Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104712 articles
Browse latest View live

Profesa Ndalichako Afanya Usafi Ocean Road, Atoa Misaada..!!!!

$
0
0

Katika kuadhimisha Siku ya Wanawake Duniani, Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Joyce Ndalichako amefanya usafi na kutoa msaada wa vitu mbalimbali vyenye thamani ya Sh 4.5 milioni katika Taasisi ya Satarani ya Ocean Road.

Misaada iliyokabidhiwa jana asubuhi ni pamoja na kanga, sabuni za kuogea na kufulia, dawa za meno, juisi, maji ya kunywa, pampers na mabeseni.

Akizungumza mara baada ya kukabidhi msaada huo, Profesa Ndalichako alisema katika kusherehekea wanawake wa Mkoa wa Dar es Salaam kupitia Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) waliadhimia kuwatembelea wanawake wanaotibiwa saratani.

“Tunatambua kwamba wana mahitaji pia, kama ilivyo wanawake ndiyo nguzo ya maendeleo kwa hiyo anavyougua kwa muda mfupi familia hutetereka, tumekuja hapa na vifaa mbalimbali ambavyo tunaamini hawa wagonjwa wanavihitaji,” amesema Profesa Ndalichako.



TTB Yaitangaza Tanzania Eneo Bora la Utalii Duniani..!!!

$
0
0

Bodi ya Utalii Tanzania(TTB) imejipanga kuitangaza Tanzania kama eneo bora la utalii katika maonyesho ya Kimataifa ya Utalii yajulikanayo kama Internationalle Tourismus Borse (ITB) yaliyoanza rasmi jijini Berlin Ujerumani katika eneo la Messe Berlin na kuhudhuriwa na jumla ya nchi 187 kutoka kote duniani.

Mratibu wa ushiriki wa Tanzania katika maonyesho hayo ambaye pia ni Meneja Masoko wa Bodi ya TTB, Geofrey Meena amesema TTB imejipanga vilivyo kuitangaza Tanzania kama eneo bora la utalii duniani ambapo pamoja na kuendelea kuvitangaza vivutio v kama vile mlima Kilimanjaro, Bonde la Ngorongoro, Hifadhi  za Taifa, fukwe na maeneo mbalimbali ya kihistoria.

Pia mwaka huu mkazo umewekwa katika kutangaza ushahidi wa nyayo za binadamu wa kale (Zamadamu) uliovumbuliwa miaka milioni nne iliyopita katika eneo la Laetoli lililoko takribani kilometa 45 kusini mwa Olduvai Gorge.

“Pamoja na kuvumbuliwa kwa fuvu la anayesadikiwa kuwa ni binadamu wa kwanza kabisa duniani huko Olduvai Gorge Ngorongoro, lakini katika kuendelea kudhihirisha kuwa Binadamu wa kwanza aliishi Tanzania tumeamua katika maonesho ya mwaka huu kuja na ushahidi unaoelezea ukweli huo kwamba Binadamu asili yake ni Tanzania,” amesema Meena.


Duh..Hiki Ndicho Alichokifanya Meya wa Ubungo Jana..!!!!

$
0
0

Halmashuri mpya ya Ubungo imetoa msaada wa vitu  mbalimbali zikiwamo khanga na sabuni katika hospitali ya wilaya ya hiyo Sinza Palestina ikiwa ni sehemu ya kuadhimisha  wanawake duniani.

Msaada wenye thamani ya zaidi ya Sh2 milioni umetolewa jana asubuhi na Meya wa Ubungo, Boniface Jacob akiambatana na maofisa wa wilaya hiyo.

Jacob amesema msaada huo ni jitahada mbalimbali za kuunga mkono siku wanawake kwa ni watu muhimu wa kuendesha gurudumu la maendeleo na kwamba halmashauri hiyo ipo katika kuboresha hospitali ya hiyo iwe ya kisasa.

Mmoja wa kinamama Ester William aliishukuru manispaa hiyo kwa kuwajali ikiwamo kuboresha huduma za afya katika hospitali hiyo na Mungu awabariki.

Haya Ndiyo Yaliyomkuta Bosi wa Simu za Samsung Duniani...!!!

$
0
0

“Niko tayari kuachia uendeshaji wa kampuni iwapo kutakuwepo mtu mwingine mwenye uwezo zaidi ya mimi kuiendesha.”

Hii ni kauli ya Lee Jae-yong, bosi wa kampuni kubwa ya Samsung ya Korea ya Kusini, kauli ambayo amekuwa akiitoa mara kwa mara katika mahojiano na mamlaka za nchi hiyo kuhusu kuhusika kwake katika kashfa ya ufisadi inayomzunguka Rais wa nchi hiyo, Park Geun-hye.

Lee Jae-yong, anaendesha kampuni hiyo ya kielectroniki ya Samsung ambayo ni kubwa zaidi duniani kwa niaba ya baba yake ambaye ameathirika kiafya.

Lakini sasa hivi Lee anaweza kulazimika kuachia madaraka ya kampuni, kwani wiki iliyopita alikamatwa kwa tuhuma za rushwa, ufujaji fedha, kusema uongo, kuhamisha mali nje ya nchi kinyume na sheria na kuficha ushahidi ili kujinufaisha kijinai.

Kutiwa kwake mbaroni kulitokana na hatua ya mahakama moja kukubali ombi kutoka kwa timu maalumu ya waendesha mashitaka iliyoomba Lee akamatwe na kuwekwa kizuizini kungojea utayarishwaji wa mashitaka halisi yanayomkabili.

Mwezi uliopita wapelelezi walimtuhumu Lee kwa kutoa rushwa ya Dola za Kimarekani 36 milioni kwa taasisi zinazomhusisha Choi Soon-sil – mwanamke mmoja mwanandani wa Rais Park. Rais Park pia yuko chini ya uchunguzi wa mahakama ya katiba ya nchi hiyo.

Jitihada za awali za timu ya waendesha mashitaka kuomba hati ya kukamatwa kwa bosi wa Samsung ziligonga mwamba, ingawa baadaye mahakama ilibatilisha uamuzi wake, baada ya timu ya waendesha ilipotoa ushahidi wa ziada kuhusu uhusika wa Lee katika jinai zinazomkabili.

Hata hivyo mahakama ilikataa ombi jingine la kukamatwa kwa afisa mwingine mkuu wa kampuni hiyo, Park Sang-jin, kwa tuhuma kama hizo. Hati ya kukamatwa kwa Lee inawapa muda wa siku 20 kumshikilia ili kuendelea na uchunguzi.

Kutiwa mbaroni kwa Lee kunaonyesha kwamba kampuni ya Samsung haikuwa tu mhanga wa ulafi (extortion) kwa upande wa mamlaka za serikali. Wandesha mashitaka wanadai kwamba kutokana na malipo yale ya Dola 36 milioni, kampuni ya Samsung iliweza kupata msaada wa serikali, kupitia shirika lake kubwa zaidi la hifadhi ya jamii – (National Pension Service – NPS).

Msaada huo kutoka serikalini ilikuwa ni wa baraka zake kuunganisha makampuni mawili dada ya Samsung — yaani kampuni hodhi yake ya Cheil Industries na ile ya ukandarasi, Samsung C&T, zoezi liliofanyika Julai 2015.

Mwezi uliopita  wandesha mashitaka walimfungulia mashitaka mkuu wa shirika la NPS kwa kosa la kutumia mamlaka vibaya. Walidai kwamba mkuu huyo aliamuru shirika kupiga kura yake kubariki muungano wa makampuni hayo mawili. Hata hivyo kampuni ya Samsung imekiri kwamba ilichotoa ni msaada wa mkopo tu na si rushwa.

Kutiwa mbaroni kwa Lee kunaashiria kwamba zile ‘njama’ zilizokuwapo baina ya mamlaka za serikali ya nchi hiyo na makundi ya makampuni makubwa ambayo ndiyo yalisukuma kukua kwa uchumi mkubwa wa nchi hiyo haziwezi tena kuendelea kuwapo.

Wachunguzi wengi wa mambo wanaona kwamba kwa muda mrefu mahakama za nchi hiyo zimekuwa zikisita kuwachukulia wamiliki wa makampuni hayo makubwa – ambayo kwa ujumla wake yanaitwa ‘chaebol.’

Inaelezwa kwamba baada ya awali mahakama kukataa kutoa hati ya kukamatwa kwa Lee mwezi uliopita, mitazamo miongoni mwa majaji ilianza kubadilika.

Mkuu wa kampuni ya Samsung, baba yake Lee Jae-yong ambaye yuko hospitali tangu 2014 alishahukumiwa mara mbili lakini kila mara alisamehewa adhabu na Rais aliyekuwapo madarakani. Hata hivyo mtoto wake bado hajafunguliwa mashitaka rasmi.

Aidha wanaharakati wa masuala ya sheria nchini humo wanasema kwamba wakuu wengine wa ‘chaebol’ – wakiwemo wale wa kampuni ya Hyundai, SK na Lotte wote wako mbioni kushughulikiwa.

Saida Karoli Asimulia Alivyoporwa Haki Zake Katika Muziki Kisa Kutojua Kusoma na Kuandika..!!!

$
0
0

Jana kupitia kipindi cha Take One  cha Clouds TV, mtangazaji Zamaradi  alimuhoji mwimbaji wa muziki wa asili  Saida Karoli ambapo alikiri kuwa hana haki kwenye nyimbo zake kutokana na mikataba aliyosainishwa na Meneja wake sababu na yeye hakuwa anajua kusoma na kuandika na akadai zaidi ya album tano hana haki nazo na meneja wake wa zamani ndio mwenye haki nazo.

Kingine alichozungumza Saida ni kuhusu wimbo wa Salome ambao Diamond Platnumz aliurudia  ambapo alisema ana hesabu kama alitoa bure kwani hata fedha aliyopewa ni kidogo na haifai kuongelea.

”Siwezi kulalamika hata kidogo, mara nyingi naulizwa nasema sina tatizo, sina haki na zile nyimbo maana yeye ndio alinipa mikataba na yeye ndio alinitengenezea, hata hii ya Diamond naweza nikasema ikawa mbaya zaidi maana fedha niliyoipata siyo ya kuongelea, kwahiyo mimi najiona nimetoa bure

”Waandishi kila siku wanakuwa wananiuliza nawambia nimempa Diamond nyimbo bure na nimetoa kwa moyo mmoja kweli, roho yangu moja

“Meneja wa zamani aliniuliza nyimbo yako inatakiwa kutumika lakini nipe idhini yako japo ni nyimbo zangu zote lakini sikuwa na haki licha ya kuwa sauti yangu imesikika kule, mimi nilimjibu nimeshakata tamaa na kuimba naona muziki kwangu hauna faida na thamani bora kuwa hata mkaanga vitumbua au maandazi kuliko kuimba

”Nilikuwa na mpango wa kurudi kijijini nyumbani nikae mtu akihitaji show atanikuta kijijini lakini meneja akanambia hapana, alisema nyimbo tumpe Diamond kwa sababu itaniinua na kunipa moyo na kuniamsha upya kama mtu aliyekufa

“Walizushaga nimekufa na nilihisigi nimekufa kweli kutokana na hali ya maisha na nilikuwa nimekata tamaa nikajua nimekufa kweli” Alisema Saida Karoli

Kwa sasa Saida yupo Dar na amekuja rasmi kwa ajili ya kufanya muziki upya kama zamani na yupo tayari kufanya kolabo na wasanii kama Ben pol, Bell 9, Diamond na Darassa.

Barcelona Yaandika Historia, Yamtandika Mtu 6-1

$
0
0
Barcelona wamebirua matokeo ya kutinga nusu fainali kwa kuizaba Paris Saint Germain kwa mabao 6-1 katika mchezo wa marudiano wa Klabu Bingwa Ulaya.

Sergi Roberto alifunga bao la 6 kwa mkwaju wa mwisho wa mchezo, na hivyo kufanya matokeo ya jumla kuwa 6-5 kwenye mchezo uliopigwa kwenye dimba la Nou Camp.

Barcelona walifunga magoli matatu katika dakika saba za mwisho. Walikuwa wakiongoza kwa 3-1.
Wiki tatu zilizopita PSG iliifunga Barcelona magoli 4-0 mjini Paris.

Hatua ya kurejesha magoli yote hayo ni kubwa kuwahi kushuhudiwa katika historia ya UEFA, na sasa Barcelona wana kila nafasi ya kunyanyua kombe la Klabu Bingwa Ulaya kwa mara ya pili katika kipindi cha miaka mitatu.

Katika mchezo mwingine, Pierre Emerick Aubameyang alipachika 'hat trick' na kuipeleka Borussia Dortmund katika robo fainali dhidi ya Benfica.

Borussia Dortmund wameshinda kwa jumla ya magoli 4-1 katika mechi mbili walizocheza.

Diamond: Sitegemei Redio na TV Kusambaza Nyimbo Zangu

$
0
0
Diamond Platnumz amesema kwa sasa redio na TV si vyombo anavyovitegemea sana kwaajili ya promotion pindi anapokuwa akiachia nyimbo.

“Mimi nikiwa natoa nyimbo yangu, promotion yangu siwazi redio wala siwazi TV, ever. Promotion yangu ya kwanza mimi nawaza nyimbo iwafikiaje watu, kuna mitandao ya kijamii, kuna digital platform nyingi,” staa huyo alisema kwenye kipindi cha Ngaz Kwa Ngaz.

Alidai kuwa zama za kundi Fulani la watu likiamua kumrudisha nyuma msanii, halipo tena kwa wasanii wenye nguvu kama yeye.

“Tufute zile ‘naweza nikamdhuru mtu fulani ninavyotaka mimi’ vile vitu havipo tena,” aliongeza.

KUTANA na Mtabibu Ostadhi Khamisi Kutoka Mombasa Kenya Kwasasa Yupo Tanzania Kwa Ajili yako

$
0
0

Kutana na ostadhi khamisi kutoka mombasa Kenya kwa sasa yupo Tanzania ni mtabibu na mtafiti Wadawa za asili anatibia kama vile:
Miguu kuuma
Miguu kufagazi
Miguu kuwakamoto
Chango lauzazi kwakina mama
Dawa ya uzazi wakina mama inapatikana
Kusafisha nyota ili uwe namuonekano kwa kila mtu
Kumrudisha mpenzi wako na liekukimbia ndani yasiku 3 bila yapingamizi yoyote
Kumshika mume au mke asitoke nnje ya ndoa
Pata pete ya Bahati inayo endana na nyota yako
Kurudisha mali ilipotea au kudhurumiwa ndani yasiku 3
Pata utajili usiokuwa namashaliti yoyote
Dawa za nguvu za kiume
Dawa ya biashara inapatikana
Dawa ya kuzuia chuma ulete kwenye biashara inapatikana
 Zindiko la nyumba au shamba
 Anatuliza familia zinazogombana DUWA pamoja navisomo vya ufunguzi wa mwili wako njoo ufunguliwe vifungo ulivyo fungwa kutana na ostadhi khamisi utimiziwe ahadi ulizo hadiwa acha kuteseka acha kuhangaika ostadh khamisi yupupo tanzania kwajili yako...

Call +255718746825 +255754765246 kwa what'sapp +255783708487

Walichokiongea Donald Trump na Rais wa Kenya Kwenye Simu

$
0
0
Siku ya Jumannne majira ya jioni rais wa Marekani Donald Trump alimpigia mwenzake wa Kenya Uhuru Kenyatta na kubadilishana mawazo kuhusu uhusiano baina ya nchi hizo mbili,biashara,masuala ya kikanda na mapambano dhidi ya ugaidi.

Uhuru Kenyatta ni rais wa tatu kutoka bara la Afrika aliyepata simu ya rais Trump tangu kuingia madarakani Januari 20 mwaka huu.

Rais Trump alimuhakikishia Uhuru kuwa Marekani itatoa msaada kwa Kenya katika kupambana na wanamgambo wa Al Shabaab .

Aidha Trump alisema kuwa serikali yake ina mipango ya kuboresha uhusiano baina ya nchi hizi mbili.

Viongozi hao wawili pia walijadiliana kuhusu ushirikiano wa kibiashara na uchumi na jinsi watakavyokabiliana dhidi ya changamoto kuu ya usalama .

Trump amefanya mazungumzo ya simu na Uhuru wiki moja baada ya Marekani kukubalia Kenya kutekeleza safari za ndege za moja kwa moja kutoka Kenya hadi Marekani.

Hapo awali baada ya kuingia White House,Trump alifanya mazungumzo ya simu na rais wa Nigeria Muhammadu Buhari na rais wa Afrika Kusini Jacob Zuma ambapo waliongea kuhusu ushirikiano katika sekta ya uchumi na usalama.

Video: Tazama Uzinduzi wa Hisa za Vodacom PLC [LIVE]

$
0
0
Shuhudia uzinduzi wa hisa za mtandao unaongoza Tanzania mubashara kutoka Hyatt Regency. Wekeza kwa maisha ya baadae, nunua hisa za Vodacom leo. Kwa maelezo zaidi ingia http://vda.cm/vodacomshares. #WekezaVodacom:

Paul Makonda Aenda Mapumziko ya Miezi Miwili South Africa

$
0
0
Wakati utata ikigubika kuhusu safari ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda kwenda nchini Afrika Kusini, imebainika kuwa kiongozi huyo atakuwa likizo nchini humo kwa zaidi ya miezi miwili.

Kwa mujibu wa habari iliyoandikwa katika gazeti la TanzaniaDaima imeeleza uwepo wa RC Makonda nchini Afrika Kusini ndio sababu ya kushindwa kuhudhuria sherehe ya maadhimisho ya Siku ya Wanawake Dunia ambapo ilitangazwa kuwa angekuwa mgeni rasmi katika sherehe zilizofanyika katika uwanja wa Mwembeyanga.

Kuondoka kwake nchini kumekuwa kwa kutatanisha wakati mamlaka husika zikishindwa kutoa taarifa kamili kuhusuana na safari yake. Wadadisi wa mambo wanahoji uhalali wa Makonda kupewa mapumziko hayo nje ya nchi huku serikali ilitangaza kuzuia ziara zote za watumishi nje ya nchi ili kubana matumizi.

Kutokana na zuio la safari za nje ya nchi kwa watumishi wa umma lililotolewa na serikali ya awamu ya tano, safari hiyo ya Paul Makonda imeibua utata juu ya uhalali wake huku mamlaka husika zikirushiana mpira juu ya nani wakuzungumzia safari ya kiongozi huyo.

Msemaji wa Serikali, Dk. Hassan Abbas alipoulizwa kama safari ya Makonda nje ya nchi yupo kikazi au binafsi alisema kuwa, swali hilo aulizwe Katibu Tawala wa Mkoa kwani ndiye mtendaji wake. Kwa upande wake Katibu Tawala wa Mkoa wa Dar es Salaam, Theresa Mmbando alipoulizwa alisema kuwa, swali hilo atafutwe Makonda mwenyewe.


VIDEO:Muigizaji Faiza Ally Alala Mahabusu, Asimulia Mkasa Mzima Baada ya Kutoka

$
0
0
Muigizaji wa Bongo Movie, Faiza Ally ukipenda muite Mama Sasha juzi alikumbwa na mkasa uliomfanya alale mahabusu hadi alipotoka jana mchana.

Msanii huyo amefunguka kupitia ukurasa wake wa Instagram ambapo ameweka video akielezea tukio zima lililompata alipokwenda hospitali.

Hapa chini ni video ya msanii huyo akielezea tukio zima:

Njama za Kumhujuma Lissu Uchaguzi TLS Zabainika, Waziri Mwakyembe Adaiwa Kuhusika

$
0
0
Siku chache baada ya Waziri wa Katiba na Sheria, Harrison Mwakyembe kutishia kukifuta Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS), kwa madai kuwa kimesahau misingi yake ya kazi na kuanza kujishughulisha na siasa, kesi ya kupinga uchaguzi wa chama hicho imefunguliwa.

Kesi hiyo imefunguliwa katika Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Dodoma ambapo mlalamikaji ni Godfrey Sabato John Wasonga dhidi ya TLS na Mwanasheria Mkuu wa Serikali.

Wasonga anaitaka mahakama ihairishe uchaguzi wa TLS hadi hapo Bunge litakapokutana mapema mwezi ujao kuweza kubadili kanuni zinazoongoza chama hicho.



Kwa taarifa za wadau kutoka kwenye mitandao ya kijamii zinadai kuwa hii ni njama ya Waziri Mwakyembe kumkwamisha Tundu Lissu kugombea urais wa TLS.

Waziri Mwakyembe hivi karibuni amenukuliwa akisema kuwa tatizo kubwa ni mtu mwenye kofia ya uongozi kwenye chama cha kisiasa kugombea urais wa TLS. Miongoni mwa wagombea ni Tundu Lissu ambaye pia ni Mwanasheria Mkuu wa CHADEMA ambapo tayari ana kofia ya uongozi kwenye chama cha siasa.

Aidha, inadaiwa kuwa, mabadiliko yanayotarajiwa kufanywa na Bunge kuhusu TLS ni kuzuia kiongozi wa chama cha siasa kuwania urais wa TLS.

Source: Swahilitimes

Mwakyembe Amkomalia Lissu Kugombea Urais wa TLS..!!

$
0
0

WAZIRI wa Mambo ya Katiba na Sheria, Dk Harrison Mwakyembe amesema Serikali haiwezi kuona Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS) kinajiingiza katika siasa.

Alisema kama wanataka hivyo, basi Serikali haitasita kuifuta Sheria ya TLS Sura ya 307 iliyoanzisha chama hicho cha wanasheria.

Dk Mwakyembe alikuwa akizungumza hayo na wageni wa TLS, waliomtembelea ofisini kwake mjini Dodoma jana, wakiongozwa na Rais wa chama hicho anayemaliza muda wake, John Seka.

“Kama wizara hatujui mwelekeo wa TLS kwa sasa, hatuwezi kuiacha TLS ikijiingiza katika siasa halafu tukawaangalia tu. Hatuna nia ya kuitawala TLS, ila tunawajibika kuwasimamia kwa kuwa Sheria yenu iko chini yetu, mkiharibu kwa lolote wizara ndio yenye wajibu wa kuwatolea maelezo katika hilo mnalotaka kulifanya sasa kuna mgongano wa maslahi, je, ninyi kama wanasheria hamkuliona au hamlioni?” Alihoji Mwakyembe.

Wagombea wa TLS Mmoja wa wanasiasa wanaowania urais wa TLS ni Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu ambaye juzi alisema kitendo cha kukamatwa baada ya kufutiwa kesi, kina nia ya kufifisha harakati zake za kuwania urais wa TLS wiki ijayo, huku akitishia kugoma kula, endapo hatapelekwa mahakamani mapema.

Lissu ambaye ni mbunge kwa tiketi ya Chadema, alikuwa na kesi katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam, akituhumiwa kutumia lugha ya uchochezi katika kampeni za uchaguzi Jimbo la Dimani, Zanzibar.

Mbali na Lissu, wagombea wengine wanaowania nafasi hiyo inayoshikiliwa na Rais wa sasa, John Seka ni kada wa Chadema, Lawrence Masha na aliyewahi kuwa rais wa chama hicho mwaka 2011 hadi 2013, Francis Stolla.

Wengine ni Godwin Mwapongo na Victoria Mandari. Uchaguzi wa chama hicho unatarajia kufanyika Machi 18, mwaka huu na mawakili 6,000 watapiga kura kumchagua Rais mpya wa TLS.

Ufafanuzi wa Mwakyembe Alisema Serikali haina shida na wanachama wa TLS kuwa wanachama wa vyama vya siasa ila ni lazima wafahamu kwamba viongozi wanaowachagua ambao ndio watakaobeba sura ya TLS na mwelekeo mzima wa chama kama wanataaluma hawapaswi kuwa na nasaba za kisiasa ili kuepusha mgongano wa maslahi unapoweza kujitokeza.

“Serikali haina shida na wanachama wa TLS kuwa wanachama wa vyama vya siasa ila tatizo linakuja pale mnapotaka kuchagua viongozi ambao tayari wanazo kofia mbalimbali za uongozi ndani ya vyama vya siasa,” alisema na kuongeza: “Hao ndio watakaobeba sura na mtazamo au mwelekeo wenu hapo hatuwezi kukubali kwa kuwa watatenganishaje uongozi wao katika chama husika na uongozi wao ndani ya TLS, huo sasa ndio mgongano wa maslahi. “Ndio maana mwanasheria yeyote akiingia katika utumishi wa umma uwakili wa kujitegemea anauweka pembeni ili kuepuka mgongano wa maslahi.”

TLS sasa imekua na haihitaji muangalizi kama ilivyokuwa miaka ya nyuma nchi ilipopata uhuru, kwani ina wasomi wengi na vijana wengi wamekuwa wanachama pia na kwa hiyo ni bora tuifute hii Sheria yenu na tuwape mwanya mkajisajili kama NGO ambako kiongozi yeyote wa chama cha siasa anaweza kuwa kiongozi wao,” alisema.

Aliwataka wafahamu kuwa dhamira ya Serikali ni njema huku ikizingatiwa kwamba sheria kama zilivyo taaluma nyingine nchini, bado zinahitaji uangalizi hasa ukizingatia uingiaji wa nchi katika utengamano wa Jumuiya ya Afrika Mashariki.

Akizungumza katika kikao hicho, Katibu Mkuu wa Wizara, Profesa Sifuni Mchome alisema kila taaluma ina namna ya uangalizi wake. Alisema kama wanasheria lazima kuhakikisha hatutoi vipaumbele kwa siasa, kama zilivyo fani nyingine nchini.

Alitaka wajiulize kama kweli hawauoni mgongano wa maslahi, huku wakizingatia kuwa wanapaswa kuhudumia jamii ya watanzania bila ya kuwabagua.

“Kama wanasheria lazima tuhakikishe hatutoi vipaumbele kwa siasa kama zilivyo fani nyingine, jiulizeni kama kweli hamlioni jambo hilo kama ni kikwazo huku mkizingatia kuwa tunatakiwa kuhudumia jamii bila ya kuwabagua sasa tukijiingiza katika siasa tutaihudumiaje jamii husika? TLS kutojihusisha na siasa ni miongoni mwa kanuni za kutuimarisha kama wanataaluma,” alisema Profesa Mchome.

Alisema Wizara ipo kuiangaliaTLS, na ndicho ilichofanya.

“Tupo hapa kuwaangalia, na ndicho tulichofanya, tumewashtua jamani mnaenda wapi? Hatuna nia mbaya ila tunawataka muwe katika mstari, hivi kweli kamati ya uchaguzi haijaona kama kuna mgongano wa maslahi hapo?

Alisema Serikali haitasita kuchukua hatua ya kuifuta Sheria ya TLS, kama chama hicho kitaendelea na msimamo wa kujihusisha na masuala ya siasa au kiuharakati.

Alisema chama hicho hakina budi kuangalia namna kinavyoweza kujikwamua katika hilo.

Kama hamuwezi kuendeleza misingi ya kitaaluma ya kutojihusisha na siasa au vyama vya siasa, basi serikali haitakuwa na namna zaidi ya kuifuta sheria ya TLS na TLS ya sasa itabidi ikajisajili kama NGO ili iendeleze harakati zake; na Serikali itaunda sheria nyingine itakayoanzisha chombo kitakachosimamia misingi ya kitaaluma.

Eheee...Simba Wamficha Niyonzima Dar,Yanga Wahaha Usiku na Mchana Kumtafuta...!!!

$
0
0

UKISEMA Simba wamemficha kiungo mshambuliaji wa Yanga, Haruna Niyonzima, utakuwa hujakosea kabisa kwani tangu kumalizika kwa mpambano wa watani hao wa jadi hajaonekana tena uwanjani.

Katika mchezo huo ambao ulimalizika kwa Simba kushinda mabao 2-1, Niyonzima ni moja ya wachezaji ambao walishindwa kuonyesha kiwango kizuri na kuwafanya mashabiki kuondoka uwanjani vichwa chini.

Kiwango cha chini alichokionyesha Niyonzima katika mchezo huo kilisababisha mashabiki wa Yanga kuanza kukumbushia miaka iliyopita alipokuwa akihisishwa mapenzi yake ndani ya Simba.

Tangu mchezo huo dhidi ya Simba, Niyonzima hajaonekana tena na kikosi cha Yanga kwenye mechi na Ruvu Shooting pamoja na ile ya juzi ya Mtibwa Sugar, l

Uchunguzi uliofanywa  umebaini kuwa sababu kubwa ya kuondolewa Niyonzima katika kikosi cha Yanga ni mechi ya Simba.

Kwa sasa Mrwanda huyo aliyejiunga na Yanga Julai 2011 akitokea APR, ameonekana kukosa nafasi katika kikosi cha kocha Mzambia, George Lwandamina, huku kukiwa na taarifa kuwa wapo kwenye mpango wa kumsajili Kenny Ally kutoka Mbeya City ili awe mbadala wake.

Wakati mashabiki, viongozi na wanachama wa Yanga wakimwondoa kiungo wao mchezeshaji kikosini kwa madai ya kuwa na mapenzi na Simba, daktari wa kikosi cha Wanajangwani, Edward Bavu, amesema kuwa Niyonzima amekosekana katika mechi hizo mbili kutokana na matatizo  yakifamilia.

“Niyonzima hana tatizo la kiafya isipokuwa hakuweza kuwepo kwenye mechi hizi mbili zilizopita kutokana na matatizo ya kifamilia ambapo uongozi una taarifa hizo.

Exclusive..Petit Man Afunguka Yaliyomkua Lupango na Kipigo Alichopigwa na Makonda,Amtaja Wema Sepetu...!!!

$
0
0

MENEJA wa msanii wa Bongo Fleva, Bill Nass na County Boy anayefahamika kama Ahmed Salum ‘Petit Man’,  ameongelea fedheha na hasara iliyomkuta alipokumbwa na kashfa ya kuhusishwa na dawa za kulevya na kujikuta akiswekwa lupango.

Katika mazungumzo  juzi, Petit Man, alisema kitendo cha kukaa mahabusu kwa wiki moja kimempotezea fedha nyingi ambazo alikuwa amepanga kuingiza kwa wiki ile ili kuwafikisha hatua nyingine wasanii wake wanaomtegemea yeye kwa asilimia kubwa.

“Naumia sana nikizungumzia suala hili kwa sababu naona ni moja ya vitu ambavyo vilitaka kunitia umasikini, pesa (fedha) niliyoipoteza wiki ile ilikuwa ya kunitoa sehemu moja kwenda nyingine, ilikuwa nyingi na nilitarajia kufanya mengi sana,” alisema Petit Man.

Aliongeza kuwa mahabusu si sehemu nzuri kwani amejifunza mengi sana na amekumbana na watu tofauti ambao wengine ameweza kuwasaidia na wengine imeshindikana.

Akizungumzia kipigo alichodaiwa kupigwa, Petit Man, alisema kutangaziwa kupigwa ilikuwa kama fedheha kwake akikiri kwamba alipata misukosuko ya kawaida na si kipigo kama ilivyovumishwa.

“Nadhani Kamanda Sirro (Simon) ni askari mkubwa na msomi, sidhani kama anaweza kutoa adhabu isiyostahili na inayokiuka haki za binaadamu na mimi nilipata adhabu yangu kama mtuhumiwa na yote hiyo ilikuwa ni kupata ukweli na si mimi pekee, nadhani wengi walipata adhabu ili waseme, sasa huo uvumi mwingine mimi siutambui na huwa sipendi kuongelea  naona kama umeniletea fedheha kwenye jamii, kila mtu anatafsiri yake,” alisema Petit Man.

Aliongeza: “Mimi sina rekodi mbaya, nina imani hii adhabu kabla ya kuisha nitapewa ruhusa ya kufanya mambo yangu kwa uhuru, hakuna asiyenijua mimi ni mtu wa aina gani, napenda sana kushirikiana na watu wa aina zote na kumsaidia mtu pale ninapoweza.”

Akizungumzia sakata la aliyekuwa swahiba wake wa muda mrefu, Wema Sepetu, kuhama chama, alisema kila mtu ana mawazo yake na utashi wake hivyo kama ameamua kufanya hivyo, basi inabidi wao wawe wasikilizaji kwani Miss Tanzania 2016 huyo ana wazazi wake na kwamba hayo ni mapendekezo ya mtu.

Hata hivyo, aliweka wazi akisema: “Mimi na Wema bado ni familia moja japokuwa kila mtu ana kampuni yake, niliamua kutoka kwenda kwenye kampuni ili kujitafutia kipato na nitaendelea kushirikiana naye kwa kazi ambazo tulikuwa tukifanya.”

Pia alizungumzia ndoa yake na mkewe, Esma Kandili ‘Esma Platinumz’ ambaye ni dada wa msanii nguli wa Bongo Fleva, Nassib Abdul ‘Diamond’, akisema anaamini ndiye mwanamke aliyechaguliwa na Mungu na katu hatafikiria kwenda kwingine.

“Nina amini Esma ndiye mwanamke niliyechaguliwa na Mungu, tulijaribu kutengena ila ilishindikana na kujikuta kila mmoja akimhitaji mwenziye na sasa ndoa yetu imerudi, ifahamike ndiye aliyenipa heshima ya kuitwa baba baada ya kufanikiwa kupata mtoto aitwaye Taraj,” alisema Petiti Man.


Madawa ya Kulevya Yanavyomaliza Kipaji cha Chris Brown...!!!

$
0
0

MWANAMUZIKI Chris Brown ni miongoni mwa mastaa waliojizolea umaarufu mkubwa kutokana na maisha yao ya kila siku kutawaliwa na vituko.

Kwa sasa supastaa huyo anatajwa kuwa na matatizo ya akili tangu alipotemwa na meneja wake. Matatizo hayo yanatajwa kuchangiwa na utumizi wa dawa za kulevya.

Meneja Mike Guirguis aliachana na Chris mwaka jana huku akidai kudundwa na mwimbaji huyo na kulazimika kulazwa hospitali.

Kwa mujibu wa taarifa ya gazeti la New York Daily News, Mike G, alidai Chris alimwalika nyumbani kwake na ghafla alianza kumshambulia kwa ngumi nzito.

Itakumbukwa hata alipomshambulia kwa makonde aliyekuwa mpenzi wake, Rihanna, mwaka 2009, Chris alitajwa kuwa alikuwa ametumia dawa za kulevya.

Siku chache baada ya tukio hilo, Chris alikiri kuhudhuria ‘rehab’. Pia, ilisemekana kuwa kuachana na Karrueche Tran kulitokana na sababu hiyo.

Lakini sasa, baada ya Mike G kujiweka kando na shughuli zote zinazomhusu Chris, imeelezwa kuwa hali ni mbaya kwa mkali huyo kwani ameongeza ‘dozi’ ya dawa za kulevya.

Taarifa zimedai Chris hayuko sawa na amekuwa akitumia dawa za kulevya  kwa kiasi kikubwa, jambo linalotishia hatima ya maisha na kazi yake ya muziki.

Mmoja kati ya walinzi wake wa karibu alisema: “Baada ya kumfanyia vile Mike G, kila kitu kiliharibika.”

“Hatukuwa na meneja wa kutuambia cha kufanya na wapi tunaelekea. (Chris) akikasirika, anaweza kuwaambia watu walale kwenye gari (badala ya hotelini). Alikuwa akiwatisha watu na polisi. Alikuwa akijiita shetani.”

Kwa mujibu wa vyanzo mbalimbali vya habari za burudani, idadi kubwa ya wafanyakazi wake wameshamkimbia Chris.

Miongoni mwao ni aliyekuwa msimamizi wa ziara za kimuziki za staa huyo, Nancy Ghosh, ambaye alidai Chris alitishia kumpiga.

Mtaalamu wake wa matangazo, Nicole Perna, naye alikimbia kibarua kwa madai kuwa bosi wake huyo alimkashifu kwa madai kuwa alishindwa kutangaza kampuni yake ya mavazi ya Black Pyramid.

Lakini pia, hata marafiki wa karibu wa Chris wamekuwa wakiogopa kumsogelea mshikaji wao huyo kutokana na hali yake ya sasa.

“Huwezi kuzungumza na ‘mteja’, mtu ambaye hayuko sawa. Haingii akilini,” alisema mmoja wa marafiki zake.

“Ni jambo unalotakiwa kulifanyia kazi. Unatakiwa kubadili mfumo wako wa maisha. Hafanyi kile kinachopaswa kufanyika ili kurejea katika uzima, hivyo hawezi kuwa sawa.”

Kwa sasa watu pekee waliobaki karibu na Chris wanatajwa kuwa ni ndugu zake wa damu akiwamo mama yake mzazi.

Kwa wasiomfahamu, jina lake halisi ni Christopher Maurice “Chris” Brown na alizaliwa Mei 5, 1989. Ngoma yake ya kwanza ni ‘Run It!’ ambayo ilishika nafasi ya kwanza kwenye chati za Billboard.

Washauri Maiti Ziondolewe Moyo na Figo Baada ya Kufariki...!!!

$
0
0

Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) imeshauri Watanzania kuwa na utamaduni wa kuandika wosia wa kuchangia viungo vya binadamu wanapofariki, ikiwamo moyo.

JKCI imetoa usahuri huo baada ya kuwa katika matarajio ya kuanza upasuaji wa kupandikiza moyo mwingine nchini, kwa wagonjwa wenye matatizo ya kiungo hicho muhimu mwilini.

Mkurugenzi wa Upasuaji na daktari bingwa wa upasuaji wa moyo na mishipa ya damu, Dk. Bashir Nyangasa alitoa ushauri huo jana jijini Dar es Salaam, alipokuwa akizungumza na vyombo vya habari kuhusu malengo ya taasisi hiyo.

“Tuko katika maandalizi ya kuandaa mapendekezo kwa ajili ya kupeleka bungeni ili Bunge liridhie na kupitisha sheria itakayoruhusu mtu kuandika wosia wa viungo vyake kutumika baada ya kufariki, ikiwamo moyo, figo na viungo vingine,” alifafanua Dk. Nyangasa.

Alisema umefika wakati kwa Watanzania kujiwekea utaratibu wa kuacha wosia wa kutumika kwa viungo vyao baada ya kufariki.

Alisema baada ya Mtanzania kufariki, kiungo husika kitatolewa kwenye maiti na kuhifadhiwa katika benki za viungo ili viweze kutumika na watu ambao wanauhitaji.

Aidha, Dk. Nyangasa amesema hospitali ya Apolo Bangalore ya India na hospitali nyingine za kimataifa za magonjwa ya moyo, kwa sasa zimehamia JKCI kutokana na huduma pamoja na vifaa vinavyopatikana katika hospitali hizo vinapatikana katika taasisi hiyo.

Kwa upande wake Naibu Mkurugenzi Huduma za Tiba, Daktari Bingwa wa Wagonjwa wa Moyo, Dk. Tulizo Shemu amesema kwa mwaka 2016 JKCI imefanya uchunguzi wa tiba kwa wagonjwa 973, kati ya wagonjwa hao 620 walipatiwa matibabu ya moyo ya bila kufungua kifua kwa kupitia mishipa ya damu (Catheterization) na wagonjwa 353 walifanyiwa upasuaji wa kufungua kifua.

Aidha, Dk. Shemu alisema kwa mwaka huu taasisi hiyo imejipanga kufanya upasuaji wa kupasua kifua kwa wagonjwa 700 na wagonjwa wengine 1,000 watafanyiwa operesheni bila ya kufungua kifua.

Taasisi hiyo inategemea kuwa na kambi maalum ya matibabu ya moyo kwa kushirikiana na Taasisi ya Open Heart International ya nchini Australia kuanzia keshokutwa; ambapo wagonjwa 25 wakiwamo watoto 15 na watu wazima 10 watafanyiwa upasuaji.

Wananchi wameombwa kujitokeza kuchangia damu kutokana na uhitaji wa damu nyingi katika upasuaji huo.

Shinda Gari ya Bure Kabisa Kutoka Kampuni ya Magari Japan

$
0
0
Umeshawahi Kufikiria Kupata Gari la Bure bila Kulipa Chochote, Basi hii Kampuni ya Cars From Japan Wanakupa Nafasi Hiyo ... 

Chakufanya ni Kubofya Link hapo chini na Ufate Maelekezo ya Jinsi ya Kuweza Kuwa Mshindi wa Gari hilo..


Kisha Jisajili kwa Kuweka Jina na Email Yako... USIWE NA WASIWASI HUDUMA HII NI SALAMA KABISA..

Jinsi ya kujiunga:

Bofya hayo maandishi ya rangi ya blue kisha itafunguka kurasa ambayo itakuwa iko hivi.


Kisha Bofya neno APPLY NOW kisha itafunguka hivi.


Kisha utajaza Form hii kisha utaBofya neno NEXT itafunguka kurasa ingine nayo ufate maelezo yake..

Mwisho wa Kujisajili ni 22 / 3 / 2017

Nape Nhauye: Nitamlinda mwekezaji wa Radio E-FM

$
0
0
WAZIRI wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo, Nape Nnauye, ameahidi kulinda uwekezaji wa mmiliki wa kituo cha Redio EFM na Tv E, Francis Ciza, maarufu Dj Majizo.

Nape alitoa kauli hiyo jana wakati alipotembelea makao makuu ya kituo hicho cha redio katika eneo la Kawe, Dar es Salaam.

Katika hotuba yake fupi aliyoitoa mbele ya watumishi wa redio hiyo jana, Nape alisema yeye ndiye waziri mwenye dhamana ya habari, hivyo ana wajibu wa kulinda habari na wawekezaji katika tasnia hiyo.

“Nataka nikuhakikishie mimi ndie waziri mwenye dhamana ya habari, kuilinda habari na tasnia yenyewe, lakini kuwalinda wanaowekeza kwenye tasnia hii, kwa sababu uwekezaji kama huu ulioufanya katika tasnia hii, ndio unanifanya mimi kama waziri niendelee kuwapo.

“Lakini ndio unaoifanya Serikali na Tanzania kuendelea kuwa nchi njema ya watu waendelee kuishi, kazi yako ni nzuri na nyinyi kwa kuwa mnasikika sana Dar es Salaam, mchango wenu wa kuifanya Dar es Salaam kuwa njema ni mkubwa na hauwezi kupuuzwa hata kidogo.

“Kwa mtu yeyote mwenye mapenzi mema na Dar es Salaam na Tanzania kwa ujumla atawalindeni, atawalinda na kuhakikisha mnapata ushirikiano wa kutosha katika kutekeleza majukumu yenu,” alisema.

Nape pia alimpongeza Majizo kwa uwekezaji mkubwa alioufanya na kuahidi kwamba serikali itampatia ushirikiano na msaada anaouhitaji ili kuhakikisha uwekezaji wake unasonga mbele.

“Kama Serikali na kama waziri mwenye dhamana ya habari, nimeshuhudia kwa macho yangu uwekezaji uliouweka hapa, tutalinda uwekezaji uliouweka usiharibiwe ovyo.

“Si Watanzania wengi wenye maono haya, najua umeanza mbali mpaka kufika hapa, si kazi rahisi, ndiyo maana nasema ukiona mtu kasimama si vizuri kwenda kumparamia ovyo.

“Ni vizuri kuheshimu kazi ambayo amehangaika nayo, jasho si la bure, uwekezaji huu ni mkubwa sana, labda iwe hujui alichowekeza, hujui kapambana kiasi gani kufika hapo ndiyo unaweza kufanya unachotaka,” alisema Nape.

 Nape alisema katika dunia yenye ushindani vita ni kubwa, hivyo akamtaka mwekezaji huyo asikatishwe tamaa na kelele za barabarani kwa sababu Serikali iko pamoja naye.

Aliwaeleza pia watumishi wa redio hiyo kwamba wasiwe na hofu kwa sababu kazi wanayoifanya ina baraka za Mungu, hivyo hawapaswi kuvunjika moyo.

“Mkiona mti unaotupiwa mawe ni ule wenye matunda, kwa miaka mitatu mafanikio mliyoyapata ni makubwa sana, lazima yatamtisha yule aliepo sokoni, kwahiyo mkiona kuna vita basi mjue ni kwa sababu kasi yenu ni kubwa mno kiasi kwamba inawatia joto wengine.

“Mtu mmoja aliwahi kuniambia wakati naanza siasa kwamba ukiona watu hawakuzungumzii jiulize kama bado unaishi au umeishakufa, ukiona watu wanakuzungumza ujue umewazidi,” alisema Nape.

Majizo ni mmoja wa watu waliohusishwa na dawa za kulevya katika kampeni iliyokuwa ikiendeshwa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda na Kamanda wa Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Simon Sirro.
Viewing all 104712 articles
Browse latest View live


Latest Images