaha ndogo pamoja na gurunati na kuanza kufyatua risasi.

Mhudumu mmoja wa hospitali ambaye aliweza kutoka nje alimuona mshambuliaji "akiwa amevalia koti jeupe amesikilia bunduki aina ya Kalashnikov na kumfyatulia risasi yeyote, wakiwemo walinzi, wagonjwa na madaktari". Mhudumu mmoja aliandika kwenye ukurasa wa Facebook: "washambuliaji wako ndaniya hospitali. Tuombeeni."

Mmoja wa washambuliaji ameuawa na wengine walikuwa wamejificha chini ya ngazi, alisema msemaji wa wizara ya ulinzi. Askari mmoja pia ameuawa na wengine watatu wamejeruhiwa na wagonjwa wanaokolewa kupitia milango ya kutokea ya dharura.

Takriban watu watatu wamekufa na wengine zaidi 60 wamejeruhiwa, wengi wao wakiwa ni wahudumu wa hospitali, amesema waziri wa afya na pia vyombo vya habari.

Uwoya Ampa Tano JK kwa Kupenda Wanawake...!!!

0
0

Muigizaji Irene Uwoya amemshukuru Rais mstaafu Jakaya Kikwete kwa kuwathamini na kuwaamini wanawake kwa kuwapa nafasi za juu katika kuongoza taifa la Tanzania.

Uwoya kupitia ukurasa wake wa Instagram amesema kuwa hawezi kumsahau Rais huyo kutokana na uamuzi wake wa kutoa nafasi kubwa kwa wanawake katika serikali yake, zikiwemo nafasi za uwaziri, majaji na hata Spika wa bunge, na kwamba, Rais huyo ndiye aliyempa motisha ya kugombea ubunge.

"Namshukuru sana Rais mstaafu... Mh. JAKAYA MRISHO KIKWETE kwa kutupa wanawake heshima na kututhamini... Alitupa nafasi nyingi sana katika nafasi za mawaziri, majaji na spika... Na hata mimi kama msanii nilihamasika na kuona naweza kugombea ubunge... Kiukweli amefungua njia na ameweka mwanga mkubwa kwa viongozi wengine na wao wakaendelea kuthamini na kuheshimu mchango wetu katika jamii ndiyo maana hata tukapata makamu wa Rais mwanamke kwa mara ya kwanza Tanzania". Amesema Irene

Katika hatua nyingine, Uwoya ameungana na wanawake wengine duniani kusherehekea siku ya wanawake, huku akionesha kukerwa na wanaume wanaowadharau wanawake huku akiongeza kuwa wanawake wana mchango mkubwa katika jamii na kwamba mwanamke ni mlezi na pia wakati mwingine husimama kulisha familia.

"Mwanamke ndiye mama wa taifa... Ndiyo maana Marekani mwaka 1911 iliadhimishwa siku ya wanawake duniani ambapo vikundi tofauti vya wanawake viliungana kupinga ukandamizaji, uonevu na ubaguzi wa jinsia hususani sehemu za kazi... " Ujumbe wa Irene Uwoya.

Duh..Hii Noma Sana...Jamaa Ajiua Baada ya Kukamatwa na Shehena ya Viroba Nyumbani Kwake..!!!

0
0

Mfanyabiashara na muagizaji wa pombe za viroba, Festo Mselia, amekutwa amejiua kwa kujipiga risasi ikiwa ni siku moja baada ya jeshi la polisi kuendesha msako na kukamata shehena ya pombe katika ghala alililokuwa akilimiki mjini Dodoma.

Katika vita ya kupambana na matumizi ya pombe za vifungashio aina ya viroba vilivyopigwa marufuku, jeshi la polisi mkoa wa Dodoma limefanikiwa kukamata shehena hiyo ya katoni 1,400 ikiwa na thamani ya shilingi bilioni moja katika ghala la mfanyabiashara huyo.

Mfanyabiashara huyo aliyejiua ni wakala mkuu wa uagizaji na usambazaji wa pombe hizo akiwa anamiliki 'store' ya Mselia Intapreses.

Awali katika msako huo ulioongozwa na kamanda wa polisi mkoa wa Dodoma, Lazaro Mambosasa, alimtaka mfanyabiashara huyo kuendelea na shughuli zake, huku akiamuru shehena hiyo isiuzwe wala kutumika wakati akisubiri maelekezo mengine.

Mambosasa amesema jeshi linaendelea na uchunguzi kabla ua kutoa taarifa rasmi.

Hii Sasa ni Zaidi ya Balaa..Mfumuko wa Bei Wazidi Kupaa...!!!

0
0

Mfumuko wa bei wa taifa kwa mwezi Februari 2017 umeongezeka hadi kufikia asilimia 5.5 kutoka asilimia 5.2 mwezi Januari 2017.

Takwimu hizo zimetolewa jana Jijini Dar es salaam na mtakwimu mkuu wa ofisi ya taifa ya takwimu (NBS) Bi. Ruth Minja wakati akitoa taarifa ya mfumuko wa bei wa taifa wa mwezi Februari na kuongeza kuwa hali hiyo inamaanisha kuwa kasi ya upatikanaji wa bei za bidhaa na huduma kwa mwaka ulioisha mwezi Februari 2017 imeongezeka ikilinganishwa na kasi ya upatikanaji ilivyokua kwa mwaka ulioisha Januari.

Amesema uwezo wa shilingi 100 ya Tanzania katika kununua bidhaa na huduma umefikia shilingi 93 na senti 48 kwa mwezi Februari.

Bodaboda Washtukiwa Juu ya Tabia Zao za Kulala Kimapenzi na Wanafunzi wa Shule..!!!

0
0

Mkuu wa Dawati la Jinsia Mkoa wa Kipolisi Kinondoni, Dar es Salaam, Inspekta Prisca Komba amewaonya madereva bodaboda kuwa na mahusiano ya kimapenzi na mabinti wa shule na badala yake wawe mstari wa mbele kulinda na kuwasaidia kutimiza malengo yao

Akizungumza leo ikiwa ni maadhimisho ya siku ya wanawake duniani kwenye kipindi cha East Africa Breakfast cha EA Radio, Inspekta Komba amesema katika dawati lake la jinsia kesi nyingi anazopata ni za madereva kuwapatia mimba wanafunzi na kisha kuwatelekeza kitu ambacho kinamuumiza zaidi ni pale binti anakuwa ammeachishwa shule na mwenye mimba anakuwa kakimbia

"Huwa naumia sana nikiwa napokea kesi za aina hii. Unajua hawa bodaboda siyo vijana wabaya lakini niwaambie kwamba, kama umempenda binti wa watu fuata njia sahihi za kumpata, siyo tena kumharibia masomo yake na mtoto umtelekeze maana hata wakati mwingine huwa hawasemi kweli wanapoishi, boda boda waacheni wanafunzi wasome.

Aidha Bi. Komba ameongeza kuwa licha ya kuhitaji mabinti walindwe kuepukana na mimba za utotoni lakini pia ameiomba jamii nzima kuhakikisha mtoto wa kike anathaminiwa kwa kupatiwa taulo za kujisitiri wakati wa hedhi hasa kwa wale wanafunzi wanaotoka katika mazingira magumu.

"Hili jambo hebu tusiachiwe wanawake tu kwa sababu lipo katika miili yetu. Kama mimi mwanamke mume wangu hatonithamini kwa kuninunulia vifaa vya kusitiria nikitumia vifaa vichafu nikipata magonjwa naye nitamuambukiza, kwa kuangalia hivyo hili jambo ni letu sote." Amesema Komba.

Imekaaje Hii..Miss Tanzania Ashauri Kuwepo na Somo Maalumu Kuhusu Hedhi Mashuleni...!!!

0
0

Miss Tanzania Mwaka 1998, Basila Mwanukuzi  ameishauri serikali kuweka somo la kuwafundisha mabinti namna ya kujihifadhi ngazi ya shule za msingi  kwa kupitia walezi (Matron)  kipindi wanapokuwa wameanza kupata mabadiliko ya ukuaji wa mwili.

Akizungumza leo katika kipindi cha East Africa Breakfast  ya East Africa Radio katika maadhimisho ya siku ya wanawake duniani Miss Mwanukuzi amesema kuwa suala linalohusu watoto wa kike kujisitiri linahusu jamii nzima na siyo waachiwe wanawake peke yao.

“Katika suala kujisitiri tusiachiwe wanawake peke yetu, hili ni suala la jamii nzima na hata serikali ina wajibu wa kusaidia mabinti na wadogo zetu kuwapatia masomo ambayo kupitia ‘Matron’ wanafunzi wa shule za msingi watapata mafunzo, kwani siyo kila mmoja anapata mafunzo hayo akiwa nyumbani” - Bi. Mwanukuzi.

Bi. Mwanukuzi amesema mila na desturi potofu ndicho chanzo cha jamii kufanya siri suala la ukuaji na hata kufikia mama kushindwa kuzungumza na binti yake na kwa kuwa kitendo hicho wakati mwingine hutafsiriwa kama ukosefu wa adabu.

Hata hivyo ameweka wazi kuwa wanawake wanapaswa kuinuana ili mambo yanayohusu wanawake waweze kusaidiana wenyewe kwa wenyewe na ndiyo sababu taasisi yake ‘Mwanukuzi Foundation’ imeliangalia suala la kuwainua kina Mama Lishe kwa kuwapatia elimu, kuwafanya watambulike na wathaminiwe zaidi.

Pamoja na hayo Bi Mwanukuzi ameongeza suala la mabinti kusaidiwa vifaa vya kujisitiria wakati wa hedhi lipewe kipaumbele kama suala la madawati na huduma nyingine  na siyo kuachiwa kwa watu wachache.

Tundu Lissu Afunguka Baada ya Kusikia Mwakyembe Amemzuia Kugombea Nafasi ya Rais wa TLS

0
0
Anaandika Wakili Msomi Tundu Lissu:

Waheshimiwa mawakili na wananchi wa nchi yetu. Nimesoma taarifa katika magazeti kadhaa ya leo kwamba Waziri wa Katiba na Sheria Dkt. Harrison George Mwakyembe amenizuia kugombea nafasi ya Rais wa Chama cha Mawakili wa Tanganyika (TLS). Kama taarifa hizo ni za kweli basi naomba kuweka masuala yafuatayo wazi:

(1) Waziri wa Sheria na Katiba hana mamlaka yoyote, kwa mujibu wa Sheria iliyoanzisha TLS na kanuni zake, ya kuzuia ama kuruhusu mwanachama yeyote wa TLS kugombea nafasi yoyote ya uongozi ndani ya TLS. Hivyo, kama kweli Dkt. Mwakyembe ametoa kauli hiyo, basi huo utakuwa uthibitisho wa ama upungufu mkubwa wa uelewa wa Sheria au hulka ya ukiukaji wa sheria (culture of impunity) ambayo imeshamiri sana katika utawala huu wa sasa.

(2) Mamlaka pekee inayohusika na uchaguzi wa TLS ni Kamati ya Uteuzi (Nominations Committee) ambayo ilikwishafanya uteuzi wa wagombea wote kwa kuzingatia sifa na vigezo vilivyowekwa na Sheria na Kanuni za Uchaguzi za TLS. Mimi ni miongoni mwa wagombea ambao Kamati ya Uteuzi ilithibitisha kuwa na sifa na vigezo vya kuteuliwa kugombea nafasi ya Rais wa TLS. Kamati ya Uteuzi haijabadilisha na wala haiwezi tena kutengua uteuzi uliokwishafanyika kwa sababu za kisiasa kama za Dkt. Mwakyembe.

(3) TLS ni taasisi huru ya kitaaluma inayojitegemea na inayojiendesha yenyewe kwa mujibu wa Sheria na kanuni zake. TLS sio idara ya serikali au taasisi iliyoko chini ya mamlaka ya serikali au ya Waziri wa Katiba na Sheria au inayoitegemea serikali kwa namna yoyote ile katika kuendesha mambo yake. Uhuru huo wa TLS unatambuliwa na Sheria za Tanzania na mikataba wa kimataifa ambayo Tanzania ni mwanachama wake.

(4) Kwa vile mimi ni mgombea halali wa nafasi ya Rais wa TLS katika uchaguzi wa wiki ijayo, kwa sasa ninaendelea na kampeni za uchaguzi na nitaenda Arusha wiki ijayo kwa ajili hiyo.

(5) Kwa haya ya Dkt. Mwakyembe na kwa mengine ambayo yamejitokeza katika TLS siku za karibuni na ukimya wa wagombea wenzangu kuhusu masuala haya, ni wazi kwamba mimi ni mgombea pekee anayesimamia uhuru, heshima na hadhi ya TLS kama taasisi huru ya kitaaluma ya wanasheria katika uchaguzi huu. Mimi ni mgombea pekee anayeweza kuirudisha TLS katika misingi halisi ya kuanzishwa kwake na ya uwepo wake: kusimamia maslahi ya kitaaluma ya mawakili na kusimamia na kutetea utawala wa sheria. Mimi ni mgombea pekee ninayeweza kutetea maslahi ya mawakili kwa sababu sihitaji kuteuliwa na Rais kuwa Jaji wa Mahakama Kuu. Nawaombeni mniunge mkono kwa kunipa kura zenu mnamo siku ya uchaguzi tarehe 18 ijayo.

Source:Henry Kilewo

VIDEO: Mtangazaji wa Clouds TV Baada ya Kunyolewa Nywele, Aliahidi Atafanya Hivyo Arsenal ikitolewa

0
0
Moja kati ya watu waliyowashangaza mashabiki wengi wa soka wiki moja iliyopita ni huyu mtangazaji wa Clouds TV James Tupatupa ambaye pia ni shabiki wa Arsenal ya England, Tupatupa aliahidi kama Arsenal itatolewa na FC Bayern Munich atanyoa nywele zote kichwani.

Ahadi hiyo James Tupatupa aliitoa baada ya Arsenal kufungwa goli 5-1 katika mchezo wa kwanza wa hatua ya 16 bora uliyochezwa katika uwanja wa Allianz Arena mjini Munich Ujerumani, hivyo mchezo wa marudiano Tupatupa alikuwa na imani Arsenal yake itaishangaza dunia.

Kwa bahati mbaya Arsenal imetolewa kwa kufungwa kipigo kama cha mwanzo cha goli 5-1 na kuondolewa kwa jumla ya kufungwa goli 10-2, Tupatupa

“Presha ya mchezo wa jana ilikuwa nzuri kwa pande zote mbili lakini mchezo uliamuliwa na refa baada ya Kolselny kuoneshwa kadi nyekundu, kwa hiki kitendo kimenikumbusha kuwa nisiunganishe utabiri na kitakachoenda kutokea uwanjani kitu kama soka ni ngumu kutabiri”


Tumia Mark Beauty Cream Kufanya Ngozi yako Iwe Soft na Kuwa Mweupe Bila Madhara

0
0

Kile kilio cha muda mrefu sasa kimepata jibu. MARK BEAUTY CREAM ni mafuta yaliyotengenezwa maalum kwa ajili ya kukufanya kuwa mweupe na soft mwili mzima na bila madhara. Acha kutumia mikorogo ili kulinda ngozi yako na afya yako kwa ujumla. Mafuta haya hayajachanganywa na viambata sumu (kemikali) na ni salama kabisa kwa mtu yoyote.
SIFA ZA CREAM HII :-
1.Kung'arisha ngozi haraka
2.Kuondoa sugu, madoa na makovu
3.Kuzuia ngozi kuchakaa (Ant aging)
4.Huzuia michirizi.
5.Haiunguzi ngozi kama mikorogo inavyofanya
Mafuta haya yametengenezwa PARIS na yanasambazwa na Markson Beauty Products kote duniani @120,000/=
Kwa bidhaa za tiba na urembo tufuatilie kwenye GOOGLE au instagram @markson_beauty_pr
@Markson_beauty_pr
@Markson_beauty_pr au wasiliana nasi kwa (+255) 0767447444 au 0714335378.

Ubunge Wammaliza Makonda,Adaiwa Analitaka Jimbo la Kitwanga Mwaka 2020...Habari Vichwa vya Magazeti ya Leo 9/3/2017...!!!

Nafasi za Kazi Tanzania Ports Authority na Makampuni Mengine Zilizotangazwa Leo

Viewing all 104415 articles
Browse latest View live




Latest Images