Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104712 articles
Browse latest View live

VIDEO:WANAFUNZI WAPAGAWA NA MZIKI WAJISAHAU NA KUANZA KUZUNGUSHA VIUNO STEJINI

$
0
0
Wanafunzi wa Shule Moja Huko Kenya ...Walipopanda Stejeni na kujisahau kuwa wao na wanafunzi na wana nguo za Shule na Kuanza Kutwerk Mbele ya Mashabiki...
Angalia Video Hapa chini ushangae mwenyewe



KIKWETE AONYESHA JEURI YA JESHI LA TANZANIA LEO, MAADUI WAJIONEA

$
0
0
Mwenye Macho haambiwi Tazama hakuna siri Leo kila rangi maadui wa nchi Na Rais wetu hawajaacha kuoona.

Vijana wamekamilika kila idara in a modern and newly Technology.

Watu msiojua,mjue Tanzania sio nchi ya mchezo katika Ulinzi.

Tunapenda amani Na upendo Na majirani.

Lakini atakayethubutu kutubeep,hatutasita kumtwanga.

Viva Kikwete,
The true Hero in an innocent land of Mwalimu Nyerere.

The Nation is proud of you son of Africa.

The Valley and the Greenland sings Your remarkable,achievement in every aspect.

We adore and Love you,

Longlive Jakaya

WANAWAKE WENGI SIKU HIZI WAMEKUWA MALIMBUKENI WA SOCIAL NETWORKS

$
0
0
Kuna mdada mmoja nilisoma naye chuo miaka fulani hapo nyuma, sasa jana katika pilikapilika zangu mjini, tukakutana ghafla maeneo fulani, kwa hiyo tukaanza kusalimiana na tukaona ni vizuri tusogee pembeni kwenye mgahawa fulani tukakaa. Basi tukawa tunapiga story za kawaida na kila mmoja akimwuuliza mwenzio yuko wapi na anafanya nini sasa. Katika kukaa naye kwa muda mfupi usiozidi nusu saa, kila baada ya sekunde kama 3 hadi tano nasikia simu yake (Sumsung galaxy S5) ikilia ndii, njee, ngaa, etc., huku akiishikilia na kucheza nayo muda wote! Sasa ikabidi nimwuulize mbona simu yako haiishi milio? Akajibu ni msgs - watu wananitumia msgs kutoka social networks mbalimbali.

Nikamwambia mmmhh, social networks gani hizo mpaka simu iwe busy muda wote? Akaniambia mie nipo (tena kwa madaha) karibu social networks zote halafu nina marafiki wengi sana, akaanza kunionyesha (sio kwamba sizijui, ila yeye alihisi mie ni mngoroko na sijui chochote kuhusu social networks), nami nikawa curious kufuatilia, maweeeeeeeeee! Mdada karibu kila social network unayoijua yupo na ni very active, halafu amejiunga na magroup kibao, singles, lovers without limit, love addicts, sijui magroup gani yaani basi:

- WhatsApp
-Viber
-Instagram
-Telegram
-Tango
-skype
-facebook
-Google+ (Google Talk)
-Twitter
-twoo
-flickr
etc.,

Kilichoniacha hoi ana contacts mpaka basi, yaani nimeona facebook ana marafiki wengi zaidi ya elfu, WhatsApp kama 3800 hivi, kwingine sikuendelea kuangalia.

Nikamwuuliza sasa hizi contacts zote unazitoa wapi? Akasema wengine tunakutana kwenye mishemishe lakini wengi ni kwenye mitandao.

Nikamwambia wewe hobby yako inaonekana kuchat! Akadakia "sana na kuangalia movie". Wakati naachana naye akawa anasisitiza nimpe namba ya simu tuwe tunawasiliana kupitia WhatsApp na social networks zingine, nikamwambia wewe nipe tu namba yako nikifika home nikatulia nitakuadd.

Natumaini wadada wengine wengi wa namna hii wapo!

Swali langu ni kwamba mwanaume ukikutana na mdada wa hivi ukaingia naye kwenye mahusiano, utakuwa na guts za kujipiga kifua kwamba utaweza kuclear strings na attachments zote alizozifanya? Watu wangapi amekutana nao, kutongozana nao na labda hata kusex nao?

Kwenye hizi social networks wanaume na wanawake mara nyingi hawaishii kuchat tu, bali hufikia hatua ya kutongozana na nimeona mahuasiano kadhaa ya ndoa au kiuchumba yaliyovunjika kwa wahusika kukutwa na msgs za kutongozana au kupeana miada ya kuchepuka!

Ukitaka mahusiano yako yabaki kuwa ndoto au yaingie matatani wewe mruhusu mwenzi (au jiruhusu mwenyewe) wako awe anachat, mara kushare photos na videos na watu wa jinsia tofauti - hata kama akidai ni ndugu zake, sijui kaka/dada wa hiari, sijui nilisoma naye chuo/sekondari, sijui mfanyakazi mwenzangu bila sababu ya msingi, utakuja kuniambia!

Leo ni siku ya muungano, epuka/piga marufuku mawasiliano yasiyokuwa na maana wala msingi wowote ili kudumisha muungano wa uhusiano wenu.

RYAN GIGGS " SASA MAN U NI KUFUNGA MAGOLI TU KUFUNGWA NOO TENA"

$
0
0
Kocha wa muda wa Manchester United, Ryan Giggs amesema amejisikia furaha kubwa kupata nafasi ya kuingoza timu hiyo kwa muda uliobaki huku akiahidi mambo mazuri kwa mechi nne zilizosalia.

Akizungumza leo na MUTV, Giggs amesema kuwa ana uhakika mashabiki wa timu ya Manchester United wataona magoli na watapata burudani nzuri.

I’ve got to say it’s the proudest moment of my life. I’ve supported Manchester United all my life, it’s been the biggest part of my life since I was 14 when I signed schoolboy forms. I’m proud, happy, a little bit nervous but just like I am as a player I can’t wait for the game on Saturday. Obviously I played under Sir Alex for so long so he was the first person to call because I wanted advice and to know what to expect. Who better to ring? Why wouldn’t I?! I’ve just said to them ‘I trust you and I know what you’re capable of and go out there and show it on Saturday and give the fans something to shout about. Entertain them, score goals, make tackles, play with speed, play with tempo.’alisema Giggs.

MWISHO MWAMPAMBA AULA APATA KAZI KITUO KIPYA CHA TV

$
0
0

Aliyekuwa mwakilishi wa mara mbili kutoka Tanzania kwenye shindano la Big Brother Africa, Mwisho Mwampamba ataonekana hivi karibuni kwenye kituo cha runinga cha TV1 kama mtangazaji.

Kupitia Instagram, TV1 wameweka picha hii ya ya baadhi ya wafanyakazi wa TV1 akiwemo Mwisho na kuandika; Guess who’ll be next as #TV1Host #tv1tanzania #comingsoon #tvproduction #tv #tanzania #africa #daressalaam #mikocheni #studios #set

FUMANIZI LA AINA YAKE NDANI YA GARI !! DUH NOMA SANA!!

$
0
0
Yelewiii!  Dereva ‘suka’ wa kampuni moja binafsi yenye makao yake makuu Kurasini jijini Dar (jina halikupatikana) Jumapili iliyopita alinaswa akifanya mapenzi na changudoa  ndani ya gari la kampuni hiyo, kikosi cha Oparesheni Fichua Maovu (OFM) kilishuhudia tukio hilo laivu.

‘suka’ baada ya kunaswa akiwa na changu (kulia).
Dereva huyo akiwa na mwenzake walifika maeneo ya Mbagala Zakhem saa 7 usiku wa Februari 16, mwaka huu bila kujua kama OFM ilikuwa katika maeneo hayo kwa ajili ya kufanya oparesheni tokomeza machangudoa.
OFM ilimshuhudia dereva huyo na mwenzake wakishuka ndani ya gari aina ya Toyota Hilux (isiyokuwa na ‘pleti’ namba upande wa  mbele) mali ya kampuni  hiyo, wakiingia kwa fujo katika moja ya madanguro maarufu na kupaki gari  kisha wakashuka kuelekea kwenye danguro la machangudoa.


Baada ya muda, mmoja wao alirejea akiwa na changudoa maarufu kwa jina la Waluwalu na kujifungia ndani ya gari hilo.
Kama kawaida yake OFM iliwataarifu askari wa Kituo cha Kizuiani waliokuwa doria katika eneo hilo ambao kwa pamoja walilivamia gari na kumuamuru dereva  ashuke.

Hata hivyo, suka huyo alikuwa mbishi akaamua kufunga milango na kupandisha vioo ili asiweze kubughudhiwa na kile alichokuwa akikifanya ndani ya gari.
Askari waliokuwa na silaha wakalizunguka gari hilo na dereva huyo alipoona mambo yamekuwa magumu alifungua mlango na kutimua mbio lakini hakufika mbali kabla ya kuwekwa chini ya ulinzi sambamba na changudoa aliyekuwa naye.

Akizungumza kwa hofu dereva huyo alisema, yeye na mwenzake ni madereva wa kampuni... (jina tunalo) na walikuwa maeneo hayo kwa bahati mbaya na si kama walifika kuwanunua machangu hao.
Dereva huyo alipotakiwa atoe sababu za kujifungia ndani ya gari hilo na changudoa kisha kutoa pleti namba ya mbele ya gari, alijitetea kwa kusema kuwa pleti namba ilidondoka barabarani tangu mchana, hivyo walikuwa wakimtafuta fundi ili awatengenezee.


na Changu wakiwa na watuhumiwa wengine walionaswa katika operesheni tokomeza uchangudoa.
Alipohojiwa changudoa waliyekuwa naye, hakuwa na lolote la kusema zaidi ya kuangua kilio na kuomba aachiwe huku akilaumu ukali wa maisha kama sababu ya kujiingiza katika biashara ya kujiuza.
Wahusika hao walifikishwa Kituo cha Polisi cha Kizuiani kabla ya kesho yake (Jumatatu) kupelekwa Mahakama ya Jiji kusomewa makosa yanayowakabili.

HATARI SANA..AGNESS MASOGANGE AWAPA MAKAVU LIVE KINA MASOGANGE FEKI

$
0
0


Mrembo Agness amefunguka kwa mara nyingine tena na kulalamikia wadau wanaofungua account fake kwenye social networks na kutapeli watu kwa kutumia jina lake. Mrembo huyo amepost picha na ujumbe huo hapa juu kupitia Instagram yake:
Duh ! Kweli watu wanapenda Miteremko .....hizo accounts zote ni Fake kwa jina la Masogange....mmhhh

BABY MADAHA ASIMULIA JINSI WASANII WENZAKE WA KIKE WANAVYOMTONGOZA

$
0
0
Baby Madaha  akipigana  denda    na  msichana  mwenzake Bar.Wakati  sakata  la  kusagana  ndani  ya  mastaa  wa  bongo  movie  likiwa  bado  bichi, Msanii  wa  muziki  na  maigizo  Baby  madaha  ameibuka  na  mapya  juu  ya  mastaa  wenye  tabia  ya  usagaji.... 
Akiongea  na  mwandishi  wetu  juzi  kati  jijini  Dar,msanii  huyo  alisema  kuna  mlolongo  wa  wasanii  wa  kike  kwenye  tasnia  ya  filamu  ambao  wamekuwa  na  tabia  hiyo  ya  kisagaji  huku  yeye  akiwa  ni  mmoja  wa  \wahanga  wa  kutongozwa  na  wasichana  wenzake....
"Hawana  hata  chembe  ya  aibu,wakishakunywa  pombe  zao  wanakuambia  live  kabisa, mimi  mwenyewe  nishatongozwa  sana  na  (  anataja  jina ).Kiukweli  wanakera  sana  ndugu  yangu" Alisema  msanii  huyo.

 Madaha  aliendelea  kutiririka  kuwa  wasanii  wengi  wa  kike  wa  filamu  wamekuwa  wakichanganywa  na  utumiaji  uliopindukia  wa  pombe  na  bangi  unaowapelekea  kufanya  mambo  ya  aibu  kwa  jamii

Ukihukumu  kwa  kutumia  picha  hii  ( hapo juu )  na  maelezo  ya  baby  madaha  kuna  ukweli  

KOCHA RYAN GIGGS AANZA VIZURI..MAN UNITED YAPIGA BAO MTU 4 BILA

$
0
0
Kete ya kwanza ya Ryan Giggs kama meneja wa muda wa Manchester United imeanza vyema usiku wa Jumamosi kwa mashetani wekunda kuichapa kichapo cha mwezi Norwich.

Wayne Rooney na Juan Mata wamefunga magoli mawili kila mmoja kwenye mechi hiyo ya Old Trafford.

Giggs aliteuliwa kuwa kocha wa muda wa timu hiyo baada ya David Moyes, kutimuliwa.

KIKWETE"MUUNGANO WETU NI MFANO WA KUINGWA AFRIKA"

$
0
0
Rais Jakaya Kikwete amesema Bara la Afrika lina jambo la kujifunza kutokana na mafanikio yaliyopatikana kwenye Muungano wa Tanganyika na Zanzibar uliodumu kwa miaka 50.

Amesema kuwa kitendo cha Muungano kudumu, kuimarika na kuendelea kustawi kwa nusu karne siyo jambo linaloweza kubezwa na nchi yoyote kwa kuwa zipo baadhi ya nchi zilizojaribu kufanya hivyo, zikashindwa.

“Wapo wenzetu barani Afrika walijaribu, lakini hawakufanikiwa kama sisi, kwani Muungano wao ulidumu muda mfupi na kusambaratika. Wapo waliokaa miaka miwili, miezi na wapo ambao wameanza majadiliano mpaka leo hawajamaliza,” alisema Kikwete.

Kikwete alisema hayo jana Dar es Salaam, wakati akipokea matembezi ya vijana na kuzungumza na wananchi kupitia vyombo vya habari.

Akinukuu maneno ya Baba wa Taifa, hayati Mwalimu Julius Nyerere, Kikwete alisema: “Tanzania ni lulu ya pekee kabisa katika historia ya Afrika, nchi nyingine zote ni za kurithi kutoka ukoloni, Tanzani ni ya kuundwa na sisi wenyewe, kwa hiari yetu wenyewe baada ya kukomboa sehemu zake kutoka ukoloni.”

Alisema, mafanikio yaliyopatikana Tanzania yanaonyesha kuwa pia Shirikisho la Afrika Mashariki linaweza, na nchi za bara la Afrika kuungana na kuwa nchi moja inawezekana.

“Ikiwepo nia thabiti, mambo yakipangwa vizuri, hakuna kisichowezekana kwani njia itapatikana, sisi tumeweza na wenzetu pia wanaweza,” alisema.

Huku hotuba yake ikikatizwa mara kwa mara na vijana waliokuwa wakishangilia, Kikwete alisema kiini cha hotuba yake ni kutaka kujibu maswali mawili yanayohusu Muungano.

Aliyataja maswali hayo kuwa ni;  kwani nini muungano wa Tanganyika na Zanzibar umewezekana na kwa nini umedumu.

Akijibu maswali hayo, alisema kuwa kwa mujibu wa Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka 2012, asilimia 91 ya Watanzania walizaliwa baada ya Muungano na kwamba asilimia tisa tu, ndiyo waliozaliwa kabla ya Muungano huo.

Hivyo, aliamua kujenga hoja za majibu yake kwa kutaja mambo sita aliyoyataja kuwa ndiyo siri ya mafanikio ya Muungano.

Mambo hayo ni kwamba waasisi wa Muungano, Nyerere na Abeid Karume, walikuwa na nia ya dhati ya kuungana, walitanguliza maslahi ya taifa mbele na kuwa watu wa Tanganyika na Zanzibar ni wamoja.

Mambo mengine ni kuwepo kwa uhusiano wa karibu kati ya viongozi wa kisiasa wa Tanganyika na Zanzibar, nia ya kutatua matatizo yanayohusu Muungano na kwamba Muungano unawanufaisha watu, vinginevyo ungekuwa umeshakufa zamani.

Lugha za matusi bungeni

Kikwete alisema kuwa amesikitishwa na matumizi ya lugha za matusi na vijembe zilizotumiwa na Wajumbe wa Bunge Maalumu la Katiba, hata baada ya kuwazuia kufanya hivyo wakati akizundua Bunge hilo.

“Inaelekea ushauri wangu hawakuuzingatia, wanatumia lugha za matusi yanayokaribia kuwa ya nguoni,” alisema.

Pia, aliwataka wajumbe wa Umoja wa Katiba wa Wananchi (Ukawa) kurejea bungeni kwa kuwa wananchi hawatawasaidia kutatua matatizo yao, badala yake watasikitika nao tu.

Alisema kuwa hakufurahishwa hata kidogo na kitendo cha Ukawa kutoka nje ya Bunge kwa kuwa anaamini suluhisho lao linapatikana ndani ya Bunge.

Vijana zaidi ya 3,000 kutoka mikoa mbalimbali nchini na maeneo tofauti jijini Dar es Salaam jana walikuwa miongoni mwa watu waliohudhuria katika ukumbi wa PTA, kusikiliza hotuba ya Rais Jakaya  Kikwete ya maadhimisho ya dhahabu ya miaka 50 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar.

Huku wakiwa wamevaa fulana nyeusi zilizokuwa na ujumbe uliosomeka ‘2 zinatosha’, ukimaanisha muundo wa Serikali mbili unaoungwa mkono na CCM.


ROSE NDAUKA "NDOA YANGU SOON!"

$
0
0
MSANII maarufu wa sinema za Kibongo, Rose Ndauka amesema kuwa watu wasiwe na wasiwasi kwani kwa mipango ya Mungu atafunga ndoa na mzazi mwenzake Maliki Bandawe hivi karibuni.

“Si muda mrefu mambo yatakuwa mazuri tulikuwa tunaendelea kujuana, nadhani sasa tunafahamiana vizuri hivyo watu wasiwe na shaka, tutafunga ndoa soon,” alisema.

Rose ambaye hivi karibuni alihamasisha zoezi la usafi na kuungwa mkono na wasanii mbalimbali akiwamo Meya wa Ilala Jerry Slaa, alisema watu wasihofu kuhusu ndoa hiyo kwani ipo njiani.

“Hatujui labda kuchelewa kwetu kuna kitu Mungu amekiepusha, siku zote haraka haraka haina Baraka,” alisisitiza Ndauka ambaye amepanga kutembea Tanzania nzima kuwahamasisha wananchi kuzingatia usafi.

HAMISA MABETO AWATISHIA AMANI WASANII WA KIKE BONGO MOVIES

$
0
0
MWANAMITINDO maarufu nchini, Hamisa Mabeto ametishia maslahi ya wasanii wa kike wa Bongo Movie baada ya kujitosa rasmi kwenye tasnia hiyo na kung’ara katika Filamu ya VIP akiwa na mastaa, Vincent Kigosi ‘Ray’ na Jacqueline Wolper.

“Wasanii wajiangalie nafasi zao baada ya Mabeto kuingia kwenye filamu maana ndani ya VIP amekamua sana na wasipokuwa makini atawasumbua kutokana na mvuto ulionao,” alisema Ray.

Mabeto ametamba kwenye ulimbwende tangu mwaka 2010 alipoibuka mshindi wa shindano XXL Back to School Bash.

Mwaka 2011 alishika nafasi ya pili katika shindano kumsaka Miss Dar Indian Ocean na baadaye Miss Kinondoni.

Mwaka 2011 alishiriki Miss Tanzania na kufika hatua ya nusu fainali ya michuano hiyo. Mwaka 2012 akafika hatua ya kumi bora kwenye Miss University.

Hivi karibuni alipata ulaji wa kupamba kava la gazeti moja la Kenya.

WARIOBA ATOA YA MOYONI "MATUSI NA UONGO BUNGE LA KATIBA VINANIUMIZA"

$
0
0
Aliyekuwa Mwenyekiti wa Tume hiyo, Jaji Joseph Warioba amesema baadhi ya wajumbe wa Bunge Maalumu la Katiba wametumia vibaya Bunge hilo kwa kumshambulia na kumsingizia mambo ya uongo kwa makusudi, akisema matusi yanayotolewa dhidi yake yanamuumiza.

Aidha, Warioba amesema ingawa haelewi kwa nini wanaomshambulia wameamua kutumia lugha za matusi dhidi yake binafsi, hatajutia kuchaguliwa kuiongoza tume hiyo kwa kuwa ilikusudia kuwaletea maendeleo wananchi wote kwa kuwapatia Katiba wanayoitaka.

Kauli hiyo ya Jaji Warioba imekuja wakati baadhi ya wajumbe wa Bunge Maalumu la Katiba na viongozi wa CCM wakiikosoa Rasimu ya Mabadiliko ya Katiba kwa maneno makali,huku wakimshutumu na kumkejeli yeye na baadhi ya wajumbe wa tume aliyoiongoza.

SIMBA WACHUKUA MAAMUZI MAGUMU,WATEMA KIKOSI KIZIMA

$
0
0
UKITAKA mafanikio lazima uchukue uamuzi mgumu ambao hakuna anayeweza kufikiria kabla.

Kocha wa Simba, Zdravko Logarusic amesema analazimika kutema wachezaji wasiopungua 11 ambao ni sawa na kikosi kizima kinachoweza kucheza mechi ya ushindani.

Lengo la Logarusic kufanya hivyo ni ili aweze kujenga upya timu ya ushindani msimu ujao.

Logarusic sasa ana uhakika wa kubaki Simba, baada ya kuhakikishiwa na Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya klabu hiyo, Zacharia Hans Pope kwani awali hakuwa na uhakika wa kuendelea kubaki katika timu hiyo kutokana na mkataba wake kumalizika.

Kocha huyo atasaini mkataba wa miaka miwili baada ya ule wa miezi sita kufikia tamati.

Katika ripoti yake kwa uongozi wa timu hiyo, Logarusic amewaeleza wazi viongozi wake kuwa, ili Simba iwe na ushiriki mzuri msimu ujao wa Ligi Kuu Bara lazima nyota 11 wa timu hiyo waachwe ili wapatikane wengine watakaoisaidia timu kufikia mafanikio.

WEMA SEPETU ALA SHAVU LA MTANDAO WA SIMU

$
0
0
Wema Sepetu Amepata shavu la Kutangaza promotion mpya ya Mtandao wa Airtell Ambayo unapata Facebook, Twitter na Whatsapp Bure, Wema Sepetu anawajoin JB na Joti Ambao nao pia kwa sasa wanatangaza Promo za Makampuni ya Simu....Hongera Wema ...
Team Wema Mpo ??

ASKARI MWENYE HIPS ZA KUDATISHA KENYA APIGWA MKWARA NA BOSI WAKE BAADA YA PICHA KUSAMBAA

$
0
0

 Yule Polisi Mwanamke Nchini Kenya kwa Jina Linda Amechimbwa mkwara na Bosi wake wa kituo cha Polisi kiambu Kenya Baada ya Picha yake Kusambaa Mitandaoni Akiwa amevaa Kijisketi cha Polisi kinacho mchora Hips na makalio yake kiasi cha kuleta utata kwenye mitandao ya kijamii kwa kusababisha Mjadala usio na Mwisho kila mtu akisifia hips na kalio lake..Vipi we Mwanamme Trafiki kama huyu akikusimamisha Barabarani ? Najua lazima uchukue Number ya Simu hahahha

KUNA WASICHANA WANAO TOA RUSHWA YA NGONO KUPATA TAJI LA MISS TANZANIA

$
0
0
Mkurugenzi wa Kampuni ya Lino International Agency, ambao ni waandaji wa Miss Tanzania, Hashim Lundenga amedai kuwa wasichana wengi wanaoingia kwenye mashindano ya Miss Tanzania hufanya mbinu za kuwalaghai baadhi ya watu kwenye kamati kwa kuwapa rushwa ya ngono ili washinde taji la miss Tanzania.

Akizungumza na Global TV, Lundenga amedai kuwa kuna wasichana wanaoingia kwenye mashindano hayo wakiwa tayari kwa kila kitu.

“Kikumbwa ninachokwambia kuna wasichana ndani ya wasichana,kuna wasichana mule ambao katika mashindano yanayokuja they are ready for every thing,wapo wasichana hao na sisi tunajua hivyo,wasichana wanakuja pale wameshajua mimi nimegombana na boyfriend wangu nimemuacha boyfriend wangu kanikataza,mama yangu, baba yangu nimekuja kwajili hiyo, nilazima nishinde, sasa anashindaje? Lazima apitepite kwa viongozi sisi,wanapitapita sana,wanajilegeza sana kwetu sisi,sasa sisi kama hatuna ethics ndiyo tunaingia kwenye mtego mbaya,kwasababu kuna mtu kwenye kamati yetu tumeshamsuspend mara mbili,tunamsuspend kwasababu ya upumbavu wake, mara mbili tumeshamsimamisha kwasababu ya upumbavu wake,” alisema.

Kuhusu tuhuma za kuwauza warembo watu wenye pesa, Lundenga alisema: Unajua hapa mjini, mimi leo siwezi kusema Musofe simjui,siwezi sema mapedejee gani simjui, najuananao ndio watu wa mjini hao,tunakula nao tunalala nao, si ndio! Sasa huwezi sema completely ukaknock-out, haiwezekani,no it’s very difficult, akina nani wote wa Musoma yule,akina nani, huwezi, hao ndio mapedejee wa mjini.”

WACHEZAJI MBEYA CITY MARUFUKU KUHAMA TIMU

$
0
0
WAKATI klabu kongwe za Simba, Yanga na Azam FC zikipiga hesabu za kuibomoa Mbeya City, Serikali imewaonya wachezaji hao kukihama kikosi hicho kinachofundishwa na Juma Mwambusi.

Zipo tetesi tofauti za wachezaji wa timu hiyo iliyomaliza ligi ikiwa katika nafasi ya tatu katika ligi kuwaniwa vikali na klabu hizo kwa ajili ya msimu ujao wa Ligi Kuu Bara.

Akizungumza na Mwanaspoti, Mwenyekiti wa timu hiyo, Mussa Mapunda alisema Aprili 24, mwaka huu walipokea barua kutoka Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo iliyosainiwa na Naibu Waziri, Juma Nkamia ikiwasisitizia jambo hilo.

“Barua tuliyoipokea iliandikwa Aprili 15 kabla ya sisi kuipokea Aprili 24, ambayo imeelekeza kuendelea kuwapa matunzo mazuri wachezaji wetu wote bila ya kubagua kwa lengo la kukiboresha kikosi chetu ili msimu ujao kiimarike zaidi.

“Imetuonya kutowaruhusu wachezaji wetu kuwaachia kwenda klabu kubwa ambazo zenyewe hazina malengo na mpangilio wa kuziendeleza timu zao,”alisema Mapunda.

Wachezaji wanaotajwa kuwaniwa na klabu za Simba, Yanga na Azam FC ni Saad Kipanga, Hassan Mwasapili na Deus Kaseke.

NGASSA AIPA YANGA BALAA LA KUKOSA UBINGWA

$
0
0
MSIMU uliopita wa Ligi Kuu Tanzania Bara, Yanga walikuwa mabingwa watetezi na walitumia zaidi ya Sh250 kuwasajili wachezaji watatu ambao ni kipa Juma Kaseja aliyevuna Sh40 milioni, Mrisho Ngassa aliyechota Sh30 mil na mshambuliaji Emanuel Okwi aliyeigharimu Sh180, mil.

Lakini imekumbana na balaa la aina yake imeshindwa kutetea ubingwa wake na kufanya winga wake machachari ambaye ni Ngassa kuandika rekodi ya mkosi kwa kupishana na ubingwa wa Ligi Kuu Bara kwa miaka mitano mfululizo.

Iko hivi; Ngassa alijiunga na Azam FC Juni 2010 kwa mkataba wa miaka mitatu akitokea Yanga ambayo kwa msimu huo uliomalizika haikunyakua ubingwa wa ligi. Simba walitwaa ubingwa wa msimu wa 2009/2010 tena kwa rekodi ya kutopoteza mchezo.

Mchezaji huyo aliichezea Azam kwenye msimu wa 2010/2011 na kuibuka mfungaji bora wa ligi akifunga mabao 18.

Lakini Azam ambayo ilikuwa haijawa tajiri kama ilivyo sasa, haikufanikiwa kutwaa ubingwa kwani ilimaliza nafasi ya tatu na pointi zake 44, huku Yanga wakiibuka mabingwa wa msimu huo.

Ngassa aliendelea kukipiga na Azam kwenye mwaka wake wa pili wa mkataba msimu wa 2011/2012 na licha ya kiwango chake kuwa juu kwenye msimu huo, timu yake iliambulia patupu ikimaliza ya pili katika ligi na Simba ikawa bingwa.

Bahati ilizidi kuwa mbaya kwa Ngassa baada ya kuuzwa na Azam kwenda Simba msimu wa 2012/2013 ambako nako alishindwa kuwasaidia Wekundu hao na kujikuta wakishika nafasi ya tatu huku Yanga ikiwa bingwa.

Nuksi ikaendelea katika msimu uliomalizika hivi karibuni ambapo alijiunga na Yanga, amepishana tena na ubingwa kwani sasa umeenda Azam. Ngassa amemaliza msimu akiwa na mabao 13 huku Yanga ikiwa imemaliza ya pili na pointi 56 huku Azam ikitwaa taji kwa pointi zake 62.

Mbeya City imemaliza ya tatu ikiwa na pointi 49 na Simba ya nne pointi 38.

TRAFIKI AFA GHAFLA AKIWA NDANI YA DALADALA ALILOLIKAMATA

$
0
0
Moshi. Ofisa wa polisi mwenye cheo cha Koplo, Wilson Mwakipesile wa Kikosi cha Usalama Barabarani mkoani Kilimanjaro amefariki dunia ghafla akiwa ndani ya daladala alilokuwa amelikamata.


Hata hivyo, haikujulikana mara moja iwapo trafiki huyo alifariki dunia akiwa njiani kulipeleka gari hilo kituo cha polisi, alifariki muda mfupi baada ya kufika kituoni au wakati anapelekwa hospitali.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro, Robert Boaz alisema polisi huyo alikufa ghafla akiwa kazini lakini alikataa kuingia kwa undani wa tukio hilo lilitokea Ijumaa kati ya saa 5:00 asubuhi na saa 6:00 mchana, baada ya trafiki huyo kukamata daladala linalofanya kazi zake kati ya Kiborloni na katikati ya mji.

Mmoja wa mashuhuda alisema “Baada ya kuikamata hiyo Hiace (Toyota) pale Kiborloni aliingia kwenye hiyo gari na kukaa kiti cha mbele pembeni ya dereva na kumwamuru kulipeleka kituoni.

“Wakati wakiwa njiani kuelekea kituoni ghafla yule trafiki akawa haongei na akawa anamwegemea dereva… hiyo hali iliendelea hadi walipofika kituoni ndipo dereva akawaeleza trafiki wenzake.” Mwili wa polisi huyo ulisafirishwa juzi kwenda Mbeya kwa mazishi.

Chanzo:MWananchi

Viewing all 104712 articles
Browse latest View live




Latest Images