Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104789 articles
Browse latest View live

MIAKA IJAYO MAHOUSE GIRL NDIO WATAKUWA WAKE WA KUOA

$
0
0
Kama nilivyo elezea kwenye kichwa cha habari hapo juu,
siku hizi watu wengi wamekuwa na mtindo wa kuajiri wasichana wa kazi (mahouse girl) ili kusaidia kazi za nyumbani.
Ndio hatukatai pengine mama mwenye nyumba anaweza kuwa anazidiwa na kazi,
Kama kufua nguo za mzee,watoto,kunyoosha, kuandaa chakula nk.
Lakini kuna wadada/wanawake wengine unakuta watu wako wawili yeye na mumewe,
eti nao wanaweka house girl sijui wa nini?eeh!!!
tena wengine sijui ni sifa eti anaajiri wawili kabisa kwa kazi zipi sasa?na wewe ufanye kazi gani?
Ya kupaka rangi kucha na kuchat kwenye mitandao? halafu bila aibu unasifia chakula alichoandaa house girl mbele ya mumeo.


Na unaangalia tu house girl anamnawisha mikono mumeo na kumkausha na taulo,wewe upo tu kwenye kiti kama umegundishwa na super glue vile.
huyo jamaa yako akila chakula kitamu cha house girl, si atataka ale na kile cha usiku aone utam wake?
hapo ndipo timing zinapoanzia na ukizingatia mahouse girl walivyo na heshima,
baba akifika na kamzigo anapokelewa kwa mikono miwili na anapigiwa goti,
wakati huo we upo upo tu kama koti la mvua linasubiri masika.
Sijui ndio kusema hamuelewi mko pale kwa ajiri gani?na house girl akiboronga kidogo tu macho na sauti ya ukali inakutoka kama nini,
Hujui kwamba unapofanya hivyo unamkomaza house girl,hapo kwako ni sawa na chuoni kwake anachukua mafunzo ya maisha.
Mumeo akisifiwa kazini nguo zake zinang'aa atamkumbuka house girl,
akisifiwa kwamba ananawili atamkumbuka house girl,
akisifiwa kwamba viatu vyake vinang'aa atamkumbuka house girl,
Ndio si house girl ndio anaye fanikisha yote hayo?wakati wewe uko bizy ku up load picha fb?
mwisho wa siku unatemwa kama big G iliyo chacha,
halafu watu wanabaki kushangaa mbona jamaa kamuacha mwanamke mzuri vile halafu kabeba house girl?
kumbe ni janga la kitaifa hajui A wala B kifupi hajitambui,
Badilikeni nyie kina Eva ma house girl watawapiga bao ohooo!!!!!!

IKIWA LEO NI SIKU YAKE YA KUZALIWA..., JACKLINE WOLPER APATA AJALI AKIWA NYUMBANI KWAKE ALIPOKUWA ANATOA GARI.

$
0
0
Leo ni siku ya kuzaliwa kwa miongoni mwa wasanii wanaofanya vizuri katika tasnia ya filamu hapa nchini Jacklyn Wolper.

Kupitia kwenye instagram Desemba 6 amepost picha ambayo ikionesha amenusurika kuumia baada ya kuondoa gari  lake kwa kasi na kupelekea kugonga tanki la maji na kusababishaa ajali.



Huu ndio ujumbe wake 'dah kuzaliwa cku moja na kufa ni cku moja nando maana kila cku nasisitiza upendo na chuki zisizokua na sababu.hvii leo ni bthday yangu lakn nilikua nauvaa ukuta wakat nasogeza gar ioshwe tayar kwa maandaliz .wakat nakanyaga brk kumbe nakanyaga mafuta maskn ya mungu nimebomoa matnk ya maji yote nimepasua mabomba yote nimegonga gar nyingne but yote nikumshukuru mungu kwakua sijaumia ila prsh ilishuka kidogo but now npo ok.asante mwenyezi mungu,mungu wa wote,kimbilio la wote na wewe ndo kimbilio langu.niombeeni maskn'Aliandika Wolper

LILE GARI LA WOLPER AINA YA BMW X6 ALILOPEWA NA DALAS LAOZEA YADI DAR

$
0
0
LILE gari aina ya BMW X6 alilokuwa akitanulia mwigizaji Jacqueline Wolper linaendelea kuoza katika yadi ya Majembe, Mwenge jijini Dar kutokana na kudaiwa ushuru.

Taarifa ambazo Risasi Jumamosi limezipata kutoka katika vyanzo tofauti, zimeeleza kuwa hakuna uwezekano wa gari hilo kurudi katika mikono ya Wolper kwani aliingizwa mkenge tangu aliponunuliwa na aliyekuwa mpenzi wake, Abdallah Mtoro ‘Dallas’.

“Wolper aliingizwa mkenge tangu aliponunuliwa lile gari, lilikuwa linadaiwa ushuru sasa yeye bila kujua akaingizwa mkenge na pedeshee Ndama na kisha mtego wa kulinasa ukafanyika, Ndama huyohuyo akaja kumgeuka akawa anaeneza uvumi kuwa Wolper kaingizwa mkenge,” kilidai chanzo.

Akizungumza na paparazi wetu hivi karibuni, Wolper aliweka bayana kuwa gari lile alilonunuliwa kwa dola 130,000 (zaidi ya Sh. Mil. 170 ) kipindi penzi lake na Dallas lilipokuwa likichanua, mwaka jana polisi wa kimataifa (Interpol) kwa kushirikiana na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) walilikamata kwa kudaiwa ushuru.

“Sina ujanja tena kwani hata mimi nilikuwa sijaelewa kama linadaiwa lakini Ndama ndiye aliyejua mchongo mzima, akaniingiza chaka. Hadi sasa linaozea pale Majembe,  sina jinsi, namuachia Mungu,” alisema Wolper na kuongeza:
“Nilipolikabidhi Majembe na kuonesha documents (nyaraka) zote, niliambiwa nitalipata baada ya muda lakini mpaka leo sijaambiwa lolote. Linaozea pale.”
Chanzo:Global P

MTOTO: NIMECHOKA KUBAKWA NA BABA

$
0
0
Stori: JOSEPH NGILISHO, Arusha
AMA kweli dunia sasa inaserereka! Katika hali ya kusikitisha, baba mzazi mwenye familia ya watoto watatu, mkazi wa Kambi ya Fisi jijini hapa, anashikiliwa na polisi kwa tuhuma za kumbaka binti yake wa kumzaa hadi mtoto akafungua kinywa na kusema: “Nimechoka kubakwa na baba.”

Tukio hilo lililobumburuka hivi karibuni limewaacha watu vinywa wazi kwa sababu mtoto huyo ana umri wa miaka minane na kwamba alianza kufanyiwa ukatili huo mwaka jana akiwa na umri wa miaka saba alipokuwa darasa la pili katika shule moja ya msingi jijini hapa (jina tunalo).

AFUMWA LAIVU!
Inadaiwa kwamba mtuhumiwa huyo aliyetajwa kwa jina moja la Pelejai (34) ambaye ni mfanyabiashara wa mkaa, amemwingilia mwanaye huyo kwa mwaka mmoja.

Taarifa zinasema, mwaka jana baba huyo aliwahi kufumwa laivu na mkewe akimtendea ubaya huo binti yake huyo.
Hata hivyo, inasemekana kuwa baada ya kunaswa chumbani kwake na mtoto, alimuomba msamaha mkewe ambaye alimsamehe kwa sharti la kutorudia tena kufanya tendo hilo la aibu na jambo hilo likawa siri kati yao.
Akizungumza kwa uchungu na gazeti hili akiwa katika Hospitali ya Mkoa ya Mount Meru anakopatiwa matibabu, mtoto huyo alisema chanzo cha baba yake kumbaka ni baada ya mzazi huyo kugombana na mama yake ambaye aliondoka nyumbani na kwenda kwao.


MARA YA KWANZA
Alisema mara ya kwanza kuingiliwa na baba yake alisikia maumivu makali mno huku akitokwa na damu nyingi.
Alieleza kuwa alijaribu kulia na kupiga kelele usiku huo lakini baba yake alimziba mdomo ili asitoe sauti.
Alisema alipomaliza kumfanyia ‘unyambilisi’ huo alimtishia kuwa endapo atasema popote, yeye atakamatwa na kufungwa na wao watabaki bila baba, hivyo watateseka kwa njaa.
Baada ya muda mtoto huyo alieleza kwamba baba yake huyo aliendelea kumwingilia mara kwa mara wakati kaka yake mkubwa wanayeishi naye akishindwa kusema baada ya kupewa fedha na baba yake.

MY GOD! KITANDA KIMOJA!
Alisimulia zaidi mtoto huyo alisema kwamba alikuwa akilala na baba yake kitanda kimoja kila siku kama mke na mume katika kipindi ambacho mama yake alipokwenda kijijini kwao Nduruma wilayani Arumeru kujifungua na kukaa kwa zaidi ya miezi mitatu.

“Ukweli nilichoka kubakwa na baba yangu lakini chanzo cha yote ni mama kutokuwepo nyumbani,” alisema mwanafunzi huyo.
Kwa upande wake, mama mzazi wa mtoto huyo alisema kuwa aligundua tukio la kubakwa kwa mwanaye tangu Machi mwaka huu na baada ya tukio hilo mumewe alimwomba tena msamaha kwa mara nyingine  na yeye kumsamehe.

Mama huyo alisema kwamba alilazimika kwenda nyumbani kwao baada ya ujauzito aliokuwa nao kuwa mkubwa.

Alisema baada ya kujifungua aliendelea kuishi huko hadi Novemba 28, mwaka huu alipolazimika kurejea na kichanga chake baada ya kupata taarifa za kupotea kwa mtoto wake huyo anayedaiwa kubakwa na baba yake.

Alisema aliporejea nyumbani kwake Kambi ya Fisi alimuuliza mtoto wake mkubwa iwapo baba yake alirudia tabia ya kumbaka mwanaye lakini mtoto huyo hakusema chochote.

Akiwa anatafakari sehemu alipokuwa mwanaye ndipo alipopata taarifa kwamba alikuwa kituo cha polisi alikopelekwa na walimu wake baada ya watoto wenzake kutoa taarifa kwa walimu kuwa mwanafunzi mwenzao amekuwa akibakwa na baba yake mzazi.

SHULENI
Mmoja wa walimu katika shule hiyo alithibitisha kubakwa kwa mwanafunzi huyo baada ya kumhoji na kumkagua na kugundua kwamba ameharibika sehemu nyeti na kuwa kama za mtu mzima.


HOSPITALINI
Mama wa mtoto huyo akisaidiwa na walimu walitoa taarifa kituo cha polisi na kupatiwa hati ya matibabu (PF-3) na kumpeleka Hospitali ya Mount Meru.

Mwalimu wa shule hiyo alisema baada ya vipimo, daktari alithibitsha kwamba mtoto huyo alibakwa na kuharibiwa sehemu zake za siri.

Baada ya taarifa hizo kulifikia jeshi la polisi, vijana wa Inspekta Said Mwema walimtia mbaroni mtuhumiwa huyo na kumfungulia kesi ya ubakaji kwa hati ya mashtaka AR/RB/16064/2013-

UBAKAJI 
Uchunguzi wa tukio hilo ukikamilika, mtuhumiwa atafikishwa mahakamani ili sheria ichukue mkondo wake.

INAUMA SANA!
Hivi karibuni kumeibuka vitendo vingi vya ubakaji na unyanyasaji kwa watoto, hivyo Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, Sophia Simba na taasisi nyingine za utetezi wanaombwa kuingilia kati ili kuwanusuru watoto na ukatili huo.
Chanzo:Global P

KUVUNJIKA KWA NDOA YA THEA, USHIRIKINA WATAJWA

$
0
0
Stori: Gladness Mallya na Hamida Hassan
SIKU chache baada ya ndoa ya mastaa wawili wa filamu Bongo, Salome Ndumbagwe Misayo ‘Thea’ na Michael Sangu ‘Mike’ kuvunjika, imedaiwa mambo ya kishirikina yanahusika kwani mauzauza yalianza siku nyingi zilizopita.

Mtu wa karibu wa mastaa hao aliyeomba jina lake liwekwe kapuni alidai kuwa mara kadhaa wasanii hao wamekuwa wakikumbwa na mambo ya ajabu yaliyoashiria kuwa ndoa yao haina uhai.

“Unajua kwa nyakati tofauti pete za ndoa za Thea na Mike ziliwahi kuwatoka kiajabu vidoleni wakiwa chooni. Haikuwa jambo la kawaida na wenyewe walishituka na kukosa amani,” alisema mtoa habari huyo.

Hata hivyo, wahusika wamekuwa wakiamini kuvunjika kwa ndoa yao ni mipango ya Mungu licha ya Mike kuhisi kuwepo kwa nguvu za giza katika kuachana kwao.

“Mimi naamini kila linalotokea ni mipango ya Mungu lakini katika hili mmh, napata mashaka,” alisema Mike.
Naye The alisema: Mungu hakupanga tu tuendelee kuwa kwenye ndoa, kwa hiyo limetokea na maisha yanaendelea.”
Chanzo:Global P

MUONEKANO WA MABASI YAENDAYO KASI YATAKAYO TUMIKA BONGO [PICHA]

$
0
0

Mabasi ya mwendo kasi 2014 kimara kivukoni.  Picha kwa hisani ya Deo Mutta Mwanatanga
Basi la kwanza la mradi wa mabasi yaendayo kasi limewasili nchini na kuanza kufanya majaribio katika barabara zilizokwisha kamilika huku mengine yakitarajiwa kuwasili mapema mwaka kesho.

Mtendaji mkuu wakala wa mradi wa mabasi yaendayo haraka Bi Asteria lambo amesema basi hilo ni miongoni mwa mabasi madogo yatakayoingia nchini yenye uwezo wa kubeba zaidi ya abiria 40 na makubwa yatabeba abiria zaidi ya 150 na kuwataka wakazi wa jiji la Dar es Salamu kuendelea kuwa na subira na kuwahakikishia mradi huo sio ndoto na adha ya usafiri itapungua mapema mwaka kesho.

Nao baadhi ya wakazi wa jiji walioshuhudia gari hilo wameelezea kufurahishwa na kuanza kuwa na imani na serikali yao ambapo wamesema kama mradi huo utakamilika kwa muda uliopangwa utakuwa faraja sana kutokana na adha kubwa ya usafiri wanayokumbana nayo  huku wakitoa wito kwa mamlaka husika kupanga mikakati ya kupunguza nauli za mabasi hayo pindi yatakapoanza kufanya safari zao.

BRAZIL FIFA WORLD CUP-HIVI NDIVYO MAKUNDI YALIVYOPAGWA

$
0
0
The 2014 FIFA World Cup draw took place in Brazil today 
lipi ni kundi la Kifo hapo?

TEAM YA TAIFA STARS KUFA NA KUPONA LEO-LAZIMA WAGANDA WAKAE

$
0
0
Kilimanjaro Stars yenye mastraika gumzo, Thomas Ulimwengu na Mbwana Samatta inashuka mjini Mombasa leo kuikabili timu ngumu ya Uganda ambayo haijaruhusu hata bao moja kwenye Chalenji msimu huu.

Mechi hiyo ni gumzo zaidi kwa Wakenya ambao timu yao inacheza na Rwanda jioni kwenye Uwanja huohuo wa Manispaa ya Mombasa. Mshindi wa mechi ya Stars atacheza na mshindi wa Kenya na Rwanda kwenye nusu fainali mjini Kisumu.

Robo fainali zingine zitapigwa kesho kwa Zambia kuivaa Burundi mchana na Ethiopia kucheza na Sudan jioni. Mechi ya Stars na Uganda inatazamiwa kuwa na mvuto wa aina yake kutokana na umahiri wa wachezaji wanaounda vikosi hivyo ambao ni maarufu zaidi kwenye ukanda wa Cecafa.

Uganda chini ya Kocha Mserbia, Sredejovic Milutin ‘Micho’ imeishinda Stars katika mechi mbili za mwisho ilizocheza nao kuwania kufuzu Chan lakini kikosi cha Kim Poulsen hakikuwa na mastraika Mbwana Samatta na Thomas Ulimwengu wanaocheza TP Mazembe wa kipa mahiri Ivo Mapunda wa Gor Mahia ya Kenya.

Mechi hiyo itakuwa na utamu wa aina yake kwani Stars itakuwa chini ya ukuta mahiri ulioruhusu goli moja wa Said Morad na Kelvin Yondani huku pembeni wakisimama Erasto Nyoni na Himid Mao.

Kwenye kiungo huenda akasimama Frank Domayo na Aboubakary Salum ‘Sureboy’ ambao watakuwa wakigawa mipira kwa Mrisho Ngassa, Ulimwengu, Samatta na Amri Kiemba.

Kikosi hicho kilicheza mechi ya mwisho dhidi ya Burundi na kutengeneza nafasi nyingi za mabao ambapo Poulsen alisema “Timu iliyocheza na Burundi ilitengeneza nafasi nyingi sana za kufunga na ilikuwa ya kushambulia zaidi, ilicheza mpira wa hali ya juu sana sioni sababu ya kuibadilisha ila tunaweza kuiboresha zaidi.”

“Tunaingia kwa nguvu kwenye robo fainali, tunakutana na timu ngumu lakini tutapambana na kuonyesha uwezo wetu tuna imani tutashinda na lengo ni kwenda nusu fainali, mashindano ndio yanaanza sasa,” alisisitiza Poulsen huku mastraika wake Samatta na Ngassa wakiahidi makubwa.

Ngassa: “Sisi tuko sawa na tumefika hapa tulipo kutokana na umahiri wetu, tutafanya kazi nzuri kwa vile tunataka kufika mbali na tunachukua hadhari kubwa.”

Uganda inaingia na ukuta imara ambayo katika mechi tatu haujaruhusu bao hata moja lakini fowadi yake imefunga mabao matano huku Stars ikiwa imefunga mawili.

Fowadi yake itakuwa na Emmanuel Okwi, Danny Serunkuma na Hamis Kiiza ambaye huenda asiwe kwenye fomu kutokana na kufiwa na baba yake mdogo juzi lakini uongozi ukamwomba abaki.

Kocha Micho alilalamika kwamba Stars imekuwa na muda mwingi wa kupumzika kuliko kikosi chake ambako kilicheza juzi Alhamisi wakati stars ilicheza Jumatano.

MAZISHI YA MAREHEMU NELSON MANDELA KUVUNJA RECORD

$
0
0

Afrika na dunia inatarajiwa kushuhudia kitu kipya katika maziko ya Rais wa zamani wa Afrika Kusini, Nelson Mandela (95) aliyefariki dunia juzi, baada ya kuugua kwa zaidi ya miezi sita.

Serikali ya Afrika Kusini imesema kiongozi huyo ambaye atazikwa Desemba 15, imeandaa mazishi ya kihistoria yanayosemekana yatazidi yale ya Papa John 11.

Matukio ya shughuli mbalimbali zinazohusu mipango ya maziko ya kiongozi huyo maarufu yanatarajiwa kushuhudiwa sehemu mbalimbali duniani, tofauti na tukio jingine lililowahi kutokea barani Afrika mbali na kombe la dunia.

Rais Jacob Zuma alisema jana kwamba “Mpendwa wetu Madiba atazikwa kwa heshima zote za Serikali. Nimeagiza bendera zote za Afrika Kusini zipepee nusu mlingoti na hiyo itaendelea hivyo hadi tutakapokamilisha mazishi yake.

Mazishi ya Mandela yanalinganishwa na yale ya Papa John Paul II mwaka 2005, ambayo yalihudhuriwa na wafalme watano, malkia sita wa falme mbalimbali na marais wapatao 70 na mawaziri kadhaa, wakiwamo wafuasi wake zaidi ya milioni mbili. Yanakadiriwa pia kulingana na maziko ya Winston Churchil aliyekuwa Waziri Mkuu wa Uingereza mwaka 1965.

Marais wote wa Marekani walio hai wanatarajiwa kuhudhuria mazishi hayo iwapo afya zao zitawaruhusu kusafiri, pamoja na Prince Charles wa Uingereza na hata Rais Robert Mugabe wa Zimbabwe. Pia watu maarufu wenye urafiki wa karibu na Mandela akiwamo msanii Oprah Winfrey wameshathibitisha kuhudhuria.

NELSON MANDELA: HAKUNA WA KUFANANA NAE

$
0
0
DUNIA yamlilia Nelson Mandela, ndivyo inavyoweza kuelezwa kwa maneno machache kuelezea namna msiba wa shujaa huyo wa vita dhidi ya ubaguzi wa rangi ulivyogusa mioyo ya watu wa rika, rangi na mataifa mbalimbali duniani.

Kifo cha Mandela, maarufu miongoni mwa raia wenzake wa Afrika Kusini kwa jina la Madiba kimethibitisha pasi na shaka kwamba, ameondoka mwanadamu maarufu zaidi duniani ambaye alama alizoacha nyuma yake zinampambanua kuwa mtu asiyeweza kulinganishwa na mwingine yeyote.

Kwa Watanzania, machungu ya kifo cha Mandela kilichotokea juzi usiku yanaweza yakalinganishwa na yale ya Oktoba 14 mwaka 1999, wakati taifa lilipompoteza Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere. 

Si ajabu hata kidogo kwamba, mwangwi wa msiba huu wa Madiba, kipenzi kikubwa kwa watu wa rangi na asili tofauti nchini mwake, umesafiri na kufika katika kona zote za dunia kwa kiwango cha kuwaliza watu maarufu zaidi hadi wale wa kawaida.

Ni kutokana na uzito wa msiba huo, ndiyo maana serikali ya Tanzania jana ilitangaza siku tatu za maombolezo ambazo zinakwenda sambamba na kupepea kwa bendera nusu mlingoti.

Hali kama hiyo ndiyo pia iliyoonekana hata nchini Marekani ambako taifa hilo kubwa kabisa duniani limeingia msibani kwa namna inayoonyesha kwamba aliyefariki dunia alikuwa raia nambari moja wa dunia. 

Ni kwa kulitambua hilo na kwa kujua ukweli kwamba Mandela hakuwa tu mali ya raia wa Afrika Kusini ndiyo maana taarifa rasmi ya kifo hicho iliyotolewa na Rais Jacob Zuma ilikuwa na maneno yenye ujumbe wenye maneno mazito.

"Taifa letu limempoteza mtoto wake mkuu wa kiume. Watu wetu wamempoteza baba. Licha ya kwamba tulifahamu kuwa siku kama hii ingemtokea, hakuna kinachopunguza upendo wetu kwake na hasara kubwa tuliyopata. Jitihada zake kutafuta uhuru zimemjengea heshima kubwa duniani.

"Unyenyekevu wake, upendo wake na utu wake, vimesababisha watu kumpenda. Mawazo yetu na sala zetu tunazielekeza kwa familia ya Mandela. Kwao tuna deni kubwa la kuwashukuru. Walijitolea kwa kiasi kikubwa na kuvumilia mengi ili watu wetu wawe huru,” alieleza Zuma wakati akitangaza kwa mara ya kwanza msiba huo mzito.

Hakuishia hapo, Zuma aliwataka watu wanaomlilia Madiba duniani kote kukumbuka mambo ambayo Madiba alipigania. 

"Hebu tujibidishe bila kupoteza nguvu kujenga Afrika Kusini yenye umoja, isiyo na ubaguzi wa rangi, isiyo na ubaguzi wa kijinsia, Afrika Kusini ya kidemokrasia na ustawi. Hebu tueleze kwa namna yetu wenyewe, shukrani kubwa tuliyonayo kwa mtu ambaye ametumia muda mwingi kuwatumikia watu wa nchi hii na kwa minajili ya utu,” alisema Zuma kwa uchungu.

MAJANGA:WAZIRI MUHONGO ASUSIA NDEGE, KISA KAKOSA FIRST CLASS SEAT

$
0
0
WAZIRI wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo, amegoma kusafiri na Watanzania wenzake kwenda nchini Algeria kwa daraja la kawaida baada ya kukosa daraja la kwanza, hivyo kuahirisha safari yake kwa siku moja, Tanzania Daima limebaini.

Profesa Muhongo ambaye amekuwa akionyesha dharau kwa Watanzania mara kadhaa, aligoma kusafiri katika Uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere, Dar es Salaam Jumapili ya Novemba 24, 2013, saa 10.45 akiwa na wenzake tisa kwenda kwenye safari ya kikazi nchini Algeria alikoenda baadaye.Moja ya kauli ya dharau iliyotolewa hivi karibuni na Waziri Muhongo ni pale aliposema wafanyabiashara Watanzania wana uwezo wa kuwekeza kwenye soda na juisi badala ya gesi na pia aliwahi kuwashambulia viongozi wa dini kwa kuwaita waongo.

Uchunguzi wa Tanzania Daima uliofanyika kwa siku kadhaa sasa, umethibitisha kwamba Muhongo alikuwa aondoke na ndege ya shirika la ndege la Emirates namba EK 726 kutoka Uwanja wa Ndege wa Mwalimu Nyerere kupitia Dubai kwenda Algeria akiwa na tiketi ya daraja la kawaida bila kujua kabla ya kufika uwanjani hapo na kisha kuanza kumfokea kila aliyekuwa anamsemesha.

“Tiketi yake na wenzake kumi ilikuwa ni Economy Class (Daraja la Kawaida), lakini akakataa akitaka asafiri kwa First Class (Daraja la Kwanza). Alibembelezwa na wenzake na wafanyakazi wa Emirates na wale wa Uwanja wa Ndege lakini akagoma huku akifoka na wenzake wakataka kuahirisha safari.

Ikawa tena ni sisi kuwaomba wasafiri ili Bwana Mkubwa (Muhongo) atafutiwe nafasi kwa daraja analotaka.
“Walimbembeleza wakamwambia kwa kutumia ‘millage’ ya safari zake watambadilishia akiwa ndani ya ndege na kumuweka daraja la kwanza lakini alionekana ameshakuwa mkali na hakuwa anamsikiliza yeyote.“Baadaye tulifanikiwa kuwashawishi wenzake kuendelea na safari na yeye sijui aliondoka na ndege gani tena maana wakubwa wetu wana mambo sana,” anasema ofisa mmoja uwanjani hapo.

Taarifa za awali kuhusu sakata hili, ziliripotiwa siku hiyo katika mtandao wa jamiiforums.com zikieleza kwamba kitendo cha Waziri Muhongo cha kususia safari hiyo, kiliwakera baadhi ya wasafiri wakiwamo raia wa kigeni ambao walishangazwa na hatua hiyo ya kiongozi wa nchi maskini inayotegemea misaada kulazimisha kusafiri kwa daraja la kwanza, daraja ambalo viongozi wa mataifa makubwa hawaruhusiwi kusafiri bila sababu maalumu.

Taarifa hiyo kwenye mtandao wa JamiiForums. Com iliripotiwa hivi: “Kweli viongozi wa nchi hii wanatia aibu, wakati mawaziri wa Uingereza wanakataa First Class, hapa kwetu kimetokea kioja. Waziri wenu wa Nishati na Madini (Muhongo) ambaye anazidi kutulaza na joto na giza leo amewaacha hoi Watanzania pale alipofika mpaka Airport na akiwa anaboard akakuta anawekwa sehemu ya abiria wa daraja la kati, baada ya kuambiwa hayuko First Class akagoma na kutoka nje ya mlango. Wakati hayo yakiendelea kumbe ana wenzake zaidi ya tisa wako economy na wawili Bussiness Class, ghafla nao wakaanza kushuka.

“Hapo ndipo hekima za mmoja wa wahusika wa Airline (Emirates) akawaomba hao waende ili yeye akabadilishe aje kesho yake.” “Jamani kweli First Class inakushushia aibu hivi Profesa na bado unasema maisha magumu Tanzania!? Inaonekana zile buti za bora ulizivalia ukiwa form V na haya ndio madhara yake, mnapewa vyeo wakati maisha yalishawapiga; mnatafuta muafaka na Yesu mkiwa madarakani,” anaeleza mtu aliyewasilisha mada husika akijulikana kwa jina la Basiasi.

Basiasi alihoji sababu ya abiria wenzake ambao nao walikuwa wakisafiri kikazi kutaka kushuka na kusababisha hasara kwa serikali au wafadhili waliokata tiketi hizo. Kwa utaratibu wa kawaida abiria anayeahirisha safari baada ya kuwa ameshaingia ndani ya eneo la kusafiria (boarding) anaweza kupoteza kabisa tiketi au kulipishwa fedha nyingi zinazoweza kuwa sawa na kununua tiketi mpya.

“Hebu kuweni wastaarabu, sasa wale watu tisa walitaka kuwashusha kwa nini na kama wamekwenda, mlishindwa kuwaambia wabaki mpaka mkaanza kuleta aibu uwanjani? Inaonekena ndege mmeanza kupanda uzeeni; najiuliza kivipi unaletewa tiketi hata kama na ‘travel agency’ halafu unashindwa kuuliza au kukagua mpaka unaenda uwanjani na unapewa ‘boarding pass’ bado unashindwa kukagua ipi ‘bussiness class’ na ipi ‘first class’!” anahoji Basiasi. Abiria mmoja aliyenukuliwa na Jamiiforums alisema kwa waziri wa nchi kama Uingereza anatakiwa kutoa maelezo ya sababu za kusafiri na daraja la kwanza (first class) ikiwa atalazimika kufanya hivyo, vingine viongozi husafiri kwa madaraja ya kawaida.

Wakati Waziri Muhongo akisusia ndege kwa kukosa nafasi ya kusafiri na daraja la kwanza, baadhi ya mawaziri wanaofanya ziara mikoani na kusafiri kwa ndege, hulazimika kuyaagiza mashangingi yao kutoka Dar es Salaam hadi katika mikoa wanayokwenda kufanya ziara hizo hata kama yatatumika kwa siku moja.

PESA ZA WATEJA WA M-PESA, TIGO PESA, AIRTEL MONEY NA Z-PESA WANAO FARIKI ZINAKWENDA WAPI?

$
0
0
Kutokana na makampuni karibu yt ya simu Tz kuwa na huduma hz za mobile money, Je inapotokea mteja amefariki, makampuni yanawajibika vipi kuhusu kurudisha pesa za mteja wao kwa msimamizi wa mirathi au warithi? 

swali hiili linazingatia kuwa wateja wanaoweza kutwa na mauti kwa vyovyote wanaweza kuwa na akiba kidogo kwenye ac zao za mitandao ya simu wanayotumia!

Je kuna sheria yoyote ambayo imeweka bayana masuala haya?

kwa wenzetu walio kwenye makampuni ya simu tafadhali mtusaidie kwa hili!
naomba kuwasilisha kwa mjadala!

LEO NDIO LEO LILE TAMASHA KUBWA LA KUPINGA RUSHWA FIKA VIWANJA VYA GENERAL TYRE UJIONEE

$
0
0

Leo ndio Leo Tamasha kubwa na la Kihistoria kufanyika jijini Arusha kwa madhumuni ya kupiga vita rushwa barani Africa likibeba kauli mbiu RUSHWA SIO!! Wasanii watakao perform ni pamoja na WEUSI( JohMakini Mwamba Wa Kaskazini NikiwaPili ,LordEyes, GNako) , NAZIZ, FID Q Chindo Vanessa MdeeStamina Kabwela Shorwebwenzi R.O.M.A Mkatoliki ,Izzo Business Linah SangaJambo Squad Na wengine Wengi.

Pia Wasanii Chipukizi watapewa Nafasi, kuonyesha Viapaji Vyao

Kama wewe ni Afrika na Afrika ni wewe

Wakati wako umefika wa kubadili historia. Fika viwanja vya General Tyre Arusha leo kujirusha huku tukionyesha jinsi gani Rushwa ilivyo sio. 

Usikose kiingilio ni Bureeeee Kabisaaa

MTIHANI UNAOWAKABILI BAADHI YA WANAWAKE WAINGIAPO KATIKA MAHUSIANO MAPYA

$
0
0
Ni pale mwanaume anapoonyesha tamaa kubwa ya ngono na kulazimisha kukutana kimwili wakati mwanamke aliweka msimamo wa kutokutana kimwili na mwanaume yeyote mpaka baada ya muda fulani tangu kufahamiana na kuwa wachumba au mpaka pale watakapofunga ndoa

Huu ni mtihani kwa wanawake wengi kwa sababu unawaweka katika wakati mgumu wa kuchagua kuvunja nadhiri waliojiwekea au kusimama imara kwenye msimamo waliyojiwekea kwa ajili yakulinda heshima zao.

Swali kwa wanawake: Je unapokabiliwa na mtihani kama huu ni uamuzi gani unaona ni sahihi kwako….?

LIVE KUTOKA KIGOMA,DR.SLAA APAMBANA NA MAANDAMANO MAKUBWA YA KUMPINGA

$
0
0

Kinachoendelea KIGOMA muda huu na hata kwenye kwenye Maandamano Makubwa ni hiki wanachama wa CHADEMA wakiandamana kupinga ujio wa Dr SLAA na viongozi wenzake mkoani.
Mods tunaomba postive na Negative Pictures anachokutana nacho Dr.slaa ziruhusiwe hapa Jukwaani,naona watu wamekaa kusifiana tu hapa.Ukweli ni Kwamba Dr.slaa amekutana na wakati Mgumu akiwa Kigoma.Picha zingine zitakuja na saambili Usiku ITV,TBC NA STAR TV wataonesha hali ya leo Kigoma walivyojitokeza Kupinga Ujio wa Dr.slaa.

ASANTE

(Photo’s) DIAMOND PLANTINUMZ ANOGESHA SIKU YA KUZALIWA YA MWANAMUZIKI K-LYNN

$
0
0
Ilikuwa ni siku ya furaha sana usiku wa kuamkia leo kwenye sherehe ya kuzaliwa Miss Klynn aka MAMA MAPACHA pande fulani hivi jijini Dar es Salaam. Party hii ilikuwa ni yaaina yake kwani ilikuwa ni kwa watu walioalikwa tu, kama unavyoona picha jinsi walivyokuwa safi na namuona Boss Mengi akiwa mwenye nyuso ya furaha baada yakutizama show kali ya Diamond.

MR BOND NAYE AFUNGUKA KUHUSU MINONG'ONO YA PENZI LAKE NA WASTARA..APONDA BLOG UCHWARA

$
0
0

"Kila jambo lina muda na wakati wake.. usilazimishe kurudisha saa nyuma wakati ulishachelewa....kubali kushindwa na jipange upya ili upate kushinda siku nyingine..thanx Wastara kwa kufanya kazi yangu pamoja na mimi kupitia kampuni yako ya Wajey film usivunjike moyo kwa mane no ya viblog uchwara na mane no ya binadamu wasiokua na akili timamu" Mr Bond

MTOTO ALIYELELEWA NA MBWA AZIDI KUTESEKA

$
0
0
Stori: Denis Mtima na Chande Abdalla
MTOTO Kulendya Rojason (3) ambaye siku za nyuma aliwahi kuripotiwa na vyombo vya habari kuwahi kulelewa na mbwa baada ya wazazi wake kumtelekeza yeye na ndugu zake, bado anazidi kuteseka kwa kukosa msaada wa chakula

Akizungumza kwa niaba ya mtoto huyo nyumbani kwao, Nyerere B, Mabatini Mwanza, dada wa mtoto huyo, Recho Rojason (18) alisema kuwa mdogo wake bado anateseka kwani hapati malezi ya kutosha kutokana na maisha yao kuwa magumu.

Recho alisema kuwa, maisha yao yamekuwa magumu baada ya mama yake kuwatelekeza na kuolewa na mwanaume mwingine huku akimwacha baba yao ambaye ametopea kwenye ulevi na kushindwa kutoa msaada wowote.

Recho ambaye ni hausigeli anayefanya kazi kwa ujira mdogo maeneo ya Mwanza Mjini, alisema wamekuwa wakipata fedha kidogo kutoka Halmashauri ya Jiji ambapo hazikidhi mahitaji yao na kuwaomba watu wajitokeze kuwasaidia.

Aliomba msaada wa kupata fedha kwa ajili ya matibabu, masomo na malazi kwa kuwa yote hayo ni mahitaji yao yeye pamoja na wadogo zake watano akiwemo Kulendya.

Akizungumzia sakata hilo jirani anayeishi na watoto hao, Chausiku Ibra alisema kuwa watoto wa familia hiyo wamegeuka machokoraa kutokana na huduma hafifu na kuongeza kuwa mtoto wa mwisho (Kulendya) ndiye yupo hatarini zaidi.   

“Huyu mtoto wa mwisho ndiye aliye hatarini zaidi kwa kuwa tangu alivyokuwa mtoto alikuwa akiletewa chakula na kutunzwa na mbwa.

Mpaka anakuwa hivi ni jambo la kumshukuru Mungu kwa kweli. Watoto hawa wanahitaji msaada jamani,” alisema jirani huyo.
Waandishi wetu walijionea, nyumba wanayoishi watoto hao ambayo imeonekana kuharibika kwa kiasi kikubwa sehemu za paa na kuta jambo ambalo ni hatari kwa watoto hao huku taarifa zikieleza kuwa, baba wa watoto hao, Rojason Ernest amelazwa katika Hospitali ya Rufaa ya Bugando akiuguza nyonga baada ya kuanguka akiwa anatokea kilabuni.
Kama umeguswa na unataka kuwasaidia watoto hao, wasiliana nao kwa namba ya jirani yao, Chausiku: 0767445683.
Imeandikwa na Global Publishers

WEMA KAMISS PENZI LA DIAMOND...TAZAMA PICHA ALIYOPOST NA MANENO ALIYOANDIKA

$
0
0
Mcheza filamu za kibongo Wema Sepetu ametuma picha ya mpenzi wake wa zaman mwanamuziki Diamond Platnamu kwenye akaunti.yake ya instagram na kuandiki
i jus happen to love dis picture
baada ya kuweka picha hiyo mashabiki wameanza kumsifia uku wakimponda mpenzi Penny ambae anaaminika ndio mpenzi wa Diamond kwa sasa
Website hii imepitia akaunti ya Diamond na kukuta picha ile ile aliyoweka Wema ikiwa na maneno kuonesha kua usiku wa jana masanii huyu alikua kwenye sherehe ya kuzaliwa mrembo wa zamani wa Tanzania Jackline Ntuyabaliwe.


KILIMANJARO STARS IMEWAVUA UGANDA UBINGWA WA CHALLENGE

$
0
0
TIMU ya Tanzania Bara,(Kilimanjaro Stars) imefanikiwa kutinga katika hatua ya nusu fainali ya mashindano ya Challenge baada ya kumtupa nje ya mashindano hayo Bingwa mtetezi timu ya Uganda The Crenes kwa mikwaju ya penalt 5-4
Viewing all 104789 articles
Browse latest View live




Latest Images